Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document) Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE __________________ MKUTANO WA TANO Kikao cha Nne – Tarehe 11 Novemba, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe.George B. Simbachawene) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 41 Serikali Kuwatengea Maeneo Wafanyabiashara Ndogondogo MHE. JOSEPHINE T. CHAGULLA aliuliza:- Biashara ndogondogo kama Wamachinga na Mama lishe, huwawezesha wananchi kujiajiri na kujipatia vipato ili kukabiliana na ugumu wa maisha:- Je, kwa nini Serikali isiwajengee wafanyabiashara hao wadogowadogo maeneo ya kufanyia biashara ili kuondoa kero na usumbufu wanaoupata? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Thabitha Chagulla, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, biashara ndogondogo ni biashara zinazoendeshwa katika mfumo wa wa sekta isiyo rasmi (Informal Sector) zikiwa na mitaji midogo. Serikali inatambua kuwepo kwa wafanyabiashara ndogondogo katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu kwa maana ya Vijijini na Mijini. Kundi hili la Watanzania linachangia katika ukuaji wa ajira za kujiajiri, kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla. Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikitenga maeneo kwa ajili ya wafanyabiashara ndogondogo likiwemo Jiji la Dar-es-Salaam ambapo katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, maeneo yaliyotengwa ni Mchikichini, Mtaa wa Kilwa, Kibasila, Kigogo Sambusa, Mtaa wa Lumumba, Soko la Kisutu, Ilala na Buguruni, masoko mapya ya Kitunda, Tabata, Segerea na Ukonga. Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, maeneo ya TAZARA, Tandika, Mbagala Rangi Tatu, Soko la Temeke Stereo na masoko mengine na Manispaa ya Kinondoni maeneo ya Kapera, Babati, Manzese, Msufini, Mikocheni, Sinza I na II, Mabibo, Mburahati, Urafiki, Tegeta, Makumbusho na Kawe. Zoezi hili ni endelevu na linasisitiza Mamlaka za Serikali za Mitaa kuendelea kutenga maeneo na kutoa elimu kulingana na upatikanaji wa fedha. Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika kupitia Mpango wa Urasimishaji wa Rasilimali na Biashara za Wanyonge, Tanzania inawezesha Watanzania kwa kuwapa mafunzo kwa lengo la kuwajengea uwezo wamiliki wa biashara ili waweze kutambuliwa rasmi katika mfumo wa Sekta rasmi na kukuza mitaji yao na kupanua wigo wa shughuli zao. 1 Kupitia Mpango huu wafanyabiashara wapatao 1,030 wamepatiwa mafunzo katika Jiji la Dar-es-Salaam kuhusu usajili wa biashara na manufaa yake, utunzaji wa kumbukumbu na hesabu za biashara, usimamizi wa biashara na utumiaji wa huduma za kibenki. Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutumia fursa hii kuziagiza Mamlaka zote za Serikali za Mitaa kutekeleza agizo la Serikali la kutenga maeneo kwa ajili ya wafanyabiashara ili kuwaondolea adha na kuongeza tija ya biashara hizo. Aidha, Halmashauri za Wilaya, Manispaa na Miji, ziweke kipaumbele cha kujenga masoko ya biashara ndogo ambayo yatakodishwa kwa wafanyabiashara hao. MHE. JOSEPHINE T. CHAGULLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri kabisa ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza swali moja la nyongeza kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kumekuwa na ongezeko kubwa sana la wafanyabiashara ndogondogo na mama lishe katika Mikoa yenye maeneo ya machimbo, kama Mkoa wa Geita. Je, Serikali haioni kuna haja ya kuwapa mikopo wafanyabiashara hawa ili angalao waweze kuinua hali zao za maisha? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Josephine Thabitha Chagulla, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hili wala hatuna ubishi nalo. Suala hili la kuwasaidia wafanyabiashara wadogowadogo, ukiangalia Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi, inawazungumzia kwa kina sana na ndio maana hapa tumetoa maelekezo. Lakini utaratibu tunaoutumia katika Halmashauri tulikuwa tunashauri kwamba, hawa wafanyabiashara, wawe wanajiunga na SACCOS ili iwe ni rahisi kuweza kuwakopesha kama inavyoelekezwa hapa. Wizara ya Maendeleo ya Jamii nayo imekuwa inatoa mikopo kwa ajili ya kuwasaidia hawa akinamama. Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ninataka nimpongeze sana Mheshimiwa Tabitha, kwa mpango huu anaokuja nao na awe na hakika kwamba tutamuunga mkono huko Geita, kwa ajili ya kuwasaidia hawa akinamama ambao siku hizi tunawaita mama lishe na wala sio mama ntilie. MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru kwa kuniona. Katika majibu yake ya msingi kuna maeneo yametajwa ambayo yako ndani ya Jimbo la Ubungo, maeneo ya masoko ya Manzese, Sinza, Mabibo pamoja na Urafiki. Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini wakati wa uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2010, Rais Kikwete alipohutubia Dar-es-Salaam aliahidi kwamba, katika kipindi hiki Serikali itajenga Machinga Complex kwa kila Manispaa za Dar-es-Salaam. Sasa kwenye haya maeneo yote yaliyotajwa ya Manispaa ya Kinondoni, hakuna eneo ambalo lina ukubwa wa kuweza kujenga Machinga Complex. Je, Ofisi ya Waziri Mkuu, iko tayari kwa kushirikiana na Wizara nyingine za Serikali, kwa kuwa eneo la Ubungo, kuna eneo pale la Ubungo Industrial Area, ambalo lina maeneo makubwa ambayo mengi yametelekezwa kwa sababu ya matatizo ya ubinafsishaji. Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali iko tayari kuchukua eneo mojawapo ili kuweza kupata eneo pana zaidi la wafanyabiashara pale Ubungo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mnyika, Mbunge wa Ubungo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa anachosema kuhusu Mheshimiwa Rais, ni kweli. Hakuagiza tu kwa ajili ya Manispaa hizi za Temeke, Ilala pamoja na Kinondoni, ameagiza kwa nchi 2 nzima, yaani na Geita na wapi, wote. Kwamba, tuwe na utaratibu ambao tutakuwa tunawasaidia vijana wetu hawa wanaofanya biashara hizi tunazozizungumzia ili wake mahali, badala ya kuwa wanatembea na soksi mkononi na sahani na kanda na nini, tuwe na utaratibu. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu tunachozungumza hapa ni the political economy of capitalism na the political economy of socialism. The relations of production ambazo zinatengenezwa pale, ndicho kinachozungumzwa hapa; mahusiano ya uzalishaji mali, ndicho kinachosemwa hapa. Kwa hiyo, sasa sisi kwa muelekeo tunaokwendanao sasa hivi hapa, tuna mwelekeo huo unaokwenda unaangalia pia. Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Mheshimiwa Mnyika, amekuja na hili wazo analolizungumza hapa. Mimi najua yeye ni Mjumbe, anaingia katika Jiji na kule kwenye Jiji, Jiji ndilo linalosimamia hizi biashara zote. Hata hii Machinga Complex ambayo tumeizungumzia hapa iko chini ya Jiji la Dar es Salaam. MWENYEKITI: Mheshimiwa, sogeza Mic. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hii tunayoizungumza hapa sasa hivi, iko chini ya Jiji. Kwa hiyo, hili eneo analosema hili la Ubungo Industrial hili, mimi siwezi kulijibia hapa kwa sababu siwezi kujua kwamba wamepanga nini. Kinachotakiwa sasa ni kuchukua wazo hili. Mimi nitamsaidia Mheshimiwa Mbunge, kuzungumza hapa na akina Kingobi pamoja na Meya, ili tuone kama hilo eneo nalolisema hapa linaweza likatumika, Kwa sababu nikijibu hapa unaweza ukakuta kwamba kule kuna mipango mingine. Kwa hiyo mimi ninakaribisha mawazo yako ni mawazo mazuri. Tutashirikiananayo ili kuhakikisha kwamba tunawasaidia katika jambo hili. MHE. ABAS Z. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Mheshimiwa Naibu Waziri, kama swali linavyojieleza ni kweli kwamba majukumu ya Machinga ni ya Jiji. Lakini kutokana na uwezo wa Jiji, Jiji linategemea Serikali iwape uwezo, kwa hiyo, bado suala hili liko chini ya Serikali Kuu. MWENYEKITI: Mheshimiwa Naibu Waziri, pamoja na hilo lakini ni lini wale Machinga wa Mchikichini watahamia kwenye jengo la Ilala? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mtemvu na swali lako Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kwa heshima yako, hili la wale wafanyabiashara wa Mchikichini pale, najua ndicho kinachosemwa. Kwa hiyo, basi wale walioko katika Machinga Complex hawaruhusiwi kuendesha biashara pale… MBUNGE FULANI: Hatusikii. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani watanisikia. Mheshimiwa Mwenyekiti, hili tatizo la Mchikichini linalosemwa hapa, hili ambalo umelizungumza hapa, tatizo hilo ni kwamba wanachozungumza ni kwamba wafanye mpango wale walioko katika lile soko la mchikichini waondoke pale ili sasa warudi kwenye hii Machinga Complex wafanye biashara pale. (Makofi) Sasa suala hili, lilinahusu Manispaa ya Ilala; wamezungumza mle na wamevutana pale, hawajaelewana. Mpaka sasa hivi tunavyozungumza pale hawajaondoka na walio wengi pale ni 30% tu ndio ambao wameingia katika hii Machinga Complex ambayo tunaizungumzia hapa. Nimecheki nao, hata asubuhi hii nimezungumza nao; tumesema hivi, waendeleze mjadala ule, wazungumze namna ya kuliondoa lile soko pale ili sasa liweze kuruhusu hili jingine. Mamlaka hizi za 3 Serikali za Mitaa zina madaraka kamili, kwa hiyo, zenyewe ndizo zinazoamua kufanya hivyo kama unavyozungumza hapa. Mheshimiwa Mwenyekiti, hili la pili analolisema Mheshimiwa Mtemvu, ni kweli hata hii Machinga Complex ambayo tumeijenga pale, Serikali Kuu ilichofanya ni ku-facilitate, kusaidia kwa maana ya kupata mkopo kutoka NSSF, ndicho kilichofanyika
Recommended publications
  • Online Document)
    NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Arobaini na Sita – Tarehe 8 Julai, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Mussa Z. Azzan) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, maswali na tunaanza na ofisi ya Waziri, Mheshimiwa Kayombo, kwa niaba yake Mheshimiwa Rage. Na. 321 Ofisi kwa ajili ya Tarafa-Mbinga MHE. ISMAIL A. RAGE (K.n.y. MHE. GAUDENCE C. KAYOMBO) aliuliza:- Wilaya ya Mbinga ina tarafa sita lakini tarafa zote hazina ofisi rasmi zilizojengwa:- Je, ni lini Serikali itajenga ofisi kwa Makatibu Tarafa? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Gaudence Cassian Kayombo, Mbunge wa Mbinga Mashariki kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Ruvuma una jumla ya tarafa 24 yaani Tunduru wako saba, Mbinga wana tarafa sita, Nyasa wana tarafa tatu, Namtumbo wana tarafa tatu na Songea wana tarafa tano. Ni kweli tarafa za Wilaya ya Mbinga hazina ofisi rasmi zilizojengwa na Serikali. Ujenzi wa hizo ofisi unafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Kwa sasa Mkoa wa Ruvuma umeweka kipaumbele katika ujenzi wa ofisi nne za tarafa katika Wilaya ya Nyasa na Tunduru. Tarafa hizo ni Luhuhu (Lituhi-Nyasa), Ruhekei (Mbamba bay-Nyasa), Mpepo (Tinga-Nyasa) na Nampungu (Nandembo-Tunduru). Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2014/2015, Mkoa ulitenga shilingi milioni mia tatu kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya Tarafa ya Luhuhu (Lituhi), Ruhekei (Mbamba bay), Mpepo (Tingi) na Nampungu (Nandembo).
    [Show full text]
  • Madini News Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Toleo Na.2 Wa Tanzania Machi, 2020 HALIUZWI
    Toleo Na.2 // Machi 2020 Yaliyomo // Biteko - Nitasimama na Mzee Tume ya Leseni ya TanzaniteOne Imefutwa na Kisangani mpaka “asimame” Kurudishwa Serikalini - Biteko... Uk.04 ... Uk.08 Madini Bilioni 66.5 zapatikana tangu Wanawake Tume ya Madini kuanzishwa kwa masoko Wawakumbuka ya madini ... Uk.10 Yatima ... Uk.18 www.tumemadini.go.tz Tume ya Madini 2020 www.tumemadini.go.tz /TAHARIRI Salamu Kutoka kwa Waziri wa Madini Maoni ya Mhariri SEKTA YA MADINI INAIMARIKA, MAFANIKIO MASOKO TUENDELEZE USHIRIKIANO YA MADINI TUMEWEZA! Katika Mwaka wa Fedha 2019/2020 Wizara ya Madini ilipanga kutekeleza majukumu yake kupitia miradi Katika kuhakikisha kuwa Sekta ya Madini inakuwa na mchango mbalimbali ikilenga katika kuimarisha Sekta ya Madini, hivyo kuwa na mchango mkubwa kwenye ukuaji wa mkubwa kwenye ukuaji wa uchumi wa Taifa, Serikali kupitia uchumi wa nchi. Tume ya Madini kuanzia Machi, 2019 ilifungua masoko ya madini Katika Toleo lililopita nilielezea kwa kifupi kuhusu yale ambayo yamesimamiwa na kutekelezwa na Wizara na vituo vya ununuzi wa madini lengo likiwa ni kudhibiti utorosh- kwa kipindi cha takribani miaka miwili tangu kuanzishwa kwake. waji wa madini kwa kuwapatia wachimbaji wa madini nchini Katika Toleo hili nitaelezea kwa kifupi mafanikio ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara kwa kipindi cha sehemu ya kuuzia madini yao huku wakilipa kodi mbalimbali kuanzia Julai, 2019 hadi Februari, 2020. Kama ambavyo nilieleza Bungeni katika Hotuba yangu wakati Serikalini. nikiwasilisha Bajeti ya Wizara kwa Mwaka 2019/2020, nilieleza kuwa, Wizara imepangiwa kukusanya Shilingi 470,897,011,000.00 katika Mwaka wa Fedha 2019/2020. Uanzishwaji wa masoko ya madini na vituo vya ununuzi wa Napenda kuwataarifu wasomaji wa Jarida hili kuwa, hadi kufikia Februari, 2020 jumla ya Shilingi madini ni sehemu ya maelekezo yaliyotolewa kwenye mkutano wa 319,025,339,704.73 zimekusanywa ambazo ni sawa na asilimia 102 ya lengo la makusanyo ya nusu mwaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tazania, Dkt.
    [Show full text]
  • Bunge La Tanzania
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Kwanza – Tarehe 9 Juni, 2009 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) WIMBO WA TAIFA (Hapa Wabunge Waliimba Wimbo wa Taifa) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta ) Alisoma Dua KIAPO CHA UAMINIFU Mbunge afuataye aliapa Kiapo cha Uaminifu na kukaa katika nafasi yake Bungeni:- Mheshimiwa Lolensia Jeremiah Maselle Bukwimba SPIKA: Ahsante sana, leo shamrashamra zimepita kiasi; nimetafuta ushauri wa sheria bado sijapewa kuhusu shamrashamra hizi kwa kiwango hiki kama inaruhusiwa kwa kanuni lakini hayo sasa ni ya baadaye. (Kicheko) T A A R I F A Y A S P I K A SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, katika Mkutano wa Kumi na Tano wa Bunge hili, tulipitisha Miswada mitano ya sheria iitwayo The Human DNA Regulation Bill, 2009, The Fertilizers Bill, 2009, The Insurance Bill, 2009, The Water Resources Management Bill, 2009 na The Water Supply and Sanitation Bill, 2009. Mara baada ya kupitishwa na Bunge na baadae kupita katika hatua zake zote za uchapishaji, Miswada hiyo ilipelekwa kwa Mheshimiwa Rais ili kupata kibali chake kwa mujibu wa Katiba. Kwa taarifa hii, nafurahi kuwaarifu Wabunge wote na Bunge hili Tukufu kwamba, tayari Mheshimiwa Rais amekwishatoa kibali kwa Miswada yote hiyo mitano na sasa ni sheria za nchi, ambapo The Human DNA Regulation Act, 2009 inakuwa ni Sheria Namba Nane ya Mwaka 2009; The Fertilizers Act, 2009 ni Sheria Namba Tisa ya 1 Mwaka 2009; The Insurance Act, 2009 ni Namba Kumi ya Mwaka 2009; The Water Resources Management, Act 2009 ni Namba Kumi na Moja ya Mwaka 2009; na Sheria Namba Kumi na Mbili ya Mwaka 2009 ni ile ya Water Supply and Sanitation Act, 2009.
    [Show full text]
  • Check Against Delivery HOTUBA YA WAZIRI MKUU, MHESHIMIWA
    Check Against Delivery HOTUBA YA WAZIRI MKUU, MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA, (MB), WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA SITA WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, DODOMA, TAREHE 9 FEBRUARI, 2007 Mheshimiwa Spika, Mkutano wa sita wa Bunge lako Tukufu umehitimisha shughuli zote zilizokuwa zimepangwa. Mkutano huu ni wa kwanza baada ya Serikali ya Awamu ya Nne kutimiza mwaka mmoja madarakani. Taarifa za mafanikio na changamoto zilizojitokeza zimewasilishwa kupitia mikutano mbalimbali ya Chama Tawala, Serikali na vyombo mbalimbali vya habari. Mheshimiwa Spika, kwa masikitiko makubwa, nachukua nafasi hii tena kwa niaba ya Serikali na wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kutoa rambirambi kwako wewe Mheshimiwa Spika, kwa Waheshimiwa Wabunge wote, kwa familia, jamaa na marafiki kwa msiba uliotokana na kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tunduru, na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Bunge na Uratibu) Marehemu Juma Jamaldin Akukweti. Wote tulimfahamu Marehemu Akukweti kwa umakini na umahiri wake hapa Bungeni. Marehemu Akukweti alifariki kutokana na ajali ya ndege iliyokuwa inamrejesha Dar es Salaam baada ya kumaliza kazi ya kukagua soko la Mwanjelwa lililoteketea kwa moto mkoani Mbeya. Katika ajali hiyo Watumishi wa Serikali walipoteza maisha. Watumishi hao ni Bibi Theresia Nyantori, Mwandishi wa Habari wa Idara ya Habari; Bwana Nathaniel Katinila, Mratibu wa Mradi wa Masoko; na Bwana George Bendera, Afisa Habari Idara ya Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu. Majeruhi katika ajali hiyo ambao bado wanapata matibabu lakini wametoka hosptali ni Bw. Nisetas Kanje, Katibu wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Bunge na Uratibu); na rubani wa ndege hiyo Bw. Martin Sumari. Tunamwomba Mwenyezi Mungu awasaidie majeruhi wote waweze kupona haraka na kurudia katika afya zao.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA KUMI NA SITA ______________ Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 27 Julai, 2009) (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita anayeuliza swali la kwanza, karibuni tena baada ya mapumziko ya weekend, nadhani mna nguvu ya kutosha kwa ajili ya shughuli za wiki hii ya mwisho ya Bunge hili la 16. Swali la kwanza linaelekezwa Ofisi ya Waziri Mkuu na linauliza na Mheshimiwa Shoka, kwa niaba yake Mheshimiwa Khalifa. Na.281 Kiwanja kwa Ajili ya Kujenga Ofisi ya Tume ya Kudhibiti UKIMWI MHE KHALIFA SULEIMAN KHALIFA (K.n.y. MHE. SHOKA KHAMIS JUMA) aliuliza:- Kwa kuwa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI inakabiliwa na changamoto ya ufinyu wa Ofisi; na kwa kuwa Tume hiyo imepata fedha kutoka DANIDA kwa ajili ya kujenga jengo la Ofisi lakini inakabiliwa na tatizo kubwa la upatikanaji wa kiwanja:- Je, Serikali itasaidia vipi Tume hiyo kupata kiwanja cha kujenga Ofisi? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU – SERA, URATIBU NA BUNGE alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shoka Khamis Juma, Mbunge wa Micheweni kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, tatizo la kiwanja cha kujenga Ofisi za TACAIDS limepatiwa ufumbuzi na ofisi yangu imewaonesha Maafisa wa DANIDA kiwanja hicho Ijumaa tarehe 17 Julai, 2009. Kiwanja hicho kipo Mtaa wa Luthuli Na. 73, Dar es Salaam ama kwa lugha nyingine Makutano ya Mtaa wa Samora na Luthuli. MHE. KHALIFA SULEIMAN KHALIFA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Waziri, naomba kumuuliza swali moja la nyongeza.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 18 Julai, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita muuliza swali la kwanza nina matangazo kuhusu wageni, kwanza wale vijana wanafunzi kutoka shule ya sekondari, naona tangazo halisomeki vizuri, naomba tu wanafunzi na walimu msimame ili Waheshimiwa Wabunge waweze kuwatambua. Tunafurahi sana walimu na wanafunzi wa shule zetu za hapa nchini Tanzania mnapokuja hapa Bungeni kujionea wenyewe demokrasia ya nchi yetu inavyofanya kazi. Karibuni sana. Wapo Makatibu 26 wa UWT, ambao wamekuja kwenye Semina ya Utetezi na Ushawishi kwa Harakati za Wanawake inayofanyika Dodoma CCT wale pale mkono wangu wakulia karibuni sana kina mama tunawatakia mema katika semina yenu, ili ilete mafanikio na ipige hatua mbele katika kumkomboa mwanamke wa Tanzania, ahsanteni sana. Hawa ni wageni ambao tumetaarifiwa na Mheshimiwa Shamsa Selengia Mwangunga, Naibu Waziri wa Maji. Wageni wengine nitawatamka kadri nitakavyopata taarifa, kwa sababu wamechelewa kuleta taarifa. Na. 223 Barabara Toka KIA – Mererani MHE. DORA H. MUSHI aliuliza:- Kwa kuwa, Mererani ni Controlled Area na ipo kwenye mpango wa Special Economic Zone na kwa kuwa Tanzanite ni madini pekee duniani yanayochimbwa huko Mererani na inajulikana kote ulimwenguni kutokana na madini hayo, lakini barabara inayotoka KIA kwenda Mererani ni mbaya sana
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Tisa – Tarehe 20 Julai, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne. S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Ifuatayo Iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO:- Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa Mwaka wa Fedha, 2011/2012. MASWALI NA MAJIBU Na. 268 Fedha za Ukarabati wa Barabara – Manispaa ya Kinondoni MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza:- (a) Je, Serikali hutenga wastani wa shilingi ngapi kwa ajili ya ukarabati ndani ya Manispaa ya Kinondoni, na ni utaratibu gani unatumika kufuatilia toka kwa Wahandisi wa Manispaa kuhakikisha kwamba barabara zote za Manispaa zinapatikana nyaraka zote? (b) Je, kuna utaratibu gani wowote wa kuthaminisha gharama zilizotumika na uhalisi wa kila kilichotengewa? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA LA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima James Mdee Mbunge wa Kawe lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- 1 (a) Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni hupata fedha kwa ajili ya miradi ya barabara, Madaraja na Makalvati kutoka katika Mfuko wa Barabara, ruzuku za fedha za maendeleo ya Serikali za mitaa na vyanzo vya mapato ndani ya Halmashauri. Katika mwaka wa fedha 2009/2010 Manispaa kupitia vyanzo hivyo ilipata jumla ya shilingi bilioni 4.3. Fedha hizi zilitumika kufanya matengenezo ya barabara za lami kilomita 1.65, kufanya matengenezo ya changarawe kilomita 48, kuziba viraka katika barabara za udongo kilomita 23.5 matengenezo ya madaraja ya madaraja 11, kujenga kalvati 1 na ununuzi wa Motor Grader 1.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA TATU Kikao cha Tano - Tarehe 4 Novemba, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali, tunaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu, atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Gaudence Kayombo, kwa niaba yake naona Mheshimiwa Mwambalaswa unaweza kumwulizia! Na. 53 Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbinga Kuwa Mamlaka Kamili MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA (K.n.y. MHE. GAUDENCE C. KAYOMBO) aliuza:- Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbinga umekamilisha vigezo vyote kuwa Mamlaka kamili ya Mji:- Je, ni lini Serikali itaridhia na kutekeleza ahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Gaudence C. Kayombo, Mbunge wa Mbinga Mashariki, kama ifuatavyo:- 1 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) [WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (TAMISEMI)] Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba, mwaka 2010, Mheshimiwa Rais, aliahidi kupandisha hadhi Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbinga kuwa Halmashauri ya Mji. Ahadi hii ilitokana na ukweli kwamba, Mamlaka hii imeonekana kukua kwa kasi, kwa maana ya ongezeko la watu na shughuli za kiuchumi na kijamii na hivyo Serikali inaona ipo haja ya kuipandisha hadhi ili kuingiza dhana ya Mpango Miji kwa lengo la kuzuia ukuaji holela, kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha huduma za jamii. Mheshimiwa Spika, hata hivyo, mchakato wa kuupandisha hadhi Mji wa Mbinga bado unaendelea na ofisi yangu bado haijapokea maombi kutoka Mkoa wa Ruvuma.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Kumi na Nne – Tarehe 2 Julai, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mne Jenista J. Mhagama) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma) Pamoja na (Utawala Bora) kwa mwaka wa Fedha 2012/2013. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (UTAWALA BORA) (K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, (UHUSIANO NA URATIBU): 1 Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Uhusiano na Uratibu kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. MHE. JOHN P. LWANJI (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma) Pamoja na (Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hizo kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. MHE. ANDREW J. CHENGE - MWENYEKITI WA KAMATI YA FEDHA NA UCHUMI: Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Uchumi, Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. MHE. KULIKOYELA K. KAHIGI - MSEMAJI WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA) PAMOJA NA (UTAWALA BORA): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani ya Ofisi ya Rais (Menejimentii ya Utumishi wa Umma) Pamoja na (Utawala Bora) Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hizo kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013.
    [Show full text]
  • Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1
    Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Kumi – Tarehe 16 Mei, 2014 (Mkutano Ulianza Saa tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na :- NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tukae. Mkutano wa Kumi na Tano unaanza. Kikao cha Kumi, Katibu tuendelee. NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MASWALI NA MAJIBU Na. 66 Kuhusu Mpango wa Kutenga Ardhi ili Imilikishwe kwa Wanawake Kuanzisha Mashamba ya Miti kwa Matumizi ya Mkaa na Kuni MHE. AMINA NASSORO MAKILAGI aliuliza:- Serikali inatilia mkazo utunzaji wa misitu na maeneo mengi kutengwa kama Hifadhi za Taifa na kupelekea nishati ya kuni na mkaa kuwa ghali na pia wanawake hawana ardhi ya kuweza kupanda miti ya kuni:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga ardhi ili imilikishwe kwa wanawake kuanzisha mashamba ya miti kwa matumizi ya mkaa na kuni? NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MAZINGIRA) alijibu:- 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), ningependa kujibu swali la Mheshimiwa Amina Nassoro Makilagi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua kwamba wanawake ni sehemu ya jamii, hivyo mipango ya Serikali iyopo inawajumuisha wanawake.
    [Show full text]
  • Did They Work for Us? Assessing Two Years of Bunge Data 2010-2012
    Did they work for us? Assessing two years of Bunge data 2010-2012 1. Introduction The ninth session of the Bunge (Parliament) was adjourned on 9 November 2012, two years since the commencement of the first session on 9 November 2010 following the general election. These Bunge sessions have been broadcast through private and public TV stations allowing citizens to follow their representatives’ actions. Another source of information regarding MP performance is provided by the Parliamentary On-line Information System (POLIS) posted on the Tanzania Parliament website (www.bunge.go.tz) An important question for any citizen is: how did my MP represent my interests in Parliament? One way to assess performance of MPs is to look at the number of interventions they make in Bunge. MPs can make three types of interventions: they can ask basic questions submitted in advance; they can add supplementary questions after basic questions have been answered by the government; or they can makecontributions during the budget sessions, law amendments or discussions on new laws. This brief presents six facts on the performance of MPs, from November 2010 to November 2012, updating similar analyses conducted by Twaweza in previous years. It includes an assessment of who were the least and most active MPs. It also raises questions on the significance of education level when it comes to effectiveness of participation by MPs in parliament. The dataset can be downloaded from www.twaweza.org/go/bunge2010-2012 The Bunge dataset includes observations on 351 members: MPs who were elected and served (233), MPs in Special Seats (102), Presidential Appointees (10) and those from the Zanzibar House of Representatives (5) and the Attorney General.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Sita – Tarehe 13Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa mwaka wa fedha 2011/2012. HOJA ZA SERIKALI Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka 2011/2012 - Wizara ya Nishati na Madini (Majadiliano yanaendelea) MICHANGO KWA MAANDISHI MHE. KISYERI W. CHAMBIRI: Mheshimiwa Spika, la kwanza, ni zaidi ya miaka kumi, umeme umepita katika maeneo ya Maweni, Majengo, Mukuyuni A, Mukuyuni B, Ari Halaa, Singu, Signo. Umeme huo ni wa msongo wa KV 33. Hakuna juhudi zozote zimefanywa kuwapatia wananchi umeme katika maeneo hayo. Nataka kufahamu lini wananchi wa maeneo hayo watapatiwa umeme? Mheshimiwa Spika, pili, katika bajeti ya TANESCO ya mwaka huu, fedha zimetengwa kupeleka umeme mtaa wa Muruki, Babati Mjini. Meneja wa Mkoa amekataa kupeleka umeme Muruki kwa kisingizio kuwa hakuna njia. Halmashauri ya Mji wameandika barua TANESCO na kuthibitisha njia ipo. Lini wananchi wa Muruki watapata umeme? Mheshimiwa Spika, tatu, ingawa tayari wameleta nguzo kwa ajili ya umeme Mamagha, Banga, Himiti, Haraa, hoja sasa ni muda mrefu sana, lini umeme utawekwa katika maeneo hayo? Mheshimiwa Spika, nne, muda mrefu sasa tumeomba umeme upelekwe Vijiji vya Imbilili, Mtuka, Malangi na Kiongozi. Lini maeneo hayo yatawekwa katika mpango na kupelekewa umeme? Mheshimiwa Spika, pamoja na hoja hizo hapo juu, nimeomba Meneja wa Mkoa atayarishe makisio ya maeneo hayo kupata umeme.
    [Show full text]