Majadiliano Ya Bunge
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Sita – Tarehe 9 Aprili, 2019
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Sita – Tarehe 9 Aprili, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu! NDG. RUTH MAKUNGU – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI: Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa mwaka wa fedha 2019/2020. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2019/2020. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Taarifa ya Mwaka na Hesabu zilizokaguliwa za Chuo Kikuu Mzumbe kwa mwaka ulioisha tarehe 30 Juni, 2017 (The Annual Report and Audited Accounts of Mzumbe University for the year ended 30th June, 2017). MWENYEKITI: Katibu! NDG. RUTH MAKUNGU – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Swali letu la kwanza leo linaelekezwa Ofisi ya Waziri Mkuu na linaulizwa na Mheshimiwa Dkt. Raphael Masunga Chegeni, Mbunge wa Busega. MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipo hapa kwa niaba. MWENYEKITI: Wewe unatoka Busega? MHE. RASHID A. SHANGAZI: Hapana, ila hili ni la kitaifa. MWENYEKITI: Aaa, sawa, kwa niaba. Na. 43 Kauli Mbiu ya Kuvutia Wawekezaji Nchini MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. DKT. -
-
Ofisi Ya Rais, Menejimenti Ya Utumishi Wa Umma Na Utawala Bora Kwa Mwaka Wa Fedha Wa 2019/20
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI – OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA. KAPT (MST) GEORGE H. MKUCHIKA (Mb.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2019/20 APRILI, 2019 A. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba, kutokana na taarifa iliyowasilishwa ndani ya Bunge lako Tukufu na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa iliyochambua bajeti ya Ofisi ya Rais, Ikulu (Fungu 20 na 30), Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma (Fungu 33), Menejimenti ya Utumishi wa Umma (Fungu 32), Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma (Fungu 67), Tume ya Utumishi wa Umma (Fungu 94), Bodi ya Mishahara na Masilahi katika Utumishi wa Umma (Fungu 09), na Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa (Fungu 04). Bunge lako Tukufu sasa lipokee na kujadili Mapitio ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha wa 2018/19. Aidha, naliomba Bunge lako Tukufu likubali kupitisha Mpango wa Utekelezaji na Makadirio ya Fedha kwa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha wa 2019/20. 2. Mheshimiwa Spika, Awali ya yote, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupatia uwezo wa kutekeleza majukumu ya kuwahudumia wananchi. Pia namshukuru Mheshimiwa Rais, kwa kuendelea kuniamini katika nafasi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora; Ninamuahidi kuwa nitatekeleza wajibu wangu kwa ufanisi na uadilifu wa hali ya juu. Aidha, nawashukuru wapiga kura wa Jimbo la Newala Mjini kwa ujumla kwa kuendelea kunipa ushirikiano wakati wote ninapoe ndelea kuwawakilisha. -
MKUTANO WA 18 TAREHE 5 FEBRUARI, 2015 MREMA 1.Pmd
5 FEBRUARI, 2015 BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE __________________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Tisa – Tarehe 5 Februari, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, leo sijamwona. Kwa hiyo tunaendelea na Maswali kwa Waziri Mkuu na atakayeanza ni Mheshimiwa Murtaza A. Mangungu. MHE. MURTAZA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa vipindi tofauti vya Bunge Mheshimiwa Peter Msigwa, Mheshimiwa Mussa Zungu na hata Mheshimiwa Murtaza A. Mangungu wamekuwa wakiuliza swali kuhusiana na manyanyaso wanayoyapata wafanyabiashara Wadogo Wadogo pamoja na Mamalishe. Kwa kipindi hicho chote umekuwa ukitoa maagizo na maelekezo, inavyoonekana mamlaka zinazosimamia hili jambo haziko tayari kutii amri yako. 1 5 FEBRUARI, 2015 Je, unawaambia nini Watanzania na Bunge hili kwa ujumla? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba nimjibu Mheshimiwa Murtaza Mangungu swali lake kama ifuatavyo:- Suala hili la vijana wetu ambao tunawajua kama Wamachinga, kwanza nataka nikiri kwamba ni suala kubwa na ni tatizo kubwa na si la Jiji la Dar es Salaam tu, bali lipo karibu katika miji mingi. Kwa hiyo, ni jambo ambalo lazima twende nalo kwa kiwango ambacho tutakuwa na uhakika kwamba tunalipatia ufumbuzi wa kudumu. Kwa hiyo, ni kweli kwamba mara kadhaa kuna maelekezo yametolewa yakatekelezwa sehemu na sehemu nyingine hayakutekelezwa kikamilifu kulingana na mazingira ya jambo lenyewe lilivyo. Lakini dhamira ya kutaka kumaliza tatizo hili la Wamachinga bado ipo palepale na kwa bahati nzuri umeuliza wakati mzuri kwa sababu jana tu nimepata taarifa ambayo nimeandikiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI ambayo wanaleta mapendekezo kwangu juu ya utaratibu ambao wanafikiri unaweza ukatatua tatizo hili ambalo lipo sehemu nyingi. -
Tarehe 12 Aprili, 2019
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Tisa – Tarehe 12 Aprili, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. NEEMA MSANGI - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Swali letu la kwanza asubuhi ya leo linaelekezwa kwa Ofisi ya Rais – TAMISEMI na linaulizwa na Mheshimiwa Shaabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Lushoto. Na. 68 Kukarabati Shule za Msingi na Sekondari - Lushoto MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Serikali imekuwa na utaratibu wa kukarabati shule zake za msingi na sekondari nchini:- Je, ni lini Serikali itazifanyia ukarabati Shule za Msingi Kwemashai, Bandi, Milungui, Kilole na Shule za Sekondari za Ntambwe, Ngulwi - Mazashai na Mdando? 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MWENYEKITI: Ahsante. Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Waitara. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shaabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Lushoto, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha mwaka 2018/2019, Serikali kupitia Program ya Lipa Kulingana na Matokeo (EPforR) imepeleka jumla ya shilingi milioni 467 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mawili, matundu sita ya vyoo na madarasa mawili katika Shule ya Msingi Shukilai (Shule ya Elimu Maalum) na ujenzi wa mabweni mawili Shule ya Sekondari Magamba, ujenzi wa bweni moja na madarasa mawili Shule ya Sekondari Umba. Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile katika mwaka wa Fedha 2018/2019, Serikali imetoa shilingi bilioni 29.9 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma 2,392 ya madarasa nchi nzima ambapo kati ya fedha hizo Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto imepewa kiasi cha Sh.512,500,000 kwa ajili ya kukamilisha maboma 46 ya madarasa shule za sekondari. -
MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao Cha Nane
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _______ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Nane – Tarehe 14 Aprili, 2020 (Bunge Lilianza Saa Nane Mchana) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Wabunge, tukae, Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU (Maswali yafuatayo yameulizwa na kujibiwa kwa njia ya mtandao) Na. 64 Kampuni Zinazofanya Kazi Ndani ya Mgodi wa Geita MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:- Kampuni ambazo zinafanya kazi ndani ya Mgodi wa Geita Gold Mine(contractors) zimekuwa zikilalamikiwa na wananchi wanaofanya kazi kwa kutopeleka fedha kwenye Mifuko ya Jamii na kutowapa mikataba:- Je, Serikali inachukua hatua gani kukomesha malalamiko hayo? WAZIRI MKUU alijibu:- 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Naibu Spika, Mgodi wa Geita Gold Mine (GGM) ni moja ya waajiri walioandikishwa na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) na watumishi wanaofanya kazi katika mgodi huo wamegawanyika katika makundi mawili ambayo ni wale walioajiriwa moja kwa moja na GGM na wale walioajiriwa na wakandarasi wanaotoa huduma ndani ya mgodi huo. Mheshimiwa Naibu Spika, mwezi Februari 2020, jumla ya shilingi bilioni 5.01 zililipwa na Mgodi wa GGM kama mchango wa mwezi Januari, 2020 kwa watumishi 2,038 walioajiriwa moja kwa moja na GGM na kuandikishwa na NSSF. Katika mwezi huo huo, jumla ya wanachama 6,128 ambao wameajiriwa na wakandarasi 39 wanaotoa huduma ndani ya mgodi huo walikuwa wameandikishwa na NSSF na kuchangiwa wastani wa shilingi bilioni 1.3 Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia OWM-KVAU imekuwa ikifanya kaguzi katika maeneo mbalimbali ya kazi ikiwemo ya migodini kwa lengo la kuimarisha utekelezaji wa Sheria za Kazi. -
Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1 MAJADILIANO YA BUNGE
Nakala ya Mtandao (Online Document) MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA ISHIRINI __________ Kikao cha Ishirini na Moja - Tarehe 5 Juni, 2015 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, napenda kuchukua nafasi hii kuwapa pole wote kwa msiba uliotupata, msiba ulitokea wakati nikiwa Geneva ambapo tulikuwa na kikao cha Kamati Ndogo ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Maspika wote duniani utakaofanyika mwezi wa Nane, sasa kuna Maspika kumi ndiyo tupo kwenye maandalizi ya mkutano huo na kilikuwa ni kikao chetu cha mwisho kabla ya mkutano huo. Kwa hiyo, wakati msiba unatokea nilikuwa huko, nilipewa taarifa na nilisikitika sana. Kwa hiyo, tutatangaza baadaye mchana, ni akina nani watakaokwenda kuzika kesho. Katibu! HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI (MHE. CHARLES M. KITWANGA): Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. NAIBU WAZIRI WA MAJI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Maji kwa mwaka wa Fedha, 2015/2016. MHE. DAVID H. MWAKYUSA (k.n.y. MHE. PROF. PETER M. MSOLLA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015, pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa Fedha 2015/2016. MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED (k.n.y. MHE. MAGDALENA H. SAKAYA - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KWA WIZARA YA MAJI): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Fedha kwa Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. -
Tarehe 3 Agosti, 2012
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _____________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Arobaini – Tarehe 3 Agosti, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Naibu Spika, (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa Mwaka wa Fedha, 2012/2013. NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha, 2012/2013. MHE. MUSSA HASSAN MUSSA (K.n.y. MHE. EDWARD N. LOWASSA - MWENYEKITI WA KAMATI YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka 2011/2012 pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha, 2012/2013. MHE. RAYA IBRAHIM KHAMIS (K.n.y. MHE. EZEKIA D. WENJE - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KWA WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA YA MASHARIKI): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani juu ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha, 2012/2013. MASWALI NA MAJIBU Na. 315 Malipo ya Malimbikizo ya Wafanyakazi – Geita MHE. DONALD K. MAX aliuliza:- Wafanyakazi wa Wilayani wananyanyaswa sana na hawalipwi malimbikizo yao na wakati mwingine fedha zao zinapoletwa wanalipwa kidogo kidogo:- Je, ni lini wafanyakazi Wilayani Geita watalipwa mafao yao? Kwani malimbikizo hadi sasa yanafikia Sh. -
Tarehe 15 Aprili, 2019
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Kumi – Tarehe 15 Aprili, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA):- Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NAIBU SPIKA: Ahsante, Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali, tutaanza na Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mheshimiwa Kiza Hussein Mayeye, Mbunge wa Viti Maalum, sasa aulize swali lake. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Na. 78 Malipo Stahiki Kwa Walimu Waliopanda Daraja MHE. KIZA H. MAYEYE aliuliza:- Serikali imekuwa ikiwapandisha madaraja walimu lakini haitoi malipo stahiki kwa madaraja hayo mapya kwa kipindi kirefu tangu walipopandishwa madaraja yao:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba walimu wanapata stahiki zao mara wanapopandishwa madaraja? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kiza Hussein Mayeye, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilisitisha kupandisha walimu na watumishi wengine madaraja katika mwaka wa fedha 2015/2016 na 2016/2017 kutokana na uhakiki wa watumishi uliohusisha uhalali wa vyeti, elimu na ngazi za mishahara. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini – Tarehe 4 Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA KAZI NA AJIRA: Randama ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kazi na Ajira kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kwa mujibu wa Kanuni ya 38, Waziri Mkuu anaweza kuulizwa maswali na Mbunge yeyote ambaye atazingatia masharti kuhusu maswali ya Bunge pamoja na mwongozo uliowekwa na Nyongeza ya 6 ya Kanuni hii. Maswali atakayoulizwa Waziri Mkuu, hayatakuwa na taarifa ya awali kama maswali yenyewe. Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu kitakuwa ni Siku ya Alhamisi kwa dakika 30, lakini chini ya kifungu kidogo cha (4) kinasema, Waziri Mkuu anaweza kutumia kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu, kutoa taarifa au ufafanuzi kuhusu suala lolote linalohusiana na shughuli za Serikali na lenye maslahi kwa umma, kwa muda usiozidi dakika kumi ikifuatiwa na maswali kwa Wabunge kwa dakika 20 kuhusu taarifa yoyote na maswali mengine ya Serikali. Kwa hiyo, ninamuita Waziri Mkuu. WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, ninaomba nikushukuru sana kwa kunipa fursa hii ili niweze kutoa taarifa fupi kwa mujibu wa Kanuni uliyoieleza sasa hivi. Taarifa hiyo ni matokeo ya mjadala wa Bajeti ya Uchukuzi, ambayo ilikuwa na mambo mengi. Nimeona nitumie fursa hii niweze kutoa ufafanuzi wa mambo yafuatayo:- Awali ya yote, ninapenda kutumia fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Peter Serukamba, Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu na Mheshimiwa Mhonga Said Ruhwanya, Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kwa Wizara ya Uchukuzi na Waheshimiwa Wabunge wote, waliochangia kwa maandishi na kwa kuzungumza kwenye majadiliano ya Wizara hii ya Uchukuzi yanayoendelea hapa Bungeni. -
Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania Mkutano Wa Saba Yatokanayo Na Kikao Cha Ishirini Na Sita 16 Mei, 2017
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA ISHIRINI NA SITA 16 MEI, 2017 MKUTANO WA SABA KIKAO CHA ISHIRINI NA SITA TAREHE 16 MEI, 2017 I. DUA: Saa 3:00 asubuhi Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mwenyekiti) alisoma Dua na kuongoza Bunge. Makatibu mezani: 1. Ndugu Theonest Ruhilabake 2. Ndugu Asia Minja 3. Ndugu Joshua Chamwela II. HATI ZA KUWASILISHA MEZANI (i) Mhe. Charles John Mwijage aliwasilisha Mezani Randama ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (ii) Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi aliwasilisha Mezani Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (iii) Mhe. Jumanne Kidera Kishimba aliwasilisha Mezani Taarifa ya Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (iv) Mhe. Masoud Abdallah Salim aliwasilisha Mezani Taarifa ya Kambi ya Upinzani kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. 1 III. MASWALI OFISI YA RAIS (TAMISEMI) Swali Na. 209: Mhe. Dkt. Pudenciana Kikwembe Nyongeza: Mhe. Dkt. Pudenciana Kikwembe Mhe. Pauline Gekul Mhe. David Cosato Chumi Swali Na. 210: Mhe. Eng. Atashasta Justus Nditiye Nyongeza: Mhe. Eng. Atashasta Justus Nditiye Mhe. Josephine Johnson Genzabuke Mhe. Almas Athuman Maige Mhe. Cecilia Daniel Paresso Mhe. Savelina Silvanus Mwijage WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO Swali Na. 211: Mhe. Daniel Edward Mtuka Nyongeza: Mhe. Daniel Edward Mtuka Mhe. Daimu Iddy Mpakate Swali Na. 212: Mhe. Mussa Bakari Mbarouk Nyongeza: Mhe. Mussa Bakari Mbarouk Mhe. Saumu Heri Sakala Mhe. Moshi Selemani Kakoso Swali Na. -
MKUTANO WA KWANZA Kikao Cha Tatu – Tarehe 12 Novemba, 2020
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KWANZA Kikao cha Tatu – Tarehe 12 Novemba, 2020 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaweza kukaa. Waheshimiwa Wabunge, karibuni sana. Natumaini kupitia tablets zenu kila mmoja ameshaiona Order Paper ya leo yaani Orodha ya Shughuli za leo ambazo ni muhimu sana. Tutaanza na Kiapo cha Uaminifu kwa Waheshimiwa Wabunge ambao bado hawajaapa. Tuna Wabunge wanne wa ACT-Wazalendo na Mbunge mmoja wa Chama cha Mapinduzi. (Makofi) Bado sina hakika kama Wabunge wa ACT wapo, lakini sisi tutawataja kama utaratibu ulivyo hapa. Kama watakuwepo, basi tutawaapisha. (Makofi) Waheshimiwa Wabunge, ajenda itakayofuata ni uthibitisho ambao mtapaswa kuufanya kwa uteuzi wa Waziri Mkuu. Kwa hiyo, nawaomba Wabunge ambao wako nje au canteen na wapi, basi waingie ndani na ninyi mlioko ndani msitoke kwa sababu jambo hili ni kubwa na mkononi sina hilo jina hivi sasa, sina kabisa. Wakati ukifika basi Mpambe wa Mheshimiwa Rais tutamruhusu aingie hapa ndani na bahasha husika na nitakabidhiwa hapa mbele yenu. (Makofi) 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Candidates ni ninyi wote, kwa hiyo, kila mtu akae sawa, isipokuwa mimi na AG. Maana yake mliobaki wote ni ma-candidate. Sasa usije ukatuangukia hapa, aah! Halafu itakuwa taabu. Tunawatakia kila la heri wote muweze kuteuliwa. (Kicheko/Makofi) Baada ya hapo tutakuwa na Uchaguzi wa Mheshimiwa Naibu Spika na pia tutakuwa na Kiapo cha Mheshimiwa Naibu Spika. Baada ya hapo tutaelezana mambo mengine yanayoendana na hayo. Basi, tuanze haya mambo. Katibu. NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: KIAPO CHA UAMINIFU KWA WABUNGE (Kiapo Kinaendelea) 355.