MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Thelathini Na Sita

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Thelathini Na Sita NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Sita – Tarehe 27 Mei, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nawaomba tukae. Waheshimiwa Wabunge tunaendelea na Mkutano wetu wa 15, leo ni Kikao cha 36. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NAIBU WAZIRI WA MADINI: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2019/2020. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. CATHERINE V. MAGIGE - K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI) Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu utekelezaji na Majukumu ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. MHE. TUNZA I. MALAPO - K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU WIZARA YA MADINI: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni juu ya Wizara ya Madini kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Tunza Malapo, tunakushukuru. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Tunaanza na TAMISEMI, swali la kwanza litaulizwa na Mheshimiwa Azza Hilal, Mbunge wa Viti Maalum - Shinyanga. Na. 297 Hitaji la Mabweni Shule za Sekondari-Shinyanga MHE. AZZA H. HAMAD aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga Mabweni katika shule za sekondari zilizoanzishwa Kitarafa ili kuwasaidia watoto wa kike waweze kupata elimu iliyo bora Mkoani Shinyanga? 2 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) SPIKA: Majibu ya swali hilo Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mheshimiwa Selemani Saidi Jafo, tafadhali. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Azza Hilal Hamad, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa shule za sekondari kuwa na mabweni ili kuboresha elimu. Kwa sasa mpango wa Serikali ni kuziboresha shule za sekondari zilizopo ambapo kipaumbele ni katika ujenzi wa miundombinu muhimu wa vyumba vya madarasa, vyoo mabweni na maabara ili kuboresha mazingira ya kufundishi na kujifunzia. Ukarabati wa shule hizo unahusisha miundombinu ya mabweni hasa kwa watoto wa kike ili kuweza kupata elimu iliyo bora. Hadi sasa, shule za sekondari 1241 zimejengewa mabweni kati ya shule za sekondari 3634 zinazotumia ruzuku ya Serikali Kuu, mapato ya ndani ya Halmashauri na mchango wa jamii. Serikali itaendelea kujenga mabweni na kushirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo kwa kadiri bajeti itakavyoruhusu. SPIKA: Mheshimiwa Azza Hillal swali la nyongeza tafadhali. MHE. AZZA H. HAMAD: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza maswali ya nyongeza. Awali ya yote niipongeze sana Serikali kwa kazi kubwa ambayo inaifanya katika kuhakikisha inaboresha miundombinu katika shule zetu. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza:- Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; Je, Serikali iko tayari sasa kuhakikisha inajenga mabweni katika shule zetu zilizoanzishwa kimkakati zaidi katika shule ya sekondari Samuye, Kizumbi, Isagenhe na Ukenyenge zilizopo katika 3 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Mkoa wa Shinyanga kwa sababu Wanafunzi wamekuwa wakitembea umbali mrefu na hivyo kukumbana na vishawishi vingi barabarani na kupelekea kupanga mitaani? Mheshimiwa Spika, swali la pili; Je, Serikali hamuoni sasa ni wakati muafaka wa kuweza kufikiria kutokuwapangia shule zilizoko mbali wanafunzi hawa kwa kuwa kila Kata sasa hivi ina shule? Mheshimiwa Spika, nakushukuru. SPIKA: Majibu ya maswali hayo Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mheshimiwa Jafo. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kwanza nikiri, Mheshimiwa Azza takribani wiki mbili au tatu zilizopita alikuwa akinijulisha suala zima la changamoto ya miundombinu ya elimu katika Mkoa ule wa Shinyanga na nilimuhakikishia kwamba Serikali tutafanya kila liwezekanalo, lile linalowezekana tutaenda kulifanyia kazi alichanganye pamoja na ajenda hiyo ya elimu pamoja na ajenda ya afya. Mheshimiwa Spika, hata hivyo naomba niseme kwamba Serikali tutaangalia kila kinachowezekana katika maeneo uliyoyaainisha lile litakalowezekana kwa sasa tutaweza kulifanya. Lakini ni azma ya Serikali kuhakikisha tunapambana miundombinu inaimarika kama tulivyofanya pale sekondari ya Tinde ambapo Mbunge tumeenda wote pamoja pale kwa ajili ya kuona eneo gani lazima tufanye hilo. Mheshimiwa Spika, suala la kutowapangia mbali kwa vile kila Kata sasa ina shule, jambo hili ndiyo kielelezo chetu ni kwamba kama katika Kata hasa zile zetu ambapo kama kuna vijana wamefaulu katika eneo lile ni vyema sasa watoto wakapangiwa kwa karibu zaidi kuepusha usumbufu huo mabao Mheshimiwa Mbunge ulizungumza. Kwa hiyo, 4 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) tumelichukua Serikali na tutalitolea maelekezo katika maeneo mbalimbali. SPIKA: Nilikuona Mheshimiwa Waziri kivuli wa Elimu. MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, pamoja na juhudi za Serikali kuhakikisha kwamba wanajenga mabweni, utakubaliana nami kwamba baadhi ya mabweni hayo yamekuwa yakiungua mara kwa mara na hivi karibuni shule ya Ashira mabweni yake mawili ya wasichana yameungua. Je, Serikali mna utaratibu gani wa kuhakikisha kwamba kunakuwa na ulinzi katika shule hizo ili hii rasilimali kubwa ambayo imeshatumika ya fedha kujenga mabweni hayo iweze kulindwa? Mheshimiwa Spika, ahsante. SPIKA: Pole sana kwa sekondari ya Ashira. Majibu Mheshimiwa Waziri wa Nchi, tafadhali. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Dada yangu Susan. Mheshimiwa Spika, ni kweli na niwape pole Wananchi wote wa Tanzania kwa sababu watoto wale, juzi nilikuwepo Ashira ile shule wkeli imeungua lakini ukija kuangalia taarifa ya awali inaonyesha kwamba ni hujuma tu kwa sababu yale mabweni mawili hayaungani na siyo kwamba kulikuwa na short ya umeme. Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni kweli inawezekana maeneo mengine kuna hujuma na nawaomba niwaeleze Serikali juzi nilisha-deploy timu yangu ya Mainjinia iko pale tokea jana inafanyakazi na leo hii haraka iwezekanavyo ndani ya wiki mbili, tatu tuanze ukarabati wa yale majengo kwa sababu siyo muda mrefu vijana wa form five wengine tutawaingiza katika maeneo yale. Kwa hiyo, tutafanya 5 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) ukarabati wa shule ile yote kwa ujumla wake kuhakikisha inarudi Ashira katika hali yake ya kawaida. Mheshimiwa Spika, lakini hata hivyo ni maelekezo yetu sasa kipaumbele suala zima la walinzi na hasa kuangalia usalama wa shule zetu nini kifanyike kwa sababu tunatumia fedha nyingi sana, haiwezekani watu wenye nia mbaya wakahujumu juhudi hii kubwa ya Serikali na Wananchi wake kwa ujumla. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge kwa sababu ya muda, naomba tuendelee na Viwanda na Biashara swali la Mheshimiwa Maria Ndila Kangoye. Mheshimiwa Maria Na. 298 Sekta Binafsi Kuanzisha Viwanda Vikubwa na vya Kati MHE. MARIA N. KANGOYE aliuliza:- Serikali iliahidi kuhamasisha sekta binafsi kuanzisha viwanda vikubwa na vya kati na kuweka utaratibu wa kuvilinda dhidi ya viwanda vya nje. (a) Je, Serikali imefikia wapi katika zma hii ambayo ni mwelekeo wa kufikia uchumi wa kati na utoaji ajira hasa kwa vijana? (b) Je, Serikali imeweka mkakati upi ili kuweza kujenga mazingira rafiki yatakayowezesha kupunguza gharama za uwekezaji na uendeshaji wa viwanda? SPIKA: Majibu ya swali hilo Mheshimiwa Naibu Waziri, Viwanda na Biashara, Mheshimiwa Eng. Stella Martin Manyanya, tafadhali. NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maria Ndila 6 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Kangoye Lyimo, Mbunge wa Viti Maalum lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, jukumu la Serikali kuhamasisha sekta binafsi kuanzisha viwanda vikubwa na vya kati ni la msingi na endelevu. Serikali imeendelea kuhamasisha wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza katika viwanda kupitia kituo cha uwekezaji Tanzania yaani TIC na mamlaka ya kuendeleza maeneo huru ya uzalishaji kwa ajili ya kuuza nje yaani EPZA. Uhamasishaji huo unaambatana na kutoa vivutio mbalimbali ikiwemo misamaha ya kodi katika mitambo na mshine zinazotumika kwneye uzalishaji. Aidha, Shirika la kuhudumia viwanda vidogo vidogo (SIDO) limekuwa likihamasisha na kusaidia uanzishwaji wa viwanda vidogo na vya kati ambavyo ni msingi wa maendeleo ya viwanda vikubwa kupitia mafunzo na uwezeshaji wa kiufundi na mitaji. Mheshimiwa Spika, pamoja na niliyoeleza katika swali namba 4404 lililojibiwa tarehe 07 Mei, 2019, ili kulinda viwanda vya ndani dhidi ya ushidani usio wa haki, Serikali kupitia Tume ya Ushindani (FCC) na Shirika la viwango Tanzania yaani TBS na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) vimekuwa vikidhibiti uingizaji wa bidhaa hafifu, bandia na zinazoingia kwa njia zisizo rasmi bila kulipiwa kodi. Vilevile Serikali imekuwa ikitoa misamaha ya kodi kwa baadhi ya bidhaa za ndani na kutozwa zaidi baadhi ya bidhaa zinazoingizwa kutoka nje. Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa mazingira bora ya biashara na uwekezaji ni kichocheo muhimu kwa maendeleo ya viwanda Nchini. Kwa kuzingatia
Recommended publications
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    NAKALA YA MTANDAO (ON LINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ BUNGE LA KUMI NA MOJA ___________ MKUTANO WA KWANZA Kikao cha Kwanza - Tarehe 17 Novemba, 2015 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) DKT. THOMAS D. KASHILILAH - KATIBU WA BUNGE: Naomba tukae. TANGAZO LA RAIS LA KUITISHA MKUTANO WA BUNGE DKT. THOMAS D. KASHILILAH - KATIBU WA BUNGE: Waheshimiwa Wabunge, kwa mujibu wa masharti ya Katiba, Mkutano huu wa Kwanza unaanza kwa Rais kuuitisha. Naomba kuchukua nafasi hii kusoma Tangazo la Rais kama ambavyo tumelipokea. Tangazo la Serikali Na. 513 la tarehe 6 Novemba, 2015. Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Sura ya Pili, hati iliyotolewa kwa mujibu wa Ibara ya 90(1). Hati ya Kuitisha Mkutano wa Bunge Jipya. KWA KUWA, Uchaguzi Mkuu ulifanyika tarehe 25 Oktoba, 2015 katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977; NA KWA KUWA, masharti ya Ibara ndogo ya kwanza ya Ibara ya 90 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, yanamtaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuitisha Mkutano wa Bunge Jipya kabla ya kupita siku saba tangu Tume ya Uchaguzi kutangaza matokeo ya Uchaguzi Mkuu; NA KWA KUWA, matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 25 Oktoba, 2015 yalitangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi tarehe 29 Oktoba, 2015; HIVYO BASI, mimi John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa mamlaka niliyonayo chini ya Ibara ya 90(1) ya 1 NAKALA YA MTANDAO (ON LINE DOCUMENT) Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, naitisha Mkutano wa Bunge Jipya la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ufanyike katika ukumbi wa Bunge uliopo Mjini Dodoma tarehe 17 Novemba, 2015 kuanzia saa tatu asubuhi.
    [Show full text]
  • Issued by the Britain-Tanzania Society No 114 May - Aug 2016
    Tanzanian Affairs Issued by the Britain-Tanzania Society No 114 May - Aug 2016 Magufuli’s “Cleansing” Operation Zanzibar Election Re-run Nyerere Bridge Opens David Brewin: MAGUFULI’S “CLEANSING” OPERATION President Magufuli helps clean the street outside State House in Dec 2015 (photo State House) The seemingly tireless new President Magufuli of Tanzania has started his term of office with a number of spectacular measures most of which are not only proving extremely popular in Tanzania but also attracting interest in other East African countries and beyond. It could be described as a huge ‘cleansing’ operation in which the main features include: a drive to eliminate corruption (in response to widespread demands from the electorate during the November 2015 elections); a cutting out of elements of low priority in the expenditure of government funds; and a better work ethic amongst government employees. The President has changed so many policies and practices since tak- ing office in November 2015 that it is difficult for a small journal like ‘Tanzanian Affairs’ to cover them adequately. He is, of course, operat- ing through, and with the help of ministers, regional commissioners and cover photo: The new Nyerere Bridge in Dar es Salaam (see Transport) Magufuli’s “Cleansing” Operation 3 others, who have been either kept on or brought in as replacements for those removed in various purges of existing personnel. Changes under the new President The following is a list of some of the President’s changes. Some were not carried out by him directly but by subordinates. It is clear however where the inspiration for them came from.
    [Show full text]
  • Bunge Newsletter
    BungeNe ewsletter Issue No 008 June 2013 New Budget Cycle Shows Relavance For the first time in recent Tanzania history the engage the government and influence it make sev- Parliament has managed to pass the next financial eral tangible changes in its initial budget proposals. year budget before the onset of that particular year. This has been made possible by the Budget Commit- This has been made possi- tee, another new innovation by Speaker Makinda. ble by adoption of new budget cycle. Under the old cycle, it was not possible to influence According to the new budget cycle, the Parliament the government to make changes in budgetary allo- starts discussing the budget in April as opposed to cations. That was because the main budget was read, old cycle where debate on the new budget started on debated and passed before the sectoral plans. After June and ends in the first or second week of August. the main budget was passed, it was impossible for the MPs and government to make changes in the When the decision was taken to implement the new sectoral budgets since they were supposed to reflect budget cycle and Speaker Anne Makinda announced the main budget which had already been passed. the new modalities many people, including Mem- bers of Parliament, were skeptical. Many stakehold- These and many other changes have been made possi- ers were not so sure that the new cycle would work. ble through the five components implemented under the Parliament five years development plan. “Govern- But Ms Makinda has managed to prove the doubt- ment and Budget Oversight and Accountability is one ers wrong.
    [Show full text]
  • Global Report
    In Focus Tanzania ruling party are no longer as united and pre- years. These include bribes paid to well- dictable as they have been throughout the connected intermediaries by the UK’s BAE country’s history as an independent nation. Systems, irregular payments of millions Political commentators of dollars from special here say that there are accounts at the central now at least two fac- bank (Bank of Tanza- tions within the party nia – BoT), inlated battling it out for in- construction contracts luence. In essence the for the BoT’s ‘twin two sides are those said towers’ headquarters, to be championing the as well as improperly ight against corruption awarded contracts for Women want more and those determined to the provision of emer- maintain the status quo gency electric power. In representation of kulindana (a Swahili one of the latter cases, Tanzania’s upcoming general elections term that can be loosely former Prime Minister, should bring great progress in women’s translated as ‘scratch Edward Lowassa, and empowerment and their participation in my back and I’ll scratch two cabinet colleagues, decision-making. That is if the ruling Chama yours’). Ibrahim Msabaha and Although it lost its Nazir Karamagi, took Cha Mapinduzi (CCM) keeps the promise status as the country’s political responsibility made in its 2005 election manifesto, that sole political party in for the so-called ‘Rich- it would achieve 50 percent women’s 1992, the Chama Cha President Jakaya Kikwete seeks election for mond affair’ by resign- participation in Parliament and local councils Mapinduzi (CCM – a second five-year term in October ing in 2008.
    [Show full text]
  • Hotuba Ya Bajeti Ya Wizara Ya Mambo Ya Nje 2012/2013 Posted: Monday August 06, 2012 1:06 PM BT
    Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje 2012/2013 Posted: Monday August 06, 2012 1:06 PM BT HOTUBA YA WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA MHESHIMIWA BERNARD KAMILLIUS MEMBE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO W A KIMATAIFA KWA MWAKA WA FEDHA 2012/2013 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), naomba sasa kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu lipokee, lijadili na kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa mwaka wa fedha 2012/2013. 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kutumia fursa hii kukupongeza wewe binafsi kwa kuliongoza kwa umahiri mkubwa Bunge hili la Bajeti la mwaka 2012/2013. Napenda pia kuwapongeza Mheshimiwa Job Ndugai (Mb.), Naibu Spika na Waheshimiwa Wenyeviti wanaokusaidia kuongoza Bunge hili kwa kazi nzuri wanayoifanya. 3. Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee nachukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa uongozi wake mahiri wa Serikali ya Awamu ya Nne. Chini ya uongozi wake Taifa letu limeendeleza utamaduni wetu wa kudumisha amani, utulivu na mshikamano. Nawaomba Watanzania wote tuendelee kudumisha hali hiyo ili kuimarisha umoja wetu ambao ni tunu isiyopatikana kwa bei yoyote. 4. Mheshimiwa Spika, niruhusu niungane na Waheshimiwa Wabunge wengine wote walionitangulia kuwapongeza kwa dhati kabisa Waheshimiwa Wabunge wapya, Mawaziri na Naibu Mawaziri walioteuliwa na Mheshimiwa Rais mwezi Mei 2012. Nawapongeza Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge waliochaguliwa kipindi hiki kutokana na mabadiliko yaliyotokea kwenye nafasi mbalimbali humu Bungeni na ndani ya Serikali.
    [Show full text]
  • Check Against Delivery HOTUBA YA WAZIRI MKUU, MHESHIMIWA
    Check Against Delivery HOTUBA YA WAZIRI MKUU, MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA, (MB), WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA SITA WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, DODOMA, TAREHE 9 FEBRUARI, 2007 Mheshimiwa Spika, Mkutano wa sita wa Bunge lako Tukufu umehitimisha shughuli zote zilizokuwa zimepangwa. Mkutano huu ni wa kwanza baada ya Serikali ya Awamu ya Nne kutimiza mwaka mmoja madarakani. Taarifa za mafanikio na changamoto zilizojitokeza zimewasilishwa kupitia mikutano mbalimbali ya Chama Tawala, Serikali na vyombo mbalimbali vya habari. Mheshimiwa Spika, kwa masikitiko makubwa, nachukua nafasi hii tena kwa niaba ya Serikali na wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kutoa rambirambi kwako wewe Mheshimiwa Spika, kwa Waheshimiwa Wabunge wote, kwa familia, jamaa na marafiki kwa msiba uliotokana na kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tunduru, na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Bunge na Uratibu) Marehemu Juma Jamaldin Akukweti. Wote tulimfahamu Marehemu Akukweti kwa umakini na umahiri wake hapa Bungeni. Marehemu Akukweti alifariki kutokana na ajali ya ndege iliyokuwa inamrejesha Dar es Salaam baada ya kumaliza kazi ya kukagua soko la Mwanjelwa lililoteketea kwa moto mkoani Mbeya. Katika ajali hiyo Watumishi wa Serikali walipoteza maisha. Watumishi hao ni Bibi Theresia Nyantori, Mwandishi wa Habari wa Idara ya Habari; Bwana Nathaniel Katinila, Mratibu wa Mradi wa Masoko; na Bwana George Bendera, Afisa Habari Idara ya Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu. Majeruhi katika ajali hiyo ambao bado wanapata matibabu lakini wametoka hosptali ni Bw. Nisetas Kanje, Katibu wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Bunge na Uratibu); na rubani wa ndege hiyo Bw. Martin Sumari. Tunamwomba Mwenyezi Mungu awasaidie majeruhi wote waweze kupona haraka na kurudia katika afya zao.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA SABA Kikao Cha Ishirini Na Tano – Tarehe 15
    NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 15 Mei, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Mussa A. Zungu) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu! NDG. CHARLES MLOKA – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. MWENYEKITI: Ahsante. Katibu. NDG. CHARLES MLOKA – KATIBU MEZANI: Maswali. 1 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MASWALI NA MAJIBU Na. 200 Mgongano wa Kiutendaji – Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Wananchi wa Songea Mjini wamekuwa wakiitumia Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma kama Hospitali yao ya Wilaya hivyo kufanya kuwepo na mgongano wa kiutendaji kati ya Mamlaka ya Mkoa inayoitambua Hospitali hiyo kama Rufaa ya ngazi ya Mkoa na Mamlaka ya Wilaya. Tarehe 10 Januari, 2016, Mheshimiwa Waziri wa Afya alifika kuona hali halisi na juhudi za wananchi wa Songea Mjini za kujenga Kituo cha Afya Mji Mwema ambacho kimefikia hatua kubwa, hivyo wakamwomba Waziri kituo hicho kipandishwe hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya, Songea Mjini. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuiacha Hospitali ya Mkoa ifanye kazi ya Rufaa Kimkoa? (b) Je, Serikali haioni haja ya kupunguza msongamano katika hospitali hiyo kwa kuanzisha Hospitali ya Wilaya Songea Mjini? (c) Je, ni lini basi Serikali
    [Show full text]
  • MKUTANO WA TATU Kikao Cha Hamsini Na Sita
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Hamsini na Sita – Tarehe 22 Juni, 2021 (Bunge Lilianza saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba tukae. Waheshimiwa tunaendelea na Mkutano wetu wa Tatu, leo ni Kikao cha Hamsini na Sita na kabla hatujaendelea nitumie nafasi hii kuwashukuru sana wasaidizi wangu wote wakiongozwa na Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa David Kihenzile, Mheshimiwa Zungu na Mheshimiwa Najma kwa kazi nzuri ambayo wameifanya wiki nzima kutuendeshea mjadala wetu wa bajeti. (Makofi) Sasa leo hapa ndio siku ya maamuzi ambayo kila Mbunge anapaswa kuwa humu ndani, kwa Mbunge ambaye Spika hana taarifa yake na hatapiga kura hapa leo hilo la kwake yeye. (Makofi) Katibu. NDG. NENELWA MWIHAMBI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Maswali na tunaanza na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Kwela. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Na. 465 Ujenzi wa Makao Makuu ya Halmashauri Katika Mji wa Laela MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi za Makao Makuu ya Halmashauri ya Sumbawanga katika Mji wa Laela baada ya agizo la Serikali la kuhamisha Makao Makuu? SPIKA: Majibu ya swali hilo muhimu la watu wa Kwela, Mheshimiwa Naibu Waziri - TAMISEMI, Mheshimiwa Dkt. Festo Dugange tafadhali. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Jimbo la Kwela kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ni miongoni mwa Halmashauri 30 zilizohamia kwenye maeneo mapya ya utawala mwaka 2019.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA TATU Kikao Cha Kumi Na Tisa – Tarehe 29 Aprili, 2021
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Kumi na Tisa – Tarehe 29 Aprili, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa, tukae. Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2021/2022. NAIBU WAZIRI WA MADINI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2021/2022. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. SAADA MONSOUR HUSSEIN - K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2020/2021 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2021/2022. NAIBU SPIKA: Ahsante sana. Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa maswali, tutaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Busega, sasa aulize swali lake. Na. 158 Serikali Kukamilisha Ujenzi wa Zahanati – Busega MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza:- Wananchi wa Kata ya Imalamate Wilayani Busega wamejenga zahanati na kumaliza maboma manne kwa maana ya zahanati moja kila kijiji:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi hao kuezeka maboma hayo ili waweze kupata huduma za afya kwenye zahanati hizo? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Dkt.
    [Show full text]
  • Issued by the Britain-Tanzania Society No 124 Sept 2019
    Tanzanian Affairs Issued by the Britain-Tanzania Society No 124 Sept 2019 Feathers Ruffled in CCM Plastic Bag Ban TSh 33 trillion annual budget Ben Taylor: FEATHERS RUFFLED IN CCM Two former Secretary Generals of the ruling party, CCM, Abdulrahman Kinana and Yusuf Makamba, stirred up a very public argument at the highest levels of the party in July. They wrote a letter to the Elders’ Council, an advisory body within the party, warning of the dangers that “unfounded allegations” in a tabloid newspaper pose to the party’s “unity, solidarity and tranquillity.” Selection of newspaper covers from July featuring the devloping story cover photo: President Magufuli visits the fish market in Dar-es-Salaam following the plastic bag ban (see page 5) - photo State House Politics 3 This refers to the frequent allegations by publisher, Mr Cyprian Musiba, in his newspapers and on social media, that several senior figures within the party were involved in a plot to undermine the leadership of President John Magufuli. The supposed plotters named by Mr Musiba include Kinana and Makamba, as well as former Foreign Affairs Minister, Bernard Membe, various opposition leaders, government officials and civil society activists. Mr Musiba has styled himself as a “media activist” seeking to “defend the President against a plot to sabotage him.” His publications have consistently backed President Magufuli and ferociously attacked many within the party and outside, on the basis of little or no evidence. Mr Makamba and Mr Kinana, who served as CCM’s secretary generals between 2009 to 2011 and 2012-2018 respectively, called on the party’s elders to intervene.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 18 Julai, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita muuliza swali la kwanza nina matangazo kuhusu wageni, kwanza wale vijana wanafunzi kutoka shule ya sekondari, naona tangazo halisomeki vizuri, naomba tu wanafunzi na walimu msimame ili Waheshimiwa Wabunge waweze kuwatambua. Tunafurahi sana walimu na wanafunzi wa shule zetu za hapa nchini Tanzania mnapokuja hapa Bungeni kujionea wenyewe demokrasia ya nchi yetu inavyofanya kazi. Karibuni sana. Wapo Makatibu 26 wa UWT, ambao wamekuja kwenye Semina ya Utetezi na Ushawishi kwa Harakati za Wanawake inayofanyika Dodoma CCT wale pale mkono wangu wakulia karibuni sana kina mama tunawatakia mema katika semina yenu, ili ilete mafanikio na ipige hatua mbele katika kumkomboa mwanamke wa Tanzania, ahsanteni sana. Hawa ni wageni ambao tumetaarifiwa na Mheshimiwa Shamsa Selengia Mwangunga, Naibu Waziri wa Maji. Wageni wengine nitawatamka kadri nitakavyopata taarifa, kwa sababu wamechelewa kuleta taarifa. Na. 223 Barabara Toka KIA – Mererani MHE. DORA H. MUSHI aliuliza:- Kwa kuwa, Mererani ni Controlled Area na ipo kwenye mpango wa Special Economic Zone na kwa kuwa Tanzanite ni madini pekee duniani yanayochimbwa huko Mererani na inajulikana kote ulimwenguni kutokana na madini hayo, lakini barabara inayotoka KIA kwenda Mererani ni mbaya sana
    [Show full text]