1458121152-Hs-15-20
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini – Tarehe 28 Mei, 2014 (Mkutano Ulianza Saa tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anna S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO: Randama za Makadirio ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI (MHE. STEPHEN J. MASELE): Randama za Makadirio ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) MASWALI NA MAJIBU Na. 138 Kujenga Barabara ya Mchepuo Uyole hadi Mbalizi Songwe 40 km (Bypass Road) MHE.DKT. MARY M. MWAJELWA aliuliza:- Jiji la Mbeya linakuwa kwa kasi sana na hivyo kuongeza idadi ya watu na magari, na ndio “Gate way Corridor” ya Kusini mwa Afrika hali inayosababisha msongamano na ajali za mara kwa mara zinazopelekea wananchi kupoteza maisha:- (a) Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka wa kurekebisha hali hiyo kwa kuchepusha barabara kutoka Uyole hadi Songwe baada ya Uwanja wa Ndege kwa ajili ya magari yetu makubwa? (b) Je, ni lini mpango huo utatekelezwa? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Dkt. Mary Machuche Mwanjelwa, Mbunge wa Viti maalum, Swali lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, ni kweli hivi sasa katika Jiji la Mbeya upo msongamano mkubwa wa magari hali ambayo husababisha usumbufu kwa wafanyabiashara katika soko la Mwanjelwa na wananchi kwa ujumla. Kwa kuzingatia hali hiyo, Serikali inakubaliana na pendekezo la kujenga barabara ya mchepuo kutoka Uyole hadi Songwe (Mbalizi) ili magari hasa ya mizigo yanayoenda nchi jirani yaweze kupita katika barabara hiyo bila kulazima kuingia katikati ya Jiji. Barabara hiyo inakadiriwa kuwa na urefu wa kilometa 40 kuanzia Mlima Nyoka, kupitia katika Kata za Ilomba, Mwakibete, Iyela, Nzovwe, Iyunga, Iwambi na kuunganishwa na barabara kuu ya eneo la Mbozi. 2 Nakala ya Mtandao (Online Document) (b) Mheshimiwa Spika, kabla ya kuanza ujenzi wa barabara hiyo, Serikali itafanyia upembuzi yakinifu (feasibility study) ambao utasaidia kujua gharama halisi za kutekeleza mradi huo wa barabara inayokadiriwa kuwa na urefu wa km 40. Aidha, hatua hiyo itawezesha Serikali kubaini wananchi watakaoathirika kutokana na utekelezaji wa maradi na kuhitaji kulipwa fidia. Hata hivyo utekelezaji wa mpango huu utategemea upatikanaji wa fedha. Kwa mantiki hiyo namwomba Mheshimiwa Mbunge avute subira wakati Serikali inakamilisha taratibu za awali. SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Mwanjelwa swali la nyongeza. MHE. DKT. MARY M. MWAJELWA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri kama nilivyoulizwa kwenye Swali langu kwamba, Mbeya ni Gate way Corridor za nchi nyingi za Kusini mwa Afrika. Hili suala limekuwa ni tatizo la muda mrefu sana, tumelijadili mpaka kwenye vikao vyetu vya Road Board bila mafanikio. Mheshimiwa Naibu Waziri, sasa anaponiambia upembuzi yakinifu mpaka pesa zitakapopatikana tukumbuke kwamba barabara hii imesababisha ajali na vifo vingi sana licha ya kwamba barabara yenyewe pia inaharika. Sasa hili jibu kwa kweli mimi namba niseme haliridhishi. Naomba atupatia jibu la uhakika. Nashukuru. SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Spika, mimi naomba niseme kitu kimoja, Mheshimiwa Mbunge anasema jambo la maana sana hapa. Jambo kubwa tu zuri.Yaani kule kuna Songwe International Airport. Kule kuna watu wanakwamba barabarani, kuna ajali zinatokea, wamelileta hili jambo limekuja kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu na Mstahiki Meya ndiye amelileta hili jambo kwa Waziri Mkuu. Wamezungumza habari hii Mheshimiwa Waziri Mkuu amemwandikia amemwandikia barua Mheshimiwa John Pombe Magufuli. (Makofi/Kicheko) Hela zinazotakiwa hapa kwa kifupi niwaambie ili tuweze kuelewana vizuri. Barabara kilomita moja unahitaji shilingi bilioni moja pamoja na madaraja 3 Nakala ya Mtandao (Online Document) yalikuwepo pale zipo kilomita pale 40, jumla ni shilingi bilioni 42. Halmashauri ya Jiji la Mbeya pale, imetengewa katika Bajeti hii tunayopitisha hapa bilioni moja na milioni 42 (1,420,000,000/=). Mheshimiwa Spika, nikisema hapa leo nikamwambia dada yangu Mwanjelwa, sawa! Ofisi ya Waziri Mkuu inaahidi mwaka huu tutamaliza feasibility study na kila kitu tutaweka barabara pale. Wataniuliza hivi bwana wewe ulikuwa umekunywa pombe asubuhi ukajibu vitu hivi?Mimi naomba niseme kitu kimoja hapa. Mheshimiwa huyu anasema jambo kubwa na la msingi. Tutakachofanya sisi barua hizi zimekwenda ninazo nakala zote kama anataka nimwonyeshe, ninazo correspondence zote. (Makofi) Leo asubuhi nimezungumza pale na Engineer Killian Haule ameniambia kwamba wao Halmashauri ya Jiji, tukiwaachia hawataweza. Mimi nataka nimuahidi ninazo barua zote, ninazo correspondence zote. Moja tunaiomba Wizara ya Ujenzi, Serikali itusaidie jambo hili na yapo maelekezo ya mapelekwa kule, amepeleka rai kuomba barabara hii na barua hiyo ya Waziri Mkuu ninayo hapa na file lote ninalo hapa. Ninataka nimwahidi kwamba sisi tutashughulikia jambo hili ili hicho anachokisema kiweze kufanyika. Ni kwa ajili ya taifa zima, barabara inayokwenda mpaka Johannesburg kule Afrika Kusini. SPIKA: Samahani. Umeahidi vyote hivi lakini hata hivyo tunaendelea, Mheshimiwa Aliko Kibona. Wamemalizia muda wangu. MHE. ALIKO N. KIBONA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Pia nimeshukuru kwa majibu ya Waziri lakini nina Swali moja la nyongeza. Kwa sababu mchakato unaendelea kama alivyotuahidi hapa na hali kule ni mbaya wananchi wanapata ajali wanachelewa kufika makazini na kurudi majumbani. Je, Serikali inaweza kuchukua hatua gani za dharura wakati pesa hizo nyingi bilioni 42 zikisubiriwa ili wananchi waweze kuishi maisha kama walio huru katika nchi yao? Mheshimiwa Spika, ahsante sana. 4 Nakala ya Mtandao (Online Document) SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri naomba unijibu kwa kifupi sana maana yake jibu lenyewe ushajibu! NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Spika, nitajibu kwa kifupi sana. Mheshimiwa Kibona anakuja tena na angle nyingine. Sasa mkishaanza nyinyi mtarudisha hii halafu tutawaambia twende tukatengeneze barabara ya moramu pale halafu utarudisha hili jambo litarudi nyuma litaanguka hili. Mheshimiwa Spika, mimi naomba tufanye hivi hii mambo ya watu wanagongwa na nini, ni suala la sisi, trafiki na watu wa mambo ya ndani tuzungumze nao vizuri tuweze kuweka pale kama ni matuta ama tutaweka utaratibu wa kusimamia watoto wasigongwe na magari na vitu vingine. Hilo tutafanya. Kama kuna wazo hapa kwamba sasa kwamba ebu nenda ukaweke hata barabara ya moramu watu wawe wanapitia huko! Sisi tutakwenda kuliangalia hili jumla lakini at the end of the day, Halmashauri ya Jiji la Mbeya ndio linatakiwa liseme hivyo. Liseme kwamba sasa achana na barabara ya lami hebu twende tukaweke moramu pale tuone kama itawezekana. Mimi nawaomba tusimame hapa tusiwe kama kina Tomaso msirudi nyuma tena mnaanza kusema kwamba tuanze kuangalia na nini mtalirudisha hili jambo nyuma, sisi tutasimama nalo, tutamwomba Mheshimiwa Waziri Mkuu tuweze kuzungumza na wenzetu wa Ujenzi. Na. 139 Maombi ya Kupatiwa Leseni ya Uchimbaji Mdogo wa Madini MHE. ALLY KEISSY MOHAMED (K.n.y. MHE. AHMED ALI SALUM) aliuliza:- 5 Nakala ya Mtandao (Online Document) Kikundi cha wachimbaji wadogo cha Nyaligongo Gold Mine Group Kata ya Mwakitolyo kiliomba leseni ya uchimbaji tangu tarehe 18 Januari, 2013 katika Ofisi ya Madini Shinyanga. Je, leseni hiyo itatolewa lini kwa kuwa hadi sasa hakuna majibu yoyote yaliyotolewa? NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI (MHE. STEPHEN J. MASELE) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati na Madini,, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ahmed Ally Salum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, nianze kwa kutoa ufafanuzi kuwa, Kikundi cha Wachimbaji Wadogo cha Nyaligongo Gold Mine Group Kata ya Mwakitolyo hakijawahi kuwasilisha rasmi ombi la kupewa leseni ya uchimbaji mdogo wa Madini katika eneo la Mwakitolyo kama Sheria ya Madini (2010) na Kanuni zake zinavyoelekeza. Kwa mujibu wa Kanuni ya 3(2) ya Kanuni za Madini za mwaka 2010, utaratibu wa kuomba leseni za Uchimbaji Mdogo (Primary Mining License) ni pamoja na kujaza Fomu MPF 5 inayotumika kuombea leseni ya Uchimbaji Mdogo wa Madini. Fomu hiyo huambatishwa na mchoro unaoonesha eneo husika na baada ya kukamilika huwasilishwa kwa Afisa Madini wa Kanda inayohusika na usimamizi wa eneo hilo ikiambatana na malipo ya ada ya ombi ambayo hivi sasa ni shilingi 50,000/= kwa kila leseni inayoombwa. Mheshimiwa Spika, Kikundi cha wachimbaji wadogo cha Nyaligongo Gold mine Group kiliwasilisha maombi yao ya leseni kwa njia ya barua bila kufuata utaratibu nilioutaja. Barua hiyo ya kuomba leseni ililetwa kwa mkono na wahusika kwa Afisa Madini Kanda ya Kati Magharibi tarehe 22 Januari, 2013. Baada ya kupokelewa, mwakilishi wa Kikundi hicho alielekezwa kufuata utaratibu wa kisheria kuwasilisha ombi hilo, lakini hadi sasa kikundi hicho hakijawahi kufanya hivyo. Mheshimiwa Spika, kufuatia ukaguzi uliofanywa na Ofisi ya Madini Kanda ya Kati Magharibi (Shinyanga), imebainika kuwa eneo ambalo Nyaligongo Gold Mine Group wanaomba kupewa leseni ya PML tayari lina leseni ya PL No. 5044/2008 inayomilikiwa na kampuni ya Pangea Minerals Ltd. Hivyo, haitawezekana