MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao Cha

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao Cha Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Ishirini na Tatu – Tarehe 8 Julai, 2009 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:- Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010. MHE. MUSSA A. ZUNGU (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA): Taarifa ya Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka 2008/2010 pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2009/2010. MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM - MSEMAJI WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2009/2010. NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO Randama za makadirio ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa mwaka wa fedha 2009/2010. 1 MASWALI NA MAJIBU Na. 171 Kutangazwa kwa Miji Midogo MHE. DORAH H. MUSHI aliuliza:- Kwa kuwa tarehe 17/09/2004 Miji midogo ipatato 90 ilitangazwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 353 ambapo Mji wa Mererani ni miongoni mwa Miji iliyotangazwa ukiwa na wakazi wapatao 48,000. (a) Je, miongoni mwa Miji iliyotangazwa ni Miji mingapi imekwishaanza? (b) Je, ni Miji mingapi iliyopata ruzuku moja kwa moja ya kujiendesha toka Serikali Kuu? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dora Mushi, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Naibu Spika, Mamlaka ya miji midogo ni Mamlaka ya Serikali za Mitaa iliyopo kwenye Mamlaka ya Wilaya. Mamlaka hizi zinaanzishwa pale ambapo palikuwa na kijiji ambacho kimeanza kuendelezwa na kuwa na mazingira ya ki-mji. Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa amepewa madaraka ya kutangaza kijiji au vijiji vilivyofikia sifa zilizowekwa kuwa Mamlaka za Miji midogo. Mheshimiwa Naibu Spika, miongoni mwa Miji midogo 90 iliyotangazwa kupitia gazeti la Serikali Na. 353 la mwaka 1994 ni miji 41 iliyoanzishwa rasmi ikiwemo Mamlaka ya Mji mdogo wa Mererani. Mji huu ulizinduliwa rasmi tarehe 12 Agosti, 2008. Mamlaka hii ya Mji mdogo wa Mererani ina wajumbe 19, pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu ambaye ameteuliwa na Baraza la Mamlaka ya Mji mdogo. Aidha, vijiji vilivyokuwa ndani ya Mamlaka ya Mji mdogo vimefutwa na sasa kuna vitongoji. (b)Mheshimiwa Naibu Spika, hakuna miji midogo iliyokwisha anzishwa ambayo imepokea ruzuku moja kwa moja ya kujiendesha kutoka Serikali Kuu. Mamlaka za Miji midogo, bado zinaendelea kupokea ruzuku zinazopitia kwenye Mamlaka za Wilaya zilizomo kwa kuzingatia Bajeti zilizojiwekea. Mamlaka ya Mji mdogo wa Mererani haukutengewa fedha yoyote kwa mwaka wa fedha 2008/2009 kwa sababu ilikuwa haijaanzishwa rasmi. Katika mwaka 2009/2010, 2 Mamlaka ya Mji Mdogo, wa Mererani imeandaa Bajeti yake ambayo imejumuishwa na ile ya Halmashauri ya Wilaya Simanjiro. MHE. DORAH H. MUSHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la pili. Pamoja na majibu mazuri ya Waziri naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa umbali wa kutoka Mji mdogo wa Mererani kwenda Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro ni km 145; na kwa kuwa Mji huu wa Mererani una wakazi wapatao 48,000. Je, Serikali haioni sasa kuna haja ya kuwapa ruzuku moja kwa moja ili miji hii iweze kuwahudumia wananchi hawa? Swali la pili; kwa kuwa mji mdogo wa Mererani umepata neema ya kuwa miongoni mwa miji iliyotangazwa kama eneo maalum kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda na kwa kuwa mji huu sasa unahitaji wawekezaji. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuhakikisha kwamba ina boresha miundombinu ya kuwavutia wawekezaji ikiwa ni pamoja na barabara kwa kuweka lami, barabara inayo toka KIA kwenda Mererani? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la kupewa ruzuku moja kwa moja na Serikali; kwa mujibu wa Sheria mpaka sasa hivi Sheria yetu inasema kwamba miji yote midogo inapata ruzuku yao kupitia kwenye Halmashauri husika kwa sababu Sheria hiyo haijabadilika inabidi ruzuku hizo zipitie kwenye Halmashauri husika hadi hapo Sheria itakapobadilika. (Makofi) Nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge kwamba ni kweli umbali kutoka Mererani mpaka Simanjiro ni mrefu sana na ndiyo maana tumeuanzisha huo mji mdogo wa Mererani ili uweze kupanuka na ili baadaye uweze kujitegemea kuwa mji kamili na wakati ukiwa mji kamili utakuwa unapewa ruzuku moja kwa moja. Kuhusu suala la wawekezaji nafahamu kabisa kwamba Mererani kuna uwekezaji na wawekezaji wengi wanavutika kwenda huko na miundombinu yake sio mizuri sana. Lakini Mheshimiwa Dorah kama anavyofahamu kwamba barabara kutoka KIA hadi Mererani inaboreshwa mwaka hadi mwaka ili iweze kupitika vizuri na barabara hiyo inapitika vizuri. Ombi lake naomba nishirikiane na wenzangu wa miundombinu kuona kwamba kama kuna uwezekano wa kuweka lami kutoka Mererani hadi KIA. MHE. GAUDENCE C. KAYOMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa vile mji wa Mbinga una hadhi hiyo ya kuwa mji mdogo na kwa kuwa tangu mwaka 2004 wamekuwa wakijaribu kuanzisha Mamlaka ya Mji mdogo na bado hawajafanikiwa. Je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari hata leo kuongea na Mkurugenzi 3 kubaini ni tatizo gani linalowapata watu wa Mbinga hadi sasa kushindwa ku-operate kama Mji mdogo? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi kwamba mwaka 2004 tulitangaza Mamlaka za Miji midogo 90 lakini mpaka sasa hivi iliyoanzishwa ni Mamlaka za Miji midogo 41 tu. Hii ni kutokana na Halmashauri zenyewe kujipanga vizuri. Kama wameamua hata leo kwamba Mamlaka yetu iwe ina kuwepo, kwa sababu sisi upande wa Serikali tumeshatimizi wajibu wetu wa kutangaza ni wao katika Halmashauri husika kujipanga na kuamua kwamba sasa mji mdogo wetu tuuendeleze na procedure Wakurugenzi wanazifahamu Waheshimiwa baadhi ya Wabunge wanazifahamu na baadhi ya Mamlaka za Miji Midogo zimeanzishwa na sasa hivi zimekuwa zimefikia katika hadhi ya kuwa Mamlaka za Miji kamili. (Makofi) Na. 172 Kituo cha Afya Kikombo Kupewa Mgao wa Dawa na Vifaa MHE. EPHRAIM N. MADEJE aliuliza:- Kwa kuwa ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kikombo ulikamilishwa na Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma zaidi ya miaka miwili iliyopita; na kwa kuwa utaratibu wa uanzishwaji wa kituo hicho ulikwishakamilika. (a) Je, kwa nini Serikali haijaanza kupeleka mgao wa dawa na vifaa ili kukiwezesha kituo hicho kutoa huduma zinazostahili kutolewa na Kituo cha Afya? (b) Je, Serikali iko tayari kuanza kupeleka dawa na vifaa hivyo haraka ili wananchi waanze kupata huduma hiyo muhimu? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ephraim Nehemia Madeje, Mbunge wa Dodoma Mjini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kukubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba, ujenzi na taratibu zote za uanzishwaji wa Kituo cha Afya cha Kikombo ulikamilika katika mwaka wa fedha 2007/2008. Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma tayari imewasilisha maombi kwa Waziri Afya na Ustawi wa Jamii ili kituo hicho 4 kiingizwe kwenye orodha ya vituo vya afya na kuweza kupatiwa madawa kulingana na hadhi ya Kituo cha Afya. (b) Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na maombi ya Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma kwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia kwa Mfamasia Mkuu wa Wizara hiyo, Kituo cha Afya Kikombo kilianza kupokea madawa ya stahili ya Kituo cha Afya kuanzia robo ya nne ya mwaka wa fedha 2008/2009 yaani mwezi Aprili hadi Juni, 2009. Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma imekuwa ikikitambua Kituo cha Afya Kikombo na kukinunulia dawa za ziada zinazohitajika ili kuwezesha wananchi kupata huduma zinazolingana na zile za Kituo cha Afya. Sambamba na jitihada hizo Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma imepeleka watumishi wenye hadhi ya Kituo cha Afya akiwemo Daktari Msaidizi mmoja, Afisa Muunguzi mmoja pamoja na vifaa vinavyotakiwa. MHE. EPHRAIM N. MADEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri ambayo kwa kweli yanaleta matumaini wananchi wa Kikombo kwamba sasa watapata huduma za afya kwa uhakika zaidi. Pamoja na hayo naomba niulize maswali mawili. Kwa kuwa majengo ya Kituo hiki cha afya yalikaa muda mrefu sana kabla hayajaanza kutumika. Baadhi yake haya majengo hivi sasa yana hali mbaya na hasa senyenge yake. Je, Serikali iko tayari kutoa fedha za ziada ili kuyakarabati majengo hayo? Je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari hivi sasa kuja awe mgeni rasmi katika uzinduzi rasmi wa kituo hicho cha Afya ambacho tunatarajia kuufanya hivyo hivi karibuni? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Nchi naomba ujibu kwa kifupi sana kwenda huko najua utakubali tu. (Kicheko) WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA : Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli hicho kituo cha Afya baadhi ya majengo yamekaa kwa muda mrefu bila kutumika, kwa hiyo yameanza kuharibika. Nikubaliane naye kweli senyenge kwa kweli imeanza kuanguka. Niseme kwamba kwa kushirikiana na Manispaa ya Dodoma tutahakikisha kwamba tutakiboresha kile kituo cha Afya kwa sababu kinatoa huduma kwa watu wengi zaidi hata sisi Waheshimiwa Wabunge wakati mwingine tunaweza tukapata huduma katika sehemu hiyo. Kuhusu kuwa mgeni rasmi aliyepangiwa ratiba ni Mheshimiwa Waziri Mkuu bahati mbaya katika ratiba hiyo haikuweza kutimizwa. Sasa kama Mheshimiwa Waziri 5 Mkuu ataniruhusu nikawe mgeni rasmi badala yake kwa sababu ile aliiahirisha mimi niko tayari kuja na kukifungua kituo hicho rasmi.
Recommended publications
  • Issued by the Britain-Tanzania Society No 114 May - Aug 2016
    Tanzanian Affairs Issued by the Britain-Tanzania Society No 114 May - Aug 2016 Magufuli’s “Cleansing” Operation Zanzibar Election Re-run Nyerere Bridge Opens David Brewin: MAGUFULI’S “CLEANSING” OPERATION President Magufuli helps clean the street outside State House in Dec 2015 (photo State House) The seemingly tireless new President Magufuli of Tanzania has started his term of office with a number of spectacular measures most of which are not only proving extremely popular in Tanzania but also attracting interest in other East African countries and beyond. It could be described as a huge ‘cleansing’ operation in which the main features include: a drive to eliminate corruption (in response to widespread demands from the electorate during the November 2015 elections); a cutting out of elements of low priority in the expenditure of government funds; and a better work ethic amongst government employees. The President has changed so many policies and practices since tak- ing office in November 2015 that it is difficult for a small journal like ‘Tanzanian Affairs’ to cover them adequately. He is, of course, operat- ing through, and with the help of ministers, regional commissioners and cover photo: The new Nyerere Bridge in Dar es Salaam (see Transport) Magufuli’s “Cleansing” Operation 3 others, who have been either kept on or brought in as replacements for those removed in various purges of existing personnel. Changes under the new President The following is a list of some of the President’s changes. Some were not carried out by him directly but by subordinates. It is clear however where the inspiration for them came from.
    [Show full text]
  • Conference Report
    2 ND GOPAC GLOBAL CONFERENCE Arusha, Tanzania September 19-23, 2006 FINAL REPORT GLOBAL ORGANISATION OF PARLIAMENTARIANS AGAINST CORRUPTION: 2ND GLOBAL CONFERENCE Acknowledgements The Global Organisation of Parliamentarians Against Corruption wishes to thank the following organisations for their contributions to the 2nd Global Conference: Parliament of Tanzania African Parliamentarians Network Against Corruption (APNAC) Barrick Gold Canadian International Development Agency (CIDA) US Agency for International Development (USAID) World Bank Institute (WBI) Events Hosts Dr. Zainab A. Gama, MP, Chair, APNAC – Tanzania Arusha Regional Commissioner Col (Rtd). Samuel Ndomba H.E. Dr. Ali Mohamed Shein the Vice President of the United Republic of Tanzania Hosted by Hon. Samuel Sitta, MP – Speaker of the National Assembly Guest Speakers Deputy Barrister Emmanuel Akomaye, Economic and Financial Crimes Commission of Nigeria Doris Basler, Transparency International Hon. Ruth Kavuma, MP, Vice Chair, APNAC Uganda Mr. Paul Wolfowitz, President, World Bank (Taped message) Conference and Workshop Speakers Conference Chair: John Williams MP (Canada) Edward Doe Adjaho, MP (Ghana) Naser Al Sane, MP (Kuwait) Edgardo Angara, Senator (Philippines) Stella Cittadini, Senator (Argentina) Roy Cullen, MP (Canada) César Jauregui, Senator (Mexico) Edith Mastenbroek, MEP (Netherlands) J.T.K. Green-Harris, MP (Gambia) Mary King, Senator (Trinidad and Tobago) Omingo Magara, MP (Kenya) Augustine Ruzindana, Former MP (Uganda) Willibroad Slaa, MP (Tanzania) Navin Beekarry (IMF) Giovanni Gallo (UNODC) Scott Hubli (UNDP) Latifah Merican Cheong (World Bank) Carmen Lane (DAI) Luis Gerardo Villanueva, Former MP (Costa Murray Michel (Egmont Group and Rica) FATF) Patrick Moulette (IMF) Keith Schulz (USAID) Ingeborg Schwarz (IPU) Emiko Todoroki (WB) Frederick Stapenhurst (WBI) Stuart Yikona (WB) GOPAC wishes to thank the following individuals for their significant contribution to the conference and its administration: Canadian High Commission - Tanzania Parliament of Tanzania H.E.
    [Show full text]
  • 1458125471-Hs-6-8-20
    [Show full text]
  • TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who Will Benefit from the Gas Economy, If It Happens?
    TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who will benefit from the gas economy, if it happens? TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who will benefit from the gas economy, if it happens? TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013 Who will benefit from the gas economy, if it happens? Supported by: 2 TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who will benefit from the gas economy, if it happens? ACKNOWLEDGEMENTS Policy Forum would like to thank the Foundation for Civil Society for the generous grant that financed Tanzania Governance Review 2013. The review was drafted by Tanzania Development Research Group and edited by Policy Forum. The cartoons were drawn by Adam Lutta (Adamu). Tanzania Governance Reviews for 2006-7, 2008-9, 2010-11, 2012 and 2013 can be downloaded from the Policy Forum website. The views expressed and conclusions drawn on the basis of data and analysis presented in this review do not necessarily reflect those of Policy Forum. TGRs review published and unpublished materials from official sources, civil society and academia, and from the media. Policy Forum has made every effort to verify the accuracy of the information contained in TGR2013, particularly with media sources. However, Policy Forum cannot guarantee the accuracy of all reported claims, statements, and statistics. Whereas any part of this review can be reproduced provided it is duly sourced, Policy Forum cannot accept responsibility for the consequences of its use for other purposes or in other contexts. ISBN:978-9987-708-19-2 For more information and to order copies of the report please contact: Policy Forum P.O. Box 38486 Dar es Salaam Tel +255 22 2780200 Website: www.policyforum.or.tz Email: [email protected] Suggested citation: Policy Forum 2015.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE ________________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 17 Julai, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO:- Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa mwaka wa Fedha 2012/2013. NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:- Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa Fedha 2012/2013. MHE. EUGEN E. MWAIPOSA (K.n.y. MHE. EDWARD LOWASSA - MWENYEKITI WA KAMATI YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA):- Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka 2011/2012 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. MHE. VINCENT J. NYERERE – MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani juu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tunaanza maswali kwa Ofisi ya Waziri Mkuu, atakayeuliza swali letu la kwanza ni Mheshimiwa Beatrice Matumbo Shellukindo kwa niaba yake Mheshimiwa Herbert Mntangi.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________________ MKUTANO WA KUMI Kikao cha Saba – Tarehe 6 Februari, 2008 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita Katibu kwa orodha ya shughuli za leo, ninapenda kwanza nimpongeze Corporal Fauster. Napenda niwafahamisheni, ni mara ya kwanza katika historia ya Bunge letu Spika kutanguliwa na Sergeant-At-Arms ambaye ni mwanamke. Tulikwishasema awali Bunge hili litaendeshwa kwa viwango na viwango ni pamoja na kuzingatia jinsia. Hakuna kazi ambazo ni za wanaume tu peke yao. Ahsante sana Corporal Fauster. (Makofi) Waheshimiwa Wabunge, nimerejea, nimesitisha safari ya Marekani. Nalazimika kutoa maelezo kwa sababu ya maneno mengi tu. Safari ile kwenda kule ilipangwa kwa kuzingatia mambo mawili :- Moja, ni umuhimu tu wake. Wenzetu Amerika, wiki ya pili ya Mwezi Februari kila mwaka mihimili yote mitatu ya Dola wanakaa pamoja kwa mlo wa asubuhi, inaitwa National Prayer Breakfast. Pamoja na mambo mengi yatakayofanyika, Rais wao ataongea pale kwenye Prayers Breakfast. Lakini wanawatambua baadhi ya viongozi mashuhuri ambao wana ushirikiano mwema nao. Mimi kama Spika wa Bunge hili, nilialikwa kwa msingi huo. Kwa hiyo, hoja kwamba labda ningeweza kumtuma mtu mwingine, haipo kwa sababu ni mwaliko wa heshima kwa jina. (Makofi) La pili ni kwamba, nikitazama ratiba na Kanuni ya 24 ya Bunge, ilikuwa ni kwamba Miswada inaendelea na kwa hiyo, nilidhani mambo mengine kama vile taarifa za Kamati yangekuja kama ilivyo kawaida katika wiki ya mwisho, na mimi nilikuwa narudi Ijumaa asubuhi. Kwa hiyo, yote yangewezekana. Sasa hilo lilishindikana, niliwaarifu wenyeji wetu kule Marekani na wamesikitika, lakini wamesema kama wanasiasa, wameelewa,kwa sababu niliwaeleza mazingira ambayo yalinifanya nisiende.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge Mkutano Wa Kumi Na Nane
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Tatu - Tarehe 28 Januari, 2010 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Muuliza swali wa kwanza ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani. MHE. HAMAD RASHID MOHAMED : Mheshimiwa Spika, ahsante. Mheshimiwa Waziri Mkuu nafikiri unakumbuka tarehe 5 Novemba, 2009 Dr. Aman Abeid Karume na Maalim Seif Sharif Hamad, walikutana na hatimaye chama cha CUF kikamtambua na kuitambua Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Ni nini position ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania juu ya maridhiano haya? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, wako watu watatu au wanne wakisimama najua ni yaleyale tu. (Kicheko) Mheshimiwa Spika, sina hakika kama nitakuwa na jibu zuri sana, lakini niseme kwamba tunao mfumo mzuri sana wa namna ya kufanya maamuzi makubwa kama haya. Sasa ni kweli jambo hili limetokea pale Zanzibar lakini mimi imani yangu ni kwamba katika kutekeleza ule mfumo wa namna ya kufanya maamuzi yafikie ukomo wake naamini ndani ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na kwa kutumia Kamati maalumu ya Chama cha Mapinduzi ndani ya Zanzibar bila shaka jambo hili litakuwa tayari limeshazungumzwa, ndiyo imani yangu mimi. (Makofi) Naamini vilevile kwamba baada ya hapo hatua itakayofuata ni kulileta jambo hili sasa formally kwenye Chama cha Mapinduzi kupitia Kamati Kuu pamoja na Halmashauri Kuu ya Taifa. Kwa hiyo, kama ni jibu sahihi juu ya nini mtazamo wa Serikali itakuwa ni baada ya chama kuwa kimefanya maamuzi na kuielekeza Serikali ifanye nini katika jambo hili.
    [Show full text]
  • Bunge La Tanzania
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Kwanza – Tarehe 9 Juni, 2009 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) WIMBO WA TAIFA (Hapa Wabunge Waliimba Wimbo wa Taifa) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta ) Alisoma Dua KIAPO CHA UAMINIFU Mbunge afuataye aliapa Kiapo cha Uaminifu na kukaa katika nafasi yake Bungeni:- Mheshimiwa Lolensia Jeremiah Maselle Bukwimba SPIKA: Ahsante sana, leo shamrashamra zimepita kiasi; nimetafuta ushauri wa sheria bado sijapewa kuhusu shamrashamra hizi kwa kiwango hiki kama inaruhusiwa kwa kanuni lakini hayo sasa ni ya baadaye. (Kicheko) T A A R I F A Y A S P I K A SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, katika Mkutano wa Kumi na Tano wa Bunge hili, tulipitisha Miswada mitano ya sheria iitwayo The Human DNA Regulation Bill, 2009, The Fertilizers Bill, 2009, The Insurance Bill, 2009, The Water Resources Management Bill, 2009 na The Water Supply and Sanitation Bill, 2009. Mara baada ya kupitishwa na Bunge na baadae kupita katika hatua zake zote za uchapishaji, Miswada hiyo ilipelekwa kwa Mheshimiwa Rais ili kupata kibali chake kwa mujibu wa Katiba. Kwa taarifa hii, nafurahi kuwaarifu Wabunge wote na Bunge hili Tukufu kwamba, tayari Mheshimiwa Rais amekwishatoa kibali kwa Miswada yote hiyo mitano na sasa ni sheria za nchi, ambapo The Human DNA Regulation Act, 2009 inakuwa ni Sheria Namba Nane ya Mwaka 2009; The Fertilizers Act, 2009 ni Sheria Namba Tisa ya 1 Mwaka 2009; The Insurance Act, 2009 ni Namba Kumi ya Mwaka 2009; The Water Resources Management, Act 2009 ni Namba Kumi na Moja ya Mwaka 2009; na Sheria Namba Kumi na Mbili ya Mwaka 2009 ni ile ya Water Supply and Sanitation Act, 2009.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Tano - Tarehe 16 Julai, 2003 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Pius Msekwa) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA SAYANSI, TEKNOLOJIA NA ELIMU YA JUU: Hotuba ya Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu kwa Mwaka wa Fedha 2003/2004. MHE. MARGARETH A. MKANGA (k.n.y. MHE. OMAR S. KWAANGW’ - MWENYEKITI WA KAMATI YA HUDUMA ZA JAMII): Taarifa ya Kamati ya Huduma za Jamii kuhusu utekelezaji wa Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu katika mwaka uliopita, pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka 2003/2004. MASWALI NA MAJIBU Na. 239 Majimbo ya Uchaguzi MHE. JAMES P. MUSALIKA (k.n.y. MHE. DR. WILLIAM F. SHIJA) aliuliza:- Kwa kuwa baadhi ya Majimbo ya Uchaguzi ni makubwa sana kijiografia na kwa wingi wa watu; je, Serikali itashauriana na Tume ya Uchaguzi ili kuongeza Majimbo ya Uchaguzi katika baadhi ya maeneo nchini katika Uchaguzi wa mwaka 2005? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (MHE. MUHAMMED SEIF KHATIB) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kabla ya kujibu swali la Mheshimiwa Dr. William Shija, Mbunge wa Sengerema, naomba kutoa maelezo yafuatayo:- Mheshimiwa Spika, lilipokuwa linajibiwa swali la Mheshimiwa Ireneus Ngwatura, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi na pia swali la Mheshimiwa Sophia Simba, Mbunge wa Viti Maalum, CCM 1 katika Mikutano ya Saba na Kumi na Moja sawia ya Bungeni, nilieleza kwamba, kwa mujibu wa Ibara ya 75(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungao wa Tanzania 1977, Jamhuri ya Muungano inaweza kugawanywa katika Majimbo ya Uchaguzi kwa idadi na namna itakavyoamuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi baada ya kupata kibali cha Mheshimiwa Rais.
    [Show full text]
  • Issued by the Britain-Tanzania Society No 105 May - Aug 2013
    Tanzanian Affairs Text 1 Issued by the Britain-Tanzania Society No 105 May - Aug 2013 Even More Gas Discovered Exam Results Bombshell Rising Religious Tensions The Maasai & the Foreign Hunters Volunteering Changed my Life EVEN MORE GAS DISCOVERED Roger Nellist, the latest volunteer to join our panel of contributors reports as follows on an announcement by Statoil of their third big gas discovery offshore Tanzania: On 18 March 2013 Statoil and its co-venturer ExxonMobil gave details of their third high-impact gas discovery in licence Block 2 in a year. The new discovery (known as Tangawizi-1) is located 10 kilometres from their first two discoveries (Lavani and Zafarani) made in 2012, and is located in water depth of 2,300 metres. The consortium will drill further wells later this year. The Tangawizi-1 discovery brings the estimated total volume of natural gas in-place in Block 2 to between 15 and 17 trillion cubic feet (Tcf). Depending on reservoir characteristics and field development plans, this could result in recoverable gas volumes in the range of 10-13 Tcf from just this one Block. These are large reserves by international stand- ards. By comparison, Tanzania’s first gas field at Songo Songo island has volumes of about 1 Tcf. Statoil has been in Tanzania since 2007 and has an office in Dar es Salaam. It operates the licence on Block 2 on behalf of the Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) and has a 65% working interest, with ExxonMobil Exploration and Production Tanzania Limited holding the remaining 35%. It is understood that under the Production Sharing Agreement that governs the operations, TPDC has the right to a 10% working participation interest in case of a development phase.
    [Show full text]
  • TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity?
    TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? With Partial Support from a TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? ACKNOWLEDGEMENTS This review was compiled and edited by Tanzania Development Research Group (TADREG) under the supervision of the Steering Group of Policy Forum members, and has been financially supported in part by Water Aid in Tanzania and Policy Forum core funders. The cartoons were drawn by Adam Lutta Published 2013 For more information and to order copies of the review please contact: Policy Forum P.O Box 38486 Dar es Salaam Tel: +255 22 2780200 Website: www.policyforum.or.tz Email: [email protected] ISBN: 978-9987 -708-09-3 © Policy Forum The conclusions drawn and views expressed on the basis of the data and analysis presented in this review do not necessarily reflect those of Policy Forum. Every effort has been made to verify the accuracy of the information contained in this review, including allegations. Nevertheless, Policy Forum cannot guarantee the accuracy and completeness of the contents. Whereas any part of this review may be reproduced providing it is properly sourced, Policy Forum cannot accept responsibility for the consequences of its use for other purposes or in other contexts. Designed by: Jamana Printers b TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? TABLE OF CONTENTS POLICY FORUM’s OBJECTIVES .............................................................................................................
    [Show full text]
  • Tanzania Human Rights Report 2008
    Legal and Human Rights Centre Tanzania Human Rights Report 2008: Progress through Human Rights Funded By; Embassy of Finland Embassy of Norway Embassy of Sweden Ford Foundation Oxfam-Novib Trocaire Foundation for Civil Society i Tanzania Human Rights Report 2008 Editorial Board Francis Kiwanga (Adv.) Helen Kijo-Bisimba Prof. Chris Maina Peter Richard Shilamba Harold Sungusia Rodrick Maro Felista Mauya Researchers Godfrey Mpandikizi Stephen Axwesso Laetitia Petro Writers Clarence Kipobota Sarah Louw Publisher Legal and Human Rights Centre LHRC, April 2009 ISBN: 978-9987-432-74-5 ii Acknowledgements We would like to recognize the immense contribution of several individuals, institutions, governmental departments, and non-governmental organisations. The information they provided to us was invaluable to the preparation of this report. We are also grateful for the great work done by LHRC employees Laetitia Petro, Richard Shilamba, Godfrey Mpandikizi, Stephen Axwesso, Mashauri Jeremiah, Ally Mwashongo, Abuu Adballah and Charles Luther who facilitated the distribution, collection and analysis of information gathered from different areas of Tanzania. Our 131 field human rights monitors and paralegals also played an important role in preparing this report by providing us with current information about the human rights’ situation at the grass roots’ level. We greatly appreciate the assistance we received from the members of the editorial board, who are: Helen Kijo-Bisimba, Francis Kiwanga, Rodrick Maro, Felista Mauya, Professor Chris Maina Peter, and Harold Sungusia for their invaluable input on the content and form of this report. Their contributions helped us to create a better report. We would like to recognize the financial support we received from various partners to prepare and publish this report.
    [Show full text]