1 Bunge La Tanzania
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
Online Document)
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Arobaini na Sita – Tarehe 8 Julai, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Mussa Z. Azzan) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, maswali na tunaanza na ofisi ya Waziri, Mheshimiwa Kayombo, kwa niaba yake Mheshimiwa Rage. Na. 321 Ofisi kwa ajili ya Tarafa-Mbinga MHE. ISMAIL A. RAGE (K.n.y. MHE. GAUDENCE C. KAYOMBO) aliuliza:- Wilaya ya Mbinga ina tarafa sita lakini tarafa zote hazina ofisi rasmi zilizojengwa:- Je, ni lini Serikali itajenga ofisi kwa Makatibu Tarafa? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Gaudence Cassian Kayombo, Mbunge wa Mbinga Mashariki kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Ruvuma una jumla ya tarafa 24 yaani Tunduru wako saba, Mbinga wana tarafa sita, Nyasa wana tarafa tatu, Namtumbo wana tarafa tatu na Songea wana tarafa tano. Ni kweli tarafa za Wilaya ya Mbinga hazina ofisi rasmi zilizojengwa na Serikali. Ujenzi wa hizo ofisi unafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Kwa sasa Mkoa wa Ruvuma umeweka kipaumbele katika ujenzi wa ofisi nne za tarafa katika Wilaya ya Nyasa na Tunduru. Tarafa hizo ni Luhuhu (Lituhi-Nyasa), Ruhekei (Mbamba bay-Nyasa), Mpepo (Tinga-Nyasa) na Nampungu (Nandembo-Tunduru). Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2014/2015, Mkoa ulitenga shilingi milioni mia tatu kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya Tarafa ya Luhuhu (Lituhi), Ruhekei (Mbamba bay), Mpepo (Tingi) na Nampungu (Nandembo). -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Tatu – Tarehe 15 APRILI, 2010 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU NAIBU SPIKA: Maswali kwa Waziri Mkuu leo kiongozi wa Upinzani Bungeni hayupo kwa hiyo nitaenda na orodha za wachangiaji na nitakuwa ninakwenda kufuatana na itikadi ya chama, upande, gender na vitu kama hivyo. Kwa hiyo, walioko hapa wasidhani watakwenda kama ilivyoorodheshwa. Kwa hiyo, nitaanza na msemaji wa kwanza Mheshimiwa Dr. Willibrod Slaa. MHE. DR. WILLIBROD P. SLAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kunipa nafasi, Mheshimiwa Waziri Mkuu sasa ni takribani mwaka mzima tangu nilipoanza kuhoji, mimi na Wabunge wenzangu, tulipoanza kuhoji kuhusu ubadhirifu na tuhuma mbalimbali zilizokuwa zinakabili matumizi ya fedha za umma zilizofanywa na makampuni kama Mwananchi Gold Company, Tan Gold, Kagoda, Deep Green na mengine mengi ambayo yalitajwa ndani ya ukumbi huu. Kwa nyakati tofauti maelezo mbalimbali yametolewa ndani ya Bunge. Mpaka leo hatujapata taarifa ya kinachoendelea. Bunge hili lenye jukumu la kuisimamia Serikali halijui au wananchi hawajui kama kuna kitu kinaendelea je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu ubadhirifu huo? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naamini kabisa Dr. Slaa, hutegemei kwamba kweli nitaweza kujibu maswali hayo uliyoyauliza kwamba mimi nina maelezo juu ya Kagoda, maelezo juu ya nani, is not possible nadhani si sahihi kabisa. (Makofi) Mimi ninachoweza kusema ni kwamba jitihada za Serikali zipo zimekuwa zikionekana katika maeneo ambayo yameshaanza kufanyiwa kazi. Sasa kama kuna maeneo ambayo bado hayajafanyiwa kazi jitihada za Serikali zitaendelea kwa kadri itakavyowezekana. -
Mkutano Wa Kwanza
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA KWANZA YATOKANAYO NA KIKAO CHA PILI 18 NOVEMBA, 2015 MKUTANO WA KWANZA YATOKANAYO NA KIKAO CHA PILI - TAREHE 18 NOVEMBA, 2015 I. DUA: Spika wa Bunge, Mhe. Job Y. Ndugai alisomwa dua saa 3.00 asubuhi na kikao kiliendelea. II. KIAPO CHA UAMINIFU KWA WABUNGE WOTE: Wabunge wafuatao waliapishwa na Mhe. Spika:- 1. Mhe. Sophia Mattayo Simba 2. Mhe. Munde Tambwe Abdalla 3. Mhe. Alex Raphael Gashaza 4. Mhe. Esther Nicholas Matiko 5. Mhe. Hafidh Ali Tahir 6. Mhe. Halima Abdallah Bulembo 7. Mhe. Halima James Mdee 8. Mhe. Hamad Yussuf Masauni, Eng. 9. Mhe. Hamida Mohammed Abdallah 10. Mhe. Hamisi Andrea Kigwangalla, Dkt. 11. Mhe. Hasna Sudi Katunda Mwilima 12. Mhe. Hassan Elias Masala 13. Mhe. Hassani Seleman Kaunje 14. Mhe. Hawa Abdulrahman Ghasia 15. Mhe. Hawa Subira Mwaifunga 16. Mhe. Hussein Nassor Amar 17. Mhe. Innocent Lugha Bashungwa 18. Mhe. Innocent Sebba Bilakwate 19. Mhe. Issa Ali Mangungu 20. Mhe. Jacquiline Ngonyani Msongozi 21. Mhe. James Francis Mbatia 22. Mhe. James Kinyasi Millya 23. Mhe. Janeth Zebedayo Mbene 2 24. Mhe. Jasmine Tisekwa Bunga, Dkt. 25. Mhe. Jasson Samson Rweikiza 26. Mhe. Jitu Vrajlal Soni 27. Mhe. John John Mnyika 28. Mhe. John Wegesa Heche 29. Mhe. Joseph George Kakunda 30. Mhe. Joseph Michael Mkundi 31. Mhe. Josephat Sinkamba Kandege 32. Mhe. Josephine Johnson Genzabuke 33. Mhe. Josephine Tabitha Chagula 34. Mhe. Joshua Samwel Nassari 35. Mhe. Joyce Bitta Sokombi 36. Mhe. Joyce John Mukya 37. Mhe. Juliana Daniel Shonza 38. Mhe. Juma Kombo Hamad 39. Mhe. Juma Selemani Nkamia 40. -
Process in Tanzania the Political, Civil and Economic Society
Tanzania has been independent in 2011 for 50 years. While most neighbouring states have Jonas gone through violent conflicts, Tanzania has managed to implement extensive reforms with- out armed political conflicts. Hence, Tanzania is an interesting case for Peace and Develop- ment research. E Challenges for the This dissertation analyses the political development in Tanzania since the introduction of wald the multiparty system in 1992, with a focus on the challenges for the democratisation process democratisation in connection with the 2000 and 2005 elections. The question of to what extent Tanzania has moved towards a consolidation of democracy, is analysed through an analysis of nine different institutions of importance for democratisation, grouped in four spheres, the state, Challenges for the process in Tanzania the political, civil and economic society. Focus is on the development of the political society, and the role of the opposition in particular. The analysis is based on secondary and primary Moving towards consolidation 50 years material collected in the period September 2000 to April 2010. after indepencence? The main conclusion is that even if the institutions of liberal democracy have gradually developed, in practice single-party rule has continued, manifested in the 2005 election when the CCM won 92% of the seats in the parliament. Despite an impressive economic growth, poverty remains deep and has not been substantially reduced. On a theoretical level this brings the old debate between liberal and substantive democracy back to the fore. Neither the economic nor the political reforms have apparently brought about a transformation of the political and economic system resulting in the poor majority gaining substantially more political influence and improved economic conditions. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE ________________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 17 Julai, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO:- Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa mwaka wa Fedha 2012/2013. NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:- Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa Fedha 2012/2013. MHE. EUGEN E. MWAIPOSA (K.n.y. MHE. EDWARD LOWASSA - MWENYEKITI WA KAMATI YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA):- Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka 2011/2012 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. MHE. VINCENT J. NYERERE – MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani juu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tunaanza maswali kwa Ofisi ya Waziri Mkuu, atakayeuliza swali letu la kwanza ni Mheshimiwa Beatrice Matumbo Shellukindo kwa niaba yake Mheshimiwa Herbert Mntangi. -
Bunge La Tanzania
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Kwanza – Tarehe 9 Juni, 2009 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) WIMBO WA TAIFA (Hapa Wabunge Waliimba Wimbo wa Taifa) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta ) Alisoma Dua KIAPO CHA UAMINIFU Mbunge afuataye aliapa Kiapo cha Uaminifu na kukaa katika nafasi yake Bungeni:- Mheshimiwa Lolensia Jeremiah Maselle Bukwimba SPIKA: Ahsante sana, leo shamrashamra zimepita kiasi; nimetafuta ushauri wa sheria bado sijapewa kuhusu shamrashamra hizi kwa kiwango hiki kama inaruhusiwa kwa kanuni lakini hayo sasa ni ya baadaye. (Kicheko) T A A R I F A Y A S P I K A SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, katika Mkutano wa Kumi na Tano wa Bunge hili, tulipitisha Miswada mitano ya sheria iitwayo The Human DNA Regulation Bill, 2009, The Fertilizers Bill, 2009, The Insurance Bill, 2009, The Water Resources Management Bill, 2009 na The Water Supply and Sanitation Bill, 2009. Mara baada ya kupitishwa na Bunge na baadae kupita katika hatua zake zote za uchapishaji, Miswada hiyo ilipelekwa kwa Mheshimiwa Rais ili kupata kibali chake kwa mujibu wa Katiba. Kwa taarifa hii, nafurahi kuwaarifu Wabunge wote na Bunge hili Tukufu kwamba, tayari Mheshimiwa Rais amekwishatoa kibali kwa Miswada yote hiyo mitano na sasa ni sheria za nchi, ambapo The Human DNA Regulation Act, 2009 inakuwa ni Sheria Namba Nane ya Mwaka 2009; The Fertilizers Act, 2009 ni Sheria Namba Tisa ya 1 Mwaka 2009; The Insurance Act, 2009 ni Namba Kumi ya Mwaka 2009; The Water Resources Management, Act 2009 ni Namba Kumi na Moja ya Mwaka 2009; na Sheria Namba Kumi na Mbili ya Mwaka 2009 ni ile ya Water Supply and Sanitation Act, 2009. -
MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA NANE Kikao Cha Kumi Na Tano
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Kumi na Tano – Tarehe 3 Julai, 2007 (Kikao Kilianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI:- Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, mkiangalia Order Paper yetu ya leo, hati za kuwasilisha Mezani iko, Ofisi ya Makamu wa Rais, yuko Mwenyekiti wa Kamati ya Maliasili na Mazingira, tumemruka Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba na Sheria na Utawala, halafu atakuja Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MAZINGIRA): Hotuba ya Bajeti ya Wizari wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais kwa Mwaka wa Fedha wa 2007/2008. MWENYEKITI WA KAMATI YA MALIASILI NA MAZINGIRA: Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Maliasili na Mazingira kuhusu Utekelezaji wa Ofisi ya Makamu wa Rais kwa Mwaka wa Fedha uliopita pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Ofisi hiyo kwa Mwaka 2007/2008. MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA (MHE. RAMADHAN A. MANENO): Tarifa ya Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala kuhusu Utekelezaji wa Ofisi ya Makamu wa Rais – Muungano kwa mwaka wa Fedha 2006/2007 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2007/2008. MHE. RIZIKI OMARI JUMA (k.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI BUNGENI): 1 Maoni ya Kambi ya Upinzani kuhusu Utekelezaji wa Ofisi ya Makamu wa Rais kwa Mwaka wa Fedha uliopita pamoja Maoni ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Ofisi hiyo kwa Mwaka 2007/2008. -
Check Against Delivery HOTUBA YA WAZIRI MKUU, MHESHIMIWA
Check Against Delivery HOTUBA YA WAZIRI MKUU, MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA, (MB), WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA SITA WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, DODOMA, TAREHE 9 FEBRUARI, 2007 Mheshimiwa Spika, Mkutano wa sita wa Bunge lako Tukufu umehitimisha shughuli zote zilizokuwa zimepangwa. Mkutano huu ni wa kwanza baada ya Serikali ya Awamu ya Nne kutimiza mwaka mmoja madarakani. Taarifa za mafanikio na changamoto zilizojitokeza zimewasilishwa kupitia mikutano mbalimbali ya Chama Tawala, Serikali na vyombo mbalimbali vya habari. Mheshimiwa Spika, kwa masikitiko makubwa, nachukua nafasi hii tena kwa niaba ya Serikali na wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kutoa rambirambi kwako wewe Mheshimiwa Spika, kwa Waheshimiwa Wabunge wote, kwa familia, jamaa na marafiki kwa msiba uliotokana na kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tunduru, na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Bunge na Uratibu) Marehemu Juma Jamaldin Akukweti. Wote tulimfahamu Marehemu Akukweti kwa umakini na umahiri wake hapa Bungeni. Marehemu Akukweti alifariki kutokana na ajali ya ndege iliyokuwa inamrejesha Dar es Salaam baada ya kumaliza kazi ya kukagua soko la Mwanjelwa lililoteketea kwa moto mkoani Mbeya. Katika ajali hiyo Watumishi wa Serikali walipoteza maisha. Watumishi hao ni Bibi Theresia Nyantori, Mwandishi wa Habari wa Idara ya Habari; Bwana Nathaniel Katinila, Mratibu wa Mradi wa Masoko; na Bwana George Bendera, Afisa Habari Idara ya Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu. Majeruhi katika ajali hiyo ambao bado wanapata matibabu lakini wametoka hosptali ni Bw. Nisetas Kanje, Katibu wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Bunge na Uratibu); na rubani wa ndege hiyo Bw. Martin Sumari. Tunamwomba Mwenyezi Mungu awasaidie majeruhi wote waweze kupona haraka na kurudia katika afya zao. -
MKUTANO WA PILI Kikao Cha Tisa
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA PILI Kikao cha Tisa - Tarehe 17 Februari, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Taarifa ya mwaka ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali za Mitaa kwa mwaka wa fedha unaoishia tarehe 30 Juni, 2004. Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. MASWALI NA MAJIBU Na. 94 Uwekaji wa Lami Barabara ya Kigogo - Mabibo - Mandela - Tabata MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka lami kwenye barabara ya Kigogo- Mabibo hadi barabara ya Mandela kuelekea Tabata ili kupunguza msongamano wa magari katika barabara ya Morogoro? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima Mdee, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- 1 Mheshimiwa Spika, barabara ya Kigogo - Mabibo- Mandela kuelekea Tabata ni barabara ya mjini yaani urban road na inahudumiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Barabara hii ni muungano wa barabara tatu ambazo ni Kigogo - Mabibo, Mabibo - Mandela na Mandela - Tabata. Barabara hii imekuwa ikifanyiwa matengenezo ya mara kwa mara na Manispaa ya Kinondoni. Kwa mwaka 2005/2006 jumla ya shilingi 9,836,000 zilitumika kuweka kifusi kwenye sehemu korofi na kuichonga kwa greda. Mheshimiwa Spika, barabara hii inapitika isipokuwa katika mpaka wa Manispaa za Kinondoni na Ilala eneo la Tabata ambapo pana mkondo wa maji na hakuna daraja. -
TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity?
TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? With Partial Support from a TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? ACKNOWLEDGEMENTS This review was compiled and edited by Tanzania Development Research Group (TADREG) under the supervision of the Steering Group of Policy Forum members, and has been financially supported in part by Water Aid in Tanzania and Policy Forum core funders. The cartoons were drawn by Adam Lutta Published 2013 For more information and to order copies of the review please contact: Policy Forum P.O Box 38486 Dar es Salaam Tel: +255 22 2780200 Website: www.policyforum.or.tz Email: [email protected] ISBN: 978-9987 -708-09-3 © Policy Forum The conclusions drawn and views expressed on the basis of the data and analysis presented in this review do not necessarily reflect those of Policy Forum. Every effort has been made to verify the accuracy of the information contained in this review, including allegations. Nevertheless, Policy Forum cannot guarantee the accuracy and completeness of the contents. Whereas any part of this review may be reproduced providing it is properly sourced, Policy Forum cannot accept responsibility for the consequences of its use for other purposes or in other contexts. Designed by: Jamana Printers b TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? TABLE OF CONTENTS POLICY FORUM’s OBJECTIVES ............................................................................................................. -
1458125147-Hs-6-4-20
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA SITA Kikao cha Nne – Tarehe 3 Februari, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA MASOKO: Taarifa ya Mwaka na Hesabu zilizokaguliwa za Tume ya Ushindani kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010 [The Annual Report and Audited Accounts of Fair Competition Commission for the Financial year 2009/2010]. NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Serikali ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge juu ya Uendeshaji wa Sekta Ndogo ya Gesi Nchini. MASWALI NA MAJIBU Na. 39 Uwekezaji wa Kibiashara wa Nchi ya Libya Tanzania MHE. JOSEPH O. MBILINYI aliuliza:- Aliyekuwa Kiongozi wa Libya Marehemu Kanali Muamar Gaddafi, alijulikana sana kwa kuwekeza mabilioni ya dolla kwenye nchi mbalimbali za Kiafrika, kibiashara na kijamii kama hoteli, barabara na misikiti: (a) Je, Tanzania ilifaidikaje na uwekezaji wa Gaddafi kibiashara hapa nchini? (b) Kwa kuwa, Serikali ya Tanzania haitambui Serikali ya mpito ya Libya. Je, ni nani anayesimamia uwekezaji wa biashara wa Marehemu Kanali Gaddafi hapa nchini? NAIBU SPIKA: Ahsante sana, mabadiliko hayo hayabadilishi maudhui ya swali. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Osmund Mbilinyi, Mbunge wa Mbeya Mjini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo katika Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Marehemu Kanali Muammar Gaddafi hakuwahi binafsi kuwekeza kibiashara hapa nchini. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA SITA _________________ Kikao cha Thelathini na Mbili – Tarehe 18 Julai, 2009 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010. Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha kwa Mwaka wa Fedha 2007/2008 (The Annual Report and Accounts of Arusha International Conference Center for the Year 2007/2008) MWENYEKITI WA KAMATI YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA: Taarifa ya Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa Mwaka 2008/2009, pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010. MHE. HEMED MOHAMMED HEMED (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KWA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA): Taarifa kwa Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010. NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: 1 Randama za Makadirio ya Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010. HOJA ZA SERIKALI Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka 2009/2010 – Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA: Mheshimiwa Naibu Spika, kufuatia Taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), naomba kutoa hoja kwamba, Bunge lako Tukufu, likubali kujadili na kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010.