Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
Tarehe 30 Machi, 2021
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Kwanza – Tarehe 30 Machi, 2021 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) WIMBO WA TAIFA NA WIMBO WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI (Hapa Kwaya ya Bunge iliimba Wimbo wa Taifa na Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: TAARIFA YA SPIKA NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nitaleta kwenu Taarifa ya Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Job Yustino Ndugai. Waheshimiwa Wabunge, kama ambavyo wote tunafahamu aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alifariki dunia tarehe 17 Machi, 2021 katika Hospitali ya Mzena, Jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Waheshimiwa Wabunge, kufuatia msiba huo wananchi wa Tanzania walipata fursa ya kutoa heshima za mwisho kama ifuatavyo; tarehe 20 hadi 21 Machi, 2021 Mkoani Dar es Salaam, tarehe 22 Machi, 2021 Mkoani Dodoma ambapo pia ilifanyika hafla ya kitaifa. Tarehe 23 Machi, 2021 ilikuwa Zanzibar na tarehe 24 Machi, 2021 ilikuwa mkoani Mwanza. Waheshimiwa Wabunge, nazisikia kelele sina hakika kama wote tuko pamoja kwenye jambo hili zito lililolipata Taifa letu. Tarehe 25 hadi 26 mkoani Geita na Chato. Waheshimiwa Wabunge, mazishi ya aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli yalifanyika siku ya Ijumaa tarehe 26 Machi, 2021 nyumbani kwake Chato, Mkoani Geita. Waheshimiwa Wabunge, kwa kuwa leo ni siku ya kwanza kwa Bunge hili kukutana tangu ulipotokea msiba huo naomba Waheshimiwa Wabunge tusimame kwa dakika moja ili kumkumbuka mpendwa wetu. -
MKUTANO WA TATU Kikao Cha Kumi Na Tisa – Tarehe 29 Aprili, 2021
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Kumi na Tisa – Tarehe 29 Aprili, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa, tukae. Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2021/2022. NAIBU WAZIRI WA MADINI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2021/2022. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. SAADA MONSOUR HUSSEIN - K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2020/2021 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2021/2022. NAIBU SPIKA: Ahsante sana. Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa maswali, tutaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Busega, sasa aulize swali lake. Na. 158 Serikali Kukamilisha Ujenzi wa Zahanati – Busega MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza:- Wananchi wa Kata ya Imalamate Wilayani Busega wamejenga zahanati na kumaliza maboma manne kwa maana ya zahanati moja kila kijiji:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi hao kuezeka maboma hayo ili waweze kupata huduma za afya kwenye zahanati hizo? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Dkt. -
MKUTANO WA PILI Kikao Cha Nne – Tarehe 5 Februari, 2021 (Bunge
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA PILI Kikao cha Nne – Tarehe 5 Februari, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. ASIA MINJA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali tutaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini sasa aulize swali lake. Kwa niaba yake Mheshimiwa Innocent Bilakwate. Na. 42 Ujenzi wa Vituo vya Afya kwa Nguvu za Wananchi MHE. INNOCENT S. BILAKWATE (K.n.y. MHE. ALMAS A. MAIGE) aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Tabora Kaskazini wamejitolea kujenga Vituo vya Afya katika Kata za llolangulu, Mabama, Shitagena na Usagari katika Kijiji cha Migungumalo:- Je, Serikali ipo tayari kuanza kuchangia miradi hiyo? 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua mchango mkubwa wa wananchi katika ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya kote nchini. Hivyo, Serikali ina dhamira ya dhati ya kuchangia nguvu hizo za wananchi katika kukamilishaji vituo hivyo ili vianze kutoa huduma kwa wananchi. Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa ukarabati na ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya nchini ikiwemo kukamilisha maboma ya majengo ya kutolea huduma za afya yaliyojengwa na wananchi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, ambapo ujenzi wake ulisimama kwa kukosa fedha. -
Tarehe 4 Aprili, 2017
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Kwanza – Tarehe 4 Aprili, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) WIMBO WA TAIFA (Hapa Waheshimiwa Wabunge Waliimba Wimbo wa Taifa) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Natoa nafasi kwa Waheshimiwa Wabunge mnaoingia, naomba mfanye haraka kidogo. Waheshimiwa Wabunge, nawakaribisha kwenye Mkutano wa Saba, Kikao cha Kwanza, Katibu! (Vigelegele) DKT. THOMAS KASHILILAH – KATIBU WA BUNGE: KIAPO CHA UAMINIFU Mheshimiwa Mbunge afuatae aliapa Kiapo cha Uaminifu:- Mhe. Salma Rashid Kikwete. (Vigelegele/Makofi) SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nashukuru kwa makofi yenu. Tuendelee sasa maana nilikuwa nasubiri kidogo nione mama anakaa wapi ili akisimama kwenye maswali 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) nijue yupo wapi maana leo nataka nimpe swali la kwanza. Katibu tuendelee! (Makofi/Kicheko/Vigelegele) DKT. THOMAS KASHILILAH – KATIBU WA BUNGE: TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, katika Mkutano wa Sita wa Bunge, Bunge lilipitisha Miswada ya Sheria ya Serikali miwili ifuatayo:- (i) Muswada wa Sheria ya Huduma ya Msaada wa Kisheria (The Legal Aid Bill, 2016); na (ii) Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na.4 wa Mwaka 2016 (The Written Laws (Miscellaneous Amendment) No. 4 Bill 2016) Kwa Taarifa hii, napenda kuliarifu Bunge hili Tukufu kwamba tayari Miswada hiyo miwili imepata kibali cha Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwa sheria za nchi zinazoitwa:- (i) Sheria ya Huduma ya Msaada wa Kisheria Na.1 ya Mwaka 2017 (The Legal Aid Act No.1, 2017); na (ii) Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na.4 ya Mwaka 2017 (The Written Laws (Miscellaneous Amendment) No.4, Act No.2 2017). -
1 Bunge La Tanzania
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 9 Mei, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu. NDG. LINA KITOSI – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Randama ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NAIBU SPIKA: Katibu. NDG. LINA KITOSI - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU Na. 207 Hospitali za Wilaya MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:- Wilaya ya Itilima na Busega ni Wilaya mpya na hazina Hospitali za Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali za Wilaya kwenye Wilaya hizo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri za Wilaya ya Itilima na Busega zilianzishwa mwaka 2015 na zina idadi ya watu 346,170 kwa Itilima na 224,527 kwa Busega. Ni kweli kwamba Halmashauri hizi bado hazina Hospitali za Wilaya na wananchi wanapata huduma kupitia zahanati 45 na vituo vya afya saba ambapo kati ya hivyo zahanati 27 na vituo vya afya vitatu vipo Halmashauri ya Wilaya ya Itilima na zahanati 18 na vituo vya afya vinne vipo Halmashauri ya Wilaya ya Busega. -
Majadiliano Ya Bunge ______
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ BUNGE LA KUMI NA MOJA MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini na Moja – Tarehe 6 Mei, 2019 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa tukae. Katibu. NDG. PAMELA PALLANGYO – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa mwaka wa fedha, 2018/2019. MWENYEKITI: Ahsante. Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. PAMELA PALLANGYO – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Swali letu la kwanza leo linaulizwa na Mheshimiwa Ruth Mollel, Mbunge wa Viti Maalum na linaelekezwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Na. 166 Athari za Mtambo wa Kuchoma Takataka za Hospitali na Dawa Zilizokwisha Muda – Mkuranga MHE. RUTH H. MOLLEL aliuliza:- Mtambo wa kuchoma takataka za hospitali na dawa zilizokwisha muda wake upo katika Kijiji cha Dundani Wilayani Mkuranga. Uchomaji unapofanyika moshi mzito huingia kwenye nyumba na maeneo ya wananchi wanaoishi karibu na mtambo huo na kuhatarisha afya zao:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kunusuru afya na maisha ya wananchi wanaoishi karibu na mtambo huo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ruth Hiyob Mollel, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba upo mtambo wa kuchomea taka na dawa zilizokwisha muda wake uliojengwa na mwekezaji katika Kijiji cha Dundani, Wilaya ya Mkuranga. -
Tarehe 11 Mei, 2017
NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Ishirini na Mbili – Tarehe 11 Mei, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. CHARLES MLOKA – KATIBU MEZANI: MASWALI KWA WAZIRI MKUU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tutaanza na maswali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu. Waheshimiwa Wabunge, tutaanza na Mheshimiwa Freeman Aikaeli Mbowe, Kiongozi wa Upinzani Bungeni. MHE. FREEMAN A. MBOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kwanza ya kumuuliza Waziri Mkuu swali. Mheshimiwa Waziri Mkuu, Bunge kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 63(2), ndicho chombo kikuu chenye mamlaka na wajibu wa kuisimamia na kuishauri Serikali. Katika Bunge hili, Bunge la Kumi na Mabunge mengine kadhaa, Bunge limekuwa linatoa Maazimio kadhaa kuitaka Serikali itoe taarifa na Serikali imekuwa inaahidi kutoa taarifa, lakini taarifa nyingi ambazo ni Maazimio ya Bunge yamekuwa hayatekelezwi na Serikali. 1 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, kuna Maazimio ya Bunge kuhusiana na Tokomeza mpaka leo Serikali haijaleta majibu. Kuna Maazimio ya Bunge kuhusiana na ESCROW na IPTL, Serikali mpaka leo haijatoa majibu. Kuna Maazimio ya Bunge kuhusu mabilioni ya Uswis, Serikali mpaka leo haijatoa majibu na Maazimio mengine mengi. (Makofi) Mheshimiwa Waziri Mkuu unaliambia nini Bunge na unaliambia nini Taifa. Wewe kama Kiongozi wa Serikali Bungeni, utapenda kusema kwamba -
THE UNIVERSITY in Africa and Democratic Citizenship Hothouse Or Training Ground?
THE UNIVERSITY IN AFRICA AND DEMOCratiC CITIZENSHIP Hothouse or Training Ground? Report on Student Surveys conducted at the University of Nairobi, Kenya, the University of Cape Town, South Africa, and the University of Dar es Salaam, Tanzania Thierry M Luescher-Mamashela with Sam Kiiru, Robert Mattes, Angolwisye Mwollo-ntallima, Njuguna Ng’ethe and Michelle Romo Published by the Centre for Higher Education Transformation (CHET), House Vincent, First Floor, 10 Brodie Road, Wynberg Mews, Wynberg, 7800 Telephone: +27(0)21 763–7100 | Fax: +27(0)21 763–7117 E-mail: [email protected] | www.chet.org.za © CHET 2011 ISBN 978–1-920355–67–8 Produced by COMPRESS.dsl | www.compressdsl.com Cover illustration by Raymond Oberholzer Distributed by African Minds 4 Eccleston Place, Somerset West, 7130, South Africa [email protected] www.africanminds.co.za For orders from outside Africa: African Books Collective PO Box 721, Oxford OX1 9EN, UK [email protected] www.africanbookscollective.com iii Contents Acknowledgements v The Project Group vii Executive Summary ix CHAPTER 1: HERANA Higher Education and Democracy: The Student Governance Surveys 1 1.1 Project overview 1 1.2 Analytical framework of the study 3 1.3 Research questions 12 1.4 Survey design and methods 14 1.5 Overview of the report 19 CHAPTER 2: Background and Context: Three Countries, Universities and Student Bodies 21 2.1 Governance in Kenya, South Africa, and Tanzania in international comparison 21 2.2 Democracy in Kenya, the University of Nairobi and student politics 22 -
Ten Years of Jakaya Kikwete's Presidency
TEN YEARS OF JAKAYA KIKWETE’S PRESIDENCY: Promises, Achievements and Challenges in Education November 2015 TEN YEARS OF JAKAYA KIKWETE’S PRESIDENCY: PROMISES, ACHIEVEMENTS AND CHALLENGES IN EDUCATION | 1 ACKNOWLEDGEMENTS This report was written by Prof. Kitila Mkumbo on behalf of HakiElimu. Technical advice was provided by John Kalage and Godfrey Boniventura. We also thank Robert Mihayo and Presscodd James for their editorial contribution in this report. HakiElimu acknowledges the contribution of all those who made the production of this report possible. HakiElimu, P.O.Box 79401, Dar es Salaam Tel: (255 22) 2151852/3 Fax: (255 22) 2152449 Email: [email protected] Website: www.hakielimu.org ISBN – 978-9987-18-049-3 Any part of this publication may be produced for education and non commercial purposes, provided provenance is made to the source and at least a copy is provided to HakiElimu. 2 | TEN YEARS OF JAKAYA KIKWETE’S PRESIDENCY: PROMISES, ACHIEVEMENTS AND CHALLENGES IN EDUCATION TABLE OF CONTENTS Tables ....................................................................................................................................... 4 Figures ..................................................................................................................................... 4 Abbreviations ........................................................................................................................... 5 Summary ................................................................................................................................. -
MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao Cha Saba – Tarehe 11 Aprili
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Saba – Tarehe 11 Aprili, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Najma Murtaza Giga) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa tukae, Katibu. NDG. RUTH MAKUNGU – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazi ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Repoti ya Mwaka ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Kuhusu Taarifa za Fedha za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017 (The Annual General Report of the Controller and Audit General of the Financial Statement of Local Governments For the Year Ended 30th June, 2017). Taarifa ya Majibu ya Serikali na Mpango Kazi wa Utekelezaji wa Mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Ripoti ya Ukaguzi wa Ufanisi ya Hali ya Uharibifu wa Ardhi na Misitu (Study on the Status of Environment With the Focus on Land Degradation, Forest Degradation and Deforestation) Repoti ya Ukaguzi wa Ufanisi na Usimamizi wa Taka za Kielektroniki (Performance Audit Report on Electronic Waste Management) NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Repoti Kuu ya Mwaka ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Kuhusu Taarifa za Fedha za Taasisi za Serikali Kuu kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017 (The Annual General Report of The Controller and Auditor General on Financial Statement of Central Government for the Year ended 30th June, 2017). -
Tarehe 12 Mei, 2017
NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Ishirini na Tatu – Tarehe 12 Mei, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Tukae. Katibu. NDG. ZAINAB ISSA – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kwa mwaka wa fedha 2017/2018. MWENYEKITI: Ahsante. Katibu 1 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. ZAINABU ISSA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU Na. 190 Malipo ya Wafanyakazi wa Kiwanda cha Chumvi – Uvinza MHE. HASNA S. K. MWILIMA aliuliza:- (a) Je, Serikali inawaeleza nini wafanyakazi wa Kiwanda cha Chumvi ambao walistaafishwa bila malipo ya kiinua mgongo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwabana wamiliki wa kiwanda hicho ili waboreshe mazingira ya kiwanda pamoja na mazingira ya wafanyakazi? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANA NA AJIRA) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hasna Sudi Katunda Mwilima, Mbunge wa Kigoma Kusini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, suala la wafanyakazi wa Kiwanda cha Chumvi ambao walistaafishwa bila malipo ya kiinua mgongo lilishashughulikiwa, ambapo wafanyakazi husika walilipwa mafao yao kwa mujibu wa sheria ikiwemo kiinua mgongo. Aidha, kwa kuzingatia Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 2 ya mwaka 2016 yaliyopitishwa na Bunge lako Tukufu wakati wa Kikao cha Bajeti, kama kuna mfanyakazi au wafanyakazi wanaoona kuwa hawakulipwa stahiki zao za kupunguzwa kazi ipasavyo, wanayo fursa ya kuwasilisha moja kwa moja madai yao kwenye Tume ya Usuluhishi na Uamuzi pasipo kupitishia kwa Kamishna wa Kazi. -
Przegląd Tygodniowy Ambasady RP W Dar Es Salaam (31 Marca – 7 Kwietnia 2021 R.)
Przegląd tygodniowy Ambasady RP w Dar es Salaam (31 marca – 7 kwietnia 2021 r.) Tanzania. Nowy rząd prezydent Samii Suluhu Hassan – bez rewolucji, ale z silnym sygnałem probiznesowym. Powołaniem szeregu nowych sekretarzy stanu w dniu 6 kwietnia br. prezydent Samia Suluhu Hassan (PSSH) zakończyła proces budowy nowego rządu Tanzaniii. Kluczowe zmiany objęły: resort spraw zagranicznych, gdzie ministrem została doświadczona dyplomatka Liberata Mulamula, ministerstwo finansów, które objął doświadczony bankowiec i ekonomista Mwigulu Nchemba, oraz resort przemysłu i handlu, którym kierować będzie były sekretarz stanu w ministerstwie wody oraz minister ds. inwestycji profesor Kitila Mkumbo. Prezydent Hassan usunęła także ze stanowisk dotychczasowego sekretarza rządu Bashiru Ally oraz szefów tanzańskiego urzędu podatkowego (Tanzanian Revenue Authority, TRA), tanzańskiego urzędu portowego (Tanzanian Port Authority, TPA), tanzańskiej agencji spedycyjnej (Tanzania Shipping Agency, TSA) oraz urzędów związanych z regulacją mediów. Uzasadniając zmiany prez. Hassan podkreśliła, że dla osiągnięcia celów rozwojowych Tanzanii zawartych w dokumencie Vision 2025, obejmujących uzyskanie przez nią statusu kraju o średnim dochodzie oraz przychodów z przemysłu równych tym z rolnictwa, państwo musi w większym stopniu oprzeć się na sektorze prywatnym, w tym inwestorach zagranicznych. PSSH jasno stwierdziła, że w chwili obecnej, wskutek bałaganu prawnego i nadmiernej agresji administracji podatkowej i imigracyjnej biznes lokalny „się załamuje” a inwestorzy zagraniczni „raczej uciekają niż planują nowe inwestycje”. Prezydent przywołała dane rządowe wskazujące, że od 2015 roku w samym dystrykcie Dar es Salaam zlikwidowano ponad 7200 firm prywatnych. Oceniła również, że obecne procedury przyznawania zezwoleń na pracę i pobyt dla cudzoziemców są „nie do zaakceptowania”. Podkreśliła też, że w pełni rozumie firmy zagraniczne preferujące w ramach swoich inwestycji w Tanzanii zatrudnianie obcokrajowców, z uwagi na brak odpowiednio wykwalifikowanych specjalistów miejscowych.