Online Document)
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1 BUNGE LA TANZANIA
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ________________________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Kumi na Tisa – Tarehe 27 Mei, 2014 (Mkutano Ulianza Saa tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA: Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha kwa Mwaka 2012/2013 (The Annual Report and Accounts of Arusha International Conference Centre for the Year 2012/2013). Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. BETTY E. MACHANGU (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na Maoni ya Kamati 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. ABDULKARIM E.H. SHAH (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA ARDHI, MALIASILI NA MAZINGIRA): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. -
Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Tano – Tarehe 15 Mei, 2014 (Kikao Kilianza Saa tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, leo ni siku ya Alhamisi, kwa hiyo Kiongozi wa Kambi ya Upinzani hayupo hata ukikaa karibu hapo wewe siyo kiongozi. Kwa hiyo, nitaendelea na wengine kadiri walivyoleta, tunaanza na Mheshimiwa Eugen Mwaiposa. HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na :- NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Hotuba ya Makadirio ya Matumizi na Mapato ya Fedha ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa mwaka wa fedha 2014/2015. NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. NYAMBARI C. NYANGWINE (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha wa 2013/2014 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. 1 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) MHE. CYNTHIA H. NGOYE (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ulinzi na Usalama Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumuzi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. -
Majadiliano Ya Bunge ______
NAKALA YA MTANDAO (ON LINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ BUNGE LA KUMI NA MOJA ___________ MKUTANO WA KWANZA Kikao cha Kwanza - Tarehe 17 Novemba, 2015 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) DKT. THOMAS D. KASHILILAH - KATIBU WA BUNGE: Naomba tukae. TANGAZO LA RAIS LA KUITISHA MKUTANO WA BUNGE DKT. THOMAS D. KASHILILAH - KATIBU WA BUNGE: Waheshimiwa Wabunge, kwa mujibu wa masharti ya Katiba, Mkutano huu wa Kwanza unaanza kwa Rais kuuitisha. Naomba kuchukua nafasi hii kusoma Tangazo la Rais kama ambavyo tumelipokea. Tangazo la Serikali Na. 513 la tarehe 6 Novemba, 2015. Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Sura ya Pili, hati iliyotolewa kwa mujibu wa Ibara ya 90(1). Hati ya Kuitisha Mkutano wa Bunge Jipya. KWA KUWA, Uchaguzi Mkuu ulifanyika tarehe 25 Oktoba, 2015 katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977; NA KWA KUWA, masharti ya Ibara ndogo ya kwanza ya Ibara ya 90 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, yanamtaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuitisha Mkutano wa Bunge Jipya kabla ya kupita siku saba tangu Tume ya Uchaguzi kutangaza matokeo ya Uchaguzi Mkuu; NA KWA KUWA, matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 25 Oktoba, 2015 yalitangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi tarehe 29 Oktoba, 2015; HIVYO BASI, mimi John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa mamlaka niliyonayo chini ya Ibara ya 90(1) ya 1 NAKALA YA MTANDAO (ON LINE DOCUMENT) Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, naitisha Mkutano wa Bunge Jipya la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ufanyike katika ukumbi wa Bunge uliopo Mjini Dodoma tarehe 17 Novemba, 2015 kuanzia saa tatu asubuhi. -
Conference Report
2 ND GOPAC GLOBAL CONFERENCE Arusha, Tanzania September 19-23, 2006 FINAL REPORT GLOBAL ORGANISATION OF PARLIAMENTARIANS AGAINST CORRUPTION: 2ND GLOBAL CONFERENCE Acknowledgements The Global Organisation of Parliamentarians Against Corruption wishes to thank the following organisations for their contributions to the 2nd Global Conference: Parliament of Tanzania African Parliamentarians Network Against Corruption (APNAC) Barrick Gold Canadian International Development Agency (CIDA) US Agency for International Development (USAID) World Bank Institute (WBI) Events Hosts Dr. Zainab A. Gama, MP, Chair, APNAC – Tanzania Arusha Regional Commissioner Col (Rtd). Samuel Ndomba H.E. Dr. Ali Mohamed Shein the Vice President of the United Republic of Tanzania Hosted by Hon. Samuel Sitta, MP – Speaker of the National Assembly Guest Speakers Deputy Barrister Emmanuel Akomaye, Economic and Financial Crimes Commission of Nigeria Doris Basler, Transparency International Hon. Ruth Kavuma, MP, Vice Chair, APNAC Uganda Mr. Paul Wolfowitz, President, World Bank (Taped message) Conference and Workshop Speakers Conference Chair: John Williams MP (Canada) Edward Doe Adjaho, MP (Ghana) Naser Al Sane, MP (Kuwait) Edgardo Angara, Senator (Philippines) Stella Cittadini, Senator (Argentina) Roy Cullen, MP (Canada) César Jauregui, Senator (Mexico) Edith Mastenbroek, MEP (Netherlands) J.T.K. Green-Harris, MP (Gambia) Mary King, Senator (Trinidad and Tobago) Omingo Magara, MP (Kenya) Augustine Ruzindana, Former MP (Uganda) Willibroad Slaa, MP (Tanzania) Navin Beekarry (IMF) Giovanni Gallo (UNODC) Scott Hubli (UNDP) Latifah Merican Cheong (World Bank) Carmen Lane (DAI) Luis Gerardo Villanueva, Former MP (Costa Murray Michel (Egmont Group and Rica) FATF) Patrick Moulette (IMF) Keith Schulz (USAID) Ingeborg Schwarz (IPU) Emiko Todoroki (WB) Frederick Stapenhurst (WBI) Stuart Yikona (WB) GOPAC wishes to thank the following individuals for their significant contribution to the conference and its administration: Canadian High Commission - Tanzania Parliament of Tanzania H.E. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Tatu – Tarehe 15 APRILI, 2010 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU NAIBU SPIKA: Maswali kwa Waziri Mkuu leo kiongozi wa Upinzani Bungeni hayupo kwa hiyo nitaenda na orodha za wachangiaji na nitakuwa ninakwenda kufuatana na itikadi ya chama, upande, gender na vitu kama hivyo. Kwa hiyo, walioko hapa wasidhani watakwenda kama ilivyoorodheshwa. Kwa hiyo, nitaanza na msemaji wa kwanza Mheshimiwa Dr. Willibrod Slaa. MHE. DR. WILLIBROD P. SLAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kunipa nafasi, Mheshimiwa Waziri Mkuu sasa ni takribani mwaka mzima tangu nilipoanza kuhoji, mimi na Wabunge wenzangu, tulipoanza kuhoji kuhusu ubadhirifu na tuhuma mbalimbali zilizokuwa zinakabili matumizi ya fedha za umma zilizofanywa na makampuni kama Mwananchi Gold Company, Tan Gold, Kagoda, Deep Green na mengine mengi ambayo yalitajwa ndani ya ukumbi huu. Kwa nyakati tofauti maelezo mbalimbali yametolewa ndani ya Bunge. Mpaka leo hatujapata taarifa ya kinachoendelea. Bunge hili lenye jukumu la kuisimamia Serikali halijui au wananchi hawajui kama kuna kitu kinaendelea je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu ubadhirifu huo? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naamini kabisa Dr. Slaa, hutegemei kwamba kweli nitaweza kujibu maswali hayo uliyoyauliza kwamba mimi nina maelezo juu ya Kagoda, maelezo juu ya nani, is not possible nadhani si sahihi kabisa. (Makofi) Mimi ninachoweza kusema ni kwamba jitihada za Serikali zipo zimekuwa zikionekana katika maeneo ambayo yameshaanza kufanyiwa kazi. Sasa kama kuna maeneo ambayo bado hayajafanyiwa kazi jitihada za Serikali zitaendelea kwa kadri itakavyowezekana. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE ________________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 17 Julai, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO:- Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa mwaka wa Fedha 2012/2013. NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:- Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa Fedha 2012/2013. MHE. EUGEN E. MWAIPOSA (K.n.y. MHE. EDWARD LOWASSA - MWENYEKITI WA KAMATI YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA):- Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka 2011/2012 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. MHE. VINCENT J. NYERERE – MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani juu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tunaanza maswali kwa Ofisi ya Waziri Mkuu, atakayeuliza swali letu la kwanza ni Mheshimiwa Beatrice Matumbo Shellukindo kwa niaba yake Mheshimiwa Herbert Mntangi. -
Majadiliano Ya Bunge Mkutano Wa Kumi Na Sita
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Tano – Tarehe 15 Juni, 2009 (Mkutano ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- MWENYEKITI WA KAMATI YA FEDHA NA UCHUMI: Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha Mezani Taarifa ya Kamati ya Fedha na Uchumi Kuhusu Utekelezaji wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2008/2009 na Mwelekeo wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2009/2010. MHE. MWADINI ABBAS JECHA K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA WIZARA YA FEDHA NA UCHUMI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Wizara ya Fedha na Uchumi, naomba kuwasilisha Mezani Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Wizara ya Fedha na Uchumi juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka 2009/2010. MASWALI NA MAJIBU Na. 33 Athari za Milipuko ya Mabomu - Mbagala MHE. KHADIJA SALUM ALI AL-QASSMY K.n.y. MHE. ANIA S. CHAUREMBO aliuliza:- Kwa kuwa, tukio la tarehe 29 Aprili, 2009 la milipuko ya mabomu kwenye Kambi ya Jeshi la Wananchi – JWTZ, Mbagala Kizuiani, limesababisha hasara kubwa kama vile, watu kupoteza maisha, watu wengi kujeruhiwa, uharibifu mkubwa wa mali na 1 nyumba za wananchi, kuharibika kwa miundombinu na kadhalika. Na kwa kuwa, kuna Kamati maalum inayoshughulikia majanga yanapotokea ambayo iko chini ya Ofisi ya waziri Mkuu:- Je, ni sababu zipi zilizofanya Kamati hiyo isifike kwa haraka kwenye eneo la tukio na kutoa msaada wa haraka uliotakiwa? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU – SERA, URATIBU NA BUNGE alijibu:- Mheshimiwa Spika, kabla sijajibu swali hili naomba kutoa mkono wa pole sana kwa Mheshimiwa Ania Chaurembo, kwa msiba wa Mama yake Mzazi. -
Hotuba Ya Rais Wa Zanzibar Na Mwenyekiti Wa Baraza La Mapinduzi, Mhe
1 HOTUBA YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI, MHE. DK. ALI MOHAMED SHEIN, KATIKA SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR, UWANJA WA AMAAN TAREHE 12 JANUARI, 2014 Waheshimiwa Wageni wetu, Wakuu wa Nchi na Serikali na Mawaziri wa Nchi Rafiki mliohudhuria hapa leo, Mheshimiwa Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Dk. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Kwanza wa Rais, Zanzibar; Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi, Makamu wa Pili wa Rais, Zanzibar; Mheshimiwa Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Dk. Salmin Amour Juma, Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi; Mheshimiwa Dk. Amani Abeid Karume, Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi; Viongozi Wakuu Wastaafu Mliohudhuria; Waheshimiwa Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar; Mheshimiwa Mama Anne Makinda, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; 2 Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho, Spika wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar; Mheshimiwa Othman Chande Mohamed, Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Omar Othman Makungu, Jaji Mkuu wa Zanzibar; Waheshimiwa Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa; Mheshimiwa Abdalla Mwinyi, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi; Waheshimiwa Viongozi wa Serikali na Vyama vya Siasa; Ndugu Wananchi, Mabibi na Mabwana; Assalaam Alaykum, Kwa unyenyekevu mkubwa, namshukuru Mwenyezi Mungu, Muumba Mbingu na Ardhi na vyote vilivyomo ndani yake, kwa kutujaalia uhai na uzima wa afya, tukaweza kukusanyika hapa leo kuadhimisha miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, ya tarehe 12 Januari, 1964. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Kumi na Tatu – Tarehe 10 Februari, 2010 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI (MHE. OMAR YUSSUF MZEE): Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Benki ya Posta Tanzania, kwa Mwaka 2008 [The Annual Report and Accounts of The Tanzania Postal Bank for the Year 2008]. The Mid-Term Review of the Monetary Policy Statement of The Bank of Tanzania for the Year 2009/2010. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini juu ya Taarifa ya Serikali Kuhusu Ubinafsishwaji wa Mgodi wa Kiwira. Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Mchakato wa Zabuni ya Kuzalisha Umeme wa Dharura Ulioipa Ushindi Kampuni ya Richmond Development Company LLC. Houston Texas - Marekani Mwaka 2006. MWENYEKITI WA KAMATI YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Miundombinu Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelzaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Uendeshaji Usioridhisha wa Shirika la Reli Tanzania uliofanywa na Kampuni ya RITES ya India. 1 Taarifa ya Kamati ya Miundombinu Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Utendaji wa Kazi Usioridhisha wa Kampuni ya TICTS. MASWALI NA MAJIBU Na. 145 Usimamizi wa Ukaguzi wa Fedha za Halmashauri MHE. HERBERT J. MNTANGI aliuliza:- Kwa kuwa, kiasi cha fedha kinachopelekwa katika Halmashauri za Wilaya, Manispaa na Jiji ni kikubwa na kinahitaji usimamizi wa ziada:- Kwa kuwa kitengo cha ukaguzi wa ndani kipo chini ya Mkurugenzi Mtendaji. -
MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA NANE Kikao Cha Kumi Na Tano
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Kumi na Tano – Tarehe 3 Julai, 2007 (Kikao Kilianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI:- Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, mkiangalia Order Paper yetu ya leo, hati za kuwasilisha Mezani iko, Ofisi ya Makamu wa Rais, yuko Mwenyekiti wa Kamati ya Maliasili na Mazingira, tumemruka Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba na Sheria na Utawala, halafu atakuja Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MAZINGIRA): Hotuba ya Bajeti ya Wizari wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais kwa Mwaka wa Fedha wa 2007/2008. MWENYEKITI WA KAMATI YA MALIASILI NA MAZINGIRA: Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Maliasili na Mazingira kuhusu Utekelezaji wa Ofisi ya Makamu wa Rais kwa Mwaka wa Fedha uliopita pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Ofisi hiyo kwa Mwaka 2007/2008. MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA (MHE. RAMADHAN A. MANENO): Tarifa ya Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala kuhusu Utekelezaji wa Ofisi ya Makamu wa Rais – Muungano kwa mwaka wa Fedha 2006/2007 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2007/2008. MHE. RIZIKI OMARI JUMA (k.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI BUNGENI): 1 Maoni ya Kambi ya Upinzani kuhusu Utekelezaji wa Ofisi ya Makamu wa Rais kwa Mwaka wa Fedha uliopita pamoja Maoni ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Ofisi hiyo kwa Mwaka 2007/2008. -
Python Challenge #1 in Python, We Can Use Lists To
Python Challenge #1 In Python, we can use lists to store related items together in a single place. Two examples are: tanzanian_election_years = [1995, 2000, 2005, 2010, 2015] tanzanian_presidents = [“John Magu uli!, “Ja"aya #i"$ete!, “%en&a'in M"apa!, ( “)li *assan M$inyi!, “Julius +yerere!] 1. On a computer or tablet, write a Python program that prints out each year that Tanzania has had a general election. In Python, you can loop over the items of a list like this: or ite' in list, - do so'ething $ith ite' 2. Using your answer for #1, change it slightly so that it only prints out the years in which Tanzania has had a general election after the year 1999. 3. Sometimes we want to work with two lists at the same time. Say we are given the following list of Tanzanian vice presidents: tanzanian_.ice_presidents = [“/a'ia /uluhu!, “Moha'ed 0hari1 %ilal!, ( “2'ar )li Ju'a!, “3leopa Msuya!, “)1oud Ju'1e!] and we want to match each vice president with the president he or she served with. We can use Python’s zip() function to do this. To illustrate how zip() works, type the following into your Python interpreter (note: don’t type the “>>>”, that is printed by the Python interpreter itself): 444 ruits = [“apple!, “grape!, “1lue1erry!] 444 colors = [“green!, “purple!, “1lue!] 444 zip5 ruits, colors6 [57apple8, 7green86, 57grape8, purple86, 571lue1erry8, 71lue86] Notice how Python matched each of the fruits in our first list with its corresponding color in the second list. The zip() function itself returns a list, which we can use in our own for loops. -
6 MEI, 2013 MREMA 1.Pmd
6 MEI, 2013 BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Tisa – Tarehe 6 Mei, 2013 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tukae. Waheshimiwa, mtakuwa mmepata Supplementary Order Paper, halafu na ile paper ya kwanza Supplementary hiki ni Kikao cha 19, wameandika 18 ni Kikao cha 19. Kwa hiyo, mtakuwa na Supplementary Order Paper. Katibu tuendelee? HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatayo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. 1 6 MEI, 2013 MHE. AUGUSTINO M. MASELE (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ulinzi na Usalama Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. MHE. GRACE S. KIWELU (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. MASWALI NA MAJIBU Na. 145 Wajibu wa Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji MHE. MARIAM R. KASEMBE (K.n.y. MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA) aliuliza:- Msingi mkubwa wa Maendeleo ya Jamii huanzia kwenye ngazi ya Mitaa na Vijiji ambapo hutegemea ubunifu na utendaji wa Viongozi wa ngazi husika.