MKUTANO WA KUMI NA SABA Kikao Cha
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA SABA Kikao cha Kwanza – Tarehe 5 Novemba, 2019 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) WIMBO WA TAIFA D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge naomba tukae sasa. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge katika Mkutano wa Kumi na Sita wa Bunge, Bunge lilipitisha Miswada minne ya Sheria ya Serikali ifuatayo:- Kwanza, Muswada wa Sheria ya Serikali Mtandao ya Mwaka 2019 (The e- Government Bill, 2019). Pili, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali Na. 4 wa Mwaka 2019 (The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 4, Bill, 2019). Tatu, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 5 wa Mwaka 2019, (The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 5, Bill, 2019. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Nne, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali Na. 6 wa Mwaka 2019, ((The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 6, Bill, 2019. Kwa Taarifa hii, napenda kuliarifu Bunge kwamba tayari Miswada hiyo minne imepata kibali cha Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwa sheria za nchi, sasa zimekuwa sheria za nchi zinazoitwa kama ifuatavyo;- (Makofi) Sheria ya kwanza, ni Sheria ya Serikali Mtandao Na. 10 ya Mwaka 2019 (The e- Government Act No. 10 of 2019. Ya pili, ni sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali Na. 4, Sheria Na. 11 ya Mwaka 2019 ((The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 4, Act No.11 of 2019; na Tatu, Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na.
[Show full text]