Majadiliano Ya Bunge

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

Majadiliano Ya Bunge Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Ishirini na Nane – Tarehe 12 Julai, 2010 (Mkutano ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI: Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na: NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI (MHE. MWANTUMU B. MAHIZA): Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa Mwaka 2010/2011. Taarifa ya Mwaka ya Mamlaka ya Elimu Tanzania kwa Mwaka 2008/2009 [The Annual Report of Tanzania Education Authrority for the Year 2008/2009]. MHE. OMARI SHABANI KWAANGW’ - MWENYEKITI WA KAMATI YA HUDUMA ZA JAMII: Taarifa ya Kamati ya Huduma za Jamii Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010 pamoja na maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha, 2010/2011. MHE. NURU AWADH BAFADHIL K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: 1 Taarifa ya mwaka na Hesabu zilizokaguliwa za Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2008/2009 [The Annual Report and Audited Accounts of the Local Authorities Pensions Fund (LAPF) for the Year 2008/2009]. NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI (MHE. OMAR YUSSUF MZEE): Randama za Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Fedha na Uchumi kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. MASWALI NA MAJIBU Na. 201 Migogoro Katika Shule Za Sekondari za Kata – Mwibara MHE. DR. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. CHARLES M. KAJEGE) aliuliza:- Kwa kuwa, mojawapo ya vyanzo vya migogoro katika Shule za Sekondari za Kata katika Jimbo la Mwibara ni Bodi za Shule hizo:- (a) Je, Serikali inatambua hilo? (b) Je, ni sifa/vigezo gani vinatumika kuwachagua Wajumbe wa Bodi hizo? (c) Je, Serikali imefanya juhudi gani za kumaliza hilo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, kabla sijajibu swali la Mheshimiwa Kajege, ninakuomba kwa unyenyekevu mkubwa uniruhusu kwa niaba ya wananchi wa Jimbo langu la Siha, nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye Mkutano Mkuu umempitisha kwa kishindo na ninataka nimthibitishie kwamba wananchi wa Siha wapo na yeye na wataendelea kumpa ushirikiano. Kwa kipekee, pia nimpongeze Mheshimiwa Makamu wa Rais Dr. Shein, kwa kupitishwa na Halmashauri ya Kuu ya Taifa kuwa mgombea wa Serikali ya Mapinduzi, Zanzibar pamoja na Dr. Bilal kwa kuteuliwa kuwa mgombea mwenza. (Makofi) Mheshimiwa Spika, baada ya hayo yote nakushukuru sana kwa kunipa ruksa hiyo. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, kabla ya kujibu swali la Mheshimiwa Charles Muguta Kajege Mbunge wa Mwibara, lenye sehemu (a), (b) na (c) naomba kutoa ufafanuzi kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Jimbo la Mwibara lina Shule za Sekondari za Kata 8 na shule moja ni ya binafsi. Shule hizo ni hizi zifuatazo; Bulamba, Chitengule, Chisorya, 2 Kwiramba, Muranda, Mwigundu, Nansimo na Nyeruma. Shule zote 8 katika Kata ya Jimbo la Mwibara zina Bodi ambazo zimeundwa kisheria kwa kuzingatia sheria ya elimu namba 25 ya mwaka 1978 kama ilivyorekebishwa na sheria namba 10 ya mwaka 1995. Kwa kuzingatia sheria hiyo, Bodi za shule zimepewa majukumu ya kusimamia uongozi na uendeshaji wa mipango yote ya maendeleo ya shule, kusimamia nidhamu kwa walimu na wanafunzi na kusimamia matumizi ya fedha za shule. Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo sasa napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa kulikuwa na migogoro katika shule mbili za Sekondari za Kata katika Jimbo la Mwibara, ambayo ni migogoro katika shule za Sekondari za Nyeruma na Muranda. Mgogoro wa shule za Sekondari Nyeruma ulikuwa ni kati ya Bodi ya Shule na Mkuu wa Shule. Chanzo cha Mgogoro huu ni Mkuu wa Shule kutoshirikisha Bodi ya Shule katika uendeleshaji wa shule, kutothamini michango yao ya mawazo na kutokusoma mapato na matumizi ya michango kutoka kwa wazazi. Mgogoro wa shule ya Sekondari ya Muranda ulikuwa kati ya uongozi wa shule na baadhi ya viongozi wa Kata ya Namhula, baada ya kutokea mgomo wa wanafunzi tarehe 19 mpaka terehe 20 Februari, 2009 uliosababishwa na mwanafunzi mmoja kuja na silaha (panga) shuleni na kutishia kuwajeruhi walimu wa shule hiyo, kinyume na taratibu za shule, hasa baada ya shule kuwafukuza wanafunzi 14 waliobainika kuchochea mgomo wa wanafunzi wa tarehe 19 mpaka tarehe 20 Februari, 2009. (b) Mheshimiwa Spika, sifa au vigezo vinavyohitajika katika kuteua wajumbe wa Bodi za shule ni hizi zifuatazo:- (i) Mjumbe wa Bodi ya Shule asiwe kwenye Bodi za shule zaidi ya tatu. (ii) Mjumbe asitoke nje ya mkoa. (iii) Mjumbe asiwe na majukumu mengi ya kitaifa. (iv) Wajumbe wanaopendekezwa watoke kwenye maeneo mbali mbali kama Taasisi za Kidini na Jumuiya zisizo za Serikali. (v) Wadau wa Elimu wanaoendelea na kazi zao Serikalini. Mfano, Wakaguzi wa Shule, Walimu, Maafisa elimu, walimu waliostaafu, wanaruhusiwa pia. (c) Mheshimiwa Spika, juhudi zilizochukuliwa katika kutatua mgogoro wa Shule ya Sekondari Nyeruma, ni uongozi wa Halmashauri ya Wilaya kwenda shuleni Nyeruma, kukutana na wajumbe wa Bodi ya Shule, Walimu, Wazazi na kusikiliza pande zote. Mapendekezo yaliyofikiwa ni kumhamisha Mkuu wa Shule, kupisha Ukaguzi wa vitabu vya fedha katika shule hiyo. Aidha, hatua zilizochukuliwa kutatua mgogoro wa shule ya Sekondari Muranda, ni kuwafukuza wanafunzi baada ya kukiuka taratibu za 3 shule, kurejesha hali ya utulivu shuleni, kuagiza uongozi wa shule kuitisha Kikao cha Bodi ya shule na kumhamisha Mkuu wa Shule na kupeleka Mkuu wa Shule mwingine. MHE. DR. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa, Mheshimiwa Naibu Waziri, ameelezea sifa na vigezo vya hawa wajumbe wa Bodi wa Shule za Sekondari. Kwa kuwa, matatizo yaliyojitokeza Mwibara, yanafanana na shule nyingi za sekondari hapa nchini na kwamba baadhi ya Wajumbe wa Bodi, wanatoka maeneo ambayo ni mbali na zilipo shule na hivyo kuchochea mfumuko wa gharama za kuwahudumia wanapokuja kwenye mkutano wa Bodi. Je, ni kwa nini Serikali isingeona umuhimu wa kuainisha zaidi vigezo vya Wajumbe wa Bodi watokane na maeneo ambayo wananchi au wana jamii waweze kushiriki katika kuwachagua ili waweze kuteuliwa kwenye hizi Bodi, badala ya kumwachia Mwalimu Mkuu, kuteua watu ambao yeye anadhani wanafaa kufanyanao kazi? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dr. Raphael Chegeni, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, labda kwanza nieleze kwamba ilikuwaje, halafu na sasa ikoje. Mheshimiwa Spika, zamani aliyekuwa anawateuwa wajumbe wa Bodi, alikuwa ni Waziri mwenye dhamana, yaani maana yeke ni kwamba Profesa Maghembe ndiye angekuwa anawateuwa, lakini sasa alichofanya amekasimu madaraka yale yakawa yanapitia kwa ma-REO.Wale Wakuu wa Shule walioko pale walichoagizwa ni kwamba wahakikishe, na hapa nimeisoma, kwamba wale wanaowateuwa na wale wanaowapendekeza ambao hatimaye watapelekwa mpaka kwa Mheshimiwa Waziri, wawe ni watu wanaotoka katika maeneo yale na ni watu ambao wanaweza wakapatikana. Mheshimiwa Spika, sasa msisitizo ambao anauweka hapa, mimi ninauona. Kwa sababu ukisema wajumbe wa Bodi kama ni wa Manyara wakatoka Mtwara, ukawaleta pale ukaanza kuwasafirisha kuwapeleka pale ni kazi ngumu. Lakini nafikiri ninachoweza kukiona hapa ni kwamba Mheshimiwa Mbunge, ana pointi kubwa na anachosema ni kwamba tuhakikishe kwamba wanatoka katika Mkoa uleule. Lakini hata kama wanatoka katika Mkoa uleule anachosisitiza yeye ni kwamba watoke pale karibu na shule ili waweze kuisaidia shule. Mimi ninalichukua hili na ninajua kwamba tutafanya mawasiliano na Mheshimiwa Waziri wa Elimu, ili tuweze kuona kwamba hilo linafanyika kama anavyoshauri. MHE. JUMA H. KILLIMBAH: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa, sasa hivi kuna wingi wa shule hizi za Sekondari hasa kwenye maeneo ya Kata. Na kwa kuwa, mara nyingi uteuzi kama anavyoeleza, utaratibu wa kuchukua watu wanaotoka maeneo yaliyo karibu na wanaopatikana katika Mkoa huo uko sahihi, lakini liko tatizo moja kubwa juu 4 ya uelewa wa wajibu wao katika kufanya shughuli katika Bodi hizo. Na mara nyingi wanaonekana kuburuzwa na walimu kwa sababu hawaelewi wajibu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba inawaelimisha ili kuondoa hiyo tofauti iliyopo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Killimbah, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, labda hili nalo nilisemee. Ni kwamba kwanza kabisa ushauri unaotolewa hapa, ukimpleka mtu anayeingia katika Bodi ya Shule, minimum qualification walao awe amemaliza Form IV. Ukifanya hivyo inakusaidia sana uelewa, kwa sababu hata kama utapeleka watu wa pale ni lazima uwe na watu ambao wataelewa watakapoeleweshwa. Lakini mara kwa mara, kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na TAMISEMI, tumekuwa tunatoa Semina kwa ajili ya wajumbe hawa ili waweze kuongeza uelewa wao. Kwa hiyo, hili analolisema Mheshimiwa Killimbah, tunakubaliana na yeye na tutafanya hivyo. Lakini suala la qualification hapa kwa wajumbe, nalo ni muhimu pia. (Makofi) MHE. SIJAPATA F. NKAYAMBA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, Kata nyingi sasa hivi zina Sekondari na zote zimeshafikia Form IV. Na kwa kuwa, wanafunzi wanapoanza Form I, huwa wanaambiwa wapeleke meza na viti. Je, vile viti vingine huwa vimeenda wapi? SPIKA: Amechomekea tu, lakini labda Mheshimiwa Waziri wa Elimu; maana hili sasa limekuwa mahususi mno. (Makofi/Kicheko) WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi nijibu swali la nyongeza. Lakini pia napenda nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa majibu mazuri ambayo ameyatoa katika masali ya awali yaliyoulizwa juu ya suala hili.
Recommended publications
  • Ruaha Journal of Business, Economics and Management Sciences, Vol.1, Issue 1, 2018  Ms Hadija Matimbwa , Faculty of Business and Management Science, RUCU Iii
    RUAHA JOURNAL of Business, Economics and Management Sciences Faculty of Business and Management Sciences Vol 1, Issue 1, 2018 A. Editorial Board i. Executive Secretarial Members Chairman: Dr. Alex Juma Ochumbo, Dean Faculty of Business and Management Sciences, RUCU Chief Editor: Prof. Robert Mabele, Faculty of Business and Management Sciences, RUCU Managing Editor: Dr.Venance Ndalichako, Faculty of Business and Management Sciences, RUCU Business Manager: Dr. Alberto Gabriel Ndekwa, Faculty of Business and Management Science, RUCU Secretary to the Board: Ms. Hawa Jumanne,Faculty of Business and Management Science, RUCU ii. Members of the Editorial Board Dr. Dominicus Kasilo, Faculty of Business and Management Science, RUCU Bishop Dr. Edward Johnson Mwaikali,Bishop of Mbeya, Formerly with RUCU Dr. Theobard Kipilimba, Faculty of Business and Management Science, RUCU Dr. Esther Ikasu, Faculty of Business and Management Science, RUCU ii Ruaha Journal of Business, Economics and Management Sciences, Vol.1, Issue 1, 2018 Ms Hadija Matimbwa , Faculty of Business and Management Science, RUCU iii. Associate Editors Prof. Enock Wicketye Iringa University,Tanzania. Dr. Enery Challu University of Dar es Dr. Ernest Abayo Makerere University, Uganda. Dr. Vicent Leyaro University of Dar es Salaam Dr. Hawa Tundui Mzumbe University, Tanzania. B. Editorial Note Ruaha Journal of Business, Economics and Management Sciences would like to wish all our esteemed readers on this first appearance A HAPPY NEW YEAR. We shall be appearing twice a year January and July. We hope you will be able to help us fulfill this pledge by feeding us with journal articles, book reviews and other such journal writings and stand ready to read from cover to cover all our issues.
    [Show full text]
  • Issued by the Britain-Tanzania Society No 114 May - Aug 2016
    Tanzanian Affairs Issued by the Britain-Tanzania Society No 114 May - Aug 2016 Magufuli’s “Cleansing” Operation Zanzibar Election Re-run Nyerere Bridge Opens David Brewin: MAGUFULI’S “CLEANSING” OPERATION President Magufuli helps clean the street outside State House in Dec 2015 (photo State House) The seemingly tireless new President Magufuli of Tanzania has started his term of office with a number of spectacular measures most of which are not only proving extremely popular in Tanzania but also attracting interest in other East African countries and beyond. It could be described as a huge ‘cleansing’ operation in which the main features include: a drive to eliminate corruption (in response to widespread demands from the electorate during the November 2015 elections); a cutting out of elements of low priority in the expenditure of government funds; and a better work ethic amongst government employees. The President has changed so many policies and practices since tak- ing office in November 2015 that it is difficult for a small journal like ‘Tanzanian Affairs’ to cover them adequately. He is, of course, operat- ing through, and with the help of ministers, regional commissioners and cover photo: The new Nyerere Bridge in Dar es Salaam (see Transport) Magufuli’s “Cleansing” Operation 3 others, who have been either kept on or brought in as replacements for those removed in various purges of existing personnel. Changes under the new President The following is a list of some of the President’s changes. Some were not carried out by him directly but by subordinates. It is clear however where the inspiration for them came from.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Tatu – Tarehe 15 APRILI, 2010 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU NAIBU SPIKA: Maswali kwa Waziri Mkuu leo kiongozi wa Upinzani Bungeni hayupo kwa hiyo nitaenda na orodha za wachangiaji na nitakuwa ninakwenda kufuatana na itikadi ya chama, upande, gender na vitu kama hivyo. Kwa hiyo, walioko hapa wasidhani watakwenda kama ilivyoorodheshwa. Kwa hiyo, nitaanza na msemaji wa kwanza Mheshimiwa Dr. Willibrod Slaa. MHE. DR. WILLIBROD P. SLAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kunipa nafasi, Mheshimiwa Waziri Mkuu sasa ni takribani mwaka mzima tangu nilipoanza kuhoji, mimi na Wabunge wenzangu, tulipoanza kuhoji kuhusu ubadhirifu na tuhuma mbalimbali zilizokuwa zinakabili matumizi ya fedha za umma zilizofanywa na makampuni kama Mwananchi Gold Company, Tan Gold, Kagoda, Deep Green na mengine mengi ambayo yalitajwa ndani ya ukumbi huu. Kwa nyakati tofauti maelezo mbalimbali yametolewa ndani ya Bunge. Mpaka leo hatujapata taarifa ya kinachoendelea. Bunge hili lenye jukumu la kuisimamia Serikali halijui au wananchi hawajui kama kuna kitu kinaendelea je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu ubadhirifu huo? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naamini kabisa Dr. Slaa, hutegemei kwamba kweli nitaweza kujibu maswali hayo uliyoyauliza kwamba mimi nina maelezo juu ya Kagoda, maelezo juu ya nani, is not possible nadhani si sahihi kabisa. (Makofi) Mimi ninachoweza kusema ni kwamba jitihada za Serikali zipo zimekuwa zikionekana katika maeneo ambayo yameshaanza kufanyiwa kazi. Sasa kama kuna maeneo ambayo bado hayajafanyiwa kazi jitihada za Serikali zitaendelea kwa kadri itakavyowezekana.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Kumi na Tatu – Tarehe 10 Februari, 2010 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI (MHE. OMAR YUSSUF MZEE): Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Benki ya Posta Tanzania, kwa Mwaka 2008 [The Annual Report and Accounts of The Tanzania Postal Bank for the Year 2008]. The Mid-Term Review of the Monetary Policy Statement of The Bank of Tanzania for the Year 2009/2010. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini juu ya Taarifa ya Serikali Kuhusu Ubinafsishwaji wa Mgodi wa Kiwira. Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Mchakato wa Zabuni ya Kuzalisha Umeme wa Dharura Ulioipa Ushindi Kampuni ya Richmond Development Company LLC. Houston Texas - Marekani Mwaka 2006. MWENYEKITI WA KAMATI YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Miundombinu Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelzaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Uendeshaji Usioridhisha wa Shirika la Reli Tanzania uliofanywa na Kampuni ya RITES ya India. 1 Taarifa ya Kamati ya Miundombinu Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Utendaji wa Kazi Usioridhisha wa Kampuni ya TICTS. MASWALI NA MAJIBU Na. 145 Usimamizi wa Ukaguzi wa Fedha za Halmashauri MHE. HERBERT J. MNTANGI aliuliza:- Kwa kuwa, kiasi cha fedha kinachopelekwa katika Halmashauri za Wilaya, Manispaa na Jiji ni kikubwa na kinahitaji usimamizi wa ziada:- Kwa kuwa kitengo cha ukaguzi wa ndani kipo chini ya Mkurugenzi Mtendaji.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA KUMI NA MBILI ___Kikao Cha Sita
    Hii ni nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA KUMI NA MBILI __________ Kikao cha Sita - Tarehe 18 Juni, 2003 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Juma J. Akukweti) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 50 Upungufu wa Watumishi - Hospitali ya Wilaya ya Mbulu MHE. PHILIP S. MARMO aliuliza:- Kwa kuwa siku zilizopita Wizara imekiri upungufu mkubwa wa watumishi katika Hospitali ya Wilaya ya Mbulu katika fani zote kama Madaktari, Wauguzi, Wataalam wa X-ray na Famasia na mfano mmoja ukiwa ni kwamba mashine mpya za chumba cha X- ray hazitumiki kwa sababu ya ukosefu wa wataalam. Je, ni lini Serikali itawaajiri wataalam niliowataja ili kutatua tatizo hilo sugu? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Philip Marmo, Mbunge wa Mbulu, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tarehe 18 Julai, 2002 wakati nikijibu swali Na. 873 la Mheshimiwa Mbunge, nilikiri upungufu wa wataalam wa afya katika Hospitali ya Wilaya ya Mbulu. Naomba kumpongeza kwanza Mheshimiwa Philip Marmo, Mbunge wa Mbulu, kwa juhudi zake kubwa sana anazozichukua katika kutatua matatizo yaliyoko katika Hospitali ya Wilaya ya Mbulu ikiwa ni pamoja na upungufu wa watumishi. Halmashauri 1 za Wilaya nyingi hapa nchini bado zina upungufu wa wataalam katika fani mbalimbali. Ofisi ya Rais, pamoja na Idara Kuu ya Utumishi inajitahidi sana kutoa vibali vya ajira, lakini waombaji wa kazi hizo mara nyingi wamekuwa ni wachache. Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Wilaya ya Mbulu ni moja ya Hospitali za Wilaya ambazo zina upungufu wa Madaktari, Wauguzi na wataalam wengine.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 18 Julai, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita muuliza swali la kwanza nina matangazo kuhusu wageni, kwanza wale vijana wanafunzi kutoka shule ya sekondari, naona tangazo halisomeki vizuri, naomba tu wanafunzi na walimu msimame ili Waheshimiwa Wabunge waweze kuwatambua. Tunafurahi sana walimu na wanafunzi wa shule zetu za hapa nchini Tanzania mnapokuja hapa Bungeni kujionea wenyewe demokrasia ya nchi yetu inavyofanya kazi. Karibuni sana. Wapo Makatibu 26 wa UWT, ambao wamekuja kwenye Semina ya Utetezi na Ushawishi kwa Harakati za Wanawake inayofanyika Dodoma CCT wale pale mkono wangu wakulia karibuni sana kina mama tunawatakia mema katika semina yenu, ili ilete mafanikio na ipige hatua mbele katika kumkomboa mwanamke wa Tanzania, ahsanteni sana. Hawa ni wageni ambao tumetaarifiwa na Mheshimiwa Shamsa Selengia Mwangunga, Naibu Waziri wa Maji. Wageni wengine nitawatamka kadri nitakavyopata taarifa, kwa sababu wamechelewa kuleta taarifa. Na. 223 Barabara Toka KIA – Mererani MHE. DORA H. MUSHI aliuliza:- Kwa kuwa, Mererani ni Controlled Area na ipo kwenye mpango wa Special Economic Zone na kwa kuwa Tanzanite ni madini pekee duniani yanayochimbwa huko Mererani na inajulikana kote ulimwenguni kutokana na madini hayo, lakini barabara inayotoka KIA kwenda Mererani ni mbaya sana
    [Show full text]
  • MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao Cha Hamsini Na Tatu
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Tatu – Tarehe 19 Juni, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. PAMELA PALLANGYO – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU (K.n.y. WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO): Taarifa ya mwaka na Hesabu zilizokaguliwa za Bodi ya Mfuko wa Barabara kwa mwaka wa fedha 2014/2015 (The Annual Report and Audited Accounts of the Roads Fund Board for the Financial Year 2014/2015). NAIBU SPIKA: Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. PAMELA PALLANGYO – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU Na. 447 Kupandisha Hadhi Kituo cha Afya Sinza Kuwa Hospitali ya Wilaya MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:- Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alipotembelea Kituo cha Afya cha Palestina kilichopo Kata ya Sinza alitangaza kukipandisha hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, bado Serikali inaendelea kuipatia fedha hospitali hiyo kama Kituo cha Afya. Je, ni lini Serikali itaitambua hospitali hiyo kama Hospitali ya Wilaya kwa kuipa fedha na vitendea kazi vinavyofanana na hadhi yake? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saed Ahmed Kubenea, Mbunge wa Ubungo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya cha Palestina kimekuwa kinafanya kazi kama Hospitali ya Wilaya kufuatia tamko la Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne la tarehe 11 Disemba, 2012.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao Cha Pili – Tarehe 11 Juni, 20
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Pili – Tarehe 11 Juni, 2008 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kama kawaida yetu, tunaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu na atakayeuliza swali la kwanza leo ni Mheshimiwa Bakar Shamis Faki. Na. 11 Bunge Kuahirishwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu MHE. ABUBAKAR KHAMIS BAKARY (K.n.y. MHE. BAKAR SHAMIS FAKI) aliuliza:- Kwa kuwa Bunge ni moja kati ya mihimili mitatu ya Dola ambalo lina bajeti yake ya kujitegemea; na kwa kuwa Mheshimiwa Spika ndiye Kiongozi wa mhimili huo:- Je, kwa nini Hoja ya Kuahirisha Bunge inatolewa na Waziri Mkuu ambaye ni sehemu ya mihimili mingine badala ya Mheshimiwa Spika ambaye ndiye Kiongozi wa mhimili wa Bunge? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (MHE. PHILIP S. MARMO) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba nimjibu Mheshimiwa Bakar Shamis Faki, Mbunge wa Ole, swali lake kama ifuatavyo:- Ni kweli Bunge ni moja ya mihimili mitatu ya Dola na hili limetamkwa katika Katiba yetu, mihimili mingine ni Serikali na Mahakama. Waziri Mkuu, akishathibitishwa na Bunge kushika madaraka yake Kikatiba, ndiye Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni na anatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba, Sheria za Nchi na Kanuni za Bunge hili Tukufu. 1 Mheshimiwa Naibu Spika, nafasi ya kutoa Hoja ya Kuahirisha Bunge, baada ya Shughuli za Bunge zilizopangwa kufanyiwa kazi na Mkutano wa Bunge kumalizika ni kuzingatia matakwa ya Katiba.
    [Show full text]
  • Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
    JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA SITA (DAILY SUMMARY RECORD OF PROCEEDINGS) 11 NOVEMBA, 2014 MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA KIKAO CHA SITA – 11 NOVEMBA, 2014 I. DUA Saa 3.00 Asubuhi kikao kilianza kikiongozwa na Mhe. Naibu Spika (Mhe Job Y. Ndugai) na alisoma Dua. Makatibu Mezani 1. Ramadhani Abdallah Issa 2. Asia Minja 3. Hellen Mbeba II. MASWALI Maswali yafuatayo yaliulizwa na yalijibiwa:- 1. OFISI YA WAZIRI MKUU Swali . 67 – Mhe. Charles J.P. Mwijage Nyongeza (i) Mhe. Charles Mwijage (ii) Mhe. Joshua Nassari Swali. 68- Mhe. Hezekiah Chibulunje (K.n.y – Mhe. David Mallole) Nyongeza (i) Mhe. Hezekiah Chibulunje Swali. 69 – Mhe. Josephat Sinkamba Kandege Nyongeza (i) Mhe. Josephat Kandege 2. OFISI YA RAIS (UTAWALA BORA) Swali. 70 – Mhe. Amina Abdulla Amour 2 Nyongeza (i) Mhe. Amina Abdullah Amour 3. OFISI YA RAIS (MAHUSIANO NA URATIBU) Swali. 71 – Mhe. Leticia Mageni Nyerere Nyongeza i. Mhe. Leticia Nyerere ii. Mhe. Mohammed Habib Mnyaa 4. OFISI YA MAKAMU WA RIAS (MAZINGIRA) Swali. 72 – Mhe. Victor Kilasile Mwambalaswa Nyongeza i. Mhe. Victor Kilasile Mwambalaswa. 5. WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Swali. 73 – Mhe. Diana Mkumbo Chilolo Nyongeza i. Mhe. Diana Mkumbo Chilolo 6. WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA Swali. 74 – Mhe. Sylvestry Francis Koka Nyongeza i. Mhe. Sylvestry Koka ii. Mhe. Salim Masoud 7. WIZARA YA UCHUKUZI Swali. 75 – Mhe. Prof. David Mwakyusa (k.n.y Mhe. Luckson Mwanjale). Nyongeza i. Mhe. Prof. David Mwakyusa. 3 Swali. 76 – Mhe.
    [Show full text]
  • MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao Cha Arobaini Na Moja
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Moja – Tarehe 31 Mei, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Tunaanza kikao chetu cha Arobaini na Moja, Katibu. NDG. LINA KITOSI – KATIBU MEZANI:- HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2018/19. MHE. CATHERINE V. MAGIGE (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu utekelezaji wa Bajeti na Majukumu ya Wizara 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019. MWENYEKITI: Ahsante. Katibu. NDG. LINA KITOSI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Swali letu la kwanza linaelekezwa Ofisi ya Waziri Mkuu na linaulizwa na Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, kwa niaba yake Mheshimiwa Amina Mollel. Na. 341 Utekelezaji wa Mpango wa Ukimwi 90-90-90 MHE. AMINA S. MOLLEL (K.n.y MHE. HAWA M. CHAKOMA) aliuliza:- Je, Serikali inatekelezaje Mpango wa UKIMWI wa 90- 90-90? MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Mollel. Majibu, Mheshimiwa Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA NA VIJANA) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge Mkutano Wa Kumi Na Sita
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA KUMI NA SITA _________________ Kikao cha Kumi na Tano – Tarehe 27 Juni, 2009 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Zubeir Ali Maulid) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MAZINGIRA NA MUUNGANO):- Randama za Ofisi ya Makamu wa Rais, (Mazingira na Muungano) kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010. HOJA ZA SERIKALI Makadirio ya Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2009/2010 Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (Majadiliano yanaendelea) MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge jana wakati Mheshimiwa Spika anamalizia shughuli, jana jioni alitawangazia wachangiaji watatu watakaomalizia mchango leo asubuhi. Kwa hiyo naomba nimwite Mheshimiwa Magdalena Hamis Sakaya, atafuatiwa na Mheshimiwa Magale John Shibuda na Mheshimiwa Estherina Kilasi, hivyo ajiandae. MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi hii kukushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia hoja iliyoko mbele yetu. Pia nawapongeza Waheshimiwa Mawaziri wote wa Menejimenti ya 1 Utumishi wa Umma, pamoja na Utawala Bora kwa kuweza kuandaa hotuba hii na kuileta hapa Bungeni ili tuweze kuijadili. Mheshimiwa Mwenyekiti, niende moja kwa moja kwenye mchango wangu, mchango wa kwanza unaenda kwenye utendaji wa watumishi hasa Serikalini, imekuwa ni jambo la kawaida kwamba kuna utendaji duni sana kwa watumishi umma usiokuwa na tija kwa taifa. Watumishi wanafanya kazi bila malengo mkuu wa kitengo anakaa mahali mwezi mzima kwenye idara yake hajawa na malengo kwamba amelenga wapi kwa hiyo mwanzo wa mwezi hana malengo kwamba mwisho wa mwezi atakuwa amezalisha kitu gani.
    [Show full text]
  • Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1 MAJADILIANO YA BUNGE
    Nakala ya Mtandao (Online Document) MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA ISHIRINI __________ Kikao cha Ishirini na Moja - Tarehe 5 Juni, 2015 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, napenda kuchukua nafasi hii kuwapa pole wote kwa msiba uliotupata, msiba ulitokea wakati nikiwa Geneva ambapo tulikuwa na kikao cha Kamati Ndogo ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Maspika wote duniani utakaofanyika mwezi wa Nane, sasa kuna Maspika kumi ndiyo tupo kwenye maandalizi ya mkutano huo na kilikuwa ni kikao chetu cha mwisho kabla ya mkutano huo. Kwa hiyo, wakati msiba unatokea nilikuwa huko, nilipewa taarifa na nilisikitika sana. Kwa hiyo, tutatangaza baadaye mchana, ni akina nani watakaokwenda kuzika kesho. Katibu! HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI (MHE. CHARLES M. KITWANGA): Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. NAIBU WAZIRI WA MAJI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Maji kwa mwaka wa Fedha, 2015/2016. MHE. DAVID H. MWAKYUSA (k.n.y. MHE. PROF. PETER M. MSOLLA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015, pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa Fedha 2015/2016. MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED (k.n.y. MHE. MAGDALENA H. SAKAYA - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KWA WIZARA YA MAJI): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Fedha kwa Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016.
    [Show full text]