7 Mei, 2020 1 Bunge La Tanzania

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

7 Mei, 2020 1 Bunge La Tanzania 7 MEI, 2020 BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 7 Mei, 2020 (Bunge Lilianza Saa Nane Mchana) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa naomba tukae. Katibu. NDG. RAMADHANI ABDALLAH -KATIBU MEZANI HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Hotuba ya Bajeti ya Wizara na Randama ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021. MHE. TIMOTHEO P. MNZAYA - (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ARDHI MALIASILI NA UTALII): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021. 1 7 MEI, 2020 SPIKA: Ahsante sana. Katibu ! NDG. RAMADHANI ABDALLAH -KATIBU MEZANI MASWALI NA MAJIBU (Maswali yafuatayo yameulizwa na kujibiwa kwa njia ya mtandao) Na. 222 Halmashauri Kutenga 10% kwa ajili ya Wanawake na Vijana MHE. GODFREY W. MGIMWA aliuliza:- Ilani ya Chama cha Mapinduzi inaeleza wazi juu ya kuwawezesha wananchi kiuchumi hasa kwenye suala la ujasiriamali:- Je, Serikali ipo tayari kutoa agizo la msisitizo kwa Halmashauri zote nchini kutenga fedha za asilimia 10 kwa wanawake na vijana bila kukosa kila mwaka kama inavyotakiwa? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Godfrey William Mgimwa, Mbunge wa Kalenga, kama ifuatavyo;- Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya marekebisho ya Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura 290 kwa kuongeza Kifungu cha 37A(1) – (4) kinachoelekeza Halmashauri zote kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa ajili ya vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu. Aidha, ili kuimarisha usimamizi wa Sheria, Waziri mwenye dhamana ametunga Kanuni za usimamizi wa utoaji na urejeshaji wa mikopo hiyo zilizotangazwa kwenye Tangazo 2 7 MEI, 2020 la Serikali Na. 286 la tarehe 5 Aprili, 2019. Hivyo, suala la mikopo hiyo kwa sasa linasimamiwa kwa mujibu wa sheria tofauti na awali. Na. 223 Kituo cha Afya Kata ya Ulowa – Ushetu MHE. LUCY T. MAYENGA aliuliza:- Serikali ilitenga fedha kujenga Kituo cha Afya eneo la Nyalwelwe katika Kata ya Ulowa, Wilayani Ushetu:- Je, nini sababu ya kutopelekwa fedha hizo? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lucy Thomas Mayenga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali imetumia jumla ya Shilingi bilioni 1.9 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu na Kituo cha Afya Ukene katika Halmashauri hiyo. Mpango wa Serikali ni kuendelea na ujenzi wa miundombinu ya vituo vya kutolea huduma za afya katika maeneo yaliyobaki kikiwemo Kituo cha Afya cha Ulowa kadri upatikanaji wa fedha utakavyoruhusu. Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa kawaida huwa inapokea vipaumbele vya vituo vya kupeleka fedha kutoka kwenye Halmashauri na Mikoa na sio sahihi kuwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI huwa inachagua maeneo ya kupeleka fedha. Kwa mwaka 2020/2021, tumetenga fedha kwa ajili ya kukamilisha jumla ya maboma 555 ya Zahanati na Vituo vya Afya kwenye Halmashauri 184 na Halmashauri zote tayari zimewasilisha Vituo vyao vya kipaumbele. Kwa Halmashauri ya Ushetu wao wamewasilisha maboma ya Zahanati za Bugomba A, Makongoro na Nshimba. Sina 3 7 MEI, 2020 taarifa kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI iliwahi kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya kwenye Eneo la Nyalwelwe. Na. 224 Vijana Wanaohifadhi Kasa MHE. ANGELINA A. MALEMBEKA aliuliza:- Suala la ukusanyaji mapato ni la Muungano:- (a) Je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za vijana wa Nungwi Mnarani Kaskazini Unguja ambao wanahifadhi Kasa? (b) Kwa kuwa wageni mbalimbali hutembelea eneo hilo na kulipa pesa kidogo: Je, Serikali haioni umuhimu wa kutoa ruzuku ili kuboresha shughuli hiyo na Serikali kujipatia mapato kwa kazi hiyo? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA) alijibu:- Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:- (a) Serikali inatambua juhudi na michango ya makundi mbalimbali yanayoshiriki katika kuchangia pato la Taifa ikiwemo kundi la vijana wa Nungwi Mnarani, Kaskazini Unguja ambao wanahifadhi Kasa. (b) Ofisi imepokea ushauri wa Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka na kuahidi kulifanyia kazi kwa kuliwasilisha suala hili, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais ili iweze kuangalia uwezekano wa kutoa ruzuku na kushauri kuongezwa kiingilio kwa ajili ya kuboresha shughuli ya uhifadhi na hatimaye kuimarisha mapato. 4 7 MEI, 2020 Mheshimiwa Spika, aidha, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Malembeka kuwa, moja ya vipaumbele vya Serikali zetu mbili ni kuhakikisha inashajihisha makundi yote ambayo yanajitoa katika kuchangia pato la Taifa kwa namna moja au nyingine ikiwemo kundi la vijana. Na. 225 Wajawazito Wanaoenda Kliniki bila Wenza MHE. ZAINAB M. BAKAR aliuliza:- Kumekuwa na tabia ya baadhi ya zahanati kutotoa huduma kwa akinamama wajawazito wanapoenda kuanza kliniki bila ya wenza wao:- Je, Serikali haioni kwamba tabia hii inaendeleza vifo kwa wajawazito kwa kukosa huduma hiyo? WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zainab Mussa Bakar, Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaendelea kuimarisha Huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto ikiwemo huduma kwa akinamama kabla ya ujauzito, wakati wa ujauzito na baada ya kujifungua. Aidha, Serikali imeendelea kutoa huduma kwa akinamama wakati wa ujauzito katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya, zikiwa ni pamoja na kupimwa wingi wa damu, shinikizo la damu, magonjwa mbalimbali kama Malaria, UKIMWI na Kaswende. Mheshimiwa Spika, lengo ni kutambua dalili za hatari au magonjwa wakati wa ujauzito na kuweza kuchukua hatua stahiki mapema ili kuzuia matatizo yatokanayo na 5 7 MEI, 2020 uzazi. Vilevile, Serikali inasisitiza wajawazito wote kuhudhuria kliniki mapema wakiwa na wenza wao ili kuweza kupata huduma hizi ndani ya muda muafaka. Mheshimiwa Spika, kulingana na Sera ya Afya ya mwaka 2007, huduma za afya ya uzazi hutolewa bure bila malipo na huduma hizi hutolewa muda wote katika vituo vya kutolea huduma za afya. Aidha, huduma hizi hutolewa kwa kila mjamzito bila kujali kama amekwenda na mwenza wake au hakwenda. Hata hivyo, Serikali inasisitiza kwamba ni vyema mjamzito akaambatana na mwenza wake ili wapate elimu ya afya kwa pamoja na ikibidi wapate baadhi ya vipimo kwa pamoja ili kuweza kuhakikisha afya bora ya mtoto aliyeko tumboni. Katika eneo hili la utoaji huduma kwa wanawake wakati wa ujauzito (Antenatal Care). Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imefanikiwa kuongeza kiwango cha akinamama wajawazito 1,744,668 waliohudhuria kliniki wakati wa ujauzito, ambapo wajawazito 1,343,228 walitimiza mahudhurio manne au zaidi (ANC4+) sawa na asilimia 77 ikilinganishwa na asilimia 41 kwa mwaka 2015/2016 wakati Serikali ya Awamu ya Tano ikiingia madarakani. Hii ni kutokana na huduma nzuri zinazopatikana katika vituo vya kutolea huduma za afya ambapo watoa huduma za afya wanawahudumia akinamama wajawazito bila kujali kama wameenda na wenza wao ama hawakwenda nao. Aidha, Serikali inaendelea kuwasisitiza wanaume juu ya umuhimu wa kuwasindikiza wenza wao pindi wanapohudhuria kliniki ya ujauzito. Na. 226 Mradi wa Maji wa Mabokweni Hadi Chongoleani MHE. MUSSA B. MBAROUK aliuliza:- Miongoni mwa Miradi ya Maji Vijijini ya Vijiji Kumi (10) kwa kila Halmashauri ni pamoja na Mradi wa Maji wa 6 7 MEI, 2020 Mabokweni, Kiruku, Mpirani, Bwagamoyo hadi Chongoleani; Mradi huu hautoi maji na wananchi wanaendelea kutaabika:- Je, tatizo ni nini? WAZIRI WA MAJI alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Bakari Mbarouk, Mbunge wa Tanga Mjini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Mradi wa Maji Mabokweni uliopo katika Halmashauri ya Jiji la Tanga ulisanifiwa kuhudumia vijiji/ mitaa mitano (5) ya Mleni, Kibafuta, Mpirani, Ndaoya na Chongoleani. Mradi huu ambao unagharimu kiasi cha Sh.2,412,977,490.00 utakapokamilika utawapatia huduma ya majisafi na salama wananchi wapatao 15,750. Mpaka sasa matenki mawili (water sump & storage tank) yamejengwa, ujenzi wa nyumba ya pampu na ufungaji wa pampu na umeme pamoja na ujenzi wa vituo 24 vya kuchotea maji umekamilika. Mheshimiwa Spika, hivi sasa, Serikali kupitia Wizara ya Maji imeukabidhi mradi huo kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Jiijini Tanga kwa kuzingatia Sheria ya Maji Na.5 ya mwaka 2019 kwa ajili ya kuukamilisha na hatimaye kusimamia uendeshaji ili wananchi wanufaike na mradi huo. Hadi sasa, wananchi wapatao 2,500 wa Vijiji vya Kibafuta na Kiruku wanapata huduma ya maji kufuatia kuunganisha maji katika vituo vitano vilivyopitiwa na mtandao. Mheshimiwa Spika, Mradi huu unatekelezwa kwa kutumia Wataalam wa ndani (Force Account) ili kukamilisha mradi huo kwa wakati na kwa gharama nafuu. Mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2020. 7 7 MEI, 2020 Na. 227 Mradi wa Maji wa Igongwi MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:- Mradi wa Maji wa Igongwi unaotarajiwa kuhudumia Vijiji vya Kitulila, Luponde, Njomlole Uwemba, Ikisa na Madobole umechukua muda mrefu kukamilika:- Je, nini kauli ya Serikali kuhusu mradi huu muhimu kwa wananchi? WAZIRI WA MAJI alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Edward Franz Mwalongo, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Mradi wa Maji Igongwi ni miongoni mwa miradi ya maji iliyoanza kutekelezwa katika Programu ya Sekta ya Maji kabla ya kukabidhiwa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira (RUWASA) Wilaya ya Njombe. Mradi huu unajumuisha Vijiji vya Kitulila, Luponde, Njomlole, Uwemba, Ikisa, Madobole, Luvuyo na Madope. Mradi wa Maji wa Igongwi ulipangwa kutekelezwa katika vipande vitano (Lot one hadi Lot five) na hadi sasa umefikia asilimia 63.
Recommended publications
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    NAKALA YA MTANDAO (ON LINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ BUNGE LA KUMI NA MOJA ___________ MKUTANO WA KWANZA Kikao cha Kwanza - Tarehe 17 Novemba, 2015 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) DKT. THOMAS D. KASHILILAH - KATIBU WA BUNGE: Naomba tukae. TANGAZO LA RAIS LA KUITISHA MKUTANO WA BUNGE DKT. THOMAS D. KASHILILAH - KATIBU WA BUNGE: Waheshimiwa Wabunge, kwa mujibu wa masharti ya Katiba, Mkutano huu wa Kwanza unaanza kwa Rais kuuitisha. Naomba kuchukua nafasi hii kusoma Tangazo la Rais kama ambavyo tumelipokea. Tangazo la Serikali Na. 513 la tarehe 6 Novemba, 2015. Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Sura ya Pili, hati iliyotolewa kwa mujibu wa Ibara ya 90(1). Hati ya Kuitisha Mkutano wa Bunge Jipya. KWA KUWA, Uchaguzi Mkuu ulifanyika tarehe 25 Oktoba, 2015 katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977; NA KWA KUWA, masharti ya Ibara ndogo ya kwanza ya Ibara ya 90 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, yanamtaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuitisha Mkutano wa Bunge Jipya kabla ya kupita siku saba tangu Tume ya Uchaguzi kutangaza matokeo ya Uchaguzi Mkuu; NA KWA KUWA, matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 25 Oktoba, 2015 yalitangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi tarehe 29 Oktoba, 2015; HIVYO BASI, mimi John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa mamlaka niliyonayo chini ya Ibara ya 90(1) ya 1 NAKALA YA MTANDAO (ON LINE DOCUMENT) Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, naitisha Mkutano wa Bunge Jipya la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ufanyike katika ukumbi wa Bunge uliopo Mjini Dodoma tarehe 17 Novemba, 2015 kuanzia saa tatu asubuhi.
    [Show full text]
  • 1458125471-Hs-6-8-20
    [Show full text]
  • Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA PILI Kikao cha Nane – Tarehe 4 Februari, 2016 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge tukae. Tunaendelea na Kikao chetu cha Nane katika Mkutano huu wa Pili wa Bunge la Kumi na Moja. Orodha ya Shughuli zetu za leo mnayo. Katibu! HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Muhtasari wa Tamko la Sera ya Fedha (Mapitio ya Nusu Mwaka 2015/2016 [Monetary Policy Statement (The Mid-Year Review 2015/2016)] 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) MASWALI NA MAJIBU Na. 92 Watumishi Wasio na Sifa Katika Vituo vya Afya na Zahanati Nchini MHE. RIZIKI S. MNGWALI aliuliza:- Kumekuwa na tatizo sugu nchini kwa baadhi ya vituo vya afya na zahanati kuwa na watumishi wasio na sifa za utabibu:- Je, Serikali inatumia vigezo gani kuwapeleka watumishi wasio na sifa katika zahanati na vituo vya afya? MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Naibu Waziri (TAMISEMI). Subiri kidogo Mheshimiwa Waziri. Waheshimiwa Wabunge, jana tulipewa taarifa kwamba Mheshimiwa Waziri Mkuu leo hatakuwepo Bungeni kwa sababu yupo nje ya Dodoma. Kwa mujibu wa Kanuni zetu yeye ni Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni na Serikali imo humu. Mheshimiwa Waziri Mkuu anapokuwa hayupo Dodoma, anaweza kuwa ofisini lakini yupo, anapokuwa nje ya Dodoma, Kanuni zinataka awepo Kaimu Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni. Kwa leo Mheshimiwa William Lukuvi ndiye Kaimu Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni. Tunaendelea, Naibu Waziri TAMISEMI, Mheshimiwa Jafo. (Makofi) NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), napenda kujibu swali la Mheshimiwa Riziki Shahari Mngwali, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu ambao unatumika kuajiri watumishi wa kada za afya ni kuwapanga moja kwa moja kwenye vituo vya kazi kadiri wanavyohitimu na ufaulu wa masomo yao.
    [Show full text]
  • NCT NEWSLETTER Final Design
    ISSN: 2683-6564 NATIONAL COLLEGE OF TOURISM NCTNEWSLETTER VOL 1 JULY - SEPT 2019 WELCOME NATIONAL COLLEGE OF TOURISM “A Ladder to Excellence” TABLE OF CONTENTS Greetings from NCT’s CEO 2 NCT Long Courses 4 NCT Certified Apprenticeship 5 NCT Short Courses 6 NCT Services 7 NCT Stakeholders Involvement 8 NCT Sta Engagement 9 NCT Technology 10 NCT Future Plans 11 NCT Board Members 12 GREETINGS FROM NCT’s CEO 1 The National College of Tourism (NCT) is a public institution under the Ministry of Natural Resources and Tourism with the mandate to oer training, research and consultancy services in hospitality and tourism. To enhance communication with stakeholders, NCT is delighted to introduce its quarterly newsletter, in which we shall be sharing insights and news regarding our guests and activities to improve Tourism and Hospitality through training and best practices. With more than 50 years of experience, we continue to be committed to oering high quality educa- tion and training to everyone wishing to take up a lucrative career in the Hospitality and Tourism industry. It is in this spirit that we thank you for your interest in joining the National College of Tourism and welcome you to experience Tanzania like never before. It still feels like my first month at work with all this enthusiasm, growth and creativity within me. This has been supported endlessly by the NCT staff as well as the Ministry of Natural Resourc- es and Tourism. Image We stand prepared to improve the training environment for our students, offer quality education and to provide the industry with able minded and well groomed candidates.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao Cha Arobaini Na Moja – Tareh
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Arobaini na Moja – Tarehe 9 Juni, 2020 (Bunge lilianza Saa Nane Kamili Mchana) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Naomba tukae. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI - KATIBU WA BUNGE: AZIMIO LA BUNGE Azimio la Bunge la kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, kwa namna alivyoongoza Taifa katika mapambano dhidi ya Janga la Ugonjwa wa Corona (Covid – 19). MASWALI NA MAJIBU (Maswali yafuatayo yameulizwa na kujibiwa kwa njia ya mtandao) Na. 386 Upungufu wa Vituo wa Afya Tabora MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Jimbo la Tabora mjini lina Kata 29 lakini - lina kituo cha kimoja tu cha afya. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuongeza Vituo vya Afya katika Manispaa ya Tabora? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini, kama ifuatavyo; Mheshimiwa Spika, halmashauri ina jumla ya vituo vya kutolea huduma za afya vya Serikali, vikijumuisha Hospitali mbili, Kituo cha Afya kimoja na Zahanati 22. Katika mwaka wa fedha 2020/21 Serikali imetenga shilingi milioni 100 kwa ajili ya kukamilisha maboma ya Zahanati ya Ituru na Igombe. Vilevile Serikali imetenga shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Manispaa ya Tabora. Serikali itaendelea kujenga, kuratabati na kupanua vituo vya kutolea huduma za afya Manispaa ya Tabora kwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Na.
    [Show full text]
  • Ruaha Journal of Arts and Social Sciences (RUJASS), Volume 7, Issue 1, 2021
    RUAHA J O U R N A L O F ARTS AND SOCIA L SCIENCE S (RUJASS) Faculty of Arts and Social Sciences - Ruaha Catholic University VOLUME 7, ISSUE 1, 2021 1 Ruaha Journal of Arts and Social Sciences (RUJASS), Volume 7, Issue 1, 2021 CHIEF EDITOR Prof. D. Komba - Ruaha Catholic University ASSOCIATE CHIEF EDITOR Rev. Dr Kristofa, Z. Nyoni - Ruaha Catholic University EDITORIAL ADVISORY BOARD Prof. A. Lusekelo - Dar es Salaam University College of Education Prof. E. S. Mligo - Teofilo Kisanji University, Mbeya Prof. G. Acquaviva - Turin University, Italy Prof. J. S. Madumulla - Catholic University College of Mbeya Prof. K. Simala - Masinde Murilo University of Science and Technology, Kenya Rev. Prof. P. Mgeni - Ruaha Catholic University Dr A. B. G. Msigwa - University of Dar es Salaam Dr C. Asiimwe - Makerere University, Uganda Dr D. Goodness - Dar es Salaam University College of Education Dr D. O. Ochieng - The Open University of Tanzania Dr E. H. Y. Chaula - University of Iringa Dr E. Haulle - Mkwawa University College of Education Dr E. Tibategeza - St. Augustine University of Tanzania Dr F. Hassan - University of Dodoma Dr F. Tegete - Catholic University College of Mbeya Dr F. W. Gabriel - Ruaha Catholic University Dr M. Nassoro - State University of Zanzibar Dr M. P. Mandalu - Stella Maris Mtwara University College Dr W. Migodela - Ruaha Catholic University SECRETARIAL BOARD Dr Gerephace Mwangosi - Ruaha Catholic University Mr Claudio Kisake - Ruaha Catholic University Mr Rubeni Emanuel - Ruaha Catholic University The journal is published bi-annually by the Faculty of Arts and Social Sciences, Ruaha Catholic University. ©Faculty of Arts and Social Sciences, Ruaha Catholic University.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA SABA Kikao Cha Ishirini Na Tano – Tarehe 15
    NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 15 Mei, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Mussa A. Zungu) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu! NDG. CHARLES MLOKA – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. MWENYEKITI: Ahsante. Katibu. NDG. CHARLES MLOKA – KATIBU MEZANI: Maswali. 1 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MASWALI NA MAJIBU Na. 200 Mgongano wa Kiutendaji – Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Wananchi wa Songea Mjini wamekuwa wakiitumia Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma kama Hospitali yao ya Wilaya hivyo kufanya kuwepo na mgongano wa kiutendaji kati ya Mamlaka ya Mkoa inayoitambua Hospitali hiyo kama Rufaa ya ngazi ya Mkoa na Mamlaka ya Wilaya. Tarehe 10 Januari, 2016, Mheshimiwa Waziri wa Afya alifika kuona hali halisi na juhudi za wananchi wa Songea Mjini za kujenga Kituo cha Afya Mji Mwema ambacho kimefikia hatua kubwa, hivyo wakamwomba Waziri kituo hicho kipandishwe hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya, Songea Mjini. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuiacha Hospitali ya Mkoa ifanye kazi ya Rufaa Kimkoa? (b) Je, Serikali haioni haja ya kupunguza msongamano katika hospitali hiyo kwa kuanzisha Hospitali ya Wilaya Songea Mjini? (c) Je, ni lini basi Serikali
    [Show full text]
  • Issued by the Britain-Tanzania Society No 124 Sept 2019
    Tanzanian Affairs Issued by the Britain-Tanzania Society No 124 Sept 2019 Feathers Ruffled in CCM Plastic Bag Ban TSh 33 trillion annual budget Ben Taylor: FEATHERS RUFFLED IN CCM Two former Secretary Generals of the ruling party, CCM, Abdulrahman Kinana and Yusuf Makamba, stirred up a very public argument at the highest levels of the party in July. They wrote a letter to the Elders’ Council, an advisory body within the party, warning of the dangers that “unfounded allegations” in a tabloid newspaper pose to the party’s “unity, solidarity and tranquillity.” Selection of newspaper covers from July featuring the devloping story cover photo: President Magufuli visits the fish market in Dar-es-Salaam following the plastic bag ban (see page 5) - photo State House Politics 3 This refers to the frequent allegations by publisher, Mr Cyprian Musiba, in his newspapers and on social media, that several senior figures within the party were involved in a plot to undermine the leadership of President John Magufuli. The supposed plotters named by Mr Musiba include Kinana and Makamba, as well as former Foreign Affairs Minister, Bernard Membe, various opposition leaders, government officials and civil society activists. Mr Musiba has styled himself as a “media activist” seeking to “defend the President against a plot to sabotage him.” His publications have consistently backed President Magufuli and ferociously attacked many within the party and outside, on the basis of little or no evidence. Mr Makamba and Mr Kinana, who served as CCM’s secretary generals between 2009 to 2011 and 2012-2018 respectively, called on the party’s elders to intervene.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka.
    [Show full text]
  • 16 MEI, 2013 MREMA 1.Pmd
    16 MEI, 2013 BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na Saba – Tarehe 16 Mei, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tukae. Waheshimiwa Wabunge Kikao cha Ishirini na Saba kinaanza. Mkutano wetu wa Kumi na Moja. HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI:- Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. 1 16 MEI, 2013 MHE. PROF. JUMA A. KAPUYA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA MIUNDOMBINU): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Uchukuzi kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. MHE. PAULINE P. GEKUL (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA WIZARA YA UCHUKUZI): Taaqrifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Wizara ya Uchukuzi Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. MASWALI KWA WAZIRI MKUU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge kama kawaida yetu siku ya Alhamisi tunakuwa na Kipindi cha Maswali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu na swali la kwanza la siku ya leo linaulizwa na Mheshimiwa Stephen Hilary Ngonyani. MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kunipa chakula cha msaada kule kwenye jimbo langu. Swali linalokuja ni hivi. Mheshimiwa Naibu Spika, Kitengo cha Maafa ni Kitengo ambacho kiko chini ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, nchi nzima kinajua jinsi unavyosaidia wananchi.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Nane – Tarehe 20 Juni, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 76 Mpango wa Kurasimisha Ardhi Vijijini MHE. PETER J. SERUKAMBA (K.n.y. MHE JENISTA J. MHAGAMA) aliuliza:- Mpango wa kurasimisha ardhi vijijini unakwama kwa kuwa Halmashauri nyingi zinashindwa kutenga fedha kutokana na ufinyu na ukomo wa Bajeti. Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka wa kutenga fungu la kuwezesha mkakati huo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama, Mbunge wa Peramiho, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, mpango wa kurasimisha ardhi ni azma ya Serikali kuwawezesha wananchi kiuchumi na kuondokana na umaskini. Mpango huu unalenga kupima ardhi za Vijiji na kuwapatia wananchi Hati za kumiliki za kimila (Certificate of Occupancy) ili kuzitumia kama dhamana kupata mikopo katika mabenki. Mkakati huu unatekelezwa chini ya Mpango wa Kurasimisha rasilimali na biashara za wanyonge nchini (MKURABITA). 1 Malengo mengine ya mpango huo ni kuondoa migogoro ya ardhi kwa kuweka mipaka kati ya vijijini na vijiji na kupanga matumizi bora ya ardhi kwa kutenga maeneo kwa ajili ya matumizi bora na matumizi mbalimbali kama vile wafugaji, kilimo na uwekezaji. Mheshimiwa Spika, Wizara yenye dhamana ya masuala ya ardhi hutenga fedha kwa ajili ya kujenga uwezo katika ngazi za Mamlaka za Serikali za Mitaa. Aidha, Serikali inao mfuko (Revolving Fund) unatumika kuziwezesha Halmashauri kupima ardhi na kufanya marejesho ili fedha hizo zitumike kwa ajili ya kupima ardhi katika Halmashauri nyingine.
    [Show full text]
  • Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania
    JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA KUMI NA TISA (DAILY SUMMARY RECORD OF PROCEEDINGS) 28 NOVEMBA, 2014 MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA KUMI NA TISA (SUMMARY RECORD OF PROCEEDINGS – NINETEENTH SITTING) TAREHE 28 NOVEMBA, 2014 I. DUA: Mhe. Spika Anne S. Makinda alisoma Dua saa 3.00 asubuhi na Kikao kiliendelea. MAKATIBU MEZANI: 1. Ndg. Theonest Ruhilabake 2. Ndg. Lawrence Makigi 3. Ndg. Neema Msangi II. MASWALI Maswali yafuatayo yaliulizwa na kujibiwa; 1. OFISI YA WAZIRI MKUU Swali Na. 229: Mhe. Hamoud Abuu Jumaa Nyongeza: (i) Mhe. Hamoud Abuu Jumaa (ii) Mhe. Murtaza Ally Mangungu Swali Na. 230: Mhe. Suzan A. J. Lyimo Nyongeza: (i) Mhe. Suzan A. J. Lyimo (ii) Mhe. Michael L. Laizer (iii) Mhe. Mch. Peter Msigwa Swali Na. 231: Mhe. Ismail Aden Rage [kny: Mhe. Dkt. Hamis Kigwangalla] Nyongeza: (i) Mhe. Ismail Aden Rage (ii) Mhe. Ezekia Dibogo Wenje 2 2. WIZARA YA NISHATI NA MADINI Swali Na. 232: Mhe. Faith Mohammed Mitambo [kny: Mhe. Fatma Mikidadi] Nyongeza: (i) Mhe. Faith Mohammed Mitambo Swali Na. 233: Mhe. John Paul Lwanji Nyongeza: (i) Mhe. John Paul Lwanji (ii) Mhe. Joseph Osmund Mbilinyi Swali Na. 234: Mhe. John Damiano Komba [kny. Mhe.Juma Abdallah Njwayo] Nyongeza: (i) Mhe. John Damiano Komba (ii) Mhe. Mtutura Abdallah Mtutura (iii) Mhe. Moshi Selemani Kakoso 3. WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI Swali Na. 235: Mhe. AnnaMaryStella John Mallac Nyongeza: (i) Mhe. AnnaMaryStella John Mallac (ii) Mhe. Rukia Kassim Ahmed Swali Na.
    [Show full text]