Tarehe 12 Mei, 2017

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

Tarehe 12 Mei, 2017 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Ishirini na Tatu – Tarehe 12 Mei, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Tukae. Katibu. NDG. ZAINAB ISSA – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kwa mwaka wa fedha 2017/2018. MWENYEKITI: Ahsante. Katibu 1 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. ZAINABU ISSA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU Na. 190 Malipo ya Wafanyakazi wa Kiwanda cha Chumvi – Uvinza MHE. HASNA S. K. MWILIMA aliuliza:- (a) Je, Serikali inawaeleza nini wafanyakazi wa Kiwanda cha Chumvi ambao walistaafishwa bila malipo ya kiinua mgongo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwabana wamiliki wa kiwanda hicho ili waboreshe mazingira ya kiwanda pamoja na mazingira ya wafanyakazi? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANA NA AJIRA) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hasna Sudi Katunda Mwilima, Mbunge wa Kigoma Kusini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, suala la wafanyakazi wa Kiwanda cha Chumvi ambao walistaafishwa bila malipo ya kiinua mgongo lilishashughulikiwa, ambapo wafanyakazi husika walilipwa mafao yao kwa mujibu wa sheria ikiwemo kiinua mgongo. Aidha, kwa kuzingatia Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 2 ya mwaka 2016 yaliyopitishwa na Bunge lako Tukufu wakati wa Kikao cha Bajeti, kama kuna mfanyakazi au wafanyakazi wanaoona kuwa hawakulipwa stahiki zao za kupunguzwa kazi ipasavyo, wanayo fursa ya kuwasilisha moja kwa moja madai yao kwenye Tume ya Usuluhishi na Uamuzi pasipo kupitishia kwa Kamishna wa Kazi. Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa Serikali ni kuendelea kuimarisha mikakati na huduma za usimamizi na 2 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) ukaguzi kazi kwa kuchukua hatua stahiki kwa waajiri wanokiuka sheria ili kuboresha mazingira ya kiwanda na mazingira ya wafanyakazi. Aidha, kupitia Marekebisho ya Sheria za Kazi ya mwaka 2016, Maafisa Kazi wamepewa mamlaka ya kuwatoza faini za papo kwa papo waajiri wanaokiuka sheria. Kanuni kwa sasa zinaandaliwa ili kuweka mwongozo na utaratibu mzuri wa utekelezaji wa suala hili. Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nivisihi vyama vya wafanyakazi nchini, navyo vitimize wajibu wao wa kutetea na kusimamia haki za wafanyakazi pamoja na kukuza tija na uzalishaji sehemu za kazi. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Hasna Mwilima, swali la nyongeza. MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nina masikitiko makubwa sana, itabidi Naibu Waziri anipe uhakika wa hao wafanyakazi 389 walilipwa lini na wapi. Mheshimiwa Naibu Spika, ninapoongea hivi nina ushahidi, suala hili hata Mheshimiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali analifahamu. Lilifanyiwa uhakiki, watu walitumwa kutoka Hazina wakaja Uvinza wakafanya uhakiki, wakaona kweli wafanyakazi hawa wana haki hawakulipwa mshahara wao wa mwisho na hawakulipwa nauli. Mheshimiwa Naibu Spika, kumefanyiwa uhakiki Mwanasheria Mkuu wa Serikali analifahamu bahati mbaya leo hayupo hapa, lakini analifahamu, alihakikisha na akatoa ushauri kwamba hawa wafanyakazi walipwe, wanadai zaidi ya shilingi milioni 320.9; je, Waziri yupo tayari kuniletea ushahidi kwamba walilipwa lini na nani, kwa sababu ninavyofahamu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha anayo haya madai juu ya meza yake? Swali langu la pili, Kiwanda cha Chumvi hivi tunavyoongea wamiliki wameuza kila kitu, wameuza vifaa vyote, wameuza vyuma, wameuza magari, wameuza 3 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) matofali, kila kitu. Tunajua kabisa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuimarisha viwanda, vilivyopo na kufufua vingine na kuhamasisha vingine ili viweze kujengwa. Swali langu ni kwa nini, kama dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuendeleza viwanda, leo tunaachia kiwanda kama kile cha chumvi ambacho wananchi wa Uvinza akina mama.. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa naomba umalize tafadhali. MHE. HASNA S. MWILIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu kwa nini wanaachia wamiliki wanaoendesha kiwanda hiki kufunga kiwanda kinyume na utaratibu? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANA NA AJIRA): Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza kuhusu kuleta orodha, jambo ambalo linaweza kufanyika hapa ambalo ni rahisi la kuweza kuwasaidia wafanyakazi wetu, katika majibu yangu ya msingi nilisema kama wako wale ambao wanahisi kwamba madai yao hayakulipwa ipasavyo na bado wana malalamiko, mimi na Mheshimiwa Mbunge tunaweza kuchukua hizi taarifa zote mbili tukazioanisha ili tupate muafaka wa kuweza kuwasaidia wafanyakazi hawa wa Kiwanda cha Chumvi. Kwa hiyo, nimuondoe hofu tu Dada yangu Mheshimiwa Mwilima kwamba nalichukua jambo lako kwa uzito mkubwa sana, na kwa namna alivyozungumza kwa masikitiko makubwa, na mimi niungane nae kwamba tutakwenda pamoja wote kuangalia arodha hii ili kama bado kuna mapungufu tutafanya kazi ya kushughulikia pamoja na taasisi husika. (Makofi) Mheshimiwa Naibu Spika, pili kuhusu kufunga viwanda na wakati tunasema nchi yetu ni ya uchumi na viwanda. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba hata hili nalo pia linahitaji kuweza kufahamu hasa changamoto ambazo 4 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) zimepelekea jambo hili kutokea, lakini nimuahidi tu kwamba chini ya Wizara ya Ofisi ya Waziri Mkuu, tunashughulikia masuala ya kazi na ajira na mategemeo yetu na matazamio yetu makubwa ni kuona kwamba viwanda vingi vinakuwepo, uwepo wa viwanda ndipo ajira zinatengenezwa. Mheshimiwa Mbunge hata katika taarifa ya ILO ya mwaka 2014 ya The Global Employment Trend inasema ya kwamba ili kuendelea kuongeza nafasi za ajira hasa kwa vijana ni vema tuwe na viwanda vingi zaidi. Ninakachokisema hapa ni kwamba, nakwenda kufuatilia kufahamu changamoto na tatizo ambalo limepelekea kiwanda hiki kufungwa ili tuweze kupata suluhisho la kudumu, vijana wa Kigoma waweze kupata ajira. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Japhary swali la nyongeza. MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwa kuwa suala la Kigoma – Uvinza lipo sawa la Kiwanda cha Magunia Moshi na Kiwanda cha Kiritimba ambapo nimeshauliza swali la msingi hapa Bungeni na Serikali ikajibu kwamba ipo tayari kwenda kuonana na wale wafanyakazi ambao hawakulipwa mafao yao ili waweze kuwaeleza, kwa nini hawakuwalipa na kama wamewalipa, waliwalipa kwa vipi. Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali inipe commitment kama ni lini itakwenda kuonana na wafanyakazi wa magunia waliostaafishwa na wafanyakazi wa Kiritimba wa Mkoa wa Kilimanjaro. Ahsante. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANA NA AJIRA): Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anahitaji commitment ya Serikali ya lini tutakwenda kuwaona na kusikiliza matatizo ambayo yanayowakabili wafanyakazi hawa, nimuahidi tu kwanza kwa kuanzia Jumatatu 5 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) nitamuagiza Afisa Kazi aliopo pale Moshi aende kukutana na Wafanyakazi hao na baada ya hapo akishanipatia taarifa kama kuna haja ya Naibu Waziri ama Waziri kwenda kufanya kazi hiyo basi nimtoe hofu Mbunge kwamba tutakwenda kuonana nao na tutatatua matatizo ambayo yanawakabili wafanyakazi hao. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Innocent Bashungwa, swali la nyongeza. MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kumekuwa na changamoto kubwa ya vijana ambao wanaajiriwa kwa mikataba ya muda mfupi kuzungushwa pale wanapoenda kwenye Mifuko ya Pensheni kudai mafao yao ili waweze kuyatumia kama mitaji ya kujiajiri. Kwa mfano, kule Karagwe Kampuni ya Ujenzi ya Chico iliajiri vijana kwa utaratibu wa mikataba ya vibarua, mpaka hivi sasa wanazungushwa vijana hawa. Je, Serikali inawasaidiaje vijana hawa kudai mafao yao ili waweze kutumia hela hii kama mitaji ya kujiajiri?(Makofi) NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu majibu. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue nafasi ya pekee sana kumpongeza Mheshimiwa Mbunge, kwa sababu amekuwa mstari wa mbele sana kufuatilia haki za wananchi katika Jimbo lake na hilo ni jambo jema. Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba tumekuwa na malalamiko ya namna moja ama nyingine ya wafanyakazi wa namna hiyo ambao wamekuwa wakiajiriwa kwa mikataba, mikataba yao 6 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) inapoisha walizoea kuwa na fao ambalo si fao sahihi lakini lililokuwa linaitwa fao la kujitoa. Baada ya kupitia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kifungu cha 11, lakini kupitia Sera ya Hifadhi ya Jamii katika nchi yetu na sheria tulizonazo, Serikali pamoja na wafanyakazi wenyewe na vyama vya wafanyakazi, tumekubaliana sasa kuna haja ya kuangalia namna nzuri ya kuwasaidia wafanyakazi wote ambao wamekuwa wakikumbwa na jambo hilo kwa kuanzisha fao lingine ambalo litaitwa ni Bima ya kukosa ajira. Mheshimiwa Naibu Spika, kazi hiyo tumeshaanza kuifanya vizuri kwa kushirikiana na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi, niwaombe wafanyakazi wote nchini ambao walikuwa wanaelekea katika fao hilo wavute subira ili matakwa ya kisheria yafanyiwe kazi na ndipo fao hilo litaanza kutolewa kwa mujibu wa sheria ambayo itakuwa imetungwa na Bunge. Pia ni maagizo ya Mheshimiwa Rais siku ya Mei Mosi alipokuwa pale Moshi ameendelea kusisitiza kwamba sasa tushughulikie suala hilo na liweze kufungwa kisheria na Wafanyakazi
Recommended publications
  • Tarehe 30 Machi, 2021
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Kwanza – Tarehe 30 Machi, 2021 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) WIMBO WA TAIFA NA WIMBO WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI (Hapa Kwaya ya Bunge iliimba Wimbo wa Taifa na Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: TAARIFA YA SPIKA NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nitaleta kwenu Taarifa ya Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Job Yustino Ndugai. Waheshimiwa Wabunge, kama ambavyo wote tunafahamu aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alifariki dunia tarehe 17 Machi, 2021 katika Hospitali ya Mzena, Jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Waheshimiwa Wabunge, kufuatia msiba huo wananchi wa Tanzania walipata fursa ya kutoa heshima za mwisho kama ifuatavyo; tarehe 20 hadi 21 Machi, 2021 Mkoani Dar es Salaam, tarehe 22 Machi, 2021 Mkoani Dodoma ambapo pia ilifanyika hafla ya kitaifa. Tarehe 23 Machi, 2021 ilikuwa Zanzibar na tarehe 24 Machi, 2021 ilikuwa mkoani Mwanza. Waheshimiwa Wabunge, nazisikia kelele sina hakika kama wote tuko pamoja kwenye jambo hili zito lililolipata Taifa letu. Tarehe 25 hadi 26 mkoani Geita na Chato. Waheshimiwa Wabunge, mazishi ya aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli yalifanyika siku ya Ijumaa tarehe 26 Machi, 2021 nyumbani kwake Chato, Mkoani Geita. Waheshimiwa Wabunge, kwa kuwa leo ni siku ya kwanza kwa Bunge hili kukutana tangu ulipotokea msiba huo naomba Waheshimiwa Wabunge tusimame kwa dakika moja ili kumkumbuka mpendwa wetu.
    [Show full text]
  • Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Kumi na Mbili - Tarehe 30 Machi, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali leo tunaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu, Mheshimiwa Conchesta Rwamlaza, atauliza swali la kwanza. Na. 117 Mwakilishi wa Wazee katika Vyombo vya Maamuzi MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza:- Kwa muda mrefu wazee wa nchi hii wamekuwa wakililia uwakilishi katika vyombo mbalimbali vya maamuzi kama vile Bunge, Halmashauri, Vijiji na kadhalika kama ilivyo kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu ili sauti zao zisikike:- Je, ni lini Serikali itasikia kilio cha wazee hawa? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, URATIBU NA BUNGE) alijibu:- Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Utaratibu wa kupata wawakilishi katika vyombo vya maamuzi kama vile Bunge, umeelezwa katika Ibara ya 66 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Ibara hii imefafanua aina za Wabunge na namna ya kuwapata. Utaratibu wa kuwapata wawakilishi katika Halmashauri umeelezwa 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) katika Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Sura ya 292 yaani The Local Authority Election Act, Cap. 292. Aidha, utaratibu wa kuwapata wawakilishi katika vijiji hutawaliwa na Sheria ya Serikali za Mitaa, Sura ya 287 na Sheria ya Serikali za Mitaa, Sura ya 288. Mheshimiwa Spika, wawakilishi wanaowakilisha makundi mbalimbali katika Bunge, Halmashauri na Vijiji, kwa mfano, wanawake, vijana, watu wenye ulemavu na kadhalika, wamekuwa wakipatikana kupitia mapendekezo yanayowasilishwa na vyama vya siasa kwenye vyombo vinavyosimamia uchaguzi katika ngazi hizo.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA TATU Kikao Cha Kumi Na Tisa – Tarehe 29 Aprili, 2021
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Kumi na Tisa – Tarehe 29 Aprili, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa, tukae. Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2021/2022. NAIBU WAZIRI WA MADINI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2021/2022. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. SAADA MONSOUR HUSSEIN - K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2020/2021 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2021/2022. NAIBU SPIKA: Ahsante sana. Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa maswali, tutaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Busega, sasa aulize swali lake. Na. 158 Serikali Kukamilisha Ujenzi wa Zahanati – Busega MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza:- Wananchi wa Kata ya Imalamate Wilayani Busega wamejenga zahanati na kumaliza maboma manne kwa maana ya zahanati moja kila kijiji:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi hao kuezeka maboma hayo ili waweze kupata huduma za afya kwenye zahanati hizo? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Dkt.
    [Show full text]
  • Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1
    Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Pili – Tarehe 13 Mei, 2015 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu! MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa, maswali tunaanza na ofisi ya Waziri Mkuu, anayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Josephine J. Genzabuke, kwa niaba yake Mheshimiwa Likokola! Na. 11 Fedha za Mfuko wa JK kwa Wajasiriamali Wadogo MHE. DEVOTHA M. LIKOKOLA (K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE) aliuliza:- Mfuko wa Wajasiriamali wadogowadogo maarufu kama mabilioni ya JK uliwavuta wengi sana lakini masharti ya kupata fedha hizo yamekuwa magumu:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kufanya mpango huo uwe endelevu kwa lengo la kuwanufaisha wanyonge? (b) Je, ni wananchi wangapi wa Mkoa wa Kigoma wamenufaika na mpango huo? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007, Serikali ilianzisha mpango wa uwezeshaji wananchi kiuchumi na kuongeza ajira kwa kutoa mikopo yenye masharti nafuu. Lengo la mpango huu ni kuwawezesha wananchi mijini na vijijini kupata mikopo ya kuanzisha au kuendeleza shughuli za kiuchumi ili kuongeza ajira na kipato. Masharti ya kupata mikopo hii si magumu sana ikilingalishwa na ile inayotolewa na mabenki, kwa sababu riba inayotozwa kwa mikopo hii ni asilimia 10, ikilinganishwa na riba inayotozwa na mabenki mengine, ambayo ni zaidi ya asilimia 20.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Mbili - Tarehe 22 Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kwa masikitiko makubwa natoa taarifa kwamba Mheshimiwa Mussa Hamisi Silima, Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar, jana Jumapili, tarehe 21 Agosti, 2011 majira ya jioni kama saa mbili kasorobo hivi walipokuwa wakirejea kutoka Dar es Salaam, yeye na familia yake walipata ajali mbaya sana katika eneo la Nzuguni, Mjini Dodoma. Katika ajali hiyo, mke wa Mbunge huyo aitwaye Mwanaheri Twalib amefariki dunia na mwili wa Marehemu upo hospitali ya Mkoa hapa Dodoma ukiandaliwa kupelekwa Zanzibar leo hii Jumatatu, tarehe 22 August, 2011 kwa mazishi yatanayotarajiwa kufanyanyika alasili ya leo. Kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Wabunge tusimame dakika chache tumkumbuke. (Heshima ya Marehemu, dakika moja) (Hapa Waheshimiwa Wabunge walisimama kwa dakika moja) Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, amina. Ahsanteni sana, tukae. Kwa hiyo sasa hivi tunavyoongea Mheshimiwa Mbunge ambae nae pia ameumia vibaya na dereva wake wanaondoka na ndege sasa hivi kusudi waweze kupata yanayohusika kule Dar es Salaam na pia kule watakuwa na watu wa kuwaangalia zaidi. Lakini walikwenda Zanzibar kumzika kaka yake na Marehemu huyu mama. Kwa hiyo, wamemzika marehemu basi wakawa wanawahi Bunge la leo ndiyo jana usiku wamepata ajali. Kwa hiyo, watakaokwenda kusindikiza msiba, ndege itaondoka kama saa tano watakwenda wafuatao, watakwenda Wabunge nane pamoja na mfawidhi zanzibar yeye anaongozana na mgonjwa sasa hivi lakini ataungana na wale kwenye mazishi.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Moja – Tarehe 5 Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Randama ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. NAIBU WAZIRI WA KAZI NA AJIRA: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kazi na Ajira kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. MHE. JENISTA J. MHAGAMA - MWENYEKITI WA KAMATI YA MAENDELEO YA JAMII: Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Jamii kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Kazi na Ajira kwa Mwaka 2010/2011 Pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. MHE. REGIA E. MTEMA - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KWA WIZARA YA KAZI NA AJIRA: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani juu ya Wizara ya Kazi na Ajira kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. MASWALI NA MAJIBU Na. 373 Kuboreshwa kwa Maslahi ya Madiwani MHE. FELISTER A. BURA aliuliza:- Madiwani ni nguzo muhimu katika kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi na nia ya Serikali ni kuboresha maslahi ya Madiwani iil waweze kutimiza wajibu wao ipasavyo;- Je, ni lini maslahi ya Madiwani yataboreshwa? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Felister Bura, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba, Waheshimiwa Madiwani ni nguzo muhimu katika kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA PILI Kikao Cha Nne – Tarehe 5 Februari, 2021 (Bunge
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA PILI Kikao cha Nne – Tarehe 5 Februari, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. ASIA MINJA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali tutaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini sasa aulize swali lake. Kwa niaba yake Mheshimiwa Innocent Bilakwate. Na. 42 Ujenzi wa Vituo vya Afya kwa Nguvu za Wananchi MHE. INNOCENT S. BILAKWATE (K.n.y. MHE. ALMAS A. MAIGE) aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Tabora Kaskazini wamejitolea kujenga Vituo vya Afya katika Kata za llolangulu, Mabama, Shitagena na Usagari katika Kijiji cha Migungumalo:- Je, Serikali ipo tayari kuanza kuchangia miradi hiyo? 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua mchango mkubwa wa wananchi katika ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya kote nchini. Hivyo, Serikali ina dhamira ya dhati ya kuchangia nguvu hizo za wananchi katika kukamilishaji vituo hivyo ili vianze kutoa huduma kwa wananchi. Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa ukarabati na ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya nchini ikiwemo kukamilisha maboma ya majengo ya kutolea huduma za afya yaliyojengwa na wananchi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, ambapo ujenzi wake ulisimama kwa kukosa fedha.
    [Show full text]
  • Tarehe 4 Aprili, 2017
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Kwanza – Tarehe 4 Aprili, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) WIMBO WA TAIFA (Hapa Waheshimiwa Wabunge Waliimba Wimbo wa Taifa) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Natoa nafasi kwa Waheshimiwa Wabunge mnaoingia, naomba mfanye haraka kidogo. Waheshimiwa Wabunge, nawakaribisha kwenye Mkutano wa Saba, Kikao cha Kwanza, Katibu! (Vigelegele) DKT. THOMAS KASHILILAH – KATIBU WA BUNGE: KIAPO CHA UAMINIFU Mheshimiwa Mbunge afuatae aliapa Kiapo cha Uaminifu:- Mhe. Salma Rashid Kikwete. (Vigelegele/Makofi) SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nashukuru kwa makofi yenu. Tuendelee sasa maana nilikuwa nasubiri kidogo nione mama anakaa wapi ili akisimama kwenye maswali 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) nijue yupo wapi maana leo nataka nimpe swali la kwanza. Katibu tuendelee! (Makofi/Kicheko/Vigelegele) DKT. THOMAS KASHILILAH – KATIBU WA BUNGE: TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, katika Mkutano wa Sita wa Bunge, Bunge lilipitisha Miswada ya Sheria ya Serikali miwili ifuatayo:- (i) Muswada wa Sheria ya Huduma ya Msaada wa Kisheria (The Legal Aid Bill, 2016); na (ii) Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na.4 wa Mwaka 2016 (The Written Laws (Miscellaneous Amendment) No. 4 Bill 2016) Kwa Taarifa hii, napenda kuliarifu Bunge hili Tukufu kwamba tayari Miswada hiyo miwili imepata kibali cha Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwa sheria za nchi zinazoitwa:- (i) Sheria ya Huduma ya Msaada wa Kisheria Na.1 ya Mwaka 2017 (The Legal Aid Act No.1, 2017); na (ii) Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na.4 ya Mwaka 2017 (The Written Laws (Miscellaneous Amendment) No.4, Act No.2 2017).
    [Show full text]
  • Tanzania Human Rights Report 2015 Tanzania Mainland Legal and Human Rights Centre (LHRC) Tanzania Human Rights Report 2015
    Tanzania Human Rights Report 2015 Tanzania Mainland Legal and Human Rights Centre (LHRC) Tanzania Human Rights Report 2015 Publishers Legal and Human Rights Centre Justice Lugakingira House, Kijitonyama P.O. Box 75254, Dar es Salaam, Tanzania Tel: +255222773038/48, Fax: +255222773037 Email: [email protected] Website: www.humanrights.or.tz Partners - LHRC Accountability in Tanzania (AcT) The Embassy of Norway The Embassy of Sweden ISBN: 978-9987-740-25-3 © LHRC 2016 - ii - Tanzania Human Rights Report 2015 Editorial Board Dr. Helen Kijo-Bisimba Adv. Imelda Urrio Ms. Felista Mauya Adv. Anna Henga Mr. Castor Kalemera Researchers/Writers Mr. Paul Mikongoti Mr. Pasience Mlowe Mr. Fundikila Wazambi Design & Layout Mr. Rodrick Maro - iii - Tanzania Human Rights Report 2015 Acknowledgement Legal and Human Rights Centre (LHRC) has been producing the Tanzania Human Rights Report, documenting the situation in Tanzania Mainland since 2002. In the preparation and production of this report LHRC receives both material and financial support from different players, such as the media, academic institutions, other CSOs, researchers and community members as well as development partners. These players have made it possible for LHRC to continue preparing the report due to its high demand. In preparing the Tanzania Human Rights Report 2015, LHRC received cooperation from the Judiciary, the Legislature and the Executive arms of the State. Various reports from different government departments and research findings have greatly contributed to the finalization of this report. Hansards and judicial decisions form the basis of arguments and observations made by the LHRC. The information was gathered through official correspondences with the relevant authorities, while other information was obtained online through various websites.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Nne - Tarehe 24 Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua NAIBU SPIKA:Waheshimiwa Wabunge, kufuatia kikao cha pamoja cha Kamati ya Uongozi na Tume ya Huduma za Bunge kilichofanyika jana mchana Wajumbe walikubaliana na kupanga utaratibu wa namna watakavyoshiriki katika mazishi ya Mheshimiwa Mussa Khamis Silima, yatakayofanyika leo tarehe 24 Mwezi wa Agosti 2011 Zanzibar. Walikubaliana kuwa mwili wa Marehemu uchukuliwe Dar es Salaam na kwenda Zanzibar moja kwa moja na Waheshimiwa Wabunge watasafirishwa kwa ndege itakayowachukua kutoka Dodoma hadi Zanzibar kwenye mazishi na kuwarudisha Dodoma baadaye leo hii. Vile vile, wajumbe walikubaliana kuwa makundi yafuatayo ndiyo yatakayokwenda kushiriki katika mazishi hayo. Kwanza Wajumbe wa Kamati ya Uongozi, pia Wajumbe wa Tume ya Huduma za Bunge, tatu wajumbe nane kutoka Zanzibar na nne ni baadhi ya Wabunge kutoka Kamati ya Nishati na Madini pamoja na Menejimenti ya Ofisi ya Bunge. Waheshimiwa Wabunge, kuhusu utaratibu wa usafiri ni kwamba Ofisi ya Katibu wa Bunge imepata ndege mbili, moja yenye uwezo wa kubeba abiria kumi na moja na nyingine yenye uwezo wa kubeba abiria 49 hivyo jumla ya watakaohudhuria mazishi ni 60. Ndege ya kwanza itakayoondoka itabeba abiria 11 kama nilivyosema na itaondoka Dodoma saa Nne asubuhi hii. Ndege ya pili itakayobeba abiria 49 itaondoka saa nne na nusu asubuhi ya leo. Wote wanaosafiri wanaombwa kufika uwanja wa ndege wa Dodoma kuanzia saa tatu na nusu asubuhi hii. Waheshimiwa Wabunge, shughuli za ibada na mazishi zitaanza saa sita na nusu mchana huko Zanzibar na mazishi yatafanyika saa saba mchana mara baada ya mazishi ndege zitaanza kuondoka kurudi Dodoma, Ndege inayobeba abiria 49 itaondoka Zanzibar kurudi Dodoma saa tisa alasiri.
    [Show full text]
  • Uongozi Kuanzia 1961
    UONGOZI KATIKA SEKTA YA MAJI TANZANIA BARA KUANZIA UHURU MWAKA 1961 HADI LEO Utangulizi: Orodha ya Uongozi katika Sekta ya Maji Tanzania bara kuanzia mwaka 1961 mpaka sasa. Kuanzia mwaka 1961 Tanzania ilipopata NA WAZIRI MWAKA NA KATIBU MKUU MWAKA uhuru wake, Sekta ya Maji imekuwa chini 1 Dereck Bryeson 1961 - 1964 1 Ibrahim Sapi Mkwawa 1962 - 1964 ya wizara mbalimbali. Jumla ya Wizara 2 Alhaji Tewa S. Tewa 1964 - 1966 2 Dickson A. Nkembo 1964 - 1965 3 Cleopa D. Msuya 1965 - 1967 20 ziliundwa kwa nyakati tofauti katika 3 Said A. Maswanya 1966 - 1968 4 Ernest A. Mulokozi 1967 - 1968 kipindi hicho ili kusimamia Sekta ya Maji. 5 David A. Mwakosya 1968 - 1968 Mwanzoni baada ya Uhuru, katika 4 Abdurahman Mohamed Babu 1968 - 1970 6 Awinia Mushi 1968 - 1969 muundo sekta ya maji ilikuwa ni Idara ya 7 Timothy Apiyo 1969 - 1970 Maji na Umwagiliaji ikiwa chini ya Wizara 5 Dkt. Wilbert Chagula 1971 - 1974 6 E. Elinawinga 1974 - 1975 8 Frederick Rwegarulila 1970 - 1978 ya Ardhi,Upimaji Ramani na Maji Dkt. Wilbert Chagula 1976 - 1978 (Ministry of Lands, Survey and Water) na E. Elinawinga 1978 - 1982 9 Harith B. Mwapachu 1978 - 1981 1981 - 1984 mwaka 1961 ilihamishiwa Wizara ya 7 Al Noor Kassum 1982 - 1986 10 Athumani Janguo 11 Fulgence M. Kazaura 1984 - 1985 Kilimo. 12 H. Z. Talawa 1985 - 1987 8 Dkt. Pius Yasebasi Ng’wandu 1986 - 1990 13 N. K. Nsimbira 1987 - 1990 Mwaka 1970 sekta ya maji iliweka 9 Christian Kisanji 1990 - 1990 14 Paul J. Mkanga 1990 - 1990 10 Jakaya Mrisho Kikwete 1990 - 1995 15 Prof.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Kumi na Nane – Tarehe 6 Julai, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (MAHUSIANO NA UTARATIBU): Mheshimiwa Spika, Kabla sijawasilisha Hati Mezani ninapenda kutumia dakika yako moja kutoa shukrani za dhati kabisa kwako. Kwanza kwa kuwa wa kwanza kutangaza msiba wa Mama yangu na vilevile kuwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge wote ambao wameniletea rambirambi kwa namna moja au nyingine kwa njia ya sms na kwa simu na hii imefanyika kwa wananchi wengi nchini kote. 1 Mheshimiwa Spika, ninawashukuru sana wote sina kitu cha kufanya isipokuwa kuwaambia kuwa asanteni sana, nimepata faraja na Mama yetu tumemwweka mahali pema katika nyumba yake ya milele. Kwa hiyo, baada ya maelezo hayo mafupi na kwa kuwapongeza na kuwashukuru wote naomba sasa kuwakilisha Hati Mezani. Taaarifa ya Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano, 2011/2012 - 2015/2016. NAIBU WAZIRI WA MAJI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha, 2012/2013. MASWALI NA MAJIBU Na.143 Serikali Kujenga Nyumba za Walimu MHE. SULEIMAN M. N. SULEIMAN (K.n.y. MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA) aliuliza:- Shule nyingi za msingi zina upungufu mkubwa wa nyumba za walimu hivyo kusababisha walimu kuishi katika mazingira magumu na kutoripoti katika shule kama Nyamsebhi, Mnekezi, Shibela, Kageye, Ntono na Nyasalala katika Jimbo la Busanda. 2 Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za walimu katika shule hizo na nyingine ili kuboresha mazingira ya walimu kufanya kazi? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lolesia Bukwimba, Mbunge wa Busanda kwa kutoa maelezo yafuatayo.
    [Show full text]