Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Kumi na Moja – Tarehe 23 Aprili, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 120 Kutoridhisha kwa Hadhi ya Mkoa wa Dodoma MHE. MOZA A. SAIDY aliuliza:- Pamoja na kuwepo kwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA), bado hadhi ya Mkoa wa Dodoma zikiwemo barabara hairidhishi:- (a) Je, kuna tatizo gani katika Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA)? (b) Je, ni lini barabara za Mji wa Dodoma za Ipagala, Ilazo, Kisasa, Swaswa, Makulu na kadhalika zitatengenezwa ili ziwe na hadhi inayoendana na dhana ya Makao Makuu? SPIKA: Mheshimiwa Moza utahama hiyo microphone, Waziri Majibu. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Moza Abeid Saidy, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- 1 (a) Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma ilianzishwa kwa lengo la kupanga na kuendeleza Mji wa Ddoma ili kuwa na hadhi ya Makao Makuu nchini. Ili kutekeleza kazi hii, mwaka 1976 uliandaliwa mpango kabambe ( Master Plan ) wa Mji Mkuu uliotenga maeneo kwa ajili ya matumizi mbalimbali. Kwa mfano barabara, mfumo wa maji taka na maji safi, maeneo ya viwanja vya makazi, Huduma za Jamii, Biashara, Taasisi, Viwanda, maeneo ya wazi na kadhalika. Mwaka 2011 Mamlaka ilianza kufanya mapitio ya Mpango Kabambe ili uweze kwenda na wakati. Zoezi hili linatarajiwa kukamilika hivi karibuni. Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu haijafanikiwa kutekeleza mpango wake kama ilivyotarajiwa kutokana na tatizo kubwa la upatikanaji wa fedha za kutosha.
[Show full text]