Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE __________________ MKUTANO WA TANO Kikao cha Nne – Tarehe 11 Novemba, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe.George B. Simbachawene) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 41 Serikali Kuwatengea Maeneo Wafanyabiashara Ndogondogo MHE. JOSEPHINE T. CHAGULLA aliuliza:- Biashara ndogondogo kama Wamachinga na Mama lishe, huwawezesha wananchi kujiajiri na kujipatia vipato ili kukabiliana na ugumu wa maisha:- Je, kwa nini Serikali isiwajengee wafanyabiashara hao wadogowadogo maeneo ya kufanyia biashara ili kuondoa kero na usumbufu wanaoupata? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Thabitha Chagulla, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, biashara ndogondogo ni biashara zinazoendeshwa katika mfumo wa wa sekta isiyo rasmi (Informal Sector) zikiwa na mitaji midogo. Serikali inatambua kuwepo kwa wafanyabiashara ndogondogo katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu kwa maana ya Vijijini na Mijini. Kundi hili la Watanzania linachangia katika ukuaji wa ajira za kujiajiri, kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla. Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikitenga maeneo kwa ajili ya wafanyabiashara ndogondogo likiwemo Jiji la Dar-es-Salaam ambapo katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, maeneo yaliyotengwa ni Mchikichini, Mtaa wa Kilwa, Kibasila, Kigogo Sambusa, Mtaa wa Lumumba, Soko la Kisutu, Ilala na Buguruni, masoko mapya ya Kitunda, Tabata, Segerea na Ukonga. Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, maeneo ya TAZARA, Tandika, Mbagala Rangi Tatu, Soko la Temeke Stereo na masoko mengine na Manispaa ya Kinondoni maeneo ya Kapera, Babati, Manzese, Msufini, Mikocheni, Sinza I na II, Mabibo, Mburahati, Urafiki, Tegeta, Makumbusho na Kawe. Zoezi hili ni endelevu na linasisitiza Mamlaka za Serikali za Mitaa kuendelea kutenga maeneo na kutoa elimu kulingana na upatikanaji wa fedha. Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika kupitia Mpango wa Urasimishaji wa Rasilimali na Biashara za Wanyonge, Tanzania inawezesha Watanzania kwa kuwapa mafunzo kwa lengo la kuwajengea uwezo wamiliki wa biashara ili waweze kutambuliwa rasmi katika mfumo wa Sekta rasmi na kukuza mitaji yao na kupanua wigo wa shughuli zao. 1 Kupitia Mpango huu wafanyabiashara wapatao 1,030 wamepatiwa mafunzo katika Jiji la Dar-es-Salaam kuhusu usajili wa biashara na manufaa yake, utunzaji wa kumbukumbu na hesabu za biashara, usimamizi wa biashara na utumiaji wa huduma za kibenki. Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutumia fursa hii kuziagiza Mamlaka zote za Serikali za Mitaa kutekeleza agizo la Serikali la kutenga maeneo kwa ajili ya wafanyabiashara ili kuwaondolea adha na kuongeza tija ya biashara hizo. Aidha, Halmashauri za Wilaya, Manispaa na Miji, ziweke kipaumbele cha kujenga masoko ya biashara ndogo ambayo yatakodishwa kwa wafanyabiashara hao. MHE. JOSEPHINE T. CHAGULLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri kabisa ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza swali moja la nyongeza kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kumekuwa na ongezeko kubwa sana la wafanyabiashara ndogondogo na mama lishe katika Mikoa yenye maeneo ya machimbo, kama Mkoa wa Geita. Je, Serikali haioni kuna haja ya kuwapa mikopo wafanyabiashara hawa ili angalao waweze kuinua hali zao za maisha? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Josephine Thabitha Chagulla, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hili wala hatuna ubishi nalo. Suala hili la kuwasaidia wafanyabiashara wadogowadogo, ukiangalia Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi, inawazungumzia kwa kina sana na ndio maana hapa tumetoa maelekezo. Lakini utaratibu tunaoutumia katika Halmashauri tulikuwa tunashauri kwamba, hawa wafanyabiashara, wawe wanajiunga na SACCOS ili iwe ni rahisi kuweza kuwakopesha kama inavyoelekezwa hapa. Wizara ya Maendeleo ya Jamii nayo imekuwa inatoa mikopo kwa ajili ya kuwasaidia hawa akinamama. Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ninataka nimpongeze sana Mheshimiwa Tabitha, kwa mpango huu anaokuja nao na awe na hakika kwamba tutamuunga mkono huko Geita, kwa ajili ya kuwasaidia hawa akinamama ambao siku hizi tunawaita mama lishe na wala sio mama ntilie. MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru kwa kuniona. Katika majibu yake ya msingi kuna maeneo yametajwa ambayo yako ndani ya Jimbo la Ubungo, maeneo ya masoko ya Manzese, Sinza, Mabibo pamoja na Urafiki. Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini wakati wa uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2010, Rais Kikwete alipohutubia Dar-es-Salaam aliahidi kwamba, katika kipindi hiki Serikali itajenga Machinga Complex kwa kila Manispaa za Dar-es-Salaam. Sasa kwenye haya maeneo yote yaliyotajwa ya Manispaa ya Kinondoni, hakuna eneo ambalo lina ukubwa wa kuweza kujenga Machinga Complex. Je, Ofisi ya Waziri Mkuu, iko tayari kwa kushirikiana na Wizara nyingine za Serikali, kwa kuwa eneo la Ubungo, kuna eneo pale la Ubungo Industrial Area, ambalo lina maeneo makubwa ambayo mengi yametelekezwa kwa sababu ya matatizo ya ubinafsishaji. Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali iko tayari kuchukua eneo mojawapo ili kuweza kupata eneo pana zaidi la wafanyabiashara pale Ubungo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mnyika, Mbunge wa Ubungo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa anachosema kuhusu Mheshimiwa Rais, ni kweli. Hakuagiza tu kwa ajili ya Manispaa hizi za Temeke, Ilala pamoja na Kinondoni, ameagiza kwa nchi 2 nzima, yaani na Geita na wapi, wote. Kwamba, tuwe na utaratibu ambao tutakuwa tunawasaidia vijana wetu hawa wanaofanya biashara hizi tunazozizungumzia ili wake mahali, badala ya kuwa wanatembea na soksi mkononi na sahani na kanda na nini, tuwe na utaratibu. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu tunachozungumza hapa ni the political economy of capitalism na the political economy of socialism. The relations of production ambazo zinatengenezwa pale, ndicho kinachozungumzwa hapa; mahusiano ya uzalishaji mali, ndicho kinachosemwa hapa. Kwa hiyo, sasa sisi kwa muelekeo tunaokwendanao sasa hivi hapa, tuna mwelekeo huo unaokwenda unaangalia pia. Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Mheshimiwa Mnyika, amekuja na hili wazo analolizungumza hapa. Mimi najua yeye ni Mjumbe, anaingia katika Jiji na kule kwenye Jiji, Jiji ndilo linalosimamia hizi biashara zote. Hata hii Machinga Complex ambayo tumeizungumzia hapa iko chini ya Jiji la Dar es Salaam. MWENYEKITI: Mheshimiwa, sogeza Mic. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hii tunayoizungumza hapa sasa hivi, iko chini ya Jiji. Kwa hiyo, hili eneo analosema hili la Ubungo Industrial hili, mimi siwezi kulijibia hapa kwa sababu siwezi kujua kwamba wamepanga nini. Kinachotakiwa sasa ni kuchukua wazo hili. Mimi nitamsaidia Mheshimiwa Mbunge, kuzungumza hapa na akina Kingobi pamoja na Meya, ili tuone kama hilo eneo nalolisema hapa linaweza likatumika, Kwa sababu nikijibu hapa unaweza ukakuta kwamba kule kuna mipango mingine. Kwa hiyo mimi ninakaribisha mawazo yako ni mawazo mazuri. Tutashirikiananayo ili kuhakikisha kwamba tunawasaidia katika jambo hili. MHE. ABAS Z. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Mheshimiwa Naibu Waziri, kama swali linavyojieleza ni kweli kwamba majukumu ya Machinga ni ya Jiji. Lakini kutokana na uwezo wa Jiji, Jiji linategemea Serikali iwape uwezo, kwa hiyo, bado suala hili liko chini ya Serikali Kuu. MWENYEKITI: Mheshimiwa Naibu Waziri, pamoja na hilo lakini ni lini wale Machinga wa Mchikichini watahamia kwenye jengo la Ilala? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mtemvu na swali lako Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kwa heshima yako, hili la wale wafanyabiashara wa Mchikichini pale, najua ndicho kinachosemwa. Kwa hiyo, basi wale walioko katika Machinga Complex hawaruhusiwi kuendesha biashara pale… MBUNGE FULANI: Hatusikii. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani watanisikia. Mheshimiwa Mwenyekiti, hili tatizo la Mchikichini linalosemwa hapa, hili ambalo umelizungumza hapa, tatizo hilo ni kwamba wanachozungumza ni kwamba wafanye mpango wale walioko katika lile soko la mchikichini waondoke pale ili sasa warudi kwenye hii Machinga Complex wafanye biashara pale. (Makofi) Sasa suala hili, lilinahusu Manispaa ya Ilala; wamezungumza mle na wamevutana pale, hawajaelewana. Mpaka sasa hivi tunavyozungumza pale hawajaondoka na walio wengi pale ni 30% tu ndio ambao wameingia katika hii Machinga Complex ambayo tunaizungumzia hapa. Nimecheki nao, hata asubuhi hii nimezungumza nao; tumesema hivi, waendeleze mjadala ule, wazungumze namna ya kuliondoa lile soko pale ili sasa liweze kuruhusu hili jingine. Mamlaka hizi za 3 Serikali za Mitaa zina madaraka kamili, kwa hiyo, zenyewe ndizo zinazoamua kufanya hivyo kama unavyozungumza hapa. Mheshimiwa Mwenyekiti, hili la pili analolisema Mheshimiwa Mtemvu, ni kweli hata hii Machinga Complex ambayo tumeijenga pale, Serikali Kuu ilichofanya ni ku-facilitate, kusaidia kwa maana ya kupata mkopo kutoka NSSF, ndicho kilichofanyika