30 Oktoba, 2013

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

30 Oktoba, 2013 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA TATU Kikao cha Pili - Tarehe 30 Oktoba, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- MWENYEKITI WA KAMATI YA BAJETI: Maoni ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti juu ya Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka 2014/2015. MHE. DAVID E. SILINDE (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA FEDHA NA UCHUMI): Maoni ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Fedha na Uchumi juu ya Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka 2014/2015. 1 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaanza na Maswali, Ofisi ya Waziri Mkuu na atakayeuliza swali letu la kwanza ni Mheshimiwa Ismail Aden Rage. MHE. ISMAIL A. RAGE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana awali ya yote ninakupa pole ya msiba uliopata na ninaomba swali sasa lijibiwe. Na.15 Kusimama kwa Ujenzi wa Hospitali ya Kitete MHE. ISMAIL A. RAGE aliuliza:- Hospitali ya Kitete ilikuwa kwenye ukarabati lakini Mkandarasi amesimama muda mrefu:- Je, Serikali ni nini hatma ya kukamilisha majengo hayo? SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Waziri majibu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA(ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ismail Aden Rage, Mbunge wa Tabora Mjini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, ukarabati wa miundombinu katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora Kitete unafanyika kwa hisani ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB), utekelezaji wa mradi huu katika awamu ya kwanza ulianza tarehe 1/8/2009 na ulitakiwa kukamilika tarehe 27/4/2011. 2 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) Katika kutekeleza awamu hii, Wizara ya Afya ya ustawi wa jamii ilifanya mchakato wa kupata mkandarasi wa kutekeleza mradi huu ambapo kampuni ya Humphrey Construction Ltd. ilishinda zabuni. Mheshimiwa Spika, sababu za kusimama kwa mradi huu ni Mkandarasi kushindwa kutimiza masharti ya mkataba wake kama ilivyokusudiwa. Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Tabora alikagua mradi huo mwezi Julai, 2012 na kuagiza Mkandarasi awe amekamilisha kazi hiyo ifikapo Agosti, 2012. Hata hivyo, Mkandarasi alishindwa kukamilisha kazi hiyo. Hatua ambayo Serikali ilikusudia kuchukua ni kusitisha mkataba wake na kutafuta Mkandarasi mwingine. Mheshimiwa Spika, kabla ya kutangaza upya kazi hiyo, Serikali iliendelea na zoezi la kufanya tathimini ya kazi zilizobaki ili kujua gharama halisi za kukamilisha mradi huo ambao kwa sasa umesimama. Mradi huu unatarajiwa kukamilika ifikapo Juni, 2014. MHE. ISMAIL A. RAGE: Mheshimiwa Spika, nina masikitiko makubwa sana kwa sababu majibu niliyoyapata hayakunifurahisha wala hayakuniridhisha, mimi binafsi nimefika mpaka Wizarani nikaonana na Idara inayohusika na masuala ya ukarabati jambo la kushangaza Hospitali hii ya Tabora ndiyo Hospitali ya Rufaa na ndiyo Hospitali ya Manispaa inayotegemewa, matokeo yake imeshindwa kutoa huduma kwa wananchi na wananchi wamekosa imani na watendaji wa Hospitali hiyo. Je, haioni kuwa sasa ni wakati muafaka Waziri atamke katika Bunge hili rasmi Mkandarasi mpya ambaye ninaambiwa amekwishapatikana ataanza kazi lini na itakwisha lini? Mheshimiwa Spika, hela zipo ni za Africa Development Bank na Serikali inachangia na kwenye Bajeti iliyopita tulitenga pesa kwa ajili hiyo, ni maswali hayo tu Mheshimiwa Spika. 3 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII: Mheshimiwa Spika, ninapenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Rage kama ifuatavyo:- Kilichochelewesha kupatikana kwa Mkandarasi mpya ili aanze kazi mara moja ni utaratibu wa Kisheria wa kuvunja Mkataba wa Mkandarasi wa kwanza. Lakini ninapenda kutoa taarifa kwamba hatua hiyo imeshakamilika yule Mkandarasi wa kwanza Mkataba wake umeshavunjwa. Mkandarasi wa pili ameshapatikana kwa sababu wamechukua walewale ambao wamefanya kazi katika sehemu nyingine na wakafanya kwa ufanisi. Kwa hiyo, walifanya selective tendering na imeshakamilika muda wowote kuanzia sasa atakwenda katika eneo ili akakamilishe hatua iliyobaki. Ninaomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira na tutampa tarehe kwa ufasaha baada ya kutoka hapa. MHE. SUSAN A. LYIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii kuuliza swali dogo la nyongeza. Suala alilozungumzia Mheshimiwa Rage linafanana sana na tatizo la Hospitali ya Mkoa wa Kilimanjaro ya Mawenzi ambayo kwa muda mrefu imefanyiwa ukarabati lakini kubwa zaidi ni ujenzi wa theater kwa ajili ya akina mama ambayo imechukua muda mrefu sana, hivyo kusababisha akina mama wengi kupoteza maisha wakati wanapopelekwa KCMC au hospitali nyingine. Nilitaka maelezo au kauli ya Serikali ni lini theater hiyo itamalizwa ili akina mama wasipate matatizo kama ambavyo yanapatikana sasa hivi, hususani ya vifo? SPIKA: Mheshimiwa Waziri maelezo. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA(ELIMU): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Suzan Lyimo, kama ifuatavyo:- 4 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) Mara nyingi tumekuwa tukizungumza katika Bunge hili suala la ujenzi wa Hospitali ya Mawenzi na hasa ukamilishaji wa theater na majengo mengine. Jambo hili bado lipo linashughulikiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro na kwa maana hiyo tunayo nafasi ya kupata maelezo kutoka kwa Katibu Tawala wa Mkoa. Ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa baada ya session hii ya maswali tutafanya mawasiliano na Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro ili nijue position ya ujenzi inayoendelea kwa sasa ili tupate majibu sahihi. Mheshimiwa Spika, tutafanya msukumo mkubwa kwa hatua iliyobaki ili jambo hili liweze kukamilika mara moja. SPIKA: Ahsante, Mheshimiwa Kabati sasa na wewe utauliza kuhusu Hospitali ya Iringa halafu mnasema yanafanana, haya Mheshimiwa Kabati. MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, Hospitali ya Wilaya iliyopo katika Manispaa ya Iringa ilianzishwa ili kupunguza msongamano uliopo katika Hospitali Kuu na kwa kuwa sasa hivi kuna ujenzi ambao unaendelea wa mawodi ya kulaza wazazi. Ni lini Serikali itatuletea pesa ili kukamilisha ujenzi huo kwa sababu kuna nguvu ya wananchi na ya Manispaa ambayo imeshatumika kwa muda mrefu? Ili msongamano huo uishe unategemeana na kukamilishwa kwa hayo mawodi. SPIKA: Maswali ya namna hiyo mkipata majibu hayaridhishi mkubali, Mheshimiwa Naibu Waziri kwa sababu hayafanani na lile la kwanza. 5 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA(ELIMU): Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa Sera ya Serikali ya ukamilishaji wa Zahanati katika kila Kijiji na vituo vya afya katika kila Kata na Hospitali za Wilaya katika ngazi za Wilaya bado unaendelea na uimarishaji unaendelea, kupitia Bajeti yetu ya mwaka huu tumetenga fedha kupitia mipango miwili. Kuna basket fund kwa ajili ya ukamilishaji wa miundombinu na vifaa tiba. Lakini pia tuna MAM ambayo inashughulikia ukarabati ambao kwa sasa tumeshafanya mgao na kwa kuwa swali limekuja sasa nitafanya mapitio ya kuona ni kiasi gani cha fedha tulitenga kwa ajili ya Mkoa wa Iringa na Hospitali ya Wilaya ili tuweze kukamilisha kazi hiyo. SPIKA: Ahsante tunaendelea na Mheshimiwa Paul Lwanji kwa swali linalofuata. Na. 16 Ahadi ya Kuupatia Mji wa Itigi Maji ya Kutosha MHE. JOHN P. LWANJI aliuliza:- Mheshimiwa Rais alitoa ahadi ya kuupatia Mji wa Itigi maji ya kutosha. Je, Serikali imefikia wapi katika kutekeleza ahadi hiyo. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa John Paul Lwanji, Mbunge wa Manyoni Magharibi, kama ifuatavyo:- 6 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) Mheshimiwa Spika, ni kweli mnamo mwezi Novemba, 2012 Mheshimiwa Rais akiwa katika ziara katika Mji wa Itigi alitoa maagizo kwa uongozi wa Mkoa na Wilaya kushughulikia Mji wa Itigi. Mahitaji ya maji kwa wakazi wa Mji huo ni lita 1,300,000 kwa siku. Mheshimiwa Spika, ili kutekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kuwapatia maji wananchi wa Mji wa Itigi, Halmashauri katika Bajeti ya mwaka 2013/2014 kupitia programu ya Tekeleza kwa matokeo Makubwa Sasa (BRN), ilidhinishwa shilingi 258,000,000 kwa ajili ya kufanya ukarabati wa visima viwili ambavyo ni SG 37/73 na SG 15/73. Ukarabati huu utaongeza upatikanaji wa huduma ya maji kwa asilimia 25 ya mahitaji. Mheshimiwa Spika, awamu ya pili ya programu ya Kuendeleza Sekta ya Maji (WSDP) kwa mwaka 2014/2015 Mji wa Itigi utapewa kipaumbele katika mradi itakayotekelezwa kupitia utaratibu wa maji mjini. Katika awamu hii kazi itakuwa ni kufanya usanifu upya ili kupata vyanzo vya maji vya uhakika vitakavyokidhi mahitaji ya maji kwa wakazi wa eneo hilo la Itigi. MHE.JOHN P. LWANJI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina swali moja la nyongeza. Mkutano wa Bunge uliopita Naibu Waziri wa Maji alipata nafasi ya kutembelea Mji wa Itigi na akajionea tatizo kubwa la maji ukilinganisha na idadi ya wakazi wa Mji huo. Mimi ningependa kujua katika Bajeti ya 2013/2014 kila Mbunge aligombea sana na tukaongeza Bajeti Wizara hii ya Maji ziliongezwa shilingi bilioni 184.5. Tunachohitaji katika Mji wa Itigi ni shilingi milioni 200 ningependa kujua katika nyongeza hiyo sisi katika Jimbo la Manyoni Magharibi tumepata kiasi gani na kwa nini Serikali
Recommended publications
  • MKUTANO WA TATU Kikao Cha Hamsini Na Sita
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Hamsini na Sita – Tarehe 22 Juni, 2021 (Bunge Lilianza saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba tukae. Waheshimiwa tunaendelea na Mkutano wetu wa Tatu, leo ni Kikao cha Hamsini na Sita na kabla hatujaendelea nitumie nafasi hii kuwashukuru sana wasaidizi wangu wote wakiongozwa na Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa David Kihenzile, Mheshimiwa Zungu na Mheshimiwa Najma kwa kazi nzuri ambayo wameifanya wiki nzima kutuendeshea mjadala wetu wa bajeti. (Makofi) Sasa leo hapa ndio siku ya maamuzi ambayo kila Mbunge anapaswa kuwa humu ndani, kwa Mbunge ambaye Spika hana taarifa yake na hatapiga kura hapa leo hilo la kwake yeye. (Makofi) Katibu. NDG. NENELWA MWIHAMBI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Maswali na tunaanza na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Kwela. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Na. 465 Ujenzi wa Makao Makuu ya Halmashauri Katika Mji wa Laela MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi za Makao Makuu ya Halmashauri ya Sumbawanga katika Mji wa Laela baada ya agizo la Serikali la kuhamisha Makao Makuu? SPIKA: Majibu ya swali hilo muhimu la watu wa Kwela, Mheshimiwa Naibu Waziri - TAMISEMI, Mheshimiwa Dkt. Festo Dugange tafadhali. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Jimbo la Kwela kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ni miongoni mwa Halmashauri 30 zilizohamia kwenye maeneo mapya ya utawala mwaka 2019.
    [Show full text]
  • Tarehe 4 Februari, 2013
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA KUMI Kikao cha Tano – Tarehe 4 Februari, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 53 Hospitali ya Wilaya ya Nyang’hwale Kupatiwa Watumishi MHE. JOSEPHINE T. CHAGULLA aliuliza:- Hospitali ya Karumwa ambayo ni ya Wilaya mpya ya Nyang’hwale haina watumishi wa kutosha kwani ina daktari mmoja, Manesi watatu na mtaalam mmoja wa Maabara:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka watumishi wa kutosha katika hospitali hiyo? 1 NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Tabitha Chagulla, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Kituo cha Afya, Karumwa kilichoko katika Wilaya mpya ya Nyang’hwale kina Daktari mmoja, Manesi watatu na Mtaalam mmoja wa maabara. Kutokana na tatizo la upungufu wa watumishi wa sekta ya afya kuwepo katika hospitali, vituo vya afya na Zahanati zote nchini kikiwemo kituo cha afya Karumwa, Serikali imechukua jitihada za makusudi kuhakikisha kuwa udhahili wa wanafunzi wanaojiunga na fani za Udaktari na Uuguzi unaongezeka katika vyuo vikuu na vyuo vya ngazi ya Diploma na cheti. Aidha, Serikali imerejesha kada za chini za afya zilizokuwa zimefutwa. Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na jitihada hizo, hivi sasa Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inawapanga wahitimu wa fani za afya moja kwa moja katika vituo vya kazi baada ya kibali kutolewa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka.
    [Show full text]
  • Tarehe 15 Aprili, 2011
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Nane – Tarehe 15 Aprili, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Taarifa ya Mwaka na Hesabu zilizokaguliwa za Tume ya Ushindani kwa Mwaka wa Fedha 2008/2009 (The Annual Report and Audited Accounts of the Fair Competition Commission (FCC) for the Financial Year 2008/2009). Taarifa ya Mwaka na Hesabu zilizokaguliwa za Wakala wa Usajili wa Biashara na Utoaji Leseni kwa Mwaka wa Fedha 2006/2007 na Mwaka wa Fedha 2007/2008 (The Annual Reports and Audited Accounts of Business Registrations and Licensing Agency (BRELA) for the Financial Years 2006/2007 and 2007/2008). MASWALI NA MAJIBU Na. 100 Mpango wa Kutwaa Ardhi kwa Ajili ya Kupanga na Kupanua Mji MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.N.Y. MHE. PHILIPA G. MTURANO) aliuliza:- Serikali ina mpango wa kutwaa ardhi za Wananchi wa Kata ya Somangila, Mitaa ya Kizani na Mwera kupima viwanja kwa lengo la kupanua mji; na kwa mujibu wa Sheria ya Vijiji ya Mwaka 1999 na Kanuni zake zinazitaka mamlaka zinazotwaa ardhi za Vijiji kulipa fidia kamili ya haki na ilipwe kwa wakati:- (a) Je, ni Wakazi wangapi wa Mitaa ya Kizani na Mwera wamelipwa fidia ya mali zao, usumbufu, malazi, upotevu wa faida na usafiri? 1 (b) Je, mpaka hivi sasa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke imekamilisha zoezi la ulipaji fidia kwa mujibu wa Sheria husika? (c) Ni kiasi gani cha fedha kimeshatumika katika zoezi hilo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Philipa Mturano, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a), (b) na (c), kwa pamoja kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, ninapenda kumfahamisha Mheshimiwa Mbunge kuwa, hadi sasa hakuna Mkazi wa Mtaa wa Kizani na Mwera aliyelipwa fidia.
    [Show full text]
  • Kamati Ya Uangalizi Wa Uchaguzi Tanzania Temco
    KAMATI YA UANGALIZI WA UCHAGUZI TANZANIA TEMCO RIPOTI YA WATAZAMAJI WA UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA, 2015 MAY 2016 YALIYOMO YALIYOMO .......................................................................................................... I ORODHA YA MAJEDWALI .............................................................................. VI ORODHA YA VIELELEZO ............................................................................. VIII ORODHA YA VIAMBATANISHO ...................................................................... IX VIFUPISHO ......................................................................................................... X CHAPTER 1 MFUMO WA TEMCO WA UTAZAMAJI WA UCHAGUZI ............... 1 1.1 Usuli na Muktadha ............................................................................................................................ 1 1.2 Dira na Malengo ............................................................................................................................... 1 1.3 Upeo katika Utazamaji wa Chaguzi .................................................................................................. 2 1.4 Faida Zitokanazo na Utazamaji wa Chaguzi na Vigezo vyaTathmini .............................................. 4 1.5 Mfumo wa Utazamaji wa Uchaguzi Mkuu ....................................................................................... 5 1.6 Mpango wa Mgawanyo wa Vituo na Waangalizi ............................................................................. 9 1.7 Ripoti za Awali kuhusu
    [Show full text]
  • 1 Bunge La Tanzania
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Kumi na Nane – Tarehe 4 Julai, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alikalia Kiti HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA PAMOJA NA UTAWALA BORA: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma pamoja na (Utawala Bora) kwa mwaka wa Fedha 2011/2012. Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Uhusiano na Uratibu kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. MHE. PINDI H. CHANA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA: Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, pamoja na Utawala Bora, kwa Mwaka 2010/2011 pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hizo kwa mwaka wa Fedha 2011/2012. MHE. DR. ABDALLAH O. KIGODA - MWENYEKITI WA KAMATI YA FEDHA NA UCHUMI: Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha, Kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Rais, Uhusiano na Uratibu, kwa Mwaka 2010/2011 pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha, 2011/2012. 1 MHE. SUZAN A. J. LYIMO - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA, PAMOJA NA UTAWALA BORA: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma) pamoja na (Utawala Bora) Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hizo kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012.
    [Show full text]
  • August 2015 Has Been Used in Preparation of This Directory
    Information as of 3 August 2015 has been used in preparation of this directory. PREFACE The Central Intelligence Agency publishes and updates the online directory of Chiefs of State and Cabinet Members of Foreign Governments weekly. The directory is intended to be used primarily as a reference aid and includes as many governments of the world as is considered practical, some of them not officially recognized by the United States. Regimes with which the United States has no diplomatic exchanges are indicated by the initials NDE. Governments are listed in alphabetical order according to the most commonly used version of each country's name. The spelling of the personal names in this directory follows transliteration systems generally agreed upon by US Government agencies, except in the cases in which officials have stated a preference for alternate spellings of their names. NOTE: Although the head of the central bank is listed for each country, in most cases he or she is not a Cabinet member. Ambassadors to the United States and Permanent Representatives to the UN, New York, have also been included. Key To Abbreviations Adm. Admiral Admin. Administrative, Administration Asst. Assistant Brig. Brigadier Capt. Captain Cdr. Commander Cdte. Comandante Chmn. Chairman, Chairwoman Col. Colonel Ctte. Committee Del. Delegate Dep. Deputy Dept. Department Dir. Director Div. Division Dr. Doctor Eng. Engineer Fd. Mar. Field Marshal Fed. Federal Gen. General Govt. Government Intl. International Lt. Lieutenant Maj. Major Mar. Marshal Mbr. Member Min. Minister, Ministry NDE No Diplomatic Exchange Org. Organization Pres. President Prof. Professor RAdm. Rear Admiral Ret. Retired Sec. Secretary VAdm.
    [Show full text]
  • Hansard Ambayo Aliyasema: “This Book Is Written Using Curriculum Developed and Approved for the United Republic of Tanzania Ya Mwaka 2005
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI Kikao cha Tisa – Tarehe 8 Februari, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Jenista J. Mhagama) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA FEDHA: Muhtasari wa Tamko la Sera ya Fedha, Mapitio ya Nusu Mwaka Februari, 2013 (Monetary Policy Statement – The Mid Year Review February, 2013). Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ruhusa yako kabla sijawasilisha mezani taarifa niliyo nayo, naomba nitoe salaam za rambirambi na pole kwa waumini wote wa Kanisala Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Kati pamoja na familia ya Baba Askofu Thomas Laizer, kwa kifo kilichotokea jana cha Askofu wa Dayosisi hiyo. Tunamwomba Mwenyezi Mungu ailaze Roho yake mahali pema peponi. Amina. Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya salaam hizo, sasa naomba kwa niaba ya Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwasilisha mezani. Taarifa ya Mwaka na Hesabu zilizokaguliwa za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa Mwaka ulioishia tarehe 30 Juni, 2011 (The Annual Report and Audited Accounts of the National Housing Corporation (NHC) Year ended 30th June, 2011). Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Waziri na tumepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo hicho cha Askofu. Naomba sasa nimwite Mheshimiwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, nimemwona Mheshimiwa Naibu Waziri, tafadhali! NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, naomba kuwasilisha mezani.
    [Show full text]
  • Information As of 1 April 2014 Has Been Used in Preparation of This Directory. PREFACE
    Information as of 1 April 2014 has been used in preparation of this directory. PREFACE The Central Intelligence Agency publishes and updates the online directory of Chiefs of State and Cabinet Members of Foreign Governments weekly. The directory is intended to be used primarily as a reference aid and includes as many governments of the world as is considered practical, some of them not officially recognized by the United States. Regimes with which the United States has no diplomatic exchanges are indicated by the initials NDE. Governments are listed in alphabetical order according to the most commonly used version of each country's name. The spelling of the personal names in this directory follows transliteration systems generally agreed upon by US Government agencies, except in the cases in which officials have stated a preference for alternate spellings of their names. NOTE: Although the head of the central bank is listed for each country, in most cases he or she is not a Cabinet member. Ambassadors to the United States and Permanent Representatives to the UN, New York, have also been included. Page 2 of 211 Key to Abbreviations Adm. Admiral Admin. Administrative, Administration Asst. Assistant Brig. Brigadier Capt. Captain Cdr. Commander Cdte. Comandante Chmn. Chairman, Chairwoman Col. Colonel Ctte. Committee Del. Delegate Dep. Deputy Dept. Department Dir. Director Div. Division Dr. Doctor Eng. Engineer Fd. Mar. Field Marshal Fed. Federal Gen. General Govt. Government Intl. International Lt. Lieutenant Maj. Major Mar. Marshal Mbr. Member Min. Minister, Ministry NDE No Diplomatic Exchange Org. Organization Pres. President Prof. Professor RAdm. Rear Admiral Ret.
    [Show full text]
  • Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1 BUNGE LA TANZANIA
    Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA ISHIRINI _________ Kikao cha Nane – Tarehe 20 Mei, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Lediana M. Mng’ong’o) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Randama za Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. MHE. DKT. LUCY S. NKYA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2014/2015 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2015/2016. MHE. KURUTHUM J. MCHUCHULI (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI JUU YA WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Matumizi ya fedha kwa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. MASWALI NA MAJIBU Na. 53 Ujenzi Kwenye Maeneo ya Wazi Mji wa Himo MHE. DKT. ANTONY G. MBASSA (K.n.y. MHE. DKT. AUGUSTINO L. MREMA) aliuliza:- 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) Wako watu wamejenga kwenye maeneo ya wazi katika Mji Mdogo wa Himo na kuna mchakato unaoendelea katika Halmashauri ya Wilaya ya Moshi wa kuwamilikisha maeneo hayo:- (a) Je, ni nini msimamo wa Serikali juuu ya hao waliovamia na kujenga kwenye maeneo hayo? (b) Je, Maafisa wa Ardhi walioyatoa maeneo hayo wamechukuliwa hatua gani za kinidhamu? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt.
    [Show full text]
  • Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1 BUNGE LA TANZANIA
    Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Kumi na Nne – Tarehe 1 Aprili, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 143 Wananchi Kuchangia Ujenzi wa Maabara Nchini MHE. PAULINE P. GEKUL (K.n.y. MHE. ROSE K. SUKUM) aliuliza:- Utoaji wa Elimu bora ni pamoja na kuwa na Maabara nzuri zenye vifaa vya kutosha na vilivyo bora; kutokana na ukweli huo, Mheshimiwa Rais alitoa agizo la ujenzi wa Maabara kwa kuhusisha michango ya Wananchi hali inayowanyanyasa sana Wananchi hivyo kuwa kero kubwa toka kwa Watendaji wa Vijiji na Kata kwa maagizo ya Mkurugenzi na Wakuu wa Wilaya:- Je, Serikali kupitia agizo la Mheshimiwa Rais imechangia kiasi gani kwa kila Wilaya kama kielelezo cha utekelezaji wa agizo hilo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rose Kamili Sukum, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, ujenzi wa miundombinu ya shule nchini umekuwa unatekelezwa kwa ubia kati ya Serikali, wananchi na wadau wa maendeleo. Wakati wa ujenzi wa shule nyingi za wananchi zijulikanazo kama Shule za Kata, baadhi ya miundombinu muhimu ikiwemo maabara haikukamilika. Kutokana na umuhimu wa maabara, Mheshimiwa Rais alitoa agizo ambalo kimsingi lilikuwa ni kukumbushia uzingatiaji wa kila shule kuwa na Maabara tatu. Kila Halmashauri ilipaswa kutekeleza kupitia vyanzo vya ndani na wananchi wamekuwa wakishirikishwa kupitia mikutano na vikao katika ngazi mbalimbali ili waone umuhimu wa kushiriki kwa hiari yao.
    [Show full text]
  • Tarehe 6 Agosti, 2012 (Mkutano Ulianza Saa T
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Arobaini na Moja – Tarehe 6 Agosti, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI: Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA(TAMISEMI): Taarifa ya Mwaka na Hesabu zilizokaguliwa za Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (DART) kwa mwaka ulioshia tarehe 30 Juni, 2011 (The Annual Report and Audited Accounts of Dar es Salaam Rapid Transit for the year Ended 30th June, 2011. NAIBU WAZIRI, WIZARA YA KAZI NA AJIRA: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kazi na Ajira kwa Mwaka wa Fedha, 2012/2013. NAIBU WAZIRI, WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA: Hotuba ya Makadirio na Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa Mwaka wa Fedha, 2012/2013. MHE. BETTY E. MACHANGU (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa mwaka 2011/2012 pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha, 2012/2013. MHE. RAYA IBRAHIM KHAMIS (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Juu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha, 2012/2013.
    [Show full text]