4 FEBRUARI, 2019.Pmd
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
Majadiliano Ya Bunge ___Mkutano Wa Kumi Na Moja
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Saba– Tarehe 25 Aprili, 2018 (Bunge Lilianza Saa 3:00 Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Mussa A. Zungu) Alisoma Dua MWENYEKITI: Katibu. NDG. JOSHUA CHAMWELA – KATIBU WA MEZANI: HATI ZA KUWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa mwaka wa fedha 2018/2019. NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Taarifa ya Mwaka ya Mamlaka ya Usimazi wa Udhibiti wa Nishati na Maji kwa Mwaka unaoishia tarehe 30 Juni 2017 [The Annual Report of Energy and Water Utilities Regulatory Authority (EWURA) for the Year Ended 30th June, 2017]. MWENYEKITI: ahsante, Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge tunaanza na maswali yetu ya kawaida, tunaanza Ofisi ya Waziri Mkuu, Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza Mbunge wa Chumbuni, kwa niaba ya Mheshimiwa Machano. Na. 135 Kuwakamata Wafanyabiashara Wakubwa wa Dawa za Kulevya MHE. MACHANO OTHMAN SAID (K.n.y. MHE. USSI SALUM PONDEZA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itachukua hatua dhidi ya wauzaji wakubwa wa dawa za kulevya wanaoingiza na kuuza badala ya kuakamata waathirika ambao wanahitaji misaada na ushauri nasaha wa kuachana na matumizi ya dawa hizo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. ANTONY P. MAVUNDE) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza, Mbunge wa Chumbuni kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imejipanga na inaendelea kukabiliana na wafanyabiashara wakubwa na wadogo wa dawa za kulevya ambao wote wanasababisha madhara kwa jamii kwa kufanya biashara hiyo. -
MKUTANO WA KUMI NA SABA Kikao Cha
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA SABA Kikao cha Kwanza – Tarehe 5 Novemba, 2019 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) WIMBO WA TAIFA D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge naomba tukae sasa. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge katika Mkutano wa Kumi na Sita wa Bunge, Bunge lilipitisha Miswada minne ya Sheria ya Serikali ifuatayo:- Kwanza, Muswada wa Sheria ya Serikali Mtandao ya Mwaka 2019 (The e- Government Bill, 2019). Pili, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali Na. 4 wa Mwaka 2019 (The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 4, Bill, 2019). Tatu, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 5 wa Mwaka 2019, (The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 5, Bill, 2019. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Nne, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali Na. 6 wa Mwaka 2019, ((The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 6, Bill, 2019. Kwa Taarifa hii, napenda kuliarifu Bunge kwamba tayari Miswada hiyo minne imepata kibali cha Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwa sheria za nchi, sasa zimekuwa sheria za nchi zinazoitwa kama ifuatavyo;- (Makofi) Sheria ya kwanza, ni Sheria ya Serikali Mtandao Na. 10 ya Mwaka 2019 (The e- Government Act No. 10 of 2019. Ya pili, ni sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali Na. 4, Sheria Na. 11 ya Mwaka 2019 ((The Written Laws Miscellaneous Amendments No. 4, Act No.11 of 2019; na Tatu, Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. -
Tarehe 6 Aprili, 2018
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Nne - Tarehe 6 Aprili, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe.Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Tukae, Katibu. NDG.YONA KIRUMBI - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Maswali, Waheshimiwa karibuni kwenye Mkutano wetu, kikao chetu cha nne na swali letu la kwanza linaelekezwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI na linaulizwa na Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda. Na. 24 Ujenzi wa Vituo Vya Afya Ikuti na Ipinda MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi unaoendelea katika Vituo vya Afya Ikuti, Wilayani Rungwe na Ipinda Wilayani Kyela utakamilika ili kuwawezesha wananchi wa maeneo hayo kupata huduma kwa wakati? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:- 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya cha Ikuti kimekarabatiwa katika awamu ya kwanza ya ukarabati wa vituo vya afya 44 ulioanza tarehe 10 Oktoba, 2017 na kukamilika tarehe 31 Januari, 2018 kwa gharama ya shilingi milioni 500 ili kuongeza huduma za upasuaji wa dharura kwa mama wajawazito. Aidha, shilingi milioni 220 zimetolewa kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba vya upasuaji na samani. Kituo hicho kinaendelea kutoa huduma zote za matibabu isipokuwa huduma za upasuaji wa dharura. Ujenzi wa majengo ya Kituo cha Afya Ikuti umekamilika na kinachosubiriwa kwa sasa ni vifaatiba kutoka Bohari ya Dawa (MSD). -
Tarehe 7 Februari, 2017
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA SITA Kikao cha Saba – Tarehe 7 Februari, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Tukae. Katibu. NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na: MHE. PROF. NORMAN A. S. KING – MWENYEKITI WA KAMATI YA BUNGE YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kwa kipindi cha kuanzia Januari, 2016 hadi Januari, 2017. MHE. DOTO M. BITEKO -MWENYEKITI WA KAMATI YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa kipindi cha kuanzia Januari 2016 hadi Januari 2017. NAIBU SPIKA: Ahsante. Katibu! NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na maswali, Ofisi ya Rais - TAMISEMI. Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, Mbunge wa Viti Maalum, sasa aulize swali lake. Na. 69 Tatizo la Ulevi MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza:- 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Ulevi wa kupita kiasi hasa wa pombe za kienyeji umekuwa na athari kubwa za kiafya na kiakili kwa Watanzania wenye tabia ya ulevi wa kukithiri:- Je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na tatizo hilo hasa ikizingatiwa kuwa Sheria ya Vileo ya mwaka 1969 ni ya zamani sana kiasi kwamba inawezekana kabisa haikidhi mabadiliko ya hali halisi ya vileo kwa wakati huu. NAIBUWAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, pombe za kienyeji zimeainishwa katika Kifungu cha pili (2) cha tafsiri katika Sheria ya Vileo, Sura ya 77. -
Tarehe 12 Aprili, 2021
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Saba – Tarehe 12 Aprili, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na Mkutano wetu wa Tatu, leo ni Kikao cha Saba. Natumaini mlikuwa na weekend njema Waheshimiwa Wabunge, ingawaje weekend ilikuwa na mambo yake hii. Jana nilimtafuta Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba kwa mambo yetu haya ya Bunge kuhusiana na uchangiaji wa Mpango wa Maendeleo akaniambia Mheshimiwa Spika tafadhali niache. Aah! Sasa nakuacha kuna nini tena? Anasema nina stress. Kumbe matokeo ya juzi yamempa stress. (Makofi/Kicheko) Pole sana Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba, na Wanayanga wote poleni sana. Taarifa tulizonazo ni kwamba wachezaji wana njaa, hali yao kidogo, maana yake wamelegealegea hivi. Kwa hiyo Waheshimiwa Wabunge baadaye tunaweza tukafanya mchango kidogo tuwasaidie Yanga ili wachezaji… (Kicheko) Katibu, tuendelee. (Kicheko) NDG. EMMANUEL MPANDA – KATIBU MEZANI: 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA NA VIJANA) (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2021/2022. NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu. Katibu! NDG. EMMANUEL MPANDA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Swali la kwanza linaelekea TAMISEMI na litaulizwa na Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani Msongozi, Mbunge kutoka kule Ruvuma. Na. 49 Hitaji la Vituo vya Afya – Tunduru MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya afya katika Kata za Tinginya, Muhimba, Kalulu, Mindu, Nalasi Magharibi na Nalasi Mashariki Wilayani Tunduru? SPIKA: Majibu ya Serikali kuhusu ujenzi wa vituo vya afya Ruvuma na nchi nzima, Mheshimiwa Naibu Waziri TAMISEMI, Mheshimiwa David Silinde, tafadhali. -
Tarehe 9 Mei, 2019
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 9 Mei, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu. NDG. JOSHUA CHAMWELA – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa mwaka wa fedha 2019/2020. MHE. ASHA MSHIMBA JECHA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa mwaka wa fedha 2018/ 2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. QAMBALO W. QULWI – NAIBU MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Kuhusu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NAIBU SPIKA: Ahsante. Waheshimiwa tunaendelea. Katibu. NDG. JOSHUA CHAMWELA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Maswali, tutaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi sasa aulize swali lake. Na. 196 Serikali Kuzipatia Waganga Zahanati za Jimbo la Manyoni Magharibi MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Wananchi wa Manyoni Magharibi kwa kushirikiana na Serikali kupitia miradi mbalimbali ikiwemo TASAF wamejenga zahanati katika Vijiji vya Gurungu, Sanjaranda, Kitopeni, Ipande, Doroto, Itagata, Kalangali, Makale, Mwamagembe na Kintanula, lakini mpaka sasa zahanati hizi hazina Waganga:- Je, ni lini Serikali itazipatia zahanati hizo Waganga, ili wananchi wapate huduma kufuatana na sera yake? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu. -
Tanzania Human Rights Report 2015 Tanzania Mainland Legal and Human Rights Centre (LHRC) Tanzania Human Rights Report 2015
Tanzania Human Rights Report 2015 Tanzania Mainland Legal and Human Rights Centre (LHRC) Tanzania Human Rights Report 2015 Publishers Legal and Human Rights Centre Justice Lugakingira House, Kijitonyama P.O. Box 75254, Dar es Salaam, Tanzania Tel: +255222773038/48, Fax: +255222773037 Email: [email protected] Website: www.humanrights.or.tz Partners - LHRC Accountability in Tanzania (AcT) The Embassy of Norway The Embassy of Sweden ISBN: 978-9987-740-25-3 © LHRC 2016 - ii - Tanzania Human Rights Report 2015 Editorial Board Dr. Helen Kijo-Bisimba Adv. Imelda Urrio Ms. Felista Mauya Adv. Anna Henga Mr. Castor Kalemera Researchers/Writers Mr. Paul Mikongoti Mr. Pasience Mlowe Mr. Fundikila Wazambi Design & Layout Mr. Rodrick Maro - iii - Tanzania Human Rights Report 2015 Acknowledgement Legal and Human Rights Centre (LHRC) has been producing the Tanzania Human Rights Report, documenting the situation in Tanzania Mainland since 2002. In the preparation and production of this report LHRC receives both material and financial support from different players, such as the media, academic institutions, other CSOs, researchers and community members as well as development partners. These players have made it possible for LHRC to continue preparing the report due to its high demand. In preparing the Tanzania Human Rights Report 2015, LHRC received cooperation from the Judiciary, the Legislature and the Executive arms of the State. Various reports from different government departments and research findings have greatly contributed to the finalization of this report. Hansards and judicial decisions form the basis of arguments and observations made by the LHRC. The information was gathered through official correspondences with the relevant authorities, while other information was obtained online through various websites. -
MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Ishirini Na Tano
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 10 Mei, 2019 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Tukae, Katibu. NDG. RUTH MAKUNGU – KATIBU MEZANI: Maswali. MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Maswali, Waheshimiwa Wabunge tutaanza na Ofisi ya Rais TAMISEMI. Mheshimiwa Joel Mwaka Makanyaga Mbunge wa Chilonwa, sasa aulize swali lake. Na. 200 Kukamilisha Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji – Chilonwa MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Chilonwa iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi ambayo kwa sasa imefikia kwenye linta? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:- 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joel Mwaka Makanyaga, Mbunge wa Chilonwa, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Chilonwa ni miongoni mwa Kata 36 za Wilaya ya Chamwino, ina vijiji viwili vya Nzali na Mahama, Kata ina huduma za Zahanati moja iliyopo katika Kijiji cha Nzali. Wananchi wa kijiji cha Mahama walianzisha ujenzi wa Zahanati ya Kijiji ambayo kwa sasa jengo limefikia hatua ya lInta. Katika kuunga mkono juhudi za wananchi, Halmashauri ya Chamwino katika mwaka wa fedha 2019/2020 kupitia mapato yake ya ndani imetenga shilingi milioni 30 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa zahanati hiyo katika Kijiji cha Mahama. Ahsante. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Joel Makanyaga, swali la nyongeza. -
Annual Report 2013/14 Highlights
H E KI RU MA NI UHU UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM ANNUAL REPORT 2013 - 2014 University of Dar es Salaam ANNUAL REPORT 2013-14 VISION STATEMENT A leading centre of intellectual wealth spearheading the quest for sustainable and inclusive development. MISSION STATEMENT To advance the economic, social and technological development of Tanzania and beyond through excellent teaching and learning, research and knowledge exchange. GUIDING THEME The focus of the University of Dar es Salaam activities during the reporting period, continued to be guided by the following theme: “Enhanced quality outputs in teaching, research and public service”. Multi-media Laboratory at CoICT – Kijitonyama Campus University of Dar es Salaam ANNUAL REPORT 2013-14 i ANNUAL REPORT 2013/14 HIGHLIGHTS ii University of Dar es Salaam ANNUAL REPORT 2013-14 University of Dar es Salaam ANNUAL REPORT 2013-14 ANNUAL REPORT 2013/14 HIGHLIGHTS University of Dar es Salaam ANNUAL REPORT 2013-14 University of Dar es Salaam ANNUAL REPORT 2013-14 iii ANNUAL REPORT 2013/14 HIGHLIGHTS iv University of Dar es Salaam ANNUAL REPORT 2013-14 University of Dar es Salaam ANNUAL REPORT 2013-14 ANNUAL REPORT 2013/14 HIGHLIGHTS 7 University of Dar es Salaam ANNUAL REPORT 2013-14 University of Dar es Salaam ANNUAL REPORT 2013-14 v TABLE OF CONTENTS Vision Statement ........................................................................................................................ i Mission Statement ................................................................................................................... -
Tarehe 21 Aprili, 2016
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Tatu – Tarehe 21 Aprili, 2016 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, leo ni Kikao cha Tatu cha Mkutano wetu wa Tatu, Katibu. HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi zake kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla hatujaendelea nimepokea barua ambayo inatoka kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu ikisema kwamba, atakuwa nje ya Dodoma leo siku ya Alhamisi, tarehe 21 Aprili, 2016. Kwa hiyo, shughuli za Mkuu wa Shughuli za Serikali Bungeni kwa siku ya leo zitasimamiwa na Mheshimiwa William Lukuvi ambaye tunamwona yuko pale. (Makofi) Katibu! 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) MASWALI NA MAJIBU Na. 21 Maafa Yaliyosababishwa na Mvua ya Tarehe 3 Machi, 2016 MHE. EZEKIEL M. MAIGE aliuliza:- Mvua ya theluji ilionyesha terehe 3 Machi, 2015 ilisababisha maafa makubwa ambapo familia zilikosa makazi na Mheshimiwa Rais wakati huo aliwaahidi wahanga wa maafa hayo kuwa Serikali itasaidia kujenga nyumba 343:- (a) Je, ni nyumba ngapi hadi sasa zimejengwa katika kutekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais? (b) Je, ni kiasi gani cha pesa kinahitajika kwa ajili ya utekelezaji wa ahadi hiyo? (c) Je, ni kiasi gani cha fedha na misaada ya kibinadamu ya aina nyingine iliyotolewa na Serikali katika kukabiliana na janga hilo? NAIBU WAZIRI WA SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU (MHE. -
1 Bunge La Tanzania
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI Kikao cha Tano – Tarehe 5 Februari, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae, Katibu. NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: KIAPO CHA UAMINIFU Mhe. Dkt. Adelardus Lubango Kilangi NAIBU SPIKA: Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- MHE. MOSHI S. KAKOSO - K.n.y MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA - K.n.y MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu shughuli za kamati kwa mwaka 2017. NAIBU SPIKA: Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU Na. 55 Changamoto Zinazowakabili Walemavu MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:- Watanzania wenye ulemavu wanakabiliwa na kero mbalimbali za kimaisha ikiwemo ukosefu wa ajira kama ilivyo kwa Watanzania wengine, aidha, zipo changamoto za jumla kama vile kijana mwenye ulemavu wa ngozi asiye na ajira ana changamoto ya mahitaji ya kujikimu na pia ana changamoto za kipekee za mahitaji ya kiafya na kiusalama. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu umuhimu wa kuwatazama vijana wenye ulemavu mbalimbali kwa namna ya pekee na kama zipo sera na mikakati ya kiujumla kwa vijana wote nchini? NAIBU SPIKA: Ofisi ya Waziri Mkuu sijui nani anayejibu maswali. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, niko hapa. -
1 Bunge La Tanzania
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Sita – Tarehe 24 Mei, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. ATHUMAN HUSSEIN - KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI:- Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019. MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI):- Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Hamida. Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani siioni. Tunawashukuru kwa kutupatia nusu saa ya bure, Katibu. NDG. ATUMAN HUSSEIN - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Tunaanza na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mheshimiwa Omari Abdallah Kigoda, Mbunge wa Handeni, uliza swali lako tafadhali. Na. 307 Asilimia Tano ya Mapato ya Halmashauri kwa ajili ya Vijana na akina Mama MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni kwa kiasi gani Serikali inasimamia suala la asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri kwa ajili ya vijana na akina mama? SPIKA: Jamani hili swali Waheshimiwa Mawaziri wamejibu sana, basi tuendelee kulijibu. Naomba Waheshimiwa Wabunge wote sasa mlisikilize tusilione tena swali hili la asilimia 10.