Kitabu Cha Kumbukumbu Za Wabunge
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
-
MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Thelathini Na Sita
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Sita – Tarehe 27 Mei, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nawaomba tukae. Waheshimiwa Wabunge tunaendelea na Mkutano wetu wa 15, leo ni Kikao cha 36. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NAIBU WAZIRI WA MADINI: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2019/2020. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. CATHERINE V. MAGIGE - K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI) Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu utekelezaji na Majukumu ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. MHE. TUNZA I. MALAPO - K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU WIZARA YA MADINI: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni juu ya Wizara ya Madini kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Tunza Malapo, tunakushukuru. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Tunaanza na TAMISEMI, swali la kwanza litaulizwa na Mheshimiwa Azza Hilal, Mbunge wa Viti Maalum - Shinyanga. -
MKUTANO WA TATU Kikao Cha Hamsini Na Sita
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Hamsini na Sita – Tarehe 22 Juni, 2021 (Bunge Lilianza saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba tukae. Waheshimiwa tunaendelea na Mkutano wetu wa Tatu, leo ni Kikao cha Hamsini na Sita na kabla hatujaendelea nitumie nafasi hii kuwashukuru sana wasaidizi wangu wote wakiongozwa na Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa David Kihenzile, Mheshimiwa Zungu na Mheshimiwa Najma kwa kazi nzuri ambayo wameifanya wiki nzima kutuendeshea mjadala wetu wa bajeti. (Makofi) Sasa leo hapa ndio siku ya maamuzi ambayo kila Mbunge anapaswa kuwa humu ndani, kwa Mbunge ambaye Spika hana taarifa yake na hatapiga kura hapa leo hilo la kwake yeye. (Makofi) Katibu. NDG. NENELWA MWIHAMBI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Maswali na tunaanza na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Kwela. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Na. 465 Ujenzi wa Makao Makuu ya Halmashauri Katika Mji wa Laela MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi za Makao Makuu ya Halmashauri ya Sumbawanga katika Mji wa Laela baada ya agizo la Serikali la kuhamisha Makao Makuu? SPIKA: Majibu ya swali hilo muhimu la watu wa Kwela, Mheshimiwa Naibu Waziri - TAMISEMI, Mheshimiwa Dkt. Festo Dugange tafadhali. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Jimbo la Kwela kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ni miongoni mwa Halmashauri 30 zilizohamia kwenye maeneo mapya ya utawala mwaka 2019. -
MKUTANO WA TATU Kikao Cha Kumi Na Tisa – Tarehe 29 Aprili, 2021
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Kumi na Tisa – Tarehe 29 Aprili, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa, tukae. Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2021/2022. NAIBU WAZIRI WA MADINI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2021/2022. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. SAADA MONSOUR HUSSEIN - K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2020/2021 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2021/2022. NAIBU SPIKA: Ahsante sana. Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa maswali, tutaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Busega, sasa aulize swali lake. Na. 158 Serikali Kukamilisha Ujenzi wa Zahanati – Busega MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza:- Wananchi wa Kata ya Imalamate Wilayani Busega wamejenga zahanati na kumaliza maboma manne kwa maana ya zahanati moja kila kijiji:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi hao kuezeka maboma hayo ili waweze kupata huduma za afya kwenye zahanati hizo? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Dkt. -
Mkutano Wa Tatu
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA TATU YATOKANAYO NA KIKAO CHA KUMI NA TISA 13 MEI, 2016 MKUTANO WA TATU - YATOKANAYO NA KIKAO CHA KUMI NA TISA TAREHE 13 MEI, 2016 I. DUA: Saa 3.00 asubuhi Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) alisoma Dua na Kuongoza Bunge. Makatibu Mezani 1. Ndg. Theonest Ruhilabake 2. Ndg. Zainab Issa II. HATI ZA KUWASILISHA MEZANI: Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani:- 1. Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi; Mhe. Hamad Yusuff Masauni aliwasilisha Mezani Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017. 2. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye aliwasilisha Mezani Hotuba ya Bajeti ya Wizara yake kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017. 3. Mhe. Juma Selemani Nkamia aliwasilisha Mezani Taarifa ya Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka 2015/2016 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa 2016/2017. 4. Naibu Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Juu ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Devota Minja aliwasiisha Taarifa ya Kambi juu ya Wizara hii kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017. III. MASWALI Maswali yafuatayo yaliulizwa na Waheshimiwa Wabunge; OFISI YA RAIS (TAMISEMI): Swali Na.155 – Mhe. Kiteto Zawadi Koshuma Swali la nyongeza: (i) Mhe.Kiteto Zawadi Koshuma 2 (ii) Mhe. Suzan Anselm Lyimo (iii) Mhe. Edward Franz Mwalongo (iv) Mhe. -
Hotuba Ya Mheshimiwa Doto Mashaka Biteko (Mb.), Waziri Wa Madini Akiwasilisha Bungeni Makadirio Ya Mapato Na Matumizi Ya Fedha Kwa Mwaka 2021/2022
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA MHESHIMIWA DOTO MASHAKA BITEKO (MB.), WAZIRI WA MADINI AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2021/2022 DODOMA APRILI, 2020 1 Mhe. Doto M. Biteko, Waziri wa Madini akiwa na watendaji wa Wizara pamoja na Taasisi zake wakati wa uzinduzi wa kitabu cha Mwongozo wa Uchukuaji wa Sampuli. 2 JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA MHESHIMIWA DOTO MASHAKA BITEKO (MB.), WAZIRI WA MADINI Doto M. Biteko (Mb.), Waziri Wa Madini Prof. Shukrani E. Manya (Mb.) Prof. Simon S. Msanjila Naibu Waziri wa Madini Katibu Mkuu i ORODHA YA PICHA A. UTANGULIZI ............................................................... 1 Namba ya Na. Maelezo ya Picha B. MCHANGO WA SEKTA YA MADINI KATIKA PATO Picha (a) Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, 1. LA TAIFA................................ .......................................... 13 aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania C. MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO NA (b) Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, 2. BAJETI KWA MWAKA 2020/2021 .................................. 13 aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alipokuwa akitoa hotuba baada ya I. MAPATO .................................................................. 14 kusainiwa kwa Hati ya Makubaliano ya II. MATUMIZI ................................................................. 14 kuanzishwa kampuni ya Twiga Minerals (c) Baadhi ya mitambo ya kusafisha dhahabu 3. III. VIPAUMBELE VILIVYOTEKELEZWA KWA MWAKA katika kiwanda cha kusafisha dhahabu cha 2020/2021 ..................................................................... 15 Mwanza Precious Metals Refinery IV. UTEKELEZAJI KATIKA MAENEO MENGINE .................... 46 (d) Madini ya ujenzi (maarufu kama Tanga stone) 4. yakiwa tayari kwa matumizi katika eneo la V. UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO ................... 59 Mkinga mkoani Tanga VI. KAZI NYINGINE ZILIZOTEKELEZWA NA TAASISI ZILIZO (e) Mchimbaji mdogo akiendelea na shughuli za 5. -
Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Nne – Tarehe 9 Mei, 2014 (Mkutano Uianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA: Randama za Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA) PAMOJA NA (UTAWALA BORA): Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma) pamoja na (Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (MAHUSIANO NA URATIBU): Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. JAKU HASHIM AYOUB (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA): Taarifa ya Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), (Utawala Bora) pamoja na (Mahusiano na Uratibu) kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na maoni 1 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hizo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. PROF. KULIKOYELA K. KAHIGI - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA), (UTAWALA BORA) PAMOJA NA (MAHUSIANO NA UTARATIBU):- Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), (Utawala Bora) pamoja na (Mahusiano na Uratibu) kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hizo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015 MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaanza Maswali na Ofisi ya Waziri Mkuu. -
1447734501-Op Kikao
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA ORODHA YA SHUGHULI ZA LEO MKUTANO WA KWANZA KIKAO CHA KWANZA 17 NOVEMBA, 2015 ORODHA YA SHUGHULI ZA LEO _________________ MKUTANO WA KWANZA KIKAO CHA KWANZA – TAREHE 17 NOVEMBA, 2015 Kikao Kuanza Saa Tatu Kamili Asubuhi I. TANGAZO LA RAIS LA KUITISHA MKUTANO WA BUNGE: II. UCHAGUZI WA SPIKA: III. KIAPO CHA UAMINIFU NA KIAPO CHA SPIKA: IV. WIMBO WA TAIFA NA DUA KUSOMWA: V. KIAPO CHA UAMINIFU KWA WABUNGE WOTE: DODOMA DKT. T. D. KASHILILAH 17 NOVEMBA, 2015 KATIBU WA BUNGE 2 1. Mhe. George Mcheche Masaju 2. Mhe. Andrew John Chenge 3. Mhe. Mary Michael Nagu, Dkt. 4. Mhe. William Vangimembe Lukuvi 5. Mhe. Richard Mganga Ndassa 6. Mhe. Tulia Ackson, Dkt. 7. Mhe. Abbas Ali Hassan Mwinyi, Capt. 8. Mhe. Abdallah Ally Mtolea 9. Mhe. Abdallah Dadi Chikota 10. Mhe. Abdallah Haji Ali 11. Mhe. Abdallah Hamis Ulega 12. Mhe. Abdul-Aziz Mohamed Abood 13. Mhe. Agnes Mathew Marwa 14. Mhe. Adadi Mohamed Rajab, Balozi. 15. Mhe. Ahmed Ally Salum 16. Mhe. Ahmed Juma Ngwali 17. Mhe. Ahmed Mabkhut Shabiby 18. Mhe. Aida Joseph Khenan 19. Mhe. Aisharose Ndogholi Matembe 20. Mhe. Ajali Rashid Akbar 21. Mhe. Upendo Furaha Peneza 3 22. Mhe. Joseph Leonard Haule 23. Mhe. Joseph Osmund Mbilinyi 24. Mhe. Albert Obama Ntabaliba 25. Mhe. Alex Raphael Gashaza 26. Mhe. Ali Hassan Omar, King 27. Mhe. Ali Salim Khamis 28. Mhe. Allan Joseph Kiula 29. Mhe. Ally Mohamed Keissy 30. Mhe. Ally Saleh Ally 31. Mhe. Ally Seif Ungando 32. Mhe. Almas Athuman Maige 33. Mhe. -
Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA THELATHINI NA SITA 29 MEI, 2017 MKUTANO WA SABA KIKAO CHA THELATHINI NA SITA TAREHE 29 MEI, 2017 I. DUA: Dua ilisomwa Saa 3.00 Asubuhi na Mhe. Spika, Job Ndugai alikiongoza Kikao hadi saa 4.20 asubuhi ambapo alimpisha Mwenyekiti wa Bunge Mhe. Mussa Zungu ambae aliendelea kukiongoza Kikao. Makatibu mezani: 1. Ndugu Laurence Makigi 2. Ndugu Zainab Issa II. HATI ZA KUWASILISHA MEZANI (i) Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji kwa niaba ya Waziri aliwasilisha Mezani Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (ii) Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba aliwasilisha Mezani Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (iii) Mhe. Juliana Shonza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama aliwasilisha Mezani Taarifa ya Kamati kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa fedha 2016/2017 pamoja na maoni ya Kamati juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. 1 (iv) Mhe. Riziki Mngwali kwa niaba ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani aliwasilisha Mezani Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. -
MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao Cha Arobaini Na Sita
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Arobaini na Sita – Tarehe 15 Juni, 2020 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tukae, tunaendelea na Mkutano wetu wa 19, Kikao cha 46, bado kimoja tu cha kesho. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na: NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Maelezo ya Waziri wa Fedha na Mipango kuhusu Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2020 (The Finance Bill, 2020). Muhtasari wa Tamko la Sera ya Fedha kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 (Monetary Policy Statement for the Financial Year 2020/2021). MHE. ALBERT N. OBAMA - K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI:Maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2020 (The Finance Bill, 2020). 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. RHODA E. KUNCHELA - K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KWA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO: Maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu Muswada wa Sheria ya fedha wa mwaka 2020 (The Finance Bill, 2020). MHE. DKT. TULIA ACKSON - MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KANUNI ZA BUNGE: Azimio la Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kanuni za Bunge kuhusu Marekebisho ya Kanuni za Bunge SPIKA: Asante sana Mheshimiwa Naibu Spika, Katibu MASWALI NA MAJIBU (Maswali yafuatayo yameulizwa na kujibiwa kwa njia ya mtandao) Na. 426 Migogoro ya Mipaka MHE. -
13 Aprili, 2012 1 Bunge La Tanzania
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) 13 APRILI, 2012 BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Nne – Tarehe 13 Aprili, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Jenista J. Mhagama) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge tunaendelea na ratiba ya Mkutano wetu wa Saba wa Bunge ambao leo ni kikao cha Nne, Katibu. MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge leo hatuna Hati za Kuwasilishwa Mezani kwa hiyo tunaenda moja kwa moja kwenye maswali yaliyopo kwenye Ratiba ya Shughuli za leo na swali la kwanza linaenda ofisi ya Waziri Mkuu na litaulizwa na Mhehsimiwa Rukia Kassim Ahmed Mbunge wa Viti Maalum. Na. 39 Shule ya Kolo kuwa na Wanafunzi watatu Kidato cha Nne MHE. RUKIA K. AHMED aliuliza:- Kukosekana kwa walimu wa kutosha, vifaa vya maabara na mazingira magumu katika shule ya Sekondari ya Kolo- Wilaya ya Kondoa kumesababisha wanafunzi wengi kuacha 1 13 APRILI, 2012 shule na kubakiwa na wanafunzi watatu (3) tu katika Kidato cha Nne:- (a) Je, Serikali inawasaidiaje wanafunzi hao waliokumbwa na kadhia hiyo? (b) Je, Serikali haioni kwamba wanafunzi hao wana haki ya kupata elimu kama wanafunzi wengine? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rukia Kassim Ahmed, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a)Mheshimiwa Mwenyekiti, takwimu zilizopo kuhusu walimu na wanafunzi katika shule ya Sekondari Kolo kwa kipindi cha miaka minne ni kama ifuatavyo:- Mwaka 2008 shule ilikuwa na walimu 5 na wanafunzi 36, mwaka 2009 shule ilikuwa na walimu 3 na wanafunzi 28, mwaka 2010 shule ilikuwa na walimu 5 na wanafunzi 26, mwaka 2011 shule ilikuwa na walimu 7 na wanafunzi 25. -
21 MEI, 2013 MREMA 1.Pmd
21 MEI, 2013 BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini – Tarehe 21 Mei, 2013 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu tuendelee? HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI (MHE. STEPHEN J. MASELLE): Randama za Makadirio ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. 1 21 MEI, 2013 MASWALI NA MAJIBU Na. 243 Upotevu wa Fedha Kwenye Halmashauri Nchini MHE. RAMADHAN HAJI SALEH aliuliza:- Kumekuwa na upotevu wa fedha nyingi katika Halmashauri nyingi nchini, hali ambayo imesababisha miradi mingi isiweze kutekelezwa. Je, Serikali, imechukua hatua gani dhidi ya Watendaji wanaobainika kuhusika na wizi huo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ramadhan Haji Saleh, Mbunge wa Bumbwini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge, kuwa, kumekuwepo na matuimizi mabaya ya fedha katika baadhi ya Mamlaka za Serikali za Mitaa Nchini. Katika kukabuliana na hali hiyo Serikali, imechukua hatua mbalimbali za kuboresdha mfumo wa udhibiti wa fedha na kuwachukulia hatua watumishi wanaobainika kuhusika na ubadhirifu huo. Mheshimiwa Spika, hatua mbalimbali zimekuwa zikichukuliwa dhidi ya watumishi, zikiwemo kufikishwa katika vyombo vya dola, kuvuliwa madaraka, kushushiwa mishahara na kufukuzwa kazi. Kwa kipindi cha mwaka 2006 mpaka 2012 Wakurugenzi 24 walivuliwa madaraka, Wakurugenzi 24 mchakato wa hatua za nidhamu upo katika hatua mbalimbali, Mkurugenzi mmoja alishushiwa mshahara na Wakurugenzi 8 wamefikishwa Mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.