MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Ishirini Na Nane
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini na Nane – Tarehe 15 Mei, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Tukae. Katibu! NDG. RUTH MAKUNGU – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani:- WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Randama za Makadirio ya Mapato na matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NDG. RUTH MAKUNGU – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali. Tutaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Mheshimiwa Omari Mohamed Kigua, Mbunge wa Kilindi, sasa aulize swali lake. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Na. 230 Kununua Hospitali ya Wilaya inayomilikiwa na Kanisa la KKKT MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:- Kwa muda mrefu sasa Wilaya ya Kilindi haina Hospitali ya Wilaya lakini wanayo Hospitali ya Rufaa inayomilikiwa na Kanisa la KKKT, lakini watumishi wote na huduma zote za Hospitali hiyo zinagharamiwa na Halmashauri ya Wilaya (DED) na wao KKKT ni wamiliki wa majengo:- Je, Serikali haioni imefika wakati wa kufanya makubaliano ya kununua Hospitali hiyo ili kupunguza gharama kwa Serikali ya kujenga Hospitali ya Wilaya? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omary Mohamed Kigua, Mbunge wa Kilindi, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2010 Serikali kupitia Halmashauri ya Kilindi iliingia mkataba na Kanisa la Kilutheri Dayosisi ya Kaskazini Mashariki kwa lengo la kutumia majengo yanayomilikiwa na kanisa hilo kwa ajili ya utoaji wa huduma za afya kwa wananchi wa Kilindi. Hospitali hiyo Teule ya Wilaya (DDH) ya Kilindi inahudumia wananchi wapatao 264,000. Serikali inatumia utaratibu huo ikiwa ni ushirikiano na Taasisi binafsi yakiwemo Mashirika ya Dini pale ambapo hakuna Hospitali ya Wilaya ya Serikali. Mheshimiwa Naibu Spika, katika hospitali hiyo, Serikali inalipa mishahara ya baadhi ya watumishi walioajiriwa na Serikali na kupeleka fedha kwa ajili ya uendeshaji wa hospitali ambazo zinatumika kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vifaa tiba. Katika mwaka wa fedha 2018/2019, hospitali hiyo 2 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) iliidhinishiwa shilingi 153,646,500/= kutoka Mfuko wa Pamoja wa Afya ambapo ni asilimia 25 ya fedha zote za Mfuko wa Afya kwa Hospitali ya Wilaya. Vilevile, katika mwaka wa fedha 2019/2020, hospitali hiyo imetengewa jumla ya shiligni 153,646,500/= kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vifaa tiba. Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haina mpango wa kununua Hospitali ya Wilaya ya Kilindi inayomilikiwa na KKKT. Mpango wa Serikali ni kuhakikisha kila Halmashauri inakuwa na Hospitali ya Halmashauri ya Serikali. Pale ambapo bado Serikali haijajenga, itaendelea kushirikiana na sekta binafsi kama inavyofanyika sasa. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Omari Kigua, swali la nyongeza. MHE. OMARIM. KIGUA: Ahsante Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli kabisa nami naungana na Serikali kwamba kuna umuhimu wa Serikali kushirikiana na sekta binafsi katika kuwaletea Watanzania huduma. Pamoja na hali hiyo, zimejitokeza changamoto nyingi sana sana katika Hospitali hii ya KKKT mojawapo ni suala la utawala. Swali: Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari sasa kuangalia utaratibu ulio mzuri ili dhana hasa ya ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi iweze kufikiwa? (Makofi) Swali la pili, kwa kuwa Kilindi haina Hospitali ya Wilaya: Je, Serikali iko tayari sasa kuitengea fedha Wilaya ya Kilindi ili iweze kupata Hospitali ya Wilaya? Ahsante. (Makofi) NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa 3 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Naibu Spika, ni azma na lengo la Serikali kuhakikisha kwamba zile hospitali ambazo tunashirikiana katika kutoa huduma kwa maana ya DDH, suala la utawala bora inakuwa ni kipaumbele. Mheshimiwa Naibu Spika, nawe ni shuhuda kwamba katika swali lake amesema kuna tatizo la utawala. Sasa ni vizuri Mheshimiwa Kigua tukitoka hapa tuelekezane hasa tatizo ni nini ili tuweze kutoa ufumbuzi ili wafanyakazi nao waweze kuona ni sawa na ambavyo wanafanya katika hospitali zetu za Wilaya. Kwa sababu suala la kuwa na utawala bora ni jambo la msingi kabisa. Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Kigua atakubaliana na Serikali kwamba azma ya kuhakikisha kwamba hospitali zinajengwa katika maeneo yote ambayo Halmashauri hazina Hospitali za Wilaya inafikiwa. Kwa kuanzia, yeye mwenyewe ni shuhuda, katika bajeti ambayo Bunge lako Tukufu limetupitishia, tumeweza kuwatengea kwa kuanzia shilingi milioni 200 kwa ajili ya kujenga Kituo cha Afya cha Msente. Naamini baada ya kuhakikisha kwamba tunakamilisha ujenzi wa hospitali 67 tulizoanza nazo na 52, hakika naomba nimtoe shaka kwamba na Kilindi tutakwenda. (Makofi) NAIBU SPIKA: Waheshimiwa, nimwite Mheshimiwa Dkt. Jasmine Tisekwa Bunga, Mbunge wa Viti Maalum, sasa aulize swali lake. Na. 231 Hitaji la Barabara – Tarafa ya Mgeta Mvomero MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:- Barabara zinazotoka Kidiwa hadi Tandali, Daraja la Mgeta hadi Likuyu, Visomolo hadi Lusungi na Langali SACCOS hadi Shule ya Sekondari Langali Tarafa ya Mgeta Wilayani Mvomero zimejengwa kwa nguvu za wananchi, lakini bado 4 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) hazipitiki kutokana na vikwazo vya miundombinu na madaraja:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara hizo ili kuondoa adha wanazopata wananchi? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Jasmine T. Bunga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Kidiwa – Tandali – Maguruwe yenye urefu wa kilometa 13.8 imefanyiwa upembuzi yakinifu na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) na kubaini zinahitajika shilingi bilioni 2.81 kwa ajili ya matengenezo makubwa (Rehabilitation Works) kwa kiwango cha zege katika sehemu za maeneo ya milimani na ujenzi wa miundombinu ya madaraja. Serikali inaendelea na mpango wa kutafuta fedha kwa kizingatia uwingi wa fedha zinazohitajika. Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali imetenga jumla ya shilingi milioni 34.6 kwa ajili ya matengenezo ya muda maalum (Periodical Maintenance) kwenye barabara za kibaoni – Lukuyu na barabara ya Visomoro – Bumu – Mwalazi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa daraja (vented drift) katika Mto Songa. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Jasmine Bunga, swali la nyongeza. MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri yenye matumaini hasa kwa mwaka huu kutengewa hizo shilingi milioni 34, lakini hii barabara ya Kidiwa - Tandali 5 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) imeshafanyiwa upembuzi yakinifu, ingawa sasa hizo fedha zitatafutwa mpaka lini? Hapo sasa napenda kufahamu. Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimwambie Mheshimiwa Waziri kwamba Tarafa ya Mgeta kama alivyotembelea miaka ya nyuma, landscape yake bado ni ile ile ya milimani na watu wanaishi milimani. Kwa sasa tunategemea barabara hii kubwa moja toka Sangasanga kwenda mpaka Nyandila - Kikeo. Barabara hii ni mbovu sana hasa wakati wa masika; na tulishaahidiwa. Nakumbuka miaka ya 1970s alipokuja Mheshimiwa Abdu Jumbe aliahidi kwamba tutatengenezewa kwa kiwango cha lami. Ni kweli naweza nikalia. Mheshimiwa Naibu Spika, pia Rais Mstaafu, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete alipokuja aliahidi kwamba barabara hii itatengenezwa kwa kiwango cha lami kulingana na ubovu wake na nauli inakuwa kubwa: Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kujenga barabara hii ya Sangasanga mpaka Nyandila kwa kiwango cha lami? Swali la pili. Katika kutatua changamoto za usafiri katika Tarafa hii ya Mgeta, wananchi wamejitolea kutengeneza barabara nyembamba za kupita pikipiki, lakini wanakutana na changamoto ya utaalamu; wakati mwingine hawajui barabara iende hivi, kwa hiyo, wanakutana na changamoto hizo, lakini pia wanakutana na changamoto sehemu nyingine inabidi ijengwe madaraja au karavati. Je, Serikali sasa iko tayari kuungana na wananchi hawa wa Tarafa ya Mgeta ili kupeleka wataalam pamoja na kuwajengea madaraja ili tuweze pia kutumia usafiri wa pikipiki kuunganisha vijiji na Kata? Ahsante. (Makofi) NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, machozi tuliyoshuhudia yakitoka kwa 6 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Mbunge wa Mlimba pale, yanatosha kwa Mkoa wa Morogoro. Kwa hiyo, isingependeza tukapata machozi mengine. Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Dkt. Tisekwa akubaliane nami kwamba ahadi zote zinazotolewa na Viongozi Wakuu kwa maana ya Marais, hata kama Rais aliyetangulia ndio aliyetoa ahadi, sisi kama Serikali, ahadi hizo tunazitunza na ni wajibu wetu kuhakikisha kwamba ahadi za viongozi wetu tunazitekeleza. Mheshimiwa Naibu Spika, hivi karibuni Mheshimiwa Mbunge atakuwa shuhuda, katika ahadi ambazo zimetolewa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, katika bajeti ambayo tumepitisha, tumeanza kutekeleza katika