Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
Tarehe 30 Machi, 2021
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Kwanza – Tarehe 30 Machi, 2021 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) WIMBO WA TAIFA NA WIMBO WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI (Hapa Kwaya ya Bunge iliimba Wimbo wa Taifa na Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: TAARIFA YA SPIKA NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nitaleta kwenu Taarifa ya Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Job Yustino Ndugai. Waheshimiwa Wabunge, kama ambavyo wote tunafahamu aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alifariki dunia tarehe 17 Machi, 2021 katika Hospitali ya Mzena, Jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Waheshimiwa Wabunge, kufuatia msiba huo wananchi wa Tanzania walipata fursa ya kutoa heshima za mwisho kama ifuatavyo; tarehe 20 hadi 21 Machi, 2021 Mkoani Dar es Salaam, tarehe 22 Machi, 2021 Mkoani Dodoma ambapo pia ilifanyika hafla ya kitaifa. Tarehe 23 Machi, 2021 ilikuwa Zanzibar na tarehe 24 Machi, 2021 ilikuwa mkoani Mwanza. Waheshimiwa Wabunge, nazisikia kelele sina hakika kama wote tuko pamoja kwenye jambo hili zito lililolipata Taifa letu. Tarehe 25 hadi 26 mkoani Geita na Chato. Waheshimiwa Wabunge, mazishi ya aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli yalifanyika siku ya Ijumaa tarehe 26 Machi, 2021 nyumbani kwake Chato, Mkoani Geita. Waheshimiwa Wabunge, kwa kuwa leo ni siku ya kwanza kwa Bunge hili kukutana tangu ulipotokea msiba huo naomba Waheshimiwa Wabunge tusimame kwa dakika moja ili kumkumbuka mpendwa wetu. -
Nakala Ya Mtandao (Online Document)
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Kumi na Mbili - Tarehe 30 Machi, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali leo tunaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu, Mheshimiwa Conchesta Rwamlaza, atauliza swali la kwanza. Na. 117 Mwakilishi wa Wazee katika Vyombo vya Maamuzi MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza:- Kwa muda mrefu wazee wa nchi hii wamekuwa wakililia uwakilishi katika vyombo mbalimbali vya maamuzi kama vile Bunge, Halmashauri, Vijiji na kadhalika kama ilivyo kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu ili sauti zao zisikike:- Je, ni lini Serikali itasikia kilio cha wazee hawa? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, URATIBU NA BUNGE) alijibu:- Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Utaratibu wa kupata wawakilishi katika vyombo vya maamuzi kama vile Bunge, umeelezwa katika Ibara ya 66 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Ibara hii imefafanua aina za Wabunge na namna ya kuwapata. Utaratibu wa kuwapata wawakilishi katika Halmashauri umeelezwa 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) katika Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Sura ya 292 yaani The Local Authority Election Act, Cap. 292. Aidha, utaratibu wa kuwapata wawakilishi katika vijiji hutawaliwa na Sheria ya Serikali za Mitaa, Sura ya 287 na Sheria ya Serikali za Mitaa, Sura ya 288. Mheshimiwa Spika, wawakilishi wanaowakilisha makundi mbalimbali katika Bunge, Halmashauri na Vijiji, kwa mfano, wanawake, vijana, watu wenye ulemavu na kadhalika, wamekuwa wakipatikana kupitia mapendekezo yanayowasilishwa na vyama vya siasa kwenye vyombo vinavyosimamia uchaguzi katika ngazi hizo. -
Mkutano Wa Kwanza
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA KWANZA YATOKANAYO NA KIKAO CHA PILI 18 NOVEMBA, 2015 MKUTANO WA KWANZA YATOKANAYO NA KIKAO CHA PILI - TAREHE 18 NOVEMBA, 2015 I. DUA: Spika wa Bunge, Mhe. Job Y. Ndugai alisomwa dua saa 3.00 asubuhi na kikao kiliendelea. II. KIAPO CHA UAMINIFU KWA WABUNGE WOTE: Wabunge wafuatao waliapishwa na Mhe. Spika:- 1. Mhe. Sophia Mattayo Simba 2. Mhe. Munde Tambwe Abdalla 3. Mhe. Alex Raphael Gashaza 4. Mhe. Esther Nicholas Matiko 5. Mhe. Hafidh Ali Tahir 6. Mhe. Halima Abdallah Bulembo 7. Mhe. Halima James Mdee 8. Mhe. Hamad Yussuf Masauni, Eng. 9. Mhe. Hamida Mohammed Abdallah 10. Mhe. Hamisi Andrea Kigwangalla, Dkt. 11. Mhe. Hasna Sudi Katunda Mwilima 12. Mhe. Hassan Elias Masala 13. Mhe. Hassani Seleman Kaunje 14. Mhe. Hawa Abdulrahman Ghasia 15. Mhe. Hawa Subira Mwaifunga 16. Mhe. Hussein Nassor Amar 17. Mhe. Innocent Lugha Bashungwa 18. Mhe. Innocent Sebba Bilakwate 19. Mhe. Issa Ali Mangungu 20. Mhe. Jacquiline Ngonyani Msongozi 21. Mhe. James Francis Mbatia 22. Mhe. James Kinyasi Millya 23. Mhe. Janeth Zebedayo Mbene 2 24. Mhe. Jasmine Tisekwa Bunga, Dkt. 25. Mhe. Jasson Samson Rweikiza 26. Mhe. Jitu Vrajlal Soni 27. Mhe. John John Mnyika 28. Mhe. John Wegesa Heche 29. Mhe. Joseph George Kakunda 30. Mhe. Joseph Michael Mkundi 31. Mhe. Josephat Sinkamba Kandege 32. Mhe. Josephine Johnson Genzabuke 33. Mhe. Josephine Tabitha Chagula 34. Mhe. Joshua Samwel Nassari 35. Mhe. Joyce Bitta Sokombi 36. Mhe. Joyce John Mukya 37. Mhe. Juliana Daniel Shonza 38. Mhe. Juma Kombo Hamad 39. Mhe. Juma Selemani Nkamia 40. -
MKUTANO WA TATU Kikao Cha Kumi Na Tisa – Tarehe 29 Aprili, 2021
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Kumi na Tisa – Tarehe 29 Aprili, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa, tukae. Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2021/2022. NAIBU WAZIRI WA MADINI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2021/2022. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. SAADA MONSOUR HUSSEIN - K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2020/2021 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2021/2022. NAIBU SPIKA: Ahsante sana. Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa maswali, tutaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Busega, sasa aulize swali lake. Na. 158 Serikali Kukamilisha Ujenzi wa Zahanati – Busega MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza:- Wananchi wa Kata ya Imalamate Wilayani Busega wamejenga zahanati na kumaliza maboma manne kwa maana ya zahanati moja kila kijiji:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi hao kuezeka maboma hayo ili waweze kupata huduma za afya kwenye zahanati hizo? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Dkt. -
Did They Perform? Assessing fi Ve Years of Bunge 2005-2010
Policy Brief: TZ.11/2010E Did they perform? Assessing fi ve years of Bunge 2005-2010 1. Introducti on On July 16th 2010, following the completi on of the 20th session of the Bunge, the President of Tanzania dissolved the 9th Parliament. This event marked the end of the term for Members of Parliament who were elected during the 2005 general electi ons. Now that the last session has been completed it allows us to look back and to consider how MPs performed during their tenure. Did they parti cipate acti vely and represent their consti tuencies by asking questi ons and making interventi ons, or were they silent backbenchers? The Bunge is the Supreme Legislature of Tanzania. The Bunge grants money for running the administrati on and oversees government programs and plans. The Bunge oversees the acti ons of the Executi ve and serves as watchdog to ensure that government is accountable to its citi zens. To achieve all this, Members of Parliament pass laws, authorize taxati on and scruti nize government policies including proposal for expenditure; and debate major issues of the day. For the Bunge to eff ecti vely carry out its oversight role, acti ve parti cipati on by Members of Parliament is criti cal. MPs can be acti ve by making three kinds of interventi ons: they can ask basic questi ons, they can ask supplementary questi ons and they can make contributi ons during debates. This brief follows earlier briefs, the last of which was released in August 2010. It presents seven facts on the performance of MPs, including rati ng who were the most acti ve and least acti ve MPs. -
1447734501-Op Kikao
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA ORODHA YA SHUGHULI ZA LEO MKUTANO WA KWANZA KIKAO CHA KWANZA 17 NOVEMBA, 2015 ORODHA YA SHUGHULI ZA LEO _________________ MKUTANO WA KWANZA KIKAO CHA KWANZA – TAREHE 17 NOVEMBA, 2015 Kikao Kuanza Saa Tatu Kamili Asubuhi I. TANGAZO LA RAIS LA KUITISHA MKUTANO WA BUNGE: II. UCHAGUZI WA SPIKA: III. KIAPO CHA UAMINIFU NA KIAPO CHA SPIKA: IV. WIMBO WA TAIFA NA DUA KUSOMWA: V. KIAPO CHA UAMINIFU KWA WABUNGE WOTE: DODOMA DKT. T. D. KASHILILAH 17 NOVEMBA, 2015 KATIBU WA BUNGE 2 1. Mhe. George Mcheche Masaju 2. Mhe. Andrew John Chenge 3. Mhe. Mary Michael Nagu, Dkt. 4. Mhe. William Vangimembe Lukuvi 5. Mhe. Richard Mganga Ndassa 6. Mhe. Tulia Ackson, Dkt. 7. Mhe. Abbas Ali Hassan Mwinyi, Capt. 8. Mhe. Abdallah Ally Mtolea 9. Mhe. Abdallah Dadi Chikota 10. Mhe. Abdallah Haji Ali 11. Mhe. Abdallah Hamis Ulega 12. Mhe. Abdul-Aziz Mohamed Abood 13. Mhe. Agnes Mathew Marwa 14. Mhe. Adadi Mohamed Rajab, Balozi. 15. Mhe. Ahmed Ally Salum 16. Mhe. Ahmed Juma Ngwali 17. Mhe. Ahmed Mabkhut Shabiby 18. Mhe. Aida Joseph Khenan 19. Mhe. Aisharose Ndogholi Matembe 20. Mhe. Ajali Rashid Akbar 21. Mhe. Upendo Furaha Peneza 3 22. Mhe. Joseph Leonard Haule 23. Mhe. Joseph Osmund Mbilinyi 24. Mhe. Albert Obama Ntabaliba 25. Mhe. Alex Raphael Gashaza 26. Mhe. Ali Hassan Omar, King 27. Mhe. Ali Salim Khamis 28. Mhe. Allan Joseph Kiula 29. Mhe. Ally Mohamed Keissy 30. Mhe. Ally Saleh Ally 31. Mhe. Ally Seif Ungando 32. Mhe. Almas Athuman Maige 33. Mhe. -
MKUTANO WA 18 TAREHE 5 FEBRUARI, 2015 MREMA 1.Pmd
5 FEBRUARI, 2015 BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE __________________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Tisa – Tarehe 5 Februari, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, leo sijamwona. Kwa hiyo tunaendelea na Maswali kwa Waziri Mkuu na atakayeanza ni Mheshimiwa Murtaza A. Mangungu. MHE. MURTAZA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa vipindi tofauti vya Bunge Mheshimiwa Peter Msigwa, Mheshimiwa Mussa Zungu na hata Mheshimiwa Murtaza A. Mangungu wamekuwa wakiuliza swali kuhusiana na manyanyaso wanayoyapata wafanyabiashara Wadogo Wadogo pamoja na Mamalishe. Kwa kipindi hicho chote umekuwa ukitoa maagizo na maelekezo, inavyoonekana mamlaka zinazosimamia hili jambo haziko tayari kutii amri yako. 1 5 FEBRUARI, 2015 Je, unawaambia nini Watanzania na Bunge hili kwa ujumla? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba nimjibu Mheshimiwa Murtaza Mangungu swali lake kama ifuatavyo:- Suala hili la vijana wetu ambao tunawajua kama Wamachinga, kwanza nataka nikiri kwamba ni suala kubwa na ni tatizo kubwa na si la Jiji la Dar es Salaam tu, bali lipo karibu katika miji mingi. Kwa hiyo, ni jambo ambalo lazima twende nalo kwa kiwango ambacho tutakuwa na uhakika kwamba tunalipatia ufumbuzi wa kudumu. Kwa hiyo, ni kweli kwamba mara kadhaa kuna maelekezo yametolewa yakatekelezwa sehemu na sehemu nyingine hayakutekelezwa kikamilifu kulingana na mazingira ya jambo lenyewe lilivyo. Lakini dhamira ya kutaka kumaliza tatizo hili la Wamachinga bado ipo palepale na kwa bahati nzuri umeuliza wakati mzuri kwa sababu jana tu nimepata taarifa ambayo nimeandikiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI ambayo wanaleta mapendekezo kwangu juu ya utaratibu ambao wanafikiri unaweza ukatatua tatizo hili ambalo lipo sehemu nyingi. -
“I Had a Dream to Finish School” Barriers to Secondary Education in Tanzania
“I Had a Dream to Finish School” Barriers to Secondary Education in Tanzania For a word version of this document, please email: [email protected] Copyright © 2017 Human Rights Watch All rights reserved. Printed in the United States of America ISBN: 978-1-6231-34419 Cover design by Rafael Jimenez Human Rights Watch defends the rights of people worldwide. We scrupulously investigate abuses, expose the facts widely, and pressure those with power to respect rights and secure justice. Human Rights Watch is an independent, international organization that works as part of a vibrant movement to uphold human dignity and advance the cause of human rights for all. Human Rights Watch is an international organization with staff in more than 40 countries, and offices in Amsterdam, Beirut, Berlin, Brussels, Chicago, Geneva, Goma, Johannesburg, London, Los Angeles, Moscow, Nairobi, New York, Paris, San Francisco, Sydney, Tokyo, Toronto, Tunis, Washington DC, and Zurich. For more information, please visit our website: http://www.hrw.org FEBRUARY 2017 ISBN: 978-1-6231-34419 “I Had a Dream to Finish School” Barriers to Secondary Education in Tanzania Summary............................................................................................... 1 Key Recommendations ...................................................................... 10 To the Government of Tanzania To International Donors and UN Agencies Methodology ....................................................................................... 14 I. Background: Secondary Education in Tanzania -
MKUTANO WA PILI Kikao Cha Nne – Tarehe 5 Februari, 2021 (Bunge
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA PILI Kikao cha Nne – Tarehe 5 Februari, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. ASIA MINJA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali tutaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini sasa aulize swali lake. Kwa niaba yake Mheshimiwa Innocent Bilakwate. Na. 42 Ujenzi wa Vituo vya Afya kwa Nguvu za Wananchi MHE. INNOCENT S. BILAKWATE (K.n.y. MHE. ALMAS A. MAIGE) aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Tabora Kaskazini wamejitolea kujenga Vituo vya Afya katika Kata za llolangulu, Mabama, Shitagena na Usagari katika Kijiji cha Migungumalo:- Je, Serikali ipo tayari kuanza kuchangia miradi hiyo? 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua mchango mkubwa wa wananchi katika ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya kote nchini. Hivyo, Serikali ina dhamira ya dhati ya kuchangia nguvu hizo za wananchi katika kukamilishaji vituo hivyo ili vianze kutoa huduma kwa wananchi. Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa ukarabati na ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya nchini ikiwemo kukamilisha maboma ya majengo ya kutolea huduma za afya yaliyojengwa na wananchi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, ambapo ujenzi wake ulisimama kwa kukosa fedha. -
Tarehe 4 Aprili, 2017
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Kwanza – Tarehe 4 Aprili, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) WIMBO WA TAIFA (Hapa Waheshimiwa Wabunge Waliimba Wimbo wa Taifa) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Natoa nafasi kwa Waheshimiwa Wabunge mnaoingia, naomba mfanye haraka kidogo. Waheshimiwa Wabunge, nawakaribisha kwenye Mkutano wa Saba, Kikao cha Kwanza, Katibu! (Vigelegele) DKT. THOMAS KASHILILAH – KATIBU WA BUNGE: KIAPO CHA UAMINIFU Mheshimiwa Mbunge afuatae aliapa Kiapo cha Uaminifu:- Mhe. Salma Rashid Kikwete. (Vigelegele/Makofi) SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nashukuru kwa makofi yenu. Tuendelee sasa maana nilikuwa nasubiri kidogo nione mama anakaa wapi ili akisimama kwenye maswali 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) nijue yupo wapi maana leo nataka nimpe swali la kwanza. Katibu tuendelee! (Makofi/Kicheko/Vigelegele) DKT. THOMAS KASHILILAH – KATIBU WA BUNGE: TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, katika Mkutano wa Sita wa Bunge, Bunge lilipitisha Miswada ya Sheria ya Serikali miwili ifuatayo:- (i) Muswada wa Sheria ya Huduma ya Msaada wa Kisheria (The Legal Aid Bill, 2016); na (ii) Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na.4 wa Mwaka 2016 (The Written Laws (Miscellaneous Amendment) No. 4 Bill 2016) Kwa Taarifa hii, napenda kuliarifu Bunge hili Tukufu kwamba tayari Miswada hiyo miwili imepata kibali cha Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwa sheria za nchi zinazoitwa:- (i) Sheria ya Huduma ya Msaada wa Kisheria Na.1 ya Mwaka 2017 (The Legal Aid Act No.1, 2017); na (ii) Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na.4 ya Mwaka 2017 (The Written Laws (Miscellaneous Amendment) No.4, Act No.2 2017). -
Tarehe 11 Novemba, 2016
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _____________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA TANO Kikao cha Kumi – Tarehe 11 Novemba, 2016 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tukae. Katibu! NDG. THOMAS D. KASHILILAH – KATIBU WA BUNGE: TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kwa masikitiko makubwa nawatangazia msiba tuliopata wa mwenzetu Mheshimiwa Hafidh Ali Tahir, Mbunge wa Dimani Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi, msiba uliotokea saa nane kamili usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya General hapa Dodoma. Marehemu Hafidh Ali Tahir aliugua kwa muda mfupi ambapo baada ya kujisikia vibaya aliamua kwenda hospitali mwenyewe usiku wa jana na alipofika alikutwa na tatizo la moyo na akiwa katika matibabu alifariki. Ni masikitiko makubwa kwa sababu ni jana tu mimi nilikuwa naye katika Kikao cha Bunge Sports Club na pia alishughulika katika semina mbalimbali za Wabunge zilizofanyika Dodoma Hotel na hapa Bungeni na pia baadhi yetu tulikuwa naye katika kikao cha Bunge humu ndani na tulifanya kazi vizuri sana kwa pamoja. Vile vile Marehemu Hafidh Ali Tahir alikuwa ni mmoja wa Wabunge walioomba kwenda Urambo kwenye maziko ya Mheshimiwa Mzee Samuel Sitta, Spika Mstaafu wa Bunge la Tisa na alikuwemo katika orodha ya Wabunge ambao walihitajika kwenda kushiriki katika msiba huo. 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Tumeondokewa na Mbunge mchapa kazi, mcheshi, mwanamichezo na pia Mbunge aliowajali sana wapiga kura wake. Waheshimiwa Wabunge, kwa mujibu wa Kanuni zetu za Kudumu za Bunge, Toleo la Januari 2016; Kanuni ya 152 kuhusu utaratibu baada ya kifo cha Mbunge inasema na hapa nanukuu: “Endapo Mbunge atafariki wakati Bunge likiwa katika shughuli zake, Spika ataahirisha shughuli za Bunge kwa siku hiyo kwa ajili ya maombolezo. -
1 Bunge La Tanzania
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 9 Mei, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu. NDG. LINA KITOSI – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Randama ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NAIBU SPIKA: Katibu. NDG. LINA KITOSI - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU Na. 207 Hospitali za Wilaya MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:- Wilaya ya Itilima na Busega ni Wilaya mpya na hazina Hospitali za Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali za Wilaya kwenye Wilaya hizo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri za Wilaya ya Itilima na Busega zilianzishwa mwaka 2015 na zina idadi ya watu 346,170 kwa Itilima na 224,527 kwa Busega. Ni kweli kwamba Halmashauri hizi bado hazina Hospitali za Wilaya na wananchi wanapata huduma kupitia zahanati 45 na vituo vya afya saba ambapo kati ya hivyo zahanati 27 na vituo vya afya vitatu vipo Halmashauri ya Wilaya ya Itilima na zahanati 18 na vituo vya afya vinne vipo Halmashauri ya Wilaya ya Busega.