(Online Document) 1 BUNGE LA TANZANIA
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _____________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Sita – Tarehe 18 Mei, 2015 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kutokana na maagizo yaliyotolewa humu wiki iliyopita kuhusu Hati za kuwasilisha Mezani. Kama kuna kundi lolote, Kamati, Serikali au Upinzani hawajaleta Hati hazisomwi. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais! Mheshimiwa Naibu Waziri! HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO): Randama za Makadirio ya Matumizi kwa Ofisi ya Makamu wa Rais na Taasisi zake kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma) pamoja na (Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (MAHUSIANO NA URATIBU): Hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. MHE. JASSON S. RWEIKIZA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA: 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), (Utawala Bora na Mahusiano na Uratibu) kwa mwaka wa fedha 2014/2015 pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. MHE. ESTHER N. MATIKO - MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI KWA OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA, UTAWALA BORA NA MAHUSIANO NA URATIBU: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Fedha kwa Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Utawala Bora na Mahusiano na Uratibu kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016 SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tunaanza maswali Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Mheshimiwa Engineer Athumani Mfutakamba.
[Show full text]