Tarehe 6 Mei, 2016

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

Tarehe 6 Mei, 2016 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Kumi na Nne - Tarehe 6 Mei, 2016 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa fedha 2016/2017. MHE. VICKY P. KAMATA (K.n.y MWENYEKITI WA KAMATI YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA): Taarifa ya Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016, pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2016/2017. MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2016/2017. NAIBU SPIKA: Katibu! NDG. JOSHUA CHAMWELA- KATIBU MEZANI: Maswali. 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) MASWALI NA MAJIBU Na. 110 Utengenezaji wa Barabara ya Kutoka Njianne hadi Nandete kwa Kiwango cha Lami MHE. VEDASTO E. NGOMBALE aliuliza:- Moja ya matukio makubwa ya kihistoria katika nchi yetu ni vita ya Majimaji iliyopiganwa kati ya mwaka 1905 – 1907 kati ya Watanganyika na Wajerumani. Pamoja na kufahamu kwamba vita hivyo vilienea katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu, lakini vilianza katika Kijiji cha Nandete, Wilaya ya Kilwa; Serikali inaonesha jitihada mbalimbali ya kuienzi historia hiyo, ikiwa ni pamoja na kujenga mnara katika Kijiji hicho:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza barabara ya kutoka Njianne hadi Nandete kwa kiwango cha lami ili kulifanya eneo hilo la kihistoria kufikiwa kwa urahisi na kuliongezea umaarufu kwa kutembelewa na watalii hususani wa kutoka Ujerumani jambo ambalo litaiongezea mapato Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa na Taifa kwa ujumla. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vedasto Edgar Ngombale, Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa kujenga barabara ya lami kwenda eneo hili la kihistoria ni la msingi, lakini kwa sasa wakati Serikali inajenga barabara kuu zote nchini kwa kiwango cha lami hasa zikiunganisha Makao Makuu ya Mikoa yote. Hata hivyo, Serikali imekuwa ikitenga bajeti ya fedha kwa ajili ya matengenezo ili kuifanya ipitike wakati wote. Kupitia Wakala wa barabara Mkoa wa Lindi, katika mwaka wa fedha 2015/2016, zilitengwa shilingi milioni 58.8 kwa ajili ya matengenezo ya kawaida kilomita 43 na matengenezo ya muda maalum kwa kiwango cha changarawe urefu wa kilomita sita, kwa jumla ya gharama ya shilingi milioni 192.3. Matengenezo ya barabara hii yameanza chini ya Mkandarasi Ungando Contractors Company wa Kibiti – Rufiji. Aidha, katika bajeti ya mwaka 2016/2017, barabara hii iko katika mpango wa kufanyiwa matengenezo. 2 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa kilomita 10 zinazohudumiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, katika mwaka 2015/2016, zimetengwa shilingi milioni 70 ambazo zitatumika kwa ajili ya matengenezo ya muda maalum kwa urefu wa kilomita nane. Katika mwaka wa fedha 2016/2017, zimetengwa shilingi milioni 967.6 ambazo zitatumika kwa ajili ya matengenezo ya barabara katika Wilaya ya Kilwa. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Vesto Ngombale swali la nyongeza. MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa vita ya Majimaji au harakati za awali za kudai uhuru wa Tanganyika zilitokana na chokochoko na misingi imara ya kukataa kuonewa na kudai uhuru kulikofanywa na majemedari wetu wakati wa vita vya Majimaji. Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga barabara hii ili kuwawezesha Watanzania kwenda katika eneo hilo wakajifunze namna gani nchi yetu ilivyojengwa katika misingi ya kudai haki? (Makofi) Mheshimiwa Naibu Spika, pili, kwa kuwa barabara hii haipitiki kabisa Serikali ina mpango gani wa kuweka lami katika sehemu korofi kwa mfano mlima Ndundu, Mlima Ngoge pale Chumo, Mlima Kinywanyu na Mlima Karapina pale Kipatimu? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi kwamba umuhimu wa barabara hii na Mheshimiwa Mbunge amesema kwamba sehemu hii ndiyo chemichemi za harakati ya ukombozi wa nchi yetu. Naomba nikiri kwamba, kuna maeneo mengi sana ya kijiografia ambayo wakati wa uhuru kama Tanzania tulipokuwa tunaenda katika mchakato walishiriki kwa kiwango kikubwa sana katika kufanikisha uhuru wa nchi yetu, nawapongeza sana ndugu zetu wa Kilwa katika hilo. Mheshimiwa Naibu Spika, nakiri wazi kwamba kwa sababu umuhimu wa barabara hii kama nilivyosema awali katika jibu langu, tukirejea tena marejeo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi, lengo lake kubwa ni kuhakikisha wananchi wanafikiwa wa maeneo mbalimbali. Mheshimiwa Ngombale tutafanya juhudi siyo hapo Kilwa tu, isipokuwa maeneo mbalimbali. Ndiyo maana Ofisi ya Rais, TAMISEMI ilikuwa ikifanya mikakati katika maeneo mbalimbali, tulianza hasa katika miji tumeenda katika halmashauri, lengo letu ni kwamba maeneo mbalimbali yaweze kufikika chini ya miradi yetu ambayo sasa hivi tuna mradi wa TSP Project ambayo inahusisha ujenzi wa miundombinu ya barabara za lami katika maeneo mbalimbali. 3 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hili litakuwa katika mpango wetu, mkakati mpana wa kuhakikisha Halmashauri nyingi zinafikiwa na haya ni mambo ambayo tunayafikiria, ndiyo maana hata ukiangalia bajeti yetu ya mwaka huu tuna bajeti takribani ya bilioni 43 kwa ajili ya kuondoa vikwazo, lakini bilioni zaidi ya 200 kwa ajili ya kuhakikisha Halmashauri ziweze kufikiwa vizuri. Kwa hiyo, ni mambo ambayo Serikali yetu inayaangalia na ndani ya miaka mitano tuna imani tutafanya mambo makubwa sana. Mheshimiwa Naibu Spika, lakini lile la kuhusu sasa vile vipande korofi ikiwezekana viwekewe lami na najua Halmashauri ya Kilwa jinsi gani jiografia yake ilivyo na wakati mwingine malori yanashindwa kupanda. Tutawaelekeza wenzetu wa TANROAD ambao tunashirikiana nao kwa karibu zaidi na barabara takribani kilomita 48 zinahudumiwa na TANROAD, tutahakikisha Serikali inayapa kipaumbele yale maeneo korofi ambayo mvua ikinyesha barabara hazipitiki kwa kuyafikiria kwa jicho la karibu zaidi. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Gekul MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Pamoja na mikakati ya Serikali kujenga barabara za lami, lakini kuna ahadi ya Mheshimiwa Rais ambayo aliitoa katika maeneo yetu wakati anaomba kura, ya ujenzi wa barabara za lami. Katika Bunge hili tuliomba tupatiwe time frame kwamba ni muda gani hizi ahadi zinatekelezwa. Nataka kufahamu ni lini Mheshimiwa Waziri atatuletea ratiba ya ujenzi wa barabara hizo za lami kwa ahadi ya Rais ili tufuatilie kwa karibu ikiwemo Jimbo langu la Babati Mjini kilomita ishirini za lami? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, TAMISEMI jibu fupi tafadhali! NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ni lini, kifupi time frame ya ujenzi wa utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi, imeainishwa ndani ya miaka mitano 2015- 2020. Jukumu letu kubwa ni kuhakikisha ndani ya kipindi hiki zile ahadi ambazo tumeahidi kwa kadri ilani yetu ilivyojielekeza, tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo, ili mwisho wa siku tuone kwamba ilani yetu imetekelezwa kwa ajili ya kuwapatia wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania maendeleo ya kutosha na siyo Babati peke yake, isipokuwa kwa Tanzania nzima kwa mujibu wa Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi. 4 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Na. 111 Kurekebisha Mishahara ya Walimu Waliopandishwa Vyeo MHE. DOTO M. BITEKO aliuliza:- Je, kwa nini Serikali inachukua muda mrefu sana kurekebisha mishahara ya Walimu baada ya kupandishwa vyeo? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Doto Mashaka Biteko, Mbunge wa Bukombe, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba miaka ya nyuma kulikuwepo na ucheleweshaji wa kurekebisha mishahara kwa kuwa mfumo wa taarifa za kiutumishi na mishahara wa wakati huo ulimtaka kila Mwajiri kuwasilisha marekebisho ya Watumishi wake Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma. Mheshimiwa Naibu Spika, kuanzia mwaka 2012 Mfumo huu wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara uliimarishwa kutoka Toleo la 7 kwenda Toleo la 9 la Lawson ambapo mwajiri alisogezewa huduma ya kufanya marekebisho mbalimbali ya kiutumishi yanayotokea katika ofisi yake bila ya kulazimika kusafiri kwenda Dar es Salaam. Utaratibu huu umekuwa na manufaa ambapo kwa sasa mabadiliko mbalimbali ya kiutumishi yanafanywa na mwajiri kwa kuzingatia mzunguko wa malipo ya mishahara kwa kila mwezi. Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na utaratibu huu mzuri, mazingira machache yanayoweza kuchelewesha marekebisho ya mishahara kufanyika kwa wakati, kutokana na kuingizwa kwa taarifa za watumishi kwenye mfumo baada ya orodha ya malipo ya mishahara katika mwezi husika kufungwa, au waajiri kufanya mabadiliko bila ya kuweka taarifa muhimu hususan viambatisho kama vile barua za kupandishwa
Recommended publications
  • Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1 BUNGE LA TANZANIA
    Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ________________________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Kumi na Tisa – Tarehe 27 Mei, 2014 (Mkutano Ulianza Saa tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA: Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha kwa Mwaka 2012/2013 (The Annual Report and Accounts of Arusha International Conference Centre for the Year 2012/2013). Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. BETTY E. MACHANGU (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na Maoni ya Kamati 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. ABDULKARIM E.H. SHAH (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA ARDHI, MALIASILI NA MAZINGIRA): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015.
    [Show full text]
  • MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Thelathini Na Sita
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Sita – Tarehe 27 Mei, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nawaomba tukae. Waheshimiwa Wabunge tunaendelea na Mkutano wetu wa 15, leo ni Kikao cha 36. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NAIBU WAZIRI WA MADINI: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2019/2020. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. CATHERINE V. MAGIGE - K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI) Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu utekelezaji na Majukumu ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. MHE. TUNZA I. MALAPO - K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU WIZARA YA MADINI: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni juu ya Wizara ya Madini kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Tunza Malapo, tunakushukuru. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Tunaanza na TAMISEMI, swali la kwanza litaulizwa na Mheshimiwa Azza Hilal, Mbunge wa Viti Maalum - Shinyanga.
    [Show full text]
  • Issued by the Britain-Tanzania Society No 124 Sept 2019
    Tanzanian Affairs Issued by the Britain-Tanzania Society No 124 Sept 2019 Feathers Ruffled in CCM Plastic Bag Ban TSh 33 trillion annual budget Ben Taylor: FEATHERS RUFFLED IN CCM Two former Secretary Generals of the ruling party, CCM, Abdulrahman Kinana and Yusuf Makamba, stirred up a very public argument at the highest levels of the party in July. They wrote a letter to the Elders’ Council, an advisory body within the party, warning of the dangers that “unfounded allegations” in a tabloid newspaper pose to the party’s “unity, solidarity and tranquillity.” Selection of newspaper covers from July featuring the devloping story cover photo: President Magufuli visits the fish market in Dar-es-Salaam following the plastic bag ban (see page 5) - photo State House Politics 3 This refers to the frequent allegations by publisher, Mr Cyprian Musiba, in his newspapers and on social media, that several senior figures within the party were involved in a plot to undermine the leadership of President John Magufuli. The supposed plotters named by Mr Musiba include Kinana and Makamba, as well as former Foreign Affairs Minister, Bernard Membe, various opposition leaders, government officials and civil society activists. Mr Musiba has styled himself as a “media activist” seeking to “defend the President against a plot to sabotage him.” His publications have consistently backed President Magufuli and ferociously attacked many within the party and outside, on the basis of little or no evidence. Mr Makamba and Mr Kinana, who served as CCM’s secretary generals between 2009 to 2011 and 2012-2018 respectively, called on the party’s elders to intervene.
    [Show full text]
  • India-Tanzania Bilateral Relations
    INDIA-TANZANIA BILATERAL RELATIONS Tanzania and India have enjoyed traditionally close, friendly and co-operative relations. From the 1960s to the 1980s, the political relationship involved shared commitments to anti-colonialism, non-alignment as well as South-South Cooperation and close cooperation in international fora. The then President of Tanzania (Mwalimu) Dr. Julius Nyerere was held in high esteem in India; he was conferred the Jawaharlal Nehru Award for International Understanding for 1974, and the International Gandhi Peace Prize for 1995. In the post-Cold War period, India and Tanzania both initiated economic reform programmes around the same time alongside developing external relations aimed at broader international political and economic relations, developing international business linkages and inward foreign investment. In recent years, India-Tanzania ties have evolved into a modern and pragmatic relationship with sound political understanding, diversified economic engagement, people to people contacts in the field of education & healthcare, and development partnership in capacity building training, concessional credit lines and grant projects. The High Commission of India in Dar es Salaam has been operating since November 19, 1961 and the Consulate General of India in Zanzibar was set up on October 23, 1974. Recent high-level visits Prime Minister Mr. Narendra Modi paid a State Visit to Tanzania from 9-10 July 2016. He met the President of Tanzania, Dr. John Pombe Joseph Magufuli for bilateral talks after a ceremonial
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka.
    [Show full text]
  • Two Ideas for Cash on Delivery Aid for Education in Tanzania: a Briefing Note Nancy Birdsall, Rita Perakis and William Savedoff1
    Two ideas for Cash on Delivery Aid for Education in Tanzania: A Briefing Note Nancy Birdsall, Rita Perakis and William Savedoff1 Introduction This note outlines two possible ways for Tanzania and its development partners to implement a new foreign aid mechanism, Cash on Delivery Aid (COD Aid),2 that puts greater attention on outcomes and country ownership. Based on our research, the Government of Tanzania is in a good position to request support for its education sector in the form of a COD Aid agreement. The ideas presented here are meant to serve as a starting point for discussions in the hope that they might facilitate the design and implementation of such pilots. I. COD Aid for increased learning in primary education (early grades) Background In the past decade Tanzania has made tremendous strides in expanding primary and secondary schooling, and is on track to achieve the education Millennium Development Goal. However, assessments of school age children indicate alarmingly low levels of learning in Tanzania’s public primary schools. A majority of students cannot pass an assessment of basic literacy and numeracy – in Kiswahili, English and arithmetic, at the Standard II level. 3 For instance, 71.7 percent of Standard III students could not read a basic story in Kiswahili in 2011 (see table below). 1 This note is based on a visit to Tanzania from March 12 to 16, 2012, in collaboration with CGD partner Twaweza. It reflects discussions and inputs from a wide range of actors from government, civil society, universities and think tanks who were kind enough to take the time to meet with us.
    [Show full text]
  • MAWASILIANO SERIKALINI Mkuu Wa Kitengo Cha Florence Temba 022 2122942 0784246041 Mawasiliano Serikalini KITENGO CHA UGAVI NA UNUNUZI
    OFISI YA RAIS IKULU NA SEKRETARIETI YA BARAZA LA MAWAZIRI 1 Barabara ya Barack Obama, S.L.P 9120, 11400 Dar es Salaam Simu: 022 2116898/0222116900; Nukushi: 022 2128585 Email: [email protected]; Website http://www.statehouse.go.tz JINA KAMILI CHEO SIMU YA SIMU YA OFISINI MKONONI Mhe. Dkt.John Pombe Rais wa Jamhuri ya - - Magufuli Muungano wa Tanzania Mwandishi Mwendesha Mary G. Teu 022 211 6920 - Ofisi Rose E. Wabanhu Katibu Mahsusi 022 213 4924 - Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John William Mkuu wa Utumishi wa 022 211 6679 - Kijazi Umma na Katibu wa Baraza la Mawaziri Magdalena A. Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6679 - Kilongozi Mwandishi Mwendesha Eva Z. Mashallah 022 213 9649 - Ofisi Peter A. Ilomo Katibu Mkuu 022 211 0972 - Salma M. Mlinga Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 0972 - Mwandishi Mwendesha Euphrazia M. Magawa 022 212 9045 - Ofisi OFISI BINAFSI YA RAIS - Katibu wa Rais 022 211 6538 - Yunge P. Massa Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6538 - Joyce E. Pachi Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6538 - Muhidin A. Mboweto Naibu Katibu wa Rais 022 211 6908 - Usamba K. Faraja Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6908 - Katibu Msaidizi Lumbila M. Fyataga 022 211 6917 - Mwandamizi wa Rais Beatrice S. Mbaga Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6917 - Kassim A. Mtawa Katibu wa Rais Msaidizi 022 211 6917 - Alice M. Mkanula Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6917 - Col. Mbarak N. Mpambe wa Rais 022 211 6921 - Mkeremy Leons D. Nkama Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 116 921 - Rajabu O. Luhwavi Msaidizi wa Rais (Siasa) 022 212 8584 - Anande Z.
    [Show full text]
  • Land Tenure Reforms and Investment in Tanzania
    LAND TENURE REFORMS AND INVESTMENT IN TANZANIA Suzana Sylivester M.A. (Economics) Dissertation University of Dar es Salaam September, 2013 LAND TENURE REFORMS AND INVESTMENT IN TANZANIA By Suzana Sylivester A Dissertation Submitted in (Partial) Fulfillment of the Requirements for the Degree of Master of Arts (Economics) of the University of Dar es Salaam University of Dar es Salaam September, 2013 i CERTIFICATION The undersigned certifies that he has read and hereby recommends for the acceptance by the University of Dar es Salaam a dissertation entitled: Land Tenure Reforms and Investment in Tanzania, in partial fulfillment for the degree of Masters of Arts (Economics) of the University of Dar es Salaam. ……………………………………………… Dr. Razack B. Lokina (Supervisor) Date: ………………………………….. ii DECLARATION AND COPYRIGHT I, Sylivester Suzana, declare that this dissertation is my own original work and that it has not been presented and will not be presented to any other university for a similar or any other degree award. Signature ………………………………………….. This thesis is copyright material protected under the Berne Convention, the copyright Act 1999 and other International and national enactments, in that behalf on intellectual property. It may not be produced by any means, in full or in part, except for short extracts in fair dealings, for research or private study, critical scholarly review or discourse with an acknowledgement, without the written permission of Director of Postgraduate Studies, on behalf of both the author and the University of Dar es Salaam. iii ACKNOWLEDGEMENT I would like to give my special thanks to Almighty God for the Gift of life. My study has been successful by his Grace “I will glorify his name” This study could not have been written without the help of so many people and institutions, beginning with the UDSM-Sida Natural Resources and Governance Program, Department of Economics and EFD-Tanzania for their financial support.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 18 Julai, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita muuliza swali la kwanza nina matangazo kuhusu wageni, kwanza wale vijana wanafunzi kutoka shule ya sekondari, naona tangazo halisomeki vizuri, naomba tu wanafunzi na walimu msimame ili Waheshimiwa Wabunge waweze kuwatambua. Tunafurahi sana walimu na wanafunzi wa shule zetu za hapa nchini Tanzania mnapokuja hapa Bungeni kujionea wenyewe demokrasia ya nchi yetu inavyofanya kazi. Karibuni sana. Wapo Makatibu 26 wa UWT, ambao wamekuja kwenye Semina ya Utetezi na Ushawishi kwa Harakati za Wanawake inayofanyika Dodoma CCT wale pale mkono wangu wakulia karibuni sana kina mama tunawatakia mema katika semina yenu, ili ilete mafanikio na ipige hatua mbele katika kumkomboa mwanamke wa Tanzania, ahsanteni sana. Hawa ni wageni ambao tumetaarifiwa na Mheshimiwa Shamsa Selengia Mwangunga, Naibu Waziri wa Maji. Wageni wengine nitawatamka kadri nitakavyopata taarifa, kwa sababu wamechelewa kuleta taarifa. Na. 223 Barabara Toka KIA – Mererani MHE. DORA H. MUSHI aliuliza:- Kwa kuwa, Mererani ni Controlled Area na ipo kwenye mpango wa Special Economic Zone na kwa kuwa Tanzanite ni madini pekee duniani yanayochimbwa huko Mererani na inajulikana kote ulimwenguni kutokana na madini hayo, lakini barabara inayotoka KIA kwenda Mererani ni mbaya sana
    [Show full text]
  • Annual Report 2016
    ECONOMIC AND SOCIAL RESEARCH FOUNDATION (ESRF) Annual Report 2016 Economic and Social Research Foundation (ESRF) 51 Uporoto Street, off Ali Hassan Mwinyi Road P.O. Box 31226, Dar es Salaam, Tanzania Tel: (255-22) 2926084-9 Fax: (255-22) 2926083 E-mail: [email protected] Website: www.esrftz.org ESRF Managed Websites: (Tanzania Online): www.tzonline.org Tanzania Knowledge Network (TAKNET): www.taknet.ortz ESRF ANNUAL REPORT 2016 i TABLE OF CONTENTS LIST OF ABBREVIATIONS .................................................................................................v ACKNOWLEDGEMENT .....................................................................................................vi NOTE FROM THE EXECUTIVE DIRECTOR.......................................................................1 1. INTRODUCTION ..........................................................................................................4 1.1 About the Economic and Social Research Foundation ......................................... 5 1.2 The Mandate of ESRF ........................................................................................................ 5 1.3 ESRF’s Strategic Objectives .............................................................................................. 6 1.4 Country Context in 2016 .................................................................................................. 6 2. THE MEDIUM TERM STRATEGIC PLAN 2016-2020 .............................................8 2.1 Inclusive growth, employment and industrialization .............................................
    [Show full text]
  • Unlikely Allies? the Intersections of Conservation and Extraction in Tanzania
    Unlikely Allies? The Intersections of Conservation and Extraction in Tanzania Devin Holterman A DISSERTATION SUBMITTED TO THE FACULTY OF GRADUATE STUDIES IN PARTIAL FULFILLMENT OF THE REQUIREMENTS FOR THE DEGREE OF DOCTOR OF PHILOSOPHY Graduate Program in Geography York University Toronto, Ontario October 2020 © Devin Holterman, 2020 Abstract Tanzania is largely considered the epicenter of the Second Poaching Crisis, having experienced dramatic declines in wildlife populations, in particular elephants. In response, the country has established a new (para)military wildlife authority, enhanced international partnerships and projects aimed at curbing illegal elephant killings, and embarked on widespread anti-poaching operations as part of the country’s so-called “war on poaching.” Attuned to these characteristics of green militarization and the conditions of biodiversity crisis in Tanzania, this dissertation examines the emergence of anti-poaching partnerships between conservation and extractive industry actors. Based on 11 months of research in Tanzania, focusing specifically on the Selous Game Reserve, I illustrate that mainstream state and non-state conservation efforts, under the conditions of biodiversity crisis, enable the expansion of the mining, oil and gas industries. Building on this argument, the dissertation offers three contributions to political ecological and broader critical geographical scholarship. First, I show how Tanzania’s categorization of the poacher as an “economic saboteur” who threatens the national economy forms one aspect of a broader economic rationale directing the country’s increasingly militarized approach to conservation. Such an economic rationale, utilized by both state and non-state conservation actors, authorizes controversial partnerships with the extractive industries. Second, I show how Tanzania’s militarization of conservation is enabled in part by extractive industry actors who, in addition to securing access to its desired mineral deposits, temporarily “fix” the broader social and political crises facing the industry.
    [Show full text]
  • 20 MAY 2019.Pmd
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Moja – Tarehe 20 Mei, 2019 (Bunge Lilianza saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na Mkutano wetu wa 15, leo kikao cha 31. Katibu! NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nasikitika kuwatangazia kifo cha mwanasiasa mkongwe na kiongozi aliyepata kuhudumia kwa muda mrefu hasa kule kwenye Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Marehemu Ally Juma Shamhuna. Waheshimiwa Wabunge, katika uhai wake, marehemu Ally Juma Shamhuma amepata kushika nyadhifa mbalimbali zikiwemo hizi zifuatazo; amepata kuwa Mkurugenzi wa Mifugo, amewahi kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, amewahi kuwa Katibu Mkuu, Export Processing Zone Zanzibar, amewahi kuwa Waziri wa Mipango, amekuwa Waziri wa Nchi, Afisi ya Waziri Kiongozi, aliwahi kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo na wakati huo huo akiwa ni 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Naibu Waziri Kiongozi, katika uhai wake amekuwa Waziri wa Ardhi, Maji na Nishati na alipata kuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali. Aidha, Marehemu Mheshimiwa Shamhuna kwa muda mrefu alikuwa ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi kutokea Zanzibar na baadhi yenu humu Wabunge mtamkumbuka marehemu Mheshimiwa Shamhuna kama Mbunge wa Bunge la Katiba na alikuwa Mjumbe wa Kamati namba 8 kwenye Bunge la Katiba, Kamati ambayo nilikuwa Mwenyekiti wake. Kwa niaba yenu Waheshimiwa Wabunge, tunatoa pole kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Tunatoa pole kwa Wazanzibari wote na Watanzania wote kwa ujumla kufuatia kifo hicho na tunamuomba Mwenyezi Mungu aihifadhi roho yake mahali pema peponi, amina.
    [Show full text]