MKUTANO WA TATU Kikao Cha Kumi Na Saba
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ______ MKUTANO WA TATU Kikao cha Kumi na Saba - Tarehe 11 Mei, 2016 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Mussa A. Zungu) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu! NDG. JOSHUA CHAMWELA - KATIBU MEZANI: Hati za kuwasilisha mezani. HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto kwa mwaka wa fedha 2016/2017. MHE. PETER J. SERUKAMBA - MWENYEKITI WA KAMATI YA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa mwaka wa fedha 2015/2016, pamoja na Maoni ya Kamati, kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya mwaka fedha 2016/2017. 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) MHE. GRACE V. TENDEGA – K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KWA WIZARA YA AFYA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2016/2017. MWENYEKITI: Ahsante, Katibu. NDG. JOSHUA CHAMWELA- KATIBU MEZANI: Maswali. MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, swali letu la kwanza linaenda Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Tebweta Omary. Na.140 Asilimia Tano ya Fedha kwa Ajili ya Vijana na Kina Mama kwa kila Halmashauri MHE.
[Show full text]