Online Document)

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

Online Document) Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _____________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Kumi na Tatu – Tarehe 31 Machi, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAJI: Taarifa ya Nane ya Mwaka ya EWURA kwa mwaka 2014 (The 8th EWURA Annual Report for the year 2014). MASWALI NA MAJIBU Na. 130 Hitaji la Maji MHE. RIZIKI S. LULIDA aliuliza:- Vijiji vya Mvuleni, Mloo, Mnang‟ole, Kilolambwani na Minambwe vina shida kubwa ya maji na wananchi wanapata shida kutembea umbali mrefu kwenda kutafuta maji:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo hilo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Riziki Said Lulida, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua ukubwa wa tatizo la maji na adha inayowakabili wananchi wa vijiji vya Mvuleni, Mlolo, Mnang‟ole, Kilolambwani na Minambwe. Halmshauri ya Wilaya ya Lindi ikishirikiana na Bonde la Mto Ruvuma na Pwani ya Kusini tayari imefanya utafiti wa maji chini ya ardhi katika vijiji vya Mvuleni na Kilolambwani. Hata hivyo, sampuli za maji zilizochukuliwa kutoka kijiji cha Kilolambwani zilionyesha kuwa maji hayo hayafai kwa matumizi ya binadamu kwani yana chumvi nyingi. 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri imepanga kufanya utafiti mwingine katika chanzo kingine cha maji katika kijiji cha Kilolambwani. Vijiji vya Mvuleni na Kilolambwani ni miongoni mwa vijiji 10 vilivyopo katika Mpango wa Utekelezaji wa Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji kwa mwaka wa fedha 2015/2016. Bajeti iliyotengwa katika Halmashauri kwa ajili ya miradi ya maji kwa mwaka 2015/2016 ni shilingi milioni 565.6 ambapo kati ya hizo shilingi milioni 357.5 zitatumika kwa ajili ya miradi ya vijiji vya Mvuleni, Mlolo, Kilolambwani na Minambwe. Mheshimiwa Naibu Spika, katika kijiji cha Mnang‟ole utafiti wa maji chini ya ardhi umefanyika. Ujenzi wa mradi wa maji umepangwa kutekelezwa katika bajeti ya mwaka 2015/2016 ambapo zimetengwa shilingi milioni 27.5 kupitia fedha za ruzuku ya maendeleo (CDG). Mheshimiwa Naibu Spika, Minambwe ni kitongoji katika kijiji cha Kilangala „A‟ ambapo kuna mradi wa maji uliojengwa na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA). Halmashauri ikishirikiana na jamii imekuwa ikiufanyia ukarabati ili kuongeza huduma ya maji katika maeneo ya kijiji. Mpaka sasa kupitia Mpango wa Matokeo ya Haraka (quick wins), Halmashauri imekwishanunua jenereta kwa ajili ya mradi huu. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, nakushukuru. MHE. RIZIKI S. LULIDA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitoe shukrani za dhati kwa Waziri mwenye dhamana ya Maji wakati nilipompelekea tatizo hili alinipatia maafisa kutoka Bonde la Mto Ruvuma, Ndugu Msengi na Ndugu Amadeus tukaenda katika maeneo hayo na kuona matatizo yalipofikia. Hayo maeneo ni mapito ya wanyama na wananchi wanatembea kwa kilomita nyingi zaidi ya 20 kutafuta maji usiku na hivyo kuwa ni kero kubwa. Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo basi, kwa vile imeshindikana na hali inaonekana ni tete kutokana usemi wako kuwa maji ni mabaya hayafai kwa matumizi ya binadamu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuvuna maji ya mvua ili wananchi wapate maji? Wananchi wa kule wanasema wanataka maji kwa sababu imeshakuwa kero, akina mama wanakwenda kujifungua hospitalini na hawana maji. Kwa nini wasitumie njia ya kuvuna maji ya mvua ili kupunguza kero? Hilo la kwanza. Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, tukishirikiana mimi na Mama Jane Goodall alipeleka fedha kwa ajili ya kuchimba kisima katika kijiji cha Mnyangara na alipeleka kila kitu lakini mpaka leo wananchi hawajapata huduma hiyo kwani kumetokea upungufu mkubwa. Je, Serikali itakuwa tayari kutumia fedha angalau shilingi milioni 10 ili kumaliza tatizo hilo ili na wale wananchi wa Mnyangara waweze kusaidiwa? Ahsante! NAIBU SPIKA: Majibu ya swali hilo, Naibu Waziri wa Maji, Mheshimiwa Amos Makalla. NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ambayo kwa kiasi kikubwa yametosheleza katika swali lile la msingi. Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, nimhakikishie kwamba wiki mbili zilizopita nimefanya ziara katika Mkoa wa Lindi na nilikuwa katika Jimbo la Mchinga ambapo vijiji hivi anavyovitaja nimepata taarifa zake. Nilikuwa na Mbunge, Mheshimiwa Mtanda lakini nimshukuru kwa kazi kubwa hiyo aliyoifanya lakini nataka nimhakikishie tu kwamba vijiji alivyovitaja ikiwemo Kilolambwani ambako yalipatikana maji yaliyokuwa na chumvi, walipima tena na huu mradi umewekwa katika WSDP, Awamu ya II. 2 Nakala ya Mtandao (Online Document) Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ushauri alioutoa wa kuvuna maji ya mvua, ni mzuri. Naomba Waheshimiwa Wabunge muendelee kuhamasisha huko tunakoishi katika Majimbo yetu kwani itatusaidia katika maeneo ambayo ni vigumu zaidi kupata maji ardhini au sehemu nyingine zozote zile. Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Kijiji cha Mnyangara, hili tumelipokea, tutakaa na Mheshimiwa Lulida na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo pia na wataalam ili tuone ni namna gani tunaweza tukalikabili tatizo hili pamoja na jitihada kubwa ambazo zimeshafanywa na huyo mfadhili ambaye umemtaja. Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. NAIBU SPIKA: Tunaendelea, Mheshimiwa Waziri wa Maji, Profesa Maghembe, majibu ya nyongeza! WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa. Niendelee kuwashukuru Naibu Mawaziri kwa majibu mazuri sana waliyotoa. Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nitaongezea kidogo kwenye jibu la swali la nyongeza la pili lililotolewa na Mheshimiwa Amos Makalla. Mheshimiwa Lulida ameuliza kama Serikali iko tayari kutoa shilingi milioni 10 ili kumaliza hilo tatizo dogo ambalo lipo katika Kijiji alichokitaja. Napenda nimhakikishie kwamba Serikali itatoa fedha hizo ili kutatua tatizo hilo. (Makofi) NAIBU SPIKA: Nakushukuru sana. Tunaendelea na swali linalofuata la Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola. Na. 131 Tatizo la Maji Safi na Salama Kata za Igowole na Nyololo MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Kata ya Igowole na Nyololo zinakabiliwa na tatizo la maji safi na salama:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la maji katika Kata hizi za Igowole na Nyololo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola Mbunge wa Mufindi Kusini kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua ukubwa wa tatizo na hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Jimbo la Mufindi Kusini zikiwemo Kata za Igowole na Nyololo. Kwa kuzingatia hali hiyo, Serikali imekuwa ikitenga bajeti kila mwaka kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji kwa kuzingatia vipaumbele vilivyowekwa. Katika mwaka wa fedha wa 2014/2015 Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi iliidhinishiwa shilingi 940,998,278/= kwa ajili ya kukamilisha utekelezaji wa miradi katika vijiji kumi. Fedha zilizopokelewa hadi sasa ni shilingi 292,258,930/=. Mheshimiwa Naibu Spika, ili kutatua tatizo la maji katika Kata ya Nyololo, Serikali inatekeleza mradi wa maji wa mtiririko katika kijiji cha Maduma ambapo katika bajeti ya mwaka 2013/2014 zilitengwa shilingi 74,434,248/= kupitia Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) na 3 Nakala ya Mtandao (Online Document) fedha zote zimeshapokelewa. Mradi huu unategemewa kukamilika Mei, 2015. Mradi mwingine ambao unatekelezwa na Serikali katika Kata ya Nyololo ni mradi wa pamoja unaojumuisha vijiji vitatu (3) vya Nyololo, Shuleni, Njojo na Lwing‟ulo. Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Kata ya Igowole, Serikali imepanga kutekeleza miradi ya maji katika vijiji vya Sawala, Mtwango, Lufuna, Kibao, Luhunga na Igoda katika mwaka 2015/2016. Jumla ya shilingi 949,827,800/= zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji katika vijiji hivyo. Serikali itaendelea kuweka kipaumbele na kutenga bajeti kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji kadri upatikanaji wa rasilimali fedha utakavyoruhusu. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Kigola, swali la nyongeza. MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niishukuru Serikali kwa kutekeleza miradi ya maji katika kijiji cha Ikiliminzoo ambapo niliomba shilingi 750,000,000/= na Serikali ilishaleta na mradi ule umekamilika na namuomba Waziri wa Maji atembelee na kufungua mradi ule mkubwa sana. Kwa hiyo, sasa hivi Ikiliminzoo wanaendelea kupata maji. Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile huu mradi wa Maduma, naishukuru Serikali kwa kutusikiliza sisi Wabunge tukiomba msaada na mmeshafanya kazi nzuri na kweli fedha zilishakwenda mradi unafanyiwa kazi. (Makofi) Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niulize maswali madogo mawili. Swali la kwanza, nimeuliza kuhusu Kata ya Mtwango na Igowole ni tofauti. Kwanza, namshukuru kwamba Kata ya Sawala tatizo la maji litatatuliwa na sasa hivi kuna shilingi 200,000,000/= niliambiwa zimeshatayarishwa. Nimeuliza kuhusu Kata ya Mtwango Mjini hakuna maji kabisa. Mimi Mbunge nimechimba kisima kirefu ambacho kimegharimu karibu shilingi 17,000,000/=. Je, Serikali inaweza ikaniongezea hata shilingi 50,000,000/= ili niweze kufunga motor kwa ajili ya kupeleka maji kwenye tenki la maji? Kwa sababu pale mjini hakuna maji kabisa, wananchi wananunua ndoo moja ya maji kwa shilingi 50/=. Je, Serikali inaweza ikanisaidia na mimi niongezee pale ili wananchi wa Kata ya Igowole waweze kupata maji? Mheshimiwa Naibu Spika,
Recommended publications
  • Issued by the Britain-Tanzania Society No 105 May - Aug 2013
    Tanzanian Affairs Text 1 Issued by the Britain-Tanzania Society No 105 May - Aug 2013 Even More Gas Discovered Exam Results Bombshell Rising Religious Tensions The Maasai & the Foreign Hunters Volunteering Changed my Life EVEN MORE GAS DISCOVERED Roger Nellist, the latest volunteer to join our panel of contributors reports as follows on an announcement by Statoil of their third big gas discovery offshore Tanzania: On 18 March 2013 Statoil and its co-venturer ExxonMobil gave details of their third high-impact gas discovery in licence Block 2 in a year. The new discovery (known as Tangawizi-1) is located 10 kilometres from their first two discoveries (Lavani and Zafarani) made in 2012, and is located in water depth of 2,300 metres. The consortium will drill further wells later this year. The Tangawizi-1 discovery brings the estimated total volume of natural gas in-place in Block 2 to between 15 and 17 trillion cubic feet (Tcf). Depending on reservoir characteristics and field development plans, this could result in recoverable gas volumes in the range of 10-13 Tcf from just this one Block. These are large reserves by international stand- ards. By comparison, Tanzania’s first gas field at Songo Songo island has volumes of about 1 Tcf. Statoil has been in Tanzania since 2007 and has an office in Dar es Salaam. It operates the licence on Block 2 on behalf of the Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) and has a 65% working interest, with ExxonMobil Exploration and Production Tanzania Limited holding the remaining 35%. It is understood that under the Production Sharing Agreement that governs the operations, TPDC has the right to a 10% working participation interest in case of a development phase.
    [Show full text]
  • Human Rights and Business Report 2015
    LEGALLEGAL AND AND HUMAN HUMAN RIGHTS RIGHTS CENTRE CENTRE HUMANHUMAN RIGHTS RIGHTS AND AND BUSINESS BUSINESS REPORT REPORT OF 2015 2015 Taking Stock of Labour Rights, Land Rights, Gender, Taxation, Corporate Accountability,Taking Stock Environmental of Labour Justice Rights, and Performance Land Rights, of Regulatory Gender, Authorities Taxation, Corporate Accountability, Environmental Justice and Performance of Regulatory Authorities LEGAL AND HUMAN RIGHTS CENTRE HUMAN RIGHTS AND BUSINESS REPORT 2015 PUBLISHER Legal and Human Rights Centre Justice Lugakingira House, Kijitonyama P.O Box 75254, Dar es Salaam, Tanzania Tel.: +255222773038/48 Fax: +255222773037 Email: [email protected] Website: www.humanrights.or.tz PARTNERS ISBN:978-9987-740-26-0 © July, 2016 ii ii EDITORIAL BOARD Dr. Helen Kijo-Bisimba, Adv. Imelda Lulu Urrio Adv. Anna Henga Ms. Felista Mauya Mr. Castor Kalemera RESEARCH COORDINATOR Adv. Masud George ASSISTANT RESEARCHERS 29 Assistant Researchers 14 Field Enumerators REPORT WRITER Adv. Clarence Kipobota LAYOUT & DESIGN Mr. Rodrick Maro Important Message of the Year 2015 LHRC endorses the United Nations’ call to all nations (and everyone) to promote sustained, inclusive and sustainable economic growth, with full and productive employment and decent work for all as it is implied under Goal 8 of the United Nations Strategic Development Goals (SDGs) 2030. iii iii DISCLAIMER The opinions expressed by the sampled respondents in this report do not necessarily reflect the official position of the Legal and Human Rights Centre (LHRC). Therefore, no mention of any authority, organization, company or individual shall imply any approval as to official standing of the matters which have implicated them. The illustrations used by inferring some of the respondents are for guiding the said analysis and discussion only, and not constitute the conclusive opinion on part of LHRC.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA TATU Kikao Cha Hamsini Na Sita
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Hamsini na Sita – Tarehe 22 Juni, 2021 (Bunge Lilianza saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba tukae. Waheshimiwa tunaendelea na Mkutano wetu wa Tatu, leo ni Kikao cha Hamsini na Sita na kabla hatujaendelea nitumie nafasi hii kuwashukuru sana wasaidizi wangu wote wakiongozwa na Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa David Kihenzile, Mheshimiwa Zungu na Mheshimiwa Najma kwa kazi nzuri ambayo wameifanya wiki nzima kutuendeshea mjadala wetu wa bajeti. (Makofi) Sasa leo hapa ndio siku ya maamuzi ambayo kila Mbunge anapaswa kuwa humu ndani, kwa Mbunge ambaye Spika hana taarifa yake na hatapiga kura hapa leo hilo la kwake yeye. (Makofi) Katibu. NDG. NENELWA MWIHAMBI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Maswali na tunaanza na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Kwela. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Na. 465 Ujenzi wa Makao Makuu ya Halmashauri Katika Mji wa Laela MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi za Makao Makuu ya Halmashauri ya Sumbawanga katika Mji wa Laela baada ya agizo la Serikali la kuhamisha Makao Makuu? SPIKA: Majibu ya swali hilo muhimu la watu wa Kwela, Mheshimiwa Naibu Waziri - TAMISEMI, Mheshimiwa Dkt. Festo Dugange tafadhali. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Jimbo la Kwela kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ni miongoni mwa Halmashauri 30 zilizohamia kwenye maeneo mapya ya utawala mwaka 2019.
    [Show full text]
  • Tarehe 4 Aprili, 2019
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Tatu – Tarehe 4 Aprili, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba tukae. Leo ni kikao cha tatu cha Mkutano wetu wa Kumi na Tano. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI: Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, AJIRA, KAZI VIJANA NA WAZEE NA WENYE ULEMAVU: Taarifa ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2019/2020. MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA: Taarifa 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020. MHE. HASNA S.K. MWILIMA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu utekelezaji wa Bajeti ya Mfuko wa Bunge kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Mfuko huo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA - MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MASUALA YA UKIMWI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu utekelezaji wa Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu (Tume ya Uratibu na Udhibiti wa UKIMWI) kwa mwaka wa fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Mbili - Tarehe 22 Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kwa masikitiko makubwa natoa taarifa kwamba Mheshimiwa Mussa Hamisi Silima, Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar, jana Jumapili, tarehe 21 Agosti, 2011 majira ya jioni kama saa mbili kasorobo hivi walipokuwa wakirejea kutoka Dar es Salaam, yeye na familia yake walipata ajali mbaya sana katika eneo la Nzuguni, Mjini Dodoma. Katika ajali hiyo, mke wa Mbunge huyo aitwaye Mwanaheri Twalib amefariki dunia na mwili wa Marehemu upo hospitali ya Mkoa hapa Dodoma ukiandaliwa kupelekwa Zanzibar leo hii Jumatatu, tarehe 22 August, 2011 kwa mazishi yatanayotarajiwa kufanyanyika alasili ya leo. Kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Wabunge tusimame dakika chache tumkumbuke. (Heshima ya Marehemu, dakika moja) (Hapa Waheshimiwa Wabunge walisimama kwa dakika moja) Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, amina. Ahsanteni sana, tukae. Kwa hiyo sasa hivi tunavyoongea Mheshimiwa Mbunge ambae nae pia ameumia vibaya na dereva wake wanaondoka na ndege sasa hivi kusudi waweze kupata yanayohusika kule Dar es Salaam na pia kule watakuwa na watu wa kuwaangalia zaidi. Lakini walikwenda Zanzibar kumzika kaka yake na Marehemu huyu mama. Kwa hiyo, wamemzika marehemu basi wakawa wanawahi Bunge la leo ndiyo jana usiku wamepata ajali. Kwa hiyo, watakaokwenda kusindikiza msiba, ndege itaondoka kama saa tano watakwenda wafuatao, watakwenda Wabunge nane pamoja na mfawidhi zanzibar yeye anaongozana na mgonjwa sasa hivi lakini ataungana na wale kwenye mazishi.
    [Show full text]
  • Tarehe 3 Februari, 2021
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA PILI Kikao cha Pili – Tarehe 3 Februari, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Tukae. Katibu. NDG. RUTH MAKUNGU – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaanza na maswali Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, sasa aulize swali lake. Na. 16 Ujenzi wa Barabara za Lami - Mji wa Mafinga MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza Ujenzi wa Barabara za lami na kufunga taa za barabarani katika Mji wa Mafinga chini ya Mpango wa Uendelezaji Miji nchini? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NAIBU WAZIRI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyenijalia mimi na Waheshimiwa Wabunge wote afya njema na kutuwezesha kuwa wawakilishi wa wananchi kupitia Bunge lako Tukufu. Mheshimiwa Naibu Spika, pili, naomba nichukue nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa imani kubwa aliyonipa kwa kuniteua kuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Namshukuru sana Mheshimiwa Rais. (Makofi) Mheshimiwa Naibu Spika, tatu, nawashukuru sana wananchi wa Jimbo la Wanging’ombe kwa kunichagua na kuchagua mafiga
    [Show full text]
  • Online Document)
    Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ________________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini – Tarehe 10 Juni, 2014 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge Maswali tunaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu, atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Josephat Kandege. Na. 216 Kugawa Jimbo la Kalambo MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Wilaya ya Kalambo ni Jimbo moja lenye eneo kubwa sana la Kiutawala ikipakana na nchi za Zambia na Congo DRC:- Je, Serikali haioni kuwa ipo haja ya kuligawa Jimbo hilo ili kupunguza eneo la uwakilishi wa wananchi? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege, Mbunge wa Kalambo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Ibara ya 75(1) – (5) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano a Tanzania ya Mwaka 1977 imeainisha utaratibu na vigezo vinavyotumiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika kufikia uamuzi wa kugawa mipaka ya Majimbo ya Uchaguzi angalau kila baada ya kipindi cha miaka kumi (10). Vigezo vinavyozingatiwa na Tume ni pamoja na ukubwa wa eneo la utawala; upatikanaji wa njia ya mawasiliano; Idadi ya Watu na hali ya kijiografia katika jimbo linalokusudiwa kugawanywa. Vigezo vingine vinavyotumika ni hali ya uchumi; mipaka ya kiutawala; jimbo moja lisiwe ndani ya Wilaya/Halmashauri mbili, Kata moja isiwe ndani ya Majimbo mawili; Mazingira ya Muungano, Mgawanyo wa Wastani wa Idadi ya Watu; uwezo wa Ukumbi wa Bunge; Idadi ya Viti Maalum vya Wanawake na mpangilio wa maeneo ya makazi ya watu yaliyopo.
    [Show full text]
  • Report on the State of Pastoralists' Human Rights in Tanzania
    REPORT ON THE STATE OF PASTORALISTS’ HUMAN RIGHTS IN TANZANIA: SURVEY OF TEN DISTRICTS OF TANZANIA MAINLAND 2010/2011 [Area Surveyed: Handeni, Kilindi, Bagamoyo, Kibaha, Iringa-Rural, Morogoro, Mvomero, Kilosa, Mbarali and Kiteto Districts] Cover Picture: Maasai warriors dancing at the initiation ceremony of Mr. Kipulelia Kadege’s children in Handeni District, Tanga Region, April 2006. PAICODEO Tanzania Funded By: IWGIA, Denmark 1 REPORT ON THE STATE OF PASTORALISTS’ HUMAN RIGHTS IN TANZANIA: SURVEY OF TEN DISTRICTS OF TANZANIA MAINLAND 2010/2011 [Area Surveyed: Handeni, Kilindi, Bagamoyo, Kibaha, Iringa-Rural, Morogoro-Rural, Mvomero, Kilosa, Mbarali and Kiteto Districts] PARAKUIYO PASTORALISTS INDIGENOUS COMMUNITY DEVELOPMENT ORGANISATION-(PAICODEO) Funded By: IWGIA, Denmark i REPORT ON THE STATE OF PASTORALISTS’ RIGHTS IN TANZANIA: SURVEY OF TEN DISTRICTS OF TANZANIA MAINLAND 2010/2011 Researchers Legal and Development Consultants Limited (LEDECO Advocates) Writer Adv. Clarence KIPOBOTA (Advocate of the High Court) Publisher Parakuiyo Pastoralists Indigenous Community Development Organization © PAICODEO March, 2013 ISBN: 978-9987-9726-1-6 ii TABLE OF CONTENTS ACKNOWLEDGEMENTS ..................................................................................................... vii FOREWORD ........................................................................................................................viii Legal Status and Objectives of PAICODEO ...........................................................viii Vision ......................................................................................................................viii
    [Show full text]
  • Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania
    JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA KUMI YATOKANAYO NA KIKAO CHA NANE 08 FEBRUARI, 2018 MKUTANO WA KUMI KIKAO CHA NANE TAREHE 08 FEBRUARI, 2018 I. DUA Saa 3:00 Asubuhi Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), Naibu Spika alisoma Dua na kuongoza Bunge. MAKATIBU MEZANI: 1. Ndg. Stephen Kagaigai 2. Ndg. Nenelwa Wankanga 3. Ndg. Lawrence Makigi II. HATI ZA KUWASILISHA MEZANI: (a) Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Watu Wenye Ulemavu) - Mhe. Jenista J. Mhagama aliwasilisha Taarifa ya Hali ya Dawa za Kulevya ya Mwaka 2016; (b) Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba na Sheria - Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa aliwasilisha Mezani Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017; (c) Mhe. Esther Mmasi K.n.y Mwenyekiti wa Kamati ya Sheria Ndogo aliwasilisha Mezani Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017; (d) Mhe. Maidah Abdallah K.ny Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa aliwasilisha Mezani Taarifa ya Kamati hiyo kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017. 1 III. MASWALI KWA WAZIRI MKUU: Waheshimiwa Wabunge wafuatao waliuliza maswali:- (a) Mhe. Richard Mganga Ndassa - CCM (b) Mhe. Margareth Simwanza Sitta - CCM (c) Mhe. Devota Methew Minja - CHADEMA (d) Mhe. Zubeir Mohamed Kuchauka - CUF (e) Mhe. Balozi Diodorus Kamala - CCM IV. MASWALI YA KAWAIDA: Maswali yafuatayo yaliulizwa na kujibiwa kama ifuatavyo:- OFISI YA RAIS (TAMISEMI): Swali Na. 99 Mhe. Flatei Gregory Massay Nyongeza (i) Mhe. Flatei Gregory Massay (ii) Mhe.
    [Show full text]
  • Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1 BUNGE LA TANZANIA
    Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Tatu - Tarehe 16 Juni, 2014 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tukae. Katibu! HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI: Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na :- MWENYEKITI WA KAMATI YA BAJETI: Taarifa ya Kamati ya Bajeti Juu ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2013 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka 2014/2015 Pamoja na Tathmini ya Utekelezaji wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2013/2014 na Mapendekezo ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA OFISI YA RAIS, MAHUSIANO NA URATIBU): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) Juu ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2013 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. CHRISTINA LISSU MUGHWAI (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA WIZARA YA FEDHA): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Wizara ya Fedha juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. Na. 240 Ukosefu wa Hati Miliki MHE. NYAMBARI C. M. NYANGWINE aliuliza:- Ukosefu wa Hatimiliki za Kimila Vijijini unasababisha migogoro mingi ya ardhi baina ya Kaya, Kijiji na Koo na kupelekea kutoweka kwa amani kwa wananchi kama inavyotokea huko Tarime. 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) (a) Je, ni kwa nini Serikali haitoi
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Moja – Tarehe 5 Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Randama ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. NAIBU WAZIRI WA KAZI NA AJIRA: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kazi na Ajira kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. MHE. JENISTA J. MHAGAMA - MWENYEKITI WA KAMATI YA MAENDELEO YA JAMII: Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Jamii kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Kazi na Ajira kwa Mwaka 2010/2011 Pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. MHE. REGIA E. MTEMA - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KWA WIZARA YA KAZI NA AJIRA: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani juu ya Wizara ya Kazi na Ajira kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. MASWALI NA MAJIBU Na. 373 Kuboreshwa kwa Maslahi ya Madiwani MHE. FELISTER A. BURA aliuliza:- Madiwani ni nguzo muhimu katika kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi na nia ya Serikali ni kuboresha maslahi ya Madiwani iil waweze kutimiza wajibu wao ipasavyo;- Je, ni lini maslahi ya Madiwani yataboreshwa? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Felister Bura, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba, Waheshimiwa Madiwani ni nguzo muhimu katika kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi.
    [Show full text]
  • MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA TATU Kikao Cha
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Arobaini na Tatu – Tarehe 3 Juni, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba tukae. Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na Mkutano wetu wa Tatu, leo ni Kikao cha Arobaini na Tatu. Katibu NDG. NENELWA MWIHAMBI, ndc – KATIBU WA BUNGE: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, aah sasa hivi unavaa sketi ndefu, hataki ugomvi na Mgogo. (Kicheko) Tunaendelea, Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. NENELWA MWIHAMBI, ndc – KATIBU WA BUNGE: MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Maswali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Waziri Mkuu karibu sana. (Makofi) Waheshimiwa Wabunge, nawakumbusha tena kuhusu maswali ya kisera sio matukio, sio nini, ni ya kisera. Tunaanza na Mheshimiwa Mbunge wa Liwale, Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka, maswali kwa kifupi. MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kwanza kuuliza swali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu. Mheshimiwa Spika, swali langu litahusu sekta ya korosho. Mwaka huu tumepata taarifa kwamba Serikali ilijipanga kutupatia pembejeo wakulima wa zao la korosho kwa maana kwamba waje kuzilipa baadaye kwenye mjengeko wa bei. Hata hivyo, kuna taharuki kubwa kwa wakulima wetu wa korosho baada ya Bodi ya Korosho kuleta waraka kwenye Halmashauri zetu, wakiwaambia kila mkulima akipeleka zao lile kwenye mnada kila kilo moja itakatwa shilingi 110 bila kujali kwamba mkulima yule amechukua pembejeo kwa kiwango gani.
    [Show full text]