Tarehe 21 Mei, 2015
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Tisa – Tarehe 21 Mei, 2015 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kwa mujibu wa Kanuni ya 33(1) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2013; tarehe 15 Mei, 2015 nilitoa taarifa kwamba Miswada tisa ya Sheria ya Serikali iliyopitishwa katika Mkutano wa Kumi na Tisa wa Bunge ilikwishapata kibali cha Mheshimiwa Rais na kuwa Sheria za nchi. Kwa taarifa hii ya leo, napenda kuliarifu Bunge hili Tukufu kwamba Miswada mitano iliyokuwa imebaki nayo imekwishapata kibali cha Mheshimiwa Rais na kuwa sheria ziitazwo:- Ya kwanza, Sheria ya Udhibiti na Usimamizi wa Dawa za Kulevya ya Mwaka 2015 (The Drug Control and Enforcement Act, 2015) Na. 5 ya Mwaka 2015. Ya pili, Sheria ya Usimamizi wa Maafa ya Mwaka 2015, (The Disaster Management Act, 2015) Na. 7 ya Mwaka 2015. Ya tatu, Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Uhamiaji ya Mwaka 2015 (The Immigration Amendment Act, 2015) Na. 8 ya Mwaka 2015. Ya nne, Sheria ya Usimamizi wa Kodi ya Mwaka 2015, (The Tax Administration Act, 2015) Na. 10 ya Mwaka 2015 na; Ya Tano, Sheria ya Bajeti ya Mwaka 2015 (The Budget Act) Na. 11 ya Mwaka 2015. 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) Kwa hiyo, Waheshimiwa sasa hii ni Miswada ya kisheria. (Makofi) HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa na:- SPIKA: Waheshimiwa Wabunge hati za kuwasilisha mezani, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi! Mheshimiwa Naibu Waziri! NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Randama za Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2015/2016.
[Show full text]