Tarehe 9 Mei, 2019

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

Tarehe 9 Mei, 2019 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 9 Mei, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu. NDG. JOSHUA CHAMWELA – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa mwaka wa fedha 2019/2020. MHE. ASHA MSHIMBA JECHA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa mwaka wa fedha 2018/ 2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. QAMBALO W. QULWI – NAIBU MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Kuhusu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NAIBU SPIKA: Ahsante. Waheshimiwa tunaendelea. Katibu. NDG. JOSHUA CHAMWELA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Maswali, tutaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi sasa aulize swali lake. Na. 196 Serikali Kuzipatia Waganga Zahanati za Jimbo la Manyoni Magharibi MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Wananchi wa Manyoni Magharibi kwa kushirikiana na Serikali kupitia miradi mbalimbali ikiwemo TASAF wamejenga zahanati katika Vijiji vya Gurungu, Sanjaranda, Kitopeni, Ipande, Doroto, Itagata, Kalangali, Makale, Mwamagembe na Kintanula, lakini mpaka sasa zahanati hizi hazina Waganga:- Je, ni lini Serikali itazipatia zahanati hizo Waganga, ili wananchi wapate huduma kufuatana na sera yake? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. 2 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA)alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika kwa Mwaka wa Fedha 2017/ 2018 na 2018/2019 Serikali imeajiri watumishi 8,444 wa afya katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa ambapo watumishi 46 walipangwa kwenye vituo vya afya na zahanati katika Jimbo la Manyoni Magharibi. Zahanati za Gurungu, Sanjaranda, Kitopeni, Ipanda, Doroto, Itagata, Kalangali, Makale, Mwamagembe na Kitanula zimepatiwa Waganga na wataalam mbalimbali wa afya ambao wanatoa huduma hadi hivi sasa. Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya vituo vya afya vya kutolea huduma za afya sambamba na kuajiri wataalam wa afya kwa awamu kwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Ahsante. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Yahaya Massare, swali la nyongeza. MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali na tumeona kweli Serikali sasa imeonesha nia ya kupunguza kadhia hii ya watumishi wa kada ya afya. Nina maswali madogo mawili ya nyongeza:- Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, dhamira ya Serikali, lakini na wananchi katika Jimbo la Manyoni Magharibi, Halmashauri ya Itigi ni kujikwamua, wameanza kutumia nguvu zao katika kujenga zahanati na vituo vya afya katika vijiji vyao, lakini nguvu zao zinaonekana kuisha. Je, Serikali iko tayari sasa kuwasaidia wananchi wa vijiji ambao wameanza kujenga zahanati kwa nguvu zao? 3 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika swali ambalo niliuliza mwaka jana kipindi kama hiki majibu ya Serikali ilikuwa yameonesha kwamba na Hansard iko hapa ninayo kwamba, Serikali ilikuwa imetenga milioni 600 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, lakini hadi tunapozungumza leo hii bajeti nyingine ya Wizara ya TAMISEMI ilishasomwa, hospitali hii bado hatujaletewa pesa. Je, Serikali iko tayari sasa basi kupeleka hizi pesa ambazo iliahidi na wananchi walisikia kwamba zitapelekwa katika Halmashauri ya Itigi kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na nimpe pole sana kwamba, alipata ajali mbaya hivi karibuni, lakini pamoja na kwamba, alikuwa na machungu ya maumivu aliweza kuwakumbuka wananchi wake wa Manyoni na akaanza kuandika swali hili ambalo nalijibu hapa leo. Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba nijibu maswali ya nyongeza mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba, sisi Serikali tunahimiza wananchi na wenyewe Waheshimiwa Wabunge wamekuwa mstari wa mbele kuwahamasisha wananchi kushiriki kujenga vituo vya afya na zahanati na kuna maboma mengi. Naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba, jitihada na nia ya Serikali iko palepale, kadri ambavyo uwezo utapatikana tutapeleka fedha za maboma, lakini pia kupeleka wataalam na vifaa tiba ili kuweza kuboresha huduma za wananchi wetu katika maeneo yao na hii itakuwa ni kwa nchi nzima. 4 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, anauliza habari za hospitali yake ya Itigi; naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba, tutaendelea kuliangalia hili kulingana na uwezo wa Serikali. Kama mwaka huu bajeti hii haikupelekwa katika eneo lake la Hospitali ya Itigi kama alivyotaja Mheshimiwa Mbunge, basi tunalichukua kulifanyia kazi ili wakati ujao aweze kupata fedha na kuweza kupata huduma na kuboresha hospitali yake ya wilaya. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Shukuru Kawambwa swali la nyongeza. MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Nitangulize kutoa shukrani za wananchi wa Bagamoyo kwa juhudi kubwa ya Serikali katika kuboresha huduma ya afya. Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Bagamoyo kwa muda mrefu sana wamehangaika na ujenzi wa zahanati katika Vijiji viwili, kimoja cha Buma Kata ya Kilomo, kingine Kitame katika Kata ya Makurunge. Hivi sasa zahanati ya Makurunge imekamilika na Buma wakati wowote tutamaliza, tunamalizia ujenzi wa choo. Swali langu kwa Mheshimiwa Waziri, je, ni lini tutaweza kupatiwa watumishi na vifaa tiba katika zahanati hizi kwa kuzingatia kwamba, kwa muda mrefu wananchi hawa hawajapata huduma? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nijibu swali la Mheshimiwa Dkt. Shukuru Kawambwa, Mbunge wa Bagamoyo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, tumeshaomba kibali maalum kwenye Ofisi, Wizara ya Utumishi cha kuajiri Madaktari, Waganga na Wauguzi. Naomba nimwahidi 5 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Mbunge kwamba, maeneo yote ambayo zahanati zimekamilika na vituo vya afya ambavyo vinajengwa nchi nzima na hospitali za wilaya na pale palipo na upungufu mkubwa tutazingatia maeneo hayo ikiwepo na eneo lake la Bagamoyo na zahanati mbili ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Venance Mwamoto, swali la nyongeza. MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa, Wilaya ya Kilolo inapitiwa na barabara kuu (High Way) kutoka Tanzania kwenda Zambia, lakini pia ni barabara ambayo ukitoka Mikumi ni mpakani na Ruaha Mbuyuni mpaka ukifika Ilula ni kilometa zaidi ya 200, lakini hapo hakuna kituo cha afya. Mara nyingi accidents zimekuwa zikitokea, wananchi wa Mbeya, Malawi, Zambia, wamekuwa wakipata matatizo na wamepoteza maisha kwa sababu, inabidi waende wakatibiwe Iringa Mjini ambako ni mbali; na kwa kuwa, wananchi sasa wa Ruaha Mbuyuni wameonesha nia ya kujenga Kituo cha Afya, je, Serikali itakuwa tayari kuwasaidia kwa haraka ili kuokoa maisha ya watu ambao wamekuwa wakiyapoteza pale? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge Venance Mwamoto, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwa swali mojawapo la nyongeza hapa, hivi leo asubuhi kwamba, ni nia ya Serikali kuendelea kuboresha huduma za afya na 6 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja yatazingatiwa katika kuboresha. Kama wananchi wamechukua juhudi za kuanza ujenzi tunawapongeza sana, sisi kama Serikali tuko pamoja nao na mimi hivi karibuni nitaenda kutembelea Jimbo la Mheshimiwa Mwamoto. Hivyo nitaomba tutembelee eneo hili tuone juhudi za wananchi ili tuweze kutia nguvu katika eneo hilo. Ahsante sana. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Paschal Haonga, swali la nyongeza. MHE. PASCHAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Mji Mdogo wa Mlowo ulioko Wilaya ya Mbozi una wakazi wapatao elfu 70 na zaidi, lakini bahati mbaya sana mji huu una zahanati tu ambayo inahudumia watu hao zaidi ya 70,000. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kujenga kituo cha afya ili kuweza kuwahudumia wale wananchi ambao ni wengi na wanapata tabu sana na wanasumbuka wakati wa kupata matibabu? NAIBU SPIKA:
Recommended publications
  • 1458137638-Hs-4-4-20
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE KIKAO CHA NNE – TAREHE 14 JUNI, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 37 Ardhi Iliyotolewa Kujenga Shule ya Msingi Kiraracha MHE. AUGUSTINO L. MREMA aliuliza:- Mzee Pauli Sananga Lekule wa Kijiji cha Kiraracha, Kata ya Marangu, Wilaya ya Moshi Vijijini, alitoa ardhi yake ikatumika kujenga shule ya msingi Kiraracha, Marangu miaka 10 iliyopita akiahidiwa na Serikali kupewa eneo jingine kama fidia lakini mpaka sasa hajapewa eneo jingine kama fidia jambo lililomfanya aione Serikali haikumtendea haki. Je, ni lini Serikali itamlipa haki yake kutokana na makubaliano hayo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Lyatonga Mrema, Mbunge wa Vunjo kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa Ndugu Pauli Sananga Lekule wa Kijiji cha Kiraracha, Kata ya Marangu Magharibi, alitoa ardhi yake kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi Kiraracha, Kata ya Marangu Magharibi kwa ahadi ya kufidiwa eneo lililoko Njia panda. Aidha eneo ambalo Halmashauri ya Wilaya ya Moshi ilitarajia kumfudia Ndugu Lekule lipo katika mgogoro na kesi bado inaendelea Mahakama Kuu. 1 Mheshimiwa Spika, kwa kuwa eneo lililopimwa viwanja na kutarajia mlalamikaji lipo katika mgogoro wa kisheria kati ya Halmashauri na wananchi, Serikali inaendelea kufuatilia mwenendo wa kesi na mara shauri litakapomalizika Mahakamani mhusika atapewa eneo lake. Mheshimiwa Spika, katika jitihada za Serikali kuhakikisha shauri hili haliendelei kuchukua muda mrefu, Halmashauri ya Wilaya ya Moshi imeunda timu kwa ajili ya kufuatilia na kuharakisha shauri hili ili ikiwezekana limalizike nje ya Mahakama ili Ndugu Lekule Sananga aweze kupata haki yake mapema.
    [Show full text]
  • Issued by the Britain-Tanzania Society No 105 May - Aug 2013
    Tanzanian Affairs Text 1 Issued by the Britain-Tanzania Society No 105 May - Aug 2013 Even More Gas Discovered Exam Results Bombshell Rising Religious Tensions The Maasai & the Foreign Hunters Volunteering Changed my Life EVEN MORE GAS DISCOVERED Roger Nellist, the latest volunteer to join our panel of contributors reports as follows on an announcement by Statoil of their third big gas discovery offshore Tanzania: On 18 March 2013 Statoil and its co-venturer ExxonMobil gave details of their third high-impact gas discovery in licence Block 2 in a year. The new discovery (known as Tangawizi-1) is located 10 kilometres from their first two discoveries (Lavani and Zafarani) made in 2012, and is located in water depth of 2,300 metres. The consortium will drill further wells later this year. The Tangawizi-1 discovery brings the estimated total volume of natural gas in-place in Block 2 to between 15 and 17 trillion cubic feet (Tcf). Depending on reservoir characteristics and field development plans, this could result in recoverable gas volumes in the range of 10-13 Tcf from just this one Block. These are large reserves by international stand- ards. By comparison, Tanzania’s first gas field at Songo Songo island has volumes of about 1 Tcf. Statoil has been in Tanzania since 2007 and has an office in Dar es Salaam. It operates the licence on Block 2 on behalf of the Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) and has a 65% working interest, with ExxonMobil Exploration and Production Tanzania Limited holding the remaining 35%. It is understood that under the Production Sharing Agreement that governs the operations, TPDC has the right to a 10% working participation interest in case of a development phase.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Nane – Tarehe 11 Juni, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Tukae Waheshimiwa. Tunaendelea na Mkutano wetu wa Kumi na Moja, Kikao cha Arobaini na Nane, Katibu. NDG. ATHUMAN HUSEIN – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Maswali, leo tutaanza na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, swali linaulizwa na Mheshimiwa Martha Umbulla. Mheshimiwa Martha, tafadhali. Na. 405 Taasisi Zinazotoa Mikopo kwa Wanawake na Vijana MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:- Changamoto ya fedha za mikopo inayotolewa na Halmashauri za Wilaya kwa makundi ya wanawake na vijana 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) nchini ni urejeshaji hafifu pamoja na kutorejeshwa kwa fedha hizo kabisa; kuna taasisi za fedha hapa nchini zinatoa mikopo kwa makundi tajwa hapo juu kwa ufanisi mkubwa na kwa uzoefu wa muda mrefu:- Je, kwa nini Serikali isipitishe utoaji wa mikopo hiyo kwenye taasisi hizo zenye ufanisi wa muda mrefu na watalaam wa kutosha kama WEDAC ili kuepusha upotevu wa fedha za Serikali na mikopo kuwafikia walengwa? SPIKA: Majibu ya swali hilo, Mheshimiwa Naibu Waziri, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mheshimiwa Kandege. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Martha Jachi Umbulla, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali ilianzisha Mfuko wa Wanawake na Vijana baada ya kubaini kuwa wanawake na vijana wanashindwa kupata mikopo kutoka taasisi zingine za fedha ambazo zina masharti magumu.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka.
    [Show full text]
  • Years of Communications in Tanzania —
    YEARS OF COMMUNICATIONS S IN TANZANIA — - - • S ____ mfl Rusumo UIIIt. I N a tn any — a E3u ?ratnu o orna Ka any •Mwa U- Shinya N 0 Nzeya 0 Man 1) LU 'NORTHERN RINnga Id., K,9 Uvinlabora o TA N ZA A Panaan c! fflLako WESTERN RINGDma T:anrka\ • I) 1' 'I LiA1ES-SALAA5 Irna • 0' • Snbawanga Makainba J lThf7C .Meya KiwaMasoko•ocEAI Tunduma KasurnIo SOUTHERN RING Lake Lind _Nyasa Tunduru Mtwara Tanzania National lOT Broadband Backbone Or'40A, ^;rAT l PL MWEINGEIZII W1\ KUWASILISHA MALALAMIKEI Wasilisha Malalamiko kwa Mtoa Huduma (Kampuni ya simu, Posta,Wasafirisha vifurushi,Televisheni, Redio, n.k) Endapo hujaridhika Wasilisha Malalamiko kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Endapo hakuna suluhu katika hatua yo pill Kata Rufaa katika Kamatiya Malalamiko ya Mamlaka ya Mawasuliano Tanzania -- Endapo hujaridhika no maamuziya Kamati yo Malalamiko Kata Rufaa katika Baraza Pa Uamuzi wa Haki (Fair Competition Tribunal) Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi: Mawasiliano Towers, Kiwanja Na. 2005/5/1, Kitalu C, Barabara ya Sam Nujoma, S.L.P 474, Dar es Salaam Simu: +255 784 558270/71, +255222412011/12, +25522 2199706-9 Nukushi: +255 22 2412009/2412010 Piga: 080 000 8888 bure Tuma ujumbe 15454 - Barua pepe: dg(a tcra.go.tz . malalamiko(atcra.go.tz, [email protected] Tovuti: www.tcra.go.tz Na ofisi zetu za Kanda: Arusha, Mwanza, Zanzibar, Dodoma, Mbeya na Dar es Salaam The Regulator is published quarterly by the Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA), an independent goverment agency established under the Tanzania Communications Regulatory Authori- ty Act No. 12 of 2003 to regulate telecommunications, broadcasting and postal sectors in Tanzania.
    [Show full text]
  • Mchanganuo Wa Wabunge Katika Kamati Za
    KIAMBATISHO JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MCHANGANUO WA WABUNGE KATIKA KAMATI MPYA ZA BUNGE LA KUMI NA MOJA (11) ___________________ 21 JANUARI, 2016 ii YALIYOMO I. VIGEZO VILIVYOTUMIKA ............................................................................................................ 2 II. IDADI YA WAJUMBE WA KILA KAMATI KWA MCHANGANUO WA VYAMA .............................. 3 III. KAMATI YA UONGOZI ............................................................................................................... 4 IV. KAMATI YA KANUNI ZA BUNGE ................................................................................................ 5 V. KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE ........................................................... 7 VI. KAMATI YA MASUALA YA UKIMWI ........................................................................................... 9 VII. KAMATI YA BAJETI .................................................................................................................. 11 VIII. KAMATI YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA ................................................................ 13 IX. KAMATI YA KATIBA NA SHERIA ............................................................................................... 15 X. KAMATI YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA ....................................................................... 17 XI. KAMATI YA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII ................................................................... 19 XII. KAMATI YA ARDHI, MALIASILI
    [Show full text]
  • 20 MAY 2019.Pmd
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Moja – Tarehe 20 Mei, 2019 (Bunge Lilianza saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na Mkutano wetu wa 15, leo kikao cha 31. Katibu! NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nasikitika kuwatangazia kifo cha mwanasiasa mkongwe na kiongozi aliyepata kuhudumia kwa muda mrefu hasa kule kwenye Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Marehemu Ally Juma Shamhuna. Waheshimiwa Wabunge, katika uhai wake, marehemu Ally Juma Shamhuma amepata kushika nyadhifa mbalimbali zikiwemo hizi zifuatazo; amepata kuwa Mkurugenzi wa Mifugo, amewahi kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, amewahi kuwa Katibu Mkuu, Export Processing Zone Zanzibar, amewahi kuwa Waziri wa Mipango, amekuwa Waziri wa Nchi, Afisi ya Waziri Kiongozi, aliwahi kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo na wakati huo huo akiwa ni 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Naibu Waziri Kiongozi, katika uhai wake amekuwa Waziri wa Ardhi, Maji na Nishati na alipata kuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali. Aidha, Marehemu Mheshimiwa Shamhuna kwa muda mrefu alikuwa ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi kutokea Zanzibar na baadhi yenu humu Wabunge mtamkumbuka marehemu Mheshimiwa Shamhuna kama Mbunge wa Bunge la Katiba na alikuwa Mjumbe wa Kamati namba 8 kwenye Bunge la Katiba, Kamati ambayo nilikuwa Mwenyekiti wake. Kwa niaba yenu Waheshimiwa Wabunge, tunatoa pole kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Tunatoa pole kwa Wazanzibari wote na Watanzania wote kwa ujumla kufuatia kifo hicho na tunamuomba Mwenyezi Mungu aihifadhi roho yake mahali pema peponi, amina.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA 18 TAREHE 5 FEBRUARI, 2015 MREMA 1.Pmd
    5 FEBRUARI, 2015 BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE __________________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Tisa – Tarehe 5 Februari, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, leo sijamwona. Kwa hiyo tunaendelea na Maswali kwa Waziri Mkuu na atakayeanza ni Mheshimiwa Murtaza A. Mangungu. MHE. MURTAZA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa vipindi tofauti vya Bunge Mheshimiwa Peter Msigwa, Mheshimiwa Mussa Zungu na hata Mheshimiwa Murtaza A. Mangungu wamekuwa wakiuliza swali kuhusiana na manyanyaso wanayoyapata wafanyabiashara Wadogo Wadogo pamoja na Mamalishe. Kwa kipindi hicho chote umekuwa ukitoa maagizo na maelekezo, inavyoonekana mamlaka zinazosimamia hili jambo haziko tayari kutii amri yako. 1 5 FEBRUARI, 2015 Je, unawaambia nini Watanzania na Bunge hili kwa ujumla? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba nimjibu Mheshimiwa Murtaza Mangungu swali lake kama ifuatavyo:- Suala hili la vijana wetu ambao tunawajua kama Wamachinga, kwanza nataka nikiri kwamba ni suala kubwa na ni tatizo kubwa na si la Jiji la Dar es Salaam tu, bali lipo karibu katika miji mingi. Kwa hiyo, ni jambo ambalo lazima twende nalo kwa kiwango ambacho tutakuwa na uhakika kwamba tunalipatia ufumbuzi wa kudumu. Kwa hiyo, ni kweli kwamba mara kadhaa kuna maelekezo yametolewa yakatekelezwa sehemu na sehemu nyingine hayakutekelezwa kikamilifu kulingana na mazingira ya jambo lenyewe lilivyo. Lakini dhamira ya kutaka kumaliza tatizo hili la Wamachinga bado ipo palepale na kwa bahati nzuri umeuliza wakati mzuri kwa sababu jana tu nimepata taarifa ambayo nimeandikiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI ambayo wanaleta mapendekezo kwangu juu ya utaratibu ambao wanafikiri unaweza ukatatua tatizo hili ambalo lipo sehemu nyingi.
    [Show full text]
  • MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao Cha Arobaini Na Moja
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Moja – Tarehe 31 Mei, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Tunaanza kikao chetu cha Arobaini na Moja, Katibu. NDG. LINA KITOSI – KATIBU MEZANI:- HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2018/19. MHE. CATHERINE V. MAGIGE (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu utekelezaji wa Bajeti na Majukumu ya Wizara 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019. MWENYEKITI: Ahsante. Katibu. NDG. LINA KITOSI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Swali letu la kwanza linaelekezwa Ofisi ya Waziri Mkuu na linaulizwa na Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, kwa niaba yake Mheshimiwa Amina Mollel. Na. 341 Utekelezaji wa Mpango wa Ukimwi 90-90-90 MHE. AMINA S. MOLLEL (K.n.y MHE. HAWA M. CHAKOMA) aliuliza:- Je, Serikali inatekelezaje Mpango wa UKIMWI wa 90- 90-90? MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Mollel. Majibu, Mheshimiwa Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA NA VIJANA) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa
    [Show full text]
  • MKUTANO WA KUMI NA SABA Kikao Cha
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA SABA Kikao cha Kwanza – Tarehe 5 Novemba, 2019 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) WIMBO WA TAIFA D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge naomba tukae sasa. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge katika Mkutano wa Kumi na Sita wa Bunge, Bunge lilipitisha Miswada minne ya Sheria ya Serikali ifuatayo:- Kwanza, Muswada wa Sheria ya Serikali Mtandao ya Mwaka 2019 (The e- Government Bill, 2019). Pili, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali Na. 4 wa Mwaka 2019 (The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 4, Bill, 2019). Tatu, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 5 wa Mwaka 2019, (The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 5, Bill, 2019. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Nne, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali Na. 6 wa Mwaka 2019, ((The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 6, Bill, 2019. Kwa Taarifa hii, napenda kuliarifu Bunge kwamba tayari Miswada hiyo minne imepata kibali cha Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwa sheria za nchi, sasa zimekuwa sheria za nchi zinazoitwa kama ifuatavyo;- (Makofi) Sheria ya kwanza, ni Sheria ya Serikali Mtandao Na. 10 ya Mwaka 2019 (The e- Government Act No. 10 of 2019. Ya pili, ni sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali Na. 4, Sheria Na. 11 ya Mwaka 2019 ((The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 4, Act No.11 of 2019; na Tatu, Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na.
    [Show full text]
  • Tarehe 28 Juni, 2017
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Hamsini na Tano – Tarehe 28 Juni, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu. NDG. THEONEST RUHILABAKE – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- MHE. GEORGE M. LUBELEJE (K.n.y. MHE. KAPT. MST. GEORGE H. MKUCHIKA - MWENYEKITI WA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE): Taarifa ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shauri la Kudharau Mamlaka ya Spika linalomhusu Mheshimiwa Joshua Samwel Nassari, Mbunge na Shauri la Kusema Uwongo Bungeni linalomhusu Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza, Mbunge. NAIBU SPIKA: Ahsante sana. Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. THEONEST RUHILABAKE – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali tutaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu. Mheshimiwa Mgeni Jadi Kadika, Mbunge wa Viti Maalum, kwa niaba yake Mheshimiwa Mheshimiwa Mwanne Mchemba. Na. 452 Mradi wa MIVARF MHE. MWANNE I. MCHEMBA (K.n.y. MHE. MGENI JADI KADIKA) aliuliza:- Mradi wa MIVARF ni wa Muungano na Makao Makuu yapo Arusha ambapo kazi yake kuu ni kujenga masoko, miundombinu ya barabara, kuongeza thamani na kupeleka maendeleo vijijini:- Je, ni kwa kiasi gani mradi huu umechangia kuleta maendelezo Zanzibar? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANA NA AJIRA) alijibu: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mgeni Jadi Kadika, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, MIVARF ni programu inayohusika na miundombinu ya masoko, uongezaji thamani ya mazao na huduma za kifedha vijijini.
    [Show full text]
  • Tarehe 6 Aprili, 2018
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Nne - Tarehe 6 Aprili, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe.Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Tukae, Katibu. NDG.YONA KIRUMBI - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Maswali, Waheshimiwa karibuni kwenye Mkutano wetu, kikao chetu cha nne na swali letu la kwanza linaelekezwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI na linaulizwa na Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda. Na. 24 Ujenzi wa Vituo Vya Afya Ikuti na Ipinda MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi unaoendelea katika Vituo vya Afya Ikuti, Wilayani Rungwe na Ipinda Wilayani Kyela utakamilika ili kuwawezesha wananchi wa maeneo hayo kupata huduma kwa wakati? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:- 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya cha Ikuti kimekarabatiwa katika awamu ya kwanza ya ukarabati wa vituo vya afya 44 ulioanza tarehe 10 Oktoba, 2017 na kukamilika tarehe 31 Januari, 2018 kwa gharama ya shilingi milioni 500 ili kuongeza huduma za upasuaji wa dharura kwa mama wajawazito. Aidha, shilingi milioni 220 zimetolewa kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba vya upasuaji na samani. Kituo hicho kinaendelea kutoa huduma zote za matibabu isipokuwa huduma za upasuaji wa dharura. Ujenzi wa majengo ya Kituo cha Afya Ikuti umekamilika na kinachosubiriwa kwa sasa ni vifaatiba kutoka Bohari ya Dawa (MSD).
    [Show full text]