Bunge La Tanzania ______
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA KUMI NA SITA ______________ Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 27 Julai, 2009) (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita anayeuliza swali la kwanza, karibuni tena baada ya mapumziko ya weekend, nadhani mna nguvu ya kutosha kwa ajili ya shughuli za wiki hii ya mwisho ya Bunge hili la 16. Swali la kwanza linaelekezwa Ofisi ya Waziri Mkuu na linauliza na Mheshimiwa Shoka, kwa niaba yake Mheshimiwa Khalifa. Na.281 Kiwanja kwa Ajili ya Kujenga Ofisi ya Tume ya Kudhibiti UKIMWI MHE KHALIFA SULEIMAN KHALIFA (K.n.y. MHE. SHOKA KHAMIS JUMA) aliuliza:- Kwa kuwa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI inakabiliwa na changamoto ya ufinyu wa Ofisi; na kwa kuwa Tume hiyo imepata fedha kutoka DANIDA kwa ajili ya kujenga jengo la Ofisi lakini inakabiliwa na tatizo kubwa la upatikanaji wa kiwanja:- Je, Serikali itasaidia vipi Tume hiyo kupata kiwanja cha kujenga Ofisi? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU – SERA, URATIBU NA BUNGE alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shoka Khamis Juma, Mbunge wa Micheweni kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, tatizo la kiwanja cha kujenga Ofisi za TACAIDS limepatiwa ufumbuzi na ofisi yangu imewaonesha Maafisa wa DANIDA kiwanja hicho Ijumaa tarehe 17 Julai, 2009. Kiwanja hicho kipo Mtaa wa Luthuli Na. 73, Dar es Salaam ama kwa lugha nyingine Makutano ya Mtaa wa Samora na Luthuli. MHE. KHALIFA SULEIMAN KHALIFA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Waziri, naomba kumuuliza swali moja la nyongeza. -
MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao Cha Arobaini Na Moja
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Moja – Tarehe 31 Mei, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Tunaanza kikao chetu cha Arobaini na Moja, Katibu. NDG. LINA KITOSI – KATIBU MEZANI:- HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2018/19. MHE. CATHERINE V. MAGIGE (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu utekelezaji wa Bajeti na Majukumu ya Wizara 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019. MWENYEKITI: Ahsante. Katibu. NDG. LINA KITOSI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Swali letu la kwanza linaelekezwa Ofisi ya Waziri Mkuu na linaulizwa na Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, kwa niaba yake Mheshimiwa Amina Mollel. Na. 341 Utekelezaji wa Mpango wa Ukimwi 90-90-90 MHE. AMINA S. MOLLEL (K.n.y MHE. HAWA M. CHAKOMA) aliuliza:- Je, Serikali inatekelezaje Mpango wa UKIMWI wa 90- 90-90? MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Mollel. Majibu, Mheshimiwa Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA NA VIJANA) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Ishirini na Saba - Tarehe 9 Julai, 2010 (Mkutano ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anna S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZlLIZOWASILISHWA MEZANI: Hati Zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha, 2010/2011. MHE. WILLIAM H. SHELLUKINDO - MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya ya Nishati na Madini Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. MHE.SAVELINA S. MWIJAGE (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMATI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA NISHATI NA MADINI): Taarifa ya Msemaji wa Mkuu wa Kambi ya Upinzani Kuhusu Makadiro ya Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI (MHE. MWANTUMU BAKARI MAHIZA): 1 Randama za Makadiro ya Matumizi ya Wizara ya Elimu na Mfunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI (MHE. OMAR YUSSUF MZEE): Taarifa ya Majumuisho ya Mpango Mkakati wa Kujibu Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu za Wizara, Idara za Serikali na Mikoa kwa Mwaka wa Fedha 2008/2009. MASWALI NA MAJIBU Na. 191 Kuhusu Barabara ya Makutupa Bumila Jimbo la Mpwapwa MHE. GEOREGE M. -
Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania Mkutano Wa Saba Yatokanayo Na Kikao Cha Ishirini Na Sita 16 Mei, 2017
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA ISHIRINI NA SITA 16 MEI, 2017 MKUTANO WA SABA KIKAO CHA ISHIRINI NA SITA TAREHE 16 MEI, 2017 I. DUA: Saa 3:00 asubuhi Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mwenyekiti) alisoma Dua na kuongoza Bunge. Makatibu mezani: 1. Ndugu Theonest Ruhilabake 2. Ndugu Asia Minja 3. Ndugu Joshua Chamwela II. HATI ZA KUWASILISHA MEZANI (i) Mhe. Charles John Mwijage aliwasilisha Mezani Randama ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (ii) Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi aliwasilisha Mezani Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (iii) Mhe. Jumanne Kidera Kishimba aliwasilisha Mezani Taarifa ya Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (iv) Mhe. Masoud Abdallah Salim aliwasilisha Mezani Taarifa ya Kambi ya Upinzani kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. 1 III. MASWALI OFISI YA RAIS (TAMISEMI) Swali Na. 209: Mhe. Dkt. Pudenciana Kikwembe Nyongeza: Mhe. Dkt. Pudenciana Kikwembe Mhe. Pauline Gekul Mhe. David Cosato Chumi Swali Na. 210: Mhe. Eng. Atashasta Justus Nditiye Nyongeza: Mhe. Eng. Atashasta Justus Nditiye Mhe. Josephine Johnson Genzabuke Mhe. Almas Athuman Maige Mhe. Cecilia Daniel Paresso Mhe. Savelina Silvanus Mwijage WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO Swali Na. 211: Mhe. Daniel Edward Mtuka Nyongeza: Mhe. Daniel Edward Mtuka Mhe. Daimu Iddy Mpakate Swali Na. 212: Mhe. Mussa Bakari Mbarouk Nyongeza: Mhe. Mussa Bakari Mbarouk Mhe. Saumu Heri Sakala Mhe. Moshi Selemani Kakoso Swali Na. -
1458125901-Hs-15-39
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 24 Juni, 2014 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anna S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu! MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaanza Maswali na Ofisi ya Waziri Mkuu, atakayeuliza swali la kwanza Mheshimiwa Maryam Salum Msabaha. Na. 293 Tatizo la Uchafu Katika Jiji la Dar es Salaam MHE. MARYAM S. MSABAHA aliuliza:- Jiji la Dar es Salaam linaongoza kwa uchafu na ombaomba, jambo ambalo linasababisha kero kwa wakazi wake na wageni wanaofika nchini. (a) Je, Serikali ina mikakati gani ya kumaliza tatizo la ukusanyaji wa taka katika Jiji hilo? 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) (b) Je, Serikali inasema nini katika kutumia taka kutengeneza vitu vingine kama mbolea au kutumia taka hizo kufua umeme kama zinavyofanya nchi nyingine? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Salum Msabaha, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, changamoto inayolikabili Jiji la Dar es Salaam kuhusu usafi ni kuwepo kwa kiwango kikubwa cha uzalishaji wa taka ikilinganishwa na uwezo wa Jiji kuzoa taka hizo. Uzalishaji wa taka katika Jiji kwa sasa ni wastani wa tani 4,252 kwa siku wakati uwezo uliopo wa kuzoa taka ni wastani wa tani 2,126 kiasi cha 50% kwa siku. Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na changamoto hii Jiji limetumia shilingi bilioni moja (bilioni 1) kwa ajili ya kununulia mtambo mpya wa kusukuma taka, yaani Buldozer D.8, ununuzi wa malori mawili yenye tani 18 kwa ajili ya kuzoa taka na ununuzi wa Compactor moja kwa ajili ya kushindilia taka. -
3 APRILI 2019.Pmd
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _______ MAJADILIANO YA BUNGE _______ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Pili - Tarehe 3 Aprili, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa, tukae. Waheshimiwa Wabunge, leo ni Kikao cha Pili cha Mkutano wa Kumi na Tano, tunaendelea. Katibu. NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI SPIKA: Hati za kuwasilishwa Mezani, Ofisi ya Waziri Mkuu, tafadhali. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU:- Taarifa ya Matoleo ya Gazeti la Serikali pamoja na nyongeza zake yaliyochapishwa tangu Mkutano wa Bunge uliopita kama ifuatavyo:- Toleo Na. 04 la tarehe 25 Januari, 2019; Toleo Na. 05 la tarehe 01 Februari, 2019; Toleo Na. 06 la tarehe 08 Februari, 2019; Toleo Na. 07 la tarehe 15 Februari, 2019; Toleo Na. 08 la tarehe 22 Februari, 2019; 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Toleo Na. 09 la tarehe 01 Machi, 2019; Toleo Na. 10 la tarehe 08 Machi, 2019; Toleo Na. 11 la tarehe 15 Machi, 2019; na Toleo Na. 12 la tarehe 22 Machi, 2019. Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Taasisi zilizo chini yake kwa mwaka wa fedha, 2019/2020. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu. Katibu. NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Maswali leo tunaanza na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, swali la Mheshimiwa Ahmed Ally Salum Mbunge wa Solwa. Kwa niaba yake, ahsante nakuruhusu. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE ________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Nne – Tarehe 16 Agosti, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hazi zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. MUSTAFA HAIDI MKULO): Taarifa ya Mwaka na Hesabu Zilizokaguliwa za Consolidated Holding Corporation kwa mwaka ulioishia tarehe 31 Desemba, 2005 (The Annual Report and Audited Accounts of the Consolidated Holding Corporation for the year ended 31st December, 2005) MASWALI NA MAJIBU Na. 413 Nyumba kwa Wafanyakazi MHE. MKIWA A. KIMWANGA (k.n.y. MHE. SAVELINA S. MWIJAGE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwatafutia nyumba za kuishi wafanyakazi wapya wanaoajiriwa au kuhamishwa na kupangiwa vituo vya kazi nje ya Mikoa yao? NAIBU WAZIRI WA MIUNDOMBINU (MHE. DR. MILTON M. MAHANGA) alijibu:- Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Savelina Silvanus Mwijage, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, kwa kawaida, Serikali ina wajibu wa kuwatafutia nyumba wafanyakazi na viongozi wenye stahili ya kupewa nyumba na Serikali kwa mujibu wa 1 masharti ya ajira zao. Kwa hiyo, wafanyakazi wa aina hii, wawe wapya au wanaohamishwa na kupangiwa vituo vipya vya kazi, hupewa nyumba au posho ya nyumba pale ambapo nyumba ya Serikali haijapatikana. Serikali haina jukumu la kimkataba kuwatafutia nyumba watumishi wengine wasio na stahili. Hata hivyo, kutokana na uamuzi wa Serikali wa kuuzia watumishi na viongozi wa Serikali nyumba za zamani walizokuwa wanaishi, watumishi na viongozi wa aina hii na ambao wana stahili, wanapohamishwa wakati wamekwishauziwa nyumba katika vituo vyao vya zamani, wanategemewa kupanga nyumba kibiashara au katika nyumba za wakala zilizotengwa kupangishwa kibiashara. -
ESRF FACILITATES the DEVELOPMENT of REGIONAL INVESTMENT GUIDES in Response to the Call Made by Hon
VOLUME 19, NUMBER 2 ISSN 0856 - 5791 JULY - DECEMBER, 2019 ESRF FACILITATES THE DEVELOPMENT OF REGIONAL INVESTMENT GUIDES In response to the call made by Hon. Kassim Majaliwa - the Prime Minister of the United Republic of Tanzania that every region in Tanzania should have an Investment Guide, eight ( 8) Regions have launched their guides in this second half of the year 2019. These Guides intent to avail investment information to potential investors; individuals, firms and institutions from within the country and outside with the view of attracting them to exploit the regions’ rich investment potentials. The regions which launched their Investment Guides included; Dodoma, Hon. Kassim Majaliwa - The Prime Minister United Republic of Tanzania cutting Ruvuma, Kagera, Manyara, Geita, a ribbon to mark the official launch of Mtwara Region Investment Guide. On Pwani, Mtwara and Lindi. Some of his left are: Hon. Angellah Kairuki - Minister of State in Prime Minister’s Office - the launching ceremonies were done Investment, Dr. Tausi Kida - Executive Director ESRF and Hon. Japhet Hasunga during the Regional Investment Forums - Minister of Agriculture. On his right are: Ms. Christine Musisi - UNDP Resident Representative and Hon. Gelasius Byakanwa - Mtwara Regional Commissioner. >>> Page 2 INSIDE THIS ISSUE GRAIN STAKEHOLDERS MEET IN DAR TO DISCUSS OPPORTUNITIES Editorial ...................................................2 Strategic Research and Publications ......3 Between 28th – 29th August, would provide grain stakeholders Commissioned Research -
Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1 BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA K
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Tano - Tarehe 21 Machi, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Mussa A. Zungu) Alisoma Dua MWENYEKITI: Tukae. Katibu! MISWADA YA SHERIA YA SERIKALI Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Stakabadhi Ghalani wa Mwaka 2014 (The Warehouse ReceiptS( Amendment) Bill, 2014) (Kusomwa Mara ya Pili) NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja kwamba mapendekezo ya Marekebisho ya Sheria ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghalani wa Mwaka 2014 (The Warehouse Receipts (Amendment) Bill, 2014) sasa usomwe mbele ya Bunge lako Tukufu kwa mara ya pili. Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kukushukuru sana wewe binafsi, Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamati ya Uchumi, Viwanda na Biashara na Mwenyekiti mwenza na Wajumbe wa Kamati ya Kilimo Mifugo na Maji, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na wadau wa mfumo wa Stakabadhi za Ghala kwa mapendezo na maoni yao ya kurekebisha sheria hii kwa lengo la kuboresha Muswada huu. Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumo wa Stakabadhi za Ghala ni mfumo unaorasimisha matumizi ya bidhaa kwa kupata stakabadhi kwa ajili ya kuhifadhi, kufanya biashara na huduma za kifedha kama benki na kadhalika. Stakabadhi hiyo inaonesha umiliki, kiasi, ubora na thamani ya bidhaa husika. Mfumo huu ulipitishwa kwa Sheria ya Bunge Namba 10 ya mwaka 2005 na kuanza kutumika rasmi mwaka 2007 baada ya Kanuni zake kupitishwa mwaka 2006. Hadi kufikia Desemba 2014, mfumo huu umetumika kwenye mazao ya korosho, kahawa, ufuta, alizeti, mahindi, mpunga na mbaazi na kuwezesha tani 950,000 za mazao kuuzwa. -
Tarehe 5 Aprili, 2006
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Saba – Tarehe 5 Aprili, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samwel John Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na :- NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Taarifa ya Mwaka wa Hesabu zilizokaguliwa na Hifadhi za Taifa Tanzania kwa Mwaka ulioishia tarehe 30 Juni, 2005 [The Annual Report and Audited Accounts of the Tanzania National Parks for the year ended 30th June, 2005] NAIBU WAZIRI WA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA:- Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Bodi ya Sukari Tanzania kwa Mwaka ulioishia tarehe 30 Juni, 2005 (The Annual Report and Accounts of the Sugar Board of Tanzania for the year ended 30th June, 2005) Taarifa ya Ishirini ya Utendaji na Hesabu za Bodi ya Tumbaku Tanzania kwa Mwaka ulioishia tarehe 31 Machi, 2005 (The 20th Annual Performance Report and Audited Accounts of the Tanzania Tobacco Board for the year ended 31st March, 2005) MASWALI NA MAJIBU Na. 90 Chakula cha Njaa Wilaya Mpwapwa 1 MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Kwa kuwa, Wilaya ya Mpwapwa ina Tarafa tatu (3) Kata Kumi na nane (18) na Vijiji Themanini na nne (84) na wakazi wapatao 254,000 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2002, na kwa kuwa katika tathmini ya tatizo la njaa iliyofanyika Januari, 2006 imeonekana kuwa watu wengi wana tatizo kubwa la njaa kwa mwezi Februari, 2006 Wilaya hiyo ilipata tani 449 tu na mahitaji halisi ni zaidi ya tani 2000 kwa mwezi. -
1458123221-Hs-15-26
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini na Sita – Tarehe 4 Juni, 2014 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE: MWIGULU L. M. MCHEMBA): Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Fedha kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. ESTHER L. M. MIDIMU (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA UCHUMI, VIWANDA NA BIASHARA): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Viwanda na Biashara Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Fedha kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE.CHRISTINA M. LISSU (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KWA WIZARA YA FEDHA): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani, kwa Wizara ya Fedha Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Swali letu la kwanza kama ilivyo ada linaelekezwa Ofisi ya Waziri Mkuu na linaulizwa na Mheshimiwa Agripina Zaituni Buyogera, Mbunge wa Kasulu Vijijini. Kwa niaba yake Mheshimiwa Rajab Mbarouk Mohammed. Na. 182 Uwekezaji Kwenye Pori la Makere Kusini MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED (K.n.y. MHE. AGRIPINA Z. BUYOGERA) aliuliza:- 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) Licha ya kwamba kuna uwekezaji unaoendelea kwenye Pori la Makere Kusini (Kagera Nkanda) katika Jimbo la Kasulu Vijijini; bado kuna -
Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Nane – Tarehe 5 Septemba, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Hiki ni Kikao cha nane cha Mkutano wetu wa kumi na mbili. Nawakaribisheni nyote, Katibu. MASWALI KWA WAZIRI MKUU NAIBU SPIKA: Maswali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu. Nina orodha ya Wabunge 15 kama ambavyo nimekuwa nikisisitiza ni vizuri yeyote atakayepata nafasi kuuliza swali aulize kwa kifupi iwezekanavyo, kama kuna la nyongeza vile vile kwa kifupi iwezekanavyo ili kuwapa nafasi Wabunge wengine wenye nia ya kuuliza maswali. Kama ilivyo ada tunaanza na Mheshimiwa Kiongozi wa Upinzani Bungeni endapo ana swali. 1 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) MHE. FREEMAN A. MBOWE: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru kunipa nafasi ya kumwuliza Mheshimiwa Waziri Mkuu swali. Mheshimiwa Waziri Mkuu nchi yetu sasa iko katika kipindi kigumu ambapo Taifa linashiriki mchakato wa kuipata Katiba mpya ya Taifa letu. Ni dhahiri kwamba mchakato wa kuipata Katiba mpya unahitaji ustahimilivu, ushirikiano, uwazi, ukweli, dhamira njema na kipekee sisi ambao ni Wabunge ndani ya Bunge hili tunatambua na tunastahili kutambua kwamba wako wadau wengi sana nje ya Bunge hili ambao nao ni wadau kama sisi katika mustakabali mzima wa Katiba. Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa matukio ambayo yalitokea juana ndani ya Bunge lako, panaonekana kuwepo ufa mkubwa ambao unaweza ukafanya dhamira njema ya kuiandika upya Katiba ya Taifa letu ikapata ufa mkubwa katika hatua hii ya kutunga na kurekebisha Sheria hii.