25 JUNI, 2013 MREMA FULL.Pmd
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Tatu – Tarehe 12 Julai, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Jenista J. Mhagama) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. MASWALI NA MAJIBU Na. 213 Ugumu wa Kutekeleza Kazi za Kiutawala Jimbo la Kwela MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:- Jimbo la Kwela, limegawanyika katika Makao Makuu Mawili yaliyojitenga Kijiografia, yaani eneo la ukanda wa juu (Mlimani) na eneo la ukanda wa chini (Bonde la Mto Rukwa) ambapo husababisha ugumu katika kuzitekeleza kazi za kiutawala za uwakilishi hasa ikizingatiwa pia kuwa miundombinu ya barabara ni duni sana:- (a) Je, Serikali haioni kuwa inafaa kuligawa eneo hilo kulingana na Jiografia ili kupata Jimbo jingine au Wilaya? (b) Je, ni kasoro gani zilizosababisha jimbo hilo kukosa sifa za kugawanywa kupata Majimbo mawili kulingana na Jiografia jinsi ilivyo? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE alijibu:- 1 Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ignas Aloyce Malocha, Mbunge wa Kwela, kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Uchaguzi hugawanywa kwa kuzingatia Vigezo 13, kama ifuatavyo:- 1. Idadi ya watu; 2. Upatikanaji wa mawasiliano; 3. Hali ya kijiografia; 4. Mgawanyo wa wastani wa idadi ya watu; 5. Hali ya kiuchumi ya Jimbo; 6. Ukubwa wa eneo la Jimbo husika; 7. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka. -
Tarehe 15 Aprili, 2011
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Nane – Tarehe 15 Aprili, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Taarifa ya Mwaka na Hesabu zilizokaguliwa za Tume ya Ushindani kwa Mwaka wa Fedha 2008/2009 (The Annual Report and Audited Accounts of the Fair Competition Commission (FCC) for the Financial Year 2008/2009). Taarifa ya Mwaka na Hesabu zilizokaguliwa za Wakala wa Usajili wa Biashara na Utoaji Leseni kwa Mwaka wa Fedha 2006/2007 na Mwaka wa Fedha 2007/2008 (The Annual Reports and Audited Accounts of Business Registrations and Licensing Agency (BRELA) for the Financial Years 2006/2007 and 2007/2008). MASWALI NA MAJIBU Na. 100 Mpango wa Kutwaa Ardhi kwa Ajili ya Kupanga na Kupanua Mji MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.N.Y. MHE. PHILIPA G. MTURANO) aliuliza:- Serikali ina mpango wa kutwaa ardhi za Wananchi wa Kata ya Somangila, Mitaa ya Kizani na Mwera kupima viwanja kwa lengo la kupanua mji; na kwa mujibu wa Sheria ya Vijiji ya Mwaka 1999 na Kanuni zake zinazitaka mamlaka zinazotwaa ardhi za Vijiji kulipa fidia kamili ya haki na ilipwe kwa wakati:- (a) Je, ni Wakazi wangapi wa Mitaa ya Kizani na Mwera wamelipwa fidia ya mali zao, usumbufu, malazi, upotevu wa faida na usafiri? 1 (b) Je, mpaka hivi sasa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke imekamilisha zoezi la ulipaji fidia kwa mujibu wa Sheria husika? (c) Ni kiasi gani cha fedha kimeshatumika katika zoezi hilo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Philipa Mturano, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a), (b) na (c), kwa pamoja kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, ninapenda kumfahamisha Mheshimiwa Mbunge kuwa, hadi sasa hakuna Mkazi wa Mtaa wa Kizani na Mwera aliyelipwa fidia. -
Majadiliano Ya Bunge ______
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Thelathini na Mbili – Tarehe 19 Juni, 2015 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaanza maswali na Ofisi ya Waziri Mkuu, swali la kwanza linaulizwa na Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, kwa niaba yake Mheshimiwa Dkt. Limbu. Na. 224 Mradi wa Kupandishwa Hadhi Barabara kuwa za Mkoa MHE. DKT. FESTUS B. LIMBU (K.n.y. MHE. DEO K. SANGA) aliuliza:- Tuliomba barabara ya kutoka Mtwango kupitia Kichiwa hadi Ikuna Nyombo, pia barabara ya kutoka Makambako-Mlowa-Manga-Usetuke- Kifumbe-Ibatu-Itandililo kuunganishwa na barabara ya Mgololo:- (a) Je, ni lini barabara hizo zitapandishwa hadhi kuwa za Mkoa? (b) Je, ni lini zitaanza kutengenezwa? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Njombe Kaskazini, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:- 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) (a) Mheshimiwa Spika, kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Njombe kilichofanyika tarehe 04 Juni, 2012, kilipendekeza barabara za kupandishwa hadhi kama ifuatavyo:- (i) Mtwanga-Kichiwa-Ikuna hadi Nyombo yenye kilomita 28.6; (ii) Makambako – Mlowa – Manga – Kifumba - Kichiwa hadi Kitandulilo yenye kilomita 35; (iii) Mfiliga – Ikangasi - Itambo hadi Idete yenye kilomita 65; na (iv) Makambako - Usetule hadi Kitandililo yenye kilomita 34. Mheshimiwa Spika, hapo tarehe 30 Julai, 2013, Mkuu wa Mkoa wa Njombe alimwandikia Waziri wa Ujenzi barua yenye Kumb. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA KUMI NNE Kikao cha Saba – Tarehe 4 Februari, 2008 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 83 Umiliki na Uendeshaji wa Shirika la Ndege ATCL MHE. LUCAS L. SELELII aliuliza:- Kwa kuwa, Serikali imerejesha umiliki w Shirika la Ndege (ATCL) ili kuliongezea ufanisi na masafa ya ndani na ya kimataifa:- (a) Je, kuna hatua gani za makusudi za kuipa ATCL mtaji wa kutosha? (b) Je, ni sababu zipi zimeifanya ATCL kupata hasara na kuwa na madeni? NAIBU WAZIRI WA MIUNDOMBINU alijibu:- Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Selelii, Mbunge wa Nzega, lenye sehemu (a) na )b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kuliwezesha Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kupata mtaji wa kuendesha shughuli zake kwa ufanisi, Serikali imemtafuta na kumpata mwekezaji binafsi ambaye yuko tayari kuingia ubia na Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL) kwa kununua hisa zipatazo asilimia 49 za Serikali ndani ya ATCL. (Makofi) Mwekezaji huyo ni kampuni ya China SONANGOL International Limited (CSIL) kutoka Jamhuri ya Watu wa China ambayo imekubali kushirikiana na Serikali kutafuta fedha za kutekeleza mpango mkakati wa ATCL ambapo unahusu kununua ndege tisa za aina mbalimbali kwa matumizi ya safari za ndani na nje ya nchi, mafunzo kwa Marubani 1 na Wahandisi na kubadili mifumo mbalimbali ya uendeshaji ili kuwezesha Kampuni kutoa huduma zake kwa ufanisi na kuweza kuhimili ushindani. Kwa sasa Serikali imekamilisha nyaraka muhimu zitakazowezesha uuzaji wa hisa hizo kufanywa kabla ya kusaini mkataba na mwekezaji huyo. -
Speech by the Minister for Finance Hon. Mustafa Haidi
SPEECH BY THE MINISTER FOR FINANCE HON. MUSTAFA HAIDI MKULO (MP.), INTRODUCING TO THE NATIONAL ASSEMBLY, THE ESTIMATES OF GOVERNMENT REVENUE AND EXPENDITURE FOR THE FISCAL YEAR 2011/2012 INTRODUCTION: 1. Madam Speaker , I beg to move that this esteemed House now resolves to debate and approve Government proposals for Revenue and Expenditure estimates for Fiscal Year 2011/12. Together with this speech, there are four volumes of books which provide detailed explanation of the budget estimates: volume one presents revenue estimates; volume two describes recurrent expenditure estimates for ministries, and government independent departments while volume three provides recurrent expenditure estimates for regions and local government authorities, and volume four presents development expenditure estimates for ministries, government independent departments, regions and local government authorities. In addition, there is a Finance Bill of the year 2011 which is part of this budget. 2. Madam Speaker, I am privileged at this juncture, to take this opportunity to congratulate His Excellency Dr. Jakaya Mrisho Kikwete for having been elected for a second term to lead the fourth phase Government. I would also like to congratulate Hon. Dr. Mohamed Gharib Billal for being elected as Vice President of the United Republic of Tanzania. Similarly, I congratulate Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda (MP.) for being elected Member of Parliament and re- appointed by the President and endorsed by the Parliament to become the Prime Minister for the second term of the fourth phase Government. 3. Madam Speaker, I congratulate you, Hon. Speaker Anne Makinda (MP.) for being elected as Speaker and thus become the first woman to lead the Parliament in East Africa. -
1458123221-Hs-15-26
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini na Sita – Tarehe 4 Juni, 2014 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE: MWIGULU L. M. MCHEMBA): Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Fedha kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. ESTHER L. M. MIDIMU (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA UCHUMI, VIWANDA NA BIASHARA): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Viwanda na Biashara Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Fedha kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE.CHRISTINA M. LISSU (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KWA WIZARA YA FEDHA): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani, kwa Wizara ya Fedha Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Swali letu la kwanza kama ilivyo ada linaelekezwa Ofisi ya Waziri Mkuu na linaulizwa na Mheshimiwa Agripina Zaituni Buyogera, Mbunge wa Kasulu Vijijini. Kwa niaba yake Mheshimiwa Rajab Mbarouk Mohammed. Na. 182 Uwekezaji Kwenye Pori la Makere Kusini MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED (K.n.y. MHE. AGRIPINA Z. BUYOGERA) aliuliza:- 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) Licha ya kwamba kuna uwekezaji unaoendelea kwenye Pori la Makere Kusini (Kagera Nkanda) katika Jimbo la Kasulu Vijijini; bado kuna -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA NNE Kikao cha Kumi na Moja – Tarehe 17 Desemba, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Mussa Z. Azzan) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- MHE. JOSEPHINE J. NGENZABUKE (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA BUNGE YA UCHUMI, VIWANDA NA BIASHARA): Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Uchumi, Viwanda na Biashara Kuhusu Utekelezaji wa Shughuli zake kwa Mwaka 2013. MHE. LUCKSON N. MWANJALE (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA BUNGE YA MASUALA YA UKIMWI): Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi Kuhusu Utekelezaji wa Shughuli zake kwa Mwaka 2013. 1 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) MASWALI NA MAJIBU Na. 120 Kuleta Walimu na Kujenga Nyumba Zao MHE. MWIGULU L. N. MADELU (K.n.y. MHE. DKT. HAMISI A. KIGWANGALLA) aliuliza:- Kwa kutumia jitihada binafsi na Mfuko wa Jimbo, Mbunge wa Jimbo la Nzega ameanzisha ujenzi wa shule tatu za Kidato cha Tano na Sita:- (a) Je, ni lini Serikali itaunga mkono jitihada hizi kwa kujenga nyumba za Walimu kwenye shule hizo? (b) Je, Serikali itakuwa tayari kuleta Walimu na kusajili shule hizo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Hamisi Andrea Kigwangalla, Mbunge wa Nzega, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Dkt. Hamisi Andrea Kigwangalla, kwa jitihada anazozifanya kuboresha utoaji wa elimu nchini. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Thelathini na Nane – Tarehe 2 Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA UCHUKUZI (RELI, BANDARI NA USAFIRI WA MAJINI): Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. MASWALI NA MAJIBU Na. 348 Uchimbaji wa Bwawa Jimboni Mbogwe MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Serikali imewazuia Wananchi wa Kijiji cha Nsango, Kata ya Iponya, kunywesha maji mifugo yao katika mto ulioko katika Hifadhi ya Msitu wa Kigosi Muyowosi kwa ahadi kwamba kutakuwa na Mradi wa Uchimbaji wa Bwawa ambalo lingetoa huduma mbadala ya maji ya mto:- Je, ni lini Serikali itakamilisha uchimbaji wa bwawa hilo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, ni kweli taratibu za hifadhi za wanyamapori haziruhusu shughuli zozote za kijamii kufanyika ndani ya hifadhi ikiwemo unyweshaji wa mifugo. Kutokana na sababu hiyo, Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe katika Mwaka wa Fedha wa 2010/2011, iliandaa andiko la Mradi wa Ujenzi wa Bwawa na kuliwasilisha kwenye Mfuko wa Wanyamapori wa Taifa, ikiomba kupatiwa shilingi milioni 78.1 kwa ajili ya kazi hiyo. Mfuko wa Wanyamapori wa Taifa ulikubali kutoa kiasi cha shilingi milioni 25 kwa kazi ya ujenzi wa bwawa hilo. -
Hotuba Ya Waziri Wa Fedha, Mheshimiwa Mustafa Haidi Mkulo (Mb), Akiwasilisha Bungeni Mapendekezo Ya Serikali Kuhusu Makadirio Ya Mapato Na Matumizi Kwa
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWA MUSTAFA HAIDI MKULO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2011/2012 UTANGULIZI: 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu likubali kujadili na kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2011/2012. Pamoja na hotuba hii, vipo vitabu vinne vinavyoelezea kwa kina takwimu mbalimbali za Bajeti. Kitabu cha Kwanza kinahusu makisio ya mapato. Kitabu cha Pili kinaelezea makisio ya matumizi ya kawaida kwa Wizara na Idara zinazojitegemea ambapo cha Tatu kinahusu makisio ya matumizi ya kawaida kwa Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa na cha Nne kinaelezea makadirio ya matumizi ya maendeleo kwa Wizara, Idara zinazojitegemea, Mikoa pamoja na Mamlaka za Serikali za Mitaa. Aidha, upo Muswada wa Sheria ya Fedha wa mwaka 2011 ambao ni sehemu ya Bajeti hii. 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuchaguliwa tena kuongoza kwa muhula wa 2 pili wa Serikali ya Awamu ya Nne. Aidha, ninamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa imani kubwa aliyonayo kwangu kwa kunichagua kwa mara nyingine tena kuongoza Wizara kubwa na nyeti, ninamuahidi kuwa sitamuangusha. Pia ninampongeza Dkt. Mohammed Gharib Billal kwa kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Vile vile, ninampongeza Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda (Mb.) kwa kuchaguliwa kuwa Mbunge na kuteuliwa tena na hatimaye kupitishwa na Waheshimiwa Wabunge kuwa Waziri Mkuu kwa muhula wa pili wa Serikali ya Awamu ya Nne. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Sita – Tarehe 26 Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Taarifa ya Majibu ya Serikali kuhusu Mapendekezo ya Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kwa Mwaka wa Fedha 2008/2009. NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. PEREIRA AME SILIMA): Hati za Uhamishaji Fedha Na. 1 na Na. 2 za Mwaka 2011/2012 (Statements of Reallocation Warrants No. 1 and 2 of 2011/2012). Majibu ya Serikali kuhusu Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali kwa kipindi kilichoishia tarehe 30 Juni, 2009. Majibu ya Serikali kuhusu Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma kwa kipindi kilichoishia tarehe 30 Juni, 2009. NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI: Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Chuo Kikuu cha Dodoma kwa miaka ya 2008/2009 na 2009/2010 (The Annual Report and Accounts of the University of Dodoma for the years 2008/2009 and 2009/2010). MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tunaanza na maswali ya Ofisi ya Waziri Mkuu na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Zarina Shamte Madabida. Na. 490 Kuwawezesha Wajasiriamali MHE. ZARINA S. MADABIDA aliuliza:- Vijana wengi wanaomaliza Vyuo na kuwa na ujuzi mbalimbali lakini hawana ajira wala hawawezi kujiajiri baada ya kukosa mitaji -
MKUTANO WA NANE Kikao Cha Kumi Na Sita
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Kumi na Sita – Tarehe 4 Julai, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Silvester M. Mabumba) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa Mwaka wa Fedha, 2012/2013. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MAZINGIRA): Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) kwa Mwaka wa Fedha, 2012/2013. 1 MHE. FAKHARIA KHAMIS SHOMAR – (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) kwa mwaka 2011/2012 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. MHE. ABDULKARIM I. H. SHAH – MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA: Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) kwa Mwaka 2011/2012 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. MHE. TUNDU A. M. LISSU - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MAZINGIRA): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani juu ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013.