HOTUBA YA WAZIRI WA UJENZI, MHESHIMIWA DKT. JOHN POMBE MAGUFULI (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MPANGO WA MAENDELEO NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2014/15

A. UTANGULIZI

1. Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa iliyowasilishwa leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ndani ya Bunge lako Tukufu, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu likubali kupokea na kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara ya Ujenzi kwa Mwaka wa fedha 2013/14. Aidha, naomba Bunge lako Tukufu lijadili na kupitisha Mpango na Bajeti ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka wa fedha 2014/15.

2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kuchukua nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunilinda na kunipa nguvu za kuiongoza Wizara ya Ujenzi na kuniwezesha kusimama hapa mbele ya Bunge lako Tukufu kuwasilisha bajeti hii ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka wa fedha 2014/15.

3. Mheshimiwa Spika, kwa heshima kubwa nachukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa , kwa kuendelea 1

kuiongoza nchi yetu vyema na kwa utekelezaji mahiri wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010. Mheshimiwa Rais amekuwa mstari wa mbele katika kutafuta fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo iliyomo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 ikiwemo miradi ya barabara. Aidha, nawapongeza Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa namna ambavyo wamemsaidia Mheshimiwa Rais kusimamia na kuongoza shughuli zote za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa umahiri.

4. Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kukupongeza wewe binafsi, Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge kwa hekima, umahiri na busara mnazotumia katika kuliongoza Bunge hili Tukufu.

5. Mheshimiwa Spika, naomba kuchukua nafasi hii kutoa rambirambi na salamu za pole kwako wewe Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa wabunge, familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu na wananchi wote wa Jimbo la Kalenga kufuatia kifo cha aliyekuwa Waziri wa Fedha Hayati Dkt. . Aidha, natoa pole nyingi kwa familia, ndugu, jamaa na wananchi wa Jimbo la Chalinze kufuatia kifo cha Marehemu Saidi Bwanamdogo, aliyekuwa 2

Mbunge wa Jimbo la Chalinze. Naungana na Waheshimiwa Wabunge wenzangu kutoa pole na kumwomba Mwenyezi Mungu aendelee kutoa faraja kwa familia, ndugu, wewe binafsi Mheshimiwa Spika na Bunge lako Tukufu. Mwenyezi Mungu aziweke roho za marehemu mahali pema peponi, Amina.

6. Mheshimiwa Spika, nachukua fursa hii kuwapongeza Mheshimiwa (Mb.) kwa kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Kalenga na Mheshimiwa (Mb.) kuwa Mbunge wa Jimbo la Chalinze. Ushindi wao ni kielelezo tosha kuwa wananchi wana imani kubwa na CCM katika kuwaletea maendeleo.

7. Mheshimiwa Spika, nawapongeza wajumbe wote wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu chini ya uongozi wa Mwenyekiti Mheshimiwa Peter Joseph Serukamba (Mb.) na Makamu Mwenyekiti Mheshimiwa Profesa Juma Athumani Kapuya (Mb.) kwa ushauri wao wenye tija kwenye sekta ya Ujenzi. Wizara ya Ujenzi inazingatia ushauri unaotolewa na Kamati hii katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku.

8. Mheshimiwa Spika, napenda kuungana na Waheshimiwa Wabunge wenzangu, katika kumpongeza Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda, Mbunge wa Jimbo la Katavi na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hotuba 3

yake inayobainisha mafanikio katika mwaka wa fedha 2013/14 na mwelekeo wa jumla wa mipango ya Serikali katika kipindi cha mwaka wa fedha 2014/15. Naomba pia niwapongeze Waheshimiwa Wabunge waliochangia hotuba hiyo. Ni matumaini yangu kuwa maoni yao yatasaidia kuboresha mipango ya Serikali katika sekta mbalimbali ikiwemo Sekta ya Ujenzi ninayoisimamia.

DIRA NA DHIMA YA WIZARA

9. Mheshimiwa Spika, Dira ya Wizara ya Ujenzi ni kuwa na Barabara, Madaraja, Vivuko, Nyumba za Serikali na Huduma za Ujenzi zenye ubora wa kiwango cha juu, zenye gharama nafuu na zinazozingatia usalama na utunzaji wa mazingira. Aidha, dhima ya Wizara ni kuwa na Barabara, Vivuko, Nyumba za Serikali na Huduma za Ujenzi zilizo na uwiano na ambazo zinakidhi mahitaji kwa viwango bora na kwa bei nafuu zinazoendana na mikakati ya Serikali ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii na wakati huo huo zikiwa endelevu kiuchumi na kimazingira.

MAJUKUMU YA WIZARA

10. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ujenzi ina majukumu ya kusimamia Sera za Ujenzi na Usalama Barabarani; ujenzi na matengenezo ya barabara, madaraja na vivuko; ujenzi na ukarabati wa majengo ya Serikali; pamoja na masuala ya ufundi na umeme. Aidha, Wizara 4

inasimamia shughuli za usajili wa Makandarasi, Wahandisi, Wabunifu Majengo na Wakadiriaji majenzi; masuala ya usalama barabarani na mazingira katika sekta ya ujenzi; uboreshaji wa utendaji na uendelezaji wa watumishi wa Wizara; pamoja na kusimamia utekelezaji wa majukumu ya Wakala/Taasisi zilizo chini ya Wizara.

MALENGO YA WIZARA

11. Mheshimiwa Spika, katika kufanikisha utekelezaji wa majukumu yake, Wizara imelenga kujenga barabara ili kufungua fursa za maendeleo na kuhakikisha miji yote mikuu ya mikoa inaunganishwa kwa barabara za lami ifikapo mwaka wa fedha 2017/18; kufanya matengenezo ya barabara kuu na za mikoa; kujenga barabara za kupunguza msongamano wa magari mijini hususan katika Jiji la Dar es Salaam; kuhakikisha kuwa usafiri wa vivuko unaimarishwa katika maeneo yote yanayohitaji huduma hiyo; na kusimamia ujenzi wa nyumba za Serikali na watumishi. Aidha, Wizara itaendelea kusajili na kusimamia Makandarasi, Wahandisi, Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi kwa kutumia bodi husika pamoja na kuweka mazingira mazuri ya kuvutia sekta binafsi kuwekeza katika Sekta ya Ujenzi. Wizara pia itaendelea kusimamia masuala ya usalama na mazingira katika barabara na vivuko pamoja na kufanya matengenezo na ukarabati wa magari ya Serikali na mitambo. Vile vile Wizara 5

itaendelea kushirikiana na taasisi husika katika kushughulikia masuala mtambuka kama vile kampeni za kupunguza maambukizi ya ugonjwa hatari wa UKIMWI, uhifadhi wa mazingira, masuala ya jinsia pamoja na uendelezaji wa matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Serikali.

MIKAKATI YA WIZARA KATIKA KUFIKIA MALENGO

12. Mheshimiwa Spika, ili kuweza kutekeleza malengo yake, Wizara itaendelea kuzingatia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010, Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano kuanzia mwaka wa fedha 2011/12 – 2015/16, Ahadi za Viongozi Wakuu wa Serikali na Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania (MKUKUTA). Aidha, Wizara ya Ujenzi inazingatia utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now - BRN) na Programu ya Uwekezaji katika Sekta ya Miundombinu ya Usafirishaji (Transport Sector Investment Programme – TSIP) ambayo ni programu ya miaka kumi (2006/07-2016/17) inayolenga kuimarisha na kuboresha miundombinu ya usafirishaji. Wizara inatekeleza Sera ya Taifa ya Ujenzi (2003), Sera ya Usalama Barabarani (2009) na Sera ya Ushirikiano kati ya Serikali na Sekta Binafsi (Public Private Partnership - PPP). Wizara pia itaendelea kusimamia utoaji elimu kwa wananchi kuhusu

6

matumizi ya barabara kwa mujibu wa Sheria ya Barabara Na. 13 ya mwaka 2007 pamoja na sheria nyingine ili miundombinu ya barabara iweze kutunzwa na kudumu kwa muda uliokusudiwa. Wizara vile vile itaboresha mfumo wa upimaji magari ya mizigo kwa kuweka mizani itakayopima uzito wa magari yakiwa kwenye mwendo (Weigh-in-Motion - WIM) kwa lengo la kupunguza msongamano na ucheleweshaji katika vituo vya mizani.

13. Mheshimiwa Spika, mikakati mingine ni pamoja na kusimamia fedha za Mfuko wa Barabara ili kazi za matengenezo ya barabara, madaraja na vivuko zinazotekelezwa zilingane na thamani ya fedha iliyotumika (Value for Money). Wizara pia itaendelea kutafuta vyanzo vipya vya mapato ili kupanua wigo wa Mfuko wa Barabara. Aidha, Wizara itaendelea kuzifanyia marekebisho sheria za kisekta ili ziweze kuendana na mazingira ya sasa na kufikia viwango vinavyokubalika kimataifa na kikanda kama vile Jumuiya ya Afrika Mashariki (East African Community - EAC) na Jumuiya ya Uchumi ya Nchi za Kusini mwa Afrika (Southern Africa Development Community - SADC). Wizara itahakikisha kuwa Makandarasi, Wahandisi Washauri, Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi wa kizalendo wanahusishwa kikamilifu katika ujenzi wa miradi mikubwa hususan miradi ya barabara, madaraja, nyumba na vivuko inayogharamiwa na Serikali badala ya

7

kutegemea kampuni za nje. Lengo ni kuwajengea wazalendo uzoefu stahili katika Sekta ya Ujenzi na kupunguza kasi na wingi wa fedha zinazotokana na vyanzo vyetu kuhamishiwa nje ya nchi kwa kulipia kazi zinazofanywa na kampuni za nje.

B: TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MPANGO NA BAJETI YA MWAKA WA FEDHA 2013/14

Ukusanyaji wa Mapato

14. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa fedha 2013/14, Wizara ilipanga kukusanya jumla ya Shilingi 45,047,550.00 kupitia Idara zenye vyanzo vya mapato. Idara hizo ni Utawala, Huduma za Ufundi na Idara ya Menejimenti ya Ununuzi na Ugavi. Hadi kufikia Aprili, 2014, jumla ya Shilingi 40,385,200.00 zilikuwa zimekusanywa. Makusanyo hayo ni sawa na asilimia 89.65 ya malengo ya Mwaka wa fedha 2013/14.

Bajeti ya Matumizi ya Kawaida

15. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, Wizara ilitengewa kiasi cha Shilingi 381,205,760,000.00 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida. Hadi kufikia Aprili 2014, Shilingi 372,088,829,186.73 zilitolewa na HAZINA kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida. Kiasi hicho ni sawa na asilimia 97.61 ya kiasi kilichoidhinishwa na Bunge la Jamhuri ya 8

Muungano wa Tanzania kwa mwaka wa fedha 2013/14. Kati ya fedha hizo zilizotolewa, Shilingi 18,196,824,680.00 ni kwa ajili ya Mishahara ya Watumishi wa Wizara na Taasisi zake, Shilingi 352,114,418,206.73 ni fedha za Mfuko wa Barabara na Shilingi 1,777,586,300.00 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo ya Wizara na Taasisi zake.

UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO KWA MWAKA WA FEDHA 2013/14

16. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, Wizara iliidhinishiwa na Bunge Shilingi 845,125,979,000.00 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Kati ya fedha hizo, Shilingi 448,174,599,000.00 ni fedha za ndani na Shilingi 397,051,380,000.00 ni fedha za nje. Fedha zilizotolewa hadi Aprili, 2014 ni Shilingi 604,405,943,800.00 ambazo zinajumuisha Shilingi 347,328,096,167.00 fedha za ndani na Shilingi 257,077,847,633.00 fedha za nje. Kiasi cha fedha zilizotolewa ni sawa na asilimia 71.52 ya fedha iliyoidhinishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kutekeleza miradi ya maendeleo kwa mwaka wa fedha 2013/14.

17. Mheshimiwa Spika, kati ya mwezi Januari na mwezi Aprili, 2014, nchi yetu ilikumbwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa. Mikoa iliyoathirika zaidi ni Dar es 9

Salaam, Pwani, Morogoro, Lindi, Tanga, Rukwa, Ruvuma, Mtwara, Mbeya, Katavi, Dodoma, Iringa na Arusha ambapo sehemu kadhaa za barabara zilikatika. Wizara ya Ujenzi ilifanikiwa kurejesha sehemu za barabara zilizokatika hususan katika jiji la Dar es Salaam katika kipindi cha siku tatu na kwa sasa usafiri kwenye barabara hizo zilizokuwa zimeathirika upo katika hali yake ya kawaida. Aidha, maeneo mengine yanaendelea kuboreshwa.

Utekelezaji wa Miradi ya Barabara na Madaraja

18. Mheshimiwa Spika, nchi ya Tanzania ina mtandao wa barabara wenye jumla ya kilometa 87,581. Kati ya hizo, kilometa 35,000 ni Barabara Kuu na za Mikoa zinazosimamiwa na Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS). Kilometa 52,581 zinazobaki ni barabara za Wilaya na zinasimamiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI kupitia Mamlaka za Serikali za Mitaa. Aidha, kuna jumla ya Madaraja 4,880 katika Barabara Kuu na za Mikoa.

19. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS) ilipanga kufanya matengenezo ya kawaida (routine maintenance) ya barabara kuu na barabara za mikoa zenye urefu wa kilomita 30,656, matengenezo ya muda 10

maalum kilomita 5,109.90 na matengenezo ya madaraja 2,577. Hadi kufikia Aprili, 2014, matengenezo yaliyofanyika katika Barabara Kuu ni jumla ya kilomita 7,412 na madaraja 836 na kwa upande wa Barabara za Mikoa matengenezo yaliyofanyika ni kilomita 14,192 na madaraja 707.

20. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, Wizara ilipanga kutekeleza miradi ya ujenzi na ukarabati wa Barabara Kuu, ambapo kilomita 495 ni ujenzi mpya kwa kiwango cha lami na kilomita 190 ni za ukarabati kwa kiwango cha lami na kuendelea na ujenzi wa madaraja 11. Hadi kufikia Aprili, 2014, miradi mipya ya Barabara Kuu iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami ni jumla ya kilometa 600.17. Aidha, kilometa 193.5 za ukarabati wa Barabara Kuu kwa kiwango cha lami zilikuwa zimekamilika.

21. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa barabara za mikoa, kazi zilizopangwa kwa mwaka wa fedha 2013/14 zinahusisha ujenzi wa kilometa 66.1 kwa kiwango cha lami, ukarabati wa kilometa 867.6 kwa kiwango cha changarawe na ujenzi wa madaraja 35. Hadi kufikia Aprili, 2014, kilometa 59.25 zilikuwa zimekamilika kujengwa kwa kiwango cha lami. Kwa upande wa ukarabati, jumla ya kilometa 424.5 za Barabara za Mikoa zilifanyiwa ukarabati kwa

11

kiwango cha changarawe. Aidha, ujenzi wa madaraja 9 yamekamilika.

22. Mheshimiwa Spika, kuhusu upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa miradi ya barabara, kazi hiyo imekamilika kwa upande wa barabara ya Mpemba – Isongole (km 49) na inasubiri kuanza ujenzi. Aidha, miradi kumi na saba (17) inaendelea kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.

23. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ujenzi kupitia TANROADS inaendelea na maandalizi ya ujenzi wa barabara mbadala kati ya Dar es Salaam na Chalinze (km 100) kwa kiwango cha Expressway kwa utaratibu wa kushirikisha Serikali na Sekta Binafsi (Public – Private Partnership – PPP). Barabara hiyo mbadala ambayo itakuwa ni ya kulipia itajengwa kwa njia sita (6 lanes). Barabara iliyopo sasa itaendelea kutoa huduma kwa wale ambao hawako tayari kutumia barabara ya kulipia. Wizara imefanya maandalizi ya ujenzi wa mradi huu ikiwa ni pamoja na kufanya upembuzi yakinifu wa awali (pre-feasibility study), kutoa tangazo la kualika kampuni kuonyesha nia (Expression of Interest) ya kushiriki katika ujenzi wa barabara hii kwa utaratibu wa PPP ambapo kampuni 12 zimeonyesha kuwa na uwezo wa kujenga barabara hiyo. Aidha, Wizara inaendelea na taratibu za kumpata Mtaalam Mwelekezi wa mradi (Transaction Advisor - TA) ambaye 12

ataisaidia Serikali katika kufanya upembuzi yakinifu na usanifu, kuandaa nyaraka za zabuni kwa ajili ya kumpata mbia pamoja na kushauri masuala ya kifedha na kisheria.

24. Mheshimiwa Spika, kazi za ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara ya Wazo Hill - Bagamoyo - Makofia-Msata (km 108) kwa sehemu ya Bagamoyo – Msata (km 64) zinaendelea. Hadi kufikia Aprili, 2014 kilomita 56.2 za tabaka la lami zimekamilika. Aidha, Mkandarasi ameanza maandalizi ya ujenzi wa Daraja la Ruvu Chini.

25. Mheshimiwa Spika, barabara ya Bagamoyo – Saadani – Tanga yenye urefu wa kilometa 178 inahusisha kufanya usanifu wa kina kwa ajili ya kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami. Hadi kufikia Aprili, 2014, kazi ya usanifu wa kina wa barabara hii imefikia hatua za mwisho.

26. Mheshimiwa Spika, mradi wa barabara ya Usagara – Geita - Buzirayombo - Kyamyorwa yenye urefu wa kilometa 422 unahusu kuijenga kwa kiwango cha lami ambapo awamu ya kwanza ilihusisha ujenzi wa barabara kutoka Kyamyorwa hadi Geita (km 220). Awamu ya pili inahusisha ujenzi wa barabara kutoka Geita hadi Usagara (km 90). Awamu ya tatu inahusu ujenzi wa barabara ya Uyovu hadi Biharamulo kupitia Bwanga (km 112). Mradi huu 13

unagharamiwa na Serikali ya Tanzania kwa asilimia 100 na utekelezaji wake ni kama ifuatavyo:

(i) Kyamyorwa – Buzirayombo (km 120)

Kazi za ujenzi wa km 120 zilikamilika tarehe 10 Februari 2008. Kipindi cha uangalizi (Defects Liabilities Period) cha miaka mitatu kiliishia Agosti, 2011. Hata hivyo, kutokana na mashimo kujitokeza mapema katika baadhi ya maeneo katika barabara hiyo kipindi cha uangalizi kiliongezwa hadi Agosti, 2012. Mkandarasi anaendelea kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza kwa gharama zake mwenyewe.

(ii) Buzirayombo – Geita (km 100)

Ujenzi wa barabara hii ulikamilika Februari 2008 na kipindi cha uangalizi kimeisha Machi, 2011. Barabara hii imepokelewa rasmi na TANROADS. Hata hivyo katika mwaka wa fedha 2013/14 mradi huu umetengewa fedha kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai ya mkandarasi.

(iii) Usagara – Geita (km 90) (Lot 1 na Lot 2)

Mradi huu umegawanyika katika sehemu mbili ambazo ni Geita – Sengerema (km 50) na Sengerema – Usagara (km 40). Kazi za ujenzi kwa sehemu ya Geita – Sengerema (km 50) zilikamilika mwezi Januari 2010 na kipindi cha 14

uangalizi (Defects Liability Period) cha miaka mitatu (3) kiliisha Januari 2013. Mradi umepokelewa na TANROADS tarehe 12 April, 2013. Ujenzi wa kipande cha Sengerema – Usagara (km 40) ulikamilika tarehe 7 Agosti 2010. Kipindi cha uangalizi kiliisha tarehe 7 Agosti 2013. Mradi umepokelewa rasmi na TANROADS.

(iv) Uyovu - Biharamulo (km 112)

Kazi za ujenzi kwa kiwango cha lami ilianza Desemba, 2012 na ujenzi unaendelea.

27. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa barabara ya Kigoma – Kidahwe – Uvinza – Kaliua – Tabora (km 431.7) kwa kiwango cha lami ni kama ifuatavyo: -

(i) Tabora – Ndono – Urambo (km 94)

Ujenzi wa kipande hiki kwa kiwango cha lami unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Ili kurahisisha utekelezaji, mradi huu umegawanywa katika sehemu mbili ambazo ni Tabora - Ndono (km 42) na Ndono - Urambo (km 52). Hadi kufikia Aprili, 2014 utekelezaji wake ni kama ifuatavyo: -

15

Lot 1: Tabora - Ndono (km 42)

Kazi zilizokamilika ni ujenzi wa tuta la barabara km 42, ujenzi wa tabaka la chini la msingi (sub- base) km 42 na ujenzi wa tabaka la juu la lami (base course) km 42. Kazi za ujenzi kwa kiwango cha lami zimekamilika.

Lot 2: Ndono - Urambo (km 52)

Kazi zilizokamilika ni ujenzi wa tuta la barabara km 43.5, tabaka la chini la msingi (sub-base) km 20 na tabaka la juu la msingi (Base course) km 14 .

(ii) Daraja la Kikwete katika mto Malagarasi na Barabara zake (km 48)

Lengo la mradi huu ni kujenga daraja katika mto Malagarasi na barabara za kuingilia kila upande wa daraja. Mradi huu unatekelezwa katika awamu mbili. Awamu ya kwanza inahusisha ujenzi wa daraja na makalavati pamoja na barabara yenye urefu wa km 11. Awamu ya pili inahusisha ujenzi wa barabara yenye urefu wa km 37 kwa kiwango cha lami. Mradi huu unafadhiliwa na Mfuko wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Kiuchumi (Economic Development Cooperation Fund) wa Korea. Utekelezaji wa mradi huu ni kama ifuatavyo:

16

Awamu ya Kwanza

Kazi ya ujenzi wa daraja na barabara yenye urefu wa km 11 imekamilika tarehe 19 Novemba, 2013 na kwa sasa mradi huu upo katika kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja.

Awamu ya Pili (km 37)

Kazi zifuatazo zimekamilika; ujenzi wa tuta km 34 na tabaka la lami km 22 limekamilika. Aidha, makalavati yote makubwa yamekamilika.

(iii) Uvinza – Kidahwe (km 76.6)

Ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami unafadhiliwa na Abu Dhabi Fund pamoja na Serikali ya Tanzania. Kazi ya ujenzi ilikamilika tarehe 16 Oktoba, 2013 na kwa sasa mradi upo katika kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja hadi tarehe 15 Oktoba 2014.

(iv) Kaliua – Kazilambwa (km 56)

Ujenzi wa barabara ya Kaliua hadi Kazilambwa (km 56) kwa kiwango cha lami ni sehemu ya barabara ya Kaliua – Malagarasi – Ilunde (km 156). Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania.

(v) Tabora – Sikonge (km 70)

Barabara ya Tabora – Usesula (km 30) ni sehemu ya barabara ya Tabora – Sikonge. Mkataba kwa 17

ajili ya ujenzi wa barabara hii umesainiwa mwezi Aprili, 2014 na tayari Mkandarasi ameanza maandalizi ya kuanza kazi (Mobilization).

(vi) Uvinza – Malagarasi (km 51.1)

Lengo la mradi huu ni kujenga barabara ya Uvinza – Malagarasi kwa kiwango cha lami. Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika. Mazungumzo yanaendelea kati ya Serikali na Abu-Dhabi Fund kwa ajili ya kupata fedha za ujenzi.

28. Mheshimiwa Spika, kuhusu mradi wa barabara ya Marangu – Tarakea – Rongai – Kamwanga na Bomang‟ombe – Sanya Juu, ujenzi umegawanywa katika sehemu zifuatazo:

Lot 1: Tarakea – Rongai – Kamwanga (km 32)

Mradi wa ujenzi wa barabara hii ulikamilika.

Lot 2: Tarakea – Rombo Mkuu (km 32)

Mradi wa ujenzi wa barabara hii ulikamilika.

Lot 3: Marangu – Rombo Mkuu na Kilacha – Mwika (km 32)

Mradi umekamilika na kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja kiliisha tarehe 27 Machi, 2014.

18

Lot 4: Bomang’ombe – Sanya Juu – Kamwanga (km 100) Sehemu ya Sanya Juu – Kamwanga (km 75)

Lengo la mradi huu ni kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami barabara ya Bomang‟ombe – Sanya Juu – Kamwanga (km 100) sehemu ya Sanya Juu – Kamwanga yenye urefu wa kilometa 75. Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kuwa taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi kwa sehemu ya Sanya Juu – Alerai (km 32.2) zinaendelea na zipo katika hatua za mwisho.

29. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa barabara ya Arusha – Moshi – Holili pamoja na Arusha Bypass (km 140), lengo la mradi huu ni kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami kwa njia nne barabara ya Arusha – Moshi – Holili/Taveta- Voi kwa kuanzia na sehemu ya Sakina-Tengeru (km 14.10) na sehemu ya Arusha Bypass (km 42.41) kwa kutumia fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB). Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kuwa taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi zinaendelea ambapo zabuni za ujenzi zimetangazwa mwishoni mwa mwezi Machi, 2014.

30. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi wa KIA – Mererani (km 26) ni kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Mkataba wa ujenzi wa 19

barabara ya KIA – Mererani umesitishwa mwezi Februari, 2014 kutokana na Mkandarasi kushindwa kutimiza masharti ya Mkataba. Taratibu za kumpata Mkandarasi mwingine wa kuendelea na ujenzi wa barabara hii zinaendelea.

31. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi wa barabara ya Nangurukuru – Mbwemkulu yenye urefu wa kilometa 95 lilikuwa ni kujenga kwa kiwango cha lami kwa utaratibu wa Sanifu na Jenga (Design & Build). Ujenzi ulikamilika mwaka 2008. Hata hivyo, Wizara ya Ujenzi ilikataa kupokea mradi huu kwa kuwa haukukamilika kwa kiwango kilichokusudiwa na hivyo kuwepo kwa marekebisho yanayohitajika kufanyika. Kazi ya kufanya marekebisho imekamilika na mradi umepokelewa na TANROADS.

32. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Dodoma - Manyoni yenye urefu wa kilomita 127, lengo la mradi huu lilikuwa ni kujenga kwa kiwango cha lami kwa utaratibu wa Design & Build. Mradi huu uligharamiwa na Serikali ya Tanzania na ulikamilika tarehe 22 Novemba, 2009. Kipindi cha uangalizi cha miaka mitatu kiliisha Novemba, 2012.

33. Mheshimiwa Spika, mradi wa barabara ya Mbwemkuru - Mingoyo yenye urefu wa kilometa 95 lengo lake lilikuwa ni kujenga kwa kiwango cha lami kwa utaratibu maalum wa 20

Design & Build. Ujenzi wa mradi huu ulikamilika Desemba 2007 na kipindi cha uangalizi wa mradi cha miaka 3 kilimalizika tarehe 10 Desemba, 2010. Katika mwaka wa fedha 2013/14 fedha zilitengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai ya mkandarasi.

34. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Manyoni - Singida (km 117), lengo lilikuwa ni kujenga kwa kiwango cha lami kwa utaratibu wa kusanifu na kujenga (Design & Build). Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania na umegawanywa katika sehemu mbili: -

(i) Isuna – Singida (km 63)

Ujenzi wa barabara hii ulikamilika tarehe 30 Juni, 2008 na kipindi cha uangalizi wa ufanisi wa mradi cha miaka mitatu kilimalizika tarehe 30 Juni, 2011. Mradi ulipokelewa tarehe 30 Juni, 2011.

(ii) Manyoni – Isuna (km 54)

Ujenzi wa kilometa 54 za lami ulikamilika tarehe 7 Januari, 2011 na kipindi cha uangalizi cha miaka mitatu kilimalizika tarehe 7 Januari, 2014.

35. Mheshimiwa Spika, mradi wa barabara ya Nelson Mandela wenye urefu kilometa 15.6 ulihusu uimarishaji wa barabara na kuboresha 21

mfumo wa mifereji pamoja na taa za barabarani na zile za kuongozea magari. Aidha, mizani ya kupimia uzito wa magari iliwekwa nje ya lango la kutokea bandarini ili kudhibiti uzito wa magari ya mizigo yanayotoka bandarini. Mradi huu umegharamiwa kwa msaada kutoka Jumuiya ya Nchi za Ulaya pamoja na mchango wa Serikali ya Tanzania ulikamilika tarehe 30 Juni, 2011. Kipindi cha uangalizi wa mradi cha mwaka mmoja kimeisha mwezi Juni, 2012. Hata hivyo Serikali imeendelea kukamilisha mchango wake katika mwaka wa fedha 2013/14.

36. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi wa barabara ya Dumila – Kilosa yenye urefu wa kilometa 78 ni kuijenga kwa kiwango cha lami. Mradi huu umegawanywa katika sehemu mbili ili kurahisisha utekelezaji; sehemu ya Dumila – Rudewa (km 45) na sehemu ya Rudewa - Kilosa (km 18). Utekelezaji wa mradi ni kama ifuatavyo: - (i) Dumila – Rudewa (km 45)

Kazi za ujenzi zilikamilika tarehe 4 Desemba, 2013 na kwa sasa mradi upo katika kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja hadi tarehe 3 Desemba, 2014.

22

(ii) Sehemu ya Rudewa - Kilosa (km 18)

Usanifu umekamilika. Ujenzi wa sehemu hii kwa kiwango cha lami unatarajiwa kuanza katika mwaka wa fedha 2014/15.

37. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Sumbawanga –Matai-Kasanga Port yenye urefu wa kilometa 112, lengo la mradi huu ni kujenga kwa kiwango cha lami kwa utaratibu wa kusanifu na kujenga (Design & Build). Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Hadi kufikia Aprili, 2014, kazi zilizofanyika ni usanifu wa kina km 100, kusafisha barabara km 80, tuta la barabara km 62, tabaka la msingi (subbase) km 54, tabaka la juu (base course) km 36.8 na tabaka la lami km 32.8. Madaraja madogo (box culverts) 10 na makalavati 172 yamekamilika.

38. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa madaraja makubwa unajumuisha kujenga daraja la Kirumi kwenye barabara ya Makutano – Sirari, daraja la Nangoo kwenye barabara ya Mingoyo – Masasi – Tunduru, daraja la Sibiti kwenye barabara ya Ulemo – Gumanga – Sibiti, daraja la Maligisu (Mwanza) kwenye barabara ya Bukwimba – Kadashi - Maligisu, daraja la Kilombero kwenye barabara ya Mikumi - Ifakara – Mahenge, daraja la Kavuu kwenye barabara ya Majimoto-Inyonga, daraja la Mbutu kwenye 23

barabara ya Igunga-Manonga, daraja la Ruhekei kwenye barabara ya Mbinga-Mbamba Bay, daraja la Ruhuhu (Ruvuma), daraja la Momba katika barabara ya Kibaoni – Kililyamatundu/Kamsamba – Mlowo na ununuzi wa Mabey Compact Emergency Bridge Parts na Crane Lorry. Utekelezaji wa ujenzi wa madaraja makubwa hadi kufikia Aprili, 2014 ni kama ifuatavyo:

(i) Daraja la Kirumi

Kazi za usanifu wa kina kwa ajili ya ukarabati wa daraja hili zimekamilika. Taratibu za kumpata Mhandisi Mshauri wa kufanya mapitio (review) ya usanifu na kusimamia kazi za ukarabati zinaendelea.

(ii) Daraja la Nangoo

Ujenzi wa daraja la Nangoo umekamilika.

(iii) Daraja la Sibiti

Maandalizi ya awali ya kuleta mitambo yamefikia asilimia 75 na ya rasilimali watu asilimia 100. Kazi zilizokamilika ni kusafisha eneo la kujenga tuta km 20.15 na ujenzi wa tuta km 17.97. Pia ujenzi wa makalavati makubwa umeshaanza na nguzo za msingi wa daraja zimekamilika.

24

(iv) Daraja la Maligisu

Ujenzi wa Daraja la Maligisu umekamilika.

(v) Daraja la Mto Kilombero

Kazi zipo katika hatua za awali ambapo Mkandarasi anajenga daraja la muda kwa ajili ya kuvushia vifaa na vitendea kazi.

(vi) Daraja la Kavuu

Ujenzi wa msingi na nguzo za daraja unaendelea. Aidha, ununuzi wa vyuma vya daraja (Mabey Bridge Parts) umekamilika.

(vii) Daraja la Mbutu

Hadi kufikia Aprili, 2014, kazi kwa ujumla zimefikia asilimia 96 ambapo ujenzi wa barabara na makalavati umekamilika kwa asilimia 100, ujenzi wa nguzo za msingi umekamilika kwa asilimia 100 pamoja na ujenzi wa kuta za daraja umekamilika kwa asilimia 100. Ujenzi wa Deki unaendelea.

25

(viii) Ununuzi wa Mabey Compact Emergency Bridge Parts na Crane Lorry

Ununuzi wa Mabey Compact Emergency Bridge Parts upo katika hatua za mwisho. Ununuzi wa Crane Lorry umekamilika.

(ix) Daraja la Ruhekei

Kazi za ujenzi zimekamilika Septemba, 2013.

(x) Daraja la Ruhuhu

Usanifu kwa ajili ya ujenzi wa daraja hili unaendelea.

(xi) Daraja la Momba

Kazi ya usanifu wa kina wa daraja hili inaendelea. Kazi ya ujenzi itaanza baada ya usanifu wa kina kukamilika.

39. Mheshimiwa Spika, mradi wa barabara ya New Bagamoyo (Kawawa JCT – Tegeta) unahusu ukarabati na upanuzi wa barabara hii yenye urefu wa (km 17.2) kwa kiwango cha lami kutoka njia mbili za sasa kuwa njia nne (Dual Carriageway) kutoka Mwenge (Makutano ya Barabara ya Sam Nujoma) hadi Tegeta Kibaoni. Mradi huu unafadhiliwa na Serikali ya Japan kupitia Shirika lake la Maendeleo la JICA. Hadi 26

kufikia Aprili, 2014, katika awamu ya kwanza (Mwenge – Tegeta: km 12.9), kazi ya upanuzi zinaendelea ikiwa ni pamoja na ujenzi wa daraja la Lugalo. Maendeleo ya kazi za ujenzi ni kama ifuatavyo: kuondoa miundombinu asilimia 99, tuta la barabara km 12.2, tabaka la chini (subbase) km 12.43 (dual carriageway), tabaka la juu (base course) km 11.4 (dual carriageway) na madaraja asilimia 87.3. Maendeleo ya mradi kwa jumla ni asilimia 97.5. Kwa upande wa awamu ya pili (Morocco – Mwenge: km 4.3), usanifu wa kina unaendelea na unatarajiwa kukamilika Novemba, 2014. Kazi za ujenzi zinatarajiwa kuanza Julai, 2015.

40. Mheshimiwa Spika, mradi wa barabara ya Kyaka – Bugene yenye urefu wa km 59.1 unahusisha ujenzi kwa kiwango cha lami kutoka Kyaka katika makutano ya barabara ya Mutukula – Bukoba hadi Bugene kupitia makao makuu ya wilaya ya Karagwe ikijumuisha ujenzi wa daraja moja la Mwisa pamoja na makalavati. Hadi kufikia Aprili, 2014, kazi za ujenzi zilizofanyika ni kujenga tuta la barabara km 41.1, kujenga tabaka la msingi (subbase) km 18.0, kujenga tabaka la juu (Base) km 12.90, tabaka la lami km 9.2, makalavati madogo 101, makalavati makubwa (Box Culverts) -10 na daraja moja la Mwisa limekamilika. Kwa ujumla kazi zimekamilika kwa asilimia 49.7.

27

41. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Isaka – Lusahunga – Rusumo (km 392), lengo la mradi huu ni kufanya ukarabati kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Isaka – Lusahunga (km 242). Aidha, mradi unahusu usanifu wa kina kwa sehemu ya Lusahunga – Rusumo/Nyakasanza – Kobero (km 150). Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Hadi kufikia Aprili, 2014, hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kama ifuatavyo: -

(i) Sehemu ya Isaka – Lusahunga (km 242)

Mradi huu umegawanyika katika sehemu mbili (2) ili kuharakisha utekelezaji: Isaka – Ushirombo (km 132) na Ushirombo – Lusahunga (km 110).

Lot 1: Isaka – Ushirombo (km 132)

Ujenzi wa barabara hii umekamilika Machi, 2014.

Lot 2: Ushirombo – Lusahunga (km 110)

Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami umekamilika kwa km 53.5. Ujenzi unaendelea kwa sehemu iliyobaki.

28

(ii) Sehemu ya Lusahunga – Rusumo/Nyakasanza – Kobero (150).

Kazi za usanifu wa kina zimekamilika kwa asilimia 80 kwa ajili ya kuanza kuikarabati barabara kwa kiwango cha lami.

42. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi wa barabara ya Manyoni – Itigi – Tabora yenye urefu wa kilometa 264.35 ni kuijenga kwa kiwango cha lami. Mradi huu umegawanyika katika sehemu kuu tatu, ambazo ni Manyoni – Itigi – Chaya (km 89.35), Chaya – Nyahua (km 90) na Nyahua – Tabora (km 85). Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kama ifuatavyo:-

Lot 1: Manyoni – Itigi – Chaya (km 89.35)

Mkandarasi anaendelea na kazi ambapo kazi za ujenzi zilizokamilika ni pamoja na tuta la barabara km 84, tabaka la chini la msingi (subbase) km 40, tabaka la msingi (base course) km 38.35 na tabaka la lami km 37.9.

Lot 2: Tabora – Nyahua (km 85)

Mkandarasi anaendelea na kazi na hatua aliyofikia ni kujenga tuta la barabara km 44.4, tabaka la msingi km 35.5 tabaka la juu km 35.3 na tabaka la lami km 31.8.

29

Lot 3: Chaya - Nyahua (km 90)

Taratibu za kumpata Mhandisi Mshauri kwa ajili ya kufanya mapitio ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina zinaendelea. Taarifa ya uchambuzi wa mapendekezo ya kitaalam (technical evaluation report) ya Makampuni yaliyoomba kufanya kazi hii imewasilishwa Kuwait Fund kwa ajili ya kutoa kibali (No Objection) cha kuendelea na hatua ya kutangaza zabuni ya kumpata Mhandisi Mshauri.

43. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Korogwe – Handeni yenye urefu wa kilometa 65, lengo ni kuijenga kwa kiwango cha lami. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Mkandarasi amekamilisha ujenzi wa barabara yote km 65 kwa kiwango cha lami. Barabara ilifunguliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete tarehe 25 Machi, 2014.

44. Mheshimiwa Spika, lengo katika barabara ya Handeni – Mkata yenye urefu wa kilomita 54 lilikuwa kuijenga kwa kiwango cha lami. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Kazi ya ujenzi zilikamilika Novemba, 2012 na kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja kilikamilika Novemba, 2013. Barabara ilifunguliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete tarehe 25 Machi, 2014. 30

45. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa barabara za mikoa, kazi zilizopangwa kwa mwaka wa fedha 2013/14 zinahusisha ujenzi wa kilometa 35.5 kwa kiwango cha lami, ukarabati wa kilometa 515.6 kwa kiwango cha changarawe na ujenzi wa madaraja 17. Hadi kufikia Aprili, 2014, kilometa 22.30 zimekamilika kujengwa kwa kiwango cha lami sawa na asilimia 63. Kwa upande wa ukarabati, jumla ya kilometa 145.1 za Barabara za Mikoa zilifanyiwa ukarabati kwa kiwango cha changarawe na ujenzi wa madaraja 9 unaendelea. Aidha, maandalizi ya kufanya uchambuzi wa barabara za mijini unaendelea.

46. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Mwanza/Shinyanga border – Mwanza, lengo lilikuwa kufanya ukarabati wa sehemu zilizoharibika yenye urefu wa kilometa 10. Hadi kufikia Aprili, 2014, kazi za ukarabati wa sehemu hizo zilizoharibika zimekamilika.

47. Mheshimiwa Spika, barabara ya kutoka Mwandiga hadi Manyovu (km 60) inayounganisha Mkoa wa Kigoma na nchi jirani ya Burundi imejengwa kwa kiwango cha lami. Mradi huu uligharamiwa na Serikali ya Tanzania. Ujenzi wa barabara hii ulikamilika Oktoba, 2010. Hata hivyo katika mwaka wa fedha 2013/14 mradi huu umetengewa fedha kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai ya Mkandarasi. 31

48. Mheshimiwa Spika, daraja la Umoja katika mto Ruvuma eneo la Mtambaswala/Negomane limejengwa ili kuunganisha nchi za Tanzania na Msumbiji. Daraja hili lilijengwa kwa utaratibu wa kusanifu na kujenga (Design and Build). Mradi huu uligharamiwa na Serikali za Tanzania na Msumbiji na ulikamilika Mei, 2010. Hata hivyo katika mwaka wa fedha 2013/14 mradi huu umetengewa fedha kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai ya Mkandarasi.

49. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14 Wizara imeendelea kutekeleza miradi ya barabara za kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam zenye urefu wa kilometa 109.35. Barabara hizo na utekelezaji wake ni kama ifuatavyo: -

(i) Ubungo Bus Terminal – Mabibo – Kigogo Round about (km 6.4)

Lengo la mradi huu ni kujenga na kukarabati barabara hii kwa kiwango cha lami. Kazi ya ujenzi imekamilika Machi, 2013 na kwa sasa mradi upo katika kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja.

32

(ii) Kigogo Round About – Bonde la Msimbazi – Twiga/Msimbazi Jct (km 2.7)

Lengo la mradi huu ni kujenga, kufanya upanuzi na kukarabati kwa kiwango cha lami. Mkandarasi anaendelea na kazi ambapo kazi zilizofanyika ni kusafisha (clearing and grubbing) km 2.7, tuta la barabara km 2.6, tabaka la msingi km 2 na tabaka la juu la lami km 2 zimekamilika. Maendeleo ya mradi kwa ujumla yamefikia asilimia 75.

(iii) Jet Corner – Vituka – Devis Corner (km 10.30)

Lengo la mradi huu ni kujenga, kufanya upanuzi na kukarabati barabara hii kwa kiwango cha lami. Mradi huu ni sehemu ya mpango wa kupunguza msongamano wa magari yanayotumia barabara hasa katikati ya jiji la Dar es Salaam. Mkandarasi amemaliza kazi zote na kukabidhi mradi Septemba, 2013.

(iv) Tabata Dampo – Kigogo (km 1.65) na Ubungo Maziwa - External (km 2.25)

Lengo la mradi ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara hii. Kazi za ujenzi zimekamilika kwa asilimia 100 kwa sehemu ya Ubungo Maziwa - External. Kwa sehemu ya Tabata Dampo – Kigogo (km 1.65) kazi za ujenzi zinaendelea. 33

(v) Mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka (Bus Rapid Transit Infrastructure - BRT)

Mradi wa ujenzi wa miundombinu ya mabasi yaendayo haraka (Bus Rapid Transit Infrastructure - BRT) na vituo vyake upo katika hatua mbalimbali za ujenzi. Hatua za utekelezaji ni kama ifuatavyo:-

 Package 1– Ujenzi wa Barabara

Mradi unahusisha ujenzi wa barabara kutoka Kimara hadi Kivukoni yenye urefu wa km 15.8 kwenye barabara ya Morogoro, Barabara ya Kawawa toka Magomeni hadi Morocco (km 3.4) na Barabara ya Msimbazi toka Fire hadi Kariakoo km (1.7). Aidha, kuna vituo vya mabasi 27, vituo vikubwa (depots) vya mwisho vitatu katika maeneo ya Kimara, Ubungo na Moroco na madaraja ya waenda kwa miguu matatu. Hadi kufikia Aprili, 2014, kazi zilizofanyika ni kusafisha barabara km 13.5, tuta la barabara km 12.5, ujenzi wa msingi wa madaraja ya waenda kwa miguu asilimia 66, ujenzi wa msingi wa vituo vya mabasi asilimia 70, upanuzi wa makalavati asilimia 100, tabaka la msingi (subbase) km 12.5, tabaka la juu (Base) km 11.4, tabaka la lami la awali km 11.4 na barabara ya zege km 12.4. Maendeleo ya mradi kwa ujumla yamefikia asilimia 65. 34

 Package 2- Ujenzi wa Karakana (Depot) na Kituo cha Mabasi cha Ubungo

Mradi huu unahusisha ujenzi wa Karakana (Depot), Kituo Kikuu cha Ubungo na uboreshaji wa Kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo mikoani (Ubungo Up-Country Bus Terminal). Mradi huu ulichelewa kuanza kutokana na ucheleweshaji katika kufidiwa kwa eneo la mradi. Uamuzi umefanywa ili kurejea usanifu baada ya kuondolewa kwa kituo cha mabasi yaendayo mikoani, hivyo zabuni zitatangazwa mapema mwakani. Hadi kufikia Aprili, 2014 Mhandisi Mshauri kwa ajili ya kufanya mapitio ya usanifu ameshaanza kazi.

 Package 3 - Ujenzi wa Karakana (Depot) ya Jangwani

Mradi huu unahusisha ujenzi wa Karakana (Depot) ya Jangwani. Hadi sasa mkandarasi amekamilisha ujenzi wa tabaka la uwekaji wa tuta (platform) asilimia 95, tabaka la msingi (subbase) asilimia 95, tabaka la juu la zege asilimia 25, jengo la utawala asilimia 95 na jengo la ofisi kuu asilimia 95. Maendeleo ya mradi kwa ujumla ni asilimia 70.

 Package 4 - Ujenzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi (Terminal) cha Kivukoni

Mradi huu unahusisha ujenzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi cha Kivukoni. Hadi sasa ujenzi wa 35

majengo umefikia asilimia 95. Maendeleo ya mradi kwa jumla ni asilimia 95.

 Package 5 - Ujenzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi (Terminal) cha Kariakoo

Mradi huu utahusisha ujenzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi eneo la Gerezani Kariakoo. Mradi ulipangwa kutekelezwa kwa miezi 12. Kazi haikuweza kuanza kama ilivyopangwa kutokana na zuio la Mahakama. Mazungumzo na Mkandarasi ya kuhuisha mkataba yalishindikana kwa hiyo zabuni zilitangazwa upya na kufunguliwa tarehe 30 Julai, 2013. Tathmini ya kumpata Mkandarasi imekamilika na mkataba mpya ulisainiwa tarehe 27 Desemba, 2013. Mkandarasi yuko katika hatua za maandalizi ya kuanza kazi (mobilization).

 Package 6 – Ujenzi wa Vituo vya Mlisho (Feeder Stations)

Mradi huu unahusisha ujenzi wa Vituo vya Mlisho vya Mabasi (Urafiki, Shekilango, Magomeni Mapipa, Kinondoni, Mwinyijuma na Fire). Hadi Aprili, 2014, maendeleo ya kazi ni kama ifuatavyo: Kituo cha Shekilango asilimia 25, kituo cha Magomeni Mapipa asilimia 30, kituo cha Kinondoni asilimia 40, Kituo cha Mwinyijuma asilimia 25. Ujenzi wa vituo vya Fire na Urafiki umechelewa kuanza kutokana na kuchelewa kupata maeneo ya ujenzi. Maendeleo ya mradi kwa jumla ni asilimia 45.

36

 Package 7 – Uhamishaji wa Miundombinu ya Umeme

Mradi huu unahusisha kuhamisha miundombinu ya umeme kupisha ujenzi wa miundombinu ya barabara na vituo vya mabasi kwa ajili ya mradi wa usafiri wa Mabasi yaendayo haraka Jijini Dar es Salaam. Kazi zilizokuwa kwenye mkataba zimekamilika.

(vi) Mbezi (Morogoro Road) –Malamba Mawili – Kinyerezi - Banana (km 14)

Lengo la mradi huu ni kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Mradi huu ni sehemu ya mpango wa Serikali wa kupunguza msongamano wa magari katika barabara za jiji la Dar es Salaam. Barabara hii itakuwa ni njia mbadala kwa magari yanayotokea bara na maeneo ya karibu kama vile mkoa wa Pwani kuelekea uwanja wa ndege au kusini mwa jiji la Dar es Salaam. Mkataba wa ujenzi wa mradi huu umesainiwa na maandalizi ya kuanza ujenzi yanaendelea.

(vii) Tegeta Kibaoni-Wazo Hill – Goba - Mbezi Mwisho (km 20)

Lengo la mradi huu ni kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Barabara hii inasaidia kupunguza msongamano hasa katika barabara ya Morogoro kuingia na kutoka katikati ya jiji. 37

Pia kwa magari yanayotokea kaskazini mwa Dar es Salaam kama vile Bagamoyo kuelekea uwanja wa ndege na kusini mwa jiji la Dar es Salaam watatumia njia hii. Barabara hii ni kiunganisho cha barabara ya pete (DSM Outer Ring Road) ambayo utekelezaji wake umepangwa kufanyika chini ya mpango wa Matokeo Makubwa Sasa. Mkataba wa ujenzi umesainiwa na maandalizi ya kuanza ujenzi yanaendelea.

(viii) Tangi Bovu-Goba (km 9)

Lengo la mradi huu pia ni kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Barabara hii inasaidia kupunguza msongamano hasa katika barabara ya Bagamoyo kuingia na kutoka katikati ya jiji. Magari yanayokwenda Uwanja wa ndege na hata kusini mwa jiji yatapita njia hii badala ya kupita katikati ya jiji. Mkataba wa ujenzi umesainiwa na maandalizi ya kuanza ujenzi yanaendelea.

(ix) Kimara Baruti-Msewe (km 2.6)

Lengo la mradi huu ni kujenga na kupanua barabara hii kwa kiwango cha lami. Barabara hii inasaidia kupunguza msongamano wa magari hasa katika barabara ya Morogoro kuingia na kutoka katikati ya jiji. Mkataba wa ujenzi umesainiwa na maandalizi ya ujenzi yanaendelea.

38

(x) Kimara-Kilungule-External Mandela Road (km 9)

Lengo la mradi huu ni kujenga na kufanya upanuzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami. Barabara hii inasaidia kupunguza msongamano wa magari hasa katika barabara ya Morogoro kuingia na kutoka katikati ya jiji. Mradi huu unatekelezwa kwa awamu, ambapo awamu ya kwanza ni kutoka makutano ya barabara ya External na Mandela hadi Maji Chumvi (km 3.0). Mkataba wa ujenzi umesainiwa na maandalizi ya kuanza ujenzi yanaendelea.

(xi) Kibamba – Kisopwa (km 12.0)

Lengo la mradi huu ni kujenga barabara ya Kibamba – Kisopwa kwa kiwango cha lami. Mkataba wa ujenzi umesainiwa na kazi za ujenzi zinaendelea.

50. Mheshimiwa Spika, mradi wa barabara ya Ndundu – Somanga (km 60), lengo lake ni kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Mradi huu unafadhiliwa kwa pamoja na Kuwait Fund, OPEC Fund na Serikali ya Tanzania. Kazi zilizokamilika ni kama ifuatavyo: Kusafisha eneo la ujenzi (clearing & grubbing) km 57.07, kujenga tuta la barabara km 52.69, tabaka la msingi (subbase) km 48.8, tabaka la juu (base course) km 46.3 na tabaka la lami km 41.77. Ujenzi wa makalavati makubwa na madogo

39

umekamilika kwa asilimia 100. Mradi huu unatarajiwa kukamilika Septemba, 2014.

51. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Kidatu hadi Ifakara (km 106), lengo ni kuijenga kwa kiwango cha lami chini ya msaada wa Serikali ya Marekani kupitia Shirika lake la Maendeleo la USAID, Shirika la Maendeleo la Uingereza (DFID) na Jumuiya ya Ulaya (EU). Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kwamba kazi za upembuzi yakinifu na usanifu zimefikia asilimia 25 kwa kutumia fedha za msaada kutoka USAID.

52. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi wa barabara ya Tabora - Ipole – Koga – Mpanda yenye urefu wa kilomita 359 ni kufanya upembuzi yakinifu pamoja na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Hatua ya utekelezaji ni kwamba kazi za upembuzi yakinifu pamoja na usanifu wa kina wa barabara hii zimekamilika. Mkataba wa ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya Tabora –Uselula yenye urefu wa km 30 umesainiwa ambapo Mkandarasi anaendelea na maandalizi ya kuanza kazi za ujenzi. Aidha, Serikali inatafuta fedha zaidi kwa ajili ya ujenzi wa sehemu iliyobaki ambapo Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) imeonyesha nia ya kugharamia ujenzi wa sehemu ya barabara hii.

40

53. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa barabara ya Makutano – Natta – Mugumu (km 125) na Loliondo – Mto wa Mbu (km 213), lengo ni kufanya usanifu wa kina ikiwa ni maandalizi kwa ajili ya ujenzi wa barabara hizi kwa kiwango cha lami. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kama ifuatavyo:

Lot 1: Loliondo – Mto wa Mbu (km 213)

Usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika na ujenzi umepangwa kuanza katika mwaka wa fedha 2014/15.

Lot 2: Makutano – Natta (km 80): Sehemu ya Makutano – Sanzate (km 50)

Kazi za ujenzi wa sehemu ya Makutano-Sanzate (km 50) zimeanza ambapo kazi ya kusafisha barabara (clearing and grubbing) imefanyika katika km 42 na utekelezaji wa mradi unaendelea.

54. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Ibanda – Itungi/Kiwira (km 26), lengo ni kuanza ujenzi wa barabara ya Ibanda – Itungi/Kiwira (km 26) sehemu ya Kajunjumele – Kiwira Port (5.6km) kwa kiwango cha lami. Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kwamba taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi zinaendelea. 41

55. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa mradi wa barabara ya Nzega - Tabora yenye urefu wa kilomita 115, lengo ni kujenga kwa kiwango cha lami. Mradi huu umegawanyika katika sehemu kuu mbili: Nzega-Puge (km 58.8) na Puge-Tabora (km 56.10) na utekelezaji wake ni kama ifuatavyo: -

(i) Sehemu ya Nzega – Puge (km 58.8)

Mkandarasi anaendelea na ujenzi ambapo kazi zilizokamilika ni kama ifuatavyo:- kusafisha barabara km 57.7, tuta la barabara km 39 na makalavati 59 na tabaka la lami km 5.

(ii) Sehemu ya Puge-Tabora (km 56.1)

Mkandarasi amekamilisha kazi zifuatazo: kujenga tuta la barabara km 48.6, tabaka la juu la msingi wa barabara (base course) km 25, tabaka la lami km 25 na ujenzi wa makalavati makubwa 20 na madogo 100 umekamilika.

56. Mheshimiwa Spika, barabara ya Sumbawanga – Mpanda – Kanyani – Nyakanazi (km 829) inaendelea kujengwa kwa awamu kwa kiwango cha lami. Mradi huu umegawanyika katika sehemu kuu nne: Sumbawanga – Kanazi (km 75), Kanazi – Kizi - Kibaoni (km 76.6), Sitalike – Mpanda (km 36.9) na Mpanda – Uvinza – Kanyani – Nyakanazi (Km 582.4). Maendeleo ya ujenzi ni kama ifuatavyo: - 42

(iii) Sumbawanga – Kanazi (km 75)

Kazi zilizofanyika ni kusafisha barabara kilomita 45, tuta la barabara km 34.81, tabaka la chini la msingi (subbase) km 27.53, tabaka la juu la msingi (base course) km 25.04 na tabaka la lami km 25.04. Madaraja madogo 89 na Madaraja makubwa 12 yamekamilika.

(iv) Kanazi – Kizi – Kibaoni (km 76.6)

Kazi zilizokamilika ni kama ifuatavyo: kusafisha barabara kilometa 76.6, tuta la barabara km 25, tabaka la chini la msingi (subbase) km 2.06, tabaka la juu la msingi wa barabara (base course) km 0.15, madaraja madogo (box culverts) 14 na makalavati 96.

(v) Sitalike – Mpanda (km 36.9)

Hatua zifuatazo za ujenzi zimefikiwa: kujenga tuta la barabara kilometa 12, kujenga tabaka la kwanza la msingi (subbase) kilometa 8, madaraja madogo (box culverts) 4 na makalavati 35.

(vi) Mpanda – Uvinza (km 195.4)

Usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika na ujenzi utafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha ambapo awamu ya kwanza itahusisha sehemu ya Mpanda – Mishamo (km 100). Hatua za kutangaza zabuni zinaandaliwa. 43

57. Mheshimiwa Spika, barabara ya mpakani mwa Simiyu/Mara - Musoma yenye urefu wa kilomita 85.5 inaendelea kufanyiwa ukarabati kwa kiwango cha lami. Aidha, ujenzi wa mchepuo (Bypass) wa Usagara – Kisesa (km 17) unaendelea kwa kiwango cha lami. Vile vile barabara ya Nansio - Kisorya - Bunda sehemu ya Bulamba - Kisorya (km 51) mkataba wa ujenzi umesainiwa. Miradi hii inagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kama ifuatavyo: -

(i) Mpakani mwa Simiyu/Mara – Musoma (km 85.5)

Kazi ambazo zimefanyika hadi sasa ni: tuta la barabara (embankment widening) km 83.5, ujenzi wa tabaka la kwanza la msingi (subbase) km 81.30, kujenga tabaka la juu la msingi (base course) km 80, ujenzi wa tabaka la lami km 76.2.

(ii) Mchepuo wa Usagara – Kisesa (km 17)

Lengo la mradi huu ni kupunguza msongamano wa magari katikati ya jiji la Mwanza. Kazi za ujenzi kwa kiwango cha lami zinaendelea. Aidha kilometa 10.18 za tuta zimekamilika.

44

(iii) Bulamba - Kisorya (km 51)

Mkandarasi anaendelea na maandalizi ya kuanza ujenzi (vifaa, mitambo na rasilimali watu).

58. Mheshimiwa Spika, mradi wa barabara ya Magole – Mziha (km 83.8) lengo lake ni kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Mradi huu umegawanyika katika sehemu kuu mbili: Magole -Turiani (km 48) na Turiani – Mziha (km 35.8) na utekelezaji wake ni kama ifuatavyo: -

(i) Magole – Turiani (km 48.8)

Mkandarasi amekamilisha kazi zifuatazo: Kujenga tuta la barabara km 40.7, tabaka la kwanza la msingi (subbase) km 8.2, ujenzi wa madaraja asilimia 85.5, ujenzi wa makalavati makubwa 20 na madogo 100.

(ii) Mziha – Turiani (km 35.8)

Usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika na ujenzi utafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.

59. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Bariadi – Lamadi (km 71.8), lengo la mradi huu ni kuijenga kwa kiwango cha lami. Mradi huu ni sehemu ya barabara ya Mwigumbi – 45

Maswa – Bariadi na unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kusafisha barabara (clearing and grubbing) km 62.9, ujenzi wa tuta km 50, tabaka la chini la msingi (sub-base) km 30, tabaka la juu la msingi (base course) km 31.89 na tabaka la lami km 28. Aidha, taratibu za kumpata Mkandarasi kwa ajili ya sehemu ya Mwigumbi – Maswa – Bariadi zinaendelea.

60. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Ipole – Rungwa (km 95), lengo ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili kuijenga kwa kiwango cha lami. Hadi Aprili, 2014 taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mhandisi Mshauri wa kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ziko katika hatua za mwisho.

61. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Kidahwe – Kasulu – Kibondo – Nyakanazi (km 310), lengo ni kujenga barabara yote kwa awamu kwa kuanza na sehemu ya Nyakanazi – Kibondo yenye urefu wa kilometa 50 na sehemu ya Kidahwe – Kasulu yenye urefu wa kilometa 50 kwa kiwango cha lami. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Mikataba ya ujenzi wa sehemu ya Kidahwe – Kasulu (km 50) na Nyakanazi – Kibondo (km 50) kwa kiwango cha lami imesainiwa na Makandarasi wanafanya maandalizi ya kuanza ujenzi. 46

62. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa barabara ya kwenda Uwanja wa Ndege wa Mafia (Mafia Airport Access Road) yenye urefu wa kilometa 14, lengo ni kuijenga kwa kiwango cha lami. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania kwa asilimia 100. Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kuwa Mkandarasi amefanya kazi za kusafisha barabara kilomita 12.8, tuta la barabara km 9.5 na tabaka la chini la msingi (Sub-base) km 7.0. Ujenzi wa kambi ya Mhandisi Mshauri na uletaji wa vifaa pamoja na wataalam umekamilika kwa asilimia 85.

63. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Chuo Kikuu cha Dodoma (Dodoma University Road) yenye urefu wa km 12, lengo la mradi ni kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania kwa asilimia 100. Hadi Aprili, 2014 Mkandarasi amekamilisha ujenzi wa km 4 za tuta.

64. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa daraja la Kigamboni lengo la mradi ni kujenga daraja la Kigamboni linalounganisha Kurasini na Kigamboni. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF). Hadi kufikia Aprili, 2014, utekelezaji wa kazi za ujenzi umefikia asilimia 47.

47

65. Mheshimiwa Spika, barabara ya Tunduma – Sumbawanga (km 223.2) lengo lake ni kuijenga kwa kiwango cha lami. Mradi huu unafadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia Shirika la Changamoto za Milenia (MCC). Mradi huu umegawanywa katika mikataba mitatu na utekelezaji wake ni kama ifuatavyo: -

Lot 1: Tunduma – Ikana (km 63.7)

Hadi kufikia Aprili, 2014 mradi umekamilika kwa asilimia 100. Mradi uko kwenye kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja.

Lot 2: Ikana – Laela (km 64.2)

Hadi kufikia Aprili, 2014 mradi umekamilika kwa asilimia 100. Mradi uko kwenye kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja.

Lot 3: Laela – Sumbawanga (km 93.3)

Kazi za ujenzi zilizofanyika ni kama ifuatavyo: kujenga tuta la barabara km 65.6, kujenga tabaka la kwanza la msingi (sub base) km 62.7, kujenga tabaka la kokoto km 65.16, kujenga tabaka la kwanza la lami km 57.8 na tabaka la pili la lami km 47,18. Kwa ujumla kazi imekamilika kwa asilimia 70.5.

66. Mheshimiwa Spika, mradi wa barabara ya Kagoma – Lusahunga (km 154) ni sehemu ya 48

barabara ya Mutukula – Bukoba – Biharamulo – Lusahunga (km 294). Ujenzi wa sehemu ya barabara ya Mutukula – Muhutwe – Kagoma (km 140) ulikamilika chini ya ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Mfuko wa OPEC. Aidha, Benki ya Maendeleo ya Afrika ilitoa mkopo wa ujenzi wa sehemu ya Kagoma – Lusahunga yenye urefu wa kilometa 154 kwa kiwango cha lami. Baada ya Mkandarasi CSCEC wa China kushindwa kutekeleza mkataba wa awali na kuondolewa, mkataba mpya wa kumalizia ujenzi wa sehemu ya barabara ya Kagoma – Lusahunga (km 154) kwa kiwango cha lami ulisainiwa. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania baada ya ADB kujitoa. Kazi ya ujenzi imekamilika tarehe 1 Desemba, 2013 na kwa sasa mradi upo katika kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja hadi tarehe 30 Novemba, 2014.

67. Mheshimiwa Spika, barabara ya Arusha – Namanga (km 105) ni sehemu ya mradi wa barabara ya Arusha – Namanga – Athi River unaofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (African Development Bank - ADB), Benki ya Ushirikiano wa Kimataifa ya Japan (Japan Bank of International Cooperation - JBIC) na Serikali za Tanzania na Kenya kupitia Jumuiya ya Afrika Mashariki. Utekelezaji wa mradi umepangwa katika sehemu kuu mbili, yaani Arusha – Namanga (Lot T) na Athi River – Namanga (Lot K). Urefu wa mradi huu kwa 49

ujumla ni kilometa 240 ambapo sehemu ya Arusha – Namanga (Lot T) ni kilometa 105 na sehemu ya Athi River – Namanga (Lot K) ni kilometa 135. Aidha, mradi unahusisha kazi za nyongeza za ujenzi wa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani (One Stop Border Post - OSBP) ambapo kazi zilianza Desemba, 2011. Mradi huu umekamilika kwa kiwango cha kukubalika (substantially completed) ambapo kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja kiliisha Februari, 2014. Ujenzi wa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) umefikia asilimia 96.67 na kazi inatarajiwa kukamilika Juni, 2014.

68. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa barabara ya Arusha - Minjingu – Babati – Singida yenye urefu wa kilomita 327.5, lengo la mradi ni kuijenga kwa kiwango cha lami sehemu ya Minjingu – Babati – Singida (km 223.5) kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na mchango wa Serikali ya Tanzania. Kwa sehemu ya Minjingu – Arusha (km 104) lengo ni kuifanyia ukarabati kwa kiwango cha lami kwa mkopo kutoka Benki ya Dunia. Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kama ifuatavyo: -

(i) Singida – Kateshi (km 65.1)

Kazi zimekamilika tarehe 29 Februari, 2012 na kipindi cha uangalizi (Defects liability period) cha 50

mwaka mmoja kiliishia tarehe 28 Februari, 2013. Barabara imepokelewa na Serikali.

(ii) Kateshi – Dareda (km 73.8)

Kazi imekamilika tarehe 1 Agosti, 2012 na kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja kilikamilika tarehe 31 Julai, 2013. Barabara imepokelewa na Serikali.

(iii) Dareda – Babati – Minjingu (km 84.6)

Kazi imekamilika tarehe 1 Agosti, 2012 na kipindi cha uangalizi (Defects Liability Period) cha mwaka mmoja kilikamilika tarehe 31 Julai, 2013. Barabara imepokelewa na Serikali.

(iv) Minjingu - Arusha (km 104)

Mkandarasi anaendelea na kazi ya ukarabati ambapo kazi zilizofanyika ni kama ifuatavyo: tuta la barabara km 92.2, tabaka la kwanza la msingi km 90.2, tabaka la juu la msingi (base course) km 88.0 na tabaka la lami km 85.0.

69. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa barabara ya Dar es Salaam – Mbagala (Kilwa Road) yenye urefu wa kilometa 12.9, lengo lake ni kukarabati na kupanua barabara ya lami kutoka njia mbili hadi nne kati ya Bendera Tatu na Mbagala Rangi Tatu na Bendera Tatu- KAMATA kwa msaada kutoka Serikali ya Japan na Serikali ya Tanzania. Mradi huu 51

unatekelezwa kwa awamu nne ambapo awamu ya kwanza inahusisha sehemu ya Bendera Tatu- Mtoni Mtongani (km 5), awamu ya pili inahusisha sehemu ya Mtoni Mtongani -Mbagala Zhakhem (km 5.1), awamu ya tatu inahusisha sehemu ya Mbagala Zhakhem-Mbagala Rangi Tatu (km 1.5) na awamu ya nne inahusisha upanuzi wa sehemu ya Bendera Tatu-KAMATA (km 1.3). Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kama ifuatavyo: -

Awamu ya Kwanza - Bendera Tatu-Mtoni Mtongani (km 5)

Awamu ya kwanza imekamilika kwa msaada wa fedha kutoka Serikali ya Japan.

Awamu ya Pili - Mtoni Mtongani -Mbagala Zhakhem (km 5.1)

Kilometa 5.1 kutoka Mtoni Mtongani hadi Mbagala Zakhem zilikamilika Septemba, 2009 lakini hazikupokelewa na Serikali kutokana na mapungufu yaliyojitokeza. Mkandarasi M/s KAJIMA alirudia kazi hiyo kwa gharama zake mwenyewe na kuikamilisha barabara hiyo Desemba, 2012. Barabara imepokelewa na TANROADS.

52

Awamu ya Tatu - Mbagala Zhakhem- Mbagala Rangi Tatu (km 1.5)

Kazi ya ujenzi wa kipande cha Mbagala Zakhem mpaka Mbagala Rangi Tatu (km 1.5) ilikamilika Aprili, 2012.

Awamu ya Nne: Bendera Tatu-KAMATA (km 1.3)

Taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi kwa ajili ya upanuzi wa sehemu ya Bendera Tatu-KAMATA (km 1.3) zinaendelea kwa fedha za msaada kutoka Serikali ya Japan.

70. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Msimba – Ruaha/Ikokoto – Mafinga – Igawa (km 367.4) lengo ni kufanya ukarabati wa barabara ya lami ya Dar es Salaam – Tunduma (TANZAM) kwa sehemu ya Iyovi - Kitonga Gorge (km 86.3), Ikokoto - Iringa (km 60.9), barabara ya mchepuo kuingia Iringa mjini (km 2.1), Iringa-Mafinga (km 69.4) na Mafinga – Igawa (Km 137.9). Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kama ifuatavyo: -

(i) Msimba – Ruaha Mbuyuni/Ikokoto – Iringa/Mchepuo wa Kuingia Iringa Mjini (km 149.3)

Kazi za ukarabati zilikamilika tarehe 18 Septemba, 2011 na kipindi cha uangalizi cha 53

mwaka mmoja kimeisha. Mradi huu uligharamiwa kwa fedha za mkopo kutoka Serikali ya Denmark na mchango wa Serikali ya Tanzania.

(ii) Iringa – Mafinga (km 69.4)

Kazi za ukarabati zilikamilika Agosti, 2013. Mradi huu upo kwenye kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja.

(iii) Mafinga – Igawa (km 146.0)

Zabuni kwa ajili ya ukarabati wa barabara hii kwa kiwango cha lami zimetangazwa tarehe 21 Februari, 2014. Mradi huu utagharamiwa kwa fedha za ufadhili kutoka Benki ya Dunia na mchango wa Serikali ya Tanzania.

71. Mheshimiwa Spika, barabara ya Korogwe - Mkumbara –Same (km 172) ambayo ni sehemu ya barabara ya Segera – Moshi – Arusha lengo ni kuifanyia ukarabati. Mradi huu umegawanyika katika sehemu mbili:- Korogwe – Mkumbara (km 76) na Mkumbara – Same (km 96) na unafadhiliwa na Benki ya Dunia. Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kama ifuatavyo: -

(i) Korogwe - Mkumbara (km 76)

Mkandarasi anaendelea na ukarabati ambapo kazi zilizofanyika ni: ujenzi wa tuta la barabara 54

km 72.8, tabaka la kwanza la msingi (subbase) km 59.2, tabaka la juu la msingi (base course) km 56.5 na tabaka la lami km 52.7.

(ii) Mkumbara – Same (km 96)

Mkandarasi amekamilisha kazi zifuatazo: ujenzi wa tuta la barabara km 31, tabaka la kwanza la msingi (subbase) km 28, tabaka la juu la msingi (base course) km 25 na tabaka la lami km 22. Kutokana na kasi ndogo ya utekelezaji, Mkandarasi ametahadharishwa na kutakiwa kufanya marekebisho yanayostahili kuongeza kasi na ufanisi wa mradi huu.

72. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Mbeya hadi Makongolosi (km 115), lengo ni kuijenga kwa kiwango cha lami. Ujenzi wa barabara hii umegawanyika katika sehemu tatu ambazo ni: Mbeya – Lwanjilo (km 36), Lwanjilo- Chunya (km 36) na Chunya-Makongolosi (km 43). Kwa sehemu ya Makongolosi – Rungwa – Itigi – Mkiwa (km 413), lengo ni kufanya usanifu wa kina. Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kama ifuatavyo:-

(i) Mbeya – Lwanjilo (km 36)

Mkataba mpya wa ujenzi ulisainiwa baada ya kuvunjwa kwa mkataba wa awali Aprili, 2009 kutokana na Mkandarasi kushindwa kufanya kazi. Mkandarasi anaendelea na kazi ya ujenzi 55

ambapo amekamilisha ujenzi wa tuta la barabara km 22.8.

(ii) Lwanjilo – Chunya (km 36)

Kazi zilizofanyika ni kujenga tuta la barabara km 34.31, tabaka la msingi (subbase) km 25.75, tabaka la juu (base course) km 23,96, tabaka la lami km 20.2, madaraja asilimia 83.75 na makalavati asilimia 92. Hadi Aprili, 2014, maendeleo ya jumla ya mradi ni asilimia 75.

(iii) Chunya - Makongolosi (km 43)

Usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika. Serikali inatafuta fedha za ujenzi kwa kiwango cha lami.

(iv) Makongolosi – Rungwa – Itigi – Mkiwa (km 413)

Usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika na ujenzi utaanza baada ya fedha kupatikana.

73. Mheshimiwa Spika, barabara ya Chalinze - Segera hadi Tanga (km 245) lengo lake ni kuifanyia ukarabati na upanuzi. Ili kurahisisha utekelezaji, mradi huu umegawanyika katika sehemu mbili ambazo ni: Chalinze-Kitumbi (km 125) na Kitumbi-Segera- Tanga (km 120). Utekelezaji wake ni kama ifuatavyo: -

56

(i) Chalinze – Kitumbi (km 125)

Ujenzi wa sehemu hii ulikamilika mwezi Oktoba, 2010. Kipindi cha uangalizi kilitakiwa kukamilika mwezi Oktoba, 2011. Hata hivyo, kipindi hicho kiliongezwa kwa miaka miwili zaidi baada ya kuonekana barabara ina mapungufu katika ubora. Kipindi hicho kilikwisha kimkataba mwezi Oktoba 2013. Barabara hii haijapokelewa rasmi kutokana na mapungufu yaliyojitokeza. Mkandarasi anaendelea kufanya marekebisho ya kasoro zilizojitokeza kwa gharama zake.

(ii) Kitumbi – Segera – Tanga (Km 120)

Maendeleo ya mradi ni kama ifuatavyo: ujenzi wa tuta la barabara km 25, tabaka la msingi (subbase) km 25, tabaka la juu (base course) km 25 na tabaka la lami km 120 zimekamilika.

74. Mheshimiwa Spika, kuhusu daraja la Ruvu, lengo la mradi ni kujenga daraja jipya katika mto Ruvu katika barabara ya Dar es Salaam – Tunduma (TANZAM). Utekelezaji wake ni kuwa mradi ulikamilika mwaka 2009. Katika mwaka wa fedha 2013/14 fedha za ndani zilitengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai ya Mkandarasi.

75. Mheshimiwa Spika, barabara ya Dodoma – Iringa (km 259.8) lengo lake ni ni kuijenga kwa kiwango cha lami kwa fedha za mikopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika 57

(ADB) na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Japan (JICA). Utekelezaji wa mradi huu umegawanywa katika sehemu tatu ambazo ni:- Iringa-Migori (km 95); Migori-Fufu Escapment (km 94) na Fufu Escapment-Dodoma (km 71) na hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kama ifuatavyo: -

(i) Iringa – Migori (km 95.1)

Kazi zifuatazo zimekamilika: kusafisha eneo la ujenzi kilometa 86, kujenga tuta la barabara km 85.9, kujenga tabaka la kwanza la msingi (sub- base) km 83,1, kujenga tabaka la juu la chini la msingi (base course) km 67.3 na kujenga tabaka la lami km 69.15. Ujenzi wa makalavati makubwa 41 na kujenga makalavati madogo 195.

(ii) Migori – Fufu Escarpment (km 93.8)

Maendeleo ya kazi za ujenzi ni kama ifuatavyo: kusafisha eneo la ujenzi km 93.8, kujenga tuta la barabara km 91.70, kujenga tabaka la kwanza la msingi (subbase) km 72.20 km, tabaka la juu (base course) km 69.20 na tabaka la lami km 68.20, ujenzi wa makalavati makubwa 62 na kujenga makalavati madogo 219.

58

(iii) Fufu Escarpment - Dodoma (km 70.9)

Mkandarasi amekamilisha kazi zifuatazo: kusafisha eneo la ujenzi km 70.9, kujenga tuta la barabara km 70.9, kujenga tabaka la kwanza la msingi (subbase) km 70.9, tabaka la juu la msingi (base course) km 70.9, tabaka la lami km 68, ujenzi wa makalavati makubwa 52 na makalavati madogo 98.

76. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa barabara ya Dodoma – Kondoa – Babati yenye urefu wa kilometa 251.4, lengo ni kuijenga kwa kiwango cha lami. Mradi huu umegawanywa katika sehemu nne ili kurahisisha utekelezaji:- Dodoma-Mayamaya (km 43.65), Mayamaya - Mela (km 99.35), Mela - Bonga (km 88.80) na Bonga-Babati (km 19.60). Utekelezaji wa mradi ni kama ifuatavyo: -

(i) Dodoma – Mayamaya (km 43.65)

Mkandarasi amekamilisha kazi zifuatazo za ujenzi: kujenga tuta la barabara km 37.1, kujenga tabaka la kwanza la chini la msingi (subbase) km 35.0, kujenga tabaka la juu (base course) km 34.0, ujenzi wa tabaka la lami km 34.13.

59

(ii) Bonga – Babati (km 19.2)

Kazi ya ujenzi imekamilika tarehe 1 Aprili, 2013 na kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja kiliisha tarehe 30 Machi, 2014.

(iii) Mayamaya – Mela (km 99.35)

Mkandarasi anaendelea na maandalizi (mobilisation) kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii. Mradi huu unagharamiwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Japan (JICA) pamoja na mchango wa Serikali ya Tanzania.

(iv) Mela - Bonga (km 88.80)

Mkandarasi anaendelea na maandalizi (mobilisation) kwa ajili ya kuanza ujenzi. Mradi huu unagharamiwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Japan (JICA) pamoja na mchango wa Serikali ya Tanzania.

77. Mheshimiwa Spika, barabara ya Masasi- Songea – Mbamba Bay yenye jumla ya kilometa 1154.70 lengo lake ni kuijenga kwa kiwango cha lami. Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kama ifuatavyo:-

60

(i) Masasi - Mangaka (km 54)

Awamu ya kwanza ya mradi (km 15) ilikamilika tarehe 31 Machi, 2009. Awamu ya pili ya mradi (km 17.6) ilikamilika tarehe 31 Machi, 2010, Awamu ya tatu (km 22.5) ilikamilika tarehe 31 Desemba, 2011 na kipindi cha uangalizi kiliisha tarehe 31 Desemba, 2012. Mradi uligharamiwa kwa msaada kutoka Serikali ya Japan kupitia JICA.

(ii) Mangaka – Nakapanya (km 70.50)

Mkataba wa ujenzi wa sehemu ya Mangaka - Nakapanya umesainiwa tarehe 17 Februari, 2014. Mradi huu unagharamiwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Japan (JICA) pamoja na mchango wa Serikali ya Tanzania.

(iii) Nakapanya – Tunduru (km 66.50)

Mkataba wa ujenzi kwa sehemu ya Nakapanya - Tunduru umesainiwa tarehe 17 Februari, 2014 kwa kipindi cha miezi 24. Mradi huu unagharamiwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Japan (JICA) pamoja na mchango wa Serikali ya Tanzania.

61

(iv) Mangaka – Mtambaswala (km 65.50)

Mkandarasi anaendelea na maandalizi (mobilisation) kwa ajili ya kuanza ujenzi. Mradi huu unagharamiwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Japan (JICA) pamoja na mchango wa Serikali ya Tanzania.

(v) Tunduru – Matemanga (km 58.7)

Kutokana na kasi ndogo na isiyoridhisha kimkataba, mkataba wa awali ulisitishwa mwezi Januari, 2013 na Mkandarasi kuamriwa kuondoka eneo la mradi. Mkataba mpya wa ujenzi umesainiwa tarehe 17 Februari, 2014 ambapo Mkandarasi anaendelea na maandalizi ya kuanza kazi.

(vi) Matemanga - Kilimasera (km 68.2)

Kutokana na kasi ndogo na isiyoridhisha kimkataba, mkataba ulisitishwa mwezi Januari 2013 na Mkandarasi kuamriwa kuondoka eneo la mradi. Mkataba mpya wa ujenzi umesainiwa tarehe 30 Aprili, 2014 ambapo Mkandarasi anaendelea na maandalizi ya kuanza ujenzi.

(vii) Kilimasera – Namtumbo (km 60.7)

Kutokana na kasi ndogo na isiyoridhisha kimkataba, mkataba ulisitishwa mwezi Januari, 2013 na Mkandarasi kuamriwa kuondoka eneo 62

la mradi. Mkataba mpya wa ujenzi umesainiwa tarehe 17 Februari, 2014 ambapo Mkandarasi anaendelea na maandalizi ya kuanza ujenzi.

(viii) Namtumbo - Songea (km 72.00)

Kazi ya ujenzi imekamilika tarehe 14 Novemba, 2013 na kwa sasa mradi upo katika kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja hadi tarehe 13 Novemba, 2014. Mradi huu uligharamiwa na Serikali ya Marekani kupitia MCC.

(ix) Peramiho – Mbinga (km 78)

Kazi ya ujenzi imekamilika tarehe 29 Novemba, 2013 na kwa sasa mradi upo katika kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja. Mradi huu uligharamiwa na Serikali ya Marekani kupitia MCC.

(x) Mbinga - Mbamba Bay (km 66)

Usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika. Kazi ya ukarabati itafanyika baada ya kupatikana fedha.

(xi) Makambako – Songea (km 295)

Usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika. Kazi ya ukarabati itafanyika baada ya kupatikana fedha.

63

(xii) Mtwara – Mingoyo - Masasi (km 200)

Usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika. Kazi ya ukarabati itafanyika baada ya kupatikana fedha.

(xiii) Mtwara – Newala - Masasi (km 209)

Kazi ya usanifu inaendelea. Mara baada ya kazi ya usanifu kukamilika, zabuni kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami zitatangazwa .

78. Mheshimiwa Spika, Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) una mpango wa kujenga jengo la ofisi za Makao Makuu yake ili kuondokana na kutumia Ofisi za kulipia pango. Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kuwa maandalizi ya kununua kiwanja Dodoma kwa ajili ya kuanza ujenzi yanaendelea.

79. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Chuo cha Uongozi cha Bagamoyo, lengo ni kujenga barabara ya mchepuo kutoka barabara ya Bagamoyo kuingia kwenye Chuo cha Uongozi pamoja na barabara zilizoko ndani ya Chuo hicho. Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kuwa usanifu wa kina na utayarishaji wa nyaraka za zabuni kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami unaendelea.

80. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ujenzi kupitia TANROADS imeendelea kuzifanyia barabara upembuzi yakinifu na usanifu wa kina 64

kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara ikiwa ni maandalizi ya kuzijenga kwa kiwango cha lami barabara hizo. Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa hadi Aprili, 2014 ni kama ifuatavyo: -

(i) Bagamoyo (Makurunge) – Saadani – Pangani – Tanga (km 178)

Lengo la mradi huu ni kujenga barabara ya Bagamoyo (Makurunge) – Saadani – Tanga kwa kiwango cha lami. Mradi huu utafadhiliwa na ADB na JICA kupitia Sekretariat ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwa ni sehemu ya mradi wa Malindi-Lunga Lunga/Tanga-Bagamoyo. Aidha, TANROADS imeingia mkataba mpya na Mhandisi Mshauri aitwaye Aurecon wa Afrika ya Kusini kumalizia kazi ya usanifu wa kina baada ya Mhandisi Mshauri wa awali UNETEC kushindwa kufanya kazi hiyo. Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kwamba kazi ya upembuzi yakinifu imekamilika. Kazi ya usanifu wa kina na utayarishaji wa nyaraka za zabuni inaendelea na inatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2014.

(ii) Sumbawanga – Kasesya/Matai - Kasanga Port (km 162): Sehemu ya Matai – Kasesya (km 50)

Lengo la mradi huu ni kufanya usanifu wa kina wa sehemu ya Matai-Kasesya (km 50) ili kuijenga kwa kiwango cha lami. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Hatua ya 65

utekelezaji ni kuwa taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mhandisi Mshauri kwa ajili ya kuanza usanifu wa kina kwa sehemu ya Matai- Kasesya (km 50) zinaendelea. Kwa sasa TANROADS wako hatua za mwisho za kisheria za kusaini mkataba.

(iii) Barabara ya Ifakara – Mahenge (km 67)

Lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Hadi Aprili, 2014, kazi ya usanifu wa kina inaendelea.

(iv) Kibondo – Mabamba (km 35)

Lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Mkataba kwa ajili ya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina umesainiwa tarehe 11 Aprili, 2014 na Mhandisi Mshauri anaendelea na maandalizi ya kazi.

(v) Mpemba – Isongole (km 49)

Lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Hadi Aprili, 2014 usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika.

66

(vi) Omugakorongo – Kigarama - Murongo (km 105)

Lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Mkataba kwa ajili kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina utasainiwa wakati wowote kuanzia sasa.

(vii) Kyaka – Bugene - Kasulo (km 178): Sehemu ya Bugene – Kasulo (km 124)

Lengo la mradi huu ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Kyaka – Bugene – Kasulo yenye urefu wa kilometa 178. Barabara hii imepangwa kujengwa kwa awamu. Awamu ya kwanza inahusu ujenzi wa sehemu ya Kyaka-Bugene (km 59.1). Kazi ya ujenzi kwa kiwango cha lami inaendelea. Awamu ya pili itahusu usanifu na ujenzi wa sehemu ya Bugene - Kasulo yenye urefu wa kilometa 124. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania kwa asilimia 100. Taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mhandisi Mshauri kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii zinaendelea.

67

(viii) Handeni - Kiberashi - Kijungu - Kibaya – Goima – Chemba - Kwamtoro - Singida (FS & DD) (km 461)

Lengo la mradi huu ni kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina barabara ya Handeni – Kiberashi – Goima – Chemba – Kwamtoro - Singida kwa lengo la kuijenga kwa kiwango cha lami. Kazi ya upembuzi yakinifu imekamilika. Kazi za usanifu wa kina na utayarishaji wa nyaraka za zabuni zinaendelea.

(ix) Mbezi (Morogoro Road) – Malambamawili – Kinyerezi – Banana (km 16.90)

Lengo la mradi huu ni kuanza maandalizi na ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Mbezi (Morogoro Road) – Malambamawili – Kinyerezi – Banana. Lengo la ujenzi wa barabara hii ni kupunguza msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam. Mkataba wa ujenzi wa mradi huu umesainiwa Desemba, 2013 na maandalizi ya kuanza ujenzi yanaendelea kufanywa na makandarasi.

(x) Daraja Jipya Katika Mto Wami

Lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na utayarishaji wa nyaraka za zabuni kwa ajili ya kujenga daraja jipya katika mto Wami kwenye barabara ya 68

Chalinze-Segera ili kuboresha usalama katika daraja hilo. Hadi Aprili, 2014 kazi ya usanifu inaendelea.

(xi) Kidatu – Ifakara – Lupilo – Malinyi – Londo – Lumecha/Songea (km 396)

Lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Taratibu za kumpata Mhandisi Mshauri zimekamilika na rasimu ya mkataba tayari imeandaliwa na kuwasilishwa ADB kwa ajili ya “No Objection”. Mradi huu unagharamiwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania.

(xii) Mtwara – Newala – Masasi (km 209)

Usanifu unaendelea na ukikamilika ujenzi kwa kiwango cha lami utaanza.

(xiii) Kolandoto – Lalago – Mwanhuzi – Matala –Oldeani Jct (km 328)

Lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Mkataba kwa ajili kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina utasainiwa wakati wowote kuanzia sasa.

69

(xiv) Mwanangwa - Misasi - Salawe - Kahama (km 149)

Lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Mwanangwa - Misasi - Salawe - Kahama (km 149). Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kuwa taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mhandisi Mshauri kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina zinaendelea.

(xv) Itoni - Ludewa - Manda (km 211)

Lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Utekelezaji ni kuwa mkataba wa kufanya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina umesainiwa tarehe 20 Februari 2014 na kazi inaendelea.

(xvi) Arusha – Kibaya - Kongwa (km 430)

Lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hii. Hatua ya utekelezaji iliyofikiwa ni kwamba taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mhandisi Mshauri kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina zinaendelea.

70

81. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, kazi zilizopangwa kutekelezwa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara ni kufanya ukarabati wa jumla ya kilometa 400.0 kwa kiwango cha changarawe na kujenga kilometa 31.6 kwa kiwango cha lami pamoja na madaraja 18. Hadi Aprili, 2014, kazi zilizotekelezwa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara ni kufanya ukarabati wa jumla ya kilometa 312.00 kwa kiwango cha changarawe na kujenga kilometa 19.40 kwa kiwango cha lami.

Utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi na Ukarabati wa Vivuko, Maegesho ya Vivuko na Matengenezo ya Magari

82. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) ilipanga kununua boti moja mpya ya uokoaji, kununua kivuko kipya cha kutoa huduma kati ya mwambao wa Bahari ya Hindi (Dar es Salaam na Bagamoyo) pamoja na kukamilisha manunuzi ya vivuko vya Kahunda/Maisome (Mkoani Geita) na Itungi Port (Mkoani Mbeya). Aidha, TEMESA ilipanga kukamilisha ukarabati wa vivuko vya MV Chato (Geita), MV Magogoni (Dar es Salaam), MV Geita & MV Kome I (vilivyopo Mkoani Mwanza) na MV Kilombero I (Mkoani Morogoro). Malengo mengine ni kujenga maegesho ya Msangamkuu (Phase II), Kilambo, Ukara, 71

Bugolora, Kilombero (Upande wa Ulanga), Kahunda/Maisome, Itungi Port, Ilagala, upanuzi wa maegesho ya upande wa Kigamboni na ujenzi wa maegesho matatu kwenye mwambao wa Bahari ya Hindi kati ya Magogoni (Dar es Salaam) na Bagamoyo. Vile vile Wakala ulipanga kufanya matengenezo ya magari ya Serikali katika Karakana zote zilizopo kila Mkoa hapa nchini.

83. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili, 2014 Wakala wa Ufundi na Umeme umetekeleza yafuatayo:

(i) Ujenzi/Ununuzi wa Vivuko

Ujenzi wa kivuko cha MV Malagarasi mkoani Kigoma umekamilika na kuzinduliwa mnamo tarehe 25/10/2013 na Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilali, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ujenzi wa kivuko kitakachotoa huduma ya usafiri kati ya Dar es Salaam na mwambao wa Bahari ya Hindi hadi Bagamoyo unaendelea nchini Bangladesh ambapo kinatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni, 2014; ujenzi wa kivuko cha Kahunda/Maisome unaendelea mkoani Mwanza na ujenzi wa kivuko cha Msangamkuu na boti ya uokozi (Rescue Boat) itakayotoa huduma mkoani Mwanza katika vivuko vya Kisorya – Rugezi unaendelea.

72

(ii) Ujenzi wa Maegesho ya Vivuko

Maegesho yaliyokamilika kujengwa hadi kufikia Aprili, 2014 ni ya Msangamkuu, Muharamba, Kikumbaitale na Senga. Ujenzi wa maegesho ya Kahunda na Maisome unaendelea. Aidha, taratibu za manunuzi kwa ajili ya kuwapata Makandarasi wa ujenzi wa maegesho ya Kilambo, Ukara, Ilagala, Bugolora na maegesho ya Kivuko kwa usafiri wa majini kati ya Dar es Salaam na Bagamoyo zinaendelea.

(iii) Ukarabati wa Vivuko

Ukarabati wa kivuko cha MV Chato umekamilika na kinaendelea kutoa huduma; ukarabati mkubwa wa vivuko vya MV Kome 1 na MV Geita unaendelea mkoani Mwanza na ukarabati wa kivuko cha MV Magogoni na MV Kilombero I upo kwenye hatua ya kumpata Mkandarasi.

(iv) Matengenezo ya Magari

Jumla ya magari 6,252 yalitengenezwa na TEMESA katika karakana zake hadi kufikia mwezi Aprili, 2014.

Utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi na Ukarabati wa Nyumba na Majengo ya Serikali

84. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14 Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala 73

wa Majengo (TBA) ilipanga kukamilisha ujenzi wa miradi inayoendelea pamoja na kuongeza jitihada katika kununua viwanja zaidi mikoani ili kuiwezesha Wakala kujenga nyumba nyingi zaidi za watumishi mikoani; kuendelea na mradi wa ujenzi wa nyumba 10,000 za Watumishi nchi nzima; kuimarisha utoaji wa huduma za ushauri wa kitaalam kwa miradi ya ujenzi wa nyumba za watumishi na ofisi za Serikali kwa kuzingatia mahitaji na matakwa ya watu wenye ulemavu na kuendelea kufanya matengenezo ya nyumba za Serikali na ununuzi wa samani kwa nyumba za viongozi.

85. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili, 2014, miradi mbalimbali ilikuwa katika hatua za umaliziaji. Miradi hiyo ni ujenzi wa nyumba 25 za Watumishi eneo la Bunju (Dar es Salaam), ujenzi wa jengo la ghorofa 8 lenye „flats‟ 16 lililopo SIDA Estate (Dar es Salaam), ujenzi wa jengo lenye ghorofa 6 lililopo mtaa wa Moshi (Dodoma), Ujenzi wa ofisi ya TBA (Manyara), ujenzi wa jengo la ghorofa nne eneo la Mbezi Beach EX – NMC (Dar es Salaam), ujenzi wa jengo la kitegauchumi lililopo barabara ya Wachaga (Arusha), ujenzi wa nyumba 57 za Grade B katika Mikoa 17 ya Tanzania Bara.

86. Mheshimiwa Spika, miradi mingine ya ujenzi wa majengo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Miradi hiyo ni ujenzi wa nyumba 130 za Watumishi wa Serikali kati ya 851 eneo 74

la Bunju (Dar es Salaam); ujenzi wa nyumba 16 za Watumishi wa Serikali katika mikoa mipya ya Simiyu (4), Geita (4), Njombe (4), Katavi (4); Ujenzi wa nyumba 4 za Watumishi wa Serikali Chalinze (Pwani); ujenzi wa nyumba za Majaji katika Mikoa ya Dar es Salaam (1), Mtwara (1), Kilimanjaro (1), Kagera (1) na Shinyanga (1); ujenzi wa Jengo la Ghorofa 10 Mtaa wa Semion/Goliondoi (Arusha) na ujenzi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi awamu ya tatu.

87. Mheshimiwa Spika, Wakala wa Majengo umenunua viwanja kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa nyumba 10,000 za Watumishi wa Umma katika Mikoa ya Arusha (40), Dar es Salaam (653), Dodoma (37), Geita (24), Iringa (64), Kagera (2), Katavi (100), Kigoma (164), Kilimanjaro (63), Lindi (141), Manyara (32), Mara (267), Mbeya (74), Morogoro (378), Mtwara (90), Mwanza (63), Njombe (102), Rukwa (70), Ruvuma (8), Shinyanga (131), Simiyu (308), Singida (22), Tabora (42), Tanga (123) na Pwani (12). Aidha, Wakala umenunua maeneo matatu mkoani Arusha yenye ukubwa wa ekari 10.41, Dodoma ekari 630, Kilimanjaro ekari 39, Mbeya ekari 774 na Pwani ekari 1,036.4.

Usalama Barabarani na Mazingira

88. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14 Wizara iliendelea kuratibu na kuimarisha shughuli za usalama barabarani, 75

mazingira na kudhibiti uzito wa magari yanayotumia barabara zetu. Miradi iliyopangwa kutekelezwa ni ujenzi wa mizani ya kisasa inayopima uzito wa gari ikiwa katika mwendo (Weigh in Motion) katika eneo la Vigwaza, kuanzishwa kwa Wakala wa Usalama Barabarani (National Road Safety Agency), kuweka mfumo wa upatikanaji na utoaji wa taarifa zinazohusu ajali za Barabarani (Road Accident Information System), ukaguzi wa barabara zetu (Road Safety Audit) hususan wakati wa usanifu, ujenzi na baada ya ujenzi ili kubaini kama sheria, kanuni na miongozo ya usalama barabarani imezingatiwa na kutoa elimu kuhusu Sheria ya Mazingira Na.20 ya mwaka 2004 ili izingatiwe katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi.

89. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili, 2014, Wizara ilitekeleza kazi za kuratibu na kuimarisha shughuli za usalama barabarani na mazingira kama ifuatavyo:

i) Hatua za kuwapata Wataalamu Washauri (Consultants) wa kuweka mfumo wa kisasa wa upimaji wa gari likiwa katika mwendo (Automated Weigh-In-Motion) ili kudhibiti uzito wa magari yanayotumia barabara pamoja na ukaguzi wa usalama barabarani (Road Safety Audit) zimekamilika na kazi imeanza.

76

ii) Kazi ya kuanzisha Wakala wa Usalama Barabarani (National Road Safety Agency) inaendelea. Uandaaji wa rasimu ya nyaraka (Business Analysis, Strategic Plan and Framework Document) za uanzishaji Wakala huo umekamilika na kupitiwa na wadau mbalimbali. Hivi sasa Wizara inaboresha nyaraka hizo kwa kuzingatia maoni ya wadau. iii) Mradi wa kuweka mfumo wa upatikanaji na utoaji wa taarifa zinazohusu ajali za barabarani, unaofadhiliwa na Benki ya Dunia unaendelea. iv) Programu ya kutoa Elimu ya Usalama Barabarani mashuleni (Road Safety Education) katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa inaendelea. Taratibu za kumpata Mtaalam Mshauri wa kutoa Elimu ya Usalama Barabarani kwa Umma (Road Safety Awareness Campaign) zinaendelea. v) Kuandaa mapendekezo ya rasimu ya Sheria ya Usalama Barabarani. vi) Kutoa elimu ya usalama barabarani kwa Shule za Msingi ili kupunguza ajali kwa wanafunzi. vii) Kuandaa na kuendesha kampeni za kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa usalama barabarani na athari zake. viii) Kuendeleza ushirikiano na wadau muhimu kama vile Jeshi la Polisi, Wizara ya Afya, Wizara ya Elimu, Wizara ya Sheria na Katiba n.k. katika kutoa elimu ya usalama 77

barabarani na kusimamia utekelezaji wa sheria zilizopo.

UTEKELEZAJI WA MASUALA MTAMBUKA

Ushirikishwaji wa Wanawake Katika Kazi za Barabara

90. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, Wizara ilipanga kutekeleza kazi mbalimbali zenye lengo la kuongeza ushiriki wa wanawake katika kazi za barabara, zikiwa ni pamoja na; kuendesha semina moja kwa waratibu wa mikoa katika ushirikishwaji wa wanawake, kuendelea kuandaa mwongozo wa ushiriki wa wanawake katika kazi za barabara, kufanya ufuatiliaji (monitoring) katika miradi ya barabara inayoendelea ili kujua kiwango cha ushiriki wa wanawake katika miradi hiyo na ufuatiliaji wa maendeleo ya wanawake waliopatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo katika kujenga na kuzifanyia matengenezo barabara. Hadi kufikia Aprili, 2014, Wizara ilitekeleza kazi zifuatazo:-

(i) Semina moja kwa Waratibu wa mikoa 25 iliendeshwa kwa ajili ya kuwakumbusha, kuwapa majukumu na kuelimishana kuhusu será ya Wizara ya Ushirikishwaji wa Wanawake na kupanga mikakati ya pamoja kuhakikisha ushiriki wa

78

wanawake katika kazi za barabara unaongezeka katika ngazi zote. (ii) Kutambua vikundi vya wanawake na makandarasi wanawake waliopata nafasi ya kushindana na hatimaye kupata kazi za ujenzi au matengenezo ya barabara tangu tulipoanza kutoa mafunzo. (iii) Kufuatilia (monitoring) maendeleo ya ushiriki wa wanawake katika miradi ya barabara ili kujua kiwango cha ushiriki katika ngazi mbalimbali katika miradi. (iv) Ukusanyaji wa maoni ya wadau wa ndani umefanyika ili kuboresha rasimu ya miongozo ya Ushirikishwaji wa Wanawake katika kazi za barabara.

Ushiriki wa Wizara Katika Jumuiya Mbalimbali za Kimataifa

91. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14 Wizara imeendelea kushiriki katika masuala yanayohusu Sekta ya Ujenzi katika Jumuiya za Kimataifa na Kikanda hususan Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC). Wizara imeshiriki katika masuala ya EAC kikamilifu katika utekelezaji wa miradi ya barabara zinazounganisha nchi wanachama ambapo miradi ifuatayo imepata ufadhili kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika:

79

(i) Arusha – Moshi – Holili Pamoja na Arusha Bypass (km 140) & Mzani wa Himo.

Taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata mkandarasi zinaendelea ili kuijenga kwa kiwango cha lami kwa njia nne barabara ya Arusha – Moshi – Holili/Taveta-Voi kwa kuanzia na sehemu ya Sakina-Tengeru (km 14.10) na Arusha Bypass (km 42.41).

(ii) Barabara ya Malindi – LungaLunga/Tanga - Bagamoyo

Barabara hii inaunganisha Tanzania na Kenya ambapo kwa barabara ya Bagamoyo (Makurunge) – Saadani – Tanga, kazi ya upembuzi yakinifu imekamilika. Kazi ya usanifu wa kina na utayarishaji wa nyaraka za zabuni inaendelea ili kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami.

(iii) Miradi mingine inayotekelezwa

Serikali ya Tanzania imeendelea kutekeleza kikanda miradi ya daraja la Rusumo, Vituo vya pamoja vya mipakani (One Stop Boarder Post - OSBP) vya Namanga, Rusumo, Kabanga, Tunduma/Nakonde, Kasumulu, Holili, Sirari na Horohoro.

92. Mheshimiwa Spika, Benki ya Dunia inafadhili ujenzi wa mizani zifuatazo chini ya 80

Mradi wa Uwezeshaji na Usafirishaji wa Biashara wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (East Africa Trade and Transport Facilitation Project – EATTFP):

(i) Ujenzi wa Mizani ya Vigwaza

Ujenzi ulianza tarehe 24 Juni, 2013 na umepangwa kukamilika Juni, 2014. Ujenzi pia utahusisha kuweka mizani itakayopima uzito wa magari yakiwa kwenye mwendo (Weigh–in– Motion Weighbridge).

(ii) Ujenzi wa Mizani ya Horohoro

Mkataba wa ujenzi ulisainiwa tarehe 21 Juni, 2013 na ujenzi ulianza Septemba, 2013. Hadi kufikia Aprili, 2014 utekelezaji umefikia asilimia 46.

(iii) Ujenzi wa Mizani ya Sirari

Mkataba wa ujenzi ulisainiwa tarehe 4 Novemba, 2013 na Mkandarasi anaendelea na ujenzi ambao hadi kufikia Aprili, 2014 umefikia asilimia 27.

93. Mheshimiwa Spika, Wizara pia ilishiriki katika maandalizi ya Sheria ya Udhibiti wa Uzito wa Magari katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Vehicle Load Control Act, 2013). Aidha, Wizara inashiriki katika maandalizi ya kutunga

81

kanuni za Sheria ya Udhibiti wa Uzito wa Magari katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.

94. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa SADC, Wizara ilishiriki katika mikutano mbalimbali ukiwemo Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali uliofanyika mwezi Agosti, 2013 nchini Malawi ambapo masuala ya utekelezaji wa Mpango Kamambe wa Kuendeleza Miundombinu (SADC Regional Infrastructure Development Master Plan) yalijadiliwa. Lengo ni nchi wanachama kwa kushirikiana na Sekretarieti ya SADC kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango Kamambe wa Kuendeleza Miundombinu ili kuwa na miundombinu ya uhakika itakayoziunganisha nchi wanachama na hatimaye kupunguza gharama za usafirishaji na kurahisisha biashara. Mpango huo unahusisha uendelezaji wa miradi ya kipaumbele ya miundombinu katika Sekta za Nishati, Uchukuzi, Utalii, Maji, Mawasiliano na Hali ya Hewa. Miradi ya barabara inayojumuishwa katika Mpango Kamambe ni: i) Dar es Salaam – Chalinze Expressway (km 100) kwa ajili ya kurahisisha usafirishaji wa bidhaa za DRC, Malawi na Zambia; ii) Barabara ya Mtwara – Mbamba Bay sehemu ya barabara ya Mbinga – Mbamba Bay (km 66) inayoiunganisha Tanzania na nchi za Malawi na Zambia;

82

iii) TANZAM Highway sehemu ya barabara ya Makambako – Songea (km 289) inayoiunganisha Tanzania na nchi ya Msumbiji; na iv) Barabara ya Manyoni – Tabora – Kigoma sehemu za barabara ya Nyahua – Chaya (km 90) na Kidahwe – Kasulu – Nyakanazi (km 310) zitakazoiunganisha Tanzania na nchi za DRC, Zambia na Burundi.

95. Mheshimiwa Spika, Wizara iliendelea kushiriki kikamilifu katika Majadiliano ya Biashara ya Huduma (Trade In Services) kwa nchi wanachama wa SADC. Majadiliano hayo yanahusisha maeneo ya sekta ya Ujenzi, ambapo maeneo yanayopendekezwa yanahusisha kazi za ujenzi (general construction works), huduma za kihandisi kwa kazi za ujenzi (general construction works engineering), “installations and assembly works”, kazi za umaliziaji wa majengo (building completion and finishing works) na kazi za ujenzi za ufundi maalum (special trade construction works). Aidha, suala la utambuzi wa taaluma (mutual recognition) za uhandisi, ubunifu majengo na ukadiriaji majenzi linahusishwa katika makubaliano hayo. Kimsingi, makubaliano haya yatazingatia Sera ya Ujenzi ya mwaka, 2003 na Sheria zinazodhibiti masuala ya usajili katika Sekta ya Ujenzi kama vile Sheria za Usajili wa Wabunifu Majengo, Wakadiriaji Majenzi, Makandarasi na Wahandisi.

83

Maendeleo ya Watumishi

96. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, Wizara ya Ujenzi imeendelea kuwaendeleza watumishi wake kitaaluma kwa kuwapeleka watumishi 7 katika mafunzo ya muda mrefu. Kati ya watumishi hao, 5 walichukua mafunzo ndani ya nchi na 2 walienda nje ya nchi. Aidha, hakuna watumishi waliopelekwa mafunzo ya muda mfupi kutokana na ukosefu wa fedha. Watumishi 6 waliajiriwa katika Masharti ya Kudumu na Malipo ya Uzeeni, Watumishi 4 waliajiriwa katika Masharti ya Kawaida, watumishi 38 walipandishwa vyeo, watumishi 4 walibadilishwa vyeo na watumishi 4 walithibitishwa kazini.

Mapitio ya Sera ya Ujenzi

97. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, Wizara ya Ujenzi ilipanga kufanyia mapitio Sera ya Ujenzi ya mwaka 2003 ili iweze kukidhi mazingira ya sasa katika sekta ya ujenzi. Kazi iliyofanyika hadi Aprili, 2014 ni pamoja na kuandaa Hadidu za Rejea kwa ajili ya kumpata Mtaalam Mwelekezi na kufanya tathimini ya kampuni za ndani na nje zilizotuma maombi ya kufanya kazi hiyo.

84

Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)

98. Mheshimiwa Spika, Wizara inaendelea kuboresha matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ili kuongeza ufanisi na kutoa huduma kwa wakati. Tovuti ya Wizara imeboreshwa ili kuhakikisha kuwa wananchi wengi wanapata taarifa mbalimbali zinazohusiana na Sekta ya Ujenzi. Aidha, Wizara imeendelea kununua vifaa vya TEHAMA kama kompyuta, printa, mashine za kudurufu na vitunza kumbukumbu kwa ajili ya watumishi wake kulingana na mahitaji yaliyopo. Wizara imeshiriki katika mikutano na mafunzo yanayolenga matumizi ya TEHAMA ili kuboreshaji utendaji wa kila siku. Wizara pia imekamilisha Database inayotoa taarifa kuhusu maendeleo ya ujenzi wa barabara, madaraja, vivuko, nyumba na majengo ya Serikali.

Mawasiliano kwa Umma

99. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14 Wizara iliendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu utunzaji wa barabara, vivuko na majengo ya Serikali hapa nchini. Aidha, Wizara iliandaa na kurusha vipindi maalum vya matukio mbalimbali kwenye televisheni, radio, tovuti ya Wizara na mitandao ya jamii (blogs) mbalimbali. Wizara pia iliandaa majarida na machapisho pamoja na kushiriki 85

kwenye maonyesho mbalimbali kwa madhumuni hayo hayo ya kutoa elimu kwa umma.

UTEKELEZAJI WA TAASISI ZILIZO CHINI YA WIZARA

Bodi ya Mfuko wa Barabara (RFB)

100. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14 Bodi ya Mfuko wa Barabara ilipanga kutekeleza kazi zifuatazo: -

(i) Kukusanya jumla ya Shilingi bilioni 504.3 kutoka katika tozo ya mafuta ambacho ndicho chanzo kikuu cha mapato ya Mfuko. (ii) Kuandaa na kuwasilisha Serikalini mapendekezo ya kuongeza mapato ya Mfuko kwa kupendekeza vyanzo vipya vya mapato na marekebisho ya tozo kwa vyanzo vilivyopo. (iii) Kuendelea kushirikiana na Wizara ya Ujenzi, TANROADS, EWURA na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kufuatilia na kuweka mikakati ya kuziba mianya ya uvujaji wa mapato kwenye vyanzo vya mapato ya Mfuko. (iv) Kukamilisha uandaaji wa Kanuni za Sheria ya Mfuko wa Barabara (Regulations) na miongozo mbalimbali ili kuboresha usimamizi wa fedha za Mfuko. (v) Kuimarisha ufuatiliaji wa matumizi ya fedha za Mfuko kwa kutumia wataalam 86

washauri na wataalam wa ndani kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa kiufundi wa ubora wa kazi (value for money) katika mikoa yote nchini wakati miradi ya matengenezo ya barabara inaendelea. (vi) Kushirikiana na TANROADS kufanya tathmini ya mfumo mzima wa kupima uzito wa magari kwenye vituo vya mizani na kuwekeza katika teknolojia ya kisasa ya mizani na kuimarisha mfumo wa mawasiliano (Management Information System). (vii) Kuweka mfumo wa mawasiliano (Management Information System - MIS) ili kuboresha utendaji kazi wa Bodi. (viii) Kupitia Mpango Mkakati wa Bodi ya Mfuko wa Barabara ili uendane na mahitaji ya hivi sasa.

101. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili, 2014, Bodi ya Mfuko wa Barabara ilikusanya kiasi cha Shilingi bilioni 496.22. Aidha, Bodi ya Mfuko wa Barabara iliandaa mapendekezo ya kuongeza vyanzo vya mapato. Mapendekezo yalijumuisha tozo ya leseni za magari makubwa na kurekebisha kiwango cha tozo ya mafuta ili kufidia mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya Shilingi. Mapendekezo haya yaliwasilishwa Serikalini kwa hatua zaidi. Bodi pia ilifuatilia kwa karibu mapato yatokanayo na tozo ya mafuta na pale kunapojitokeza kiashiria cha uvujaji wa mapato, 87

EWURA na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) huarifiwa ili hatua za kuziba mianya ya uvujaji wa mapato zichukuliwe. Katika mwaka wa fedha 2013/14 Bodi iliendelea kufanya Ukaguzi wa Kiufundi (Technical Audit) katika mikoa 18 kwa Taasisi zinazotumia fedha za Mfuko wa Barabara ili kubaini thamani halisi ya fedha (value for money). Bodi imeendeleza utaratibu wa kuwatumia Wahandisi Washauri wa ndani (Local Consultants) kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa kiufundi na ubora wa kazi (value for money) wakati miradi ya matengenezo ya barabara ikiwa inaendelea (Preventive Audits). Kazi nyingine iliyofanywa ni kuandaa rasimu ya mwongozo unaoelezea hatua za kuchukua kwa wale wote watakaokwenda kinyume na taratibu za matumizi ya fedha za Mfuko. Mwongozo huo utaanza kutumika mara baada ya kupata kibali kutoka Serikalini. Aidha, Mfumo wa Mawasiliano (MIS) umeanza kutekelezwa.

Bodi ya Usajili wa Wahandisi

102. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, Bodi ya Usajili wa Wahandisi ilipanga kutekeleza kazi zifuatazo:

(i) Kusajili Wahandisi 800, Mafundi Sanifu 200 na kampuni za ushauri wa kihandisi 25.

88

(ii) Kusimamia utekelezaji wa mpango wa mafunzo kwa vitendo kwa Wahandisi wahitimu 1,000.

(iii) Kufanya ukaguzi wa kina katika miradi ya Ujenzi, Viwanda, Taasisi za Elimu ya Juu zinazofundisha uhandisi pamoja na makampuni yanayoajiri Wahandisi upande wa Tanzania Bara.

(iv) Kuendelea kuwashawishi Wahandisi wataalam waanzishe kampuni za uhandisi mikoani na kutembelea mikoa yote kuhamasisha utekelezaji wa sheria mpya ya usajili wa Wahandisi.

(v) Kuandaa mitihani ya kitaaluma, kozi fupi fupi na mihadhara ya kitaaluma kwa Wahandisi nchini.

103. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili 2014, Bodi ya Usajili wa Wahandisi ilikuwa imesajili Wahandisi 543 na Kampuni za Ushauri 12. Hivyo, jumla ya Wahandisi wote waliosajiliwa nchini katika ngazi mbalimbali ni 13,148. Idadi hii inajumuisha Wahandisi 11,922 wa kizalendo na Wahandisi 1,226 wa kigeni. Aidha, Bodi ilifuta usajili wa Wahandisi 235 na Kampuni za Ushauri wa Kihandisi 29 kwa kukiuka sheria za usajili wa Wahandisi.

89

104. Mheshimiwa Spika, kazi zingine zilizofanywa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi katika mwaka wa fedha 2013/14 ni:

(i) Kuendelea kusimamia utekelezaji wa utaratibu wa mafunzo ya kujiendeleza kitaaluma kwa Wahandisi wote ili kuwafanya Wahandisi kwenda sambamba na mabadiliko ya kisayansi na kiteknolojia na hivyo kuwafanya Wahandisi waendelee kufanya shughuli zao za kihandisi kwa ufanisi, na vile vile kuwafanya Wahandisi kumudu ushindani unaoletwa na utandawazi. Wahandisi watalaam 2,709 walihudhuria mafunzo mbalimbali ya kujiendeleza.

(ii) Kukagua miradi ya ujenzi wa barabara ili kuhakikisha kuwa inajengwa kwa ubora na inajengwa na Wahandisi waliosajiliwa. Katika kipindi hiki, jumla ya miradi 276 ilikaguliwa. Aidha Wahandisi wa kigeni 49 walibainika kufanya kazi bila usajili na kuchukuliwa hatua mbalimbali za kisheria. Kati yao 47 walikuwa na sifa na hivyo walisajiliwa, na 2 walikataliwa usajili kwa sababu hawakuwa na sifa za kutosha na hivyo kurejeshwa kwao.

(iii) Kuendelea kusimamia utekelezaji wa mpango wa mafunzo kwa vitendo kwa Wahandisi wahitimu. Katika kipindi hiki 90

Bodi ilisimamia mafunzo ya Wahandisi wahitimu 733. Kati ya Wahandisi hao, Wahandisi wahitimu 139 wa kike wanafadhiliwa na Serikali ya Norway. Jumla ya Wahandisi wahitimu 2,552 wameshapitia mpango huu tangu uanzishwe mwaka 2003. Aidha, Wahandisi wahitimu zaidi ya 220 kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa na Taasisi za Serikali wameshahitimu mafunzo hayo na kusajiliwa na Bodi kama Wahandisi watalaam.

(iv) Kukagua miradi na kuhakiki kama Makandarasi wana Wahandisi wa kutosha na wenye sifa za kutekeleza miradi wanayotekeleza. Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2013/14, Bodi ilikagua jumla ya miradi 276. Makandarasi waliobainika kutokuwa na Wahandisi wa kutosha, walilazimishwa kuajiri Wahandisi wenye sifa na wa kutosha kutekeleza miradi husika.

Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi

105. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, Bodi ilipanga kusajili Wabunifu Majengo wapya 25 na Wakadiriaji Majenzi wapya 28. Bodi pia ilipanga kusajili Kampuni za Wabunifu Majengo mpya 20 na Kampuni za 91

Wakadiriaji Majenzi mpya 14. Hadi kufikia Aprili, 2014, Bodi ya Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi ilisajili Wabunifu Majengo 28 na kufanya jumla yao kuwa 358 na Wakadiriaji Majenzi 29 na kufanya jumla yao kuwa 251 pamoja na Kampuni 19 za Wabunifu Majengo na Kampuni 10 za Wakadiriaji Majenzi na hivyo kufanya jumla ya kampuni za Ubunifu Majengo na Ukadiriaji Majenzi zilizosajiliwa na Bodi kuwa 286. Aidha, Bodi iliwafutia usajili Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi 6 pamoja na Kampuni 6 za Ubunifu Majengo na Ukadiriaji Majenzi kutokana na kukiuka sheria na taratibu za Bodi.

106. Mheshimiwa Spika, kazi zingine zilizofanywa na Bodi ya Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi katika mwaka wa fedha 2013/14 ni kusimamia Mpango wa Mafunzo kwa Vitendo ambapo jumla ya wahitimu 49 waliandikishwa na kutafutiwa nafasi za mafunzo katika kampuni za kitaalam zilizosajiliwa na Bodi. Mpango huu ni moja ya njia kuu za kuharakisha usajili wa wahitimu katika fani ya Ubunifu Majengo na Ukadiriaji Majenzi. Aidha, Bodi ilifanya kazi ya kukuza uelewa na kuelimisha jamii kuhusu taaluma za Ubunifu Majengo na Ukadiriaji Majenzi ambapo Bodi iliandaa mikutano ya mashauriano na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa pamoja na Jeshi la Polisi. Mashauriano hayo yalifanyika Dodoma na Dar es Salaam. 92

Bodi ya Usajili wa Makandarasi

107. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14 Bodi ya Usajili wa Makandarasi ilipanga kusajili Makandarasi 807 wa fani za Majengo, Majenzi (Civil Works), Umeme, Mitambo, Kazi Maalum (Specialists Contractors), Makandarasi wa muda (Temporary Contractors) na makandarasi wanaofanya kazi kwa ubia. Aidha, Bodi ilipanga kuendesha jumla ya kozi za mafunzo 6 katika mikoa mbalimbali ya Tanzania na zaidi ya makandarasi 270 walitarajiwa kuhudhuria mafunzo hayo. Hadi kufikia Aprili, 2014 Bodi ilisajili Makandarasi wapya 827 na hivyo kufanya jumla ya Makandarasi waliosajiliwa kufikia 7,149. Aidha, Bodi ilifanya ukaguzi wa miradi 2,687 ya ujenzi, ambapo miradi 1,866 haikuwa na kasoro na miradi 821 ilikuwa na kasoro. Makandarasi katika miradi yenye mapungufu walichukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria. Katika mwaka 2013 Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB) imefuta usajili wa Makandarasi 752 kwa kukiuka sheria na taratibu za usajili. Bodi pia iliendesha kozi za mafunzo 6 katika mikoa ya Dar es Salaam (2), Kilimanjaro (1), Ruvuma (1), Mwanza (1) na Lindi (1) ambapo jumla ya makandarasi 231 walishiriki mafunzo hayo.

93

Baraza la Taifa la Ujenzi

108. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, Baraza lilipanga kutoa msukumo katika utekelezaji wa Sera ya Ujenzi; kuandaa Kanuni za Utekelezaji wa Sheria CAP 162, Revised Edition 2008 iliyoanzisha Baraza; kuratibu na kutoa mafunzo katika sekta ya ujenzi; kutoa ushauri wa kiufundi na utatuzi wa migogoro. Aidha, Baraza lilipanga kuendelea na ukamilishaji ujenzi wa jengo la ghorofa 23 la ofisi kwa kushirikiana na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na mwekezaji binafsi (Lindi Express Limited). Kazi zingine ni kuratibu mfumo wa majaribio wa kutoa taarifa muhimu za miradi ya ujenzi ili kukuza uwazi na uwajibikaji (Construction Sector Transparency Initiative (CoST)) katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi.

109. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili 2014, Baraza la Taifa la Ujenzi liliandaa hadidu za rejea kwa ajili ya Wataalam Washauri watakaoandaa Rasimu za Kanuni za Utekelezaji wa Mabadiliko ya Sheria (Cap 162, Revised Edition (R.E.) 2008). Wataalam Washauri waliandaa Rasimu za kanuni za utekelezaji wa sheria na hivi sasa zinafanyiwa kazi na menejimenti ya Baraza kabla ya kuwasilishwa kwa wadau ili wachangie na baadaye kuwasilishwa kwa Bodi ya Wakurugenzi ya Baraza. Kuhusu ujenzi wa jengo (Samora Tower), mihimili ya ghorofa zote 23 ilikuwa zimekamilika 94

na kazi za umaliziaji zinaendelea ikiwa ni pamoja na kupaka rangi, kujenga miundombinu ya maji safi na maji taka, umeme na simu. Aidha, Baraza liliendesha mafunzo kwa wadau 23 wa sekta ya ujenzi kuhusu usuluhishi wa migogoro ya ujenzi. Baraza vile vile liliendesha mafunzo maalum (tailor made course) huko Morogoro mwezi Novemba, 2013 kwa ajili ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) ambapo wadau 12 walipatiwa mafunzo kuhusu menejimenti ya mikataba ya ujenzi.

110. Mheshimiwa Spika, kazi zingine zilizotekelezwa ni ukaguzi wa kiufundi wa miradi ya ujenzi 50 chini ya Bodi ya Mfuko wa Barabara (Road Funds Board) kwenye Halmashauri za Wilaya na TANROADS kwenye mikoa minne ya Mbeya, Iringa, Katavi na Rukwa. Ukaguzi mwingine wa kiufundi ulihusisha matawi matatu ya Benki ya NMB yaliyopo Mbagala, Kilosa na USA River. Baraza Vile vile lilitoa ushauri wa kiufundi kwa wadau mbalimbali wanaojumuisha, National Audit Office (NAO), KOIKA and Badr E.A Enterprises, USAID Africa Infrastructure Project-REFIT Program, National Microfinance Bank (NMB), Energy Services Limited Dar es Salaam, Bank of Tanzania (BoT) na National Ranching Company Limited (NARCO). Pia Baraza lilishughulikia usuluhishi wa migogoro ya miradi ya ujenzi ipatayo 57. Aidha, Baraza limeendelea na utekelezaji wa majaribio wa mfumo wa kukuza 95

uwazi na uwajibikaji (transparency and accountability) katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi ya umma ujulikanao kwa jina la “Construction Sector Transparency Initiative (CoST)” kuanzia mwaka 2007. Majaribio haya yanafadhiliwa na kuratibiwa katika ngazi ya kimataifa na Shirika la Maendeleo la Uingereza (DFID). CoST inatekelezwa kwa majaribio katika nchi saba yaani Ethiopia, Malawi, Philippines, Tanzania, Uingereza, Vietnam na Zambia. Aidha, Baraza likishirikiana na CoST limeandaa Rasimu ya Mpango Mkakati kwa kipindi cha miaka mitatu (Three Year Sustainable Strategic Action Plan 2013 – 2015).

111. Mheshimiwa Spika, Baraza liliendelea kushirikiana na World Wide Fund for Nature Tanzania Country Office (WWF-TCO) katika matumizi ya Teknolojia ya Nguvu Kazi (Labour Based Technology) kwenye utekelezaji wa miradi 24 ya ujenzi katika vijiji vilivyo karibu na Mbuga za Hifadhi za Wanyama kwenye Mikoa mitano ya Arusha, Mara, Manyara, Iringa na Tabora. Jumla ya Vijiji vinavyohusika ni 45 katika mgawanyiko ufuatao: Arusha (8); Manyara (6), Mara (5), Iringa (22) na Tabora (4). Madhumuni ya mradi ni kujenga miundombinu ya maeneo yanayozunguka hifadhi za mbuga za wanyama pamoja na kuwaongezea kipato wanavijiji wa maeneo haya kwa kuwashirikisha katika ujenzi wa miundombinu ya hifadhi hizo.

96

Vikosi vya Ujenzi (Corporation Sole Works Superintendent)

112. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14 Vikosi vya Ujenzi vilipanga kufanya kazi za ujenzi na ukarabati wa majengo pamoja na kazi zingine zinazohusiana na shughuli za ujenzi. Vikosi vilipanga kutekeleza miradi ya ujenzi wa nyumba za viongozi wa Serikali Dar es Salaam na Mwanza, ujenzi wa maegesho ya vivuko vya Msangamkuu -Mtwara na Senga - Geita. Aidha, Vikosi vilipanga kufanya maboresho ya utendaji kazi kwa kufanya ukarabati wa Ofisi za Vikosi vya ujenzi pamoja na kuongeza vitendea kazi na kufanya ukarabati wa karakana za Vikosi vya Ujenzi Dar es Salaam na Dodoma pamoja kuanzisha mradi wa utengenezaji wa vifaa vya ujenzi.

113. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili 2014, Vikosi vya Ujenzi vilitekeleza miradi 9 inayohusu ujenzi wa maegesho ya Vivuko vya Msangamkuu-Mtwara, Senga-Geita na Kahunda - Sengerema; ukarabati na upanuzi wa Ofisi ya TANROADS Mkoa wa Dar es Salaam; ujenzi wa jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza; ujenzi wa nyumba za Viongozi Mwanza; ujenzi wa jengo la kituo cha afya Muheza; ujenzi wa uzio katika kivuko cha Magogoni-Kigamboni Dar es Salaam na ujenzi wa uzio katika kiwanja cha ndege cha Ziwa Manyara. Aidha, Vikosi vimekamilisha awamu ya kwanza ya ukarabati 97

wa ofisi zake Dar es Salaam, Dodoma na Mwanza na kuanza ukarabati wa karakana za Dar es Salaam na Dodoma. Vile vile Vikosi vimeanzisha mradi wa utengenezaji wa vifaa vya ujenzi (blocks and pre-cast concrete elements). Vikosi pia vimeweza kujiimarisha kwa kuongeza vitendea kazi ili kuongeza ufanisi kwa kununua magari mawili.

Kituo cha Usambazaji wa Teknolojia Katika Sekta ya Ujenzi na Uchukuzi (Tanzania Transportation Technology Transfer Centre)

114. Mheshimiwa Spika, madhumuni ya Kituo hiki ni kuimarisha/kuboresha sekta ya ujenzi na uchukuzi kwa ujumla kwa kutumia mbinu ya usambazaji wa teknolojia katika sekta ya barabara kwa wadau. Katika mwaka wa fedha 2013/14, Kituo kilipanga kutekeleza kazi zifuatazo: -

i) Kusambaza kwa wadau 120,000 jumla ya makala na taarifa 150 zinazohusu tekinolojia mbalimbali katika sekta ya ujenzi na uchukuzi. ii) Kuanza kutekeleza mradi wa kuboresha mifumo ya ujenzi, matengenezo na usimamizi wa miundombinu ya usafiri hapa nchini kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Morgan State University ya Marekani pamoja na wadau wengine. 98

iii) Kuandaa warsha na kozi zinazolenga kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya ujenzi na Uchukuzi. iv) Kutoa huduma za maktaba ya kituo kuhusu sekta ya ujenzi na uchukuzi na kuboresha njia za utunzaji wa kumbukumbu na upashanaji habari.

115. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili, 2014, Kituo cha Usambazaji wa Teknolojia katika Sekta ya Ujenzi na Uchukuzi kilitekeleza kazi zifuatazo:-

i) Kituo kilisambaza makala na taarifa 75 kwa wadau 108,200 zinazoelezea teknolojia mbalimbali katika sekta ya ujenzi na uchukuzi. ii) Kituo kiliyafanyia kazi maombi 36 kutoka kwa wadau wa sekta ya ujenzi na uchukuzi kuhusu taarifa na makala katika maeneo mbalimbali ya sekta ya ujenzi na uchukuzi. iii) Kituo kwa kushirikiana na Shirika la Barabara Duniani (World Road Association) na wadau wengine wa hapa nchini na nje ya nchi, iliandaa na kuendesha Semina ya Mafunzo ya Kimataifa kuhusu "Utendaji na Utawala Bora wa Mamlaka za Barabara na Uchukuzi" (Performance and Governance of Road and Transport Administrations) iliyofanyika tarehe 24-27 Septemba, 2013 jijini Arusha, Tanzania na kuhudhuriwa na washiriki 137 kutoka nchi 23 duniani. 99

iv) Kituo kimeshiriki katika mradi wa "Training Needs Analysis Pertaining to Capacity Building" unaotekelezwa na Umoja wa Mamlaka za Barabara katika nchi za SADC (ASANRA). Mradi huu unalenga kutambua mapungufu ya ujuzi na hivyo kutoa mapendekezo ya kujenga uwezo kwa watendaji wa Mamlaka za Barabara katika nchi za SADC. v) Kituo kiliendelea na utekelezaji wa mpango wa muda mfupi na mrefu wa kuimarisha huduma za Kituo za Usambazaji wa Teknolojia hapa nchini.

Chuo cha Ujenzi Morogoro

116. Mheshimiwa Spika, Chuo cha Ujenzi cha Morogoro katika mwaka wa fedha 2013/14 kilipanga kufundisha jumla ya wanafunzi 800 katika fani za ufundi stadi wa kazi za barabara, majengo pamoja na udereva. Aidha, Chuo kilipanga kuendeleza ujenzi wa jengo jipya la madarasa na karakana ya ufundi pamoja na kununua samani na zana ndogo ndogo za kufundishia. Hadi kufikia Aprili 2014, jumla ya wanafunzi 965 walipata mafunzo ya fani mbalimbali za ujenzi katika Chuo cha Ujenzi Morogoro kama ifuatavyo: Basic Technical Course - 281, Basic Driving Course - 405, PSV Driving Course – 113 na Technician Maintenance Management course - 166. Aidha, Chuo kilifanya ukarabati wa majengo, ununuzi wa samani na 100

vifaa vya mabweni pamoja na vifaa vya kufundishia.

Chuo cha Matumizi Stahiki ya Teknolojia ya Nguvukazi Mbeya (ATTI)

117. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, Chuo cha Matumizi Stahiki ya Teknolojia ya Nguvukazi (Appropriate Technology Training Institute –ATTI) kilichopo Mbeya kilipanga kutoa mafunzo kwa kada mbalimbali ya Wasimamizi wa Barabara (Wahandisi na Mafundi Sanifu) kutoka Wakala wa Barabara, Mamlaka za Serikali za Mitaa na Makandarasi wa Barabara. Aidha, Chuo kilipanga kutoa mafunzo maalum kwa Makandarasi wanawake, vikundi vya wanawake vya matengenezo ya barabara na viongozi wa vikundi vya matengenezo ya barabara vijijini (village gang leaders). Hadi kufikia Aprili, 2014 Chuo cha ATTI kilitoa mafunzo juu ya Matumizi ya Teknolojia ya Nguvukazi kwa kazi za barabara kwa makundi mbalimbali kama ifuatavyo:

(i) Mafunzo ya kuwajengea uwezo makandarasi wanawake yalifanyika mjini Moshi na kushirikisha jumla ya washiriki thelathini na moja (31) kutoka mikoa ya Simiyu, Katavi, Tanga, Dar es Salaam, Manyara, Pwani, Singida, Kilimanjaro na Arusha.

101

(ii) Mafunzo ya uwekaji tabaka la lami nyepesi (surface dressing) kwa washiriki kumi na wanne (14); kumi (10) kati ya hao ni kutoka Halmashauri mbalimbali nchini na wanne (4) kutoka Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi – Zanzibar; (iii) Mafunzo maalum kwa viongozi wa vikundi (village gang leaders) thelathini na sita (36) kutoka Halmashauri za Mikoa ya Pwani na Morogoro yaliyofanyikia kijijini Matema, Kilombero. Mafunzo haya yalitekelezwa kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI kupitia kitengo chake cha Fursa na Vikwazo katika Maendeleo (Opportunities and Obstacles for Development); (iv) Mafunzo maalum ya kimataifa (awamu ya pili) kwa Wahandisi tisa (9) kutoka nchini Somalia yaliendeshwa na Chuo kwa muda wa majuma manane (8); (v) Katika kuhamasisha matumizi ya Teknolojia ya Nguvukazi nchini, Chuo kiliweza kuwafikia Wananchi zaidi ya mia tano (500) kupitia ushiriki wake kwenye maonesho mbalimbali ya Kitaifa na Kimataifa yaliyofanyika hapa Nchini.

118. Mheshimiwa Spika, Chuo cha Matumizi Stahiki ya Teknolojia ya Nguvukazi pia kimeendelea kuzifanyia matengenezo ya kawaida barabara za mafunzo zenye jumla ya kilometa mia moja (100) zilizoko katika wilaya za Rungwe 102

na Kyela katika Mkoa wa Mbeya. Wakati wa utekelazaji wa kazi hizo za barabara, jumla ya wananchi wapatao mia moja sabini na saba (177) walijipatia ajira ya muda mfupi na hivyo kujiingizia kipato. Aidha, Chuo kimeendelea kuwaendeleza kitaaluma wakufunzi na watumishi wa kada zingine watatu (3) katika masomo ya Vyuo Vikuu na vyuo vingine vya taaluma mbalimbali.

C: MAKADIRIO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2014/15

Makadirio ya Mapato

119. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ujenzi inatarajia kukusanya mapato ya jumla ya Shilingi 41,123,000 katika mwaka wa fedha 2014/15 kutoka Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Idara ya Huduma za Ufundi na Idara ya Menejimenti ya Ununuzi.

Matumizi ya Kawaida

120. Mheshimiwa Spika, bajeti ya Matumizi ya Kawaida ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2014/15, ni Shilingi 557,483,565,000.00. Kati ya fedha hizo, Shilingi 24,338,319,000.00 ni kwa ajili ya Mishahara ya Watumishi, Shilingi 6,944,846,000.00 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo ya Wizara na Taasisi na Shilingi

103

526,200,400,000.00 ni fedha za Mfuko wa Barabara.

Makadirio ya Bajeti ya Maendeleo

121. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Wizara ya Ujenzi imetengewa jumla ya Shilingi 662,234,027,000.00 kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Kati ya fedha hizo, Shilingi 450,000,000,000.00 ni fedha za ndani na Shilingi 212,234,027,000.00 ni fedha za nje. Vipaumbele vya miradi itakayotekelezwa ni katika miradi inayoendelea kutekelezwa, miradi inayofadhiliwa na wahisani, utekelezaji wa miradi iliyo katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010, miradi ya kuleta Matokeo Makubwa Sasa na Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2011/12 – 2015/16). Mgawanyo wa fedha za maendeleo pamoja na miradi iliyotengewa fedha kwa mwaka wa fedha 2014/15 ni kama inavyooneshwa katika Kiambatisho Na.1. Aidha, maelezo ya kila mradi ni kama ifuatavyo: - MIRADI YA VIVUKO NA NYUMBA ZA SERIKALI

Ujenzi wa Maegesho ya Vivuko Shilingi Milioni 5,990.00

122. Mheshimiwa Spika, mradi huu una lengo la kujenga maegesho (Landing Ramps) ili vivuko viweze kuegeshwa na kuwezesha abiria na magari kupanda na kushuka kwenye vivuko 104

kwa urahisi na usalama. Katika mwaka wa fedha 2014/15, mradi huu umetengewa Shilingi milioni 5,990.00 kwa ajili ya kazi za ujenzi wa maegesho ya kivuko cha Dar es Salaam – Bagamoyo katika maeneo ya Magogoni, Jangwani Beach na Rungwe Oceanic (Shilingi milioni 4,180.00), ujenzi wa majengo ya abiria kwa kivuko cha Dar es Salaam – Bagamoyo katika maeneo ya Magogoni, Jangwani Beach na Rungwe Oceanic (Shilingi milioni 810.00) pamoja na upanuzi wa sehemu ya Maegesho ya Kigamboni (Shilingi milioni 350.00).

123. Mheshimiwa Spika, kazi nyingine ni ujenzi wa maegesho ya Bukondo na Zumacheli (Shilingi milioni 150.00), ujenzi wa maegesho ya Iramba – Majita (Shilingi milioni 180.00) na maandalizi ya kuanzisha usafiri wa majini katika mwambao wa ziwa Victoria ili kupunguza msongamano katika Jiji la Mwanza (Shilingi milioni 200.00). Usimamizi na ufuatiliaji wa miradi hii umetengewa Shilingi milioni 120.

Ununuzi wa Vivuko Vipya Shilingi Milioni 4,512.32

124. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15 mradi huu umetengewa Shilingi milioni 4,512.32 kwa ajili ya kazi zifuatazo: ununuzi wa kivuko kitakachofanya kazi kati ya Magogoni – Kigamboni (Shilingi milioni 3,900.00), ununuzi wa mashine za kisasa za 105

kukatia tiketi (ticket vending machines) kwa ajili ya vivuko vya Kisorya, Ilagala na Pangani (Shilingi milioni 150.00) na ununuzi wa vifaa vya karakana za TEMESA katika mikoa ya Manyara, Singida, Lindi, Mwanza, Kagera na Ruvuma (Shilingi milioni 404.32). Kiasi cha Shilingi milioni 58.00 kimetengwa kwa ajili ya ufuatiliaji wa miradi hii.

Ukarabati Wa Vivuko Shilingi Milioni 2,102.21

125. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 2,102.21 kwa ajili ya kukarabati vivuko vya MV Magogoni (Shilingi milioni 660.00), MV Mwanza (Shilingi milioni 500.00), „Tug boat‟ MV Kiu- Morogoro (Shilingi milioni 400.00) na MV Pangani II- Tanga (Shilingi milioni 472.21). Kiasi cha Shilingi milioni 70.00 kimetengwa kwa ajili ya ufuatiliaji wa miradi hii.

Ujenzi na Ukarabati wa Nyumba na Majengo ya Serikali Shilingi Milioni 2,689.46

126. Mheshimiwa Spika, mradi huu unalenga kujenga nyumba kwa ajili ya makazi ya Viongozi na Watumishi wa Serikali. Kipaumbele kwa sasa ni katika ujenzi wa nyumba za Majaji pamoja na viongozi wengine

106

wa Serikali wenye stahili ya kupewa nyumba na Serikali.

127. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15 Shilingi milioni 200.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa nyumba ya makazi ya Mkuu wa Wilaya ya Urambo na Shilingi milioni 540.00 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa nyumba za Majaji katika Mikoa ya Shinyanga (1), Kagera (1), Mtwara (1), Kilimanjaro (1) na Dar es Salaam (1). Aidha, kiasi cha Shilingi milioni 200.00 kimetengwa kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa jengo la Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi (awamu ya nne).

128. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Shilingi milioni 100.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa uzio na kuweka mfumo wa ulinzi katika nyumba za viongozi wa Serikali zilizopo Mikocheni, Kijitonyama na Msasani Peninsular. Shilingi milioni 480.00 zitatumika kufanyia matengenezo na ukarabati wa nyumba za viongozi wa Serikali, na Shilingi milioni 500.00 zimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa samani kwenye nyumba za viongozi wa Serikali wenye stahili ya kupewa samani.

129. Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 160.00 zimetengwa kwa ajili ya ukarabati wa Karakana za Serikali chini ya Wakala wa 107

Ufundi na Umeme (TEMESA) katika Mikoa ya Mwanza, Arusha, Dar es Salaam na Dodoma. Shilingi milioni 50.00 zimetengwa kwa ajili ya kufanya maboresho ya kiutendaji kwa kufanya ukarabati wa karakana za Vikosi vya Ujenzi (Carpentry Workshops) zilizopo Dar es Salaam na Dodoma, ukarabati wa Ofisi Dar es Salaam, Dodoma na Arusha pamoja na kuongeza vifaa na vitendea kazi ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa miradi.

130. Mheshimiwa Spika, Wizara itaendelea na jitihada za kuwajengea uwezo Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi, ambapo kwa mwaka wa fedha 2014/15 Shilingi milioni 150.00 zimetengwa kwa kazi hiyo. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 308.62 (fedha za ndani) zimetengwa kwa ajili ya kulipia gharama za ushauri, usimamizi na ufuatiliaji wa miradi.

MIRADI YA BARABARA NA MADARAJA

DAR ES SALAAM-CHALINZE – MOROGORO EXPRESSWAY (KM 200) SEHEMU YA DAR ES SALAAM – CHALINZE (KM 100) - SHILINGI MILIONI 750.00

131. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga barabara ya Dar es Salaam – Chalinze – Morogoro (Km 200) sehemu ya Dar es Salaam – Chalinze (Km 100) kwa kiwango cha 108

“Expressway”. Maandalizi ya utekelezaji wa mradi huu utakaotekelezwa kwa ubia baina ya Serikali na Sekta binafsi “Public Private Partnership” (PPP) yanaendelea.

132. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, kiasi cha Shilingi milioni 100 kimetengwa kwa ajili ya kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa Awamu ya Kwanza ya mradi huo itakayohusisha sehemu ya Dar es Salaam – Chalinze (km 100).

133. Mheshimiwa Spika, chini ya mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) utafanyika ukarabati na kuimarisha (Backlog Maintenance) jumla ya kilometa 194 za barabara ya Dar es Salaam – Chalinze – Morogoro sehemu ya Mlandizi – Chalinze, Lusahunga – Rusumo na Nyakasanza – Kabanga. Katika mwaka wa fedha 2014/15 kiasi cha Shilingi milioni 150.00 kimetengwa kwa ajili ya kuanza kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Dar es Salaam – Chalinze kwa ajili ya upanuzi kuwa njia sita. Aidha, Kiasi cha Shilingi milioni 500.00 kimetengwa kwa ajili ya kukarabati na kuimarisha (Backlog Maintenance) jumla ya kilometa 194 za barabara ya Dar es Salaam – Chalinze – Morogoro sehemu ya Mlandizi – Chalinze (km 44.24), Lusahunga – Rusumo (km 91.46) na Nyakasanza – Kabanga (km 58.5).

109

BARABARA YA WAZO HILL – BAGAMOYO – MSATA - SHILINGI MILIONI 10,885.24

134. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga kwa kiwango cha lami sehemu ya Bagamoyo – Makofia - Msata (km 64) na ujenzi wa Daraja la Ruvu Chini. Kazi ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami inaendelea. Aidha, lengo pia ni kukamilisha usanifu wa kina kwa barabara ya Bagamoyo – Sadani – Tanga (km 178).

135. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 10,441.10 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara ya Bagamoyo – Msata (km 64) kwa kiwango cha lami pamoja na ujenzi wa Daraja la Ruvu Chini. Kiasi cha Shilingi milioni 444.14 kimetengwa kwa ajili ya kukamilisha usanifu wa kina kwa barabara ya Bagamoyo – Sadani – Tanga (km 178).

BARABARA YA USAGARA – GEITA – KYAMYORWA (KM 422) SEHEMU YA UYOVU – BIHARAMULO (KM 112) - SHILINGI MILIONI 9,800.00

136. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Kyamyorwa – Buzirayombo – Geita hadi Usagara (km 310) na sehemu ya Uyovu - 110

Biharamulo (km 112). Awamu ya kwanza ilihusisha ujenzi wa barabara ya Kyamyorwa - Geita (km 220) ambayo ilikamilika Februari, 2008. Awamu ya pili ilihusisha ujenzi wa barabara ya Geita - Usagara (km 90) ambapo ujenzi wake ulianza Februari, 2008 na ulikamilika mwezi Januari, 2010. Awamu ya tatu inahusisha ujenzi wa barabara ya Uyovu - Biharamulo kupitia Bwanga (km 112) ambapo ujenzi wake ulianza Desemba, 2012.

137. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 8,000.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Uyovu – Biharamulo (km 112), kiasi cha Shilingi milioni 800.00 kimetengwa kwa ajili ya ukarabati wa barabara ya Kyamyorwa –Buzirayombo (km120) na kiasi cha Shilingi milioni 1,000.00 kimetengwa kwa ajili ya malipo ya mwisho ya mkandarasi kwa sehemu ya Geita - Usagara (lot 1 na 2) (km 90).

BARABARA YA KIGOMA – KIDAHWE –UVINZA – KALIUA – TABORA (KM 430) –SHILINGI MILIONI 36,596.34

138. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya usanifu na ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kati ya Kigoma na Tabora (km 430) pamoja na ujenzi wa Daraja la Kikwete katika Mto Malagarasi na barabara za maingilio 111

ya daraja (km 48). Kazi ya ujenzi wa daraja ilikamilika Novemba, 2013. Ujenzi wa barabara ya Kidahwe - Uvinza (km 76.6) umekamilika Oktoba, 2013 na ujenzi wa barabara ya Tabora- Ndono (km 42) umekamilika Januari 2014. Kazi za ujenzi wa barabara ya Ndono-Urambo (km 52) zinaendelea. Aidha, ujenzi wa barabara ya Kaliua – Kazilambwa (km 56) umeanza na unaendelea. Maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara za Uvinza - Malagarasi (km 51.10), Urambo – Kaliua (km 33) na Kazilambwa – Chagu (km 40) yanayojumuisha utafutaji fedha kutoka vyanzo vya ndani na nje ya nchi yanaendelea.

139. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 2,139.53 fedha za ndani na Shilingi milioni 10,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa Daraja la Kikwete katika Mto Malagalasi. Kiasi cha Shilingi milioni 2,131.95 fedha za ndani na Shilingi milioni 1,450 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya malipo ya mwisho ya Mkandarasi wa barabara ya Kidahwe-Uvinza (km 76.6).

140. Mheshimiwa Spika, kiasi cha Shilingi milioni 6,837.80 kimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya malipo ya mwisho ya mkandarasi wa barabara ya Tabora - Ndono (km 42), Shilingi milioni 7,189.04 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi sehemu ya Ndono -Urambo (km 52) na kiasi cha 112

Shilingi milioni 4,848.02 kimetengwa kwa ajili ya sehemu ya Kaliua – Kazilambwa (km 56). Kwa upande wa barabara ya Uvinza – Malagarasi (km 51), Urambo – Kaliua (km 33) na Kazilambwa – Chagu (km 40) kiasi cha Shilingi milioni 2,000 zimetengwa kwa ajili ya kuanza maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami.

BARABARA YA MARANGU – TARAKEA – KAMWANGA/BOMANG’OMBE – SANYA JUU (KM 173), ARUSHA – MOSHI – HOLILI (KM 140), SAME - HIMO - MARANGU & MOMBO - LUSHOTO (KM 132), KIA-MERERANI (26), KWA SADALA – MASAMA – MACHAME JCT (KM 15.5) NA KIBOROLONI – KIHARARA – TSUDINI – KIDIA (KM 10.80) SHILINGI MILIONI 13,133.63

141. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga barabara ya Marangu – Tarakea – Rongai – Kamwanga (km 96) na Sanya Juu – Kamwanga (km 75) kwa kiwango cha lami na kukarabati barabara ya Arusha – Moshi – Holili pamoja na Arusha Bypass (km 140). Ujenzi huo utachochea ukuaji wa sekta ya utalii kuzunguka mlima Kilimanjaro na hivyo kukuza uchumi wa nchi. Ujenzi wa sehemu ya Tarakea – Rongai – Kamwanga (km 32) ulikamilika Septemba, 2009, ujenzi wa sehemu ya Tarakea – Rombo Mkuu (km 32) ulikamilika Januari, 2011 na kazi za ujenzi wa sehemu ya Marangu – Rombo Mkuu na Kilacha – Mwika (km 32 ) zilikamilika Machi, 113

2013. Kazi za ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala – Masama –Machame Jct (km 15.5) zinaendelea. Aidha, kazi za ujenzi kwa kiwango cha lami sehemu za KIA – Mererani (km 26) zimesitishwa mwezi Februari, 2014 kutokana na Mkandarasi kushindwa kutimiza masharti ya Mkataba. Taratibu za kumpata mkandarasi mwingine wa kuendelea na ujenzi wa barabara hiyo zinaendelea.

142. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 487.71 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kulipia sehemu ya malipo ya mwisho ya Mkandarasi wa Tarakea – Rombo na Shilingi milioni 1,145.92 kwa ajili ya malipo ya Mkandarasi wa Marangu – Rombo Mkuu na Mwika- Kilacha (km 34). Aidha, kiasi cha Shilingi milioni 5,000.00 kimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa sehemu ya Sanya Juu – Kamwanga (km 75). Jumla ya Shilingi milioni 1,000.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa njia nne kutoka njia mbili za sasa mradi wa Arusha – Moshi – Holili/Taveta-Voi sehemu ya Sakina-Tengeru (km 14.10) na njia mbili kwa sehemu ya Arusha Bypass (km 42.41). Aidha, Shilingi milioni 2,500 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara ya KIA-Mererani (km 26) na kiasi cha Shilingi milioni 1,000.00 kimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala - Masama – Machame Juction (km 15.5) na

114

Shilingi milioni 2,000.00 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara Kiboroloni – Kiharara – Tsudini – Kidia (km 10.80).

NANGURUKURU - MBWEMKULU (KM 95) – SHILINGI MILIONI 2,000.00

143. Mheshimiwa Spika, mradi huu ni sehemu ya barabara ya Dar es Salaam – Lindi – Mingoyo ambayo ni kiungo muhimu kati ya Dar es Salaam na Mikoa ya Kusini. Ujenzi wa barabara hii ulikamilika Januari, 2008.

144. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 2,000.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya malipo ya mwisho kwa Mkandarasi.

DODOMA – MANYONI (KM 127) – SHILINGI MILIONI 1,309.28

145. Mheshimiwa Spika, mradi huu umehusisha kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Dodoma - Manyoni (km 127) kwa utaratibu wa kusanifu na kujenga (Design & Build). Mradi huu uligharamiwa na Serikali ya Tanzania na ulikamilika mwezi Novemba, 2009. Aidha, mradi huu unahusisha pia ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya mchepuo kuingia Manyoni mjini (km 4.8). 115

146. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 1,309.28 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara ya mchepuo kuingia Manyoni mjini (km 4.8) na kulipa sehemu ya malipo ya mwisho ya Mkandarasi wa sehemu ya Dodoma - Manyoni (km 127).

MBWEMKURU – MINGOYO (KM 95) – SHILINGI MILIONI 535.00

147. Mheshimiwa Spika, mradi huu umehusisha kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mbwemkuru - Mingoyo yenye urefu wa kilomita 95 kwa utaratibu wa kusanifu na kujenga (Design & Build). Mradi huu ni sehemu ya barabara ya Dar es salaam – Lindi – Mingoyo na ujenzi wake ulikamilika Desemba, 2007. Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2014/15, barabara hii imetengewa kiasi cha Shilingi milioni 535.00 fedha za ndani kwa ajili ya kulipa sehemu ya malipo ya mwisho ya Mkandarasi.

PORT ACCESS ROAD (NELSON MANDELA ROAD) REHABILITATION (KM16.8)– SHILINGI MILIONI (1,650.00)

148. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu lilikuwa ni kukarabati na kuimarisha barabara ya Nelson Mandela (km15.6) iliyokuwa imeharibika ili kurahisisha usafiri wa magari ya mizigo yanayotoka Bandari ya Dar es Salaam na 116

kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam. Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2014/15, barabara hii imetengewa Shilingi milioni 1,500.00 fedha za ndani kwa ajili ya kulipa malipo ya mwisho ya Mkandarasi. Aidha, katika mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) maandalizi ya upanuzi wa barabara ya Nelson Mandela sehemu ya Dar Port – TAZARA (km 6.0) kuwa njia sita yataanza. Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2014/15, kiasi cha Shilingi milioni 150.00 kimetengwa kwa ajili ya maandalizi ya upanuzi wa barabara ya Nelson Mandela sehemu ya Dar Port – TAZARA (km 6.0) kuwa njia sita.

BARABARA YA DUMILA – KILOSA (KM 78) – SHILINGI MILIONI 8,000.00

149. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga barabara kwa kiwango cha lami kutoka Dumila – Kilosa (km 78). Kazi ya ujenzi wa barabara ya Dumila - Rudewa (km 45) imekamilika Desemba, 2013. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15 barabara ya Dumila – Kilosa (km 78) imetengewa Shilingi milioni 8,000.00 fedha za ndani kwa ajili ya kulipa madai ya Mkandarasi na kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Rudewa-Kilosa (km 24).

117

BARABARA YA SUMBAWANGA – MATAI – KASANGA PORT (KM 112) – SHILINGI MILIONI 10,241.37

150. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Sumbawanga –Matai-Kasanga Port (km. 112) kwa kiwango cha lami. Mradi unagharamiwa na Serikali ya Tanzania na unatekelezwa kwa utaratibu wa kusanifu na kujenga (Design and Build). Kazi za ujenzi zinaendelea. Katika mwaka wa fedha 2014/15, barabara hii imetengewa kiasi cha Shilingi milioni 10,241.37 kwa ajili ya kuendelea na kazi za ujenzi.

UJENZI WA MADARAJA YA KIRUMI, NANGOO, SIBITI, MALIGISU, KILOMBERO, KAVUU, MBUTU, RUHEKEI, RUHUHU, MOMBA, SIMIYU, WAMI, LUKULEDI II NA UNUNUZI WA EMERGENCY MABEY BRIDGE PARTS – SHILINGI MILIONI 25,500.00

151. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga Daraja la Kirumi (Mara), Daraja la Nangoo kwenye barabara ya Mingoyo – Masasi – Tunduru, Daraja la Sibiti kwenye barabara ya Ulemo – Gumanga – Sibiti, Daraja la Maligisu (Mwanza) kwenye barabara ya Bukwimba – Kadashi - Maligisu, Daraja la Kilombero kwenye barabara ya Mikumi - Ifakara – Mahenge, Daraja la Kavuu kwenye barabara ya Majimoto-Inyonga, Daraja la Mbutu kwenye barabara ya Igunga- 118

Manonga, Daraja la Ruhekei katika barabara ya Mbinga-Mbamba Bay, Daraja la Ruhuhu (Ruvuma), Daraja la Momba kwenye barabara ya Sitalike-Kilyamatundu/Kamsamba-Mlowo (Rukwa/Mbeya Border), Daraja la Simiyu kwenye barabara Mwanza – Musoma, Daraja la Wami katika barabara ya Chalinze – Segera, Daraja la Lukuledi II kwenye barabara Mtama – Kitangali – Newala na kununua Emergency Mabey Bridge Parts.

152. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, kiasi cha Shilingi milioni 1,500.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya ukarabati wa Daraja la Kirumi, Daraja la Nangoo limetengewa Shilingi milioni 500.00, Daraja la Sibiti Shilingi milioni 3,000.00, Daraja la Maligisu Shilingi milioni 200, Daraja la Kilombero Shilingi milioni 7,500.00, Daraja la Kavuu limetengewa Shilingi milioni 1,000.00, Daraja la Mbutu Shilingi milioni 5,300.00, Daraja la Ruhekei Shilingi milioni 250.00, Daraja la Momba Shilingi milioni 2,000.00, Daraja la Simiyu Shilingi milioni 1,300.00, Daraja Jipya la Wami (New Wami Bridge) Shilingi milioni 200.00 na Daraja la Lukuledi II Shilingi milioni 1,000.00. Aidha, Shilingi milioni 1,050.00 zimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa Emergency Mabey Bridge Parts, Shilingi milioni 500.00 kwa ajili ya usanifu wa daraja la Ruhuhu na Shilingi milioni 200.00 kwa ajili ya maboresho ya daraja la Selander. 119

BARABARA YA NEW BAGAMOYO (KAWAWA JCT - TEGETA KM 17.1) – SHILINGI MILIONI 14,500.00

153. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kupanua barabara hii kutoka njia mbili za sasa hadi njia nne kuanzia makutano ya barabara za Kawawa na Ali Hassan Mwinyi eneo la Morocco hadi Tegeta ili kupunguza msongamano wa magari katika barabara hiyo. Mradi huu unafadhiliwa na Serikali ya Japan kupitia Shirika la Maendeleo ya Kimataifa (JICA). Mradi huu unatekelezwa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza inahusisha mradi wa Mwenge – Tegeta (km12.9) na awamu ya pili ni mradi wa Kawawa Jct – Mwenge (km 4.2).

154. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 2,500.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 12,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na kazi za ujenzi ikiwa ni pamoja na kuhamisha miundombinu kwenye eneo la ujenzi (mabomba ya maji, nguzo na nyaya za umeme/simu n.k) sehemu ya Kawawa Jct – Mwenge (km 4.2).

BARABARA YA KYAKA –BUGENE – KASULO (KM 178) – SHILINGI MILIONI 6,037.53

155. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga barabara ya Kyaka – Bugene – Kasulo 120

(sehemu ya Kyaka-Bugene) yenye urefu wa kilometa 59.1 kwa kiwango cha lami. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Kazi za ujenzi zinaendelea. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 6,037.53 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi.

BARABARA YA ISAKA – LUSAHUNGA (KM 242) NA LUSAHUNGA - RUSUMO NA NYAKASANZA - KOBERO (KM 150)- SHILINGI MILIONI 20,520.480

156. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kufanya ukarabati wa sehemu ya Isaka – Lusahunga yenye urefu wa kilometa 242 kwa kiwango cha lami. Mradi wa ukarabati wa barabara hii unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Mradi huu umegawanyika katika sehemu mbili (2) ili kuharakisha utekelezaji: Isaka – Ushirombo (km 132) na Ushirombo – Lusahunga (km 110). Kwa sehemu ya Isaka – Ushirombo, kazi ya ukarabati ilikamilika Novemba, 2013. Kazi ya ukarabati wa sehemu ya Ushirombo – Lusahunga inaendelea.

157. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, barabara ya Isaka – Ushirombo imetengewa fedha za ndani Shilingi milioni 11,512.72 kwa ajili ya kulipa malipo ya mwisho ya Mkandarasi na Shilingi milioni 9,007.76 fedha za ndani zimetengwa kwa sehemu ya 121

Ushirombo – Lusahunga kwa ajili ya kuendelea na ukarabati.

BARABARA YA MANYONI – ITIGI – TABORA (KM 264) – SHILINGI MILIONI 21,499.57

158. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Manyoni - Itigi – Tabora kwa kuanzia sehemu ya Manyoni – Itigi - Chaya yenye urefu wa kilometa 89.35 na sehemu ya Tabora –Nyahua yenye urefu wa kilometa 85 kwa kutumia fedha za ndani. Kazi za ujenzi zinaendelea kwa sehemu zote mbili. Aidha, maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara ya Nyahua - Chaya (km 90) yanaendelea.

159. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 10,000.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi kwa sehemu ya Tabora – Nyahua na Shilingi milioni 10,299.57 kwa sehemu ya Manyoni – Itigi – Chaya. Kwa upande wa barabara ya Nyahua - Chaya (km 90) kiasi cha Shilingi milioni 1,200.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami.

BARABARA YA KOROGWE – HANDENI (KM 65) – SHILINGI MILIONI 6,356.73

160. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kuijenga kwa kiwango cha lami barabara ya 122

Korogwe – Handeni (km 65). Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Kazi za ujenzi zilikamilika Novemba, 2013. Katika mwaka wa fedha 2014/15 kiasi cha Shilingi milioni 6,356.73 kimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai ya mkandarasi.

BARABARA ZA MIKOA SHILINGI MILIONI 31,915.27

161. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kuzifanyia ukarabati barabara za Mikoa kwa kiwango cha changarawe, kujenga kwa kiwango cha lami na kujenga madaraja katika mikoa yote ya Tanzania Bara.

162. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15 kazi zilizopangwa kutekelezwa kwa upande wa barabara za mikoa ni ukarabati wa jumla ya kilometa 685 kwa kiwango cha changarawe, kujenga kilometa 78 kwa kiwango cha lami na ujenzi wa madaraja 14. Aidha, kazi ya upembuzi yakinifu kwa barabara zenye urefu wa kilometa 1,520.50 itaendelea. Kazi za ukarabati kwa kiwango cha changarawe zitafanyika katika mikoa yote ya Tanzania Bara. Orodha ya miradi ya barabara za mikoa kwa kutumia fedha za Bajeti ya Maendeleo imeonyeshwa katika Kiambatisho Na. 2.

123

BARABARA YA MWANZA/SHINYANGA BORDER – MWANZA (KM 10) SHILINGI MILIONI 50.00

163. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kuendelea na kufanya ukarabati wa sehemu zilizoharibika. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 50.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ukarabati.

BARABARA YA HANDENI – MKATA (KM 54) – SHILINGI MILIONI 4,484.75

164. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kuijenga kwa kiwango cha lami barabara ya Handeni – Mkata (km 54). Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Kazi ya ujenzi ilikamilika Machi, 2013. Katika mwaka wa fedha 2014/15 barabara hii imetengewa Shilingi milioni 4,484.75 kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai ya Mkandarasi.

BARABARA YA MWANDIGA – MANYOVU (KM 60) – SHILINGI MILIONI 500.00

165. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kuijenga barabara ya kutoka Mwandiga hadi Manyovu inayounganisha Mkoa wa Kigoma na nchi jirani ya Burundi kwa kiwango cha lami. Mradi huu uligharamiwa na Serikali ya Tanzania. Ujenzi wa barabara hii ulikamilika Oktoba, 2010. Katika mwaka wa fedha 2014/15 kiasi cha Shilingi milioni 500.00 kimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya malipo ya mwisho ya Mkandarasi. 124

DARAJA LA UMOJA – SHILINGI MILIONI 500.00

166. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu lilikuwa ni kujenga Daraja katika mto Ruvuma eneo la Mtambaswala/Negomane ili kuunganisha nchi za Tanzania na Msumbiji. Daraja hili lilijengwa kwa utaratibu wa kusanifu na kujenga (Design and Build). Mradi huu uligharamiwa na Serikali za Tanzania na Msumbiji na ulikamilika Mei, 2010. Katika mwaka wa fedha 2014/15 daraja hili limetengewa Shilingi milioni 500.00 kwa ajili ya kulipa sehemu ya malipo ya mwisho ya Mkandarasi.

BARABARA ZA KUONDOA MSONGAMANO KATIKA JIJI LA DAR ES SALAAM (KM109.35) SHILINGI MILIONI 28,945.00

167. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga, kufanya upanuzi na ukarabati wa barabara za Dar es Salaam ili kupunguza msongamano wa magari. Barabara hizo ni: Kawawa Round About-Msimbazi Valley – Jangwani/Twiga Jct (km 2.7), Jet Corner – Vituka-Devis (km 10.3), sehemu ya Ubungo – Maziwa – External, sehemu ya Tabata Dampo – Kigogo (km 2.25), Kimara – Kilungule – External (km 9.00), Mbezi – Malambamawili – Kinyerezi – Banana (km 14), Tegeta – Kibaoni – Wazo Hill – Goba – Mbezi (Morogoro Road) (km 20), Tangi 125

Bovu – Goba (km 9.00), Kimara Baruti – Msewe, Kibamba – Kisopwa, Banana – Kitunda – Kivule – Msongola (km 14.7) na Ardhi – Makongo (km 4.00). Aidha, mradi wa ujenzi wa miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka (Bus Rapid Transit Infrastructure) na vituo vyake unaendelea.

168. Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2014/15, kiasi cha Shilingi milioni 605.00 kimetengwa kwa ajili ya kukamilisha kazi zilizobakia kwa barabara ya Kawawa Round About - Msimbazi Valley – Jangwani/Twiga Jct. Shilingi milioni 1,290.00 kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai ya Mkandarasi wa barabara ya Jet Corner – Vituka - Devis Corner, Shilingi milioni 2,500.00 kwa ajili ya kuanza ujenzi barabara ya Ubungo – Maziwa – External na Tabata Dampo – Kigogo, Shilingi milioni 5,000.00 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara ya Kimara – Kilungule – External, Shilingi milioni 6,000.00 kwa ajili ya barabara ya Mbezi – Malambamawili – Kinyerezi – Banana, Shilingi milioni 5,000.00 kwa ajili ya barabara ya Tegeta – Kibaoni – Wazo Hill – Goba – Mbezi (Morogoro Road).

169. Mheshimiwa Spika, Shilingi milioni 3,000.00 zimetengwa kwa ajili ya barabara ya Tangi Bovu – Goba, Shilingi milioni 1,500.00 kwa ajili ya barabara ya Kimara Baruti – Msewe – Changanyikeni, Shilingi milioni 1,500.00 kwa ajili ya barabara ya Kibamba – Kisopwa, Shilingi 126

milioni 1,000.00 kwa ajili ya barabara Banana – Kitunda – Kivule – Msongola (km 14.7) na Shilingi milioni 1,500.00 kwa ajili ya barabara ya Ardhi – Makongo. Aidha, kiasi cha Shilingi milioni 50.00 zitatumika kufuatilia na kusimamia ujenzi wa miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka (Bus Rapid Transit Infrastructure).

BARABARA YA NDUNDU – SOMANGA (KM 60) - SHILINGI MILIONI 5,287.74

170. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga barabara sehemu ya Ndundu - Somanga yenye urefu wa kilometa 60 kwa kiwango cha lami. Mradi unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15, kiasi cha Shilingi milioni 5,287.74 fedha za ndani kimetengwa kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa barabara hii.

KIDATU - IFAKARA - LUPILO - MALINYI - LONDO - LUMECHA/SONGEA (KM 396) SHILINGI MILIONI 1,600.00

171. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Kidatu hadi Lumecha/Songea chini ya msaada wa Benki ya Maendeleo ya Afrika na mchango wa Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15 barabara hii imetengewa Shilingi milioni 100.00 fedha za 127

ndani na Shilingi milioni 1,500.00 fedha za nje kwa ajili ya kuanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.

BARABARA YA TABORA - IPOLE - KOGA – MPANDA (KM 351.40) - SHILINGI MILIONI 7,260.00

172. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga barabara ya Tabora – Ipole – Koga – Mpanda yenye urefu wa kilometa 351.40 kwa kiwango cha lami. Mradi unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 2,560.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami sehemu ya Mpanda – Koga – Ipole (km 261.40) na Shilingi milioni 4,700.00 kwa sehemu ya Tabora - Sikonge - Ipole (km 90.00).

BARABARA YA MAKUTANO - NATTA – MUGUMU/ LOLIONDO – MTO WA MBU (KM 452) – SHILINGI MILIONI 9,617.63

173. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Ujenzi wa barabara ya Makutano – Natta – Mugumu (km 125) sehemu ya Makutano – Sanzate (km 50) unaendelea. Aidha, kazi ya usanifu wa kina wa barabara ya Mto wa Mbu – Loliondo (km 213) ilikamilika mwaka 2011. 128

174. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 5,617.63 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Makutano -Sanzate (km 50) na Shilingi milioni 4,000.00 kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami sehemu ya Mto wa Mbu – Loliondo (km 213).

BARABARA YA IBANDA – ITUNGI/KIWIRA PORT (KM 26) – SHILINGI MILIONI 1,000.00

175. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kufanya ukarabati wa barabara ya Ibanda – Itungi/Kiwira Port (km 26) kwa kiwango cha lami. Barabara hii ni kiungo muhimu kwa bandari ya Itungi/Kiwira. Katika mwaka wa fedha 2014/15 kiasi cha Shilingi milioni 1,000.00 fedha za ndani kimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ukarabati wa barabara ya Ibanda – Itungi/Kiwira Port sehemu ya Kajunjumele – Kiwira Port yenye urefu wa kilomita 5.6.

BARABARA YA TANGA – HOROHORO (KM 65) – SHILINGI MILIONI 130.00

176. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Tanga – Horohoro (km 65). Mradi huu ulikamilika Oktoba, 2012. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 130.00

129

fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya malipo ya mwisho ya fidia.

BARABARA YA NZEGA – TABORA (KM 115) – SHILINGI MILIONI 13,169.34

177. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga barabara ya Nzega – Tabora (km 115) kwa kiwango cha lami. Mradi huu umegawanyika katika sehemu mbili za Nzega- Puge (km 58.8) na Puge-Tabora (km 56.10). Kazi za ujenzi kwa kiwango cha lami zinaendelea.

178. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 6,696.04 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Nzega – Puge na Shilingi milioni 6,473.30 kwa ajili ya sehemu ya Puge – Tabora.

BARABARA YA SUMBAWANGA – MPANDA - NYAKANAZI (KM 829) – SHILINGI MILIONI 28,858.72

179. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga barabara ya Sumbawanga – Mpanda – Uvinza (km 440.4) kwa kiwango cha lami. Kazi za ujenzi kwa sehemu za Sumbawanga-Kanazi (km 75), Kizi – Sitalike - Mpanda (km 36.9) na Kanazi – Kizi - Kibaoni (km 75.6) zinaendelea.

130

180. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Shilingi milioni 8,850.94 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na kazi ya ujenzi wa sehemu ya Sumbawanga- Kanazi, Shilingi milioni 8,850.94 kwa sehemu ya Kanazi – Kizi - Kibaoni na Shilingi milioni 6,617.63 kwa sehemu ya Kizi - Sitalike - Mpanda. Kiasi cha Shilingi milioni 4,539.21 kimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa sehemu ya Mpanda - Mishamo (km 100).

BARABARA YA NYANGUGE – MUSOMA (KM 183) NA MCHEPUO WA USAGARA - KISESA (KM 17) SHILINGI MILIONI 19,235.26

181. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kuikarabati barabara ya Nyanguge-Musoma (km 85.5) na kujenga kwa kiwango cha lami kilometa 17 za mchepuo barabara ya Usagara - Kisesa. Kazi za ujenzi kwa sehemu ya Simiyu/Mara Border – Musoma (km 80) zinaendelea. Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Nansio - Kisorya - Bunda sehemu ya Kisorya - Bulamba (km 51) umeanza na unaendelea. Aidha, maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Nyamuswa – Bunda yenye urefu wa kilomita 24.5 yanaendelea.

182. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, mradi umetengewa Shilingi milioni 2,500.00 kwa ajili ya kuendelea na kazi ya ukarabati wa barabara ya Nyanguge – 131

Simiyu/Mara Border (km 85.5) kiasi cha Shilingi 7,235.26 zimetengwa kwa ajili ya ukarabati wa sehemu ya Simiyu /Mara Border – Musoma (km 80). Kiasi cha Shilingi milioni 4,000.00 kimetengwa kwa sehemu ya barabara ya Kisesa – Usagara Bypass kwa ajili ya kuendelea na kazi ya ujenzi. Aidha, kiasi cha Shilingi milioni 4,500.00 kimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Nansio - Kisorya – Bunda - Nyamuswa sehemu ya Kisorya - Bunda (km 50) na kiasi cha Shilingi milioni 1,000.00 kimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi sehemu ya Nyamuswa - Bunda (km 24.5).

BARABARA YA MAGOLE - MZIHA (MAGOLE- TURIANI KM 48.8) – SHILINGI MILIONI 6,156.84

183. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga barabara ya Magole – Mziha (km 115) kwa kiwango cha lami sehemu ya Magole – Turiani yenye urefu wa kilomita 48.8. Kazi ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami inaendelea. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 6,156.84 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi sehemu ya Magole – Turiani (km 48.8).

132

UJENZI WA FLYOVERS DSM NA BARABARA ZA MAINGILIO – SHILINGI MILIONI 19,150.00

184. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga „Flyover‟ ya TAZARA kwa utaratibu wa Usanifu na Kujenga (Design and Build) ikiwa ni sehemu ya mikakati ya kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam kwenye makutano ya barabara za Mandela na Nyerere. Lengo lingine ni kuboresha makutano ya Chang'ombe, Ubungo, Uhasibu, KAMATA, Magomeni, Mwenge,Tabata/Mandela na Morocco katika jiji la Dar es Salaam.

185. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 1,000.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 15,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa „Flyover‟ ya TAZARA na Shilingi milioni 3,000.00 zimetengwa kwa ajili ya maboresho ya makutano ya Chang'ombe, Ubungo, Uhasibu, KAMATA, Magomeni, Mwenge, Tabata/Mandela na Morocco. Vilevile, katika mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) maandalizi kwa ajili ya upanuzi wa barabara ya TAZARA – JNIA (km 6.0) kuwa njia sita yataanza. Kiasi cha Shilingi milioni 150.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya maandalizi ya upanuzi wa barabara TAZARA – JNIA (km 6.0) kuwa njia sita.

133

BARABARA YA MWIGUMBI – MASWA – BARIADI – LAMADI (KM 171.8) (BARIADI- LAMADI – KM 71.8) – SHILINGI MILIONI 10,965.65

186. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga barabara ya Mwigumbi-Maswa- Bariadi-Lamadi yenye jumla ya kilometa 171.8 kwa kiwango cha lami. Kazi ya ujenzi wa sehemu ya Bariadi – Lamadi (km 71.8) inaendelea. Aidha, maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya Mwigumbi - Maswa - Bariadi (km 100) yanaendelea.

187. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, kiasi cha Shilingi milioni 6,465.65 kimetengwa kwa ajili ya kuendelea na kazi ya ujenzi wa barabara ya Bariadi – Lamadi (km 71.8) na kiasi cha Shilingi milioni 4,500.00 kimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara ya Mwigumbi - Maswa - Bariadi (km 100). Zabuni zimetangazwa kwa sehemu ya Mwigumbi – Maswa.

BARABARA YA TABORA – IPOLE - RUNGWA (IPOLE-RUNGWA – KM 95) – SHILINGI MILIONI 50.00

188. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami sehemu ya Ipole – Rungwa yenye urefu wa kilometa 95.00. Mradi huu unagharamiwa na 134

Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15 mradi huu umetengewa Shilingi milioni 50.00 kwa ajili ya kukamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.

BARABARA YA KIDAHWE – KASULU – KIBONDO - NYAKANAZI (KM 310) – SHILINGI MILIONI 10,000.00

189. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga barabara ya Kidahwe – Kasulu – Kibondo - Nyakanazi (km 310) kwa kiwango cha lami. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 10,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa kilomita 100 za barabara ya Kidahwe – Kasulu – Kibondo – Nyakanazi (km 310) kwa kiwango cha lami. Mikataba ya ujenzi kwa sehemu ya Kidahwe – Kasulu (km 50) na Nyakanazi – Kibondo (km 50) imekwishasainiwa na Makandarasi wako kwenye maeneo ya kazi (sites) kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami.

BARABARA YA KWENDA UWANJA WA NDEGE WA MAFIA (MAFIA AIRPORT ACCESS ROAD, KM 14) – SHILINGI MILIONI 2,471.17

190. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kuingia uwanja wa ndege wa Mafia (Mafia Airport Access Road) ili kutekeleza makubaliano 135

yaliyofikiwa kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Marekani kupitia Shirika la Changamoto za Milenia (MCC) ambalo limetoa fedha za ujenzi wa uwanja wa ndege wa Mafia kuhusu Serikali ya Tanzania kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Kazi ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami inaendelea. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 2,471.17 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi.

DODOMA UNIVERSITY ROAD (KM 12) – SHILINGI MILIONI 3,000.00

191. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Chuo Kikuu cha Dodoma yenye urefu wa kilomita 12. Kazi ya ujenzi kwa kiwango cha lami inaendelea. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 3,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi.

DARAJA LA KIGAMBONI NA BARABARA YA MAINGILIO YA DARAJA – SHILINGI MILIONI 7,451.56

192. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga daraja litakalounganisha jiji la Dar es Salaam na mji wa Kigamboni ikiwa ni pamoja na barabara ya maingilio ya Mjimwema – Vijibweni yenye urefu wa kilomita 10.

136

193. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 4,951.56 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na kazi ya ujenzi wa daraja, na Shilingi milioni 2,500.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara ya maingilio ya Mjimwema – Vijibweni (km 10). Mradi unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Serikali na NSSF ambapo Serikali itachangia asilimia 40 na NSSF watachangia asilimia 60 ya gharama za ujenzi.

UJENZI WA BARABARA YA SAM NUJOMA (4 KM) – SHILINGI MILIONI 21.51

194. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi lilikuwa ni kupanua barabara ya Sam Nujoma kutoka njia mbili kuwa njia nne pamoja na njia za waenda kwa miguu kuanzia Mwenge hadi Ubungo. Mradi huu umegharamiwa na Serikali ya Tanzania na kazi za ujenzi wa barabara zilikamilika Julai, 2009. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 21.51 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya malipo ya mwisho ya Mkandarasi.

137

UJENZI WA NJIA ZA MAGARI MAZITO NA MAEGESHO YA DHARURA KWA AJILI YA KUIMARISHA BARABARA KATIKA UKANDA WA KATI (PROVIDING LANE ENHANCEMENT INCLUDING CLIMBING LANES, PASSING BAYS, REST AND EMERGENCY LAY BAYS ON CENTRAL CORRIDOR) – SHILINGI MILIONI 200.00

195. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga njia za magari mazito na maegesho ya dharura kwa ajili ya kuimarisha barabara katika ukanda wa kati (providing lane enhancement including climbing lanes, passing bays, rest and emergency lay bays on central corridor. Mradi huu upo katika mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 200.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kufanya utafiti wa maeneo ya kujenga njia hizo.

UPANUZI WA BARABARA YA JNIA – PUGU (KM 8.0) KUWA NJIA SITA – SHILINGI MILIONI 150.00

196. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kupanua barabara ya PUGU sehemu ya JNIA – Pugu (km 8.0) kuwa njia sita. Mradi huu upo katika mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big 138

Results Now) na unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 150.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuanza usanifu.

UPANUZI WA BARABARA YA KIMARA – KIBAHA (KM 25.7) IKIJUMUISHA UPANUZI WA MADARAJA YA KIBAMBA, KILUVYA NA MPIJI – SHILINGI MILIONI 250.00

197. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kupanua barabara ya Kimara – Kibaha ikijumuisha madaraja ya Kibamba, Kiluvya na Mpiji. Mradi huu upo katika mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 250.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuanza usanifu.

UJENZI WA BARABARA YA KISARAWE – MLANDIZI (KM 52) – SHILINGI MILIONI 400.00

198. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga barabara ya Kisarawe – Mlandizi kwa kiwango cha lami. Mradi huu upo katika mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 400.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuanza usanifu. 139

UPANUZI WA BARABARA YA BANDARI, UJENZI WA BARABARA YA DOCKYARD NA MIVINJENI (KM 2.9) – SHILINGI MILIONI 50.00

199. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni upanuzi wa barabara ya Bandari (km 1.2), ujenzi wa barabara ya Dockyard (km 0.7) na Mivinjeni (km 1.0). Mradi huu upo katika mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 50.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi.

UJENZI WA BARABARA YA PUGU – KIFURU – MBEZI MWISHO – MPIJI MAGOE – BUNJU (KM 34) – SHILINGI MILIONI 1,000.00

200. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kupanua barabara ya Pugu – Kifuru – Mbezi Mwisho – Mpiji Magoe – Bunju (km 34) kuwa njia tatu. Mradi huu unatekelezwa katika sehemu mbili; sehemu ya kwanza ni Pugu – Kifuru – Mbezi Mwisho (km 12.7) na sehemu ya pili ni Mbezi Mwisho – Kifuru – Mpiji Magoe – Bunju (km 21.3). Mradi huu upo katika mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 500.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuanza usanifu wa sehemu ya Pugu – 140

Kifuru – Mbezi Mwisho (km 12.7). Aidha, kiasi cha Shilingi milioni 500.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuanza usanifu wa sehemu ya Mbezi Mwisho – Magoe Mpiji – Bunju (km 21.3).

UJENZI WA MIZANI KARIBU NA BANDARI YA DAR ES SALAAM – SHILINGI MILIONI 100.00

201. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga mizani mipya karibu na bandari ya Dar es Salaam. Mradi huu upo katika mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 100.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya maandalizi ya usanifu wa mizani hiyo.

BARABARA YA TUNDUMA - SUMBAWANGA (KM 224.81) – SHILINGI MILIONI 1,057.88

202. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga barabara ya Tunduma – Sumbawanga yenye urefu wa kilomita 224.81 kwa kiwango cha lami. Mradi huu unagharamiwa kwa fedha za msaada kutoka Serikali ya Marekani kupitia Millennium Challenge Corporation (MCC) na mchango wa Serikali ya Tanzania. Utekelezaji wa mradi umegawanywa katika sehemu tatu ambazo ni;-Tunduma – Ikana (km 63.7); Ikana – Laela (km 64.2); Laela – Sumbawanga (km 95.3) na sehemu ya Tunduma mjini (km 1.6). 141

203. Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 17.0 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuhamisha miundombinu katika eneo la ujenzi na usimamizi kwa sehemu ya Tunduma – Ikana, Shilingi milioni 17.0 kwa sehemu ya Ikana-Laela, Shilingi milioni 23.88 kwa sehemu ya Laela – Sumbawanga na kiasi cha Shilingi milioni 1,000.00 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa sehemu ya Tunduma mjini (km 1.6).

BARABARA YA KAGOMA – LUSAHUNGA (KM 154) – SHILINGI MILIONI 9,600.00

204. Mheshimiwa Spika, mradi huu ni sehemu ya barabara ya Mutukula – Bukoba – Biharamulo – Lusahunga yenye urefu wa kilometa 294. Ujenzi wa sehemu ya barabara ya Mutukula – Muhutwe – Kagoma ulikamilika Septemba 2004 chini ya ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Mfuko wa OPEC. Awali Benki ya Maendeleo ya Afrika ilitoa mkopo wa ujenzi wa sehemu ya Kagoma – Lusahunga (km 154) kwa kiwango cha lami. Baada ya Mkandarasi China State Construction Engineering Corporation Ltd (CSCEC) kushindwa kutekeleza matakwa ya mkataba wa awali na kuondolewa, mkataba mpya wa kumalizia kazi za ujenzi wa barabara ya Kagoma – Lusahunga (km154) kwa kiwango cha lami ulisainiwa tarehe 18 Juni, 2009 na kazi za ujenzi zimekamilika

142

Desemba, 2013. Kazi za ujenzi zinagharamiwa na Serikali ya Tanzania.

205. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa fedha 2014/15 barabara ya Kagoma – Lusahunga (km154) imetengewa kiasi cha Shilingi milioni 9,600.00 kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai ya Mkandarasi.

BARABARA YA ARUSHA – NAMANGA (KM 105) - SHILINGI MILIONI 4,517.12

206. Mheshimiwa Spika, mradi wa barabara ya Arusha – Namanga (km 105) – Athi River ni sehemu ya mradi wa kikanda ya Jumuiya ya Afrika Mashariki unaojumuisha nchi za Tanzania na Kenya ambao unafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika Japan Bank for International Cooperation (JBIC) kwa kushirikiana na Serikali za Tanzania na Kenya. Lengo la mradi ni kukarabati barabara hii kwa kiwango cha lami. Kazi za ujenzi zimekamilika Desemba, 2012. atika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 2,228.12 fedha za ndani na Shilingi milioni 2,289.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai ya Mkandarasi.

143

BARABARA YA SINGIDA - BABATI – MINJINGU - ARUSHA (KM 321.5) - SHILINGI MILIONI 10,444.83

207. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga kwa kiwango cha lami sehemu ya Singida - Babati -Minjingu yenye urefu wa kilomita 223.5 na kukarabati kwa kiwango cha lami sehemu ya Minjingu-Arusha yenye urefu wa kilometa 98.

208. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa barabara ya Singida - Babati - Minjingu umegawanywa katika sehemu tatu za Singida – Katesh (km 65.1), Katesh – Dareda (km 73.8 ) na Dareda – Babati – Minjingu (km 84.6). Kazi za ujenzi zilikamilika Agosti 2012. Miradi hii imegharamiwa na ADB, JICA na Serikali ya Tanzania. Aidha, ukarabati wa sehemu ya Minjingu-Arusha (km 98) unagharimiwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Dunia na kazi za ukarabati zinaendelea.

209. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15 kiasi cha Shilingi milioni 444.83 fedha za ndani na Shilingi milioni 10,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ukarabati wa barabara ya Minjingu hadi Arusha yenye urefu wa kilomita 98.

144

BARABARA YA DAR ES SALAAM – MBAGALA (KILWA ROAD) – GEREZANI (SEHEMU YA KAMATA – BENDERA TATU KM 1.5) – SHILINGI MILIONI 8,000.00

210. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kukarabati na kupanua barabara ya lami sehemu ya Gerezani (KAMATA – Bendera Tatu) kutoka njia mbili za sasa hadi njia nne chini ya msaada kutoka Serikali ya Japan na mchango wa Serikali ya Tanzania. Usanifu wa kina na utayarishaji wa nyaraka za zabuni zimekamilika. Kazi za kuhamisha miundombinu iliyoko kwenye eneo la ujenzi zinaendelea. Aidha, taratibu za kumtafuta Mkandarasi zinaendelea. Katika mwaka wa fedha 2014/15 mradi huu umetengewa Shilingi milioni 2,000.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 6,000.00 fedha za nje kwa ajili ya kukamilisha ulipaji fidia na kuanza ujenzi wa sehemu ya KAMATA – Bendera Tatu (km 1.5)

BARABARA YA MSIMBA – RUAHA/IKOKOTO MAFINGA (KM 517.40) – SHILINGI MILIONI 43,284.28

211. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya ukarabati wa barabara ya lami ya Dar es Salaam – Tunduma (TANZAM). Ukarabati wa sehemu ya Iyovi - Kitonga Gorge (km 86.3), Ikokoto - Iringa (km 60.9) na barabara ya kuingia Iringa Mjini (km 2.1) 145

ulikamilika Septemba 2012. Ukarabati wa barabara ya Iringa - Mafinga (km 68.9) ulikamilika Agosti 2013. Mradi huu unagharamiwa kwa mkopo kutoka Serikali ya Denmark pamoja na mchango wa Serikali ya Tanzania. Aidha, maandalizi ya kuanza ukarabati kwa kiwango cha lami wa barabara ya Mafinga - Igawa (km 137.9) yanaendelea kwa mkopo kutoka Benki ya Dunia. Maandalizi kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa kutumia fedha za ndani barabara za Rujewa- Madibira-Mafinga (km152), Njombe-Ndulamo- Makete (km 109), Njombe-Lupembe-Madeke (km 125).

212. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 4,016.513 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai ya mkandarasi barabara ya Iringa – Mafinga (Km 68.9). Jumla ya Shilingi milioni 200.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 34,644.527 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya ukarabati wa barabara ya Mafinga-Igawa yenye urefu wa kilometa 137.9. Aidha, Shilingi milioni 500 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kufanya maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Igawa-Madibira-Mafinga, Shilingi milioni 2,823.24 kwa ajili ya ujenzi wa Njombe-Ndulamo-Makete, na Shilingi milioni 1,000.00 kwa ajili ya ujenzi wa Njombe- Lupembe-Madeke.

146

BARABARA YA KOROGWE – MKUMBARA - SAME (KM 172)- SHILINGI MILIONI 15,200.00

213. Mheshimiwa Spika, barabara ya Korogwe - Mkumbara –Same (km 172) ambayo ni sehemu ya barabara ya Segera – Moshi – Arusha ambayo ilijengwa kwa kiwango cha lami katika miaka ya sabini imechakaa na kuhitaji kufanyiwa ukarabati. Mradi huu wa ukarabati unafadhiliwa na Benki ya Dunia. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 200.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 15,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na kazi ya ukarabati wa barabara hii.

214. Mheshimiwa Spika, barabara ya Korogwe – Mkumbara - Same (km 172) imegawanywa katika sehemu mbili kama ifuatavyo:

(i) Korogwe – Mkumbara (km 76)

Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 100.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 5,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili kuendelea na kazi ya ukarabati wa barabara ya Korogwe – Mkumbara.

147

(ii) Mkumbara – Same (km 96)

Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 100.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 10,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili kuendelea na kazi ya ukarabati wa barabara ya Mkumbara - Same.

BARABARA YA MBEYA - MAKONGOLOSI (KM 115) – SHILINGI MILIONI 13,340.12

215. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga barabara ya Mbeya hadi Makongolosi (km 115) kupitia Chunya kwa kiwango cha lami. Ujenzi wa barabara hii umegawanyika katika sehemu tatu ambazo ni: Mbeya – Lwanjilo (km 36); Lwanjilo - Chunya (km 36) na Chunya-Makongolosi (km 43). Ujenzi wa sehemu ya Mbeya – Lwanjilo (km 36) ulianza Septemba, 2007 na ulitegemewa kukamilika Machi, 2010. Hata hivyo, mkataba wa ujenzi ulisitishwa Aprili 2009 baada ya Mkandarasi a awali kushindwa kutimiza matakwa ya mkataba. Mkataba na Mkandarasi mwingine ulisainiwa na kazi za ujenzi zinaendelea. Aidha, kwa sehemu ya Lwanjilo - Chunya (Km 36) kazi za ujenzi zinaendelea pia.

216. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 6,528.78 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi kwa sehemu ya Mbeya-Lwanjilo, Shilingi 148

milioni 5,008.00 kwa sehemu ya Lwanjilo- Chunya na Shilingi milioni 1,495.50 kwa sehemu ya Chunya – Makongolosi. Aidha, Shilingi milioni 307.84 zimetengwa kwa ajili ya kumalizia deni la Mhandisi Mshauri aliyefanya kazi ya usanifu wa kina wa sehemu ya Makongolosi – Rungwa – Itigi – Mkiwa.

BARABARA YA CHALINZE – SEGERA - TANGA (KM 248) – SHILINGI MILIONI 3,500.00

217. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kuifanyia ukarabati na upanuzi barabara ya Chalinze - Segera hadi Tanga. Utekelezaji wa mradi umegawanyika katika sehemu mbili ambazo ni: Chalinze-Kitumbi (km 125) na Kitumbi-Segera-Tanga (km 120). Ujenzi wa sehemu ya Chalinze-Kitumbi ulikamilika Oktoba, 2010. Ukarabati wa sehemu ya Kitumbi-Segera-Tanga ulikamilika Februari, 2014. Aidha, kazi ya ujenzi wa sehemu ya Msoga – Msolwa (Chalinze Bypass) zinaendelea.

218. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 2,500.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai ya Mkandarasi wa sehemu ya Kitumbi-Segera-Tanga. Aidha, Shilingi milioni 1,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara ya Msoga – Msolwa (Chalinze Bypass).

149

BARABARA YA ITONI – LUDEWA – MANDA (KM 211) – SHILINGI MILIONI 4,400.00

219. Mheshimiwa Spika, Lengo la mradi huu ni kujenga barabara ya Itoni – Ludewa – Manda kwa kiwango cha lami. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 4,400.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa sehemu ya kilometa 50 za barabara ya Itoni – Ludewa – Manda.

DARAJA LA RUVU CHINI (LOWER RUVU BRIDGE) – SHILINGI MILIONI 700.00

220. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga daraja jipya katika Mto Ruvu kwenye barabara ya Bagamoyo – Msata. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 700.00 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la Ruvu Chini.

BARABARA YA DODOMA – IRINGA (KM 260) – SHILINGI MILIONI 21,739.31

221. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Dodoma – Mtera – Iringa (km 260). Mradi huu unagharamiwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Shirika la Misaada ya Kimataifa la Japan (JICA). Utekelezaji wa mradi umegawanywa katika sehemu tatu za Iringa-Migori (km 95.2), Migori- 150

Fufu Escarpment (km 93.8) na Fufu Escarpment- Dodoma (km 70.9).

222. Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2014/15, kiasi cha Shilingi milioni 615.68 fedha za ndani na Shilingi milioni 10,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi sehemu ya Iringa - Migori, Shilingi milioni 538.73 ` fedha za ndani na Shilingi milioni 5,000.00 fedha za nje kwa ajili ya sehemu ya Migori – Fufu Escarpment na Shilingi milioni 584.90 fedha za ndani na Shilingi milioni 5,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kugharamia ujenzi wa sehemu hiyo ya barabara.

BARABARA YA DODOMA – BABATI (KM 261) – SHILINGI MILIONI 28,392.41

223. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Dodoma – Kondoa – Babati (km 261). Utekelezaji wa mradi huu umegawanyika katika sehemu tatu ambazo ni: Dodoma-Mayamaya (km 43.65), Mayamaya-Bonga (km188.15) na Bonga- Babati (km 19.2).

224. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa barabara sehemu ya Dodoma-Mayamaya (km 43) unaendelea. Ujenzi wa sehemu ya Bonga – Babati (km 19.2) ulikamilika Aprili 2013. Ujenzi wa sehemu hizi mbili unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Aidha, kazi za ujenzi kwa kiwango

151

cha lami sehemu ya Mayamaya-Bonga (km 188.15) zinaendelea kwa fedha za mkopo kutoka ADB na JICA.

225. Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2014/15, kiasi cha Shilingi milioni 5,006.15 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Dodoma – Mayamaya na Shilingi milioni 2,386.26 wa sehemu ya Bonga – Babati zimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai ya Mkandarasi.

226. Mheshimiwa Spika, Shilingi milioni 1,000.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 20,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kundelea na ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya Mayamaya – Bonga ambayo imegawanywa katika sehemu mbili kama ifuatavyo:

(i) Mayamaya - Mela (km 99.35) Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 500.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 10,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi.

(ii) Mela - Bonga (km 88.80)

Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 500.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 10,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi.

152

MASASI- SONGEA – MBAMBA BAY (KM 659.7) – SHILINGI MILIONI 68,383.08

227. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kuijenga kwa kiwango cha lami barabara ya Masasi- Songea – Mbamba Bay (km 659.7). Utekelezaji wa mradi umegawanyika katika sehemu za Masasi – Mangaka (km 54), Mangaka – Nakapanya - Tunduru (km 146), Mangaka- Mtambaswala (km 65.5), Namtumbo - Kilimasera (km 60.7), Kilimasera-Matemanga (km 68.2), Matemanga –Tunduru (km 58.7), Mbinga - Mbamba Bay (km 66) na Masasi - Newala – Mtwara (km 209).

228. Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2014/15, Shilingi milioni 533.88 fedha za ndani na Shilingi milioni 10,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Mangaka- Nakapanya na Shilingi milioni 532.57 fedha za ndani na Shilingi milioni 10,000.00 fedha za nje kwa sehemu ya Nakapanya – Tunduru. Shilingi milioni 532.93 fedha za ndani na Shilingi milioni 10,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa sehemu ya Mangaka-Mtambaswala na Shilingi milioni 567.32 fedha za ndani na Shilingi milioni 10,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi kwa sehemu ya Tunduru-Matemanga. Kwa sehemu ya Matemanga-Kilimasera, Shilingi milioni 679.20 fedha za ndani na Shilingi milioni 153

10,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili kuendelea na ujenzi.

Aidha, Shilingi milioni 679.18 fedha za ndani na Shilingi milioni 10,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya sehemu ya Kilimasera – Namtumbo. Fedha zilizotengwa kwa ajili ya gharama za usimamizi na ufuatiliaji wa mradi katika kipindi cha uangalizi ni Shilingi milioni 17.00 fedha za ndani kwa barabara ya Songea – Namtumbo na Shilingi milioni 17.00 fedha za ndani kwa barabara ya Peramiho – Mbinga. Kiasi cha Shilingi milioni 2,324.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami sehemu ya Mbinga-Mbamba Bay, na Shilingi milioni 2,500.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kugharimia usanifu na maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Masasi - Newala – Mtwara.

UJENZI WA MAKAO MAKUU YA WAKALA WA BARABARA – SHILINGI MILIONI 2,934.35

229. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga Makao Makuu ya Wakala wa Barabara pamoja na kuanza ujenzi wa Ofisi za mikoa ya Dar es Salaam, Katavi, Geita, Simiyu, Njombe na Lindi. Mradi huu unagharamiwa kwa fedha za ndani. Usanifu wa jengo la Makao Makuu ya Wakala umekamilika. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni

154

2,934.35 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuanza kazi ya ujenzi.

UJENZI WA BARABARA YA KUINGIA UONGOZI INSTITUTE SHILINGI MILIONI 1,500.00

230. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga barabara ya kutoka barabara ya Bagamoyo kuingia kwenye Chuo cha Uongozi pamoja na barabara zilizoko ndani ya Chuo hicho. Katika mwaka wa fedha 2014/15, jumla ya Shilingi milioni 1,500.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuanza maandalizi ya ujenzi wa barabara ya kutoka barabara ya Bagamoyo kuingia Chuo cha Uongozi pamoja na barabara zilizoko ndani ya Chuo hicho.

USALAMA BARABARANI NA MAZINGIRA

Usalama Barabarani - Shilingi. Milioni 4,899.00

231. Mheshimiwa Spika, mradi huu una lengo la kuratibu na kuimarisha shughuli za usalama barabarani na kudhibiti uzito wa magari yanayotumia barabara zetu.

232. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, kiasi cha Shilingi milioni 1,399 fedha za ndani na Shilingi milioni 3,500 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza miradi

155

mbalimbali ya usalama barabarani kama ifuatavyo:-

(i) Mradi wa ujenzi wa mizani 8 za kisasa zinazopima uzito wa gari likiwa katika mwendo (Weigh In Motion) umepangwa kutekelezwa chini ya Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN). Katika mwaka wa fedha 2014/15 mizani moja itaanza kujengwa katika eneo la Mikese ambapo imetengewa Shilingi milioni 208 fedha za ndani; (ii) Ujenzi wa vituo vya pamoja vya ukaguzi (One Stop Inspection Stations) zimetengwa Shilingi milioni 815 fedha za ndani; (iii) Uanzishwaji wa Wakala wa Usalama Barabarani nchini (National Road Safety Agency) umetengewa Shilingi milioni 200 fedha za ndani na Shilingi milioni 1000 fedha za nje; (iv) Mapitio ya marekebisho ya Sheria ya Usalama Barabarani zimetengwa Shilingi milioni 45 fedha za ndani na Shilingi milioni 1000 fedha za nje. (v) Ukaguzi wa Usalama Barabarani (Road Safety Audit) umetengewa Shilingi milioni 120 fedha za ndani; na (vi) Uwekaji Mfumo wa Upatikanaji na Utoaji Taarifa za Ajali Barabarani (Road Accident Information System) umetengewa Shilingi milioni 11 fedha za ndani na Shilingi milioni 1500 fedha za nje. 156

Usalama, Mazingira na Marekebisho ya Mfumo - Shilingi Milioni 720.00

233. Mheshimiwa Spika, mradi huu una lengo la kugharamia shughuli za Usalama na Mazingira pamoja na Marekebisho ya Mfumo wa utekelezaji wa shughuli katika maeneo haya. Mradi huu unagharamiwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Tanzania na DANIDA. Katika Mwaka wa fedha 2014/15 mradi huu umetengewa jumla Shilingi milioni 720.00 ambapo Shilingi milioni 370 ni fedha za ndani na Shilingi milioni 350 fedha za nje. Kiasi cha Shilingi milioni 110 za ndani na Shilingi milioni 100 za nje zimetengwa kwa ajili ya kutoa Elimu ya Usalama Barabarani kwa shule za nyanda za juu kusini kwa mikoa ya Rukwa, Katavi, Ruvuma, Mbeya na Iringa. Aidha, kiasi cha Shilingi milioni 240 za ndani na Shilingi milioni 150 za nje zimetengwa kwa ajili ya kutoa Elimu ya Usalama Barabarani kwa umma kupitia vyombo vya habari kama radio, runinga, magazeti na vipeperushi. Shilingi milioni 20 za ndani na Shilingi milioni 100 za nje zimetengwa kwa ajili ya kuwajengea uwezo watumishi (capacity building).

Menejimenti na Utunzaji wa Mazingira – Shilingi Milioni 502.34

234. Mheshimiwa Spika, mradi huu una lengo la kuelimisha na kuwezesha utekelezaji wa sheria ya mazingira katika sekta ya Ujenzi. 157

Vilevile kuandaa programu mbalimbali za udhibiti wa uchafuzi wa kimazingira unaosababishwa na shughuli zitokanazo na kazi za ujenzi.

235. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Shilingi milioni 301.84 fedha za ndani na Shilingi milioni 200. 50 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya:

(i) Kusimamia utekelezaji na uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004 kwa miradi ya ujenzi inayotekelezwa na itakayotekelezwa; (ii) Kutoa mafunzo kuhusu tathmini na usimamizi wa mazingira katika sekta ya ujenzi kwa wahandisi na mafundi sanifu kutoka TANROADS, TEMESA, TBA, Vikosi vya Ujenzi na wadau mbalimbali katika sekta ya Ujenzi; (iii) Kutoa mafunzo kuhusu utumiaji na usimamizi wa mazingira katika sekta ya ujenzi kwa Wakurugenzi na Mameneja kutoka TANROADS, TEMESA, TBA Vikosi vya Ujenzi na wadau mbalimbali katika sekta ya Ujenzi. (iv) Kuandaa programu za udhibiti wa uchafuzi wa mazingira katika sekta (pollution control programme) ikiwa ni pamoja na kufanya mafunzo ya kuzuia utupaji taka ovyo kando ya 158

barabara na kuandaa mfumo wa kutunza na kuhifadhi mazingira.

FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA KWA MWAKA WA FEDHA 2014/15

236. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Mfuko wa Barabara unatarajiwa kukusanya jumla ya Shilingi 751,700,000,000.00. Kati ya fedha hizo, Wizara ya Ujenzi na Taasisi zake imetengewa jumla ya Shilingi 526,200,400,000.00 na Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI imetengewa jumla ya Shilingi 225,499,600,000.00.

237. Mheshimiwa Spika, katika fedha zilizotengwa chini ya Wizara ya Ujenzi ambazo ni Shilingi 526,200,400,000.00, TANROADS imetengewa Shilingi 469,494,900,000.00 kwa ajili ya matengenezo ya barabara na Wizara ya Ujenzi imetengewa Shilingi 52,166,100,000.00 kwa ajili ya kazi za ukarabati wa barabara, kazi za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara, ukarabati na ununuzi wa vivuko, usalama barabarani pamoja na usimamizi na ufuatiliaji wa miradi hiyo. Aidha, Shilingi 4,539,400,000.00 zitatumika kugharamia uendeshaji wa Bodi ya Mfuko wa Barabara.

238. Mheshimiwa Spika, fedha za Mfuko wa Barabara zilizotengwa kwa ajili ya Wizara ya

159

Ujenzi zitatumika kutekeleza miradi kama ifuatavyo:-

(i) Miradi ya Barabara za Mikoa ambayo imetengewa Shilingi 30,090,836,592.11

(ii) Miradi ya Barabara Kuu ambayo imetengewa Shilingi 13,572,928,972.66.

(iii) Miradi ya vivuko imetengewa jumla ya Shilingi 4,722,374,362.29. Kati ya fedha hizo Shilingi 3,138,730,000.00 ni kwa ajili ya ununuzi wa Kivuko cha Pangani na maegesho ya kivuko cha Dar es Salaam – Bagamoyo, Shilingi 1,348,644,362.29 zimetengwa kwa ajili ya ukarabati na matengenezo ya vivuko na Shilingi 235,000,000.00 ni kwa ajili ya ufuatiliaji wa miradi.

(iv) Usimamizi na ufuatiliaji wa miradi Shilingi 2,078,327,261.98.

(v) Masuala ya Usalama Barabarani na Mazingira Shilingi 1,701,632,810.96.

160

Mchanganuo wa fedha za Mfuko wa Barabara zilizotengwa kwa ajili ya Wizara ya Ujenzi umeonyeshwa katika Kiambatanisho Na. 3.

MAELEZO YA MIRADI YA BARABARA INAYOTEKELEZWA KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA KWA MWAKA WA FEDHA 2014/15

(i) MIRADI YA BARABARA KUU ITAKAYOFANYIWA UPEMBUZI YAKINIFU NA USANIFU WA KINA

239. Mheshimiwa Spika, fedha zilizotengwa kwa mwaka wa fedha 2014/15 kutoka Mfuko wa Barabara kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na ujenzi ni Shilingi 13,572,928,972.66 kama ifuatavyo: -

Barabara ya Bagamoyo – Saadani - Tanga (Km 178) – Shilingi Milioni 1,488.144

240. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga barabara ya Bagamoyo – Saadani – Tanga kwa kiwango cha lami. Mradi huu utafadhiliwa na ADB na JICA kupitia Secretariat ya Jumuia ya Afrika Mashariki ikiwa ni sehemu ya mradi wa Malindi- Lungalunga/Horohoro-Tanga-Bagamoyo. Kwa upande wa Tanzania kazi ya upembuzi yakinifu imekamilika. Kazi ya usanifu wa kina na utayarishaji wa nyaraka za zabuni inaendelea na 161

inatarajiwa kukamilika mwaka wa fedha 2014/15.

Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 1,488.144 za ndani zimetengwa kwa ajili ya kumlipa Mhandisi Mshauri anayefanya usanifu wa kina na utayarishaji wa nyaraka za zabuni.

Barabara ya Sumbawanga – Matai – Kasanga/ Kasesya 162km) (Matai – Kasesya 50km) - Shilingi Milioni 100.00

241. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga barabara ya Sumbawanga – Matai/Kasanga – Kasesya kwa kiwango cha lami. Ujenzi wa sehemu ya Sumbawanga-Matai- Kasanga Port (km112) kwa kiwango cha lami unaendelea. Usanifu wa kina kwa sehemu ya Matai-Kasesya (km 50) unaendelea. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 100.00 zimetengwa kwa ajili ya kumlipa Mhandisi Mshauri atakayefanya usanifu wa kina ikiwa ni pamoja na utayarishaji wa Nyaraka za Zabuni.

162

Mafunzo ya Kitaalamu (Training and Technical Assistance) kwa watumishi wa TANROADS - Shilingi Milioni 100.00

242. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kuendelea kutoa mafunzo ya kitaalam kwa wafanyakazi wa TANROADS. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 100.00 zimetengwa kwa ajili ya kuwapatia mafunzo wafanyakazi wa TANROADS kwenye maeneo yanayohitaji utaalamu maalum.

Barabara ya Ifakara– Mahenge (Km 67) - Shilingi Milioni 200.00

243. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Ifakara – Mahenge. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 200.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Barabara ya Kibondo – Mabamba (Km 35) - Shilingi Milioni 200.00

244. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kibondo- Mabamba. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi

163

milioni 200.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Barabara ya Mpemba – Isongole (Km 49) - Shilingi Milioni 200.00

245. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Mpemba- Isongole. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 200.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Barabara ya Omugakorongo – Kigarama - Murongo (Km 105) Shilingi Milioni 300.00

246. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 300.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Barabara ya Kyaka – Bugene – Kasulo (178 Km) – Sehemu Ya (Bugene-Kasulo Km 124) Shilingi Milioni 300.00

247. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Kyaka – Bugene – Kasulo yenye urefu wa kilomita 178. Barabara hii imepangwa kujengwa kwa awamu. Awamu ya kwanza inahusu ujenzi 164

wa sehemu ya Kyaka-Bugene (km 59.1). Kazi ya ujenzi kwa kiwango cha lami inaendelea. Awamu ya pili itahusu upembuzi yakinifu na usanifu na ujenzi wa sehemu ya Bugene-Kasulo yenye urefu wa kilometa 124. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania.

248. Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 300.00 zimetengwa kutoka Mfuko wa Barabara kwa ajili ya kuanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Bugene- Kasulo yenye urefu wa km 124.

Barabara ya Handeni - Kiberashi - Kijungu - Kibaya - Njoro - Olboloti - Mrijo Chini - Dalai - Bicha - Chambalo - Chemba - Kwamtoro - Singida Km 460 (FS & DD)

249. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina barabara ya Handeni – Kiberashi – Kondoa kwa lengo la kuijenga kwa kiwango cha lami. Kazi za usanifu zinaendelea na zinatarajiwa kukamilika katika kipindi cha Mwaka wa fedha 2014/15. Katika mwaka wa fedha 2014/15, fedha hazikutengwa kwa ajili ya mradi huu kwa kuwa fedha zilizotengwa mwaka wa fedha 2013/14 Shilingi milioni 900 zinatosha kumlipa Mhandisi Mshauri pindi atakapokamilisha usanifu wa kina.

165

Barabara ya Mbezi (Morogoro Road) – Malambamawili – Kinyerezi – Banana - Shilingi Milioni 700.00

250. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kuanza maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Mbezi (Morogoro Road) – Malambamawili – Kinyerezi – Banana. Lengo la ujenzi wa barabara hii ni kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 700.00 zimetengwa kutoka Mfuko wa Barabara kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami.

Daraja Jipya la Wami - Shilingi Milioni 300.00

251. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga daraja jipya katika mto Wami kwenye barabara ya Chalinze-Segera ili kuboresha usalama katika daraja hilo. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 300.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina pamoja na utayarishaji wa nyaraka za zabuni.

Barabara ya Kidatu – Ifakara – Lupilo – Malinyi – Londo – Lumecha (Km 396) - Shilingi Milioni 50.00

252. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu 166

wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Mradi huu unafadhiliwa kwa msaada wa Benki ya Maendeleo ya Afrika na mchango wa Serikali ya Tanzania. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 50.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili kufuatilia na kusimamia kazi hiyo.

Road Flyovers in Dar Es Salaam - Shilingi Milioni 100.00

253. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kulipa fidia kwa mali na kuhamisha miundombinu ya huduma za kijamii zitakazoathirika na ujenzi wa “flyover” katika eneo la TAZARA. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 100.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Barabara ya Mtwara – Newala – Masasi (Km 209) - Shilingi Milioni 300.00

254. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kumalizia usanifu wa kina, kuandaa nyaraka za zabuni na kutangaza zabuni kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 300.00 za ndani zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

167

Barabara ya Kolandoto – Lalago – Mwanhuzi – Matala –Oldeani Jct (Km 328) Shilingi Milioni 700.00

255. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 700.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Vifaa vya Maabara, Ufuatiliaji na Usimamizi wa Kazi za Ujenzi wa Barabara (Central Materials Laboratory) - Shilingi Milioni 526.00

256. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni ununuzi wa vifaa vya Maabara, usimamizi na ufuatiliaji wa ujenzi wa miradi ya barabara ili kuhakikisha ujenzi huo unakidhi viwango vilivyowekwa. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 526.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Barabara ya Mwanangwa - Misasi - Salawe - Kahama (Km 149) - Shilingi Milioni 200.00

257. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 200.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo. 168

Barabara ya Itoni - Ludewa - Manda (Km 211) - Shilingi Milioni 1,400.00

258. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 1,400.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Barabara ya Arusha - Kibaya - Kongwa (Km 430) - Shilingi Milioni 250.61

259. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 250.61 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Barabara ya Musoma - Makojo - Busekela Road (Km 92) - Shilingi Milioni 400.00

260. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 400.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

169

Barabara ya Nyamirembe Port – Katoke (Km 50) - Shilingi Milioni 150.00

261. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 150.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Miradi ya Kupunguza Msongamano katika jiji la DSM (Decongestion of DSM Roads) – Shilingi Milioni 3,058.175

262. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kupunguza msongamano katika barabara za jiji la Dar es Salaam. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi miloni 3,058.175 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Ufuatiliaji na Usimamizi wa Kazi za Ujenzi wa Barabara na Ununuzi wa Gari (TANROADS) - Shilingi Milioni 400.00

263. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kuweka mfumo wa kusimamia, kufuatiliaji na kutathimini kazi za miradi ya barabara ili kuona kama inakidhi viwango, mahitaji ya Mpango wa Miaka Mitano wa Serikali, Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now- BRN), Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010, Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 170

2025, Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania (MKUKUTA), Sera ya Uchukuzi (2003) na Mpango Mkakati wa Wakala ikiwa ni pamoja na kutathimini miradi inayofadhiliwa na Wahisani mbalimbali. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 400.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Ufuatiliaji na Usimamizi wa Miradi (Monitoring and Other Related Activities) na Ununuzi wa Gari- Shilingi Milioni 900.00

264. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya usimamizi na ufuatiliaji wa miradi ya barabara. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 900.00 zimetengwa kwa ajili ya wataalamu wa Wizara watakaohusika na kazi hiyo.

Kupanua Barabara kwenye Maeneo yenye Miinuko Makalai (Provision of Escape Ramps for Long Steep Grades and Climbing Lanes along Major Trunk Roads) - Shilingi Milioni 150.00

265. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa Escape Ramps na Climbing Lanes katika barabara kuu. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 150.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo. 171

Kuboresha Mwongozo wa Usanifu [Design Manual (1989)] na Mwongozo na Uchambuzi wa Vigezo vya Kiuchumi (Economic Analysis Manuals for TANROADS) – Shilingi Milioni 300.00

266. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kuboresha Draft Design Manual ya mwaka 1989 ili kukidhi mahitaji ya sasa na kuandaa Technical Specifications for Bridge Works na Mwongozo wa kufanya tathmini za kiuchumi za barabara (Economic Appraisal Manual). Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Draft Road Manual (1989) imeandikwa upya kulingana na mahitaji ya sasa, kwa kushirikiana na Mamlaka ya Barabara wa Norway (Norwegian Public Road Administration).

267. Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 300.00 zimetengwa kwa ajili ya kumalizia sehemu ya deni la Mhandisi Mshauri (Norwegian Public Road Administration) na kuanza kuandaa „Economic Appraisal Manual‟. Aidha, Maandalizi ya Economic Appraisal Manual yapo katika ya hatua ya manunuzi ya Mtaalamu Mwelekezi.

172

Usimamizi wa Miradi ya Upembuzi yakinifu na Usanifu wa kina wa Barabara Kuu na za Mikoa na Matayarisho ya Bajeti na Mpango Mkakati wa TANROADS Shilingi Milioni 175.00

268. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kusimamia miradi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina pamoja na matayarisho ya bajeti na mpango mkakati wa miradi ya barabara kuu na za Mikoa. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 175.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Kufanya Mapitio ya Mfumo wa Utendaji wa TANROADS na Kushauri Hatua za Kuchukua ili Kuboresha Mapungufu Yatakayoainishwa (High Level Business Process Mapping - BPM) Shilingi Milioni 175.00

269. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya mapitio ya mfumo wa utendaji wa TANROADS na kuchukua hatua za uboreshaji wa utendaji kazi. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 175.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

173

Kufanya Mapitio ya Gharama za Uendeshaji wa Magari (Vehicle Operating Costs) Pamoja na Mafunzo Kuhusu Mfumo wa Kufanya Tathmini za Kiuchumi na Kihandisi (HDM-4) - Shilingi Milioni 175.00

270. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kufanya mapitio ya gharama za uendeshaji wa magari kwa ajili ya kutumika katika kufanya upembuzi yakinifu wa barabara na kujenga uwezo wa wataalam wanaotumia mifumo ya kufanya tathmini za kiuchumi na kihandisi za barabara (HDM-4). Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 175.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Kuweka Mifumo ya Kompyuta (Software) kwa ajili ya Usanifu wa Barabara na Kuandaa Mipango ya Usafiri (Highway /Transport Planning) – Shilingi Milioni 175.00

271. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kuweka mifumo ya Kompyuta (software) kwa ajili ya kuandaa mipango ya Usafiri na kufanya usanifu wa barabara na kutoa mafunzo kwa wataalam kwa ajili ya utumiaji wa mifumo hiyo. Katika mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya Shilingi milioni 175.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

174

(ii) BARABARA ZA MIKOA ZITAKAZOTEKELEZWA KWA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA

272. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, kazi zilizopangwa kutekelezwa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara ni kufanya ukarabati wa jumla ya kilometa 914.80 kwa kiwango cha changarawe na kujenga kilometa 20.8 kwa kiwango cha lami. Kazi za ukarabati kwa kiwango cha changarawe zitafanyika katika Mikoa yote hapa nchini. Kazi ya upembuzi yakinifu itahusisha kilometa 833.4. Aidha, madaraja 14 yatajengwa katika mikoa ya Dodoma (1), Kigoma (4), Kilimanjaro (1), Mtwara (1), Mwanza (2), Lindi (1), Simiyu (1), Singida (1) na Ruvuma (2). Kiasi cha Shilingi 30,090,836,592.11 kitatumika kutekeleza miradi hiyo. Orodha ya miradi ya barabara za mikoa itakayotekelezwa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara imeonyeshwa katika Kiambatisho Na. 4.

MPANGO WA MATENGENEZO YA BARABARA KWA MWAKA WA FEDHA 2014/15

273. Mheshimiwa Spika, fedha za matengenezo ya barabara kuu na barabara za mikoa kwa mwaka wa fedha 2014/15 kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara ni jumla ya Shilingi 469,494,900,00.00. Mchanganuo wa mpango huo ni kama ifuatavyo: - 175

(a) Barabara Kuu: Kilomita 11,292.81 na madaraja 1,362 kwa gharama ya Shilingi 130,984,788,000.00 kutoka Mfuko wa Barabara. (b) Barabara za Mikoa: Kilomita 24,675.75 na madaraja 1,436 kwa gharama ya Shilingi 218,817,361,000.00 kutoka Mfuko wa Barabara. (c) Matengenezo ya Dharura na Tahadhari: Kiasi cha Shilingi 49,802,751,000.00 zimetengwa kwa kazi hizi kutoka Mfuko wa Barabara. (d) Mradi wa Kufanya Matengenezo ya Muda Mrefu (PMMR): Shilingi 1,000,000,000.00 zimetengwa kwa ajili ya maandalizi ya awamu ya pili ya PMMR. (e) Matengenezo, Ukarabati na Ujenzi wa Mizani Kiasi cha Shilingi 19,690,000,000.00 kimetengwa kwa kazi hizi. (f) Kazi/Shughuli Zinazohusiana na Matengenezo Zinazofanywa Kutokea Makao Makuu: Kiasi cha Shilingi 6,220,000,000.00 kutoka Mfuko wa Barabara zimetengwa kwa kazi hizo. (g) Usimamizi wa Kazi na Utawala. Kiasi cha Shilingi 30,100,000,000.00 kimetengwa kwa kazi hizi. (h) Gharama za Uendeshaji wa Mizani (Operational Costs): Kiasi cha Shilingi

176

12,880,000,000.00 kimetengwa kwa kazi hizi.

274. Mheshimiwa Spika, mpango wa matengenezo ya barabara kuu na za mikoa kwa mwaka wa fedha 2014/15 kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara umeoneshwa katika Viambatisho Na. 5A hadi 5E kama ifuatavyo:

(i) Kiambatisho 5(A - 1): Matengenezo ya Kawaida (Routine Maintenance) ya Barabara Kuu kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara Mwaka wa fedha 2014/15 – Barabara Kuu: Jumla ya Shilingi 40,753,648,000.00.

(ii) Kiambatisho 5(A - 2): Matengenezo Kawaida (Routine Maintenance) ya Barabara za Mikoa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara Mwaka wa fedha 2014/15 – Barabara za Mikoa: Jumla ya Shilingi 59,246,809,000.00.

(iii) Kiambatisho 5(B - 1): Matengenezo ya Muda Maalum (Periodic Maintenance) ya Barabara Kuu kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara mwaka wa fedha 2014/15 – Barabara Kuu: Jumla ya Shilingi 77,034,851,000.00.

(iv) Kiambatisho 5(B - 2): Matengenezo Maalum (Periodic Maintenance) ya 177

Barabara za Mikoa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara mwaka wa fedha 2014/15 – Barabara za Mikoa: Jumla ya Shilingi 116,098,082,000.00.

(v) Kiambatisho 5(C - 1): Matengenezo ya Sehemu Korofi (Spot Improvement) ya Barabara Kuu kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara mwaka wa fedha 2014/15 – Barabara Kuu za lami na changarawe: Jumla ya Shilingi 3,390,986,000.00.

(vi) Kiambatisho 5(C - 2): Matengenezo ya Sehemu Korofi (Spot Improvement) ya Barabara za Mikoa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara kwa mwaka wa fedha 2014/15 – Barabara za Mikoa za lami na changarawe: Jumla ya Shilingi 19,573,800,000.00.

(vii) Kiambatisho 5(D): Matengenezo ya Kawaida ya Madaraja (Bridges Preventive Maintenance) kwa Barabara Kuu na Barabara za Mikoa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara mwaka wa fedha 2014/15: Jumla ya Shilingi 4,220,560,000.00.

(viii) Kiambatisho 5(E): Matengenezo Makubwa ya Madaraja na Makalavati (Bridges Major Repair) kwa Barabara 178

Kuu na Barabara za Mikoa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara mwaka wa fedha 2014/15: Jumla ya Shilingi 29,483,413,000.00

MPANGO WA UTEKELEZAJI KAZI KATIKA TAASISI ZILIZO CHINI YA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2014/15

Wakala wa Barabara

275. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15 Wakala wa Barabara (TANROADS) utaendelea kusimamia kazi za kukarabati, kujenga na kufanya matengenezo ya barabara kuu na barabara za mikoa. Matengenezo ya barabara kuu na mikoa yatahusisha matengenezo ya kawaida (routine maintenance) kilomita 31,132.22, matengenezo ya muda maalum kilomita 4,450.27, matengenezo ya sehemu korofi kilometa 1,075.61 na matengenezo ya madaraja 2,802. Mpango huu pia unajumuisha shughuli za utawala na usimamizi wa kazi, udhibiti wa uzito wa magari, kazi za dharura, mradi wa matengenezo ya muda mrefu ya barabara (PMMR) na kazi zinazosimamiwa kutoka Makao Makuu za mipango, usalama barabarani na hifadhi ya barabara. Wakala pia utaendelea kusimamia miradi ya ujenzi na ukarabati wa barabara kuu ambapo kilomita 539 ni ujenzi mpya kwa kiwango cha lami na kilomita 165 ni 179

za ukarabati kwa kiwango cha lami na kuendelea na ujenzi wa madaraja 12.

276. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa miradi ya maendeleo ya barabara za mikoa, Wakala umepanga kukarabati kilomita 1,350.0 kwa kiwango cha changarawe, kujenga kilomita 94 kwa kiwango cha lami na madaraja 45.

Wakala wa Majengo ya Serikali

277. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Wakala wa Majengo ya Serikali (TBA) umepanga kukamilisha miradi inayoendelea, kuanza ujenzi wa nyumba 149 za TAMISEMI katika mikoa 20 ya Tanzania Bara pamoja na kununua viwanja zaidi mikoani ili kuuwezesha Wakala kujenga nyumba nyingi zaidi za watumishi wa Umma. Aidha, Wakala utaendelea na mradi maalum wa ujenzi wa nyumba 10,000 za Watumishi wa umma pamoja na kuendelea kufanya matengenezo ya nyumba za Serikali na ununuzi wa samani kwa ajili ya nyumba za Viongozi wa umma.

278. Mheshimiwa Spika, Wakala pia utaendelea kuimarisha utoaji wa huduma na ushauri wa kitaalam kwa miradi ya ujenzi wa nyumba za Watumishi na ofisi za Serikali na kituo cha pamoja cha Forodha cha Tunduma kwa kuzingatia mahitaji na matakwa ya watu wenye ulemavu. Aidha, Wakala utaendelea 180

kuboresha ukusanyaji wa mapato kutoka kwenye vyanzo mbalimbali pamoja na kubuni na kuibua vyanzo vipya vya mapato ya Wakala.

Wakala wa Ufundi na Umeme

279. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa fedha 2014/15, Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) utanunua kivuko kipya kitakachotoa huduma kati ya Kigamboni na Magogoni na kivuko kingine kitakachotoa huduma kati ya Pangani na Bweni mkoani Tanga pamoja na kufanya ununuzi wa mashine za kielekroniki za ukatishaji tiketi katika vituo vya Kisorya – Rugezi, Pangani – Bweni na Ilagala – Kajeje. Aidha, Wakala utafanya ukarabati mkubwa wa vivuko vya MV Mwanza, MV Kiu, MV Pangani II na kumalizia ukarabati kivuko cha MV Magogoni. Wakala pia utaendelea na ukarabati wa karakana za M.T Depot Dar es Salaam na Dodoma pamoja na ununuzi wa vifaa vya karakana sita (6) ambazo ni Manyara, Singida, Lindi, Mwanza, Kagera na Ruvuma.

Wakala pia utaendelea na ujenzi wa maegesho ya Dar es Salaam – Bagamoyo (Magogoni, Rungwe Oceanic na Jangwani Beach) pamoja na upanuzi wa eneo la maegesho ya Kigamboni; ujenzi wa vituo vya abiria kwa kivuko cha Dar es Salaam – Bagamoyo katika maeneo ya Magogoni, Rungwe Oceanic na Jangwani Beach na maandalizi ya kuanzisha usafiri wa majini katika mwambao wa 181

Ziwa Victoria ili kupunguza msongamano katika jiji la Mwanza. Vile vile Wakala utajenga maegesho ya Bukondo na Zumacheli (Geita), Ilamba na Majita (Mara) na kutengeneza magari ya Serikali katika karakana zote kila Mkoa, ikiwa ni pamoja na kukodisha mitambo mbalimbali pamoja na magari maalum ya viongozi. Aidha, Wakala utaendelea kutoa ushauri wa kihandisi kwa miradi ya usimikaji wa mifumo ya umeme, mitambo, elektroniki, viyoyozi na majokofu katika nyumba za Serikali.

Bodi ya Mfuko ya Barabara

280. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Bodi ya Mfuko wa Barabara inatarajia kuendelea na jukumu lake la kukusanya fedha na kuzigawa kwa taasisi zinazofanya kazi za matengenezo ya barabara ambazo ni Wizara ya Ujenzi, Wakala wa Barabara (TANROADS) na Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI (PMORALG). Katika mwaka wa fedha 2014/15, Bodi inatarajia kukusanya jumla ya Shilingi 751,700,000,000.00. Bodi kwa kushirikiana na Taasisi zingine itafanya tafiti ili kubaini njia bora zaidi za kufanya matengenezo ya barabara na kushirikisha matokeo ya tafiti hizo na taasisi zinazofanya matengenezo ya barabara ili kuboresha utendaji kazi. Vile vile, Bodi imepanga kufanya ukaguzi wa ubora wa kazi (Technical Audit) kwa mikoa 21 na kukamilisha maandalizi ya Mpango Mkakati 182

Mpya (Strategic Plan) kwa mwaka wa fedha 2014/15 – 2016/17.

Bodi imepanga kuziwezesha Halmashauri za Wilaya na Miji kwa kuzipatia vifaa vya kupima ubora wa kazi za barabara. Bodi itashirikiana na taasisi zinazopokea fedha za Mfuko wa Barabara kuhakiki urefu, hali na aina za barabara (Road Inventory) zilizoko nchini ili kuboresha Database za barabara.

Kwa kushirikiana na TRA, EWURA na vyombo vingine vya Serikali, Bodi itaendelea kufanya tafiti kubaini mianya inayopelekea upotevu wa mapato ya Mfuko na kutoa mapendekezo jinsi ya kuziba mianya hiyo. Hii itasaidia kuboresha mapato ya Mfuko.

281. Mheshimiwa Spika, ili kuwezesha umma kufahamu kazi zinazofanywa na Mfuko, Bodi itaendelea kutoa taarifa mbalimbali kwa jamii kwa ujumla juu ya utendaji wa Bodi kwa kupitia mtandao, vijarida, magazeti, Taarifa ya Mwaka na kushiriki maonyesho mbalimbali ya kitaifa.

Bodi ya Usajili wa Wahandisi

282. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Bodi imepanga kusajili Wahandisi 800, Mafundi Sanifu 200 na Kampuni za Ushauri wa Kihandisi 25. Bodi pia 183

itasimamia mpango wa mafunzo kwa vitendo kwa wahandisi wahitimu 692 ambapo wahandisi wahitimu 442 ni wanaoendelea na 250 watakuwa wapya. Vilevile, Bodi itasimamia mafunzo ya kujiendeleza kitaaluma kwa wahandisi wataalam na wahandisi washauri.

Bodi pia itafanya ukaguzi wa shughuli za kihandisi nchini ili kuhakikisha kuwa shughuli zote za kihandisi zinafanywa na Wahandisi waliosajiliwa na kufuata maadili ya uhandisi. Aidha, Bodi itaendelea kuwashauri wahandisi wataalam waanzishe makampuni ya ushauri wa kihandisi mikoani ili kusogeza huduma hii muhimu karibu na watumiaji. Vile vile bodi itaendelea kuwaapisha wahandisi wataalamu na wahandisi washauri wote waliosajiliwa na wanaoendelea kusajiliwa ili kuhakikisha kuwa Wahandisi wanatekeleza majukumu yao kwa weledi na kuzingatia sheria.

Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi

283. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15 Bodi inatarajia kusajili Wabunifu Majengo 25, Wakadiriaji Majenzi 35, Kampuni 24 za Wabunifu Majengo na 10 za Wakadiriaji Majenzi. Aidha, Bodi itaendelea kukagua shughuli za wataalamu hao kwenye miradi iliyopo nchini inayostahili kukaguliwa kwa mujibu wa sheria. 184

Vile vile, Bodi itaendelea na mpango wa kuwawezesha wahitimu katika fani ya Ubunifu Majengo na Ukadiriaji Majenzi kupata mafunzo kwa vitendo, ili kuhakikisha wanapata maarifa na uzoefu unaokidhi matakwa ya sekta ya ujenzi kulingana na sheria. Aidha, Bodi itaanzisha programu za kutangaza na kuelimisha umma kuhusu shughuli za Bodi na umuhimu wa kushirikisha Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi katika kubuni nyumba za gharama nafuu kwa mashindano ya ubunifu.

Bodi ya Usajili wa Makandarasi

284. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Bodi imepanga kusajili jumla ya Makandarasi 834 wa fani mbalimbali pamoja na kukagua miradi ya ujenzi 2,500. Aidha, Bodi itaendesha kozi tano za mafunzo kwa Makandarasi katika mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Mara, Rukwa na Dodoma. Bodi pia itaendeleza Mfuko Maalum wa Kutoa Dhamana ya Kusaidia Makandarasi Wadogo na wa Kati (Contractors Assistance Fund). Jitihada za kuhamasisha Makandarasi wazalendo kujiunga ili kuomba zabuni kwa mfumo wa ubia zitaendelea, ambapo Bodi imeandaa mkutano wa mafunzo ya utekelezaji wa miradi kwa ubia kwa Makandarasi wa Kanda ya Kusini utakaofanyika mjini Iringa.

185

Baraza la Taifa la Ujenzi

285. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Baraza litaendelea kufanya tafiti mbalimbali kwa ajili ya kuendeleza Sekta ya Ujenzi, kuandaa taarifa na takwimu na majarida ya kiufundi kuhusu Sekta ya Ujenzi pamoja na kuboresha ukusanyaji, uwekaji na utoaji wa takwimu na taarifa za Sekta ya Ujenzi. Vilevile, Baraza litaendelea kuratibu na kutoa mafunzo katika sekta, ushauri wa kiufundi, utatuzi wa migogoro pamoja na ukaguzi wa kiufundi wa miradi ya ujenzi.

Baraza pia litaendelea na utekelezaji wa miradi kwa njia ya ubia kati ya Serikali na Sekta Binafsi. Hii ni pamoja na kuendelea kukamilisha ujenzi wa jengo la ghorofa 23 barabara ya Samora, Dar es Salaam. Aidha, Baraza litafanya upembuzi yakinifu kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya kitega uchumi – Regent Estate, Mbezi Beach jijini Dar es Salaam na kiwanja chake kilichopo Dodoma.

286. Mheshimiwa Spika, ili kukuza uwazi na uwajibikaji katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi, Baraza litaendelea kuratibu mfumo wa majaribio wa kutoa taarifa muhimu za miradi ya ujenzi (Construction Sector Transparency Initiative (CoST)). Aidha, Baraza litaendelea na jitihada za kutunisha/kuanza kazi kwa Mfuko

186

wa Maendeleo ya Sekta ya Ujenzi (Construction Industry Development Fund (CIDF)).

Vikosi vya Ujenzi

287. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Vikosi vya Ujenzi vimepanga kuendelea na ujenzi na ukarabati wa majengo ya ofisi na nyumba za Serikali, ukarabati wa ofisi na maghala ya Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA) Dar es Salaam pamoja na ujenzi wa maegesho ya vivuko mbalimbali.

Aidha, Vikosi vitaendelea kuimarisha mradi wa utengenezaji na uuzaji wa vifaa vya ujenzi “Building Materials Centre” Dar es Salaam na Dodoma pamoja na kuendeleza viwanja 38 vinavyomilikiwa na Vikosi vya Ujenzi Mjini Dodoma.

Chuo cha Ujenzi Morogoro

288. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Chuo kimepanga kuendeleza ujenzi wa jengo jipya la madarasa na karakana ya ufundi pamoja na kukarabati majengo matatu. Aidha, Chuo kitatoa mafunzo kwa wanafunzi 1,060 kwa fani za ufundi sanifu wa barabara, majengo na mitambo, Madereva wa Umma (Public Professional Drivers), pamoja na Madereva wa magari ya abiria (PSV).

187

Chuo cha Matumizi ya Teknolojia Stahiki ya Nguvukazi (Appropriate Technology Training Institute – ATTI) cha Mbeya

289. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Chuo cha Matumizi ya Teknolojia Stahiki ya Nguvukazi kilichopo Mbeya kitaendelea kutoa mafunzo juu ya matumizi ya teknolojia ya nguvukazi kwa kazi za barabara. Kazi zitakazofanyika ni pamoja na kuendesha mafunzo ya ukarabati na matengenezo ya barabara za changarawe, kutoa mafunzo ya uwekaji tabaka la lami nyepesi (surface dressing) kwa kutumia nguvukazi pamoja na kushirikiana na Wizara katika kuandaa na kuendesha mafunzo ya kuwajengea uwezo wanawake katika kushiriki kazi za barabara. Aidha, Chuo kimepanga kupanua wigo wake wa uhamasishaji matumizi ya teknolojia ya nguvukazi nchini kwa njia ya kushiriki maonesho mbalimbali, kugawa vipeperushi na kwa kupitia vyombo vya habari (magazeti, redio na luninga).

Kituo cha Usambazaji wa Teknolojia Katika Sekta ya Uchukuzi (Tanzania Transportation Technology Transfer Centre)

290. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Kituo kimepanga kusambaza kwa wadau 156,000 jumla ya makala na taarifa 260 zinazohusu tekinolojia mbalimbali katika sekta ya barabara na uchukuzi kwa ujumla 188

pamoja na kuendelea kutoa huduma ya maktaba ya Kituo. Aidha, kwa kushirikiana na taasisi zinazohusika na ujenzi, matengenezo na usimamizi wa miundombinu ya barabara na uchukuzi kwa ujumla hapa nchini pamoja na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Morgan State University ya Marekani na wadau wengine, Kituo kimepanga kuendelea kutekeleza mradi unaolenga kuboresha mifumo ya ujenzi, matengenezo na usimamizi wa miundombinu ya barabara na uchukuzi hapa nchini. Kwa kushirikiana na wadau wengine, Kituo kimepanga kufanya utafiti unaolenga kutatua changamoto za msongamano wa magari katika miji hapa nchini kwa kuanzia na jiji la Dar es Salaam. Kituo kimepanga kuandaa na kuendesha mafunzo kwa njia ya semina, warsha na kozi yatakayolenga kutatua changamoto nyingine zinazoikabili sekta ya barabara na uchukuzi na zitahudhuriwa na wadau wapatao 300.

MASUALA MTAMBUKA

Maendeleo ya Rasilimali Watu

291. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Wizara itaendelea kuajiri watumishi wapya wa kada mbalimbali ili kuiwezesha kutoa huduma kwa ukamilifu, kuwathibitisha kazini na kuwapandisha vyeo watumishi wanaostahili. Aidha, Wizara 189

itaendelea kuwaendeleza watumishi wake kitaaluma kwa kuwapeleka katika mafunzo ya ndani na nje ya nchi ili kuboresha utendaji wao wa kazi. Mafunzo hayo yatakuwa ni ya muda mrefu na muda mfupi.

Habari, Elimu na Mawasiliano

292. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Wizara itaendeleza mawasiliano na wadau wote ili kuboresha utoaji wa elimu na taarifa kwa umma. Wizara itaendelea kutoa taarifa za utekelezaji wa shughuli zake kupitia vipindi vya televisheni, radio, tovuti (www.mow.go.tz) pamoja na machapisho.

Ushirikishwaji wa Wanawake katika Kazi za Barabara Nchini

293. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuhamasisha na kuelimisha wanawake na jamii kwa ujumla ili wanawake washiriki kwa wingi zaidi katika kazi za ujenzi na matengenezo ya barabara. Katika mwaka wa fedha 2014/15, Wizara itaendelea kukamilisha uandaaji wa miongozo ya ushirikishwaji wa wanawake katika kazi za barabara na kuwaelimisha wadau wa barabara kuhusu miongozo hiyo. Wizara itatoa mafunzo ya ukandarasi kwa wanawake makandarasi na vikundi vya wanawake 30 kwa kutumia teknolojia ya nguvukazi, kufuatilia maendeleo ya Makandarasi na vikundi vya 190

wanawake waliopatiwa mafunzo ya kujenga na kutengeneza barabara kwa kutumia teknolojia ya nguvukazi pamoja na kuhamasisha wanawake wengi zaidi kushiriki katika kazi za barabara kama makandarasi au wafanyakazi katika ngazi mbalimbali. Vile vile, juhudi zitaendelea kuhamasisha wasichana wa shule za sekondari kusoma masomo ya sayansi ili wawe wahandisi wa baadaye.

Mikakati ya Kupambana na UKIMWI

294. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15 Wizara itaendelea kutoa elimu ya kujikinga na maambukizi ya UKIMWI na VVU kwa watumishi pamoja na kuhamasisha upimaji wa afya kwa hiari. Aidha, Wizara itaendelea na jitihada za kuwawezesha watumishi waliojitokeza, watakaojitokeza na wanaoishi na virusi vya UKIMWI kupata huduma za virutubisho, lishe na dawa.

Kudhibiti Rushwa

295. Mheshimiwa Spika, Wizara katika mwaka wa fedha 2014/15, itaendelea kutoa elimu juu ya madhara ya kutoa na kupokea rushwa kupitia vipeperushi na mikutano mbalimbali hususan Baraza la Wafanyakazi kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU). Aidha, Wizara itaimarisha dawati la malalamiko la 191

Wizara ili kuweza kutatua kero za rushwa katika sekta ya ujenzi.

Mapitio ya Sera ya Ujenzi

296. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15, Wizara ya Ujenzi itaendelea na kazi ya mapitio ya Sera ya Ujenzi ya mwaka 2003 ili iweze kukidhi mazingira ya sasa katika Sekta ya Ujenzi. Hii ni pamoja na kuwajengea uwezo Makandarasi wa ndani na kuishirikisha kikamilifu sekta binafsi katika uendelezaji wa miundombinu.

SHUKURANI

297. Mheshimiwa Spika, napenda nitumie fursa hii kuwashukuru kwa dhati Waheshimiwa Wabunge wote wa Bunge hili tukufu na kipekee kuishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu chini ya Uenyekiti wa Mheshimiwa , Mbunge wa Kigoma Mjini kwa michango, ushauri na ushirikiano waliotupa katika kuimarisha utendaji wa Wizara.

298. Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Wizara ya Ujenzi, napenda kuwashukuru kwa dhati wale wote walioshirikiana nasi katika kipindi cha mwaka wa fedha 2013/14 katika kutimiza malengo yetu. Shukrani za pekee ziwaendee Washirika wa Maendeleo walioendelea 192

kushirikiana nasi katika kutekeleza programu na mipango yetu katika kuendeleza Sekta ya Ujenzi. Washirika hao ni pamoja na Abu Dhabi, Denmark (DANIDA), Japan (JICA), Korea, Marekani (MCC), Uingereza (DFID), Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB), Benki ya Dunia (WB), Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Afrika (BADEA), Jumuiya ya Afrika Mashariki, Jumuiya ya Nchi za Ulaya (EU), Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID), Kuwait Fund, SIDA na OPEC Fund.

299. Mheshimiwa Spika, nitakuwa mchoyo wa fadhila nisipowashukuru viongozi wenzangu katika Wizara nikianzia na Mhe. Eng. Gerson H. Lwenge (Mb.), Naibu Waziri; Eng. Mussa I. Iyombe, Katibu Mkuu na Eng. Joseph M. Nyamhanga, Naibu Katibu Mkuu. Aidha, ninawashukuru Viongozi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara, Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo pamoja na wafanyakazi wote wa Wizara ya Ujenzi na Taasisi zote zilizo chini ya Wizara kwa kujituma na kujitolea kwa juhudi na maarifa katika kutekeleza malengo na majukumu ya Wizara yetu.

300. Mheshimiwa Spika, tunawashukuru wadau wote wa sekta ya ujenzi, na hasa sekta binafsi, ambao wametupa ushirikiano wa kutosha katika kuendeleza sekta hii. Aidha, nachukua fursa hii kuvipongeza vyombo mbalimbali vya habari kwa ushirikiano wao na 193

jinsi ambavyo vimekuwa vikifuatilia na kutoa taarifa za shughuli zinazohusiana na malengo, sera, sheria na kanuni mbalimbali zinazosimamiwa na Wizara ya Ujenzi. Shukrani zangu za dhati pia nazitoa kwa Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali na Wafanyakazi wote wa Ofisi ya Mpiga chapa Mkuu wa Serikali kwa kuchapa hotuba hii kwa ubora wa hali ya juu na kwa wakati.

301. Mheshimiwa Spika, hotuba yangu hii inapatikana katika tovuti ya Wizara ya Ujenzi - (www.mow.go.tz).

MAOMBI YA FEDHA KATIKA MWAKA WA FEDHA 2014/15

302. Mheshimiwa Spika, ili Wizara iweze kutekeleza majukumu yake ya kuendeleza sekta ya ujenzi, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu liidhinishe jumla ya Shilingi 1,219,717,592,000.00 kwa ajili ya matumizi ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2014/15. Kati ya fedha hizo, Shilingi 557,483,565,000.00 ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida ambazo zinajumuisha Shilingi 24,338,319,000.00 za mishahara ya Watumishi (PE), Shilingi 6,944,846,000.00 za matumizi mengineyo (OC) na Shilingi 526,200,400,000.00 za Mfuko wa Barabara.

194

Bajeti ya Miradi ya Maendeleo ni Shilingi 662,234,027,000.00. Kati ya fedha hizo, Shilingi 450,000,000,000.00 ni fedha za ndani na Shilingi 212,234,027,000.00 ni fedha za nje.

MUHTASARI WA BAJETI YA WIZARA YA UJENZI KWA MWAKA WA FEDHA 2014/15

A. Matumizi ya Kawaida MAELEZO KIASI (SHILINGI) Mishahara 24,338,319,000.00 Mfuko wa Barabara 526,200,400,000.00 Matumizi Mengineyo 6,944,846,000.00 Jumla Fedha za Matumizi 557,483,565,000.00 ya Kawaida B. Fedha za Maendeleo Fedha za Ndani za Miradi ya 450,000,000,000.00 Maendeleo Fedha za Nje za Miradi ya 212,234,027,000.00 Maendeleo Jumla Fedha za Maendeleo 662,234,027,000.00 JUMLA YA FEDHA ZA 1,219,717,592,000.00 MATUMIZI YA KAWAIDA NA MAENDELEO

303 Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

195