Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document) Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA TANO Kikao cha Tano – Tarehe 14 Novemba, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 54 Tatizo la Maji katika Mji wa Namanyere MHE. MCH. LUCKSON N. MWANJALE (K.n.y. MHE. ALLY MOHAMED KEISSY) aliuliza:- Mji wa Namanyere ambao ni Makao Makuu ya Wilaya ya Nkasi una wakazi zaidi ya 15,000, Hospitali ya Wilaya, Chuo cha Manesi, Shule za Msingi Sita, Sekondari Tatu na Kituo cha Afya, lakini una uhaba mkubwa wa maji hasa ifikapo mwezi Julai hadi Novemba. Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo hilo ili kuwaondolewa kero hiyo wananchi wa Mji wa Namanyere? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA LA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Mohamed Keissy, Mbunge wa Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Mji wa Namanyere wenye wakazi zaidi ya 19,000 unapata maji chini ya asilimia 20 kutokana na ukosefu wa vyanzo vya maji vya uhakika. Mheshimiwa Spika, Serikali kufuatia agizo la Mheshimiwa Rais, alililotoa mwezi Oktoba, 2010 imefanya upembuzi yakinifu (Feasibility study) ili kubaini vyanzo vipya vya maji kwa ajili ya Mji wa Namanyere. Baada ya upembuzi yakinifu gharama zimekadiriwa kufikia bilioni 1.9. Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi katika bajeti ya mwaka 2011/2012 iliomba maombi maalum ili kupata fedha hizo kwa lengo la kukabiliana na changamoto za upatikanaji wa huduma za maji. Fedha hizi hazikupatikana. Aidha, Halmashauri kupitia programu ya maji na usafi wa mazingira imeidhinishiwa shilingi 600,000,000 kwa ajili ya miradi ya maji ya vijiji kumi (10). Mheshimiwa Spika, mipango ya Halmashauri ya kukabiliana na matatizo ya maji yaliyopo ni pamoja na kuandaa rasimu ya sheria ndogo ya uvunaji wa maji ya mvua ambayo mpaka sasa iko katika mchakato wa kukamilika, kuwekwa kwa sharti la kuhakikisha kila mchoro wa nyumba unakuwa na mfumo wa uvunaji wa maji ya mvua ili upitishwe na mamlaka zinazohusika na kufanya tathimini ya kutumia nishati ya umeme wa jua kwa ajili ya kuendesha pampu za maji. Wananchi wa Mji wa Namanyere kwa sasa wanapata maji kutoka katika visima vinne vilivyochimbwa pamoja na bwawa la Msiri ambavyo ni vyanzo vinavyotumia pampu zinazohitaji nishati ya umeme. Halmashauri imenunua generator ili kuvuta maji kutoka katika visima hivyo kwenda wa wananchi. 1 MHE. ALLY MOHAMED KEISSY: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri nina maswali ya nyongeza kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Mji wa Namanyere ni Mji unaokua siku hadi siku na wananchi wanapata tabu hata ya kujenga nyumba, maji ya kunywa na kila kitu hivyo visima vinne havitoshi kabisa na huwa vinaharibika mara kwa mara pampu zake. Watu wa Namanyere wanapata shida siku hadi siku yaani hata maji ya kunawa hakuna na hizo alizosema shilingi milioni 600,000,000 walizotenga zimeshindwa kukidhi. Wamechimba visima kule maji hakuna na hizo fedha hazijatumika hata senti tano. Je, Serikali ina mpango gani wa haraka kusaidia wakazi wa Namanyere? (Makofi) NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Mohamed Keissy, kama ifuatavyo:- Kwanza nakubali kweli Mji wa Namanyere kutokana na ongezeko la watu mahitaji ya maji hayatoshi. Kitu kinachofanyika sasa hivi tumekasimu madaraka kwa Mamlaka ya Sumbawanga kufanya stadi tuweze kuona mahitaji, kuainisha vyanzo mbalimbali kwa ajili ya matumizi ya Mji wa Namanyere na miji mingine kama Laila kwa miaka 20 ijayo kazi hiyo imeshaanza kuainishwa term of reference na tutaiingiza katika program ya maji awamu ya pili. MHE. MCH. LUCKSON N. MWANJALE: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tatizo la Namanyere karibu linalingana na Mji Mdogo wa Mbalizi ambao una watu karibu 60,000 naomba kuuliza ni lini Mji huo utapewa maji ya uhakika kwa sababu mpaka sasa hivi kuna matatizo makubwa sana? Ahsante. (Makofi) NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwanjale kama ifuatavyo:- Kama nilivyojibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Keissy Miji Mikuu ya Wilaya na Miji Midogo yote tunaifanyia stadi ili tuweze kuainisha mahitaji ya maji kwa miaka 20 ijayo ndio kazi ambayo tunaifanya sasa. (Makofi) Na. 55 Ujenzi wa Miundombinu ya Maji MHE. TUNDU A. M. LISSU aliuliza:- Katika mwaka wa fedha wa 2010/2011 jumla ya shilingi 534,865,999/= zilitengwa kwa ajili ya kujenga miundombinu ya maji Halmashauri ya Wilaya ya Singida likiwemo Jimbo la Singida Mashariki, lakini fedha hizo zimetengwa wakati Wilaya mpya ya Ikungi yenye majimbo mawili ya Singida Mashariki na Singida Magharibi na Halmashauri havijaanzishwa rasmi:- (a) Je, kati ya fedha hizo ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya Wilaya mpya ya Ikungi hasa Jimbo la Singida Mashariki kwa kusudi hilo? (b)Je, ni Vijiji na Kata zipi za Jimbo la Singida Mashariki zitanufaika na ujenzi wa miundombinu ya maji iliyotengewa fedha hizo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA LA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tundu Antiphas Mughwai Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Singida katika mwaka 2010/2011 ilitengewa shilingi 664,470,000 kupitia programu ya maji na usafi wa mazingira vijijini kwa ajili ya 2 miradi ya maji katika vijiji 10. Kati ya fedha hizo kiasi kilichopokelewa ni shilinig 532,451,429 na zilizotumika ni shilingi 379,264,336. Fedha hizi zilitengwa kwa ajili ya miradi ya maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida na hakukuwa na bajeti kwa ajili ya Wilaya mpya ya Ikungi na Jimbo jipya la Singida Mashariki ambayo ilikuwa haijaanzishwa wakati huo. Wilaya mpya ikiwemo ya Ikungi zitaanza baada ya kukamilika kwa hatua za mwisho za utoaji maoni, mapendekezo na pingamizi kama zipo kufuatia notisi ya kuanzisha Mikoa na Wilaya iliyotolewa tarehe 9/9/2011. Aidha, Bajeti ya Halmashauri inayoandaliwa huzingatia vipaumbele vya miradi iliyopangwa kutekelezwa bila kujali iko katika Jimbo lipi la uchaguzi. (b) Mheshimiwa Spika, vijiji na Kata za Jimbo la Singida Mashariki zilizopata mgao wa bajeti hiyo kwa ajili ya miradi ya maji kwa mwaka 2010/2011 ni Kijiji cha Siuyu kilichopo katika Kata ya Siuyu na Kijiji cha Nkuhi kilichoko katika Kata ya Issuna. Kiasi cha fedha kilichotumika kwa ajili ya miradi katika Vijiji hivyo ni shilingi 84,503,200. Kati ya fedha hizo shilingi 33,484,000 zilitumika kwa ajili ya uchimbaji wa kisima kimoja (1) katika Kijiji cha Siuyu, utafiti wa maji ardhini, upembuzi yakinifu na usanifu wa mradi na shilingi 51,019,200 zilitumika kwa ajili ya uchimbaji wa visima vitatu katika Kijiji cha Nkuhi, utafiti wa maji ardhini, upembezi yakinifu na usanifu wa mradi. MHE. TUNDU A. M. LISSU: Mheshimiwa Spika, naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, swali la nyongeza naomba Mheshimiwa Naibu Waziri aliambie Bunge lako Tukufu kama ana taarifa kwamba shilingi milioni 51,000,000 zinazodaiwa kutumika Kijiji cha Nkuhi hazijatumika, hakuna maji na matokeo yake imebidi Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo la Singida Mashariki utoe shilingi milioni 4 ili kuwapatia wananchi wa Kijiji cha Nkuhi maji. Kama atakubali kwamba fedha hazijatumika naomba alieleze Bunge Tukufu ni hatua gani zitakazochukuliwa na Serikali ili kushughulikia hawa ambao wanapelekewa fedha kwa ajili ya maji ya wananchi halafu anazielekeza kwingine? (Makofi) SPIKA: Pamoja na kurudisha hela zako za jimbo. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA LA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tundu A. M. Lissu kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, sina tatizo na anachosema Mheshimiwa Lissu, yeye kama amekwenda ametumia hela za constituency development catalyst fund kwa ajili ya shughuli za maji pale mimi sioni tatizo kabisa hela hizi zilikusudiwa kuchochea maendeleo ya wananchi pale walipo. Kwa hiyo, kama ametumia Mbunge ameonyesha tu busara yake kwamba mimi nafikiria ni priority area kuna tatizo akapeleka pale there is no problem. Anachokizungumza hapa anatuambia kwamba milioni 51,000,000 ana hakika kwamba hazikuelekezwa kule zilizokwenda. Na mimi nilipokuja hapa wala sijaja hapa kwamba nakuja hivi hapa nasikia usingizi kwa sababu ya kujiandaa kwa ajili ya kujibu swali hili. De-central contradiction iliyoko katika vijiji hivi anavyozungumza Mheshimiwa Tundu Lissu ni kwamba visima vimekwenda vimechimbwa lakini watu hawajaanza kupata maji. Kwa maana ya kwamba hawajapeleka katika simtanki na kuanza kusambaza na kupeleka. Wanacho kigezo walichokitumia hapa. Kuna kitu kinachoitwa counter part fund wakasema wale wananchi ambao wamejitoa wakatoa michango na wale ambao wamefanya kazi kwa mikono yao wanawapa kipaumbele namba moja. Asilimia inayotumika pale ni asilimia 5. asilimia 2.5 wananchi na 2.5 kutoka kwenye Halmashauri. Wakaenda wakachukua vijiji vyote pale Singida wakaviorodhesha. Hiki kijiji kinachosemwa ninacho hapa ninacho na Mheshimiwa Lissu akitaka tutakaa tutazungumza vizuri. 3 Wakasema hivi tunatoa kipaumbele kwa vile vijiji ambavyo vilionyesha nia ya kuchangia mpango huu. Vijiji hivi anavyovitaja hapa havikukidhi hiyo haja vikasukumwa mbele kwa ajili ya program inayokuja. Sasa mimi nataka niseme maneno yafuatayo: Ametaka kujua kwamba ni hatua gani zinazochukua? Mimi hapa nikimaliza natoka nje nazungumza na Mkurugenzi namwambia hivi taarifa mliyonipa Mbunge amekataa anasema kwamba milioni 51,000,000 hazikutumika hatuwezi tukakaa hapa ndani tukaambiwa milioni 51,000,000 hazikutumika,
Recommended publications
  • Hotuba Ya Mgeni Rasmi Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) Waziri Mkuu Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Katika Ufunguzi Wa Mkuta
    HOTUBA YA MGENI RASMI MHE. KASSIM MAJALIWA MAJALIWA (MB) WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KATIKA UFUNGUZI WA MKUTANO WA MWAKA WA WADAU WA LISHE, SEPTEMBA 10, 2019 Mheshimiwa Jenista Mhagama (Mb), Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu, Mheshimiwa Ummy Mwalimu (Mb), Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mheshimiwa Suleiman Jafo (Mb), Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI. Mheshimiwa Prof. Joyce Ndalichako (Mb), Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango (Mb), Waziri wa Fedha na Mipango. Mheshimiwa Japhet Hasunga (Mb), Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Luhaga Mpina (Mb), Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mheshimiwa Innocent Bashungwa (Mb), Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwezeshaji, Mheshimiwa Prof. Makame Mbarawa (Mb), Waziri wa Maji na Umwagiliaji. Mheshimiwa Doto Biteko (Mb), Waziri wa Madini, Waheshimiwa Manaibu Waziri na Makatibu Wakuu, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Bilinith Mahenge; pamoja na viongozi wengine wa ngazi za Mkoa na Halmashauri mliopo, Waheshimiwa Wabunge na viongozi wa Vyama vya Siasa, Waheshimiwa Mabalozi wanaoziwakilisha nchi mbalimbali, Ndugu Viongozi waandamizi wa Idara, Taasisi, Wakala za Serikali, Wakuu wa Vyuo vya Elimu ya Juu, Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa, Wadau wa Maendeleo na Asasi za Kiraia, 1 Ndugu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania, Ndugu Wageni Waalikwa, Waandishi wa habari na wadau wote wa Lishe, Mabibi na Mabwana. Habari za asubuhi Kwa mara nyingine tena nina furaha kubwa sana kujumuika na wadau wa lishe siku hii ya leo. Hii ni mara yangu ya tatu kuhudhuria mkutano wa mwaka wa wadau wa lishe nchini na hivyo nahisi kuwa mwanafamilia wa wadau waliohamasika katika masuala ya lishe.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Tatu – Tarehe 15 APRILI, 2010 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU NAIBU SPIKA: Maswali kwa Waziri Mkuu leo kiongozi wa Upinzani Bungeni hayupo kwa hiyo nitaenda na orodha za wachangiaji na nitakuwa ninakwenda kufuatana na itikadi ya chama, upande, gender na vitu kama hivyo. Kwa hiyo, walioko hapa wasidhani watakwenda kama ilivyoorodheshwa. Kwa hiyo, nitaanza na msemaji wa kwanza Mheshimiwa Dr. Willibrod Slaa. MHE. DR. WILLIBROD P. SLAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kunipa nafasi, Mheshimiwa Waziri Mkuu sasa ni takribani mwaka mzima tangu nilipoanza kuhoji, mimi na Wabunge wenzangu, tulipoanza kuhoji kuhusu ubadhirifu na tuhuma mbalimbali zilizokuwa zinakabili matumizi ya fedha za umma zilizofanywa na makampuni kama Mwananchi Gold Company, Tan Gold, Kagoda, Deep Green na mengine mengi ambayo yalitajwa ndani ya ukumbi huu. Kwa nyakati tofauti maelezo mbalimbali yametolewa ndani ya Bunge. Mpaka leo hatujapata taarifa ya kinachoendelea. Bunge hili lenye jukumu la kuisimamia Serikali halijui au wananchi hawajui kama kuna kitu kinaendelea je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu ubadhirifu huo? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naamini kabisa Dr. Slaa, hutegemei kwamba kweli nitaweza kujibu maswali hayo uliyoyauliza kwamba mimi nina maelezo juu ya Kagoda, maelezo juu ya nani, is not possible nadhani si sahihi kabisa. (Makofi) Mimi ninachoweza kusema ni kwamba jitihada za Serikali zipo zimekuwa zikionekana katika maeneo ambayo yameshaanza kufanyiwa kazi. Sasa kama kuna maeneo ambayo bado hayajafanyiwa kazi jitihada za Serikali zitaendelea kwa kadri itakavyowezekana.
    [Show full text]
  • Process in Tanzania the Political, Civil and Economic Society
    Tanzania has been independent in 2011 for 50 years. While most neighbouring states have Jonas gone through violent conflicts, Tanzania has managed to implement extensive reforms with- out armed political conflicts. Hence, Tanzania is an interesting case for Peace and Develop- ment research. E Challenges for the This dissertation analyses the political development in Tanzania since the introduction of wald the multiparty system in 1992, with a focus on the challenges for the democratisation process democratisation in connection with the 2000 and 2005 elections. The question of to what extent Tanzania has moved towards a consolidation of democracy, is analysed through an analysis of nine different institutions of importance for democratisation, grouped in four spheres, the state, Challenges for the process in Tanzania the political, civil and economic society. Focus is on the development of the political society, and the role of the opposition in particular. The analysis is based on secondary and primary Moving towards consolidation 50 years material collected in the period September 2000 to April 2010. after indepencence? The main conclusion is that even if the institutions of liberal democracy have gradually developed, in practice single-party rule has continued, manifested in the 2005 election when the CCM won 92% of the seats in the parliament. Despite an impressive economic growth, poverty remains deep and has not been substantially reduced. On a theoretical level this brings the old debate between liberal and substantive democracy back to the fore. Neither the economic nor the political reforms have apparently brought about a transformation of the political and economic system resulting in the poor majority gaining substantially more political influence and improved economic conditions.
    [Show full text]
  • Madini News Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Toleo Na.2 Wa Tanzania Machi, 2020 HALIUZWI
    Toleo Na.2 // Machi 2020 Yaliyomo // Biteko - Nitasimama na Mzee Tume ya Leseni ya TanzaniteOne Imefutwa na Kisangani mpaka “asimame” Kurudishwa Serikalini - Biteko... Uk.04 ... Uk.08 Madini Bilioni 66.5 zapatikana tangu Wanawake Tume ya Madini kuanzishwa kwa masoko Wawakumbuka ya madini ... Uk.10 Yatima ... Uk.18 www.tumemadini.go.tz Tume ya Madini 2020 www.tumemadini.go.tz /TAHARIRI Salamu Kutoka kwa Waziri wa Madini Maoni ya Mhariri SEKTA YA MADINI INAIMARIKA, MAFANIKIO MASOKO TUENDELEZE USHIRIKIANO YA MADINI TUMEWEZA! Katika Mwaka wa Fedha 2019/2020 Wizara ya Madini ilipanga kutekeleza majukumu yake kupitia miradi Katika kuhakikisha kuwa Sekta ya Madini inakuwa na mchango mbalimbali ikilenga katika kuimarisha Sekta ya Madini, hivyo kuwa na mchango mkubwa kwenye ukuaji wa mkubwa kwenye ukuaji wa uchumi wa Taifa, Serikali kupitia uchumi wa nchi. Tume ya Madini kuanzia Machi, 2019 ilifungua masoko ya madini Katika Toleo lililopita nilielezea kwa kifupi kuhusu yale ambayo yamesimamiwa na kutekelezwa na Wizara na vituo vya ununuzi wa madini lengo likiwa ni kudhibiti utorosh- kwa kipindi cha takribani miaka miwili tangu kuanzishwa kwake. waji wa madini kwa kuwapatia wachimbaji wa madini nchini Katika Toleo hili nitaelezea kwa kifupi mafanikio ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara kwa kipindi cha sehemu ya kuuzia madini yao huku wakilipa kodi mbalimbali kuanzia Julai, 2019 hadi Februari, 2020. Kama ambavyo nilieleza Bungeni katika Hotuba yangu wakati Serikalini. nikiwasilisha Bajeti ya Wizara kwa Mwaka 2019/2020, nilieleza kuwa, Wizara imepangiwa kukusanya Shilingi 470,897,011,000.00 katika Mwaka wa Fedha 2019/2020. Uanzishwaji wa masoko ya madini na vituo vya ununuzi wa Napenda kuwataarifu wasomaji wa Jarida hili kuwa, hadi kufikia Februari, 2020 jumla ya Shilingi madini ni sehemu ya maelekezo yaliyotolewa kwenye mkutano wa 319,025,339,704.73 zimekusanywa ambazo ni sawa na asilimia 102 ya lengo la makusanyo ya nusu mwaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tazania, Dkt.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Kumi na Tatu – Tarehe 10 Februari, 2010 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI (MHE. OMAR YUSSUF MZEE): Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Benki ya Posta Tanzania, kwa Mwaka 2008 [The Annual Report and Accounts of The Tanzania Postal Bank for the Year 2008]. The Mid-Term Review of the Monetary Policy Statement of The Bank of Tanzania for the Year 2009/2010. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini juu ya Taarifa ya Serikali Kuhusu Ubinafsishwaji wa Mgodi wa Kiwira. Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Mchakato wa Zabuni ya Kuzalisha Umeme wa Dharura Ulioipa Ushindi Kampuni ya Richmond Development Company LLC. Houston Texas - Marekani Mwaka 2006. MWENYEKITI WA KAMATI YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Miundombinu Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelzaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Uendeshaji Usioridhisha wa Shirika la Reli Tanzania uliofanywa na Kampuni ya RITES ya India. 1 Taarifa ya Kamati ya Miundombinu Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Utendaji wa Kazi Usioridhisha wa Kampuni ya TICTS. MASWALI NA MAJIBU Na. 145 Usimamizi wa Ukaguzi wa Fedha za Halmashauri MHE. HERBERT J. MNTANGI aliuliza:- Kwa kuwa, kiasi cha fedha kinachopelekwa katika Halmashauri za Wilaya, Manispaa na Jiji ni kikubwa na kinahitaji usimamizi wa ziada:- Kwa kuwa kitengo cha ukaguzi wa ndani kipo chini ya Mkurugenzi Mtendaji.
    [Show full text]
  • 1458137638-Hs-4-4-20
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE KIKAO CHA NNE – TAREHE 14 JUNI, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 37 Ardhi Iliyotolewa Kujenga Shule ya Msingi Kiraracha MHE. AUGUSTINO L. MREMA aliuliza:- Mzee Pauli Sananga Lekule wa Kijiji cha Kiraracha, Kata ya Marangu, Wilaya ya Moshi Vijijini, alitoa ardhi yake ikatumika kujenga shule ya msingi Kiraracha, Marangu miaka 10 iliyopita akiahidiwa na Serikali kupewa eneo jingine kama fidia lakini mpaka sasa hajapewa eneo jingine kama fidia jambo lililomfanya aione Serikali haikumtendea haki. Je, ni lini Serikali itamlipa haki yake kutokana na makubaliano hayo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Lyatonga Mrema, Mbunge wa Vunjo kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa Ndugu Pauli Sananga Lekule wa Kijiji cha Kiraracha, Kata ya Marangu Magharibi, alitoa ardhi yake kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi Kiraracha, Kata ya Marangu Magharibi kwa ahadi ya kufidiwa eneo lililoko Njia panda. Aidha eneo ambalo Halmashauri ya Wilaya ya Moshi ilitarajia kumfudia Ndugu Lekule lipo katika mgogoro na kesi bado inaendelea Mahakama Kuu. 1 Mheshimiwa Spika, kwa kuwa eneo lililopimwa viwanja na kutarajia mlalamikaji lipo katika mgogoro wa kisheria kati ya Halmashauri na wananchi, Serikali inaendelea kufuatilia mwenendo wa kesi na mara shauri litakapomalizika Mahakamani mhusika atapewa eneo lake. Mheshimiwa Spika, katika jitihada za Serikali kuhakikisha shauri hili haliendelei kuchukua muda mrefu, Halmashauri ya Wilaya ya Moshi imeunda timu kwa ajili ya kufuatilia na kuharakisha shauri hili ili ikiwezekana limalizike nje ya Mahakama ili Ndugu Lekule Sananga aweze kupata haki yake mapema.
    [Show full text]
  • Bspeech 2008-09
    HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA, MHESHIMIWA STEPHEN MASATO WASIRA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA KWA MWAKA 2008/2009 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu baada ya kuzingatia taarifa iliyowasilishwa hapa Bungeni leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kilimo Mifugo na Maji inayohusu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, sasa lijadili na kukubali kupitisha makadirio ya Matumizi ya Kawaida na ya Maendeleo ya Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika kwa mwaka wa Fedha wa 2008/2009. 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitumie fursa hii kuungana na Watanzania wenzangu kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuchaguliwa kwake kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika. Kuchaguliwa kwake, na mchango wake alioutoa tangu kuchaguliwa kwake kuwa Mwenyekiti wa Umoja huo umelijengea Taifa letu heshima kubwa katika medani ya kimataifa. Aidha, uongozi wake na juhudi zake za kupambana na maovu katika jamii yetu, licha ya kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa ajili ya Uchaguzi wa Mwaka 2005 ni kielelezo dhahiri kuwa ni kiongozi anayejali haki na maendeleo ya nchi yetu. Juhudi zake hizo zimedhihirisha uwezo wake mkubwa wa kuongoza na utumishi wake uliotukuka aliouonyesha katika nyadhifa mbali mbali alizowahi kushika katika Serikali na Chama cha Mapinduzi. Wananchi wanaendelea kuwa na imani na matumaini makubwa kwa uwezo wake katika kuliongoza Taifa letu. 1 3. Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii pia kumpongeza Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda (MB) kwa kuteuliwa kwake kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka.
    [Show full text]
  • Tarehe 23 Mei, 2016
    NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Ishirini na Sita – Tarehe 23 Mei, 2016 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Najma Murtaza Giga) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu! NDG. CHARLES J. MLOKA – KATIBU MEZANI: Hati za kuwasilisha mezani. HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa mwaka wa fedha 2016/2017. MWENYEKITI: Katibu! NDG. CHARLES J. MLOKA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge tunaanza na maswali Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mheshimiwa Richard Philip Mbogo Mbunge wa Nsimbo, sasa aulize swali lake. 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Na. 209 Uchaguzi wa Madiwani katika Kambi ya Katumba MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza: - Chaguzi za Madiwani zilifanyika katika kambi ya wakimbizi Katumba wa 2015:- Je, ni lini Serikali itapeleka fedha ili kukamilisha chaguzi za Serikali za Vijiji na Mtaa? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Richard Philip Mbogo, Mbunge wa Nsimbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata ya Katumba, Vijiji ambavyo havijafanya uchaguzi wa Vviongozi wa Serikali za Mitaa kwa mwaka 2014 ni 14 na vitongoji 51. Uchaguzi ulishindwa kufanyika kwa sababu Kata hiyo ilikuwa ni kambi ya wakimbizi ambao walikuwa hawajapata uraia wa Tanzania kwa mujibu wa sheria za nchi. Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya Serikali kuwapa uraia wananchi wa maeneo hayo, Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo inaendelea na maandalizi ya kufanya uchaguzi mdogo katika vijiji na vitongoji hivyo na tayari katika bajeti ijayo ya mwaka 2016/2017 zimetengwa sh.
    [Show full text]
  • MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao Cha
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Nne - 29 Januari, 2010 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 39 Watumishi Hewa Wizara ya Elimu na Wizara ya Afya MHE. MOHAMED H. MISSANGA aliuliza:- Kwa kuwa, mwaka 2006/2007 Serikali ilipofanya uchunguzi wa ajira za Watumishi katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi iligundua kuwepo kwa Watumishi hewa zaidi ya elfu moja (1,000) ambao walisababisha hasara ya mabilioni ya fedha za Serikali; na kwa kuwa, mwaka 2008/2009 uchunguzi huo huo ulifanywa katika Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na kugundua kuwepo watumishi hewa zaidi ya elfu moja (1,000) pia; na kwa kuwa, ajira Serikalini hutawaliwa na kuongozwa na Sheria, Kanuni na taratibu mbalimbali za ajira:- (a) Je, ajira ya watumishi hewa inasababishwa na nini? (b) Je, katika kipindi cha miaka minne (mwaka 2006 hadi 2009) Serikali imepoteza fedha kiasi gani kwa kulipa watumishi hewa na ni kutoka Wizara na Taasisi zipi? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA alijibu:- 1 Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Hamisi Misanga - Mbunge wa Singida Kusini, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:- (a)Mheshimiwa Naibu Spika, katika utafiti uliofanyika ilionekana kuwa, watumishi hewa husababishwa na watumishi wameajiriwa na Serikali kihalali ambao utumishi wao umekoma kutokana na kustaafu kazi, kufariki, kuacha kazi, kufukuzwa kazi na hivyo kuendelea kulipwa mishahara isiyo halali kutokana na waajiri husika kutochukua hatua za kuwaondoa kwenye payroll na kusababisha kuwepo kwa malipo hewa ya mishahara.
    [Show full text]
  • 6 MEI, 2013 MREMA 1.Pmd
    6 MEI, 2013 BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Tisa – Tarehe 6 Mei, 2013 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tukae. Waheshimiwa, mtakuwa mmepata Supplementary Order Paper, halafu na ile paper ya kwanza Supplementary hiki ni Kikao cha 19, wameandika 18 ni Kikao cha 19. Kwa hiyo, mtakuwa na Supplementary Order Paper. Katibu tuendelee? HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatayo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. 1 6 MEI, 2013 MHE. AUGUSTINO M. MASELE (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ulinzi na Usalama Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. MHE. GRACE S. KIWELU (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. MASWALI NA MAJIBU Na. 145 Wajibu wa Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji MHE. MARIAM R. KASEMBE (K.n.y. MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA) aliuliza:- Msingi mkubwa wa Maendeleo ya Jamii huanzia kwenye ngazi ya Mitaa na Vijiji ambapo hutegemea ubunifu na utendaji wa Viongozi wa ngazi husika.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Tisa – Tarehe 20 Julai, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne. S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Ifuatayo Iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO:- Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa Mwaka wa Fedha, 2011/2012. MASWALI NA MAJIBU Na. 268 Fedha za Ukarabati wa Barabara – Manispaa ya Kinondoni MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza:- (a) Je, Serikali hutenga wastani wa shilingi ngapi kwa ajili ya ukarabati ndani ya Manispaa ya Kinondoni, na ni utaratibu gani unatumika kufuatilia toka kwa Wahandisi wa Manispaa kuhakikisha kwamba barabara zote za Manispaa zinapatikana nyaraka zote? (b) Je, kuna utaratibu gani wowote wa kuthaminisha gharama zilizotumika na uhalisi wa kila kilichotengewa? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA LA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima James Mdee Mbunge wa Kawe lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- 1 (a) Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni hupata fedha kwa ajili ya miradi ya barabara, Madaraja na Makalvati kutoka katika Mfuko wa Barabara, ruzuku za fedha za maendeleo ya Serikali za mitaa na vyanzo vya mapato ndani ya Halmashauri. Katika mwaka wa fedha 2009/2010 Manispaa kupitia vyanzo hivyo ilipata jumla ya shilingi bilioni 4.3. Fedha hizi zilitumika kufanya matengenezo ya barabara za lami kilomita 1.65, kufanya matengenezo ya changarawe kilomita 48, kuziba viraka katika barabara za udongo kilomita 23.5 matengenezo ya madaraja ya madaraja 11, kujenga kalvati 1 na ununuzi wa Motor Grader 1.
    [Show full text]