MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Ishirini Na Nane

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Ishirini Na Nane NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini na Nane – Tarehe 15 Mei, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Tukae. Katibu! NDG. RUTH MAKUNGU – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani:- WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Randama za Makadirio ya Mapato na matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NDG. RUTH MAKUNGU – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali. Tutaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Mheshimiwa Omari Mohamed Kigua, Mbunge wa Kilindi, sasa aulize swali lake. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Na. 230 Kununua Hospitali ya Wilaya inayomilikiwa na Kanisa la KKKT MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:- Kwa muda mrefu sasa Wilaya ya Kilindi haina Hospitali ya Wilaya lakini wanayo Hospitali ya Rufaa inayomilikiwa na Kanisa la KKKT, lakini watumishi wote na huduma zote za Hospitali hiyo zinagharamiwa na Halmashauri ya Wilaya (DED) na wao KKKT ni wamiliki wa majengo:- Je, Serikali haioni imefika wakati wa kufanya makubaliano ya kununua Hospitali hiyo ili kupunguza gharama kwa Serikali ya kujenga Hospitali ya Wilaya? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omary Mohamed Kigua, Mbunge wa Kilindi, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2010 Serikali kupitia Halmashauri ya Kilindi iliingia mkataba na Kanisa la Kilutheri Dayosisi ya Kaskazini Mashariki kwa lengo la kutumia majengo yanayomilikiwa na kanisa hilo kwa ajili ya utoaji wa huduma za afya kwa wananchi wa Kilindi. Hospitali hiyo Teule ya Wilaya (DDH) ya Kilindi inahudumia wananchi wapatao 264,000. Serikali inatumia utaratibu huo ikiwa ni ushirikiano na Taasisi binafsi yakiwemo Mashirika ya Dini pale ambapo hakuna Hospitali ya Wilaya ya Serikali. Mheshimiwa Naibu Spika, katika hospitali hiyo, Serikali inalipa mishahara ya baadhi ya watumishi walioajiriwa na Serikali na kupeleka fedha kwa ajili ya uendeshaji wa hospitali ambazo zinatumika kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vifaa tiba. Katika mwaka wa fedha 2018/2019, hospitali hiyo 2 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) iliidhinishiwa shilingi 153,646,500/= kutoka Mfuko wa Pamoja wa Afya ambapo ni asilimia 25 ya fedha zote za Mfuko wa Afya kwa Hospitali ya Wilaya. Vilevile, katika mwaka wa fedha 2019/2020, hospitali hiyo imetengewa jumla ya shiligni 153,646,500/= kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vifaa tiba. Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haina mpango wa kununua Hospitali ya Wilaya ya Kilindi inayomilikiwa na KKKT. Mpango wa Serikali ni kuhakikisha kila Halmashauri inakuwa na Hospitali ya Halmashauri ya Serikali. Pale ambapo bado Serikali haijajenga, itaendelea kushirikiana na sekta binafsi kama inavyofanyika sasa. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Omari Kigua, swali la nyongeza. MHE. OMARIM. KIGUA: Ahsante Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli kabisa nami naungana na Serikali kwamba kuna umuhimu wa Serikali kushirikiana na sekta binafsi katika kuwaletea Watanzania huduma. Pamoja na hali hiyo, zimejitokeza changamoto nyingi sana sana katika Hospitali hii ya KKKT mojawapo ni suala la utawala. Swali: Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari sasa kuangalia utaratibu ulio mzuri ili dhana hasa ya ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi iweze kufikiwa? (Makofi) Swali la pili, kwa kuwa Kilindi haina Hospitali ya Wilaya: Je, Serikali iko tayari sasa kuitengea fedha Wilaya ya Kilindi ili iweze kupata Hospitali ya Wilaya? Ahsante. (Makofi) NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa 3 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Naibu Spika, ni azma na lengo la Serikali kuhakikisha kwamba zile hospitali ambazo tunashirikiana katika kutoa huduma kwa maana ya DDH, suala la utawala bora inakuwa ni kipaumbele. Mheshimiwa Naibu Spika, nawe ni shuhuda kwamba katika swali lake amesema kuna tatizo la utawala. Sasa ni vizuri Mheshimiwa Kigua tukitoka hapa tuelekezane hasa tatizo ni nini ili tuweze kutoa ufumbuzi ili wafanyakazi nao waweze kuona ni sawa na ambavyo wanafanya katika hospitali zetu za Wilaya. Kwa sababu suala la kuwa na utawala bora ni jambo la msingi kabisa. Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Kigua atakubaliana na Serikali kwamba azma ya kuhakikisha kwamba hospitali zinajengwa katika maeneo yote ambayo Halmashauri hazina Hospitali za Wilaya inafikiwa. Kwa kuanzia, yeye mwenyewe ni shuhuda, katika bajeti ambayo Bunge lako Tukufu limetupitishia, tumeweza kuwatengea kwa kuanzia shilingi milioni 200 kwa ajili ya kujenga Kituo cha Afya cha Msente. Naamini baada ya kuhakikisha kwamba tunakamilisha ujenzi wa hospitali 67 tulizoanza nazo na 52, hakika naomba nimtoe shaka kwamba na Kilindi tutakwenda. (Makofi) NAIBU SPIKA: Waheshimiwa, nimwite Mheshimiwa Dkt. Jasmine Tisekwa Bunga, Mbunge wa Viti Maalum, sasa aulize swali lake. Na. 231 Hitaji la Barabara – Tarafa ya Mgeta Mvomero MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:- Barabara zinazotoka Kidiwa hadi Tandali, Daraja la Mgeta hadi Likuyu, Visomolo hadi Lusungi na Langali SACCOS hadi Shule ya Sekondari Langali Tarafa ya Mgeta Wilayani Mvomero zimejengwa kwa nguvu za wananchi, lakini bado 4 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) hazipitiki kutokana na vikwazo vya miundombinu na madaraja:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara hizo ili kuondoa adha wanazopata wananchi? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Jasmine T. Bunga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Kidiwa – Tandali – Maguruwe yenye urefu wa kilometa 13.8 imefanyiwa upembuzi yakinifu na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) na kubaini zinahitajika shilingi bilioni 2.81 kwa ajili ya matengenezo makubwa (Rehabilitation Works) kwa kiwango cha zege katika sehemu za maeneo ya milimani na ujenzi wa miundombinu ya madaraja. Serikali inaendelea na mpango wa kutafuta fedha kwa kizingatia uwingi wa fedha zinazohitajika. Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali imetenga jumla ya shilingi milioni 34.6 kwa ajili ya matengenezo ya muda maalum (Periodical Maintenance) kwenye barabara za kibaoni – Lukuyu na barabara ya Visomoro – Bumu – Mwalazi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa daraja (vented drift) katika Mto Songa. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Jasmine Bunga, swali la nyongeza. MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri yenye matumaini hasa kwa mwaka huu kutengewa hizo shilingi milioni 34, lakini hii barabara ya Kidiwa - Tandali 5 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) imeshafanyiwa upembuzi yakinifu, ingawa sasa hizo fedha zitatafutwa mpaka lini? Hapo sasa napenda kufahamu. Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimwambie Mheshimiwa Waziri kwamba Tarafa ya Mgeta kama alivyotembelea miaka ya nyuma, landscape yake bado ni ile ile ya milimani na watu wanaishi milimani. Kwa sasa tunategemea barabara hii kubwa moja toka Sangasanga kwenda mpaka Nyandila - Kikeo. Barabara hii ni mbovu sana hasa wakati wa masika; na tulishaahidiwa. Nakumbuka miaka ya 1970s alipokuja Mheshimiwa Abdu Jumbe aliahidi kwamba tutatengenezewa kwa kiwango cha lami. Ni kweli naweza nikalia. Mheshimiwa Naibu Spika, pia Rais Mstaafu, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete alipokuja aliahidi kwamba barabara hii itatengenezwa kwa kiwango cha lami kulingana na ubovu wake na nauli inakuwa kubwa: Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kujenga barabara hii ya Sangasanga mpaka Nyandila kwa kiwango cha lami? Swali la pili. Katika kutatua changamoto za usafiri katika Tarafa hii ya Mgeta, wananchi wamejitolea kutengeneza barabara nyembamba za kupita pikipiki, lakini wanakutana na changamoto ya utaalamu; wakati mwingine hawajui barabara iende hivi, kwa hiyo, wanakutana na changamoto hizo, lakini pia wanakutana na changamoto sehemu nyingine inabidi ijengwe madaraja au karavati. Je, Serikali sasa iko tayari kuungana na wananchi hawa wa Tarafa ya Mgeta ili kupeleka wataalam pamoja na kuwajengea madaraja ili tuweze pia kutumia usafiri wa pikipiki kuunganisha vijiji na Kata? Ahsante. (Makofi) NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, machozi tuliyoshuhudia yakitoka kwa 6 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Mbunge wa Mlimba pale, yanatosha kwa Mkoa wa Morogoro. Kwa hiyo, isingependeza tukapata machozi mengine. Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Dkt. Tisekwa akubaliane nami kwamba ahadi zote zinazotolewa na Viongozi Wakuu kwa maana ya Marais, hata kama Rais aliyetangulia ndio aliyetoa ahadi, sisi kama Serikali, ahadi hizo tunazitunza na ni wajibu wetu kuhakikisha kwamba ahadi za viongozi wetu tunazitekeleza. Mheshimiwa Naibu Spika, hivi karibuni Mheshimiwa Mbunge atakuwa shuhuda, katika ahadi ambazo zimetolewa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, katika bajeti ambayo tumepitisha, tumeanza kutekeleza katika
Recommended publications
  • Hotuba Ya Mgeni Rasmi Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) Waziri Mkuu Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Katika Ufunguzi Wa Mkuta
    HOTUBA YA MGENI RASMI MHE. KASSIM MAJALIWA MAJALIWA (MB) WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KATIKA UFUNGUZI WA MKUTANO WA MWAKA WA WADAU WA LISHE, SEPTEMBA 10, 2019 Mheshimiwa Jenista Mhagama (Mb), Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu, Mheshimiwa Ummy Mwalimu (Mb), Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mheshimiwa Suleiman Jafo (Mb), Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI. Mheshimiwa Prof. Joyce Ndalichako (Mb), Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango (Mb), Waziri wa Fedha na Mipango. Mheshimiwa Japhet Hasunga (Mb), Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Luhaga Mpina (Mb), Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mheshimiwa Innocent Bashungwa (Mb), Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwezeshaji, Mheshimiwa Prof. Makame Mbarawa (Mb), Waziri wa Maji na Umwagiliaji. Mheshimiwa Doto Biteko (Mb), Waziri wa Madini, Waheshimiwa Manaibu Waziri na Makatibu Wakuu, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Bilinith Mahenge; pamoja na viongozi wengine wa ngazi za Mkoa na Halmashauri mliopo, Waheshimiwa Wabunge na viongozi wa Vyama vya Siasa, Waheshimiwa Mabalozi wanaoziwakilisha nchi mbalimbali, Ndugu Viongozi waandamizi wa Idara, Taasisi, Wakala za Serikali, Wakuu wa Vyuo vya Elimu ya Juu, Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa, Wadau wa Maendeleo na Asasi za Kiraia, 1 Ndugu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania, Ndugu Wageni Waalikwa, Waandishi wa habari na wadau wote wa Lishe, Mabibi na Mabwana. Habari za asubuhi Kwa mara nyingine tena nina furaha kubwa sana kujumuika na wadau wa lishe siku hii ya leo. Hii ni mara yangu ya tatu kuhudhuria mkutano wa mwaka wa wadau wa lishe nchini na hivyo nahisi kuwa mwanafamilia wa wadau waliohamasika katika masuala ya lishe.
    [Show full text]
  • TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who Will Benefit from the Gas Economy, If It Happens?
    TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who will benefit from the gas economy, if it happens? TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who will benefit from the gas economy, if it happens? TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013 Who will benefit from the gas economy, if it happens? Supported by: 2 TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who will benefit from the gas economy, if it happens? ACKNOWLEDGEMENTS Policy Forum would like to thank the Foundation for Civil Society for the generous grant that financed Tanzania Governance Review 2013. The review was drafted by Tanzania Development Research Group and edited by Policy Forum. The cartoons were drawn by Adam Lutta (Adamu). Tanzania Governance Reviews for 2006-7, 2008-9, 2010-11, 2012 and 2013 can be downloaded from the Policy Forum website. The views expressed and conclusions drawn on the basis of data and analysis presented in this review do not necessarily reflect those of Policy Forum. TGRs review published and unpublished materials from official sources, civil society and academia, and from the media. Policy Forum has made every effort to verify the accuracy of the information contained in TGR2013, particularly with media sources. However, Policy Forum cannot guarantee the accuracy of all reported claims, statements, and statistics. Whereas any part of this review can be reproduced provided it is duly sourced, Policy Forum cannot accept responsibility for the consequences of its use for other purposes or in other contexts. ISBN:978-9987-708-19-2 For more information and to order copies of the report please contact: Policy Forum P.O. Box 38486 Dar es Salaam Tel +255 22 2780200 Website: www.policyforum.or.tz Email: [email protected] Suggested citation: Policy Forum 2015.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge Mkutano Wa Kumi Na Mbili
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Kumi na Tano – Tarehe 1 Julai, 2008 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 132 Kuimarisha Ulinzi na Usalama Jiji Dar es Salaam MHE. CHARLES N. KEENJA : Kwa kuwa, Serikali ya Awamu ya Nne imechukua hatua madhubuti za kuimarisha Ulinzi na Usalama kwenye Jiji la Dar es Salaam kwa kuligawa Jiji kwenye Mikoa na Wilaya za Ki-ulinzi ; na kwa kuwa, hatua hiyo haikwenda sanjari na ile ya kuigawa Mikoa ya Kiutawala:- (a) Je, ni lini Serikali itachukua hatua za kuligawa eneo la Jiji la Dar es Salaam kwenye Mkoa/Wilaya zinazokwenda sanjari na zile za Ulinzi na Usalama ? (b) Je, Serikali haioni kwamba Viongozi kwenye eneo lenye hadhi zinazotofautiana kunaleta matatizo ya ushirikiano na mawasiliano hatimaye kukwamisha utendaji kazi ? (c) Kwa kuwa, zaidi ya 10% ya wananchi wa Tanzania wanaishi Dar es Salaam. Je, Serikali haioni kwamba sasa ni wakati muafaka wa kuweka utaratibu mzuri zaidi wa Uongozi kwenye Jiji hilo ? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- 1 Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Charles Keenja, Mbunge wa Ubungo, lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa katika hatua za kuimarisha Ulinzi na Usalama kwenye Jiji la Dar es Salaam Serikali iliamua kuligawa eneo katika ngazi ya Mikoa ambapo Wilaya zote tatu za Kinondoni, Temeke na Ilala ni Mikoa ya Kiulinzi na ngazi ya Mkoa kupewa hadhi ya Kanda Maalum ya Ulinzi na Usalama.
    [Show full text]
  • Tarehe 30 Juni, 2017
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Hamsini na Saba – Tarehe 30 Juni, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Tunaendelea na Mkutano wetu wa Saba, leo ni Kikao cha Hamsini na Saba. Katibu! NDG. RAMADHANI ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Tunaanza na Ofisi ya Mheshimiwa Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Swali la kwanza linaulizwa na Mheshimiwa Stanslaus Haroon Nyongo, Mbunge wa Maswa Mashariki. Mheshimiwa Nyongo. Na. 468 Mikopo kwa Walimu Kwa Ajili ya Ujenzi wa Nyumba MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza:- Walimu Wilayani Maswa wana uhaba wa nyumba za kuishi; pamoja na juhudi za wananchi kujenga nyumba za walimu wa shule za msingi na sekondari lakini walimu hao bado wanahitaji kujenga nyumba zao wenyewe za kudumu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Je, ni lini Serikali itaweka utaratibu maalum wa kutoa mikopo kwa walimu hao ili wajenge nyumba zao binafsi? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Haroon Nyongo, Mbunge wa Maswa Mashariki kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ina uhitaji wa nyumba za walimu 1,358. Nyumba zilizopo ni 479 na hivyo upungufu ni nyumba 879. Mheshimiwa Spika, kutokana na upungufu huu Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ina mpango wa kujenga nyumba 16 katika mwaka wa fedha 2017/2018. Aidha, kati ya nyumba hizo, nyumba nane zitajengwa kwa bajeti ya 2017/2018 (CDG) na nyumba nyingine nane zitajengwa kwa kutumia mapato ya ndani y (own source) ya Halmashauri.
    [Show full text]
  • MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Thelathini Na Sita
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Sita – Tarehe 27 Mei, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nawaomba tukae. Waheshimiwa Wabunge tunaendelea na Mkutano wetu wa 15, leo ni Kikao cha 36. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NAIBU WAZIRI WA MADINI: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2019/2020. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. CATHERINE V. MAGIGE - K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI) Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu utekelezaji na Majukumu ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. MHE. TUNZA I. MALAPO - K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU WIZARA YA MADINI: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni juu ya Wizara ya Madini kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Tunza Malapo, tunakushukuru. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Tunaanza na TAMISEMI, swali la kwanza litaulizwa na Mheshimiwa Azza Hilal, Mbunge wa Viti Maalum - Shinyanga.
    [Show full text]
  • Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania Mkutano Wa Tatu Yatokanayo Na Kikao Cha Arobaini Na Saba 21 Juni, 2016
    JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA TATU YATOKANAYO NA KIKAO CHA AROBAINI NA SABA 21 JUNI, 2016 MKUTANO WA TATU - YATOKANAYO NA KIKAO CHA AROBAINI NA SABA TAREHE 21 JUNI, 2016 I. DUA: Saa 3.00 Asubuhi Naibu Spika (Mhe. Dkt.Tulia Ackson) alisoma Dua na Kuongoza Bunge. Makatibu Mezani: 1. Ndg. Theonest Ruhilabake 2. Ndg. Zainab Issa Wabunge wa Kambi ya Upinzani walitoka nje ya ukumbi wa Bunge baada ya dua kusomwa na Mhe. Naibu Spika. II. MASWALI: Maswali yafuatayo yaliulizwa na Waheshimiwa Wabunge na kujibiwa na Serikali:- OFISI YA WAZIRI MKUU: Swali Na.399 – Mhe. Raphael Masunga Chegeni [kny. Mhe. Salome Makamba] Swali la nyongeza: (i) Mhe. Raphael Masunga Chegeni (ii) Mhe. Abdallah Hamisi Ulega (iii) Mhe. Joseph Kasheku Musukuma (iv) Mhe. Mariam Nassoro Kisangi OFISI YA RAIS (TAMISEMI): Swali Na.400 Mhe. Oran Manase Njeza Swali la nyongeza: (i) Mhe. Oran Manase Njeza (ii) Mhe. Desderius John Mipata (iii) Mhe. Goodluck Asaph Mlinga Swali Na.401 – Mhe. Boniventura Destery Kiswaga Swali la nyongeza: (i) Mhe. Boniventura Destery Kiswaga (ii) Mhe. Augustino Manyanda Maselle (iii) Mhe. Richard Mganga Ndassa (iv) Mhe. Dkt. Dalali Peter Kafumu Swali Na. 402 – Mhe. Fredy Atupele Mwakibete Swali la Nyongeza: (i) Mhe. Fredy Atupele Mwakibete (ii) Mhe. Njalu Daudi Silanga (iii) Mhe. Halima Abdallah Bulembo (iv) Mhe. Azza Hilal Hamad 2 WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Swali Na.403 – Mhe Joseph Kakunda. kny Mhe. Ally Saleh Ally Swali la nyongeza: (i) Mhe. Joseph George Kakunda (ii) Mhe. Mussa Azzan Zungu (iii) Mhe. Cosato David Chumi (iv) Mhe.
    [Show full text]
  • Issued by the Britain-Tanzania Society No 124 Sept 2019
    Tanzanian Affairs Issued by the Britain-Tanzania Society No 124 Sept 2019 Feathers Ruffled in CCM Plastic Bag Ban TSh 33 trillion annual budget Ben Taylor: FEATHERS RUFFLED IN CCM Two former Secretary Generals of the ruling party, CCM, Abdulrahman Kinana and Yusuf Makamba, stirred up a very public argument at the highest levels of the party in July. They wrote a letter to the Elders’ Council, an advisory body within the party, warning of the dangers that “unfounded allegations” in a tabloid newspaper pose to the party’s “unity, solidarity and tranquillity.” Selection of newspaper covers from July featuring the devloping story cover photo: President Magufuli visits the fish market in Dar-es-Salaam following the plastic bag ban (see page 5) - photo State House Politics 3 This refers to the frequent allegations by publisher, Mr Cyprian Musiba, in his newspapers and on social media, that several senior figures within the party were involved in a plot to undermine the leadership of President John Magufuli. The supposed plotters named by Mr Musiba include Kinana and Makamba, as well as former Foreign Affairs Minister, Bernard Membe, various opposition leaders, government officials and civil society activists. Mr Musiba has styled himself as a “media activist” seeking to “defend the President against a plot to sabotage him.” His publications have consistently backed President Magufuli and ferociously attacked many within the party and outside, on the basis of little or no evidence. Mr Makamba and Mr Kinana, who served as CCM’s secretary generals between 2009 to 2011 and 2012-2018 respectively, called on the party’s elders to intervene.
    [Show full text]
  • Tarehe 4 Aprili, 2019
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Tatu – Tarehe 4 Aprili, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba tukae. Leo ni kikao cha tatu cha Mkutano wetu wa Kumi na Tano. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI: Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, AJIRA, KAZI VIJANA NA WAZEE NA WENYE ULEMAVU: Taarifa ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2019/2020. MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA: Taarifa 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020. MHE. HASNA S.K. MWILIMA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu utekelezaji wa Bajeti ya Mfuko wa Bunge kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Mfuko huo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA - MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MASUALA YA UKIMWI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu utekelezaji wa Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu (Tume ya Uratibu na Udhibiti wa UKIMWI) kwa mwaka wa fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020.
    [Show full text]
  • Tarehe 2 Novemba, 2016
    NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA TANO Kikao cha Pili – Tarehe 2 Novemba, 2016 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Mussa A. Zungu) Alisoma Dua MWENYEKITI: Tukae. Katibu! NDG. CHARLES MLOKA - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Waheshimiwa kama kawaida tunaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu. Mheshimiwa Ezekiel Maige, kwa niaba Mheshimiwa Mwambalaswa! Na. 16 Kuanzisha Mfuko wa Maafa Kitaifa MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA (K.n.y. MHE. EZEKIEL M. MAIGE) aliuliza:- Kutokana na mabadiliko ya tabia nchi matukio ya majanga na maafa kama mvua za mawe pamoja na matetemeko ya ardhi yameanza kutokea mara kwa mara na mara zote Serikali imekuwa haina maandalizi ya kifedha na vifaa vya kusaidia wahanga kwa muda mfupi na muda mrefu na badala yake imekuwa ikitegemea zaidi wasamaria wema wa Mataifa mengine:- (a) Je, ni kwa nini Serikali imekuwa haisaidii kifedha na vifaa zaidi ya kuhamasisha wasamaria wema wasaidie na wenyewe kubaki na jukumu la kupeleka wataalam kama Madaktari na kuratibu misaada pekee? 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) (b) Je, ni kwa nini Serikali isianzishe Mfuko wa Maafa Kitaifa ambao utakuwa unachangiwa wakati wote kwa njia endelevu? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WATU WENYE ULEMAVU alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ezekiel Magolyo Maige, Mbunge wa Msalala, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kulifahamisha Bunge lako Tukufu kwamba, Serikali inatambua kuwa ni wajibu wake kusaidia wananchi pindi wanapokumbwa na maafa yanayoharibu mfumo wa maisha ya kila siku.
    [Show full text]
  • Tarehe 3 Februari, 2021
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA PILI Kikao cha Pili – Tarehe 3 Februari, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Tukae. Katibu. NDG. RUTH MAKUNGU – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaanza na maswali Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, sasa aulize swali lake. Na. 16 Ujenzi wa Barabara za Lami - Mji wa Mafinga MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza Ujenzi wa Barabara za lami na kufunga taa za barabarani katika Mji wa Mafinga chini ya Mpango wa Uendelezaji Miji nchini? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NAIBU WAZIRI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyenijalia mimi na Waheshimiwa Wabunge wote afya njema na kutuwezesha kuwa wawakilishi wa wananchi kupitia Bunge lako Tukufu. Mheshimiwa Naibu Spika, pili, naomba nichukue nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa imani kubwa aliyonipa kwa kuniteua kuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Namshukuru sana Mheshimiwa Rais. (Makofi) Mheshimiwa Naibu Spika, tatu, nawashukuru sana wananchi wa Jimbo la Wanging’ombe kwa kunichagua na kuchagua mafiga
    [Show full text]
  • THRDC's Report on the Situation of Human Rights Defenders in Tanzania
    THE 2018 REPORT ON THE SITUATION OF HUMAN RIGHTS DEFENDERS AND CIVIC SPACE IN TANZANIA RESEARCHERS ADVOCATES JONES SENDODO, DEOGRATIAS BWIRE, LEOPOLD MOSHA WRITERS ADVOCATES JONES SENDODO, DEOGRATIAS BWIRE, LEOPOLD MOSHA EDITORS PILI MTAMBALIKE ONESMO OLENGURUMWA The 2018 Report on the Situation of Human Rights Tanzania Human Rights Defenders Coalition Defenders and Civic Space in Tanzania ii [THRDC] Table of Contents ABREVIATIONS vi LIST OF STATUTES AND INTERNATIONAL INSTRUMENTS vii ACKNOWLEDGMENT ix PREFACE x VISION, MISSION, VALUES xi THE OVERAL GOAL OF THE THRDC xii EXECUTIVE SUMMARY xiii Chapter One 1 GENERAL INTRODUCTION 1 1.0 Introduction 1 1.1 Protection Mechanisms for Human Rights Defenders 3 1.1.1 Legal Protection Mechanism at International Level 4 1.1.2 Legal Protection Mechanism at Regional Level 7 1.1.3 Legal Protection Mechanism at the National Level 11 1.1.4 Challenges with Both International and Regional Protection Mechanisms for HRDS 13 1.2 Non Legal Protection mechanism 13 1.2.1 Non Legal Protection mechanism at International level 14 1.2.2 Non Legal Protection Mechanism at Regional level 15 1.2.3 Protection Mechanism at National Level 16 Chapter Two 20 VIOLATIONS COMMITTED AGAINST HUMAN RIGHTS DEFENDERS 20 2.0 Overview of the Chapter 20 2.1 Violations Committed against Human Rights Defenders in 2018 21 2.1.1 Arrests and Prosecution against HRDs in 2018 Other Strategic Litigation Cases for HRDs in Tanzania 21 2.2 Physical violence, Attacks, and Torture 30 2.2.1 Pastoralists Land Rights Defenders and the Situation in
    [Show full text]
  • 20 MAY 2019.Pmd
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Moja – Tarehe 20 Mei, 2019 (Bunge Lilianza saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na Mkutano wetu wa 15, leo kikao cha 31. Katibu! NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nasikitika kuwatangazia kifo cha mwanasiasa mkongwe na kiongozi aliyepata kuhudumia kwa muda mrefu hasa kule kwenye Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Marehemu Ally Juma Shamhuna. Waheshimiwa Wabunge, katika uhai wake, marehemu Ally Juma Shamhuma amepata kushika nyadhifa mbalimbali zikiwemo hizi zifuatazo; amepata kuwa Mkurugenzi wa Mifugo, amewahi kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, amewahi kuwa Katibu Mkuu, Export Processing Zone Zanzibar, amewahi kuwa Waziri wa Mipango, amekuwa Waziri wa Nchi, Afisi ya Waziri Kiongozi, aliwahi kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo na wakati huo huo akiwa ni 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Naibu Waziri Kiongozi, katika uhai wake amekuwa Waziri wa Ardhi, Maji na Nishati na alipata kuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali. Aidha, Marehemu Mheshimiwa Shamhuna kwa muda mrefu alikuwa ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi kutokea Zanzibar na baadhi yenu humu Wabunge mtamkumbuka marehemu Mheshimiwa Shamhuna kama Mbunge wa Bunge la Katiba na alikuwa Mjumbe wa Kamati namba 8 kwenye Bunge la Katiba, Kamati ambayo nilikuwa Mwenyekiti wake. Kwa niaba yenu Waheshimiwa Wabunge, tunatoa pole kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Tunatoa pole kwa Wazanzibari wote na Watanzania wote kwa ujumla kufuatia kifo hicho na tunamuomba Mwenyezi Mungu aihifadhi roho yake mahali pema peponi, amina.
    [Show full text]