Majadiliano Ya Bunge ______
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA TATU Kikao Cha Thelathini Na Saba
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Thelathini na Saba – Tarehe 6 Juni, 2016 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu! NDG. ZAINAB ISSA - KATIBU MEZANI: Maswali. MASWALI NA MAJIBU Na. 303 Upanuzi wa Hospitali ya Mkoa wa Pwani MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:- Upanuzi wa hospitali ya Mkoa ya Pwani ijulikanayo kama Hospitali ya Tumbi umesimama kwa takribani miaka mitatu, sasa nondo na zege la msingi na nguzo zinaoza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo ili kuondoa hasara na kuleta tija katika huduma ya afya Kibaha? 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Silvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua changamoto zinazoikabili hospitali ya rufaa ya Tumbi – Kibaha ambazo zimesababishwa kwa sehemu kubwa na ufinyu wa majengo ya kutolea huduma na uchache wa vifaa tiba. Hadi sasa Serikali imetumia shilingi bilioni 5.98 kwa ajili ya upanuzi wa hospitali hiyo. Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 imetenga shilingi bilioni 1.4 kwa ajili ya kuendeleza upanuzi wa hospitali ya Tumbi Kibaha ili kuboresha huduma za afya kwa wananchi. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Silvestry Koka, swali la nyongeza. MHE. SILVESTRY F. KOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali na kwa niaba ya wananchi wa Kibaha nishukuru kwa kutupatia hiyo 1.4 bilioni katika upanuzi wa hospitali hii, nina maswali mawili ya nyongeza. -
20 Juni, 2013
20 JUNI, 2013 BUNGE LA TANZANIA _____________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Tatu – Tarehe 20 Juni, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua KIAPO CHA UTII Mbunge afuataye alikula Kiapo cha Utii na Kukaa katika nafasi yake Bungeni:- Mhe. Yussuf Salim Hussein. MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kufuatana na Kanuni yetu, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani hayupo, kwa hiyo, nitaenda moja kwa moja kumwita anayefuatia, Mheshimiwa Rashid Ali Abdallah! MHE. RASHID ALI ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza, sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu, kwa kunijalia leo hii kusimama hapa. Mheshimiwa Waziri Mkuu, rushwa na ufisadi vinaliangamiza Taifa letu. Hivi karibuni tulimsikia Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akisikitishwa sana na jinsi rushwa ilivyokithiri katika Chaguzi za Chama chake. Tarehe 16 tumemsikia Spika akikemea na kusikitishwa na rushwa. Siyo hao tu, tumemsikia Jaji Kiongozi wa 1 20 JUNI, 2013 Mahakama Kuu ya Tanzania, akisikitishwa pia na suala la rushwa. Mihimili yote mitatu inalalamika kuhusu rushwa ilivyokithiri. Je, Serikali ina mikakati gani madhubuti ya kuweza kudhibiti au kuondoa rushwa hii? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Rashid Ali Abdallah, swali lake zuri sana kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, kwanza, niseme kwamba, Viongozi hawa wanaposema siyo kwamba wanalalamika, ni namna ya kuwatahadharisha Watanzania, muda wote wakae wanajua kwamba rushwa siyo jambo zuri, ni jambo la hovyo. Huo ndiyo ujumbe ambao wote wanajaribu kutupa. Hata Bungeni, mnapokuwa mna jambo, juzi nili- attend ule Mkutano wa APNAC, yale siyo malalamiko ni namna ya kuwaambia Wananchi na Watanzania juu ya uovu wa jambo hili. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Kumi na Tatu – Tarehe 10 Februari, 2010 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI (MHE. OMAR YUSSUF MZEE): Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Benki ya Posta Tanzania, kwa Mwaka 2008 [The Annual Report and Accounts of The Tanzania Postal Bank for the Year 2008]. The Mid-Term Review of the Monetary Policy Statement of The Bank of Tanzania for the Year 2009/2010. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini juu ya Taarifa ya Serikali Kuhusu Ubinafsishwaji wa Mgodi wa Kiwira. Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Mchakato wa Zabuni ya Kuzalisha Umeme wa Dharura Ulioipa Ushindi Kampuni ya Richmond Development Company LLC. Houston Texas - Marekani Mwaka 2006. MWENYEKITI WA KAMATI YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Miundombinu Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelzaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Uendeshaji Usioridhisha wa Shirika la Reli Tanzania uliofanywa na Kampuni ya RITES ya India. 1 Taarifa ya Kamati ya Miundombinu Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Utendaji wa Kazi Usioridhisha wa Kampuni ya TICTS. MASWALI NA MAJIBU Na. 145 Usimamizi wa Ukaguzi wa Fedha za Halmashauri MHE. HERBERT J. MNTANGI aliuliza:- Kwa kuwa, kiasi cha fedha kinachopelekwa katika Halmashauri za Wilaya, Manispaa na Jiji ni kikubwa na kinahitaji usimamizi wa ziada:- Kwa kuwa kitengo cha ukaguzi wa ndani kipo chini ya Mkurugenzi Mtendaji. -
TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity?
TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? With Partial Support from a TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? ACKNOWLEDGEMENTS This review was compiled and edited by Tanzania Development Research Group (TADREG) under the supervision of the Steering Group of Policy Forum members, and has been financially supported in part by Water Aid in Tanzania and Policy Forum core funders. The cartoons were drawn by Adam Lutta Published 2013 For more information and to order copies of the review please contact: Policy Forum P.O Box 38486 Dar es Salaam Tel: +255 22 2780200 Website: www.policyforum.or.tz Email: [email protected] ISBN: 978-9987 -708-09-3 © Policy Forum The conclusions drawn and views expressed on the basis of the data and analysis presented in this review do not necessarily reflect those of Policy Forum. Every effort has been made to verify the accuracy of the information contained in this review, including allegations. Nevertheless, Policy Forum cannot guarantee the accuracy and completeness of the contents. Whereas any part of this review may be reproduced providing it is properly sourced, Policy Forum cannot accept responsibility for the consequences of its use for other purposes or in other contexts. Designed by: Jamana Printers b TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? TABLE OF CONTENTS POLICY FORUM’s OBJECTIVES ............................................................................................................. -
MKUTANO WA TATU Kikao Cha Hamsini Na Sita
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Hamsini na Sita – Tarehe 22 Juni, 2021 (Bunge Lilianza saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba tukae. Waheshimiwa tunaendelea na Mkutano wetu wa Tatu, leo ni Kikao cha Hamsini na Sita na kabla hatujaendelea nitumie nafasi hii kuwashukuru sana wasaidizi wangu wote wakiongozwa na Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa David Kihenzile, Mheshimiwa Zungu na Mheshimiwa Najma kwa kazi nzuri ambayo wameifanya wiki nzima kutuendeshea mjadala wetu wa bajeti. (Makofi) Sasa leo hapa ndio siku ya maamuzi ambayo kila Mbunge anapaswa kuwa humu ndani, kwa Mbunge ambaye Spika hana taarifa yake na hatapiga kura hapa leo hilo la kwake yeye. (Makofi) Katibu. NDG. NENELWA MWIHAMBI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Maswali na tunaanza na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Kwela. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Na. 465 Ujenzi wa Makao Makuu ya Halmashauri Katika Mji wa Laela MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi za Makao Makuu ya Halmashauri ya Sumbawanga katika Mji wa Laela baada ya agizo la Serikali la kuhamisha Makao Makuu? SPIKA: Majibu ya swali hilo muhimu la watu wa Kwela, Mheshimiwa Naibu Waziri - TAMISEMI, Mheshimiwa Dkt. Festo Dugange tafadhali. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Jimbo la Kwela kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ni miongoni mwa Halmashauri 30 zilizohamia kwenye maeneo mapya ya utawala mwaka 2019. -
Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Pili – Tarehe 13 Mei, 2015 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu! MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa, maswali tunaanza na ofisi ya Waziri Mkuu, anayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Josephine J. Genzabuke, kwa niaba yake Mheshimiwa Likokola! Na. 11 Fedha za Mfuko wa JK kwa Wajasiriamali Wadogo MHE. DEVOTHA M. LIKOKOLA (K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE) aliuliza:- Mfuko wa Wajasiriamali wadogowadogo maarufu kama mabilioni ya JK uliwavuta wengi sana lakini masharti ya kupata fedha hizo yamekuwa magumu:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kufanya mpango huo uwe endelevu kwa lengo la kuwanufaisha wanyonge? (b) Je, ni wananchi wangapi wa Mkoa wa Kigoma wamenufaika na mpango huo? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007, Serikali ilianzisha mpango wa uwezeshaji wananchi kiuchumi na kuongeza ajira kwa kutoa mikopo yenye masharti nafuu. Lengo la mpango huu ni kuwawezesha wananchi mijini na vijijini kupata mikopo ya kuanzisha au kuendeleza shughuli za kiuchumi ili kuongeza ajira na kipato. Masharti ya kupata mikopo hii si magumu sana ikilingalishwa na ile inayotolewa na mabenki, kwa sababu riba inayotozwa kwa mikopo hii ni asilimia 10, ikilinganishwa na riba inayotozwa na mabenki mengine, ambayo ni zaidi ya asilimia 20. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Mbili - Tarehe 22 Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kwa masikitiko makubwa natoa taarifa kwamba Mheshimiwa Mussa Hamisi Silima, Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar, jana Jumapili, tarehe 21 Agosti, 2011 majira ya jioni kama saa mbili kasorobo hivi walipokuwa wakirejea kutoka Dar es Salaam, yeye na familia yake walipata ajali mbaya sana katika eneo la Nzuguni, Mjini Dodoma. Katika ajali hiyo, mke wa Mbunge huyo aitwaye Mwanaheri Twalib amefariki dunia na mwili wa Marehemu upo hospitali ya Mkoa hapa Dodoma ukiandaliwa kupelekwa Zanzibar leo hii Jumatatu, tarehe 22 August, 2011 kwa mazishi yatanayotarajiwa kufanyanyika alasili ya leo. Kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Wabunge tusimame dakika chache tumkumbuke. (Heshima ya Marehemu, dakika moja) (Hapa Waheshimiwa Wabunge walisimama kwa dakika moja) Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, amina. Ahsanteni sana, tukae. Kwa hiyo sasa hivi tunavyoongea Mheshimiwa Mbunge ambae nae pia ameumia vibaya na dereva wake wanaondoka na ndege sasa hivi kusudi waweze kupata yanayohusika kule Dar es Salaam na pia kule watakuwa na watu wa kuwaangalia zaidi. Lakini walikwenda Zanzibar kumzika kaka yake na Marehemu huyu mama. Kwa hiyo, wamemzika marehemu basi wakawa wanawahi Bunge la leo ndiyo jana usiku wamepata ajali. Kwa hiyo, watakaokwenda kusindikiza msiba, ndege itaondoka kama saa tano watakwenda wafuatao, watakwenda Wabunge nane pamoja na mfawidhi zanzibar yeye anaongozana na mgonjwa sasa hivi lakini ataungana na wale kwenye mazishi. -
AUDITED FINANCIAL STATEMENTS for the YEAR ENDED 30Th JUNE 2017
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA PRIME MINISTER’S OFFICE DRUG CONTROL AND ENFORCEMENT AUTHORITY (VOTE 091) AUDITED FINANCIAL STATEMENTS FOR THE YEAR ENDED 30th JUNE 2017 AUDITED FINANCIAL STATEMENTS 1 FOR THE YEAR ENDED 30th JUNE 2017 Drug Satchets VISION To have a society with zero tolerance on drug abuse and trafficking. MISSION To protect the well-being of Tanzanians against drug and related effects by defining, promoting and coordinating the Policy of the Government of the URT for the control of drug abuse and illicit trafficking. CORE VALUES In order to achieve the above Vision and Mission, the Authority has put forward core values, which are reliability, cooperation, accountability, innovativeness, professionalism, confidentiality, efficiency and effectiveness. Heroin Cocain Cannabis Miraa Precursor Chemicals AUDITED FINANCIAL STATEMENTS i FOR THE YEAR ENDED 30th JUNE 2017 THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA PRIME MINISTER’S OFFICE DRUG CONTROL AND ENFORCEMENT AUTHORITY (VOTE 091) TABLE OF CONTENTS List of Acronyms ......................................................................................................................iii General Information .................................................................................................................iv Statement from the Honorable Minister for State, Prime Minister’s Office; Policy, Parliamentary Affairs, Labour, Employment, Youth and the Disabled ..........................1 Statement by the Accounting Officer .......................................................................................3 -
MKUTANO WA 18 TAREHE 3 FEBRUARI, 2015 MREMA 1.Pmd
3 FEBRUARI, 2015 BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Saba - Tarehe 3 Februari, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- SPIKA: Hati za kuwasilisha mezani, Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama au kwa niaba yake Mheshimiwa Capt. John Chiligati. MHE. CAPT. JOHN Z. CHILIGATI (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA): Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ulinzi na Usalama Katika Kipindi cha Januari, 2014 hadi Januari, 2015. MHE. SELEMANI S. JAFO (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA MAMBO YA NJE YA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA): Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Katika kipindi cha Januari, 2014 hadi Januari, 2015. 1 3 FEBRUARI, 2015 MHE. DUNSTAN L. KITANDULA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA UCHUMI, VIWANDA NA BIASHARA): Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uchumi, Viwanda na Biashara Katika Kipindi cha Januari, 2014 hadi Januari, 2015. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tumeletewa taarifa kwamba kwa sababu mgeni tulionao ndani ya nchi hii Rais wa Ujerumani vipindi vya TBC asubuhi hii vitakuwa kwenye TBC 2 na siyo TBC1, kwa sababu kule kuna mapokezi huko uwanja wa Taifa kule. Kwa hiyo, tutarudia tena baada ya mapokezi hayo kumalizika. Lakini pia jioni kwa sababu kutakuwa na dhifa ya kitaifa, pia matangazo hayatakuwa kwenye TBC1 na siyo vinginevyo. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 18 Julai, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita muuliza swali la kwanza nina matangazo kuhusu wageni, kwanza wale vijana wanafunzi kutoka shule ya sekondari, naona tangazo halisomeki vizuri, naomba tu wanafunzi na walimu msimame ili Waheshimiwa Wabunge waweze kuwatambua. Tunafurahi sana walimu na wanafunzi wa shule zetu za hapa nchini Tanzania mnapokuja hapa Bungeni kujionea wenyewe demokrasia ya nchi yetu inavyofanya kazi. Karibuni sana. Wapo Makatibu 26 wa UWT, ambao wamekuja kwenye Semina ya Utetezi na Ushawishi kwa Harakati za Wanawake inayofanyika Dodoma CCT wale pale mkono wangu wakulia karibuni sana kina mama tunawatakia mema katika semina yenu, ili ilete mafanikio na ipige hatua mbele katika kumkomboa mwanamke wa Tanzania, ahsanteni sana. Hawa ni wageni ambao tumetaarifiwa na Mheshimiwa Shamsa Selengia Mwangunga, Naibu Waziri wa Maji. Wageni wengine nitawatamka kadri nitakavyopata taarifa, kwa sababu wamechelewa kuleta taarifa. Na. 223 Barabara Toka KIA – Mererani MHE. DORA H. MUSHI aliuliza:- Kwa kuwa, Mererani ni Controlled Area na ipo kwenye mpango wa Special Economic Zone na kwa kuwa Tanzanite ni madini pekee duniani yanayochimbwa huko Mererani na inajulikana kote ulimwenguni kutokana na madini hayo, lakini barabara inayotoka KIA kwenda Mererani ni mbaya sana -
Audited Financial Statements
DRUG CONTROL AND ENFORCEMENT AUTHORITY AUDITED FINANCIAL STATEMENTS FOR THE YEAR ENDED 30th JUNE 2018 The Guest of Honour Mama Samia Suluhu Hassan the Vice President of the Government of URT (centre) in a souvenir photo with Tanzania Artist participants of DCEA workshop held at JNICC Dar es salaam, on her right is Hon. Jenista Joakim Mhagama (MP) Minister of State (Policy, Parliamentary Affairs, Labour, Youth, Employment and Disabled), and Rogers W. Siyanga DCEA Commissioner General, and on her left is Hon. Harrison Mwakiembe (MP) Minister of Information, Culture and Sports and Paul Makonda Dar es Salaam Regional Commissioner VISION To have a society with zero tolerance on drug abuse and trafficking. MISSION To coordinate and enforce measures towards control of drugs, drug use and trafficking through harmonizing stakeholders’ efforts, conducting investigation, arrest, search, seizure, educating the public on adverse effects of drug use and trafficking. CORE VALUES In order to achieve the above vision and mission the Authority has put forward the following core values which are reliability, cooperation , accountability, innovativeness, proffesionalism, confidentiality, efficiency and effectiveness Heroin Cocain Cannabis Miraa Precursor Chemicals AUDITED FINANCIAL STATEMENTS i FOR THE YEAR ENDED 30th JUNE 2018 THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA PRIME MINISTER’S OFFICE DRUG CONTROL AND ENFORCEMENT AUTHORITY (VOTE 091) CORE VALUES In order to achieve the above vision and mission the Authority has put forward the following core values: v Integrity: We will be guided by ethical principles, honesty and fairness in decisions and judgments v Cooperation: We will promote cooperation with domestic stakeholders and international community in drug control and enforcement measures.