Tarehe 8 Novemba, 2018
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Tatu – Tarehe 15 APRILI, 2010 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU NAIBU SPIKA: Maswali kwa Waziri Mkuu leo kiongozi wa Upinzani Bungeni hayupo kwa hiyo nitaenda na orodha za wachangiaji na nitakuwa ninakwenda kufuatana na itikadi ya chama, upande, gender na vitu kama hivyo. Kwa hiyo, walioko hapa wasidhani watakwenda kama ilivyoorodheshwa. Kwa hiyo, nitaanza na msemaji wa kwanza Mheshimiwa Dr. Willibrod Slaa. MHE. DR. WILLIBROD P. SLAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kunipa nafasi, Mheshimiwa Waziri Mkuu sasa ni takribani mwaka mzima tangu nilipoanza kuhoji, mimi na Wabunge wenzangu, tulipoanza kuhoji kuhusu ubadhirifu na tuhuma mbalimbali zilizokuwa zinakabili matumizi ya fedha za umma zilizofanywa na makampuni kama Mwananchi Gold Company, Tan Gold, Kagoda, Deep Green na mengine mengi ambayo yalitajwa ndani ya ukumbi huu. Kwa nyakati tofauti maelezo mbalimbali yametolewa ndani ya Bunge. Mpaka leo hatujapata taarifa ya kinachoendelea. Bunge hili lenye jukumu la kuisimamia Serikali halijui au wananchi hawajui kama kuna kitu kinaendelea je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu ubadhirifu huo? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naamini kabisa Dr. Slaa, hutegemei kwamba kweli nitaweza kujibu maswali hayo uliyoyauliza kwamba mimi nina maelezo juu ya Kagoda, maelezo juu ya nani, is not possible nadhani si sahihi kabisa. (Makofi) Mimi ninachoweza kusema ni kwamba jitihada za Serikali zipo zimekuwa zikionekana katika maeneo ambayo yameshaanza kufanyiwa kazi. Sasa kama kuna maeneo ambayo bado hayajafanyiwa kazi jitihada za Serikali zitaendelea kwa kadri itakavyowezekana. -
MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Sita – Tarehe 9 Aprili, 2019
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Sita – Tarehe 9 Aprili, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu! NDG. RUTH MAKUNGU – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI: Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa mwaka wa fedha 2019/2020. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2019/2020. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Taarifa ya Mwaka na Hesabu zilizokaguliwa za Chuo Kikuu Mzumbe kwa mwaka ulioisha tarehe 30 Juni, 2017 (The Annual Report and Audited Accounts of Mzumbe University for the year ended 30th June, 2017). MWENYEKITI: Katibu! NDG. RUTH MAKUNGU – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Swali letu la kwanza leo linaelekezwa Ofisi ya Waziri Mkuu na linaulizwa na Mheshimiwa Dkt. Raphael Masunga Chegeni, Mbunge wa Busega. MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipo hapa kwa niaba. MWENYEKITI: Wewe unatoka Busega? MHE. RASHID A. SHANGAZI: Hapana, ila hili ni la kitaifa. MWENYEKITI: Aaa, sawa, kwa niaba. Na. 43 Kauli Mbiu ya Kuvutia Wawekezaji Nchini MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. DKT. -
Ofisi Ya Rais, Menejimenti Ya Utumishi Wa Umma Na Utawala Bora Kwa Mwaka Wa Fedha Wa 2019/20
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI – OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA. KAPT (MST) GEORGE H. MKUCHIKA (Mb.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2019/20 APRILI, 2019 A. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba, kutokana na taarifa iliyowasilishwa ndani ya Bunge lako Tukufu na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa iliyochambua bajeti ya Ofisi ya Rais, Ikulu (Fungu 20 na 30), Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma (Fungu 33), Menejimenti ya Utumishi wa Umma (Fungu 32), Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma (Fungu 67), Tume ya Utumishi wa Umma (Fungu 94), Bodi ya Mishahara na Masilahi katika Utumishi wa Umma (Fungu 09), na Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa (Fungu 04). Bunge lako Tukufu sasa lipokee na kujadili Mapitio ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha wa 2018/19. Aidha, naliomba Bunge lako Tukufu likubali kupitisha Mpango wa Utekelezaji na Makadirio ya Fedha kwa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha wa 2019/20. 2. Mheshimiwa Spika, Awali ya yote, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupatia uwezo wa kutekeleza majukumu ya kuwahudumia wananchi. Pia namshukuru Mheshimiwa Rais, kwa kuendelea kuniamini katika nafasi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora; Ninamuahidi kuwa nitatekeleza wajibu wangu kwa ufanisi na uadilifu wa hali ya juu. Aidha, nawashukuru wapiga kura wa Jimbo la Newala Mjini kwa ujumla kwa kuendelea kunipa ushirikiano wakati wote ninapoe ndelea kuwawakilisha. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Kumi na Tatu – Tarehe 10 Februari, 2010 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI (MHE. OMAR YUSSUF MZEE): Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Benki ya Posta Tanzania, kwa Mwaka 2008 [The Annual Report and Accounts of The Tanzania Postal Bank for the Year 2008]. The Mid-Term Review of the Monetary Policy Statement of The Bank of Tanzania for the Year 2009/2010. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini juu ya Taarifa ya Serikali Kuhusu Ubinafsishwaji wa Mgodi wa Kiwira. Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Mchakato wa Zabuni ya Kuzalisha Umeme wa Dharura Ulioipa Ushindi Kampuni ya Richmond Development Company LLC. Houston Texas - Marekani Mwaka 2006. MWENYEKITI WA KAMATI YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Miundombinu Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelzaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Uendeshaji Usioridhisha wa Shirika la Reli Tanzania uliofanywa na Kampuni ya RITES ya India. 1 Taarifa ya Kamati ya Miundombinu Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Utendaji wa Kazi Usioridhisha wa Kampuni ya TICTS. MASWALI NA MAJIBU Na. 145 Usimamizi wa Ukaguzi wa Fedha za Halmashauri MHE. HERBERT J. MNTANGI aliuliza:- Kwa kuwa, kiasi cha fedha kinachopelekwa katika Halmashauri za Wilaya, Manispaa na Jiji ni kikubwa na kinahitaji usimamizi wa ziada:- Kwa kuwa kitengo cha ukaguzi wa ndani kipo chini ya Mkurugenzi Mtendaji. -
MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao Cha Hamsini Na Tatu
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Tatu – Tarehe 19 Juni, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. PAMELA PALLANGYO – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU (K.n.y. WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO): Taarifa ya mwaka na Hesabu zilizokaguliwa za Bodi ya Mfuko wa Barabara kwa mwaka wa fedha 2014/2015 (The Annual Report and Audited Accounts of the Roads Fund Board for the Financial Year 2014/2015). NAIBU SPIKA: Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. PAMELA PALLANGYO – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU Na. 447 Kupandisha Hadhi Kituo cha Afya Sinza Kuwa Hospitali ya Wilaya MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:- Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alipotembelea Kituo cha Afya cha Palestina kilichopo Kata ya Sinza alitangaza kukipandisha hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, bado Serikali inaendelea kuipatia fedha hospitali hiyo kama Kituo cha Afya. Je, ni lini Serikali itaitambua hospitali hiyo kama Hospitali ya Wilaya kwa kuipa fedha na vitendea kazi vinavyofanana na hadhi yake? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saed Ahmed Kubenea, Mbunge wa Ubungo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya cha Palestina kimekuwa kinafanya kazi kama Hospitali ya Wilaya kufuatia tamko la Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne la tarehe 11 Disemba, 2012. -
Tarehe 12 Aprili, 2019
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Tisa – Tarehe 12 Aprili, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. NEEMA MSANGI - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Swali letu la kwanza asubuhi ya leo linaelekezwa kwa Ofisi ya Rais – TAMISEMI na linaulizwa na Mheshimiwa Shaabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Lushoto. Na. 68 Kukarabati Shule za Msingi na Sekondari - Lushoto MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Serikali imekuwa na utaratibu wa kukarabati shule zake za msingi na sekondari nchini:- Je, ni lini Serikali itazifanyia ukarabati Shule za Msingi Kwemashai, Bandi, Milungui, Kilole na Shule za Sekondari za Ntambwe, Ngulwi - Mazashai na Mdando? 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MWENYEKITI: Ahsante. Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Waitara. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shaabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Lushoto, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha mwaka 2018/2019, Serikali kupitia Program ya Lipa Kulingana na Matokeo (EPforR) imepeleka jumla ya shilingi milioni 467 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mawili, matundu sita ya vyoo na madarasa mawili katika Shule ya Msingi Shukilai (Shule ya Elimu Maalum) na ujenzi wa mabweni mawili Shule ya Sekondari Magamba, ujenzi wa bweni moja na madarasa mawili Shule ya Sekondari Umba. Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile katika mwaka wa Fedha 2018/2019, Serikali imetoa shilingi bilioni 29.9 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma 2,392 ya madarasa nchi nzima ambapo kati ya fedha hizo Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto imepewa kiasi cha Sh.512,500,000 kwa ajili ya kukamilisha maboma 46 ya madarasa shule za sekondari. -
MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao Cha Arobaini Na Moja
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Moja – Tarehe 31 Mei, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Tunaanza kikao chetu cha Arobaini na Moja, Katibu. NDG. LINA KITOSI – KATIBU MEZANI:- HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2018/19. MHE. CATHERINE V. MAGIGE (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu utekelezaji wa Bajeti na Majukumu ya Wizara 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019. MWENYEKITI: Ahsante. Katibu. NDG. LINA KITOSI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Swali letu la kwanza linaelekezwa Ofisi ya Waziri Mkuu na linaulizwa na Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, kwa niaba yake Mheshimiwa Amina Mollel. Na. 341 Utekelezaji wa Mpango wa Ukimwi 90-90-90 MHE. AMINA S. MOLLEL (K.n.y MHE. HAWA M. CHAKOMA) aliuliza:- Je, Serikali inatekelezaje Mpango wa UKIMWI wa 90- 90-90? MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Mollel. Majibu, Mheshimiwa Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA NA VIJANA) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa -
MKUTANO WA KUMI NA SABA Kikao Cha
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA SABA Kikao cha Kwanza – Tarehe 5 Novemba, 2019 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) WIMBO WA TAIFA D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge naomba tukae sasa. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge katika Mkutano wa Kumi na Sita wa Bunge, Bunge lilipitisha Miswada minne ya Sheria ya Serikali ifuatayo:- Kwanza, Muswada wa Sheria ya Serikali Mtandao ya Mwaka 2019 (The e- Government Bill, 2019). Pili, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali Na. 4 wa Mwaka 2019 (The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 4, Bill, 2019). Tatu, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 5 wa Mwaka 2019, (The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 5, Bill, 2019. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Nne, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali Na. 6 wa Mwaka 2019, ((The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 6, Bill, 2019. Kwa Taarifa hii, napenda kuliarifu Bunge kwamba tayari Miswada hiyo minne imepata kibali cha Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwa sheria za nchi, sasa zimekuwa sheria za nchi zinazoitwa kama ifuatavyo;- (Makofi) Sheria ya kwanza, ni Sheria ya Serikali Mtandao Na. 10 ya Mwaka 2019 (The e- Government Act No. 10 of 2019. Ya pili, ni sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali Na. 4, Sheria Na. 11 ya Mwaka 2019 ((The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 4, Act No.11 of 2019; na Tatu, Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. -
Tarehe 6 Aprili, 2018
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Nne - Tarehe 6 Aprili, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe.Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Tukae, Katibu. NDG.YONA KIRUMBI - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Maswali, Waheshimiwa karibuni kwenye Mkutano wetu, kikao chetu cha nne na swali letu la kwanza linaelekezwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI na linaulizwa na Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda. Na. 24 Ujenzi wa Vituo Vya Afya Ikuti na Ipinda MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi unaoendelea katika Vituo vya Afya Ikuti, Wilayani Rungwe na Ipinda Wilayani Kyela utakamilika ili kuwawezesha wananchi wa maeneo hayo kupata huduma kwa wakati? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:- 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya cha Ikuti kimekarabatiwa katika awamu ya kwanza ya ukarabati wa vituo vya afya 44 ulioanza tarehe 10 Oktoba, 2017 na kukamilika tarehe 31 Januari, 2018 kwa gharama ya shilingi milioni 500 ili kuongeza huduma za upasuaji wa dharura kwa mama wajawazito. Aidha, shilingi milioni 220 zimetolewa kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba vya upasuaji na samani. Kituo hicho kinaendelea kutoa huduma zote za matibabu isipokuwa huduma za upasuaji wa dharura. Ujenzi wa majengo ya Kituo cha Afya Ikuti umekamilika na kinachosubiriwa kwa sasa ni vifaatiba kutoka Bohari ya Dawa (MSD). -
Tarehe 7 Februari, 2017
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA SITA Kikao cha Saba – Tarehe 7 Februari, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Tukae. Katibu. NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na: MHE. PROF. NORMAN A. S. KING – MWENYEKITI WA KAMATI YA BUNGE YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kwa kipindi cha kuanzia Januari, 2016 hadi Januari, 2017. MHE. DOTO M. BITEKO -MWENYEKITI WA KAMATI YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa kipindi cha kuanzia Januari 2016 hadi Januari 2017. NAIBU SPIKA: Ahsante. Katibu! NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na maswali, Ofisi ya Rais - TAMISEMI. Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, Mbunge wa Viti Maalum, sasa aulize swali lake. Na. 69 Tatizo la Ulevi MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza:- 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Ulevi wa kupita kiasi hasa wa pombe za kienyeji umekuwa na athari kubwa za kiafya na kiakili kwa Watanzania wenye tabia ya ulevi wa kukithiri:- Je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na tatizo hilo hasa ikizingatiwa kuwa Sheria ya Vileo ya mwaka 1969 ni ya zamani sana kiasi kwamba inawezekana kabisa haikidhi mabadiliko ya hali halisi ya vileo kwa wakati huu. NAIBUWAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, pombe za kienyeji zimeainishwa katika Kifungu cha pili (2) cha tafsiri katika Sheria ya Vileo, Sura ya 77. -
MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao Cha Nane
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _______ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Nane – Tarehe 14 Aprili, 2020 (Bunge Lilianza Saa Nane Mchana) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Wabunge, tukae, Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU (Maswali yafuatayo yameulizwa na kujibiwa kwa njia ya mtandao) Na. 64 Kampuni Zinazofanya Kazi Ndani ya Mgodi wa Geita MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:- Kampuni ambazo zinafanya kazi ndani ya Mgodi wa Geita Gold Mine(contractors) zimekuwa zikilalamikiwa na wananchi wanaofanya kazi kwa kutopeleka fedha kwenye Mifuko ya Jamii na kutowapa mikataba:- Je, Serikali inachukua hatua gani kukomesha malalamiko hayo? WAZIRI MKUU alijibu:- 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Naibu Spika, Mgodi wa Geita Gold Mine (GGM) ni moja ya waajiri walioandikishwa na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) na watumishi wanaofanya kazi katika mgodi huo wamegawanyika katika makundi mawili ambayo ni wale walioajiriwa moja kwa moja na GGM na wale walioajiriwa na wakandarasi wanaotoa huduma ndani ya mgodi huo. Mheshimiwa Naibu Spika, mwezi Februari 2020, jumla ya shilingi bilioni 5.01 zililipwa na Mgodi wa GGM kama mchango wa mwezi Januari, 2020 kwa watumishi 2,038 walioajiriwa moja kwa moja na GGM na kuandikishwa na NSSF. Katika mwezi huo huo, jumla ya wanachama 6,128 ambao wameajiriwa na wakandarasi 39 wanaotoa huduma ndani ya mgodi huo walikuwa wameandikishwa na NSSF na kuchangiwa wastani wa shilingi bilioni 1.3 Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia OWM-KVAU imekuwa ikifanya kaguzi katika maeneo mbalimbali ya kazi ikiwemo ya migodini kwa lengo la kuimarisha utekelezaji wa Sheria za Kazi. -
Tarehe 9 Mei, 2019
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 9 Mei, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu. NDG. JOSHUA CHAMWELA – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa mwaka wa fedha 2019/2020. MHE. ASHA MSHIMBA JECHA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa mwaka wa fedha 2018/ 2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. QAMBALO W. QULWI – NAIBU MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Kuhusu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NAIBU SPIKA: Ahsante. Waheshimiwa tunaendelea. Katibu. NDG. JOSHUA CHAMWELA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Maswali, tutaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi sasa aulize swali lake. Na. 196 Serikali Kuzipatia Waganga Zahanati za Jimbo la Manyoni Magharibi MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Wananchi wa Manyoni Magharibi kwa kushirikiana na Serikali kupitia miradi mbalimbali ikiwemo TASAF wamejenga zahanati katika Vijiji vya Gurungu, Sanjaranda, Kitopeni, Ipande, Doroto, Itagata, Kalangali, Makale, Mwamagembe na Kintanula, lakini mpaka sasa zahanati hizi hazina Waganga:- Je, ni lini Serikali itazipatia zahanati hizo Waganga, ili wananchi wapate huduma kufuatana na sera yake? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu.