Media Watch Match 2021
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Thelathini Na Sita
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Sita – Tarehe 27 Mei, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nawaomba tukae. Waheshimiwa Wabunge tunaendelea na Mkutano wetu wa 15, leo ni Kikao cha 36. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NAIBU WAZIRI WA MADINI: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2019/2020. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. CATHERINE V. MAGIGE - K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI) Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu utekelezaji na Majukumu ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. MHE. TUNZA I. MALAPO - K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU WIZARA YA MADINI: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni juu ya Wizara ya Madini kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Tunza Malapo, tunakushukuru. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Tunaanza na TAMISEMI, swali la kwanza litaulizwa na Mheshimiwa Azza Hilal, Mbunge wa Viti Maalum - Shinyanga. -
Issued by the Britain-Tanzania Society No 124 Sept 2019
Tanzanian Affairs Issued by the Britain-Tanzania Society No 124 Sept 2019 Feathers Ruffled in CCM Plastic Bag Ban TSh 33 trillion annual budget Ben Taylor: FEATHERS RUFFLED IN CCM Two former Secretary Generals of the ruling party, CCM, Abdulrahman Kinana and Yusuf Makamba, stirred up a very public argument at the highest levels of the party in July. They wrote a letter to the Elders’ Council, an advisory body within the party, warning of the dangers that “unfounded allegations” in a tabloid newspaper pose to the party’s “unity, solidarity and tranquillity.” Selection of newspaper covers from July featuring the devloping story cover photo: President Magufuli visits the fish market in Dar-es-Salaam following the plastic bag ban (see page 5) - photo State House Politics 3 This refers to the frequent allegations by publisher, Mr Cyprian Musiba, in his newspapers and on social media, that several senior figures within the party were involved in a plot to undermine the leadership of President John Magufuli. The supposed plotters named by Mr Musiba include Kinana and Makamba, as well as former Foreign Affairs Minister, Bernard Membe, various opposition leaders, government officials and civil society activists. Mr Musiba has styled himself as a “media activist” seeking to “defend the President against a plot to sabotage him.” His publications have consistently backed President Magufuli and ferociously attacked many within the party and outside, on the basis of little or no evidence. Mr Makamba and Mr Kinana, who served as CCM’s secretary generals between 2009 to 2011 and 2012-2018 respectively, called on the party’s elders to intervene. -
20 MAY 2019.Pmd
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Moja – Tarehe 20 Mei, 2019 (Bunge Lilianza saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na Mkutano wetu wa 15, leo kikao cha 31. Katibu! NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nasikitika kuwatangazia kifo cha mwanasiasa mkongwe na kiongozi aliyepata kuhudumia kwa muda mrefu hasa kule kwenye Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Marehemu Ally Juma Shamhuna. Waheshimiwa Wabunge, katika uhai wake, marehemu Ally Juma Shamhuma amepata kushika nyadhifa mbalimbali zikiwemo hizi zifuatazo; amepata kuwa Mkurugenzi wa Mifugo, amewahi kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, amewahi kuwa Katibu Mkuu, Export Processing Zone Zanzibar, amewahi kuwa Waziri wa Mipango, amekuwa Waziri wa Nchi, Afisi ya Waziri Kiongozi, aliwahi kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo na wakati huo huo akiwa ni 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Naibu Waziri Kiongozi, katika uhai wake amekuwa Waziri wa Ardhi, Maji na Nishati na alipata kuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali. Aidha, Marehemu Mheshimiwa Shamhuna kwa muda mrefu alikuwa ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi kutokea Zanzibar na baadhi yenu humu Wabunge mtamkumbuka marehemu Mheshimiwa Shamhuna kama Mbunge wa Bunge la Katiba na alikuwa Mjumbe wa Kamati namba 8 kwenye Bunge la Katiba, Kamati ambayo nilikuwa Mwenyekiti wake. Kwa niaba yenu Waheshimiwa Wabunge, tunatoa pole kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Tunatoa pole kwa Wazanzibari wote na Watanzania wote kwa ujumla kufuatia kifo hicho na tunamuomba Mwenyezi Mungu aihifadhi roho yake mahali pema peponi, amina. -
Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA THELATHINI NA MBILI 23 MEI, 2017 MKUTANO WA SABA KIKAO CHA THELATHINI NA MBILI TAREHE 23 MEI, 2017 I. DUA: Mwenyekiti (Mhe. Mussa A. Zungu) alisoma Dua Saa 3.00 Asubuhi na kuongoza Bunge. Makatibu mezani: 1. Ndugu Joshua Chamwela 2. Ndugu Neema Msangi II. HATI ZA KUWASILISHA MEZANI (1) Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii – Mhe. Ramo Makani aliwasilisha Mezani:- - Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (2) Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii – Mhe. Khalifa Salum Suleiman aliwasilisha Mezani:- - Taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (3) Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kwa Wizara ya Maliasili na Utalii – Mhe. Roman Selasini aliwasilisha Mezani:- - Taarifa ya Upinzani kuhusu Wizara ya Maliasili na Utalii juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. 1 III. MASWALI Maswali yafuatayo yaliulizwa na kujibiwa:- WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO Swali Na. 254: Mhe. Ritta Kabati (Kny. Mhe. Mahmoud H. Mgimwa) Nyongeza: Mhe. Ritta Kabati Mhe. Elias J. Kwandikwa Mhe. James Mbatia Mhe. Venance Mwamoto Swali Na. 255: Mhe. Ignas A. Malocha Nyongeza: Mhe. Ignas A. Malocha Mhe. Oran Njenza Mhe. Omary T. Mgimba Mhe. Adamson E. Mwakasaka Mhe. Zuberi Kuchauka Mhe. -
MKUTANO WA PILI Kikao Cha Nne – Tarehe 5 Februari, 2021 (Bunge
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA PILI Kikao cha Nne – Tarehe 5 Februari, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. ASIA MINJA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali tutaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini sasa aulize swali lake. Kwa niaba yake Mheshimiwa Innocent Bilakwate. Na. 42 Ujenzi wa Vituo vya Afya kwa Nguvu za Wananchi MHE. INNOCENT S. BILAKWATE (K.n.y. MHE. ALMAS A. MAIGE) aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Tabora Kaskazini wamejitolea kujenga Vituo vya Afya katika Kata za llolangulu, Mabama, Shitagena na Usagari katika Kijiji cha Migungumalo:- Je, Serikali ipo tayari kuanza kuchangia miradi hiyo? 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua mchango mkubwa wa wananchi katika ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya kote nchini. Hivyo, Serikali ina dhamira ya dhati ya kuchangia nguvu hizo za wananchi katika kukamilishaji vituo hivyo ili vianze kutoa huduma kwa wananchi. Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa ukarabati na ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya nchini ikiwemo kukamilisha maboma ya majengo ya kutolea huduma za afya yaliyojengwa na wananchi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, ambapo ujenzi wake ulisimama kwa kukosa fedha. -
Tarehe 15 Aprili, 2019
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Kumi – Tarehe 15 Aprili, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA):- Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NAIBU SPIKA: Ahsante, Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali, tutaanza na Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mheshimiwa Kiza Hussein Mayeye, Mbunge wa Viti Maalum, sasa aulize swali lake. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Na. 78 Malipo Stahiki Kwa Walimu Waliopanda Daraja MHE. KIZA H. MAYEYE aliuliza:- Serikali imekuwa ikiwapandisha madaraja walimu lakini haitoi malipo stahiki kwa madaraja hayo mapya kwa kipindi kirefu tangu walipopandishwa madaraja yao:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba walimu wanapata stahiki zao mara wanapopandishwa madaraja? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kiza Hussein Mayeye, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilisitisha kupandisha walimu na watumishi wengine madaraja katika mwaka wa fedha 2015/2016 na 2016/2017 kutokana na uhakiki wa watumishi uliohusisha uhalali wa vyeti, elimu na ngazi za mishahara. -
Tarehe 27 Juni, 2019
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Hamsini na Nne – Tarehe 27 Juni, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu! NDG. ATHUMAN HUSSEIN – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Maelezo ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 3) wa Mwaka 2019 [The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (No.3) Bill, 2019]. MHE. NAJMA MURTAZA GIGA - MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA: Maoni ya Kamati ya Katiba na Sheria kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 3) wa Mwaka 2019 [The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (No.3) Bill, 2019]. MHE. JOSEPH R. SELASINI K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU WIZARA YA KATIBA NA SHERIA: 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Maoni ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu Wizara ya Katiba na Sheria juu ya Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 3) wa Mwaka 2019 [The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (No.3) Bill, 2019]. NAIBU SPIKA: Ahsante sana, nimuite Katibu. NDG. ATHUMAN HUSSEIN – KATIBU MEZANI: MISWADA YA SHERIA YA SERIKALI Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2019 (The Finance Bill, 2019) (Majadiliano Yanaendelea) NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tutaendelea na majadiliano kama ambavyo tulianza jana. Nahitaji nipate majina kutoka kwenye vyama vyenye uwakilishi kama kuna wachangiaji, lakini pia kama hawapo tunaweza kuendelea na ratiba yetu. -
1 Bunge La Tanzania
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI Kikao cha Tano – Tarehe 5 Februari, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae, Katibu. NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: KIAPO CHA UAMINIFU Mhe. Dkt. Adelardus Lubango Kilangi NAIBU SPIKA: Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- MHE. MOSHI S. KAKOSO - K.n.y MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA - K.n.y MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu shughuli za kamati kwa mwaka 2017. NAIBU SPIKA: Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU Na. 55 Changamoto Zinazowakabili Walemavu MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:- Watanzania wenye ulemavu wanakabiliwa na kero mbalimbali za kimaisha ikiwemo ukosefu wa ajira kama ilivyo kwa Watanzania wengine, aidha, zipo changamoto za jumla kama vile kijana mwenye ulemavu wa ngozi asiye na ajira ana changamoto ya mahitaji ya kujikimu na pia ana changamoto za kipekee za mahitaji ya kiafya na kiusalama. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu umuhimu wa kuwatazama vijana wenye ulemavu mbalimbali kwa namna ya pekee na kama zipo sera na mikakati ya kiujumla kwa vijana wote nchini? NAIBU SPIKA: Ofisi ya Waziri Mkuu sijui nani anayejibu maswali. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, niko hapa. -
Majadiliano Ya Bunge ______
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 7 Mei, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa tukae. Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na Kikao cha Ishirini na Tano cha Mkutano wetu wa Tatu. Katibu. NDG. NEEMA MSANGI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Ofisi ya Waziri Mkuu, swali la kwanza litaulizwa na Mheshimiwa Dkt. Alice Karungi Kaijage, Mbunge wa Viti Maalum, tafadhali. Na. 205 Kukitumia Kikamilifu Kitengo cha Kukuza Tija Kilichopo Ofisi ya Waziri Mkuu MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukitumia kikamilifu Kitengo cha Kukuza Tija kilichopo Ofisi ya Waziri Mkuu ili 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) kuhakikisha utekelezaji wa miradi mikubwa nchini unakuwa wa tija na kuwanufaisha Watanzania? SPIKA: Majibu ya swali hilo Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, tafadhali. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Alice Kapungi Kaijage, Mbunge wa Viti Maalum, CCM kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha Kitengo hiki kinatekeleza majukumu yake kikamilifu, Serikali imepanga kutekeleza mipango ifuatayo:- Moja, kuandaa Sera ya Taifa ya Tija na Ubunifu (National Productivity and Innovation Policy) ambayo itaweka mfumo thabiti wa kupima tija na ubunifu katika ngazi ya taasisi, sekta na Taifa ikiwa ni pamoja na miradi mikubwa ya Kitaifa. Pili, kuanzisha kanzidata ya makubaliano, matamko na taarifa za Kitaifa, Kikanda na Kimataifa kuhusu tija, ubunifu na ufanisi wa viwanda. -
Mwaka Wa Vipaji
jarida la Toleo la 09 WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO Limeandaliwa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini - GCU | www.habari.go.tz | Juni Mwaka wa Vipaji Wizara HabariTz Wizara_habaritz Wizara_HabariTZ Wiza ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo SERIKALI KUBORESHA MAZINGIRA YA SANAA NA MICHEZO Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katikati ya mwezi Juni 2021 akiwa Jijini Mwanza akizungumza na vijana alisema kuanzia mwezi Desemba mwaka huu wasanii wataanza kulipwa Mirabaha yao kupitia kazi za Sanaa zinazochezwa katika redio, runinga na mitandao ya kijamii. Kauli hiyo ya Mhe. Rais na Serikali imekuwa jibu la kilio cha wasani kwa muda mrefu, huku maamuzi hayo ya Serikali yamekuja wakati ambapo sekta ya Sanaa, Utamaduni na Michezo zinaa- jiri vijana wengi. “Tumeanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Michezo ili kusaidia timu zetu za Taifa, tumefuta kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) katika nyasi bandia. Hivyo, majiji na Manispaa changamkieni fursa hii kupata viwanja bora”. Pia Mheshimiwa Rais alilipigia chapuo suala hili. Aidha, Mhe. Rais alitoa wito kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kutumia fursa hiyo kuboresha viwanja ambavyo inavimiliki katika mikoa na majiji yote nchini ili kuweka mazingira sahihi ya kuendesha michezo nchini. Sisi Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo tunayachukulia maagizo ya Mhe. Rais aliy- oyatoa kwa Wizara akiwa Jijini Mwanza kwa uzito wake kuanzisha vituo vya michezo (Sports Academy) kila Mkoa ili kukuza vipaji na Sekta ya Michezo hapa nchini. Tunaamini maagizo haya yamekuja wakati sahihi kwa mfano suala la mrabaha lililokuwa kero kubwa kwa wasanii, ni vizuri wafanyabiashara, wadau wa wasanaa na jamii kwa ujumla tushiriki- ane kuhakikisha wasanii wanapata haki zao ili kuikuza sanaa ya kitanzania na kuibua fursa nyingi zaidi za ajira. -
MKUTANO WA PILI Kikao Cha Pili
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA PILI Kikao cha Pili - Tarehe 27 Januari, 2016 (Kikao kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Tunaendelea na Kikao cha Pili cha Mkutano wetu wa Pili. Katibu! NDG. JOHN N. JOEL – NAIBU KATIBU WA BUNGE: Kiapo cha Uaminifu! KIAPO CHA UAMINIFU Mheshimiwa Mbunge afuataye aliapa kiapo cha uaminifu. Mhe. Prof. Joyce Lazaro Ndalichako. SPIKA: Katibu! NDG. JOHN N. JOEL – NAIBU KATIBU WA BUNGE: Maswali! MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Maswali kwa siku ya leo tunaanza na Ofisi ya Mheshimiwa Rais (TAMISEMI) na swali la kwanza ni la Mheshimiwa Kiswaga Boniventura Destery, Mbunge wa Jimbo la Magu. 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Na. 16 Uhaba wa Nyumba za Walimu na Mishahara Midogo MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:- Nyumba za kuishi walimu ni chache katika maeneo yao ya kazi na mishahara yao pia ni midogo kuweza kumudu upangaji wa nyumba mitaani. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za walimu na kuboresha mishahara yao? NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA) alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kiswaga Boniventura Destery, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, mahitaji ya nyumba za walimu wa Shule za Msingi katika Halmashauri ya Magu ni 1,447, zilizopo ni nyumba 284 na upungufu ni nyumba 1,183. Aidha, Shule za Sekondari zina mahitaji ya nyumba 396, zilizopo ni nyumba 53 na upungufu ni nyumba 343. Mheshimiwa Spika, kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari ya Awamu ya Pili (MMES II), Halmashauri imepokea shilingi milioni 326.8 ambazo zitatumika kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya nyumba za walimu. -
Majadiliano Ya Bunge ___Mkutano Wa Kumi Na Tano
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Hamsini na Mbili – Tarehe 25 Juni, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tukae. Waheshimiwa Wabunge tunaendelea na Mkutano wetu wa Kumi na Tano, Kikao hiki cha leo ni cha Hamsini na Mbili, Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Maswali, tunaanza na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, swali la kwanza litauliza na Mheshimiwa Oscar Rwegasira Mukasa, Mbunge wa Biharamulo Magharibi. Mheshimiwa Mukasa, tafadhali kwa niaba yake nimekuona Mheshimiwa Shangazi. Na. 447 Mahitaji ya Ardhi na Upangaji wa Makazi – Mamlaka ya Mji Mdogo Biharamulo MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. OSCAR R. MUKASA) aliuliza:- Kata ya Biharamulo Mjini imetangazwa kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo hivi karibuni; kwa sasa kuna mahitaji makubwa ya upangaji wa ardhi na makazi hasa katika hadhi ya kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo:- 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Je, Serikali ipo tayari kuwaunga mkono wananchi wa Biharamulo Mjini wakati huu ambapo wao wenyewe wanaendelea na jitihada za ndani kuhakikisha wanakuwa na upangaji wa makazi unaoendana na hadhi mpya ya Mamlaka ya Mji Mdogo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oscar Rwegasira Mukasa, Mbunge wa Biharamulo Magharibi kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali ipo tayari kuwaunga mkono wananchi wa Mamlaka ya Mji Mdogo Biharamulo katika upangaji wa makazi ya mji huo.