1 Bunge La Tanzania
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA KUMI NA NNE (DAILY SUMMARY RECORD OF PROCEEDINGS) 21 NOVEMBA, 2014 MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI SABA KIKAO CHA KUMI NA NNE – 21 NOVEMBA, 2014 I. DUA Mwenyekiti wa Bunge Mhe. Mussa Azzan Zungu alisoma Dua saa 3.00 Asubuhi na kuliongoza Bunge. MAKATIBU MEZANI – i. Ndg. Asia Minja ii. Ndg. Joshua Chamwela II. MASWALI: Maswali yafuatayo yaliulizwa na wabunge:- 1. OFISI YA WAZIRI MKUU Swali Na. 161 – Mhe. Betty Eliezer Machangu [KNY: Mhe. Dkt. Cyril Chami] Nyongeza i. Mhe. Betty E. Machangu, mb ii. Mhe. Michael Lekule Laizer, mb iii. Mhe. Prof. Peter Msolla, mb Swali Na. 162 - Mhe. Richard Mganga Ndassa, mb Nyongeza (i) Mhe Richard Mganga Ndassa, mb Swali Na. 163 - Mhe. Anne Kilango Malecela, mb Nyongeza : i. Mhe. Anne Kilango Malecela, mb ii. Mhe. John John Mnyika, mb iii. Mhe. Mariam Nassor Kisangi iv. Mhe. Iddi Mohammed Azzan, mb 2 2. OFISI YA RAIS (UTUMISHI) Swali Na. 164 – Mhe. Ritta Enespher Kabati, mb Nyongeza i. Mhe. Ritta Enespher Kabati, mb ii. Mhe. Vita Rashid Kawawa, mb iii. Mhe. Mch. Reter Msingwa, mb 3. WIZARA YA UJENZI Swali Na. 165 – Mhe. Betty Eliezer Machangu, mb Nyongeza :- i. Mhe. Betty Eliezer Machangu, mb ii. Mhe. Halima James Mdee, mb iii. Mhe. Maryam Salum Msabaha, mb Swali Na. 166 – Mhe. Peter Simon Msingwa [KNY: Mhe. Joseph O. Mbilinyi] Nyongeza :- i. Mhe. Peter Simon Msigwa, Mb ii. Mhe. Assumpter Nshunju Mshama, Mb iii. Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa 4. -
-
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Tano - Tarehe 16 Julai, 2003 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Pius Msekwa) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA SAYANSI, TEKNOLOJIA NA ELIMU YA JUU: Hotuba ya Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu kwa Mwaka wa Fedha 2003/2004. MHE. MARGARETH A. MKANGA (k.n.y. MHE. OMAR S. KWAANGW’ - MWENYEKITI WA KAMATI YA HUDUMA ZA JAMII): Taarifa ya Kamati ya Huduma za Jamii kuhusu utekelezaji wa Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu katika mwaka uliopita, pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka 2003/2004. MASWALI NA MAJIBU Na. 239 Majimbo ya Uchaguzi MHE. JAMES P. MUSALIKA (k.n.y. MHE. DR. WILLIAM F. SHIJA) aliuliza:- Kwa kuwa baadhi ya Majimbo ya Uchaguzi ni makubwa sana kijiografia na kwa wingi wa watu; je, Serikali itashauriana na Tume ya Uchaguzi ili kuongeza Majimbo ya Uchaguzi katika baadhi ya maeneo nchini katika Uchaguzi wa mwaka 2005? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (MHE. MUHAMMED SEIF KHATIB) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kabla ya kujibu swali la Mheshimiwa Dr. William Shija, Mbunge wa Sengerema, naomba kutoa maelezo yafuatayo:- Mheshimiwa Spika, lilipokuwa linajibiwa swali la Mheshimiwa Ireneus Ngwatura, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi na pia swali la Mheshimiwa Sophia Simba, Mbunge wa Viti Maalum, CCM 1 katika Mikutano ya Saba na Kumi na Moja sawia ya Bungeni, nilieleza kwamba, kwa mujibu wa Ibara ya 75(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungao wa Tanzania 1977, Jamhuri ya Muungano inaweza kugawanywa katika Majimbo ya Uchaguzi kwa idadi na namna itakavyoamuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi baada ya kupata kibali cha Mheshimiwa Rais. -
MKUTANO WA PILI Kikao Cha Tisa
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA PILI Kikao cha Tisa - Tarehe 17 Februari, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Taarifa ya mwaka ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali za Mitaa kwa mwaka wa fedha unaoishia tarehe 30 Juni, 2004. Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. MASWALI NA MAJIBU Na. 94 Uwekaji wa Lami Barabara ya Kigogo - Mabibo - Mandela - Tabata MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka lami kwenye barabara ya Kigogo- Mabibo hadi barabara ya Mandela kuelekea Tabata ili kupunguza msongamano wa magari katika barabara ya Morogoro? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima Mdee, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- 1 Mheshimiwa Spika, barabara ya Kigogo - Mabibo- Mandela kuelekea Tabata ni barabara ya mjini yaani urban road na inahudumiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Barabara hii ni muungano wa barabara tatu ambazo ni Kigogo - Mabibo, Mabibo - Mandela na Mandela - Tabata. Barabara hii imekuwa ikifanyiwa matengenezo ya mara kwa mara na Manispaa ya Kinondoni. Kwa mwaka 2005/2006 jumla ya shilingi 9,836,000 zilitumika kuweka kifusi kwenye sehemu korofi na kuichonga kwa greda. Mheshimiwa Spika, barabara hii inapitika isipokuwa katika mpaka wa Manispaa za Kinondoni na Ilala eneo la Tabata ambapo pana mkondo wa maji na hakuna daraja. -
TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity?
TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? With Partial Support from a TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? ACKNOWLEDGEMENTS This review was compiled and edited by Tanzania Development Research Group (TADREG) under the supervision of the Steering Group of Policy Forum members, and has been financially supported in part by Water Aid in Tanzania and Policy Forum core funders. The cartoons were drawn by Adam Lutta Published 2013 For more information and to order copies of the review please contact: Policy Forum P.O Box 38486 Dar es Salaam Tel: +255 22 2780200 Website: www.policyforum.or.tz Email: [email protected] ISBN: 978-9987 -708-09-3 © Policy Forum The conclusions drawn and views expressed on the basis of the data and analysis presented in this review do not necessarily reflect those of Policy Forum. Every effort has been made to verify the accuracy of the information contained in this review, including allegations. Nevertheless, Policy Forum cannot guarantee the accuracy and completeness of the contents. Whereas any part of this review may be reproduced providing it is properly sourced, Policy Forum cannot accept responsibility for the consequences of its use for other purposes or in other contexts. Designed by: Jamana Printers b TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? TABLE OF CONTENTS POLICY FORUM’s OBJECTIVES ............................................................................................................. -
Tanzania Human Rights Report 2008
Legal and Human Rights Centre Tanzania Human Rights Report 2008: Progress through Human Rights Funded By; Embassy of Finland Embassy of Norway Embassy of Sweden Ford Foundation Oxfam-Novib Trocaire Foundation for Civil Society i Tanzania Human Rights Report 2008 Editorial Board Francis Kiwanga (Adv.) Helen Kijo-Bisimba Prof. Chris Maina Peter Richard Shilamba Harold Sungusia Rodrick Maro Felista Mauya Researchers Godfrey Mpandikizi Stephen Axwesso Laetitia Petro Writers Clarence Kipobota Sarah Louw Publisher Legal and Human Rights Centre LHRC, April 2009 ISBN: 978-9987-432-74-5 ii Acknowledgements We would like to recognize the immense contribution of several individuals, institutions, governmental departments, and non-governmental organisations. The information they provided to us was invaluable to the preparation of this report. We are also grateful for the great work done by LHRC employees Laetitia Petro, Richard Shilamba, Godfrey Mpandikizi, Stephen Axwesso, Mashauri Jeremiah, Ally Mwashongo, Abuu Adballah and Charles Luther who facilitated the distribution, collection and analysis of information gathered from different areas of Tanzania. Our 131 field human rights monitors and paralegals also played an important role in preparing this report by providing us with current information about the human rights’ situation at the grass roots’ level. We greatly appreciate the assistance we received from the members of the editorial board, who are: Helen Kijo-Bisimba, Francis Kiwanga, Rodrick Maro, Felista Mauya, Professor Chris Maina Peter, and Harold Sungusia for their invaluable input on the content and form of this report. Their contributions helped us to create a better report. We would like to recognize the financial support we received from various partners to prepare and publish this report. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Tatu – Tarehe 12 Julai, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Jenista J. Mhagama) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. MASWALI NA MAJIBU Na. 213 Ugumu wa Kutekeleza Kazi za Kiutawala Jimbo la Kwela MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:- Jimbo la Kwela, limegawanyika katika Makao Makuu Mawili yaliyojitenga Kijiografia, yaani eneo la ukanda wa juu (Mlimani) na eneo la ukanda wa chini (Bonde la Mto Rukwa) ambapo husababisha ugumu katika kuzitekeleza kazi za kiutawala za uwakilishi hasa ikizingatiwa pia kuwa miundombinu ya barabara ni duni sana:- (a) Je, Serikali haioni kuwa inafaa kuligawa eneo hilo kulingana na Jiografia ili kupata Jimbo jingine au Wilaya? (b) Je, ni kasoro gani zilizosababisha jimbo hilo kukosa sifa za kugawanywa kupata Majimbo mawili kulingana na Jiografia jinsi ilivyo? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE alijibu:- 1 Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ignas Aloyce Malocha, Mbunge wa Kwela, kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Uchaguzi hugawanywa kwa kuzingatia Vigezo 13, kama ifuatavyo:- 1. Idadi ya watu; 2. Upatikanaji wa mawasiliano; 3. Hali ya kijiografia; 4. Mgawanyo wa wastani wa idadi ya watu; 5. Hali ya kiuchumi ya Jimbo; 6. Ukubwa wa eneo la Jimbo husika; 7. -
13 DESEMBA, 2013 MREMA 1.Pmd
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA NNE Kikao cha Tisa – Tarehe 13 Desemba, 2013 (Mkutano ulianza saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Mussa Zungu Azzan) Alisoma HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- MHE. JUMA SURURU JUMA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA BUNGE YA HUDUMA ZA JAMII): Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii Kuhusu Utekelezaji wa Shughuli zake kwa Mwaka 2013. MHE. SAID MTANDA (K.n.y. MWENYEKITI KAMATI YA BUNGE NA MAENDELEO YA JAMII): Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii Kuhusu Utekelezaji wa Shughuli zake kwa Mwaka 2013. 1 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) MASWALI NA MAJIBU Na. 92 Hitaji la Gari la Wagonjwa Jimbo la Mwibara. MHE. ALPHAXARD K. N. LUGOLA aliuliza:- Je, ni lini Jimbo la Mwibara litapatiwa gari la kubebea wagonjwa hususan katika Kituo cha Afya cha Kasahunga? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kangi Lugola, Mbunge wa Jimbo la Mwibara, kama ifuatavyo: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna tatizo la kukosekana kwa gari la wagonjwa katika kituo cha Afya cha Kasahunga kilichoko katika Jimbo la Mwibara. Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ina jumla ya vituo 48 vya kutolea huduma za afya ambavyo ni Hospitali 2 vituo vya Afya 6 na Zahanati 40. Hospitali zilizopo ni pamoja na Hospitali ya Bunda DDH na Hospitali ya Mission ya Kibara. -
Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA SITA (DAILY SUMMARY RECORD OF PROCEEDINGS) 11 NOVEMBA, 2014 MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA KIKAO CHA SITA – 11 NOVEMBA, 2014 I. DUA Saa 3.00 Asubuhi kikao kilianza kikiongozwa na Mhe. Naibu Spika (Mhe Job Y. Ndugai) na alisoma Dua. Makatibu Mezani 1. Ramadhani Abdallah Issa 2. Asia Minja 3. Hellen Mbeba II. MASWALI Maswali yafuatayo yaliulizwa na yalijibiwa:- 1. OFISI YA WAZIRI MKUU Swali . 67 – Mhe. Charles J.P. Mwijage Nyongeza (i) Mhe. Charles Mwijage (ii) Mhe. Joshua Nassari Swali. 68- Mhe. Hezekiah Chibulunje (K.n.y – Mhe. David Mallole) Nyongeza (i) Mhe. Hezekiah Chibulunje Swali. 69 – Mhe. Josephat Sinkamba Kandege Nyongeza (i) Mhe. Josephat Kandege 2. OFISI YA RAIS (UTAWALA BORA) Swali. 70 – Mhe. Amina Abdulla Amour 2 Nyongeza (i) Mhe. Amina Abdullah Amour 3. OFISI YA RAIS (MAHUSIANO NA URATIBU) Swali. 71 – Mhe. Leticia Mageni Nyerere Nyongeza i. Mhe. Leticia Nyerere ii. Mhe. Mohammed Habib Mnyaa 4. OFISI YA MAKAMU WA RIAS (MAZINGIRA) Swali. 72 – Mhe. Victor Kilasile Mwambalaswa Nyongeza i. Mhe. Victor Kilasile Mwambalaswa. 5. WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Swali. 73 – Mhe. Diana Mkumbo Chilolo Nyongeza i. Mhe. Diana Mkumbo Chilolo 6. WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA Swali. 74 – Mhe. Sylvestry Francis Koka Nyongeza i. Mhe. Sylvestry Koka ii. Mhe. Salim Masoud 7. WIZARA YA UCHUKUZI Swali. 75 – Mhe. Prof. David Mwakyusa (k.n.y Mhe. Luckson Mwanjale). Nyongeza i. Mhe. Prof. David Mwakyusa. 3 Swali. 76 – Mhe. -
Bunge La Tanzania ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _____________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Tisa – Tarehe 25 Julai, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Jenista J. Mhagama) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI: Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. MUSTAFA HAIDI MKULO): Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa mwaka 2004/2005 [The Annual Report and Accounts of Tanzania Revenue Authority for the year 2004/2005] NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI (MHE. BERNARD KAMILLIUS MEMBE: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2006/2007. MWENYEKITI WA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA: (MHE. WILLIAM J. KUSILA): Maoni ya Kamati ya Ulinzi na Usalama Kuhusu Utekelezaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha Uliopita, Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka 2006/2007. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI: (MHE. MUHONGA S. RUHWANYA): Maoni ya Kambi ya Upinzani Kuhusu Utekelezaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha Uliopita, Pamoja na Maoni Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka 2006/2007. MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge kabla ya maswali, kwa kuwa leo ni hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kwa kweli kwa heshima tutatumbue wageni wa Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, 1 Mheshimiwa Kapten Chiligati, lakini wageni hao wamekuja pia kwa niaba ya Mheshimiwa John Lwanji, hao wote ni Wabunge wanaotoka kwenye Halmashauri moja. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA TISA Kikao cha Saba – Tarehe 7 Novemba, 2007 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ILIYOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- MHE. MOHAMED H. MISSANGA - MWENYEKITI WA KAMATI YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Miundombinu kwa Mwaka 2006. MASWALI NA MAJIBU Na. 86 Ufanisi wa Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali MHE. ESTHERINA J. KILASI aliuliza:- Kwa kuwa, Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali, imekuwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na ufanisi unaonekana kuwa si mzuri sana:- Je, ni lini ofisi hiyo itakuwa wakala ili iweze kufanya kazi zake kwa ufanisi zaidi? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa idhini yako kabla ya kujibu swali la Mheshimiwa Estherina Kilasi naomba kutoa pongezi zangu za dhati kwa Chama cha Mapinduzi, kwa kukamilisha chaguzi zake. Nikupongeze wewe Mheshimiwa Spika, kwa kuongoza vizuri Kamati ile ya usimamizi kwa kufanyakazi kwa kasi na viwango inavyotakiwa. Nawapongeza wote waliopita katika sekretarieti na wajumbe wa Kamati.Kwa niaba ya 1 Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Estherina Kilasi, Mbunge wa Mbarali, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Idara ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali, ina dhamana ya kuchapa Nyaraka muhimu zote za Serikali Kuu, Serikali za Mitaa na Taasisi za Serikali za Mitaa na Taasisi za Serikali. Idara hiyo bado haijawa Wakala wa Serikali kwa kuwa ushauri huo ulikuwa bado tunaufanyia kazi. Kwa hivi sasa Serikali imekamilisha uchambuzi wake na kukubalika kwamba Idara ya Mpigachapa wa Serikali, haiwezi kuingia kwenye mfumo wa uwakala mpaka ukamilike mpango wa kuipatia mitambo na vitendea kazi ambavyo vitawezesha kukifanya kifanye kazi kwa ufanisi. -
Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1 MAJADILIANO YA BUNGE
Nakala ya Mtandao (Online Document) MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA ISHIRINI __________ Kikao cha Ishirini na Moja - Tarehe 5 Juni, 2015 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, napenda kuchukua nafasi hii kuwapa pole wote kwa msiba uliotupata, msiba ulitokea wakati nikiwa Geneva ambapo tulikuwa na kikao cha Kamati Ndogo ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Maspika wote duniani utakaofanyika mwezi wa Nane, sasa kuna Maspika kumi ndiyo tupo kwenye maandalizi ya mkutano huo na kilikuwa ni kikao chetu cha mwisho kabla ya mkutano huo. Kwa hiyo, wakati msiba unatokea nilikuwa huko, nilipewa taarifa na nilisikitika sana. Kwa hiyo, tutatangaza baadaye mchana, ni akina nani watakaokwenda kuzika kesho. Katibu! HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI (MHE. CHARLES M. KITWANGA): Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. NAIBU WAZIRI WA MAJI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Maji kwa mwaka wa Fedha, 2015/2016. MHE. DAVID H. MWAKYUSA (k.n.y. MHE. PROF. PETER M. MSOLLA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015, pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa Fedha 2015/2016. MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED (k.n.y. MHE. MAGDALENA H. SAKAYA - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KWA WIZARA YA MAJI): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Fedha kwa Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016.