Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
-
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Tano - Tarehe 16 Julai, 2003 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Pius Msekwa) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA SAYANSI, TEKNOLOJIA NA ELIMU YA JUU: Hotuba ya Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu kwa Mwaka wa Fedha 2003/2004. MHE. MARGARETH A. MKANGA (k.n.y. MHE. OMAR S. KWAANGW’ - MWENYEKITI WA KAMATI YA HUDUMA ZA JAMII): Taarifa ya Kamati ya Huduma za Jamii kuhusu utekelezaji wa Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu katika mwaka uliopita, pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka 2003/2004. MASWALI NA MAJIBU Na. 239 Majimbo ya Uchaguzi MHE. JAMES P. MUSALIKA (k.n.y. MHE. DR. WILLIAM F. SHIJA) aliuliza:- Kwa kuwa baadhi ya Majimbo ya Uchaguzi ni makubwa sana kijiografia na kwa wingi wa watu; je, Serikali itashauriana na Tume ya Uchaguzi ili kuongeza Majimbo ya Uchaguzi katika baadhi ya maeneo nchini katika Uchaguzi wa mwaka 2005? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (MHE. MUHAMMED SEIF KHATIB) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kabla ya kujibu swali la Mheshimiwa Dr. William Shija, Mbunge wa Sengerema, naomba kutoa maelezo yafuatayo:- Mheshimiwa Spika, lilipokuwa linajibiwa swali la Mheshimiwa Ireneus Ngwatura, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi na pia swali la Mheshimiwa Sophia Simba, Mbunge wa Viti Maalum, CCM 1 katika Mikutano ya Saba na Kumi na Moja sawia ya Bungeni, nilieleza kwamba, kwa mujibu wa Ibara ya 75(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungao wa Tanzania 1977, Jamhuri ya Muungano inaweza kugawanywa katika Majimbo ya Uchaguzi kwa idadi na namna itakavyoamuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi baada ya kupata kibali cha Mheshimiwa Rais. -
1 Bunge La Tanzania
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA TISA Kikao cha Tatu – Tarehe 1 Novemba, 2007 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 28 Majibu ya Maswali Bungeni MHE. JUMA HASSAN KILLIMBAH aliuliza:- Kwa kuwa baadhi ya majibu ya Serikali kwa maswali ya Waheshimiwa Bungeni, mara nyingi yamekuwa hayamridhishi muuliza swali na hata wananchi anaowawakilisha Bungeni hasa pale Serikali ilipotoa majibu kama Mheshimiwa Mbunge avute subira, Mheshimiwa Mbunge ashirikiane na Halmashauri yake na au hali ya Serikali itakapokuwa nzuri na kadhalika. (a) Je, Serikali inaweza kutueleza ni taratibu gani zinazostahili kuchukuliwa hasa pale ambapo majibu ya maswali yamepitiliza muda wa utekelezaji na vile vile kutofanikiwa kwa juhudi na nyingine za kupata ufumbuzi kutoka kwenye Halmashauri? (b) Je, kwa nini Serikali isitoe majibu yenye ukomo ili muuliza swali awe na majibu ya kuwapa wapiga kura wake badala ya kuambiwa avute subira isiyo na mwisho? (c) Je, Serikali iko tayari kuwa na utaratibu wa kufuatilia majibu ya Mawaziri na kuhimiza utekelezaji wa ahadi za Serikali? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, MAAFA NA KAMPENI DHIDI YA UKIMWI (MHE. DR. LUCAS SIYAME) alijibu:- 1 Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juma Hassan Killlimbah, Mbunge wa Iramba Magharibi, lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Naibu Spika, maswali ya Waheshimiwa Wabunge, yanapatiwa majibu kamilifu kutoka Serikali kwa mujibu wa Kanuni za Bunge hili Tukufu. Majibu ya Serikali kwa kuzingatia Kanuni ya 37 A (1), (2) na (3) yamekuwa yakionyesha hatua zilizochukuliwa, zinazochukuliwa au zitakazochukuliwa na Serikali katika utekelezaji wa jambo lenyewe. -
Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA SITA (DAILY SUMMARY RECORD OF PROCEEDINGS) 11 NOVEMBA, 2014 MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA KIKAO CHA SITA – 11 NOVEMBA, 2014 I. DUA Saa 3.00 Asubuhi kikao kilianza kikiongozwa na Mhe. Naibu Spika (Mhe Job Y. Ndugai) na alisoma Dua. Makatibu Mezani 1. Ramadhani Abdallah Issa 2. Asia Minja 3. Hellen Mbeba II. MASWALI Maswali yafuatayo yaliulizwa na yalijibiwa:- 1. OFISI YA WAZIRI MKUU Swali . 67 – Mhe. Charles J.P. Mwijage Nyongeza (i) Mhe. Charles Mwijage (ii) Mhe. Joshua Nassari Swali. 68- Mhe. Hezekiah Chibulunje (K.n.y – Mhe. David Mallole) Nyongeza (i) Mhe. Hezekiah Chibulunje Swali. 69 – Mhe. Josephat Sinkamba Kandege Nyongeza (i) Mhe. Josephat Kandege 2. OFISI YA RAIS (UTAWALA BORA) Swali. 70 – Mhe. Amina Abdulla Amour 2 Nyongeza (i) Mhe. Amina Abdullah Amour 3. OFISI YA RAIS (MAHUSIANO NA URATIBU) Swali. 71 – Mhe. Leticia Mageni Nyerere Nyongeza i. Mhe. Leticia Nyerere ii. Mhe. Mohammed Habib Mnyaa 4. OFISI YA MAKAMU WA RIAS (MAZINGIRA) Swali. 72 – Mhe. Victor Kilasile Mwambalaswa Nyongeza i. Mhe. Victor Kilasile Mwambalaswa. 5. WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Swali. 73 – Mhe. Diana Mkumbo Chilolo Nyongeza i. Mhe. Diana Mkumbo Chilolo 6. WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA Swali. 74 – Mhe. Sylvestry Francis Koka Nyongeza i. Mhe. Sylvestry Koka ii. Mhe. Salim Masoud 7. WIZARA YA UCHUKUZI Swali. 75 – Mhe. Prof. David Mwakyusa (k.n.y Mhe. Luckson Mwanjale). Nyongeza i. Mhe. Prof. David Mwakyusa. 3 Swali. 76 – Mhe. -
Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1 MAJADILIANO YA BUNGE
Nakala ya Mtandao (Online Document) MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA ISHIRINI __________ Kikao cha Ishirini na Moja - Tarehe 5 Juni, 2015 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, napenda kuchukua nafasi hii kuwapa pole wote kwa msiba uliotupata, msiba ulitokea wakati nikiwa Geneva ambapo tulikuwa na kikao cha Kamati Ndogo ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Maspika wote duniani utakaofanyika mwezi wa Nane, sasa kuna Maspika kumi ndiyo tupo kwenye maandalizi ya mkutano huo na kilikuwa ni kikao chetu cha mwisho kabla ya mkutano huo. Kwa hiyo, wakati msiba unatokea nilikuwa huko, nilipewa taarifa na nilisikitika sana. Kwa hiyo, tutatangaza baadaye mchana, ni akina nani watakaokwenda kuzika kesho. Katibu! HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI (MHE. CHARLES M. KITWANGA): Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. NAIBU WAZIRI WA MAJI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Maji kwa mwaka wa Fedha, 2015/2016. MHE. DAVID H. MWAKYUSA (k.n.y. MHE. PROF. PETER M. MSOLLA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015, pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa Fedha 2015/2016. MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED (k.n.y. MHE. MAGDALENA H. SAKAYA - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KWA WIZARA YA MAJI): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Fedha kwa Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. -
MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NANE Kikao
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ________________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Kumi na Mbili – Tarehe 28 Juni, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge leo ni siku nyingine ya Alhamisi ambayo tunakuwa na nusu saa kwa maswali ya Waziri Mkuu na baadaye maswali mengine ya kawaida. Namwona Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni kwamba yupo leo, kama kanuni yetu inavyoruhusu yeye ndiye ataanza kuuliza swali la kwanza. MHE. FREEMAN A. MBOWE – KIONGOZI WA UPINZANI BUNGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la kwanza kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu. 1 Mheshimiwa Waziri Mkuu, wewe ni Kiongozi Mkuu na Kiongozi muhimu katika Serikali na kauli yako ni kauli nzito sana. Siku ya jana ulitoa kauli ambayo kama mzazi ama kama baba imetia hofu kubwa sana katika Taifa, pale ulipokuwa unazungumzia mgomo wa Madaktari na hatimaye ukasema na linalokuwa na liwe. Mheshimiwa Waziri Mkuu, kuanzia jana baada ya kauli yako vilevile zilipatikana taarifa zingine kwamba Rais wa Madaktari Dkt. Ulimboka ametekwa juzi usiku, ameteswa, amevunjwa meno, ameng’olewa kucha na mateso mengine mengi sana na kwa sababu uliahidi Mheshimiwa Waziri Mkuu kwamba mtatoa kauli ya Serikali leo. Jambo hili sasa limechukua sura mpya na katika maeneo mbalimbali ya nchi, tayari Madaktari wengine wako kwenye migomo. Wewe kama Waziri Mkuu unalieleza nini Taifa kuhusu kauli yako ya litakalokuwa na liwe na Serikali inafanya nini cha ziada ku-address tatizo hili? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba nijaribu kutoa ufafanuzi kwenye maeneo mawili ambayo Mheshimiwa Mbowe ameyazungumza. -
MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao Cha Ishirini
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TAZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 16 Julai, 2008 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Jenista J. Mhagama) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii kwa Mwaka wa Fedha 2008/2009. MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA HUDUMA ZA JAMII: Taarifa ya Kamati ya Huduma za Jamii kuhusu utekekelezaji wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa Mwaka wa Fedha uliopita, pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadrio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka 2008/2009. MHE. OMAR ALI MAZEE K.n.y. MSEMAJI WA KAMBI YA UPINZANI WA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII: Taarifa ya Msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu utekelezaji wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa Mwaka wa Fedha uliopita, pamoja na maoni ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2008/2009. MASWALI NA MAJIBU Na. 222 Mtaji Ulioanzisha BOT MHE. DR. HAMAD RASHID MOHAMMED aliuliza:- Je, nini msimamo wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania juu ya mtaji ulioanzisha Benki Kuu ya Tanzania, BOT? NAIBU WAZIRI FEDHA NA UCHUMI (MHE. JEREMIA S. SUMARI) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, ruhusa yako na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Uchumi, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Hamad Rashid Mohammed, Mbunge wa Jimbo la Wawi na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, Benki Kuu ya Tanzania, BOT, ilianzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania ya mwaka 1965, mtaji wa awali ulioanzisha Benki Kuu ulitoka kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na ulikuwa kiasi cha shilingi 20,000,000/=. -
MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao Cha
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Ishirini na Tatu – Tarehe 8 Julai, 2009 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:- Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010. MHE. MUSSA A. ZUNGU (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA): Taarifa ya Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka 2008/2010 pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2009/2010. MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM - MSEMAJI WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2009/2010. NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO Randama za makadirio ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa mwaka wa fedha 2009/2010. 1 MASWALI NA MAJIBU Na. 171 Kutangazwa kwa Miji Midogo MHE. DORAH H. MUSHI aliuliza:- Kwa kuwa tarehe 17/09/2004 Miji midogo ipatato 90 ilitangazwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 353 ambapo Mji wa Mererani ni miongoni mwa Miji iliyotangazwa ukiwa na wakazi wapatao 48,000. (a) Je, miongoni mwa Miji iliyotangazwa ni Miji mingapi imekwishaanza? (b) Je, ni Miji mingapi iliyopata ruzuku moja kwa moja ya kujiendesha toka Serikali Kuu? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dora Mushi, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Naibu Spika, Mamlaka ya miji midogo ni Mamlaka ya Serikali za Mitaa iliyopo kwenye Mamlaka ya Wilaya. -
Majadiliano Ya Bunge Mkutano Wa Kumi Na Mbili
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Sita – Tarehe 17 Julai, 2008 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda ) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, leo ni siku ya alhamisi, kwa hiyo tuna kipindi kile cha Maswali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu kama kawaida yetu. Katibu tuendelee na Order Paper. MASWALI KWA WAZIRI MKUU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Mgana Msindai. MHE. MGANA I. MSINDAI: Mheshimiwa Naibu Spika……! MHE. HAMAD RASHID MOHAMED: Mwongozo wa Spika. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mgana Msindai samahani naomba ukae. Nilikuwa sijamwangalia Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni. Kwa kawaida utaratibu wetu hapa akiwepo Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni inabidi yeye apewe nafasi ya kwanza ya kuuliza swali. Sasa nilikuwa nimepitiwa. Mheshimiwa Hamad Rashid Mohamed, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni. MHE. HAMAD R. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Swali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu. Mheshimiwa Waziri Mkuu mwaka 1992 Mahakama ya Rufaa katika kesi ya Seif Sharrif Hamad, Waziri Kiongozi wa SMZ ilibaini kuwa kuna utata mkubwa katika 1 vifungu vingi vya Katiba na Mahakama ya Rufaa ikapendekeza kwa Mamlaka mbili kwamba zikae kitako ili kutatua matatizo hayo pamoja na vifungu vingine vya Katiba ambavyo vina utata. Tokea wakati huo mpaka leo Mamlaka hizo mbili hazijachukua hatua yoyote mpaka tumefikia leo kuna matatizo. Je, Mheshimiwa -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Thelathini na Tatu – Tarehe 31 Julai, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Job J. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI: Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii kwa Mwaka wa Fedha 2006/2007. MHE. DR. HAJI MWITA HAJI - (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA HUDUMA ZA JAMII): Maoni ya Kamati ya Huduma za Jamii Kuhusu Utekelezaji wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa Mwaka wa Fedha Uliopita, Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka 2006/2007. MHE. DR. ALI TARAB ALI - MSEMAJI WA MKUU WA KAMBI YA UPINZANI: Maoni ya Kambi ya Upinzani Kuhusu Utekelezaji wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, kwa Mwaka wa Fedha Uliopita, Pamoja na Maoni Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka 2006/2007. MASWALI NA MAJIBU Na. 307 Wilaya ya Geita Kuwa Mkoa MHE. ERNEST G. MABINA aliuliza:- 1 Kwa kuwa moja ya vigezo vya kupata Mkoa ni pamoja na idadi ya watu na kwa kuwa Wilaya ya Geita ina watu zaidi ya laki saba na Sengerema ina watu zaidi ya laki tano kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2002. (a) Je, ni lini Serikali itatoa kibali cha kuanzisha Mkoa wa Geita ambao utachanganywa na Sengerema na kuwa na idadi ya watu milioni moja na laki mbili? (b) Kama Geita na Sengerema zitachanganywa na bado Mkoa usitoshe. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Kumi na Nane - Tarehe 28 Juni, 2010 (Mkutano ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI: Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani:- NAIBU WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. MWENYEKITI WA KAMATI YA HUDUMA ZA JAMII: Taarifa ya Kamati ya Huduma za Jamii Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010 pamoja na maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha, 2010/2011. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII: Taarifa ya Msemaji wa Mkuu wa Kambi ya Upinzani Kuhusu Makadiro ya Matumizi ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. NAIBU WAZIRI WAZIRI WA MIUONDOMBINU: Randama za Makadiro ya Matumizi ya Wizara ya Miundombinu kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. MASWALI NA MAJIBU Na. 121 1 Matatizo Katika Hospitali ya Wilaya - Geita MHE. ESTHER K. NYAWAZWA aliuliza:- Kwa kuwa, Hospitali ya Wilaya ya Geita inahudumia Kata 33 na madaktari Bingwa ni wawili (2) tu, na kwa kuwa upanuzi unasuasua na utawala ni mbovu:- Je, ni lini Serikali itarekebisha matatizo hayo? NAIBU WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Kabadi Nyawazwa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Kumi na Moja – Tarehe 23 Aprili, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 120 Kutoridhisha kwa Hadhi ya Mkoa wa Dodoma MHE. MOZA A. SAIDY aliuliza:- Pamoja na kuwepo kwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA), bado hadhi ya Mkoa wa Dodoma zikiwemo barabara hairidhishi:- (a) Je, kuna tatizo gani katika Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA)? (b) Je, ni lini barabara za Mji wa Dodoma za Ipagala, Ilazo, Kisasa, Swaswa, Makulu na kadhalika zitatengenezwa ili ziwe na hadhi inayoendana na dhana ya Makao Makuu? SPIKA: Mheshimiwa Moza utahama hiyo microphone, Waziri Majibu. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Moza Abeid Saidy, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- 1 (a) Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma ilianzishwa kwa lengo la kupanga na kuendeleza Mji wa Ddoma ili kuwa na hadhi ya Makao Makuu nchini. Ili kutekeleza kazi hii, mwaka 1976 uliandaliwa mpango kabambe ( Master Plan ) wa Mji Mkuu uliotenga maeneo kwa ajili ya matumizi mbalimbali. Kwa mfano barabara, mfumo wa maji taka na maji safi, maeneo ya viwanja vya makazi, Huduma za Jamii, Biashara, Taasisi, Viwanda, maeneo ya wazi na kadhalika. Mwaka 2011 Mamlaka ilianza kufanya mapitio ya Mpango Kabambe ili uweze kwenda na wakati. Zoezi hili linatarajiwa kukamilika hivi karibuni. Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu haijafanikiwa kutekeleza mpango wake kama ilivyotarajiwa kutokana na tatizo kubwa la upatikanaji wa fedha za kutosha.