Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document)

BUNGE YA ______

MKUTANO WA NANE ______

Kikao cha Ishirini na Mbili – Tarehe 12 Julai, 2007

(Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi)

D U A

Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua

MASWALI NA MAJIBU

Na. 194

Madiwani Viti Maalum

MHE. ESTHER K. NYAWAZWA aliuliza:-

Kwa kuwa, Udiwani wa Viti Maalum ni njia ya kupitia katika Uchaguzi ili kuongeza idadi ya Madiwani wanawake katika Halmashauri au Wilaya na kwa kuwa, mikopo mingi itolewayo na Halmashauri za Wilaya huelekezwa zaidi kwa vikundi vya wanawake; na kwa kuwa katika Halmashauri/Wilaya ya Sengerema Madiwani wa Viti Maalum hutolewa katika Kamati ya Mikopo na kuna nafasi za kugombea miongoni mwa Madiwani wenzao hukatazwa mfano Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri/Wilaya au Naibu Meya wa Jiji, Mwenyekiti Kamati ya Maadili na kadhalika.

(a) Je, ni kigezo gani hutumika katika kuwatoa Madiwani Viti Maalum katika Kamati ya kutoa mikopo?

(b) Je, ni Sheria ipi inayomtoa Diwani wa Viti Maalum, asigombee nafasi zilizotajwa hapo juu na kwa nini na kama sheria hiyo ipo Serikali haioni kuwa haiwatendei haki Madiwani hao na kwamba inavunja Katiba?

(c) Kama sheria hiyo ipo, Serikali haioni kuwa imepitwa na wakati na hivyo iletwe Bungeni irekebishwe?

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA LA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nyawazwa, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-

1 (a) Mheshimiwa Spika, uratibu uliotumika kuunda Kamati ya mikopo ya Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ni kwa kufuata mwongozo wa uendeshaji Mfuko uliotolewa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, katika Halmashauri zote nchini. Ujumbe wa Kamati ya kutoa mikopo haugombewi bali umewekwa bayana kulingana na mwongozo uliotolewa na Serikali. Kamati ya mikopo katika Halmashauri inaundwa kwa mujibu wa mwongozo nilioutaja hapo juu kwa mujibu wa mwongozo huo kamati ya mikopo ngazi ya Halmashauri inaundwa na wajumbe wafuatao:-

(i) Mkurugenzi wa Halmashauri – Mwenyekiti;

(ii) Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri – Katibu;

(iii) Afisa Maendeleo ya Jamii (jinsia);

(iv) Afisa Mipango wa Halmashauri naye ni mjumbe;

(v) Wabunge wote waliomo ndani ya Halmashauri husika ni wajumbe;

(vi) Wawakilishi wawili wanawake wa vikundi vya uzalishaji mali nao ni wajumbe pamoja; na

(vii) Kamati inaweza kumwalika mtaalam yeyote kwa kadri ivyoona.

(b) Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa kifungu cha 36 (2) cha sheria Na. 7 ya mwaka 1982 ya Serikali za Mitaa (Mamlaka ya Wilaya) na kifungu cha 20 (3) cha sheria Na. 8 ya mwaka 1982 ya Serikali ya Mitaa (Mamlaka ya Miji), Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Meya na Naibu Meya wa Halmashauri husika ni lazima awe Diwani wa kuchaguliwa na wananchi. Aidha, Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Halmashauri, anachaguliwa kutoka miongoni mwa Madiwani wanaounda Kamati hiyo. Kwa kuzingatia sheria nilizozitaja hapo juu, ni dhahiri kwamba Serikali haivunji Katiba bali inadumisha dhana ya utawala bora.

(c) Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuwahusisha Madiwani wa Viti Maalum katika Kamati mbalimbali zikiwemo Kamati za Mikopo. Baada ya uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, kwa kulitambua hilo, Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kupitia kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika tarehe 5/4/2006 kiliwachagua Madiwani wawili wa Viti Maalum kuingia katika Kamati ya Mikopo. Hata hivyo, kulingana na mwongozo wa uendeshaji wa mfuko ulitolewa na Wizara kuna wawakilisha wawili wanawake wa vikundi vya uzalishaji mali.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa sasa haina mpango wowote wa kurekebisha sheria nilizozitaja kwa sababu ni mwaka jana tu baadhi ya vipengele vimerekebishwa kupitia Bunge lako Tukufu. The Local Government Law Miscellaneous Amendment Act Na. 13 ya mwaka 2006.

2 MHE. ESTHER K. NYAWAZWA: Mheshimiwa Spika, nafurahi sana kupata maelezo mazuri kutoka kwa Mheshimiwa Naibu Waziri kwa swali langu la msingi.

Lakini ukizingatia kwamba tunapozungumza wakiwa ndani ya Halmashauri ya Wilaya, Madiwani, wanakuwa ni Madiwani wote. Je, sasa inafikiaje tunapoanza kugawana madaraka tunaanza kubagua Viti Maalum, naomba hapo miongozo haiwezi kurekebishwa? (Makofi)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA LA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni mwaka jana tu mwezi Desemba, sheria hii ya Serikali za Mitaa ililetwa hapa Bungeni na vipengele mbalimbali vimerekebishwa. Kama Mheshimiwa Mbunge angeona kuna ulazima mimi nafikiri kwa kipindi hicho angetoa hilo angalizo na sisi tungeliangalia. Lakini kwa sasa kurudiarudia, mwaka jana tumefanya amendment na mwaka huu tuanze tena kufanya amendment mimi nafikiri kwa Bunge lako Tukufu itakuwa ni usumbufu. Naomba tuvute subira na wakati ukifika tunaweza tukaliangalia jambo hili kwa undani zaidi. (Makofi)

MHE. ZAYNAB M. VULU: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tuko katika hatua maalum ya kutaka kuingia kwenye fifty fifty na kwa kuwa sheria zinatungwa na sisi Wabunge tukiwa humu ndani. Je, Serikali haioni kwamba kuna haja ya kuirekebisha hiyo sheria hata kama tutakuwa tunarudiarudia lakini kurudia huko ni kwa ajili ya kujenga? (Makofi)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA LA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA : Mheshimiwa Spika, kwa sasa hilo suala liko kwenye mchakato. Mimi nafikiri tungengojea huo mchakato ukiisha uingie Bungeni ndiyo tutarekebisha hili suala. Lakini naomba Waheshimiwa Wabunge, katika mchakato huu washiriki kikamilifu ili sheria hii ipite haraka. Hata mimi mwenyewe nitafurahi iwapo asilimia hamsini kwa hamsini itapita. (Makofi)

Na. 195

Ruzuku ya Maendeleo

MHE. SIRAJU JUMA KABOYONGA aliuliza:-

Kwa kuwa katika miaka ya fedha ya 2004/2005 na 2005/2006 Manispaa ya Tabora haikupata fedha za ruzuku ya Maendeleo kwa kushindwa kukidhi baadhi ya masharti ya ruzuku hiyo, kama vile kutokuwa na Mkurugenzi wa Mji na kwa sababu hiyo wananchi wakakosa fedha hizo ambazo wanazihitaji sana:-

(a) Je, kwa nini Serikali iinyima Manispaa ya Tabora fedha za Maendeleo kwa kushindwa kutimiza sharti ambalo liko nje ya uwezo wa Manispaa na Wananchi wa Tabora?

3 (b) Kwa kufanya hivyo. Je, Serikali haioni kwamba haikuwatendea haki wananchi wa Manispaa hiyo?

(c) Je, kwa nini Serikali isiwe na utaratibu wa kuwafidia Manispaa inaposhindwa kutimiza masharti ya vigezo vya ruzuku ya Maendeleo kwa sababu zilizo nje ya uwezo wake kama kutokuwa na watendaji ambao wanateuliwa na mamlaka nyingine kama vile Mheshimiwa Rais, Waziri Mkuu au Waziri wa Serikali za Mitaa?

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA LA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Siraju Juma Kaboyonga, Mbunge wa Tabora Mjini, lenye sehemu (a) (b) na (c) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Manispaa ya Tabora haikupata ruzuku ya fedha za maendeleo (Local Government Capital Development Grants) kwa mwaka 2004/2005 na 2005/2006 kwa sababu ya ubadhirifu wa zaidi ya shilingi milioni 88 uliobainika kutokea. Hiki ndicho kigezo kikubwa kilichosababisha hiyo Halmashauri kukosa fedha hizo. Pia wakati upimaji unafanyika, Mkurugenzi wa Manispaa, mweka Hazina na baadhi ya Watumishi wa Idara ya Fedha, walikuwa wamesimamishwa kazi kutokana na ubadhirifu huo.

(b) Mheshimiwa Spika, kwa kufanya hivyo, Serikali ilikuwa inaweka mazingira mazuri ili wananchi wa Tabora wanufaike na matumizi mazuri ya fedha za maendeleo. Kwa mazingira ya ubadhirifu isingekuwa kwa maslahi ya umma kupeleka fedha nyingi mahali hapo kwani uwezekano wa fedha hizo kutowafikia wananchi ungekuwa mkubwa. Kwa sasa Serikali imepeleka watendaji wapya katika Halmashauri hiyo. Katika upimaji wa mwaka 2006/07 Halmashauri hii ilifuzu vigezo vinavyotakiwa ikiwa ni pamoja na kupata hati safi ya Ukaguzi toka kwa Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali katika kipindi cha mwaka 2005/06.

(c) Mheshimiwa Spika, hakuna utaratibu wa kufidia Halmashauri yoyote inaposhindwa kutimiza masharti ya vigezo vya ruzuku ya maendeleo kutokana na utendaji mbovu. Kuhusu kutoteua watendaji wapya mapema katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, Serikali isingeweza kuteua watendaji wengine hadi kesi zilizokuwa zinawakabili wale watuhumiwa zimalizike mahakamani. Suala hilo ni kwa mujibu wa sheria na Kanuni za utumishi wa umma zilizopo kwa sasa. Hata hivyo, kigezo cha kukosa watumishi muhimu siyo kigezo pekee kilifanya kusababisha Halmashauri kukosa ruzuku ya Maendeleo. Vipo vigezo vingine vinavyoweza kukosesha Halmashauri fedha za ruzuku, vigezo hivyo ni pamoja na:-

- Hesabu za mwisho za mwaka wa fedha uliopita zilizoandaliwa kwa mujibu wa sheria za fedha Serikali za Mitaa, ziwe zimewasilishwa kwa ukaguzi wakati uliowekwa.

4 - Halmashauri iwe haikupokea Hati chafu ya ukaguzi kwa hesabu za mwisho zilizokaguliwa.

- Pasiwepo na ubadhirifu katika usimamizi wa fedha uliotolewa taarifa ama na wakaguzi wa ndani au wa nje kwa miezi 12 iliyopita na kuthibitishwa.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri zote zinazokosa fedha za ruzuku ya Maendeleo hupewa fedha za kujengewa uwezo (Capacity Building) ili kuwajengea uwezo baadaye ziweze kupata na kutumia fedha za ruzuku ya Maendeleo ipasavyo.

MHE. SIRAJU JUMA KABOYONGA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa wakati mfumo mzima wa kutoa ruzuku (Capital Development Grand) ulipoanzishwa ni dhahiri zilikuwepo Manispaa au District Councils ambazo zilikuwa na vitabu vichafu na inachukua muda takriban zaidi ya mwaka mmoja mpaka miwili kurekebisha vitabu. Sasa utaratibu wa kutoa ruzuku hii ni sawa sawa na mbio ambazo zinatakiwa zianzie pamoja lakini mbio zile zinafanya wengine wawe mbele wengine wawe nyuma halafu mnatakiwa mfike mwisho kwa pamoja. Haiwezekani.

SPIKA: Mheshimiwa Mbunge, nenda kwenye swali sasa.

MHE. SIRAJU JUMA KABOYONGA: Je, kwa nini utaratibu huu usitoe muda wa mpito ili zile Halmashauri ambazo zilikuwa haziko sawa zijipange na wakati wa kipindi kile cha mpito iwepo namna ya kufidia?

La pili, kwa kuwa Naibu Waziri amekiri kwamba ni kweli katika Manispaa ya Tabora hakukuwa na uongozi takriban kwa miaka mitatu anasema pamoja na kwamba hicho siyo kigezo lakini ni kigezo. Watu wa Tabora wasingeweza kuwa-appoint Mkurugenzi au wale watendaji wengine kesi ilikuwa mahakamani hawa ni wabadhirifu, kama ni wabadhirifu sheria ya wabadhirifu ichukue mkondo wake. Suala la watu wa Tabora kunyimwa ruzuku kwa sababu ya wabadhirifu ni kuwaonea. Je, kwa nini waliopata matatizo ya ubadhirifu wasingeshughulikiwa na sheria na halafu ile habari ya ruzuku iendelee kama ilivyo? (Makofi)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA LA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA : Mheshimiwa Spika, vigezo ambavyo vimewekwa kwa ajili ya kupata ruzuku ya Maendeleo ni vigezo vya kawaida kabisa. Ni Financial Regulations, ni sheria za manunuzi ya umma na sheria zote zinazohusiana na fedha, siyo vigezo ambavyo viko nje na sheria za fedha. Kwa hiyo, wakaguzi wanapoenda pale wanaangalia vigezo vinavyofuatana na sheria ambazo tumeziweka sisi wenyewe. Pia wakati wa ukaguzi kama kuna matatizo Halmashauri husika inapewa miezi miwili kurekebisha yale mambo ambayo hayakutolewa ufafanuzi. Kwa hiyo, hicho ni kipindi ambacho kinawasaidia pia kupungufu zile queries.

Tatu, kuna uwezekano wa kukata rufaa kama Halmashauri imeona kwamba imeonewa wanakata rufaa kwa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa. Kwa hiyo,

5 vyote hivi vinawekwa ili kutoonea Halmashauri fulani. Mwisho ni kwamba wananchi wanawakilishwa kikamilifu kwa sababu kuna vikao vya Madiwani, kuna vikao vya Kamati ya fedha. Vile vikao ndivyo vinavyosimamia mapato na matumizi ya Halmashauri. Kwa hiyo, hapo wananchi wanawakilishwa ipasavyo.

Kwa swali lake la pili, la kuhusu kuwaonea Halmashauri ya Manispaa ya Tabora. Kwa kipindi hicho kama nilivyosema kwamba kesi zilikuwa mahakamani kama kesi zikiwa mahakamani suala hilo halitakiwi kuchukuliwa hatua za nidhamu wala hatua nyingine zozote mpaka kesi hiyo iwe imekwisha mahakamani. Baada ya kesi hiyo kuishi ndipo wale watendaji wakachukuliwa hatua za kinidhamu na wengine wamefukuzwa kazi na baadaye ndipo sisi tulipoweza kuwachagua watendaji wengine katika Halmashauri hiyo. Kwa hiyo, ni mchakato ambao unaweza kuwakwamua wananchi wakapata hela zao za ruzuku kama kawaida. Kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Wabunge, tushirikiane tuhakikishe kwamba kwenye Halmashauri zetu financial regulations zinafuatwa kama kawaida. Wawakilishi wetu Madiwani pamoja na sisi tutimize wajibu wetu kuhakikisha kwamba ukaguzi unafanyika kila wakati na mapato na matumizi tunayasimamia ipasavyo.

SPIKA: Mheshimiwa Waziri Mkuu majibu ya ziada.

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Naibu Waziri Kompani kwa kujibu maswali vizuri sana hapa Bungeni. Lakini ni kweli hatua hizi tunazochukua kwa upande mwingine zinaweza kuonekana kwamba tunaonea wananchi ambao hawana kosa inasababishwa na viongozi. Lakini tatizo ni kwamba fedha nyingi za Local Government Capital Development Grand nyingi ni za wafadhili. Tulijadiliana nao juu ya jambo hili kwamba uamuzi huu tunaofanya unawaumiza sana wananchi ambao hawakuhusika, waliohusika ni watumishi wa Serikali. Lakini nasikitika kusema kwamba wafadhili walitukatalia moja kwa moja na walifika mahali walikuwa tayari kwa hoja hii kuvunja mkataba. Tukaona hakuna sababu ya kuvunja mkataba isipokuwa tumechukua hatua kujihami ili jambo kama hili linapotokea Mkurugenzi anaposimamishwa kwa jambo lolote tunachukua hatua za kumteua mwingine mara moja ili tatizo hili lisiendelee kutokea. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Waziri Mkuu ufafanuzi huo umetusaidia.

Na. 196

Ndege Waharibifu wa Mazao

MHE. EZEKIEL M. MAIGE aliuliza:-

Kwa kuwa kumekuwepo na mlipuko wa ndege waharibifu wa mazao maarufu kama quelea quelea kila mwaka katika kata za Bulige, Ngaya na Kananga katika jimbo la Msalala:-

6 (a) Je, Serikali inayo taarifa juu ya kuwepo kwa tatizo hilo na ni nini chanzo chake? (b) Je, kwa nini Serikali haijapata ufumbuzi wa kudumu kwa tatizo hilo?

(c) Je, Serikali sasa ina mikakati gani endelevu ya kukomesha tatizo hilo?

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA (MHE. DR. DAVID M. DAVID) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kabla ya kujibu swali la Mheshimiwa , Mbunge wa Msalala, napenda kutoa maelezo ya awali kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ndege waharibifu wa mazao ya kilimo waitwao quelea quelea ni mojawapo ya viumbe wa asili wanaopatikana katika maeneo mengi ya Bara la Afrika kuanzia Afrika ya Kusini hadi Kaskazini ya Sudani na kuanzia Ethiopia hadi Afrika Magharibi. Hapa nchini ndege hao wanapatikana katika Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, Kati, Kaskazini na Mikoa iliyoko Kusini mwa Ziwa Victoria ukiwemo Mkoa wa Shinyanga. Quelea quelea wamekuwepo katika maeneo hayo kwa muda mrefu pengine hata kabla binadamu hajaanza shughuli za kilimo katika maeneo hayo. Ndege hao wana tabia ya kuhamahama wakifuata upatikanaji wa mvua ili wapate mbegu za nyasi ambazo ndicho chakula chao cha asili. Aidha, ndege hao huzaliana kwa wingi na kuishi katika makundi makubwa yenye wastani wa ndege milioni moja hadi milioni saba. Baada ya maelezo hayo naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Ezekiel Maige, lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-

(a) Serikali inayo taarifa juu ya kuwepo kwa tatizo la quelea quelea katika Mkoa wa Shinyanga. Serikali inafahamu kwamba quelea quelea wanaofanya mashambulizi katika maeneo ya Kahama hutokea maficho yaliyopo katika mapori ya Bulige, Malilita na Mwambiti. Mashambulizi ya Shinyanga Vijijini hutokea mapori ya Mwashagi na Kimandaguli. Aidha, chanzo cha milipuko hiyo mara nyingi hutokana na kizazi cha ndege wanaotoka mapori yaliyo katika Mikoa ya Dodoma na Morogoro.

(b) Quelea quelea wamejijengea uwezo na mbinu zinazotoa changamoto kubwa kwa watafiti na wanasayansi Barani Afrika katika kutafuta mbinu endelevu za kuwadhibiti. Shughuli za utafiti zimekuwa zikifanyika Afrika ya Kusini, Msumbiji, Botswana, Malawai, Zambia, Kenya na Sudan, pia katika mataifa yaliyoendelea kama Marekani, Uingereza na Australia kwa muda mrefu. Utafiti unaendelea ili kupata ufumbuzi wa kudumu ingawa uwezo na mbinu za ndege hao umekuwa ni changamoto kubwa inayokwamishwa kupatikana kwa ufumbuzi wa kudumu dhidi ya ndege hao hadi sasa.

(c) Mkakati uliopo katika kuwadhibiti ndege waharibifu ni kwa kuwashirikisha wananchi ambapo wananchi watafundishwa mbinu za kuwatambua, kutoa taarifa mapema kuwaua kwa kutumia viatilifu. Aidha, unafanyika utafiti wa kuangalia uwezekano wa kuwatumia ndege hao kama chanzo cha protini kwa ajili ya matumizi ya binadamu au mifugo.

7 MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Spika, naomba nimshukuru sana Naibu Waziri kijana mwenzangu Dr. Mathayo kwa majibu yake mazuri. Kwa kuwa Serikali imekiri kwamba tatizo hili lipo kwa miaka mingi pengine hata binadamu hajaanza kufanya shughuli za kilimo na katika mikakati inayofanyika ni utafiti tu:-

(a) Je, kwa nini Serikali isiimarishe idara ya kilimo Wilayani hasa Wilaya ya Kahama ambayo hasa imekuwa ikipata tatizo hili mara kwa mara ili kunapotokea wananchi waweze kupata msaada wa haraka? (Makofi)

(b) Kwa kuwa tatizo hili limekuwa ni chanzo cha uhaba wa chakula kwenye maeneo ya kata hizo za Burige, Kinaga, Mwalugulu, Isaka na Nangaya. Je, kwa nini Serikali isisaidie kuanzishwa kwa mfumo wa stakabadhi za mazao ili wananchi waweze kuwa na mfumo endelevu wa kuwa na akiba ya chakula mwaka hata mwaka? (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA (MHE. DR. DAVID M. DAVID): Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kusema kwamba kama nilivyoeleza mwanzoni kwamba ndege hawa wanahama hama kwa mfano ndege ambao wameingia katika msimu uliopita ama msimu huu ambao tunaendelea nao walitokea Malawi na Msumbiji. Ndege hawa wana uwezo wa kutembea kilomita 30 kwa siku na kurudi katika viota vyao. Sasa hatuwezi tukasema tu kwamba tunaimarisha Wilayani kwa ajili ya ku-control quelea quelea hili ni tatizo la kitaifa ambalo linatokea maeneo mengi. Kwa mfano sasa hivi tunachotaka ni kuimarisha kilimo anga, katika uwanja wa ndege wa Arusha kusudi tuweze baadaye katika Bajeti zijazo tuweze kununua ndege moja kwa ajili ya kunyunyizia na ku-control hawa ndege lakini pia tuajiri marubani pamoja na mainjinia wawili wawili. Wizara pia ina inafanya utafiti kusudi tuweze kuangalia ni jinsi gani tunaweza tukavuna ndege hawa kwa ajili ya protein kwa ajili ya mifugo na binadamu. Lakini pia kuwaelimisha wananchi kutoa taarifa mapema ili kusudi out break hii inapotokea tuweze ku-control mapema.Swali la pili, suala hili la stakabadhi za mazao limeshaanza na Serikali inahamasisha na mwanzoni kabisa ilianza kwenye mazao ya kahawa na pamba na sasa hivi inaelekea kwenye mazao ya korosho. Kwa hiyo, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge, kabisa kwamba kuna haja katika majimbo yetu kuhamasisha utaratibu wa stakabadhi ya mazao kwenye maghala kusudi iweze kusaidia wananchi waweze kupata bei nzuri baada ya mavuno kumalizika.

Na. 197

Vyama vya Msingi na Vyama Vikuu vya Ushirika

MHE. ROSEMARY K. KIRIGINI aliuliza:-

Kwa kuwa Ushirika ni silaha mojawapo ya kupambana na unyonyaji, lakini historia ya ushirika imekuwa mchanganyiko wa mafanikio na matatizo kabla na baada ya Azimio la Arusha:-

8 (a) Je, hadi sasa ni vyama vingapi vya msingi na Vyama Vikuu vilivyo hai kiuchumi na vina wanachama wangapi ambao wana mamlaka kamili ya kuvidhibiti vyama hivyo?

(b) Je, Serikali inaweza kutoa tamko Bungeni kuhusu Maendeleo ya ushirika hapa nchini?

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA (MHE. DR. DAVID M. DAVID) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kabla ya kujibu swali la Mheshimiwa Rosemary Kirigini, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) napenda kutoa maelezo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, ushirika ni chombo muhimu cha kupambana na umaskini kwa njia ya kuunganisha nguvu za wananchi wenye uwezo mdogo ambao ndiyo wengi kwa kuwawezesha kuweka mitaji yao pamoja na kuweza kukopeshana au kutekeleza shughuli za kibiashara kupitia vyama vyao vya ushirika. Kwa hiyo, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge, kuwa vyama vya Ushirika ni vyombo ambavyo vinawawezesha wananchi ambao ni wanyonge kutekeleza mambo makubwa ya kiuchumi au kibiashara kwa pamoja.

Mheshimiwa Spika, vyama vya ushirika kama vyombo vingine vya kibiashara vinakabiliwa na matatizo mbalimbali yakiwemo ya menejimenti, uwezo mdogo wa kushindana kibiashara na uimarishaji wa mitaji. Ili kutatua matatizo hayo, Serikali kwa kuzingatia maelekezo ya Sera ya ushirika 2002 na Sheria ya Ushirika ya 2003 imeandaa programu kabambe ya mageuzi na Modenaizesheni ya Ushirika nchini ambayo lengo lake kuu ni kubwa na vyama vya Ushirika imara kiuchumi vinavyoanzishwa kutokana na mahitaji ya wanachama na kusimamiwa na wanachama wenyewe. Programu hii ambayo imeanza kutekelezwa mwaka 2005 ni ya kipindi cha miaka kumi kuanzia 2005 hadi 2015.

Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo sasa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rosemary Kirigini, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Kufikia Mei 2007 idadi ya vyama vya Msingi vya Ushirika vilivyo hai ni vyama 5,832 vyenye jumla ya wanachama hai milioni 1.3. Aidha, idadi ya vyama vikuu vya ushirika ambavyo viko hai kiuchumi ni 12. (Makofi)

(b) Tamko la Serikali kuhusu Maendeleo ya Ushirika hapa nchini ni kuhakikisha tunatekeleza programu kabambe ya mageuzi na modenaizesheni ya Ushirika kama ifuatavyo:-

(i) Kukamilisha chaguzi za viongozi wa vyama vya ushirika vya msingi.

(ii) Kusimamia chaguzi za viongozi wa vyama vikuu vya ushirika ili kuhakikisha wanachaguliwa viongozi waadilifu na wenye upeo katika masuala ya uongozi na

9 ushirika. Aidha, kazi kubwa iliyo mbele yetu ni kuviwezesha vyama vya ushirika viweze kufanya maboresho yaliyokusudiwa kwa ufanisi.

Mheshimiwa Spika, napenda kutumia fursa hii kutoa wito kwa Waheshimiwa Wabunge na viongozi wa siasa na Serikali nchini tushirikiane kuhamasisha wananchi wengi zaidi waweze kujiunga kwenye vyama vya ushirika ili waweze kuvimiliki na kuvitumia kwa Maendeleo yao.

MHE. ROSEMARY K. KIRIGINI: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa vyama hivi vya ushirika vilianzishwa kwa ajili ya mpango mzima wa kununua na kuuza mazao ya wakulima:-

(a) Je, Serikali sasa ina mpango gani wa kuongeza mkakati mzima wa vyama hivi vya ushirika kuweza kuzalisha mazao na kuviongezea Maendeleo zaidi kiuchumi?

(b) Mheshimiwa Spika, wale wakulima ambao wote walikuwa wameuza mazao yao kwenye vyama hivi vya ushirika, kwa mfano Mkoani kwangu Mara nilikuwa nataka kujua ni lini hawa watarudishiwa madeni yao? Ahsante. (Makofi)

SPIKA: Kabla sijakuita Mheshimiwa Naibu Waziri kutoa majibu kwa maswali hayo ya nyongeza. Nawakumbusha Waheshimiwa Wabunge kwamba kuendelea kuleta vikaratasi vinavyotambulisha wageni hapa, wakati wa kipindi cha maswali ni kupoteza muda tu. Tulikwisha kubaliana kwamba majina yote ya wageni yawe yamenifikia saa 2.30 siku husika. Kwa hiyo, nasikitika leo wale wote kwanza wanapoteza muda kwa sababu wakiendelea kuwapata Wasaidizi hapa sitayasoma. Kwa hiyo, hayana maana tena. Ahsante sana. (Makofi)

WAZIRI WA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA: Mheshimiwa Spika, kwanza kabla ya kumjibu naomba kumpongeza Naibu Waziri kwa majibu mazuri sana ambayo anayatoa katika Bunge letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, dhana ya ushirika ninawapa nafasi washirika wenyewe kuamua ni jambo gani wanataka kushirikiana. Yako maeneo mengi ambayo wanatakiwa kushirikiana. Historia ya ushirika huko nyuma ilianzishwa kwa ajili ya ushirika wa mazao. Kwa sababu hilo ndiyo lilikuwa tatizo kubwa la wakulima kwa wakati huo. Wakulima walikuwa wananyonywa na wanunuzi binafsi na wakaamua kushirikiana ili kujiondoa katika tatizo hilo. Na wakaanzisha vyama vya kununua na kuuza mazao.

Lakini Sheria ya Ushirika inawapa fursa ya kuanzisha aina mbalimbali za ushirika, siyo kwa ajili ya kilimo tu lakini hasa kwa ajili ya viwanda na maeneo mengine yakiwemo uanzishaji wa SACCOS ambazo ni sehemu inayowasaidia kupata mitaji kwa ajili ya kujikopesha na kuendeleza uchumi wao. Kwa hiyo, wakulima na wananchi wote wanashauriwa watazame matatizo yao na waanzishe ushirika unaolingana na matatizo waliyonayo kwa nia ya kujikomboa. Hilo swali la kwanza.

10 Swali la pili, lilihusiana na Mara Cooperative Union na mikopo ambayo wakulima wa Mara walipeleka mazao yao na hawakulipwa. Hili ni tatizo la siku nyingi na maelezo tuliyatoa katika swali la msingi kwamba ubadhirifu ndiyo uliowafikisha hapo. Sasa imepita karibu miaka 10 hawa wakulima wanadai na Serikali tumekwishatoa tamko Bungeni hapa kwamba tutawalipa wakulima wale, siyo kwa sababu Serikali iliwakopa lakini kwa sababu Serikali ina wajibu wa kusimamia kilimo na kuhakikisha kwamba haki inatendeka kwa wale ambao wanaweza kuwa wamedhulumika kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao. Wakulima hao ni pamoja na wakulima wa Mara na maeneo kama Chunya ambao tumekwishasema tutawalipa na tunayo orodha ya maeneo ambayo tutawalipa na tutajitahidi kulipa kuanzia Bajeti ya mwaka huu ambayo tunaendelea nayo sasa hivi. (Makofi)

SPIKA: Maeneo hayo, Mheshimiwa Waziri ni pamoja na Urambo. (Kicheko/Makofi)

MHE. PHARES K. KABUYE: Nakushukuru Mheshimiwa Spika, kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa vyama vya ushirika vya asili vilivyokuwa vimeanzishwa na wananchi, Serikali ilipiga marufuku na baadaye ikaleta vyama vya ushirika ambavyo vinafanana fanana kama vya kiserikali na kwa kuwa sasa vyama hivyo navyo vimekufa na kwa mtindo huo wananchi wameshakata tamaa katika kufufua naomba Waziri aniambie atafanye kurudisha moyo kwa wakulima ili wapende vyama vya ushirika? (Makofi)

WAZIRI WA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA: Mheshimiwa Spika, kwanza siyo kweli kwamba Serikali ilipiga marufuku aina fulani ya vyama vya ushirika. Kilichotokea ni kwamba kumekuwepo na matatizo katika mfumo wa vyama vya ushirika. Kwa hiyo, kila mara Serikali imekuwa ikichukua hatua ya nia njema kujaribu kuvisaidia. Lakini siyo kupiga marufuku. Ilipofika mahali ikaonekana ubadhirifu umezidi sana na dhuluma ndiyo imechukua nafasi ya haki ambayo ndiyo ilikuwa msingi wa kuanzishwa kwa vyama vya ushirika. Serikali iliwahi kuchukua hatua ya kuvifuta lakini kuvifuta vyama vikuu siyo vya msingi, halafu baadaye ikavirudisha tena. Kwa hiyo, mfumo na mabadiliko yaliyokuwa yanatokea ni sehemu ya historia ya ushirika katika Tanzania. Lakini haikutokana na kupigwa marufuku.

Kuhusu kurudisha imani, imani inatokana na imani. Ukijenga msingi ambao unaonyesha ya kwamba kuna watu wanachaguliwa na wanaanza kuonyesha kwa vitendo kwamba wanatenda kazi yao kwa ajili ya maslahi ya wakulima imani itarudi. Kwa hiyo mimi nina imani vile vile wakulima wakiwa na imani na viongozi wao wa vyama ushirika imani yao itaendelea kukua na imani haiamki tu asubuhi ikawepo, inakuzwa. Kwa hiyo, ningependa niwaombe Waheshimiwa Wabunge wote tujitahidi kuwaeleza wananchi waelewe ya kwamba ushirika ni njia ya pekee ambayo wakulima wadogo wadogo wanaweza kuimarika. Wakulima ambao hawawezi kukopesheka bila mtaji lazima wawe na ushirika ili uwe mtaji wao. Kwa hiyo, ninafikiri kwa maelezo hayo na kwa imani waliyonayo kwa Serikali ya CCM ya Awamu ya Nne mimi nadhani hili linawezekana.

11 SPIKA: Tutaenda haraka haraka kidogo maana tumechukua muda mrefu kwa maswali haya yaliyotangulia. Sasa ni zamu ya Wizara ya Maliasili na Utalii.

Na. 198

Kifuta Jasho kwa mtu aliyeuawa na Mnyamapori

MHE. JOHN P. LWANJI aliuliza:-

Kwa kuwa kifuta jasho cha shilingi elfu hamsini (50,000/=) kinachotolewa na serikali kutokana na kifo cha mtu aliyeuawa na wanyamapori ni kiwango kidogo sana:-

(a) Je, kiwango hicho kiliwekwa lini na kwa kuzingatia vigezo gani?

(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kurekebisha kiwango hicho ili kiwe fidia kamili badala ya kifuta jasho ili ilipwe kwa familia ya Marehemu?

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa John P. Lwanji, Mbunge wa Manyoni Magharibu, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Spika, nchi yetu imebahatika kuwa na wanyamapori wengi na wa aina mbalimbali ambao huishi katika maeneo yasiyokuwa na uzio. Kutokana na hali hiyo, kumekuwepo na matukio mengi ya migongano kati ya wanyamapori na binadamu kutokana na ongezeko la binadamu. Kwa mfano, kutoka watu milioni 8 wakati wa uhuru hadi watu takriban milioni 35 kwa takwimu za mwaka 2002. Sambamba na ongezeko la watu kuna mahitaji ya maeneo zaidi kwa shughuli zingine za binadamu mama vile kilimo, ufugaji, makazi na kadhalika.

Vile vile wanyamapori walioko ndani ya maeneo yaliyohifadhiwa huwa wanatoka nje ya maeneo hayo kufuata malisho na maji hasa wakati wa ukame. Aidha, katika baadhi ya maeneo shughuli za kilimo na makazi zinafanyanyika katika ushoroba ambao ni njia za asili za wanyamapori. Katika mazingira hayo, kumekuwepo na mwingiliano mkubwa kati ya binadamu na wanyamapori hali ambayo inasababisha maisha ya binadamu waishio kwenye maeneo hayo na mali zao kuathiriwa na wanyamapori.

Mheshimiwa Spika, kwa kutambua uharibifu huo, mwaka 2000 Serikali iliamua kuweka utaratibu wa kutoa kifuta machozi kwa kiwango cha shilingi elfu hamsini (50,000) kwa familia ya Marehemu aliyeuawa na mnyamapori. Uamuzi wa kuweka kiwango hicho ulizingatia uwezo wa Serikali kifedha na hakuna vigezo vilivyotumika katika kuweka kiwango hicho ikizingatiwa kwamba maisha ya mtu aliyeuawa na mnyamapori hayawezi kuthamanishwa na fedha au vitu.

(c) Mheshimiwa Spika, Serikali imeangalia upya kiwango cha kifuta machozi kilichokuwa kikitolewa kwa kila familia ya Marehemu iliyopoteza ndugu yao kwa

12 kuuawa na mnyamapori cha shilingi elfu hamsini (50,000) na kukiongeza kuwa shilingi laki mbili (200,000) kuanzia mwezi Julai, 2007. (Makofi)

MHE. JOHN P. LWANJI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, majibu ambayo yanaonyesha wazi kwamba Serikali inasikia kilio cha wanyonge. Nina maswali mawili ya nyongeza.

(a) Kwa kuwa kiwango hiki cha awali cha shilingi 50,000 kiwango kidogo sana na ndicho kigezo kilichofanya wa-drive hii shilingi laki mbili. Je, Serikali haioni kwamba bado shilingi laki mbili ni kiwango kidogo sana? (Makofi)

(b) Kwa kuwa Mheshimiwa Spika, kuna mtu anayeuawa ndani ya hifadhi au mbuga za akiba na kuna yule anayeuawa nje ya hifadhi hizi yuko kijijini kwake anajifanyia shughuli, kwa mfano yule bibi aliyeuawa pale Mabondeni na simba wakamtafuna kijijini. Je, isingekuwa vyema kwamba tungepata viwango viwili tofauti kwamba kuwe na shilingi hilo laki mbili kwa yule anayeuawa ndani ya hifadhi na shilingi milioni 2 kwa yule nayeuawa kijijini? (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kusema kweli kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi maisha ya binadamu hayawezi kuthamanishwa na fedha au kitu chochote kwa hivi Serikaliona iongeze kile kiwango kilichokuwa kikitolewa cha shilingi 50,000 kuwa 200,000 ambacho ni kifuta machozi. Hata hivyo, Serikali itaangalia hicho kiwango cha shilingi 200,000 kitafanyiwa marejeo kulingana na mhitaji na nyakati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili, ningependa niliarifu Bunge lako Tukufu kwamba watu hatuwategemei kuingia katika hifadhi zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya wanyamapori. Sehemu hizo wanakwenda wale ambao wanafanyakazi huko kwa mfano askari wetu wa wanyamapori ama watu ambao wamekwenda kule kwa shughuli za uwindaji wa kitalii. Kwa hiyo, kama mtu atakuwa ameingia katika hifadhi za wanyamapori bila kibali atakuwa ametenda kosa. Na kwa kweli tutamhesabu ni kama jangili na Serikali haitoi kifuta machozi kwa majangili tunatoa kifuta machozi kwa wale watu tu ambao ni raia wamepata athari hiyo kutokana na wanyamapori ambao wameingia katika maeneo ya watu. Na kwa wale ambao wanafanya kazi katika hifadhi kuna mpango wa kuwalipa. Ahsante. (Makofi)

Na. 199

Kushindwa kwa kampuni za Kitalii Zilizouzwa/Binafsishwa

MHE. JANETH M. MASSABURI aliuliza:-

Kwa kuwa baadhi ya mashirika ya umma yaliyobinafsishwa/yaliyouzwa yameshindwa kujiendesha hali ambayo inasababisha Serikali kutopata mapato yanayotokana na kodi:-

13 Je, Serikali inasema nini juu ya hali hiyo kwa Kampuni inayoendesha lodge zilizopo katika mbuga za wanyama kama Ngorongoro Wildlife Lodge, Lake Manyara na Seronera?

SPIKA: Uhandisi, kuna tatizo la taa sasa, sijui vipi tena huko!

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (K.n.y. WAZIRI WA MIPANGO, UCHUMI NA UWEZESHAJI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Maurice Massaburi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Hoteli zilizokuwa zinamilikiwa na kampuni ya Serengeti Safari Lodges Limited na kusimamiwa na Kampuni ya TAHI (Tanzania Hotels Investment) zilibinafsishwa mwaka 2003 kwa Kampuni ya Hotels and Lodges (T) Ltd. Hoteli hizi ni:-

Hotel ya Ziwa Manyara; Loji ya Ngorongoro; Loji ya Seronera ; na Loji ya Lobo.

Mheshimiwa Spika, Kampuni ya Hotels and Lodges Limited ilinunua hoteli hizi baada ya kushinda zabuni chini ya Tume ya Rais ya Kurekebisha Mashirika ya Umma yaani PSRC. Hoteli hizi zilikabidhiwa rasmi kwa mwekezaji tangu mwezi Desemba mwaka 2003. Tangu zimekabidhiwa zimeendelea kutoa huduma na kulipa kodi kwa mujibu wa sheria. Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2006 kiasi cha shilingi 4.7 bilioni zilikuwa zimelipwa kama kodi. Hata hivyo kiasi cha kodi kinacholipwa sasa kingeweza kuongezeka kama mpango wa uwekezaji (Investment Plan) wa Hotels and Lodges Ltd ungetekelezwa kama ulivyoainishwa katika mikataba ya mauzo wakati wa ubinafsishaji.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia PSRC imempa mwekezaji huyu kipindi cha mwaka mmoja kuhakikisha kwamba anatekeleza wa Mpango wa Uwekezaji (Investment Plan) wa loji hizo ilivyoainishwa katika mkataba wa mauzo (Sale of Assets Agreement) na kama atashindwa basi loji hizi zitarudishwa kwa ajili ya kumpatia mwekezi mwingine.

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu itaendelea kufuatilia utekelezaji wa mkataba huu kwa karibu sana. Aidha, Serikali inamhakikishia Mheshimiwa Massaburi, na Waheshimiwa Wabunge wote kuwa haitasita kunyang’anya hoteli hizi endapo mwekezaji atashindwa kutekeleza makubaliano kama yalivyowekwa katika mkataba wa mauzo katika kipindi alichoongezewa.

MHE. JANETH M. MASSABURI: Nakushukuru Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, nina swali dogo la nyongeza. Je, Serikali inasema nini juu ya Maendeleo ya Mikumi Lodge?

14 WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (K.n.y. WAZIRI WA MIPANGO, UCHUMI NA UWEZESHAJI): Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwisha kusema katika jibu langu la msingi kwamba Serikali sasa hivi inazipa muda hoteli hizi ambazo zilikuwa zimebinafsishwa kuweza kutekeleza mkataba wa mauzo kama ilivyo katika mkataba huu wa mauzo. Na haitasita kuzinyang’anya hoteli hizi ambazo zitashindwa kutekeleza. Mifano ipo, tumeshachukua hoteli ya Moshi Hotel na kampuni zingine ambazo zimeshindwa kutekeleza mikataba ya mauzo tumechukua.

Kuna kampuni TAFICO tumekwisha irudisha, kampuni DABAGA tumerudisha. Kwa hivyo, napenda tu kueleza kwamba na Mikumi kama itashindwa kuridhia na kutekeleza mkataba huo wa mauzo basi na yenyewe hatutasita kuirejesha. (Makofi)

Na. 200

Walinzi wa Jadi – Sungusungu

MHE. LUCAS L. SELELII aliuliza:-

Kwa kuwa walinzi wa jadi maarufu kama sungusungu wanafanya kazi nzuri kupunguza tatizo la ujambazi hasa wizi wa ng’ombe Kanda ya Ziwa na ulinzi wa raia wa nchi zao na kwa kuwa Serikali ya Awamu ya Nne imepania kupambana na ujambazi, kupunguza ujambazi nchini:-

(a) Je, kwa nini inapotokea katika ulinzi huo jambazi au mwizi akiuawa, sungusungu hao hukamatwa na kufunguliwa kesi ya mauaji?

(b) Je, Serikali iko tayari kuwaachia huru na kufuta kesi za sungusungu waliopambana na majambazi lakini wamewekwa ndani?

NAIBU WAZIRI WA USALAMA WA RAIA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Usalama wa Raia kabla ya kujibu swali la Mheshimiwa Selelii, Mbunge wa Nzega, lenye sehemu (a) na (b) napenda kutoa maelezo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, jukumu la msingi la jeshi la polisi ni kuzuia na kupeleka uhalifu, kulinda na kudumisha amani na usalama wa wananchi na mali zao. Katika majukumu hayo, Polisi hushirikiana na Polisi Wasaidizi (Auxilliary Police), wanamgambo na sungusungu.

Mheshimiwa Spika, wakati wa kutekeleza majukumu yao askari polisi, polisi wasaidizi, mgambo na sungusungu wanapaswa kuzingatia sheria na taratibu zilizopo pamoja na kuheshimu haki na uhuru wa wananchi kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

15 Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa kifungu namba 11 cha Sheria ya mwenendo wa Mashtaka Na. 9/1985 Sura ya 20 Revised Edition 2002, askari polisi, mwanamgambo au sungusungu wanaruhusiwa kumkamata mhalifu, hata hivyo kifungu namba 12 cha sheria hiyo kinamkataza askari polisi, mwanamgambo au sungusungu kumpiga, kumjeruhi au kumuua mhalifu wakati au baada ya kumkamata, hivyo askari yeyote atakayetenda kinyume na sheria tajwa atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria husika.

Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Usalama wa Raia, napenda sasa kwa umakini mkubwa kujibu swali la Mheshimiwa Selelii, Mbunge wa Nzega, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Spika, walinzi wa jadi maarufu kama sungusungu, wanamgambo, polisi wasaidizi na polisi wanapotekeleza majukumu hayo niliyoyataja hapo awali, hawapaswi kukamatwa na kufunguliwa kesi za mauaji bila sababu za msingi.

Ni pale tu inapothibitika kuwa wamekwenda kinyume cha sheria husika katika kumkamata mhalifu au kupoteza maisha ya mtu huyo, ndipo huchukuliwa hatua za kisheria na kufikishwa mahakamani.

(b)Mheshimiwa Spika, nchi yetu inatawaliwa kwa misingi ya utawala wa sheria na hivyo haitakuwa sahihi kufuta kesi zilizopo mahakamani ikiwa zina ushahidi wa kutosha kuwa wahusika walitenda makosa na kupoteza maisha ya watu. Ni vyema kuiachia Mahakama itoe uamuzi ili kila mmoja apate haki yake kwa mujibu wa sheria. Hata hivyo, Mkurugenzi wa Mashtaka (Director of Public Prosecutions) ndiye mwenye mamlaka kisheria ya kuondoa mashtaka ya jinai dhidi ya mtuhumiwa yeyote wakiwemo sungusungu ikiwa itaonekana hana hatia au hakuna ushahidi wa kutosha kuthibitisha kosa dhidi yake.

Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa hii kutoa wito kwa askari polisi, polisi wasaidizi na sungusungu kuzingatia sheria na kanuni wakati wa kumkamata mhalifu. Kwa upande mwingine tutaendelea kutoa mafunzo maalum kwa sungusungu wetu na askari wengine ili kuzielewa na kuziheshimu taratibu za sheria wakati wa kutekeleza majukumu yao ili kuepuka kufanya makosa wanafanya wajibu wao.

MHE. LUCAS L. SELELII: Nashukuru sana Mheshimiwa Bwana Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Lakini nasikitisha sana Mwanasheria hayupo na Waziri wa Katiba hayupo. Lakini nitaomba Serikali inijibu, kwa kuwa swali langu nimeuliza majambazi sijauliza wahalifu. Mimi nasisitiza majambazi na jambazi anapokuja kuiba au mifugo, au kuiba nyumbaji bila silaha. Inapotokea kwa wasungusungu au wanamgambo wamejihami na ikatokea yule jambazi ameuawa kule mjini husema, au polisi husema ameuawa na wananchi wenye hasira kali. Sasa inakuwaje hawa wanakijiji ambao ni wasungusungu inakuwaje wao hawana hasira kali wakati huyu jambazi ana silaha? Hilo swali la kwanza. (Makofi)

Swali la pili Mheshimiwa Bwana Spika, katika kufunga bajeti yake Waziri wa Sheria na Katiba niliuliza kwamba wasungusungu walioko katika mikoa ya Mwanza,

16 Shinyanga, Tabora wamewekwa ndani katika kutekeleza kupambana na majambazi. Waziri wa Sheria akasema nilete majina ya wasungusungu walioko ndani, nikamwambia mimi siyo Sekali ninyi Serikali mnawafahamu. Lakini kwa ushahidi wapo wasungusungu wa jimbo langu mpaka leo wako ndani na wengine wamekufa humo humo ndani hawajaachiwa. Sasa Serikali inasemaje juu ya kuwaachia huru hawa sungusungu wanaofanya kazi nzuri ya kupambana na majambazi ambao wanakuwa na silaha? (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA USALAMA WA RAIA: Mheshimiwa Spika, nilichosema ni kwamba Serikali siku zote itaheshimu misingi ya sheria, kwa wale ambao wanazungumzia suala la majambazi kwenye suala la kujihami, siku zote ipo sheria ya kujihami na hiyo huwa huchukuliwi kwamba wewe ni muaji. Lakini pale inapothibitika umekwenda kinyume na utaratibu huu wa sheria ndipo pale unapothibitisha kwamba wewe ni muuaji.

Kuhusu watu wanaosema Mheshimiwa Selelii hawa sita, ambao sasa hivi upelelezi wao umekamilika na kwa upande wa upelelezi umeonyesha kwamba watu hao wamekwenda kinyume na taratibu baada ya jalada lao kupelekwa kwa Mwanasheria wa Serikali Kanda ya Tabora. Na hivi sasa kesi hiyo imeshafunguliwa Mahakama Kuu. Hivyo ninamwomba Mheshimiwa Mbunge angoje uamuzi wa Mahakama Kuu ili haki itendeke, kufanya vingine na ushahidi unaonyesha kwamba yapo makosa yalifanyika itakuwa ni kinyume kuchukua utaratibu mwingine wowote ambapo mwingine atakosa haki yake. (Makofi)

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kumpongeza Mohamed Aboud kwa majibu yake mazuri sana hapa. Lakini ningependa kusema kwamba Serikali inaheshimu na kuthamini sana kazi nzuri inayofanywa na sungusungu katika Mikoa inayohusika. (Makofi)

Lakini Mheshimiwa Selelii anasema kule mjini wale wameuawa na watu wenye hasira kali. Hao wenye hasira kali na sungusungu wakifanya kinyume cha sheria lazima sheria ichukue mkondo wake. Serikali haitambui suala la watu kuua wenzao kwa utaratibu tu wa hasira kali halafu tukasema ni sheria. Hapana. Kwa hiyo, wa mjini na hawa wa sungusungu watekeleze sheria za nchi ndizo tutakazoheshimu. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Waziri kwa ufafanuzi huo. Tunaendelea na Wizara hiyo hiyo, swali sasa linauzwa na Mheshimiwa Phares Kashemeza Kabuye, Mbunge wa Biharamulo Magharibi.

Na. 201

Upungufu wa askari polisi

MHE. PHARES K. KABUYE aliuliza:-

17 Kwa kuwa upungufu wa askari polisi umechangia kwa kiwango kikubwa kuongezeka kwa uhalifu nchini:-

Je, ni lini Serikali itafikiria kuongeza idadi ya polisi kwa kupeleka vijana wengi katika vyuo vya polisi ili kupunguza uhaba wa watumishi hao na kudumisha amani nchini?

SPIKA: Kabla hujajibu Mheshimiwa Kabuye kipaaza sauti yako pale ni mbovu, haifanyi kazi? Mainjinia waangalie hiyo. Mheshimiwa Waziri wa Usalama wa Raia.

NAIBU WAZIRI WA USALAMA WA RAIA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Usalama wa Raia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Phares Kashemeza Kabuye, Mbunge wa Biharamulo Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, upungufu wa askari sio sababu pekee inayosababisha kuongezeka kwa uhalifu nchini. Zipo sababu nyingine ambazo ni za kiuchumi, kisiasa na kijamii zinazochangia kuongezeka na kushamiri kwa matukio makubwa ya uhalifu hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, Serikali inachukua hatua mbalimbali za kufanya maboresho kwa lengo la kulipatia jeshi la polisi uwezo zaidi wa kukabiliana na changamoto za uhalifu zinazojitokeza ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya askari wanaoajiriwa kila mwaka ili kuendana na kiwango cha askari mmoja kuhudumia idadi ya watu kati ya 400 na 700 ambayo ni uwiano unaokubalika kimataifa.

Mheshimiwa Spika, ili kufikia matarajio yanayolengwa na maboresho, Serikali katika mwaka huu wa fedha itaajiri askari 2611 kutoka idadi ya askari 2000 walioajiriwa mwaka 2006/2007 kwa lengo la kupata askari bora na waadilifu. Hata hivyo, pamoja na upungufu wao, Askari Polisi wetu bado wana uwezo mkubwa wa kudhibiti hali ya uhalifu nchini.

Mheshimiwa Spika, sanjari na maboresho hayo, Jeshi la Polisi litaimarisha ulinzi shirikishi kwa sababu ni moja kati ya mikakati thabiti ya kusaidia juhudi za polisi katika kukabiliana na uhalifu nchini, tutaendelea kuwa wabunifu katika kupanga, kuratibu na kusimamia mikakati mbalimbali itakayoliwezesha jeshi la polisi kutenda kazi kisasa zaidi.

MHE. PHARES K. KABUYE: Nakushukuru Mheshimiwa Spika, kwa kuwa masharti ya dunia yanafuatwa wakati wa amani na kwa kuwa Tanzania sasa majambazi yamezidi na kwa kuwa tu tabia ya kufanya crush programme matatizo yanapotufika na kwa kuwa polisi wanachukua miezi sita tu kupata mafunzo, wakati walimu wa miaka miwili wanaweza wakakidhi haja wakawepo kila kijiji. Ni kitu gani kinazuia Serikali kuweza kupeleka vijana wengi angalau kwa muda fulani tukafumba macho juu ya sheria za mataifa kwa kujaribu kutokomeza ujambazi katika nchi yetu?

18 NAIBU WAZIRI WA USALAMA WA RAIA: Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuimarisha ulinzi na inachukua jitihada mbalimbali kuongeza idadi ya askari wetu kutokana na hali halisi ya uwezo wa Serikali.

Lakini kubwa zaidi ni mafunzo ambayo kwa sasa tunayatoa kwa askari wetu na namna ambavyo wanaweze kuhimili katika kupambana na uhalifu. Pamoja na hilo kama nilivyosema katika jibu langu la awali tuna utaratibu wa polisi jamii ambao unawashirikisha wananchi katika kushirikiana kupambana na uhalifu.

Mheshimiwa Spika, kila siku ninasema hapa tulikuwa tunafanya tathmini ya kina kwenye kutafuta na kujua hasa ni mahali gani na wapi panahitajika kujengwa vituo vya polisi kwa nia hiyo hiyo ya kuongeza idadi ya askari karibu zaidi na wananchi.

Kwa hivyo naomba Mheshimiwa Kabuye afahamu kwamba kazi hiyo sasa imekwisha malizika na hata kule jimboni kwake tumeona kwamba kuna mahitaji ya vituo kadhaa vikiwemo katika vijiji vya Chamtakara, Kanihaa, Mtumagu, Nyamgombe, Katahoka, Nemba, Nyamigogo vijiji hivyo vyote tuna utaratibu wa kujenga vituo saba kule jimboni kwako kwa kadri hali fedha zitakavyopatikana.

Kwa hiyo, nakuomba uvute subira nakuhakikishia kwamba jeshi letu limejipanga vizuri kushirikiana na vyombo vingine vya dola kuhakikisha kwamba nchi yetu inakuwa salama na amani.

Na. 202

Utekelezaji wa Silaha Haramu

MHE. PARMUKH SINGH HOOGAN aliuliza:-

Kwa kuwa ujambazi ulikithiri sana miaka ya nyuma na kwa kuwa miongoni mwa hatua zilizochukuliwa ili kupunguza ujambazi huo ni pamoja na kuwaomba wananchi wasalimishe silaha haramu zote na hatimaye kutekelezwa na Serikali kwa kuchoma moto:-

(a) Je, Serikali inaweza kulieleza Bunge ni silaha haramu ngapi zilizokwisha tekelezwa mpaka sasa?

(b) Je, utaratibu kama huo wa kutekeleza silaha haramu hauwezi kutumika Tanzania Zanzibar?

NAIBU WAZIRI WA USALAMA WA RAIA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa ruhusa yako na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Usalama wa Raia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Parmukh Singh Hoogan, Mbunge wa Kikwajuni, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

19 (a) Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi ilianza kutekeleza mkakati wa kupambana na kutokomeza uzagaaji holela wa silaha ndogo ndogo na nyepesi mwezi Julai, 2001. Mpaka sasa silaha za aina mbalimbali 9,157 zimekamatwa au kusalimishwa, kati ya hizo silaha 8,540 zimeteketezwa kwa moto katika Mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, Kigoma na Zanzibar.

(b) Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza katika jibu langu sehemu ya (a), utaratibu wa kutekeleza silaha haramu unatumika pia Tanzania Visiwani. Kati ya silaha 8,540 zilizotekelezwa, silaha 1,000 ziliteketezwa katika Uwanja wa Amani – Zanzibar, tarehe 25 Julai, 2004.

MHE. PARMUKH SINGH HOOGAN: Mheshimiwa Spika, naomba kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri maswali mawili madogo ya nyongeza.

(a) Je, ni mafanikio gani yameshapatikana tangu operation hiyo kuanzishwa?

(b) Je, ni hatua gani zimechukuliwa ili kudhibiti silaha haramu zisiingie kiholela hapa nchini?

NAIBU WAZIRI WA USALAMA WA RAIA: Mheshimiwa Spika, kwa ruhusa yako na kwa niaba ya Waziri wa Usalama wa Raia naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Parmukh Singh Hoogan lenye sehemu a na b kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi mafanikio yaliyopatikana ni kukamatwa kwa silaha 9,157 na silaha 8,540 kuteketeza, kuhakiki silaha 52,700, wananchi kupata elimu ya hatari ya uzagaaji wa silaha na elimu ya kutunza silaha zao, wamiliki wa silaha wameweza kuona umuhimu wa kufuata taratibu zilizowekwa za kumiliki silaha na ili silaha hizo zisizagae ovyo, kuendesha operation za pamoja na nchi jirani ili kuzuia uingiaji wa silaha haramu, Serikali inapitia upya sheria ili kuiboresha zaidi kuhakikisha kwamba utaratibu wa umilikaji wa silaha unakuwa mzuri zaidi.

Mheshimiwa Spika, kwenye upande wa hatua ni kwamba kwanza ni kuimarisha ulinzi katika maeneo ya mipakani, kufanya operation na doria mbalimbali kuhakikisha kwamba silaha hizo haziingii nchini, kushirikiana na nchi jirani pamoja na Interpol kuhakikisha kwamba huko zinapotoka tuweze kuzizuia kabla ya kuingia nchini kwetu, kuelimisha wananchi kwa njia ya polisi jamii ili kutoa taarifa pale ambapo itaonekana kuna silaha iliyo kinyume na taratibu.

Mheshimiwa Spika, lakini kubwa zaidi baada ya kuhakiki tumeweza kutambua nani na nani alimiliki silaha kinyume na taratibu na wale waliomiliki kinyume na taratibu hatua zimechukuliwa dhidi yao.

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, muda wa maswali umepita na yapo matangazo kama kawaida. Kwanza ni kuhusu wageni na wale ni mara yao ya kwanza ningeomba

20 waelewe kwamba nitakapowatamka ni vizuri wasimame ili Waheshimiwa Wabunge waweze kuwatambua. Ninayo furaha kutangaza wageni wa Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi Prof. Juma A. Kapuya na Spika kwa sababu wanatoka majimbo ya Urambo Mashariki na Magharibi nao ni Waheshimiwa Madiwani kutoka Wilaya ya Urambo pale kwenye Speakers Gallery. Ningependa nimtambue Mwenyekiti wao Mheshimiwa Adam Malunkwi, ninashukuru Adam na wenzio wote Madiwani kwa jinsi mnavyoendesha Halmashauri ya Urambo huwa hainyimwi zile Capital Grant kwa sababu vigezo vyote mnatimiza, ahsante sana na muendelee hivyo na sisi Wabunge wenu wawili tuko tayari kuwaunga mkono, karibuni sana. (Makofi/Kicheko)

Naomba nimtambulishe Mheshimiwa Willium Chambala, Mwenyekiti wa Wilaya ya Urambo, sisi tuna bahati kwamba kule Urambo Mwenyekiti wetu wa CCM ni msomi aliyesomea Agricultural Economics. Kwa hiyo, sikufuata upayukaji halafu basi unachagua hapana, karibu sana Mheshimiwa Chambala na tunashukuru sana kuwa na wewe, pamoja nao ningeomba kwa upendeleo maalum wasimame ili watambuliwe Waheshimiwa Madiwani wa Viti Maalum na wamefuatana na wataalamu wafuatao Bi. Merry Luhuluha Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya, Bonaventura Sofu ambaye ni mwandishi wa vikao vya Halmashauri, Bwana Paulo Shija ni Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Mashariki ambaye ni Spika, Bwana Yasini Masebu ni Katibu wa Mbunge wa Urambo Magharibi ambaye ni Waziri wa Ulinzi. Tunaye pia kijana hapa Abdul Abdi maarufu kule Urambo kwa jina la Chepe ni mpiga debe mzuri sana. Chepe naomba usiingie katika kuvuta sigara na pombe nakuhitaji sana mwaka 2010, karibuni sana. (Makofi/Kicheko)

Waheshimiwa Wabunge tunao wageni wengine kama ifuatavyo Mheshimiwa Monica Mbega Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma na Mbunge wa Iringa Mjini anao wageni wake wafuatao ambao ni viongozi wa SACCOS za pale Iringa Mjini. Kwenye soko kuu wanaongozwa na ndugu Herman Sanga na wenzake wako tisa nao Emmanuel Mioka, Eliza Nyalusi, Yusta Mbilinyi, Raphael Ngulo, Shem Mpagama, Magnus Mwapinga, Hemed Kawago na George Mwaitege. Mheshimiwa Rosemary Kirigini anaye mgeni wake ambaye ni mdogo wake anaitwa Paul Kirigini, Mheshimiwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Mheshimiwa Sophia Simba, ana wageni kutoka Ilala ambao ni Bwana Mtoro Omary Shah, Twalib Kassim Berege, Bi. Mwasiti Shaban na Bwana Waziri Yahaya Waziri. Mheshimiwa Zungu angaliangalia kwa sababu naona hawa wageni wanatajwa wanatoka Ilala isije ikawa ni wapiga kura wanatorokea kwa Mheshimiwa Sophia Simba, karibuni sana. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Zaynab Matitu Vulu, Katibu wa Kamati ya Wabunge wanaotoka mikoa inayolima zao la korosho ameniomba nitangaze kwamba leo saa saba Waheshimiwa Wabunge wote wanaotoka katika maeneo na mikoa inayolima zao la korosho wanaombwa kukutana na Mheshimiwa Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika katika Ukumbi wa Pius Msekwa saa saba mchana, Waheshimiwa Wabunge kutoka mikoa ya korosho saa saba mchana Ukumbi wa Pius Msekwa kwa maongezi na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika.

21 Mheshimiwa Sophia Simba Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto ameniomba nitoe tangazo kwamba zile barua kwa Waheshimiwa Wabunge za kuchangia uanzishwaji wa Benki ya Wanawake Tanzania zimetolewa tangu jana tarehe 11, Wizara inaomba wale waliozijaza waziwasilishe kwa Mheshimiwa Waziri au Naibu Waziri wakati wanatoka baada ya kikao hiki na pia Waheshimiwa mnakumbushwa kuwa Afisa wa Wizara na Mtaalamu mwelekezi wa suala hili muhimu bado ataendelea kuwepo ghorofa ya pili chumba na 227. Kwa hiyo michango yote kuhusu Benki ya Wanawake Tanzania ishughulikiwe kwa njia hiyo, kuwaona Waziri au Naibu Waziri na pia kuwaona wataalamu chumba 227 jengo la utawala.

Mheshimiwa Halima Mdee ameniomba nitangaze kwamba Wabunge wote wa Kambi ya Upinzani watakutana leo saa saba mchana, amefumba sijui watakutana wapi lakini nadhani kwa sababu mbinu za Upinzani ni za chini chini wanajua wenyewe watakavyokutana saa saba mchana. Mheshimiwa Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Mheshimiwa amekamilisha zoezi la kuonyesha mgao wa fedha za mfuko wa barabara zinazoenda katika kila Halmashauri Tanzania kwa mwaka 2007/2008 na waraka huo umesambazwa katika sehemu zenu kwenye visanduku pale.

Kwa hiyo, kila Mheshimiwa Mbunge ataelewa kiasi gani cha fedha kimepelekwa katika Halmashauri yake kuhusu miradi ya barabara 2007/2008 lakini kwa tahadhari ameniomba niseme yafuatayo kwamba, inawezekana kuna Halmashauri kuwa ni kubwa kieneo lakini ikapata fedha ndogo za maintenance kwa sababu mtandao wao wa barabara ni mfupi. Hali kadhalika inawezekana kwamba kuna Halmashauri yenye eneo dogo ikaonekana imepata fedha nyingi za matengenezo ya barabara kwa sababu mtandao wake wa barabara ni mrefu zaidi, hii ni tahadhari tu ili orodha hii isianze tena kuwa ni kero na watu waanze manung’uniko kuhusu hayo. Hayo ndio matangazo sasa Katibu kwa orodha ya shughuli tena.

HOJA ZA SERIKALI

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka 2007/2008 Wizara ya Miundombinu.

(Majadiliano yanaendelea)

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tulikuwa bado tunaendelea na majadiliano na Orodha yangu jinsi inaonyesha naona kama imekaa pembeni lakini nakumbuka mchangiaji wa kwanza ni Mheshimiwa , Mbunge wa Kigoma Mjini na wengine wanaofuata ni Mheshimiwa Fatma Mikidadi, Mheshimiwa Wilson Masilingi na Mheshimiwa Lucas Selelii. Niseme tu kwamba katika orodha hii kwa bahati mbaya meza ilitumia ile sheria ya kusema wanaorudia kusema au waliosema mara moja na kadhalika. Basi wasiorodheshwe na matokeo yake nimegundua kwamba kwenye Kambi ya Upinzani hatuna wasemaji ilihali waliomba kwa hiyo baada ya majina haya manne nitapenyeza kutoa nafasi kwa Mheshimiwa Khalifa na baadaye karibu ya mwisho kwa Mheshimiwa Sanya ili tuweze kuwa na mchanganyiko mzuri, sasa namwita Mheshimiwa Peter Serukamba. (Makofi)

22 MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Spika, …..

SPIKA: Niwie radhi kuna tangazo la kikao cha Kamati ya Kilimo na Ardhi saa tano asubuhi chumba namba 428, Mheshimiwa Peter Serukamba endelea.

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Spika, nishukuru kwa kunipa nafasi kuwa mchangiaji wa kwanza asubuhi ya leo.

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kutoa pongezi kwa Waziri wa Miundombinu, kwa kweli hotuba yake ilikuwa nzuri sana na ameandaliwa vizuri nimpongeze yeye, Manaibu wake, Watendaji Wakuu wakiongozwa na Katibu Mkuu kwa kweli wameandaa hotuba vizuri sana. Baada ya hapo nichukue nafasi hii kumpongeza Waziri kwa mambo makubwa mawili aliyoyafanya. Waziri amefanya uteuzi katika ATC yetu na kilichonivutia zaidi Mkurugenzi Mkuu amempa bwana David Mataka naomba niseme mbele ya Bunge letu Tukufu hakuna asiyejua umahiri wake ni matumaini yangu sasa umahiri ule atauhamishia kwenye ATC yetu. Lakini pia amefanya uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa TANROADS kwa bahati nzuri mimi nimefanya kazi TANROADS kabla sijaingia kwenye Bunge lako Tukufu, hakika ninaamini TANROADS imepata kiongozi mzuri kwa sababu matatizo ya TANROADS yaliyokuwa ni uongozi walikuwa wana-lack management, matatizo makubwa TANROADS ni contract management na wamepata mtu wa kufanya kazi hiyo, ni matarajio yangu bwana Mrema atatupeleka kwa hari mpya, nguvu mpya na kasi mpya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo nilitaka nianze na kuelezea umuhimu wa infrastructure katika maendeleo ya nchi yetu, sisi Tanzania tumepata bahati kubwa sana, bahati yetu ni ambako Mungu aliamua nchi hii iwe hapa iliko leo na maana yake ni geography position ya nchi yetu. Sasa tunapopanga mipango yetu lazima tutumia advantage ya jiografia yetu kwa sababu engine ya maendeleo ni infrastructure, mimi siijui nchi yoyote iliyoendelea Duniani bila kuwa na infrastructure. Kwa hiyo tunapokuwa tunapanga barabara zetu, tunapanga resources zetu lazima tujenge barabara hizi kule ambako tunaamini tukipeleka pesa zetu zitarudi, kuna barabara ambazo ni muhimu sana kwa maendeleo ya nchi yetu barabara ya kwanza ni Manyoni, Itigi, Tabora na Kigoma. Siyasemi haya kwa sababu labda natoka Kigoma lakini nitawaambia advantage tukijenga barabara hii Kongo ya Mashariki kuna mzigo wa tani milioni nne, tunao mzigo Burundi, tunao mzigo Rwanda ukijenga ile transit business peke yake itatuingizia pesa nyingi sana kwenye nchi yetu kwa hiyo lazima maamuzi yetu yaende haraka tuweze kufanya vizuri kwenye area hiyo. Tunayo barabara ya Tunduma, Sumbawanga, Mpanda mpaka Kanyani tunayo barabara ya Kigoma Nyakanazi, Mwandiga, Manyovu, Mpanda, Tabora, Sumbawanga mpaka Kasanga Port. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, barabara hizi nimezitaja ili tuone umuhimu wa barabara hizi kwani unaposema hizi barabara maana yake unaenda kutafuta dola zilizolala kwenye nchi za jirani. Leo hii Kigoma ukifungua pakawa ni export zone una hakika watu wote watakuja kutoka DRC, kutoka Burundi, kutoka Zambia wote watakuja kufanya vitu vyao pale. Leo hii ukienda Uganda, Uganda walikuwa na hali mbaya sana huko nyuma lakini

23 sasa uchumi wao unakuwa kwa kasi kweli kweli lakini moja ya sababu kubwa ni wao kuwa wamepakana na Sudani ya Kusini kwa hiyo Waganda wale wanafanya imputation wanatoa vitu Dubai, wanatoa vitu Japan na Dunia ni kote wakishavifikisha pale Uganda na wao wanavi-export kwenda Kusini mwa Sudani, sasa ukiangalia barabara ya kutoka Kampala kwenda kule Gulu na kwenda Kusini flat ya magari inayoenda ni kubwa na matokeo yake wanapata dola nyingi sana. Ninaomba na sisi tuitumie fursa hii ya hapa Mungu alipotuweka, ninaamini Mungu alikuwa na sababu. Jiografia yetu ni muhimu sana na tukijenga barabara hizi hata gharama ya kufanya biashara ya ndani itapungua, kwa hiyo maana yake hata kukuza uchumi ni rahisi. Leo hii kuna maeneo ukienda Rukwa kule gunia la mahindi ni Sh.3,000/= lakini gunia hilo hilo Mwanza Sh.15,000/= kwa hiyo ukitaka kumkomboa mwananchi huyu wa Rukwa mfanye a-access hiyo market ya Mwanza tayari umeokoa maisha yao. Ukienda pale Kigoma kule Manyovu, Manyovu mkungu wa ndizi ambao unakaribia urefu wangu ni Sh.1,000/= lakini mkungu huo ungeufikisha hapa Dodoma, ungeufikisha Dar es Salaam mtu huyu umemkomboa tayari. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo suala la infrastructure tafadhalini tupambana nalo na nina amini Serikali ya awamu ya nne inaliweza hili, tukishaanza hilo kuna suala la Bandari ya Dar es Salaam, Bandari ya Kigoma na Bandari ya Kasanga hizi nazo ni za muhimu sana kwa maendeleo yetu. Singapore ni nchi ndogo sana lakini wamefanikiwa kwa sababu biashara kubwa ni ya bandari, ukienda kwenye bandari yao ni kubwa kweli kweli kwa hiyo maana yake na sisi Mungu ametupa maji haya tuyatumie kwa maendeleo yetu kwa hiyo lazima wenzetu wanaopanga mipango hii waipange kulingana na tunavyotaka kwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo nilitaka nichangie ni suala la ICT, tuna huu mkonga wa Taifa, Dunia ya leo ni IT World tunakoenda sasa ni Dunia ya mtandao, mna bahati nzuri Waziri amesema angependa wilaya zetu zote tunazi-connect kwenye mtandao, kwenye elimu faida ni kubwa, kufanya biashara itakuwa ni rahisi lakini lazima tu-invest kwenye jambo na kweli niwapongeze watu wa TCRA wanafanyakazi nzuri sana kwenye area hii cha msingi tuwape nguvu, tuwape pesa ili kazi iweze kwenda haraka.Jambo lingine ambalo nilitaka nichangie ni kwamba kuna suala la contract management maana Serikali imetenga pesa nyingi sana, kuna area moja tusipokuwa waangalifu gharama za miradi yetu siku zote zitakuwa zinaongezeka maana unaangalia anakuja mtu analeta certificate yake au analeta invoice yake, consultant anaipitisha na akishaipitisha huna choice lazima muilipe inakuja Wizarani, Wizarani pale wanaiangalia lakini lazima uipeleke Wizara ya Fedha ile certificate, maana yake ni nini? Huu mlolongo ni mkubwa matokeo yake wanasema kuna contract zingine ukishapitisha siku 30 au 50 unaanza kulipa interest, unaanza kulipa damages na ndio maana jana Waziri amesema na kwenye Kamati yetu tumesema kuna bilioni karibu 128 za wakandarasi wanadai zipo na hazijafanyiwa mambo. Kwa hiyo mimi naomba sana watu wa Wizara ya Fedha watusaidie mimi sioni kwa nini hizi certificate ziende Wizara ya Fedha unless hatuaminiani hapa, tunampa agent wetu wa kufanyakazi ya kujenga barabara ni Wizara ya Miundombinu, ndio kazi tunawapa hawa lakini sasa tuwasimamie wafanye hii kazi lakini tukisema wakishaleta certificate na sisi kwetu zije tuanze kuzikagua, hivi unavyokagua certificate kwanza barabarani haukwenda, unakagua nini? Kwa hiyo mimi

24 ningeomba jambo hili nalo tulifanyie kazi sana. Lakini kuna huu mradi wa barabara wanaita special project, special project inayo matatizo yake lakini nashukuru sana Waziri alivyofika kwenye Wizara hii kazi ya kwanza ilikuwa ni kutatua matatizo ya special project lakini kuna jambo moja lazima tulikubali, maamuzi yaliyofanywa ya kujenga special project ni maamuzi mazuri ni maamuzi ya kujitegemea na heshima ya Taifa lolote ni kujitegemea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa naziangalia hapa kwenye kitabu kwa sasa tunajenga kwa hela zetu, nitataja barabara chache lakini kuna Kyamiolo – Msagala kilometa 312, kuna Samnajoma kilometa nne, kuna Tarakea – Kamanga kilometa 32, kuna Nangulukuru – Mbwemkuru kilometa 95, Mbwemkuru – Mingoyo kilometa 95, Dodoma – Manyoni 127, Singida – Manyoni 118 jumla ni kilometa 785. Sasa ukiangalia barabara zote hizi tunapofika Desemba, 2008 tutakuwa tumemaliza kuzijenga na zingine zitamalizwa mapema sasa ningeomba wenzetu wa miundombinu idea hii iliyoanzishwa isije ikafika sehemu ikaachwa, inatakiwa tujipange unapomaliza barabara moja ile fedha unaihamishia kwenye barabara nyingine. Unatoka Tabora kuna Tabora – Nzega ni kilometa 116 kwa hiyo ukimaliza hii unapeleka, kuna Shinyanga – Bariadi ukimaliza hapa unahamishia ile pesa kule unaenda taratibu. Hili tusiliache ilikuwa ni idea nzuri ni idea ya kupata heshima kwenye nchi yetu, ni idea ya kujitegemea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini nilitaka niongeze pia jambo lingine, jana rafiki yangu Kaboyonga aliliongea hapa, ujenzi wa barabara unahitaji pesa nyingi sana na mimi nakubali lakini lipo suala la kutumia long term bonds, long term bonds ni sources of finance ni govern papers hizi tunazoziuza, ziko advantage za kutumia hizi long term bonds na advantage ya kwanza ni non inflationary lakini advantage ya pili tunatumia internal source of finance lakini rahisi ku-meet our development goals tumepanga kufanya jambo hili hatuna pesa government inauza zile government bonds kwa hivi financial institutions miaka 10 au miaka 15 inapofika miaka 10 hujaweza kulipa ile pesa ni rahisi una-issue nyingine ili upate pesa umlipe huyu unaenda mbele. Halafu tuitumie road fund board yetu iwe inatenga fedha kidogo kwa ajili ya kulipia hizo interest kwenye hizo long term bonds zetu, nawaambieni tukifanya jambo hili nchi hii tutawashangaza Mataifa, tutajenga nchi hii na tutaenda kwa kasi kubwa kweli kweli.

Lakini pia jambo lingine ni suala la ma-contractor tumeweka hela nyingi sana, mimi naomba tufanya kila tunaloweza tutengeneze uwezo wa ma-contractor wetu na mimi ningesema siyo vibaya tukitengeneza data base tukawa hata na ma-contractor 20 wakubwa tuwajenge, tukiwajenga hawa nitawaambia faida zake faida ya kwanza watatoa employment, faida ya pili watapata kazi nyingi watapata pesa nyingi. Ma-contractor wa ndani wakipata pesa nyingi faida ya kwanza ni kodi, wakipata bilioni 500 maana yake 30 percent inaenda Serikalini this very clear, siku moja Rais Mwinyi mwaka 1987 alimuuliza Mahafili alikuwa PM wa Malaysia kwamba nyie mnafanyaje? Akasema mimi kazi moja ninayofanya kubwa ni kubwa ni kuendeleza private sector, sasa private sector ndio engine ya growth lakini anasema nikimuendeleza private sector kila faida anayopata ya dola 100, dola 30 ni za kwangu kwa hiyo unapanua wigo wa kodi kwa hiyo mimi ningeomba tuwaendeleze watu wetu hawa. (Makofi)

25 Baada ya hilo la ma-contractor nilitaka pia nichangie suala la postal code, sasa hivi tunaenda kutafuta vyeti vya uraia (Identity Cards) haziwezi kufanya kazi kama hakuna postal code lakini postal code ukiangalia hapa kwenye bajeti yetu hatujaipa kipaumbele cha kutosha, ninaomba wenzetu waweke pesa ya kutosha ili mradi huu tuumalize na sisi twende kulingana na wenzetu. Nilitaka pia nichangie suala la CADCO, tumeanzisha ATC yetu naomba sana wale CADCO tumewapa anga la Kilimanjaro, anga lile wanapaki magari tafadhalini tukubaliane ilo anga tuwape ATC kwa sababu tunapotaka kuipeleka ATC yetu siyo hapa karibu tunataka kuwashangaza Mataifa kwamba Watanzania wanaweza hatuwezi kuwashangaza hatuna pa kutengeneza ndege zetu. Naomba sana watu wa CADCO waturudishie anga letu ili ATC wafanye kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la mwisho ninataka kuwapongeza TTCL kwa kuanzisha mobile, nina hakika tunaenda mbali zaidi. Lakini ukurasa wa 101 wa kitabu hiki nataka tu baadaye Waziri aniambie wamepanga contraction ya Mwanza na Kigoma Airport bilioni moja na milioni 100 nilitaka tu nijue ni shilingi ngapi zinaenda Kigoma Airport basi hilo ndio nilitaka nifahamu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo naomba tujipange upya na watu wetu wa mipango watusaidie ku-scrunize hii mipango yetu ili tuweze kwenda mbali zaidi naomba kuunga hoja mkono. (Makofi)

MHE. FATMA ABDALLAH MIKIDADI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ili nami niweze kuzungumzia hoja hii ambayo ipo mbele yetu.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa, napenda kuchukua nafasi hii kuipa pole familia ya ndugu yetu Chifupa kwa kufiwa na mwanaye. Mwenyezi Mungu amweke mahali pema peponi Mheshimiwa Amina Chifupa Mpakanjia. Tunaomba sana familia hiyo iwe na subira, amen.

Mheshimiwa Spika, jambo la kwanza ambalo napenda kulizungumzia katika suala hili la miundombinu ni suala la airport Lindi. Sisi Lindi tulikuwa na airport tangu wakati wa Mkoloni. Airport hii ilikuwa inatumiwa wakati wa vita ya pili ya dunia ya mwaka 1939-1945. Airport hii ilishindiliwa vizuri sana naweza kusema kwamba ni moja kati ya airport imara nchini. Tatizo la airport ya Lindi ni lami tu kama ingewekwa lami nafikiri ingeweza kutumika kufungua milango ya biashara Kusini na nchi zote za Kusini mwa Tanzania nchi za SADEC na ukizingatia kwamba EPZ itakuja Mtwara, mlango wa biashara Mtwara, kwa kutumia airport ya Lindi biashara itafunguka endapo airport itakarabatiwa.

Mheshimiwa Spika, naomba airport ya Lindi ikarabatiwe ili iweze kutumika hapo baadaye kwa sababu sasa hivi msongamano wa airport ya Mtwara ni mkubwa sana. Watu wa Lindi wote wanakuja Mtwara, watu wa Ruvuma wote wanakuja Mtwara kupanda ndege. Sisi njia zetu kubwa za usafiri ni anga. Sasa tunaomba tafadhali tusaidiwe airport ya Lindi iweze kukarabatiwa ili nasi tuweze kupata usafiri. Hilo la kwanza. (Makofi)

26 Mheshimiwa Spika, la pili, ni suala la mawasiliano ya simu za mkono. Sisi Mikoa ya Lindi na Mtwara tuna matatizo ya simu. Kama walivyozungumza katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri, sehemu nyingi tuna simu zile za kukoroga. Sasa tunaomba maeneo ambayo hayana simu basi tusaidiwe. Sisi katika Mkoa wa Lindi katika Wilaya zake za Liwale, Nachingwea, Ruangwa, Kilwa na Lindi Vijijini kuna baadhi ya maeneo hayana simu mpaka sasa, simu za mkono. Kuna maeneo ambayo yana simu za kukoroga lakini hata na zenyewe hazifanyi kazi. Kwa mfano Wilaya ya Ruangwa simu zake za kukoroga ziliibiwa nyaya zake tangu mwaka 2005 mpaka leo nyaya zile hazijatengenezwa kwa hiyo mawasiliano hakuna. Sasa tukiwekewa simu za mkono itakuwa ni rahisi mno. Kuna maeneo mengine ya Kilwa ambayo ni nyeti tunahitaji simu za mkono ziweze kutusaidia. Kwa mfano ya Seleou Kilwa, ambapo watalii wengi wanakuja na uwindaji unafanyika, wale wanahitaji simu za mkono. Kuna sehemu za Zinga Kibaoni, Miguruwe, Migeregere, Njinjo, Nanjirinji, hivyo Kilwa tunahitaji simu za mkono. Naomba sana na sisi tupelekewe hao Waheshimiwa wanaohusika na simu za mkono kama vile Zantel, Tigo, Vodacom, Celtel na kadhalika. Hilo ni ombi langu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni wimbo wa Kusini wa barabara ya Kibiti – Lindi. Barabara hii mpaka imeongezeka ikawa Kibiti - Mingoyo. Barabara hii ni wimbo wa Kusini kwa sisi kwetu Lindi kwa sababu tumeizungumzia miaka nenda rudi tangu tumepata uhuru. Mimi naomba tafadhali katika bajeti hizi za sasa zinazokuja ibaki sasa historia tu. Tukiondoa tatizo la barabara ya Lindi – Kibiti – Dar es Salaam nafikiri Kusini hatutakuwa na matatizo tena. Suala la kipande cha kutoka Daraja la Mkapa kuja huku Lindi hadi Somanga pale ni matatizo makubwa ni kilomita 69 pana matatizo makubwa sana. Tatizo hili limeweza kugundulika wakati waliposafiri wenzetu waliotoka kwenye kampeni Ruvuma kuja Dar es Salaam walipopigwa makofi pale ndipo tatizo likajulikana lakini pale tatizo kila siku lipo. Watu wanapigwa, wananyang’anywa mizigo, ndani ya gari, pale ndipo majambazi wa silaha wanapoishi kwani wanajua watapata kitu kwa sababu pale yanapopita magari, hayaendi kwa haraka huenda polepole kwa sababu kuna mashimo makubwa, kuna pori kubwa, kuna mchanga mwingi na hakuna ukarabati unaofanywa, kwa hiyo majambazi hupata urahisi wa kuvamia. Tunaomba Serikali itengeneze sehemu hiyo haraka.

Mheshimiwa Spika, sasa kipande kile angalau pangewekwa changarawe wakati tunasubiri mkandarasi aendelee na kazi zake ingekuwa ni msaada mkubwa sana. Kwa hiyo, tafadhali tusaidieni hiki kipande cha kilomita 69 kutoka Daraja la Mheshimiwa Mkapa kuja Kilwa (Somanga).

Mheshimiwa Spika, lingine ambalo napenda kuzungumzia ni suala hili la barabara nyingine za kawaida barabara za Halmashauri. Kuna barabara moja inayotoka Nanganga – Ruangwa. Barabara hii ilipewa msaada wa HIPIC ambapo zile nchi maskini huwa zinapewa msaada kutoka HIPIC. Barabara hii ni kilomita 60. Baada ya kupewa msaada huu ilikuwa itengenezwe kilomita 60. Kwa bahati mbaya tenda ilichelewa kwa hiyo muda wake ukawa umepita, thamani ya pesa ikawa imepanda. Kwa hiyo, badala ya kutengeneza kilomita 60 zikawa zimebaki fedha za kilomita 40. Kwa hiyo, sasa hivi mpango wake ni kutengeneza kilomita 40 kutoka Nanganga – Mitope badala ya Nanganga – Ruangwa na hivyo dhamira ya kufikia mjini Ruangwa

27 haitakuwepo.Tunaomba kilomita 20 zilizoachwa kwa mpango wa HIPIC (World Bank) kutokana na kucheleweshwa kwa tenda hizi tungeomba basi angalau Serikali ya Tanzania iweze kumalizia kulipia hiyo kilomita 20 kwa sababu sio kosa la wananchi hawa wa Ruangwa. Hili ni kosa Kitaifa, wasiadhibiwe wananchi wa Ruangwa.

Mheshimiwa Spika, halafu hawa waliopewa tenda kwa kweli mpaka sasa wanasuasua wameweka vifaa pale Nanganga lakini kazi inayofanyika ni ndogo sana. Mwaka huu watu wengi wanaotoka Ruangwa kuja Lindi kwa shughuli mbalimbali wamezama sana kwa ubovu wa barabara. Yaani ile barabara badala ya kutengemaa sasa hivi watu wanazama. Zamani walikuwa wanapita vizuri tu lakini sasa hivi watu wanazama kwa sababu wameingiza matope. Kwa hiyo, ni matatizo. Kwa hiyo, tungeomba usimamizi wa dhati ufanyike pale ili kazi iende kwa sababu tenda ilikuwa ni miezi 18, sasa hivi ni mwaka wa pili sasa kazi haiendi popote. Tunaomba sana suala hili lifuatiliwe.

Mheshimiwa Spika, halafu kuna barabara ya Ruangwa – Mbwenkuru – Nangurukuru ambayo sisi wananchi tulidhani kwamba tukiifanyia kazi tunaweza kupunguza kilomita 100. Ukipitia Lindi barabara hii inatoka Masasi – Ruangwa – Mbwenkuru – Nangukuru. Kwa hiyo, tukajitahidi wananchi sisi wa Kilwa na Ruangwa kujenga daraja wenyewe kwa hiari yetu na kwa kujitolea daraja lenye gharama ya Sh.200mil ili kufuta kilomita 100 tusipite Lindi, tupite shortcut ya Nangurukuru kupitia Mbwenkuru, unatoka Masasi – Ruangwa – Mbwenkuru – Nangukuru – Dar es Salaam, unafuta kilometa 100. Hii barabara wananchi wa Kilwa na Ruangwa tayari wameshajenga daraja kwa hiari yao, lililogharimu milioni 200 na liko tayari magari yanapita, daraja ambalo ni imara kabisa. Tunaomba basi Serikali barabara hii iangaliwe kwa macho mawili kwa sababu ni shortcut inafuta kilomita 100. Vile vile ni barabara nzuri ambayo ingeweza kuwa mbadala ya barabara hii ambayo inachelewa ya Kibiti – Lindi. Tunaomba Serikali isaidie waiweke iwe aidha ya Kitaifa au ya Mkoa. Sasa hivi iko tu pale kama ya Halmashauri. Tunaomba waiangalie kwa jicho la huruma barabara ile.

Mheshimiwa Spika, lingine ni barabara itokayo Kilwa halafu Njia Nne – Kipatimu kupitia Chumo. Barabara hii ilipewa tenda kwa D. Shapria lakini imechukua muda mrefu kweli kuanza mpaka sasa inasuasua tu. Wale waliowekewa X tangu mwaka jana mpaka sasa wanasubiri malipo yao hawajafanya kitu chochote. Sasa kuna kero pale. Wanasema ni vipi mbona hatupewi chochote hatuambiwi chochote. Badala ya sisi kupewa zile pesa na kwenda mahali pengine kujenga lakini hatuambiwi kitu chochote. Tumewekewa X hatupewi fedha zetu, barabara haitengenezwi. Hayo yalijitokeza nilipokwenda kijiji cha Chumo Wilayani Kilwa katika ziara na wakaomba msaada walipwe fidia za majumba yao na mazao yao na vile vile basi kazi ya ujenzi ianze ili barabara iwe safi. Nami ninawasilisha suala hili hapa Bungeni rasmi.

Mheshimiwa Spika, kwa maoni yangu ningeshauri kwamba uchunguzi wa kina ufanyike aidha huyu D Shapria aangaliwe ni kitu gani kinamfanya asitengeneze barabara ile wakati tenda amepewa labda hajapewa pesa au vinginevyo, badala ya kumwacha. Wananchi wanalalamika na wao hawaonekani. (Makofi)

28 Mheshimiwa Spika, lingine ambalo napenda kulizungumzia ni suala la vivuko. Suala hili, namshukuru Mheshimiwa Waziri Chenge, Mheshimiwa Dr. Mahanga, Mheshimiwa Maua Daftari na Katibu Mkuu Ndugu Bukuku kwa kazi nzuri waliyoifanya kwa kushughulikia vivuko. Kwa kweli vivuko vina thamani yake ya peke yake. Wametaja ukarabati wa vivuko mbalimbali kwa mfano Kigamboni, Kigogo, ununuzi wa kivuko cha Ruhuhu, ununuzi wa kivuko cha Kilombero na matengenezo ya kivuko cha Elina na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, naomba baada ya kutengeneza vivuko hivi vikubwa na maarufu sana au vilivyokuwa vinahitajika sana katika nchi hii, vile vile sasa waangalie katika maeneo mengine ambayo yanahitaji vivuko. Kuna maeneo ambayo yanahitaji vivuko kama hivi, lakini Serikali sijui kama ina habari lakini kama haina habari basi mimi nawataarifu. Katika Mkoa wa Lindi kuna maeneo mawili ambayo kwa kweli tunahitaji vivuko. Kwa mfano kuna eneo la kivuko kutoka Lindi Mjini kwenda Kitunda. Kitunda ni mahali ambapo wananchi wa Lindi mjini ndiko wanakolima sana. Hawawezi kufika huko mpaka upande boti. Wanapanda boti ndogo ndogo wengine wanakufa njiani kwa ajali wengine wanafika lakini kule ni sehemu nyeti sana kwa kilimo.

Sasa tungeomba waangalie sasa vivuko vingine vidogo vidogo ambavyo watatumia kwenda kule badala ya kutumia boti ndogo basi watusaidie na sisi kuangalia vivuko hivi. Hiki kinatoka Lindi mjini kwenda Kitunda. Kingine kinatoka Kilwa Masoko kwenda Kilwa Kisiwani. Kule kuna shughuli za utalii na kilimo wanatumia mashua wasaidieni vivuko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine la mwisho ambalo nataka kuzungumzia ni masuala ya barabara na hasa msongamano wa magari Dar es Salaam. Ingawa mimi sihusiki na Dar es Salaam lakini nahusika kwa namna moja au nyingine. Wakati napita kuja Dodoma nakanyaga Dar es Salaam.

Wakati nakaa Dar es Salaam kwa ajili ya shughuli mbalimbali za Kamati katika Bunge pale ndipo napokumbana na adha ya Dar es Salaam. Wakati mwingine huwa nafikiria hii ni kwa sababu Wabunge wote 300 na zaidi wako Dar es Saalam na magari yao ni mengi! Kwa hiyo, tunaomba mtusaidie.

Mheshimiwa Spika, wazo langu mimi ni kwamba Serikali ifanye mpango wa dharura wa kuweka usafiri wa treni. Sasa hivi tuna mabehewa mengi ambayo hayatumiki. Ninashauri kwamba mabehewewa hayo yafanyiwe ukarabati kama mabehewa 5 (matano) ili yawe yanatumika katika maeneo yenye laini ya treni na vituo vya treni mjini Dar es Salaam. Kama yale ya reli ya Kiwalani, Tabata Relini, TAZARA, Ilala na Railway Station, pia katika mitaa ya Ubungo, Tabata Relini, Mabibo, Buguruni na Yombo Vituko. Nchi nyingine za nje hufanya hivyo kwa kutumia treni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, ninaunga mkono hoja hii mia kwa mia ahsante. (Makofi)

29 MHE. WILSON M. MASILINGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia hoja ya Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu.

Mheshimiwa Spika, leo ni siku yangu ya kuzaliwa. (Makofi)

SPIKA: Happy Birthday.

MHE. WILSON M. MASILINGI: Nashukuru sana Mheshimiwa Spika.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa leo ni siku yangu ya kuzaliwa, nianze kwa kumshukuru Mungu kwa mara nyingine kuniruhusu nisherehekee siku yangu ya kuzaliwa nikiwa ndani ya ukumbi wa Bunge. Leo nimefikisha miaka 51. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa hili. Namshukuru mke wangu na watoto kwa salamu za pongezi. Nakushukuru sana Mheshimiwa Spika huwa unanitakia mema na kunipongeza siyo tu kwa siku ya kuzaliwa bali hata kunipa ushirikiano ndani ya Bunge na nje ya Bunge. (Makofi)

Aidha, naishukuru Redio Tumaini na watangazaji wake, siwajui majina bahati mbaya na sijawahi kuitembelea lakini mfufulizo karibu miaka mitano huwa wananiimbia kawimbo ka happy birthday. Leo nimepigiwa simu nyingi kutoka Dar es Salaam kwamba wametangaza tena. Ninawashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kweli mimi nilikuwa nasahau siku yangu ya kuzaliwa mpaka nilipooa na huwa wananikumbusha sana siku hii ambayo sijawahi kuisherehekea bali ni kumshukuru Mungu kwamba aendelee kuniweka hapa duniani nikae miaka mingi sana. (Kicheko).

Nawashukuru Waheshimiwa Wabunge mlionipongeza, ninawashukuru marafiki zangu wote na napeleka pongezi za dhati kabisa kwa rafiki yangu Engineer Kanali Rwabukambala ambaye naye anakumbuka siku ya kuzaliwa kwake na amenipigia simu asubuhi tunasherehekea wote naye namwombea miaka mingi zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa rafiki yangu hapa Mheshimiwa Lekule amenipa ofa ya kwenda kula nyama choma ambayo haina Rift Valley. Nakubali mwaliko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda kuungana na Waheshimiwa Wabunge wenzangu kutoa salam za rambirambi kufuatia msiba mkubwa uliotufika kufuatia kifo cha Mbunge mwenzetu Mheshimiwa Amina Chifupa Mpakanjia na Marehemu wote waliotangulia mbele ya haki. Naomba Mwenyezi Mungu azilaze roho zao mahali pema peponi, amen.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kusema naunga mkono hoja iliyowasilishwa na Mheshimiwa Waziri na nampongeza Mheshimiwa Waziri, Manaibu Waziri wote, Katibu Mkuu na watendaji wote ndani ya Wizara kwa kazi nzuri ambayo wanaendelea kuifanya katika kutuletea maendeleo ya miundombinu. (Makofi)

30 Mheshimiwa Spika, jana wakati najiandaa kuchangia nilikuwa na mashaka kama mchango wangu utakuwa na nguvu sana. Lakini leo asubuhi niliposikiliza kwenye vyombo vya habari nikasikia kauli nzito alizozitoa Mheshimiwa Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Jakaya Kikwete Mwanza huko, nimefarijika kwamba nitachangia kwa raha kabisa.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais amenukuliwa na nitasahihishwa kama hakuyasema. Amesema “watendaji wamsaidie kuishauri Serikali kwa kufikiria mambo mazito na kwa kutazama mbele zaidi kwa kiwango cha hata miaka 50 mbele sio mambo ya hapa hapa karibu. Akatahadharisha kwamba Watanzania tuna matatizo ya kusema sana na kutekeleza kidogo“. Hizo ndizo kauli anazonukuliwa kuzisema kwenye vyombo vya habari na mimi naviamini vyombo vya habari.

Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Rais kwa kurudia maneno haya. Mimi nimemsikia mara nyingi akisema kauli nzito za namna hii za kuthubutu. Ni kiongozi anayependa kuthubutu. Watendaji ushauri wangu wa kwanza kwa washauri wetu wanaowashauri Waheshimiwa Mawaziri na Manaibu Mawaziri na Mheshimiwa Bukuku Katibu Mkuu naye namfahamu labda kama amebadilika baada ya kuingia Miundombinu ni mkereketwa wa kuthubutu, shaurini Serikali mambo mazito ya kuthubutu bila woga na mlipatie Bunge changamoto ya kutoa maazimio ya kuweza kuharakisha maendeleo ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda nisisitize kwamba ushauri uliotolewa na Kamati yetu ya Bunge ya Miundombinu na hoja ambazo zimewasilishwa kupitia taarifa ya Mwenyekiti na maswali yaliyoulizwa naomba Serikali iyajibu kwa makini na hasa hili suala la madeni ya makandarasi. Sisi hatupo kwenye Kamati ya Miundombinu lakini wasiwasi ulioelezwa na Kamati ya Bunge kwa niaba yetu ni vema yatolewe maelezo kulikoni imekuaje tunalimbikiza madeni ya makandarasi jambo ambalo linatishia kusitisha kasi za ujenzi wa barabara zetu?

Mheshimiwa Spika, katika eneo la barabara, napenda kuishukuru Serikali kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Muleba Kusini, kwa kuwa kazi ya kujenga barabara kwa kiwango cha lami kutoka Kigoma – Muleba – Biharamuro – Lusahunga imenza na barabara ya Kyamyorwa – Kimwani na Nyakabango – Buzirayombo na yenyewe inaendelea vizuri sana mpaka Geita Usagara. Mimi kwa niaba ya wananchi naishukuru Serikali na nawahakikishieni ushirikiano wetu kuwasaidia pale mtakapohitaji msaada wetu.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu, naomba barabara ya Nyakanazi – Sumbawanga – Tunduma ipewe uzito wa kipekee sana na barabara ya Manyoni – Itigi – Tabora – Urambo – Kigoma. Hayo ndio mambo mazito ambayo Mheshimiwa Rais anaomba mumsaidie. Tumepewa taarifa kwamba Mheshimiwa Rais anahangaika kutafuta fedha za barabara hizi. Wataalam tusaidieni kutafuta fedha za barabara hizi. Wataalam tusaidieni fedha hizi zinaweza kupatikanaje? Sisi ni wanasiasa. Mheshimiwa Kaboyonga ni mtaalam wa kifedha ingawaje ni mwanasiasa. Mimi kila anapochangia natamani nipunguziwe dakika tano amalizie hoja zake. (Makofi)

31 Mheshimiwa Spika, nadhani ifike wakati tuangalie uwezekano wa kubadilisha kanuni zetu ili kuruhusu mchangajiaji usimame uruhusu dakika tano zikatwe kwenye nafasi yako baadaye ili mtu amalize hoja nzito za namna hii. Uingereza inafanyika mtu una-yield dakika na mwanzoni baada ya uhuru hapa ilikuwa inafanyika pia. Namkopesha anachangia mambo mazito. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ushauri mwingine. Mheshimiwa Waziri wakati unajibu hoja nakuomba tafadhali sana jaribu kutupatia taarifa ya kiporo kuhusu fidia ya wananchi wa Kagoma, Muleba, Kasharunga, Lusahunga na Kyamyorwa, Kimwani, Nyakabango ambao wameahidiwa valuation kufanyika mara ya pili na wataalam wamenieleza isivyo rasmi kwamba imefanyika, hatua ya Serikali imefikia wapi kuwafidia? Kila ninapoenda Jimboni naulizwa hili. Mheshimiwa Waziri Mkuu katika ziara yake aliulizwa hili pale Muleba na Kasharunga. Sasa ni kutoa maelezo kama pesa hazijapatikana zikipatikana walipwe haraka sana kwa sababu kweli barabara ya lami tunaipenda sana na hawa wananchi ambao wamevunjiwa nyumba zao kwa ajili ya kupitisha barabara au mazao yao kuharibiwa ni vema na wenyewe tuwape fidia ya kuwafariji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ushauri unaofuata. Kwenye kitabu chako Mheshimiwa Waziri nimeona umetenga Sh.105milioni kwa ajili ya barabara ya Muleba, Nshamba, Kamachumu Muhutwe. Ninaomba nishauri hivi, pesa hizi kwa sababu ni kidogo na barabara hiyo sio mpya kuna vijiji kila baada ya mita 500, vijana wetu hawana ajira, akina mama hawana ajira, toeni Sh.105milioni hizi kwa wananchi hawa, tutawapatia makoleo, tunaweza kukodisha malori yakasomba kokoto na kukodisha hata vijiko tutumie fedha hizi tutaikarabati barabara nzima badala ya kilomita 10. Huo ndio ushauri wangu kwa sababu barabara hii inapita vijijini.

Mheshimiwa Spika, kuhusu usafiri wa majini. Katika Ziwa Victoria, meli ya M.V. Victoria imesimama. Nilikwenda Jimboni kwa siku tatu hivi ilibidi nilale Mwanza baada ya ndege kutua jioni saa kumi na moja nikakuta Precision imeondoka. Meli ya M.V. Victoria haifanyi kazi, wanatumia kimeli cha mizigo cha Serengeti ambacho ni hatari kwa sababu hakiwezi kuhimili mawimbi. Tafadhali sana Serikali ushauri ninaowapa kwa vile mmeona tumeingia ubia wa ndege umeshindikana hata kwenye maji tumejaribu miaka 10 imeshindikana, Serikali irudi kusaidia usafiri wa maji. Nunueni meli kubwa kuliko M.V. Victoria iliyonunuliwa karibu miaka 40 iliyopita. Nunueni meli zaidi ya moja izunguke Ziwa Victoria Kisumo, Jinja, tufanye biashara, tukaribishe utalii na tuwapunguzie wananchi wetu kero ya usafiri wa maji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu usafiri wa anga. Uwanja wa ndege wa Bukoba ni mzuri. Ni kweli kama taarifa inavyozungumza uko kwenye kiwango cha changarawe. Lakini kwa mazingira ya Bukoba wengi mnafahamu Bukoba mvua zinanyesha mfululizo mwaka mzima. Hata nilipokuwa Jimboni tarehe 5 na 6 mvua ilinyesha kubwa ndege yetu ya Precision ilichelewa badala ya kuondoka saa tano tuliondoka saa kumi kutoka Mwanza kwenda Bukoba. Tulipotua uwanja ulikuwa matope na ni hatari na ukimwangalia Rubani, bwana Mazura rafiki yangu yeye hatui huko siku hizi alikuwa anatua zamani alipokuwa Pilot mdogo sasa hivi ni mtu mzito anaendesha Boeing ambayo

32 haiendi Bukoba, lakini sisi tunaowaangalia Marubani wakiwa wanatua Bukoba wanakaza uso, mishipa, shingo wakati wa ku-land mpaka sote tunaogopa atamudu hii ndege? Je, wakiwa wanatua Marais wetu, Waziri Mkuu na viongozi wengine, ni hatari. Kwa hiyo, Bukoba iangaliwe sio kama viwanja vingine vidogo vidogo, kwa ajili ya usalama wa abiria iwekwe lami haraka sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Air Tanzania ni kweli Mkurugenzi Mkuu Mataka ni mchapakazi, Mwenyekiti wake na Bodi nzima na wote tunafahamu Air Tanzania ni wachapa kazi lakini tusipowaruhusu wakafanya kazi kibiashara, tukarudisha ATC ya zamani ya kuwabanabana, shirika la umma, shirika la umma, hii tunayosema ndoto tunajidanganya. Wapeni pesa.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwanza tuwaondolee deni la dola milioni 4, lichukuliwe na Serikali halafu tuwape mabilioni wanayotaka kwa sababu biashara ya ndege ni biashara sio huduma tu, wafanye biashara washindane na Precision na watue Bukoba pia kwa sababu Precision imetufanyia kazi nzuri naipongeza kwa kupata Hati Safi. Bila Precision sijui Bukoba tungekuwa wapi? Pongezi za dhati kwa niaba ya wananchi. Precision muendelee ili muipe changamoto Air Tanzania.

Mheshimiwa Spika, kuhusu uwanja wa Nyerere wa Kimataifa, jamani wakaribisheni PPF na NSSF wajenge pale. Haya mambo ya kuzungumza mabilioni ya fidia watu wa Kipawa hatutazipata na kilio hiki cha barabara? Gaweni viwanja hivyo kwa PPF, NSSF, wale watu wa Kipawa sitaki wahamishwe, watengewe maeneo fulani tu tuwajengee maghorofa wakae pale pale.

Mheshimiwa Spika, hivi kwa nini umtoe mtu Kipawa umpeleke Pwani? Wale ni wachache sana unaweza ukawaweka kwenye ghorofa mbili tu zinatosha, wote flat vyumba viwili vya kulala, sebule na jiko mpaka ghorofa ya 15 wanakaa sehemu moja eneo linakuwa wazi kwa ajili ya kupanua uwanja kuliko kujenga uwanja mwingine. Mimi siungi mkono kuuhamisha ule uwanja. Kujenga VIP na yenyewe tutafute mwekezaji? Terminal, PPF na NSSF wanashindwa? Baada ya ma-treasury bond Mheshimiwa Waziri wa Fedha kuyasimamisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba mlete simu za mkono Muleba na Kimwani huko hatusikii vizuri sehemu nyingine mpaka tupande kwenye miti lakini of course minara ipo lakini haitoshi.

Mheshimiwa Spika, pongezi kwa Waziri wa Fedha kwa kuanza kusimamia hawa watu wa mafuta. Nakupongeza sana. Katika kuchangia Bajeti yako nilisema wasiwamiwe na umeanza.

Lakini ninachoshauri ni kwamba mlifanye zoezi hili kwa uangalifu sana wabane wasafirishaji, wabane wanaotoa mafuta nje huko Uarabuni na wanaoyauza ndani ya nchi. Lakini pia Serikali muanzishe strategic reserve ya mafuta, hawa wakisitisha tuta paralise, tujenge uwezo wa kuwa na mafuta wakituletea hujuma tunamwaga mafuta kwenye soko. Halafu hawa akina Haruna, Masebu na Israel Sekirasa ni watendaji wazuri

33 sana wapewe nguvu ili waweze kufanya zoezi la usimamizi litakalo tusaidia kupitia EWURA na SUMATRA.

Mheshimiwa Spika, mwisho ni reli. Reli yetu wanasema haina faida, kipande tu kinazalisha bilioni 46 mwaka ulioisha na 2005/2006 bilioni 62.4. Hii reli kwa kweli hatujashauriwa vizuri. Wataalamu wa mambo ya uchumi wanasema bandari na reli ni mabilioni ya dola, sasa sisi tunaanza kuleta watu kutoka nje halafu kumbe hawana hela tunawakopea kutoka IFC! Mimi imenistua sana hii, IFC hawatukopeshi sisi, Serikali haikopesheki mpaka aje mwekezaji kutoka nje? Kwa nini tusiligeuze sasa badala ya huyo kutoka nje tuunde NICO nyingi hapa yaani wakopeshe NICO wajenge reli hii. Mimi nashawishika kupingana na hilo.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja mia kwa mia kwani mmefanya kazi nzuri muendelee. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Wilson M. Masilingi kwa niaba ya sisi wabunge wote naendelea kutamka kwamba tunakutakia siku njema ya furaha ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwako, ahsante sana.

Namwita sasa Mheshimiwa Lucal L. Selelii, atafuatiwa na Mheshimiwa Khalifa S. Khalifa, wakati huohuo Mheshimiwa Vedastusi Manyinyi, ajiandae.

MHE. LUCAS L. SELELII: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa asubuhi nami niweze kuhutubia Bunge lakini nianze kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Nzega kutoa salamu za rambirambi kwa misiba ambayo Bunge hili imezipata, Mwenyezi Mungu azilaze roho za Marehemu mahali pema peponi, Ameni!

Mheshimiwa Spika, Wizara hii ya Miundombinu ni pana. Zamani Wizara hii ilikuwa imebeba Wizara mbili yaani Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi na Wizara ya Barabara. Lakini ninaamini Mheshimiwa Rais alitumia busara kwa sababu hapo zamani utakumbuka watu waliokuwa wakienda Pwani wajukuu zetu wa Pwani kuanzia Walugulu, Wazaramo na Wazanzibar akina Yakhe kazi nzito wakishindwa walikuwa wakiwasubiri Wanyamwezi na wakati ule yaani zamani zile mtu yeyote akitoka Bara alikuwa ni Mnyamwezi, sasa naamini Mheshimiwa Rais ametumia busara zake kumpa kazi nzito Mheshimiwa Andrew J. Chenge na Makongoro Mahanga kuhimili kazi hii ya Miundombinu. Kwa hiyo, nawapa hongera kwa kazi nzito ambayo mmeifanya lakini mtegemee kupata changamoto kwa sababu Wizara hii ni kubwa mno na sisi wote tuna vilio mbalimbali katika kuendeleza maeneo yetu na hasa masuala ya Barabara na Miundombinu ya simu na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, lakini la pili kwa dhati kabisa ya moyo wangu napenda niipongeze Kamati yako Tukufu ya Bunge ikiongozwa na Mheshimiwa Mohamed Hamisi Missanga, imetusaidia sana. Utakumbuka siku niliyokuwa nachangia kwenye bajeti nilichangia kwa uchungu kweli na nilisema inauma sana, ilikuwa inauma sana vile vitabu vya mwanzoni ambavyo vilikuwa vimeinyima miradi mbalimbali katika maeneo yetu hasa katika maeneo ya Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi.

34 Nawashukuru Kamati hii kwa kazi nzuri waliyoifanya hadi kuweka kitu cha kihistoria cha kufumua bajeti tukaongezewa shilingi bilioni 100, ahsanteni sana na nawaomba muisimamie Serikali kwa umakini uleule ili hizi kazi ambazo zimepangwa ziweze kufanyika kama ambavyo zimepangwa na bajeti inavyosema.

Mheshimiwa Spika, la tatu ni kwamba bajeti hii iko pande mbili kuna maeneo mawili kama alivyosema Mheshimiwa Waziri Mtoa hoja, kuna maeneo ambayo yanastahili kupewa pongezi na ninajua mimi nikitoa pongezi natoa pongezi za dhati. Kwa kweli nawapongeza na nisije nikasahau kwa kazi nzuri ambayo mmezifanya. Hongera sana. (Makofi)

Lakini kuna maeneo mengine ambayo ameomba hata yeye tuweze kumsaidia katika kuyarekebisha, namshukuru sana kwa moyo huo nadhani ni vizuri hata Mawaziri wengine wakafuata moyo wa namna hiyo kwa sababu ni moyo wa Wana CCM. Wana CCM tuna msemo unaosema “Kukosoa na Kukosolewa ni Kujiimarisha” kwa hiyo mimi napongeza kazi ambazo zimefanyika vizuri lakini kuna maeneo ambayo nitapenda kusema ili tuweze kufanya vizuri zaidi na ndiyo azma ya Chama chetu cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, narudi kwenye hoja. Kupanga ni kuchagua na hapa tulipofika sasa inabidi sisi wote tuweze kuamua maamuzi mazito, na katika kupanga ni kuchagua tumekuwa tukitoa ushauri huu mbalimbali tangu wakati ule wa awamu ya tatu na wale ambao mnakumbuka katika awamu ya tatu tulisema ifike mahali ambapo Barabara zetu zijengwe kwa kuangalia uchumi wa kijiografia. Sina ubaya na wenzetu ambao wameshajengewa Barabara, sawa, lakini sasa tufike mahali ambapo tunajenga Barabara kwa kufuata uchumi wa kijiografia.

Mheshimiwa Spika, kwa hali hiyo, hakuna ambaye atabisha au kukataa kwamba kwa barabara ambayo itaweza kutusaidia kujenga uchumi wa kijiografia ni Barabara ambazo hata Mheshimiwa Waziri amezitaja katika ukurasa wa 23 kwamba ni Korido ya Kati, hizo ndizo Barabara ambazo zitatukukomboa kuleta uchumi wa kijiografia. Barabara ya kutoka hapa Dodoma ukaenda Manyoni, ukifika Manyoni uende Itigi, Itigi, Tabora mpaka Kigoma hiyo Barabara namba moja. Ukifika Manyoni uende Singida, Nzega na kuelekea Mwanza hiyo ni Barabara namba moja. Ukifika Nzega, uende Tabora, Ipole mpaka Mbeya hiyo ni Barabara namba moja, na ndiyo Kanda ambayo ameitaja Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mimi nashauri yafuatayo:-

Kwanza, katika kitabu chake ameeleza Barabara ya kutoka Dodoma mpaka Manyoni itakamilika 2008, nakumbushia tu kwamba hizi Barabara zimeanza kujengwa mwaka 2003 na mimi nazingatia maoni ya Kamati yaliyosema kwamba hebu tufike mahali Serikali itimize wajibu wake kwa sababu ninazo habari kwamba ilifikia mahali Wakandarasi wakaondoka kwenye site kwa sababu walikuwa hawalipwi. Sasa ifike

35 mahali Serikali ifanye kazi yake kwa kuona kwamba Barabara hii ifike kweli 2008 imekamilika kwa kiwango cha lami.

Barabara nyingine ambayo ameitaja kwenye hotuba yake ni Barabara ya Manyoni, Singida ambayo kwa sasa ina 50%, kipande cha Manyoni mpaka Isuna chenyewe bado hakijapata Mkandarasi na hapa napenda kutoa maoni kwamba Waziri pamoja na Wizara nzima waone namna gani wanafanya ili eneo hili la kilomita 60 liweze kupitika bila matatizo. Sikuona chochote alichokisema Mheshimiwa Waziri katika Barabara ya Singida kwenda Shelui. Singida kwenda Shelui ndiyo kiini cha Barabara hii yenye utata.

Mheshimiwa Spika, wako wenzetu wa Bukoba inabidi wasafiri kwenda mpaka Kampala, Kisumu, Nairobi na warudi Namanga ndiyo waje Dar es Salaam. Sasa hivi tunakaribia kufikisha miaka 50 ya Uhuru, ni aibu, aibu kubwa sana. Ninapenda kutoa rai mahali ambapo ni pabaya kuliko pote katika Barabara hii ya kuanzia Dodoma, Manyoni, Singida, Nzega na Mwanza ni Sekenke. Pale toka mwaka 2004/2005/2006 mpaka leo hapakamiliki hivi tatizo la pale Sekenke ni kitu gani? Inafikia mahali ambapo unaweza ukaamini pengine hawa watu hawafanyi kazi ya kujenga daraja peke yake wana mambo mengine, pale pana Madini watu wanasema wale hawajengi madaraja, hawajengi Barabara bali wanachimba Madini. Pia pale watu wanakufa, nenda hata sasa hivi hata leo jioni utakuta kuna kuna foleni ya magari ya kwenda Magharibi pale yamekwama kwa sababu ni pabaya na ni pafupi mno, pafupi sana haizidi kilomita nne.

MJUMBE FULANI: Ndiyo!

MHE. LUCAS L. SELELII: Mheshimiwa Spika, ifike mahali Wizara iamue kwa makusudi kwamba juhudi zote tufungue Sekenke, ukifungua Sekenke umekomboa Barabara hii ya Magharibi. Hiyo ni sehemu ya kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sehemu ya pili, nakuja kwenye Barabara ya Itigi, Tabora kuelekea Kigoma. Katika vitabu vya Mheshimiwa Waziri anaieleza Barabara kuanzia Kigoma mpaka Malagarasi kwenda Ilunde. Pia katika vitabu vyake anaelezea kwamba imewekewa fedha kiasi cha shilingi bilioni 4 kwa dhana ya uchumi wa kijiografia ndiyo maana tunaomba Barabara hii sasa itamkwe ni Barabara ya Kitaifa siyo Barabara ya Kimkoa kwa sababu bado imewekwa katika hadhi ya Kimkoa ndiyo maana imetengewa shilingi milioni 150, milioni 150 utafanya kazi gani kwa Barabara muhimu kama hii ya uchumi wa kijiografia?

Mheshimiwa Spika, wenzetu wa Rwanda jana tulikatazwa kutaja baadhi ya nchi lakini lazima tutaje. Wenzetu wa Rwanda wanatumia akili ya kutuwahi….

(Hapa kengele ililia kuashiria muda wa mzungumzaji kumalizika)

MHE. LUCAS L. SELELII: Khee! Kengele ya pili hii?

MBUNGE FULANI: Kengele ya kwanza!

36 MHE. LUCAS L. SELELII: Wenzetu rwanda wanatumia akili ya kutuwahi ndiyo maana wamewahi wanataka kufanya biashara na Kongo, wamewahi kuwahi kupata ile Reli ya Isaka kwenda Kigali, taarifa nilizo nazo ni kwamba tayari wameshatengeneza daraja kuanzia mto mmojawapo kule Rwanda ili wafanye biashara na Kongo sisi tunazubaa badala ya kuimarisha Reli kutoka Dar es Salaam kuja mpaka Dodoma kwenda Tabora, Kigoma, Kigoma ili pale Uvinza uweze kuvunjika ukaenda mpaka Rwanda (Kigali) na ukafanya biashara na Rwanda lakini tunazubaa na ndiyo maana Mzee Mwinyi alituambia sisi ni kichwa cha mwendawazimu.

Mheshimiwa Spika, hapa ni lazima tuchangamkie biashara, kwa dunia ya leo bila pesa utakuwa unanyanyasika na utakuwa unababaika hebu tuimarishe reli ya kutoka Tabora, Kigoma kwa maana ya kuvuna vilevile Rwanda pamoja Burundi wasije wakatufuata huku Isaka kwa faida ya wao kufanya biashara na DRC Congo.

Lakini vilevile Barabara hii ya Itigi – Tabora ni muhimu sana kwa biashara ya DRC Congo, Congo ina wananchi milioni 14 hiyo hiyo Kongo Mashariki peke yake wale wakiteremka kuja Mashariki huku ni tayari biashara. Kongo ina tani milioni 4 za kubeba kusafirisha kwa sababu hawana Bandari, wakisafirisha hata tani milioni 2 tu tayari ni biashara peke yake ya kutosha.

Kwa hali hiyo, tukubaliane hapa kuamua maamuzi ya uhakika ambayo yatatusaidia kuchochea uchumi huu ndiyo mtekenyo wa kiuchumi kwa Barabara hii. (Makofi)

Ukikataa ukikubali lazima ufanye maamuzi ya kuamua katika kuamua kuimarisha barabara hii na mimi naomba Kigoma baadaye ibadilike iwe Hub ya kusaidia kuibua uchumi wa Kongo, Burundi na kuibua uchumi wa Rwanda. Pia kuna Bandari kule chini ya Kasanga katika Mkoa wa Rukwa ninasema uchumi wa kijiografia kwani pale Bandari ya Kasanga itasaidia vilevile Kongo ya Kusini pamoja na Zambia. Sasa tunayasema haya ili wenzetu hasa Wataalamu waweze kuyatafsiri katika kutenda.

Mheshimiwa Spika, hapa ninakuomba Bunge lako lifikie mahali pa kusema sasa tunaamua Barabara ya Itigi mpaka Tabora iwe ni Barabara ya Kitaifa kwa sababu huku Kigoma ameitaja, kutoka Kigoma mpaka Ilunde ameitaja lakini inakuwa je kutoka Itigi mpaka Tabora hajaitaja? Mheshimiwa Spika, mwaka jana utakubmbuka kwamba tuligombana sana juu ya Barabara hii, Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa heshima zote akasimama akaahidi ndani ya miaka hii 2005 – 2010 itajengwa kwa lami. Kujenga lami ndugu zangu huwezi kuanza mwaka 2010 ukamaliza, sasa hakuna juhudi zozote zinazoonekana katika kujenga Barabara ya Itigi kwenda Tabora? Ndiyo maana siku hiyo nilisema inauma sana. Lakini nitafurahi sana Mheshimiwa Waziri aliyepewa mzigo huu mzito kuubeba akanijibu jioni leo kwenye vifungu kwamba ni hatua gani za makusudi zinachukuliwa kuimarisha Barabara ya Itigi kwenda Tabora kwa kuzingatia ahadi ya Rais, Waziri Mkuu, Serikali na ahadi ya CCM kwamba Barabara inajengwa kwa kiwango cha lami.

37 Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa haya ambayo nimeyasema juu ya Barabara.

Mheshimiwa Spika, la mwisho nimalizie, Air Tanzania. Shirika letu la Ndege la Tanzania. Naomba Shirika la Ndege la Tanzania liachiwe lifanye kazi ya kibiashara, tusiilingilie kwenye mambo yetu ya kisiasa. Bodi imeteuliwa ipewe uhuru kwa 100% ifanye kazi ya kibiashara kama ambavyo wenzetu wanafanya katika nchi nyingine. Lakini la pili, vilevile naomba Shirika la Ndege likodi ndege katika mpango wa kukodi na kununua, ikodi kwa kufanya biashara hata hizi biashara za ndani viwanja vya ndege vya Tabora, Kigoma, Shinyanga, Ruvuma kwa maana ya Songea iweze kufika na ndiyo itatoa (sura) image kwamba hili ni Shirika la Ndege la Watanzania wenyewe.

Kwa sababu tunataka kuimarisha utalii liweze kufika kubeba watalii, tukiacha kuwafuata watalii wakafuatwa na Mashirika ya Ndege ya Kenya, South Africa tayari pale watakuwa wametushinda kibiashara. Liende katika maeneo ambayo watalii wanatoka ili liweze kufanya biashara na kuitangaza nchi yetu. Ndugu zetu kwa hali ya sasa hivi lazima ujitangaze kwani bila kujitangaza na kuchacharika huwezi kupata kitu. Kwa hiyo, naomba ili Air Tanzania mpya hili Shirika la Tanzania jipya liweze kufanya kazi ya kibiashara na kutangaza nchi yetu hasa katika masuala ya kiutalii.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii na ninamwomba Mheshimiwa Waziri jioni aweze kulijibu Bunge lako hatua muhimu hasa ya Barabara na hatua muhimu za kuimarisha uchumi wa kijiografia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa na sasa ni zamu ya Mheshimiwa Khalifa Suleiman Khalif, atafuatiwa na Mheshimiwa Vedastus M. Manyinyi, kisha ajiandae Mheshimiwa Lekule.

MHE. KHALIFA SULEIMAN KHALIFA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na mimi kwa kunipa nafasi ya kuchangia katika hizi nafasi za mwisho mwisho mimi naziita za upendeleo maana yake nilikwisha kata tamaa ya kuwa nitapata nafasi.

Mheshimiwa Spika, na mimi nianze haraka haraka kuungana na wenzangu wote waliosema humu kutoa pole za dhati kabisa kwa vifo vilivyowapata Watanzania wenzetu, ajali zimetokea nyingi na bahati mbaya zinaendelea kutokea na msingi wake ni haya matatizo ambayo wanayazungumza wenzetu yaani ni Barabara na mambo mengine mengi.

Lakini pole kubwa zaidi naitoa kwa familia ya Mheshimiwa Marehemu Amina Chifupa Mpakanjia,kwa sababu yeye siyo tu alikuwa Mbunge mwenzetu hapa lakini alikuwa ni kijana ambaye anainukia vizuri, anatoa michango ya maana humu Bungeni na mimi nasikitika kwa sababu Mheshimiwa Spika ni wewe Mwenyewe ulitutuma pamoja na Mheshimiwa Amina Chifupa Mpakanjia na Wabunge wenzetu kwenda kujifunza masuala ya kibunge katika nchi ya Uingereza. Kijana yule alifanya kazi nzuri kabisa na

38 wewe ni shahidi alikuwa akiwasiliana na wewe katika kila hatua ya ziara yetu. Sisi tumesikitika sana lakini kwa sababu sisi ni wa Mwenyezi Mungu na sote tutarejea kwake lazima tukubali hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wabunge wote wanaosema hapa wanazungumzia kitu cha namna moja yaani wanazungumzia matatizo ya wananchi kuhusu masuala ya Barabara, Bandari na hata Meli ni kwa sababu hayo ndiyo masuala ya msingi.

Mimi napenda kuzungumzia Barabara lakini niizungumzie Barabara, tunapata fursa bahati nzuri ya kutembea humu nchini wananchi wengine wanalalamika na wanalalamika ukiona malalamiko yao unaiona sababu ya msingi, leo ni karibu miaka 50 ya Uhuru mtu aliyeko Rukwa, Mpanda hajaona hata kilomita 10 za Barabara ya lami hivi asilalamike afanye nini?

Mheshimiwa Spika, atalalamika tu, tena wana lugha ya ajabu sana wanakwambia sisi tuko Tanganyika bwana, ana maana ya kuwa wametengwa na Watanzania wengine kwa sababu ya ile Barabara tu, simu ipo ati kama anataka kumpigia mtu wa Dar es Salaam atampia lakini akitaka kuondoka kuja Dar es Salaam afunge safari ya siku tatu, inasikitisha sana. (Makofi)

Sasa mimi nafikiri Serikali yetu ingekuwa na vipaumbele na ninaomba sana mimi kipaumbele kikubwa katika nchi hii kwa sasa kiwe ni Barabara, Barabara tu, kwa sababu kama hujajenga Barabara ni tatizo kubwa huwezi kuiunganisha nchi lazima tukubali na wote unaowasikia hapa wanasema katika Bunge lako wanalalamikia hilo na huo ndiyo ukweli. Unajua Waingereza wanasema if you want to please all you please money, sisi tunafanya vitu vingi kwa wakati mmoja ndiyo tatizo letu na ndiyo maana umeona hizo nchi jirani ambazo watu wanasifu hapa wameamua miaka miwili au mitatu wanakabiliana na Barabara acha watu walalamike, ndiyo wanavyofanya. Sasa mimi nafikiri tufikie mahali hapo.

Watu waliopo Rukwa na Mpanda wana mazao mengi na akiba ya chakula lakini watakiuza wapi? Watakifikisha lini kwenye mazao?

Jalia mkungu wa ndizi unaoukata Rukwa, kata mikungu 10,000 hivi kweli itafika pale Tunduma haijaiva? Itaiva tu mtu ataona aaah! ni upuuzi ataachana nayo, lakini wenye mahindi mahindi hayo yanashindwa kununuliwa wako nayo kule na nimeuliza swali katika Wizara ya Kilimo wala sikuwa na nia mbaya lakini ni kwa maana kwamba watu wana vyakula lakini wanashindwa kuviuza kwa Barabara mbaya tu.

Sasa tuwajengee Barabara naomba sana Barabara hii ya Tunduma – Mpanda itazamwe ni mbaya mno tena mno na tukitaka kuwakomboa watu wa kule tuwajengee ile Barabara na kwa hili wala hawana itikadi wao, aaaah! mtu yeyote ukienda wanakwambia tusaidie kwa hili.

Tulikwenda sehemu moja kufanya mikutano watu wakatuambia aaah! sisi tulifikiri unakuja kutueleza habari ya Barabara kumbe unatujia na habari nyingine, Nkasi

39 pale walituuliza habari hizo wananchi. Sasa inaonekana hili ndiyo tatizo lao. Naondoka kwenye Barabara.

Mheshimiwa Spika, nakuja kwenye ATC. Shirika la Ndege la ATC liliuzwa au lilibinafsishwa na Serikali kama kumbukumbu zangu ni sahihi iliuza 51% lakini kwenda na kurudi imelirudisha. Sasa hii transaction hasa tulipoouza na tuliporudisha tumepoteza nini na tumepata nini? Ni vizuri Mheshimiwa Waziri akaeleza kwa sababu vitu hivi leo unauza kesho unachukua, leo unauza na kesho unabinafsisha ni matatizo makubwa haya ni vizuri basi tukawaeleza wananchi wamefaidika vipi katika hili.

Lakini sasa niseme Shirika la ATC tumelichikua tena hebu tulifanye Shirika la Ndege kama tunataka kukuza uchumi wa nchi hii basi suala la kukuza Shirika la Ndege ni muhimu. Hayo masuala mnayosikia wananchi wanalalamikia kwa mfano ndege ya Rais labda anunue ndege kwa sababu hakuna shirika la ndege lenye ndege. Wageni wote tunaowaona wanakuja katika nchi yetu wanakuja na ndege kubwa za Mashirika yao wenyewe hata wale maskini sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi nimeona pale kwetu Zanzibar ndege za Eritrea mbili 767 ndege kubwa wameleta pale wanakodisha kuchukua watalii, jamani Eritrea? Aaah! Hapana bwana. Ni lazima tuone aibu kwenye baadhi ya vitu vingine, tuone aibu kwa kweli.

Shirika hili mimi naomba Serikali ilipe injection ya kweli kweli ya pesa ilitafutie wabia wenyewe tu hawataweza, jana tuliambiwa tusiwataje majirani lakini mimi nafikiri tusiwataje tunapowazunguzia vibaya na msingi wake ni kuwa jana alisema mtu mmoja hapa akataja watu fulani akasema watu wa nchi fulani ni wezi, akaambiwa huwezi kusema Bungeni humu kwamba nchi fulani ni wezi hiyo ni lugha mbaya mno. Lakini tukiwataja kwa wema tunaweza kuwataja.

Mheshimiwa Spika, Kenya msingi wa uchumi wao kukua ni kwa sababu ya Shirika la Ndege lile, ukienda pale Nairobi hivi sasa kila wakati kuna ndege zisizopungua 10 tena wide bodies zinaweza zikaenda popote duniani wana ndege inayokwenda London kila siku kupitia Amsterdam, ndege inayokwenda Marekeni kila siku. Sasa Mkenya gani aliye mzalendo atasafiri na ndege ya shirika lingine? Mambo haya kama tunataka kweli kukuza utalii wetu na uchumi wetu ni lazima tujenge hili Shirika la Ndege. (Makofi)

Nchi zote ambazo zina Shirika kubwa la ndege utalii wao ni mzuri, tutazame Egypt, Egypt wanapata watalii milioni 10 kwa mwaka mmoja yaani ten million lakini ndilo shirika ambalo lina ndege nyingi kabisa katika Bara zima la Afrika. Hata hawa Kenya wanapata watalii wengi kwa sababu wanawafuata mtalii alipo nao wanapunguza bei na kila kitu. Lengo ni kukuza uchumi. Nawaomba sana Serikali ithubutu kwa hilo.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais ambaye ndiye Kiongozi wetu Mkuu mimi najua ana uwezo mkubwa wa kuthubutu. Rais mwaka jana alikuwa anakwenda kwenye Mkutano Addis Ababa siku ya nyuma yake alikuwa Davos lakini kwa sababu kulikuwa

40 na mazungumzo muhimu yanayohusu msaada wa nchi hii wa dola zisizopungua milioni 800, alirudi nchini hapa akafika jioni. Mheshimiwa Rais huyu akafanya mazungumzo na wahusika kwa faida ya nchi hii asubuhi akaja Addis Ababa. Kwa hiyo, anaweza kuthubutu. Sasa wale wanaomsaidia kaka zangu hawa wanaomsaidia wamshauri na mimi naamini ana nia nzuri ili tuweze kuona vipaumbele vya kukuza uchumi. (Makofi)

Si kweli kuwa tukifanya kila kitu tutafika, hatuwezi kufanya vitu vyote kwa pamoja watu wengi wamesifu hapa kuhusu masuala ya Sekondari kwa sababu watu wameamua sasa na sasa wakiamua tena tutaweza kukuza elimu, tukiamua tutaweza kujenga barabara na pia tukiamua tutaweza kukuza Shirika la Ndege, naondoka hapa.

Mheshimiwa Spika, nije katika suala la Bandari. Wapo wataalam wanasema ni aibu kuwa una bandari halafu ukawa maskini. Tanzania ina bandari tano kubwa yaani kuna Bandari ya Zanzibar, Tanga, Dar es Salaam, Kigoma na Bandari ya Mtwara mbali ya hizo nyingine za Kasanga na kadhalika. Hivi tumezitumiaje Bandari hizi katika kukuza uchumi wa nchi hii? Tunazitumiaje hizi bandari? Kwa sababu issue si kuwa na bandari tu lakini unaitumia vipi?

Ukienda bandari za nchi za wenzetu kwa mfano Malindi Kenya, ile bandari wala siyo kubwa kuliko Bandari zetu lakini tuangalie ni namna gani wanavyopata revenue bandarini, sasa mambo yote haya yanahitaji uangalifu kwa ajili ya kukuza uchumi wa nchi hii. Niseme tu katika suala hili la bandari na bahari kwa ujumla ninaomba sana Wizara hii iweze kuangalia vyombo vya baharini. Sisi watu tunaotoka visiwani tumeshakufa sana kwa sababu mbili. Kwanza hivi vyombo vinavyopata ruhusa watu mimi naamini kwa sababu na mimi mara nyingi napanda katika hivyo vyombo havina vifaa vinavyostahili kuchukua watu, huwezi kuiacha boti inapakia watu unaiona bandarini hata radio call haina boti hiyo, ni kuhatarisha maisha ya watu. Naomba Serikali iliangalie jambo hili ili wananchi wawe salama vinginevyo watu wetu wataendelea kufa kwa sababu hatuvisimamii hivi vyombo. (Makofi)

Nizungumzie simu, tunashukuru karibu kona zote za Tanzania leo kuna simu za mikononi lakini mtaani watu wanakwambia aaah! Eeh Bwana we umenunua simu au umeongeza mke? Kwa habari ya gharama inakuwa kubwa mno. Eeeh! ndiyo, kama ingelikuwa watu wanavyonunua kadi za simu pesa zile wanawalisha kwa wanawake majumbani wangenenepa mno lakini ndiyo ukweli huo kwa sababu bei ya simu hapa kwetu ni ghali kidogo. Ni vizuri Wizara ikawashauri hawa kwa sababu Mheshimiwa Waziri amesema katika kitabu chake hapa juu ya matumizi ya hii Fibre Optic System. Inaonekana tu kuna mashirika fulani yanatumia shirika kama la Reli, Posta na Simu na hata TANESCO wanatumia. Hivi kwa nini hatu–centralize haya matumizi ikawa kuna system moja tu ya Fibre Optic katika nchi ili haya makampuni ya simu na wao wakafaidika na hiyo bei ingeweza kupungua kidogo. Lakini sasa hivi kila siku mh! hapana jamani watuhurumie. Tunawashukuru sana kwa kutuletea lakini bei inakuwa kubwa. (Kicheko/Makofi)

41 Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa mkoloni. Sote tuliomo humu ndani na Watanzania waliopo nje wanakubali kuwa ametufanyia mambo mengi mabaya. Lakini tukitaka kuwa wakweli tukubali kuwa ametuachia Reli kutoka Kigoma mpaka Dar es Salaam, tukitaka kukubali. Ile reli hivi tumeshindwa nini kuitunza? Hivi hatuoni tunawaumiza wananchi wanaoondoka Dar es Salaam kuja kupandia Reli hapa Dodoma? Kulikoni? Kumetokea nini ambacho Serikali yetu hii haiwezi kuwatengenezea reli hii ya kutoka hapa Dodom kwenda Dar es salaam. (Makofi)

Nina jamaa zangu hawa aliowasema Mheshimiwa Lucas Lumambo Selelii, Wasukuma ni wepesi sana kwa kuwaibia. Kwa vile jamaa wanawatega katika mambo haya Dar es Salaam hama wanawaibia. Kule kwetu Pemba huja wakalima wakapata pesa wakija hapa wanakupigia simu kwamba Baba nimeibiwa! wataibiwa kweli, kwa sababu hivi sasa kule Dar es Salaam sasa wanalala stendi.

Akija hapa ameshaachwa na treni analala, analala...... ! Hapana bwana, tengenezeni, vinginevyo watakuwa wakiibiwa kila siku jamaa hawa na sisi tunataka pesa wanazozipata wakaimarishe familia kule nyumbani. Tunasema mambo haya kwa nia nzuri.

Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii mwisho, na kwa umuhimu wake naiweka mwisho, nawashukuru sana sana viongozi hawa wa Kambi ya Upinzani wanavyotuunganisha vizuri kwa hotuba zao nzuri. Nina hakika ndani ya maneno yao pamoja na kuwa inategemea mtu aliyapokea vipi, lakini kuna maneno mengi ya maana, kuna ushauri mwingi wa maana ambao tukiutumia kwa nia ya kujenga nchi yetu, tutapiga hatua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nakushukuru sana kwa kunipa fursa hii. Sijui niseme naunga mkono au siungi mkono, lakini asilimia ngapi itategemea na tafsiri ya walionisikia nikisema. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Khalifa, kama kawaida yako mchango wenye ufasaha na wa Uzalendo, nakushuru sana. Sasa namwita Mheshimiwa Vedastus Manyinyi, Mbunge wa Musoma Mjini, akifuatiwa na Mheshimiwa Michael Laizer na Mheshimiwa Anne Kilango Malecela ajiandae.

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii ili nami niweze kuchangia katika hii Wizara ya Miundombinu. Awali ya yote, nami naungana na Waheshimiwa Wabunge wenzangu na Watanzania kwa ujumla kupeleka salamu za rambirambi kwa familia ya dada yetu na mpendwa wetu, Amina Chifupa. Kwa kweli hili ni pigo kubwa ambalo familia imelipata lakini na sisi Wabunge ambao tulishirikiana naye kwa karibu sana katika kujenga hoja za kujenga nchi yetu ya Tanzania.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwapongeza Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu, Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu pamoja na watendaji wote wa Wizara,

42 kwa kazi nzuri ambayo wanaonekana wameifanya hasa ukiangalia hotuba yao kwa namna walivyoweza kuipanga imejieleza vizuri, imetoa ufafanuzi mzuri, hata ukifungua kule nyuma kuna majedwali yameonyesha mkoa kwa mkoa, barabara kwa barabara kwa kadri fedha zilivyoweza kupatikana. Kwa hiyo, nawapongeza sana na naomba kusema moja kwa moja kwamba nami naunga mkono hoja hii. (Makofi) Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naomba sasa nianze kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika kukuza uchumi wa nchi na katika kukuza uchumi hasa wa Mkoa wa Mara, kwa kweli suala la miundombinu ni suala ambalo linahitaji tulipe kipaumbele cha hali ya juu. Mkoa wa Mara katika mazingira au mahali ulipokaa umekaa kaskazini magharibi mwa nchi yetu ya Tanzania na ukiangalia ili uweze kwenda Mkoa wa Mara njia pekee ambayo inapitika kwa sasa lazima uende Mwanza halafu utokee Mwanza kwenda Mara lakini labda kutoka kwenda Kenya ndiyo rahisi zaidi.

Mkoa wa Mara unategemea sana Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Dar es Salaam maana huko ndiko tunakopata sukari, ngano na mahitaji mbalimbali na kwa kweli si mbali kutoka Mara kwenda Arusha ni kama kilomita mia tano, lakini sasa kutokana na mazingira yaliyopo kwa kweli tunapata tabu sana watu wa Mkoa wa Mara. Leo tunazungumza suala la mfumuko wa bei ambalo sisi watu wa Mkoa wa Mara sasa kila bidhaa bei zake zipo juu na hii si kwa sababu nyingine bali ni kwa sababu tunazungukwa na mbuga ya Serengeti

Mheshimiwa Spika, naomba kusema kama ifuatavyo: Ni kweli kwamba mbuga ya Serengeti ni faida kwa nchi yetu ya Tanzania, lakini nasikitika kusema kwamba sisi kama wananchi wa Mara badala ya kufurahia kwamba imekuwa vizuri kuwa na mbuga ya Serengeti lakini sasa tunasikitika kuwa na hiyo. Kwa nini nasema hivyo? Kama nilivyosema umbali wa kutoka Musoma kwenda Arusha si zaidi ya kilomita 500. Umbali wa kutoka Arusha kwenda Dar es Salaam ni zaidi ya kilomita mia sita. Lakini leo cha ajabu, ili utoke Musoma kwenda Arusha ni lazima uzunguke Nairobi, ndiyo uje Arusha ambako ni zaidi ya kilomita 1,200.

Kwanza kiusalama ni hatari, mwanao akizunguka kule unakuwa hulali mpaka usikie amefika. Lakini vilevile, pamoja na huo umbali mfupi wa kutoka Musoma kuja Arusha, ukiangalia leo bei ya mfuko wa sementi unagharimu si chini ya sh. 6,000/=, mfuko wa sukari unagharimu si chini ya sh. 6,000/=. Lakini huo huo umbali ambao ni wa kutoka Arusha kwenda Dar es Salaam ambako ni mbali zaidi kuliko Arusha – Musoma, mfuko huo wa sementi unagharimu si zaidi ya sh. 2,000. Sasa hebu jaribu kuangalia tofauti hapo pamoja na umbali wa Arusha-Dar es Salaam lakini bado mfuko wa sementi unasafirishwa kwa sh. 2,000/= lakini mfuko huo huo unasafirishwa kwa Sh. 6,000/=, matokeo yake kuna zaidi ya Sh. 4,000/=. Mheshimiwa Spika, hali hii ni kwa sababu tunaendelea kuzuiwa siku hadi siku kukatiza kwenye hii mbuga ya Serengeti. Hivi leo unaanzia wapi kumshawishi au kumwambia mtu wa Mara kwamba anafaidika na hii mbuga ya Serengeti. Kibaya zaidi, maana hili hata mwaka jana nimelizungumzia, kila kunavyokucha ndivyo vikwazo vinazidi kuwekwa katika hii mbuga ya Serengeti kwa maana ya Mkoa wa Mara.

43 Kwanza, Mkoa mzima wa Mara unategemea magari kumi peke yake yaweze kuhudumia ambayo ndiyo yaliyopewa kibali. Kwa hiyo, gari likipata break down basi Mkoa wa Mara tumelala na njaa. Lakini mbali na hilo kutokana na hali hiyo juzi tu tena cha kushangaza kabisa hata kwenye hayo magari kumi ambayo yanaruhusiwa kupita gharama za kupita Ngorongoro au hiyo Serengeti zimeongezwa.

Mheshimiwa Spika, leo gari la tani kumi linapita kwa sh. 400,000.00 Maana yake sasa ile tofauti ya sh. 4,000/= iliyokuwepo ukiangalia sh. 400,000.00 kwa mifuko mia mbili unazungumzia sh. 2,000/= imepanda juu. Sasa kwa tafsiri yake tofauti ya Arusha na Dar es Salaam inapanda kwenda mpaka sh. 6,000/= kwa mfuko.

Si hivyo tu, unapongumzia nauli ya basi kutoka Arusha kwenda Dar es Salaam unazungumzia sh. 14,000/= lakini Musoma-Arusha unazungumzia si chini ya sh.30,000/=. Kutokana na hali hiyo, ndiyo maana tunasema ni vizuri tukaangalia namna ya kuokoa tatizo la Mkoa wa Mara maana kinyume na hapo ni kwamba tunaendelea kuwa katika kisiwa na hata ugumu wa maisha unaendelea kutugawa siku hadi siku.

Mheshimiwa Spika, mimi nashangaa, kuna mikoa mingi na barabara nyingi zinazopita katika mbuga ambazo ni pamoja na barabara za Mikumi. Magari yanayopita kule hayalipi chochote. Hivi sisi wa Mkoa wa Mara tuna tatizo gani? Kwa hiyo, ndiyo maana tunadhani Serikali inahitaji iliangalie hili kwa macho ya huruma.

Maana wenzangu wengi wamekuwa wakichangia hapa kwamba kweli kuna tatizo la miundombinu katika nchi hii. Mimi nimekuwa nikilifananisha na nini; nimekuwa nikilifananisha na mtu ambaye ana miguu mitupu na angependa kununuliwa viatu. Sasa Mara hatuna viatu wala miguu. Sisi tunachoomba turuhusiwe angalau kupita katika barabara hiyo ambayo ni ya vumbi kwa sababu kwa kupita katika barabara hiyo itasababisha gharama ziwe chini na mwananchi wa kawaida aweze kuishi kuliko hali ilivyo sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimemsikia Mheshimiwa Waziri katika hotuba yake vizuri sana, amezungumzia suala la reli ya Tanga-Musoma. Reli ya Tanga-Musoma imezungumzwa toka mwaka 1995 na ilizungumzwa na mpaka ikaandikwa kwenye Ilani na hatimaye hata leo nilikuwa nafungua Ilani, kumbe imeshafutwa. Kama iliweza kuandikwa kwenye Ilani lakini bado haikuweza kujengwa maana yake ni kwamba hata leo bado haitajengwa. Sasa nini kifanyike?

Kwanza, naomba kuchukua nafasi hii kumshukuru Rais, juzi alikuwa Serengeti alisema barabara ya Mto wa Mbu-Mugumu-Musoma itajengwa, namshukuru kwa hilo. Lakini vilevile kwa bahati mbaya sana ile ni barabara inayopigwa vita kwa muda mrefu, lakini kitu kikubwa ambacho nimegundua ni kwamba kumbe utafiti kamili ulikuwa haujafanyika. Barabara ile imekuwa ikipigwa vita kwa maana kwamba ni barabara ambayo itaharibu mazingira ya wanyama.

44 Mheshimiwa Spika, baada ya kuwa utafiti wa kina umefanyika si zaidi ya kilomita hamsini ambazo ndiyo tutaingia porini. Kutokana na hilo ombi langu kwa Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu ni kwamba, sisi watu wa Mara ambao tunaomba magongo kabla ya viatu tunajiuliza nini kifanyike sasa kwa kuwa suala la barabara ile leo hata ukiangalia kwenye bajeti zimetengwa sh. 500,000,000/= kwa ajili ya upembuzi yakinifu.

Off course hilo ni suala ambalo linaweza kuchukua miaka kumi au kumi na tano. Sasa naomba Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu na katika hili naomba kaka yangu anikubalie, mimi mwenyewe nipo tayari kuondoka, anipatie angalau Mheshimiwa Naibu Waziri hata na mwingine mwenyeji wetu wa kule, Mbunge wa Ngorongoro maana naye Loliondo inahusika twende pamoja na wahandisi, twende tukaangalie ile barabara.

Mheshimiwa Spika, naamini tukienda kule pamoja na mipango yenu ya upembuzi yakinifu kwa kuwa ile ni mbuga naamini kwamba angalau hata greda likipita huku na huku barabara ile itatengemaa, itakuwa tayari hata kwa kiwango kibovu kibovu lakini ilimradi magari yawe yanapita na watu wetu wa Mara wapate bidhaa kwa gharama nafuu. Hizi fedha ambazo Serengeti kwa maana ya TANAPA wanatulipiza sh. 400,000/= kwa gari, fedha hizo tutaendelea kuzitumia kuendeleza barabara wakati utaratibu wenu wa upembuzi yakinifu unaendelea mpaka tutakapopata barabara nzuri. Kwa hiyo tunadhani kwamba ukitukubalia hili, hilo ni zoezi ambalo litachukua ndani ya miezi mitatu mpaka sita barabara ile itapitika.

Kwa hiyo, tunadhani kwamba kwa kufanya hivyo utakuwa umetusaidia kuliko huu utaratibu ambao reli ya mwaka 1995 hadi leo ni zaidi ya miaka kumi na mbili hakuna cha reli na kutokana na hali hiyo tunadhani tutaendelea kupata adha kubwa. Ni matumaini yangu kwamba jioni Mheshimiwa Waziri atakapokuwa anahitimisha atanikubalia hilo ombi na kwa kweli mimi ningependa twende katika hiki kipindi cha Bunge ili tupate majibu kwamba suala hilo linawezekana na zoezi lianze mara moja.

Mheshimiwa Spika, mwisho, ningependa kugusa kwa haraka haraka suala la viwanja vya ndege pamoja na suala la usafiri wa anga kwa ujumla. Mimi nashukuru kwamba Serikali ina mipango madhubuti na mikakati kamili ya kuimarisha Shirika letu la ndege. Lakini ndugu zangu, pamoja na juhudi za SUMATRA kuzielekeza kuhakikisha kwamba usafiri haupandi, hivi hii SUMATRA haiwezi kujielekeza kwenye usafiri wa anga?

(Hapa kengele ililia)

SPIKA: Mheshimiwa ahsante sana.

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja hii. (Makofi)

MHE. LEKULE M. LAIZER: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili nami nichangie katika Wizara hii ya Miundombinu na natanguliza kusema kwamba naunga mkono hoja. (Makofi)

45 Mheshimiwa Spika, nami ningependa kutoa pole kwa wafiwa wote waliotangulia mbele ya haki. Napenda kusema kwamba Mungu aziweke roho zao mahali pema peponi. Amina!

Mheshimiwa Spika, napenda kuzungumzia barabara. Nianze na barabara ya Kamwanga-Sanya Juu-Boma Ng’ombe. Katika kipindi kilichopita niliongea kwa uchungu sana kuhusu barabara hii na kilichonikasirisha sana ni kusikia kwamba barabara ya lami inajengwa kuanzia Rombo mpaka Kamwanga. Nikajiuliza hapa Kamwanga kuna nini kwa sababu ingeanzishwa wakati huo barabara hiyo ingetajwa Rombo-Tarakea-Kamwanga-Sanya Juu-Boma Ng’ombe. Hiyo ndiyo ingekuwa barabara sahihi. Lakini mara ya kwanza Serikali ilikuwa inaishia Kamwanga na ningependa kuiambia Serikali kwamba sisi watu wa Longido tunalia kwa uchungu sana kwa sababu barabara hiyo ilipofika Kamwanga nyumba za wananchi walalahoi zimevunjwa, barabara imeishia hapo, Serikali haina hata mpango wa kutoa fidia, watu wanahangaika kweli.

Mheshimiwa Spika, nampongeza sana Naibu Waziri Dr. Mahanga amepita na kuangalia na nadhani kuna shahidi wangu mwingine hapa Mheshimiwa Waziri Mwandosya amezunguka mlima wa Kilimanjaro, ameona hiyo barabara. Nawaambia bila hiyo barabara ya lami kufika Sanya Juu kuungana na barabara ya lami inayofika Sanya Juu kutoka Boma la Ng’ombe haina maana.

Upembuzi yakinifu ungefanywa wakati ule siyo sasa, naona mmeweka fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu, kwa sasa lakini mmechelewa. Naomba huyo mkandarasi anayejenga sasa asiache, hiyo barabara iendelee ndiyo na sisi tutajiona watu wa Longido kwamba tupo Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, barabara ya pili ambayo ningependa kuzungumzia ni barabara ya Ketumbene-Longido au Longido-Ketumbene. Sasa Longido ni Wilaya, hiyo barabara inaunganishwa Wilaya ya Ngorongoro na Longido kwa sababu hiyo barabara inakwenda mpaka Natron isiishie Ketumbene.

Nampongeza sana Mheshimiwa Rais alipita barabara hiyo akaenda Ketumbene akatangaza siku hiyo hiyo kwamba hii barabara iwe barabara ya Mkoa na ni barabara inayounganisha Wilaya ya Longido na Ngorongoro. Kwa hiyo, isisemekane ni barabara ya Longido-Ketumbene, ni Longido-Ketumbene-Loliondo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ningependa kusema kwamba ukitoka Kamwanga kwenda Longido ambayo ndiyo Makao Makuu ya Wilaya yao wanazunguka mlima Kilimanjaro mpaka Sanya Juu. Mheshimiwa Mwanri ni shahidi, mpaka Hai waende Arusha wazunguke kwenda Longido ni kilomita mia mbili sabini. Lakini kuna barabara tulipendekeza kutoka Kamwanga mpaka Longido ambayo ni kilomita sabini na sita na tumeomba iwe ya Mkoa na ndugu yangu Chenge naomba utukubalie. (Makofi) Mheshimiwa Spika, barabara nyingine ambayo ningependa kuizungumzia ni barabara ya Arusha-Namanga. Mimi nimeingia Bungeni nimekuta bajeti ya mwaka

46 1996, barabara hii ipo. Kuanzia wakati huo ipo katika bajeti, ukiangalia bajeti zote mpaka leo hii hiyo barabara ipo kila wakati. Siamini hata sasa kwamba hiyo barabara itajengwa. Ni barabara inayozungumzwa kila siku kwenye bajeti lakini haijengwi na kila wakati inapangiwa fedha.

Naomba hizi fedha mlizoandika kipindi hiki zifanye kazi. Ukiangalia maintanance ya hiyo barabara kila mwaka shilingi 176,000,000 zinatengwa kwa ajili ya maintanance ya barabara ya Longido-Namanga, hizo fedha zingemaliza hata hiyo barabara mapema. Kwa hiyo naomba na hiyo barabara isirudi tena kama ilivyorudi miaka mingine.

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni kuhusu reli. Wakoloni walitujengea reli katika Ukanda wa Kaskazini kutoka Dar es Salaam mpaka Tanga-Kilimanjaro-Arusha. Wakati ule hatukuwa na mahitaji sana na wametengeneza kwa ajili yao wenyewe. Sasa tumekuja kuwa na mahitaji kwa sababu tumekuwa wengi na sisi tuna biashara kubwa lakini tumeiacha. Naomba hiyo reli ifufuliwe, tupate reli ya mizigo na ya abiria kwa sababu hata mabasi yaliyopo hayatoshelezi usafiri na kuna watu ambao hawawezi kulipa bei hii ya sasa. Tungekuwa na reli na treni tungefaidika sana.

Nimeona kwenye hotuba ukurasa wa 82 kuhusu usafiri wa reli, nchi za Afrika Mashariki zimeamua kuwa na mpango kabambe (railway master plan) kuendesha safari ya reli utakaounganisha nchi hizi. Mtaalamu mwekezaji wa kuandaa mpango huu amekwishapatikana. Nimeona hii reli ya Tanga-Kilimanjaro-Arusha-Musoma naona hata kelele za ndugu yangu Mheshimiwa Mathayo Manyinyi zitapungua kwa sababu hiyo reli ikifika mpaka Musoma itaunganisha na Jinja, huu usafiri utakuwa umeimarika. Naomba Serikali izingatie hiyo reli na sisi huko Kaskazini tuweze kupata huduma.

Mheshimiwa Spika, jambo jingine ni mawasiliano. Tuna Tarafa tunayoita ya Ketumbene, tarafa hii haina mawasiliano. Niliwahi kusema hapa Bungeni kwamba watu wa Tarafa ile wanaacha simu Longido kwa sababu hawatakuwa na kazi nayo wakienda huko. Na hiyo Tarafa inaungana na Tarafa ya Salieku huko Ngorongoro nao hawana mawasiliano. Wasomali, wale majangili wapo katika Tarafa hizo mbili, hakuna hata namna ya kutoa taarifa. Watu wakitoka Longido wanaacha simu wanasema tunakwenda Tanganyika. Kule Lake Natron hakuna mawasiliano. Kwa hiyo, naomba Wizara hii ipeleke mawasiliano kule. Hata TTCL hakuna, hakuna mawasiliano ya aina yoyote. Kwa hiyo, ningependa kusema kwamba mtusaidie ili tuwe na mawasiliano na wenzetu walioko huko Ketumbene.

Lingine ambalo ningependa kulizungumzia ni Wakurugenzi katika Wilaya hizi mpya. Asubuhi Mheshimiwa Spika, ulitoa taarifa kwamba fedha zilikwishatumwa kwa kila Halmashauri.

Nategemea ni pamoja na Halmashauri zile mpya, Halmashauri ya Longido, Hai, Siha na zote mpya. Sasa nashangaa hizi Halmashauri zetu mmemtumia nani hizi fedha,

47 hatuna Mkurugenzi, hatuna Accountant na Serikali ilisema kwamba tarehe 1 Halmashauri zote mpya watakuwa na Wakurugenzi, wako wapi hawa wakurugenzi tunawahitaji?

Mkishatengana na Halmashauri nyingine ile Halmashauri Mama hakuna tena mawasiliano vizuri. Naiomba Serikali itamke kesho kwamba hawa Wakurugenzi tuwapate, tufanye kazi, kwa sababu tuna hamu ya kukimbia ili tupate maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo jingine ni udhibiti wa fedha za barabara. Hapa ndiyo kuna kasheshe. Kama kuna fedha zinazoliwa nchi hii ni fedha zinazoitwa za barabara na zinaliwa bila huruma.

Kama kuna asilimia kumi inayotembea ni katika fedha za barabara, hakuna ukaguzi wa barabara. Rais alipita kwenye barabara yangu ya Ketumbene hajanambia lakini nadhani alishangaa kwa sababu siyo barabara ni korongo maji yanafuata kwenye hiyo barabara mpaka iende kupata Mto, yakifika kwenye mto ndiyo yaikwepe.

Hakuna ukaguzi! Naiomba Serikali itoe fedha na ihakikishe kuwe na timu ya kufuatilia katika kila Wilaya. Isitupe fedha ikakaa, itupe fedha halafu ifuatilie kuangalia kwamba hizo fedha zimefanya kazi gani. Naomba muwarudishe Madiwani katika zile Bodi za Tenda. Mimi naomba kabisa hili Serikali iliangalie. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo nakushukuru kwa kunipa nafasi hii na naunga mkono hoja. (Makofi)

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, kwanza nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia hoja ya Miundombinu. Naanza kwa kuunga mkono hoja hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Miundombinu, lakini japo ni Mjumbe ni vyema nizungumze kwa sababu mimi ni Mbunge ninaowakilisha wananchi na siku zote ninapoongea Bungeni ninakuwa nimetumwa na wananchi ambao walinipa kura.

Mheshimiwa Spika, nina mambo matatu ya kuzungumza ambayo yote ni ya msingi sana. Mambo mawili nimetumwa na wananchi wangu wa Same Mashariki na moja ni la kwangu mwenyewe.

Mheshimiwa Spika, tarehe 30 Septemba, 2005 kama saa nne na dakika 28 hivi aliyekuwa mgombea wa Urais, Mheshimiwa ambaye ni Rais sasa hivi, Jakaya Mrisho Kikwete alifika Jimboni kwangu kuomba kura pamoja na kuniombea kura mimi pamoja na Madiwani.

Mheshimiwa Spika, jambo la kwanza ambalo nilimshukuru sana Mgombea wa Urais, ni kuongea na mimi kabla ya kuzungumza na wananchi na aliniuliza, “Anne Kilango hapa kwako ni lipi ambalo ni kubwa unaona nilizungumze?” Nilimwambia

48 mambo mawili tu, mengine aliongeza mwenyewe. Kwanza, nilimwambia, “hapa kwangu barabara ya kutoka Mkomazi kupitia Ndungu-Kisiwani mpaka Same ni siasa”. Akasema, “naifahamu hiyo barabara.” La pili, nikamwambia, “ni mradi wa umwagiliaji wa maji wa Wajapani mradi wa Ndungu, Mheshimiwa mengine utaongeza mwenyewe.”

Mheshimiwa Spika, Mgombea Urais aliposimama akanishika mkono vizuri akawaomba na kuwaambia wananchi wa Same Mashariki, “mpeni kura Mheshimiwa Anna Kilango Malecela anisaidie kazi tutaboresha na kutengeneza barabara ya Ndungu mpaka Same na barabara za Milimani”, wananchi walifurahi wakacheza ngoma mbele yake. Shahidi yangu ni Mheshimiwa Cynthia Ngoye ambaye yupo kwenye Bunge hili, ndiye alikuwa Mkuu wa Mkoa ambapo aliandamana na mgombea Urais. Lakini nilipoona ahadi ya Mheshimiwa Rais hajatekelezwa, barabara hiyo haijatengenezwa, Kama nilivyosema barabara ni siasa kule kwangu, Mheshimiwa Waziri naomba hiyo barabara itengenezwe nimetumwa na wananchi niwasilishe ombi hili. Mheshimiwa Spika, jambo la pili, mimi linaniuma kweli kweli! Amemaliza kulizungumzia Mheshimiwa Lekule Laizer sasa hivi, ni kuhusu barabara vijijini. Mimi nina barabara ambayo leo ndiyo nitaililia hapa ndani. Barabara yangu ya kilomita 8 kutoka Lungulu kwenda Ndungu.

Mheshimiwa Spika, mimi nina Kata nane ambazo zote ni za milimani na wewe unazifahamu uliwahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Katika sehemu ya tambarare nina Kata nne tu. Kata ya Lungulu na Mtii iko Milimani sana na inategemea kuuza mazao yake yote katika sehemu tambarare.

Mheshimiwa Spika, naishukuru Serikali ya Chama cha Mapinduzi sana tena sana, kuanzia mwaka 2002 Serikali ya CCM ilikuwa inatenga fedha kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Same kujenga barabara ya kilomita 8 tu kutoka Lungulu kufika Ndungu kwenye soko kuu.

Mheshimiwa Spika, lakini maajabu barabara ile haikujengwa. Wananchi wangu sasa hivi ninavyoongea hapa wanabeba tangawizi kilo 50 kichwani, wanaanza safari ya kwenda sokoni saa sita usiku ili wafike Ndungu saa mbili asubuhi kilomita 25 kwenda kuuza tangawizi kilo 50 tu kilomita 25.

Lakini Serikali ya CCM ilijitahidi ikatenga fedha kuanzia mwaka 2002 barabara ijengwe ya kilomita 8 ili wananchi wateremke kilomita 8 kutoka Lungulu Mtii kuja Ndungu sokoni, kuliko wazunguke kilomita 25 wajengwe barabara ya kilomita 8. Fedha zile zilikwenda wapi?

Mheshimiwa Spika, nikaenda kwenye Bodi ya Barabara, tarehe 20 Aprili, 2006, nikaomba barabara ya Ndungu-Lungulu mwaka 2004, fedha zilizotolewa kadhaa, fedha zilizotumika kadhaa kazi imekamilika. Pale pale nikamwambia Mhandisi tutoke nje twende, nikatoka na yule Mhandisi nikamwambia barabara ipi umesema kazi imekamilika ya Ndungu-Lungulu ni barabara yangu ninayoijua haipo!

49 Mheshimiwa Spika, ni kichaka, akaniambia, “Mheshimiwa Mbunge, nitatafuta nafasi niongee na wewe,” nikamwambia, “ mimi siongei na wewe, wewe siyo size yangu, nitaongea na Mkurugenzi”. Nikarudi nikamwandikia Mkurugenzi barua anieleze fedha zilizotolewa na Serikali Kuu za kujenga barabara ya kilomita 8 zimekwenda wapi? Ninayo nakala yake hapa. (Makofi) Mheshimiwa Spika, Serikali ya Chama cha Mapinduzi inatoa fedha jamani. Kipindi hiki imetenga shilingi bilioni 65 kupeleka katika barabara za Vijijini, lakini hizi fedha, mimi nina ushahidi hazijenga barabara vijijini. Nikamwandikia Mkurugenzi barua, Mkurugenzi akamwandikia Mhandisi barua anijibu. Mhandisi akanijibu hili hapa jibu lake. Hakuna kitu alichonijibu, alizunguka kwa sababu zile fedha alizitumia kama anavyojua yeye, hakujenga barabara ile. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi nikatumia majibu yake dhaifu, nikamwandikia Mkuu wa Mkoa barua ninayo hapa. Nikamwambia Mkuu wa Mkoa nataka barabara. Kilichofanyika Mkurugenzi, Mheshimiwa Waziri Mkuu alikwishamfukuza kazi kabla hata mimi sijagundua hili; kilichofanyika eti ni yule Mhandisi sijui akapelekwa Nkansi, nikaletewa Mhandisi mpya. Kwangu mimi hiyo siyo solution, solution ni kupata barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi silali kwa sababu ya hii barabara. Yupo shahidi anayejua silali, ni Mbunge wa Mtera anajua silali. Mimi nataka barabara ya Lungulu - Ndungu, sitaki Mkurugenzi afukuzwe kazi, sitaki Mhandisi ahamishwe I want my road! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wananchi wanahangaika. Juzi nimezungumza hapa watu wakaguna, umaskini wa wananchi wetu vijijini ni sisi viongozi pamoja na watendaji wabovu. Lakini wananchi wetu wasingekuwa maskini hivyo. Mkuu wa Mkoa ni kweli amemwondoka Mhandisi sijui ni yeye, lakini Mhandisi ameondolewa, nimeletewa mwingine. Lakini tatizo lipo pale pale wananchi wangu wa Lungulu na Mtii ni maskini kuliko kiasi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ile Serikali maskini naishukuru ilikwishatoa fedha tena nyingi. Nilikwenda kufanya audit mimi mwenyewe fedha nyingi Serikali ilitoa, lakini hakuna barabara!

Mheshimiwa Spika, nimekwenda mpaka leo ni kichaka. Mimi na Diwani na Lungulu kila siku tunazungumzia hii barabara. Nikaiomba Halmashauri waandike barua Serikalini waniletee kipindi hiki nimpe Waziri. Hii hapa ninayo nimeletewa kwa fax jana, Waziri nitamkabidhi, hakuna barabara! Ninakusihi Mheshimiwa Waziri wewe ulitoka Bariadi ukaacha kote, ukaja ukaoa kule kwetu huko huko Lungulu. Wale ni wakwe zako, waonee huruma, naomba hiyo barabara jamani najisikia hata kulia. Kilomita 8 tu! Nafikiri Mheshimiwa Waziri amenisikia. Kweli kabisa kwa unyenyekevu mkubwa mlitoa fedha Serikali zimetumika vibaya. Naomba hii barabara itengenezwe ili wananchi wangu waendelee kuwa na imani na Serikali ya CCM. (Makofi/Kicheko)

50 Mheshimiwa Spika, wakati nawaomba kura walilalamika kuhusu hiyo barabara, nasema ukweli mimi ninapozungumza siongeze wala sipunguzi katika kura mia moja Lungulu na Mtii kwa hasira ya hiyo barabara walinipa asilimia 30 tu katika asilimia 100. Lakini hasira ilikuwa ni barabara wakaiadhibu Serikali ya CCM, kumbe siyo Serikali ya CCM ni mtu! Hilo limeeleweka na Mheshimiwa Waziri nafikiri amenielewa atawaangalia wakwe zake vizuri.

Mheshimiwa Spika, niongelee suala la tatu. Kupanga ni Kuchagua. Hili sikutumwa na wananchi ni la kwangu kama Mbunge napaswa kuzungumza ya Jimbo langu na nizungumze ya nchi. Jamani Kupanga ni Kuchagua. Sisi Tanzania tunakumbwa na njaa kila wakati. Kwa sisi Wapare kaya yenye njaa kila siku inadharaulika. Tanzania tusikubali kudharaulika kila wakati kwamba sisi ni watu wa njaa, tunasema tuna ukame ni kweli.

Mheshimiwa Spika, lakini kuna maeneo hayana ukame. Nilikwenda katika Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika kufanya utafiti kuna Mkoa wa Iringa, kuna Mkoa wa Mbeya, kuna Mkoa wa Rukwa na kuna Mkoa wa Ruvuma. Mimi naizungumza mikoa ambayo nimekwenda kuifanyia utafiti.

Hii mikoa ina bahati nzuri ya kuwa na hali ya hewa nzuri na mvua za kutosha. Lakini naomba niwaambie ukweli kuwa utafiti niliofanya unahusu maeneo yote ambayo yanafaa kulimwa ambayo sasa hayalimwi. Eneo lisilolimwa Iringa ni asilimia 89, Mbeya ni asilimia 91; Rukwa ni asilimia 85; Ruvuma ni asilimia 91. Mimi sikuchukua data hizi kwenye intaneti, nilikwenda katika Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika. Lakini hayo maeneo hayalimwi kwa sababu gani? Jamani hakuna miundombinu itakayowezesha mazao hayo kufika kwenye masoko makubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mikoa hiyo minne tu ingeweza kulisha nchi yetu na bado tuka-export. Serikali kupanga ni kuchagua. Ninawasihi waweke mpango wa muda mrefu, wafungue njia ili tuweze ku-utilize hii ardhi. Jamani wengi tutakwenda kuwekeza siyo lazima investors kutoka nje. Wengine tunapenda kulima, tutaenda kuwekeza ilimradi nchi iondokane na adha ya njaa. Rukwa wakilima leo asilimia 100 watasafirisha namna gani hayo mazao kutoka Rukwa wakati hakuna barabara. Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, aibu ya njaa tuhakikishe tunaiondoa na tutaiondoa tu pole pole kwa kupanga na kuchagua. Je, tumechagua kuwa watu wa njaa? Haya kama tumeamua kuondokana na njaa pole pole kwa mpango wa muda mrefu. Leo tunaondoa hapa tunasogeza pale mpaka hayo mazao yafike sokoni, tutaondokana na tatizo la njaa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashukuru kwanza kwa kupata hii nafasi. Lakini nashukuru kwamba leo nimezungumza kuhusu Lungulu na Mtii inarudi pale pale. Naomba kuunga mkono hoja hii. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Mbunge, ahsante sana. Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu mambo haya muyaangalie inaelekea Wahandisi wanaweza hata kuvunja

51 ndoa za watu. Mheshimiwa Mwinchoum Msomi atafuatiwa na Mheshimiwa na tutamalizia na Mheshimiwa Dr. . (Makofi/Kicheko)

MHE. MWINCHOUM A. MSOMI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu, Naibu Mawaziri wake na Watendaji wote wa Wizara ya Miundombinu kwa jinsi hotuba yao ilivyo nzuri.

Mheshimiwa Spika, vilevile nachukua fursa hii kutoa pole kwa familia ya marehemu Amina Chifupa, Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi. Amin!

Mheshimiwa Spika, naomba niende kwenye Jimbo langu. Tuna barabara kule katika Tarafa ya Kigamboni barabara ya kutoka Kongowe hadi Feri.

Mheshimiwa Spika, barabara hiyo tulipata matatizo kiasi kama miezi minne au mitano iliyopita. Wenzetu wa TANROADS walikuja kuweka X barabara hiyo kuanzia Kongowe hadi Feri. Lakini kwa bahati mbaya sana bajeti kwa ajili ya utekelezaji wa barabara hiyo ilikuwa hakuna; na kuna agizo la Mheshimiwa Waziri Mkuu kwamba ikiwa bajeti hakuna, basi X zisiwekwe. Kwa hiyo, walikiuka maagizo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kwanza.

Mheshimiwa Spika, lakini pamoja na yote hayo tulikubaliana kwenye kikao chetu cha TANROADS Mkoa kwamba yafanyike mambo yafuatayo:- Moja, tulikubaliana kwamba uwekaji wa X si sahihi kwa misingi hiyo. Kwa hiyo, X zifutwe mpaka fedha zitakapopatikana kwa ajili mradi huo. La pili, tukawa na ugomvi na mvutano baina ya TANROADS na wananchi wa Jimbo la Kigamboni hasa Tarafa ya Kigamboni kwamba ilipoendelezwa barabara kutoka kiwango cha kokoto hadi lami barabara ile ilijengwa na ADUKO ikawekwa hifadhi ya barabara ambayo ni mita 16 kila upande.

Mheshimiwa Spika, lakini watu wa TANROADS walivyokuja mara hii wamezidisha vipimo kutoka mita 16 pini ambayo wameweka wenyewe kwa kutumia ADUKO, wameingia ndani zaidi hadi mita 22.5 sawa na kama mita 45 kwa pande zote mbili.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ugomvi uliopo wa wananchi ni kwamba wanathamini vipimo vya awali vya mita 16 kila upande. Katika zoezi la kuendeleza barabara hawana ugomvi, lakini wanaomba na tumekubaliana kwenye Kikao chetu cha barabara Mkoa kwamba kuanzia mita 16 kuingia ndani walizozidisha kwenye zoezi lao la juzi la kuweka X, wananchi hawana budi walipwe fidia.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri nakuomba sana utakapofikia hatua ya kuendeleza barabara hiyo makubaliano yetu hayo yazingatiwe na yaheshimiwa. Wananchi wanasema hawana ugomvi, aliyejenga katika kipimo kilichopimwa na ADUKO wako tayari kuvunjiwa bila fidia. Lakini wale ambao wamejenga nje ya kipimio cha ADUKO basi walipwe fidia. Nafikiri Mheshimiwa Waziri amenielewa na uongozi wa Wizara ya Miundombinu umenielewa. Naomba lizingatiwe hilo.

52 Mheshimiwa Spika, la pili, kuna suala la kivuko. Kwanza, napenda kuishukuru Serikali kwa kuweka kwenye bajeti mwaka jana kununua kivuko kipya. Vilevile naipongeza Serikali kwa matengenezo ya MV Alina ambayo hivi sasa tunategemea baada ya siku mbili au tatu itaanza kufanya kazi vizuri tu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini naomba kutoa rai kwa Serikali kwamba kivuko hiki kimoja hakitasaidia watu wa Kigamboni kwa sababu ongezeko la wananchi wa Kigamboni ni kubwa sana. Kuna vivutio vya utalii, kuna fukwe za Kigamboni ni kubwa sana. Kwa hiyo, matumizi ni makubwa mno kupita miaka ambayo sisi tunaijua huko nyuma. Naomba Serikali iandae pole pole kwa kutenga kwenye bajeti fedha kwa ajili ya kununua kivuko kingine kipya ili adha, udhia na dhahama za Kigamboni zimalizike. Naiomba Serikali izingatie hilo kujiweka tayari kuagiza kivuko kingine ili pale Kigamboni pawe salama kwa miaka ijayo mingi tu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pale kwenye kivuko cha Kigamboni upande wa huku ng’ambo ya Kigamboni huduma zimekuwa finyu kidogo. Kwa mfano, gari likikaa kwenye line ya kuvuka, kukitokea dharura ya aina yoyote, hivi sasa hakuna njia ya kutoka. Mwenyezi Mungu atusitiri gari likilipua moto pale itakuwa balaa kubwa. Kwa hiyo, naomba TANROADS kwenye mipango yake wafikirie jambo hilo. Magari yanayoweza kuingia yawe na uwezekano wa kutoka kwa dharura. Vinginevyo kama nilivyosema Mwenyezi Mungu atuepusha, panaweza kutokea balaa kubwa tukaangamiza wananchi wetu. Kwa hiyo, naomba hilo kwa heshima na taadhima litafuatiwe mbinu japo fidia za nyumba pale zilizopo tuweze kutafuta njia za kuweza kuweka njia za dharura. Vilevile kuna huduma za choo. Ng’ambo ya mji hatuna matatizo, ng’ambo ya Kigamboni vyoo vinafungwa wananchi hawapati huduma ya vyoo. Hali kadhalika tunaomba tabia ile ya kufunga mageti kwa kufuli iondolewe. Likitokea tatizo lolote pale kwa ghafla tutauana sana. Hili linawezekana kabisa bila bajeti ya aina yoyote. Suala la choo naomba lizingatiwe vilevile. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wakati Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anazindua ujenzi wa barabara ya Kilwa, aliagiza Wizara ya Miundombinu kwamba ifanye utaratibu wa kumalizia barabara ile kutoka Mbagala Rangi tatu hadi Kongowe mwisho. Sijui Wizara imefikia wapi katika agizo hilo la Mheshimiwa Rais kama imeshatenga fedha au wapo katika hatua gani. Wananchi wa Kigamboni wanaomba kuelezwa Wizara imefikia hatua gani katika hilo.

Mheshimiwa Spika, kuna suala la ATCL. Naipongeza sana Serikali kwa kumiliki asilimia 100. Pia naiomba Bodi ifanye kazi kwa uadilifu kurudisha hadhi ya ATC, motisha kwa wafanyakazi ili wafanye kazi vizuri na kwa uadilifu vilevile na kurudisha safari za nje na wenzangu wamelichangia kuhusu kuboresha huduma za ndege na kadhalika. Kuna kitengo Wizara ya Miundombinu cha Wakala wa Majengo ya Serikali. Naomba kutoa wito kwamba Kigamboni inaendelezwa vizuri na itakuwa ni mji wa pekee. Nawaomba sana Wakala wa Majengo ya Serikali waweze kutumia fursa hiyo

53 kuiona Kigamboni kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hizo za viongozi na watumishi wa Serikali. Mheshimiwa Spika, daraja la Kigamboni. Suala hili tumelizungumzia kwa muda mrefu sana ndani ya Bunge na ndani ya Kamati za Bunge zinazohusiana na Wizara inayohusika. Kwa bahati nzuri Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu alilizungumza hili kwamba wawekezaji wanategemewa kupatikana, lakini Serikali inafanya uchambuzi ili kazi iweze kuanza mwaka huu. Kwa hiyo, naipongeza Serikali kwa hatua hiyo. Naiomba Serikali ione kwamba suala hili ni muhimu na lipewe uzito unaostahili. Kulikuwa na mpango huko nyuma wa kuendeleza Kigamboni. Walijitokeza Marekani ili kuwaweka wananchi kwenye maghorofa bila kuwahamisha, kuiendeleza Kigamboni. Naomba kuelezwa mpango huo umefikia wapi? Wananchi wa Kigamboni waliupokea kwa furaha na kama upo basi naomba uendelezwe.

Mheshimiwa Spika, kuna suala la mabasi yaendayo kwa kasi. Naomba kuelezwa pia kwamba katika mpango wa ujenzi wa barabara ya Kilwa ili kuepusha gharama za baadaye; je, mpango huo umezingatiwa au hakuzingatiwa? Kama haukuzingatiwa basi naomba katika kuendeleza barabara zetu nyingine tuweka mpango huo wa mabasi yaendayo kwa kasi kwa sababu miji inakua sana na inapanuka; na wananchi wanatoka katikati ya mji wanahamia nje ya mji. Kuna barabara itokayo Feri hadi Kibada, barabara hiyo ipo kwenye kiwango cha changarawe, lakini imeungana na maeneo ambayo vimepimwa viwanja vingi sana, eneo la Kisota na eneo Vijibweni. Naiomba Serikali kwa heshima na taadhima iangalie barabara hiyo ya Feri Kibada kwa misingi kwamba inakwenda kwenye viwanja ambavyo vimepimwa vya kisasa na vyenye ukubwa wa kila aina na wananchi tayari wamekwishaomba; na wingi wa wananchi wa Kigamboni na matumizi ya barabara hii ili iweze kutengenezwa kwa kiwango cha lami katika mipango yao ijayo.

Mheshimiwa Spika, mpango wa kupunguza msongamano wa magari kwa kupitia baharini. Katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu ya mwaka jana alizungumzia suala hili kwa kirefu sana. Lakini kwa bahati mbaya hotuba ya safari hii haijasema hata kidogo. Je, mpango huo umefikia wapi wa kupunguza msongamano wa magari ambao ulikuwa uanzie Kunduchi hadi kufika Feri na kwenda mitaa ya Kigamboni. Serikali inasema nini kuhusu mpango huo ambao ulizungumzwa kwa undani kabisa katika hotuba ya bajeti ya mwaka jana? Kuna uwanja wa ndege. Nitazungumzia suala la bridge. Madaraja yale ya kupandia ndege na kushukia abiria kwa International Flights. Madaraja sasa yaanza kubomoka hayaridhishi. Naiomba Serikali kupitia Wizara ya Miundombinu kuyaangalia madaraja hayo ili yaendane na wakati. Kwa kweli yanatishia maisha, ukipita sehemu nyingine zinabonyea, akipita mtu mzito kama mimi mguu kidogo unatikisika. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, kuna suala la huduma za simu za mkononi. Mwaka jana hapa niliomba sana, lakini naishukuru sana Wizara ya Miundombinu imesaidia kwa kiwango kikubwa sana, kiwango ambacho huduma hizo zimezagaa kwa mapana na marefu ndani ya Jimbo la Kigamboni hasa maeneo ya fukwe za baharini za Kigamboni. Kampuni ambazo zilijitokeza kwa hili ni CELTEL na TIGO, lakini naomba kutoa wito kwa VODACOM nao wapeleke huduma zao kule ili wananchi wawe na chaguzi zaidi.

54 Mheshimiwa Spika, hali kadhalika naomba kutoa pongezi nyingi sana kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa mpango wake wa barabara tatu katika Mkoa wa Dar es Salaam. Naomba wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wafanye matumizi ya barabara hizo kwa heshima na taratibu zilizopo za trafiki na wazingatie maelekezo ya trafiki ili kupunguza matatizo yote ya ajali na matatizo mengineyo. Lakini pia nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Zaynab Vulu ambaye alizungumzia sana masuala ya vivuko kuhusu mambo ya bima kwa ajili ya tahadhari ya wananchi likitokea lolote. Namshukuru, lakini alisahau moja tu kumwomba Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu afuatane naye kwenda kuangalia vivuko huko Kigamboni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja. (Makofi)

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi mchana huu na mimi nichangie katika hotuba ya Wizara ya Miundombinu. Lakini awali ya yote naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri na wataalamu wake wote kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya katika Wizara hii. Lakini nianze kwa kusema kwamba naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini naomba pia nizipongeze Taasisi zilizopo chini ya Wizara hii, Taasisi hizi zipo nyingi, kuna Reli, ATC, Bandari, Simu, Posta, Hali ya Hewa, SUMATRA, TICRA, Viwanja vya Ndege na kadhalika.

Taasisi hizi ndiyo roho ya nchi hii. Narudia kusema taasisi zilizoko chini ya Wizara ya Miundombinu, bandari, reli, ndege na kadhalika ndiyo roho ya uchumi wa nchi yetu. Niwaombe wataalamu kama walivyoshauri Wabunge wenzangu sitaki kurudia, kanuni haziruhusu, endapo mtasimamia vizuri yale yaliyosemwa na Waheshimiwa Wabunge nina uhakika nchi yetu itasonga mbele na ninawaomba tuimbe wimbo mmoja, tusitofautiane katika kuimba.

Mheshimiwa Spika, kule Ukerewe kuna wimbo, wakati mnapiga makasia ziwani huwa tunaimba, “alimselema adija, alimselema adija!” Sasa endapo taasisi hizi zilizopo chini ya Wizara ya Miundombinu kama zitaimba wimbo alimselema adija nina uhakika tutasonga mbele. Lakini endapo baadhi yao badala ya kuimba alimselema lishoka, tutarudi nyuma. Maana yake ni kwamba badala ya kupiga kasia kwenye kasia, unatupa kurudi nyuma. Sasa badala ya kupiga kasia kwa kurudi nyuma unapiga kasia kwa kwenda mbele. Kwa maana hiyo, utakuwa unapingana na wenzako na maendeleo ndivyo yanavyotakiwa kwenda sote tuimbe wimbo mmoja.

Mheshimiwa Spika, pili, naipongeza sana Benki ya Dunia kwa ule mpango wake wa Mpango wa Mradi Maalumu wa kufanyia matengenezo Barabara zetu katika mikoa mitatu ukiwemo Mkoa wa Mwanza. Mpango huu utasaidia kwa Mkoa wa Mwanza kabla ya kilomita 1,470 kilomita 361 zitahusika. Kwa sababu zipo barabara zingine ambazo hazitakuwepo kwenye mpango huo kwa baadhi ya Wilaya, Wilaya yangu ya Kwimba imeguswa, lakini Wilaya zingine za Magu Misungwi, Geita pamoja na Ukerewe

55 hazikuguswa. Zinabaki kilomita 761, kwa sababu hiyo unaweza ukaita kama saving. Kwa kuwa mradi huu ni wa miaka mitano zile pesa ambazo zingeweza kutumika kujenga kilomita 361 sasa World Bank wanasimamia kwa muda wa miaka 5. Hizi kilomita 761 kwa mkoa mzima ambao mimi naita kama saving naomba ikiwezekanaTANROADS wasimamie kwa miaka mitano tusije tukaambiwa kwamba barabara hizi ni mbaya sasa.

Mheshimiwa Spika, wananchi wangu wa jimbo la Sumve kufuatana na hii saving nina maombi mawili. Barabara yangu ya kutoka Fulo inapita Sumve kwenda Nyambiti madukani, wataalamu wa TANROADS, Wizara ya Miundombinu barabara hiyo waliifahamu vizuri zaidi. Tangu mwaka 1996 mpaka leo barabara hiyo haijatengenezwa na kupangiwa fedha, inapangiwa fedha kidogo kidogo. Sasa si vizuri kuzungumzia suala lile lile kila siku lakini naomba wenzangu TANROADS, Mheshimiwa Waziri, Manaibu na wataalamu hasa yule Mkurugenzi wa Barabara Vijijini, barabara hii sasa naomba itengenezwe kwa kiwango cha changarawe iwe nzuri zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwezi Aprili niliuliza swali hapa kuhusu daraja la Mto Simiu upande wa Maligisu Kabila. Katika majibu ya Serikali alijibu Naibu Waziri Mahanga lakini alijibu kwa niaba ya Waziri. Kwa hiyo, Serikali iliahidi baada ya kuomba ikasema basi angalau kitengwe kiasi cha shilingi milioni 50 kwa ajili ya upembuzi yakinifu. Serikali ilikubali ikasema itaangalia, najua imekubali. Naomba sasa daraja hili lijengwe na ikiwezekana katika majibu ya leo Waziri anijibu. Lakini lingine ipo barabara ya muda mrefu ambayo kwenye Ilani imetajwa, barabara ya Mziha, Mvomero iko kwenye Ilani ya Uchaguzi, hiyo iko Morogoro, naomba nayo tupatiwe majibu.

Mheshimiwa Spika, naomba nizungumzie usafiri wa anga. Wenzangu wameipongeza ATC, mimi naungana nao, lakini naomba nizungumzie viwanja vya ndege. Mimi nitazungumzia Kiwanja cha Ndege cha KIA. Nilipokuwa mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) katika kipindi cha nyuma tulikwenda pale KIA lakini kwa masikitiko makubwa kile kiwanja sijui tuna utaratibu gani kwa jinsi kilivyo. Mheshimiwa Rais alizungumzia kuhusu kurekebisha mikataba ambayo haina manufaa kwa Watanzania, mkataba huu wa hao wenzetu wa KADICO najua una walakini mkubwa. Tulipiga kelele humu ndani lakini sasa tunaomba tupate majibu ya Serikali, hivi kweli mpaka leo tukiuliza huyu tuliyemkabidhi kusimamia ule uwanja wa KIA ameuendeleza kwa kiasi gani? Hivi yale malipo ya Dola za Marakeni 1,000 na thamani ya eneo kubwa lile je, inajitosheleza? Kwa sababu tunasikia yeye sasa hivi kwanza ameshindwa kuuendeleza, lakini kuna baadhi ya mashamba yeye ameyakodisha. Lakini papo hapo ndege ya KLM ikitua pale yeye nasikia anapata mapato ya Dola karibu milioni 5 kila inapotua. Kama ni kweli iko haja sasa ya kuangalia mkataba huu ili ulete manufaa kwa Watanzania.

Mheshimiwa Spika, naomba kuzungumzia suala la ubora wa barabara zetu. Nawaomba Wahandisi kuwa fedha ambazo kwa kweli Serikali imetenga na inazotoa, ingekuwa ni vizuri zaidi Wahandisi washauri na wasimamizi wakasimamia barabara zetu ili zitengenezwe vizuri zaidi. Juzi juzi wewe ni shahidi tulisimamia hapa tukapitisha

56 Wabunge wote tukakubali tukasema kwamba kila lita moja ya mafuta tuongeze shilingi mia, tunataka tuambiwe shilingi mia imezaa matunda haya na haya. Lingine nilitaka nizungumzie suala la TEHAMA, lakini fibre optic hii ni nyenzo kubwa sana kama tutaisimamia vizuri. Huyu ndio mkombozi kwetu, kwenye shule zetu, hospitali zetu na biashara zetu, naomba hili tulisimamie.

Suala la TEMESA nilishasema wakati nikiwa Mwanza kwenye Road Board. Unaweza ukacheza na barabara lakini naomba usicheze na maji yanayotembea au yaliyotulia ziwani au baharini. Cheza na vitu vingine vyote vile lakini sio ucheze na maji. Sasa hivi hapa vivuko pantoni. Mheshimiwa Masilingi amesema asubuhi hapa, Ziwa Victoria hatuna boti, Ziwa Victoria hakuna meli, lakini wale wananchi waliwataka wafanye biashara.

Kuna biashara Kisumu, Mombasa, Kagera lakini hamna usafiri wa uhakika. Lakini pantoni iliyoharibika Dar es Salaam wataalamu wapo lakini hatutaki kutumia wataalamu tunatumia watu wengine, nashauri na kuomba tutumie wataalamu wetu waliopo, tusitumie watu ambao sio wataalamu sana ili kwenda kuchukua watu wengine ambao hawavijui vivuko hivi, vinaweza vikaleta matatizo.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana naomba kusema kwamba naunga mkono hoja hii lakini naomba barabara yangu ya Fulo, Nyambiti nijibiwe, lakini pili daraja la mto Shimilu naomba lipewe kipaumbele katika bajeti hii. Nakushukuru sana na naunga mkono hoja.

MHE. DR. HARRISON G. MWAKYEMBE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kunipa fursa na mimi nichangie hoja iliyoko mbele yetu iliyowasilishwa kwa ufasaha mkubwa jana na Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya wananchi waishio Wilaya ya Kyela, ningependa nianze kwa kumshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, kwa kuwa kiongozi wa kwanza katika historia ya nchi yetu aliyeitembelea Kyela, akabaini tatizo kuu linaloshikilia maendeleo ya Kyela na akaamua hapo hapo kulifanyia kazi. Tatizo lenyewe ni la miundombinu mibovu hususan barabara muhimu kwa utalii na usafirishaji mazao ya kutoka Kikusya hadi Ipinda, kutoka Ipinda hadi Matema Beach. Mheshimiwa Rais akasema ataifanyia kazi. Kweli ameifanyia kazi kwa sababu baada ya Mheshimiwa Rais kuondoka Kyela, Naibu Waziri wa Miundombinu, Dr. Milton Makongoro Mahanga akaja Kyela. Tukaikagua hiyo barabara ambayo kwa kweli ni mahandaki kutoka Kikusia mpaka mwisho wake. Namshukuru sana Dr. Mahanga, kwa kazi kubwa aliyoifanya na leo hii nasimama mbele yenu hapa kwa furaha kwamba kwa mara ya kwanza hiyo barabara eti nayo imejitokeza mpaka kwenye bajeti ya Wizara!

Mheshimiwa Spika, tayari consultant ameteuliwa, tayari feasibility study inafanyika na detailed design inafanyika. Jamani hapo nimeishiwa nguvu , naunga hoja hii mkono bila ya kigugumizi. Ila kwa kuwa uchumi wa Wilaya tatu za Kyela, Rungwe na Ileje una mzunguko mmoja, nitashukuru kusikia kutoka kwa Waziri maendeleo

57 kuhusu barabara ya Katumba, Isange/Mbambo hadi Tukuyu ambayo vilevile Mheshimiwa Rais aliahidi.

Mheshimiwa Spika, ukurasa wa 33 na 34 wa hotuba ya Waziri una maelezo kwamba katika mwaka wa fedha 2006/2007 Wizara ilifanya matengenezo ya kilomita 8,611 ya barabara za mikoa. Sasa najiuliza hapa, hivi hizi kilomita zote hizo zinajumuisha na barabara ile ya Kyela iliyo chini ya mkoa ya kutoka njiapanda ya Kasumulu hadi Itungi Port? Najiuliza kwa sababu hiyo barabara ina mashimo ya muda mrefu kweli kweli na yanazidi kuongezeka. Kuna tatizo la periodic maintenance kwa upande wa TANROADS. Naomba Wizara wawe wakali kipindi hiki kwa sababu fedha inayotumika ni fedha ya walipakodi.

Mheshimiwa Spika, nimeshukuru sana kusikia kwamba kipande kilichobakia baada tu ya Ipyana cha barabara hiyo hiyo mpaka Itungi Port, sasa hivi kinafanyiwa kazi na Wizara. Ningeomba nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu na wasaidizi wake kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Ombi langu kubwa kwa Mheshimiwa Waziri na kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ni kuomba wahakikishe uboreshaji wa Bandari ya Itungi unafanyika haraka iwezekanavyo. Kwa sababu Bandari hii wakati wa kiangazi mchanga unakusanyika na meli zinashindwa kuingia Bandarini hivyo zinakwenda kutia nanga kwenye kabandari ka muda kanaitwa Kiwira.

Lakini kutumia Kiwira kuna matatizo. Kwa sababu kwanza, barabara ya kwenda Kiwira ni barabara ya udongo, inapita kijijini inahudumiwa na Halmashauri ambayo haina fedha na inabeba magari mazito yanayopeleka shehena kwenye meli, magari yenye shehena tani 20, 25 30. Kwa kweli imetuletea madhara makubwa ya mahandaki kule. Mheshimiwa Spika, lakini la pili , barabara iko karibu na Mto Kiwira. Magari yakipita yale mazito, unaona kabisa mto unachemka na ndio sababu hata samaki wale wazuri wa Kyela wameanza kupotea pole pole, wanashangaa huu muziki unatoka wapi! Na halafu hatuelewi seapage kule chini inakwenda wapi. Kwa hiyo katika muda mrefu tunaweza tukapata madhara makubwa sana. Licha ya hilo, barabara ile ni nyembamba, magari hayawezi kupishana. Likiharibika moja ni msururu wa malori 30, hali mbaya inayotokea pale.

Usiku hatuna umeme, madereva na mataniboi wao wanatawanyika kwenye migomba huko kutuharibia watoto wetu. Tengenezeni Bandari ya Itungi haraka. Itafika mahali tutazuia hayo magari yasipite kule. Kwa sababu ni barabara ya kijijini haina vyoo, kwa hiyo hawa watu wamegeuza bustani za watu ndio zimekuwa WC. Namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri, Dr. Maua Daftari na Mheshimiwa Dr. Milton Mahanga, kwani wote wameiona hiyo Bandari. Tafadhali jamani chonde chonde wasije wakaniharibia watoto kule, hawa watu ni hatari sana!

Kwa kipindi kirefu toka niapishwe kuwa Mbunge nimekuwa nalalamikia sana kuhusu madaraja Kyela. Kyela imebahatika lakini bahati hiyo imekuwa adha. Tuna mito ya kudumu zaidi ya 9 na mito hiyo yote ina mamba. Hatuna madaraja, madaraja yetu ni

58 ya miti na mianzi. Tumepoteza watoto wa shule wengi; tumepoteza watu wengi ambao wangekuwa ni nguvu kazi ya kutosha kwa Wilaya ya Kyela.

Tumejenga shule sasa hivi, shule nyingine itashindikana watoto kwenda wakati wa mvua kwa sababu huwezi kuvuka maji kwenye haya madaraja yetu ya matete na hizi suspended bridges ambazo tumejengewa pale. Mheshimiwa Makongoro Mahanga amepita na mimi, ameiona hiyo sehemu. Nilimpeleka makusudi aone matatizo ninayopata mwenzake ninapokwenda kutembelea Kata ya Mwaya na Lusungo. Inabidi niingie kwenye maji.

Mheshimiwa Spika, nimebeba mpaka picha muone kwamba jamani nateseka kiasi gani. Hii picha ni ya Mbunge wa karne ya 21. Nitakuletea hii picha. Naingia kwenye maji kwenda kuhutubia, nyuma yangu ni msaidizi wangu na ameshika rambo lenye simu yangu na suruali na vitu vingine ambavyo siwezi kuvitaja hapa. Ni aibu kubwa Mheshimiwa Spika! Nalisema hili kwa sababu nimeandika barua, nimelalamika. Mheshimiwa Pinda amenisikiliza. Mheshimiwa Chenge amenisikiliza lakini naye juzi ameniandikia barua bahati mbaya ameinakili Wilayani. Madiwani wenzangu wameanza kulia kilio. Wizara inasema haiwezi kuwasaidia ila inaweza kutoa ushauri wa kiufundi. Jamani ushauri wa kiufundi kwa watu wa Kyela! Huo hatuuihitaji, tunao siku zote toka mwaka 1961 mpaka leo. Tuna-survive kwa sababu tuna ufundi wetu wenyewe wa kuvuka pale. Tunataka daraja, ushauri wa kiufundi wa nini?

Mheshimiwa Spika, ukiangalia hata hii picha nilipojishika pale ndio ufundi wenyewe huo. Namwomba Mheshimiwa Chenge anisaidie. Sina maana kuwa Mbunge wa Kyela wakati matatizo yanayojitokeza sasa hivi ni yale ambayo yangetakiwa kuwepo miaka ya nineteen kweusi huko.

Naomba Serikali inisaidie kwenye hilo. Isiponisaidia nitawaaibisha. Nitaitisha mimi fund raising campaign niwaombe kila mtu anichangie. Ni aibu Mbunge kuanza kuchangiwa vitu vya miundombinu. Nisaidie Mheshimiwa Chenge.

Mheshimiwa Spika, ukurasa wa 12, 13, na 14 wa hotuba ya Waziri unaongelea maboresho makubwa ya sekta ya simu. Lakini hotuba nzima ya Mheshimiwa Waziri haigusii kabisa kutwaliwa kwa uongozi wa uendeshaji wa Shirika letu la Simu la TTCL na Kampuni ya Wazungu kutoka Canada inaitwa SASKTEL.

Nadhani suala hilo ni kubwa, Bunge hili lilitakiwa litaarifiwe. Sioni hilo katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri. Naomba tueleze kidogo. Waswahili tuna msemo “aliyewahi kuumwa na nyoka akiona ung’ong’o hustuka”. Watanzania tumeshaumwa na nyoka, Watanzania tumeumizwa sana na Mikataba hii ya kuwaachia wageni kuendesha Mashirika yetu kwa imani kwamba wataalamu wetu sisi hawawezi.

Mheshimiwa Spika, uzoefu tulioupata TANESCO hivi karibuni unaonyesha na kuthibitisha kabisa kwamba dhana hii si sahihi. Dr. Idris na wataalamu wa kizalendo wameiendesha TANESCO kwa ufanisi mkubwa mara mbili ya Kampuni ya Wazungu ya

59 Net Group Problems aah sorry!!! Net Group Solutions. Mimi najiuliza hivi jamani lini tutajifunza? Nilikuwa naamini kwamba fedheha tuliyoipata TANESCO inatosha. Nilifikiri kwamba fedheha tuliyoipata ATCL inatosha, nikafikiri fedheha tuliyoipata kwa TTCL yenyewe chini ya MSI na chini ya CELTEL International kwamba inatosha. Bado tunaingia mikataba mingine ya kushughulikiwa. Mheshimiwa Spika, wataalamu wetu hawana matatizo ya uendeshaji, tatizo lililoko ni mitaji. Mitaji inakopwa na hata hao wazungu waliokuja hapa ni sisi wenyewe tutakopa na watatushughulikia. Mimi nina uhakika tutarudi hapa hapa tumeinamisha vichwa. Tunachohitaji ni mitaji. Kama tumepungukiwa na utaalamu si tunanunua utaalamu? Kama tunataka teknolojia , si tunanunua teknolojia, tunaajiri mtu? Naomba Waziri atujibie maswali machache tu atakaposimama kuhusu huo mkataba.

Nimesoma kwenye magazeti kwamba wakishaingia hawa Waheshimiwa, wafanyakazi 700 wa TTCL inabidi wapunguzwe. Nataka kuuliza hiyo sera ya kupunguza badala ya kuongeza ajira ni sera ya nani tena? La pili, Serikali imechukua tahadhari gani kuwa tukiwapunguza hao wazalendo, hao Waswahili, hawa wageni hawatawaleta Waganda, Wakenya, Waafrika Kusini, sijui na nani eti wanajua Kiingereza zaidi? Tuna uhakika?

Nasema hilo kwa sababu Mashirika mengi yaliyochukuliwa na Makampuni ya nje yanafanya hivyo, tena bila kujali with impunity. Wanakiuka mikataba. Mimi nitatolea mfano ninaoufahamu. I am sorry kuna Mkurugenzi wao mmoja yuko hapa. Shirika la NBC linahusika. Mkataba wa awali ulitaka expartriates 3. Leo wako 18 na wake zao na kila mtu. Wamejaa hapa , tunapunguza ajira! Tutafikia ajira milioni moja kwa double standards hizo?

La tatu, Serikali imechukua tahadhari gani kuhakikisha kuwa upungufu wote uliopelekea awali tuingizwe mjini, hauko kwenye mkataba wa sasa? Nimalizie kwa kusema tumeelezwa mara nyingi sana hapa na Waheshimiwa Mawaziri kwamba mikataba, hasa ya biashara, ni siri na kwamba Bunge hatuna haki kuiona kwa sababu tunaambiwa hiyo ndiyo best practice.

Hilo jibu liko kwenye Hansard. Whatever that means, Best practice cannot override laid down constitutional provisions. Wote tunajua hapa kwamba ibara ya 26 ya Katiba yetu inatutaka wote hapa tuheshimu na tulinde Katiba yetu. Katiba hiyo hiyo ibara ya 63 ndiyo inatoa oversight function za Bunge. Mimi naiomba Serikali inisaidie, kwenye Katiba yetu hii hapa hiyo best practice iko ibara gani?

Mheshimiwa Spika, mimi nafikiri twende kwa hoja. Msimamo wetu kama Serikali umepitwa na wakati. Unajua, ukisikia Mawaziri wanavyojibu hapa kuhusu kutokuonyesha Bunge mikataba wanatumia ile traditional system ya Westminster separation of powers na vile vile dual approach to International law. Ni ya kizamani, tunabakia peke yetu duniani tunafuata hiyo.

Uwajibikaji utapata wapi katika dunia ya leo? Kwa sababu hiyo Traditional approach ina vipengele viwili. Cha kwanza ni kwamba kuingia mikataba is an exclusive

60 province of the executive na ya pili ni kwamba hiyo mikataba ili kutumika domestically, lazima iwe domesticated na Bunge. Lakini sio leo.

Leo hii tuna Mabunge ya Dunia mengi. Kuna WTO Geneva. Ikiamua kitu, hapa sisi lazima tutekeleze. Nitatoa mifano michache. Sijui kengele imenigongea au bado...... ?

Mheshimiwa Spika, tumetunga sheria kwa mfano Sheria ya Hakimiliki na Hataza mwaka 1999. Hatukuamua sisi. WTO wamekaa wamepitisha The TRIPS Agreement yaani Trade Related Aspects of Intellectual Property Rights. Ndiyo imetulazimisha sisi tutunge hiyo. Bunge letu halina habari. Tumepitisha hapa Sheria ya Ushindani wa Biashara, Sheria ya Procument yote kutokana na maamuzi ya nje ya Kimataifa......

Mheshimiwa Spika, naunga hoja mkono.

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge muda uliosalia hautuwezeshi tena kuendelea na mchangiaji yeyote. Nilitaka kusema tu baada ya kuiona ile picha ya Mheshimiwa Mwakyembe katika jimbo lake akivuka Mto kwamba wapiga kura wa Kyela wana bahati maana yake wanaona zaidi ya sura ya Mbunge. (Makofi/Kicheko)

Waheshimiwa Wabunge saa 11.00 nitamruhusu msemaji mmoja Mheshimiwa Ibrahimi Sanya, Mbunge wa Mji Mkongwe na Waziri Kivuli wa Usalama wa Raia. Baada ya hapo saa 11.15 nitamwita Naibu Waziri Dr. Maua Daftari, saa 11.30 Naibu Waziri, Dr. Makongoro Mahanga halafu ataingia Waziri mwenyewe saa 11.45 kwa dakika zisizozidi 60, halafu tutabaki na dakika 60 za Kamati ya Matumizi. Kwa hiyo, sasa nasitisha Shughuli za Bunge hadi hapo saa 11.00 jioni.

(Saa 6.57 mchana Bunge lilifungwa mpaka saa 11.00 jioni)

(Saa 11.00 Jioni Bunge lilirudia)

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, namwita sasa mchangiaji wa mwisho kwa hoja hii ya Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu naye ni Mheshimiwa Mbunge wa Mji Mkongwe, Mheshimiwa Ibrahim Mohamed Sanya.

MHE. IBRAHIM MOHAMED SANYA:Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kupata nafasi hii na mimi kidogo nichangie kuhusu Wizara hii ya Miundombinu. Kuna msemo unaosema, when life becomes a battle ground, your mind is your best weapon. Yaani maisha yanapokuwa Uwanja wa vita basi bongo lako ndiyo silaha yako.

Sasa Tanzania tumebahatika kwamba ni nchi nzuri sana na imejengwa kwa misingi ya amani na utulivu. Ili ijengeke kiuchumi inataka minds. Namna gani?

Mheshimiwa Spika, tuanze na Air Tanzania. Baada ya kuvunjika Shirika la Ndege la Afrika Mashariki tukaanzisha Shirika la Ndege la Tanzania, likawa linakwenda vizuri

61 tu. Tukaanza ku-conquer maeneo mbalimbali, kuipeleka ndege yetu na abiria wetu na bahati nzuri tukaenda katika maeneo ambayo milango ya biashara ilifunguliwa. Watanzania walikuwa wanaelekea huko Middle East, Dubai.

Kuna kipindi kama mnakumbuka tuli-expand wings zetu mpaka London na Bombay. Bahati mbaya au nzuri kwa nia nzuri kwa dhamira safi mwaka 1995 mpaka 2000, mimi nilikuwa Mbunge ikaja AJAS kutaka kujiunga na Shirika letu kibiashara, tukajiunga nalo; na tukafanya semina nzuri hapa Bungeni. Bahati mbaya ulikuwa hupo.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, tukapewa Memo Books kwa kila Mbunge alizitumia miaka mitano, ninazo, na copy ninayo nitakupa moja; na katika ile memo book niliangalia ndani kuna picha ya simba mkubwa aliye-cover ile picha nzima.

Kuna Mbunge mmoja Mungu amrehemu, ameshakufa, wakati tunamaliza Semina akaniita na kuniuliza. “Hivi Mheshimiwa Sanya kuna siri gani ndani ya hili simba?” Nikamwambia, “limekuja kumjeruhi Twiga”. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, matokeo yake haikuchukua muda, tuka-divert, tukaingia tena kwenye Shirika la Ndege la Afrika Kusini. Shirika la Ndege la Afrika Kusini na sisi hatukuingia kwa dhamira ya kwamba tupate hasara. Wala Serikali haikuwa na nia hiyo, lakini Serikali labda ilikosa wataalamu wa kujua mbinu na njama za wajanja wachache wanaotaka kulitumia soko letu kwa kujinufaisha wao. Mwaka 2003/2004 tukapata hasara ya shilingi bilioni 5.7, 2004/2005 shilingi bilioni 9.3 na 2005/2006 kabla ya kuondoka katika shirika hilo tulitegemea kupata hasara ya shilingi bilioni 6.9, zote jumla yake ni shilingi bilioni 24.7 (Makofi)

Mheshimiwa Spika, matarajio ya Watanzania walio wengi, wanategemea Serikali iliyo makini kusimamia mikataba vizuri ili tusiwaingize hasara kwa sababu wao ndiyo walipa kodi. Bahati nzuri na hii bahati nzuri sana kuwa na Rais ambaye ndani yake kuna utu uzima na ujana. Mheshimiwa Kikwete akataka kufufua baadhi ya mikataba. Tukafanikiwa, tumetoka katika makucha na sasa hivi Shirika letu limerejea nyumbani; na bahati nzuri Twiga hakuuawa, amejeruhiwa anarejea Serengeti sasa.

Mheshimiwa Spika, Shirika la Ndege la Tanzania kama litawezeshwa kweli, kuna nafasi nzuri. Tujiulize kwa nini? Ndege kama Qatar Airway, Emirates zinakuja kila siku zinajaza abiria, wengi wao wakiwa Watanzania wafanyabishara wanao-connect from Dar es Salaam, Dubai, Bombay mpaka Gou Nzou, China. Ni tegemeo langu kwamba hii management iliyopo iwe makini sana na iwezeshwe, na Serikali iondoe mkono wake itafute wataalamu wa kuliendesha hili shirika ili na sisi tuwe na nembo yetu kitaifa tuweze kuleta na kusafirisha abiria hasa kwa vile tunainua kiwango kizuri cha utalii. (Makofi)

Ethiopian Airlines, ilianzishwa tarehe 30 Desemba, 1945, na walianzia na ndege aina ya DC3 na tarehe 8 Aprili 1946 baada ya siku 100 tu wakaanza na safari za kimataifa na safari ya kwanza ikaondoka kutoka Addis Ababa kuelekea Cairo. Lakini

62 walikuwa wana-contractor assistance ya TWA ya Mmarekani ndiyo wakaanza kufanya hivyo. Leo Ethiopia Airways imetoa ajira kwa watu 4,737. Leo Ethiopia Airways inasafiri ndani ya nchi katika Airports 30; na mataifa ya nje kuanzia Afrika Magharibi, Afrika Kusini, Afrika ya Kaskazini, Amerika, Europe, Asia, Middle East na Far East wanakwenda nchi 44. Wana ndege aina ya 737, 700 na wame-order ndege nyingine 787 dream liner ambazo watazipata mwaka wa 2008. Kwa nini tusichukue mifano au tukapeleka watu wakaenda wakajifunza Ethiopia Airways ime-pick vipi business na kuwa shirika ambalo linatambuliwa kimataifa na liko katika bara la Afrika. Ni Waafrika wenzetu wale.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, niondoke na Air Tanzania, ambapo kabla sijaondoka kuna kitu nataka nikizungumzie kidogo. Hili ni Shirika la Kitaifa, National Carrier; na juzi ilikuja Management mpya, nategemea chini ya Mheshimiwa Mustafa Nyang’anyi na Kapteni Mazola watafanya vizuri sana ili kuliendesha Shirika hili vizuri. Ni furaha yangu kwamba wametoa nafasi mbili yaani Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu, Mheshimiwa na Mheshimiwa Anne Kilango Malecela. Hili ni Shirika la Kitaifa, nafasi moja ipelekeni Zanzibar naye aende Johannesburg, aka- inaugurate hizi tiketi mpya na wala si vibaya kama mtampa Mheshimiwa Sanya.(Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, sasa nije sehemu ya pili ambayo ni Mamlaka ya Anga. Mamlaka ya Anga mwezi Oktoba /Novemba, tulikuja hapa kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa kuruhusu ndege kutumia anga yetu yaani fly over. Kwa bahati nzuri, kwa maandishi nikamuuliza Mheshimiwa Waziri; “je, Zanzibar ina anga yake”, akasema, “hapana!” Anga ni moja tu ya Tanzania. Nikamuuliza swali la pili. “Je, zinaporuka hizi ndege zinafanya malipo yoyote?” Akaniambia, “ndiyo hawaruki bure” na sasa hivi malipo yatazidi kuongezeka kwa sababu tumesaini Mkataba wa Kimataifa ambao utaruhusu kuweza kujua ndege ngapi zinapita katika anga yetu kwa kutumia rada yetu, kwa hivyo tija ya ongezeko la malipo yatakayofanywa na ndege hizo itakuwa kubwa.

Lakini niulize kitu kimoja kwa nia nzuri na kwa dhamira ya kujenga umoja wetu. Mwaka 2005/2006 kabla ya kuridhia huo Mkataba yalifanywa malipo na tukapata kiasi cha bilioni 5, is a good lump some. Kwa mwenye kuelewa nini bilioni is almost four million dollars. Je, Zanzibar imefikiriwa nayo kupatiwa gawio lake? Kwa sababu ndege zinapita pale Zanzibar. Mimi kule kwangu kuna ua usiku nakaa nasikia ndege mpaka usiku wa manane zinapita.

Najua ndiyo zile zinazofanya malipo hayo; na hiyo ni moja tu ya 2005/2006, sijui tuanzie 2000 mpaka 2006 it means kutakuwa na almost 20 million dollars. You have to support Zanzibar na wao wanataka kujiendeleza, kiwanja chao kiwe cha kisasa waweze kupata tija kutokana na vyombo vya Muungano. Kwa hiyo, ningefurahi sana Mheshimiwa Waziri leo akiniambia ni kiasi gani gawio lao na kama lilikuwa halijatayarishwa litayarishwe haraka ili lije hapa lisaidie. Kwa wale ambao wanateuliwa kule Zanzibar kuingia katika hizi Bodi nao wachangamke kidogo. Mkija huku wenzetu wana dhamira nzuri lakini bila ya kudai mkate wako ataula peke yake tu.

63 Mheshimiwa Spika, jambo jingine ni kuhusu hii reli ya kati. Muda ni mfupi tu. Hii RITES anayekuja kuwekeza ana mtaji gani? Tuelezwe mtaji wake. Isiwe tunaondoka kwenye tope za Air Tanzania tunaingia tena kwenye reli jamani! Kama hana mtaji kwa kutegemea dhamana yetu tumchukulie World Bank apate kuendesha hilo shirika kwani baada ya miaka 40 Tanzania hatuna watu ambao wanaweza kuliendesha hili Shirika baada ya Serikali kuchukua dhamana ya kupata mkopo huo kutoka World Bank na kama hatukujiinua kwa kiwango hicho tutajiinua lini? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, India is one of the best country katika Railway network, tukachukue ma-expert waje watusaidie lakini liwe chini yetu. Tutakuja kupakiwa rangi haya mabehewa tushindwe kuleta pamba Dar es Salaam kusafirishwa. Tutasafirisha abiria na mizigo na bidhaa at the end of the day hatuna kitu. Halafu unampa contract ya 25 years is not a joke. Kumbukeni Baba wa Taifa, Marehemu Mwalimu Nyerere toka ameng’atuka mpaka leo; toka ameng’atuka akawekwa Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi kuwa Rais akakaa vipindi viwili kwa miaka kumi. Akaondoka, akaja Mheshimiwa Mkapa, kakaa miaka kumi. Akaondoka ameingia sasa Mheshimiwa Kikwete mpaka amalize ndiyo miaka 25 tunampa contract huyu bwana wa RITES aje. It means 25 year tutakuwa naye huyu. Wala sijui kama kuna provision yoyote katika mkataba wa kuja kumwambia bwana stop tunakula hasara sasa hivi. Angepewa angalau katika observance ya miaka 10 au 15 au mitano na kwa nini apewe yeye? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa nini? Kwa sababu tunaona kwamba Railway Network ya India ni nzuri na huyu Mhindi anatoka India. No, is not a reason. Hasa hawa Wahindi wanaotoka India; hawa jamaa zangu wajanja sana! Ninawaelewa kwa kiasi fulani. (Makofi/Kicheko)

Kama hatukuwa makini kwamba ni soko huria, leo Wachina Kariakoo wanauza nyama na karanga ndiyo investment zao. Kwa hiyo, na huyu Mhindi akishakuja hapa, akishaona reli inafanya kazi si ajabu akachukua pamba yetu na kuipeleka Bombay. Tuwe makini tu katika utendaji wetu kuchagua Mashirika gani, watu gani wanaweza kutusaidia.

Mheshimiwa Spika, mwisho, nataka nieleze kidogo kuhusu hii TEMESA. Hii Wizara ina mainjinia wake. Mafundi umeme na mafundi wa kazi kama hizo na kukwamua kwamua hivi vivuko vinapotokea na matatizo tuwategemee hawa. Hizi agency nyingine zinazokuja hawa wanakuja kibiashara. Lazima kila Wizara ijitegemee iwe na wataalamu wake. La sivyo tutajikuta Tanzania tunafanya kazi kwa ajili ya watu wengine.

Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa, nilipokuwa ninasafiri kutoka Zanzibar kuja huku, kuhusu usalama wa hivi viwanja vyetu, mpaka naondoka Zanzibar, mashine yaku- screen mizigo Zanzibar ilikuwa haifanyi kazi na almost sixth month or more than that. Security yetu iko wapi? Na ile ni second busiest airport in Tanzania. Lazima wapelekwe wataalamu, kama mbovu haifai, itafutwe nyingine. Lakini tuangalie usalama wa viwanja vyetu na abiria wanaposafiri na ndege zetu.

64 Mheshimiwa Spika, kule kwenye Bandari ya Itungi ifanyiwe ukarabati wa haraka kuondosha ule mchanga. Na ile boti inayosafirisha watu abiria wa Tanzania wanotoka Itungi na biashara zao ndogo ndogo kwenda katika maeneo kama Manda, Itungi wengine wanakwenda mpaka sehemu nyingine za Malawi nao watafutiwe Boti ya kisasa yenye zile life jackets walau likitokea jambo la dharura nao waweze kujihisi kwamba Serikali yao inawathamini. Boti imechakaa mno, wanasafiri akinamama wengine wajawazito na wengine watoto wadogo.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

MICHANGO KWA MAANDISHI

MHE. EZEKIEL M. MAIGE:Mheshimiwa Spika, nampongeza Rais wetu, Mheshimiwa Jakaya Kikwete na Serikali yake ya Awamu ya Nne, kwa kutoa kipaumbele kwenye Bajeti. Pia niseme naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Spika, awali ya yote, nami niipongeze Serikali kwa kutoa kipaumbele katika miundombinu katika Bajeti hii ya mwaka 2007/08. Pia nampongeza Mheshimiwa Waziri, Kaka yangu Mheshimiwa Andrew Chenge, Naibu Mawaziri wake wote wawili Mheshimiwa Dr. Milton Mahanga na Mheshimiwa Dr. Maua Abeid Daftari, kwa kufanya kazi zao kwa bidii na kwa Bajeti nzuri. Bila kusahau, nampongeza pia Katibu Mkuu wa Wizara hii, Dr. Enos Bukuku kwa kazi kubwa hasa ya kuandaa Bajeti hii.

Mheshimiwa Spika, nawapongeza sana Wabunge wenzangu wanakamati wa Kamati ya Miundombinu kwa kutoa ushauri kuwa fedha zilizokuwa zimetengwa awali kwa ajili ya miundombinu zilikuwa kidogo mno, kwa Serikali yetu sikivu ya Awamu ya Nne. Ushauri huu ulipelekea Bajeti nzima ya Serikali kufanyiwa mabadiliko kwa kila Wizara kupunguziwa 15% ya Bajeti yake ili kuimarisha miundombinu nchini.

Mheshimiwa Spika, baada ya pongezi hizi, sasa niizungumzie Bajeti yenyewe. Kwa ujumla Bajeti hii ni nzuri kwa kuzingatia hali halisi ya uchumi wetu. Ni mwanzo mzuri, hivyo naiunga mkono.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, kuna maeneo kadhaa ambayo hayajapewa umuhimu unaostahili, hivyo ningependa Serikali itoe majibu ya bayana nini inafanya katika maeneo haya.

Mheshimiwa Spika, kwanza ni barabara ya Kahama - Kakola yenye urefu wa kilomita 76. Barabara hii ina matatizo mengi kama ifuatavyo:-

Kwanza Serikali haijaitaja kabisa katika Bajeti yake ya mwaka huu. Ingawa ni kweli kwa mujibu wa makubaliano ya Serikali na KMCL mwaka 1997 kuwa KMCL watakuwa wanaifanyia matengenezo barabara hii kwani wao ndiyo watumiaji wakubwa, Serikali haijaonyesha ukweli huu. Naomba Serikali iwaeleze wananchi wa Kata za Malunga, Ngogwa, Ntobo, Segese, Lunguya na Bugarama ambao wanapitiwa na barabara

65 hii, Serikali inamsimamiaje mwekezaji huyu ambaye kimkataba anahusika na ukarabati wa barabara hii.?

Pili, barabara hii ni ya vumbi. Pamoja na kwamba barabara hii ina-traffic kubwa sana, kwani inapitiwa na wastani wa malori 50 kwa siku yenye kubeba kifusi cha dhahabu pamoja na mafuta na mitambo ya contractors wa mgodi wa Bulyanhulu na wakati mwingine mgodi jirani wa Geita. Malori haya yamekuwa yakitimua vumbi kubwa sana kwa wananchi wa Kata hizi na kuathiri afya zao kwani wengi wao wanapata magonjwa yatokanayo na mfumo wa hewa. Wananchi wa Kata hizi nilizozitaja wangependa waambiwe ni lini Serikali itapata ufumbuzi wa tatizo hili la vumbi ?

Mheshimiwa Spika, wiki iliyopita niliuliza swali la nyongeza kuhusu barabara hii, jibu la Serikali kuwa haina uwezo halikuwafurahisha wananchi waathirika kwani lilimaanisha kuwa Serikali iko tayari kuwaona wakiendelea kuathirika kiafya bila ukomo !

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Msalala wanasema, tatizo si pesa, bali ni uamuzi kwa upande wa Serikali. Kama Serikali inalipwa dola milioni saba kwa mwaka kwa hiari na Barrick, inalipwa dola 200,000 kwa mwaka au dola 800,000 kwa migodi 4 ya Barrick, kwaa miaka sita toka mwaka 2001, Serikali imelipwa dola milioni 23 kutokana na mrahaba kwenye mchanga wa dhahabu, kwa miaka saba toka mwaka 1999, Serikali imelipwa dola milioni 78 kutokana na madini ya dhahabu na kama wawekezaji wa Barrick wanatumia dola 150,000 kwa mwaka kwa ukarabati wa barabara hii kwa vumbi na wako tayari kuzungumza na Serikali juu ya kushirikiana kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami, iashindwaje kuamua na kutumia vyanzo hivi vya pesa kupata dola milioni 27m zinazohitajika kuiwekea barabara hii lami. Hizi dola milioni 27 ni gharama ya shilingi 400,000,000 kwa kilomita moja kuitia lami kutoka kwenye hali ya barabara ilivyo kwa sasa.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaweza kabisa kuchukua ule mrahaba wa hiari wa Barrick kwa miaka mitatu (dola milioni 21), kuwaomba Barrick watoe fedha ambazo zingetumika kwa ukarabati wa barabara hii kwa miaka 10 (dola milioni 1.5) na kuchukua sehemu ya mrahaba utokanao na mchanga wa dhahabu (dola milioni 5) na kuijenga barabara hii. Wananchi wamechoka kusimangwa na wenzao wa sehemu zingine za nchi kuwa wanatimuliwa vumbi tu na kuachiwa mashimo. Wanataka kusikia kauli ya Serikali kuhusu jambo hili, hasa kwa kuzingatia kuwa hata vyanzo vya mapato wamependekeza..

Mheshimiwa Spika, pili nizungumzie usafiri wa barabara kutoka Dodoma – Singida – Shinyanga - Mwanza. Pamoja na Serikali kutenga fedha za kuendelea na ujenzi wa hizi sehemu za Dodoma - Singida na Singida - Shelui, naikumbusha Serikali juu ya kuhakikisha kuwa barabara hii inakamilika mapema iwezekanavyo kwani tayari wananchi wa Mikoa ya Kagera, Shinyanga, Mara, Mwanza, Tabora, Kigoma, Rukwa na Singida wameumia sana kiuchumi kutokana na kutokuwepo kwa barabara ya lami niliyoitaja. Kwa sasa, nauli Dar es Salaam – Kahama (kilomita 900) ni shilingi 45,000 wakati nauli ya Dar es Salaam – Arusha (kilomita 800) ni shilingi 20,000 na Dar es Salaam – Mbeya (kilomita 1000) ni shilingi 25,000. Wananchi wa maeneo haya wanalipa

66 bei mara mbili ya wenzao wa Mbeya na Arusha kwa kuwa tu hakuna barabara ya lami Dodoma - Mwanza. Katika mazingira haya, watawezaje kushindana na wenzao katika maendeleo?

Mheshimiwa Spika, kuhusu usafiri wa Reli ya Kati umekuwa na matatizo kwa muda mrefu. Najua Serikali inajua athari za kijamii na kiuchumi kwa Taifa zinazotokana na ubovu wa Reli ya Kati, engine za treni na mabehewa. Kutokana na ubovu wa reli, bei ya bidhaa kama saruji, bati, sukari, ngano na kadhalika kwa Mikoa ya Magharibi ni juu, na hivyo umaskini utaendelea kukua., bei ya nauli ni juu, nalo linaathiri Marginal Propensity to Save (MPS) ya wananchi wa maeneo husika. MPS ndogo inasababisha Marginal Propensity to Invest (MPI) na bila saving in investment, umaskini hautaisha.

Mheshimiwa Spika, tunashindwa kupata pato litokanalo na kusafirisha shehena ya mizigo na abiria wa Burundi, DRC, Rwanda na Uganda hivyo kupoteza mapato, shehena ya mzigo mzito inaposafirishwa kwa barabara (Dar es Salaam – Dodoma) inasababisha uharibifu wa barabara. Hii ni hasara kwa Taifa, naiomba Serikali itupie macho usafiri wa Reli ya Kati.

Mheshimiwa Spika, kabla sijamaliza mchango wangu, naomba nitoe shukrani za kipekee kwa Naibu Waziri Mheshimiwa Dr. Maua Abeid Daftari na Kampuni ya simu ya Celtel kwa kuanza ujenzi wa minara katika vijiji vya Chela, Busangi, Ngaya na Bulige jimboni Msalala, wananchi wamefurahi sana. Hata hivyo, wanaichagisha kampuni hii imalizie ujenzi wa minara hiyo haraka kabla ya kipindi cha mvua kwani maeneo hayo hayana barabara nzuri hivyo inaweza kuwa tatizo mvua zikianza kunyesha.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naomba kusema naunga mkono hoja hii. Ahsante sana.

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia. Awali ya yote napenda kumshukuru Waziri wa Miundombinu pamoja na Naibu Mawaziri wote na watendaji wote wa Wizara kwa kuandaa hotuba hii.

Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza Msemaji wa Kambi ya Upinzani kwa hotuba yake.

Mheshimiwa Spika, miundombinu ni sawa sawa na moyo wa uchumi wa nchi, kwani pakiwepo na barabara zinazopitika wakati wote tutaimarisha soko la ndani kwa kutoa bidhaa sehemu fulani mpaka nyingine bila matatizo.

Mheshimiwa Spika, leo hii Rukwa ni kati ya mikoa mitano inayotoa mazao ya chakula kwa wingi nchini lakini utakuta wakati mwingine ni rahisi kununua chakula nje kuliko hapa nchini, mfano ni aghali kutoa mzigo wa mahindi kutoka Rukwa mpaka Kilimanjaro.

Mheshimiwa Spika, nashauri uimarishaji wa barabara uwe katika ngazi zote kuanzia vijijini mpaka barabara kuu.

67 Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa imetenga kwenye Bajeti fedha za ukarabati wa barabara hasa vijijini kupitia TAMISEMI lakini kwa ujumla matengenezo ya barabara hizi yamekuwa hafifu na imekuwa ni kama njia ya kupoteza pesa za mlipa kodi.

Mheshimiwa Spika, ningeshauri kama ilivyo TANROADS sheria hii iangaliwe kama barabara za vijijini ziwe chini ya TANROADS kwani ukarabati wa barabara za vijijini hauridhishi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu viingilio vya public area, Serikali ilipiga marufuku ulipaji wa kodi hizi na kuzitoa (kodi za kero). Lakini viwanja vya ndege Dar es Salaam, Ubungo Bus Terminal bado kuna malipo. Je, ni kwa jinsi gani haya malipo yamesaidia maeneo husika na haya makusanyo wanakusanya kwa sheria ipi na kama Serikali imebadilisha agizo lake kwa nini zisitumike risiti za Serikali na agizo hili lilibadilishwa lini?

Mheshimiwa Spik,a kuhusu Air Tanzania, nashukuru kwa Serikali kulirudisha Shirika la ATC mikononi mwake. Huu ubia wa ATC na SAA ulikuwa ni kati ya mikataba mibovu iliyofanywa nchini. Je, Tanzania (ATC) ilipata hasara gani kuingia ubia na South Africa(SAA)? Na waliohusika kwa mikataba hii mibovu ilikuwa ni wana taaluma ya sheria ama ilikuwa uzembe? Je, Serikali itawachukulia hatua gani wahusika na waliotufikisha hapa?

Mheshimiwa Spika, kuhusu Railways, nchi zote duniani usafiri wa reli ni rahisi kuliko usafiri wa aina nyingine zote. Reli yetu tangu ijengwe na wakoloni hatukuweza kujenga reli ya kupishana ili treni moja ikitoka Dar es Salaam - Kigoma nyingine itoke Kigoma - Dar es Salaam. Tumebaki na moja na sasa badala ya kuishia Dar es Salaam - Kigoma inaanzia Dodoma - Kigoma.

Mheshimiwa Spika, ninaelewa harakati za ubinafsishaji zinakamilika na fununu zilizopo mbia huyo ni Shirika la Reli la Serikali ya India. Je, ni nini kilipelekea hali ya reli kudorora na kufikia hali hii duni? Hivi kweli kulikuwa hakuna review report za kuangalia matatizo na kuyashughulikia kabla hatujafikia hali kama hii kwa Board of Directors?

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu ni kuwa Serikali iwe na utaratibu/utamaduni wa kuzuia kuliko kusubiri kitu kiharibike ndio tutengeneze. Hawa wote waliotufikishia Shirika hili mpaka hapa lazima wawajibishwe. Serikali ina mpango gani na watu hawa?

Mheshimiwa Spika, kuhusu utengenezaji wa magari ya Serikali, hainiingii akilini kwa sababu gani ya kuwa na wakala wa Serikali wa kutengeneza magari halafu unaona tena magari ya Serikali yanapelekwa kwenye Private Garage kutengenezwa? Huu siyo ufujaji wa fedha za Serikali?

Mheshimiwa Spika, Serikali iimarishe wakala wake (TEMESA) ili magari yote ya Serikali yatengenezwe katika karakana hizi. Naomba kuwasilisha.

68 MHE. DR. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Waziri wa Miundombinu, Mheshimiwa Andrew Chenge, kwa kuandaa hotuba nzuri pamoja na kukabiliwa na ufinyu wa Bajeti. Sambamba na Waziri, pia nawapongeza wasaidizi wake Naibu Mawaziri pamoja na Katibu Mkuu na watendaji wote.

Mheshimiwa Spika, Bajeti hii nashauri sana ijaribu kuzingatia maombi yangu yafuatayo:-

Kwanza ni kuhusu ukarabati wa barabara ya Lamadi - Sapiwi hadi Bariadi – Shinyanga, hii ni barabara muhimu na ni kiungo cha usafirishaji kwa wananchi wa Mikoa hii. Magari yanayotumika barabara hii ni mengi na kwamba barabara hii haimudu uzito wa magari yanayopita. Mfano pale Lamadi kuna kibao kinachoonyesha uzito usizidi tani 10 hadi magari yanayopita pale yana tani 30 - 40. Je, ni kwa vipi barabara hii inaweza kuhimili uzito huo? Nashauri pesa ya matengenezo iongezwe kukidhi haja ya mahitaji.

Mheshimiwa Spika, pili ni kuhusu barabara ya Nyashimo - Ngasamo - Dutwa. Hii ni barabara muhimu sana kwa kusafirishia mazao na wananchi. Naomba fedha ya kutosha itengwe ili matengenezo yaendane sambamba na ubora wa barabara kwani kiasi cha fedha kinachotolewa hakitoshi kabisa hata kujenga baadhi ya madaraja. Mfano pale Malili kuna daraja ambalo karibu linaanguka lakini hakuna jitihada zozote za kulitengeneza?

Tatu, ni kuhusu barabara za Jiji la Mwanza, kwa kuwa Mwanza ni Jiji ni vema ile ahadi ya Serikali ikatekelezwa ya kulisaidia Jiji kuboresha barabara za ndani ya Jiji kwa kiwango cha lami ili Jiji lifanane na sura halisi ya Jiji. Mfano barabara ya Makongoro - Isamilo - U-tunu, Pamba Road, Lumumba na Uhuru - Thaqafa - Isamilo. Nashauri sana Wizara itenge fedha kwa ajili ya kusaidia matengenezo ya barabara hizi muhimu kwa Mwanza.

Mheshimiwa Spika, nne ni kuhusu barabara ya Mwigumbi - Maswa - Bariadi - Lamadi, kuna haja ya kuharakisha matengenezo ya barabara hizi, kwani ahadi ya Serikali ni kuwa mwaka huu wa fedha inapaswa kuwa imeanza kutekelezwa. Kuhusu Mwanza Airport, ijengwe mapema! Mwisho, nashauri Wizara licha ya ufinyu wa Bajeti, ni muhimu ikaweka kipaumbele kuzingatia umuhimu wa mahitaji ya barabara na uchumi wa nchi bila kusahau kuwa barabara zote zenye link na Mikoa kama nilizozitaja zinapewa umuhimu. Pia mkakati wa kuboresha Jiji la Mwanza kufuatia ahadi ya Serikali unatekelezwa. Ahsante.

MHE. MOHAMED H. MISSANGA: Mheshimiwa Spika, nampongeza Waziri Mheshimiwa Andrew Chenge, pamoja na Naibu Mawaziri wote wawili. Aidha, nampongeza sana Katibu Mkuu Dr. Enos Bukuku na Naibu wake Ndugu Omar Chambo na watendaji wengine.

69 Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali na hasa Wizara ya Miundombinu kwa kufanikisha mazungumzo na wakandarasi ambayo yamewezesha ujenzi wa barabara ya Dodoma - Manyoni hadi Singida. Naomba mchakato wa kumpata mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa cha Isuna hadi Manyoni kilomita 55 uharakishwe na ateuliwe mkandarasi mwenye uzoefu na vifaa vya kutosha na atakiwe kuanza kazi haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali kwa kuhakikisha kuwa barabara ya Singida - Babati hadi Minjingu - Indaza kujengwa kwa kiwango cha lami kuanzia mwaka huu. Napenda kurudia kusisitiza kuwa barabara hii iwe na package tatu kwa maono ya wakandarasi watatu na kwamba mkandarasi mmoja aanzie Singida kwenda Babati

Mheshimiwa Spika, napongeza makampuni ya simu za mkononi kwa kutuwekea mtandao wa simu zao Singida Mjini na hata Vijijini. Nawashukuru sana Celtel na Mobitel kwa kutoa huduma za simu zao katika jimbo la Singida Kusini. Naomba Celtel iangalie uwezekano wa kuweka minara katika vijiji vya Mlandala, Mgungira ambako soko lipo.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

MHE. SAID A. ARFI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri na timu yake yote kwa kazi ya kupunguza matatizo yetu mengi, hususan miundombinu katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, kupitia kwako naomba kutoa maombi yafuatayo tusaidiwe pamoja na matatizo mengi na uhaba wa fedha kwa Wizara hii nilikuwa naomba kwanza kuongezwa kwa mabehewa daraja la tatu kwa reli iendayo Mpanda na hasa wakati huu wasafiri wanaongezeka baada ya kipindi cha mavuno. Aidha, kutopunguzwa mabehewa ya daraja la kwanza na pili kwa sababu ni moja kwa kila daraja unapoondoa behewa unaleta usumbufu mkubwa kwa wasafiri wa Mpanda. Ziada ya muda wa kuondoka Tabora kwenda Mpanda uzingatiwe kwa ufanisi na kupunguza malalamiko ya wananchi.

Mheshimiwa Spika, pili, naomba Wizara itume wataalamu wake wakakague ujenzi unaoendelea wa barabara ya Ipole – Koga - Mpanda. Nimebahatika kupita barabara hiyo wiki hii, wananchi wanahoji kinachofanyika sasa ni sahihi? Kupitisha greda katika maeneo ya mchanga na kutoshindilia kumeleta adha kubwa kwa watumiaji wa barabara hiyo na hata ile thamani ya pesa iliyowekezwa haionekani wananchi leo wanapoambiwa shilingi milioni 600 zimetumika matarajio yao ni kuona barabara hiyo inafanana na shilingi milioni 600 na si vinginevyo. Lipo tatizo la maji katika barabara hiyo lakini isiwe sababu ya kutokufikiwa kwa kiwango cha barabara kinachohitajika. Ufuatiliaji na ukaguzi wa kazi zote za barabara ni muhimu kuondoa malalamiko.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2006/2007 World Bank hawakutoa pesa kwa matengenezo ya barabara za Mwanza na Rukwa na matokeo yake barabara ya Mpanda/Sumbawanga ikafungika kupitika katika msimu wa mvua uliopita, sasa Bajeti hii ya mwaka 2007/2008 pia mategemeo fedha za World Bank kwa miradi ile ile ikiwemo

70 barabara ya Mpanda/Sumbawanga, naomba fedha zielekezwe kwenye barabara hiyo wakati huu kabla ya mvua kuanza iwapo fedha za World Bank zitachelewa barabara hiyo haitapitika, inahitaji matengenezo ya haraka.

MHE. ALOYCE B. KIMARO: Mheshimiwa Spika, nampongeza sana Waziri wa Miundombinu na timu yake kwa hotuba nzuri.

Mheshimiwa Spika, wakati wa Kampeni Mheshimiwa Rais aliahidi kwamba kwa kuwa lami aliyokuwa ameleta Mrema kwa ajili ya kutengeneza barabara ya Marangu Kilema imeharibika na kwa kuwa Mrema kama mpinzani alikuwa anadanganya atajenga hiyo barabara lakini uwezo alikuwa hana.

Mheshimiwa Spika, Rais Mheshimiwa Jakaya Kikwete aliahidi akiingia madarakani pamoja na Mbunge wake Aloyce Kimaro, barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami kutoka Marangu Mtoni kupitia Kilema Kirua Vunjo hadi kuungana na barabara kuu ya Himo Moshi. Hii ahadi wananchi wanaingojea sana ukijua jimbo hili lilikuwa la Upinzani. Mheshimiwa Waziri naomba utuokoe kwa kutoa ufafanuzi mzuri ili wapinzani wasitubeze.

Mheshimiwa Spika, la pili ujenzi wa bodi za mabasi hauna viwango. Basi likipata ajali linachanika na kuua watu wengi. Nashauri viwango viwekwe na mabasi yajaribiwe kabla ya kuingizwa barabarani.

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mtwara Vijijini (Mtwara – Mkoa) na wananchi wa Jimbo la Mtama (Lindi). Tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa Wizara ya Miundombinu kwa juhudi zake za kufanikisha shughuli za ujenzi wa barabara katika mikoa yetu kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Wizara ya Miundombinu kwa kutuwezesha kukarabati kwa kiasi barabara ya Mpapaura – Kitere - Makao.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2006/2007 tulimuomba Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu (mimi na Mbunge wa Mtama Mheshimiwa ) kututengea fedha kwa ajili ya ukarabati/ujenzi wa barabara ya Mpapura - Kitere - Makao, barabara hii inaunganisha Majimbo yetu mawili ya Mtama na Mtwara Vijijini katika Mikoa ya Mtwara na Lindi.

Mheshimiwa Spika, Waziri wa Miundombinu Mheshimiwa alimuandikia Mheshimiwa Waziri Mkuu kuwa ombi letu lilichelewa lakini aliahidi kuwa fedha kiasi cha shilingi 1,700,000,000/= zingetengwa kwenye Bajeti ya mwaka 2007/2008.

Mheshimiwa Spika, nashukuru kuwa kwa kutumia kiasi ambacho kilitengwa mwaka 2006/2007 sehemu ya barabara hii kwa upande wa Mtwara ilikarabatiwa.

71 Mheshimiwa Spika, napenda kupata maelezo toka kwa Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu kama kweli kiasi kilichoahidiwa kama kimetengwa kwenye Bajeti ya mwaka 2007/2008 kwa ajili ya kukamilisha kazi ambayo tayari imeanza na imeanza kuleta faraja na kama fedha hizo hazijatengwa, Mheshimiwa anieleweshe kwa kiasi gani fedha hizi zitapatikana ili tuweze kuunganishwa Majimbo ya Mtwara Vijijini na Mtama katika Mikoa ya Mtwara na Lindi.

MHE. DR. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Spika, napenda niwapongeze wote Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Spika, naomba muangalie tatizo la mawasiliano katika maeneo yafuatayo ya Jimbo la Hanang, Balang’dalalu, Gisambalang, Gehandu na vile vile eneo la jirani ya Jimbo la Mandi na Sabilo. Celtel, Tigo na Vodacom wote waombwe.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Manyara ni mkoa mpya, barabara zake hazijaunganisha Wilaya na Makao ya Mkoa, tafadhali angalieni. Tunaomba barabara zipandishwe daraja, orodha tayari tumeleta, ili ziwe za Mkoa.

MHE. OMAR YUSSUF MZEE: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa naunga mkono hoja asilimia mia moja. Pili, napongeza uongozi wote wa Wizara kwa kazi nzuri ya ujenzi wa miundombinu nchini kwetu.

Mheshimiwa Spika, naomba unisaidie kupata ufafanuzi katika mambo yafuatayo:

Kwanza Rais Mstaafu Mheshimiwa Benjamin Mkapa aliahidi kumaliza ujenzi wa barabara ya Amani - Mtoni, hadi sasa ni muda mrefu sasa barabara hiyo haijapata ufumbuzi na ni barabara ambayo inapitiwa na magari mengi.

Mheshimiwa Spika, pili, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema kuwa bandari ni suala la Muungano, je, Mheshimiwa Waziri kuna utaratibu gani wa kusaidia ujenzi wa bandari ya Zanzibar? Kwa maana ya kuipanua zaidi ili iweze kusaidiana na bandari ya Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, wahalifu wanatumia zaidi simu za mikononi kwa mawasiliano yanayopelekea kufanya uhalifu kwa ufanisi zaidi. Hali hii inatokana na kuwa sim card zinauzwa kwa bei poa shilingi 500/= na hakuna usajili wa wale wenye kutumia namba hizo. Je. Serikali lini itaanza utaratibu wa kuorodhesha namba zote za simu za mikononi pamoja na kuziuza sim card kwa bei ya juu angalau shilingi 10,000/= kama wanavyofanya nchi ya UAE, Uingereza na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, kwa sehemu kubwa tunaweza kupunguza kero za Muungano, kama vyombo vya Muungano vitaonyesha sura ya Muungano.

Mheshimiwa Spika, je, Bodi ya ATCL inaonyesha sura ya Muungano? Sisi wenzenu huwa tunapata wakati mgumu kama hatuyasemei masuala kama haya. Tunaomba sana.

72 Mheshimiwa Spika, mwisho, nashukuru sana kwa uongozi mzuri wa Wizara. Mungu ibariki Wizara ya Miundombinu na viongozi wake.

MHE. MARIA I. HEWA: Mheshimiwa Spika, kwanza niipongeze Wizara kwa kazi nzuri inazofanya hasa upande wa Miundombinu (barabara) karibu nchi nzima ikiwemo ahadi ya kukamilisha barabara ziungazo mikoa mwaka 2010. Hoja yangu ni lini kwa kutaja mwaka kivuko cha Busige - Kigongo kitakamilika? Ilikuwa kiwe tayari Machi, 2007 hadi leo bado wakaahidi Juni, 2007 bado hadi sasa.

Je, hatuoni kuwa huu ni uvivu na uongo wa kisirisiri, kiuwajibikaji? Je, Serikali inasemaje katika hili? Kwa nini Serikali isiwe wazi kama ucheleweshwaji huu unasababishwa na malipo/fedha kutopewa ili waikamilishe kazi hii?

Mheshimiwa Spika, nilipongeze Shirika hili kwa kuwa na nia ya kujitegemea tofauti na wakati wa nyuma. Lakini ninahoja zifuatazo:-

Kwanza hofu yangu ni rushwa, kumeanza kujitokeza ndani ya watumishi na hasa wa ngazi za kati kutokuwa wazi na nafasi kwa wasajili kuambiwa nafasi zimekwisha hasa upande wa daraja la kawaida (Economic) ili baadae wazirushe tiketi kwenda daraja la kwanza (VIP) kwa wanaofukuzia nafasi (wacheleweshaji). Katika kufanya hivyo tutawakimbiza wateja.

Pili, kutokujali muda kazini, hii nina ushahidi ambapo mimi mwenyewe nilitaka kuachwa na ndege asubuhi nikimsubiri mtumishi anipe tiketi saa 11.00 asubuhi badala yake akaja saa 12.15 asubuhi na ndege inaondoka saa 12.30. Tutaliua Shirika kwa muundo huo. Kuhusu usafiri na uchukuzi katika maziwa, pamoja na ongezeko la wasafiri katika maziwa tuliyonayo, pia wasajili wengi wamepoteza maisha yao aidha kwa kukosa elimu ya kujiokoa wakati ajali itakapotokea majini hata kama boya liko mbele yake, hajui jinsi ya kulitumia, ni kweli kwamba meli au boti nyingi zinayo maboya, lakini hayatoshi kwa kila msajili aliyemo katika vyombo wanavyosafiria humu majini pindi ajali itakapotokea. Nashauri kila chombo majini kiendane na maboya kwa idadi ya wasafiri.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ujenzi wa uwanja wa ndege Mwanza, kwanza niipongeze Wizara kwa maamuzi ya kuupanua uwanja wa ndege Mwanza. Ila unajengwa pole pole mno, je, ukikamilika utakuwa tayari kupewa heshima kama viwanja vya J. K. Nyerere au Kilimanjaro International Airport? Tafadhali naomba jibu. Nashauri mkandarasi aongeze speed ya ujenzi.

MHE. ELIZABETH N. BATENGA: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu pamaoja na Naibu Mawaziri wake kwa hotuba nzuri sana iliyosomwa mbele ya Bunge lako Tukufu. Aidha, niwapongeze watendaji wote wa Wizara kwa maandalizi yote waliyofanya.

73 Mheshimiwa Spika, naomba kuiuliza Serikali, ni lini hasa itaona umuhimu wa kuutengeneza uwanja wa ndege wa Bukoba ili ndege kubwa ziweze kutua lakini pia ikizingatiwa kwamba eneo la Bukoba lina mvua nyingi hivyo mara nyingi uwanja huo hujaa maji. Usafiri wa ndege ni muhimu sana kwa ajili ya wafanyabiashara wanaoinukia, watumishi wa Serikali na wananchi wengine wenye uwezo hivyo uwanja imara (ujengwe kwa lami) ni muhimu sana. Tunapongeza kufufuliwa Shirika letu la Ndege la ATC. Ningeshauri ATC ifikirie kuwa na ndege ndogo ya kuunganisha wasafiri wanaosafiri toka Dar es Salaam - Mwanza - Bukoba kwa ATC.

Mheshimiwa Spika, kuhusu usafiri ndani ya Ziwa Victoria, naiomba Wizara pamoja na kuzidi kuifanyia matengenezo muhimu meli MV Victoria ifanye kila linalowezekana kupata wawekezaji wa usafiri katika Ziwa Victoria. Usafiri wa meli ndio usafiri rahisi na mwepesi kwa wakazi wa Mkoa Kagera kwa ajili ya watu, bidhaa toka mashambani kwenda kwa walaji na pia bidhaa za viwanda kwa ajili ya wananchi. Kuhusu barabara ya lami ya Kagoma - Rusahunga ujenzi wake unasuasua sana. Mkandarasi aliyepewa kazi hiyo speed yake haieleweki kwa kuangalia kwa macho hakuna chochote kilichofanyika. Kwa hiyo, naomba afuatiliwe kwa karibu. Sisi tungependa kuona kazi inakwenda kasi. Kukamilika kwa barabara hiyo ni ukombozi kwa wana Kagera na Watanzania kwa jumla. Naunga mkono hoja.

MHE. MANJU S. O. MSAMBYA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nachukua fursa hii kuunga mkono hoja. Nitaelekeza mchango wangu katika kuihoji na kuishauri Serikali kwa kutazama maeneo mahsusi kwa utaratibu ufuatao:-

Kuhusu SUMATRA na usalama Ziwa Tanganyika, wakati nikichangia hotuba ya Waziri Mkuu nilitoa ombi kwa Serikali kuangalia uwezekano wa kulegeza masharti ya usalama kwa vyombo vya usafiri Ziwa Tanganyika. Ni kweli wasafiri katika mitumbwi, mashua na majahazi (maboti) wanatakiwa wapatiwe maboya kwa ajili ya usalama na kujiokoa inapotokea ajali ya boti ama kuzama au kupinduka ama kwa tufani au dharuba ya upepo. Vifaa hivi vinatakiwa vitolewe na mtumie chombo cha usafiri. Ni bahati mbaya kuwa vifaa hivi vinatozwa kodi kubwa kiasi kwamba wamiliki wa maboti/mashua wanashindwa kumudu gharama zake.

Mheshimiwa Spika, duniani kote vifaa vya kuokoa maisha huwa havitozwi kodi. Sheria ya Income Tax ya mwaka 1973 ilitamka wazi kutotoza kodi vifaa vya uokoaji. Lakini sheria hiyo iliporekebishwa mwaka 2004 ilikaa kimya kuhusu kutoza/kutotoza ushuru vifaa vya uokoaji, hali iliyofanya TRA watoze ushuru maboya ya uokoaji majini. Sasa hivi boya linalotakiwa kuuzwa kwa shilingi 15,000/= vinauzwa shilingi 65,000/= kama nilivyojulishwa na Mkuu wa Chuo cha Ubaharia wakati nilipowatembelea mwisho wa juma lililopita.

Mheshimiwa Spika, ushauri ni kuwa ni vyema Waziri wa Miundombinu na Waziri wa Fedha wakutane ili upatikane ufumbuzi wa haraka kwa lengo la kusaidia kuokoa maisha ya wasafiri katika Ziwa Tanganyika na Maziwa mengine. Ikibidi sheria ifanyiwe marekebisho under certificate of urgency.

74 Mheshimiwa Spika, kuhusu huduma za simu na simu za mkononi, naipongeza Wizara kwa juhudi zinazofanywa kuwezesha mawasiliano ya simu yasambae nchi nzima. Hata hivyo ni vyema Serikali ikaangalia kupeleka simu tangu za TTCL hadi zile za mkononi mwambao wa Ziwa Tanganyika, Kusini mwa Mkoa wa Kigoma. Maeneo haya kwanza yana biashara kubwa na pia yanahitaji mawasiliano ya simu kwa sababu za kiusalama.

Mheshimiwa Spika, kadhalika naiomba Wizara itazame Kigoma Kaskazini, mwambao wa Ziwa Tanganyika ambapo wanatumia mitambo ya Voda Burundi kwa kubahatisha tu. Wanapata mawasiliano kwa taabu na ni yale maeneo yaliyo mpakani na Burundi.

Ushauri, Celtel wameweka mnara eneo la Ngumba jimbo la Kigoma Kusini, lakini haujazinduliwa fungu limejengwa na hivyo kutofanya kazi na kuwanyima wananchi mawasiliano. Nashauri Wizara ipeleke huduma hiyo kwa kuzindua mnara huo.

Kuhusu vivuko na madaraja, wakati nikichangia hoja ya Waziri Mkuu nilihoji kutoshughulikiwa Kivuko Ilagala, Mto Malagarasi (Kijiji cha Ilagala) kwenye barabara ya Ilagala - Kalija (Kusini mwa Ziwa Tanganyika). Kimkoa kivuko hiki kilipelekwa kikiwa kibovu toka Rufiji na kimekuwa hakitoi huduma vizuri. Kinakuwa kizima wiki moja lakini kibovu kwa zaidi ya mwezi mara kwa mara. Nashauri, ama tupatiwe kivuko kipya na kikubwa au tujengewe daraja. Bajeti imezungumzia vivuko maeneo mengi ya nchi lakini hiki hakikutajwa. Pia watumishi wa kivuko hasa kiongozi wao anabidi achunguzwe kwani hana lugha safi kwa wavukaji na watumiaji wa kivuko. Mara nyingi anakaripia watu na kutoza nauli kwa stakabadhi za madatfari. Pia anatoza mafuta sio chini ya lita 20 ambapo ni kinyume cha sheria.

Kuhusu barabara ya Kigoma/Tabora/Itigi/Manyoni, barabara hii ni muhimu kwa uchumi wa nchi. Barabara inahitaji daraja. Hotuba inaonyesha shilingi milioni 200 tu kwa ajili ya daraja. Sielewi pesa hizi ni za kazi ipi? Ningeomba wakati wa majumuisho atuonyesha na kutufafanuliwa ni namna gani pesa hizi zitatumika kuwezesha kutengeneza daraja. Barabara ya Kigoma – Tabora – Itigi - Manyoni imekuwa haipewi umuhimi inayostahili japo Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete anaipa umuhimu. Nitaomba Mheshimiwa Waziri atapokuwa anajumuisha atueleze ni mikakati gani aliyonayo kwa barabara hii.

Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Ilagala – Kalya, barabara hii inaufungua Mkoa wa Kigoma, Kusini mwa Ziwa Tanganyika. Inasikitisha kusema kuwa juhudi za wananchi hazikupewa hadhi inayostahili kwani wametumia nguvu zao kung’oa visiki. Lakini pesa zilizotolewa ni kiduchu, shilingi milioni 950 tu. Waziri atueleze atatusaidia vipi kukamilisha barabara hii kwa wakati muafaka ili ituletee maendeleo. Ataenzi vipi nguvu za wananchi ambazo wamezitoa tayari. Eneo la Kigoma Kusini mwambao wa Ziwa Tanganyika ni eneo muhimu la uzalishaji wa kilimo. Shughulikia barabara hii.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Shirika la reli Tanzania (TRC), naomba Wizara ijitahidi kukamilisha ukodishaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC). Wasafiri na mzigo

75 wanapata matatizo. Utaratibu wa treni kuanzia na kuishia Dodoma unaleta adha na kudumaza maendeleo ya watumiaji na huduma hiyo. Gharama za maisha zinapanda kutokana na bidhaa kama saruji/sukari/nishati ya mafuta na kadhalika kuuzwa bei ghali kutokana na huduma hafifu za shirika hili.

Kuhusu meli ziendazo kasikatika Ziwa Tanganyika, mwaka 2004 kutokana na mgongano kati ya Waziri wa Ujenzi (sio Wizara) na Waziri wa Mawasiliano (sio Wizara) mradi wa meli ziendazo kasi na meli za uchukuzi Ziwa Tanganyika ulikosekana. Mradi huu ambao ungegharimu dola milioni 30 na ambao ungetoa ajira 700 ulipigwa danadana. Mradi ulikuwa uwe kama ifuatavyo:- boti za kasi Ziwa Tanganyika (boti 4), boti au meli za mizigo nne na meli (Tanker) mbili za mafuta.

Mheshimiwa Spika, vyombo hivi vingeweza kufanya kazi kati ya Kigomliya, Kalemi, Baraka, Uvira/Miba (DRC) na Bujumbura (Burundi) hali ambayo ingeweza kupatia nchi yetu 30% ya mapato ambayo yangeweza kupatikana toka kwa mwekezaji, Waswahili husema: “Mafahari wawili wanapogombana, zinaumia nyasi.” Naiomba Wizara itazame upya hoja ya boti hizi kuruhusiwa ili zisaidie kutoa huduma na kukuza uchumi.

Mwisho naiomba Wizara izingatie yale niliyoyaainisha hapo juu. Kadhalika naomba Ofisi yako inipatie ufafanuzi kwa yale niliyoomba kupatiwa ufafanuzi tu. Namalizia tena kutamka kuwa naunga mkono hoja. Ahsante.

MHE. MUSSA AZZAN ZUNGU: Mheshimiwa Spika, naomba nipate maelezo juu ya ombi letu la Bodi ya TANROADS ya Mkoa wa Dar es Salaam kuhusu Serikali kuichukua na kuitengeneza kwa kiwango cha lami barabara ya Uhuru, Mkoa wa Dar es Salaam. Barabara hii ina mchango mkubwa kwa maendeleo ya mkoa wetu na ndio inayochukua viongozi wa Kitaifa na Mataifa pamoja na kuweka taa za barabarani.

Mheshimiwa Spika, TANROADS ina jukumu kubwa ya kuwasha taa barabarani lakini mpaka sasa hatujaona. Serikali ina mpango gain? Serikali sasa itachukua hatua zipi za uhakika kuhakikisha Shirika la Ndege la ATC kutoingia tena na mikataba mibovu?

MHE. DR. FESTUS B. LIMBU: Mheshimiwa Spika, naipongeza Wizara kwa kuwa na asilimia ndogo sana (0.20%) chini ya kifungu 261100: “Other goods and services not classified.” Ni ndogo nafikiri kuliko Wizara zote. Hii inaonyesha umakini wa kupanga mipango. Hongera sana.

Pili, interconnectivity baina ya Jimbo na Jimbo, Wilaya na Wilaya ni muhimu sana. Interconnectivity baina ya Wilaya ya Magu – Bariadi - Kwimba na Maswa haipo. Pia daraja la Simiyo kati ya Vijiji vya Kabila (Wilaya ya Magu) na Maligisu (Wilaya ya Kwimba) limetengewe shilingi milioni 50 kwa ajili ya upembuzi yakinifu Bajeti hii (toka kwenye saving ya fedha za World Bank za barabara ya Magu – Ngudu) kama alivyozungumza Mheshimiwa Richard Ndassa kwa ajili ya kutengewa fedha mwaka ujao.

76 Mheshimiwa Spika, barabara ya Bariadi iunganishwe na Magu kupitia ama Kasoli - Bugatu - Ng’haya au Mwamlapa – Salama – Sayaka - Kisamba. Hizi ni njia za mkato kabisa zinaunganisha Wilaya hizi mbili. Barabara nyingine ya mkato ni Mahaha (Magu) kwenda Lugulu.

Tatu, ni kuhusu msongamano wa magari Dar es Salaam. Dar es Salaam inalipa kodi karibu asilimia 75 ya kodi yote inayolipwa nchi nzima. Ukizibua msongamano wa magari Dar es Salaam unazibua misongamano mingi sana nchi nzima. Wizara ya Miundombinu iyafikirie mawazo yaliyotolewa kwenye ukurasa wa kwanza wa Gazeti la the Guardian toka UCLAS ya kuzibua msongamano wa magari Dar es Salaam kwa kuweka flyover kwenye junction za Dar es Salaam. Ni muhimu sana hili kufanyika haraka.

Nne, kuhusu PPP ushiriki wa sekta binafsi kwenye miundombinu nchini, it is high time Wizara inashirikisha sekta binafsi kuendeleza/kujenga miundombinu nchini. Utaratibu uliotumika kujenga daraja la Kigamboni uigwe maeneo mengine; viwanja vya Ndege na kadhalika. Kanuni na miongozo iliyotajwa na Waziri ikamilishwe haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Spika, tano, napongeza shilingi bilioni 13.7 kutengwa kwa Rail rehabilitation; shilingi bilioni 19.7 kwa ajili ya reli ya Dar es Salaam – Dodoma na shilingi bilioni 12.2 kwa ajili ya reli ya Singida - Manyoni.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.

MHE. DR. CHARLES O. MLINGWA: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri, Waheshimiwa Naibu Mawaziri , Katibu Mkuu na safu nzima ya watendaji kwa kazi nzuri wanazozifanya kuhusu maendeleo ya miundombinu nchini. Hongereni sana na nawatakia kila la kheri.

Mheshimiwa Spika, hususan nawapongeza kwa mipango ya Wizara kuhusu ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Shinyanga (Ibadakuli) na ujenzi wa barabara ya lami kilomita 10 kati ya Shinyanga Mjini na Old Shinyanga.

Mheshimiwa Spika, kuhusu vituo vya kunasa matangazo ya televisheni na redio, naomba Wizara ishawishi Kampuni/Taasisi za Televisheni zijenge/ziweke booster stations Shinyanga ili kuboresha huduma za habari kupitia Televisheni Mkoani. Kilima cha Busanda kinafaa sana kuweka boosters. Pia Redio Tanzania nayo iboreshe mitambo yake ya kusambaza habari, pengine nayo kwa kuweka booster station mkoani Shinyanga.

MHE. STEPHEN J. GALINOMA: Mheshimiwa Spika, kwanza, nampongeza Waziri, Naibu Mawaziri wake na Katibu Mkuu kwa hotuba nzuri yenye kina na ufasaha mkubwa.

77 Pili, napongeza kwa dhati kabisa uamuzi wa kutenga fedha kwa ajili ya barabara yangu ya lami ya Iringa kuja Dodoma. Nafurahi mno kwa hatua hii, hasa nikizingatia faida za kiuchumi na kijamii ambazo zitatokana na mradi huo. Kubwa sana ni utekelezaji. Natumaini kwamba Wizara itafanya kweli. Tatu, napendekeza kwa nguvu zangu zote kwamba Kiwanja cha Ndege cha Nduli - Iringa kitumike kikamilifu, hakitumiki ipasavyo ingawa hakina tatizo linalofahamika. Huko nyuma kilikuwa kinatumika zaidi kwa abiria lakini kingeweza kutumika hata kwa mizigo nyepesi. Ndege za Dakota Friendship na ndogo ndogo ziliweza kutua na kukaa bila matatizo. Nashauri Iringa iunganishwe na flights toka Mtwara, Songea, Mbeya, Dodoma na Dar es Salaam. Najua itadaiwa kwamba abiria ni wachache. Ndiyo ni kweli kwa sababu wanajua kuwa hakuna ndege. Nina hakika ndege zikipangwa watajitokeza kutumia huduma hizo. Isitoshe, si kweli kwamba huduma hiyo hufuata watu, ni kinyume chake. ATC mpya na Precision Air waombwe kutekeleza pendekezo hilo.

Nne, miaka ya 1990 Serikali ilikuwa na sera ya kuanzisha na kukuza Southern Tourist Circuit lakini imegota kwa sababu ya miundombinu duni. Destination ni Ruaha National Park ukiacha vivutio chungu mzima vya utalii bila kuacha uwezekano wa kuunganisha Mikumi National Park na Selous Game Reserve na Udzungwa National Park.

Mheshimiwa Spika, nashauri Wizara ianze kufikiria uwezekano wa kuanza kujenga miundombinu yake hasa barabara ya kutoka Kalenga kwangu kwenda Msembe (Ruaha National Park) na Kiwanja cha Ndege ambacho kiko huko na kingeweza kuwa springboard ya Southern Tourist Circuit.

Tano, naomba makampuni ya simu za mikononi yaombwe kujenga mnara/minara Mahoga katika Tarafa ya Kifunzelo.

Mheshimiwa Spika, mwisho naunga mkono hoja hii moja kwa moja. Sitachangia kwa kusema, hivyo, ukiweza nitakushukuru kama utayatolea kauli hapa siyo hoja zote ili wananchi wangu wasikie.

MHE. CYNTHIA H. NGOYE: Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza sana Waziri Mheshimiwa Andrew Chenge, kwa hotuba nzuri ya Wizara yake na kwa kazi nzuri wanayofanya katika Wizara.

Mheshimiwa Spika, Ukanda wa Maendeleo wa Mtwara, kuhusu Kiwanja cha Ndege cha Songwe, pongezi kwa hatua iliyofikiwa, lakini kazi inakwenda pole pole sana. Tunaomba kufahamu ni kazi zipi zimekwamisha utekelezaji? Kwa kuwa Kanda hizi zilianzishwa ili kuhamasisha uwekezaji katika Mikoa husika, wawekezaji wengi katika sekta za kilimo, madini na kadhalika, nashauri mradi huo sasa upewe kipaumbele.

Mheshimiwa Spika, kuhusu usafiri kuzunguka Ziwa Nyasa, kwa kuwa private sector hawataki kuwekeza katika Ziwa Nyasa, wakati umefika sasa Serikali yenyewe

78 iamue kununua meli kubwa kukidhi usafiri kwa vijiji vyote vilivyopo kando kando ya Ziwa vya Wilaya za Kyela, Ludewa na Mbinga.

Kuhusu mawasiliano ya simu za TTCL na mashirika mengine ya simu za mikononi. Katika maeneo hayo hasa yaliyopo Wilaya ya Ludewa, hakuna mawasiliano ya aina yoyote, simu wala barabara. Tunaomba Serikali itembelee kwanza maeneo hayo ione ni namna gani itayasaidia na hasa kwa usafiri na mawasiliano ya simu.

Mheshimiwa Spika, kuhusu matumizi ya matuta makubwa katika barabara kuu, nashauri suala hili liangaliwe vizuri, kwani matuta mengi yanachangia katika ajali au uharibifu wa magari. Ni vyema njia inayotumika kujenga matuta itumike kwa mafunzo ya madereva ili wadhibiti mwendo wa magari wanayoendesha. Madereva wa Tanzania waanze kujifunza uendeshaji unaoafuta alama rasmi za barabarani kama wanavyofanya wenzao katika nchi zinazoendelea na zilizoendelea.

Mheshimiwa Spika, namtakia Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu utekelezaji mzuri wa kazi zake katika mwaka 2007/2008.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja ya Wizara hii kwa asilimia mia moja.

MHE. JAMES D. LEMBELI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote ninaunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Lakini pia kwa vile sina mambo mengi ya kuchangia niipongeze Wizara kwa hotuba nzuri ambayo kwa kweli imeandikwa kukidhi mahitaji ya nchi yetu kwa maendeleo yake.

Mheshimiwa Spika, nampongeza Waziri Mheshimiwa Andrew Chenge, kwa kazi na hotuba nzuri ambayo imewapa Watanzania walio wengi hata wale ambao walikwishakata tamaa. Nawapongeza pia Naibu Mawaziri kwa kazi nzuri ya kumsaidia Waziri kazi ambayo wanaimudu kikweli kweli na ndiyo maana Mheshimiwa Andrew Chenge, anafanya kazi nzuri.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu kwa hoja hii ni barabara ya kati inayounganisha Dar es Salaam na Mikoa ya Magharibi ya Shinyanga, Mwanza, Kagera, Mara na Singida kupitia Dodoma.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa maelezo yaliyopo katika ukurasa wa 30 (Mradi Maalumu wa Ujenzi wa Barabara Kuu) maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Dodoma - Manyoni, Manyoni - Singida na Singida - Shelui sioni taarifa ya kipande cha Singida - Shelui. Je, kipande hiki cha barabara kimesahaulika au kuna tatizo gani. Katika kitabu cha Bajeti cha maendeleo kipande hiki cha barabara kimetengewa shilingi 19,692,000,000. Je, ni kwa nini katika hotuba yake Waziri hakutaja maendeleo ya ujenzi wake akionyesha pia lini mradi huo (Singida-Shelui ) utakamilika?

Mheshimiwa Spika, tatizo langu ni kwamba kipande hiki cha barabara hakitamalizika sambamba na hizo barabara nyingine za Dodoma – Manyoni - Singida tatizo litaendelea kubaki pale pale.

79 MHE. PHILIP S. MARMO: Mheshimiwa Spika, kwanza barabara ya Mbuyu wa Jerumani –Mbulu kilomita 47. Barabara hii ni muhimu sana kwa wananchi wa Mbulu, inapunguza umbali kwenda Makao Makuu ya Mkoa (Babati) kwa kilomita 70; na kwenda Arusha ambapo wananchi hupata huduma zote kwa kilomita 80. Ombi langu ni kuwa barabara hii kufikiriwa kuwekewa lami laini (otter seal) kwa kuanzia maeneo korofi sana ya Rift Wall kilomita 27.

Pili, barabara ya Mto Sibiti (Shinyanga/Singida border) hadi Haydom na Mbulu ni barabara muhimu sana kwa wananchi wa Wilaya ya Mbulu, Hanang, Babati, Iramba Meatu, Maswa na Kishapu, Mameneja wa TANROADS wa Mikoa ya Singida, Manyara na Shinyanga wafanye tathmini ya traffic ya barabara hii wakati huu wa kiangazi. Magari mengi ya abiria na mizigo yanayotumia barabara hii sasa itabidi wasimamishe shughuli nyakati za masika. Tathmini hiyo itasaidia katika kuimarisha barabara hiyo kuanzia mwaka huu wa fedha.

MHE. PROF. PHILEMON M. SARUNGI: Mheshimiwa Spika, napenda kutamka kuwa ninaunga mkono hoja ya Waziri wa Miundombinu. Naomba nichangie hotuba ya Waziri katika eneo la matengenezo ya barabara za Mikoa kama ifuatavyo:-

Napongeza Wizara kwa kazi nzuri kuhusu matengenezo ya barabara za Mkoa- Wilaya ya Rorya. Barabara kutoka Rika hadi Rusi Port Sota yenye urefu wa kilomita 50 matengenezo yalianza mwaka 2002 baada ya kupandishwa daraja kuwa barabara ya Mkoa. Mwaka 2002 barabara hii iliingizwa chini ya mpango wa majaribio ya barabara tano ambazo zingetengenezwa kwa kutumia otter seal. Kwa kuwa sera ya Serikali ni kutengeneza barabara zinazounganisha Makao Makuu ya Mkoa na Wilaya na barabara zinazounganisha nchi yetu na nchi jirani kwa lami.

Mheshimiwa Spika, naomba Mheshimiwa Waziri na wasaidizi wake barabara hii sasa iingizwe chini ya mpango wa matengenezo kwa kutumia otter seal. Hivi sasa Jimbo la Rorya sasa limekuwa Wilaya, hivyo barabara hii ambayo ndiyo barabara kuu inastahili kuwekewa lami.

MHE. JANETH M. MASSABURI: Mheshimiwa Spika, naomba nimpongeze Waziri wa Miundombinu, Naibu Mawaziri na watendaji wote wa Wizara hii kwa hotuba nzuri yenye kuleta matumaini. Pamoja na pongezi hizo naomba nipendekeze yafuatayo:-

Moja, kuhusu huduma ya kivuko cha Kigamboni, Serikali ingeruhusu makampuni binafsi yenye uwezo wa kutoa huduma katika kivuko cha Kigamboni na kwingineko hapa nchini. Hatua hiyo itasaidia Serikali kupunguza matatizo ya usafiri wa majini.

Mheshimiwa Spika, naomba Waziri atakapotoa majumuisho atueleze ni sababu gani zinazochelewesha kutoa maamuzi wa kuruhusu sekta binafsi kutoa huduma za usafiri wa majini?

80 Mheshimiwa Spika, pili, kuhusu TANROADS Dar es Salaam. Naomba TANROADS Mkoa wa Dar es Salaam waende site kukagua miradi ili kuzuia malalamiko ya mara kwa mara. Waige mfano wa Mheshimiwa Rais wetu na Mheshimiwa Waziri Mkuu wanavyokagua miradi na kuhakikisha inakamilika kwa kipindi kilichopangwa.

Tatu, Bodi yaWakandarasi, naiomba Serikali ipatie uwezo wa Bodi ya Wakandarasi ili waweze kusaidiana na TANROADS katika kuboresha miundombinu ya barabara, majengo na kadhalika. Nne, ni kuhusu barabara ya Uhuru (Ilala). Naiomba Serikali ipandishe hadhi barabara ya Uhuru ili iweze kuhudumiwa na TANROADS. Hii inatokana na uwezo wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kuwa mdogo. Lakini pia barabara hii ni njia muhimu sana ambayo viongozi mashuhuri duniani hupitishwa katika barabara hiyo. Kwa sababu hizo tunaiomba Serikali itoe tamko kuhusu barabara ya Uhuru.

Mheshimiwa Spika, mwisho nawaomba TANROADS Mkoani Dar es Salaam wawe wepesi kukagua maeneo mbalimbali kwa mfano, barabara, taa za barabarani, wasingoje vyombo vya habari vinawakumbusha na kikubwa zaidi TANROADS iwe makini kuteua Wakandarasi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.

MHE. GIDEON A. CHEYO: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Mheshimiwa Andrew Chenge, Waziri wa Miundombinu, kwa hotuba yake nzuri na kwa kuiongoza Wizara yake tangu alipoteuliwa, nawapongeza Waheshimiwa Naibu Mawaziri wote wawili, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara kwa mchango wao mkubwa katika kuimarisha na kuboresha miundombinu nchini.

Mheshimiwa Spika, naomba nianze kuchangia eneo la barabara. Kwanza, napenda kuipongeza TANROADS Mkoani Mbeya kwa jitihada zake za kutengeneza barabara kadri ya uwezo wao. Kutokana na mvua nyingi za msimu uliopita, barabara nyingi zimeharibika sana. Kwa hiyo, naomba TANROADS Mkoani Mbeya iendelee kufanya tathmini ya kina kuhusu uharibifu wa barabara na madaraja uliotokea na kuchukua hatua za haraka kufanya matengenezo ili barabara hizo ziweze kupitika kwa wakati wote. Kwa msingi huo naomba TANROADS iendelee kufanya matengenezo katika barabara zilizo chini yake Wilaya ya Ileje, nazo ni Mpemba - Isoko, Isongole - Shigamba, Luswisi - Ibungu, Ndembo – Kasumulu na Shigamba - Ibaba.

Mheshimiwa Spika, naishukuru Wizara kwa matengenezo ya barabara kwa kiwango cha lami katika Mji Mkuu wa Wilaya Itumba. Kwa kuwa Mji Mkuu wa Wilaya ya Itumba umeunganika kimpango Mji (Master Plan) wa miaka ishirini (1996-2016) na Mji mdogo wa Isongole, naomba mradi wa matengenezo ya barabara kwa kiwango cha lami uunganishe Itumba na Isongole.

Mheshimiwa Spika, naomba nirudie ombi langu la mwaka jana kuhusu barabara ya kutoka Mpemba (Mbozi) hadi Isongole(Ileje). Ombi letu ni kuipandisha hadhi

81 barabara hiyo kuwa ya Kitaifa (Trunk Road) na ijengwe kwa kiwango cha lami. Barabara hiyo inaunganisha nchi yetu Tanzania na nchi jirani ya Malawi. Ombi limepitia hatua zote pamoja na Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Mbeya. Tunachoomba ni kauli ya Serikali kukubali ombi hilo, hata kama kazi haiwezi kuanza sasa hivi. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri na Naibu Mawaziri wote wawili hawajafika Ileje, naomba kutumia nafasi hii kuwakaribisha kutembelea Wilaya yetu mwaka huu, ikiwezekana mwezi Septemba, 2007. Njoo muone hali halisi .

Mheshimiwa Spika, nazishukuru kampuni za Celtel na Tigo kwa huduma zao za simu za mkononi. Naomba waendelee kueneza huduma zao Wilaya nzima. Natoa wito kwa kampuni ya Vodacom nayo ilete huduma zake Ileje.

Mheshimiwa Spika, baada ya mchango huo mdogo, napenda kutamka kwamba naunga mkono hoja na nawatakia mafanikio mema.

MHE. OMARI S. KWAANGW’: Mheshimiwa Spika, moja, barabara ya Minjingu - Babati - Singida Namba 4183, nimeona kwenye programme ya mwaka 2007/2008. Nashukuru. Pamoja na hayo ni vema kama tutajua mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, lini hasa mradi unatazamiwa utaanza? Je, mradi utajengwa wote au hatua kwa hatua (phases) kati ya Minjingu – Babati - Singida na kama phases zitaanza kwa mara moja au moja moja na ni lini mradi huu au phases zake zitakamilika?

Mheshimiwa Spika, ratiba hii ni muhimu ili wananchi waendelee kuwa na imani na utekelezaji wa kazi za Serikali.

Pili, Babati - Dodoma Road namba 4196, barabara hii imetengewa fedha ambayo haionyeshi kuwa kuna kazi itakayofanyika, shilingi milioni 30 kama ilivyoonyeshwa ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa mwaka huu 2007/2008. Fedha za kazi hii zimetengwa kwenye kifungu kipi cha fedha katika kitabu cha Vol. IV-? Naomba kufahamu. Tatu, Project under Road Fund Financing, Manyara katika barabara ya Babati Orkesment/Kibaya new access road kilomita 250. Barabara hii imepangiwa fedha za rehabilitation pamoja na kutengewa fedha. Ningependa kufahamu kama katika fungu la rehabilitation kuna fungu la routine maintenance kwa lile eneo la Singe – Gallapo - Gedman ambalo ndilo lililoanza wakati mradi unaanza kwamba zipo sehemu ambazo zimeharibika kutokana na mvua. Ushauri wangu ni kuwa sehemu hiyo ipate fedha za maintenance ili isiendelee kuharibika. Hili ni eneo linalopitisha magari makubwa yanayobeba mazao kati ya Babati - Gallapo.

Nne, kuhusu uwanja wa ndege wa Manyara, Mkoa wa Manyara ulikwisha omba kupata uwanja wa ndege na zipo sehemu ambazo zilipendekezwa. Kwenye hotuba sijaona maelezo yoyote. Tatizo litakalotokea ni maeneo yaliyopendekezwa kuvamiwa kama hayataendelezwa kwa nia ya kujenga uwanja wa ndege. Naomba nipate maelezo kama azma ya ujenzi wa uwanja wa ndege Manyara bado upo au la.

82 Tano, mafuriko Babati. Controller and Auditor General kwa mara ya kwanza ametoa ripoti ambayo tumepewa hapa Bungeni kuhusu mafuriko case study Babati. Naomba kufahamu namna Wizara/TANROADS walivyojiandaa kukabiliana na maeneo yaliyoonyeshwa kwenye ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu.

MHE. AMEIR ALI AMEIR: Mheshimiwa Spika, kwanza sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia uhai na uzima na kunipa uwezo kuchangia hotuba hii ya Wizara ya Miundombinu. Pia niwashukuru wapiga kura wa Jimbo la Fuoni na Chama changu cha CCM kwa kuniteua na kunichagua kuwa Mbunge wa Jimbo hilo la Fuoni.

Mheshimiwa Spika, sasa nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake nzuri iliyojitosheleza, pia niwashukuru Naibu Mawaziri na watendaji wote waliomsaidia Mheshimiwa Waziri kutengeneza hotuba hii.

Mheshimiwa Spika, kutokana na uzuri na namna ilivyowasilishwa hotuba hii, nina mchango mdogo sana. Mheshimiwa Spika, mchango wangu ni kuiomba Wizara hii kuzingatia sana kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM hasa hasa ahadi za Rais wetu alizozitoa kipindi cha kampeni pamoja na ahadi zilizoachwa na Marais wastaafu.

Mheshimiwa Spika, kuna ahadi nyingi zilizotolewa na Marais wetu bado hazijatekelezwa zinazohusu barabara na madaraja katika Jamhuri yetu ya Tanzania.

Mheshimiwa Spika, fedha zilizotolewa katika Wizara hii ni kidogo lakini naomba zipewe kipaumbele zile barabara ambazo zinaunganisha Mikoa yetu ambazo zitawaondolea shida wananchi wetu na kuwapunguzia ukali wa maisha, hasa ukizingatia wananchi walio wengi ni wakulima itakuwa njia rahisi ya kubadilishana mazao baina ya Mkoa na Mkoa na kwa bei rahisi sana.

Mheshimiwa Spika, pia isisahaulike barabara ya Mtoni Zanzibar inayoitwa Benjamin Mkapa ambayo Rais wa Awamu ya Tatu wakati alipoifungua njia hiyo aliahidi kuimalizia sehemu iliyobakia, lakini kwa bahati mbaya awamu yake ilikwisha na hadi leo hakuna jitihada zozote zinazoonesha ukamilishwaji wa barabara hiyo.

Mheshimiwa Spika, hivi sasa kwa kuwa kipindi ni kirefu kuna masuala mengi kwa wakazi na watumiaji wa barabara hiyo na baadhi ya wananchi hutoa maneno yasiyofaa kwa viongozi wa Chama chetu. Ninamwomba Waziri wakati wa majumuisho aitolee maelezo barabara hiyo katika kutekeleza ahadi hiyo.

Mheshimiwa Spika, daraja la Kigamboni limo katika ahadi na pia katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM. Lakini utekelezaji wake unazungumzwa tu ndani ya vitabu na

83 karatasi na utekelezaji wake hauonekani na tunasikia ununuzi wa kivuko kipya na ukarabati wa vivuko vilivyopo.

Mheshimiwa Spika, hivi sasa tunamaliza mwaka wa pili, nina wasiwasi tusije tukamaliza miaka mitano hakuna kilichofanyika na itakuwa aibu kubwa na kuwapa mdomo wasioitakia mema nchi hii.

Mheshimiwa Spika, daraja la Kigamboni ndio ukombozi pekee wa kuondoa tatizo la usafiri, kujikinga na majanga ya binadamu na kulinda usalama wa mali za raia. Pia kukipa Chama chetu heshima kwa viongozi wa Serikali yetu ya Awamu ya Nne. Mheshimiwa Andrew John Chenge, Taifa linakuamini na macho yote yanakuangalia wewe pamoja na Naibu Mawaziri wako, ondoeni yale yote yanayokwamisha ujenzi huo.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.

MHE. CLEMENCE B. LYAMBA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kupata nafasi ya kuchangia katika hoja hii muhimu katika maendeleo ya uchumi wa Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, kwanza nakupongeza unavyoliongoza Bunge letu kwa mitindo mizuri na ya kipekee. Inawahamasisha na kuwavutia Wabunge na wananchi wengi kufuatilia vipindi vya vikao vya Bunge letu.

Mheshimiwa Spika, pili naungana na Wabunge wenzangu kutoa pole nyingi kwa familia ya Marehemu Amina Chifupa Mpakanjia, aliyekuwa Mbunge jasiri, shupavu na aliyejitoa mhanga kukemea maovu dhidi ya biashara na matumizi ya dawa za kulevya na rushwa. Mungu ailaze roho ya Marehemu Amina Chifupa na Marehemu wengine peponi, Amin.

Mheshimiwa Spika, kuhusu hoja iliyopo mbele yetu, naanza kwa kuipongeza sana Serikali na hususan Waziri wa Miundombinu, kwa mtiririko huo, kwa kutoa kipaumbele kwa Wizara hii kuwa miongoni mwa zile zilizotengewa asilimia kubwa katika Bajeti ya Serikali mwaka huu na pia kwa mpangilio mzuri sana wa hotuba na majedwali yaliyosheheni takwimu zinazoeleweka vizuri kabisa.

Mheshimiwa Spika, ili fedha nyingi zilizotengwa kwa matumizi ya Serikali kuu na Halmashauri za Wilaya zilete mafanikio mazuri haraka, naishauri Serikali mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, moja, Serikali izitoe fedha hizi haraka (disbursement) ili zikaanze kazi za utekelezaji haraka kwa kuwa kazi zilizopo mbele yetu za kukarabati wa barabara na kujenga au kusanifu upya ni nyingi kubwa. Pili, Serikali isiishie hapo, ifuatilie kazi zote kwa timu maalumu kuona kwamba mawakala na Halmashauri zetu zinafuata kanuni za zabuni hadi uteuzi wa Wakandarasi ambao wana sifa za kweli (genuine) kumudu kutekeleza kazi za ujenzi wa barabara za vijijini na mijini. Kwa Halmashauri mkazo na mtazamo mahsusi

84 unahitajika kwa sababu Wakandarasi uchwara, wababaishaji ndiyo mara nyingi huteuliwa ili wazifuje fedha za Serikali kwa urahisi. Usimamizi mzuri utajenga barabara nzuri na pia utapunguza au kuondoa audit querries za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Mheshimiwa Spika, tatu, ili kupunguza matumizi makubwa ya routine maintenance ya barabara za vijijini naishauri Serikali itathmini viability ya kununua na kusambaza Wilayani, hasa zenye hali mbaya, Town Graders zinazovutwa na trekta za kawaida. Pamoja na hatua hii, Serikali irudishe magenge ya kutengeneza barabara vijijini kama ilivyokuwa zamani ili kudhibiti haraka uharibifu mdogo wa barabara kila unapotokea kabla haujageuka kuhitaji matengenezo makubwa.

Mheshimiwa Spika, jambo muhimu hapa ni kuimarisha usimamizi na udhibiti kwa waliokabidhiwa kazi hii. Hatua hizi kwa pamoja zitaongeza maisha ya barabara na kuruhusu shughuli za uzalishaji na usafirishaji mizigo na mazao kuwa na ufanisi mzuri zaidi kwa uchumi wa vijijini.

Mheshimiwa Spika, nne, swali moja la msingi ambalo naiomba Serikai ilifafanue ni kwamba, je, capacity ya vifaa vya routine maintenance na rehabilitation ya barabara zinazotakiwa kutengenezwa katika kila Wilaya almost simultaneously, baada ya fedha kutolewa ipo? Nauliza swali hili nikijua kuwa kila Halmashauri ina shauku ya kuanza kazi hii haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mikumi na wananchi kwa jumla naipongeza sana Serikali kwa kuwahi kuitengea shilingi milioni 800 barabara ya lami kutoka Mikumi hadi Kidatu ambayo imeanza kuharibika; sehemu nyingine imeharibika vibaya sana.

Mheshimiwa Spika, pia naipongeza sana Serikali kwa kutimiza ahadi yake katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005 kwa kukamilisha upembuzi yakinifu wa awali kwa barabara ya Mikumi – Kilosa - Dumila, ambayo imepangwa kujenga kwa kiwango cha lami kabla ya mwaka 2010 kumalizika. Nimefarijika zaidi kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mikumi ambao nitawaaarifu kuona kwamba Serikali imetenga jumla ya shilingi milioni 250 kwa ajili ya usanifu wa kina (detailed designs) kwa barabara hii kutoka Mikumi hadi Mziha katika mwaka huu wa fedha.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na usanifu wa kina nina ombi maalumu kwa Serikali ambalo nililiwasilisha kwa aliyekuwa Waziri wa Miundombinu mwaka jana Mheshimiwa Basil Mramba, alipofanya ziara mwezi Agosti, 2006 kwa barabara ya Dodoma, kupitia Lumuma, Kilosa hadi Mikumi.

Mheshimiwa Spika, tukiwa katika msafara pamoja na Naibu Waziri wa Fedha Mheshimiwa , tulisimama vijiji vya Zombo na Ulaya na kwenda kuangalia Mto Miyombo, ambao unaambaa sambamba na barabara hiyo umbali kama wa kilomita 0.3 Magharibi ya barabara. Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu na Naibu Waziri wa Fedha, walishuhudia tatizo kubwa la ukosefu wa madaraja makubwa jumla

85 ya matatu kuvusha mazao mengi ya mahindi ambayo hulimwa kila mwaka, ufuta, maharage, alizeti na pamba ambayo yanalimwa na kustawi sana ng’ambo ya Mto Miyombo. Mto Miyombo ni mkubwa na korofi sana wakati wa masika. Uliyabomoa madaraja matatu yaliyokuwepo awali wakati wa mvua za El-Nino. Gharama za kujenga madaraja hayo haiwezekani kubebwa na Bajeti ya Halmashauri, kwani itakula fedha nyingi mno.

Mheshimiwa Spika, kutokana na kutambua tatizo hili, Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu alikubali ombi langu kwamba kutokana na sababu zilizoelezwa hapo juu, madaraja haya matatu yataingizwa kwa kujengewa hoja maalumu katika usanifu wa kina wa barabara hii ikiwa ni element iliyo wazi itakayoongeza Economic and Financial viability ya mradi huu wa barabara.

Mheshimiwa Spika, ombi langu maalumu kwa niaba ya wakulima wengi stadi wanaotarajiwa kuongeza uzalishaji sana baada ya kuwa na madaraja ya uhakika ya kuvusha mazao yao ni kuwa naiomba Serikali iyajumuishe katika usanifu wa kina madaraja hayo, moja lipo kijiji cha Zombo na mawili katika kijiji cha Ulaya Mbuyuni. Lengo ni kwamba gharama za ujenzi wa madaraja hayo ambayo ni jirani kabisa na barabara kuu inayopita ng’ambo ya eneo kubwa lenye mazao mengi yasiyoweza kuvushwa na kusafirishwa katika barabara hiyo pasipo madaraja kujengwa, ziingizwe katika gharama ya mradi mzima wa barabara hiyo.

Mheshimiwa Spika, naliwasilisha Serikalini ombi hili wakati nilikwishamwandikia barua tarehe 14 Novemba, 2006 yenye maelezo haya kwa kina kwa Waziri wa Miundombinu Mheshimiwa Andrew Chenge, ambaye naamini hakunijibu kutokana na kutingwa na shughuli nyingi.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali kuwa pamoja na kuwepo vigezo maalumu vinavyotumika kuipandisha ngazi barabara iliyo chini ya mamlaka ya Halmashauri ili kuipandisha kuwa chini ya TANROADS umefika sasa wakati ambapo special circumstances ziwe exceptional.

Mheshimiwa Spika, mifano hai barabara tatu ambazo naamini under exceptional circumstance ingefaa zihudumiwe na TANROADS kwa sababu ni muhimu sana kwa kusafirisha chakula kingi kutoka sehemu moja kupeleka sehemu nyingine. Barabara hizo ni kama zifuatazo:-

Kwanza, barabara kutoka Miyombo (Junction - Kilosato Mikumi) kwenda Kilangali, pili, barabara kutoka Miyombo (Junction - Kilosato Mikumi) kwenda Lumuma na tatu, barabara kutoka Ruaha Mbuyuni kwenda Malolo.

Mheshimiwa Spika, Kilangali upo mradi mkubwa unaozalisha mpunga kwa wingi sana na uliigharimu fedha nyingi kujenga miundombinu thabiti ya umwagiliaji, lakini barabara ni mbaya mno kiasi mazao huoza na kuharibika kutokana na usafiri kuwa haba, ambao utadumaza uzalishaji mkubwa uliokuwepo awali.

86 Mheshimiwa Spika, miradi ya gharama kubwa pia ya umwagiliaji uliofadhiliwa na wahisani pamoja na Serikali yetu ipo Lumuma na Malolo katika Wilaya ya Kilosa, ambako zao kubwa ni vitunguu na mpunga. Mazao hayo kwa sehemu kubwa huharibikia huko huko badala ya kusafirishwa hata kufika Kilosa. Maeneo hayo yenye utajiri mkubwa wa chakula yako land locked wakati lengo la Serikali lilikuwa yawe source of food to other disadvantaged areas short of food. Inasikitisha vitunguu vya high grade kuozea mashambani.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mkoa wa Morogoro umeteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa chanzo cha ghala la kuzalisha na kuhifadhi chakula nchini na kwa kuzingatia ukaribu wa Mkoa huu na Mikoa jirani yenye mahitaji makubwa ya chakula. Naiomba Serikali itathmini upya umuhimu wa barabara zake zinazoelekea kwenye mashamba yanayozalisha chakula kwa wingi ili huduma ya barabara hizo iwekwe chini ya usimamizi wa TANROADS ambayo itahakikisha zinapitika kwa wakati wote kwa kusafirisha au kuhifadhi chakula.

Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo naunga mkono hoja na kuitakia Wizara hii mafanikio makubwa.

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, nachukua nafasi hii kukupongeza pamoja na Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge lako Tukufu kwa kutuendeshea vizuri shughuli za Bunge.

Mheshimiwa Spika, pia napenda kuwapongeza Waziri wa Miundombinu, Mheshimiwa Andrew Chenge, Naibu wake Mheshimiwa Dr. Milton Mahanga na Mheshimiwa Dr. Maua Abeid Daftari, Katibu Mkuu wa Wizara pamoja na watendaji wote wa Wizara hiyo kwa kutekeleza kwa makini Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi kwa kuhakikisha kuwa miundombinu ya barabara inapewa kipaumbele.

Mheshimiwa Spika, nimetumiwa maoni na malalamiko kutoka kwa wananchi wa Dar es Salaam kupitia ofisi ya Bunge/Posta, naomba kwa niaba yao nikukabidhi ramsi barua hizo na ukiri kupokea ili na wao wenyewe wasikie na kuona kuwa mchango wao umepokelewa kwani nami siwafahamu ila wamependa kunituma.

Mheshimiwa Spika, suala la barabara ya Masasi - Tunduru - Songea na Mbambabay ni kero kubwa. Ushauri wangu ni kwamba kama pesa hazitoshi kwa nini tusiweke lami angalau kwenye sehemu korofi kama vile kile kipande cha kilomita tano kutoka Mbinga mjini kwenda Undengo na kwenye kona za Ambaross kufika Mbambabay. Pia eneo la Mchomoro na Matemanga na hizo sehemu nyingine ziwekwe kifusi cha changarawe na sio hilo vumbi linalowekwa na kuondoka mara baada ya mvua.

Mheshimiwa Spika, kuhusu madaraja, upembuzi yakinifu ufanyike pia wakati wa mvua ili kuona pia ukomo wa maji. Ni aibu, kwa nini daraja limewekwa leo ikinyesha mvua linaondoka na maji? Wahandisi hao ni kweli waliohitimu au mnawatumia watu wasio Wahandisi? Kama sio ni uzembe ni nini? Hii ni kunyanyasa fani ya Uhandisi. Hatuwezi tu kusingizia mvua kwani hatujui kuwa daraja kazi yake ni pamoja na kupitisha

87 maji wakati wa mvua? Hasara inayopatikana inafidiwa vipi? Je, ni mikakati gani mliyoandaa kukabiliana na tatizo hilo pamoja na matunzo ya barabara hizo kwa ujumla kwani ni pesa nyingi zinatumika. Nimeseme hivyo kwa sababu Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa Mikoa iliyoathirika sana katika kipindi cha mwaka 2006/2007.

Mheshimiwa Spika, kuhusu TIRDO mimi ni mjumbe wa Bodi, inao wataalamu waliohakikiwa Kimataifa na vyombo vyenye uwezo wa kupima madaraja (zege) pamoja na nondo zake kwa kutumia teknolojia ya kisasa kabisa (Non Destrcutive Test – NDT) kwa njia ya Miale ya X na Gamma (X and Y Rays). Lakini pia wanalo gari la kuzunguka (mobile workshop) la kuweza kuzunguka sehemu mbalimbali lakini taasisi hiyo haitumiki kikamilifu wakati ni taasisi ya Serikali ambayo ingesaidia kuokoa mali zetu. Teknolojia hiyo imeshawahi kutumiwa na watu kama ZAKHEM ambao walipewa mkataba wa kutandika mabomba ya gesi ya Automus Mtwara. Hata hivyo hamna sheria inayoelekeza. Je, mko tayari kushirikiana na TIRDO?

Mheshimiwa Spika, kuhusu ATCL, ongezeni ndege. Nendeni Songea, acheni uzembe wa kuacha kukatisha ticket siku za holiday tulipata malalamiko kwa wateja Johannesburg. Litolewe tamko la kutoa kipaumbele kwa watumishi wa Serikali na mashirika ya umma kusafiri na ATCL ili hela yetu irudi ndani. Mnaonaje mkiwafundisha na kuwaajiri warembo wetu katika kazi ya uhudumu ndani ya ndege? Mzee Mataka, kaka yangu wewe ni mtaalamu wa biashara.

Mheshimiwa Spika, mara nyingi nikichangia kwa maandishi huwa sisikii majibu. naomba tafadhali nijibiwe. Nawasilisha.

MHE. EMMANUEL J. LUHAHULA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, nimpongeze Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na watendaji wote katika Wizara kwa kuandaa hotuba hii nzuri.

Mheshimiwa Spika, tatizo la mawasiliano, Serikali itusaidie kupata mawasiliano katika baadhi ya maeneo. Mfano kati ya Ushirombo - Runzewe katikati kuna msitu mkubwa ambapo pana kilomita 40 hamna mawasiliano. Eneo hilo naomba tusaidiwe kwani lina ujambazi mwingi. Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Bukombe yenye ukubwa wa takribani kilomita za mraba 10.482 maeneo yafuatayo hayana mawasiliano ambayo ni Mbogwe, Lugunga, Ikunguigazi Bulega na Iyogelo. Hadi sasa yapo makampuni ya Celtel na Vodacom naomba wafike maeneo hayo ili wananchi wafaidike.

Mheshimiwa Spika, niongelee suala zima la mawasiliano ya barabara. Naishukuru Serikali kwa uamuzi wa kutengeneza/kukarabati barabara ya Isaka - Bukombe - Lusahunga.

Mheshimiwa Spika, barabara hii kwa sasa haifai, inaangusha magari na kusababisha ajali nyingi. Naomba ukarabati huu uanze mapema ingawa kwa hali ilivyo si ukarabati bali ni matengnezo mapya.

88 Mheshimiwa Spika, Bukombe ina barabara zenye urefu wa kilomita 531.8 kati ya hizo barabara zenye urefu wa kilomita 108 tu ndizo hupitika, kilomita 423 hazipitiki. Kwa hali hii, Bukombe mnaiweka mahali gani katika uchumi wa Taifa letu?

Mheshimiwa Spika, katika kitabu cha hotuba ukurasa wa 124 Serikali imetenga fedha kidogo sana za kukarabati barabara ya Ushirombo - Buseresere tena ukarabati huu ni kilomita tano kati ya kilomita zaidi ya 40 na barabara hii ni mbovu sana. Je, Serikali itawezaje kuliboresha eneo hili?

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali inipatie ufafanuzi ili wananchi wa Bukombe waelewe. Barabara za TANROAD zifuatazo hazitafanyiwa ukarabati na kama zitafanyiwa ukarabati fedha yake iko wapi? Barabara zenyewe ni Runzewe - Bwanga na Mwalo – Iyogelo.

Naomba Serikali itusaidie kupandisha hadhi barabara zifuatazo ambazo Baraza la Madiwani limetoa baraka, barabara hizo ni Mwalo - Iyogelo - Bugelenga - Iponya - Masumbwe - Lugunga - Bwela - Ivumwa na nyingine Buntulili - Bulega - Lulembela - Kashelo - Bwela.

Mheshimiwa Spika, usafiri wa reli ya kati, naomba Serikali iendelee na juhudi zake haraka ili wananchi wa Kanda ya Ziwa tuondokane na tatizo la usafiri toka Dar es Salaam - Shinyanga - Mwanza. Naipongeza Serikali kwa jitihada zake za kushughulikia reli ya Isaka - Kigali huu ni mpango mzuri sana kwani wananchi wa Bukombe watanufaika na reli hii. Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja hii kwa kuwa yaliyomo ni mazuri ikiwa ni pamoja na uboreshaji wa Mwanza Airport. Mungu awabariki sana na kuwalinda.

MHE. MGANA I. MSINDAI: Mheshimiwa Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri wote wawili, Katibu Mkuu na Manaibu wake, Wakurugenzi na watumishi wote wa Wizara hii kwa kweli wanafanya kazi nzuri. Pia napongeza kitabu mlichotengeneza maana kinaeleza kila kitu kwa uwazi.

Mheshimiwa Spika, naomba niandike machache kuhusiana na barabara kuu na barabara za Mkoa zilizoko katika Jimbo la Iramba Mashariki. Barabara ya Singida - Shelui ambayo inaendelea kujengwa inapitia Jimboni kwangu napongeza mpaka sasa ujenzi unaendelea vizuri. Hata hivyo huko nyuma barabara hiyo ilikuwa inapitia katikati ya mji mdogo wa Igugumo, Serikali ikaamua barabara hiyo isiingie Igugumo Mjini. Serikali iliahidi kutengeneza barabara ya zamani inayoingia mji mdogo wa Igugumo kwa kuweka lami na izunguke na kuungana na barabara mpya tena. Sasa hivi barabara imetengenezwa hadi Igugumo Mjini lakini haijaunganishwa upande wa pili. Naomba barabara hiyo ikamilishwe na iungane na ile mpya ili magari toka Singida/Shelui yanayotaka na kuingia mjini yafanye hivyo na kutokea upande wa pili.

Mheshimiwa Spika, naishukuru Serikali imeona umuhimu wa kuanza kufanya upembuzi yakinifu juu ya kutengeneza daraja la Mto Sibiti. Mwaka huu umetenga shilingi milioni 200. Naomba sana kazi hiyo ianze mara moja na hatimaye fedha za

89 kujenga daraja hilo zitafutwe haraka kwa ajili ya kuinua uchumi wa Mikoa yote ya Kanda ya Ziwa ikiwemo Singida, Shinyanga, Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Tanga na kadhalika na nchi jirani za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Kongo (Zaire) na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, barabara namba R 425 Igugumo - Nduguti - Gumanga inahitaji sana kuimarishwa kama ifuatavyo; kujenga daraja imara kati ya Igugumo na Kinyangiri eneo la Mwembeni. Kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo hiyo kati ya Nduguti na Gumanga eneo la Mto Kamulungu hadi Gumanga.

Mheshimiwa Spika, barabara R 226 (kilomita 20.5) Kidarata - Nkungi ni barabara inayounganisha Mkoa wa Singida na Manyara. Ni barabara muhimu sana tena inayopita kwenye maeneo ya uzalishaji mkubwa wa mazao mbalimbali kama vile vitunguu, alizeti, pamba, ngano, giligilani na kadhalika. Pia ndiyo barabara pekee inayotumiwa na wananchi wengi wa Singida Kaskazini, Iramba Mashariki, Shinyanga na kadhalika kwenda hospitali kubwa ya Haydom. Barabara hii imeharibika sana na miaka zaidi ya saba haijatengenezwa kikamilifu. Naomba sana itengewe fedha na itengenezwe kikamilifu.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa mawasiliano ya simu, napongeza Celtel wamemaliza kujenga mnara kule Ibaga. Nawaomba Celtel, Tigo na Vodacom waendelee kujenga minara Nduguti, Nkungi, Mwanga, Mwangeza, Gumanga, Kikhonda, Kimgangiri na Nkinto. Wakazi wa Jimbo langu wana fedha nyingi.

Mheshimiwa Spika, sasa ajali za barabarani imekuwa kero kubwa sana. Sasa umefika wakati kwa Serikali kusimamia kwa kutoruhusu mabasi yanayokwenda mbali kuendeshwa na dereva mmoja. Serikali ipige marufuku malori (chassis) kugeuzwa na kutengenezwa kuwa mabasi tena kwenye gereji za mitaani, kila basi iwe na mlango wa dharura, Wizara ya Miundombinu kwa kushirikiana na Wizara ya Usalama wa Raia wahakikishe mabasi yanakwenda kwa ratiba kama ilivyokuwa zamani. Ma-traffic wasikae kituo kimoja kwa miaka mingi. Kama kweli kuna vidhibiti mwendo basi vifungwe kwenye magari (mabasi) yote na pia adhabu kwa wahalifu hawa iwe kubwa sana.

MHE. : Mheshimiwa Spika, kwanza nachukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri wake wote wawili pamoja na watendaji wao wa Wizara hii na wale wote ambao kwa namna moja au nyingine wamechangia katika kuiandaa na kuifanya hotuba hii kuonekana kuwa ni ya matumaini makubwa iwapo itasimamiwa na kutekelezwa ipasavyo. Nawapongeza sana kwa hilo.

Mheshimiwa Spika, baada ya pongezi zangu hizo, sasa niende kwenye mchango wangu ambao moja kwa moja nagusia kwenye huduma za simu za mkononi wa hasa katika kampuni ya Zantel.

Mheshimiwa Spika, kama tunavyoelewa kwamba huduma za mawasiliano ni jambo muhimu sana katika maendeleo ya jamii hususan mawasiliano ya simu na hasa

90 hizi simu za mikononi kwani zinarahisisha mtu kuwasiliana na mwenzake popote alipo kwa urahisi na kwa haraka kabisa. Mheshimiwa Spika, kampuni hii ya Zantel ilianzia kule Zanzibar ambako ndiko ilikojikita kibiashara kwa kiasi kikubwa sana na baadaye wakapanua biashara yao huku Tanzania Bara. Sasa ninachotaka kukizungumzia hapa ni juu ya huduma zao hivi sasa zinavyowasumbua wateja wao wakati wa mawasiliano hasa kuanzia nyakati za jioni, inakuwa ni vigumu kumpata mtu unayetaka kuwasiliana naye na mitambo huwa inajibu kwamba; “mteja unayetaka kuwasiliana naye hapatikani kwa sasa au yuko nje ya eneo,” au unajibiwa na mitambo; “simu imezimwa au iko nje ya eneo.” Lakini jambo la kushangaza wakati utakapompata mtu unayetaka kuongea naye atakwambia hajazima simu wala hajatoka nje ya eneo ambalo mawasiliano yanapatikana.

Mheshimiwa Spika, hili jambo/usumbufu linauma sana kwani wakati mwingine unakuwa na mgonjwa au mtu kapatwa na msiba anataka kutoa taarifa kwa wahusika lakini anashindwa na kusababisha usumbufu mkubwa kwa wakati kama huo. Napenda kujua kunakuwa na matatizo gani hata kufikia kampuni ya Zantel kuwasababishia usumbufu wateja wake?

Mheshimiwa Spika, la pili, namwomba Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu kuyahamasisha makampuni mengine ya simu kama vile TTCL, Voda, Tigo na kadhalika yaje kupanua huduma zao kule Zanzibar zifike vijijini ili wananchi waweze kujiunga katika mitandao hiyo na kuweza kutoa ushindani mkubwa na kampuni hii ya Zantel.

Mheshimiwa Spika, kwa kweli wananchi wanahitaji huduma za mitandao hiyo ili tu zifikishwe vijijini kama vile walivyofanya Zantel na tunaamini huduma hizi zikipanuliwa Zanzibar wananchi watafurahia na watatokana na usumbufu wanaoupata hivi sasa.

Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Ahsante sana.

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kusema kwamba naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Spika, pili, napenda niipongeze Serikali kwa hotuba thabiti ilizochukua katika Bajeti ya mwaka 2007/2008 kwa kuongeza pesa kwa ajili ya kuboresha miundombinu nchini, hasa barabara zote nchini. Mheshimiwa Spika, pamoja na pongezi hizo, ningependa nipate maelezo katika masuala yafuatayo; meli za MV Clarias na MV Butiama. Meli hizi zimekuwa zikifanya kazi kati ya Nansio, Ukerewe na Mwanza. Lakini kwa muda mrefu sasa zimekuwa haziaminiki kutokana na kuharibika mara kwa mara zikiwa katikati ya Ziwa. Lakini cha kushangaza ni kwamba Serikali haikupanga kiasi chochote cha pesa kwa ajili ya kutengeneza meli hizo. Naomba maelezo.

Mheshimiwa Spika, kivuko cha Kisorya - Ukerewe, kwa muda mrefu sasa kivuko hiki kimekuwa hakifanyi kazi na kusababisha kero kubwa kwa wananchi wa Ukerewe,

91 Mwibara na Tanzania kwa ujumla. Je, kwa nini Serikali haikupanga kiasi chochote cha fedha kwa ajili ya kivuko hiki? Naomba maelezo.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Bunda - Nansio, wakati wa kampeni za uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete wakati akiwa Ukerewe na pia mwaka 2006 akiwa Kasuguti aliahidi kwamba barabara hiyo ingetengenezwa kufikia kiwango cha lami kabla ya uchaguzi ujao wa mwaka 2010. Je, ni kwa nini pamoja na ahadi za Wizara ilizotoa katika swali langu la mwaka 2006 kwamba barabara hiyo ingeanza kutengenezwa katika mwaka huu wa fedha wa 2007/2008, haikutengewa fedha hata za usanifu yakinifu? Naomba maelezo.

Mheshimiwa Spika, je, ni miradi mingapi iliongezwa katika miradi iliyopo baada ya Serikali kuongeza fedha zaidi za barabara katika mwaka wa fedha 2007/2008? Naomba miradi hiyo ibainishwe.

MHE. BALOZI KHAMIS S. KAGASHEKI: Mheshimiwa Spika, namshukuru Waziri Mheshimiwa Andrew Chenge kwa hotuba yake aliyoitoa wakati akipendekeza Makadirio ya Matumizi ya fedha kwa mwaka 2007/2008. Naomba kupata majibu kutoka kwa Mheshimiwa Andrew Chenge kuhusu yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, ni miaka mitatu hivi sasa Serikali imetamka kwa kujiamini kabisa kwamba raia wa Watanzania ataweza kuwasha gari lake toka Bukoba mpaka Dar es Salaam kwa barabara ya lami. Nini kimetokea kuhusu kauli hii? Katika hotuba ya Waziri ukurasa 31 na 32 yahusu mradi maalumu wa ujenzi wa barabara kuu, naomba nipate jibu kuhusu barabara ya Bukoba - Biharamulo - Mwanza, kulikoni? Mheshimiwa Spika, kuhusu eneo la usafiri wa majini, ukurasa wa 38 na usafiri na uchukuzi katika Maziwa, ukurasa wa 42. Naomba nimkumbushe Waziri kwamba usafiri wa majini katika Ziwa Victoria ni mgumu sana na hali inazidi kuwa mbaya. Nilitegemea budget yake ingetupa matumaini lakini naona katika hotuba hii matumaini hayapo.

Mheshimiwa Spika, takribani miaka kumi iliyopita MV Bukoba ilizama na kuna watu karibu elfu moja walifariki lakini na mitaji ya fedha ilitokomea ndani ya Ziwa. Tegemeo kubwa limekuwa MV Victoria, lakini hii ni meli ya miaka mingi karibu miaka 45 au zaidi. Imechoka na kila wakati iko katika matengenezo na hivi sasa haifanyi kazi. Badala yake ipo MV Serengeti, hii siyo meli ya abiria. Kumekuwa na watu binafsi wameweka vyombo majini ambavyo vimezama na kuna watu (meli ya ndugu Kishimba ni mojawapo). Nimesikitika kutosikia Waziri akitamka lolote kuhusu usafiri wa majini katika Ziwa Victoria kwa shabaha ya kuwahudumia watu wa Kagera.

Mheshimiwa Spika, ukurasa wa 60 wa hotuba ya Mheshimiwa Waziri yahusu uendelezaji wa viwanja vya ndege. Nasikitika kusema kwamba taarifa tuliyopewa ni kwamba World Bank imetoa pesa za kutengeneza baadhi ya viwanja vya ndege kikiwemo cha Bukoba Mjini. Naomba Mheshimiwa Waziri atazame hotuba yake ya mwaka 2006/2007, ukurasa wa 14. Naomba majibu kuhusu tofauti ya misimamo hii. Naomba

92 Waziri awahakikishie watu wa Kagera na Bukoba kwamba uwanja wa Bukoba utawekwa lami.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Kagera umetengwa sana kimiundombinu. Huu ni Mkoa wa pembezoni. Barabara zinayoiunga Bukoba na sehemu nyingine za Tanzania ni matatizo makubwa. Usafiri wa majini ni matatizo makubwa na usafiri wa anga ni matatizo. Naomba Mheshimiwa Waziri ajibu hoja hii kuhusu kusafiri wa aina zote kuingia na kutoka Mkoani Kagera na hasa Makao Makuu ya Mkoa. Naomba majibu

Mheshimiwa Spika, natanguliza shukrani.

MHE. ZAYNAB M. VULU: Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa hii kuipongeza Wizara ikiwa ni pamoja na Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu, Wakuu wa Idara na wafanyakazi wote kwa ujumla. Mheshimiwa Spika, maendeleo yoyote hayaji bila ya kuwa na barabara za uhakika na umaskini hauwezi kutoka bila ya kuwa na barabara za uhakika. Mkoa wa Pwani unakabiliwa na umaskini hii inatokana na wananchi wa huko kushindwa kuuza au kupeleka bidhaa zao kwenye masoko kutokana na tatizo la usafiri kwa maana ya kwamba barabara ni za msimu. Hivyo basi Wizara iuangalie Mkoa wa Pwani katika nyanja ya kuweza kupata maendeleo kwa kuwa na barabara za uhakika.

Mheshimiwa Spika, uzoefu unaonyesha mara nyingi upembuzi yakinifu iwe wa barabara au madaraja huchukua muda mrefu sana. Ni nini hasa kinachofanya upembuzi huo uchukue muda mrefu?

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tunataka kuleta mabadiliko ya barabara zetu ambazo nyingi zake ni mbovu au ndogo hivyo basi tunaowategemea ni hao wataalamu ambao wanafanya upembuzi yakinifu na kuweza kupata ufumbuzi iweje wachukue muda mrefu?

Wakati umefika sasa kwa barabara zinazojengwa kuwa na uwezekano wa kuweka njia za wapanda baiskeli, mikokoteni na kutengeneza mazingira ya kuwawezesha walemavu kupita kwa urahisi.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naomba kuunga mkono hoja.

MHE. MWANAWETU S. ZARAFI: Mheshimiwa Spika, kwanza naipongeza Wizara hii kwa kuzidi kuongeza mikakati ya ujenzi wa barabara ya Kusini, Kibiti – Lindi.

Katika kitabu hiki cha Bajeti sijaona sehemu yoyote inayohusu ukarabati wa kiwanja cha ndege cha Kilwa Masoko ukizingatia kwamba Kilwa hivi sasa ina rasilimali nyingi na vivutio mbalimbali ambapo wageni, viongozi, watalii hutumia ndege ambazo wakati wa mvua huzama katika matope wakati wa kutua. Naomba kufahamishwa ni kwa nini Kilwa haimo katika ukarabati wa kiwanja? Lini Kilwa itawekwa katika orodha ya kukarabatiwa miundombinu ya kiwanja hicho?

93 Mheshimiwa Spika, ni ushauri au ombi tu kwa TANROADS. Wanapojenga barabara zao washirikiane na Mkurugenzi wa Halmashauri ili aweze kuwaweka wataalamu wake wa maeneo hayo kwani wao ndio wanaofahamu hali halisi ya barabara hizo na nini kifanyike, ahsante. MHE. MUSTAFA H. MKULO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuuweka mradi wa barabara ya Mikumi - Kilosa - Magole - Mziha, katika mipango yenu ya mwaka 2007/2008.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa ujumla Wilaya ya Kilosa imepata a raw deal. Barabara zote tatu zinazoingia Makao Makuu ya Wilaya - Dumila/Kilosa, Melela/Kilosa na Mikumi/Kilosa, ni mbovu sana baada ya mvua za vuli. Bila kuzitengeneza hadi msimu ujao, mji wa Kilosa utakuwa kisiwani.

Mheshimiwa Spika, Kata za Lumuma na Kidete sasa hivi hazina mawasiliano. Treni zinaishia Dodoma na barabara ya Kilosa - Lumuma - Kidete haipitiki kwa sababu madaraja na karavati zote zilibomoka na kusombwa na maji wakati wa mafuriko ya vuli. Nilizungumza na ndugu Madina, Regional TANROADS Manager, kuhusu barabara hizi. Lakini sijaona popote kama barabara hizi zitahusika katika mpango wa ukarabati mwaka huu. Naomba na barabara hizi zijumuishwe katika mpango wa ukarabati mwaka huu wa fedha 2007/2008.

Mheshimiwa Spika, kata za Lumuma na Kidete ni maeneo yenye miradi mikubwa ya umwagiliaji (irrigation schemes) iliyofadhiliwa na Serikali pamoja na wafadhili kutoka Denmark. Kuna wakulima wengi sana wa vitunguu. Ukosefu wa usafiri wa barabara wa treni umesababisha wakulima wa maeneo hayo wapate hasara kubwa mwaka huu.

Mheshimiwa Spika, ili wakulima hawa waendelee kuhamasika kulima vitunguu nakuomba Mheshimiwa Waziri uone uwezekano wa kuhakikisha barabara nilizozitaja zinafanyiwa ukarabati mapema iwezekanavyo katika mwaka huu wa fedha. Naunga mkono hoja.

MHE. SAID J. NKUMBA: Mheshimiwa Spika, naomba kuchukua fursa hii kukushukuru kwa kuniwezesha kupata nafasi nami niweze kutoa mchango wangu.

Mheshimiwa Spika, aidha, nampongeza Waziri kwa hotuba yake nzuri kwa namna ya pekee nimpongeze pia Naibu Waziri Mheshimiwa Dr. Milton Mahanga kwa kufika kwake Sikonge na kuvumilia kusafiri kwa muda mrefu akikagua barabara ya Tabora - Ipole – Ruangwa, barabara ambayo hali yake si nzuri kwa muda mrefu. Mheshimiwa Spika, kwa sababu nimetumwa na wananchi wa Sikonge kuja hapa Bungeni kuwakilisha kero zao, kwa ufupi, naomba niseme kero hizo.

Kwanza ni ile barabara itokayo Tabora - Ipole - Rungwa. Naiomba sana Serikali kusikiliza kilio cha wananchi wa Sikonge katika kuhakikisha kwamba barabara hii inapitika wakati wote bila bughudha kama hii wanayoipata wananchi wa Sikonge. Aidha,

94 naipongeza Serikali kwa kutenga fedha kiasi ingawa hazitatosheleza mahitaji lakini angalau zikisimamiwa vizuri kwenye matumizi inawezekana tatizo hili linaweza kupata ufumbuzi.

Mheshimiwa Spika, pili, niiombe Wizara iangalie uwezekano wa kuhakikisha Wilaya ya Sikonge inapata huduma za Posta kikamilifu kwa kuhakikisha wanajenga jengo la kisasa la kutoa huduma zote za Posta.

Mheshimiwa Spika, mwisho, narudia kukushukuru kwa kunipa nafasi hii, naipongeza Wizara na naunga mkono hoja.

MHE. FUYA G. KIMBITA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, niwapongeze wote kwa niaba ya wananchi wa Hai nikianzia kwa Mheshimiwa Waziri, Waheshimiwa Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Wakurugenzi wa Idara pamoja na watendaji wengine wote Wizarani kwa kazi ngumu lakini nzuri mnayoitenda.

Mheshimiwa Spika, sina mengi sana ya kusema kwani hotuba yenu imeeleza mambo mengi na kwa kina kabisa hivyo kwa lugha za kisiasa tunasema ni kuongezea nyama tu kwani mfupa wenyewe umeshajaa.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kuchangia upande wa usalama ambapo nianze kwa kushauri kwamba Wizara kwa kushirikiana na Wizara nyingine pamoja na taasisi nyingine kuimarisha usalama kwa ujumla wake kwenye sekta za anga, barabara, reli na usafiri wa majini. Pamoja na usalama pia napendekeza hatua za tahadhari zizingatiwe sana kwani tungeweza kuepusha vifo na madhara makubwa tuliyokwisha yapata mfano kwenye mabasi mengi siku hizi hata emergency doors, mwendo mkali, kuzidisha abiria au mizigo kwa maana ya ujazo pamoja na uzembe. Nashauri mtandao wa barabara kwa nchi nzima uimarishwe kwa mbinu zote zile barabara kuu pamoja na zile za Wilayani mpaka vijijini kwani bila network nzuri ya barabara itakuwa ni vigumu sana kufikia malengo. Mheshimiwa Spika, naomba nikumbushie ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni ya kujenga barabara inayotoka Kwasadala kupitia Masama Mula kwa kiwango cha lami kule Wilayani Hai, Mkoani Kilimanjaro kwani pamoja na shughuli na umuhimu wa hii barabara kwa uchumi wa Hai sasa kuna mpango mwingine mkubwa sana wa kufungua njia mpya ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa maana ya kukuza uchumi wa Taifa kwa ujumla kupitia barabara hii na kipande cha lami ya ahadi ya Mheshimiwa Rais ni cha kilomita kumi na mbili na nusu tu ambapo ni kutoka Kwasadala - Kanisa la Masama Kati, Masama Mula - Salali, Sonu.

Mheshimiwa Spika, pamoja na barabara hii kuna zile za Moshi vijijini ambapo tuliandikiwa barua na Waziri Mheshimiwa Andrew Chenge kwamba hizi barabara za ahadi za Mheshimiwa Rais zingepewa pesa za kufanya upembuzi yakinifu mwaka huu wa pesa lakini sijaziona hizo pesa ili kazi rasmi ya ujenzi ianze mwaka ujao wa pesa sasa wale wananchi tutaweleza nini? Naomba majibu hapa Bungeni ili na wananchi wasikie wenyewe.

95 Mheshimiwa Spika, huduma nyingine za mawasiliano kwa jumla wake zinakwenda vizuri na kwa speed nzuri.

Mheshimiwa Spika, kwa kumalizia, naomba usimamizi mzuri sana wa pesa kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Spika, ninaunga hoja mkono kwa asilimia mia moja.

MHE. DR. WILBROD P. SLAA: Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia kama ifuatavyo katika hotuba ya miundombinu.

Mheshimiwa Spika, kwanza napenda Mheshimiwa Waziri wakati wa majumuisho anihakikishie kama barabara ya Oldeani Junction (Njia Panda) - hadi Qanded - Matala - Lalago yaani inayounganisha Mkoa wa Arusha na Shinyanga ni moja ya barabara itakayonufaika na fedha shilingi 44,454,000,000.

Mheshimiwa Spika, hii barabara, hasa sehemu ya Oldeani Junction - Mang’ola imetolewa ahadi na Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete mara mbili na Mheshimiwa Rais Mstaafu Benjamin Mkapa aliagiza fedha za dharura shilingi milioni 238 zitolewe kujenga Daraja la Baray katika barabara hiyo. Hii ni kutokana na umuhimu wa kiuchumi na kijamii na barabara hii.

Mheshimiwa Spika, sihitaji kueleza umuhimu wa barabara hii kwa vile nimefanya hivyo katika nafasi tofauti. Nahitaji tu maelezo kama barabara hii imetengewa fedha na iwapo jibu ni ndiyo imetengewa kiasi gani kwa mwaka huu wa 2007/2008?

Mheshimiwa Spika, nashukuru kuwa kampuni yetu ya ATCL imerudi katika umiliki kamili na Serikali yetu. Kwa vile katika Bajeti ya mwaka 2007/2008 haionyeshi popote kama fedha zimetengwa kufufua Shirika/kampuni hii, je, Serikali inaweza kulithibitishia Bunge hili kuna mpango upi wa muda mfupi na wa muda mrefu wa kufufa kampuni ya ATCL utakaohakikisha kampuni hii sasa kweli imefufuka na kuwa na hadhi inayostahili na itakayohimili ushindani mkali ulioko katika biashara ya usafirishaji wa anga?

Mheshimiwa Spika, tatu, kwa vile uwanja wa ndege wa Manyara ni hub ya usafiri wa kitalii kati ya mbuga za wanyama ya Manyara na Ngorongoro, je, ni lini Serikali itapanua uwanja huo na kuweka vifaa vya kisasa kwa ajili ya usalama wa abiria na hasa kwa kuzingatia uwanja huo pia unatumika mara nyingi na viongozi wa Kimataifa wanaotembelea mbuga zetu. Napenda kupata ufafanuzi.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, sasa naomba kupatiwa ufafanuzi.

MHE. SALIM HEMED KHAMIS: Mheshimiwa Spika, nawapongeza Waziri wa Miundombinu, Naibu wake wawili na watendaji wake wote kwa kuisimamia vizuri Wizara hii.

96 Mheshimiwa Spika, Shirika la Reli Tanzania (TRC) ni usafiri ambao unategemewa na Watanzania walio wengi. Ni njia pekee ambayo wanyonge huitegemea kwa kusafiri na kusafirisha mizigo yao ikiwemo mazao ya kilimo. Tumefikia mahali sasa inaonyesha Serikali kupitia Wizara hii imeshindwa kuelimisha Shirika la Reli.

Sasa suala la ubinafsishwaji wa TRC haliepukiki. Kampuni ya RITES ndiyo iliyokubalika, lakini lazima tuwe waangalifu sana na wawekezaji hawa kwa sababu hatuna uzoefu na utendaji wao. Mheshimiwa Spika, sisi Wabunge hatujui mikataba ya makubaliano kati ya RITES na Serikali, lakini Serikali ichukue uzoefu wa City Water ya kuboresha upatikanaji wa maji hii hali ilikuwa ngumu zaidi.

Kuhusu barabara, Tanzania ni nchi kubwa kwa hiyo ukifikiria ujenzi wa barabara leo utaona haiwezekani hasa ukifikiria ufinyu wa Bajeti yetu mwaka hadi mwaka. Barabara inaunganisha nchi, inachangia maendeleo ya kilimo na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, inabidi sasa tutoe kipaumbele kwa barabara kwa kutumia kiasi kikubwa cha fedha kwa kujenga barabara tukiweka malengo maalumu kuwa baada ya miaka mitatu barabara zote zinazounganisha Mkoa na Wilaya ziwe zimejengwa kwa lami. Tatizo lililopo sasa ni kuwa hata hizo pesa chache zinazotengwa zinajenga barabara zinazoharibika kwa muda mfupi sana. Je, tatizo ni nini? Ni uhandisi, ni usimamizi au ni wizi au ni nini? Serikali ilione hili haraka na hatua zichukuliwe ili kujenga barabara za kudumu japo ni chache.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Shirika la Ndege Tanzania (ATC), Tanzania haikufanikiwa hata kidogo katika ubia wake na Afrika Kusini yaani South African Airways (SAA). Sasa tunalimiliki wenyewe kwa asilimia mia moja. Sisi kwa sasa ni kwa sababu ya sera zetu za kujiondoa katika biashara hatutaweza kamwe kuliongoza Shirika la ATC. Tujifunze kwani tulishindwaje ? Nashauri Serikali itafute mbia mwingine ili waendeshe ATC. Hatuwezi kutegemea majina ya watu kuongoza Shirika. Tunategemea sera yetu hawa wakiondoka duniani (wakifa) nani ataongoza ATC ?

Mheshimiwa Spika, kuhusu Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), Watanzania wanategemea mamlaka hii kwa mambo mengi mimi naizungumzia TMA kwa taarifa ya hali ya hewa kwa wakulima.

Kwa taarifa ya Mkurugenzi Mkuu wa TMA, mamlaka hii ina vifaa na zana za kutosha na pia ina wataalamu wa kutosha. Hivyo basi, tungetegemea taarifa zao zikawa ndiyo msingi wa mipango yetu ya kilimo. Lakini hali haiko hivyo. Mara nyingi utabiri wao unawaingiza wakulima katika hasara kwa kuwa kile wanachokitabiri siyo kinachotokea.

Mheshimiwa Spika, naomba wawasaidie wakulima kwa kuwapa utabiri wa uhakika. Mheshimiwa Spika, kuhusu utabiri wa majanga, TMA itoe taarifa ya muda mrefu wa majanga kama mafuriko, kimbunga, volcano na kadhalika. Wavuvi wetu na wale

97 wanaotumia bahari, lakini hata sisi tulio katika nchi kavu tunashtukizwa na vimbunga ambavyo vinaathiri mali na maisha yetu. Ahsante

MHE. FELIX N. KIJIKO: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia Wizara ya Miundombinu kama ushauri wangu katika vipengele vifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusu vivuko/meli, hivi karibuni kumekuwepo na wimbi la kuzama kwa baadhi ya vyombo vya usafiri ikiwa ni pamoja na meli. Kwa sababu kazi hii inasimamiwa na Wizara, ni vema kukawa na kumbukumbu nzuri kuhusu abiria wanaokuwamo kwenye vyombo hivyo ili ajali ikitokea na hasa baada ya chombo kuzama iwe ni rahisi kuwatambua abiria wa chombo hicho tofauti na hali ilivyo sasa kwamba huwa hakuna kumbukumbu zilizo sahihi. Hali hii huwa inajitokeza kutokana na baadhi ya abiria kupanda vyombo vya usafiri kwa kutumia majina ambayo siyo yaliyoandikwa kwenye tiketi.

Mheshimiwa Spika, malipo kwa barabara zinazopanuliwa yamekuwa yakijitokeza malalamiko kutoka kwa wananchi wanaokumbwa katika jitihada za Wizara kupanuliwa. Naishauri Wizara ujipange vizuri katika hili ili kuhakikisha kabla ya wananchi kuvunjiwa nyumba kwa upanuzi wa barabara zitengwe fedha kuwalipa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu msongamano wa magari, kwa makusudi mazima naishauri Wizara ijikite kuhakikisha utaratibu wa kutengeneza ama kupanua barabara zinazotoka Jijini Dar es Salaam kwenda nje zinasimamiwa vizuri.

Mheshimiwa Spika, tatizo la Reli ya Kati. Tatizo hili la reli hiyo kutokufanya kazi kuanzia Dar es Salaam ni tatizo zito. Pamoja na jitihada za Serikali kuanza matengenezo ya reli hiyo, bado Wizara naishauri ijikite katika hili kwa usimamizi wa karibu ili kuhakikisha kazi hiyo inakwenda kwa kasi inayostahili ili kuwaondolea wananchi wanaokwenda mikoa ya Mwanza, Tabora na Kigoma wananeemeka.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. MHE. HAMAD RASHID MOHAMED: Mheshimiwa Spika, kwanza natoa pongezi kwa hotuba nzuri na nyenye uchambuzi wa kina. Hongera Mheshimiwa Waziri na wasaidizi wako wote.

Mheshimiwa Spika, manunuzi katika Wizara na asasi zake, katika hotuba umeelezea namna baadhi ya asasi za Wizara ya Miundombinu kutumia mtandao katika shughuli zake (E-commerce na E-government) naomba kushauri kuwa Wizara ina utalaamu wa kutumia internet na kwa kuwa Wizara ina manunuzi makubwa nashauri muanze kufanyia kazi teknolojia ya E-procurement ambayo Mheshimiwa Dr. Milton Mahanga, anaielewa sana.

Kuhusu BOT, BOOT na PPP, naomba utueleze ni lini miradi itakayoingia ndani ya mpango huu itatangazwa? Natumai unanielewa kwani wanaotaka kuingia katika mpango huu wapo, lakini Serikali haijawa wazi na utaratibu wa kufuata.

98 Kuhusu kuzifanya mamlaka zijitegemee, mamlaka nyingi zilizoanzishwa chini ya Wizara hii zina uwezo wa kujitegemea kama Serikali itaziagiza taasisi ziwe na cooperate plan na Serikali kuwapa rentation ya mapato na pia kuruhusiwa kukopa benki kama TIB, aidha asasi hizi zikiweza kuingizwa kwenye utaratibu wa PPP zinaweza kuzipunguzia mzigo Serikali.

Mheshimiwa Spika, SINOTASHIP. Inasikitisha kuwa shirika hili shughuli zake haziko wazi sana na kama litafuatiliwa vizuri, shirika hili lingeingiza fedha nyingi hasa kwa kuzingatia kuwa biashara ya meli kwa kiwango kikubwa kama kuna usimamizi mzuri. Katika hotuba, Mheshimiwa Waziri hakuonyesha mapato ya miaka miwli au hasara ya miaka hiyo. Aidha, hatujui hata hisa za Serikali ni ngapi. Naomba uchambuzi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Rada na ndege ya Rais, naomba utupatie taarifa juu ya uchunguzi uliofanywa na asasi za rushwa za ndani na nje juu ya taarifa za rushwa hasa ndege ya Rais. Aidha, naomba kujua hatua zinazochukuliwa na Serikali angalau kupata fedha za ziada iliyolipwa kwa madalali.

Aidha, ushauri wetu wa kuiuza ndege ya Rais, bado tunaona ni wa msingi sana kwani huu mzigo mzito kwa walipa kodi wa Tanzania. Naomba maelezo ya hatua hiyo ya kuuza ndege hiyo. Nakushukuru kwa kunijibu maswali yangu.

MHE. JACKSON M. MAKWETTA: Mheshimiwa Spika, kwanza natoa pongezi kwa kazi nzuri inayofanywa na Wizara ya Miundombinu.

Mheshimiwa Spika, Tanzania tuna bahati ya kuzungukwa na nchi nane. Hii ni bahati na siyo balaa. Huu ni utajiri usioondosheka kama madini au mafuta. Hakuna athari za ukame. Kwa bahati mbaya hatutumii neema hii. Hata bila mazao ya kutosha au viwanda Tanzania ingeweza kupiga hatua kubwa kiuchumi.

Mheshimiwa Spika, ili kutimiza ndoto hizi nashauri zijengwe barabara zifuatazo; Kigoma - Uvinza - Malagarasi - Kaliua - Urambo - Tabora - Itigi - Manyoni - (Kigoma - Dar es Salaam), Kasanga Port (Lake Tanganyika) - Matai - Tunduma (TAZARA), Isongole – Malawi na Mtambaswala – Mozambique.

Mheshimiwa Spika, najua ziko barabara nyingi za aina hii, mtindo wa sasa wa kugawa fedha za barabara (Holy Communion) hautatufikisha popote, tutachelewa. Barabara hizi za mpakani zitatupa fedha ambazo zitatupa nguvu ya kutengenezea barabara za Wilaya na Mikoa. Kukopa fedha ili kujenga shule, barabara na hospitali ni jambo zuri tu kama nchi itakuwa na fedha za kutunzia huduma hizi (sustainability). Vinginevyo nazo zitakufa na nchi haitakuwa na barabara.

Mheshimiwa Spika, jiografia yetu ni mgodi ulioondosheka, tomorrow is now. Either we do or we perish.

99 MHE. PROF. IDRIS A. MTULIA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kutoa pongezi nyingi kwa Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara hii ya Miundombinu.

Mheshimiwa Spika, naishukuru Wizara ya Miundombinu kwa kuipa Rufiji kivuko cha Utete kama mlivyoahidi kutekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kuhakikisha kuwa barabara ya Kibiti - Utete ipitike wakati wote. Shilingi milioni 155 kujenga barabara hiyo haitoshi, lakini bado nashukuru ila ningeomba fedha za barabara Kibiti - Utete ziongezwe. Aidha, hobuta inatuhakikishia kuwa kila barabara inayounganisha mkoa na Makao Makuu ya Wilaya itajengwa kwa kiwango cha lami au changarawe. Naomba barabara ya Nyamwaga - Utete (Makao Makuu ya Wilaya ya Rufiji) ijengwe kwa umadhubuti mkubwa.

Mheshimiwa Spika, tunaiomba Wizara ichukue barabara ya Ikwiriri - Mkongo - Mloka (kilomita 110) iende Vikumburu - Kisarawe - Kibaha (Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani) ichukuliwe na kuhudumiwa na TANROADS Mkoa wa Pwani. Barabara hii inakidhi viegezo vya kupandishwa hadhi ya kuchukuliwa na TANROADS Mkoa wa Pwani.

Naomba kushukuru sana kwa watoa huduma za mawasiliano yaani Celtel, Vodacom, Tigo na Zantel (simu za mkononi), lakini naomba niwasifu Celtel kwani hawa ndiyo wanaohudumia wateja wengi Wilaya ya Rufiji. Mheshimiwa Waziri Warufiji tunaomba Celtel waendelee kujenga minara katika vijiji vifuatavyo; kijiji cha Mkola (Kitovu cha Utalii wa Selous), kijiji cha Nyaminywili (Njiani kwenda Mloka), kijiji cha Kilimani (Njiani kwenda Mloka), kijiji cha Ngarambe (Kingupira Selous) na kijiji cha Mbwara.

Mheshimiwa Spika, minara hiyo itafungua maisha, itaongeza sana biashara ya utalii na kupanua Selous Game Reserve Tourism. Tunaomba muwaambie Celtel kuwa katika Bunge hili tumepitisha sheria ya kuwapa motisha watoa huduma za mawasiliano katika vijijini, wapewe Celtel ili wakamilishe ujenzi wa minara katika vijiji nilivyoainisha hapo juu.

Mheshimiwa Spika, mwisho, napenda kupongeza na kushukuru sana kwa kutubadilishia mitambo ya mawasiliano ya zamani na kusimika mitambo mipya kule Utete ambako ni Makao Makuu ya Wilaya ya Kibiti na Ikwiriri. Ahsante sana na naomba kuwashukuru watendaji wote wa Wizara yako.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja asilimia mia moja. Ahsante.

MHE. IDDI M. AZZAN: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa jiji la Dar es Salaam linakabiliwa na tatizo la msongamano wa magari kutokana na ubovu wa barabara za pembeni, lakini Wizara haikutoa kipaumbele ili kukabiliana na tatizo hilo badala yake zimetengwa pesa nyingi kwa ajili ya barabara za Jimbo la Ukonga na Kawe, ili kuonda tatizo la msongamano ni vyema Wizara ikaangalia uwezekano wa kusaidia kujenga

100 barabara za Jimbo la Kinondoni ambazo zikitengenezwa tutaondoa msongamano katika Morogoro Road, Ally Hassan Mwinyi Road, Kawawa Road na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, naomba maelezo kuhusu barabara ya Kawe Beach kutokea Club Oasis mbona haikutengewa pesa na ilipitishwa na Bodi ya Barabara Mkoa wa Dar es Salaam?

Mheshimiwa Spika, kuhusu tatizo la usairi wa wanafunzi, naomba Wizara kupitia SUMATRA iandae utaratibu mzuri ili wanafunzi wasiendelee kuteseka na usafiri, ikibidi hata nauli iongezwe kutoka shilingi 50/= hadi 100/= ili wenye daladala washawishike kuwapakia kwenye magari yao.

Mheshimiwa Spika, mwisho naipongeza Wizara kwa kazi nzuri sana iliyofanyika hasa wakati wa kipindi cha mvua. Lakini pia kwa Bajeti nzuri ya mwaka 2007/2008. Naunga mkono hoja.

MHE. RUTH B. MSAFIRI: Mheshimiwa Spika, kwanza naunga mkono hoja ya Waziri wa Miundombinu.

Mheshimiwa Spika, naomba nipate ufafanuzi kwa yafuatayo; kwanza, niipongeze EWURA kwa kusimamia vizuri ongezeko la bei ya mafuta Mkoani Kagera. Juzi tarehe 9 Julai, 2007 bei ilikuwa imeongezeka kwa shilingi 100/= tu, kutoka shilingi 1600/= za wakati kabla ya Bajeti na sasa Petroli/ Dizeli ni shilingi 1700/=.

Mheshimiwa Spika, pongezi hizi zina masikitiko, nauli za Mkoani zimepanda ghafla kutoka shilingi 500/= hadi 1000/=, shilingi 1000/= mpaka 1500/= na kadhalika, ili mradi kila penye usafiri imeongezwa si chini ya shilingi 500/= hadi 1000/=.

Mheshimiwa Spika, napenda Serikali inifafanulie hata kama haifanyi biashara na haisimamii tena nauli, je, inaunga mkono hali hii ya wenye kutoa huduma ya usafiri kupandisha nauli kiasi wanachotaka?

Mheshimiwa Spika, nataka Serikali ichukue wajibu wake basi itufafanulie stahili ya nauli toka kituo hadi kituo kulinganisha na bei ya mafuta. Mheshimiwa Spika, pili, nataka nijue ni lini mpango wa kuwa na meli imara na hasa mpya utakuwepo? MV Victoria sasa imechoka, imebaki inang’ara bodi tu, lakini ukweli imechoka. Inawezekana inataka ukarabati mkubwa sana ama inunuliwe mpya, tena iwe kubwa. Meli katika Ziwa Victoria ndiyo ukombozi wa wasafiri wote wa Kanda ya Ziwa hasa Kagera. Naomba nielezwe hali ya meli Victoria sasa ikoje na inatarajiwa kurudi lini katika kutoa huduma maana wananchi tunateseka sana bila MV Victoria.

Mheshimiwa Spika, nataka niwapongeze wamiliki wa ndege za Precision kwa huduma nzuri ya usafiri wa anga wanayoitoa nchini. Serikali iwapongeze, kazi ya Precision Air imepunguza udhaifu wa usafiri wa anga nchini japo ni wawekezaji binafsi. Wametusaidia sana, nawatakia heri sambasamba na Air Tanzania. Air Tanzania naitakia heri pia, lakini inunue ndege zinazofaa sasa. Nawasilisha.

101 MHE. ABBAS Z. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, katika hoja ya Waziri Mkuu nilichangia kuhusu Mbozi Road inayotoka Nyerere Road na Kawawa Road kuelekea katika uwanja mpya wa Kimataifa wa Temeke, barabara za viwandani Temeke kuwa za Kitaifa pamoja na hiyo ya Uwanja wa Taifa, kuhusu SUMATRA uwezo wake kwa Dar es Salaam ni mdogo sana kusimamia daladala za Dar es Salaam na pia nilizungumzia kuongeza fungu la barabara za Dar es Salaam kutokana na umuhimu wake.

Mheshimiwa Spika, naipongeza sana Wizara kwa barabara ya Jet Club - Vituka - Buza - Devi’s Corner hadi Mtongani. Hoja ya Waziri Mkuu Serikali imetenga shilingi milioni 450 kwa matengenezo ya barabara hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri utamke katika majibu yako, wananchi wa Yombo Temeke wasikie Mheshimiwa Waziri hoja hizo. Waziri Mkuu alisema utajibu wewe katika majibu yako.

Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia kuhusu Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kurudishwa njia zake zote za zamani na anga ya Kilimanjaro, anga hiyo irudishwe haraka kwa Air Tanzania.

Kuhusu UDA nashauri Serikali kulikabidhi kwa Jiji la Dar es Salaam ili lisimamiwe Shirika hilo kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Spika, narudia tena kumpongeza Mheshimiwa Waziri sana na Naibu Mawaziri wake wawili na Katibu Mkuu na Naibu wake kwa kazi nzuri na naunga mkono asilimia mia moja. Mheshimiwa Spika, namuomba tena Mheshimiwa Waziri awatamkie wananchi wa Yombo Temeke kwamba barabara ya Jet Club - Devi’s Corner - Mtongani imetengewa shilingi milioni 450. Hii ni barabara ambayo wapinzani huielezea sana kwa nia mbaya. Naomba kuwasilisha.

MHE. BENEDICT K. LOSURUTIA: Mheshimiwa Spika, naomba nimpongenze Waziri wa Miundombinu pamoja na Naibu Mawaziri wake wawili na wataalamu wake ukianzia Katibu Mkuu na wote walioko chini yake kwa hotuba nzuri.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Manyara ni mkoa mpya na umeomba kupatiwa barabara mpya za mkoa. Baada ya kupitia kitabu cha hotuba na kuangalia kwa makini nimegundua kuwa kuna barabara ambazo hazijaandikwa na Wiazra na tumepitisha katika Kikao cha RCC na baadaye tulituma tena Wizarani ili Waziri aweze kuidhinisha na kupandisha daraja kuwa za Mkoa.

Kuhusu Wilaya ya Kiteto, barabara kutoka Kijungu - Lengatei - Sonya mpaka Dongo ni barabara muhimu inaunganisha Mkoa wa Manyara na Mkoa wa Morogoro. Naomba iingizwe katika barabara za Mkoa wa Manyara.

Pili, kuna barabara muhimu sana ambazo ni ahadi ya Rais Banjamin Mkapa wakati akigawa Mkoa wa Arusha na Manyara. Moja ya ahadi yake na kukubaliana na

102 na Wilaya za Kiteto na Simanjiro kuhusu barabara ya kuunganisha kila makao makuu ya Wilaya na Makao Makuu ya Mkoa wa Babati.

Katika Wilaya ya Kiteto - Babati – Kimotarak, Simanjiro – Makami – Ndedo – Kibaya, Simanjiro – Babati – Kimotorak na Suhuru - Naberera Orkesmet. Naomba barabara hii iandikishwe Kisheria na kutegemewa fedha za matengenezo za kawaida.

Mheshimiwa Spika, natoa tahadhari kuwa bila kuandikishwa barabara haitaweza kupata fedha za matengenezo ya kawaida. Mara barabara itakapokamilika hapo mwanzoni itakuwa imeharibika ni mbaya sana.

Mheshimiwa Spika, ombi, naomba maelezo ya ziada kuhusu barabara hii na kama utekelezaji wake ni mgumu tunaomba ushauri wa kusudi mkoa wa Arusha na kufuta ile ahadi ya Rais. Wananchi wa Kiteto na Simanjiro wanasubiri Bajeti hii ili waweze kudaia kurudi mkoa wa Arudha.

MHE. JUMA H. KILLIMBAH: Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri wake, Katibu Mkuu na wasaidizi wake wote.

Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali kwa namna inavyoipa sekta hii ya miundombinu kipaumbele hasa kwa kuhakikisha mawasiliano yanaboreshwa kwa muda wote.

Mheshimiwa Spika, barabara ni kiungo muhimu sana katika kukuza Pato la Taifa na kuleta maendeleo kwa wananchi wa haraka.

Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii kwa ufupi nizungumzie maendeleo ya barabara ya Kati - Dodoma, Manyoni, Singida hadi mpakani Shelui. Tunashukuru Mungu kazi ya kuweka lami inaendelea lakini kazi inayoendelea si ya mwendo kasi, inaendelea kwa taratibu sana, mara nyingi contractors wanaofanya kazi katika barabara hii husimama kutokana na ukosefu wa fedha.

Mheshimiwa Spika, katika Bajeti ya mwaka jana Mheshimiwa Waziri aliahidi itakapofika Novemba, 2007 barabara ya kati itakukwa imekamilika. Ni dhahiri muda huo utafika na naamini barabara hii itakuwa haijakamilika. Tunaomba Serikali ielekeze nguvu ya mwisho ili kuondoa malalamiko hasa sisi Wabunge wa mkoa wa Singida kuiulizia Serikali juu ya barabara hii muda wote.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kipande cha Isuna hadi Manyoni cha kilomita 57 naomba Serikali, mzabuni aliyeshinda aanze kazi mara moja ili aendane na kazi inayofanywa na contractors wengine.

Mheshimiwa Spika, kadhalika nizungumzie barabara za TANROADS zilizopo Jimboni kwangu, barabara ya Shelui - Sekenke hadi Ntwika ya kilomita 21.7 zile fedha za mwaka 2005/2006 shilingi milioni 12.75 tangu wakati ule hakuna mwendelezo, ila

103 sehemu korofi iliyoathiriwa na Mto Kyenka Ng’ombe na niliwahi kwenda na Mheshimiwa Dr. Milton Mahanga alijionea hali mbaya ilivyo na alitoa maagizo kwa Meneja wa TANROADS Mkoa kutengenezwa kwa eneo hilo lakini hadi tunaingia Bajeti hii hakuna kilichofanyika na wananchi wameendelea kupata adha ya eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, nizungumzie kuhusu contractor anayetengeneza barabara toka Tumuli hadi Sekenke maarufu kama package three aitwaye CHICO, contractor huyo alikwenda kuainisha eneo la kupata kokoto na Ulemo kutokana na baruti zinavyofanya upasuaji ziliweza kuathiri nyumba za baadhi ya wananchi wakazi wa eneo hilo, wananchi waliunda Tume juu ya kushughulikia kero hiyo, pamoja na malalamiko kupelekwa kwa Mkuu wa Wilaya ambaye alithibitisha uharibifu huo na kuwa shahidi kwamba milipuko hiyo kusikika hadi Ikulu ndogo ya Kiomboi iliyopo umbali wa kilomita 27 na kuzitikisa nyumba.

Mheshimiwa Spika, majibu waliyopewa na Meneja wa Mkoa TANROADS ni ya kukatisha tamaa na hata kuonekana kwamba ni waongo na wanayo tamaa ya kuhitaji fidia kwa ulaghai. Ni kweli kabisa nyumba za wananchi wa eneo hili zimepata athari ya mipasuko kutokana na ulipuaji huo. Hivyo ningeomba Wizara iingilie kati na kuagiza TANROADS kufidia uharibifu uliojitokeza.

Mheshimiwa Spika, naomba pia wawekezaji wa mawasiliano ya simu za mikononi Vodacom mnara wa Magila uliopo kijiji cha Nguvumali, Kata ya Ndago wawe watimilifu kulingana na mkataba waliowekeana na kijiji, wafanye malipo kama ilivyokubalika wasikimbie kukacha kulipa.

Mheshimiwa Spika, naomba Wizara iendelee kuhimiza kampuni za simu za mikononi kutoa huduma zaidi kwa sehemu mbalimbali kama vile kujenga mnara eneo la Kidaru, Tulya, Ntwika, Mtekente, Ulughu, Mbelekese na kaselya ili Jimgo langu liwe na mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, kuhusu huduma ya Posta iendelee kuimarishwa maeneo ya Shelui, Ndago na Ulemo maeneo haya sasa yanafaa kupewa huduma ya Posta.

Mheshimiwa Spika, naomba Wizara ielekeze ahadi yake kama ilivyoahidi mwaka 2004/2005 juu ya kuweka lami nyepesi (otter seal) barabara inayounganisha makao makuu ya Wilaya kutoka Misigili hadi Kiomboi kilomita 21, barabara hii ni kiungo muhimu sana.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. MHE. PAUL P. KIMITI: Mheshimiwa Spika, kabla ya yote nitangulize shukrani na pongezi zangu kwa Waziri Mheshimiwa Andrew Chenge, Naibu wake wote wawili Mheshimiwa Dr. Maua Daftari na Mheshimiwa Dr. Milton M. Mahanga, chini ya uongozi wa mtendaji wa Wizara hii Dr. Enos Bukuku na wataalamu wake wote kwa maandalizi mazuri sana ya hoja hii ya Wizara.

104 Mheshimiwa Spika,maelezo aliyotoa na mwelekeo wa Bajeti hii kwa mwaka 2007/2008 ni dira tosha kuwa tunaelekea kuanza kujibu matarajio yaliyomo kwenye Ilani yetu ya Uchaguzi juu ya sera ya barabara na mawasiliano kwa ujumla.

Naomba haya nitakayoyaelezea yawe ni sehemu ya ziada ya mchango wangu kwa Wizara hii na Serikali kwa ujumla juu ya yale ninayoona yangesaidia sana kuimarisha utendaji kazi kwa Wizara na taasisi zake nyingi ambazo zimekabidhiwa kazi nzito ya Taifa hili.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa naomba Serikali iangalie upya majukumu mazito iliyopewa Wizara hii na fedha kidogo zilizotengwa kwa ajili ya majukumu yenyewe. Ni kutokana na uzito huo, baadhi ya taasisi zimekosa kabisa fedha za kujiendesha kwa kudhani kuwa zingeweza kutafuta vyanzo vyake vya mapato. Ni kutokana na hilo, nitaiomba Serikali kupitia kwa Mheshimiwa Rais, aone namna ya kuigawa Wizara hii ili barabara zibakie chini ya Wizara yake pekee. Siasa yetu sasa hivi number one ni barabara.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa barabara ni ajenda kubwa basi utashi wa kisiasa kama ulivyo katika Ilani ya Uchaguzi iendelee kuimarisha Mfuko wa Barabara. Kuendelea kutegemea Development Partners katika hili, tutashindwa kwenda sambamba na mahitaji ya Ilani. Barabara ya Kusini kwenda Lindi/Mtwara bila fedha yetu, zisingejengwa. Barabara za kati yaani Dodoma, Singida hadi Shelui bila fedha zetu zisingejengwa. Hii ndiyo sababu hata Barabara ya Kati ya Tunduma - Sumbawanga imesuasua kutokana na kusubiri wahisani.

Mheshimiwa Spika, ombi, pamoja na kwamba kuna ahadi toka MCC kuijenga barabara hii, lakini tusikae kimya, tusukume ili wananchi wa Rukwa ambao wamevulimia vya kutosha wasikate tamaa kwa ahadi lukuki za Serikali yao ambayo wanaipenda kwa kuendelea kuipigia kura nyingi kila mwaka. Pili, barabara ya kati ya Sumbawanga hadi Mpanda nayo isisubiri wahisani. Serikali yetu ianze kutenga mafungu kuanzia mwaka ujao ili barabara ya lami iendelee kutoka Tunduma, Sumbawanga, Mpanda hadi Kigoma. Tuufungue Mkoa huu. Pia barabara kuelekea Kasanga Port nayo ipewe umuhimu wa kiuchumi na majirani wa DRC. Hili najua Mheshimiwa Waziri analielewa. Ni vizuri akalisema kwa wazi kwa wana Rukwa kuwa ahadi yake aliyoitoa Rukwa tarehe 1 Juni, 2007 bado ipo pale pale.

Tatu, kwa kuwa ujenzi wa barabara ya lami kwa kandarasi mmoja unaweza kuifanya kwa kutandaza kilomita 30 kwa mwaka. Barabara ya TD – SU ina kilomita 30 hivyo ni vizuri wakawepo Makandarasi wasiopungua watatu ili waijenge kwa miaka mitatu. Ni vizuri sisi tulichelewa tukakimbizwa wakati wengine wakitembea. (We have to run while others are walking).

Kuhusu TAZARA na TRC ndiyo jicho la maendeleo ya kweli kwa wakulima na wafanyabiashara wa nchi hii. Ni vizuri Mheshimiwa Waziri akatoa maelezo ya kina kwa faida ya wananchi ili waone jitihada za Serikali yao inavyotekeleza maagizo ya Chama

105 Tawala. Mheshimiwa Waziri hakupata nafasi ya kutosha kuelezea haya kwenye hotuba kutokana na muda kuwa finyu ingawa yalikuwemo kwenye hotuba yake.

Mheshimiwa Spika, hoja ya ongezeko la bei ya mafuta limeleta mzozo mkubwa kwa kuwa wafanyabiashara wametumia mwanya huu kutapeli maamuzi ya kuongeza shilingi 100/= kwa lita na kuwafanya wao waongeze zaidi ya viwango vilivyo kubalika. Siyo vizuri Serikali ikalinyamazia na kutumia wajanja wachache wachafue hali ya hewa ya kisiasa. Serikali ikemee na kuwathibitishia wale wote wanaohusika. Lazima Serikali waiheshimu na kuiogopa inapotoa maagizo. Bado majukumu ya EWURA na SUMATRA yaanze kuonekana kwa vitendo bila kuogopa. Utawala wa sheria uwe nguzo ya utendaji wetu wa kila mara.

Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa kuona umuhimu wa kuimarisha na kukikarabati kiwanja cha ndege kilichoko Mjini Sumbawanga. Hii ni hatua muhimu kwa maandalizi ya vituo vyote vya zamani ambavyo ATC ilikuwa inatua. Tunashauri ATC ishirikiane na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege ili kuona maeneo ya viwanja watakavyoanza navyo mara tu ratiba ya kwanza itakapoanza kufanya kazi. Sumbawanga ipewe kipaumbele kutokana na umbali na upembezoni mwa nchi hii hata kiusalama ni kiwanja muhimu sana. Mheshimiwa Spika, karibu kipindi kilichopita cha mwaka 2006/2007 Wizara hii pamoja na ile ya Mipango, Uchumi na Uwezeshaji ilikuwa na malengo yafuatayo:-

Kwanza kujenga uwezo wa makandarasi wazalendo katika kutoa huduma bora za ujenzi na ukarabati wa barabara na pili kuhamasisha wananchi vijijini na hasa kina mama ili washughulikie kazi za barabara katika maeneo yao ili kujipatia kipato (Labour Intensive Program).

Mheshimiwa Spika, hivi katika maeneo haya nini kimefanyika? Mbona bado makandarasi wetu wanaendelea kusuasua kwa ukosefu wa vifaa? Mbona bado wafanyakazi wengi barabarani hata kwa kazi za kupalilia hawaonekani? Kuna namna? Ni vizuri suala hili likapewa msukumo wa kutosha ili kina namna nao wasionekane kuachwa nyuma. Jiji la Dar es Salaam limefanikiwa kwa hilo!

Mheshimiwa Spika, mengi yameguswa na taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu Mheshimiwa Alhaj Mohamed Missanga kwa niaba yetu. Nipende tu kuwashukuru viongozi wote watendaji wakuu wa mamlaka na taasisi zote zilizo chini ya Wizara hii kubwa kwa jinsi walivyoshirikiana nasi katika kazi na Kamati ya Kudumu ya Bunge. Wanastahili pongezi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja hii kwa hali yote.

MHE. KAIKA S. TELELE: Mheshimiwa Spika, kwanza naunga mkono hoja. Pili, nampongeza Waziri Mheshimiwa Andrew Chenge, Naibu Waziri wake Mheshimiwa Dr. Milton Mahanga na Mheshimiwa Dr. Maua Abeid Daftari, Katibu Mkuu wa Wizara ya timu nzima ya wataalam kwa kuandaa Bajeti nzuri inayolenga kumkomboa Mtanzania kimawasiliano yaani kwa barabara, simu hususan za mikononi (mobile phones).

106 Mheshimiwa Spika, nataka niamini Mheshimiwa Waziri bila shaka yoyote kuwa sasa barabara ya Mto wa Mbu - Engaresero - Loliondo sasa itajengwa kwa kiwango cha lami kwa sababu zifuatazo:-

Kwanza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete aliwaahidi hivyo wana Ngorongoro wakati wa ziara yake Wilayani Ngorongoro tarehe 20 Machi, 2007, pili, Waziri Mkuu Mheshimiwa , kwa nyakati tofauti pia alitoa ahadi hiyo kwa wananchi wa Jimbo lake la Monduli ambamo barabara hiyo inapita yaani Engaruka na Suleki, tatu, Wizara kupitia Wakala wa Barabara Arusha (TANROADS) walishafanya upembuzi yakinifu ya barabara hiyo na matokeo ni mazuri sana kutokana na manufaa ya kiuchumi wa kijamii yatakayopatikana baada ya ujenzi wa barabara hiyo na nne, haiba na utashi (commitment) wenu wenyewe watendaji wakuu wa Wizara ya Miundombinu.

Mheshimiwa Spika, naomba sana kazi ya barabara hii ianze mwaka huu wa fedha 2007/2008. Pia makandarasi wawili au watatu wenye sifa na vifaa wapewe kazi hii ili imalizike haraka. Pia naomba msiwasikilize wapinzani wa mradi huu wa maendeleo kwa hoja za mazingira na immigration ya wanyamapori hususani Nyumbu.

Mheshimiwa Spika, vile vile Mheshimiwa Rais wakati wa ziara yake Ngorongoro aliagiza Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na Halmashauri itengeneze barabara ya Olbalbal - Nasira Rock - Piyaya hadi Loliondo ili iweze kupitika wakati maandalizi ya barabara ya lami ya Ngaresero - Loliondo yanaendelea. Naomba msukumo wa Wizara katika hili.

Mheshimiwa Waziri kama ndugu, rafiki na mtani, naomba msaada wako binafsi katika hili kwamba, ninayo barabara ya kilomita 18 kutoka Masusu hadi Kijiji cha Pinyinyi iliyoko Lake Natron. Barabara hii ilijengwa na Hayati Edward Moringe Sokoine mwaka 1984. Wakati kazi ikiendelea aliaga dunia kwa ajali ya gari. Tangu kifo chake kazi hiyo ilisimama na haikuendelea. Wananchi wa Pinyinyi/ Masusu watakuenzi kama Sokoine ukiwatengenezea barabara hiyo. Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro imeshindwa kutengeneza kwa sababu ya mawe makubwa ya Bonde la Ufa.

MHE. ADAM K.A. MALIMA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote naomba nianze kwa kumpongeza ndugu yangu, mwanangu Mheshimiwa Andrew Chenge, Waziri wa Miundombinu. Kuna tofauti kubwa sana baina ya kiwango cha Bajeti ya Wizara hii mwaka huu na zile za miaka iliyopita na bila shaka ni kwa sababu ya uongozi wake makini wa Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, aidha, naomba niwapongeze Mheshimiwa Dr. Maua Abeid Daftari na Mheshimiwa Dr. Milton Mahanga, Naibu Mawaziri wa Wizara hii na ndugu yangu na mwalimu wangu Katibu Mkuu Dr. Enos Bukuku.

107 Mheshimiwa Spika, kila ninaposimama kuchangia au ninapopata nafasi ya kuchangia kwa maandishi kama hivi nimekuwa nahimiza sana umuhimu wa kipekee wa sekta hii ya miundombinu kwa maendeleo ya kiuchumi na ya kijamii kwa Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, sera nzima ya kuondoa umaskini (MKUKUTA) na sura zingine husika ambazo huibeba sera ya MKUKUTA unategemea moja kwa moja uwekezaji makini katika sekta hii. Naomba nitambue mchango wa sekta binafsi na uwekezaji unaofanywa na upande wa mawasiliano na uchukuzi, haswa mawasiliano. Naomba nitambue mafanikio mazuri yanayoonekana katika kampuni ya umma ya TTCL na huduma nzuri nyingi zinazopatikana huko. Mimi ni mteja wa TTCL wa simu za mezani, simu za mkononi na TTCL Broadband Internet ambayo ni huduma nzuri na yenye viwango.

Mheshimiwa Spika, naomba Waziri anihakikishie kwamba Wizara yake itaboresha uongozi na uwekezaji TTCL ili iweze kuhimili na kuwa kiongozi katika ushindani ndani ya biashara hii.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa mawasiliano naomba niipongeze sana Serikali kwa hatua yake ya kuirejesha Air Tanzania, katika mikono ya wananchi. Naomba hata hivyo niseme kuwa kuna wakati katika historia yake huduma na viwango vingine kama kwenda kwa ratiba (punctuality) yalikuwa ni matatizo makubwa ya shirika hili. Aidha, naomba niseme kwamba tusichukie ubia na mashirika makubwa kwa kuwa ndoa ya ATC na SAA imeishia kwenye talaka mbaya. Naiomba ATC iendelee kutafuta mashirika mengine yenye nia ya kuingia ubia na ATC. Napendekeza tutazame mashirika kama Malaysia, Singapore Airlines, Air India na kadhalika. Naomba tusijiunge kwa makampuni ya Ulaya tu.

Mheshimiwa Spika, pili, naomba Waziri anijibu kuhusu ukodishaji wa ndege aina ya Boeing 737 - 200. Ni kweli tumekuwa tunatumia ndege aina hii tangu mwaka 1977. Lakini ndege hii sasa imepitwa na wakati na ingekuwa vema tukakodi (ATC) ndege kama hiyo aina ya Boeing 737- 300 au juu zaidi, ambazo tuliwahi kukodisha kwenye miaka ya mwisho ya 1990. Aidha, naomba maelekezo, kwa nini baada ya kurejesha njia za Mashariki ya Kati na Ulaya, kwa nini sasa tusikodishe ndege kubwa zaidi kama Boeing 757 au Boeing 767 ambazo zina uwezo wa kubeba abiria wengi zaidi na kwa masafa marefu zaidi.

Mheshimiwa Spika, naomba maelezo kuhusu mikakati ya kuboresha fleet na inflight service na mafao ya crew.

Mheshmiwa Spika, naomba nizungumzie suala la ndege za Serikali. Hoja ya kuuza G5 Gulfstream si hoja yenye mtazamo wa maendeleo. Badala ya kuuza ndege hii, mimi naomba fleet ya ndege za Serikali ipanuliwe japo kwa ndege zingine mbili, moja yenye capacity ya 12 seater na nyingine yenye uwezo wa abiria 19 hadi 25 (Inclusive Configuration ya VIP seating japo mbili.

108 Mheshimiwa Spika, ndege hizi zizingatie uwezo wa kutua kwenye viwanja vingi zaidi ya Tanzania ili viongozi wa Serikali kuanzia Rais, Waziri Mkuu na Mawaziri wasafiri wakiwa wameambatana na wasaidizi wataalamu. Huko zamani Serikali ilikuwa na ndege aina ya beechcraft ambazo ni ndege nzuri na zenye hadhi. Tukinunua ndege mbili aina ya beechcraft au inayofanana hata zenye umri mdogo (hadi miaka 15) ambao ni umri mdogo kwa ndege, naamini kwamba itakuwa ni hatua nzuri ya kuimarisha usafiri wa uhakika na wa salama wa viongozi wetu.

Mheshimiwa Spika, naomba nihakikishiwe kwamba marubani na wahudumu wa viongozi ndani ya ndege za Serikali (crew) watatazamwa kwa jicho zuri zaidi. Kusafiri kwenye G5 au F28 na viongozi iwe ni experience kama kwa wenzetu kupanda Air Force One.

Mheshimiwa Spika, naomba nizungumzie suala la barabara. Naomba Waziri anihakikishie kwamba anakubaliana na mimi kwamba pamoja na umuhimu wa kukarabati barabara kuu zote ni lazima tukubali kwamba uwekezaji kwenye barabara hauwezi ukafanywa kila sehemu kidogo kidogo. Tufanye tathmini ya kina ya kiuchumi (economic evaluation) ili tuanze na barabara chache zenye kipaumbele (priority areas) cha uwekezaji katika barabara hizi zenye kipaumbele kwa uchumi.

Kwanza, barabara yenye umuhimu kuliko zote Tanzania ni Dodoma - Manyoni - Itigi - Tabora - Kigoma. Barabara hii ikikamilika itajenga barabara zingine kutokana na mapato yatokanayo, pili, barabara ndogo sana kutoka Daraja la Mkapa Ndundu hadi Somanga. Maisha ya Watanzania wa kuanzia Mkuranga hata Mtwara, Newala, Masasi zinakwamishwa na kilomita 60 tu. Maelezo ya kwamba yanajirudia kila mwaka hayatusaidii. Naomba maelezo kwa nini kilomita sitini hizi zisimalizike kabla ya Oktoba 2009.

Tatu, naomba Waziri anipe maelezo kuhusu uwekezaji unaofanywa (unaopangwa) kufanywa kwenye reli ili mataruma yawe na uwezo wa ratili 120. Uwekezaji huu lazima ufanywe na Watanzania wenyewe. Naomba maelezo kama kwenye mkataba na mwekezaji wa TRC (Rites Group of India) una kipengele cha kusitisha mkataba (exit clause) ikiwa baada ya miaka mitatu wataonekana hawatekelezi makubaliano.

Nne, naomba kufahamishwa na Waziri wa Miundombinu kama kodi ya shilingi 200 kwa kila lita ya mafuta itatumika kwa ajili ya kutengeneza na kukarabati barabara tu. Kwenye nchi za wenzetu kodi hii inahusishwa na matumizi ya barabara au Road Access Fuel Levy. Je, pesa hizi zina matumizi mengine yasiyo matengenezo ya barabara? Naomba maelezo ya kina.

Tano na mwisho, naomba Serikali, Wizara hii inihakikishie itatengeneza orodha ya wahandisi wote wa sekta ya umma na kwa kushirikiana na TAMISEMI wafanye tathmini ya usimamizi na utekelezaji wa miradi ya barabara ndani ya Halmashauri. Kwa kuwa fedha nyingi mno zinapitia kwenye miradi hii.

109 Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

MHE. PROF. MARK J. MWANDOSYA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza kwa dhati kabisa Mheshimiwa Andrew Chenge, Waziri wa Miundombinu kwa hotuba yake nzuri na ya kina na kwa kuiwasilisha hoja yake kwa ufanisi na ufasaha mkubwa. Naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Spika, nawapongeza vile vile Naibu Mawaziri, Mheshimiwa Dr. Maua Abeid Daftari na Mheshimiwa Dr. Milton Mahanga. Kuwasilishwa kwa hoja hii kunatokana na mchango mkubwa wa Naibu Mawaziri hawa. Wamemsaidia sana Mheshimiwa Andrew Chenge katika kutoa ufafanuzi mzuri na wa kina, katika majibu ya maswali ya Waheshimiwa Wabunge. Uwasilishaji wa hoja hii ni matokeo vile vile ya kazi ya watendaji wakiongozwa na Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu, Wakuu wa Idara Wizarani na Wakurugenzi Wakuu wa Taasisi, Wakala, Kampuni na Mashirika yaliyo chini ya Wizara na sekta binafsi, wamefanya kazi kubwa sana. Nimefuatilia kwa makini maendeleo ya sekta ya mawasiliano. Nawapongeza kwa dhati kabisa.

Mheshimiwa Spika, baada ya utangulizi huo, mchango wangu utajikita katika maeneo si zaidi ya matatu, kwa mtiririko ufuatao; ujenzi wa kiwanja cha ndege cha Songwe; barabara ya Katumba - Tukuyu na barabara za TANROADS na zile za Wilaya.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa kiwanja cha ndege cha Songwe, kwa muda wa zaidi ya mwaka shughuli zinazohusu ujenzi zilisimama, ingawa wananchi wengi walikata tamaa na kudhani Serikali imeuacha mradi huu. Sisi Wabunge wa Mbeya tuliwaeleza wananchi kwamba kazi hazijasimama isipokuwa kutokana na kubadilisha ufadhili wa mradi na kukamilisha awamu mbili za kwanza imebidi usanifu wa awamu ya tatu ufanyike na kandarasi mpya ianze, wametuelewa, tunaamini kama ilivyo katika hotuba, awamu ya tatu itasimamiwa ipasavyo ili kiwanja kianze kutumika kabla ya mwaka 2009. Nampongeza Wakala wa Viwanja vya Ndege kwa kuchukua changamoto kubwa ya kuanza na kusimamia ujenzi wa kiwanja hicho.

Mheshimiwa Spika, changamoto kubwa kwa Mkoa wa Mbeya na Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ni kuwa na mipango ya matumizi kamili ya kiwanja cha Songwe. Hakika kiwanja kitakuwa chimbuko la maendeleo ya kasi ya eneo hilo. Nashauri Wizara, kwa kushirikiana na mkoa husika na sekta za kilimo, viwanda, mipango, biashara na utalii, kuanzisha Songwe Development Forum ili kukitangaza kiwanja cha Songwe na fursa zitakazotokana na kuwepo kwa kiwanja hiki.

Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Katumba – Tukuyu, barabara hii ni uti wa mgongo wa uchukuzi katika Wilaya ya Rungwe. Ni barabara muhimu katika uchumi wa Mbeya hasa kutokana na usafirishaji wa mazao ya kilimo na madini. Ni kutokana na umuhimu huu Mheshimiwa Rais ameahidi barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami. Baada ya kusahaulika kuwekwa katika orodha ya ahadi za Rais yeye mwenyewe amethibitisha kwamba ametoa ahadi hiyo.

110 Mheshimiwa Spika, miaka miwili iliyopita kampuni ya Interconsult ilifanya upembuzi wa awali au upembuzi yakinifu wa barabara hii. Tulitarajia hatua hiyo ingepelekea utekelezaji wa awamu nyingine, kuelekea utekelezaji wa ahadi ya Mheshimiwa Rais. Lakini katika jedwali la hotuba ya Waziri, barabara hii haijatengewa fedha hata kidogo. Tutashukuru kupata maelezo ya Mheshimiwa Waziri kuhusu mpango wa utekelezaji wa azma hii ya Serikali itokanayo na ahadi ya Rais lakini kubwa zaidi kutokana na umuhimu wa barabara hii katika mazingira ya mvua nyingi za Rungwe.

Mheshimiwa Spika, nimepitia jedwali kwa haraka sijaona fedha zilizotengwa kwa matengenezo ya kawaida ya barabara hii. Kutokana na mvua nyingi zinazonyesha (miezi 10 kwa mwaka) barabara imeharibika sana.

Mheshiwa Spika, namalizia kwa ushauri kuhusu uhusiano kati ya TANROADS na Halmashauri za Wilaya. Uzoefu wangu hasa katika maeneo mengi ya Mkoa wa Mbeya na sehemu nyingine barabara za Wilaya zinakuwa nzuri zaidi na bora kuliko barabara za Mkoa zilizo katika Wilaya. Uangaliwe uwezekano wa TANROADS inapowezekana kukasimu usimamizi na uangalizi wa barabara za Mkoa kwa Wilaya husika au kuboresha ushirikiano katika usimamizi. Ni rahisi kwa Madiwani na viongozi wa Wilaya kusimamia barabara hizi kwani wanawajibika katika maeneo yao haraka zaidi kuliko Makao Makuu ya Mikoa.

Mwisho, kama Wizara ilivyolishughulikia suala la vivuko, Kivuko cha Kigamboni na vingine, nashauri Wizara iangalie uwezekano wa kununua meli mpya kwa ajlili ya uchukuzi Ziwa Nyasa. Ni rahisi kwa sekta binafsi kushughulikia suala hili, wajibu huu ni wa Serikali, tatizo ni kubwa nalielewa. Nimesafiri katika Ziwa hilo. Tuepukane na balaa inayotungoja.

Mheshimiwa Spika, kwa hitimisho narudia kumpongeza Mheshimiwa Waziri na sekta ya miundombinu. Naunga mkono hoja hii.

MHE. BERNADETA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Spika, nampongeza sana Waziri wa Miundombinu kwa hotuba yake nzuri sana. Nawapongeza Naibu Mawaziri wote wawili na watendaji wote wa Wizara walioandaa Bajeti hii. Vile vile napongeza kwa kazi kubwa na nzuri na mafanikio yaliyopatikana mwaka jana. Pia naishukuru Serikali kwa kutambua kuwa miundombinu bora ni kichocheo kikubwa katika kuleta maendeleo na hivyo kuipa sekta hii kipaumbele. Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali kwa juhudi iliyoonyesha katika kuboresha mtandao wa barabara mkoani Kagera. Pamoja na hayo napenda kuikumbusha Serikali ahadi ya Rais aliyotoa wakati wa uchaguzi ya kutengeneza barabara ya Kyaka - Bugene kwa kiwango cha lami. Bajeti mbili zimepita bila kuipangia barabara hii fedha za kutimiza azma ya Rais. Je, ni lini barabara hii itaanza kutengenezwa kwa kiwango cha lami?

Naipongeza Serikali katika juhudi yake inayoweka kwenye kujenga barabara ya Kagoma - Rusahunga, Kyamyorwa - Buzilayombo, Buzilayombo - Geita. Ningependa

111 kujua nini hatma ya kipande cha barabara ya Biharamulo - Bwanga? Ni lini kipande hiki kitatengenezwa kwa kiwango cha lami?

Mheshimiwa Spika, mara nyingi barabara nyingi hufanyiwa matengenezo ili ziweze kupitika mwaka mzima. Lakini barabara zinazopita kwenye milima na miinuko kila mvua zikinyesha barabara hizo huharibika tena. Napendekeza kwa Serikali barabara zinazopita kwenye milima hususan kwenye barabara ya Muhutwe - Kamachumu, barabara ya Kaisho - Murongo kwenye milima ya Rwabunuka na kwenye mlima ulio kwenye barabara ya Kyaka – Kihanga - Kayanga, sehemu hizi za barabara napendekeza zitengenezwe kwa kiwango cha lami ili kuokoa fedha zinazopotea kwa sababu ya barabara hizi kuharibika sehemu hizi za milima.

Mheshimiwa Spika, usafiri wa haraka kutoka Mwanza kwenda Bukoba ni wa ndege. Kiwanja cha ndege kilicho Bukoba ni kidogo, ndege kubwa haziwezi kutua na hakikutengenezwa kwa lami. Ndege pekee inayokuja Bukoba ni ndege ndogo ya Precission Air. Chama cha Kimataifa cha Kampuni za Ndege (International Air Transport Association - IATA) iitwayo IAT Operational Safety Audit (IOSA) imekataza kurushwa kwa ndege ndogo za aina kama zinazokuja Bukoba za Let 410.

Mheshimwa Spika, Precision Air wako tayari kuleta ndege kubwa aina ya ATR 42 lakini ndege hii haiwezi kutua kwenye kiwanja cha Bukoba kwani uwanja wa Bukoba ni kilomita 1.2, wakati zinahitajiika kilomita 1.6. Precision Air itaziondoa hizi ndege zake hivi karibuni. Hivi ukizingatia na kuwa hata meli ni mbovu, nini hatma ya wakazi wa Bukoba? Naomba Mheshimiwa Waziri atoe tamko ni lini uwanja wa ndege wa Bukoba utapanuliwa. Mheshimiwa Spika, mwisho, nilishachangia kwenye hotuba ya Waziri wa Fedha kuwa ili kuimarisha miundombinu ya usafiri majini, naomba tena mitandao ya simu zote, ifanye kazi katikati ya Ziwa Victoria.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.

MHE. GODFREY W. ZAMBI: Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi kumpongeza Waziri wa Wizara ya Miundombinu, Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu na wataalamu wote wa Wizara kwa kuandaa hotuba nzuri sana ya Bajeti kwa mwaka 2007/2008. Hata hivyo nina maoni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), kwanza napenda kuishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuvunja Mkataba baina ya Serikali na Shirika la Ndege la Afrika ya Kusini. Kimsingi mkataba baina ya pande hizo mbili haukuwa wa haki kwa upande wa Serikali ya Tanzania kwa sababu Shirika la Ndege la Afrika ya Kusini liligeuka kuwa mshindani wa ATCL badala ya kuwa mbia. Ombi au ushauri, ili Shirika letu jipya la Ndege Tanzania liweze kustawi na kufanya vizuri, basi Serikali iwalazimishe watumishi wake wote wanaosafiri ndani na nje ya nchi kwa usafiri wa ndege, watumie huduma ya Shirika letu la Ndege la Tanzania. Iwe ni kosa kwa mtumishi wa Serikali kusafiri na ndege za mashirika mengine katika sehemu zote

112 ambako ATCL inakwenda. Serikali ya Kenya ilishachukua hatua kwa kuwataka watumishi wote wa Serikali yake wawe wanasafiri kwa Shirika lao la Ndege yaani KQ.

Mheshimiwa Spika, ukamilishaji wa kiwanja cha ndege cha Songwe, Mbeya. Kiwanja hicho kilianza kujengwa takribani miaka mitatu iliyopita bila kukamilika. Kwenye hotuba ya Bajeti ya mwaka 2006/2007 tuliambiwa kwamba ujenzi wa kiwanja hicho ungekamilika mwaka 2008. Hata hivyo mwenendo wa ujenzi wa kiwanja hicho hauonyeshi kama kweli Serikali imedhamiria kumaliza ujenzi wa kiwanja hicho kama ilivyoahidi. Aidha, pesa iliyotengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa kiwanja hicho, yaani shilingi bilioni 5.3 haionyeshi kama pesa hiyo itatosha kukamilisha ujenzi wa kiwanja hicho.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali itoe tamko rasmi hivi ni lini hasa, Wabunge na wananchi wa Mkoa wa Mbeya na wananchi wa Nyanda za Juu Kusini wawe na hakika kwamba kiwanja hicho kitakamilika kujengwa? Mheshimiwa Spika, napenda pia kuishauri Serikali na Wizara kwa ujumla wafikirie upya kuhusu ujenzi wa jengo la kupumzikia kufikia abiria katika kiwanja cha ndege cha Songwe. Kwa kweli jengo la abiria ni dogo sana na haliendani kabisa na kiwanja chenye hadhi ya Kimataifa na hasa katika karne hii ya 21 ya sayansi na teknolojia.

Mheshimiwa Spika, matumizi ya treni mijini (city trains). Pamoja na mipango mizuri ya Serikali katika kutatua tatizo la usafiri jijini Dar es Salaam bado hakuna mpango wowote wa matumizi ya treni mijini hasa Jijini Dar es Salaam. Jambo hili limewahi kuzungumzwa sana huko nyuma, haijulikani utekelezaji wake unaishia wapi. Kwa mfano, reli ya kutoka Ubungo kupitia Tabata, Buguruni hadi Mjini na reli ya TAZARA kutoka Yombo Vituka, Kiwalani, Temeke hadi Bandarini Dar es Salaam kungepunguza sana msongamano wa gari mjini yaani city centre.

Mheshimiwa Spika, pamoja na mipango mingine ya kuboresha usafiri jijini kama Waziri alivyolieleza Bunge hili, bado naishauri Serikali kwa nguvu zangu zote kwamba matumizi ya usafiri wa reli mijini ni muhimu sana hasa ukizingatia kwamba ongezeko la watu mijini na hususan Dar es Salaam ni kubwa sana.

Mheshimiwa Spika, UDA. Naomba pia niishauri Serikali iendelee kuisaidia Kampuni ya Usafiri Dar es Salaam (UDA) ili iweze kujiimarisha zaidi na kwa hiyo, kufanya kazi zake vizuri. Bahati mbaya sana kwenye hotuba ya Waziri sijaona kama kuna mpango wowote wa kuisaidia UDA.

MHE. KHADIJA S. AL-QASSMY: Mheshimiwa Spika, kwanza sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia kuwa mzima na kuweza kuchangia hoja hii iliyoko mbele yetu. Vile vile napenda kumpongeza Waziri na Waziri Kivuli kwa hotuba zao zilizojaa ufasaha na kuziwasilisha vizuri.

Mheshimiwa Spika, naanza kuchangia hoja hii kwa kuanzia na nyumba za kisasa ambazo wananchi wengi tumekodi. Nyumba zile kwa kweli finishing yake ni mbaya

113 kiasi kwamba wananchi tunapata taabu sana kuhusu mabomba, masinki, ma-flash, madirisha na milango. Kwa kweli kila siku sisi tuko maofisini kutafuta mafundi kiasi kwamba inafika mahali unajuta. Tunaiomba Serikali inapoingia mikataba ya ujenzi lazima kuwe na watu maalumu wanaofuatilia ili kuhakikisha nyumba hizo zina viwango vizuri ili kuwaondolea adha wananchi. Vile vile tunaiomba Serikali inapoanza kujenga miji mipya ihakikishe inaweka miundombinu mizuri kwa mfano barabara kwani ni usumbufu mvua zikinyesha magari yanakwama na waweke taa za nje za barabarani. Vile vile tunaiomba Serikali igawe viwanja katika maeneo hayo ili watu waweze kujenga mahitaji muhimu kama misikiti, makanisa, maduka, zahanati na kituo cha polisi ili kuwapunguzia wananchi usumbufu wa kufuata mahitaji muhimu mjini.

Mheshimiwa Spika, pili, napenda kuipongeza Serikali kwa kuvunja mkataba na Afrika Kusini kuhusu ATCL, ni faraja kubwa kwa Watanzania. Vile vile naipongeza Serikali kwa kuchagua bodi mpya ambayo nina hakika watu wote waliochaguliwa wana uwezo na watatuletea matumaini mapya Watanzania. Lakini la kusikitisha zaidi katika sekta hii Serikali haikutoa hata shilingi moja katika Bajeti hii na kama tunavyojua pesa ndiyo huzaa pesa, je, Serikali kweli iko serious na jambo hili?

Mheshimiwa Spika, nilidhani Serikali itakuwa serious katika hili na kwenda kwa mwendo wa kasi ili kuwaondolea wananchi adha hasa Wazanzibar ambao wanapata taabu kuhusu kusafiri nje kwa direct flight mpaka waende Dar es Salaam ukizingatia Zanzibar inawafanyabiashara wengi. Kwa hiyo, tunaona ATCL itakuwa mkombozi mkubwa. Naiomba Serikali ifanye kila linalowezekana ili kuiwezesha ATCL kupanga safari za nje.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Wakala wa Viwanja vya Ndege, kwa kweli naomba waboreshe miundombinu kwani hali ya kiwanja hairidhishi kabisa hasa wakati wa mchana ambapo karibu ndege nyingi zinatua na convey belt ziko mbili tu, vurugu ni kubwa kiasi kwamba unapata taabu sana katika kupata mizigo.

MHE. ALI KHAMIS SEIF: Mheshimiwa Spika, licha ya mtandao wa TTCL kuenea karibu nchi nzima kuna fununu kampuni hiyo kubinafsishwa ambapo mara nyingi wafanyakazi wanaopunguzwa hupata usumbufu mkubwa wa kulipwa mafao yao. Je, kama ni kweli kampuni hiyo inataka kubinafsishwa itakuwa lini na nini hatma ya wafanyakazi wakatakopunguzwa?

Mheshimiwa Spika, nchi yetu hivi sasa zipo kampuni nyingi za simu za kiganjani, lakini kuna uzoefu mara nyingi sekta binafsi kutowasomesha wafanyakazi. Ni kweli biashara hii sasa ni huru lakini Serikali haioni kuwa umefika wakati sasa kuzishawishi kampuni hizo kuanza kuwasomesha wananchi ili waendelee kupata taaluma inayokwenda na wakati?

Mheshimiwa Spika, ninavyokumbuka Shirika la Ndege la ATCL lilianzishwa baada ya kufa Shirika la Ndege la Afrika ya Mashariki (EAA) ambapo Zanzbar ilikuwa na hisa kwenye Shirika hilo. Katika uongozi wa juu wa ATC wa sasa sijabahatika kusikia

114 Mzanzibar kuwemo katika uongozi. Kama maelezo yangu ni sahihi naomba katika safu ya uongozi wa ATCL nitajiwe Wazanzibar waliomo na wana nafasi gani.

Mheshimiwa Spika, sisi ni Watanzania kwa hiyo maisha ya Watanzania popote walipo yana umuhimu ule ule. Leo iweje meli ya MV Safari iliyokuwa ikifanya safari baina ya Dar es Salaam na Mtwara kuzuiwa bandarini kwa sababu ya kuwa na injini moja iruhusiwe kuchukua abiria baina ya Unguja na Pemba. Nadhani maisha ni muhimu kwa wananchi wote na kilichokuwa hakifai kwa Tanzania Bara pia hakifai kwa Tanzania Zanzibar. Ahsante.

MHE. RICHARD S. NYAULAWA: Mheshimiwa Spika, naomba nianze mchango wangu kwa kuwapongeza Waziri Mheshimiwa Andrew Chenge, Naibu Mawaziri, Mheshimiwa Dr. Maua Abeid Daftari na Mheshimiwa Dr. Milton Mahanga, Katibu Mkuu, Dr.Enos Bukuku na wataalamu wote wa Wizarani na wale wa Mkoa wa Mbeya kwa kazi nzuri ya kutayarisha mipango na mikakati ya utekelezaji ya mwaka 2007/2008 na Bajeti yake na kuiwasilisha Bungeni kwa umahiri. Bajeti ni nzuri na mimi naunga mkono kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu uko katika maeneo matatu. Kwanza, utaratibu wa Bajeti na utekelezaji. Katika Bajeti kuna utengaji wa fedha kwa ajili ya construction, preventive maintenance na spot maintenance. Ukifuata utaratibu huu wa Bajeti kwa barabara mbaya na zisizo na lami utengaji huu hauna maana kubwa wakati wa utekelezaji wa ujenzi au matengenezo kwa kuwa barabara nzima ni mbaya zinazohitaji matengenezo.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, barabara ya Mbalizi - Utengule kwa Mbeya Vijijini. Fedha zilizotengwa ni kama ifuatavyo, preventive maintenance shilingi 30,000,000/= construction shilingi 150,000,000/= na bridge shilingi 75,000,000/= jumla ni shilingi 525,000,000/= au barabara ya Isyonje – Kikondo, preventive maintenance shilingi 300,000,000/=, spot maintenance shilingi 514,000,000/= jumla ni shilingi milioni 351.4 kutokana na mchanganuo huu na ubaya wa barabara itakuwa vizuri endapo fedha zote zitatumika kwenye ujenzi mzuri, bora na uliokamilika kwa sehemu tu ya barabara. Fedha wakati wa utekezaji wa ujenzi zisigawanywe kama ilivyo kwenye mafungu. Fedha hazitatosha.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mbalizi - Itumba/Ileje imetengewa shilingi 70.7 ambazo ni ndogo ukilinganisha na urefu, ubaya na umuhimu wa barabara hii. Naomba fedha ziongezwe ili kujenga barabara hii yenye uwezo wa kusafirisha mazao mengi na abiria wengi wa Ileje na Mbeya Vijijini. Aidha, naomba uchambuzi yakinifu ufanyike ili kuona uwezekano wa kujenga barabara ya lami kutokana na uchumi uliopo na faida au manufaa yatakayopatikana.

Mheshimiwa Spika, barabara ya lami ya Uyole - Songwe imetengewa fedha nyingi ukilinganisha na hali halisi ya barabara hii. Fedha hazitoshi kwa upanuzi wa barabara lakini ni nyingi kwa ajili ya preventive au spot maintenance. Naomba fedha za

115 ziada za barabara hii zingetumika kwa kuongeza ujenzi wa barabara ya Mbalizi - Itumba/Ileje kama nilivyopendekeza hapo juu. Naomba kuunga mkono hoja.

MHE. ESTHERINA J. KILASI: Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja ya Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu kwa asilimia mia moja. Nawapongeza Waziri, Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu na wataalamu wote wa Wizara ya Miundombinu kwa hotuba nzuri sana. Nina ya kuchangia yafuatayo:-

Kwa kuwa barabara ya Igawa – Rujewa – Madibira – Mafinga - Kinyanambo uko kwenye mpango wa kutengenezwa kwa kiwango cha lami na kwa kuonyesha umuhimu wa barabara hii, imewekwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2005 ya CCM na ni imani ya wananchi na Mbarali kuwa ndani ya miaka hii mitano itakuwa imetengenezwa kwa kiwango cha lami. Lakini cha kushangaza ni kuwa imekuwa ikiwekewa kiasi cha kutengeneza sehemu korofi tu kwa kiasi kisichozidi 100,000,000/= kati ya 70,000,000/= hadi 100,000,000/=.

Naomba kujua ni lini mpango wa lami utaanza? Feasibility study, designing vyote vimefanyika, tatizo ni nini? Angalau madaraja basi yaanze kutengenezwa. Kuunganisha Makao Makuu ya Wilaya na barabara kuu ni ahadi ya Serikali ya muda mrefu sana. Nimekuwa nikiomba barabara ya Igawa - Rujewa yenye urefu usiozidi kilomita tano, kutoka barabara kuu mpaka Makao Makuu ya Wilaya ya Mbarali itengenezwe kwa kiwango cha lami, lakini kimekuwa ni kitendawili mpaka sasa. Hali ya barabara hii ni mbaya sana na imekuwa ikitumia shilingi milioni hamsini kila mwaka kuifanya ipitike, naomba Wizara kwa hili itilie kipaumbele ili kupunguza gharama ya matengenezo madogo madogo ambayo hayaondoi tatizo kwa kipindi cha kudumu.

Mheshimiwa Spika, mwisho, naomba kutoa shukrani zangu kwa Naibu Waziri, Mheshimiwa Dr. Maua Abeid Daftari kwa kusikia kilio cha wananchi wa Kata ya Madibira waliokaa bila mawasiliano ya simu kwa muda mrefu kwa kusaidia kwa nguvu zote na sasa wana mawasiliano ya simu za mkononi, mtandao wa Celtel.

Mheshimiwa Spika, namshukuru vile vile Naibu Waziri Mheshimiwa Dr. Milton Makongoro Mahanga alipotembelea Kata hiyo hiyo ya Madibira na kukuta daraja limekata mawasiliano ya vijiji viwili akishirikiana na mimi na kuhakikisha TAMISEMI wanatoa shilingi 36,000,000/= za kutengeneza daraja ambazo tumezipata na zimefanya kazi. Nawatakia kazi njema wote Mheshimiwa Andrew Chenge, Waziri wa Miundombinu na Katibu Mkuu Ndugu Enos Bukuku na wataalamu wote.

MHE. ANIA S. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia kwa maandishi hotuba ya Waziri wa Miundombinu kuhusu Mpango wa Maendeleo na Makadirio ya Matumizi ya fedha kwa mwaka 2007/2008. Pia napenda kumpongeza Waziri na Naibu Mawaziri na wataalamu wa Wizara.

Mheshimiwa Spika, ningependa Serikali iangalie sana ujenzi wa nyumba zinazoendelea kujengwa hivi sasa na Wizara hii kwa ajili ya viongozi na watumishi wa Serikali na wananchi kwa jumla. Nyumba hizi mfano, nyumba za kisasa zilizojengwa na

116 Jeshi la Kujenga Taifa Dodoma zina matatizo makubwa ya vyoo hafifu, mifereji ya maji safi inang’oka ovyo, hata vifaa vilivyowekwa ni hafifu vya umeme na ningependa kuwe na kamati maalumu ya kufuatilia ujenzi wa nyumba hizi ili kuzifanya kuwa na hadhi inayotakiwa badala ya kuwaachia wakandarasi peke yao.

Mheshimiwa Spika, mamlaka ya hali ya hewa ni kitengo muhimu kwa uchumi wa nchi hii na kuwafanya wananchi kupanga shughuli zao za kilimo kitaalamu na uvuvi na kadhalika. Ni vizuri Serikali ikazipatia vituo hivyo vya Tanzania Metrologizal Agency (TMA) vifaa vyote vinavyohitajika ili mamlaka hii iweze kutimiza malengo yake.

Mheshimiwa Spika, kuhusu mawasiliano, napongeza Wizara hii, sasa nchi yetu ina mtandao wa simu takribani nchi nzima, ushindani huu umeanza kuzaa matunda, sasa hata gharama zimeanza kushuka, kutokana na ushidani uliopo, lakini katika internet bado picha za upotoshaji wa maadili zinaathiri watoto wetu ambao ndio wanatumia wakati mwingi. Katika hili naomba Wizara iangalie hili, wale wenye biashara hii anapoona watoto wa umri mdogo basi waweke, utaratibu kuwasaidia watoto ili wasipotoke katika maadili.

Mheshimiwa Spika, Serikali iangalie sana na kwa karibu kuhusu usafiri wa majini kwani kumekuwa na ajali nyingi na kupoteza maisha kwa wananchi wengi. Ningependa Serikali iboreshe vyombo vya usafiri katika Maziwa, Bahari na Mito na vifaa vya kujiokolea, ningependa kujua ni mikakati gani Wizara imepanga kuhusu jambo hili.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa Serikali kutenga fedha (TAMISEMI) kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Mto Simiyu. Daraja ambalo litaunganisha Wilaya ya Meatu na Bariadi na kuruhusu watu na magari kupita muda wote na hivyo magari ya abiria na mizigo yatatoka Meatu kupitia Bariadi mpaka Mwanza na sehemu zingine.

Mheshimiwa Spika, naomba na kushauri barabara inayoanzia Nghoboko – Lubiga – Mwandoya – Kisesa – Ngambasingu – Budalabijiga – Kilulu - Bariadi ipandishwe hadhi iwe ya Mkoa na ihudumiwe na TANROADS ili kulipa hadhi daraja hilo lenye mtandao mkubwa wa watumiaji (watu na magari) na kwamba barabara yake iweze kupitika muda wote.

Mheshimiwa Spika, kuanzishwa kwa barabara ya Sola JC kwenda Sakasaka ililenga mambo makuu matatu, kurahisisha usafirishaji wa mazao (mahindi, mtama na Pamba), kuwezesha jitihada za kupambana na wizi wa mifugo (ng’ombe) kati ya Wasukuma na Wamasai na kurahisisha usafiri wa kuyafikia Makao Makuu ya Maswa Game Reserve. Mheshimiwa Spika, hivi sasa barabara inaishia Sakasaka, haijafika yalipo Makao Makuu ya Maswa Game Reserve (Buturi) na hivyo kusababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi, watumishi, wageni na ndani na nje kufika katika ofisi hiyo muhimu. Baadhi ya wawekezaji kukatishwa tamaa kabla ya kufika na kulisababishia Taifa kukosa mapato

117 na kukosa mahitaji muhimu kama matibabu na chakula. Naomba kipande kilichobaki cha kutoka Sakasaka kwenda Buturi kichongwe na kifanyiwe matengenezo.

MHE. PROF. RAPHAEL B. MWALYOSI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kuona Serikali ya Awamu ya Nne imetambua potentials za kiuchumi zilizopo Ludewa hususan katika Ukanda wa Liganga (Mundindi) - Mlangali ndiyo maana Serikali imekamilisha ujenzi wa soko la Kimataifa Mlangali, kuna mpango wa kuchimba chuma na kujenga kiwanda cha kuyeyusha chuma hicho Liganga (Mundindi).

Mheshimiwa Spika, SGR wamefungua kituo kikubwa cha kununua mahindi pale Mlangali na mwisho upanuzi mkubwa wa kilimo cha chai Ludewa licha ya mashamba makubwa ya chai ya Lusitu na Luponde katika barabara ya Malangali - Njombe. Kutokana na mvuto huo wa kiuchumi wa eneo hilo je, Wizara ya Miundombinu ina mikakati gani ya kuboresha barabara ya Madaba – Mundou – Mlangali - Njombe ili kuwezesha usafirishaji wa bidhaa katika maeneo hayo ambako barabara licha ya kuwa chini ya Mkoa (Madaba - Mlangali) na TANROADS (Mlangali - Njombe) barabara hizo ni mbaya sana na zinapitika kwa shida sana na magari makubwa ya mizigo hasa wakati wa masika naomba maelezo na msimamo wa Wizara kuhusu barabara hizo.

Mheshimiwa Spika, mwezi wa Mei, 2007 mkutano wa Mkoa wa RCC Iringa ulikubaliana kwa pamoja kuwa barabara ya Lumbila hadi Njombe inayounganisha Wilaya za Ludewa, Makele na Njombe na ile ya Mlangali hadi Mbeya inayounganisha Ludewa, Makete na Mbeya zipandishwe hadhi na kuhudumiwa na Mkoa wa Iringa. Nini msimamo wa Wizara kuhusu mapendekezo hayo ya Mkoa wa Iringa?

Mheshimiwa Spika, barabara ya Njombe – Manda - Kivuko cha Ruhuhu inayosimamiwa na TANROADS na iunganishayo Makao Makuu ya Wilaya za Njombe na Ludewa ni mbaya sana hasa eneo la njia panda ya Songea na Lusitu kwenye mashamba ya chai (Njombe) na kile cha Lwilo hadi kivuko cha Mto Ruhuhu ambako daraja moja kati ya Kandamija na Mto Ruhuhu limebomolewa na mvua, je, Serikali imetenga fedha yoyote kwa matengenezo ya barabara hiyo na daraja?

Mheshimiwa Spika, Ndugu yangu Waziri Mheshimiwa Andrew Chenge, mwenzio naumwa ingawa naendelea vizuri, sina shaka kutokuwepo Bungeni kutaninyima haki zangu na watu wangu. Nitaomba unifikirie na uwasaidie wananchi wa Ludewa na usidharau maombi haya bali uyatolee maelezo au majibu. Ahsante ndugu yangu.

MHE. ISSA KASSIM ISSA: Mheshimiwa Spika, kwanza naunga hoja kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Spika, kutokana na hotuba ya Waziri ni nzuri na hasa kuweza kumkomboa mwananchi wa kipato cha chini pamoja na mkulima, lazima tuwe na miundombinu ya uhakika. Masikitiko yangu makubwa na nitapenda Waziri mhusika atakapofafanua maelezo ya hotuba kuweza kuwaeleza kwamba Wizara inatafuta mkandarasi wa daraja la Kigamboni.

118 Napenda Waziri akumbuke Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo imesema wazi mhusika wa daraja hilo ni Shirika la NSSF, nao wameruhusiwa na awamu iliyopita na tayari wamekwishagharamia fedha za wananchi nyingi, je, gharama hizo walizitoa?

Nashauri, kazi ya daraja la Kigamboni, yoyote atakayekuja kwanza wakae pamoja na NSSF kwa sababu hao ndio hata ramani ya michoro ya daraja, wao wamemaliza, inaonekana Wizara wana mwelekeo wa kuwaweka pembeni NSSF, Waziri nitapenda anipe ufafanuzi ulio kamili juu ya suala la daraja na akitekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

MHE. JOHN M. CHEYO: Mheshimiwa Spika, pamoja na maelezo mazuri ya hotuba natoa mapendekezo yafuatayo, plant leasing (kukodi magreda) kwa kuwa fedha hazitoshi napendekeza kila zone ipate plant leasing centres ili tuweze kufungua barabara nyingi. Bariadi Mashariki na Magharibi tuna Kata nyingi mno ambazo lazima barabara. Fedha tunazopata tunaweza kutumia kukodi magreda na Halmashauri zetu zikafungua njia. Mheshimiwa Spika, connectivity maps (ramani za njia). Bariadi hatuna ramani za barabara zetu na tatizo hili lipo kwa Wilaya nyingi kwa mfano, Lugaru – Mahembe - Mahaha (Magu), Ng’wamapalala – Gambasingu – Lagangabili – Kilulu - Bariadi na kuendelea. Tunaomba Wizara ituletee wataalamu wachore barabara zote za Wilaya ya Bariadi ili ramani hizi ziwe base ya mipango mikakati ya kuunganisha Wilaya, Kata na Vijiji.

Mheshimiwa Spika, connectivity katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa lafanana lakini connectivity ndiyo ukombozi wa watu wetu. Kwa leo napenda kuweka uzito katika kuunganisha Singida via Sibiti - Ng’wamhunze – Kisesa – Simiyu – Lagangabili – Kilulu – Bariadi – Ngulyati – Mwamulapa - Nhaya au Sayaka - Magu. Tunaomba barabara hii ipewe kipaumbele kwani itafupisha njia ya kwenda Mwanza na itaimarisha biashara toka Dar es Salaam mpaka Mwanza - Uganda. Napongeza jitihada juu ya barabara ya Mwingunibi - Maswa - Bariadi - Lamadi. Tegemeo letu mwaka 2008/2009 ujenzi uanze.

Mheshimiwa Spika, kwa ujumla Wizara ibuni mipango dhahiri ya kupata fedha za ku-invest kwa barabara long term bounds ni mpango wa kuungwa mkono.

Mheshimiwa Spika, nawatakia kila la kheri kwa kazi nzito bila resources za kutosha.

MHE. JACOB D. SHIBILITI: Mheshimiwa Spika, nafurahi kupata muda wa kutoa maoni yangu katika hotuba ya Wizara ya Miundombinu.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumpongeza Waziri, Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu kwa ushirikiano walionao ambao umezaa hotuba nzuri. Kwa maelezo hayo yananifanya niunge mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.

119 Mheshimiwa Spika, nimepongeza kwa sababu kadhaa ambazo mimi ninao ushahidi wa uhakika wa kile kilichotekelezwa Jimboni kwangu na sehemu zingine. Mfano ni ule wa Bajeti ya mwaka 2007/2008, pesa zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Dodoma – Manyoni – Singida - Shelui, hii ni picha tosha kuwa Serikali iko makini katika ahadi zake. Mheshimiwa Spika, mwaka 2006/2007, barabara ya Fullo - Nyambiti ilitengewa kiasi kidogo ambacho wakati wa masika mwaka jana barabara hiyo ilijifunga kutokana na daraja la Mto Kanyerere kutopitisha magari kutokana na maji kupita juu ya daraja lililopo.

Mheshimiwa Spika, niishukuru Serikali kwa kusikia kilio cha wananchi wa maeneo hayo na kutoa pesa za dharura shilingi milioni moja ambazo zitaendelea kujenga daraja la Mto Kanyerere lakini pia Serikali kwa kulifahamu kwa kina tatizo hilo, imepanga shilingi 80,000,000/= kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa daraja hilo, nawapongeza sana.

Mheshimiwa Spika, ombi kwa kuwa daraja litakuwa zuri, naiomba Serikali iimarishe barabara hiyo kwa kuinua tuta kwani barabara hiyo ni muhimu ikiwemo kupokea au kupeleka wagonjwa Sumve Hospitali.

Mheshimiwa Spika, wakati nachangia hotuba ya Waziri Mkuu niliulizia ujenzi wa barabara ya Kisesa – Butingwa – Fella - Usagara, kasma yake ina 1,408.00 pesa za nje, hii iko ukurasa 104 wa hotuba ya Waziri kiasi hicho ni kidogo ukilinganisha na ahadi ya Serikali ya kujenga kwa kiwango cha lami mwaka huu. Je, ni kazi zipi zilizotengenezwa kiasi hicho ambacho zitafanyika na ni lini hasa ujenzi wa lami utaanza na je, ulipaji wa fidia kwa watu waliochukuliwa maeneo yao utaanza lini?

Mheshimiwa Spika, barabara ya Buhingo, Seeke, Namayinza, Mbalama, Isesa hadi Nyang’homango. Mchango wangu wakati wa hotuba ya Waziri Mkuu niliiomba Serikali ione umuhimu wa kuipandisha hadi barabara niliyoitaja hapo juu toka Halmashauri na kuwa ya Mkoa, hii ni kwa sababu barabara nyingi zinazomilikiwa na Halmashauri uwezo wa kuhimili magari ni tani 12 mwisho, mradi ulioko Ihelele utahitaji mizigo mbalimbali ikiwemo madawa ya kutibu maji na spea za mitambo na magari zaidi ya tani 40 yatapita na mradi huo wa Kitaifa uliochukua zaidi ya 260,000,000,000 na 50,000,000,000 zikiwa Ihelele tu unastahili uwe na barabara nzuri kuufikia mradi.

Mheshimiwa Spika, naomba sana Waziri aone umuhimu wa kukubali mara moja barabara hiyo iwe ya Mkoa na itengewe fedha mwaka huu hata toka OC, dharura.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Misasi - Nduha - Kasololo hadi Mbarika imekuwa ikitengewa pesa, napongeza sana safari hii tena umetenga shilingi 60,000,000 ahsante sana. Ombi, zabuni ya ujenzi itangazwe sasa kabla ya mvua kuanza ili ifikapo Novemba, 2007 iwe imejengwa. Kivuko cha Kigongo - Busisi. Naishukuru Serikali kwa ahadi ya kukamilisha kivuko ambacho Waziri ameahidi kuwa kitaanza kazi Septemba, 2007. Naomba Serikali ifuatilie kwa karibu ili kunusuru maisha ya Watanzania

120 wanaopoteza maisha kutokana na kuhofia kutumia ferry hiyo na kutumia mitumbwi ambayo mara nyingi inazama na kuua watu.

Mheshimiwa Spika, Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), nashukuru Serikali mwaka jana iliahidi kutoa simu za kukoroga (magneto) ni kweli utekelezaji nimeuona katika Wilaya yangu ya Misungwi. Ombi, ifanye kadri iwezavyo mitambo yake ihusishe eneo kubwa zaidi.

Mheshimiwa Spika, nitoe pongezi za pekee kwa Bodi ya Mfuko wa Barabara kwa kumshauri Waziri kuongeza tozo mbalimbali ambazo Waziri alizifanyia kazi na kuzifikisha kwenye Baraza la Mawaziri zikabarikiwa na hatimaye Bunge kukubali. Hii ni hatua nzuri ya kujenga nchi yetu kwa kujitegemea, hongera sana RFB. Ushauri, kazi nzuri itakayofanywa na wananchi kwa kuchangia Mfuko wa Barabara iheshimiwe. Naiomba sana Serikali iwe macho kuona pesa inafanya kazi iliyokusudiwa ili anayechanga machungu ya kuchangia yaishe badala yake ashangilie.

Mheshimiwa Spika, sisitizo lielekezwe zaidi katika Halmashauri zetu, bado zinao ukiritimba udhaifu katika kusimamia, hivyo barabara za Halmashauri zikiwemo za Vijijini. Zipandishwe madaraja ili wakulima wafaidi tozo au michango yao.

Mheshimiwa Spika, nimalizie barabara ya Mwanangwa – Misasi - Salawe. Barabara hiyo imeharibika sana kwa sababu ya mizigo mizito ya mradi wa maji wa Kahama na Shinyanga, Bajeti hii imetengewa shilingi 70,000,000, ni pesa kidogo ukilinganisha na barabara ya Old Shinyanga - Salawe iliyotengewa shilingi 150,000,000 wakati zote ziliharibiwa na mradi huo. Ombi, Waziri aone katika fungu lake la dharura aongeze barabara hiyo sehemu ya Busongo - Mwagiligili itengenezwe vizuri.

Mheshimiwa Spika, niwatakie kila la kheri kwa kazi wanayoifanya wana miundombinu wote chini ya Waziri Mheshimiwa Andrew Chenge. Narudia tena kuunga mkono hoja mia kwa mia. Hongereni sana.

MHE. STEPHEN M. WASIRA: Mheshimiwa Spika, kwa heshima kubwa naomba kuwasilisha hoja zangu za maandishi kama ifuatayo:-

Mheshimiwa Spika, Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Mara iliwasilisha mapendekezo ya kutoka sehemu ya barabara ya Bunda – Nyamswa.

Naomba barabara hiyo ijumulishwe kama sehemu ya barabara ya Makutano – Nata – Mugumu – Loliondo – Mto wa Mbu katika orodha ya miradi itakayofanyiwa upembuzi yakinifu kiambatanisho Na.2 ukurasa wa 106-107, haikujumlishwa licha ya Wizara kukubali hoja hii kwa barua ambayo nakala yake ninayo. Naomba kupata maelezo juu ya suala hili.

Mheshimiwa Spika, suala la pili ni ombi la kutaka barabara ya Balili- Mugeta – Nanchimweru ili iwe barabara ya Mkoa kutokana na umuhimu wa barabara hii. Barabara hii ni muhimu sana kwa maendeleo ya uchumi, kilimo na jamii kutokana na mazingira

121 inapofuta barabara hii kando kando ya milima. Halmashauri imeshindwa kuihudumia kutokana na ufinyu wa Bajeti ya Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo, naounga mkono hoja.

MHE. PINDI Z. CHANA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia. Pia naomba nimpongeze Waziri wa Miundombinu kwa kazi nzuri katika Wizara hii. Wilaya ya Ludewa iliwahi kuwa na kivuko. Kivuko kilizama na sasa hakuna kabisa kivuko ziwani. Ni muda mrefu Serikali imesema tutashirikiana.

Naomba leo kujua hatima ya kivuko cha Ludewa. Kivuko hiki ni muhimu sana kwa wananchi na Taifa zima. Ninapenda kujua hatima ya kivuko cha Ludewa.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Makete – Njombe ni miongoni mwa ahadi za Rais. Makete kuna rasilimali nyingi sana kama mazao na wananchi kwa ujumla.

Serikali inasema nini juu ya ahadi hii ya barabara ya Makete – Njombe? Barabara ya Njombe – Modope – Ludewa inahitaji ukarabati. Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali itengeneze barabara hii kwa kiwango cha lami kuliko kila mwaka kutenga hela za ukarabati na mwisho wa siku gharama zinakuwa kubwa kuliko lami.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya wananchi wa Iringa, nitaunga mkono hoja nitakapopata majibu yangu ya hoja nne tajwa hapo juu kwa ufasaha. Naomba kuwasilisha.

MHE. BRIG. JEN. : Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu kwa hotuba yake aliyoiwasilisha Bungeni ya Mipango ya Maendeleo na Makadirio ya Matumizi ya fedha kwa mwaka 2007/2008. Mimi binafsi nimeridhika na juhudi za Serikali katika kusimamia na kuendelea miundombinu ya Taifa letu.

Hata hivyo Serikali inajenga kwa kiwango cha lami kipande cha kilomita sita kutoka Lushoto Mjini hadi Magamba eneo ilipo Ikulu ndogo ya Lushoto. Tokea ujenzi huo uanze miaka mitatu iliyopita mpaka sasa ni kilomita mbili tu. Hili linasikitisha kuona kuwa inashindikana kukamilisha ujenzi wa kilomita nne zilizobaki. Waziri anaombwa atoe maelezo, ni lini ujenzi wa kipande kilichobaki kitakamilishwa?

MHE. MTUTURA A. MTUTURA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Nampongeza Waziri pamoja na Manaibu Mawaziri wote wa Wizara hii. Wananchi wa Tunduru wana imani kubwa na uongozi wa sasa wa Wizara hii hasa kwa kuzingatia record ya utendaji ulioonyeshwa kwa kipindi kifupi.

Wanaamini kwamba kwa kuwa upembuzi yakinifu na utangazaji wa tenda utakamilika katika mwaka huu wa fedha, wananchi wa Tunduru wamejengeka na imani

122 kwamba mwaka ujao wa fedha ujenzi wa barabara kutoka Mangaka – Tunduru – Songea hadi Mbambabay utaanza kwa kasi.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Tunduru wanaiomba Serikali wakiwa wanasubiri barabara kuu kuwekwa lami, wakala wa barabara nchini TANROAD wazifanyie matengenezo barabara kuu kwa kuweka kufusi cha changarawe badala ya kifusi cha udongo ambao unaifanya barabara itokayo Masasi –Tunduru –Songea isipitike wakati wa masika. Barabara hii ni kero kubwa sana kwa wananchi nyakati za masika. Mheshimiwa Spika, Muswada wa kuziruhusu pikipiki kubeba abiria kibiashara uletwe Bungeni haraka iwezekanavyo kwani ni nyenzo pekee kwa wenye kipato kidogo kupata usafiri wa bei nafuu na wa haraka.

MHE. SIGFRID S. NG’ITU: Mheshimiwa Spika, wananchi wa Ruangwa wameniagiza nikuulize, hivi ni lini itakamilika hadithi ya kujenga daraja katika mto Lukuledi ili waweze kupita katika mto Lukuledi kwenda Ndanda Hospitali kwa vile Ruangwa yenyewe haina Hospitali ya Wilaya? Daraja hili wala halihitaji fedha nyingi, lakini kila kiongozi apitaye pale anachojua kuongea na kutoa ahadi ni ujenzi wa daraja hili. Wananchi wanaliwa na mamba na kuzama mtoni wakati wakipita.

Katika ilani ya CCM, kura nyingi zimepatikana toka kwa wananchi wa Ruangwa katika maeneo ya Nanyumbu, Luchelegwa Ndandagala, Namahema, Michenga, Ntawilile, Mibure, Chienjere, Namakwili, Njawale na Nandanga. Kura tulizipata baada ya ahadi ya kujengewa daraja hili. Sasa hakuna kitu. Wanauliza swali: Je, mwaka 2010 tutawaeleza nini wakati daraja lenyewe gharama yake ni ndogo tu haifiki hata milioni 200?

Mheshimiwa Spika, wananchi wanaomba Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu atoe ahadi yake ili wamsikie.

MHE. ELIETTA A. SWITI: Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali kwa kuwa na mfuko wa matengenezo ya barabara na kutenga fedha nyingi za nchini kuliko zile za wafadhili. Mradi wa PMMR unaofadhiliwa na Banki ya dunia ambao utaigusa Rukwa nao naupongeza. Kipaumbele cha Rukwa ni miundombinu, hivyo basi ujio wa Rais Mkoani Rukwa na ahadi ya kutengezwa kwa barabara za lami Tunduru – Nyakanazi – Chala – Kirando – Kipili – Sumbawanga – Kasanga –Matai na Kasesya utafungua ukarasa mpya kwa maendeleo ya Rukwa. Naipongeza Serikali kwa kuiona Rukwa kwa jicho la huruma.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo wa Kwela naishukuru Serikali kwa kutenga fedha za kuitengeneza barabara ya Miangalua – Kipeta. Lakini pia kwa kuanzia kutengeneza barabara ya Mtowisa – Kipeta ambayo haijapitika kwa miaka mingi. Hivyo barabara itakuza uchumi wa Rukwa bondeni na kuzuia vifo vya watu katika mto sanuya Kata ya Kaoze –Kipeta ambapo hapakuwa na daraja. Naomba pia barabara ya Sumbawanga –Mwimbi Ulumi –Mambwe kenya ipanuliwe. Mheshimiwa Spika, kiwanja cha ndege cha Sumbawanga mjini kipo katikati ya mji. Ni hatari kwa kurusha na kutua ndege!

123 Naomba mbuga ya Kasumba – Kasote ifanyiwe utafiti wa haraka kwani sasa Rukwa chini ya uongozi wa Mkuu wa Mkoa uliitisha wawekezaji na Rais kufungua kongamano hili lililofanikiwa sana. Namshukuru Mkuu wetu wa Mkoa na pia Rais wetu kwa mapenzi hayo. Wawekezaji watakuja tu Rukwa kama usafiri ni wa haraka. Wengi wa wawekazji walipenda kuwekeza katika utalii, uchimbaji, madini na miundombinu na barabara.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Rukwa una miundombinu hafifu hata katika masuala ya simu za mkononi. Tafadhali tupieni macho Inyonga – Mpanda Mashariki. Kilio na moja Mkoa, Rukwa ni miundombinu. Nashauri miundombinu iboreshwe haraka kwa maendeleo ya Mkoa wa Rukwa. Naunga mkono hoja.

MHE. MHONGA S. RUHWANYA: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa, naomba maswali yangu yapatiwe majibu.

Mheshimiwa Spika, barabara ni sawa na mishipa ya damu, hivyo ni muhimu sana kwa ajili ya maendeleo ya nchi yoyote duniani kiuchumi. Ujenzi wa barabara zetu umekuwa wa kusuasua. Naomba Serikali itupe sababu kwanini hali hiyo inajitokeza? Mfano barabara ya Dodoma –Manyoni –Singida, Mbwemkuru –Mingoyo. Mbali ya kusuasua kwa ujenzi wa barabara nyingi nchini, naitaka Serikali itupe maelezo barabara ya kuanzia Manyoni mpaka kufika Nyakanazi – Kigoma na ile ya kupitia Tabora - Kigoma.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Kigoma ukifunguliwa, naamini wananchi watajikomboa kiuchumi miaka yote. Tunaomba barabara hiyo ijengwe. Mbona hatuelezwi haja hiyo? Kwani haki yetu kujengewa barabara maana Kigoma tunalipa kodi kama ilivyo Mikoa mingine. Kwa hiyo, ni wajibu wa Serikali kurudidha matunda ya kodi zetu kwa vitu vinavyoonekana kama barabara.

Mheshimiwa Spika, kama barabara zingelikuwa zimetengenezwa kwa lami hasa barabara kuu mfano ya Manyoni, tatizo la mvua lisingeathiri barabara zetu. Lakini kwa kuwa viwango vya barabara zetu ni vya hali ya chini, ni jambo la kawaida barabara kukaa miaka miwili barabara inaanza kupasuka.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri zetu zinatengewa pesa za kutengeneza na kujenga barabara. Lakini ujenzi wake ni wa kiwango cha chini kiasi kwamba huwezi kuona pesa zimefanya nini? Serikali iangalie upya suala hilo na ufumbuzi upatikane ili pesa zisipotee bure. Naomba Waziri atueleze kwanini pesa za ukarabati wa barabara fungu lake linapungua kila mwaka wakati maintanance ni muhimu.

Napenda Serikali itoe maelezo juu ya ujenzi wa barabara za vijijini ili wananchi waishio huko nao wawe wamefunguliwa waweze kusafirisha bidhaa zao nao waweze kupata huduma muhimu. Pamoja na kwamba yaweza kuwa chini ya TAMISEMI, lakini Wizara hii iwe ndio waratibu wa zoezi.

124 Mheshimiwa Spika, kuhusu ujenzi wa nyumba za Serikali, kwanza natoa pole kwa Serikali kwa kosa la kuuza nyumba, sasa kodi ya wananchi wanaitumika kujenga upya nyumba za wafanyakazi na viongozi badala ya ujenzi huo ungekuwa wa kuziongeza kulingana na mahitaji ya leo. Naomba Serikali ituambie ni kiasi gani kinatumika kuwapangishia viongozi na watumishi nyumba katika makazi mapya na wangapi wanalipiwa hoteli na ni kiasi gani?

Mfano, Majaji watatu wa Mahakama ya Kanda, Tabora, wanaishi Orion Tabora Hotel: Je, ni kiasi gani kimeshatumika sasa tokea wapate uteuzi wao mpaka mwezi Juni? Je, Serikali haioni kama inapoteza pesa za umeme kwa kosa la uuzaji wa nyumba?

Pamoja na kwamba kosa lilifanywa awamu ya tatu, lakini kila mara tunaambiwa hii ni Serikali inayoendelea chini ya CCM. Naomba majibu.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali itueleze ina mikakati gani ya kuiendesha Bandari ya Mkoa wa Kigoma na hadhi yake na iweze kufanya kazi kama awali, kwani ni muhimu sana kwa uchumi wa nchi yetu. Inategemewa pia na Congo, Zambia na Burundi.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali itueleze mikakati ya uendelezaji wa Airpot ya Kigoma ili iweze kuwa kiungo kizuri cha usafirishaji abiria na mali zao kutoka Kigoma – Tabora - Dar es Salaam hasa ukizingatia ni Mkoa uliopo mpakani. Hivyo, kuna wageni wengi kutoka Congo, Burundi na hata Rwanda. Hivyo uchumi utaendelea kukua.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali itupe mkakati maalum wa kufufa Reli ya Kati kikamilifu ingawa tayari imepata mwekezaji. Lakini naiomba Serikali ihakikishe inasimamia vizuri ili reli iweze kusaidia kukuza uchumi wetu kwa kusaidiana na Bandari ya Kigoma pamoja na Airport ya Kigoma.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali inipe ufafanuzi na majibu nilivyoomba nipewe katika mchango wangu.

MHE. JENISTA J. MHAGAMA: Mheshimiwa Spika, nampa hongera sana Mheshimiwa Waziri na Manaibu wake kwa kazi nzuri. Kwa mara ya kwanza, Wizara imekuja ikiwa na Hotuba yenye mgawanyo wa fedha kwa uwiano mzuri.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Peramiho, ninawaomba kutoa shukrani za dhati kwa Waziri kukumbuka na kuzingatia kutenga fedha kwa maeneo mawili muhimu ya kimiundombinu katika Wilaya yetu kama ifuatavyo:-

(i) Fedha zilizotengwa mwaka huu ili kukamilisha ujenzi wa Bairry bridge katika Mto Ruvuma – Mitomoni ni faraja kwa wananchi wa Jimbo la Peramiho. Tunashukuru sana.

125 (ii) Tunaishukuru pia Serikali kwa kutenga fedha kwa ajili ya barabara ya Ifunga –Wino. Ingawa fedha zilizotengwa ni chache, lakini haizuru, tutaanza. Hata hivyo tunaomba Serikali ifikirie mapendekezo yaliyoletwa na Ofisi ya DC na Regional Engineer kuhusu umuhimu wa barabara hiyo rahisi ya kukamilisha matengenezo ya barabara hiyo.

Mheshimiwa Spika, ninaipongeza Wizara kwa kuboresha mawasiliano katika Jimbo la Peramiho. Hata hivyo wananchi wanaomba ujenzi wa minara ya simu katika maeneo yafuatayo:- (1) Eneola Muhukuru kunakojengwa daraja mpakani kuwa Tanzania na Msumbiji biashara imeshamiri sana mpakani.

(2) Eneo la Kilagano na Mgazini. Mahali hapa ni Kituo Kikuu cha biashara ya mahindi.

(3) Eneo la mlima wa Lubereruka. Eneo hili ni la uelekeo wa eneo la vitalu vya uwindaji.

Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Mungu awabariki sana.

MHE. FATMA A. MIKIDADI: Mheshimiwa Spika, Hongera Mheshimiwa Waziri, Manaibu Waziri wote, wamejitahidi kuja Lindi kuangalia matatizo ya Lindi. Msichoke, endeleeni tu, hongera sana nami ninaunga mkono kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Spika, matatizo ya Bandari ya Lindi ni makubwa sana. Tungeomba sana tusaidiwe sana ukarabati. Sasa hivi bahari imebomoa sehemu ya bandari na maji yanapita kwenda nchi kavu kupitia bandari hiyo. Sasa hivi ikitokea Tsunami kupita Bandari hiyo kwenda Mjini Lindi, kwa kweli maji mengi yataingia Mjini na kuharibu majumba kupita bandari hiyo kwa vile sehemu ya bandari imebomoka na inapitisha maji ya bahari kwenda nchi kavu. Jengo la NBC na Jengo la Parokia ya Father Ngonyani limeanza kuingiliwa na maji. Tunaomba ukarabati ufanyike Bandari ya Lindi. Imebidi niandike kwa sababu sikuwahi kumaliza kuongea

Mheshimiwa Spika, nimalizie na suala la msongamano wa magari Jijini Dar es Salaam. Kwanza nitoe pongezi kwa jitihada zinazofanywa na viongozi wakuu akiwepo Waziri Mkuu. Hongera sana, nami nitoe wazo langu ni hili. Ushauri wangu ni kwamba, tukitumia treni; je, kwa mfano yakikarabatiwa mabehewa matano yakawa yanatumiwa katika maeneo ambayo reli imepita behewa moja sawa na abiria wa mabasi matatu madogo, treni hiyo ikawa inabeba abiria wa Kiwalani, Tabata, Relini, TAZARA Ilala na Railway station. Vilevile Mitaa ya Ubungo, Tabata, Mabibo, Buguruni, Yombo Vituka na kadhalika hasa katika maeneo yale ambayo tayari kuna reli na vituo vitakuwepo tu. Hata nchi nyingine hutumia treni Mijini angalau kwa asubuhi na jioni. Baada ya kusema hayo, basi naunga mkono hoja mia kwa mia.

126 MHE. CHARLES N. KEENJA: Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza Waziri wa Miundombinu kwa kazi nzuri zinazofanywa na Wizara yake. Katika kipindi hiki tunashuhudia maendeleo makubwa katika maeneo yote yanayosimamiwa na Wizara hii yakiwemo mawasiliano ya simu, barabara na kwa kiasi usafiri wa anga. Mafanikio haya yatachangia sana katika kuinua ubora wa maisha ya wananchi na kuharakisha kukua kwa uchumi.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri Mkuu amefanya vikao kadhaa na wadau wa usafiri katika Jiji la Dar es Salaam na hatua za muda mfupi zimechukuliwa kujaribu kupunguza msongamano wa magari katika barabara za Jiji.

Tulitegemea sana kwamba Bajeti ya mwaka huu ingeonyesha nia ya kutekeleza maagizo ya Waziri Mkuu ya kuchukuliwa kwa hatua za kupunguza msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam kwa kujenga ring roads na barabara za kuchepua magari kutoka kwenye barabara kuu. Sioni dalili za kutekelezwa kwa mpango huo na kama kuna kitu kwenye makisio haya, nitapenda kuelezwa.

Mheshimiwa Spika, Serikali za CCM zimeonyesha ubunifu na kuthubutu kwa kutumia fedha zetu wenyewe kujenga barabara. Ununuzi huu umetujengea heshima na umetufanya tuonekane kwamba hatusubiri tu wafadhili au wahisahi na unaendana na sera yetu ya ujamaa na kujitegemea.

Mheshimiwa Spika, mafunzo tuliyopata kutokana na utekelezaji wa uamuzi huu unafaa utumike kwa miradi mingine mikubwa katika Jiji la Dar es Salaam. Tungeweza kuamua kujenga fly overs, Ubungo, TAZARA Station, kwenye makutano ya barabara za Nyerere na Mandela na Kilwa.

Mheshimiwa Spika, tukiamua na Serikali ikatenga fedha kila mwaka, baada ya miaka michache vivuko hivi vitajengwa na huenda washirika wetu wa maendeleo wakajiunga na sisi na kutusaidia kukamisha ujenzi huo. Lakini ni sharti tuenze na naiomba Serikali ithubutu kuamua kwanza. Hivyo hivyo ujenzi wa Daraja la Kigamboni tunahitaji maamuzi na kuthubutu pia na tunaweza kushirkiana na wadau wengine. Mheshimiwa Spika, Jimbo la Ubungo linakabiliwa na tatizo kubwa la ukosefu na ubovu wa barabara. Jimbo hili limegawanyika katika maeneo mawili. Maeneo yaliyokaa kimji: Kata za Manzese, Makurumla, Mabibo, Mburahati, Ubungo na Sinza na kuna maeneo yaliyokaa kivijiji na ambayo yanahamiwa kwa kasi kubwa sana hivi sasa. Maeneo ya mijini yaliwahi kuwa na barabara za lami, lakini hivi sasa hakuna mahali ambapo lami hiyo imesalia. Inabidi Serikali izisaidie Mamlaka za Jiji la Dar es Salaam kutafuta fedha za kujenga barabara hizo upya.

Kwa upande wa vijijini; Goba, Kibamba, Mbezi Luis, Kimara na Makuburi kuna maeneo ambayo hayana barabara kabisa na kule ambako kuna kitu kinachofanana maeneo haya yanahamiwa kwa kasi sana hivi sasa kutokana na huduma muhimu za jamii kujengwa kwenye maeneo hayo tunaiomba Serikali na Mamlaka za Jiji kuweka utaratibu

127 maalum wa kujenga barabara kwenye maeneo hayo na ujenzi uanze sasa ili kuwezesha wananchi wafike walikojenga maskani yao.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

MHE. HEMED MOHAMED HEMED: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, nimshukuru Mola kuniwezesha siku ya leo kuamka nikiwa mzima. Pia nakushukuru wewe kwa umahiri wako wa kutuongoza hapa Bungeni, Mola akupe uzima. Napenda pia kumtakia kheri Waziri wa Miundombinu Mheshimiwa Andrew John Chenge kwa jitihada zake za kutaka kutukwamua Watanzania katika nyanja za miundombinu.

Mheshimiwa Spika, sasa niende katika mchango wangu kuhusu miundombinu ya barabara. Nchi yetu inaeleweka kwamba ndio mategemeo ya nchi jirani kwa matumizi ya kupitisha mizigo yao. Jambo ambalo hupelekea mapato makubwa kwa nchi yetu ni ukosefu wa barabara na reli. Tunakosa mamilioni ya fedha. Pamoja na kazi nzuri ya TANROAD, bado udhaifu wa barabara zetu upo. Hii inatokana na ukosefu wa Bajeti. Naiomba Serikali itujulishe ni barabara ngapi za trankroad zina hali ya kuridhisha na ngapi zinazoshughulikiwa na Halmashauri za Wilaya.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania. Tanzania Airports Authority (TAA). Chombo hiki ni muhimu sana hapa nchini, kwani nia yake ni kukuza viwanja vyetu hapa nchini. Ni lini Serikali imedhamiria kukijenga Kiwanja cha Ndege cha Dodoma huku Serikali ikiwa na nia ya kufanya Makao Makuu ya Serikali nchini? Mheshimiwa Spika, kuhusu Shirika la Ndege la Tanzania ATCL. Shirika hili ni muhimu sana na sio tu kwa huduma za anga hapa nchini, bali pia kukuza uchumi wetu. Zuri zaidi ni ile jitihada ya kampuni hii kurudisha safari zake za zamani ikiwemo kisiwa cha Pemba.

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kukishughulikia kiwanja cha ndege huko Pemba? Kwanini muda mrefu kiwanja hicho hakina huduma?

Mheshimiwa Spika, kuhusu usafiri wa nchi kavu, Watanzania walio wengi hapa nchini hutumia usafiri wa mabasi, treni ama magari madogo madogo kwa kufanikisha majukumu yao ya kila siku. Hali hii huwawezesha kibiashara na pia kuonana na familia zao. Pamoja na nia njema ya watu wetu, nasikitika kwa kila wakati wenzetu wanafariki kwa ajali za barabarani. Je, Serikali ina mpango gani kunusuru maisha ya watu wetu?

Mheshimiwa Spika, pia kuna ongeeko la upandaji wa nauli kiholela na bei za mafuta. Tunaiomba Serikali itujulishe ni kitu gani kinachosababisha mlipuko huo wa bei.

Kuhusu usafiri wa majini kwa kuzingatia umuhimu wa vyombo vya majini na kusimamiwa na SUMATRA, tunaiomba Serikali itujulishe ni muda gani inaotumia kuvicheki vyombo hivyo baharini.

128 Mheshimiwa Spika, kuhusu mawasiliano ya simu za mkononi, naishukuru Serikali kwa kuweza kufanikisha mawasiliano kwa njia ya simu, kwani ni moja ya majukumu ya Serikali kuleta maendeleo. Kwa Kanda za Pemba, ZANTEL inafanya kazi zake vizuri. Lakini iko haja minara yake ama iongezwe, kwani mawasiliano ya uhakika ni baadhi tu ya maeneo hasa maeneo ya Miji.

Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo yangu hayo, nasema ahsante.

MHE. KABUZI F. RWILOMBA: Mheshimiwa Spika, kwanza naunga mkono hoja. Nampongeza Waziri wa Miundombinu, Naibu Mawaziri wote wawili, Katibu Mkuu na Wakurugenzi wote pamoja na uongozi mzima kwa ujumla. Natoa shukrani zangu binafsi kusikia kilio changu na kukubali kutenga fedha kwa ajili ya barabara ya Usagara – Geita. Nashukuru sana Mungu awabariki. Pia napenda nishukuru Wizara kwa kutenga kiasi cha fedha kwa barabara zifuatazo:-

Chibingo – Bukondo, Geita –Nyarugusu –Bukoli, Katoro –Busanda –Ibondo – Kamena.

Pamoja na fedha hizo, barabara hizi ni chafu sana, hazipitiki, hususan barabara ya Katoro –Kamena ambayo haijatengenezwa muda mrefu ambapo mwaka jana ilipewa shilingi milioni 50, hazikufaa kitu, maana ni ndefu zaidi ya kilomita 70. Sambasamba na kushukuru, naomba niweke msisitizo kwenye njia ya Reli. Reli ndiyo inayookoa barabara zetu kwa ajili ya magari yabebayo mizigo. Pamoja na kwamba kuna barabara kutoka Kusini mpaka Bandari ya Dar es Salaam, TAZARA ni muhimu na mkombozi kwetu.

Mheshimiwa Spika, kwa hivi sasa TAZARA ina matatizo makubwa mno. Kwa mfano, wafanyakazi ni wengi ambao wangestahili kupunguzwa, reli imechoka inahitaji ukarabati makini, upungufu wa injini kubwa na ndogo, upungufu wa mabehewa ya mizigo na abiria pia na matatizo ya wastaafu kutolipwa haki zao. Kwa kweli hali ya mazingira ya TAZARA yanahitaji kutazamwa kwa haraka. Chonde chonde mkakati wa kubinafsisha TAZARA upewe msukumo wa haraka, vinginevyo Serikali ya Tanzania na Zambia ziingilie kati kwa kuiongezea fedha ili kuinusuru na kuweza kufanya kazi vizuri.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo, tunashukuru Serikali ya Tanzania kwa kutoa kiasi cha shilingi milioni 100 na Serikali ya Zambia kwa kutoa USD 120,000. Lakini hazitoshi, ni kidogo mno, sawa na kulipa ada ya mtoto shuleni bila sare za shule. Tafadhali, TAZARA ina madeni, TAZARA inakwisha.

Naomba Mheshimiwa Waziri na Katibu Mkuu kufanya ziara ya makusudi kutembelea Reli ya TAZARA kuanzia Dar es Salaam hadi Kapirimposhi na ikiwezekana iwe ni pamoja na Waziri na Katibu Mkuu wa Miundombinu toka Zambia. Naomba ufanyike ushawishi wa kila namna ili wachina wakubali kuichukua wakati wa ubinafsishaji.

Mheshimiwa Spika, mwisho, naomha fedha zilizotolewa zisimamiwe ili kazi ionekane. Mungu awabariki sana. Naunga mkono hoja.

129 MHE. ENG. LAUS O. MHINA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, napenda nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu kwa hotuba yake nzuri. Vile vile niwapongeze Naibu Mawaziri wa Miundombinu pamoja na Wizara nzima kwa jumla kwa maandalizi mazuri ya hotuba ya Waziri.

Mheshimiwa Spika, baada ya pongezi hizi, napenda nianze mchango wangu kwenye Sekta hii ya Miundombinu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Nne haina budi kupongezwa kwa ujumla kwa juhudi zake za kutoa kipaumbele katika kukarabati barabara nyingi hapa nchini. Hili tunaliona katika miji yetu mingi hapa nchini ukiwemo mji wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, hali halisi ya barabara zetu kufikia Desemba, 2006 inaonyesha kuwa tunazo jumla ya kilometa 85,000. Kati ya hizo zenye lami ni kilometa 4,430 na zisizo za lami ni kilometa 80,570. Hiki ni kiasi kidogo.

Mheshimiwa Spika, hali ya barabara hususan sizizo za lami ambazo asilimia kubwa ni zile za Tanroads, za Wilaya (District Roads) na za vijijini (Feeder roads), sio nzuri hasa nyakati za mvua. Barabara nyingi katika Jimbo la Korogwe Vijijini zimeathirika sana kutokana na mvua za vuli, hivyo zinahitaji kufanyiwa matengenezo ya dharura.

Mheshimiwa Spika, ili juhudi za kukarabati barabara zetu hususani za Wilayani ziende kwa wakati, itabidi Serikali iongeze mgao wa fedha za mfuko wa barabara (Road Fund) kwa Halmashauri zetu. Kiasi kinachotolewa kwa sasa ni kidogo sana ukilinganisha na urefu wa barabara tulizonazo.

Mheshimiwa Spika, nashauri jitihada ziongezwe zaidi kwenye programu ya ukarabati wa barabara zetu, kwani tunaambiwa na wahenga kitunze kiishi. Mpango wa kuongeza hadhi baadhi ya barabara zetu ni mpango mzuri kimaendeleo. Tunazo barabara nyingi ambazo ziko kwenye ngazi ya wilaya ambazo zinastahili kuwa ngazi ya barabara za mkoa. Mfano mzuri uko kwenye Jimbo langu katika barabara za Korogwe - Bungu ambayo huunganisha Wilaya ya Korogwe na Lushoto, Mombi - Mzeri ambayo huunganisha Wilaya ya Korogwe na Handeni na Kwetonge – Kizara - Zirai ambayo huunganisha Wilaya ya Korogwe na Muheza.

Mheshimiwa Spika, Serikali yetu imeonyesha ni jinsi gani inajali umuhimu wa mawasiliano kwa maana ya simu kwa wananchi wake. Napenda kuipongeza na kuishukuru Serikali kwa kueneza mitambo ya simu katika maeneo mengi ya Jimbo la Korogwe Vijijini. Ombi letu la kupatiwa huduma za mawasiliano katika Tarafa za Magoma na baadhi ya Bungu zimekwishatekelezwa, maeneo mengi katika Tarafa ya Magoma sasa yananufaika na huduma hii.

130 Mheshimiwa Spika, wananchi wa Korogwe Vijijini wanaomba ile ahadi ya kujenga mnara wa Vodacom katika Mji wa Magoma na maeneo ya Bungu yafanyike haraka kama Serikali ilivyoahidi kuwa ifikapo Julai, 2007 mnara wa Vodacom katika mji wa Magoma utakuwa tayari.

Mheshimiwa Spika, pia ipo haja ya kuongeza minara ya mawasiliano katika maeneo ya Mashewa, Kizara na Bunge kwenye mlima Kishaai.

Mheshimiwa Spika, Bandari ya Tanga ni moja kati ya bandari za kale sana katika ukanda wa Bahari ya Hindi na ni ya pili hapa nchini. Katika miaka ya sabini na kurudi nyuma bandari hii ilikuwa maarufu sana kwa usafirishaji wa bidhaa za hapa nchini na nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, hali hiyo ilidorora kwa muda mrefu. Hata hivyo, hali imeanza kuwa nzuri kuanzia miaka ya hivi karibuni kwani takwimu zinatuonyesha:-

2004 2005 2006 Meli zilizotia nanga 215 281 281 Usafirishaji mizigo 162,000 tons 289 tons 519,000 tons

Bila shaka takwimu hizi zitaendelea kupanda kutokana na kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Sasa umefika wakati muafaka wa kujenga bandari ya kisasa Tanga. Naomba kuunga mkono hoja.

MHE. JUMA ABDALLAH NJWAYO: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Waziri wa Miundombinu Mheshimiwa Andrew Chenge na Wasaidizi wake Manaibu Mawaziri, Mheshimiwa Maua Daftari na Mheshimiwa Dr. Milton Makongoro Mahanga pamoja na wafanyakazi wote wa wizara ya Miundombinu kwa kuitekeleza vizuri na kiasi cha kuridhisha Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2005. Kwa mujibu wa Ilani hiyo ibara 44(a)(b)(c)(e)(g)(h)(i)(j)(k)(l) na (m) ukurasa 52-55 inatekelezwa vizuri – hongera sana.

Mheshimiwa Spika, tarehe 22/6/07 Mheshimiwa Naibu Waziri Dr. Milton Makongoro Mahanga akijibu swali langu Na. 68 kuhusu upandishwaji hadhi barabara ya Mtwara – Tandahimba - Newala hadi Masasi ikiwa ni pamoja na kuiweka lami. Serikali ilitamka wazi kuwa haina mpango wa kuiweka lami barabara hiyo kutokana na ufinyu wa bajeti.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa maeneo hayo wamenipigia na kunieleza kuwa hawakupendezwa na jibu hilo. Wameomba niwaombe Wizara ya Miundombinu kuifikiria barabara hiyo katika bajeti ijayo angalau kwa kuitengea fedha kidogo kidogo kama Serikali ilivyofanya kwa barabara ya Mkuranga – Kibiti kwani barabara ya Mtwara – Tandahimba - Newala hadi Masasi inachangia kwa kiasi kikubwa pato la Taifa kupitia korosho.

131 Aidha, barabara hiyo ndio inayounganisha wilaya zote za Mkoa wa Mtwara na inasaidia kuimarisha biashara na uhusiano kati ya Tanzania na Msumbiji na pia itakuwa utekelezaji wa ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa kampeni.

Mheshimiwa Spika, ipo barabara ya Mkoa inayoanzia Tandahimba – Litehu - Mkwiti. Mwaka jana ilitengewa jumla ya shilingi milioni 60. Kazi iliyofanyika ni kuweka kifusi tu pembeni mwa barabara bila kifusi hicho kusambazwa wala kutengenezwa. Kwa kifupi hakuna matengenezo yaliyotengenezwa au kufanywa. Wananchi wamekatishwa tamaa sana na hali hii. Ningependa sana kupata maelezo ya kina kwa nini hakukuwa na maendeleo yoyote ya matengenezo ya barabara hiyo.

Mwaka wa fedha 2007/2008 tena zimetengwa shilingi milioni 100. Napata wasiwasi pia na utendaji na usimamizi wa Meneja wa Tanroad – Mtwara. Jimboni Tandahimba kuna barabara ya Mkoa inayoanzia Malamba – Namikupa – Maundo - Mahuta. Barabara hiyo ni muhimu sana kwa uchumi hasa kilimo kwa wakulima wa pembezoni mwa mto Ruvuma. Tatizo la ubovu wa barabara hiyo unachangia sana kuwakimbiza wafanyakazi hasa walimu wanaopangiwa kufanya kazi katika maeneo hayo. Pia akina mama wajawazito hupata ugumu na hatari ya kupoteza maisha inapowalazimu kwenda kituo cha afya cha Namikupa kwa dharura. Kwa muda mrefu barabara hiyo haijawahi kutengewa fungu. Aidha, utakumbuka mwezi Aprili, 2007 Mheshimiwa Andrew Chenge nilikuandikia nikikuomba uifikirie angalau kwa kuitengea kwa kiasi fulani cha fedha. Kumetokea nini? Nipe maelezo ya kina, maana uliniahidi kwa mdomo kuwa utahakikisha barabara hiyo inafikiriwa.

Mheshimiwa Spika, baada ya kupitisha bajeti ya Serikali iliyowasilishwa na Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Zakia Hamdani Meghji kumejitokeza ujanja wa wafanyabiashara wa mafuta wilayani to create scarcity ya makusudi na hivyo bei ya mafuta kuwa ya juu sana. Ni vigumu kwa EWURA na SUMATRA kusimamia mfumuko huu wa bei ya mafuta kwa ngazi za Wilaya. Ni mapendekezo yangu kuwa Wakuu wa Wilaya wapewe maagizo ya kusimamia na kudhibiti ongezeko hili la mafuta lisilo la lazima.

Mheshimiwa Spika, naomba sana suala la tendering process ya barabara ya Ndundu - Somanga lifanywe haraka ili lionekane dhahiri kazi ikiwa imeanza ili kujenga imani ya wananchi wa maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, mwisho, naunga mkono hoja.

MHE. HERBERT J. MNTANGI: Mheshimiwa Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu, Naibu Mawaziri wake na Watendaji wake kwa hotuba nzuri iliyoandaliwa kwa kina na vielelezo vya kisayansi na bayana.

Iwapo mipango ya ujenzi wa barabara zilizoainishwa itasimamiwa na kutekelezwa sawia na upatikanaji wa fedha kutoka vyanzo vilivyokusudiwa, basi

132 Tanzania itashuhudia mtandao mzuri wa barabara katika nchi ambayo ni kubwa kwa eneo kuliko nyingine katika Afrika Mashariki. Pamoja na yote hayo, Wilaya ya Muheza imesahauliwa kabisa!

Barabara ya Muheza - Amani ni barabara ya Mkoa. Katika mwaka wa fedha 2003/2004 sehemu ya barabara hiyo eneo la Muheza Mjini iliwekwa lami kilometa 1.5 (moja na nusu). Baada ya hapo haijaendelezwa tena licha ya ukweli kwamba maeneo mengine yaliyopata fedha pamoja na Muheza mwaka 2003/2004, wameendelea kupata fedha zaidi na barabara zao kuendelezwa. Nimeandika mara kadhaa na kuweka viambatanisho vya kauli za Serikali kwamba barabara ya Muheza - Amani itajengwa kwa kiwango cha lami, lakini barabara hiyo haiwekwi katika orodha ya Wizara inayoonyesha barabara zitakazojengwa kwa kiwango cha lami, lakini bado marekebisho hayo hayajafanyika. Ni matumaini ya wananchi wa Muheza hasa Tarafa ya Amani wakulima wakubwa wa chai, hifadhi ya Misitu ya Usambara na mvuto mkubwa wa utalii kwamba barabara hiyo itawekwa lami hata kama itachelewa.

Mheshimiwa Spika, upo ujenzi wa daraja unaoendelea katika barabara hiyo ya Muheza - Amani eneo la Ziggi. Niliwaarifu TANROADS Mkoa, juu ya wizi wa sementi katika eneo la kazi Ziggi na wasiwasi kwamba Mkandarasi asingeweza kumaliza kazi au ubora wa daraja hilo ungeshuka. Imetokea kweli sasa kazi zimesimama! Ni vyema uchunguzi ufanywe juu ya uwezo wa mkandarasi huyo ili kuokoa fedha za umma.

Katika barabara hiyo hiyo – Muheza – Amani, kampuni ya Chai ya EUTCO – Amani imekubali ombi nililowapa la kusaidia kuweka lami katika maeneo yenye kona kubwa na za hatari katika Milima ya Amani. EUTCO wamekubali na nimemuarifu Mkuu wa Mkoa kama Mwenyekiti TANROADS Mkoa na Meneja ZUTCO wasaidie kazi hiyo kwa usimamizi wa TANROADS. Bila shaka Mheshimiwa Waziri atasaidia kuwezesha EUTCO kupewa utaratibu wa utekelezaji.

Mwisho, Mheshimiwa Waziri asaidie kutekeleza ombi nililotoa wakati wa kujadili marekebisho ya sheria za barabara hivi karibuni ya kuunganisha barabara ya Mkoa ambayo sasa inatoka Bombani – Kimbo ili ikaungane na barabara ya Mkoa inayotoka Korogwe hadi Maguzoni (Wilaya ya Muheza). Kipande cha kuongeza Barbara hiyo ni kutoka Kimbo hadi Maguzoni. Hivi sasa TANROADS Mkoa wa Tanga wanatengeneza barabara hiyo toka Bombani – Kimbo (licha ya ukweli kwamba kwa miaka mingi utengenezaji haufiki Kimbo na Bodi ya Barabara Mkoa imepewa taarifa.

Ni vyema pia Mheshimiwa Waziri akatueleza utaratibu wa kufuata ili yale maombi yaliyokwishatolewa kupitia Bodi za Barabara za Mikoa kuhusu kuongeza orodha ya barabara mpya za Mikoa, utaratibu utakaofuatwa kwa utekelezaji hasa ukizingatia ukweli kwamba Wilaya ya Muheza ina barabara chache sana za Mkoa ukilinganisha na Wilaya nyingine. Naunga mkono hoja hii. MHE. HASSAN C. KIGWALILO: Mheshimiwa Spika, kabla sijachangia hoja iliyo mbele yetu, nami ninatoa rambirambi kwa niaba ya wananchi wa Liwale kwa familia na ndugu wa aliyekuwa Mbunge mwenzetu, Marehemu Amina Chifupa

133 kilichotokea kipindi hiki cha Bajeti, Mungu aulaze mwili wa Marehemu mahali pema Peponi. Amina!

Mheshimiwa Spika, ninaunga mkono hoja kwa asilimia 100. Aidha, ninampongeza Waziri wa Miundombinu Mheshimiwa Andrew J. Chenye na Manaibu Mawaziri wake pia. Ninawapongeza wataalam waliohusika na maandalizi ya hotuba hiyo nzuri. Haijawahi kutokea. Keep it up.

Mheshimiwa Spika, nachukuwa fursa hii kuwapongeza Waziri wa Miundombinu - Mheshimiwa Andrew J. Chenge, Naibu Mawaziri - Dr. Makongoro Mahanga na Mheshimiwa Dr. M. Daftari kwa ufuatiliaji wa karibu shughuli zote za miundombinu.

Mheshimiwa Spika, baada ya utangulizi huo, ninaomba nijikite katika Wilaya/Jimbo langu la Liwale. Mitandao ya simu za mkononi TIGO na CELTEL inafanya kazi Makao Makuu ya Wilaya Liwale Mjini pia na njia kuelekea Nachingwea – Umngara kuna mnara wa CELTEL, pia Kibutuka kuna mnara wa TIGO. Hivyo basi, mawasiliano ya simu yanapatikana hata ukiwa safarini kati ya Liwale na Nachingwea katika baadhi ya maeneo.

Pia TTCL na Vodacom wako mbioni kukamilisha mitandao yao Makao Makuu ya Wilaya Liwale. Ninashauri mitandao hiyo sasa ielekee barabara ya Liwale kwenda Kilwa. Maendeleo mengine muhimu kama Kikulyungu, Ngongowele, Nahoro na Lilombe, ambako pia kuna wachimbaji wadogo wadogo wa madini mbalimbali. Pia ninatoa shukrani sana kwa makampuni hayo ya simu kwa ushirikiano mkubwa ninaopata katika kuboresha mitandao hiyo ya simu.

Naomba minara ya Liwale Mjini ipewe nguzu zaidi ili ifike maeneo yote angalau radius ya kilometa 20 kutoka Liwale. Hivi sasa maeneo ya Makata, Mikunya, Gereza la Kipule na kadhalka. Ingawaje umbali usiozidi 10 kms. Simu haipatikani labda apande mlima au mti.

Mheshimiwa Spika, ninachukua fursa hii kuipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kuboresha barabara ya Liwale kwenda Nachingwea hasa kilomita zipatazo 30 za mchanga kutoka Liwale ambazo kilometa 13 zimeanza kushughulikiwa na kilomita nyingine 11 zitafuata. Nina imani kwamba ahadi za Mheshimiwa Rais aliyoitoa wakati wa kampeni mwaka 2005 akiwa Liwale kwamba barabara ya Liwale – Nachingwea, Nangurukulu – Liwale na daraja la Mto Ruhuu katika barabara ya Liwale kwenda Lilombe hadi Tunduru itakamilika.

Napongeza juhudi zinazoendelea, pia ninampongeza Naibu Waziri Mheshimiwa Makongoro Mahanga ambaye kwa ujasiri mkubwa sana aliona matatizo ya barabara kwa kupita barabara hizo, nazo ni Nangurukuru – Liwale. Liwale – Nachingwea. Pia alikwenda kuona Mto Ruhuu ambao maandalizi ya ujenzi wa daraja umeanza. Tunategemea Mheshimiwa Rais wakati wa ziara yake Liwale mnamo Septemba mwaka huu ataweka jiwe la msingi au kufungua daraja hilo. Hivyo ninashauri Serikali ihimize

134 TANROAD Lindi ifanye hima ipelekwe Bail Bridge Mto Ruhuu – Lilombe mapema ili ujenzi ukamilike.

Mheshimiwa Spika, mimi mwenyewe nimepita barabara ya Nangurukuru – Liwale, nimeona kazi inayoendelea vizuri ingawaje sina uhakika kama barabara hiyo itapitika wakati wa masika – vinginevyo ni hivi karibuni nimepita barabara hiyo, ilinichukua masaa manne tu toka Liwale hadi Somanga, haijawahi kutokea. Ulikuwa ni mwendo wa kutwa nzima.

Mheshimiwa Spika, ninapendekeza kwa barabara hiyo ambayo TANROADS imepania kuboresha kwa kutumia fedha za matengenezo ya kawaida ijenge makambi ili kuimarisha barabara hiyo wakati wa masika. Barabara hiyo ni ufunguo wa maendeleo ya haraka kwa wafanyabiashara na wananchi wa Liwale kwani inapolazimika kupitia Lindi kwenda Liwale ni ongezeko la zaidi ya kilomita 300. Hivyo, kuongezea gharama wafanyabiashara na wananchi wa Liwale kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, Natumaini kwa ahadi zote nilizopewa na Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu na Manaibu wake kwamba watanisaidia kuboresha miundombinu ya Liwale itakuwa ukombozi mkubwa sana kwa Wilaya hiyo ya Liwale. Ninaomba Mwenyezi Mungu awape afya na ufanisi wenye mafanikio kwa Wilaya ya Liwale. Naomba mnisamehe kwa usumbufu wowote nitapokuwa nikifuatilia kwa karibu.

Mheshimiwa Spika, Liwale ilikuwa na barabara kati ya Liwale na Wilaya Ulanga. Barabara hiyo inatokea Ndapapata Wilaya Liwale. Naomba Serikali kwa kushirikisha Wizara ya Maliasili, barabara hiyo ya umbali wa kilomita 50 kati ya Wilaya ya Ulanga na Liwale ifufuliwe ili ndugu wa Wilaya hizi waweze kutembeleana kwa urahisi zaidi. Ahsante ninaunga mkono hoja tena kwa asilimia 100.

MHE. ATHUMANI S. JANGUO: Mheshimiwa Spika, pamoja na kukupongeza wewe, Naibu Mawaziri wako wawili, Katibu Mkuu na Wasaidizi wenu kwa ujumla, naomba usikilize kilio cha wananchi wa Kisarawe. Wanasikitikia ukosefu wa barabara za kuaminika ingawa maendeleo ya sekta hii yamekuwa ya kichurachura (frog- jumping) kutoka Dar es Salaam, huko Kisarawe endeleza maeneo yaliyo mbali na Dar es Salaam.

Wanadai barabara ya Pugu - Kisarawe, Maneromango - Vikumbulu ijengwe kwa lami. Pili, wao na watalii wanaokwenda Selous waondokewe na adha ya barabara mbovu. Wanadai pia barabara ya Mlandizi – Mzenga - Maneromango ikamilishwe kwa ngazi ya changarawe. Vile vile wanadai kipande cha kilometa mbili kinachounganisha barabara za Pugu-Vikumbulu na Mzenga - Maneromango kijengwe katika ngazi ya changarawe.

Ili kupunguza mzunguko mrefu baina ya Makao Makuu ya Wilaya ya Kisarawe na Ofisi za Mkoa wa Pwani kule Kibaha, kupitia Dar es Salaam, nashauri barabara mpya ya Kiluvya – Kisarawe ijengwe katika ngazi ya lami. Vile vile msongamano wa magari baina ya Dar es Salaam na Chalinze, nashauri Serikali itazame pia uwezekano wa kurejea

135 utaratibu wa barabara ya Dar es Salaam – Kisarawe-Mzenga, Mafizi, Ngerengere hadi Morogoro. Kwa barabara hii kunahitajika ujenzi wa daraja katika Mto Ruvu.

Mheshimiwa Spika, kuhusu mawasiliano, wananchi wa Kisarawe hawana TTCL hawajaona haja ya kupeleka simu Kisarawe. Kampuni ya CELTEL ndiyo pekee inayothamini Soko la Kisarawe. Kwa hiyo, naiomba Serikali utilie mkazo suala la kuhamasisha kampuni za Vodacom na Tigo wapeleke huduma zao Wilayaji Kisarawe. Naunga mkono.

MHE. DR. JAMES M. WANYANCHA: Mheshimiwa Spika, napenda kukushukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia. Napenda kumpongeza Mheshimiwa Chenge Waziri wa Miundombinu na Manaibu Mawaziri wake kwa kazi nzuri wanayoifanya na hotuba yao nzuri.

Mheshimiwa Spika, naunga hoja mkono kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Spika, hali ya barabara za Wilaya ya Serengeti kwa sasa ni mbaya sana kutokana na mvua nyingi iliyonyesha katika mwaka 2006/2007. Barabara kama zile za kutoka Sirari Simba hadi Rung’abure, Mto Mara hadi Muguu, Mugumu hadi Fort Ikoma, Isanye hadi Ikoma Gate sasa hazipitiki baada ya kuharibika sana.

Mheshimiwa Spika, barabara hizi naona haziko katika bajeti ya mwaka 2007/2008. Tafadhali naomba jibu kwamba Serikali ina mpango gani wa kuzitengeneza hizi barabara ili ziweze kupitika?

Mheshimiwa Spika, barabara ya kutoka Mugumu hadi Fort Ikoma ni muhimu sana kwani ni kiungo muhimu sana kwa usafiri kutoka Mkoa wa Mara hadi Arusha. Hata hivyo hii barabara iko chini ya Halmashauri ya Serengeti na huwa inaharibika mara kwa mara kwa sababu Halmashauri haina uwezo wa kifedha za kuweza kuitengeneza baada ya kuharibika. Je, Serikali ina mpango gani wa kuiweka hii barabara chini ya TANROADS ili iwe inapatiwa matengenezo inayostahili mara baada ya kuharibika? Naomba Waziri anipe jibu juu ya hili.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali ina mpango wa kutengeneza barabara ipitayo Makutano, Natta, Mugumu Mjini, Tabora B, Loliondo hadi Mto wa Mbu kwa kiwango cha lami. Je, katika bajeti hii Serikali imetenga kiasi gani cha fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii? Kazi ya ujenzi itaanza lini? Tafadhali naomba majibu toka kwa Waziri wa Miundombinu.

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Spika, kwanza sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kunijalia kuwa na afya njema na kuniwezesha kuchangia hotuba hii kwa pekee. Nakishukuru Chama changu kwa kuweza kunichagua na leo kuwepo hapa.

136 Mheshimiwa Spika, nakupongeza kwa umahiri wako wa kuendesha Bunge hili bila ubaguzi na kufuatilia Sheria ya nchi na kanuni za Bunge na pamoja na Naibu Spika na Wenyeviti wake. Mheshimiwa Spika, vile vile natoa pole kwa wale wote walifariki kwa ajali mbalimbali za barabarani, majini na wale waliofariki kwa ajali ya angani na wale wanaotembea kwa miguu wakagongwa na magari au pikipiki au baiskeli.

Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Usafiri wa Anga ni moja kati ya kiungo muhimu kwa kuchangia mapato ya Taifa. Serikali kupitia Wizara ya Miundombinu katika kutekeleza majukumu yake, basi iviangalie viwanja vya ndege navyo wasivisahau.

Mheshimiwa Spika, kwa kweli kuna baadhi ya viwanja vingi ni vibovu na vidogo, vinahitaji kupanuliwa na kukarabatiwa kwa mfano kiwanja cha ndege cha Tanga, Mafia, na kiwanja cha ndege cha Karume Air Port kilichoko Pemba. Hicho kiwanja ni kibovu, ni mashimo matupu, siku za mvua hujaa maji na kidogo sana kinahitaji kupanuliwa. Watalii wengi hufika katika visiwa hivyo, lakini kutokana na mandhari ya viwanja hivyo huwa hawafurahi. Je, Waziri ni lini utatembelea viwanja hivyo?

Mheshimiwa Spika, usafiri wa majini na nchi kavu (SUMATRA), nimepata wasiwasi juu ya suala zima la usafiri wa majini juu ya usimamizi mbovu wa ukaguzi wa vyombo kama vile boti, meli, mashua na kadhlaika. Kwa mfano hai, hivi sasa vyombo vingi ni vibovu na hubeba abiria wengi mno kuliko uwezo kwake pamoja na kubeba mzigo mkubwa. Kwa hiyo, husababisha ajali ya vyombo hivyo kuzama. Kwa mfano boti ya MV Kabul iliyozama ilikuwa ikitokea Tanga kuelekea Pemba, ilizama kwa kuzidi uzito na nyinyi sio hizo tu, naiomba Serikali ijidhatiti kuokoa maisha ya watu na mali zao kwa kufanya ukaguzi mara chombo kitakapoondoka bandarini.

Mheshimiwa Spika, wasafiri wanaosafiri kwa kutumia magari au pikipiki au baiskeli kwa usalama wetu sisi wenyewe tuwe waangalifu, dereva akizidisha au akienda mwendo wa kasi, abiria waamue kushuka. Lakini naiomba Serikali, kwanza barabara zilioko vijijini mbovu, zijengwe, kwani nazo zinasababisha ajali. Vile vile madereva wanaoendesha magari hasa mabasi kama haitokuwa makini kila siku tutazika kaburi la pamoja.

Kwa hiyo, madereva akizidisha abiria ashitakiwe na apewe hukumu ya uhalifu. Nakutakia kila la kheri Waziri wa Miundombinu na Watendaji wako wote. MHE. WILLIAM M. NGELEJA: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu, Naibu Mawaziri wako, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Watendaji wa Wizara yako pamoja na Wakuu na Watendaji wote wa Taasisi zilizo chini ya Wizara yako kwa hotuba nzuri na mafanikio mliyoyapata wakati mnaendelea kutekeleza majukumu yenu. Aidha, naipongeza sana Kamati ya Miundombinu kwa kazi yao nzuri iliyojidhihirisha kwenye hotuba yao.

Mheshimiwa Spika, naishauri Wizara ifuatilie kwa karibu sana matumizi ya zile fedha ilizotoa mwanzoni mwa mwaka huu kwa ajili ya matengenezo ya dharura kwa barabara za Taifa na Mikoa (shilingi bilioni 10). Tusipokuwa makini, inawezekana

137 watendaji wasiokuwa waaminifu wanaweza kuchanganya na haya mafungu ya bajeti hii ili kuhujumu matumizi yake. Hili linawezekana kutokea kwa sehemu ambazo matumizi ya hizo fedha za dharura hayajafanyika kikamilifu mpaka sasa hivi. Udhibiti wa kina unahitajika.

Mheshimiwa Spika, nimesoma taarifa kwamba kivuko cha Kigongo - Busisi Ferry kinatarajiwa kuanza kazi Septemba, 2007. Hizi ni habari njema, ingawa imani kwa mkandarasi yule inapungua kwa vile amekuwa akibadilisha completion schedule!! Nawaomba msimamie kwa karibu zaidi. MV Sengerema iko hoi!!

Mheshimiwa Spika, napenda kumwuliza Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu: Je, ujenzi wa Usagara – Geita Rd (9 bn) utaanza lini hasa?? Tafadhali.

MHE. DR. GUIDO G. SIGONDA: Mheshimiwa Spika, miaka ya themanini Makao Makuu ya Jimbo la Songwe pale Mkwajuni kulikuwepo na miundombinu ya mawasiliano ya simu yaliyokuwa yakihudumiwa na TTCL. Miundombinu hiyo ilipoharibika katika miaka ya tisini haijarejeshwa tena. Naomba huduma hiyo irejeshwe.

Mheshimiwa Spika, pale Mkwajuni Jimboni Songwe kumejengwa mnara wa CELTEL ambao unahudumia mawasiliano ya simu za mkononi kwenye Kata tatu tu. Mkwajuni, Kanga, na Mbangala. Naomba minara mingine minne ijengwe kwenye Kata za Gua, Ngwala, Namkukwe na Kapalala. Kufanya hivyo kutasaidia kuunganisha mawasiliano ya simu za mkononi katika kata zote 10 kwenye Jimbo la Songwe. Mheshimiwa Spika, katika jimbo la Songwe huduma ya Posta hutolewa pale Mkwajuni. Huduma hizo hutolewa kwenye nyumba ya kawaida ya kuishi na huhudumiwa na mtumishi mmoja wa kike. Kutokana na huduma muhimu zinazotolewa za Posta, ni vyema mipango ikafanyika kujenga ofisi kamili. Mkwajuni ni miji mdogo.

Mheshimiwa Spika, naishukuru Serikali kwa kuainisha barabara muhimu kwenye Jimbo la Songwe katika mipango yake ya uendelezaji wa barabara nchini. Barabara hizo ni Mbalizi – Mkwajuni – Makongolosi, Gahula - Magamba - Namkukwe na sasa Kapalala.

Ninachoomba ni kwamba jitihada zilizoanza kufanyika ziendelezwe kwa kasi kidogo ili kero ya usafiri hasa wakati wa masika iweze kukabiliwa. Naunga mkono hoja.

MHE. YONO S. KEVELA: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Waziri wa Miundombinu - Mheshimiwa Andrew Chenge. Hotuba yake ni nzuri sana, imeeleweka. Pia nawapongeza sana Naibu Mawaziri - Mheshimiwa Dr. Makongoro Mahanga na Mheshimiwa Dr. Maua Daftari, pia Watendaji wa Wizara, Katibu Mkuu, kuna Mkurugenzi - Ndugu Ndunguru, nampongeza sana, aliwahi kuokoa fedha nyingi za Serikali, kawakufichua na kukamata magari ya Serikali yaliyokuwa yanatumika binafsi hivyo kuliiokolea Taifa mamilioni ya fedha. Sasa hivi naona yuko kimya, sielewi kuna nini.

138 Mheshimiwa Spika, barabara ya Dodoma – Iringa kupitia Mtera ninaomba sana Serikali yetu kwa kushirikiana na mfadhili Nordic Development Fund (NDF) ijengwe kwa kiwango cha lami. Itasaidia sana kuchochea maendeleo ya kiuchumi Nyanda za Juu Kusini. Serikali itengeneze barabara zile za muhimu kiuchumi mfano zile zinazofungua mipaka nchi za nje kama vile Kigoma – Tabora – Dodoma, Musoma – Arusha, Rukwa - Mbeya na Dodoma – Iringa – Mbeya.

Nasema hivyo kwa vile bajeti ya fedha ya Serikali ni ndogo na Wizara inajitahidi sana.

MHE. SIJAPATA F. NKAYAMBA: Mheshimiwa Spika, nyumba zilizowekewa ‘X’ ninapenda kuwapongeza Waziri na Naibu Mawaziri na watumishi wote waliopo chini yao, hotuba yao inaleta matumaini makubwa sana. Mheshimiwa Spika, ninapenda nitoe malalamiko ya wananchi wa Mkoa wa Kigoma ambao waliwekewa ‘X’ kwenye nyumba zao. Wananchi walitaka kujua: Je, ni lini watapewa taarifa ya bomoa bomoa ili waweze kujiandaa kusogeza nyumba zao nyuma? Sasa hivi yapata miaka minne na nusu. Kuna wengine wameanza kubomoa nyumba zao na hawajui kama kuna fidia au hakuna fidia. Wananchi walitaka kujua hilo.

Mheshimiwa Spika, sina nyongeza, bali naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE: Mheshimiwa Spika, pamoja na mikakati mizuri ya Serikali pamoja na bajeti yake, naomba nitoe maoni yangu na mchango wangu ili nijue mambo katika bajeti hii kuhusu barabara.

Mheshimiwa Spika, kweli wakandarasi waliopewa barabara hii ya Kigoma - Rusahunga wataweza kumaliza haraka? Tuna tatizo pamoja na wasiwasi sana! Kulingana na pori la Biharamulo barabara hiyo ingekwisha haraka kuokoa ujambazi.

Pili naomba Wizara ituwekee mawasiliano katika haya mapori mawili kati Muleba, Biharamlo na Kimisi na mara kwa mara nachangia mambo haya Bungeni. Naomba majibu kutoka kwako. Sioni katika bajeti hii kwamba mambo haya yatafanyika hata kama sio yote.

Mheshimiwa Spika, barabara za mikoani Kyetema hadi Katoro – Izimbya - Kyaka hadi Mlongo Karagwe naomba zitengenezwe.

Mheshimiwa Spika, je, uwanja wa ndege Bukoba Mjini, naomba niambiwe kweli kama utakarabatiwa au hapana tujue kama sisi watu wa Bukoba tumeshasahaulika kwa mambo yote. Uwanja unatutia aibu kubwa sana sisi wawakilishi pamoja na Serikali ya kasi mpya! Sio kasi tena, naomba nipate taarifa ya mambo hayo yote. Ni fedha kiasi gani tumetengewa kwa ajili ya barabara katika Mkoa wa Bukoba.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa bajeti kama Mkoa wa Kagera ukiwemo. Mungu awabariki Wizara nzima.

139 HAMZA A. MWENEGOHA: Mheshimiwa Spika, napenda kuanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu kwa hotuba yake nzuri sana. Pamoja na pongezi hiyo, napenda pia kuwapongeza Naibu Mawaziri wote wawili na Wakurugenzi wote wa Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, naomba kumshukuru Waziri kwa kupanga matengenezo ya kukarabati barabara kadhaa za Mkoa. Kwa bahati mbaya, Wizara imeisahau barabara ya Morogoro hadi Kisaki Station. Barabara hii ipo uk. 116 wa kitabu cha hotuba. Lakini sehemu korofi sana ya barabara hii ni Kilengezi, Mzambaraoni na Mngazi (Milengwelengwe).

Mheshimiwa Spika, pamoja na hilo, hakuna pesa zilizotengewa barabara hii tangu Morogoro hadi Kisaki. Hii ndiyo barabara kuu ya Wilaya ya Morogoro Vijijini.

Morogoro (V), ina barabara mbili ambazo ni Morogoro hadi Kisaki Station na Ubena -Ngerengere – Tununguo-Kiganila-Mvuha hadi Kisaki station.

Mheshimiwa Spika, barabara hii ina daraja la Mto Ruvu pale Kiganila ambalo litakuwa kiungo cha barabara hii kupitia Mvuha hadi Kisaki Station.

Namshukuru Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri wa Miundombinu (Mheshimiwa Makongoro Mahanga) ameitembelea barabara hii na kuona pale panapotakiwa kujenga daraja.

Mheshimiwa Spika, kitu cha kushangaza ni kwamba hakuna pesa zilizotengwa kwa daraja hili. Daraja hili pia ni ahadi ya Rais Kikwete.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mkoa ya Msalabani hadi Tawa imeachwa kabishara. Kwenye list haimo!

Mheshimiwa Spika, ninaomba nitoe shukrani zangu za dhati kwa kampuni ya CELTEL ambayo imetuwezesha kupata mawasiliano Wilaya nzima kwa mara ya kwanza tangu dunia ianze. Nawashukuru sana.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja hii.

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumpongeza Waziri wa Miundombinu pamoja na Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watendaji wote wa Wizara kwa kazi nzuri inayofanywa na Wizara hiyo.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali iwaeleze wananchi wa Dodoma wanaoishi eneo la Msalato ambapo Serikali itajenga uwanja wa ndege kuwa watalipwa lini fidia hii wahame eneo lile na kwenda maeneo mengine kwa shughuli za maendeleo? Namwomba Waziri atakapojibu hoja, alijibu na hili. Wananchi wamechoka kusubiri ahadi za Serikali kwa ajili ya malipo ya fidia. Pia uwanja wa ndege wa sasa bado unatumika, lakini uwanja

140 huo hauna taa. Je, kuweka taa uwanja wa ndege wa Dodoma unahitaji mamilioni ya pesa? Je, kuna tatizo gani linalokwamisha uwekaji wa taa uwanja wa ndege wa Dodoma?

Mheshimiwa Spika, tukumbuke kuwa uwanja huo unatumika kwa viongozi wetu wakuu wa nchi na pia wageni mbalimbali hasa kipindi cha vikao vya Bunge, hivyo kuna umuhimu wa kuimarisha uwanja wa ndege wa Dodoma kwa kuweka mahitaji muhimu. Serikali itoe programu ya uhakiki kuhusu ujenzi wa barabara ya Iringa – Dodoma – Babati. Barabara ya Dodoma – Babati ni kilometa 261. Serikali imetenga shilingi milioni 30 kwa ajili ya upembezi yakinifu na barabara ya Dodoma – Iringa kilometa 267 Serikali imetenga shilingi milioni 900 pesa za nje na shilingi milioni 50 pesa za ndani.

Mheshimiwa Waziri awaeleze wananchi kama shilingi milioni 30 zilizotengwa kwa ajili ya upembuzi yakinifu barabara ya Dodoma – Babati zitatosheleza kazi hiyo na kama hazitoshi kwa nini Serikali isitumie fedha zote kwa barabara moja, yaani Dodoma – Iringa na mwaka ujao wa fedha, fedha zikatengwa kwa ajili ya barabara Dodoma – Babati? Barabara hizo mbili zinatofautiana kwa kilometa sita tu, lakini kuna tofauti kubwa kwa fedha zilizotengwa kwa ajili ya upembuzi yakinifu. Tuelezwe pia kuwa shilingi milioni 30 zitafanya upembuzi yakinifu ya kilometa ngapi katika barabara hiyo?

Mheshimiwa Spika, mwisho naunga mkono hoja.

DR. LUCA J. B. SIYAME: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kutoa pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na Watendaji wote wa Wizara ya Miundombinu kwa hotuba nzuri iliyofanyiwa upembuzi yakinifu wa hali ya juu. Hivyo basi, naomba kuunga mkono hoja ya Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Mbozi Magharibi Mkoani Mbeya ni kati ya Majimbo yaliyoko nyuma kuliko yote nchini kimiundombinu ya mawasiliano ya barabara na simu. Ukiondoa kilomita 114 zilizoko kwenye barabara ya Tunduma – Sumbawanga inayopita kwenye Kata nne tu kati ya 11, eneo lingine hakuna mawasiliano ya barabara kwa miezi isiyopungua sita kwa mwaka. Kata hizo ni Kapele, Chiwezi, Msangano, Chitete, Chuhulumo, Kamwamba na Ivuna.

Mheshimiwa Spika, wakati wa Bunge la Bajeti la Mwaka jana Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu aliliarifu Bunge lako Tukufu kwa Daraja la Mto Momba kwenye barabara ya Mlowo – Kamsamba lilikuwa limefanyiwa upembuzi yakinifu kwa nia ya kutengeneza daraja la kudumu badala ya hilo lililoko ambalo ni la kubembea waya ambalo hakuna hata mtu anayeweza kuvusha gunia la chakula kwa baiskeli.

Kwa bahati mbaya kwa mwaka huu wa fedha hakuna fedha yoyote iliyotengwa kwa ajili ya shughuli hiyo.

Mheshimiwa Spika, pia kwa umuhimu wa barabara wa Kakozi – Kapele – Ilonga mpakani na Zambia, ni muda mrefu maombi yamekuwa yakitolewa ili barabara hii iweze

141 kutengenezwa na kupandishwa daraja kuwa ya Mkoa na hivyo kurahisisha usafiri kati ya Tunduma na Kasanga kwenye mwambao wa Ziwa Tanganyika.

Kwa sasa barabara hii kwa upande wa Mbozi iko chini ya Halmashauri ya Wilaya na haipitiki kwa miezi takribani sita kwa mwaka, wakati upande wa Jimbo la Kalambo Mkoani Rukwa ni ya Mkoa na hupitika mwaka mzima.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa mawasiliano ya simu, kama ilivyo kwa barabara, ni kata tatu tu kati ya 11 zenye mtandao wa simu aina yoyote. Kata za Kapele, Ndelambo, Chiwezi, Msanzano, Chitete, Chihulumo, Ivuna na Kamsamba hadi sasa hazina mawasiliano ya simu ya aina yoyote ile. Wananchi wa maeneo haya kutokana na kwamba yako mbali na sehemu zenye mawasiliano ya aina yoyote hulazimika kutumia njia za mawasiliano ya nyakati za ujima, yaani kutuma mtu kufikisha ujumbe sehemu nyingine. Mheshimiwa Spika, kutokana na yote niliyosema, mwananchi wa Jimbo la Mbozi Magharibi, wanaomba kwanza barabara ya Mlowo – Kamsamba pamoja na daraja la Mto Momba ili kuunganisha barabara ya Kilyamatundu katika Jimbo la Kwera Mkoani Rukwa vijengwe. Pili, barabara Kakozi – Kapele – Ilonga ijengwe. Tatu, Kata za kapele, Ndalambo, Chiwezi, Msangano, Chitete, Chuluhimo, Ivuna na Kamsamba zipatiwe huduma ya mawasiliano ya simu.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja ya Waziri wa Miundombinu kwa asilimia mia moja.

MHE. DIANA MKUMBO CHILOLO: Mheshimiwa Spika, napenda kutumia nafasi hii kwa njia ya maandishi kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tatu kwa kazi kubwa iliyofanya ya kuhakikisha barabara kuu, zote zinazounganisha Mikoa imekuwa katika mkakati wa kujenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, vile vile pongezi zangu nyingi kwa Serikali ya awamu ya nne kwa jinsi ilivyoendeleza kazi hii nzuri ya kujenga barabara hizi kwa kasi mpya, nguvu mpya na ari mpya Mwenyezi Mungu awatangulie ili kutekeleza azma yao.

Mheshimiwa Spika, sasa niwapongeze Mheshimiwa Andrew Chenge, Waziri wa Miundombinu, Mheshimiwa Maua Daftari, Naibu Waziri Mheshimiwa Makongoro Mahanga, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watendaji wote walioshiriki katika kuandaa bajeti hii kwa umahiri mkubwa yenye mwelekeo wa kuboresha miundombinu kwa maslahi ya Watanzania.

Mheshimiwa Spika, baada ya pongezi hizi, sasa nianze kuchangia kama ifuatavyo kwa lengo la kupatiwa majibu wakati Waziri/Manaibu Waziri wanafanya majumuisho.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa barabara ya Isuna – Manyoni. Naishukuru Serikali kwa jinsi inavyojitahidi kuhakikisha ujenzi wa barabara wa isuna hadi Manyoni, unakamilika baada ya kampuni ya SIETCO kushindwa kumaliza. Kwa kuwa Serikali

142 imetangaza tenda upya kwa barabara hiyo, napenda kuwatahadharisha kuwa kuna tetesi kuwa wako wakandarasi walioshindwa, bali wametuma tenda tena kwa majina mengine. Mheshimiwa Spika, vile vile naishauri Serikali ili barabara hiyo iwahi kumalizika itoe tenda kwa wakandarasi wawili kwa maana ya mmoja atoke Isuna na wa pili atoke Manyoni kama ilivyofanyika wakati wa masika. SIETCO ilikarabatiwa kilomita 25 na Konoike kilomita 30. Nimatumaini yangu muda wa kumaliza barabara hii utakuwa mfupi kuliko inavyotegemewa sasa ninaomba nijibiwe.

Mheshimiwa Spika, Uwanja wa Ndege Singida, Mkoa wa Singida bado uko nyuma kiuchumi hii ni kwa sababu ya kukosekana wawekezaji ambao wanaweza kuinua pato la wananchi. Sababu kuu ya wawekezaji kukosekana ni kukosekana kwa usafiri wa anga.

Kwa kuwa Mkoa ulianzisha ujenzi au kazi ya kukarabati na kupanua uwanja, naomba Serikali itamke kwa bajeti hii imetenga fedha kiasi gani kusaidia mradi huu wa kukarabati na kupanua uwanja wa ndege ili kuwasaidia wana Singida kupata wawekezaji na wananchi kupata usafiri wa haraka. Michango ya Serikali ya awali tunaitambua sana na tunashukuru sana.

Mheshimiwa Spika, kuhusu treni ya Dodoma hadi Singida, sina budi kuishukuru Serikali kwa kuwajali wananchi wa Singida kwa suala zima la usafiri kwa njia ya reli. Ninaomba kushauri yafuatayo ili niweze kupatiwa ufumbuzi kwa kuwa nimetumwa na wananchi.

Kwanza treni inakuja na behewa moja tu, watu wengi wanakosa nafasi na kubaki Dodoma ama Singida. Ninaomba mabehewa yaongezwe kwani injini ina uwezo wa kubeba hadi mabehewa sita. Vile vile siku za kwenda Singida ziongezewe toka siku tatu hadi tano.

Pili, reli ya Dodoma hadi Singida siyo nzuri hasa maeneo ya Mkwese, Isuna na Nkuhi wakati wa masika maji hupita na kusomba udongo. Ninaomba mataruma yabadilishwe yawekwe yenye uzito wa kutosha na tuta lishindiliwe upya. Kwa kufanya hivyo itasaidia treni isiendelee kuyumba ujumbe inapokwenda na kuwapa abiria mashaka. Nategemea majibu.

Mheshimiwa Spika, mwisho naomba nimalizie kwa kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja nikingojea majibu ili nisisumbuane na Waziri wakati wa majumuisho. Ahsante sana. MHE. ESTHER K. NYAWAZWA: Mheshimiwa Spika, nachukua fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na Watendaji wote toka Wizarani kwa kazi nzuri wanazofanya.

Mheshimiwa Spika, Wizara hii ni nyeti na kubwa inayotegemea kufungua njia za kukuza uchumi wetu kwa kuongeza ulipaji mzuri wa kodi. Tunashukuru hotuba ya

143 Waziri imetambua umuhimu wa kufanya njia za Mkoa kwa Mkoa na Wilaya kwa Wilaya, yote haya yakifanyika kufunga barabara za kufungua Mikoa.

Mheshimiwa Spika, naomba ninzungumzie barabara kuu. Dodoma - Manyoni – Singida hadi Mwanza, Dodoma – Babati – Arusha, Dodoma – Mtera – Iringa. Barabara nilizozitaja naipongeza Serikali kwa usimamizi mzuri kwa barabara kutoka Shelui – Igunga hadi Mwanza sasa ni Lami kabisa kwa kweli tunafaidi matunda ya CCM. Naomba nishauri mambo yafuatayo:

Kwanza, nashauri utengenezaji wa barabara katika Kijiji cha Isuna hadi Manyoni – TANROAD wakwangue waweke vifusi ili gari zipite bila usumbufu.

Pili, nashauri barabara ya Manyoni hadi Kijiji cha Puma lifanyiwe matengenezo ili usumbufu wa magari kukwama ziishe. Tatu, nashauri pawe na mpango maalum katika Mlima Sekenke, hapo ni eneo baya sana magari yanakwama naomba kipande cha Konokona pawekwe lami kama ya mlima Kitoka tukiwa tunasubiri barabara mpya inayotengenezwa na maendeleo yake ni mazuri nimepita pale tarehe 3/7/2007 kwa kweli madaraja yanasukwa vizuri sana.

Mheshimiwa Spika, naomba Waziri aangalie hotuba yake ukurasa 32 barabara. Kyamyorwa – Buzirayombo – Geita – Usagara ni km 312 inatarajia kukamilika Februari 2008. Nimesikitika ukurasa wa 33 maeneo kubwa barabara ya Usagara – Geita itakayoanza kujengwa mwaka 2007/2008 utakamilika Desemba 2010, namwomba Waziri anitoe wasiwasi kuisha kwa barabara hii iishe katika miradi ambayo tayari inaendelea kwa muda mrefu 2007/2008 iishe.

Mheshimiwa Spika, natoa pongezi kubwa kwa kuona umuhimu wa reli ya kasi, DSM – Dodoma – Tabora – Mwanza reli hii ni Mkombozi mkubwa kwa Watanzania wengi hivyo Wizara isimamie kwa karibu ili usumbufu uliopo hapa Dodoma uishe. Tunapata wageni sana tukiwa hapa Bungeni ni kupokea na kusafirisha kila siku. Tukomboe.

Mheshimiwa Spika, nawapongeza sana Wizara hii kwa kusimamia mawasiliano kwa kweli minara imeenea sehemu zote Tanzania, sasa ni mtu aamue awe na mtandao gani. Hongereni sana, hata maswali Bungeni yamepungua kabisa. Naomba hawa wenye mitandao wasizidishe bei ya matumizi ya simu hii, nina imani Waziri atawasimamia kwa karibu.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono bajeti ya Wizara hii ipitie bila mikwala kwa asilimia mia moja.

MHE. TEDDY L. KASELLA – BANTU: Mheshimiwa Spika, naomba kuongezea mchango wangu katika hoja iliyopo mbele yetu.

144 Mheshimiwa Spika, kwa kuwa ajali nyingi sasa zinazidi na kupoteza maisha ya raia ambao ni wazalishaji na wapiga kura zetu. Ushauri wangu mabasi yakaguliwe vyema kabla ya safari ili yawe imara na mazima kwa uhakika. Vile vile katika usafiri mrefu mfano kutoka Dar es Salaam, kwenda Mwanza kupitia Dodoma kuwa na madereva wawili au watatu ili dereva akitoka Dar es Salaam akifika Dodoma au Singida, amuachie dereva mwingine. Akichukua dereva mmoja Dodoma/Singida. Aende mpaka Mwanza na kadhalika. Hii inamfanya apumzike na mwingine fresh anapokea.

Mheshimiwa Spika, naamini madereva namaanisha dereva mmoja toka Dar es Salaam hadi Mwanza au Dar es Salaam/Tabora na kadhalika dereva anachotaka na ukiangalia na ubovu wa barabara zetu na ushenzi wa usingizi, mtu analala hata kwenye maji/tope na usingizi hauna adabu hata kama umefungwa minyororo utalala tu. Hivyo dereva akisinzia kidogo tu pale kwenye usukani, ajali tayari! Wasafiri wasio na kosa, wanakufa kwa wingi kama sisimizi. Ombi au ushauri wangu hapa, naomba matajiri wanaoajiri madereva, waajiri au watatu kwa safari ndefu.

Mheshimiwa Spika, lingine kwenye kona na milima na miteremko, madereva wapate mafunzo (training) ya kutosha na ya uhakika. Dereva makini lazima aweze kuendesha vizuri katika kupanda na kushuka milima. Kona pia ni muhimu, hasa ukizingatia barabara ubovu wa barabara. Madereva wengi wanaendesha magari yao upande ambao sio wao, wakifuata pale ambapo kidogo pazuri,sasa wote anayetoka/anayekwenda sehemu fulani mfano Singida na pana kona, madereva hawa wanagongana uso kwa uso.

Mheshimiwa Spika, ombi langu ni kwamba, pamoja na kutengeneza barabara zetu, lakini sehemu korofi nami naita kona pia hasa kona sharp (sharp corners) ziwe zinakarabatiwa mara kwa mara ili kuzuia ajali ambazo siyo za lazima.

Mheshimiwa Spika, naomba elimu ya bima comprehensive insurance ya magari (buses) ya abiria yote ili linapotokea la kutokea yaani ajali basi wasafiri walipwe, walioumia na waliokufa basi ndugu/jamaa zao wapewe fidia ili angalao kifuta jasho. Najua hii inaongeza gharama kwa matajiri/wenye magari ya abiria (buses), lakini sio ghali sana kama dhamini ya mtu aliyekufa, ambaye pengine ni nguvu kazi ya familia na taifa. Wizara ihakikishe gari (mabasi yote) ya abiria yawe na bima. Bima ziwe za aina zote za usafiri pamoja na wa majini.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja hii kwa asilimia 100. Naomba kuwasilisha.

MHE. OMAR ALI MZEE: Mheshimiwa Spika, usalama kwa vyombo vya habari ni suala nyeti kwani watu wetu wengi aidha hufanya shughuli za uvuvi katika bahari au katika maziwa kwa madhumuni ya kujipatia riziki ya kujikimu kimaisha. Lakini vyombo wanavyotumia kwa shule zao ni vyombo duni sana ambayo havikaguliwi, haviwi leseni na hata bima.

145 Kwa hiyo, naiomba Wizara husika kuvitathimini vyombo hivyo chini ya mamlaka husika na vile ambavyo vitaonekana havimudu majukumu yake viondolewe ili kupunguza uwezekano wa kuhatarisha maisha ya wavuvi husika.

Mheshimiwa Spika, minara ya kuongozea meli nyingi yao yamekuwa chakavu hasa katika bandari zetu za mwambao wa bandari ya Lindi. Vile maboya nayo yamekuwa yayawaki kama kawaida hivyo kusababisha usumbufu. Kwa vyombo vya usafiri katika bahari, hivyo basi ningependekeza Wizara kuitazama vyema minara na maboya ili iweze kufanya kazi zake kwa manufaa na usalama wa vyombo vyetu. Mheshimiwa Spika, usafiri wa nchi kavu hasa kwa Jiji la Dar es Salaam imekuwa sugu, pamoja na kutumia njia tatu wakati wa asubuhi na jioni bado tatizo linaendelea hivyo kuzifanyia ukarabati wa njia zinazoingia jijini ni jambo la aula, pamoja na kuzikarabati njia za mjini ambazo baadhi yake zimekuwa chakavu na madimbwi makubwa, zitarahisha usafiri wa jiji.

Mheshimiwa Spika, mtoto akinyea kiganja hakatwi mkono, ni vyema kumfahamisha na kumwelekeza. Hivyo, naipongeza Serikali kwa Shirika la Ndege (ATCL) limerudi tena kuwa shirika letu ambalo litakuwa mkombozi kwa Mtanzania na kwa vile asilimia 100 limekuwa letu pamoja na kuanzisha rasmi code yake. Pamoja na changamoto zinazolikabili ni budi sasa Wizara husika kuliboresha zaidi kwa madhumuni ya kufanyakazi zake bora zaidi pamoja na kuliongezea ndege na watumishi kwa manufaa ya Watanzania wote ili wapate kuruka na maisha na usafiri bora.

MHE. MICHAEL LEKULE LAIZER: Mheshimiwa Spika, napenda kuwapa hongera kwa shughuli nyingi ya Wizara yako. Napenda kuchangia baadhi ya barabara kwenye hotuba yako. Kwanza barabara toka Rombo – Tarakia – Rongai – Kamwanga. Lengo la barabara hii ni kufika Sanya Juu. Kwa kuwa wananchi wa Kamwanga huduma wanafuatia Sanya Juu, Hai na Arusha, hawazunguki mlima kuelekea Rombo. Barabara ilipofika Kamwanga nyumba nyingi zimevunjwa huku barabara imeishia hapo. Ombi naomba Serikali iende kuangalia na kuwapa fidia wale wote waliovunjiwa nyumba niliwahi kuleta idadi ya nyumba zilizovunjwa kwa Waziri husika wakati huo Mheshimiwa P. Mramba Mbunge.

Pili, Wilaya ya Longido imeomba barabara ya Kamwanga kwenda Longido Namanga Ipandishwe hadhi iwe ya Mkoa. Barabara hiyo itaungana na barabara ya Longido – Ketumbeine ambayo tayari imepandishwa hadhi inawezekana ikaungana na Ketumbeine lake Natron.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mwaka huu mmeweka bajeti ya barabara ya Arusha – Namanga ambayo kuanzia mwaka 1996 kulikuwa na ahadi kwa kila bajeti inawekwa lakini hakuna kinachofanyika mwaka huu. Naomba utekelezaji ufanyike. Kila mwaka kuna fedha za kukarabati barabara ya Arusha/Namanga ni muda mrefu ikiwa kwenye marekebisho ya ukarabati.

146 Mheshimiwa Spika, naomba kueleza tena kwamba kuna maeneo kwenye Jimbo langu ambayo haina mawasiliano. Kuna Tarafa ya Ketumbeine Wilaya ya Longido mpaka lake Natron ambayo inapakana na Tarafa ya Sale Wilaya ya Ngorongoro Loliondo. Tarafa hizi hazina mawasiliano. Jambo hili limefanya tarafa hizi kuwa makazi ya Wasomali kwa kuwa hawana mawasiliano hata wanaparamiwa hawawezi kutoa taarifa kwa ajili hakuna mawasiliano eneo hilo bado inaitwa Tanganyika kwa sababu ni eneo ambalo hakuna mawasiliano kwa kuwa kuna tetesi kwamba kuna kiwanda cha Soda Ash inayotakiwa kujengwa, basi ni afadhali kuwa na mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, reli ya ukanda ya kaskazini. Naomba Wizara ifufue reli ya Tanga/Moshi/Arusha itoe huduma ya kubeba abiria na mizigo kwani tunapoingia kwenye biashara ya Afrika ya Mashariki ni lazima miundombinu iwepo. Nadhani zamani reli ilipojengwa ni wakati huu ndiyo njia hii inahitajika zaidi kuliko wakati ule reli ilipojengwa.

Naomba reli hii ifanye kila liwezekanalo ili reli hii itoe huduma kanda ya Kaskazini na nchi ya Kenya/Uganda na Ukanda wa Ziwa ambao watachukua mizigo yao Arusha.

MHE. EPHRAIM N. MADEJE: Mheshimiwa Spika, kwanza ripoti/hotuba ni nzuri. Kazi ya Waziri na Wizara ni nzuri. Mheshimiwa Chenge na wenzake wametatua matatizo ya mikataba na ujenzi wa barabara zifuatazo katika muda mfupi sana. Ninawapongeza. Barabara ya Dodoma/Manyoni, barabara ya Manyoni, barabara ya Mbwemkuru/Migoyo.

Aidha, wameinasua ATCL kutoka kwenye makucha ya ubia na South African Airways. Matarajio wataelekeza juhudi zao kutatua matatizo ya Shirika la Posta, Reli na TAZARA. Kufuatana na vigezo vyote barabara ya Ihumwa/Mayamaya kupitia Hombolo/Gawaye, inastahili kuwa ya Mkoa. Naomba irudishiwe hadi yake kama ilivyokuwa zamani. Wananchi wa Msalato ambao wanapisha ujenzi wa kiwanja kipya tafadhali watendewe ujenzi wa Kiwanja kipya, tafadhali watendewe haki kwa kulipwa fidia. Wamesubiri kwa muda mrefu na maendeleo yao binafsi yanadumazwa.

Barabara za Dodoma Mjini zilizo chini ya TANROADS zifanyiwe matengenezo/ujenzi wa uhakika. Ni aibu kwa Kuu Street kufumuliwa na kujengwa upya kila baada ya miezi michache. Aidha, mpango ufanywe ziwekewe taa za barabarani.

Mheshimiwa Spika, barabara nyingi ya mji wa Dodoma hali yake ni duni sana. Kuitegemea Manispaa ilete maendeleo ya barabara hizi ni kujidanganya wenyewe. Naomba nielezwe kwa nini utaratibu uliotumika katika ujenzi wa barabara za Mji wa Mwanza usitumike Dodoma pia? Mradi huo umetekelezwa chini ya Wizara ya Miundombinu. Mradi wa kuzijenga kwa lami barabara za Minjingu/Dodoma na Dodoma Iringa umekuwa kwenye mpango wa maendeleo kwa miaka mingi sasa. Barabara hii ni sehemu ya The Great North Road ambayo historia yake ni ndefu na imeanza wakati wa wakoloni. Ninauliza yafuatayo:-

147 (i) Kwa nini barabara hii haipewi umuhimu unaostahili? Siyo siri kwamba miradi mingi iliyokuja nyuma sasa inatekelezwa lakini yenyewe inaachwa.

(ii) Serikali haioni kwamba nchi inajiongezea gharama bila sababu za msingi kutokana na magari yanayosafiri kutoka kaskazini mwa nchi kwenda kusini (and vice versa) inabidi yawe na mzunguko mkubwa kupitia Chalinze na Morogoro kwa kukwepa ubovu wa barabara ya Arusha/Dodoma/Iringa?

Mheshimiwa Spika, pamoja na matatizo hayo yaliyopo naunga mkono hoja.

MHE. LUDOVICK J. MWANANZILA: Mheshimiwa Spika, pongezi kwa kazi nzuri, endeleeni na wajibu huo. Naomba celtel wafungue mapema minara ya matai Kisumba Kasote na Kasanga. Bandari ya Kasanga ianze kukarabatiwa mapema kama ilivyopangwa.

Kiwanja cha ndege Sumbawanga kimesahaulika kiwekewe lami runway kuepusha rabsha wakati wa kuruka ndege za viongozi pia. Hili litasaidia ndege za kiraia kuanza kwenda Sumbawanga.

MHE. HASNAIN G. DEWJI: Mheshimiwa Spika, kwanza naipongeza sana kwa Wizara kujitahidi kuboresha barabara zetu nchini. Mimi bado nina matatizo na barabara ya Ndundu Somanga ya kilometa 65. Nilikuwa na swali hapa Bungeni kuhusu barabara hii nikaambiwa bado mkandarasi hajapatikana. Je, ni lini barabara zitaanza kutengenezwa na mkandarasi ameshapatikana? Nimeona pesa zimepatikana, zipo. Tunaomba sana barabara hiyo mkandarasi apatikane kwa haraka kabla ya mvua kubwa. Naomba kujua kuhusu barabara ya Morogoro – Dodoma ya kilometa 254.

Mheshimiwa Spika, inashangaza barabara hiyo haina ubora (sub standard), yaani imekabidhiwa, lakini ni viraka viraka. Je, Wizara imechukua hatua gani Kwa mkandarasi? Hatuoni Serikali imepoteza fedha nyingi. Nataka nifahamu juu ya ubora wa barabara yaani Morogoro – Dodoma 254. Tatizo lingine Wilayani kwetu Kilwa bado mengine hawafuatilii ubora wa barabara za Changarawe. Naomba Wizara kufuatilia Maafisa hawa ili ubora wa barabara hizo ziwe bora. Bado kuna ubovu wa kufuatilia huko Wilayani, naomba sana tuweze kuwadhibiti na kufuatilia tatizo hili.

Mheshimiwa Spika, la mwisho mifugo kupitishwa ovyo katika barabara Nangurukuru – Mbwemkuru. Ninaomba Wizara kufuatiliahawa wafugaji kwa jinsi uharibifu huu wa barabara unavyofanywa na wafugaji Wizara kuliona hilo. Naomba kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Ahsante.

MHE. SAMUEL CHITALILO: Mheshimiwa Spika, kwanza nachukua nafasi hii kukupongeza Waziri, pamoja na uongozi mzima wa Wizara husika kwa hotuba nzuri. Hii imeandaliwa vizuri sana na kwa umakini wa hali ya juu.

148 Mheshimiwa Spika, pia nashukuru sana kwa ujio wa Rais katika Jimbo langu la Buchosa.

Baada tu ya Rais kufika na kutoa maagizo ya barabara zangu zilizokuwa zinatisha kwa ubovu tayari zimeanza kushughulikiwa kupitia ofisi ya Meneja wa TANROAD Mwanza. Hivi majuzi nilikuwa huko baada ya kuona juhudi zinazoendelea za kutengeneza barabara hata nguvu ya kusema nichangie hapa nimeona sina sababu.

Natoa tu ushauri wa jumla kwa kuwa barabara za udongo zinaigharimu Serikari pesa nyingi kwani kila zikitengenezwa ni baada tu ya muda zinaharibika, jaribuni kuangalia uwezekano wa kuanza kutumia katika barabara hizi lami ya bei nafuu ili kuepuka kuharibika barabara hizi za vumbi mara kwa mara.

Ombi kutoka kwa wananchi wa Buchosa, wanaishukuru Wizara ya Miundombinu kwa kuhakikisha mradi wa ujenzi wa barabara zilizopo Wilayani Sengerema kwa pesa ya Benki ya Dunia na pesa ya hapa kwetu. Vinginevyo sina nyongeza bali naunga mkono hotuba hii kwa asilimia mia moja.

MHE. ANNE S. MAKINDA: Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri na wasaidizi wake wote kwa kazi nzuri ya kuiongoza Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, napenda kupata maelezo kuhusu mpango wa Serikali kukarabati barabara ya Mkoa wa Iringa inayotoka Njombe – Itoni hadi Ludewa. Kila mwaka barabara kutoka Itoni Uwemba, Luponde na Matola sehemu ya Kona kila mwaka inakuwa ni hali mbaya sana. Eneo hili lina uzalishaji mkubwa wa chai na viazi. Makandarasi wanaopewa barabara hii huweka udongo wa chai na siyo kifusi. Kifusi imara kipo hata kama sehemu nyingine kifusi hicho kipo mbali kidogo na hapo wakandarasi wanapojenga. Lakini kipo na ni kifusi imara sana.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali inisaidie kipande hicho cha barabara kifanyiwe matengenezo yanayostahili kiwanda cha chai cha Luponde hata hivi sasa wanapata tabu kupeleka chai iliyosindikwa kwenda Dar es Salaam, mafuta ya kiwanda kwenda kiwandani na wananchi wanashindwa kupeleka viazi kwenda kwenye soko Dar es Salaam, Songea na Dodoma.

Nina matumaini kuwa Serikali itafanyia matengenezo barabara hii hasa sehemu ambayo ni mbovu sana. Kwa kuwa mimi kama Naibu Spika siwezi kuongea Bungeni, wapiga kura wangu wanauliza sasa barabara hiyo ataisemea nani?

Mheshimiwa Spika, naomba msaada wako Mheshimiwa Waziri naunga mkono hoja hii.

MHE. DR. CYRIL AUGUST CHAMI: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu, Waheshimiwa Waziri wa Miundombinu, Waheshimiwa

149 Manaibu Waziri, Katibu Mkuu Dr. Enos Bukuku, Naibu Katibu Mkuu Eng. Chambo, Watendaji wote.

Mheshimiwa Spika, refer Kitabu cha Hotuba ya Waziri wa Miundombinu, ukurasa 115. Rehab Arusha Road – Umbwe – Kibosho road – Kirima (km. 60) rehab Uru (Rau) – mlimani road (km.5.)

Kilio changu ni juu ya barabara hizo mbili. Ni barabara ambazo Mheshimiwa Rais aliahidi kuwa zitajengwa kwa lami na amekuwa akiirudia ahadi hii kila akitembelea Kilimanjaro.

Mheshimiwa Spika, nilimwandikia Mheshimiwa Waziri, kumbukusha ahadi hii naye akanijibu kuwa zingetengewa fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu. Hali imebadilika na sasa barabara hizi zimetengewa shilingi milioni 60 na shilingi milioni 50 kwa rehabilitation na siyo kwa upembuzi yakinifu.

Mheshimiwa Spika, wakati Wabunge wengine wanasifu kuwa wameangaliwa mimi nasikitika kusema kuwa kutotenga fedha kwa barabara hizi kwa upembuzi yakinifu kutaleta masononeko makubwa Jimboni. Izingatiwe kuwa wananchi hawa walichanganya fedha wakanunua lami matanki 3,500 ambayo zaidi ya nusu imeharibika, sasa baada ya juhudi zao kutokuungwa mkono na Serikali inaendelea kuharibika.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Moshi Vijijini lilikuwa chini ya upinzani kwa miaka 10 na limerejea CCM kwa matumaini makubwa kuwa litaangaliwa. Kuchelewa kwa ahadi ya Mheshimiwa Rais kunawafanya Wapinzani waanze kusema maneno ya kuwakatisha wananchi tamaa na CCM na Serikali yake.

Mheshimiwa Spika, naiomba Wizara ibadili matumizi ya fedha hizi zilizotengwa, shilingi milioni 60 kwa barabara ya Uru ili badala ya rehabilitation ziwe kwa ajili ya upembuzi yakinifu. Urefu wa barabara hizi ni kilometa 43 kwa ile ya Kibosho na kilometa 12.5 kwa ile ya Uru.

Tafadhali chonde chonde Wizara isaidie ili imani ya wananchi kwa Rais wetu isiyumbishwe na maeneo ya Wapinzani.

Mheshimiwa Spika, nashukuru.

MHE. TEDDY L. KASELLA - BANTU: Mheshimiwa Spika, kwanza nashukuru kwa kunipa nafasi hii ili nami nichangie katika hoja iliyopo mbele yetu.

Mheshimiwa Spika, bila kuchelewa na kusahau, naunga mkono hoja hii asilimia mia moja. Pia nampongeza Mheshimiwa Waziri na Manaibu wake wawili kwa kufanya kazi kwa ari mpya na kazi mpya. Nawapongeza sana.

150 Mheshimiwa Spika, sasa niende moja kwenye moja katika barabara zilizo katika Jimbo langu la Bukene kwanza, halafu nitaendelea katika Wilaya yangu, Mkoa wangu na hatimaye Taifa.

Mheshimiwa Spika, kutokana na ahadi ya Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati alipopita mwaka 2005 akiomba kura za Mbunge wake ambaye ni mimi na Madiwani wote wa Kata zote ambao tulipata wote CCM. Bila kuchelewa ni barabara ya kutoka Tabora – Maambali – Itobo – Nzega, na Itobo – Igusule – Kagongwa – Kahama na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, barabara hii nimeiona ukurasa wa 125 na inaonyesha Maambali – Bukene na katika hotuba hii ukurasa was 167 barabara ya Nzega – Bukoba (T3). Naamini barabara hizi zikitengenezwa, basi nitakuwa nimemaliza barabara inayopita na ndio ahadi ya Mheshimiwa Rais wetu. Nashukuru kuona hii na sasa naomba itengenezwe ili iwasaidie wananchi wa Jimbo la Bukene. Barabara ni uchumi na maendeleo.

Mheshimiwa Spika, tunaomba hitimisho la barabara hii. Barabara hii ni ya kiwango cha changarawe, naomba iwe kiwango cha changarawe na sio tope. Mvua ikija, inakwenda na madaraja na udongo (ina be washed away). Tunaomba makandarasi watengeneze ili barabara ziwe imara na siyo kukwangua tu. Nawapongeza wale waliotengeneza kile kipande cha Tabora – Maambali. Hongera sana. Naomba iendelee hivyo hivyo, ubora ule ule Maambali – Bukene na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, kuna barabara inayojulikana kama Old Mwanza Road toka Tabora. Hata Naibu Waziri, Mheshimiwa Dr. Makongoro Mahanga alipotembelea kukagua barabara Mkoani Tabora, tulipofika Maambali, wananchi walimwomba kwamba barabara hii ya Old Mwanza ambayo inapita Semembela kwenda Chambo – Kahama – Geita – Mwanza. Barabara hii itawasaidia sana wananchi hasa wakulima, kwani huku ndiko kwenye mazao kweli kweli. Wasaidieni wakulima hawa ili wafikishe mazao yao sokoni, ndani na nje ya nchi ili waondokane na umaskini.

Mheshimiwa Spika, naamini kabisa wakulima wa Semembela wanaweza kulisha Tabora, Mwanza bila kuacha Nzega, Shinyanga, Dar es salaam. Naomba tuwasaidie wananchi hawa wawe na maisha bora.

Mheshimiwa Spika, kuna madaraja katika Jimbo langu ambayo yameharibika sana au yamezunjika hasa madaraja ya Kata ya Mwamala na Kata ya Ikindwa. Naomba madaraja yachukuliwe na Serikali Kuu kwani tukiyaacha kwenye Halmashauri ya Nzega, daraja moja tu la Mwamala linamaliza pesa yote (budget) yote. Kwa misingi hiyo, naomba Halmashauri ya Nzega isaidiwe, kwani ni Serikali ile ile ili kuondoa kero kwa wananchi, wakulima, wafugaji wa Jimbo la Bukene. Chonde chonde, naomba tusaidiwe madaraja haya ili tufanikishe shughuli za kiuchumi ili nasi tujikwamue na tuondokane na umaskini.

151 Mheshimiwa Spika, niende kwenye usafiri wa Reli. Naomba reli kutoka Mwanza – Tabora na Kigoma – Tabora zote kufika Dodoma, reli hii iendelee hadi Dar es Salaam. Watu wanapata taabu sana hasa akina mama na watoto.

Kwa hiyo, naomba reli hii ifike Dar es Salaam ili msafiri anapoondoka Kigoma kwenda Dar es Salaam asishuke na anapotoka Mwanza kwenda Dar es salaam pia asishuke, ni moja kwa moja mpaka Dar es Salaam.

Vile vile mizigo itasafirishwa kwa Goods Train na hivyo kuzuia uharibifu wa barabara kwani barabara nyingi ni mbovu kwa sababu kuna magari yanayopakia mizigo mizito na inapitishwa kwenye barabara ambazo haziwezi kuhimili uzito wa gari. Kama kuna njia ya reli, mizigo hii itasafirishwa kwa njia ya Goods Train na hivyo kuzuia uharibifu wa barabara.

Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha barabara siku zote zinapitika wakati wote, yaani wakati wa mvua na wakati wa kiangazi, nashauri pawe na makambi kama zamani (PWD) ili mfanyakazi/wafanyakazi wawepo kuangalia kazi kila siku kwa kipande hicho ili kuwezesha barabara kutengenezwa mapema iwezekanavyo kwani inajulikana mapema ubovu wake.

Mheshimiwa Spika, watu wa Kata ya Igusule waliniomba kwamba Train katika Railway Station ya Igusule, isimame angalau kwa dakika tano hivi kwa sababu kuna wazee, wanawake na watoto wanaoshuka au kupanda hapo Igusule. Kwa ombi hilo na kuzingatia wasafiri hawa, naomba muda uongezwe hadi kufikia angalau dakika 10 ili kuwawezesha akina mama, watoto na wazee kwa ujumla kushuka na kupanda bila matatizo na pia kuepusha ajali. Naamini ombi hili litakubaliwa kwani ni la msingi kabisa.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Kata ya Mogwa na Kata ya Isagenhe wameomba kupata Check Point, yaani Kivuko ili kuwasaidia wakulima na wafugaji waweze kuvusha mazao na mifugo kutoka Kata ya Mogwa kwenda Kata ya Isagenhe. Maombi yamekwishapelekwa kwa wahusika, imebaki kupata majibu toka Makao Makuu ya Reli Tanzania, Dar es Salaam. Naomba nipate majibu mazuri ili wananchi, wakulima na wafugaji wa Bukene wapewe kivuko hapa kati ya Kata ya Mogwa na Kata ya Isagenhe.

Mheshimiwa Spika, napongeza makampuni yote ya mtandao wa simu. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba kwa muda mfupi sana baada ya kuwafuata Kampuni ya Tigo na Celtel, wamekwishafika Bukene. Hongera sana. Ila cha kushangaza, niliwakimbilia sana watu wa Voda, lakini hadi leo hii hawajafika Bukene. Kwa kupitia hotuba hii, naendelea kuwaomba waje Bukene. Mtandao huu una shida katika Kata ya Mwangoye kwenye Centre yake ya Chamipuli. Naomba waongeze mnara/minara ili wananchi wa Chimpuli Centre, Kata ya Mwangoye wapate mawasiliano mahali popote kwani hapa unaweza kuzungumza jikoni, dukani hakuna. Kwa misingi hiyo, simu inanoga uzungumze mahali popote. Kwa taarifa tu, Mwangoye ndio sehemu inayolima

152 mpunga kwa wingi sana. Simu inahitajika sana ili kufanya biashara ya mpunga ndani na nje ya nchi na hivyo kujikwamua na kuondokana na umaskini.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia hakuna mawasiliano ya simu toka Nzega, Tabora. Hapo katikati hakuna mawasiliano. Naomba minara isawazishwe ili mawasiliano yawepo njia yote Nzega,Tabora. Naomba kuwasilisha. MHE. MOSSY SULEIMAN MUSSA: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa napenda kuunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja. Napenda pia kuungana mkono na Waheshimiwa Wabunge wenzangu kwa kutoa rambirambi zangu kwa familia ya Marehemu Amina Mpakanjia kwa msiba wa mtoto wao. Zaidi tumwombee kwa Mungu ampokee na amlaze mahali pemba Peponi. Amin.

Mheshimiwa Spika, Wizara hii ya Miundombinu ndiyo Wizara mama katika Wizara zote kwani Wizara hii ndio ufunguo wa maendeleo ya uchumi wa nchi yetu. Hivyo tunapaswa tuiunge mkono kwa dhati hasa katika kuongeza matumizi katika bajeti zinazofuata.

Mheshimiwa Spika, pamoja na msisitizo wa ujenzi wa barabara zetu, lakini bado utunzaji hauendani na gharama za ujenzi wenyewe, nina maana kile kitengo cha PWD kiimarishwe ili kifuatilie mipasuko, mifereji na nyasi ili kuepusha kile Waswahili wanachosema “usipoziba ufa, utajenga ukuta.” Hii ni sahihi kabisa kwa sababu hata katika town centre unaweza kukuta mashimo ya ajabu ambayo sio tu yanaweza kuharibu barabara nzima, lakini pia yanaweza kusababisha ajali kwa madereva. Kama ni uangalizi ni wa Halmasahrui zetu, basi Serikali Kuu itoe msukumo.

Mheshimiwa Spika, Wizara hii inajisahau mno kama ni mlezi wa maisha ya watanzania, kwani vivuko, meli, anga, sekta hizo zinazembea sana kwa kuwa kwa namna fulani, ufuatiliaji wa kiufundi unakuwa mdogo sana. Mfano, hivi karibuni Ziwa Victoria viongozi walitaka kuzama na kupoteza maisha kwa uzembe. Pia meli za Pwani, nguvu za viyoyozi vyake ni hafifu wakati zimebeba abiria zaidi ya 100, ndege kufunguka milango ikiwa angani. Naomba sana ufuatiliaji uwe wa kimataifa.

Mheshimiwa Spika, Idara ya Hali ya Hewa iboreshwe kwani wakulima, wavuvi na kadhalika wanategemea Idara hii. Inapaswa iwe na vifaa vya kisasa ili wanachokitabiri kiende sawa na matumaini ya wahusika.

Mheshimiwa Spika, lingine ni jambo ni la msingi kabisa kwamba ipo tabia ya ujenzi wa barabara kufikia umaliziaji ikaachwa na kushika barabara nyingine na hivyo kusababisha ile iliyoanzishwa kufa kabisa. Napendekeza tujenge kwa utaratibu wa “maliza kwanza, anza nyingine!” Mheshimiwa Spika, kuwe na uangalizi wa malori yanayozidisha uzito kwani ni chanzo cha kuzimaliza barabara zetu. Hivyo Maafisa wetu waangalizi wa Mizani wawe wazalendo, wenye kujali maslahi ya nchi badala ya kuwaendekeza madereva wasio waaminifu kwa ghilba ya fedha.

153 Mheshimiwa Spika, uangalizi wa madaraja ni muhimu sana kwani ujenzi wa miundombinu hiyo unahitaji gharama kubwa. Kwa hiyo, uwepo utaratibu maalum wa utunzaji wa madaraja. Mifano hai ni barabara ya Dodoma – Dar es Salaam, baadhi ya madaraja yameng’olewa support zake za pembeni, lakini hakuna immediate repair na hivyo kusababisha baadaye gharama kubwa ya kukabili tatizo hilo.

Mheshimiwa Spika, bila ya kuwapongeza watu wa huduma za simu, itakuwa si vyema. Hivyo, nawapongeza sana Celtel, Zantel, Vodacom na Tigo kwa ufanisi wao wa kutoa huduma kwa Watanzania. Nawapongeza zaidi katika support yao kwa maendeleo ya jamii katika miji na vijiji kadhaa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, naomba Wizara hii iangalie suala la ujenzi wa daraja la Kigamboni lisiwe suala la siasa, bali iwe utekelezaji hasa na ikiwezekana kabla ya uchaguzi wa 2010 ujenzi uwe umekwisha au uwe umepiga hatua kubwa. Naiomba Wizara hii ifuatilie pia vyoo vya vituo vya mabasi, ni ovyo sana wakati abiria tunachangia pesa kwao. Ni aibu wakati wa kujisaidia, kwani mnakuwa kama wanyama wakati Watanzania tunajivunia heshima zetu kwa rika tofauti. Ahsante! Naunga mkono hoja.

MHE. MWADINI ABBAS JECHA: Mheshimiwa Spika, kwa muda mrefu sasa tumekuwa tunashuhudia ajali nyingi za barabarani na pia ajali za baharini/Ziwani. Sababu ambazo zimekuwa zikitolewa mara nyingi ni uzembe wa dereva, ubovu wa magari na ulevi wa kupindukia. Lakini sio mara nyingi kutajwa ubovu wa barabara.

Ni vyema basi Serikali pamoja na kuwabana madereva kuwa makini wanapoendesha magari na kuwataka wamiliki wa magari kuhakikisha kwamba magari yanayotumika na hasa yale ya abiria na mizigo yawe ya viwango na uzima unaokubalika. Kwa kweli itakuwa ni busara kubwa pia Wizara nayo kukubali sehemu ya lawama hasa pale ajali inapotokea inahusiana na ubovu wa barabara. Kuna wakati na hasa pale mvua zinapokuwa kubwa, miundombinu mingi huharibika. Kwa bahati mbaya matengenezo ya miundombinu hiyo huchukua muda mrefu kufanyiwa matengenezo. Hali hii nayo huleta usumbufu mkubwa kwa wasafiri wa nchi kavu na pia kuongezeka kwa ajali za barabarani.

Mheshimiwa Spika, ni vyema basi Serikali ikachukua jitihada za makusudi kuhakikisha kwamba barabara zinazojengwa zinakuwa imara na madhubuti na zinazofikia viwango vinavyokubalika. Aidha, pale panapotokea uharibifu wa miundombinu ya barabara na reli, Serikali isichukue muda mrefu kutengeneza miundombinu hiyo.

Mheshimiwa Spika, usafiri wa majini nao tumekuwa tukishuhudia ajali nyingi ambazo zimesababisha vifo vya wananchi wengi. Sababu ambazo zimekuwa zinachangia ajali za majini ni pamoja na uchakavu wa vyombo vya usafiri, ukosefu au ubovu wa maboya ya kuongozea vyombo vya usafiri na ukosefu wa vyombo na vifaa vya kuokolea maisha na kadhalika. Ili kupunguza vifo vya Watanzania/binadamu katika usafiri wa majini ni vyema basi Serikali ikahakikisha kwamba vyombo vyote vya usafiri

154 vinafanyiwa ukaguzi wa kutosha kubaini uzima/uchakavu na iwapo kuna vifaa vya kutosha vya kuokolea maisha. Lakini la msingi zaidi ni kuhakikisha kwamba vyombo vya usafiri hasa vya abiria na mizigo vinawekewa bima ili kuweza kudhibiti hasara zinazoweza kutokea zinapotokea ajali za majini (Baharini/Ziwani).

Mheshimiwa Spika, ninaiomba Serikali kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa maboya ya kuongozea vyombo vya usafiri majini. Matengenezo ya maboya mabovu yasichukue muda mrefu na pale inapowezekana maboya yote machakavu yabadilishwe haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Spika, usafiri wa abiria na mizigo kati ya Pemba, Tanga na Mombasa, mara nyingi unakuwa ni wa kutumia majahazi na vyombo vingine vya mbao. Mimi nina wasi wasi iwapo Serikali inafuatilia ipasavyo viwango vya abiria na ujazo wa mizigo katika vyombo hivyo. Matokeo yake ni kwamba vyombo hivyo hupakia mizigo zaidi ya uwezo wake na kadhalika abiria.

Aidha, sidhani kama vyombo hivi vina vifaa vya kuokolea maisha. Naomba Serikali itupie sana macho usafiri wa baharini kati ya Pemba, Tanga na Mombasa kwa sababu maeneo haya hayana usafiri wa uhakika wa vyombo vya kisasa. Mheshimiwa Spika, usafiri wa ndege kati ya Tanga – Pemba, Pemba – Zanzibar na Zanzibar – Dar es Salaam, mara nyingi huwa ni wa ndege ndogo ya Mashirika ya ZanAir, Coastal, Tropical na na ndege ndogo za kukodi. Nichukue nafasi hii kuwapongeza wamiliki na watendaji wa Mashirka haya. Tatizo langu katika usafiri huu ni hofu yangu juu ya uzima wa baadhi ya ndege zinazotumika. Baadhi ya ndege zinaonekana ni za zamani, zimechakaa. Naiomba Serikali itupie macho na kuhakikisha kwamba ndege hizi zinazotumika zinafikia viwango vinavyokubalika ili kuepusha ajali zinazoweza kutokea kutokana na ubovu na uchakavu wa ndege hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja !

MHE. MWANTUMU B. MAHIZA: Mheshimiwa Spika, awali, naipongeza Wizara kwa kazi nzito. Michango, ni kuomba kupata ufafanuzi na ikibidi kwa maandishi ili nami niweze kusaidia kutoa elimu sahihi kwa wananchi wa Jimbo la Mkinga – Tanga. Naomba kufahamu yafuatayo:-

Ujenzi wa barabara utafuata michoro ipi? Yaani design ile ya kwanza au ya pili? Mchoro wa awali zipo nyumba, ilibidi zibomolewe kupisha ujenzi wa barabara hiyo ya Tanga – Horohoro. Mchoro wa pili umeainisha mpito tofauti na ule wa awali na hivyo kuzigusa nyumba nyingine ambazo hapo awali hazikuonyeshwa kuwa zitahusika. Aidha, wapo wananchi ambao walishahama na kubomoa nyumba zao kufuatia mchoro wa awali, lakini wamefutwa tena katika mchoro wa pili. Kwa hiyo, ni vyema wananchi wakajua nini ni nini. Wananchi wanapenda kufahamu nami nitaisaidia Serikali kufikisha ujumbe huo.

Mheshimiwa Spika, mchoro wa pili ulionyesha kuwa utapita kwa maeneo tofauti na hivyo kugusa maeneo yanayohusu Mahakama, shule na nyumba za walimu kwa

155 baadhi ya maeneo. Naomba kufahamu endapo maeneo hayo yatafidiwa au la, Shule ya Sekondari ya Zinzibar ilijengwa na wananchi, hivyo baada ya kuonyesha hifadhi ya barabara, shule hiyo/madarasa yaliyo mbele hayatastahili kuwepo kitaalamu.

Hivyo, naomba sana kuwaonea huruma wananchi hao kwa kuwafidia. Madarasa yatakayohusika ni manne, hivyo kama ni fidia, naomba taarifa itolewe mapema kuwaandaa kisaikolojia wananchi ili wawe tayari kujenga upya madarasa hayo. Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya wananchi wa Mkinga, nitafarijika mno kupata ufafanuzi wa mambo hayo ikiwa nini hatima ya barabara hiyo ya Tanga – Horohoro. Naunga mkono hoja.

MHE. CASTOR R. LIGALLAMA: Mheshimiwa Spika, barabara kuu ya Kidatu – Ifakara – Mahenge, mwaka 2006/2007 ilitengewa shilingi milioni 400 kama fedha za maendeleo. Lakini, ninachokiona kwenye jedwali ni shilingi bilioni 2.4 zikiwa na mchanganuo ufuatao:- Shilingi bilioni mbili kutoka Serikali ya Uswisi, shilingi milioni 400 kutoka fedha zilizotengwa mwaka 2006/2007. Fedha hizo shilingi bilioni 2.4 ni kwa ajili ya kutengeneza kilomita saba za lami katika Mji wa Ifakara kuanzia eneo la Kibaoni (Ofisi ya Mkuu wa Wilaya) mpaka Mjini eneo la Shule ya Msingi Lipangalala. Kwa hiyo, sehemu kubwa ya barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 75 (Kidatu – Ifakara) itafanyiwa matengenezo ya kawaida ya spot improvement, periodic maintenance na routine maintenance.

Mheshimiwa Spika, Waziri alipokuwa akijibu swali langu namba 393 la tarehe 11/08/2006 kuhusu barabara ya Kidatu – Ifakara – Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo, pamoja na madaraja ya Mto Kilombero na Mto Mwatisi, alisema (hapa nanukuu sehemu ya Hansard); “Barabara hiyo ya Kidatu – Ifakara – Mahenge, ni moja ya barabara zilizo kwenye mpango kabambe wa Transport Sector Investment Programme kwa kuijenga kwa lami kuanzia kipindi cha mwaka wa fedha 2006/2007 hadi 2010/2011. Wengi wa wananchi wa Wilaya hizi mbili, Kilombero na Ulanga walipomsikia Waziri walifurahia jambo hili; na kwa vile mpangio wenyewe ni kabambe, bila shaka fedha za mpango huu zilijulikana zitatoka wapi.”

Mheshimiwa Spika, katika majumuisho ya Mheshimiwa Waziri, naomba awaeleze wananchi wa Wilaya hizo ni lini hasa katika kipindi hiki cha miaka mitano barabara hii itaanza kujengwa?

Mheshimiwa Spika, madaraja katika barabara kuu ya Kidatu – Ifakara, mengi ya madaraja katika barabara hii yalijengwa wakati wa ukoloni. Kutokana na barabara hii kuwa kama mshipa wa damu katika uchumi wa Wilaya hizi mbili; Kilombero na Ulanga, magari yanayopita kwa siku hayapungui 100, yanayotoka na kuingia hasa kipindi hiki cha kuuza mazao, Juni – Machi, 2008. Magari mengi ni mazito kiasi cha kuzidi tonnage ya madaraja yaliyojengwa miaka hiyo. Mheshimiwa Spika, naomba TANROADS iangalie hali ya madaraja katika barabara hii kwa vile mengi ya madaraja hayo sio muda mrefu yatashindwa kuhimili malori ya mizigo yanayopita njia hii ili kuzuia uwezekano wa kutokea maafa.

156 Mheshimiwa Spika, wakati wa ukoloni na miaka ya mwanzo baada ya uhuru kulikuwa na kambi za kuhudumia barabara kila baada ya umbali fulani maarufu kwa jina la Public Works Department Camps (PWD Camps). Kambi hizi ziliwezesha kwa kiwango fulani kufanya barabara ziwe bora kwa mwaka mzima kwani tatizo linapoonekana kuanza, linashughulikiwa mara moja.

Mheshimiwa Spika, ni vizuri turudishe mpango ule hata ikibidi kwa mtindo wa kuanzisha Pilot Project. Napendekezza Pilot Project ya kwanza iwe katika Wilaya yangu kwa sababu miundombinu kwa maana ya nyumba, workshop, stores zinaweza kupatikana na sehemu nyingine vitu hivyo vipo. Napendekeza kambi hizo ziwe katika maeneo yafuatayo:-

§ Barabara Kuu Kidatu – Ifakara, kambi iwe Mang’ula. Hapo ni katikati, nami naahidi majengo ya awali ya kambi yatapatikana.

§ Barabara ya Ifakara – Mlimba, kambi iwe Mneta. Hapo pana majengo ya TANROADS yaliyokamilika. § Barabara ya Mlimba Taweta, kambi iwe Mpanga. Hapo napo, naahidi kupata majengo ya awali kwa kambi hiyo.

Mahitaji ya kambi hizo tatu ni kila kambi kuwa na Tipper dogo la tani 4 – 5, Spades, hoes, two or three wheel barrows, 5 – 6 staff including the driver

Mheshimiwa Spika, kuhusu kutoboa barabara ya Taweta – Madeke – Lupembe: Barabara ya Mpanga hadi Taweta imechongwa mwaka jana, bado kuwekewa mifereji ili idumu kwa muda mrefu. Ili kukuza uchumi wa wananchi wa Kata ya Masagati, inapendekezwa barabara hii iunganike na barabara inayotoka Njombe kuja Lupembe hadi Madeke. Katika jitihada hizi, tutashirikiana na wenzetu wa Njombe ambao ameishafungua barabara kutoka Lupembe hadi Mto Mfuji Juu (Mto Mfuji Chini uko Taweta). Wenzetu wa Njombe wameshajenga daraja kwenye Mto huo ambao ni mpaka.

Mheshimiwa Spika, tunaomba Wizara itupatie fedha ili tuweze kufungua barabara hii ambayo ina urefu wa kiomita 40 hivi na hamna Mto kati ya daraja hilo la Mto Mfuji Juu na Taweta. Kwa kufanya hivyo, tutawafungulia biashara watu wa Taweta na Tanganyika Masagati kwa kuuza mchele, machungwa na samaki Njombe na kununua mbao, viazi mviringo, maharage, njegere na chai kutoka Njombe na Lupembe.

Mheshimiwa Spika, Kivuko cha Mto Kilombero – Panton: Inaonekana Kivuko hiki hakikutengenezwa kwa kuangalia hali ya eneo la Mto Kilombero ama Mkandarasi haku-visit site ile ili aweze kuoanisha na hali halisi ya chombo ambacho kingefuata specifications za Panton. Kuna taarifa kwamba engine ni kubwa kuliko Kivuko na maji yanaingia.

Mheshimiwa Spika, naomba kivuko kirekebishwe ili vitu kama Keel visiwe sharp kufuatana na uegeshaji wa sehemu yenye kina kifupi.

157 Mheshimiwa Spika, maoni yangu ni kwamba, ni vizuri wakati mwingine Wizara ikashirikiana na viongozi wa Wilaya pamoja na Mbunge pindi vyombo kama hivi vinapokuja kuhudumia watu. Mimi kama Mbunge nilisoma kwenye gazeti kwamba kivuko kimefika ingawa nilikuwa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja!

MHE. PROF. PHILEMON M. SARUNGI: Mheshimiwa Spika, naomba nitumie nafasi hii kutoa salaam zangu za rambirambi kwa familia ya Marehemu Amina Chifupa Mpakanjia, aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum CCM aliyefariki tarehe 26 Juni, 2007. Mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya Marehemu mahali pema Peponi. Amen!

Aidha, natoa salaam za rambirambi kwa familia zote za waliopoteza wapendwa wao katika ajali mbalimbali zilizosababishwa na vyombo vya usafiri na usafirishaji katika Mikoa ya Arusha (Monduli), Singida na Mbeya. Mwenyezi Mungu azilaze roho za Marehemu Peponi. Amen! Mheshimiwa Spika, wananchi wa Wilaya ya Rorya wanampongeza Waziri wa Miundombinu, Mheshimiwa Andrew Chenge, Manaibu wake, Mheshimiwa Dr. Maua Daftari na Mheshimiwa Dr. Milton Mahanga kwa kazi nzuri wanayoifanya wakishirikiana na Katibu Mkuu na wataalamu wa Wizara. Barabara za Rorya zinazohudumiwa na TANROADS, zinaendelea kukarabatiwa kwa kiwango cha juu. Wananchi wanashukuru sana.

Mheshimiwa Spika, tunashauri wakandarasi wafuatao waendelee kupata zabuni katika kutengeneza barabara ambazo zimetengewa fedha. Ushauri huu haumaanishi uingiliaji utaratibu wa kutoa zabuni, bali ni kuimarisha, kuboresha na kurahishisha kazi ya ukarabati wa barabara za Wilaya ya Rorya. Wamefanya kazi nzuri na wanaendelea kukamilisha ukarabati wa barabara ya Mika – Ruari Port – Shirati. Mkandarasi aliyepewa kazi ya kukarabati barabara ya Kiruya – Utegi – Bukwe – Gemasera, anashindwa kazi na wananchi walitaka kumshambulia kwa kushindwa kukarabati barabara hii kulingana na thamani ya fedha. Tunaomba wakandarasi wawili wanaokarabati barabara ya Mika – Sota, wapewe ukarabati wa Kiruya – Utegi.

Mheshimiwa Spika, wananchi na mimi kama Mbunge wao, napenda kuungana nao kumpongeza Meneja wa TANROADS Mkoa wa Mara, Ndugu Kadashi na wasaidizi wake kwa jitihada zao katika kusimamia ujenzi na ukarabati wa barabara za Wilaya ya Rorya.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu ni kwamba uamuzi wa Serikali kuachia TANROADS kushughulikia ujenzi na ukarabati wa barabara zote zikiwamo za Wilaya, Mikoa na barabara kuu, uzingatie pia barabara za vijijini. TANROADS iongezewe nyenzo muhimu, magari, vifaa vya survey, Wahandisi wa barabara za Wilaya wawekwe chini ya usimamizi wa Meneja wa TANROADS Mkoa. Ofisi za Wilaya ziimarishwe.

158 Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya wananchi wa Rorya, nampongeza Mheshimiwa Waziri Chenge kwa Wizara yake kutekeleza Ilani ya CCM ya mwaka 2005 kuhusu usafiri majini kwa kusikia kilio cha wananchi wa Tarafa ya Suba, Kata ya Nyamunge kuhusu Kivuko. Huduma za Kivuko hiki zilisimama kwa muda wa miaka 30. Nafurahi kuona kuwa sasa huduma hizi zinarejea tena kama ilivyoelezwa kwenye hotuba ya bajeti ukurasa wa 37, Ibara 45. Naipongeza Wizara kwa kutenga fedha, nadhani shilingi milioni 552 kwa ajili ya kununua kivuko cha Kinesi (Rorya) awamu ya kwanza.

Mheshimiwa Spika, nashauri wataalam watembelee Bandari Ndogo ya Kinesi ili wawatangazie wananchi habari hii njema.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu.

MHE. ABDUL J. MAROMBWA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, ninaunga mkono hoja hii asilimia mia moja. Hotuba ya Mheshimiwa Waziri imelenga hasa kuboresha miundombinu ya nchi hii iwapo tu usimamizi na matumizi mazuri ya fedha zilizopangwa zitatumika kwa makusudio yaliyotakiwa.

Mheshimiwa Spika, mara nyingi Wizara hii inatengewa fedha za kutosha za ujenzi wa barabara, lakini kuna matatizo makubwa ya matumizi ya fedha hizo. Utashangaa kuona barabara inayotengenezwa mwaka huu, ikifika mwakani, barabara hiyo imekufa. Hali hii sio nzuri. Ni vizuri barabara zinazojengwa ziimarishwe sana ili ziweze kutumika kwa muda mrefu (Value for money + regular maintenance).

Mheshimiwa Spika, kuhusu ahadi ya Rais, nalo hili ni kitendawili. Ahadi ya barabara ya Kibiti – Ruaruke – Nyamisati, hadi sasa ujenzi wake haujulikani utaanza lini. Kinachofanyika kwa sasa ni kupewa shilingi bilioni tano kujenga barabara hii yenye urefu wa zaidi ya kilomita 30. Kwa kiwango hiki cha fedha, ahadi hii itamalizika lini? Ninaiomba Serikali itimize ahadi hiyo ya Rais ili kuwapa imani wananchi juu ya Serikali yao.

Mheshimiwa Spika, nizungumzie suala la usafiri eneo la Delta. Eneo hili tangu tupate uhuru bado miundombinu yake mibovu na haijaendelezwa hadi leo hii. Wananchi wa eneo la Delta lenye urefu wa kilomita 65 toka upande wa Kaskazini mwa Delta hadi Kusini, eneo hili lenye wakaazi zaidi ya 40,000 wanasafiri kwa mitumbwi na maisha yao yapo hatarini.

Mheshimiwa Spika, kila mara mitumbwi hiyo hupinduka na kusababisha wananchi aidha kupoteza maisha au kupoteza mali zao. Hali hii ya usafiri inasababisha wananchi wa maeneo haya kukosa huduma za jamii kama vile elimu na matibabu. Watumishi wengi hawataki kwenda kufanya kazi katika maeneo hayo. Kama Serikali itatoa boti moja kwa kila Kata kwa Kata za Salale, Maparoni, Mbuchi na Kiongoroni, zitasaidia sana kusafirisha watumishi kwenda kwenye maeneo hayo.

159 Mheshimiwa Spika, katika hotuba ya Waziri, ukurasa wa 37 amezungumzia suala la usafiri baharini. Ushauri wangu ni kuwa, usafiri huu na sheria zinazolinda usafiri huu zitumike pia katika maeneo haya ambayo yana mchanganyiko wa Mito na Bahari. Eneo hili la Delta nalo linatakiwa liwepo katika ramani ya barabara za majini ili liweze kujulikana. Eneo hili lina utajiri mwingi wa Kamba (Prawns) na ni Ramsar Site ya miti ya Mikoko.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja hii.

MHE. GOSBERT B. BLANDES: Mheshimiwa Spika, naomba nizungumzie barabara ya Kyaka – Karagwe – Kasulo. Hii ni barabara iliyotolewa ahadi na Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni yake Mjini Kayanga – Karagwe. Barabara hii inaunganisha barabara iendayo Rwanda na Uganda. Kwa kuwa barabara hii iliahidiwa kujengwa kwa kipindi cha miaka mitano, yaani 2005 – 2010; na kwa kuwa ujenzi wa barabara huchukua sio chini ya miaka mitatu kuanza hadi kukamilika; na kwa kuwa kipindi cha Awamu ya Nne kilichobaki ni karibu miaka mitatu: Je, Serikali inaanza lini ujenzi wa barabara hiyo?

Mheshimiwa Spika, mtandao ni tatizo. Jimbo langu la Karagwe linahitaji mtandao. Hili ni Jimbo lililoko pembezoni mwa Tanzania na mbali sana na Makao Makuu ya nchi yetu, hivyo mtandao ni muhimu. Kuna baadhi ya maeneo yanayopokea mtandao, lakini ni hafifu sana na ninaomba niyaeleze maeneo hayo kama ifuatavyo:- Kata ya Nyaishozi – 10%, Kata ya Ihembe – 20%, Kata ya Rugu – 20%, Kata ya Nyakasimbi – 10%, Kata ya Nyakakika – 10%, Kata ya Nyabiyonza – 20%, Kata ya Bweranyange – 20%, Kata ya Kibondo – 10%, Kata ya Kiruruma – 20%, Kata ya Igurwa – 15%, Kata ya Kituntu – 20%, Kata ya Ndama – 40%, Kata ya Kihanga – 40%, Kata ya Bugene – 60%, Kata ya Kayanga 80%, Kata ya Ihanda – 40% na Kata ya Nykahanga – 70%.

Mheshimiwa Spika, kusema kweli, asilimia kubwa ya Jimbo letu la Karagwe inahitaji mtandao. Tunaomba Kampuni za Vodacom, Tigo, Celtel, TTCL Mobile na Zantel waje wawekeze Jimboni Karagwe kwani wananchi wanao uwezo wa kuchangia. Mheshimiwa Spika, barabara za Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe ni ndefu sana ukilinganisha na barabara za maeneo mengine. Tunaomba fedha zinazogawiwa zizingatie urefu wa barabara za maeneo husika, mfano Wilayani Karagwe.

Mheshimiwa Spika, kuhusu uwanja wa ndege wa Bukoba, kutokana na hali ya hewa ya Mkoa wa Kagera kuwa na mvua nyingi za misimu miwili, inafikia wakati inakuwa vigumu ndege zetu kutua uwanjani. Tunaomba uwanja ujengwe kwa kiwango cha lami. Aidha, uwanja wa ndege ndogo wa Ihanda Wilayani Karagwe, Serikali ya Awamu ya Tatu iliahidi kuupanua na kuujenga uwanja huu. Je, Serikali inasemaje kuhusu uwanja huu?

Mheshimiwa Spika, mwisho, naunga mkono hoja.

160 MHE. JOHN P. LWANJI: Mheshimiwa Spika, pamoja na kazi nzuri ya Wizara hii, lakini ni ukweli kuwa Wizara hii ni kubwa sana kuliko Wizara yoyote ile. Kazi zake ziko overstreched. Je, lile lengo la Wizara la kuja na muundo ulioidhinishwa kabla ya/au ifikapo mwishoni mwa Februari, 2006 limetimia au bado linafanyiwa kazi? Kama bado, nashauri muundo huu uangaliwe upya. Kama tayari, basi nashauri uwe reviewed ili kutengenisha Wizara hii na kuwa mbili:- Wizara ya Mawasialiano na Uchukuzi na Wizara ya Ujenzi wa Barabara (Kwa makusudi ya kusisitiza umuhimu wa barabara zetu).

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Miundombinu kwa sasa ina Division 5, inawajibika kusimamia taasisi 27 kama ifuatavyo:- Mashirika 10, Vyuo 4, Wakala 5, Mamlaka za Udhibiti 3 na Bodi 5: Je, kuna Wizara yenye kujumuisha majukumu makubwa yenye diversity kama hii? Waziri mmoja na Manaibu wawili hawatoshi, watashindwa hata kupata nafasi ya kufika Majimboni kwao.

Mheshimiwa Spika, tatizo kubwa la Wizara hii inachangia kwa kiasi kikubwa kutosimamia vizuri ujenzi wa barabara za Mkoa. Wizara imeiachia TANROADS, matokeo yake, kazi za ujenzi hazifanywi kwa kuzingatia standards and specifications kama ilivyokuwa ikifanya TRM. Ingawa fedha zinatolewa kila mwaka, lakini fedha hizo zimekuwa zikiishia mikononi mwa Mameneja wa TANROADS na Wakandarasi. Mfano; barabara ya Itigi – Rungwa imekuwa ikitengewa fedha kila mwaka. Mwaka 2006/2007 ilitengewa zaidi ya shilingi milioni 200 lakinui kimsingi, hakuna cha maana kilichofanyika. Mvua kubwa zilizonyesha ziliwasaidia wahalifu kuficha ukweli. Hakuna value for money kwenye barabara zetu. Mkiwa – Itigi Rungwa, Chaya – Itigi – Manyoni, Manyoni – Kashangu – Jeje – Heka – Nkonko. Serikali au Wizara inatoa fedha, barabara hizi zijengwe kwa kiwango cha changarawe, lakini kinachofanyika ni kuzibomoa barabara hizo na kufukia vifusi.

Mheshimiwa Spika, naomba maelezo ya kutosha kuhusu hatima ya barabara hizi kutoka kwa Mheshimiwa Waziri. Je, nitaahidiwa kuwa Naibu wake atakuja kusimamia mwenyewe ujenzi wa barabara hizo, kwa sababu hakuna usimamizi wowote unaofanywa na TANROADS. Hebu ukaguzi ufanywe mkajionee jinsi Makandarasi wanavyoharibu barabara. Hakuna ukaguzi wa kuona kama barabara hizo zinajengwa kwa kuzingatia standards and specifications.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali itoe fedha za barabara kwa Serikali za vijiji ili wajenge wenyewe barabara hizo, wananchi washiriki wenyewe kwa kushirikiana na wenye uwezo maeneo yao wajenge barabara hizo na kuwapatia ajira wakiwemo wanawake. Naomba majibu ya faraja. Naunga mkono hoja.

MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE: Mheshimiwa Spika, kwanza, nashukuru sana kwa mgawo wa fedha katika Halmashauri yangu ya Wilaya ya Mpwapwa ambapo kwa bajeti hii tutapata takribani shilingi milioni 700 toka shilingi milioni 150 mwaka 2006/2007.

161 Mheshimiwa Spika, jambo la pili ni ombi langu la muda mrefu la barabara ya kutoka Mbande Ng’ambi – Mpwapwa – Gulwe – Kibakwe – Chogola – Kinusi – Malolo – Luaha Mbuyuni yenye urefu wa kilomita 224 tu. Ombi langu ni barabara hii kupandishwa hadhi na kuwa barabara ya Mkoa toka Mbande – Gulwe tu. Huko mbele ni ya Wilaya. Kimsingi, kipande ninachozungumzia ni cha Gulwe hadi Luaha Mbuyuni kupitia Kinusi na Malolo (Kilomita 170). Umuhimu wa barabara hii ni mkubwa sana. Barabara hii ambayo kila mwaka hujifunga ina faida zifuatazo:-

§ Itaunganisha Mikoa Mitatu: Dodoma, Iringa na Morogoro.

§ Itaunganisha moja kwa moja Wilaya tatu; Mpwapwa, Kilolo na Kilosa. § Itakuza na kufungua soko kubwa la mazao ya vitunguu, maharage, mahindi, mboga mboga na kadhalika ambayo yanalimwa kwa wingi sana.

Mheshimiwa Spika, kwa kweli barabara hii ni muhimu sana. Naomba iwe ya Mkoa, maana inazo sifa zote zilizotajwa kwenye The Roads Act, 2007, section 12. Kwa kuwa inaunganisha Trunk Road (Mbande) na Trunk Road (Luaha Mbuyuni).

Mheshimiwa Spika, kuhusu Great North Road: Dodoma – Babati, Dodoma – Iringa hebu ifike mahali tupewe ratiba kamili ya matangenezo ya barabara hii; tuelezwe mipango iliyopo kwa uwazi zaidi katika ujenzi wa barabara hii; ifike mahali tufikirie kutengeneza barabara hizi kwa fedha zetu wenyewe hatua kwa hatua na kama upembuzi yakinifu na design tayari, kwa nini tusianze kidogo kidogo? Serikali ikumbuke kuwa mwaka 2006/2007 ilisema upembuzi yakinifu, mwaka 2007/2008 tunarudia lugha ile ile, hebu tusogee kwa mfano, Dodoma – Babati, kama huo upembuzi na usanifu wa kina utakamilika, basi mwaka ujao muanze kidogo kidogo!

Mheshimiwa Spika, naomba maelezo, maana hata huo upembuzi yakinifu na design ukikaa muda mrefu kunakuwa na mabadiliko ya design. Je, design itabadilika mara ngapi? Naunga mkono hoja!

MHE. AGGREY D. J. MWANRI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya wananchi wote wa Jimbo la Siha, naomba kuchukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Andrew Chenge - Waziri wa Miundombinu kwa hotuba nzuri ambayo ameitoa asubuhi hii. Ni ukweli usiopingika kwamba hotuba ya Waziri imeainisha malengo na mipango ya hali ya juu ambayo inaonyesha kwamba kama itatekelezwa, itasaidia sana katika kuinua hali ya uchumi wa nchi yetu. Nathibitisha kuunga mkono hotuba hii.

Mheshimiwa Spika, ombi langu ni kuhusu kukumbushia uharakishwaji wa ile barabara ya Bomang’ombe – Sanya Juu, Ngarenairobi – Kamwanga. Barabara hii ina sura ya mbalamwezi inayochomoza. Kwa mara ya kwanza na kama ambavyo nimekuwa nikieleza katika vikao mbalimbali vya Bunge hili, natambua kwamba barabara hii ipo katika projections za Wizara, lakini ombi langu ni kwamba tujaribu kadri iwezekanavyo kuharakisha ujenzi wake. Mara kwa mara Serikali imesisitiza kwamba barabara hii inafanyiwa upembuzi yakinifu na kwamba masuala ya design yanaendelea. Tatizo ni kwamba ukiangalia kazi halisi hata katika maeneo hayo niliyotaja haionekani na miaka

162 inazidi kusonga mbele. Nitafurahi kama nitaelezwa mkakati uliopo wa kuhakikisha kazi hii inaharakishwa kuliko speed hii ndogo ambayo tunaendelea nayo.

Mheshimiwa Spika, umuhimu wa barabara hii kwa uchumi wa nchi hii, siwezi kuurudia. Mlima Kilimanjaro ambao ni kivutio kikubwa kwa watalii wote duniani, upo katika barabara hii. Fedha zinazopatikana kutokana na Mlima huu ni mara mbili ya mapato yote yanayopatikana kutoka Mbunga zote za Wanyama nchini Tanzania. Hapa sijazungumzia mbao, kahawa, ndizi, njegere, ngano, viazi, shayiri, mboga mboga, ng’ombe, mbuzi, kondoo na kadhalika ambayo ni mazao muhimu yanayopatikana katika maeneo yanayopitiwa na barabara hii. Aidha, Mashirika makubwa ya Serikali kama NAFCO, TBL, NARCO, yapo katika maeneo ya West Kilimanjaro ambayo yanapitiwa na barabara hii.

Mheshimiwa Spika, ni maoni ya wananchi wa Siha kwamba tukiharakisha ujenzi wa barabara hii tunaweza sana kusaidia barabara mbalimbali ambazo zinalalamikiwa katika Mikoa ya Kusini, Magharibi, Mikoa ya Singida, Dodoma na kadhalika. Tunaamini kwamba ni mgongano kutoishughulikia barabara hii kwa haraka kwani umuhimu wake hauwezi kusisitizwa kuliko ambavyo tumekuwa tukifanya mara kwa mara.

Mheshimiwa Spika, Mlima Kilimanjaro ungekuwa South Africa, asilimia 50 ya mapato ya Serikali yangetokana na Mlima huo. Narudia tena kupongeza kazi nzuri inayofanywa na Wizara na naunga mkono hotuba hii.

MHE. BALOZI ABDI H. MSHANGAMA: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu, Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na wataalamu wa Wizara kwa hotuba nzuri na kazi nzuri. Naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia maeneo yafutayo:-

Mheshimiwa Spika, uwakilishi wa TANROADS Wilayani, nashauri TANROADS wawe na Mwakilizi Mkazi (Resident Engineer) katika Wilaya zenye mtandao mkubwa wa barabara za TANROADS na au mazingira magumu ya barabara kama ilivyo Wilaya ya Lushoto au kumteua Mhandisi wa Wilaya awe Wakala wa TANROADS kwa matengenezo ya dharura.

Mheshimiwa Spika, barabara pekee ya TANROADS ya Mombo – Soni – Dochi – Lushoto ni nyembamba sana na inapita katika maeneo ya miteremko mikali na miamba kiasi kwamba ikitokea ajali, landslide na kadhalika, barabara ikijifunga, hakuna mchepuko wala barabara mbadala kati ya Mombo na Lushoto.

Mheshimiwa Spika, nashauri Wizara ikubali TANROADS Tanga wamiliki na kutengeneza barabara mbadala ya Mombo – Dochi – Lushoto (8km)

Mheshimiwa Spika, barabara ya TANROADS Lushoto – Mlalo – Makanya hujifunga kila msimu wa mvua na kuwa kero kubwa kwa wananchi. Nafaka, mboga na

163 matunda huoza, umaskini hukithiri na matumaini ya maisha bora huwa mashakani. Naomba tamko la Wizara kuhusu barabara hii. Asante! Naunga mkono hoja!

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Spika, nami naomba nichangie hotuba hii ya Wizara ya Miundombinu mawili matatu kama ifuatavyo:-

Kwanza kuhusu barabara ya Isuna – Manyoni, nashukuru kuwa zabuni kwa aili ya ujenzi wa barabara hii zimesharejeshwa na mkataba wa ujenzi wa kipande hiki utasainiwa Agosti, 2007 na ujenzi mnadai kuwa unatarajiwa kukamilika kabla ya mwaka 2010, sawa. Swali langu ni kwamba:-

(a) Kwa nini haukutajwa muda maalumu wa kukamilika ujenzi huu? Mimi napata taabu sana. Kama ukubwa wa eneo lililobaki unajulikana na wajenzi ni wataalamu wa mahesabu, kwa nini wasiseme ni lini? Hivi mwaka 2010 mbona mbali sana jamani?

(b) Je, wasipokamilisha kabla ya kipindi hicho, mnatuambia nini?

(c) Je, fedha zilizotengwa zitatosha au zinatakiwa nyingine? Tafadhali naomba majibu.

d) Naomba kufahamishwa kuwa, mjenzi mtakayemkabidhi kazi hii ataanza lini? Tafadhali chagueni atakayeanza immediate, sio mnampa mtu atakayechukua miezi mingi kuanza. Ukweli ni kwamba wananchi wa Mkoa wa Singida tumechoka na shida/adha ya usafiri wa barabara, wafanyabiashara wa mabasi wanaogopa kuleta mabasi mazuri Singida kwa ajili ya ubovu wa barabara.

Mheshimiwa Spika, naomba barabara za vijijini Mkoani Singida ziendelee kutengenezwa na ziwe imara ili wananchi waweze kufikia huduma zote muhimu katika kukuza uchumi. Ninaomba barabara za Kinyangiri kupitia ndurumo, Ishinsi hadi msingi (Iramba – Singida) itengenezwe ili watu wale watoke kisiwani, kwani wamezungukwa na mito, wakati wa masika hupata taabu sana hasa wajawazito au wagonjwa wanaohitaji kupelekwa Hospitali za Wilaya au Tarafa. Tafadhali Waziri okoa jahazi hilo.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Singida kwenda Isangu, bado inasuasua, mvua ikinyesha ni balaa. Barabara ya Ndago – Urughu pia ipewe kipaumbele.

Mheshimiwa Spika, naomba Uwanja wa Ndege wa Singida angalau mkoa huu ufarijike na hilo kwa ajili ya wawekezaji ambao naamini utaukwamua mkoa huu kutoka kuwa wa mwisho kiuchumi. Tafadhali, maana hata hiyo barabara inanipa mashaka.

Mheshimiwa Spika, niliwahi kuleta maswali hapa Bungeni kwa kuiomba Wizara kujenga Kiwanja cha Kimataifa kinachofanana na Makao Makuu ya nchi, naomba utekelezaji huo uanze na mara kitakapokamilika kuwa centre ya ndege zote kubwa ili kuufanya uwe hai ni kuwa na hadhi.

164 Mheshimiwa Spika, ili kuonyeshwa uthamani wa Kiwanja cha Dodoma (International Airport) nashauri ndege zetu za Serikali zitue Dodoma na hasa Shirika letu la Ndege (ATC) mara uwanja utakapokamilika na ikiwezekana na safari za nje zianzie Dodoma.

Mheshimiwa Spika, kuhusu usafiri wa majini, pamoja na mikakati mizuri juu ya usalama majini, lakini sijaona fungu lililotengwa la kununua vifaa vya kuokolea pindi ajali inapotokea na kama zipo ni vifaa gani na vingapi na vitatumika wapi? Naomba jibu tafadhali. Mheshimiwa Spika, kuhusu ajali za barabarani ambayo ni mabasi ya abiria, nashauri iwekwe sheria ya mwenye basi kuwalipa fidia wahanga wote kwa kiwango maalumu kitakachowekwa.

Mheshimiwa Spika, naomba mabasi yote ya abiria yawe na fire extinguishing ili moto unapotokea iweze kusaidia kuepusha janga kubwa na watu wapewe semina ya kutumia hiyo fire extinguisher.

Mheshimiwa Spika, kila basi la abiria liwe na mlango wa pili wa kutokea hasa nyuma au upande wa pili.

Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa, natoa pongezi kwa Wizara nzima ya Miundombinu kwa juhudi zote ambazo inajitahidi kufikia maeneo yote ya nchi hii na kutatua matatizo yaliyopo ya miundombinu. Ukweli, hali ni ngumu japo pesa pia walizonazo ni ndogo lakini hongereni sana.

Mheshimiwa Spika, mimi naomba tu kwa Mungu ninayemwamini awape nguvu, afya na hekima katika kuifanya kazi hii ngumu kwa usawa na upendo bila kupendelea mahali popote na Shirika letu la Ndege naliombea kheri na ninaamini Mungu atawatumia viongozi hawa wapya kulikuza na kulitangaza shirika hili na hatimaye nchi yetu ikaonekana kwenye anga za wenzetu waliotutangulia kwa maendeleo. Mungu awabariki wote na mbarikiwe kwa kutokuisahau Singida.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja, ahsante.

MHE. KIDAWA HAMID SALEHE: Mheshimiwa Spika, ninaungana na wenzangu kutoa rambirambi kwa familia na jamaa wote wa Mheshimiwa Amina Chifupa Mpakanjia, Mbunge mwenzetu ambaye amefariki dunia ikiwa bado Taifa linamuhitaji. Mungu amlaze mahali pema Peponi. Amina!

Mheshimiwa Spika, naomba kuanza kuchangia juu ya Miundombinu ya Barabara. Barabara ni maendeleo ya kiuchumi na ni maendeleo ya kijamii. Mikoa yote ambayo imefunguliwa kwa kufikishiwa barabara imepiga hatua ya kimaendeleo na watu wake wanajikwamua kutoka katika dimbwi la umaskini haraka haraka ukilinganisha na mikoa

165 ambayo hadi leo haijajengwa barabara ya uhakika. Matatizo mengi ya kijamii yanaikumba zaidi mikoa au Wilaya ambazo zimefungwa.

Mheshimiwa Spika, naomba nichukue mfano wa Wilaya ya Tunduru, kwa kuwa mimi mwenyewe nilifika huko wakati wa kampeni ya uchaguzi mdogo wa Jimbo hilo mnamo mwezi wa Machi, 2007. Wilaya ya Tunduru imekuwa kama Kisiwa ndani ya Tanzania, Wilaya inafikika kwa shida sana, hakuna barabara, siyo barabara kuu wala za vijijini zile za halmashauri.

Mheshimiwa Spika, maisha ya watu yamekuwa duni mno, fikra za watu na mawazo yao yamefungika pia kutokana na kutochanganyika na watu wa kutoka maeneo mengine kwa sababu wao hawawezi kusafiri kwenda maeneo mengine ya Tanzania kiurahisi na watu wa maeneo mengine hawawezi kufika Tunduru kiurahisi na matokeo yake kiwango cha elimu kiko chini mno. Aidha, mimba za utotoni na za wanafunzi ni nyingi mno, pia wanafunzi wanapatiwa waume wakiwa bado wanaendelea na masomo na hili limekuwa kama jambo la kawaida na wala sio jambo la aibu.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Tunduru inayo ardhi nzuri sana yenye rutuba na maji mengi sana, iko mito ambayo haikauki milele, lakini watu wanashindwa kulima kwa wingi kwani hata wakilima hawana soko la mazao yao. Mazao yanaharibika mashambani, ununuzi wa korosho ambalo ni zao la biashara pia umekuwa mgumu kwa tatizo hilo.

Mheshimiwa Spika, niliwaahidi watu wa Tunduru kuwa nitasimama bega kwa bega na Mbunge wao kutetea Tunduru ipatiwe barabara, hivyo Barabara ya Masasi – Tunduru ijengwe kwa kiwango cha lami katika kipindi hiki cha bajeti 2007/2008. Nimefurahi kuona kuwa imo katika mpango, lakini ni wajibu wangu kusisitiza.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Shirika la Posta, shirika hili bado ni muhimu sana kwa wananchi walio wengi, lakini liko katika hali mbaya, teknolojia inayotumika ni duni haiendani na karne hii ya sayansi na teknolojia na ushindani wa kibiashara.

Aidha, madeni makubwa ni mzigo kwa shirika, Serikali ibebe hili deni na kulipatia shirika mtaji wa kuwezesha kununua vitendea kazi na kukarabati majengo kwani majengo mengine yanatia aibu. Aidha, shirika nalo baada ya kufutiwa madeni litaweza kukopesheka na kupata fedha za kuendeshea biashara na kuweza kufanya kazi vizuri katika ulimwengu huu wa ushindani.

Mheshimiwa Spika, lingine ni kuhusu uwanja wa ndege wa Dodoma. Uwanja huo upanuliwe na kuwezesha ndege mbalimbali kutua. Hivi sasa watu wengi wanapenda kutembelea Dodoma lakini wanashindwa, hakuna hata ndege zinazofika kikawaida Dodoma na hata wageni wa Kimataifa wakati mwingine inabidi wasafiri kwa magari wakitaka kuja Dodoma kutokana na tatizo hilo. Mji wa Dodoma upewe hadhi yake kwa kuwa na miundombinu ya kisasa ikiwemo kiwanja cha ndege kikubwa na kizuri.

166 Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, ninaunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.

MHE. MBARUK K. MWANDORO: Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza kwa dhati Mheshimiwa Andrew Chenge - Waziri wa Miundombinu pamoja na Waheshimiwa Naibu Mawaziri wa Wizara hii, Katibu Mkuu na wataalamu wote wa Wizara na Taasisi zilizo chini ya Wizara hii kwa hotuba nzuri, utendaji mzuri na mwelekeo mzuri katika kuimarisha na kuboresha mindombinu hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, kupandishwa kwa bei ya mafuta na kutunishwa kwa mfuko wa barabara bila shaka utaleta nguvu mpya na kasi mpya katika utengenezaji wa miundombinu pamoja na ya vijijini. Ningependa kusihi kwamba Halmashauri za Wilaya zipewe fedha za utosha kwa ajili ya barabara za vijijini ambazo ni muhimu sana kwa maendeleo nchini.

Mheshimiwa Spika, nafarijika kwamba Mkoa wa Tanga ni miongoni mwa Mikoa mitatu itakayofarijika kwa awamu ya kwanza kwa program maalum ya Benki ya Dunia. Naamini kwamba Wilaya ya Mkinga itapata kipaumbele maalum kutokana na hali duni sana ya barabara katika Wilaya hiyo changa ya pembezoni.

Mheshimiwa Spika, barabara ya kuunganisha Kasera Makao Makuu ya Wilaya ya Mkinga na Kata tano zilizo Tarafa ya Maramba ni muhimu sana kiuchumi, kiutawala, kiusalama na kijamii. Hivyo zaidi ya kupatiwa fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu na usanifu katika mwaka wa fedha 2007/2008, nashauri zoezi hili lifanyike haraka iwezekanavyo ili kwamba jitihada za kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo zianze mapema katika mwaka wa fedha 2007/2008 ili hatimaye ujenzi wa barabara hiyo ufanyike mapema na kuondoa kero hiyo kubwa kama Mheshimiwa Waziri Mkuu alivyowaahidi wananchi wa Maramba mbele ya Mheshimiwa Dr. Makongoro Mahanga, Naibu Waziri walipokuwa ziarani Mkinga mwaka jana. Naomba Serikali iipe barabara hii kipaumbele maalumu.

Mheshimiwa Spika, kilio kikubwa zaidi cha wananchi wa Wilaya ya Mkinga ni barabara ya Tanga – Morogoro. Ni zaidi ya miaka sita sasa barabara hii imewekwa katika kipaumbele na ahadi za ujenzi wa barabara hiyo kujengwa kwa kiwango cha lami kutolewa mara nyingi sana Bungeni na pia Mheshimiwa Rais Jakaya M. Kikwete kutoa ahadi hiyo kama sehemu ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005 wakati wa kampeni na pia alipokuwa akitoa shukurani Tanga. Nyumba ziliwekewa alama ya NR zaidi ya miaka mitano iliyopita, lakini bado hakuna dalili ya ujenzi kwa kuanza hata baada ya usanifu kukamilika zaidi ya miaka miwili sasa. Hotuba ya Wizara na viambata vyake haikutaja lolote kuhusu barabara hii kuu pekee inayounganisha nchi mbili bila lami. Kulikoni?

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Mkinga kama sehemu ya Tanga (Northern) Development Corridor wamefadhaishwa sana kwa kutokuwepo tamko lolote kuhusu ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya corridor hiyo ikiwemo Bandari ya Tanga, Reli

167 ya Tanga – Musoma, Bandari Ndogo za Moa na Kwale. Aidha, hapana dalili za kuanza kujengwa kwa miundombinu ya EPZ ya Tanga. Kweli tutafika!

Mheshimiwa Spika, natoa shukurani kwa maendeleo yaliyopatikana kuhusu mawasiliano ya simu. Hata hivyo, bado kuna maeneo Wilayani Mkinga ambapo mawasiliano bado ni kero kubwa.

Maeneo haya ni pamoja Kata ya Mwakijembe, Kata ya Mtimbwani, Kata ya Kwale na baadhi ya sehemu za Kata za Manza na Moa. Naiomba Wizara iendelee kushawishi kampuni za simu ziendeleze jitihada ya kumaliza kero hii.

Mheshimiwa Spika, Wilaya mpya ya Mkinga haina huduma za Posta hata kidogo. Tunaiomba Wizara iunge mkono jitihada za uongozi wa Wilaya na Mkoa kulielekeza Shirika la Posta kupeleka huduma zake huko. Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja na kuitakia Wizara na wadau mafanikio mema.

MHE. BUJIKU P. SAKILA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja hii. Aidha, nampongeza Mheshimiwa Waziri, Manaibu Waziri wote na wataalamu katika Wizara hii hasa walioshiriki katika uandaaji kwanza.

Mheshimiwa Spika, naomba kwanza nitoe pongezi na shukurani kwa kuendelea kuihudumia barabara ya Mwanhaya kwenda Ilongoitale na kuifanya ipitike japo kwa shida nyakati za mvua.

Mheshimiwa Spika, ombi ni kwamba, ni muda mrefu sana tangu ijengewe tuta mpya. Kwa mwaka ujao naomba ijengewe tuta jipya na kukarabatiwa kwa kiwango cha lami nyepesi au changarawe kama lami haitawezekana. Aidha, daraja kwa Mto Mwame lijengwe upya angalau kingo zake zote ziwekwe upya. Hali inatisha wakati wa mvua.

Mheshimiwa Spika, kwa kuthibitisha kuwa mradi wa PMMR utaanza mwaka huu wa fedha, maombi yangu ni kuwa orodha ya barabara husika iwekwe wazi ilizijulikane. Pia naomba sana Mheshimiwa Waziri wakati wa majumuisho aeleze iwapo barabara ya Magu, Ngudu hadi Jojiro iliyokuwa katika orodha ya PMMR, sasa haionyeshi. Naomba sana aeleze kama haikuonyeshwa kwa makosa au ndiyo mpango. Kama kipande hicho (Ambayo ni sehemu ya ahadi ya Mheshimiwa Rais ijulikane kwa nini imeondolewa na itakarabatiwa kwa utaratibu upi wa kuweza kuimarishwa kwa kiwango cha kulingana na ahadi ya Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Spika, naomba pia Mheshimiwa Waziri wakati wa majumuisho aeleze mradi huo utaanza baada ya muda gani mara baada ya mikataba kuwekewa sahihi.

Mheshimiwa Spika, naomba hadhi ya Shirika la Ndege Tanzania irejeshwe. Napongeza kwa kuwa itaongeza hadhi ya nchi. Ombi ni kwamba, yaliyopita ni ndwele tugange yajayo tuache malumbano, kasi ya kuboresha izingatiwe na nina imani na uongozi ulioteuliwa.

168 Mtandao wa simu Kwimba, napongeza sana juhudi za Makampuni ya Simu TTCL, Vodacom na Celtel yaliyofungwa mitandao katika Wilaya yetu. Nashukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri Dr. Maua Daftari niliyekuwa nikimsumbua mara kwa mara kuhusiana na naombi ya mitambo hii ya mawasiliano. Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Kwimba na Wilaya ya Kwimba kwa jumla tunamshukuru yeye na Wizara nzima kwa mafanikio hayo. Ombi langu la muda mrefu sasa ni mtandao mmojawapo kupelekwa katika sehemu ya Kusini mwa Wilaya ya Kwimba na Jimbo la Kwimba. Mitambo yote niliyoitaja hapo juu yote iko upande wa Kaskazini. Bado ninaomba sehemu ya Kusini hususani Tarafa ya Mwanashimba, naomba sana.

Kuhusu Mwanza Airport, napongeza sana kwa uamuzi wa kupanua Airport hiyo. Mji wa Mwanza unakua kwa upana na matumizi. Tuangalie mahitaji ya jiji hili miaka 50,100 ijayo. Idadi ya watu Mwanza inakua haraka na kuna mfumko wa miji midogo midogo kando kando mwa jiji hili ikiwemo Sengerema, Misungwi, Ngudu na Magu.

Ombi ni kwamba Serikali iangalie uwezekano wa kubadilisha matumizi ya shamba la Ng’ombe Mabuki ambalo halijawa na matokeo mazuri zaidi ya miaka 20 kwa kuwepo kwake kuwa Kiwanja cha Kimataifa. Uzuri wa eneo hili ni kuwa liko mbali na milima, kuna eneo kubwa lisilohitaji fidia, ni katikati mwa Mji wa Mwanza na Shinyanga na ni rahisi kufikia Mbuga za Wanyama za Serengeti kwa kupitia Ngudu na Magu. Ni eneo ambalo ni rahisi kupanuliwa. Ninaamini Serikali ikiamua, hili linawezekana na lina mantinki. Baada ya hayo, ni matarajio yangu kuwa wakati wa majumuisho au hata baadaye nitaweza kupatiwa majibu.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha na ninaunga mkono hoja.

MHE. JUMA SAID OMAR: Mheshimiwa Spika, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uzima na afya na kuwepo katika kikao cha leo.

Mheshimiwa Spika, napenda kukupongeza wewe, Naibu Spika pamoja na wenyeviti wa Bunge kwa kuliongoza Bunge letu vizuri. Pia nawapongeza vizuri.

Mheshimiwa Spika, uchumi wa nchi yoyote duniani unategemea kwa kiasi kikubwa uhakika na uimara wa miundombinu yake.

Mheshimiwa Spika, uchumi wetu unaweza kukua kutokana na usafirishaji wa bidhaa mbalimbali pamoja na mazao ya wakulima kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine. Usafirishaji huu unaweza kufanyika kupitia nchi kavu (barabara) kwa kutumia mabasi, treni, magari madogo na kadhalika; baharini na kwenye maziwa kwa kutumia meli, boti na kadhalika; na anga kwa kutumia ndege, helikopta na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, barabara ni kichocheo cha uchumi. Kuna msongamano mkubwa wa magari katika Jiji la Dar es Salaam ambao kwa kiasi fulani unaathiri sana utendaji kazi na hivyo kuathiri uchumi na maendeleo kwa jumla.

169 Mheshimiwa Spika, usafiri wa majini una matatizo mengi katika maziwa na bahari kuu. Wasafiri katika maziwa na bahari hupoteza maisha ya watu mara kwa mara pamoja na vyombo vyao vya usafiri kama vile maboti na mitumbwi kuzama bila ya kupata msaada wowote.

Mheshimiwa Spika, kuna msaada gani au fidia inayotolewa na SUMATRA endapo mfanyabiashara fulani chombo chake kimezama na ameripoti kwa uongozi wa SUMATRA lakini muda mrefu umepita bila ya mafanikio yoyote?

Mheshimiwa Spika, ni zaidi ya miaka 45 sasa tangu nchi yetu ipate uhuru lakini miundombinu bado haijakidhi mahitaji yaliyopo. Kwa hiyo, wakati umefika sasa kwa Serikali kulitizama suala la miundombinu kwa umuhimu na uzito wake, ahsante.

MHE. AZIZA S. ALLY: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. Napenda kuchangia kama ifuatavyo: Ninaipongeza Serikali kwa kuzingatia matatizo ya usafiri wa reli na hatimaye kutafuta mwekezaji/kukodisha Shirika hilo na Serikali kuweka asilimia 49 na 51 kuwekwa na wakodishaji, hiyo inatia moyo sana kwa wananchi.

Pamoja na hayo, napenda kukiri kuwaona hao wanaochukua shirika hilo kufika Tabora juzi, tuna hata Mkurugenzi mtarajiwa kuwepo station hadi saa 4.45 wakati treni inapoondoka Tabora. Kama hali ndio hiyo, nina imani shirika linaweza kuinuka kuliko hivi sasa.

Mheshimiwa Spika, ya kuzingatia ni kwamba, biashara inazingatia faida ambayo ni mizigo na abiria, kwani mizigo ina faida kubwa sana. Sasa isiwe ndiyo itaangaliwa zaidi kuliko usafiri wa abiria ambapo wananchi waende hasa daraja la tatu (III) kubanana bila kufuata namba, haitakuwa maana ya kuona usafiri huo kuwa mbaya, hatukubali kama inavyofanyika sasa hivi.

Mheshimiwa Spika, mabehewa ya abiria yaangaliwe kabla hayajafungwa kuliko kufika njiani na mabehewa hayo kuharibikia njiani, hakuna kituo karibu na kusubiri kituo cha mbali kutafuta behewa kwani kinga ni bora kuliko tiba.

Mheshimiwa Spika, lingine ni kuhusu barabara, nilipochangia Wizara ya TAMISEMI, niliomba Barabara ya Itigi – Tabora – Kigoma. Najua Serikali ina mikakati kabambe kabisa, sasa naomba tena mikakati hiyo wakaambiwe wananchi ambapo wananchi hao wataelewa MKUKUTA, MKURABITA mipango kabambe ya Serikali na wananchi kuwasikia wenyewe kuliko wawakilishi kusema na kwenye bajeti hakuna.

Nadhani Waziri atafahamisha kuhusu ziara hiyo kama itakuwepo au haitowezekana na wananchi wa Tabora wanafahamu hilo.

Mheshimiwa Spika, nampongeza Waziri na Manaibu wote wawili kwa kazi nzuri waliyoifanya, pia pamoja na watendaji wote wa Wizara.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

170 MHE. MOHAMMED RAJAB SOUD: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, napenda kukupongeza wewe binafsi kwa umahiri na uongozi wako thabiti wa kuliongoza Bunge letu hili Tukufu kwa umakini kabisa.

Mheshimiwa Spika, napenda pia kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Manaibu Waziri wake wote wawili, Katibu Mkuu na Watendaji wote kwa kuwasilisha bajeti yao ya matumizi ya Wizara yao kwa umakini kabisa kiasi ambacho kinaleta matumaini ya kuendana sambamba na kasi, nguvu na ari mpya.

Mheshimiwa Spika, napenda kuupongeza uongozi wa Serikali kwa kupitia Wizara hii kuamua kununua Engine mbili za Ferry ya Kigamboni.

Mheshimiwa Spika, ununuzi wa Engine hizi mbili wa kivuko cha Elina ni ukombozi wa wananchi wanaokaa Kigamboni na maeneo mengine ya jirani na kuyaweka maisha ya wananchi hao katika usalama. Mheshimiwa Spika, iko haja ya kutoa kipaumbele kwenye barabara zote zilizopo jirani na nchi zote zilizotuzunguka kwani kuunganisha nchi yetu na nchi za jirani ni ukombozi wa wakazi wa maeneo ya mipakani kwa kupata mawasiliano ya biashara na matembezi kwa urahisi kabisa.

Mheshimiwa Spika, usafiri wa nchi kavu ni mzuri, lakini umekuwa na kasoro kubwa kiasi ambacho tamaa ya kusafiri na ukafika salama hasa kwa magari ya abiria ni kitendawili kwani unapoingia kwenye gari la abiria wewe unajiona tayari ni maiti kwa kusafiri na magari yasiyo na uangalifu, madereva wasiojali wajibu wao na barabara nyingine zisizokuwa na kiwango.

Mheshimiwa Spika, napenda kuipongeza Serikali kwa kulifufua Shirika la UDA kwa kuingia katika ushindani wa kibiashara kwa kutoa huduma ambazo kwa kiasi kikubwa zimeondoa usumbufu hasa kwa wanafunzi ambao ni vijana wetu tunaowategemea kwa Taifa la kesho.

Mheshimiwa Spika, baada ya haya machache napenda kutamka kuwa naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.

MHE. CAPT. JOHN Z. CHILIGATI: Mheshimiwa Spika, kwanza naipongeza Wizara hii kwa hotuba nzuri yenye kuleta matumaini ya sasa na ya baadaye. Pamoja na pongezi hizi, ninazo hoja chache zifuatazo:-

Mheshimiwa Spika, tunaupongeza mpango wa kupanua Uwanja wa Ndege wa J.K. Nyerere. Katika upanuzi huo, suala la ujenzi wa chumba cha wageni maarufu VIP lounge, chumba cha hivi sasa kwa kweli ni kidogo mno na mara nyingi wageni mahiri wengi wanapokuja tunaaibika kwani mgeni inabidi kusimama. Hii sio picha nzuri kwa nchi yetu. Dosari hii irekebishwe na hasa tunapotoka kiwanja hiki hub ya msafiri katika eneo hili la Afrika Mashariki.

171 Mheshimiwa Spika, mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni, ni moja ya ahadi muhimu sana katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM. Ni mradi unaovuta hisia za wananchi wengi kwa kuwa daraja hilo lina umuhimu mkubwa kwa wakazi wa Dar es Salaam na hasa wa Kigamboni. Wizara imesema bado inazungumza na wadau wa sekta binafsi ili kupata fedha za ujenzi. Kweli hii inaleta matumaini. Hata hivyo tunaishauri Serikali kwamba mdau yeyote atakayepewa mradi huu akiwa wa nje, iwe ni lazima aingie ubia na mbia wa ndani. Hapa ndani mbia aliyejiandaa kwa ukamilifu na NSSF. Shirika hili tayari lina viwanja 800 kule Kigamboni za ujenzi wa nyumba, jambo hili ambalo mdau wa ujenzi wa daraja hili atapenda kuwa na ardhi ya kuendelezwa kule Kigamboni ili iunganishwe na daraja. Aidha, NSSF imefanya upembuzi yakinifu, nimeandaa michoro ya daraja, sasa baada ya maandalizi hayo yote yaliyogharimu fedha nyingi tena kwa kutumwa na Serikali, ikiwekwa nje kabisa ya mradi huu itakuwa Serikali haiwatendei haki NSSF.

Matengenezo ya barabara ya Manyoni – Senza – Ikasi, barabara hii ni ya TANROADS na ina urefu wa kilometa120 na ipo katika hali mbaya sana hasa baada ya mvua za mwaka huu. Katika bajeti hii imetengewe fedha za spot improvement ya kilometa sita kwa shilingi milioni 104. Barabara hii ndiyo njia pekee inayotegemewa na Tarafa yote ya Nkonko yenye kilometa tano. Tarafa hii imetengwa kimaendeleo kwa kuhusu usafiri. Tunaomba Wizara ione uwezekano wa kuiwezesha TANROADS kuitengeneza barabara hii.

Mawasiliano ya Simu za Mkononi Tarafa ya Nkonko (Manyoni), Tarafa hii mbali ya kuhusu barabara, pia haina mawasiliano ya simu za mkononi. Wapo wananchi wengi katika tarafa hii wamenunua simu za mkononi lakini hadi waende Manyoni ndipo wapige. Tunaomba Wizara izihamasishe kampuni za simu za mikononi kupeleka huduma katika eneo hilo na soko lipo. Nipo tayari kuwatembeza katika eneo hilo ili wajionee wenyewe kwamba soko lipo.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

MHE. MKIWA A. KIMWANGA: Mheshimiwa Spika, napenda kutoa mchango wangu katika Wizara hii. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Andrew Chenge – Waziri wa Miundombinu pamoja na Naibu Mawaziri wake wote wawili Mheshimiwa Maua Daftari na Mheshimiwa Makongoro Mahanga kwa kazi zao nzuri bila ya kulala.

Mheshimiwa Spika, pili, napenda kuchangia katika upande wa SUMATRA. Inakuwaje meli kubwa kama MV Victoria inafikia mpaka kuzima engine zote mbili na ilihali ikiwa imekaguliwa?

Je, ni mara ngapi au kila baada ya muda gani ukaguzi huo hufanyika? Mheshimiwa Waziri naomba wakati wa majumuisho hayo nipate majibu hayo. Pia tunaiomba Serikali kupitia Wizara ya Miundombinu kurekebisha mishahara ya Manahodha kwani tokea mwezi wa 11 – 07 mpaka leo hii Manahodha au Makapteni wa Meli katika port Mwanza ambao huendesha meli za abiria wamehama kwa madai ya mshahara.

172 Pia hata Marubani wa Ndege za Serikali wengi wanahama kwa mishahara madogo. Hivyo nawaomba muwe macho kwa hilo. Rada hii muhimu kwa mamlaka ya hali ya hewa, kama kungekuwa na rada kubwa nadhani kimbunga ambacho kilitokea Mwanza hivi karibuni kingeonekana na kungewekwa tahadhari, lakini kwa kuwa mamlaka ya hali ya hewa hawana rada kubwa, tahadhari haikuwepo.

Je, ni lini Serikali itamalizia au kununua rada kubwa kwa ajili ya kufanikiwa kazi yao kitaalamu na kutoka hali ya hewa hata ya siku 30 mbele?

Mheshimiwa Spika, ninaiomba Serikali iangalie pia vivuko vyake vyote, viko taabani na Wilaya hii iko katikati ya maji. Tunaiomba Wizara itupie jicho la huruma kwa wanaukerewe hawa katika kuhadhari maisha yao.

Mheshimiwa Spika, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu, tulifika port Mwanza na tulitaarifiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Bandari kwa kuwa maji yanapungua na mchanga unakuwa mwingi watakodi mtambo wa kunyonya mchanga kwa geji na baadaye kununua wao. Napenda kujua zoezi hilo limefikia wapi? Mbona mchanga bado upo hasa kigongo ferry na Bandari ya Ukerewe? Yangu ni hayo. Nawatakia kazi njema, ahsante.

MHE. VUAI ABDALLAH KHAMIS: Mheshimiwa Spika, niaanze kwa kukupongeza kwa kusimamia Bunge la Jamhuri ya Muungano pamoja Naibu Spika na Wenyeviti wanaosimamia Bunge. Nasema hongereni sana na muendelee na moyo huo huo.

Mheshimiwa Spika, sina pingamizi wala choyo kwa kumshukuru Waziri wa Miundombinu – Mheshimiwa Andrew John Chenge, kwa kuwasilisha hotuba Bungeni ya mpango wa maendeleo na makadirio ya matumizi ya fedha kwa mwaka 2007/2008. Nampongeza sana pamoja na Manaibu Waziri na Watendaji wake kwa usaidizi wao. Mheshimiwa Spika, Wizara inasimamia Baraza la Bodi mbalimbali zinazohusika na utaratibu wa shughuli za kisekta kama vile uhandisi, ukandarasi, usimamizi wa vifaa, ubunifu wa majengo na ukadiriaji wa ujenzi. Naomba sana tuwe wawazi na mwenye ukweli kwa mambo haya kuzingatia nchi yetu hasa Serikali ya awamu ya nne tuondokane na maovu na bodi zisimamie.

Mheshimiwa Spika, bila miundombinu, maendeleo ya nchi yoyote ni mafupi na mabaya na nchi yetu Tanzania tunahitaji maendeleo yote tuyapate. Barabara safi, Railway safi na njia za kileo, Airport safi na ndege zake, usafiri wa baharini, pia tuwe na meli, boti hata mashua za kileo. Kwa hiyo, Serikali isimamie vizuri.

Kwa hiyo, tunakuomba sana, Mheshimiwa Waziri Chenge anaweza sana kusimamia, lakini asiagize tu, naomba asiwaamini wafanyakazi wa Wizara yake, yeye awe mbele kama tunavyomfahamu kwa maslahi ya nchi yetu ili tuepukane na mabaya kwa asilimia nyingi za huduma zetu.

173 Mheshimiwa Spika, bandari zetu zote ziboreshwe pia kuzingatia Bandari ya Zanzibar ambayo inaleta pato kubwa kwa Taifa letu. Naomba tuondoe tofauti ili pato lizidi kwa maslahi yetu na TRA waongeze juhudi pato lizidi.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Wananchi wa Magogoni na mimi mwenyewe, naunga mkono hoja kwa asilimia zote.

MHE. KHALIFA S. KHALIFA: Mheshimiwa Spika, natoa pole kwa misiba yote iliyotupata.

Mheshimiwa Spika, napenda kuanza na suala la barabara nchini mwetu. Naomba sana sana Serikali iwaangalie wananchi wa Mikoa ya Rukwa na baadhi ya Wilaya za Mkoa wa Mbeya mfano Chunya. Hali ni mbaya sana zaidi kule Rukwa ambako wananchi wanajiita Watanganyika kutokana na kutengwa na maeneo mengine ya nchi yetu ni barabara mbovu.

Mheshimiwa Spika, ATC ni chombo muhimu na naomba Serikali iwapatie mkopo mkubwa na pia kuwaunganisha na mashirika mengine ili ATC iingie ubia kama vile lilivyo Shirika la Ndege la Kenya. Mheshimiwa Spika, Wizara hii siyo tu ifikirie E-Business na E-Government bali pia ifikirie E-procurement hasa kwa kuwa inanunua vifaa vingi sana.

Mheshimiwa Spika, suala la vivuko ni muhimu sana na zaidi kile cha Kigamboni kwani kinahudumia watu wengi mno. Hivyo basi, mbali na kutafuta vivuko madhubuti bali pia ifikirie suala la umuhimu wa daraja. Naomba sana Mheshimiwa Waziri atoe maelezo kuhusu kadhia ya rada, uchunguzi wa ndani na nje umefikia wapi?

Mheshimiwa Spika, pia suala la vyombo vya usalama baharini ni muhimu mno hasa ukanda wa Magharibi ambapo ajali nyingi hutokea na maisha ya watu kupotea.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

MHE. LAZARO S. NYALANDU: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. Naomba nitoe ushauri kwa yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, ATCL, shirika sasa lifanye transformation ya kulifanya liwe la kibiashara kwa kununua ndege mpya badala ya kuendelea kutumia equipment za miaka ya 1970’s. Naiomba Serikali ilichukue deni la ATCL ili shirika liwe huru kukupa popote duniani kwa lengo la kupanua wigo wa huduma zake, kama accessing global equity and investment funds, code-sharing, global alliances such star alliance sky steam shirika liweke juhudi kuboresha tija za kuongeza kiwanja kwa huduma kwa wateja.

Kujengwa kwa Kiwanja kipya cha Ndege Tanzania. Hili ni jambo la dharura kabisa kama Tanzania itaongeza ushindanni wake kama hub katika usafiri wa anga duniani. Passenger traffic ndani na nje ya nchi hadi sasa ni chini ya 2.5m, lakini

174 potential yake na hadi abiria zaidi ya 5m kwa mwaka, DSM city should host the new airport.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa KQ wana ubia na KLM AIR FRANCE, napendekeza kwa ATC ijiunge na STAR Alliance inayoongozwa na BA na AA. Naomba Serikali imalizie kazi ya ujenzi wa Kiwanja cha Ndege Singida.

Mheshimiwa Spika, ahsante na ninaunga mkono hoja.

NAIBU WAZIRI WA MIUNDOMBINU (MHE. DR. MAUA ABEID DAFTARI): Mheshimiwa Spika, kwanza, namshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kutupa sote afya njema na kutuwezesha kukutana tena katika kujadili Bajeti ya Wizara ya Miundombinu.

Napenda nichukue nafasi hii kukushukuru wewe mwenyewe binafsi kwa kuendesha vikao vya Bunge letu na napenda niwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote kwa mara zote walikuwa wananiandikia kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wao na kwa pamoja tumejitahidi kwa kiasi kukidhi mahitaji yao. Yapo maeneo ambayo bado yanaendelea kushughulikiwa nawaomba wawe na subira.

Mheshimiwa Spika, naomba niruhusu nitoe pole kwa ndugu na familia ya Mzee Chifupa Mpakanjia kwa kifo cha mtoto wao mpendwa tegemeo kwao na kwa nchi yetu napenda nikili kuwa yeyote ambaye atataka kuiga mfano wake basi ni lazima athubutu. Yaani aamue bila woga kujitoa kwa maslahi ya nchi yetu. Naiombe roho ya marehemu Mbunge mwenzetu mahali pema peponi amina.

Mheshimiwa Spika katika kipindi hiki kifupi tumewapoteza ndugu zetu wengi katika ajali mbalimbali zilizotokea nchini kwetu. Ajali za barabarani, za majini na ajali za nchi kavu. Naomba kutoa rambirambi zangu za dhati kwa ndugu wa marehemu wote na nachukua fursa hii kwa mara nyingine tena kuwasihi madereza wote wa vyombo vya moto viwe vya baharini, barabarani au anga kuwa waangalifu wakati wa utoaji huduma kwa wananchi. Lazima wakumbuke kuwa wao wanaowajibu wa kulinda roho za abiria wanao wasafirisha na mali zao na daima wakumbuke kuwa bila ya abiria na mizigo hakuna biashara na nafsi zao ziongozwe na utu na upendo kwa wenzao.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo machache sasa naomba uniruhusu nami niweze kuchangia hoja iliyopo mbele yetu, hoja ya Wizara ya Miundombinu Sekta ya Mawasiliano na Uchukuzi.

Mheshimiwa Spika, nianze na sekta ya mawasiliano. Sekta hii imeendelea kukua na kuboreka kila leo. Aidha kuboreka kwa mawasiliano ya simu nchini kumewasaidia wananchi mijini na vijijini kurahisisha shughuli zao za kibiashara na kijamii. Upatikanaji wa taarifa kwa wakati kumesaidia jamii kuweza kufanya maamuzi ya wakati na mwafaka kwa wakati mwafaka. Nachukua nafasi hii kuzipongeza kampuni zote za simu nchi kwa kazi nzuri inazozifanya za kuboresha huduma zao katika eneo hili. Ushirika wa sekta binafsi umechangia sana uboreshaji wa uchumiwa wa nchi yetu. Changamoto kubwa

175 iliyoko mbele yetu ni kuwaomba wamiliki wa makampuni haya waendelee kupunguza bei za huduma zao ili wananchi wengi wafaidike nazo pia huduma hizi nazo ni lazima zifike vijijini ambako wengi wa wananchi wetu wanahitaji huduma hizi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wizara inayo mipango ya kuendeleza zaidi sekta hii kwa kushirikiana na sekta binafsi. Ujenzi wa mkonge wa baharini ambao utaunganishwa na mkonge wa ardhini nia ni kuona tunaunganisha mikoa miji vijiji nchini kote. Na pia kuunganisha nchi yetu na nchi za jirani Rwanda, Burundi, Zambia na kadhalika. Mitandao ya mikonga ya ardhini na makampuni mbalimbali itaimarika. Kukamilisha azma hiyo hakutokuwa na duplication ya efforts wala wastage of resources kwa maana mitandao iliyopo ya reli ya TAZARA na TRC na TANESCO itatumika kikamilifu katika kufanya shughuli hizi za mkongo. Hivi sasa TTCL inaendelea kuongeza njia mbalimbali za mikongo na TANESCO na TRC kwa pamoja. Nina hakika zitasaidia sana mawasiliano.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge wengi wameomba maeneo yao mbalimbali yaweze kufikishiwa mawasiliano ili wananchi wao wafaidike. Napenda niwakikishie kuwa tutaendelea kuwa nao sambamba na kuyasihi makampuni yetu kwa kuwaomba waweze kukidhi haja za Wabunge wetu. Hatua tuliyofikia ni kubwa katika mawasiliano. Roma haikujengwa kwa siku moja na nina hakika hatua kwa hatua maendeleo ya simu yatawafikia wananchi wengi nchini mwetu.

Mheshimiwa Spika, miji ya Ruangwa, Liwale, Nachingwea itafikiwa kwa mradi wa CDM ambao utakamilika kabla ya mwisho wa mwaka huu na sehemu nyinginezo kama za Nzige, Jinjo zitafikiwa baada ya kupata fedha za mfuko wa maendeleo ya simu vijijini. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Jenista kwamba kule kwake hatujakusahau. Peramiho, Magazini, Ifinga watashughulikiwa. Waheshimiwa Wabunge napenda kuwahakikishia kwamba tutahakikisha tunashughulikia masuala ya mawasiliano vijijini ipasavyo. Nimefurahi na roho yangu kutulia kusikia Mheshimiwa Msindai kwamba amepata simu kwake ya CELTEL kwani kadri nilivyokuwa nasukuma suala lake lilikuwa linanipa taabu kidogo. Lakini leo nimefarijika baada ya kumsikia kwamba mawasiliano yamefika.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, wewe binafsi huwezi kujisemea lakini mimi nitaendelea kukusema katika maeneo yako nawe unikumbuke kunisemea katika maeneo yangu kwa sababu na mimi sina mtu wa kunisemea. Baada ya kusema hayo machache najua yako mengi ya TTCL ya CELTEL ya ZANTEL lakini nikiri tu kwamba kwa sababu ya muda haya yawe yametosha tutayaandika na Waheshimiwa Wabunge ipasavyo.

Mheshimiwa Spika, lipo suala la Posta. Kuna ombi la ujenzi wa jengo la kisasa la Posta Wilayani Sikonge. Mheshimiwa Mkumba ushauri tumeupokea. Tunataka kukuhakikishia kwamba mchoro wa jengo hilo tayari. Tumeshafanya mawasiliano ili kupata kiwanja na Shirika limeahidi kwamba litajenga katika mji wa Sikozi, tunahangaikia kupata fedha. Fedha zikipatikana Mheshimiwa Mbunge hutalia kama ulivyosema siku zile.

176 Mheshimiwa Spika, Shirika la Posta kupatiwa mtaji, kuondolewa mzigo wa madeni na kutumia teknolojia ya kisasa, kukarabati majengo na kununua vitendea kazi ili liweze kukabiliana na ushindani wa kibiashara na kuendesha shughuli zake kwa ufanisi. Nakubaliana na haya kwa sababu si kila mtu anapenda ku-post barua. Watu wengi sasa wanatumia teknolojia ya habari kupeleka mawasiliano kuulizana hali, kupelekeana kadi lakini tutakwenda na sisi na wakati. Nia ni kuona kwamba tunalifutia madeni yake Shirika hili ili mizania yake ya mahesabu iwe mizuri na wao waweze kukopesheka. ( Makofi)

Mheshimiwa Spika, posta ya Mkwajuni, Songwe huduma ziboreshwe, tunasema sawa. Lakini Songwe huduma za pale ni za wakala, tutafanya tathimini kuangalia viwango na kupandisha daraja ili kuweza kutoa huduma kufuatana na mahitaji halisi. Napenda niwashukuru wote waliochangia katika sekta hii ya mawasiliano ya simu na posta.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba nichangie masuala la ATCL. Nikiri tu kuwashukuru kwanza Waheshimiwa Wabunge wote kwa sababu kila aliyesimama amesifia sana hatua iliyochukuliwa ya kurudisha ATCL mikononi mwa Serikali na kila aliyesimama ameshukuru na kupongeza kwamba tumepata menejimenti mpya na Bodi nzuri ambayo wana hakika itatuvusha na kuona ATCL ni mpya, iliyozaliwa upya ambayo itahimili ushindani. Nia ya Serikali kupitia Wizara yetu ni kuifufua upya Air Tanzania iweze kumudu ushindani ndani na nje ya nchi. Inayo mipango madhubuti ya kuongeza ndege na kupata routes zake za zamani na kuanzisha mpya. Ni nia ya ATCL kuwa na wafanyakazi waliohamasika wanayoipenda ATCL mpya na ambao wapo committed na tayari kujituma wakati wowote. Menejimenti imetuhakikishia kwamba itawajali wafanyakazi wake. Lakini suala jingine ambalo Menejimenti inasema ni kwamba watafanya cost wakati cutting measure kwa yale ambayo yanaweza kufanyika Tanzania yafanyike Tanzania ili kubana matumizi na fedha ziweze kutumika kwa mambo mengine lakini zaidi ni kuelimisha wafanyakazi wake.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba suala hili tunalipa uzito unaofaa na tutakodi ndege na tutanunua ndege na routes zote zile zilizokuwa hazipo zitapatikana na yule Twiga ambaye ametoweka atarudi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda kuzungumzia masuala ya viwanja vya ndege. Mamlaka ya Viwanja vya Ndege inasimamia Viwanja 62. Kwa hiyo, nitasema kwa kifupi viwanja vya wa Tabora, Kigoma, Arusha, Mafia, Shinyanga, Sumbawanga na Bukoba. Mhandisi mshauri ataanza kazi ya usanifu katikati ya mwezi wa Agosti mwaka huu. Viwanja hivi vitasanifiwa kwa ndege ATR-72, Kigoma Airport usanifu ni kwa Boeing 737 na mfadhili ni World Bank. Dodoma Airport taa za kuruhusu kuruka na kutua ndege usiku zitafungwa kuanzia mwezi Septemba mwaka huu na Msalato Mhandisi mshauri amepatikana kufanya feasibility study na usanifu na kazi itaanza mwishoni mwa mwezi huu. Compensation itaangalia baada ya kufanya review.

Mwanza Airport nimepata bahati ya kwenda jana tukiwa na Mheshimiwa Rais, ukarabati na upanuzi wa apron unaendela vizuri kwa gharama ya shilingi bilioni 7.7

177 ambazo kutoka Serikalini. Mradi mkubwa wa upanuzi utaanza Januari mwakani chini wa ufadhili wa BADEA, OPEC na Serikali. Tender document tayari wameshapata short listing ya contractors, lengo ni kumaliza awamu hii ya tatu vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Songwe Airport, hatujachelewa isipokuwa tunaingia awamu ya tatu ambayo itaanza Oktoba mwaka huu, itachukua miezi 18 na kukamilika mwezi Aprili 2009. Mfadhili ni BADEA na tumeshapata no objection kutoka BADEA. Mtwara taa za kutua ndege usiku zimefungwa kwa msaada ya Artmus. Tunawashukuru sana hivi sasa wanfanya calibration na approval TCAA. Tunategemea zitatumika mwishoni mwa mwezi huu wa Julai. Kwa hiyo, wale wanaotumia kiwanja cha ndege cha Mtwara wataweza kutua hata usiku.

Mheshimiwa Spika, JK Nyerere International Airport, awamu ya pili ya ukarabati wa pavements na taa za kuongozea ndege itaanza Oktoba mwaka huu, gharama ni Euro milioni 28. Mradi huu unafadhiliwa na ORET asilimia 50 na Serikali asilimia 50 ambao ni Mkopo kutoka Netherlands. Zile bridges ambazo zimezungumizwa zinashukuliwa kila leo.

Ni juu yetu kuona kwamba usalama wa usafiri wa anga unakuwepo. Viwanja vingine vilivyobaki Mamlaka ya Viwanja vya Ndege itaendelea kuvifanyia matengenezo ya kawaida. Na miradi itakayogharimu Serikali ni Mafia shilingi bilioni moja, kazi inaendelea na nakushukuru sana Mheshimiwa Shah kwa sababu umesema kweli. Msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Singida imezungumzwa sana. Tumetenga shilingi milioni 100 kazi ya ku-measure barabara ya ndege na apron itaanza Agosti mwaka huu.

Arusha, bilioni 1, tunatengeneza apron, taxi ways na runway na tumeweka lami mita 1200. Kigoma zimetengwa shilingi milioni 400 kuimarisha runway na kukamilisha kazi ya fence. Mheshimiwa Kagasheki asiwe na wasiwasi na Mheshimiwa Beatrice asiwe na wasi wasi.

Mwanza kwa TAA wametenga shilingi milioni 600 kwa ajili ya ujenzi wa Apron. Tutakuwa na ujenzi wa seculity fence na fedha zitatoka kama ifutavyo:- Mwanza milioni 100, Dodoma milioni 100, Arusha milioni 100, Musoma milioni 40 na Tabora milioni 65.

Mheshimiwa Spika, aluta continua! Sekta yangu ina mambo mengi sana, niruhusu mengine niyaruke kwa sababu muda ulionipa ni mfupi. Wengi wamezungumzia juu ya Bandari, kwa hiyo, nichukue nafasi hii nizungumzie juu ya Bandari.

Mheshimiwa Spika, Lake Victoria watu wa Bandari watafanya nini? Mwanza Port, watatengeneza Whare House ya South, Road Foundering System, Mwanza South na North, yale mapira ya kuzuia meli zisiharibike wakati zinafunga gati. Watatengeneza fence, wataweka way bridge ya 40 tones, wata-install mambo mbalimbali, watafanya maintenance dragging na provision of security ya Mwanza South.

Mheshimiwa Spika, Nansio Port kuna kazi vilevile zitafanyika. Kemondo Bay, Bukoba Port, Musoma Port, lakini kote huku, labda nisema Mwanza wametenga shilingi

178 milioni 485. Hizi pesa hamtoziona kwenye vitabu kwa sababu ziko katika bajeti ya TPA. Nansio wametenga shilingi milioni 215, Kemondo Bay milioni 70, Bukoba Port milioni 265, Musoma Port milioni 42. Bandari nyingine ambazo tunaziita ni Jets ni shilingi milioni 150 na kutakuwa na kifungu kidogo cha normal maintenance cha shilingi milioni 40.

Mheshimiwa Spika, tuje kwenye Lake Tanganyika ambalo alizungumzia sana Mheshimiwa Mbunge: Kigoma Port 670…...!

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, ninao ushauri, kama Mheshimiwa Waziri ataridhia, labda uchukue dakika 5 zake yeye ili abaki na dakika 55...! Naona amekubali. Kwa hiyo, ili umalize vizuri, endelea!

NAIBU WAZIRI WA MIUNDOMBINU – MHE. DR. MAUA A. DAFTARI: Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa kunipa dakika 5, kwa sababu sekta hii ni ndefu. Kaila Port milioni 400, Kalema milioni 400, Kilando milioni 400, Kasanga Port bilioni 2.5 na kutakuwa na pesa za maintenance. Jumla ya Lake Tanganyika ni 4,785,000,000/=

Mheshimiwa Spika, Lake Nyasa; Itungi Port milioni 30, Kiwira Port milioni 15.5, Mbamba Bay milioni 104.5, Liuli milioni 10, Lundu milioni 8 na kutakuwa na maintenance ya milioni 50. Lakini niseme tumefurahi kuona Mafia, zile shilingi bilioni 4, Mheshimiwa Shah zipo na hazijapotea.

Mheshimiwa Spika, sitaki nipigiwe kengele, nikiri tu kwamba sikuweza kufika hata nusu ya kusema haya ambayo nilipaswa kuyasema kwa sababu muda hauniruhusu. Naunga mkono hoja! Namwomba Mheshimiwa Waziri anisaidie kwa yale ambayo sikuyasema. (Makofi)

SPIKA: Kama kawaida, yale ambayo hayakuweza kuzungumzwa kama majibu ya hoja, tutafurahi tukiyapata kwa maandishi, yatatusaidia kupata ufahamu. Namwita sasa Mheshimiwa Naibu Waziri Dr. Makongoro Mahanga!

NAIBU WAZIRI WA MIUNDOMBINU (MHE. DR. MILTON M. MAHANGA): Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru kwa kunipa na mimi nafasi niweze kuchangia hoja hii iliyoko mbele yetu ya Wizara ya Wizara ya Miundombinu. Nianze kwa kusema kwamba naiunga mkono kwa asilimia zote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili, na mimi nitoe salamu za rambi rambi kwa ndugu, jamaa na marafiki, kwa kufiwa na wapenzi wao akiwemo marehemu Amina Chifupa aliyekuwa Mbunge kijana, shupavu sana. Mungu aziweke roho za marehemu mahali pema poponi, Amin!

Mheshimiwa Spika, nawashukuru na nawapongeza sana wapiga kura wa Jimbo la Ukonga kwa ushirikiano wao wanaoendelea kunipa katika kuendeleza Jimbo la Ukonga. Kwa kuwa barabara za Ukonga hazikutajwa hapa, kwa sababu mimi nilikuwa siruhusiwi

179 kuchangia wakati huo, nawahakikishia wapiga kura wa Ukonga kwamba wasiwe na wasiwasi, kwa kweli barabara zao zitaendelea kuboreshwa. Kutoka Banana kwenda Kitunda, tutafika kwa lami. Tabata – Segerea – Kinyelezi – Banana, Vingunguti – Chang’ombe – Segerea – Tabata Relini – Twiga – Kimanga Savana, barabara ya Mombasa – Ukonga mpaka Mazizini, barabara ya Majohe, Mongolandege na Udongoni, barabara za Kiwalani na hasa Minazi Mirefu na barabara za Kigogo – Tabata, zote tutazishughulikia.

Mheshimiwa Spika, nieleze tu kwamba hoja zilizowekwa mbele yetu ni nyingi sana, na mimi nataka niseme kwamba kwa sababu tutaziweka kwenye maandishi, nieleze tu kwamba tumechukua maoni yote ya wale waliochangia na tutawapa majibu kwa maandishi.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri atakuja kuzungumzia barabara zote zinazounganisha mikoa na zile zinazounganisha nchi yetu na nchi za jirani kwa maana ile ya Uchumi wa Kijiografia. Lakini bila barabara za Mikoa ili kuingia kwenye barabara hizi kuu, hatuwezi kuendelea. Kwa hiyo, mimi nitajitahidi kujibu zile barabara za Mikoa kwa namna tulivyoulizwa.

Mheshimiwa Spika, nieleze tu kwamba wachangiaji walikuwa ni wengi na Kanda zote. Nimejaribu kuweka kikanda. Waliochangia: Kanda ya Kati, Singida na Dodoma, Mheshimiwa DR. John Malecela, alichangia na tunamshukuru kwa mchango wake. Kuongeza ruzuku kwenye Halmashauri, tumezingatia na ndio maana fedha zimeongezeka. Sasa, wapeleke na hela hizo kwenye barabara za vijijini vilevile. Ushauri wake kuhusu barabara za kwenda kwenye mbunga za wanyama za Ruaha, tutaangalia na kupandisha barabara tutaangalia kwenye vigezo ambavyo vimewekwa kisheria.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mgana Msindai naye tumezingatia ushauri wake kuhusu Feasibility Study pale Sibiti – Iguguno – Nduguti - Kumanga, itaimarishwa, na shilingi milioni 60 zimetengwa kwa ajili ya madaraja. Daraja kwenda Nkungi limeharibika sana, ndiyo! Milioni 76 zimetengwa mwaka huu na shilingi milioni 120 zilitengwa vilevile mwaka jana. Kuhusu Iguguno iunganishwe na upande mwingine pia, kwa sasa tunaunganisha upande huu wa kutokea Singida. Ushauri kuhusu mwendo wa mabasi, milango ya dharura na kadhalika tumezingatia.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Diana Chilolo alizungumzia ujenzi wa changarawe kwamba tuachane nao, tujenge lami kidogo kidogo. Tunazingatia na ndivyo tunavyofanya. Lakini kutokana na ufinyu wa fedha na umuhimu wa barabara kila mahali, tutaendelea kujenga barabara. Amezungumzia Isuna – Manyoni, apewe Mkandarasi makini na igawanywe zehemu mbili. Tayari tunaendelea na zoezi la kuteua Mkandarasi, lakini hatuwezi kufikia ile ya kuigawa mara mbili, lakini tutazingatia umakini.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Juma Kilimbah alizungumzia Shelui – Sekenke – Ntwike, ilitengewa fedha, lakini hakuna kilichofanyia. Sehemu hiyo imeshughulikiwa kilomita 15, milioni 12.7. Lami nyepesi Misigili – Kiomboi, tulipokuwa na Mheshimiwa

180 Waziri Mkuu niliahidi na naendelea kuahidi hapa kwamba mwaka huu itaanza kujengwa kwa kiwango cha otta seal. Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Simbachawene, barabara yako tutaizingatia katika sheria ya barabara.

Mheshimiwa Spika, wachangiaji katika Kanda ya Ziwa walikuwepo pamoja na Mheshimiwa Severina Mwijage ambaye alizungumzia barabara yake, Katema - Katoro – Izimbya – Kyaka. Hali ya barabara hiyo ni nzuri kwa kweli. Vilevile alizungumzia kiasi kilichotengwa kwa barabara hiyo ya Katema - Katoro – Izimbya – Kyaka – Mlogo. Tumetenga jumla ya shilingi milioni 170 kwa barabara hizo mbili.

Mheshimiwa Wasira, alizungumzia kuunganisha Nyamswa katika upembuzi yakinifu wa Mgumu – Mto wa Mbu – Loliondo. Tumezingatia na tutafanya hivyo. Amezungumzia barabara ya Balili – Mgeta – Manchumwelu, kule nilikozaliwa mimi, tutaangalia kwenye vigezo. Mheshimiwa Charles Mlingwa alitoa pongezi kwa kujenga kutoka Shinyanga – Old Shinyanga. Tumepokea pongezi. Lakini vilevile Mheshimiwa Shibiliti alizungumzia kuweka tuta katika barabara ya Fulo – Nyambiti kule nilikokwenda. Hilo nitalizingatia. Mheshimiwa Shibiliti pia alizungumzia Kiesa by Pass, tutazingatia na barabara zake zile tutaangalia kwenye vigezo.

Mheshimiwa Chitalilo vilevile amesema tuachane na changarawe, tujenge lami, tutazingatia. Mheshimiwa Emmanuel Luhahula alizungumzia barabara zake za Isaka – Bukombe, na zenyewe zinawekewa utaratibu. Barabara ya Lunzewe – Bwanga – Iyogelo, tunafanya feasibility study, badaye tukipata fedha tujenge, baadaye barabara ya Buselesele. Kiasi tulichopata cha shilingi milioni 50 ndicho hicho hicho, tutavumiliana.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mpina, amezungumzia barabara ya Ng’oboko na barabara zile zingine. Tutazingatia vigezo hivyo kama kweli tunaweza tukapandisha. Barabara ya kutoka Sola Junction kwenda Sakasaka, tubuni barabara hapo na kutoka Butuni kwenda mpaka kule kwenye Game Reserve ya Butuni, litaangaliwa hilo.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Masilingi amezungumzia mambo ya fidia na barabara ya Muto – Kamachimu – Muleba kwamba imetengewa hela kidogo, basi wapewe wananchi. Tutalizingatia vilevile. Mheshimiwa Raichard Ndassa alizungumzia savings zilizobaki kwenye feasibility study, basi tuweke feasibility study ya Maligusu – Simiwi, ile savings ya PMMR na zile barabara zingine, tutazizingatia, kuna shilingi milioni 160.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Bujiku Sakila naye alizungumzia barabara zake, Mheshimiwa Ngeleja alitoa tahadhari ya usimamizi wa fedha, Mheshimiwa Lembeli alizungumzia barabara zake, Mheshimiwa Prof. Sarungi naye akazungumzia kuhusu udhibiti wa Makandarasi.

Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa kutoka Pwani walizungumza wengi. Mheshimiwa Dr. alizungumzia barabara yake ya Handeni – Kinore imekuwa ya Mkoa. Ambayo ni ya Mkoa ni Kibereshi – Handeni – Kinore. Lakini ile ya

181 Songe – Kibereshi ndiyo inafikiriwa katika mapango huu mpya ijenge uwezo wa kutumia makandarasi kwa kutumia fedha zilizopo, tunazingatia.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Shah, pongezi tumepokea. Kuhusu kuongezewa shilingi milioni 50 kwa ajili ya kununulia vifaa iwe milioni 150. Zimezidi, kwa kweli ziko 180, kwa hiyo zinatosha. Balozi Mshangama alishauri kuwa wawakilishi wa TANROADS waende Wilayani, tutazingatia. Kuhusu barabara mbadala ya Mbombwe – Dochi, kwa sasa tuliiacha kwa sababu tulishajenga ile ya Mombo – Lushoto. Pia alisema wakati wa mvua, Lushoto – Mlalo kunakuwa kunajifunga, sasa hivi itaimarishwa.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbarouk amezungumzia barabara zake za Maramba. Tutazingatia PMR tumeishaitaja. Mheshimiwa Mntangi naye alizungumzia barabara zake za Amani na kusema tushirikiane na wale wakulima. Tutashirikiana nao. Vilevile katika Kanda ya Pwani, Mheshimiwa Mussa Azzan alizungumzia barabara ya Uhuru. Kwa mwaka huu hatukupata fedha. Lakini Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, tutashirikiana na mimi na Mbunge pale na Diwani ili tuikarabati, lakini baadaye tutaiweka kwenye barabara za TANROADS baada ya Study ile ya JICA.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mwinchoum naye alizungumzia barabara ya Kongowe – Feri kwamba nyumba zimewekewa X kimakosa. Wale walioko ndani, hakutakuwa na makosa, lakini wale ambapo kuna makosa, tutafuatilia. Kuhusu kujenga barabara ya Feri – Kibada kwa lami, uwezo wa fedha ukiruhusu, tutajenga. Kuhusu daraja ambalo limezungumziwa sana, ushauri wote tumezingatia.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mustapha Mkullo naye alizungumzia barabara zake za Kilosa, ziko katika hali nzuri. Mheshimiwa Charles Kenja, alizungumzia kuhusu kupunguza msongamano. Kawe – TPDF Range, tayari kazi itaanza karibuni kwa lami. Feasibility study ya Goba – Banana kule kwangu, tayari inafanyika. Kwa hiyo, tumeishaanza kuchukua hatua. Kuhusu FlyOvers itategemea na fedha lakini tuangalie ile study tunayosubiri. Pia alizungumzia barabara za Ubungo, zikipatikana fedha lakini afuatilie Kinondoni.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Marombwa alizungumzia barabara zake za Kibiti – Rwaluka – Nyamiseti, akazungumzia value for money. Tunazingatia. Mheshimiwa Prof. Mtulia alizungumzia barabara za Kibiti – Utete shilingi milioni 155, kwa kweli zimetengwa milioni 255. Mheshimiwa Abbas Mtemvu alizungumzia barabara za Jeti Club – Devis Corner – Mtongani. Tumetenga shilingi milioni 546. Naka niwahakikishie wananchi wa Temeke kwamba abarabara hiyo tutaijenga. Mheshimiwa Idd Azzan alizungumzia pia Kawe – Range, nimeishaijibu. Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa amezungumzia kuhusu kujenga nyumba vilevile kwenye Wilaya badala ya kujenga Mkoani tu.

Mheshimiwa Spika, Kanda ya Magharibi walizungumza wengi. Mheshimiwa Tatu Ntimizi alizungumzia kuhusu kutoa ruzuku mapema kabla ya mvua. Kwa kweli zinatolewa kila mwezi kwenda Wilayani. Pia alisema barabara ya Itigi – Tabora imewekewa hela kidogo. Kwa kweli ni kuangalia tu vizuri, lakini zimewekwa hela nyingi

182 shilingi milioni 767.9 kwa ajili ya ukarabati mbali mbali wakati tukingojea fedha za ujenzi kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Kijiko alizungumzia fidia kabla ya bomoa bomoa, imezingatiwa. Lakini pale ambapo sheria inaruhusu tu. Suala la kupunguza msongamano wa Dar es salaam, tunaendelea. Mheshimiwa Sijapata Nkayamba alizungumzia nyumba zilizowekwa X miaka minne iliyopita. Tumeweka kama tahadhari ili wale wenye uwezo waanze kutoa. Lakini hatutawabomolea mpaka tutakapopata fedha na wakati huo tutatoa notice. Lakini wale wanaoweza waanze kutoa kwa sababu kwa kweli wako kwenye hifadhi. Mheshimiwa , alizungumzia barabara zake za Tabora – Ipole, amezungumzia sana na tumezingatia. Kuna pesa za kutosha wala siyo kidogo, shilingi bilioni 1.06, tutaanza na hizo. Mheshimiwa Spika, Selelii alizungumzia Itigi – Tabora kwamba imetengewa kiasi kidogo cha fedha. Nimeishaijibu kwa Mheshimiwa Tatu Ntimizi. Mheshimiwa Switi, barabara za Rukwa, Mheshimiwa Teddy Kasella-Bantu, barabara na madaraja, tumezingatia.

Mheshimiwa Spika, Kanda ya Kaskazini: Waliozungumzia ni Mheshimiwa Fuya Kimbita, Mheshimiwa Lucy Owenya, Mheshimiwa Dr. Slaa, barabara ya Oldei – Mang’ora – Lalago. Tayari hiyo hiyo tutaanza kuitengeneza. Mheshimiwa Mwanri, mkataba wa barabara ya Boma ng’ombe – Sanya Juu – Kamwanga uharakishwe. Tutaweka sahihi mkataba wa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina mwezi ujao. Kwa hiyo, baada ya hapo tutatafuta pesa za kujenga barabara hiyo. Mheshimiwa Lekule alizungumzia barabara hiyo na tunakubali.

Barabara ya Kitumbeine – Longido iitwe Longido – Kitumbeine – Loliondo. Tumezingatia. Kuhusu barabara ya Kamwanga – Longido iwe ya Mkoa, tutaangalia vigezo. Mheshimiwa Omary Kwaangw’ alizungumzia barabara zake za Babati, tumezingatia. Mheshimiwa Kimaro alizungumzia ahadi ya Rais kwa barabara za Marangu – Mtoni – Himo. Mheshimiwa alizungumzia ahadi ya Rais, barabara ya Ndungu – Same. Tutaendelea kuboresha barabara hiyo na ile ambayo Halmashauri hawaiteengenezi vizuri, Serikali itafutailia.

Mheshimiwa Spika, Kanda ya Kusini walizungumza wengi. Mheshimiwa Fatuma Mikidadi, Mheshimiwa , Mheshimiwa Njwayo, wametoa michango mizuri. Mheshimiwa Mikidadi ile barabara ni kwamba imejengwa kwa kilomita 40 ya kutoka Nanganga – Ruangwa, tutatafuta hela zaidi ili tuweze kujenga hizo kilomita 20. Fidia, wanaostahili Kitinku - Kipatimo watalipwa. Yule Mkandarasi amemaliza matatizo yake, yaani SHAPRIYA. Na kwamba Masasi – Lingwa – Mbwemkulu – Nangurukuru, ipandishwe hadhi, vigezo vitazingatiwa. Mheshimiwa Hawa Ghasia, tuliahidi shilingi bilioni 1.7, Waziri Mkuu. Barabara yote hiyo itafanyiwa matengenezo ya kawaida mwaka huu wa fedha. Mheshimiwa Njwayo amezungumzia barabara ya Mtwara – Tandahimba kuwa iwekwe lami. Tutazingatia katika miaka ijayo. Lakini kwa sababu mwaka huu hakuna fedha ili tuanze kidogo kidogo. Pia amesema barabara ya Tandahimba – Litihu ujenzi unasuasua mpaka Mukwitu. Mwezi huu, kazi zitaanza, Malamba na Mkiga. Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mwanawetu Said ametoa pongezi, tunashukuru. Mheshimiwa Ng’itu daraja la Lukuledi, OPEC ilifanya kazi hiyo.

183 Nyanda za Kusini kulikuwa na wachangiaji. Mheshimiwa Dr. Mwakyembe alisema madaraja ya Kyela mengi ni ya miti, Halamshauri hazina uwezo. Kutokana na ufinyu wa bajeti, Wizara haiwezi kusaidia kwa mwaka huu. Lakini tuendelee kutafuta uwezo kwenye Halmashauri, TAMISEMI na baadaye Serikali inaweza kufanya inachoweza kusaidia. Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Gideon Cheyo, alizungumzia barabara za Ileje kwamba zitengenezwe, amezitaja hapa, na sisi tumezingatia yote haya. Kuhusu kupandisha hadhi, tutaangalia sheria. Kutoka Itumba – Isongole, kwamba iwekwe lami, kwa sasa tunashughulikia pale mjini Itumba. Tutaangalia, na kwamba Mawaziri watembelee, tutaangalia. Niombe radhi kwamba nilitemblea Mkoa wa Mbeya, nikaacha tu Wilaya ya Ileje. Nitakuja rasmi kwa ajili ya Ileje.

Mheshimiwa Anna Makinda aliomba barabara ya Itoni – Ludewa ikarabatiwe. Tutaanza ukarabati huo. Mheshimiwa alisema fedha kidogo kwa barabara muhimu ya Ifingo – Wino, hapana! Imetengewa shilingi milioni 85. Mheshimiwa Prof Mwalyosi ametoa mchango wake kutoka hospitalini, akizungumzia kubadilisha barabara ya Madaba – Mundindi – Mlangali – Njombe, tutaendelea kufanya kazi hiyo. Igurusi – Njombe – Malangali – Mbeya, ipandishwe daraja, tutazingatia kulingana na vigezo. Fedha zimetengwa Njombe – Ludewa – Manda – Luhuhu, ndio hela zimetengwa shilingi milioni 173 na kivuko cha Luhuhu kitakuwa tayari mwezi wa tisa na kile kilichokuwa kimekwama, kimeishaopolewa na kinafanyiwa matengenezo na kitaanza kufanya kazi mwezi ujao.

Mheshimiwa Prof. Mwandosya amezungumzia suala la Katumba – Tukuyu. Tutaangalia kulingana na fedha kama tunaweza kuweka lami. Lakini kwa mwaka huu hakuna fedha. Sula la TANROADS kukasimu Wilayani tutaliangalia. Mheshimiwa Kilasi, barabara ile tuliyopita mimi na wewe, Igawa – Rujewa – Madiba – Mafinga, ni upatikanaji wa fedha tu, lakini ahadi ya Rais itatimia. Mheshimiwa Dr. Guido Sigonda, Mabalizi – Mkwajuni na zile barabara zingine tumezingatia. Mheshimiwa , Mheshimiwa Nyaulawa na wengine wamechangia.

Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii kukushukuru sana na kusema kwamba naomba kuunga mkono hoja hii! (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Dr. Mahanga, ahasante sana! Katika kumsindikiza Mtoa hoja kuja kwenye Mic., nilikuwa nimeguswa na mambo mawili madogo tu: Kwanza, natumaini Mheshimiwa Mtoa hoja atazingatia ile adha ya Same Mashariki ambako Mbunge Mhusika anakesha anawaza barabara ya kilomita nane. Sasa, hii siyo tu ni adha kwa wapiga kura, lakini namhurumia sana Mzee wetu… !Ningeomba sana Mheshimiwa Waziri atafakari hilo! (Kicheko/Makofi)

Ya pili ni kule Kyela. Waheshimiwa Wabunge mliokuwepo asubuhi mliona na picha ilitembezwa hapa; mwenzetu kwa kweli anavunja hadhi ya Bunge, anakwenda kwenye ule mto anavua suruali, anamkabidhi katibu wake. Upande wa pili anapopokelewa na wananchi, sijui wanamshangilia kwa dhati, au….! Kwa hiyo, hili

184 nalo ni matatizo. La mwisho kabisa ni taarifa kwamba, barabara inayotoka Tabora Mjini kwenda kwa Spika ni ya vumbi! (Kicheko/Makofi)

WAZIRI WA MIUNDOMBINU: Mheshimiwa Spika, kwanza nakushukuru sana kwa maneno yako ya utangulizi ya manjonjo manjonjo. Lakini ndio hali ya maisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii ili niweze kufanya majumuisho kwa michango mbali mbali ambayo imefanywa na Waheshimiwa Wabunge tangu niwasilishe hoja yangu jana asubuhi. Kama kawaida wamechangia Wabunge wengi, wengi, wengi! Lakini sisi Wizarani, tuseme tumefarijika sana na mchango wa kiwango cha hali ya juu sana katika maeneo mbalimbali. Tunawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi kila siku ninapowasikia humu Bungeni naona ni darasa kubwa sana kwangu. Kwa hiyo, tunawashukuruni sana mwendelee kutusimamia, mwendelee kutushauri katika azima hii ya kuwatumikia Watanzania kwa dhati. Lakini kwa kipindi hiki kweli hatuwezi kwenda goigoi, tunataka kweli twende kwa Ari Mpya, Nguvu Mpya na kasi mpya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wabunge waliochangia kwa kuzungumza humu Bungeni ni kama ifuatavyo: nianze na Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu, Mheshimiwa Mohamed Hamis Missanga, Mheshimiwa Bakari Shamis Faki, Mheshimiwa John S. Malecela, Mheshimiwa Tatu M. Ntimizi, Mheshimiwa Dr. Abbdallah Kigoda, Mheshimiwa , Mheshimiwa , Mheshimiwa Beatrice M. Shellukindo, Mheshimiwa Raymond A. Mrope, Mheshimiwa Salum Khamis Salum, Mheshimiwa Dr. Zainab Gama, Mheshimiwa George M. Lubeleje, Mheshimiwa Capt. John D. Komba.

Mheshimiwa Dr. Binilith S. Mahenge, Mheshimiwa Zainab Matitu Vullu, Mheshimiwa Suleiman Ahmed Saddiq, Mheshimiwa Mgana I. Msindai, Mheshimiwa Peter Serukamba, Mheshimiwa Fatma Abdallah Mikidadi, Mheshimiwa Wilson Massilingi Mheshimiwa Lucas Selelii, Mheshimiwa Khalifa Suleiman Khalifa, Mheshimiwa Vedastus M. Manyinyi, Mheshimiwa Michael Lekule Laizer na Mheshimiwa Anne Kilango Malecela. (Makofi)

Mheshimiwa Mwinchoum A. Msomi, Mheshimiwa Richard M. Ndassa, Mheshimiwa Dr. Harrison Mwakyembe, Mheshimiwa Ibrahim Mohamed Sanya, Mheshimiwa Dr. Milton Makongoro Mahanga na Mheshimiwa Dr. Maua Abeid Daftari ambao ni Naibu Mawaziri katika Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge waliochangia kwa maandishi ni Wabunge 130. Lakini kama utamaduni wetu unavyotaka lazima niwatambue tu. Sasa sina hakika na muda wangu.

SPIKA: Tutakuongeza muda.

185 WAZIRI WA MIUNDOMBINU: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Waliochangia kwa maandishi: nianze na Mheshimiwa Aziza Sleyum Ally, Mheshimiwa Lucy F. Owenya, Mheshimiwa Dr. Wilbrod P. Slaa, Mheshimiwa Gideon A. Cheyo, Mheshimiwa Godfrey W. Zambi, Mheshimiwa Balozi Abdi Mshangama, Mheshimiwa Felix N. Kijiko, Mheshimiwa Pindi H. Chana, Mheshimiwa Savelina S. Mwijage, Mheshimiwa Dr. Charles Mlingwa.

Mheshimiwa Easter Nyawazwa, Mheshimiwa Mbarouk K. Mwandoro, Mheshimiwa Omar Yusuf Mzee, Mheshimiwa , Mheshimiwa Issa Kassim Issa, Mheshimiwa Mgana I. Msindai, Mheshimiwa , Mheshimiwa Mwadini Abbas Jecha, Mheshimiwa Juma Killimbah, Mheshimiwa Jenista Mhagama, Mheshimiwa , Mheshimiwa Fuya Kimbita, Mheshimiwa Aggrey D.J. Mwanri, Mheshimiwa Hamad Rashid Mohamed, Mheshimiwa , Mheshimiwa Jacob Shibiliti, Mheshimiwa Sijapata F. Nkayamba na Mheshimiwa Ameir Ali Ameir.

Wengine ni Mheshimiwa Hawa Ghasia, Mheshimiwa Prof. Raphael Mwalyosi, Mheshimiwa Samuel Chitalilo, Mheshimiwa Maria Hewa, Mheshimiwa Khalifa Suleiman Khalifa, Mheshimiwa Said J. Nkumba, Mheshimiwa Bernadeta Mushashu, Mheshimiwa , Mheshimiwa Diana Chilolo, Mheshimiwa Jackson Makwetta, Mheshimiwa Kidawa Salehe.

Mheshimiwa Brg. Gen. Hassan Ngwilizi, Mheshimiwa Yono Kevela, Mheshimiwa Stephen Galinoma, Mheshimiwa Mussa Hassan Zungu, Mheshimiwa Emmanuel Luhahula, Mheshimiwa , Mheshimiwa Hasnain Dewji, Mheshimiwa Mossy Mussa, Mheshimiwa Vuai Khamis, Mheshimiwa Paul P. Kimiti, Mheshimiwa Mustafa Mkulo, Mheshimiwa John P. Lwanji, Mheshimiwa Charles Keenja, Mheshimiwa Prof. Idris Mtulia, Mheshimiwa Mtutura Abdalah Mtutura, Mheshimiwa Juma Njwayo, Mheshimiwa Omar Kwaangw’, na Mheshimiwa Bujiku Sakila. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wengine ni Mheshimiwa Dr. Guido Sigonda, Mheshimiwa Hilda Ngoye, Mheshimiwa Elizabeth Batenga, Mheshimiwa Annia Chaurembo, Mheshimiwa Ludovick Mwananzila, Mheshimiwa Mkiwa Kimwanga, Mheshimiwa Mwanawetu Zarafi, Mheshimiwa Gosbert B. Blandes.

Mheshimiwa Idi Azzan, Mheshimiwa Sigfrid Ng’itu, Mheshimiwa , Mheshimiwa , Mheshimiwa Aloyce Kimaro, Mheshimiwa Ezekiel Maige, Mheshimiwa Prof. , Mheshimiwa Esthelina Kilasi na Mheshimiwa Dr. Luka Siyame. (Makofi)

Mheshimiwa Ephraim Madeje, Mheshimiwa Capt. , Mheshimiwa Zainab Matitu Vullu, Mheshimiwa Abdul Jabir Marombwa, Mheshimiwa Ruth Msafiri, Mheshimiwa Martha Mlata, Mhe. Eng. Stella Manyanya, Mheshimiwa Eliatta Switi, Mheshimiwa Mgeni Jadi Kadika, Mheshimiwa Philip Marmo.

186 Mheshimiwa Spika, wengine ni Mheshimiwa Teddy L. Kasella – Bantu, Mheshimiwa Mohammed H. Missanga, Mheshimiwa Richard S. Nyaulawa, Mheshimiwa Michael L. Laizer, Mheshimiwa Mohammed Rajab Soud, Mheshimiwa Salum Hemed Khamis, Mheshimiwa Balozi Khamis S. Kagasheki, Mheshimiwa Profesa Philemon M. Sarungi, Mheshimiwa Abbas Z. Mtemvu, Mheshimiwa Celina O. Kombani, Mheshimiwa Kabuzi F. Rwilomba, Mheshimiwa Dr. James M. Wanyancha, Mheshimiwa Profesa Philemon M. Sarungi, Mheshimiwa Said A. Arfi, Mheshimiwa Ali Khamis Seif, Mheshimiwa Daniel N. Nsanzugwanko, Mheshimiwa Omar Ali Mzee, Mheshimiwa Juma Said Omar, Mheshimiwa Mhonga S. Ruhwanya, Mheshimiwa Charles M. Kageje, Mheshimiwa Castor R. Ligallama, Mheshimiwa Kaika S. Telele, Mheshimiwa Laus O. Mhina, Mheshimiwa Clemence B. Lyamba na Mheshimiwa Hemed Mohammed Hemed.

Mheshimiwa Spika, wengine ni Mheshimiwa Athumani Janguo, Mheshimiwa Janet M. Massaburi, Mheshimiwa Dr. Raphael M. Chegeni, Mheshimiwa Khadija Salum Ally Al-Qassmy, Mheshimiwa Manju S.O. Msambya, Mheshimiwa Bujiku P. Sakila, Mheshimiwa Ali Juma Haji, Mheshimiwa Mwantumu B. Mahiza, Mheshimiwa Benedict K. Losurutia, Mheshimiwa Adam K. A. Malima, Mheshimiwa Fatma A. Mikidadi, Mheshimiwa Felister A. Bura, Mheshimiwa Hamza A. Mwenegoha, Mheshimiwa Dr. Festus B. Limbu, Mheshimiwa Dr. Mary M. Nagu, Mheshimiwa Hassan C. Kigwalilo, Mheshimiwa John M. Cheyo, Mheshimiwa Dr. Cyril A. Chami, Mheshimiwa Mohamed R. Abdallah na mwisho kwa kutajwa siyo kwa umuhimu ni Mheshimiwa Anne K. Malecela. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wakati wa hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Waziri wa Mipango, walichangia Wabunge 26, lakini kwa vile walitajwa sisi hatuwatambui kwa maana ya kuwataja. Lakini pia katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu na hoja ya Miundombinu, walichangia Wabunge 36, hii ni idadi kubwa kweli ndiyo maana nimesema sisi tumefarijika sana na hiyo.

Mheshimiwa Spika, nina ombi moja kwako, hizi podium zetu nafahamu ni ndogo sana, tunahitaji zipanuliwe kidogo. (Makofi)

SPIKA: Suala hilo unalolisema nimenong’onezwa pia na Mheshimiwa Waziri wa Elimu. (Kicheko) WAZIRI WA MIUNDOMBINU: Nashukuru sana, great mind Speaker like you. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, malengo na mpango wa maendeleo ya Wizara yetu kwa mwaka 2007/2008, kusema kwa kweli ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005. Wizara imeainisha programu mbalimbali zitakazotekelezwa katika mwaka huu wa fedha. Miradi hiyo inajumuisha matengenezo na ujenzi wa barabara, viwanja vya ndege, reli, vivuko, masuala ya TEKNOHAMA, nyumba kwa matumizi ya watumishi wa Serikali lakini pia na zima la hali ya hewa. Hata hivyo, mahitaji halisi ya kutekeleza miradi hiyo katika mwaka huu wa fedha 2007/2008 ni makubwa sana, ikilinganishwa na rasilimali zilizotengwa kwa Wizara hii. Mahitaji ya Wizara kwa ajili

187 ya kutekeleza miradi inayoendelea kwa mwaka huu wa fedha ni shilingi bilioni 424.4 ikilinganishwa na kiasi cha shilingi bilioni 225.5 .

Kwa hiyo, mtaona hapa tuna upungufu wa shilingi bilioni 198. Pamoja na upungufu huo sisi wa Wizara ya Miundombinu, tunapenda kuishukuru sana Serikali kwa kile kilichoweza kupatikana kwa mwaka huu. Tunasema kila wakati maana Marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alikuwa anatufundisha kupanga ni kuchagua. Kilichopatikana tumeweza kugawana kidogo kidogo kama inavyoonekana. Kama mlivyosema karibu wote mliochangia, usafiri wa barabara ndiyo tegemeo kubwa la wananchi kwa shughuli zao nyingi za kiuchumi na kijamii. Inakadiriwa kuwa barabara nchini hutumika kupitisha asilimia 90 ya mizigo na abiria. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, haupo ubishi kuwa barabara nzuri hupunguza muda wa kusafiri njiani kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma. Sasa hivi watu wengine wananiambia unapiga saa nne, lakini ni mwendo mbaya sana huo, nataka niwape tahadhari, saa tano ni sawa kabisa. Kumbukeni miaka 13 iliyopita hali haikuwa hivyo hata kutoka hapa kuelekea upande wa kati. Kuteremka kwenda Kusini na Kusini zaidi imekuwa ndio hoja ya Wabunge. Hakuna ubishi pia kwamba, ukitengeneza barabara zitaboreka zitapunguza gharama za uendeshaji kwa wenye magari. Pia hakuna ubishi kwamba, barabara zikiboreshwa unawahisha mali zako, mazao yako, pembejeo zako, kwenda mashambani, kwenda sokoni na kama una mgonjwa afike hospitali haraka, kama una watoto shule wawahi shule. Kwa hiyo, uharaka huu ni mzuri, lakini pia anayesafiri anapata raha huwezi kutoka hapa unafika kule mgongo umechoka. Mama watoto anakwambia hongera na safari, hapana pale atakuambia pole na safari. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa utamaduni wetu, wewe unafahamu wanaume wa Kisukuma na Wanyamwezi, jioni ikifika saa moja moja au saa mbili, tunakuwa wapole sana kwa wake zetu. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, kwa kifupi barabara nzuri ni kichocheo muhimu sana kwa ukuaji wa uchumi. Hata hivyo ili manufaa ya barabara bora ambayo Serikali inazijenga kwa gharama kubwa yawe endelevu, lazima tukubali kuendelea kuwekeza na kutenga fedha za kutosha kwenye matengenezo ya kawaida ya barabara hizi, matengenezo ya muda maalum na matengenezo ya maeneo korofi na pia matengenezo ya dharura.

Lakini kama tulivyokumbushwa na Mheshimiwa Dr. , Mbunge wa Makete, hii agenda lazima tuifanye agenda ya kudumu, haiwezekani tukasema tutafanya tu mwaka huu halafu mwaka kesho ukasema hapana. Kama tunataka barabara za nchi hii ziboreke na kuweza kuifungua nchi yetu na kufungua fursa ambazo wananchi wetu tunataka wazipate kwenye maeneo ambayo sasa hivi hawazipati, lazima tuifanye kuwa ni agenda ya kudumu. (Makofi)

Mpaka sasa mahitaji halisi ya fedha kwa ajili ya matengenezo ya barabara zilizopo, zinazidi uwezo wa Serikali. Nimewahi kusema humu Bungeni, mahitaji halisi ni kama dola za Marekani milioni 170, yaani kama bilioni 221. Uchumi wetu bado

188 unakua kwa kasi ndogo ikilinganishwa na mahitaji halisi na hasa ikikumbukwa kwamba, Watanzania tunaongezeka kwa asilimia takribani tatu kwa mwaka. Uchumi ukikua kwa kasi kubwa ndipo mapato ya ndani ya Serikali yataongezeka. Kwa maana hiyo, tutaiongezea uwezo Serikali wa kuweza kutoa huduma katika maeneo mengi ikiwemo kwenye barabara. Kwa hiyo, suala la kutunza barabara zetu sisi tunasema ni la kufa na kupona na Ilani yetu ya Uchaguzi ya CCM inatutaka tuendelee kuimarisha Mfuko wa Barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Miundombinu, inaishukuru sana Serikali kwa kuleta Bungeni hatua mpya za kuimarisha Mfuko wa Barabara. Tunalipongeza Bunge lako Tukufu kwa kuafiki mapendekezo ya Serikali ya kuongeza ushuru wa mafuta ya petroli kutoka shilingi 100 za sasa kwa lita hadi shilingi 200 kwa lita, pamoja na kuongeza ada ya mwaka ya leseni za magari kutoka shilingi 20,000 kwa mwaka kwa gari na kuwa viwango vinne kulingana na ujazo wa injini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema Mheshimiwa Waziri wa Fedha na kama sisi Wizara ya Miundombinu kupitia SUMATRA, tutahakikisha kwamba wafanyabiashara wachache ambao wanataka kujinufaisha kwa kisingizio cha ongezeko la shilingi 100 kwa lita, tutawadhibiti kweli kweli. Hakuna cha msalie Mtume kwa hilo, tumeshaswali kabla ya pale. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, uamuzi huu unaiongezea Serikali uwezo mara dufu wa kuzifanyia matengenezo barabara zetu. Uamuzi huu ni wa kujitegemea. Kama nilivyosema kwa maana barabara nzuri zitaibua kilimo, zitaibua viwanda, zitaibua biashara na masoko na hivyo kuwezesha uchumi wa nchi yetu kukua kwa kasi kubwa.

Mheshimiwa Spika, ni vizuri Watanzania tukatambua umuhimu wa sisi wenyewe kufanya kazi kwa juhudi na maarifa, iwe katika eneo hili au maeneo mengine. Wachina wana ule msemo wao wanatukumbusha kila wakati: “Jasho jingi wakati wa amani, damu kidogo wakati wa vita.” Usemi huu una maana sana, ningelipenda tuchukue Watanzania lakini sisi twende kidogo kwa kasi maana hali hii lazima tuikabili kweli kweli ili tufungue nchi na uchumi wetu.

Mheshimiwa Spika, mtandao wa barabara hapa nchini, pamoja na mipango iliyopo, lengo lake kuu ni kuleta uwiano mzuri wa maendeleo ya barabara kwa nchi nzima na kuimarisha umoja wa taifa letu. Hivyo, una lengo la kufuta dhana ambayo imejengeka kwa baadhi yetu kwamba, yapo baadhi ya maeneo ya nchi yetu ambayo yamesahaulika. Ndiyo maana unaona katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi, mpangilio wa ahadi za CCM kwa Watanzania, una lengo la kutoa sura ya kitaifa na siyo kuona eneo moja linaelemewa, kwa maana ya barabara ambazo zinajengwa kwa kiwango cha lami. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumeshuhudia katika bajeti ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, mwaka huu fedha ambazo zimetengwa kwenda katika Mikoa yetu ni mara dufu ukilinganisha na mwaka 2006 na mwaka 2005. Ndiyo shabaha ya Serikali lakini angalia

189 sana katika maeneo ambayo tunaamini yako unaweza kusema in bracket, nyuma kidogo kimaendeleo, yamepewa rasilimali nyingi. Mimi kwa sasa hivi nimebahatika kukabidhiwa Wizara hii ya Miundombinu na ni lazima nibebe tochi hiyo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Ukiniuliza leo hii, Mheshimiwa Andrew J. Chenge hebu tupatie tu kwa muhtsari ni nini kinachoendelea, nitasema kwa furaha tu kwamba, tumeanza kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Tumeanza kuwatumikia wananchi kwa yale tuliyoahidi kuwatekelezea. (Makofi)

Sasa kwa upande wa barabara ndugu zangu niseme nimewasikia. Mheshimiwa Bakari Shamis Faki kasema statement nzuri tu lakini kuna eneo moja alipofika aliainisha zile barabara kwamba wao wangelifanya hivi bado tunaweza tukajenga barabara zile, kwanza ukiziangalia barabara zile ambazo zimeainishwa katika ibara ya 16 na 17 ya statement ya Msemaji wa Upinzani, karibu zote ni zile ambazo tunatekeleza sasa hivi. Lakini kusema kwamba tuchukue mawazo haya na mpangilio wao, naona kidogo ugumu kwa sababu naamini walikuwa na Ilani zao za Uchaguzi, sera zao zilikuwemo katika Ilani za Uchaguzi mwaka 2005. Tulipokwenda kuomba kura kwa wananchi, walizinadi kwa wananchi lakini hazikukubalika. Kwa sasa Sera za Chama cha Mapinduzi kupitia Ilani ndiyo zinang’ara na ndio maana ushindi wa Tsunami ukapatikana. (Makofi)

Nilisikitishwa sana na usemi mmoja, tarehe 19 Juni, 2007 kwamba, Serikali ya Awamu ya Nne, tangu iingie madarakani, haijajenga hata kilomita moja ya lami. Mimi sijui labda wale ambao wanasema hivyo yawezekana usiku totoro ukavaa miwani ya giza sasa utegemee nini? Ndiyo maana tumesema zimejengwa kwa kiwango cha lami kilomita 300. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, naanza kuiangalia Tanzania sasa Ukanda wa Kusini Mashariki, barabara kutoka Dar es Salaam - Kibiti - Ikwiriri mpaka Daraja la Mkapa, tumefanyakazi. Kuna sehemu moja imebaki lakini kutoka Ndundu - Somanga. Narudia ahadi ambayo Serikali iliisema humu Bungeni tarehe 19 Juni, 2007 tumepokea zabuni kutoka kwa wale ambao wameitikia wito, kwa hiyo, sasa hivi zoezi la kuzifanyia tathmini linaendelea. Tunahakikisha tutasaini mkataba na mkandarasi huyo mapema mwezi wa nane. Kwa mpangilio wetu, tunapenda sana barabara hii iwe imekamilika kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2010. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sehemu ya Somanga wote tunajua mpaka Nangurukuru ni lami, kutoka Nangurukuru kwenda Mbwekuru kazi inaendelea na itakamilika mwaka huu. Mbwenkuru - Lindi - Mingoyo, kazi ya uhakika inaendelea, itakamilika mwishoni mwa mwaka huu. Hayo ndiyo maendeleo kwa Mkoa wa Lindi na Mtwara, maendeleo ya matumaini. (Makofi)

Niliekee upande wa Mtwara na Ruvuma, sasa hivi sehemu ya kutoka Masasi - Kamangaka tumeshasaini mkataba, usanifu wa kina itajengwa kwa kiwango cha lami kwa msaada wa Serikali ya Japan. Mangaka - Lumesule kwenda Tunduru, Benki ya Maendeleo ya Afrika na Serikali za Japan, wamekubali kufanya usanifu wa kina na kuijenga kwa kiwango cha lami. Kutoka Tunduru - Matemanga mpaka Songea sasa hivi yupo mhandisi mshauri ambaye anafanya usanifu wa kina na kutoka Songea kwenda

190 Peramiho Junction - Mbinga - Mbamba Bay nayo inafanyiwa usanifu wa kina ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Tumeomba Serikali ya Marekani na imekubali kutusaidia na wametukaribisha. Serikali imekaribishwa na Serikali ya Marekani kwenda kuanza majadiliano ya kimkataba mwezi huu na kuwa very specific tarehe 31 Julai, 2007 kwenda Washington. Ningelikuwa na nafasi, ningeliongoza ujumbe huu mimi mwenyewe. Lakini najua Dr. Bukuku na watalaam wengine wapo. Kwa hiyo, tunafanya kitu cha uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niunganishe tu kwa sababu fedha ya MCC pia itahusisha barabara ya Tanga - Horohoro. Lakini kubwa zaidi ni kwamba, tumeelewana na wenzetu wa Kenya kwamba, tupate fedha kutoka hii facility ya Benki ya Maendeleo ya Afrika, inaitwa International Financing Window, ambayo masharti yake ni kuunganisha nchi moja na nyingine, tuzipate fedha hizo. Sasa tumekubaliana kwamba, wao wataomba sehemu ya Lungalunga - Mombasa mpaka Malindi na sisi tutaomba kuipata connectivity tunayoitaka tuiombee kuanzia Bagamoyo - Pangani - Tanga, jiji linagota namna hii. (Makofi)

Sasa hivi tunafanya usanifu wa kina kwa barabara ya Bagamoyo - Msata. Lakini pia mnajua kupitia bajeti hii, sehemu ya Chalinze - Segela - Tanga kuna sehemu moja kilomita 30, Serikali ya Denmark kupitia Danida, wanatusaidia kwa mwaka huu ikarabatiwe iwe katika hali nzuri. Kwa juu zaidi mtaona tunakusudia kufanyakazi kwa uhakika kwa sehemu ya Korogwe - Makumbara - Same. Lakini kwa juu tunajua tunafanya kazi ya uhakika maeneo ya kuanzia Maranga - Tarekea - Longai - Kamwanga na sasa tunafanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa sehemu ya Kamwanga - Ngarenairobi unakuja mpaka Sanya Juu, unakuja mpaka hapa Bomang’ombe. Nikiendelea huko huko sasa hivi tunafanya upembezi yakinifu kwa barabara za Mto wa Mbu, Loliondo uende mpaka Mugumu, uende mpaka Nata na kama alivyosema Naibu Waziri, sehemu ya pale kutoka Bunda mpaka Nyamuswa tutaiunganisha wakati wa kufanya usanifu wa kina. Tunafanya upembezi yakinifu lakini usanifu wa kina barabara kutoka Mwigumbi - Maswa - Bariadi - Safiwi - Mukula - Lamadi ili hatimaye ijengwe kwa kiwango cha lami. Vilevile kwa barabara ya Kolandoto - Lalago - Maswa - Lalago - Mwanuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikija hapa sote tunaona hali ilivyo, tumefanya kuweka tabaka jipya kutoka Morogoro mpaka Dodoma, tunaendelea na kazi kutoka hapa Dodoma kwenda Manyoni. Kazi hiyo itakamilika Desemba, Konoike anafanya kazi vizuri. Sehemu ya kutoka Singida mpaka Izuna, tumeelewana na mkandarasi yule kwamba aishie pale Isuna na atakamilisha barabara hiyo mwaka huu mwezi wa nane au tisa barabara yote sehemu hiyo itakuwa tayari na sisi tumeitisha tender kwa sehemu ya Isuna kuja Manyoni na tender hiyo tunataka tumpate mkandarasi mwezi ujao. Tunaendelea na kazi hiyo. (Makofi)

Kwa barabara ya kutoka Manyoni - Itigi - Tabora - Urambo - Kaliua - Nguruka - Mto Malagarasi, habari njema ni kwamba, Serikali ya Abudhabi imetuletea taarifa kwamba, timu yao inakuja mwezi huu kufanya tathmini ya barabara hiyo na barabara hiyo kama unavyofahamu tuliiombea sehemu yote. Tumefanikiwa kwa jitihada za

191 Mheshimiwa Rais, kupata fedha kwa Daraja la Malagarasi. Tunaishukuru sana Serikali ya Korea Kusini na jitihada za Mheshimiwa Rais. Lakini pia inakwenda mpaka Kigoma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, maeneo yote hayo, usanifu wa kina umeshakamilika. Sehemu ambayo tunaifanyia usanifu wa kina mwaka huu ni hii ya kutoka Ilunde - Uvinza - Kidahwe - Kigoma. Ndiyo maana mmeona kwenye hotuba yetu, kuna sehemu moja tunakamilisha usanifu mwezi wa nane mwaka huu lakini tunakusudia kuanza ujenzi wa barabara ya lami kuanzia sehemu ya Kigoma, Kidahwe kuja Uvinza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, siishii hapo, mmeona tunajenga kwenye connectivity tunaunganisha nchi yetu na nchi jirani ya Burundi - Manyovu - Mwandiga. Lakini pia mnaona sehemu ya barabara ya kutoka Isaka kwenda Lusahunga, sasa hivi haiko katika hali nzuri, ndiyo maana sasa hivi tunafanya usanifu wa kina ili mwaka ujao tuiombee fedha kuijenga tena kwa kiwango cha lami. Mkandarasi yupo sasa hivi kutoka Lusahunga kuelekea Kagoma. Mheshimiwa Wilson M. Masilingi, nimemsikia hapa asubuhi na tumefanya uamuzi makusudi sasa anajenga camp mbili; sehemu moja aanzie kutoka Biharamulo kwenda Lusahunga na nyingine kutoka Kagoma kuja mpaka Biharamulo, kazi ya uhakika. Kamiorwa, Chato, Buzarayombo, Bwanga, Geita, Sengerema, Usagara, ndiyo kazi ya uhakika tunataka kuifanya mwaka huu kwa kiwango cha lami. (Makofi)

Sehemu ya Nyanguge mpaka Musoma na Kisesa by pass mpaka Usagara katika mwaka huu tunaifanyia usanifu wa kina ili tuje tuiombee fedha mwaka ujao kujengwa kwa kiwango cha lami. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niingie kidogo Kigoma kwa sababu Kigoma tunaiona kwenye activity yake. Kuiunganisha Kigoma na mikoa ya jirani, tuna mpango wa kuijenga barabara ya kutoka Kigoma - Kanyani - Kasulu - Kibondo - Kakonko - Nyakanazi, kwa kiwango cha lami. Hivi sasa sehemu hiyo kutoka Kigoma kwenda Nyakanazi tunaifanyia usanifu wa kina. Lakini lazima tuunganishe Mkoa wa Kigoma si tu na Tabora na mikoa ya jirani ya Kagera, Shinyanga, Mwanza na Dar es Salaam, lakini pia na Rukwa. Sasa hivi kwa Mkoa wa Rukwa tunaelewa matatizo yaliyopo, kubwa ni hili la usafiri. Tunao mpango sasa hivi na Mheshimiwa Paul P. Kimiti amelisemea kwa nguvu zake zote, kuhusu suala hili. Sasa hivi kipande cha kutoka Tunduma mpaka Laela kimekamilika. (Makofi)

Kutoka Laela - Kaengesa - Sumbawanga mwezi wa tisa tunakamilisha usanifu wa kina. Kutoka Sumbawanga kuja Mpanda hapa lazima nieleze kidogo. Tunakusudia Wilaya ya Nkasi, barabara hii ya lami ambayo nayo sehemu ya Tunduma mpaka Sumbawanga tumeiombea fedha za Serikali ya Marekani za MCC. Kwa hiyo, matumaini makubwa yapo katika eneo hili. Lakini tunasema barabara hiyo ikitoka Sumbawanga, inaambaa inapita maeneo ya Mkundi, inaenda Chala, Chala ikate sasa kwenda Namanyere, ikiinga Namanyere ni lami inaambaa kurudi mpaka Paramawe. Inatoka Paramawe inaenda Lyazumbi, Lyazumbi mpaka Chizi, Chizi inaenda Kibaoni, Kibaoni mpaka Sitalike. Tumeamua ipite kule makusudi, kwa sababu sehemu ya Chizi Kibaoni

192 tumefika juzi na Mheshimiwa Rais, watu ni wengi na shughuli za uchumi ni kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna ndugu zangu Wasukuma na Wanyamwezi wengi sana ukanda huo. Lakini wakati tunasubiri hii lami, ndiyo Serikali ikasema kwa Mkoa wa Rukwa, tufanye kitu kingine kama tunavyofanya sasa kwa Mkoa wa Mwanza na Tanga, kwa Mradi wa World Bank wa majaribio unatengeneza barabara, unaisimamia kwa kipindi cha miaka mitano. Sasa tunasema wana kilomita karibu 364 ambazo zitasimamiwa kwa karibu na sehemu hiyo inahusu sehemu ya Mtendo mpaka Muze, halafu unatoka pale unaenda Chala mpaka Namanyere, unaenda mpaka Katondongoro, unaenda Kirondo, unaenda Kipili. Lazima tuzitengeze hizi, lakini bahati nzuri Serikali ya Denmark hawa marafiki zetu hawa, wanatusaidia pia kuitengeneza sehemu ya barabara inayotoka Muze kwenda Kiliyamatundu kwa Mheshimiwa Dr. Chrisant M. Mzindakaya. Lakini pia kwa Mheshimiwa Abdallah S. Sumry, ile sehemu ya kutoka Kagwila kwenda Karema, sasa hivi inatengenezwa kweli kweli, kwa shilingi bilioni moja na laki nne. Lakini pia tumetambua barabara ya kutoka Sumbawanga kwenda Mpanda, lazima tuisimamie kwa karibu nayo imo katika Mpango huu wa PMMR. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sehemu ya Mpanda - Kagwila - Kibo - Mishamo - Uvinza, ndiyo sasa tuko katika mpango. Sumbawanga - Mpanda, tunafanya usanifu wa kina hivi sasa. Sehemu ya Mpanda - Uvinza - Kanyani, tunaifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa awali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimeona niangaze nipige darubini lakini lazima niseme mambo mawili pia: Sehemu ya Mbeya - Makongorosi, ambayo ni barabara yetu muhimu sana ile tunaiita T8, hivi sasa tumepata fedha kwa kilomita 36 Mbeya - Lwanjilo ijengwe, kwa kiwango cha lami na mkandarasi atapewa contract yake wakati wowote kuanzia sasa. Daraja la Uhuru linaendelea kujengwa vizuri kweli pale Mtambaswala. Barabara kutoka Mangaka kwenda mpaka kwenye daraja nayo tunaifanyia usanifu wa kina ili tuijenge kwa kiwango cha lami. (Makofi)

Barabara ya Sam Nujoma pale mnaona kazi inayoendelea. Barabara ya Kilwa mnaona kazi inayoendelea. Daraja la Ruvu mnaona kazi inayoendelea. Kwa hiyo, kwa kifupi nimalizie, nilikuwa nakuja hapa sasa. (Kicheko)

Arusha - Minjingu sasa hivi tumekamilisha usanifu wa kina. Sehemu ya Singida - Babati - Minjingu, tumekamilisha usanifu wa kina na itajengwa kwa kiwango cha lami kuanzia mwaka huu wa fedha. (Makofi)

Sehemu ya Babati - Dodoma - Iringa kupitia Dodoma, kwa msaada wa Serikali ya Norway kupitia Mfuko wa Nordic Development Fund, wamekubali kufanya usanifu wa kina kwa sehemu yote hii. Sehemu mbili hizi kutoka Babati mpaka Dodoma na Dodoma mpaka Iringa, tutakamilisha kuweka saini mkataba mwezi huu wa saba. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nina mengi lakini muda wangu ndiyo hivyo, ilinibidi niyaseme haya kwa sababu mimi huwa sipendi ile longo longo. Naelewa kabisa

193 Mheshimiwa Waziri Mkuu, alipomshauri Mheshimiwa Rais, walisema sikuja kucheza mpira hapa. Napenda sana mpira, lakini nimekuja kufanya kazi ya kuwatumikia Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Reli ya Kati, hatukupata muda, lakini niseme kwa ufupi tu. Tumeshawekeana Mkataba na Kampuni ya RITES ya India. Wale ambao mnaitembelea sana India, mnaifahamu hii kampuni ni kubwa sana, hata adui yako kama humpendi katika hali hii, mpe haki yake. (Makofi)

Ni kweli tuna leseni hii itakuwa ya miaka 25. Mheshimiwa Ibrahim M. Sanya, aliuliza kuna nafasi gani ya kuangalia Mkataba huo? Mkataba huo una njia za kutokea, kila kipindi cha miaka mitano, lazima tuketi kitako na kufanya mapitio kupima umetekeleza hiki au haukutekeleza. (Makofi)

Niunganishe hapo hapo na upande wa Kampuni ya TTCL, ambayo sasa hivi inaongozwa na Kampuni ya SASCATEL. SASCATEL jamani angalieni kwenye internet ni kampuni inayomilikiwa asilimia 100 na Serikali ya Jimbo la Sascachuen kule Canada. Kampuni hii inafahamika sana kwenye maeneo haya, lakini wamekuja kufanya biashara. Kwa hiyo, Mkataba wao una vigezo hivyo hivyo, bench marks hizo kupima malipo yako yamewekewa malengo na malengo makubwa ni new products ambazo watatuanzishia. Lingine kubwa ni kuwa-train vijana wetu ili watakapomaliza kipindi chao, Kampuni yetu iweze kutoa ushindani wa hali ya juu. (Makofi)

Kwa hili hatutafanya mzaha. Mimi naomba Watanzania watusaidie, waliomo TTCL wawaunge mkono hawa meneja wapya kwa faida ili kampuni hii iweze kuimarika na sisi wengine tuendelee kupata ajira, lakini pia kubwa zaidi ichangie katika uchumi wa Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu ATL nisingelipenda niseme sana, Naibu Waziri amekwishasema. Lakini mtu mzima akikuambia tupeni nafasi, wewe mpe nafasi. Ndiyo maana sisi tumeamua tuyafanye mambo yetu makubwa kimya kimya. (Makofi)

Kila hatua tunaichukua lakini tunaipima sana na tunaporidhika ndipo tunachukua hatua nyingine. Tunataka ninyi Watanzania mje mshuhudie, mnaona ndege hizi zinakuja na colours zake, logo hiyo ya Twiga muulize zimetoka wapi hizo? (Makofi)

Namshukuru sana Mheshimiwa Rais, kwa kumteua Ndugu David Mataka, kuongoza Air Tanzania katika kipindi hiki kigumu. Sote tunafahamu uwezo wake. Lakini pia Balozi Mustafa Nyang’anyi, tunajua uwezo wake, amekuwa Waziri mzoefu hapa na Balozi mzoefu. Tunajua watatupeleka mbali, lakini pia wafanyakazi wote wa Air Tanzania jamani morale iko juu sasa. (Makofi)

Serikali itafanya kila lililo ndani ya uwezo wake, kuhakikisha kwamba, Air Tanzania haikwami. Hatua ambayo tunaifanya ni kusafisha mizania za Air Tanzania ili iweze kukopesheka. (Makofi)

194 Mheshimiwa Spika, kwa muda uliobaki, nitajitahidi kwa haraka kama nitaweza. Kama kawaida yetu sisi tutayaeleza yote haya kwa maandishi ili muyapate kwa uhakika. Lakini michango jamani ni mizuri tu. Mheshimiwa Dr. Charles O. Mlingwa, Mheshimiwa Kassim M. Mwandoro, umenisikia PM Mara inakuja, imechelewa Tanga, lakini early next year PM Mara inakuja kwako na Mabukweni mpaka Mombo Mtoni kilomita 62.3. (Makofi)

Nimeelezea Barabara ya Horohoro - Tanga, Mheshimiwa Kassim M. Mwandoro, nimeelezea jamani nimesikia hii lugha. Sifurahishwi, labda tupate nafasi twende tukatembelee barabara ya kutoka Singida - Iguguno - Sekenke - Shelui. Jamani ile itamalizika kwa uhakika Februari, 2008.

Yale madaraja pale Sekenke, madaraja sita katika span, muda mfupi wa kilometa moja, madaraja ya uhakika kweli, engineering feet jamani tusiache mambo, kuponda ponda fikeni mkajionee. Ninaposema hivi nasema ule wimbo wetu wa miaka ya 60. Wewe binti acha kupiga mayowe acha watu waje waone wenyewe. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, pale Tabora kwa Spika pale kuelekea Urambo, kweli ndiyo, lakini ni katika mpango huu huu. Kwa kutambua Kiongozi wetu mzito, tumesema angalau tulazimishe kidogo kilometa tatu za lami pale. (Kicheko/Makofi)

Lakini vilevile nimesikia kilio cha Mheshimiwa Dr. Harrison G. Mwakyembe, nimemwambia Naibu Waziri. Mheshimiwa Waziri amefika pale amejionea. Lakini yeye alifika wakati kidogo maji yalikuwa yako chini sana na kweli mimi alichokisema Mheshimiwa Dr. Harrison G. Mwakyembe ni kweli ile barua nimeijibu mimi mwenyewe, nikaweka na saini yangu. Lakini tumeshauriana leo ofisini, kweli kuna maeneo mengine Mheshimiwa Spika na Mheshimiwa Waziri Mkuu, lazima tukubali kufanya interventions kama Serikali Kuu. Kwa hiyo, eneo hili tutaliangalia kwa moyo wa huruma sana. (Makofi)

Kwa mama yangu na shemeji yangu Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, zile kilomita siyo nane ni kilometa 9.6, taarifa niliyoletewa ni barabara ya Halmashauri ya Wilaya ya Same. Lakini kwa hali ilivyo hata engineer wetu wa TANROAD wa Mkoa amesema, Mheshimiwa Waziri kwa hali hii ni kuwadanganya wananchi. Mkisema mnaiachia Halmashauri, haitaweza. Kwa hiyo, nayo tumesema acha tuone uwezekano ni nini, tunaweza tukafanya kusaidia. Tuangalie uwezekano wa kusaidia, lakini tusisahau tunaopita barabara ya kutoka Nzega kwenda Tinde - Isaka - Shinyanga - Ilula, ni lami ya uhakika na itakabidhiwa kipindi chochote kuanzia sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jamani najua siasa za huko, lakini yale ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri ameyasema, yamesemwa vizuri tu. Tabora - Ipole - Rungwa, Ipole - Inyonga - Mpanda, Makongorosi - Rungwa, Itigi - Mkiwa ile loop ya kutoka Itigi kwenda Mkiwa. Sasa kwa upande wa Tabora - Ipole - Rungwa zimetengwa pesa shilingi bilioni moja na zaidi, haijapata kutokea. (Makofi)

195 Ipole - Inyonga - Mpanda actually, mdogo wangu Mheshimiwa Said J. Nkumba, ndiyo ilianzia hapa. Alipoona pesa za Ipole - Inyonga - Mpanda akaniambia Mheshimiwa Andrew J. Chenge, kaka yangu, hivi kwa sababu kule ni kwa fulani, nikasema hapana. Sisi hatufanyi hivyo kwa sababu kule ni kwa Waziri. Anatoka Mpanda, hapana. Hii ni trunk road na tuna mpango kusema kweli kama nilivyoeleza kwenye Kamati ya Miundombinu, ni vizuri kwa barabara ndefu kama hii tuje na mpango mzuri zaidi wa kusimamia na kutengeneza kuliko hii ya sasa ya kidogo kidogo. Namshukuru sana Mheshimiwa Dr. Milton M. Mahanga, maana ndiyo mawazo yake hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Juma H. Killimbah, nimejibu mambo ya Manyoni, Singida. Mheshimiwa Jenista J. Mhagama yale ya kwako yanakwenda vizuri. Kile kidogo kilichopo mnashukuru na mimi naamini Mwenyekiti wetu mzuri tu, anashukuru kwa hayo mazuri yanayofanyika. Mheshimiwa Aggrey D. J. Mwanri, tumesema ya kwako tunatambua mchango wako nzuri.

Mheshimiwa Stephen J. Galinoma, umenisikia kwa uhakika na wananchi wa Kalenga wamesikia kwamba, tunataka kufanya barabara hii ijengwe kwa kiwango cha lami kwa sababu inaunganisha nchi jirani ya Zambia lakini na nchi jirani ya Kenya.

Mheshimiwa Jacob D. Shibiliti, hili la jumla limejitokeza sana. Suala la kupandisha barabara kutoka ngazi moja kwenda nyingine, linasubiri sheria hii mpya barabara ambayo tunasubiri ridhaa ya Mheshimiwa Rais aiwekee saini.

Mimi ningelipenda nimalizie kwa kuwashukuruni sana Waheshimiwa Wabunge, kwa kutuunga mkono. Kulikuwa na clarification iliombwa kuhusiana na Mtendaji wa TANROADS.

Mheshimiwa Spika, na Bunge lako Tukufu na Watanzania, nataka niwahakikishie kwamba, Serikali haikufanya kazi ya kukurupuka katika kumleta huyo Mtendaji Mkuu wa TANROAD, Bwana Ephraim Mrema. Ndiyo maana hata donors hamjawasikia wakilalamika au kusema ni nini kwa sababu wanamfahamu, ameshafanya nao kazi zaidi ya miaka 20. Changamoto tuliyonayo Wizara ya Miundombinu na TANROADS ni kuhakikisha kwamba, hii rasilimali inayotolewa na Serikali na Watanzania kwa jasho, kweli inasimamiwa vizuri na barabara zinazotengenezwa zionekane na zile zinazojengwa iwe kwa nguvu yetu sisi wenyewe au kwa kushirikiana na washirika wetu wa maendeleo, kweli zinajengwa kwa ubora unaokubalika. (Makofi)

Naelewa kwa upande wa TAMISEMI, wakishajenga uwezo mkubwa, kwa upande wa Mainjinia maana kule kuna hatari sana ya rasilimali hizi kutumika ovyo. Lakini kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, tutaona ni jinsi gani Wizara yetu tutakavyoweza kusaidia ili angalau tuanze kujenga uwezo ndani ya Halmashauri zetu.

196 Mheshimiwa Spika, mke wangu hayupo hapa kwa sababu alikuwa Bariadi kwenye Tamasha la Akina Mama Lambina, Sabasaba. Napenda nichukue nafasi hii, kuishukuru sana familia yangu kwa kunipa nguvu. Lakini pia nawashukuru sana akina mama wa Bariadi hasa Kundi la Wagalu waliochukua ushindi juzi. Naomba rafiki zangu Wagika, akiwepo Mama Mwanahamisi wa Masewa pale, asikate tamaa safari hii maana kuna kesho. Zawadi yao inakuja kupitia kwa Mbunge wao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema yote haya, nadhani nimekandamiza vya kutosha.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja. (Makofi)

(Hoja iliamuliwa na Kuafikiwa)

KAMATI YA MATUMIZI

MATUMIZI YA KAWAIDA

Fungu 98 – Wizara ya Miundombinu

Kifungu 1001 – Administration and General ...... Sh. 8,365,317,400.00

MWENYEKITI: Basi tutawaorodhesha, Mheshimiwa Hamad Rashid Mohamed, Mheshimiwa Dr. Wilbroad P. Slaa, Mheshimiwa John M. Cheyo, Mheshimiwa Halima Mdee, Mheshimiwa Chacha Z. Wangwe, Mheshimiwa Mariam S. Mfaki, Mheshimiwa Siraju J. Kaboyonga, Mheshimiwa Dr. Zainab A. Gama, Mheshimiwa Ezekiel M. Maige, Mheshimiwa Charles M. Kajege, Mheshimiwa Vedastusi M. Manyinyi, Mheshimiwa Ruth B. Msafiri, Mheshimiwa Sameer I. Lotto, Mheshimiwa George M. Lubeleje, Mheshimiwa Lucas L. Selelii, Mheshimiwa Castor R. Ligallama na Mheshimiwa Eng. Stella M. Manyanya; umesimama? (Kicheko/Makofi)

Naomba Waheshimiwa Wabunge, nikumbushe kwa mujibu wa Kanuni ya 81(ii)(b), maana ya Kamati ya Matumizi ni kupata ufafanuzi au maelezo. Ili mradi maelezo au ufafanuzi ni sahihi, sitamvumilia Mheshimiwa Mbunge ambaye atadai kifanyike tu. Mathalani, ukiambiwa kwamba barabara hii haikutengewa fedha mwaka huu ila itafikiriwa mwaka ujao, huo ndiyo ufafanuzi. Uking’ang’ania kwamba lazima ijengwe nitakukatiza hapo hapo. Tuendelee.

MHE. HAMAD RASHID MOHAMED: Asante sana Mheshimiwa Mwenyekiti. Vote 98, Programu Namba 10, Sub-Vote 1001, Kifungu 250100 - Mshahara wa Waziri, suala la Sera.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati nikichangia kwa maandishi nilikuwa nimemwuliza Mheshimiwa Waziri, kama wakati Air Tanzania inabinafsishwa Serikali ilipata mapato na wakati ilipoichukua tena Serikali ilitumia fedha. Nilichotaka kujua

197 katika hiyo sera ya kuuza na kununua, Serikali ilitumia kiasi gani na ilipoteza kiasi gani? Bahati mbaya Waziri hakujibu, naomba majibu.

WAZIRI WA MIUNDOMBINU: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumjibu Mheshimiwa Hamad Rashid Mohamed kama ifuatavyo: Ufafanuzi ambao tunautoa kwa Serikali ni kwamba, wakati tunaingia kwenye ubia na South African Airways, hatukuwa tumewekeana kwamba kuna mizani huku ya faida na mizani ya hasara. Tuliamini tumeingia katika ubia ambao utaifufua Air Tanzania iweze kuwa a profitable company, lakini siku nilipokwenda tuliona huko hatufiki ndio tukachukua uamuzi tuliouchukua. Tulichokifanya nimeeleza kwenye hotuba yangu kwamba, tumenunua hisa zetu ambazo walikuwa wamelipia wao wenyewe dola milioni 20 kama mtakumbuka. Sisi tumenunua hisa asilimia 49 kwenye kampuni yetu ambazo zilikuwa za kwao kwa a nominal figure ya dola moja ya Kimarekani.

MHE. DR. WILBROD P. SLAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na naomba nitumie vote 98, program 10, subvote 1001 250100 kuuliza swali la sera.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati ninachangia kwa maandishi, niliomba ufafanuzi kuhusu barabara inayojulikana kama Oldeani Junction - Kandeti - Makala - Lalago, ambayo miaka iliyopita ilikuwepo kwenye utaratibu na ikafanyiwa usanifu lakini kuanzia mwaka wa 2005 haikuonekana tena kwenye vitabu vya Serikali. Nilitaka kujua ni kitu gani kimetokea na kama hiyo barabara ambayo hata beacons ziliwekwa angalau katika maeneo ninayojua kwa upande wote wa Karatu kwa njia panda Kandeti - Jiobaji - Matala zile beacons ziko mpaka leo na kadri ya taarifa tulizonazo katika bajeti ya mwaka 2002 tulitumia zaidi ya shilingi milioni 200 kwa ajili ya usanifu. Sasa hii barabara kwa kuwa imepotea na tumeshatumia fedha, napenda nipate ufafanuzi je, imeachwa kwa muda tu? Nakumbuka niliuliza swali la Bunge na nikajibiwa ndani ya Bunge kwamba, kilichobaki ni fedha, zinatafutwa kwa wafadhili. Sasa pamoja na hivyo nataka kujua utaratibu huo wa kutafuta fedha kwa wafadhili bado unaendelea au umefutika moja kwa moja kwa vile hauko kwenye Kitabu cha Waziri?

WAZIRI WA MIUNDOMBINU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kimtandao wa barabara ambazo zipo, hii barabara ipo kwenye vitabu vyetu, ipo katika schedule ya Sheria ya Barabara. Kwa hiyo, siyo kwamba barabara imetoweka, barabara ipo na ndio maana katika mwaka huu wa fedha, sehemu kutoka Karatu Junction - Mang’ola - Matola, utaona kwenye vitabu zipo shilingi milioni 70 za matengenezo lakini barabara hii inakupeleka mpaka Mkoa wa Shinyanga. Ndio maana upande wa Mkoa wa Shinyanga, kuna hizi fedha zimetengwa shilingi milioni 200 kufanya upembuzi yakinifu barabara ya kutoka Ngolandoto - Lalago - Mwanuzi. Lengo la Serikali ni kwamba, kadri pesa inavyopatikana, barabara hii tutaendelea kuitengeneza. Lakini kipaumbele kama nilivyosema, mimi nabeba Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi na mkakati wa kutekeleza ndio barabara ambazo zimepewa kipaumbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kuna ahadi ambazo viongozi wetu aidha walizitoa wakati wa kampeni, nazo zinaingizwa katika utaratibu huo na nyingine ambazo wanazitoa wanapoenda kutembelea maeneo, kwa mfano, Rais akienda kutembelea Karatu

198 au upande wa Mkoa wa Shinyanga, anaweza akatoa ahadi, ndio tunasema tunazitafutia mkakati wa kuzitekeleza hatua kwa hatua kwa kutegemea upatikanaji wa fedha.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, vote 98, program 10, subvotes 1001 - Mshahara wa Waziri na ni suala la kisera.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Mheshimiwa Waziri akijibu hoja, alizungumzia kuhusiana na Mkataba baina ya Serikali na RITES. Kuhusiana na suala zima la TRC, vilevile nakumbuka mapema mwisho wa mwezi wa sita wakati Mheshimiwa Maua Abeid Daftari, akijibu swali la Mheshimiwa Siraju J. Kaboyonga, alisema kwamba TRC kutokana na mwekezaji mpya akianza kutakuwa kuna punguzo la wafanyakazi 2,931. Sasa katika mwaka wa fedha 2006/2007, walitenga shilingi bilioni 50 kwa madhumuni ya kuwalipa wale wafanyakazi ambao watakuwa wamepunguzwa kazi, sasa hivi sijaziona katika mwaka huu wa fedha. Nataka kujua kama zile shilingi bilioni 50 ambazo hata Mheshimiwa Maua Abeid Daftari alizitaja hapa Bungeni, ziko kwenye process za kuwalipa wale watu maslahi yao au zimeenda wapi na labda kama zilitumiwa katika matumizi mengine sasa hivi mbona hazipo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri aniambie kuna mpango gani kwa hawa wafanyakazi 2,931, ambao watapoteza ajira zao pale ambapo RITES itaanza kufanya kazi? Nashukuru.

WAZIRI WA MIUNDOMBINU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge kwamba, katika bajeti ya 2006/2007 tulikuwa tumetenga shilingi bilioni 50, miongoni mwa mambo mengine ni kulipia mafao ya wafanyakazi ambao ajira yao haitaendelezwa katika ajira mpya na niseme kabisa kwamba, hatuna tatizo na kulipa mafao ya wafanyakazi watakaopunguzwa na mwajiri mpya wa Kampuni ya Tanzania Railways Limited, kwa sababu fedha hizo Serikali ilikuwa imezihifadhi kwa madhumuni hayo hayo. Haingekuwa busara kujiumiza sisi wenyewe na ndio maana huzioni katika kifungu chochote cha bajeti yetu. Vilevile kwa upande wa mchango wa Serikali katika hisa zake, nazo ni hivyo hivyo, lakini fedha hizi zipo kwa hiyo, asiwe na wasiwasi wowote. Tusingependa tujiumize sisi katika operations hizo lakini sehemu pia ya fedha hiyo tulikuwa tumeitumia kuendesha TRC kwa maana ya kuinunulia mafuta.

MHE. JOHN M. CHEYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Vote 98, programu ya 10, subvote 1001 - Mshahara wa Waziri na ndugu yangu sitachukua senti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka kusema kwamba, kazi ya barabara ni kubwa na barabara nyingi zinajengwa. Mimi sijali kama ni CCM inajenga au mtu yeyote, maana barabara haina chama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, niliguswa sana na hotuba nzuri ya Mheshimiwa Waziri, ndugu yangu, page 21 alizungumzia kwamba, wametengeneza mkakati wa kuweza kuwekeza katika uchukuzi na mkakati huo utachukua shilingi bilioni tano za Kimarekani na kwamba, utekelezaji utaanza mwaka huu 2007/2008. Hotuba

199 ilinipa matumaini makubwa sana, ukigawanya katika miaka mitano ndio kusema unahitaji kama shuilingi bilioni 1.3 kwa kila mwaka. Mwaka huu Mheshimiwa Waziri, amepata hela za maendeleo karibu shilingi bilioni 478, ambayo ni kama theluthi moja ya ule mkakati ambao unapaswa kuanzwa mwaka 2007/2008.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka kufahamu, ana utaratibu gani ambao anaweza ku-share akatupa matumaini kwamba, utaratibu huu kweli tukipata kuwekeza bilioni tano za Kimarekani katika uchukuzi, nchi hii itapaa kweli. Ninakubaliana na Waziri Mkuu wa mara ya kwanza. Kwa hiyo, napenda kupata hayo matumaini; ni nini atakachofanya, najua kuna wengine wamezungumzia juu ya long term loans na nini. Napenda nipate faraja kutoka kwa ndugu yangu kwamba, atafanya nini ili mwaka kesho asije tena na bajeti ya one third ya mkakati wake, yaani theluthi moja ya makakati wake, maana akiendelea hivyo katika miaka mitano, hatakuwa amefikia lengo ambalo linaonekana ni zuri sana kwa nchi yetu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba maelezo.

WAZIRI WA MIUNDOMBINU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Napenda kumjibu ndugu yangu, Mheshimiwa John M .Cheyo kama ifuatavyo: Kwa kufafanua tu, huo mkakati ambao tunauita Tanzania Transport Sector Investment Program ni mkakati ambao tumeuweka, tumeuandaa kwa pamoja na washiriki wetu wa maendeleo na imetuchukua muda mrefu sana kukamilisha kufika hapa tulipofika. Mkakati huu unaungwa mkono sana na hawa wenzetu lakini pia na sisi ndani ya Serikali. Tunaamini haya tunayofanya, moja ya kitu ambacho kimekuwa kinawakwaza kidogo kuweza kusema wajitokeze sana ku-support hii sekta ya usafirishaji nchini na uchukuzi katika upana wake maana hatuangalii barabara tu, barabara ni sehemu moja tu lakini pia wanaangalia reli, bandari, viwanja vya ndege na yote hayo walikuwa kidogo wanaona mbona Serikali ya Tanzania inataka na sisi sasa tuchangie katika kutengeneza mtandao wa barabara zenu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hizi ni kweli tunajenga kwa pamoja lakini tunazijenga kwa gharama kubwa sana. Kama anavyoeleza hapa mara nyingi kwa average tu kujenga kilometa moja ya barabara ya lami siyo chini ya shilingi milioni 500. Sasa tunasema jamani jengeni uwezo wa kuzihudumia hizi barabara tunazojenga na sisi tutaendelea kuwasaidia mpanue network yenu ya barabara kwa kujenga barabara nyingine. Sasa rafiki yako akikupa ushauri mzuri ukiukataa, nadhani wewe kidogo lazima una tatizo la akili. Serikali hii ina watu wazuri tu, wanaelewa, ndio tukasema maeneo yapi na sasa tumekuja la kwanza lilikuwa ni sheria mpya ya barabara, Bunge hili tumeliomba limeidhinisha.

Eneo la pili ilikuwa ni measures za kuhudumia barabara zetu hizi. Nashukuru Bunge lako Tukufu tumeliomba limekubali angalau pa kuanzia sasa lingine ni la kusimamia hizi fedha kwamba pasiwe na mahali pengi pa kuvuja vuja, sasa hilo ni la Serikali na vyombo vyake kuhakikisha kwamba, fedha hizi zinapatikana halafu zinatumika kwa shabaha iliyokusudiwa. Kwa maana hiyo, imetupatia high moral

200 authority sasa hivi, kuweza kuwaambia Serikali ya Tanzania imefanya kile kilicho ndani ya uwezo wake sasa na ninyi basi hebu onesheni cha kwenu. Ndio tunachosema na wao ni waungwana, already tumepokea simu nyingi sana baada ya Bajeti ya Serikali kupita, wiki iliyopita kwamba, Serikali ya Tanzania sasa mmeanza vizuri kwenye eneo hili, endeleeni namna hiyo. (Makofi)

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Vote 98, programu ya 10, subvote 1001, kifungu 250100 - Mshahara wa Mheshimiwa Waziri. Pamoja na maelezo yako mazuri, uzoefu wa mwaka 2006 unaonesha kwamba, barabara nyingi ziliharibika na pesa nyingi sana zilitumika kwa ajili ya kuzitengeneza upya. Lakini kwa kutambua juhudi unazozifanya, niliona nikupe habari njema kwamba, TILDO sasa hivi ina teknolojia ya kisasa kabisa ya kuweza ku-test barabara pamoja na madaraja lakini wakati unatoa majibu hukulizungumzia sasa …

MWENYEKITI: Mheshimiwa ongea na Mwenyekiti, huongei na Waziri.

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Sasa kwa misingi hiyo, nikaona ni vyema ukalizungumzia sijui kama utakuwa tayari kuweza kuitumia hiyo teknolojia ambayo …

MWENYEKITI: Bado umerudi kwa Waziri, address the Chair please. MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kufahamu kama anaweza akashirikiana na taasisi hii ili kuokoa hizi pesa zinazopotea zinazotokana contractors kufanya kazi ambayo inakuwa haijahakikiwa kwa kutumia teknolojia hii ya kisasa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

MWENYEKITI: Nina hakika hilo atalikubali na hasa ukimwongoza wewe mwenyewe mkaenda huko kuweza kufika. (Kicheko/Makofi)

MHE. LUCAS L. SELELII: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Vote 98, programu ya 10, subvote 1001, wala kaka yangu asiwe na mashaka juu ya mshahara wake, kwa kazi nzuri ambayo imefanyika kwa kweli naunga mkono hoja asilimia mia kwa mia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nipate maelezo ya kina hasa katika hii barabara ambayo tumeisema muda mrefu ya kutokea Manyoni - Itigi - Tabora kwenda Kigoma. Natambua juhudi ambazo amezieleza Mheshimiwa Waziri za kuipatia pesa kupitia Mfuko wa Abudhabi. Barabara hiyo hadi sasa kwa pande zote mbili; kwa maana ya Mkoa wa Tabora na Mkoa wa Kigoma na hata Singida yenyewe, ipo katika maeneo ya barabara ya mkoa. Katika kuzungumza hapa nilitoa wito kwamba, afadhali sasa kwa umuhimu wa barabara hii na kufungua barabara hii na hasa hususan Mkoa wa Tabora na Kigoma, iwe miongoni mwa barabara ambazo zinaitwa za Central Corridor, yaani Barabara za Kitaifa.

201 Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, ninavyotambua ningependa kusahihishwa, barabara hii imeshafanyiwa design mwaka 1998, kama miaka 10 iliyopita ni miaka mingi sana kwa hali ya sasa hivi iliyopo na matokeo ya wakati ule na sasa.

Je, Serikali itakuwa tayari kufanya tathmini ya kina hasa katika design iliyofanyika miaka 10 iliyopita, kipande cha Itigi mpaka Tabora na kipande cha Ilunde mpaka Kaliuwa? Nataka ufafanuzi, asante sana.

WAZIRI WA MIUNDOMBINU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru Mheshimiwa Lucas L. Selelii, kwa ombi lake hilo. Nianze tu kwa kusema kwamba ni kweli ukichukua sheria iliyokuwa ya barabara, ilikuwa inaoneshwa sehemu ndogo ya kuanzia Manyoni pale ndio inakuwa Trunk Road, halafu kuanzia Kigoma kule kilometa kama 30 hii yote katikati ilikuwa ni Regional Road.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kutokana na ombi la Mikoa ya Tabora, Kigoma na Singida, hili suala tumekuwa nalo Wizarani na hata sasa hivi ni kwa sababu tunasubiri idhini ya Mheshimiwa Rais ipatikane. Barabara hii kwenye ramani zetu naona inaonesha imeshapewa na namba, maana barabara kuu za nchi hii tunazitambua kwa Namba T, ukiona T maana yake ni Trunk Road na R ni Regional Road. Sasa hii imepewa namba 18 kuanzia Manyoni - Tabora - Kigoma. Kwa hiyo, pasiwepo na wasiwasi wowote kwa suala hili kwamba ni Regional Road, sheria itakapopita tu mtaiona na sisi yale ambayo tunapaswa kufanya kwa sheria ile kuiweka na kuitambua, tutafanya hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli usanifu wa kina ulifanyika mwaka 1998 kutoka Manyoni mpaka Tabora, nimeelezea hivyo hivyo lakini hata hii timu ya keshokutwa inayokuja kutoka Abudhabi Fund, moja ya information ambayo tunataka tuelewane nao ni hii kwamba, je, tunaridhika sote kwamba bado inakidhi mahitaji yetu ya sasa au tunahitaji kuiboresha kidogo na grading ya information kwa kazi hizi za kihandisi haichukui kwa sababu ile misingi imeshafanywa, economic aspect tumeshafanya, tunachoweza kukuta labda kuna watu wamevamia road reserve sasa hilo ni suala tofauti.

MWENYEKITI: Kwa hiyo, niwe na hakika tu hii barabara unaposema inatoka Tabora mpaka Kigoma, ndio inapita Urambo na Kaliuwa? (Kicheko/Makofi)

WAZIRI WA MIUNDOMBINU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuthibitishie kwamba, hiyo ndio barabara tunayoiongelea siku zote, ambayo inatoka Manyoni inaenda Itigi - Tabora - Urambo - Kaliuwa - Nguruka - Malagarasi - Ilunde - Uvinza - Kidawe - Kigoma, tunamaliza kazi. (Makofi)

MWENYEKITI: Kweli jamani huyu Waziri anafaa sasa. (Kicheko/Makofi)

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, vote 98, programu ya 10, subvote 1001.

202 Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka maelezo tu ya ufafanuzi. Jana nilipokuwa nachangia hapa, nilizungumzia sana Barabara ya Mkoa kutoka Ng’ambi - Mpwapwa - Mlali - Pandambili na katika bajeti ya 2007/2008 imetengewa shilingi milioni 75 na kuna daraja ambalo limevunjika mwaka huu mwezi wa nne wakati wa mvua. Sasa nilikuwa naulizia hizi shilingi milioni 75 zitatosha kujenga na hilo daraja; kwa sababu hii ni Barabara ya Mkoa na daraja hilo lipo Mpwapwa Mjini sasa hivi magari hayapiti? Naomba maelezo.

MWENYEKITI: Mheshimiwa George M. Lubeleje, wewe ni mzoefu, unauliza maoni kama zitatosha au unauliza ufafanuzi, kwa sababu kama ni maoni hayaruhusiwi na kanuni?

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nasikitika, jana nilikuwa mtu wa 10 kuchangia, haikutajwa hata hoja moja hapa na sikujibiwa, sasa swali langu; hizi shilingi milioni 75 ambazo zimetengwa kwa Barabara hii ya Mkoa zitajenga na hilo Daraja la Mpwapwa Mjini ambalo limevunjika wakati wa mvua? Nataka maelezo.

MWENYEKITI: Sasa umelenga.

WAZIRI WA MIUNDOMBINU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba radhi kama hakutajwa kwa maana ya kwamba, hoja yake hiyo aliyokuwa ameisemea. Kama nilivyosema, hoja ni nyingi kwa hiyo, yawezekana hatukuweza kuifikia lakini ataipata kwa maandishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kuhusiana na daraja hilo kama liliharibika wakati wa mvua hizi kubwa, tunategemea kwamba, Uongozi wa Mkoa, pamoja na TANROAD, hili wamengeliingiza katika matengenezo ya dharura lakini kama halikuja katika sura hiyo, itabidi sasa tuangalie ni jinsi gani tunavyoweza kuwasaidia. Hicho ndicho ninachoweza kukisema kwa sasa hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru.

MHE. CHACHA Z. WANGWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Kwanza kabisa, napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri, kwa capacity yake. Mheshimiwa Mwenyekiti, Vote 98, programu ya 10, subvote 1001 Basic Salaries. Mheshimiwa Waziri ana capacity kubwa sana ya kuweza kukariri data na amezungumzia barabara zote na miji yote ya Tanzania mpaka nimeshangaa. Anastahili pongezi kwa sababu alikuwa hasomi ameweza kumpita Mheshimiwa Dr. Milton M. Mahanga, ambaye huwa anasoma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika hizo zote hakuweza kutaja barabara ya Tarime, Nyamwaga kuelekea Arusha, ambayo ndio barabara tunayoitegemea pale kwa

203 ajili ya uchumi wa Tarime na sasa hivi haijawahi kutengenezwa tangu mwaka 1990 na sasa imeziba kabisa hata baiskeli hazipiti na hiyo barabara hakuitaja. Pamoja na kwamba Wilaya ya Tarime kabla sijaanza kusema, naomba kama ilivyo ada katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi, ninataka kujua ya kwamba fedha zile ambazo zinakusanywa pale Tarime kutokana na Migodi, kutokana na Mbuga za Wanyama, mpaka Samaki ni percentage gani ambayo inatumika kwa ajili ya maendeleo ya Tarime, hasa katika barabara hii na kwa nini barabara hii haikupewa hata senti moja?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kuna aina ya majibu ambayo yanaendana na Ilani ya Chama cha Mapinduzi, ambayo ninayasikia hasa kwa upande wa Mheshimiwa Dr. Milton M. Mahanga, akiwajibu Wabunge wote waliochangia, majibu yenyewe yanakuwa katika misamiati. Hili tumelizingatia, tutaangalia vigezo, feasibility study imeanza, tutatafuta pesa zaidi, usanifu wa kina unaendelea na upembuzi yakinifu. Sasa aina hiyo ya majibu natarajia kwamba katika kujibu hili suala la Barabara ya Tarime, atatumia hayo ila aniambie exactly kwamba, hiyo barabara kwa nini haijengwi? Ahsante. (Kicheko/Makofi)

MWENYEKITI: Swali nadhani ni mipango ya barabara hiyo, lakini Waheshimiwa Wabunge hatuwezi kuwafundisha Waheshimiwa Mawaziri watumie lugha gani, nadhani tunauliza kwa nia safi tu maendeleo ya barabara ambayo tunayoiulizia.

WAZIRI WA MIUNDOMBINU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijamjibu Mheshimiwa Chacha Z. Wangwe, napenda nisahishe kauli yangu kuhusiana na ombi la Mheshimiwa George M. Lubeleje. Kwenye vitabu vyetu upande wa madaraja zimetengwa shilingi 550. Nadhani sasa hapo wajenge hoja kuzipata hizo shilingi milioni 75 ili daraja hili muhimu karibu na Mpwapwa liweze kujengwa, lakini fedha imetengwa katika bajeti ya mwaka huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kuhusiana na Tarime, ni kweli Mheshimiwa Chacha Z. Wangwe, aliniandikia kuhusiana na barabara hii lakini bahati mbaya mpaka nakuja ku-windup, nilikuwa sijapata taarifa yoyote ya kuweza kusaidia. Maadamu tumelipokea, kama tumeshindwa kufanya mwaka huu wa fedha, itabidi sasa tujipange vizuri tuweze kuliangalia kwa mwaka ujao kama fedha itaruhusu.

MHE. BAKARI SHAMIS FAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Vote 98, programu ya 10, subvote 1001, item 250100 - Basic Salary.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati nawasilisha Maoni ya Kambi ya Upinzani asubuhi hapa, nilitaka kujua kwamba, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu bajeti ya mwaka 2006 alieleza kwamba, wana mipango ya kuwashirikisha Sekta Binafsi katika uwekezaji na utoaji huduma katika viwanja kama vile Mwanza, Mafia, Kigoma na kadhalika. Nataka kujua yafuatayo:-

(a) Ni kwa kiasi gani mpango huu umefanikiwa?

204 (b) Ni Makampuni gani binafsi yaliyoshirikishwa katika mpango huu na ni faida kiasi gani imepatikana kutokana na ushiriki huu wa Sekta Binafsi katika mpango huu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba maelezo, ahsante.

MWENYEKITI: Hiyo iko wapi katika mipango ya mwaka huu? Tunazungumzia ufafanuzi wa mambo halisi yaliyomo katika mipango ya Wizara hii.

MHE. BAKARI SHAMIS FAKI: Haya yalikuwa yatekelezwe katika bajeti ya mwaka jana. Sasa nataka kujua kiasi gani kimetekelezwa?

MWENYEKITI: Yalikuwa katika bajeti ya mwaka jana?

MHE. BAKARI SHAMIS FAKI: Ndiyo. MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri, sio takwimu ya percent, kiasi gani, nadhani ushiriki wa jumla tu wa sekta binafsi katika sekta hiyo.

WAZIRI WA MIUNDOMBINU: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Bakari Shamis Faki kwa kutaka kupata taarifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama sote tunavyofahamu, sekta binafsi tungependa ipate nafasi mahsusi katika kusaidia Serikali kuchangia katika juhudi za maendeleo hasa kwa upande wa miundombinu. Hilo halina ubishi na ndio maana tumejipanga kwa namna hiyo, ndio hicho tunachokifanya mwaka huu kwa viwanja vya Mwanza na Daraja la Kigamboni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba, tulipopitisha Sheria ya Barabara, tumejenga ile misingi lakini sheria hiyo inasema sasa wekeni miongozo na kanuni. Tumechelewa kidogo lakini nimehakikishiwa na watu wa World Bank kwamba, yule mtaalam ambaye alikuwa ameteuliwa kwa kazi hiyo, atakamilisha ripoti yake mwezi huu na ataikabidhi Serikalini ili tuone kama mapendekezo yake yanaendana na kule tunakotaka kwenda au vipi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia sekretarieti ya Central Corridor, yenye makao makuu yake Mjini Kigali Rwanda, tulikuwa tumewaomba watufanyie kazi hii na wao tayari wanakamilisha ripoti hii ili tuje tulinganishe na yale ambayo sisi tunayaona na tunayafahamu ili sasa tuitangazie dunia kwamba sheria yetu ni hii, miongozo yetu ni hii, kanuni zetu ni hizi na miradi ambayo tunaitaka kui-package kwa utaratibu huu ni hii, wanaopenda kuja Tanzania kuwekeza na mje, karibuni. (Makofi)

MHE. SIRAJU J. KABOYONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, fungu la 98, programu ya 10, subvote 1001, item 250100 - Mshahara wa Waziri, masuala ya kisera.

La kwanza, katika mchango wangu niliomba kufahamishwa authorized capital ya Tanzania Railways Limited. Sijapata kusikia maelezo hayo. Dhamira yangu ni kufahamu

205 kwamba pamoja na mgawanyo wa asilimia 51 kwa hao wawekezaji na 49 kwa Serikali je, isingekuwa vizuri kama Serikali ingewapa wafanyakazi wa shirika la reli hisa ili kuwa na uhakika kwamba watalitumikia vizuri shirika hili? Lakini vile vile linaloambatana na hilo ni kwamba hisa hizi zimekwishalipwa yaani katika wale shareholders wamesha- subscribe into the authorized capital?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ufafanuzi wa pili ninaouhitaji ni kwamba, nilitoa rai kuwa kutokana na upungufu mkubwa wa mapato ya Serikali kwa njia ya kodi, Serikali itumie njia ya long term bonds ku-raise funds kwa ajili ya miradi ya miundombinu. Hapa sikupata msimamo wa Serikali. Naomba nipate msimamo na baada ya msimamo huo napendekeza kwamba, kwa kuwa ni rahisi kupata hizo bonds ni suala tu la Serikali kuamua Central Bank ikazitangaza zikaingia kwenye Mfuko wa Serikali. Sehemu ya bonds zitakazopatikana immediately ziende katika kuongeza fedha za barabara ya Itigi – Tabora – Urambo – Kigoma wakati tunasubiri yale marefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ufafanuzi mwingine ni kuhusu ….

MWENYEKITI: Imetosha, imetosha, ufafanuzi ni kwa masuala mawili.

MHE. SIRAJU J. KABOYONGA: Tatu.

MWENYEKITI: Hakuna ya tatu

MHE. SIRAJU J. KABOYONGA: Sio ufafanuzi ni issue.

MWENYEKITI: Hairuhusiwi. Mheshimiwa Waziri, ufafanuzi wa hayo mambo mawili kwa kifupi tu kwa sababu tumefikia muda.

WAZIRI WA MIUNDOMBINU: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumjibu Mheshimiwa Siraju J. Kaboyonga kama ifuatavyo: Wafanyakazi wa Shirika la Reli kupewa hisa, kama anavyojua yeye mwenyewe ambapo ni mzoefu, banker, suala hili unahitaji unapopewa hisa uwe na uwezo wa kuilipia. Ni wazo zuri lakini katika mfumo ambao tumeanza nao ni Serikali yenyewe, ina hisa 49 na huyo anayekuja kuendesha shughuli za reli yetu 51%.

Kwa vile ni wana hisa na ni kampuni yetu, napenda tuondokane na hii zana ya kusema kwamba, yeye analeta nini. Yeye kwa kipindi cha miaka hiyo 25 atakuwa amewekeza za kwake kama dolors milioni 283, lakini reli hii ni ya Watanzania na itaendelea kuwa hivyo na ndio maana tuna wajibu pia na hatutaiuza, tunaikodisha tu. Tukimwona hafikii viwango vya utendaji kama nilivyosema anakitoa, anaoneshwa njia.

Tunaichukua sisi wenyewe na Serikali itaamua ni nini kiwe. Lakini tunachokisema tutaendelea sisi kama Serikali kutafuta mikopo yenye masharti nafuu ili tuweze kuiboresha sana sehemu ya reli hii.

206 Tumekubaliana na yeye kwa kipindi cha miaka 25 atatengeneza ujumuisho wa urefu wa reli au kilomita 648 tu lakini mnajua reli yetu ina urefu zaidi ya hapo kwa hiyo maeneo yote lazima Serikali iendelee kugharamia yenyewe. Lakini katika maeneo ambayo tunashirikiana na yeye inabidi tunapoenda kukopa tunakopa kwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu bonds, ni ushauri mzuri na Serikali inaufanyia kazi. Sasa hivi kuna mambo mengi tunapika ndani ya Serikali lakini lengo ni kuhakikisha kwamba, tunaweza kutunisha mfuko naa kuimarisha miundombinu hasa ya barabara, reli, viwanja vya ndege na bandari.

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kanuni ya 81(6) inasema: “Zikibaki dakika kumi tu kabla ya muda wa kuahirisha Bunge kwa siku hiyo na Kamati bado haijamaliza kufikiria mafungu yote yanayohusika, Mwenyekiti atafunga mazungumzo yoyote yaliyoruhusiwa katika aya hizo za juu za kanuni hii na papo hapo atawahoji kuhusu mafungu yaliyosalia kama yapo“. Kwa hiyo, Katibu tunaingia hatua hiyo sasa.

(Kifungu Kilichotajwa hapo juu kilipitishwa na Kamati ya Matumizi bila mabadiliko yoyote)

Kif. 1002 - Finance and Accounts ...... Sh.828,967,600 Kif. 1003 - Policy and Planning …………………...... Sh.7,230,380,700 Kif. 1004 - Information Education Communication Unit …...... …...... Sh.85,140,000 Kif. 1005 - Procurement Management Unit ……..…. .... Sh.110,596,900 Kif. 2001 - Electrical and Mechanical ……………...... Sh.0 Kif. 2003 - Transport Division …….....………...... Sh.27,929,076,300 Kif. 2004 - Communication Division ………………...... Sh.348,755,900 Kif. 3001 - Supplies and Services ………………...... Sh.1,407,706,700 Kif. 5001 - Building Unit …………………………...... Sh.0 Kif. 5002 - Safety and Environment Unit …………...... Sh.219,732,900 Kif. 6001 - Trunk Roads …………………………...... Sh.0 Kif. 6002 - Road Division ……………………...... Sh.162,056,185,600 Kif. 7001 - Rural Roads ………………………...... Sh.0

(Vifungu vilivyotajwa hapo juu vilipitishwa na Kamati ya Matumizi bila mabadiliko yoyote)

MIPANGO YA MAENDELEO

Fungu 98 – Wizara ya Miundombinu

Kif. 1001 - Administration and General …………...... Sh.315,000,000 Kif. 1003 - Policy and Planning ………………...... Sh.13,858,000,000

207 Kif. 2001 - Electrical and Mechanical …………...... Sh.0 Kif. 2003 - Transport Division ………………...... Sh.33,745,600,000 Kif. 2004 - Communication Division ……………...... Sh.100,000,000 Kif. 5002 - Safety and Environment Unit …………...... Sh.1,569,000,000 Kif. 6001 - Trunk Roads ……………………………...... Sh.0 Kif. 6002 - Road Division ………………………....Sh.428,857,400,000 Kif. 7001 - Rural Roads …………………………...... Sh.0

(Vifungu vilivyotajwa hapo juu vilipitishwa na Kamati ya Matumizi bila mabadiliko yoyote)

(Bunge lilirudia)

T A A R I F A

WAZIRI WA MIUNDOMBINU: Mheshimiwa Spika, naomba kutoa taarifa kwamba, Bunge lako Tukufu limekaa kama Kamati ya Matumizi na kupitia Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Miundombinu kwa mwaka wa fedha 2007/2008, kifungu kwa kifungu na kuyapitisha bila mabadiliko. Hivyo, naomba kutoa hoja kwamba, Bunge lako Tukufu sasa liidhinishe makadirio hayo.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja. (Makofi)

WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Spika, naafiki.

(Hoja ilitolewa iamuliwe) (Hoja iliamuliwa na Kuafikiwa)

(Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Miundombinu kwa mwaka 2007/2008 yalipitishwa na Bunge)

SPIKA: Tunamtakia Waziri na timu yake utekelezaji mwema, kwa sababu italeta tofauti kubwa katika nchi yetu. (Makofi)

Baada ya hayo, kwa sababu muda wa kuahirisha shughuli za Bunge umekaribia sana, natamka kwamba shughuli za Bunge zinaahirishwa hadi kesho saa tatu asubuhi.

(Saa 01.43 usiku Bunge liliahirishwa mpaka siku ya Ijumaa Tarehe 13 Julai, 2007 Saa Tatu Asubuhi)

208 209