1458121152-Hs-15-20

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

1458121152-Hs-15-20 Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini – Tarehe 28 Mei, 2014 (Mkutano Ulianza Saa tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anna S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO: Randama za Makadirio ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI (MHE. STEPHEN J. MASELE): Randama za Makadirio ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) MASWALI NA MAJIBU Na. 138 Kujenga Barabara ya Mchepuo Uyole hadi Mbalizi Songwe 40 km (Bypass Road) MHE.DKT. MARY M. MWAJELWA aliuliza:- Jiji la Mbeya linakuwa kwa kasi sana na hivyo kuongeza idadi ya watu na magari, na ndio “Gate way Corridor” ya Kusini mwa Afrika hali inayosababisha msongamano na ajali za mara kwa mara zinazopelekea wananchi kupoteza maisha:- (a) Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka wa kurekebisha hali hiyo kwa kuchepusha barabara kutoka Uyole hadi Songwe baada ya Uwanja wa Ndege kwa ajili ya magari yetu makubwa? (b) Je, ni lini mpango huo utatekelezwa? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Dkt. Mary Machuche Mwanjelwa, Mbunge wa Viti maalum, Swali lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, ni kweli hivi sasa katika Jiji la Mbeya upo msongamano mkubwa wa magari hali ambayo husababisha usumbufu kwa wafanyabiashara katika soko la Mwanjelwa na wananchi kwa ujumla. Kwa kuzingatia hali hiyo, Serikali inakubaliana na pendekezo la kujenga barabara ya mchepuo kutoka Uyole hadi Songwe (Mbalizi) ili magari hasa ya mizigo yanayoenda nchi jirani yaweze kupita katika barabara hiyo bila kulazima kuingia katikati ya Jiji. Barabara hiyo inakadiriwa kuwa na urefu wa kilometa 40 kuanzia Mlima Nyoka, kupitia katika Kata za Ilomba, Mwakibete, Iyela, Nzovwe, Iyunga, Iwambi na kuunganishwa na barabara kuu ya eneo la Mbozi. 2 Nakala ya Mtandao (Online Document) (b) Mheshimiwa Spika, kabla ya kuanza ujenzi wa barabara hiyo, Serikali itafanyia upembuzi yakinifu (feasibility study) ambao utasaidia kujua gharama halisi za kutekeleza mradi huo wa barabara inayokadiriwa kuwa na urefu wa km 40. Aidha, hatua hiyo itawezesha Serikali kubaini wananchi watakaoathirika kutokana na utekelezaji wa maradi na kuhitaji kulipwa fidia. Hata hivyo utekelezaji wa mpango huu utategemea upatikanaji wa fedha. Kwa mantiki hiyo namwomba Mheshimiwa Mbunge avute subira wakati Serikali inakamilisha taratibu za awali. SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Mwanjelwa swali la nyongeza. MHE. DKT. MARY M. MWAJELWA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri kama nilivyoulizwa kwenye Swali langu kwamba, Mbeya ni Gate way Corridor za nchi nyingi za Kusini mwa Afrika. Hili suala limekuwa ni tatizo la muda mrefu sana, tumelijadili mpaka kwenye vikao vyetu vya Road Board bila mafanikio. Mheshimiwa Naibu Waziri, sasa anaponiambia upembuzi yakinifu mpaka pesa zitakapopatikana tukumbuke kwamba barabara hii imesababisha ajali na vifo vingi sana licha ya kwamba barabara yenyewe pia inaharika. Sasa hili jibu kwa kweli mimi namba niseme haliridhishi. Naomba atupatia jibu la uhakika. Nashukuru. SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Spika, mimi naomba niseme kitu kimoja, Mheshimiwa Mbunge anasema jambo la maana sana hapa. Jambo kubwa tu zuri.Yaani kule kuna Songwe International Airport. Kule kuna watu wanakwamba barabarani, kuna ajali zinatokea, wamelileta hili jambo limekuja kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu na Mstahiki Meya ndiye amelileta hili jambo kwa Waziri Mkuu. Wamezungumza habari hii Mheshimiwa Waziri Mkuu amemwandikia amemwandikia barua Mheshimiwa John Pombe Magufuli. (Makofi/Kicheko) Hela zinazotakiwa hapa kwa kifupi niwaambie ili tuweze kuelewana vizuri. Barabara kilomita moja unahitaji shilingi bilioni moja pamoja na madaraja 3 Nakala ya Mtandao (Online Document) yalikuwepo pale zipo kilomita pale 40, jumla ni shilingi bilioni 42. Halmashauri ya Jiji la Mbeya pale, imetengewa katika Bajeti hii tunayopitisha hapa bilioni moja na milioni 42 (1,420,000,000/=). Mheshimiwa Spika, nikisema hapa leo nikamwambia dada yangu Mwanjelwa, sawa! Ofisi ya Waziri Mkuu inaahidi mwaka huu tutamaliza feasibility study na kila kitu tutaweka barabara pale. Wataniuliza hivi bwana wewe ulikuwa umekunywa pombe asubuhi ukajibu vitu hivi?Mimi naomba niseme kitu kimoja hapa. Mheshimiwa huyu anasema jambo kubwa na la msingi. Tutakachofanya sisi barua hizi zimekwenda ninazo nakala zote kama anataka nimwonyeshe, ninazo correspondence zote. (Makofi) Leo asubuhi nimezungumza pale na Engineer Killian Haule ameniambia kwamba wao Halmashauri ya Jiji, tukiwaachia hawataweza. Mimi nataka nimuahidi ninazo barua zote, ninazo correspondence zote. Moja tunaiomba Wizara ya Ujenzi, Serikali itusaidie jambo hili na yapo maelekezo ya mapelekwa kule, amepeleka rai kuomba barabara hii na barua hiyo ya Waziri Mkuu ninayo hapa na file lote ninalo hapa. Ninataka nimwahidi kwamba sisi tutashughulikia jambo hili ili hicho anachokisema kiweze kufanyika. Ni kwa ajili ya taifa zima, barabara inayokwenda mpaka Johannesburg kule Afrika Kusini. SPIKA: Samahani. Umeahidi vyote hivi lakini hata hivyo tunaendelea, Mheshimiwa Aliko Kibona. Wamemalizia muda wangu. MHE. ALIKO N. KIBONA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Pia nimeshukuru kwa majibu ya Waziri lakini nina Swali moja la nyongeza. Kwa sababu mchakato unaendelea kama alivyotuahidi hapa na hali kule ni mbaya wananchi wanapata ajali wanachelewa kufika makazini na kurudi majumbani. Je, Serikali inaweza kuchukua hatua gani za dharura wakati pesa hizo nyingi bilioni 42 zikisubiriwa ili wananchi waweze kuishi maisha kama walio huru katika nchi yao? Mheshimiwa Spika, ahsante sana. 4 Nakala ya Mtandao (Online Document) SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri naomba unijibu kwa kifupi sana maana yake jibu lenyewe ushajibu! NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Spika, nitajibu kwa kifupi sana. Mheshimiwa Kibona anakuja tena na angle nyingine. Sasa mkishaanza nyinyi mtarudisha hii halafu tutawaambia twende tukatengeneze barabara ya moramu pale halafu utarudisha hili jambo litarudi nyuma litaanguka hili. Mheshimiwa Spika, mimi naomba tufanye hivi hii mambo ya watu wanagongwa na nini, ni suala la sisi, trafiki na watu wa mambo ya ndani tuzungumze nao vizuri tuweze kuweka pale kama ni matuta ama tutaweka utaratibu wa kusimamia watoto wasigongwe na magari na vitu vingine. Hilo tutafanya. Kama kuna wazo hapa kwamba sasa kwamba ebu nenda ukaweke hata barabara ya moramu watu wawe wanapitia huko! Sisi tutakwenda kuliangalia hili jumla lakini at the end of the day, Halmashauri ya Jiji la Mbeya ndio linatakiwa liseme hivyo. Liseme kwamba sasa achana na barabara ya lami hebu twende tukaweke moramu pale tuone kama itawezekana. Mimi nawaomba tusimame hapa tusiwe kama kina Tomaso msirudi nyuma tena mnaanza kusema kwamba tuanze kuangalia na nini mtalirudisha hili jambo nyuma, sisi tutasimama nalo, tutamwomba Mheshimiwa Waziri Mkuu tuweze kuzungumza na wenzetu wa Ujenzi. Na. 139 Maombi ya Kupatiwa Leseni ya Uchimbaji Mdogo wa Madini MHE. ALLY KEISSY MOHAMED (K.n.y. MHE. AHMED ALI SALUM) aliuliza:- 5 Nakala ya Mtandao (Online Document) Kikundi cha wachimbaji wadogo cha Nyaligongo Gold Mine Group Kata ya Mwakitolyo kiliomba leseni ya uchimbaji tangu tarehe 18 Januari, 2013 katika Ofisi ya Madini Shinyanga. Je, leseni hiyo itatolewa lini kwa kuwa hadi sasa hakuna majibu yoyote yaliyotolewa? NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI (MHE. STEPHEN J. MASELE) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati na Madini,, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ahmed Ally Salum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, nianze kwa kutoa ufafanuzi kuwa, Kikundi cha Wachimbaji Wadogo cha Nyaligongo Gold Mine Group Kata ya Mwakitolyo hakijawahi kuwasilisha rasmi ombi la kupewa leseni ya uchimbaji mdogo wa Madini katika eneo la Mwakitolyo kama Sheria ya Madini (2010) na Kanuni zake zinavyoelekeza. Kwa mujibu wa Kanuni ya 3(2) ya Kanuni za Madini za mwaka 2010, utaratibu wa kuomba leseni za Uchimbaji Mdogo (Primary Mining License) ni pamoja na kujaza Fomu MPF 5 inayotumika kuombea leseni ya Uchimbaji Mdogo wa Madini. Fomu hiyo huambatishwa na mchoro unaoonesha eneo husika na baada ya kukamilika huwasilishwa kwa Afisa Madini wa Kanda inayohusika na usimamizi wa eneo hilo ikiambatana na malipo ya ada ya ombi ambayo hivi sasa ni shilingi 50,000/= kwa kila leseni inayoombwa. Mheshimiwa Spika, Kikundi cha wachimbaji wadogo cha Nyaligongo Gold mine Group kiliwasilisha maombi yao ya leseni kwa njia ya barua bila kufuata utaratibu nilioutaja. Barua hiyo ya kuomba leseni ililetwa kwa mkono na wahusika kwa Afisa Madini Kanda ya Kati Magharibi tarehe 22 Januari, 2013. Baada ya kupokelewa, mwakilishi wa Kikundi hicho alielekezwa kufuata utaratibu wa kisheria kuwasilisha ombi hilo, lakini hadi sasa kikundi hicho hakijawahi kufanya hivyo. Mheshimiwa Spika, kufuatia ukaguzi uliofanywa na Ofisi ya Madini Kanda ya Kati Magharibi (Shinyanga), imebainika kuwa eneo ambalo Nyaligongo Gold Mine Group wanaomba kupewa leseni ya PML tayari lina leseni ya PL No. 5044/2008 inayomilikiwa na kampuni ya Pangea Minerals Ltd. Hivyo, haitawezekana
Recommended publications
  • 1458137638-Hs-4-4-20
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE KIKAO CHA NNE – TAREHE 14 JUNI, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 37 Ardhi Iliyotolewa Kujenga Shule ya Msingi Kiraracha MHE. AUGUSTINO L. MREMA aliuliza:- Mzee Pauli Sananga Lekule wa Kijiji cha Kiraracha, Kata ya Marangu, Wilaya ya Moshi Vijijini, alitoa ardhi yake ikatumika kujenga shule ya msingi Kiraracha, Marangu miaka 10 iliyopita akiahidiwa na Serikali kupewa eneo jingine kama fidia lakini mpaka sasa hajapewa eneo jingine kama fidia jambo lililomfanya aione Serikali haikumtendea haki. Je, ni lini Serikali itamlipa haki yake kutokana na makubaliano hayo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Lyatonga Mrema, Mbunge wa Vunjo kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa Ndugu Pauli Sananga Lekule wa Kijiji cha Kiraracha, Kata ya Marangu Magharibi, alitoa ardhi yake kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi Kiraracha, Kata ya Marangu Magharibi kwa ahadi ya kufidiwa eneo lililoko Njia panda. Aidha eneo ambalo Halmashauri ya Wilaya ya Moshi ilitarajia kumfudia Ndugu Lekule lipo katika mgogoro na kesi bado inaendelea Mahakama Kuu. 1 Mheshimiwa Spika, kwa kuwa eneo lililopimwa viwanja na kutarajia mlalamikaji lipo katika mgogoro wa kisheria kati ya Halmashauri na wananchi, Serikali inaendelea kufuatilia mwenendo wa kesi na mara shauri litakapomalizika Mahakamani mhusika atapewa eneo lake. Mheshimiwa Spika, katika jitihada za Serikali kuhakikisha shauri hili haliendelei kuchukua muda mrefu, Halmashauri ya Wilaya ya Moshi imeunda timu kwa ajili ya kufuatilia na kuharakisha shauri hili ili ikiwezekana limalizike nje ya Mahakama ili Ndugu Lekule Sananga aweze kupata haki yake mapema.
    [Show full text]
  • Issued by the Britain-Tanzania Society No 105 May - Aug 2013
    Tanzanian Affairs Text 1 Issued by the Britain-Tanzania Society No 105 May - Aug 2013 Even More Gas Discovered Exam Results Bombshell Rising Religious Tensions The Maasai & the Foreign Hunters Volunteering Changed my Life EVEN MORE GAS DISCOVERED Roger Nellist, the latest volunteer to join our panel of contributors reports as follows on an announcement by Statoil of their third big gas discovery offshore Tanzania: On 18 March 2013 Statoil and its co-venturer ExxonMobil gave details of their third high-impact gas discovery in licence Block 2 in a year. The new discovery (known as Tangawizi-1) is located 10 kilometres from their first two discoveries (Lavani and Zafarani) made in 2012, and is located in water depth of 2,300 metres. The consortium will drill further wells later this year. The Tangawizi-1 discovery brings the estimated total volume of natural gas in-place in Block 2 to between 15 and 17 trillion cubic feet (Tcf). Depending on reservoir characteristics and field development plans, this could result in recoverable gas volumes in the range of 10-13 Tcf from just this one Block. These are large reserves by international stand- ards. By comparison, Tanzania’s first gas field at Songo Songo island has volumes of about 1 Tcf. Statoil has been in Tanzania since 2007 and has an office in Dar es Salaam. It operates the licence on Block 2 on behalf of the Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) and has a 65% working interest, with ExxonMobil Exploration and Production Tanzania Limited holding the remaining 35%. It is understood that under the Production Sharing Agreement that governs the operations, TPDC has the right to a 10% working participation interest in case of a development phase.
    [Show full text]
  • Human Rights and Business Report 2015
    LEGALLEGAL AND AND HUMAN HUMAN RIGHTS RIGHTS CENTRE CENTRE HUMANHUMAN RIGHTS RIGHTS AND AND BUSINESS BUSINESS REPORT REPORT OF 2015 2015 Taking Stock of Labour Rights, Land Rights, Gender, Taxation, Corporate Accountability,Taking Stock Environmental of Labour Justice Rights, and Performance Land Rights, of Regulatory Gender, Authorities Taxation, Corporate Accountability, Environmental Justice and Performance of Regulatory Authorities LEGAL AND HUMAN RIGHTS CENTRE HUMAN RIGHTS AND BUSINESS REPORT 2015 PUBLISHER Legal and Human Rights Centre Justice Lugakingira House, Kijitonyama P.O Box 75254, Dar es Salaam, Tanzania Tel.: +255222773038/48 Fax: +255222773037 Email: [email protected] Website: www.humanrights.or.tz PARTNERS ISBN:978-9987-740-26-0 © July, 2016 ii ii EDITORIAL BOARD Dr. Helen Kijo-Bisimba, Adv. Imelda Lulu Urrio Adv. Anna Henga Ms. Felista Mauya Mr. Castor Kalemera RESEARCH COORDINATOR Adv. Masud George ASSISTANT RESEARCHERS 29 Assistant Researchers 14 Field Enumerators REPORT WRITER Adv. Clarence Kipobota LAYOUT & DESIGN Mr. Rodrick Maro Important Message of the Year 2015 LHRC endorses the United Nations’ call to all nations (and everyone) to promote sustained, inclusive and sustainable economic growth, with full and productive employment and decent work for all as it is implied under Goal 8 of the United Nations Strategic Development Goals (SDGs) 2030. iii iii DISCLAIMER The opinions expressed by the sampled respondents in this report do not necessarily reflect the official position of the Legal and Human Rights Centre (LHRC). Therefore, no mention of any authority, organization, company or individual shall imply any approval as to official standing of the matters which have implicated them. The illustrations used by inferring some of the respondents are for guiding the said analysis and discussion only, and not constitute the conclusive opinion on part of LHRC.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA TATU Kikao Cha Hamsini Na Sita
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Hamsini na Sita – Tarehe 22 Juni, 2021 (Bunge Lilianza saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba tukae. Waheshimiwa tunaendelea na Mkutano wetu wa Tatu, leo ni Kikao cha Hamsini na Sita na kabla hatujaendelea nitumie nafasi hii kuwashukuru sana wasaidizi wangu wote wakiongozwa na Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa David Kihenzile, Mheshimiwa Zungu na Mheshimiwa Najma kwa kazi nzuri ambayo wameifanya wiki nzima kutuendeshea mjadala wetu wa bajeti. (Makofi) Sasa leo hapa ndio siku ya maamuzi ambayo kila Mbunge anapaswa kuwa humu ndani, kwa Mbunge ambaye Spika hana taarifa yake na hatapiga kura hapa leo hilo la kwake yeye. (Makofi) Katibu. NDG. NENELWA MWIHAMBI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Maswali na tunaanza na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Kwela. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Na. 465 Ujenzi wa Makao Makuu ya Halmashauri Katika Mji wa Laela MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi za Makao Makuu ya Halmashauri ya Sumbawanga katika Mji wa Laela baada ya agizo la Serikali la kuhamisha Makao Makuu? SPIKA: Majibu ya swali hilo muhimu la watu wa Kwela, Mheshimiwa Naibu Waziri - TAMISEMI, Mheshimiwa Dkt. Festo Dugange tafadhali. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Jimbo la Kwela kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ni miongoni mwa Halmashauri 30 zilizohamia kwenye maeneo mapya ya utawala mwaka 2019.
    [Show full text]
  • Issued by the Britain-Tanzania Society No 124 Sept 2019
    Tanzanian Affairs Issued by the Britain-Tanzania Society No 124 Sept 2019 Feathers Ruffled in CCM Plastic Bag Ban TSh 33 trillion annual budget Ben Taylor: FEATHERS RUFFLED IN CCM Two former Secretary Generals of the ruling party, CCM, Abdulrahman Kinana and Yusuf Makamba, stirred up a very public argument at the highest levels of the party in July. They wrote a letter to the Elders’ Council, an advisory body within the party, warning of the dangers that “unfounded allegations” in a tabloid newspaper pose to the party’s “unity, solidarity and tranquillity.” Selection of newspaper covers from July featuring the devloping story cover photo: President Magufuli visits the fish market in Dar-es-Salaam following the plastic bag ban (see page 5) - photo State House Politics 3 This refers to the frequent allegations by publisher, Mr Cyprian Musiba, in his newspapers and on social media, that several senior figures within the party were involved in a plot to undermine the leadership of President John Magufuli. The supposed plotters named by Mr Musiba include Kinana and Makamba, as well as former Foreign Affairs Minister, Bernard Membe, various opposition leaders, government officials and civil society activists. Mr Musiba has styled himself as a “media activist” seeking to “defend the President against a plot to sabotage him.” His publications have consistently backed President Magufuli and ferociously attacked many within the party and outside, on the basis of little or no evidence. Mr Makamba and Mr Kinana, who served as CCM’s secretary generals between 2009 to 2011 and 2012-2018 respectively, called on the party’s elders to intervene.
    [Show full text]
  • Tarehe 4 Aprili, 2019
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Tatu – Tarehe 4 Aprili, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba tukae. Leo ni kikao cha tatu cha Mkutano wetu wa Kumi na Tano. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI: Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, AJIRA, KAZI VIJANA NA WAZEE NA WENYE ULEMAVU: Taarifa ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2019/2020. MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA: Taarifa 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020. MHE. HASNA S.K. MWILIMA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu utekelezaji wa Bajeti ya Mfuko wa Bunge kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Mfuko huo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA - MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MASUALA YA UKIMWI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu utekelezaji wa Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu (Tume ya Uratibu na Udhibiti wa UKIMWI) kwa mwaka wa fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Mbili - Tarehe 22 Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kwa masikitiko makubwa natoa taarifa kwamba Mheshimiwa Mussa Hamisi Silima, Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar, jana Jumapili, tarehe 21 Agosti, 2011 majira ya jioni kama saa mbili kasorobo hivi walipokuwa wakirejea kutoka Dar es Salaam, yeye na familia yake walipata ajali mbaya sana katika eneo la Nzuguni, Mjini Dodoma. Katika ajali hiyo, mke wa Mbunge huyo aitwaye Mwanaheri Twalib amefariki dunia na mwili wa Marehemu upo hospitali ya Mkoa hapa Dodoma ukiandaliwa kupelekwa Zanzibar leo hii Jumatatu, tarehe 22 August, 2011 kwa mazishi yatanayotarajiwa kufanyanyika alasili ya leo. Kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Wabunge tusimame dakika chache tumkumbuke. (Heshima ya Marehemu, dakika moja) (Hapa Waheshimiwa Wabunge walisimama kwa dakika moja) Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, amina. Ahsanteni sana, tukae. Kwa hiyo sasa hivi tunavyoongea Mheshimiwa Mbunge ambae nae pia ameumia vibaya na dereva wake wanaondoka na ndege sasa hivi kusudi waweze kupata yanayohusika kule Dar es Salaam na pia kule watakuwa na watu wa kuwaangalia zaidi. Lakini walikwenda Zanzibar kumzika kaka yake na Marehemu huyu mama. Kwa hiyo, wamemzika marehemu basi wakawa wanawahi Bunge la leo ndiyo jana usiku wamepata ajali. Kwa hiyo, watakaokwenda kusindikiza msiba, ndege itaondoka kama saa tano watakwenda wafuatao, watakwenda Wabunge nane pamoja na mfawidhi zanzibar yeye anaongozana na mgonjwa sasa hivi lakini ataungana na wale kwenye mazishi.
    [Show full text]
  • Tarehe 23 Mei, 2016
    NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Ishirini na Sita – Tarehe 23 Mei, 2016 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Najma Murtaza Giga) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu! NDG. CHARLES J. MLOKA – KATIBU MEZANI: Hati za kuwasilisha mezani. HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa mwaka wa fedha 2016/2017. MWENYEKITI: Katibu! NDG. CHARLES J. MLOKA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge tunaanza na maswali Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mheshimiwa Richard Philip Mbogo Mbunge wa Nsimbo, sasa aulize swali lake. 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Na. 209 Uchaguzi wa Madiwani katika Kambi ya Katumba MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza: - Chaguzi za Madiwani zilifanyika katika kambi ya wakimbizi Katumba wa 2015:- Je, ni lini Serikali itapeleka fedha ili kukamilisha chaguzi za Serikali za Vijiji na Mtaa? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Richard Philip Mbogo, Mbunge wa Nsimbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata ya Katumba, Vijiji ambavyo havijafanya uchaguzi wa Vviongozi wa Serikali za Mitaa kwa mwaka 2014 ni 14 na vitongoji 51. Uchaguzi ulishindwa kufanyika kwa sababu Kata hiyo ilikuwa ni kambi ya wakimbizi ambao walikuwa hawajapata uraia wa Tanzania kwa mujibu wa sheria za nchi. Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya Serikali kuwapa uraia wananchi wa maeneo hayo, Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo inaendelea na maandalizi ya kufanya uchaguzi mdogo katika vijiji na vitongoji hivyo na tayari katika bajeti ijayo ya mwaka 2016/2017 zimetengwa sh.
    [Show full text]
  • Coversheet for Thesis in Sussex Research Online
    A University of Sussex DPhil thesis Available online via Sussex Research Online: http://sro.sussex.ac.uk/ This thesis is protected by copyright which belongs to the author. This thesis cannot be reproduced or quoted extensively from without first obtaining permission in writing from the Author The content must not be changed in any way or sold commercially in any format or medium without the formal permission of the Author When referring to this work, full bibliographic details including the author, title, awarding institution and date of the thesis must be given Please visit Sussex Research Online for more information and further details Accountability and Clientelism in Dominant Party Politics: The Case of a Constituency Development Fund in Tanzania Machiko Tsubura Submitted for the Degree of Doctor of Philosophy in Development Studies University of Sussex January 2014 - ii - I hereby declare that this thesis has not been and will not be submitted in whole or in part to another University for the award of any other degree. Signature: ……………………………………… - iii - UNIVERSITY OF SUSSEX MACHIKO TSUBURA DOCTOR OF PHILOSOPHY IN DEVELOPMENT STUDIES ACCOUNTABILITY AND CLIENTELISM IN DOMINANT PARTY POLITICS: THE CASE OF A CONSTITUENCY DEVELOPMENT FUND IN TANZANIA SUMMARY This thesis examines the shifting nature of accountability and clientelism in dominant party politics in Tanzania through the analysis of the introduction of a Constituency Development Fund (CDF) in 2009. A CDF is a distinctive mechanism that channels a specific portion of the government budget to the constituencies of Members of Parliament (MPs) to finance local small-scale development projects which are primarily selected by MPs.
    [Show full text]
  • Tarehe 3 Februari, 2021
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA PILI Kikao cha Pili – Tarehe 3 Februari, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Tukae. Katibu. NDG. RUTH MAKUNGU – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaanza na maswali Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, sasa aulize swali lake. Na. 16 Ujenzi wa Barabara za Lami - Mji wa Mafinga MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza Ujenzi wa Barabara za lami na kufunga taa za barabarani katika Mji wa Mafinga chini ya Mpango wa Uendelezaji Miji nchini? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NAIBU WAZIRI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyenijalia mimi na Waheshimiwa Wabunge wote afya njema na kutuwezesha kuwa wawakilishi wa wananchi kupitia Bunge lako Tukufu. Mheshimiwa Naibu Spika, pili, naomba nichukue nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa imani kubwa aliyonipa kwa kuniteua kuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Namshukuru sana Mheshimiwa Rais. (Makofi) Mheshimiwa Naibu Spika, tatu, nawashukuru sana wananchi wa Jimbo la Wanging’ombe kwa kunichagua na kuchagua mafiga
    [Show full text]
  • Online Document)
    Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ________________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini – Tarehe 10 Juni, 2014 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge Maswali tunaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu, atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Josephat Kandege. Na. 216 Kugawa Jimbo la Kalambo MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Wilaya ya Kalambo ni Jimbo moja lenye eneo kubwa sana la Kiutawala ikipakana na nchi za Zambia na Congo DRC:- Je, Serikali haioni kuwa ipo haja ya kuligawa Jimbo hilo ili kupunguza eneo la uwakilishi wa wananchi? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege, Mbunge wa Kalambo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Ibara ya 75(1) – (5) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano a Tanzania ya Mwaka 1977 imeainisha utaratibu na vigezo vinavyotumiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika kufikia uamuzi wa kugawa mipaka ya Majimbo ya Uchaguzi angalau kila baada ya kipindi cha miaka kumi (10). Vigezo vinavyozingatiwa na Tume ni pamoja na ukubwa wa eneo la utawala; upatikanaji wa njia ya mawasiliano; Idadi ya Watu na hali ya kijiografia katika jimbo linalokusudiwa kugawanywa. Vigezo vingine vinavyotumika ni hali ya uchumi; mipaka ya kiutawala; jimbo moja lisiwe ndani ya Wilaya/Halmashauri mbili, Kata moja isiwe ndani ya Majimbo mawili; Mazingira ya Muungano, Mgawanyo wa Wastani wa Idadi ya Watu; uwezo wa Ukumbi wa Bunge; Idadi ya Viti Maalum vya Wanawake na mpangilio wa maeneo ya makazi ya watu yaliyopo.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 18 Julai, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita muuliza swali la kwanza nina matangazo kuhusu wageni, kwanza wale vijana wanafunzi kutoka shule ya sekondari, naona tangazo halisomeki vizuri, naomba tu wanafunzi na walimu msimame ili Waheshimiwa Wabunge waweze kuwatambua. Tunafurahi sana walimu na wanafunzi wa shule zetu za hapa nchini Tanzania mnapokuja hapa Bungeni kujionea wenyewe demokrasia ya nchi yetu inavyofanya kazi. Karibuni sana. Wapo Makatibu 26 wa UWT, ambao wamekuja kwenye Semina ya Utetezi na Ushawishi kwa Harakati za Wanawake inayofanyika Dodoma CCT wale pale mkono wangu wakulia karibuni sana kina mama tunawatakia mema katika semina yenu, ili ilete mafanikio na ipige hatua mbele katika kumkomboa mwanamke wa Tanzania, ahsanteni sana. Hawa ni wageni ambao tumetaarifiwa na Mheshimiwa Shamsa Selengia Mwangunga, Naibu Waziri wa Maji. Wageni wengine nitawatamka kadri nitakavyopata taarifa, kwa sababu wamechelewa kuleta taarifa. Na. 223 Barabara Toka KIA – Mererani MHE. DORA H. MUSHI aliuliza:- Kwa kuwa, Mererani ni Controlled Area na ipo kwenye mpango wa Special Economic Zone na kwa kuwa Tanzanite ni madini pekee duniani yanayochimbwa huko Mererani na inajulikana kote ulimwenguni kutokana na madini hayo, lakini barabara inayotoka KIA kwenda Mererani ni mbaya sana
    [Show full text]