MKUTANO WA NANE Kikao Cha Thelathini Na

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

MKUTANO WA NANE Kikao Cha Thelathini Na Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE __________________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Nane – Tarehe 1 Agosti, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, katika Mkutano wake wa Saba Bunge lilipitishwa Miswada minne ya Sheria iitwayo: The Business Laws, (Miscellaneous Amendments) Bill, 2012. Halafu wa pili, The Tanzania Livestock Research Institute Bill, 2012, wa Tatu, The Social Security Laws (Amendemnts) Bill, 2012, wa nne The written Laws (Miscellaneous Amendments) (No.2) Bill, 2012. Kwa taarifa hii napenda kuliarifu Bunge hili Tukufu kwamba, Miswada hiyo imekwishapata kibali cha Mheshimiwa Rais na kuwa Sheria za nchi zinazoitwa:- The Business Laws (Miscellaneous Amendments) Act, 2012, (No.3 of 2012); The Tanzania Livestock Research Institute Act, 2012, (No. 4 of 2012); The Social Security Laws (Amendemnt) Act, 2012 (No.5 of 2012), na wa nne The written Laws (Miscellaneous Amendments) (No.2) Act, 2012 (No. 6 of 2012). Waheshimiwa Wabunge, hii ndiyo Miswada tuliyokuwa tumeipitisha na Mheshimiwa Rais ameweka mkono wake. Kwa hiyo, ni sheria za nchi. Tunaendelea, Katibu tuendelee. HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI:- Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. MHE. PETER J. SERUKAMBA - MWENYEKITI WA KAMATI YA MIUNDOMBINU:- Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Uchukuzi kwa Mwaka 2011/2012 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha, 2012/2013. MHE. PAULINE P. GEKUL (K.n.y. MHE. SAID A. ARFI - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA UCHUKUZI):- Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani juu ya Wizara ya Uchukuzi Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. MASWALI NA MAJIBU Na. 300 Ujenzi wa Zahanati na Upatikanaji wa Watumishi MHE. PETER J. SERUKAMBA (K.n.y. MHE. DKT. HENRY D. SHEKIFU) aliuliza:- Mpango wa MAMM hususani ujenzi wa zanahati kila kijiji umeitikiwa vizuri na wananchi na kasi ni kubwa kuliko uwezo wa Serikali wa kupeleka watumishi na madawa:- (a) Je, Serikali inachukua hatua gani kurekebisha hali hiyo ili wananchi wasikate tamaa kujenga zahanati? (b) Je, ni lini Zahanati za Kwai na Milingano zilizopo Wilaya ya Lushoto na nyingine ambazo zipo tayari zitafunguliwa na kupelekewa watumishi? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Henry Daffa Shekifu, Mbunge wa Lushoto, kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, nia ya Serikali ya kujenga Zahanati kila kijiji ni kusogeza huduma za afya karibu na wananchi ambapo lengo ni kumfanya mgonjwa asitembee umbali zaidi ya kilometa 5 kufuata huduma hiyo kutoka pale alipo. Serikali inachukua jitihada mbalimbali ili kuhakikisha kwamba zahanati zinazojengwa zinapata watumishi wa kutosha. Mkakati mojawapo wa Serikali ni kuongeza udadhili wa wanafunzi wanaojiunga na vyuo katika fani za afya, kuwapanga madaktari wanaohitimu moja kwa moja katika vituo vya kazi na kuwatengenezea mazingira mazuri ya kufanyia kazi. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2011/2012, Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto iliomba kibali cha kupata watumishi 45 wa kada za Afya ili kukidhi mahitaji ya zahanati zilizopo. Kati ya hao, watumishi ambao wamesharipoti ni 31 na watumishi 14 hawajaripoti. Watumishi hao watapangwa katika zahanati na vituo vya vya vilivyomo katika Halmashauri hiyo ili kuondoa upungufu uliopo. (b) Mheshimiwa Spika, zahanati ya Mlingano na Kwai kwa sasa zimeshaanza kutoa huduma za afya. Zahanati ya Mlingano kwa sasa ina watumishi 3 wanaoendeleza wakati zahanati ya Kwai inayomilikiwa na Shirika la Dini ina watumishi wapatao 11 ambao wanatoa huduma za afya kituoni hapo. Mheshimiwa Spika, Serikalil itaendelea na utaratibu wa kuwapanga watumishi wa kada za afya moja kwa moja katika vituo vya kazi kadri wanavyohitimu au kufuzu mafunzo yao kila mwaka ili kuondokana na upungufu uliopo. MHE. DKT. HENRY D. SHEKIFU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri. Nina maswali mawili madogo ya nyongeza. (a) Kwa kuwa tatizo hili la watumishi katika Idara ya Afya ni kubwa; na kwa kuwa Serikali imetangaza utaratibu wa kuanzisha hospitali za kata na kasi ya kuanzisha hospitali za vijiji imekuwa kubwa kuliko uwezekano wa kupata watumishi? Je, tuwambieni nini wananchi ambao wametoa nguvu zao zahanati zipo tayari, lakini hakuna watumishi? (b) Kwa kuwa, Wilaya ya Lushoto ni kati ya Wilaya ambazo zina watu wengi sana na idadi ya kupata watumishi imekuwa ni ndogo sana. Je, Serikali inatamka nini katika kuzipa umuhimu wa kwanza zile Wilaya ambazo kwa kweli zina watu wengi na kuna tatizo kubwa la watumishi? NAIBU WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII: Mheshimiwa Spika, kwa kipindi kirefu tulikuwa na upungufu wa watumishi kwa asilimia kama 65 hivi kwenye mwaka 2005/2006. Lakini kwenye kipindi hicho hicho tumekuwa na ongezeko la Vituo vya Afya na kusudio zima tu la kuweza kufanya kila vituo vya afya viwepo na zahanati ziwepo katika maeneo yetu. Mheshimiwa Spika, sasa tumekuwa na changamoto ya kuziba mapengo ya vituo vipya ambavyo vimekuwa vikijengwa toka mwaka 2006/2007 mpaka sasa ambavyo vinazidi vituo 1,055, sasa hii ni nyongeza ya mapungufu ambayo tulikuwa nayo mwaka 2005/2006. Hivi sasa tuna upungufu wa karibu asilimia 50. Kwa tafsiri hiyo maana yake ni kwamba kumekuwa na juhudi ziada za kuongeza vyuo, kuongeza wanaodahiliwa na pia kuongeza ajira katika vituo vyetu. Lakini juhudi hizi hazikwenda sambamba na ongezeko la vituo vya Afya na Vituo vyetu vya Tiba ambavyo vinaongezeka kwa pamoja. Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, juhudi zifanyike kama ilivyokuwa kwenye kipindi cha mwaka jana ambayo inaishia mwaka huu 2011/2012 tulipata ajira nafasi za kuajiri watu 9000 na ambao wameajiri mpaka sasa ni 7000. Kwa hiyo, katika tafsiri hii maana yake juhudi zipo zinafanyika na nimwombe Mheshimiwa Mbunge ashirikiane na Halmashauri kuonyesha mahitaji yake ili angalau kwenye kipindi cha mwaka huu tuweze kuziziba nafasi hizo ambazo zipo wazi. MHE. MOSES J. MACHALI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kuniona. Fedha za MMAM ni fedha za Serikali ambazo zimekuwa zikisaidia kuweza kuimarisha miundombinu na hasa ya Afya vijijini katika nchi nzima. Kwa kuwa katika baadhi ya Halmashauri fedha hizi zimeonekana kuweza kutumika vibaya kama taarifa za CAG ambapo zimekuwa zikibainisha na Wilaya ya Kasulu ni mojawapo ya maeneo ambayo fedha hizi zimeonekana kuweza kutumika vibaya; na kwa kuwa, nimeandika barua pengine kuweza kuiomba Serikali iweze kuchukua hatua hadi leo sijaona ni kitu gani ambacho kimefanyika. Mheshimiwa Naibu Waziri ninaamini kwamba kufanya ziara katika Wilaya ya Kasulu tunaweza tukatatua tatizo hili kwa kiasi kikubwa. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri upo tayari TAMISEMI, Mheshimiwa Aggrey Mwanri hufanye ziara katika Wilaya ya Kasulu na uweze kuona ni mambo gani mengine mabaya ambayo yamekuwa yakifanyika ili kuweza kuleta tija katika matumizi ya fedha za umma? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Spika, kwanza, nikiri kwamba Mheshimiwa Mbunge amekuwa anaeleza haya matatizo, yapo matatizo mengi hayasemi hapa ambayo amekuwa ananieleza na ameonyesha hiyo. Juzi tumekwenda Kigoma pale tulizungumzia kuhusu matatizo ambayo yanajitokeza katika zahanati na katika hospitali zetu, na msimamo ambao umetolewa jana hapa Mheshimiwa Waziri alipokuwa anahitimisha hoja yale ndiyo msimamo ambao tunakwenda nao. Lakini hili la kwenda Kigoma ni wajibu wetu kufanya hivyo. Mheshimiwa Mbunge, nitakuwa tayari kufanya hivyo muda muafaka utakapofika kwa sababu tunayo ratiba kubwa ya kuzunguka nchi nzima, lakini tuta-consider hilo. Na. 301 Ruzuku kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari MHE. JOHN J. MNYIKA aliuliza:- Serikali hutoa ruzuku (Capitation Grants) kwa wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari za Umma zikiwemo za Jimbo la Ubungo, japo utekelezaji wa sera hii unasuasua sana kwa kiwango kilichowekwa kutokana na mahitaji halisi ya wanafunzi. Viwango vinavyotengwa katika Bajeti ni chini ya vinavyotajwa kwenye Sera na fedha hazitolewi zote isipokuwa hutolewa kidogo kidogo na hazifiki kikamilifu mashuleni:- (a) Je, Serikali itahakikishiaje kuwa ruzuku iliyopangwa inafika kwa kiwango cha kutosha na kwa wakati? (b) Je, kwa nini Serikali isiwe na utaratibu wa kutangaza viwango vya ruzuku vilivyotengwa kwa kila mwanafunzi na kuhakikisha shule zinaweka wazi matumizi ya fedha hizo kwa wadau wote? (c) Je, Serikali itapitia lini viwango vya ruzuku vilivyowekwa katika Sera ili kuendana na mahitaji halisi? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa John John Mnyika, Mbunge wa Ubungo lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, kila mwaka Serikali hutenga fedha za ruzuku ya uendeshaji kwa shule na shule za msingi na sekondari. Ruzuku hii hutolewa kila baada ya miezi mitatu (kila robo mwaka) kutegemeana na makusanyo ya Serikali kwa kipindi hicho. Pamoja na kuwepo changamoto katika kukusanya mapato ya ndani na nje, Serikali itaendelea kutoa kipaumbele katika kuhakikisha fedha zinapelekwa kadri zinavyopatikana katika kila Halmashauri kwa ajili ya ruzuku ya uendeshaji wa shule zetu. (b) Mheshimiwa
Recommended publications
  • 9Aprili,2013
    9 APRILI, 2013 BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kwanza - Tarehe 9 Aprili, 2013 WIMBO WA TAIFA (Hapa Waheshimiwa Wabunge Waliimba Wimbo wa Taifa) (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa msimame tena. Mtakumbuka kwamba wakati wa Vikao vyetu vya Kamati, kwa bahati mbaya sana tulimpoteza mpenzi wetu Mheshimiwa Salim Hemed Khamis. Kwa hiyo, tumkumbuke kwa dakika moja. (Hapa Waheshimiwa Wabunge walisimama kwa Dakika moja kumkumbuka Mheshimiwa Salim Hemed Khamis aliyekuwa Mbunge wa Chambani Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Amin. Ahsanteni sana na karibuni tukae. 1 9 APRILI, 2013 Waheshimiwa Wanbunge, katika Mkutano wa Tisa, Bunge lilipitisha Muswada wa Sheria ya Serikali uitwao The Plant Breeders` Rights Bill, 2012, kwa taarifa hii napenda kulialifu Bunge hili Tukufu kwamba, Mswada huo umekwisha pata kibali cha Mheshimiwa Rais na kuwa Sheria ya nchi iitwayo: The Plant Breeders` Rights Act, 2012 Na. 9 ya mwaka 2012. Kwa hiyo, ule sasa ni sheria ya Nchi. HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kuwasilisha mezani Taarifa ya Matoleo yote ya Gazeti la Serikali pamoja na nyongeza zake zilizochapishwa tangu Kikao cha mwisho cha Mkutano wa Bunge uliopita. Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. MASWALI NA MAJIBU Na. 1 Kujenga Barabara ya Old Moshi kwa Lami MHE. GODFREY W. ZAMBI (K.n.y. MHE. DKT. CYRIL A. CHAMI) aliuliza:- Je, Serikali itatekeleza lini ahadi ya kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Old Moshi inayoanzia Kiboriloni kupitia Kikarara, Tsuduni hadi Kidia? 2 9 APRILI, 2013 NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt.
    [Show full text]
  • 1458125471-Hs-6-8-20
    [Show full text]
  • Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania
    JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA KUMI (DAILY SUMMARY RECORD OF PROCEEDINGS) 17 NOVEMBA, 2014 MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI SABA KIKAO CHA KUMI - 17 NOVEMBA, 2014 I. DUA Saa 3.00 Asubuhi Mhe. Naibu Spika alisoma Dua na kuliongoza Bunge Makatibu Mezani :- 1. Ndg. Charles Mloka 2. Ndg. Neema Msangi 3. Ndg. Joshua Chamwela II. MASWALI: Maswali yafuatayo yaliulizwa na wabunge:- 1. OFISI YA WAZIRI MKUU Swali Na. 114. Mhe. Prof. Peter Mahamudu Msolla Nyongeza ;- i. Mhe. Peter Mahamudu Msolla ii. Mhe. Ally Keissy Mohammad 2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MAZINGIRA) Swali Na. 115 – All Khamis Seif, Mb Nyongeza ;- i. Mhe. Ally Khamis Seif, Mb ii. Mhe. James Francis Mbatia, Mb 3. WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI Swali Na. 116. Mhe. Dkt. Mary Machuche Mwanjelwa, Mb Nyongeza:- i. Mhe. Dkt. Mary Machuche Mwanjelwa, Mb ii. Mhe. Selemani Said Jafo, Mb iii.Mhe. Aliko Nikusuma Kibona, Mb 4. WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII Swali Na. 117 – Mhe Joseph Roman Selasini, Mb Nyongeza:- i. Mhe Joseph Roman Selasini, Mb 2 ii. Mhe. Moses Machali 5. WIZARA YA MAJI Swali Na. 118. – Mhe. Michael Lekule Laizer [KNY: Dkt. Augustine Lyatonga Mrema]. Nyongeza;- i. Mhe. Michael Lekule Laizer ii. Mhe. James Francis Mbatia, Mb 6. WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO Swali Na. 119 – Mhe. Christowaja Gerson Mtinda Nyongeza:- i. Mhe. Christowaja Gerson Mtinda ii. Mhe. Martha Moses Mlata, Mb iii. Mhe. Grace Sindato Kiwelu, Mb 7. WIZARA YA KILIMO CHAKULA USHIRIKA Swali Na.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao Cha Arobaini Na Moja – Tareh
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Arobaini na Moja – Tarehe 9 Juni, 2020 (Bunge lilianza Saa Nane Kamili Mchana) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Naomba tukae. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI - KATIBU WA BUNGE: AZIMIO LA BUNGE Azimio la Bunge la kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, kwa namna alivyoongoza Taifa katika mapambano dhidi ya Janga la Ugonjwa wa Corona (Covid – 19). MASWALI NA MAJIBU (Maswali yafuatayo yameulizwa na kujibiwa kwa njia ya mtandao) Na. 386 Upungufu wa Vituo wa Afya Tabora MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Jimbo la Tabora mjini lina Kata 29 lakini - lina kituo cha kimoja tu cha afya. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuongeza Vituo vya Afya katika Manispaa ya Tabora? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini, kama ifuatavyo; Mheshimiwa Spika, halmashauri ina jumla ya vituo vya kutolea huduma za afya vya Serikali, vikijumuisha Hospitali mbili, Kituo cha Afya kimoja na Zahanati 22. Katika mwaka wa fedha 2020/21 Serikali imetenga shilingi milioni 100 kwa ajili ya kukamilisha maboma ya Zahanati ya Ituru na Igombe. Vilevile Serikali imetenga shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Manispaa ya Tabora. Serikali itaendelea kujenga, kuratabati na kupanua vituo vya kutolea huduma za afya Manispaa ya Tabora kwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Na.
    [Show full text]
  • Online Document)
    NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Sita – Tarehe 4 Februari, 2020 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Najma Murtaza Giga) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa tukae. Katibu tunaendelea Waheshimiwa Wabunge na Mkutano wetu wa Kumi na Nane, kikao cha leo ni kikao cha tano, Katibu NDG. RAMADHANI ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati Zifuatazi Ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Taarifa ya Matoleo ya Gazeti la Serikali pamoja na Nyongeza zake yaliyochapishwa tangu Mkutano wa Bunge uliopita kama ifuatavyo:- (i) Toleo Namba 46 la tarehe 8 Novemba, 2019 (ii) Toleo Namba 47 la tarehe 15 Novemba, 2019 (iii) Toleo Namba 48 la tarehe 22 Novemba, 2019 (iv) Toleo Namba 49 la tarehe 29 Novemba, 2019 (v) Toleo Namba 51 la tarehe 13 Desemba, 2019 (vi) Toleo Namba 52 la tarehe 20 Desemba, 2019 (vii) Toleo Namba 53 la tarehe 27 Desemba, 2019 (viii) Toleo Namba 1 la tarehe 3 Januari, 2020 (ix) Toleo Namba 2 la terehe 10 Januari, 2020 (x) Toleo Namba 3 la tarehe 17 Januari, 2020 (xi) Toleo Namba 4 la terehe 24 Januari, 2020 MHE. JASSON S. RWEIKIZA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za MItaa kuhuus shughuli za Kamati hii kwa Mwaka 2019. MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE KATIBA NA SHERIA: Taarifa ya Kmaati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu shughuli zilizotekelezwa na Kamati hiyo kwa kipindi cha kuanzia Februari, 2019 hadi Januari, 2020.
    [Show full text]
  • 10 JUNI, 2013 MREMA 1.Pmd
    10 JUNI, 2013 BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Sita - Tarehe 10 Juni, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 367 Mafunzo ya Wajasiriamali Wanawake – Mbeya MHE. GODFREY W. ZAMBI (K.n.y. MHE. CYNTHIA H. NGOYE) aliuliza:- Wanawake wa Mkoa wa Mbeya wameitikia wito wa kuanzishwa kwa vikundi vya uzalishaji mali ikiwemo uanzishwaji wa vyombo vya akiba na mikopo:- (a) Je, ni lini Serikali itawapatia mafunzo ya ujasiriamali Wanawake wa Mkoa Mbeya? (b) Je, Serikali iko tayari kuhamasisha benki mbalimbali kusogeza huduma karibu na wananchi ili kukidhi azma yao ya kupatiwa mikopo na kujiwekea akiba? 1 10 JUNI, 2013 WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Cynthia Hilda Ngoye, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) ilifanya utafiti katika mkoa wa Mbeya na kubaini kuwa wananchi wengi wakiwemo wanawake wameanzisha vikundi vya uzalishaji mali ikiwemo uanzishwaji wa vikundi na mikopo. Kutokana na juhudi hizo, Baraza kwa kutumia Mfuko wa Uwezeshaji Mwananchi Kiuchumi yaani “Mwananchi Empowerment Fund” imeanza kutoa udhamini wa mikopo kwa wananchi wa Mbeya hususan Chimala SACCOS. Aidha, utaratibu na mpango wa kutoa mafunzo umeandaliwa na mafunzo yatatolewa mwanzoni mwa mwaka wa fedha 2013/2014. Mafunzo hayo yatawahusisha pia wanaume kwa vile SACCOS ya Chimala ina wanachama ambao ni wanaume.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA PILI Kikao Cha Tisa
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA PILI Kikao cha Tisa - Tarehe 17 Februari, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Taarifa ya mwaka ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali za Mitaa kwa mwaka wa fedha unaoishia tarehe 30 Juni, 2004. Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. MASWALI NA MAJIBU Na. 94 Uwekaji wa Lami Barabara ya Kigogo - Mabibo - Mandela - Tabata MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka lami kwenye barabara ya Kigogo- Mabibo hadi barabara ya Mandela kuelekea Tabata ili kupunguza msongamano wa magari katika barabara ya Morogoro? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima Mdee, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- 1 Mheshimiwa Spika, barabara ya Kigogo - Mabibo- Mandela kuelekea Tabata ni barabara ya mjini yaani urban road na inahudumiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Barabara hii ni muungano wa barabara tatu ambazo ni Kigogo - Mabibo, Mabibo - Mandela na Mandela - Tabata. Barabara hii imekuwa ikifanyiwa matengenezo ya mara kwa mara na Manispaa ya Kinondoni. Kwa mwaka 2005/2006 jumla ya shilingi 9,836,000 zilitumika kuweka kifusi kwenye sehemu korofi na kuichonga kwa greda. Mheshimiwa Spika, barabara hii inapitika isipokuwa katika mpaka wa Manispaa za Kinondoni na Ilala eneo la Tabata ambapo pana mkondo wa maji na hakuna daraja.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA SABA Kikao Cha Ishirini Na Tano – Tarehe 15
    NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 15 Mei, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Mussa A. Zungu) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu! NDG. CHARLES MLOKA – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. MWENYEKITI: Ahsante. Katibu. NDG. CHARLES MLOKA – KATIBU MEZANI: Maswali. 1 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MASWALI NA MAJIBU Na. 200 Mgongano wa Kiutendaji – Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Wananchi wa Songea Mjini wamekuwa wakiitumia Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma kama Hospitali yao ya Wilaya hivyo kufanya kuwepo na mgongano wa kiutendaji kati ya Mamlaka ya Mkoa inayoitambua Hospitali hiyo kama Rufaa ya ngazi ya Mkoa na Mamlaka ya Wilaya. Tarehe 10 Januari, 2016, Mheshimiwa Waziri wa Afya alifika kuona hali halisi na juhudi za wananchi wa Songea Mjini za kujenga Kituo cha Afya Mji Mwema ambacho kimefikia hatua kubwa, hivyo wakamwomba Waziri kituo hicho kipandishwe hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya, Songea Mjini. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuiacha Hospitali ya Mkoa ifanye kazi ya Rufaa Kimkoa? (b) Je, Serikali haioni haja ya kupunguza msongamano katika hospitali hiyo kwa kuanzisha Hospitali ya Wilaya Songea Mjini? (c) Je, ni lini basi Serikali
    [Show full text]
  • Tanzania Human Rights Report 2008
    Legal and Human Rights Centre Tanzania Human Rights Report 2008: Progress through Human Rights Funded By; Embassy of Finland Embassy of Norway Embassy of Sweden Ford Foundation Oxfam-Novib Trocaire Foundation for Civil Society i Tanzania Human Rights Report 2008 Editorial Board Francis Kiwanga (Adv.) Helen Kijo-Bisimba Prof. Chris Maina Peter Richard Shilamba Harold Sungusia Rodrick Maro Felista Mauya Researchers Godfrey Mpandikizi Stephen Axwesso Laetitia Petro Writers Clarence Kipobota Sarah Louw Publisher Legal and Human Rights Centre LHRC, April 2009 ISBN: 978-9987-432-74-5 ii Acknowledgements We would like to recognize the immense contribution of several individuals, institutions, governmental departments, and non-governmental organisations. The information they provided to us was invaluable to the preparation of this report. We are also grateful for the great work done by LHRC employees Laetitia Petro, Richard Shilamba, Godfrey Mpandikizi, Stephen Axwesso, Mashauri Jeremiah, Ally Mwashongo, Abuu Adballah and Charles Luther who facilitated the distribution, collection and analysis of information gathered from different areas of Tanzania. Our 131 field human rights monitors and paralegals also played an important role in preparing this report by providing us with current information about the human rights’ situation at the grass roots’ level. We greatly appreciate the assistance we received from the members of the editorial board, who are: Helen Kijo-Bisimba, Francis Kiwanga, Rodrick Maro, Felista Mauya, Professor Chris Maina Peter, and Harold Sungusia for their invaluable input on the content and form of this report. Their contributions helped us to create a better report. We would like to recognize the financial support we received from various partners to prepare and publish this report.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka.
    [Show full text]
  • 16 MEI, 2013 MREMA 1.Pmd
    16 MEI, 2013 BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na Saba – Tarehe 16 Mei, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tukae. Waheshimiwa Wabunge Kikao cha Ishirini na Saba kinaanza. Mkutano wetu wa Kumi na Moja. HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI:- Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. 1 16 MEI, 2013 MHE. PROF. JUMA A. KAPUYA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA MIUNDOMBINU): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Uchukuzi kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. MHE. PAULINE P. GEKUL (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA WIZARA YA UCHUKUZI): Taaqrifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Wizara ya Uchukuzi Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. MASWALI KWA WAZIRI MKUU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge kama kawaida yetu siku ya Alhamisi tunakuwa na Kipindi cha Maswali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu na swali la kwanza la siku ya leo linaulizwa na Mheshimiwa Stephen Hilary Ngonyani. MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kunipa chakula cha msaada kule kwenye jimbo langu. Swali linalokuja ni hivi. Mheshimiwa Naibu Spika, Kitengo cha Maafa ni Kitengo ambacho kiko chini ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, nchi nzima kinajua jinsi unavyosaidia wananchi.
    [Show full text]
  • Did They Perform? Assessing fi Ve Years of Bunge 2005-2010
    Policy Brief: TZ.11/2010E Did they perform? Assessing fi ve years of Bunge 2005-2010 1. Introducti on On July 16th 2010, following the completi on of the 20th session of the Bunge, the President of Tanzania dissolved the 9th Parliament. This event marked the end of the term for Members of Parliament who were elected during the 2005 general electi ons. Now that the last session has been completed it allows us to look back and to consider how MPs performed during their tenure. Did they parti cipate acti vely and represent their consti tuencies by asking questi ons and making interventi ons, or were they silent backbenchers? The Bunge is the Supreme Legislature of Tanzania. The Bunge grants money for running the administrati on and oversees government programs and plans. The Bunge oversees the acti ons of the Executi ve and serves as watchdog to ensure that government is accountable to its citi zens. To achieve all this, Members of Parliament pass laws, authorize taxati on and scruti nize government policies including proposal for expenditure; and debate major issues of the day. For the Bunge to eff ecti vely carry out its oversight role, acti ve parti cipati on by Members of Parliament is criti cal. MPs can be acti ve by making three kinds of interventi ons: they can ask basic questi ons, they can ask supplementary questi ons and they can make contributi ons during debates. This brief follows earlier briefs, the last of which was released in August 2010. It presents seven facts on the performance of MPs, including rati ng who were the most acti ve and least acti ve MPs.
    [Show full text]