3 APRILI 2019.Pmd
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Thelathini Na Sita
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Sita – Tarehe 27 Mei, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nawaomba tukae. Waheshimiwa Wabunge tunaendelea na Mkutano wetu wa 15, leo ni Kikao cha 36. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NAIBU WAZIRI WA MADINI: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2019/2020. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. CATHERINE V. MAGIGE - K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI) Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu utekelezaji na Majukumu ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. MHE. TUNZA I. MALAPO - K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU WIZARA YA MADINI: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni juu ya Wizara ya Madini kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Tunza Malapo, tunakushukuru. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Tunaanza na TAMISEMI, swali la kwanza litaulizwa na Mheshimiwa Azza Hilal, Mbunge wa Viti Maalum - Shinyanga. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA KUMI NA SITA ______________ Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 27 Julai, 2009) (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita anayeuliza swali la kwanza, karibuni tena baada ya mapumziko ya weekend, nadhani mna nguvu ya kutosha kwa ajili ya shughuli za wiki hii ya mwisho ya Bunge hili la 16. Swali la kwanza linaelekezwa Ofisi ya Waziri Mkuu na linauliza na Mheshimiwa Shoka, kwa niaba yake Mheshimiwa Khalifa. Na.281 Kiwanja kwa Ajili ya Kujenga Ofisi ya Tume ya Kudhibiti UKIMWI MHE KHALIFA SULEIMAN KHALIFA (K.n.y. MHE. SHOKA KHAMIS JUMA) aliuliza:- Kwa kuwa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI inakabiliwa na changamoto ya ufinyu wa Ofisi; na kwa kuwa Tume hiyo imepata fedha kutoka DANIDA kwa ajili ya kujenga jengo la Ofisi lakini inakabiliwa na tatizo kubwa la upatikanaji wa kiwanja:- Je, Serikali itasaidia vipi Tume hiyo kupata kiwanja cha kujenga Ofisi? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU – SERA, URATIBU NA BUNGE alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shoka Khamis Juma, Mbunge wa Micheweni kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, tatizo la kiwanja cha kujenga Ofisi za TACAIDS limepatiwa ufumbuzi na ofisi yangu imewaonesha Maafisa wa DANIDA kiwanja hicho Ijumaa tarehe 17 Julai, 2009. Kiwanja hicho kipo Mtaa wa Luthuli Na. 73, Dar es Salaam ama kwa lugha nyingine Makutano ya Mtaa wa Samora na Luthuli. MHE. KHALIFA SULEIMAN KHALIFA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Waziri, naomba kumuuliza swali moja la nyongeza. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 18 Julai, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita muuliza swali la kwanza nina matangazo kuhusu wageni, kwanza wale vijana wanafunzi kutoka shule ya sekondari, naona tangazo halisomeki vizuri, naomba tu wanafunzi na walimu msimame ili Waheshimiwa Wabunge waweze kuwatambua. Tunafurahi sana walimu na wanafunzi wa shule zetu za hapa nchini Tanzania mnapokuja hapa Bungeni kujionea wenyewe demokrasia ya nchi yetu inavyofanya kazi. Karibuni sana. Wapo Makatibu 26 wa UWT, ambao wamekuja kwenye Semina ya Utetezi na Ushawishi kwa Harakati za Wanawake inayofanyika Dodoma CCT wale pale mkono wangu wakulia karibuni sana kina mama tunawatakia mema katika semina yenu, ili ilete mafanikio na ipige hatua mbele katika kumkomboa mwanamke wa Tanzania, ahsanteni sana. Hawa ni wageni ambao tumetaarifiwa na Mheshimiwa Shamsa Selengia Mwangunga, Naibu Waziri wa Maji. Wageni wengine nitawatamka kadri nitakavyopata taarifa, kwa sababu wamechelewa kuleta taarifa. Na. 223 Barabara Toka KIA – Mererani MHE. DORA H. MUSHI aliuliza:- Kwa kuwa, Mererani ni Controlled Area na ipo kwenye mpango wa Special Economic Zone na kwa kuwa Tanzanite ni madini pekee duniani yanayochimbwa huko Mererani na inajulikana kote ulimwenguni kutokana na madini hayo, lakini barabara inayotoka KIA kwenda Mererani ni mbaya sana -
MKUTANO WA 18 TAREHE 5 FEBRUARI, 2015 MREMA 1.Pmd
5 FEBRUARI, 2015 BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE __________________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Tisa – Tarehe 5 Februari, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, leo sijamwona. Kwa hiyo tunaendelea na Maswali kwa Waziri Mkuu na atakayeanza ni Mheshimiwa Murtaza A. Mangungu. MHE. MURTAZA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa vipindi tofauti vya Bunge Mheshimiwa Peter Msigwa, Mheshimiwa Mussa Zungu na hata Mheshimiwa Murtaza A. Mangungu wamekuwa wakiuliza swali kuhusiana na manyanyaso wanayoyapata wafanyabiashara Wadogo Wadogo pamoja na Mamalishe. Kwa kipindi hicho chote umekuwa ukitoa maagizo na maelekezo, inavyoonekana mamlaka zinazosimamia hili jambo haziko tayari kutii amri yako. 1 5 FEBRUARI, 2015 Je, unawaambia nini Watanzania na Bunge hili kwa ujumla? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba nimjibu Mheshimiwa Murtaza Mangungu swali lake kama ifuatavyo:- Suala hili la vijana wetu ambao tunawajua kama Wamachinga, kwanza nataka nikiri kwamba ni suala kubwa na ni tatizo kubwa na si la Jiji la Dar es Salaam tu, bali lipo karibu katika miji mingi. Kwa hiyo, ni jambo ambalo lazima twende nalo kwa kiwango ambacho tutakuwa na uhakika kwamba tunalipatia ufumbuzi wa kudumu. Kwa hiyo, ni kweli kwamba mara kadhaa kuna maelekezo yametolewa yakatekelezwa sehemu na sehemu nyingine hayakutekelezwa kikamilifu kulingana na mazingira ya jambo lenyewe lilivyo. Lakini dhamira ya kutaka kumaliza tatizo hili la Wamachinga bado ipo palepale na kwa bahati nzuri umeuliza wakati mzuri kwa sababu jana tu nimepata taarifa ambayo nimeandikiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI ambayo wanaleta mapendekezo kwangu juu ya utaratibu ambao wanafikiri unaweza ukatatua tatizo hili ambalo lipo sehemu nyingi. -
MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao Cha Arobaini Na Moja
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Moja – Tarehe 31 Mei, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Tunaanza kikao chetu cha Arobaini na Moja, Katibu. NDG. LINA KITOSI – KATIBU MEZANI:- HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2018/19. MHE. CATHERINE V. MAGIGE (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu utekelezaji wa Bajeti na Majukumu ya Wizara 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019. MWENYEKITI: Ahsante. Katibu. NDG. LINA KITOSI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Swali letu la kwanza linaelekezwa Ofisi ya Waziri Mkuu na linaulizwa na Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, kwa niaba yake Mheshimiwa Amina Mollel. Na. 341 Utekelezaji wa Mpango wa Ukimwi 90-90-90 MHE. AMINA S. MOLLEL (K.n.y MHE. HAWA M. CHAKOMA) aliuliza:- Je, Serikali inatekelezaje Mpango wa UKIMWI wa 90- 90-90? MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Mollel. Majibu, Mheshimiwa Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA NA VIJANA) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Ishirini na Saba - Tarehe 9 Julai, 2010 (Mkutano ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anna S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZlLIZOWASILISHWA MEZANI: Hati Zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha, 2010/2011. MHE. WILLIAM H. SHELLUKINDO - MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya ya Nishati na Madini Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. MHE.SAVELINA S. MWIJAGE (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMATI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA NISHATI NA MADINI): Taarifa ya Msemaji wa Mkuu wa Kambi ya Upinzani Kuhusu Makadiro ya Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI (MHE. MWANTUMU BAKARI MAHIZA): 1 Randama za Makadiro ya Matumizi ya Wizara ya Elimu na Mfunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI (MHE. OMAR YUSSUF MZEE): Taarifa ya Majumuisho ya Mpango Mkakati wa Kujibu Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu za Wizara, Idara za Serikali na Mikoa kwa Mwaka wa Fedha 2008/2009. MASWALI NA MAJIBU Na. 191 Kuhusu Barabara ya Makutupa Bumila Jimbo la Mpwapwa MHE. GEOREGE M. -
MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NANE Kikao Cha
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Kumi na Tatu – Tarehe 29 Juni, 2007 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii kwa Kuwasilisha Hati. Naomba niwashukuru nyote jinsi tulivyoshirikiana kwa pamoja kuweza kumsindikiza mwenzetu Marehemu Amina Chifupa Mpakanjia, katika safari yake ya mwisho. Waheshimiwa Wabunge, napenda niwashukuru Kamati ya Uongozi na Tume ya Huduma za Bunge, lakini pia TWPG kwa kushirikiana vizuri sana kuweza kumsindikiza mwenzetu kwa heshima; na kipekee naomba Mheshimiwa Waziri Mkuu atutolee salamu za shukrani kwa Mheshimiwa Rais kwa jinsi ambavyo Mheshimiwa Rais alivyokuwa karibu nasi kila dakika kwa mawasiliano hadi hapo jana kule Njombe. Waheshimiwa Wabunge, narejea tena Mungu ailaze roho ya Marehemu Mheshimiwa Amina Chifupa Mpakanjia, mahali pema peponi. Amin. Hati ifuatayo iliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Shirika la Hifadhi ya Taifa (TANAPA) kwa mwaka 2005/2006 (The Annual Report and Accounts of the Tanzania National Parks for the Year 2005/2006). MASWALI NA MAJIBU Na. 106 Ubovu wa Barabara za Jiji la Dar es Salaam MHE. MUSSA A. ZUNGU aliuliza:- 1 Kwa kuwa sura ya nchi yetu iko katika Jimbo la Ilala; na kwa kuwa barabara nyingi za Jiji la Dar es Salaam ni mbovu sana hali inayosababisha msongamano wa magari na -
Bunge La Tanzania ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Moja – Tarehe 11 Agosti, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. MUSTAFA H. MKULO): Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Benki ya Uwekezaji Tanzania kwa Mwaka ulioishia Tarehe 31 Desemba, 2005 (The Annual Report and Accounts of the Tanzania Investment Bank Limited for the Year ended 31st December, 2005) NAIBU WAZIRI WA MIPANGO, UCHUMI NA UWEZESHAJI: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Mipango, Uchumi na Uwezeshaji kwa Mwaka wa Fedha 2006/2007. MHE. ADAM K. A. MALIMA - MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA FEDHA NA UCHUMI): Maoni ya Kamati ya Fedha na Uchumi kuhusu Utekelezaji wa Wizara ya Mipango, Uchumi na Uwezeshaji kwa Mwaka wa Fedha Uliopita pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka 2006/2007. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI: Maoni ya Kambi ya Upinzani kuhusu Utekelezaji wa Wizara ya Mipango, Uchumi na Uwezeshaji kwa Mwaka wa Fedha Uliopita, pamoja na Maoni kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka 2006/2007. SPIKA: Kabla ya kumwita mwuliza swali la kwanza kwa leo natangaza tu kwamba kama ilivyo kawaida wageni tutawatangaza mara baada ya kipindi cha maswali . 1 MASWALI NA MAJIBU Na. 385 Kuboresha Hospitali ya Mkoa wa Morogoro MHE. DR. OMARI M. NIBUKA aliuliza: - Kwa kuwa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro ilijengwa -
Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania Mkutano Wa Saba Yatokanayo Na Kikao Cha Ishirini Na Sita 16 Mei, 2017
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA ISHIRINI NA SITA 16 MEI, 2017 MKUTANO WA SABA KIKAO CHA ISHIRINI NA SITA TAREHE 16 MEI, 2017 I. DUA: Saa 3:00 asubuhi Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mwenyekiti) alisoma Dua na kuongoza Bunge. Makatibu mezani: 1. Ndugu Theonest Ruhilabake 2. Ndugu Asia Minja 3. Ndugu Joshua Chamwela II. HATI ZA KUWASILISHA MEZANI (i) Mhe. Charles John Mwijage aliwasilisha Mezani Randama ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (ii) Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi aliwasilisha Mezani Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (iii) Mhe. Jumanne Kidera Kishimba aliwasilisha Mezani Taarifa ya Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (iv) Mhe. Masoud Abdallah Salim aliwasilisha Mezani Taarifa ya Kambi ya Upinzani kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. 1 III. MASWALI OFISI YA RAIS (TAMISEMI) Swali Na. 209: Mhe. Dkt. Pudenciana Kikwembe Nyongeza: Mhe. Dkt. Pudenciana Kikwembe Mhe. Pauline Gekul Mhe. David Cosato Chumi Swali Na. 210: Mhe. Eng. Atashasta Justus Nditiye Nyongeza: Mhe. Eng. Atashasta Justus Nditiye Mhe. Josephine Johnson Genzabuke Mhe. Almas Athuman Maige Mhe. Cecilia Daniel Paresso Mhe. Savelina Silvanus Mwijage WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO Swali Na. 211: Mhe. Daniel Edward Mtuka Nyongeza: Mhe. Daniel Edward Mtuka Mhe. Daimu Iddy Mpakate Swali Na. 212: Mhe. Mussa Bakari Mbarouk Nyongeza: Mhe. Mussa Bakari Mbarouk Mhe. Saumu Heri Sakala Mhe. Moshi Selemani Kakoso Swali Na. -
Online Document)
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Saba - Tarehe 5 Februari, 2020 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Naomba tukae Waheshimiwa. Tunaendelea na Mkutano wetu wa Kumi na Nane, leo ni Kikao chetu cha Saba. Katibu. NDG. YONA KIRUMBI - KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI – K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019. MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Sebastian Kapufi. Nakushukuru sana kwa niaba ya Kamati. Sasa namwita Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini. Karibu Mheshimiwa Mariam Ditopile, Makamu Mwenyekiti MHE. MARIAM D. MZUZURI – MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019. (Makofi) SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Mariam. Katibu. NDG. YONA KIRUMBI - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Maswali, tunaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Swali la kwanza linaulizwa na Mheshimiwa Raphael Japhary Michael, Mbunge wa Moshi Mjini, Mheshimiwa Japhary, uliza swali lako tafadhali. 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Na. 81 Hitaji la Hospitali ya Wilaya - Manispaa ya Moshi MHE. RAPHAEL J. MICHAEL aliuliza:- Halmashauri ya Manispaa ya Moshi haina Hospitali ya Wilaya na kuifanya Hospitali ya Mkoa ya Mawenzi izidiwe na idadi ya wagonjwa:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha ili kujenga Hospitali ya Wilaya katika Manispaa ya Moshi? SPIKA: Majibu ya swali hilo Mheshimiwa Naibu Waziri, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mheshimiwa Kandege, tafadhali. -
1458125901-Hs-15-39
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 24 Juni, 2014 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anna S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu! MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaanza Maswali na Ofisi ya Waziri Mkuu, atakayeuliza swali la kwanza Mheshimiwa Maryam Salum Msabaha. Na. 293 Tatizo la Uchafu Katika Jiji la Dar es Salaam MHE. MARYAM S. MSABAHA aliuliza:- Jiji la Dar es Salaam linaongoza kwa uchafu na ombaomba, jambo ambalo linasababisha kero kwa wakazi wake na wageni wanaofika nchini. (a) Je, Serikali ina mikakati gani ya kumaliza tatizo la ukusanyaji wa taka katika Jiji hilo? 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) (b) Je, Serikali inasema nini katika kutumia taka kutengeneza vitu vingine kama mbolea au kutumia taka hizo kufua umeme kama zinavyofanya nchi nyingine? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Salum Msabaha, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, changamoto inayolikabili Jiji la Dar es Salaam kuhusu usafi ni kuwepo kwa kiwango kikubwa cha uzalishaji wa taka ikilinganishwa na uwezo wa Jiji kuzoa taka hizo. Uzalishaji wa taka katika Jiji kwa sasa ni wastani wa tani 4,252 kwa siku wakati uwezo uliopo wa kuzoa taka ni wastani wa tani 2,126 kiasi cha 50% kwa siku. Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na changamoto hii Jiji limetumia shilingi bilioni moja (bilioni 1) kwa ajili ya kununulia mtambo mpya wa kusukuma taka, yaani Buldozer D.8, ununuzi wa malori mawili yenye tani 18 kwa ajili ya kuzoa taka na ununuzi wa Compactor moja kwa ajili ya kushindilia taka.