Tarehe 24 Aprili, 2017

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

Tarehe 24 Aprili, 2017 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Kumi na Moja – Tarehe 24 Aprili, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Mussa Azzan Zungu) Alisoma Dua MWENYEKITI: Tukae. Katibu! NDG. THEONEST RUHILABAKE - KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na Taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2017/2018. NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. 1 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. STANSLAUS H. NYONGO – (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA): Taarifa ya Kamati ya Viwanda Biashara na Mazingira kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) kwa mwaka wa fedha 2016/2017 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2017/2018. MHE. CECILIA D. PARESSO – (K.n.y. MSEMAJI WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) kwa mwaka wa fedha 2017/2018. MHE. CECILIA D. PARESSO - (K.n.y. MSEMAJI WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MAZINGIRA): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) kwa mwaka wa fedha 2017/2018. MHE. JOSEPH K. MHAGAMA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KATIBA NA SHERIA): Taarifa ya Kamati ya Katiba na Sheria kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano kwa mwaka 2016/2017 pamoja na maoni ya Kamati juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2017/2018. MWENYEKITI: Katibu. 2 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. THEONEST RUHILABAKE - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU Na. 85 Utaratibu wa kuwasimamisha kazi Watumishi wa Umma MHE. MCH.PETER S. MSIGWA (K.n.y. MHE. RUTH H. MOLLEL) Aliuliza:- Nchi yetu inaendeshwa kwa kuzingatia Katiba, Sheria na Kanuni katika kuajiri na kuwasimamisha kazi watumishi wa umma. Kuna baadhi ya watumishi wa umma wamesimamishwa kazi na Mheshimiwa Rais, RC na hata DC bila kuzingatia Sheria ya Utumishi wa Umma na Kanuni zake. Je, Serikali inasemaje kuhusu hili? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA Alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ruth Mollel, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua za nidhamu katika utumishi wa umma hutekelezwa kwa kuzingatia Katiba, Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo mbalimbali. Kwa mujibu wa Ibara ya 36 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Rais ndiye mwenye mamlaka ya mwisho kuhusu usimamizi na uendeshaji wa utumishi wa umma, ikiwemo kuanzisha, kufuta Ofisi na kuchukua hatua za nidhamu. Mheshimiwa Mwenyekiti, Ibara hiyo ya 36(2) imempa Rais uwezo wa kukasimu madaraka yake kwa mamlaka mbalimbali ndani ya utumishi wa umma. Hata hivyo kukasimu madaraka hakuwezi kutafsiriwa kwamba Rais hana mamlaka hayo tena kama ilivyofafanuliwa katika Ibara ya 3 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) 36(4) ya Katiba na Kifungu cha 21(4) cha Sheria ya Utumishi wa Umma Sura ya 298. Mheshimiwa Mwenyekiti, pale maelekezo ya kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya watumishi wa umma yanapotolewa na Viongozi wa Serikali, Mamlaka za Nidhamu za watumishi husika ndizo zenye dhamana ya kuchukua hatua kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za Utumishi wa Umma. MWENYEKITI: Mheshimiwa Msigwa. MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nakubaliana naye kwamba kwa mujibu wa Sheria na Katiba yetu, Rais ndiye mwenye mamlaka ya mwisho na ndiye Mwajiri Mkuu. Swali la msingi limeulizwa kwamba kumekuwa na practice ya kuanzia Rais mwenyewe na ma-DC na RCs kutumbua au kuwasimamisha watu kwa njia ya mnada, kupigia kura atumbuliwe au asitumbuliwe, kwa hiyo, swali la msingi linaulizwa hapa, ni kwa nini Serikali isifuate utaratibu na kanuni na sheria ambazo sisi wenyewe tumeziweka? (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, hawa ma-RC na ma-DC ni kada ya kisiasa kama sisi Wabunge tulivyo, hawana weledi na ndiyo maana Baba wa Taifa alisema tuliweka sheria ngumu sana ili mtu asizuke tu na kufukuza watu ovyo ovyo. Kwa kumuenzi Baba wa Taifa ambaye alithamini sana kada ya watendaji wa umma; je, Serikali itatoa tamko sasa kwamba ma-RC na ma-DC wasikurupuke tu kuwafukuzisha watu bila kufuata taratibu na kanuni za nchi? (Makofi) MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri, majibu kwa kifupi. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa kuhusiana na kwa nini Serikali 4 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) isifuate utaratibu, napenda kuendelea kusisitiza kwamba Serikali inafuata uratatibu na kwamba kwa wateule ambao wameteuliwa na Mheshimiwa Rais, hatua zao za kinidhamu huchukuliwa na Katibu Mkuu Kiongozi kwa mujibu wa kifungu cha 4(3)(d) cha Sheria ya Utumishi wa Umma. Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisema katika Ibara ya 36(4), Mheshimiwa Rais pamoja na kukasimu bado anayo mamlaka ya mwisho na hakatazwi kutumia mamlaka yake. Kwa watumishi wengine wa umma, kwa mujibu wa kifungu cha 6(1)(b) cha Sheria ya Utumishi wa Umma, Mamlaka za Nidhamu zimepewa mamlaka yao ya mwisho kabisa ya kuweza kuchukua hatua kwa watumishi wengine ambao sio wateule wa Rais. Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuendelea kusisitiza kwamba jambo la msingi katika mamlaka za kinidhamu zinapochukua hatua, wanatakiwa wazingatie hatua tatu zifuatazo:- Kwanza kabisa waweze kutoa hati ya nashtaka; pili, watoe fursa ya kujitetea kwa yule mtuhumiwa au mtumishi; na mwisho, tatu, uchunguzi wa kina uweze kufanyika ili kuthibitisha tuhuma hizo. Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, napenda kusema, utaratibu mzima wa kina na mwongozo umefafanuliwa katika kanuni ya 46 na 47 za Kanuni za Utumishi wa Umma. Endapo kuna mtumishi wa umma anaona hajaridhika na hatua za kinidhamu zilizochukuliwa, anayo fursa kwa mujibu wa kifungu cha 25 cha Sheria ya Utumishi wa Umma kuweza kukata rufaa. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na suala la pili kwamba Serikali inatoa tamko gani katika hatua ambazo zimechukuliwa na ma-RC na ma-DC? Naendelea kusisitiza kwamba kifungu cha 6(1)(b) na kifungu cha 4(3)(d) kimeelekeza Mamlaka za Nidhamu ni zipi? Ndicho ambacho Serikali imekuwa ikifuata. (Makofi) 5 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MWENYEKITI: Mheshimiwa Silinde, ajiandae Mheshimiwa Chatanda. MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwenye majibu ya Mheshiwa Waziri amesema, endapo mtumishi hajaridhika na hatua za kinidhamu alizochukuliwa, akate rufaa. Sasa endapo mtumishi huyo ametumbuliwa na Mheshimiwa Rais na hajaridhika na hayo matokeo, wapi achukue hatua za kuja kukata rufaa? (Makofi) MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza Mheshimiwa Silinde ameuliza swali zuri sana; na kama atakuwa amefuatilia hata katika hotuba yangu ya bajeti ya Ofisi ya Rais (Utumishi), ziko kesi mbalimbali ambazo hata Ofisi ya Rais (Utumishi) pia tunashitakiwa. Wako ambao wanafungua kupinga maamuzi ya Mheshimiwa Rais, wako ambao wanafungua kesi kupinga maamuzi ya Katibu Mkuu Kiongozi, lakini pia katika Tume yetu ya Utumishi wa Umma ambayo ni mamlaka yenye Mamlaka ya Urekebu wamepokea kesi mbalimbali. Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano, katika mwaka huu wa fedha tu peke yake, zaidi ya watumishi wa umma 76 wameweza kukata rufaa katika Tume ya Utumishi wa Umma na endapo hawataridhika, bado tunacho Kitengo cha Rufaa chini ya Mheshimiwa Rais pia (Public Service Appeals) wanaweza pia wakakata rufaa nyingine. Kwa hiyo, namhakikishia tu Mheshimiwa Mbunge kwamba taratibu zipo na zinafuatwa na ziko wazi kabisa na wako ambao hata wanajikuta walikata rufaa dhidi ya Mheshimiwa Rais na wakaja kushinda endapo kama kuna taratibu inaonekana hazikufuatwa. (Makofi) MWENYEKITI: Mheshimiwa Chatanda. MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana… 6 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru sana na kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Utumishi kwa majibu mazuri sana. Nilitaka kuongezea, kuna moja ambalo limewataja Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kuchukua hatua za kuwasimamisha au kuwafukuza kazi watumishi wa umma. Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma kifungu cha (5) cha Sheria ya Tawala za Mikoa, Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya ndio wawakilishi wa Serikali Kuu kwenye maeneo yao. Ukisoma pia kifungu cha 87 cha Sheria ya Mamlaka za Serikali za Mitaa, kinawataja hawa na kwa ajili ya usahihi wa nukuu, napenda nisome kwa sababu wakati mwingine tunauliza swali lile lile kila siku. Bahati mbaya imeandikwa kwa Kiingereza, inasema hivi; “In relation to the exercise of the powers and performance of the functions of the Local Government Authorities confered by this Act, the role of the Regional Commissioner and the District Commissioner shall be to investigate the legality when questioned of the actions and decisions of the Local Government Authorities within their areas of jurisdiction and to inform the Minister to take such other appropriate action as may be required.” (Makofi) MBUNGE FULANI: Yes! WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ukisoma kifungu hiki unaona kabisa kwamba wao kuchukua hatua zozote zile, ziwe za kiutumishi ni sahihi, isipokuwa utaratibu aliouzungumza Mheshimiwa Waziri wa Utumishi ndiyo unaotakiwa. Kwa mfano, Mkuu wa Mkoa anaposema wewe hufai, umefanya makosa haya, akasema publicly, siyo ndiyo kafanya tendo hilo la kumsimamisha au kumuadhibu yule mtumishi, anachofanya pale, baada ya tamko lile, sasa Mamlaka ya Nidhamu ya mtumishi husika ndiyo inachukua hatua.
Recommended publications
  • Madini News Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Toleo Na.2 Wa Tanzania Machi, 2020 HALIUZWI
    Toleo Na.2 // Machi 2020 Yaliyomo // Biteko - Nitasimama na Mzee Tume ya Leseni ya TanzaniteOne Imefutwa na Kisangani mpaka “asimame” Kurudishwa Serikalini - Biteko... Uk.04 ... Uk.08 Madini Bilioni 66.5 zapatikana tangu Wanawake Tume ya Madini kuanzishwa kwa masoko Wawakumbuka ya madini ... Uk.10 Yatima ... Uk.18 www.tumemadini.go.tz Tume ya Madini 2020 www.tumemadini.go.tz /TAHARIRI Salamu Kutoka kwa Waziri wa Madini Maoni ya Mhariri SEKTA YA MADINI INAIMARIKA, MAFANIKIO MASOKO TUENDELEZE USHIRIKIANO YA MADINI TUMEWEZA! Katika Mwaka wa Fedha 2019/2020 Wizara ya Madini ilipanga kutekeleza majukumu yake kupitia miradi Katika kuhakikisha kuwa Sekta ya Madini inakuwa na mchango mbalimbali ikilenga katika kuimarisha Sekta ya Madini, hivyo kuwa na mchango mkubwa kwenye ukuaji wa mkubwa kwenye ukuaji wa uchumi wa Taifa, Serikali kupitia uchumi wa nchi. Tume ya Madini kuanzia Machi, 2019 ilifungua masoko ya madini Katika Toleo lililopita nilielezea kwa kifupi kuhusu yale ambayo yamesimamiwa na kutekelezwa na Wizara na vituo vya ununuzi wa madini lengo likiwa ni kudhibiti utorosh- kwa kipindi cha takribani miaka miwili tangu kuanzishwa kwake. waji wa madini kwa kuwapatia wachimbaji wa madini nchini Katika Toleo hili nitaelezea kwa kifupi mafanikio ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara kwa kipindi cha sehemu ya kuuzia madini yao huku wakilipa kodi mbalimbali kuanzia Julai, 2019 hadi Februari, 2020. Kama ambavyo nilieleza Bungeni katika Hotuba yangu wakati Serikalini. nikiwasilisha Bajeti ya Wizara kwa Mwaka 2019/2020, nilieleza kuwa, Wizara imepangiwa kukusanya Shilingi 470,897,011,000.00 katika Mwaka wa Fedha 2019/2020. Uanzishwaji wa masoko ya madini na vituo vya ununuzi wa Napenda kuwataarifu wasomaji wa Jarida hili kuwa, hadi kufikia Februari, 2020 jumla ya Shilingi madini ni sehemu ya maelekezo yaliyotolewa kwenye mkutano wa 319,025,339,704.73 zimekusanywa ambazo ni sawa na asilimia 102 ya lengo la makusanyo ya nusu mwaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tazania, Dkt.
    [Show full text]
  • Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania Mkutano Wa Tatu Yatokanayo Na Kikao Cha Arobaini Na Saba 21 Juni, 2016
    JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA TATU YATOKANAYO NA KIKAO CHA AROBAINI NA SABA 21 JUNI, 2016 MKUTANO WA TATU - YATOKANAYO NA KIKAO CHA AROBAINI NA SABA TAREHE 21 JUNI, 2016 I. DUA: Saa 3.00 Asubuhi Naibu Spika (Mhe. Dkt.Tulia Ackson) alisoma Dua na Kuongoza Bunge. Makatibu Mezani: 1. Ndg. Theonest Ruhilabake 2. Ndg. Zainab Issa Wabunge wa Kambi ya Upinzani walitoka nje ya ukumbi wa Bunge baada ya dua kusomwa na Mhe. Naibu Spika. II. MASWALI: Maswali yafuatayo yaliulizwa na Waheshimiwa Wabunge na kujibiwa na Serikali:- OFISI YA WAZIRI MKUU: Swali Na.399 – Mhe. Raphael Masunga Chegeni [kny. Mhe. Salome Makamba] Swali la nyongeza: (i) Mhe. Raphael Masunga Chegeni (ii) Mhe. Abdallah Hamisi Ulega (iii) Mhe. Joseph Kasheku Musukuma (iv) Mhe. Mariam Nassoro Kisangi OFISI YA RAIS (TAMISEMI): Swali Na.400 Mhe. Oran Manase Njeza Swali la nyongeza: (i) Mhe. Oran Manase Njeza (ii) Mhe. Desderius John Mipata (iii) Mhe. Goodluck Asaph Mlinga Swali Na.401 – Mhe. Boniventura Destery Kiswaga Swali la nyongeza: (i) Mhe. Boniventura Destery Kiswaga (ii) Mhe. Augustino Manyanda Maselle (iii) Mhe. Richard Mganga Ndassa (iv) Mhe. Dkt. Dalali Peter Kafumu Swali Na. 402 – Mhe. Fredy Atupele Mwakibete Swali la Nyongeza: (i) Mhe. Fredy Atupele Mwakibete (ii) Mhe. Njalu Daudi Silanga (iii) Mhe. Halima Abdallah Bulembo (iv) Mhe. Azza Hilal Hamad 2 WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Swali Na.403 – Mhe Joseph Kakunda. kny Mhe. Ally Saleh Ally Swali la nyongeza: (i) Mhe. Joseph George Kakunda (ii) Mhe. Mussa Azzan Zungu (iii) Mhe. Cosato David Chumi (iv) Mhe.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA TATU Kikao Cha Thelathini
    NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Thelathini na Tano - Tarehe 2 Juni, 2016 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua (Hapa Waheshimiwa Wabunge wa Kambi ya Upinzani Walitoka Nje) NAIBU SPIKA: Tukae, Katibu. MBUNGE FULANI: Hamna posho ninyi. NAIBU SPIKA: Katibu. NDG. NEEMA MSANGI – KATIBU MEZANI: Maswali. MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Viti Maalum swali lake litaulizwa na Mheshimiwa Ally Keissy. Na. 284 Unyanyasaji Unaofanywa na Mgambo/Askari Kwa Wafanyabiashara Wadogo Wadogo MHE. ALLY K. MOHAMED (K.n.y. MHE. AIDA J. KHENANI) aliuliza:- Kumekuwa na hali ya ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na mgambo na askari polisi wanapotekeleza maagizo ya Serikali dhidi ya 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) wafanyabiashara wadogo wadogo hususan mama lishe, bodaboda pamoja na machinga. Je, Serikali inatoa tamko gani juu ya hali hiyo? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri Ofisi ya Rais, TAMISEMI. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, mgambo wanafanya kazi kwa mujibu wa sheria ya polisi wasaidizi ya mwaka 1969 kwa kuzingatia sheria hiyo, Halmashauri zimeruhusiwa kuajiri askari ngambo kwa ajili ya kusaidia usimamizi wa Sheria Ndogondogo za Halmashauri za Majiji, Manispaa, Miji na Wilaya. Mheshimiwa Naibu Spika, askari mgambo anayefanya kazi katika Halmashauri anawajibika kuzingatia sheria za nchi pamoja na sheria ndogo ndogo zilizotungwa na Halmashauri.
    [Show full text]
  • Briefing on “Business & Human Rights in Tanzania” – 2020
    photo courtesy of HakiArdhi BRIEFING ON “BUSINESS & HUMAN RIGHTS IN TANZANIA” – 2020 QUARTER 1: JANUARY – MARCH In March 2020, key stakeholders from civil society, the business community and various government agencies from Tanzania mainland and Zanzibar met in Dar es Salaam to discuss the topics of “land rights and environment” during the second Annual Multi-stakeholder Dialogue on Business and Human Rights (Ref.E1). “Land rights and environment” were identified as cross-cutting issues that affect the rights of many in various ways in Tanzania. Sustainable solutions for addressing the country’s many conflicts related to land are therefore essential to guarantee basic rights for all. During the multi-stakeholder meeting, four case studies on current issues of “land rights and envi- ronment” (Ref.E2) were presented by Tanzanian civil society organisations (Ref.E1). Their studies focussed on initiatives to increase land tenure security and on the tensions between conservation and rights of local communities. The studies confirm that land is indeed a critical socio-economic resource in Tan- zania, but a frequent source of tensions in rural areas due to competing needs of different land users, such as communities versus (tourism) investors or local communities versus conservation authorities (Ref. E2, E3). Women face a number of additional barriers acquiring land rights which affect their livelihoods (Ref.E4, E5). The absence of formalized land rights and land use plans in many regions of the country aids in sus- taining land-related challenges. Therefore, initiatives to address land tenure security (Ref.E5) can have positive effects on local communities (Ref.E6).
    [Show full text]
  • For Personal Use Only Use Personal for Sider All New Mining and Special Mining Licence Applications
    Quarterly Activities Report and Appendix 5B March 2018 HIGHLIGHTS: The company was pleased to announce during the Quarter, strong progress made in a num- ber of important areas towards the successful development of its 75% owned Ngualla Rare Developing the Ngualla Earth Project including: Project into an – ethically sustainable • Oversubscribed Placement of A$6.3M announced post Quarter end – long term – high quality supplier • Recruitment of highly experienced investment banker, Peter Meurer, as of choice to the global Non-Executive Chairman high technology rare earth market • In April 2018, the Tanzanian government announced the appointments to the Mining Commission, paving the way for Peak's SML to be granted • Peak continues to proactively engage with key Tanzanian Ministers and DIRECTORS officials: Non-Executive Chairman: • Positive meeting with the Tanzanian Minister of Constitutional Peter Meurer and Legal Affairs Non-Executive Directors: John Jetter • Visit to Songwe by Deputy Minister for Minerals, Hon. Doto Biteko Jonathan Murray and the MP for Songwe, Hon. Philipo Mulugo Darren Townsend Chief Executive Officer: • Meetings with the Deputy Minister for Minerals, Hon. Stanslaus Rocky Smith Nyongo and the Commissioner for Minerals, Prof. Manya Company Secretary: Graeme Scott • Teesside Planning Application and Environmental Certificate Application submitted CORPORATE Progress on the Special Mining Licence (“SML”) DETAILS Application AS AT 31 MAR 2018: On 17 April 2018, President Magafuli announced the remaining appoint- Ordinary Shares on issue: ments to the Mining Commission. This is a key development for which615.9m Peak has been awaiting and paves the way for the assessment and grant ofListed Peak’s Options SML. PEKOB $0.06 1 November 2018: The SML application was lodged with the Ministry of Minerals in -August 81.2m2017 (ASX An nouncement 6 September 2017 titled “Peak Lodges Special Mining Licence application for Ngualla”).
    [Show full text]
  • Madini News Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Toleo Na.4 Wa Tanzania Mei, 2020 HALIUZWI
    Toleo Na.4 // Mei 2020 Yaliyomo // Sekta ya Madini Inaongoza Ujenzi Kiwanda cha Kuchakata kwa Ukuaji Nchini - Biteko Dhahabu Mwanza Washika Tume ya ... Na.04 kasi ... Na.05 Madini Profesa Msanjila Atoa Pongezi Udhibiti Utoroshaji Madini Nchini Ofisi ya Madini Singida Waimarika – Prof. Manya www.tumemadini.go.tz ... Na.06 ... Na.07 Tume ya Madini 2020 MABADILIKO YA JARIDA Tume ya Madini Tunapenda kuwajulisha wasomaji wetu kuwa Jarida hili litaanza kutoka kila baada ya miezi mitatu ambapo toleo linalofuatia litatoka mwezi Septemba, 2020. www.tumemadini.go.tz /TAHARIRI Salamu Kutoka kwa Waziri wa Madini Maoni ya Mhariri PONGEZI KWA WATUMISHI WA Tunajivunia Mafanikio WIZARA YA MADINI, MCHANGO Makubwa Sekta ya Madini WENU UMEONESHA TIJA KWENYE SEKTA Aprili 21, 2020 niliwasilisha Bungeni Hotuba yangu ya Bajeti kuhusu Ili kuhakikisha kuwa Sekta ya Madini inakuwa na mchango mkubwa kwenye ukuaji wa Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 uchumi wa nchi, Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli ilifanya Mabadiliko ya Sheria ya Madini ya Mwaka 2017 yaliyopelekea ambapo pia nilieleza utekelezaji wa Vipaumbele tulivyojiwekea kama uundwaji wa Tume ya Madini na kuondoa Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania Wizara kwa Mwaka 2019/2020. Ni dhahiri kuwa utekelezaji wa vipaum- (TMAA). bele vya Mwaka 2019/2020 vimekuwa tija katika maendeleo na ukuaji wa Sekta ya Madini pamoja na kuchangia na kukuza uchumi wa nchi yetu, Tangu kuanzishwa kwa Tume ya Madini, tumeshuhudia mabadiliko makubwa kwenye hilo halina shaka. Sekta ya Madini yaliyotokana na mafanikio kwenye usimamizi wa Sekta ya Madini huku wazawa wakinufaika na rasilimali za madini zilizopo nchini.
    [Show full text]
  • MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao Cha Arobaini Na Moja
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Moja – Tarehe 31 Mei, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Tunaanza kikao chetu cha Arobaini na Moja, Katibu. NDG. LINA KITOSI – KATIBU MEZANI:- HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2018/19. MHE. CATHERINE V. MAGIGE (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu utekelezaji wa Bajeti na Majukumu ya Wizara 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019. MWENYEKITI: Ahsante. Katibu. NDG. LINA KITOSI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Swali letu la kwanza linaelekezwa Ofisi ya Waziri Mkuu na linaulizwa na Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, kwa niaba yake Mheshimiwa Amina Mollel. Na. 341 Utekelezaji wa Mpango wa Ukimwi 90-90-90 MHE. AMINA S. MOLLEL (K.n.y MHE. HAWA M. CHAKOMA) aliuliza:- Je, Serikali inatekelezaje Mpango wa UKIMWI wa 90- 90-90? MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Mollel. Majibu, Mheshimiwa Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA NA VIJANA) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa
    [Show full text]
  • Tarehe 7 Februari, 2017
    NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA SITA Kikao cha Saba – Tarehe 7 Februari, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Tukae. Katibu. NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na: MHE. PROF. NORMAN A. S. KING – MWENYEKITI WA KAMATI YA BUNGE YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kwa kipindi cha kuanzia Januari, 2016 hadi Januari, 2017. MHE. DOTO M. BITEKO -MWENYEKITI WA KAMATI YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa kipindi cha kuanzia Januari 2016 hadi Januari 2017. NAIBU SPIKA: Ahsante. Katibu! NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na maswali, Ofisi ya Rais - TAMISEMI. Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, Mbunge wa Viti Maalum, sasa aulize swali lake. Na. 69 Tatizo la Ulevi MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza:- 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Ulevi wa kupita kiasi hasa wa pombe za kienyeji umekuwa na athari kubwa za kiafya na kiakili kwa Watanzania wenye tabia ya ulevi wa kukithiri:- Je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na tatizo hilo hasa ikizingatiwa kuwa Sheria ya Vileo ya mwaka 1969 ni ya zamani sana kiasi kwamba inawezekana kabisa haikidhi mabadiliko ya hali halisi ya vileo kwa wakati huu. NAIBUWAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, pombe za kienyeji zimeainishwa katika Kifungu cha pili (2) cha tafsiri katika Sheria ya Vileo, Sura ya 77.
    [Show full text]
  • MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA TATU Kikao Cha
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Arobaini na Tatu – Tarehe 3 Juni, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba tukae. Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na Mkutano wetu wa Tatu, leo ni Kikao cha Arobaini na Tatu. Katibu NDG. NENELWA MWIHAMBI, ndc – KATIBU WA BUNGE: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, aah sasa hivi unavaa sketi ndefu, hataki ugomvi na Mgogo. (Kicheko) Tunaendelea, Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. NENELWA MWIHAMBI, ndc – KATIBU WA BUNGE: MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Maswali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Waziri Mkuu karibu sana. (Makofi) Waheshimiwa Wabunge, nawakumbusha tena kuhusu maswali ya kisera sio matukio, sio nini, ni ya kisera. Tunaanza na Mheshimiwa Mbunge wa Liwale, Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka, maswali kwa kifupi. MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kwanza kuuliza swali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu. Mheshimiwa Spika, swali langu litahusu sekta ya korosho. Mwaka huu tumepata taarifa kwamba Serikali ilijipanga kutupatia pembejeo wakulima wa zao la korosho kwa maana kwamba waje kuzilipa baadaye kwenye mjengeko wa bei. Hata hivyo, kuna taharuki kubwa kwa wakulima wetu wa korosho baada ya Bodi ya Korosho kuleta waraka kwenye Halmashauri zetu, wakiwaambia kila mkulima akipeleka zao lile kwenye mnada kila kilo moja itakatwa shilingi 110 bila kujali kwamba mkulima yule amechukua pembejeo kwa kiwango gani.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Kumi na Tatu – Tarehe 21 Aprili, 2020 (Bunge Lilianza Saa Nane Mchana) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua NDG. RAMADHANI ISSA ABDALLAH - KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA MADINI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2020/2021. MHE. DUNSTAN L. KITANDULA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI: Maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2019/2020 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2020/2021. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. JOHN W. HECHE - MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI WA WIZARA YA MADINI: Maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2020/2021 MASWALI NA MAJIBU (Maswali yafuatayo yameulizwa na kujibiwa kwa njia ya mtandao) Na. 113 Ahadi ya Ujenzi wa Barabara za Lami-Arumeru MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Rais wa Awamu ya Nne aliahidi kujenga barabara ya Sangis Toangam Kwenda Aken, Kimundo hadi Ubungo Kwa Kiwango cha lami. Vilevile Rais Dkt. John Magufuli wakati wa kampeni aliahidi ujenzi wa barabara ya kilometa 5 kwa kiwango cha lami:- Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi hizo zilizotolewa kwa wananchi wa Arumeru Mashariki? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt.
    [Show full text]
  • 1 Bunge La Tanzania
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI Kikao cha Tano – Tarehe 5 Februari, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae, Katibu. NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: KIAPO CHA UAMINIFU Mhe. Dkt. Adelardus Lubango Kilangi NAIBU SPIKA: Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- MHE. MOSHI S. KAKOSO - K.n.y MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA - K.n.y MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu shughuli za kamati kwa mwaka 2017. NAIBU SPIKA: Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU Na. 55 Changamoto Zinazowakabili Walemavu MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:- Watanzania wenye ulemavu wanakabiliwa na kero mbalimbali za kimaisha ikiwemo ukosefu wa ajira kama ilivyo kwa Watanzania wengine, aidha, zipo changamoto za jumla kama vile kijana mwenye ulemavu wa ngozi asiye na ajira ana changamoto ya mahitaji ya kujikimu na pia ana changamoto za kipekee za mahitaji ya kiafya na kiusalama. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu umuhimu wa kuwatazama vijana wenye ulemavu mbalimbali kwa namna ya pekee na kama zipo sera na mikakati ya kiujumla kwa vijana wote nchini? NAIBU SPIKA: Ofisi ya Waziri Mkuu sijui nani anayejibu maswali. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, niko hapa.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Sitini na Moja – Tarehe 29 Juni, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Najma Murtaza Giga) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Tunaanza Kikao chetu cha Sitini na Moja, Katibu. NDG. NENELWA WANKANGA – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU): Taarifa ya Mwaka ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (Workers Compensation Fund) kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2016. Taarifa ya Mwaka ya Utekelezaji wa Shughuli za Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2016. MWENYEKITI: Ahsante sana, Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. NENELWA WANKANGA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tunaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, swali la Mheshimiwa Mulugo, Mbunge wa Songwe. Na. 510 Hospitali ya Kanisa Katoliki – Mbeya (Songwe) MHE. PHILIPO A. MULUGO aliuliza:- Je, Serikali haioni haja ya kuipandisha hadhi Hospitali Teule ambayo inamilikiwa na Kanisa Katoliki Dayosisi ya Mbeya iwe Hospitali Teule ya Wilaya ili wananchi wa Songwe waweze kupata huduma stahili? MWENYEKITI: Mheshimiwa Naibu Waziri, majibu ya swali hilo. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH S. KANDEGE) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Philipo Augustino Mulugo, Mbunge wa Songwe kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, mnamo tarehe 2 Januari, 2018, Halmashauri ya Wilaya ya Songwe ilisaini mkataba na Kanisa Katoliki, Jimbo la Mbeya uliopandisha hadhi ya Hospitali ya Mwambani kuwa Hospitali Teule ya Wilaya ya Songwe.
    [Show full text]