Majadiliano Ya Bunge ______
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka. -
Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA THELATHINI NA MBILI 23 MEI, 2017 MKUTANO WA SABA KIKAO CHA THELATHINI NA MBILI TAREHE 23 MEI, 2017 I. DUA: Mwenyekiti (Mhe. Mussa A. Zungu) alisoma Dua Saa 3.00 Asubuhi na kuongoza Bunge. Makatibu mezani: 1. Ndugu Joshua Chamwela 2. Ndugu Neema Msangi II. HATI ZA KUWASILISHA MEZANI (1) Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii – Mhe. Ramo Makani aliwasilisha Mezani:- - Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (2) Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii – Mhe. Khalifa Salum Suleiman aliwasilisha Mezani:- - Taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (3) Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kwa Wizara ya Maliasili na Utalii – Mhe. Roman Selasini aliwasilisha Mezani:- - Taarifa ya Upinzani kuhusu Wizara ya Maliasili na Utalii juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. 1 III. MASWALI Maswali yafuatayo yaliulizwa na kujibiwa:- WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO Swali Na. 254: Mhe. Ritta Kabati (Kny. Mhe. Mahmoud H. Mgimwa) Nyongeza: Mhe. Ritta Kabati Mhe. Elias J. Kwandikwa Mhe. James Mbatia Mhe. Venance Mwamoto Swali Na. 255: Mhe. Ignas A. Malocha Nyongeza: Mhe. Ignas A. Malocha Mhe. Oran Njenza Mhe. Omary T. Mgimba Mhe. Adamson E. Mwakasaka Mhe. Zuberi Kuchauka Mhe. -
1 BUNGE LA TANZANIA ___MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA SABA Kikao Cha Nne – Tarehe 8 Novemba, 20
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA SABA Kikao cha Nne – Tarehe 8 Novemba, 2019 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge tukae. Katibu. NDG. NEEMA MSANGI – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Taarifa ya Tatu ya Hali ya Mazingira Nchini (State of the Environment Report, 3). NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Taarifa ya Mwaka ya Tathmini ya Utendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma kwa mwaka wa fedha 2018/2019 (The Annual Performance Evaluation Report on Public Procurement Regulatory Authority for the Financial Year 2018/2019). 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MWENYEKITI: Ahsante sana. Katibu. NDG. NEEMA MSANGI – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Swali letu la kwanza linaelekezwa Ofisi ya Rais – TAMISEMI. Linaulizwa na Mheshimiwa Justin Joseph Monko, Mbunge wa Singida Kaskazini. Na. 40 Kuwa na Uchaguzi Mdogo wa Serikali za Mitaa MHE. JUSTIN J. MONKO aliuliza:- Inapotokea Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa/Kijiji amefariki au kupoteza sifa ya kuwa Mwenyekiti wa Mtaa au Kijiji husika huongozwa na Kaimu Mwenyekiti:- Je, kwa nini Serikali haioni umuhimu wa kuwepo uchaguzi mdogo kama ilivyo kwa Madiwani na Wabunge? MWENYEKITI: Ahsante. Majibu kwa swali hilo, Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Waitara. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA -
MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao Cha Arobaini Na Sita
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Arobaini na Sita – Tarehe 15 Juni, 2020 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tukae, tunaendelea na Mkutano wetu wa 19, Kikao cha 46, bado kimoja tu cha kesho. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na: NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Maelezo ya Waziri wa Fedha na Mipango kuhusu Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2020 (The Finance Bill, 2020). Muhtasari wa Tamko la Sera ya Fedha kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 (Monetary Policy Statement for the Financial Year 2020/2021). MHE. ALBERT N. OBAMA - K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI:Maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2020 (The Finance Bill, 2020). 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. RHODA E. KUNCHELA - K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KWA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO: Maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu Muswada wa Sheria ya fedha wa mwaka 2020 (The Finance Bill, 2020). MHE. DKT. TULIA ACKSON - MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KANUNI ZA BUNGE: Azimio la Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kanuni za Bunge kuhusu Marekebisho ya Kanuni za Bunge SPIKA: Asante sana Mheshimiwa Naibu Spika, Katibu MASWALI NA MAJIBU (Maswali yafuatayo yameulizwa na kujibiwa kwa njia ya mtandao) Na. 426 Migogoro ya Mipaka MHE. -
13 MEI, 2013 MREMA 1.Pmd
13 MEI, 2013 BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na Nne - Tarehe 13 Mei, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Ujenzi kwa Mwaka wa Fedha, 2013/2014. MHE. RITTA E. KABATI (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA MIUNDOMBINU): Taarifa ya Kamati ya Miundombinu Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Ujenzi kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. 1 13 MEI, 2013 MHE. PAULINA P.GEKUL - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA WIZARA YA UJENZI: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Wizara ya Ujenzi Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. MASWALI NA MAJIBU Na. 189 Fedha kwa Ajili ya Kuadhimisha Sherehe za Kitaifa MHE. HENRY D. SHEKIFU (K.n.y. MHE. MARY P. CHATANDA) aliuliza:- Katika kuadhimisha sherehe mbalimbali za Kitaifa nchini Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi sana. Je, Serikali itakuwa tayari kuokoa fedha kwa kuachana na Bajeti kubwa zilizotengwa kwa machapisho ya fulana (T- Shirts) na tafrija fupi ili fedha hizo ziweze kusaidia katika shughuli nyingine? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, URATIBU, SERA NA BUNGE alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Mary Pius Chatanda, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli maadhimisho ya sherehe za kitaifa nchini yamekuwa yakigharimu Serikali fedha nyingi sana. -
1 Bunge La Tanzania
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 9 Mei, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu. NDG. LINA KITOSI – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Randama ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NAIBU SPIKA: Katibu. NDG. LINA KITOSI - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU Na. 207 Hospitali za Wilaya MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:- Wilaya ya Itilima na Busega ni Wilaya mpya na hazina Hospitali za Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali za Wilaya kwenye Wilaya hizo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri za Wilaya ya Itilima na Busega zilianzishwa mwaka 2015 na zina idadi ya watu 346,170 kwa Itilima na 224,527 kwa Busega. Ni kweli kwamba Halmashauri hizi bado hazina Hospitali za Wilaya na wananchi wanapata huduma kupitia zahanati 45 na vituo vya afya saba ambapo kati ya hivyo zahanati 27 na vituo vya afya vitatu vipo Halmashauri ya Wilaya ya Itilima na zahanati 18 na vituo vya afya vinne vipo Halmashauri ya Wilaya ya Busega. -
MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao Cha Kumi Na Sita – Tarehe 24
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Kumi na Sita – Tarehe 24 Aprili, 2020 (Bunge Lilianza Saa Nane Mchana) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI - KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa mwaka wa fedha 2020/2021. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa mwaka wa fedha 2019/2020 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2020/2021. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI WA WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021. NAIBU SPIKA: Ahsante, Katibu. NDG. MOSSY LUKUVI - KATIBU MEZANI MASWALI NA MAJIBU (Maswali yafuatayo yameulizwa na kujibiwa kwa njia ya mtandao) Na. 143 Ujenzi wa Jengo la Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Wilaya ya Nyamagana ambayo ni kongwe imeanza kujenga jengo la Wilaya takribani miaka 6 sasa:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha jengo hili ili Mkuu wa Wilaya apate mahali pa kufanyia kazi zake kwa uhuru na eneo rafiki hata kwa watu wenye ulemavu? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula, Mbunge wa Nyamagana, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana ulianza katika mwaka wa fedha 2008/ 2009 chini ya Mhandisi Mshauri Wakala wa Majengo Tanzania - TBA kwa gharama ya Sh.1,836,843,148. -
Majadiliano Ya Bunge ______
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ BUNGE LA KUMI NA MOJA MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini na Moja – Tarehe 6 Mei, 2019 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa tukae. Katibu. NDG. PAMELA PALLANGYO – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa mwaka wa fedha, 2018/2019. MWENYEKITI: Ahsante. Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. PAMELA PALLANGYO – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU MWENYEKITI: Swali letu la kwanza leo linaulizwa na Mheshimiwa Ruth Mollel, Mbunge wa Viti Maalum na linaelekezwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Na. 166 Athari za Mtambo wa Kuchoma Takataka za Hospitali na Dawa Zilizokwisha Muda – Mkuranga MHE. RUTH H. MOLLEL aliuliza:- Mtambo wa kuchoma takataka za hospitali na dawa zilizokwisha muda wake upo katika Kijiji cha Dundani Wilayani Mkuranga. Uchomaji unapofanyika moshi mzito huingia kwenye nyumba na maeneo ya wananchi wanaoishi karibu na mtambo huo na kuhatarisha afya zao:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kunusuru afya na maisha ya wananchi wanaoishi karibu na mtambo huo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ruth Hiyob Mollel, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba upo mtambo wa kuchomea taka na dawa zilizokwisha muda wake uliojengwa na mwekezaji katika Kijiji cha Dundani, Wilaya ya Mkuranga. -
Majadiliano Ya Bunge ______
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Hamsini - Tarehe 24 Juni, 2016 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Tukae. Katibu! NDG. CHARLES MLOKA – KATIBU MEZANI: Maswali. MASWALI NA MAJIBU Na. 424 Kuigawa Halmashauri ya Wilaya ya Lindi MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA (K.n.y. MHE. HAMIDU H. BOBALI) aliuliza:- Jimbo la Mchinga na Mtama linaunda Halmashauri ya Wilaya ya Lindi na ukubwa wa Halmashauri hii ni kikwazo cha kuwafikia wananchi kwa urahisi katika kuwapelekea huduma za jamii. Je, kwa nini Serikali isiigawe Halmashauri hii ili kuwa na Halmashauri mbili yaani Mchinga na Mtama? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamidu Hassan Bobali, Mbunge wa Mchinga, kama ifuatavyo:- 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Naibu Spika, uanzishwaji wa Mamlaka ya Serikali za Mitaa unazingatia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara ya 145 na Ibara 146 na Sheria ya Serikali za Mitaa, Mamlaka ya Wilaya, Sura Namba 287 kifungu cha 5 ambazo kwa pamoja zinampa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa kuwa na Madaraka ya kuanzisha Mamlaka ya Serikali za Mitaa nchini. Mheshimiwa Naibu Spika, kusudio la kugawanya Halmashauri ni lazima likidhi vigezo vinavyowekwa kwa kuzingatia taratibu zilizopo ikiwa ni pamoja na kujadiliwa kwenye vikao vya kisheria, ikiwemo Mkutano Mkuu wa Vijiji, Kamati za Maendeleo za Kata, Baraza la Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC), Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) na baadae huwasilishwa kwa Waziri mwenye dhamana na Mamlaka ya Serikali za Mitaa. -
Bunge Newsletter
BungeNe ewsletter Issue No 007 MAY 2013 Parliament for the last seven Weeks in Budgetary Session The 11th Parliamentary Session, which is the budget Members of Parliament have scrutined the Gov- session, is in its 7th week since it started on 9th April, ernment and made sure that national develop- 2013. Up to now 283 normal questions have been asked ment priorities are been considered in every min- and answered in the Parliament. Within this time istry as a way of fulfilling their constitutional about 420 supplementary questions were asked and mandate of representation, legislation and oversight. all of them received answers from the Government. The number of Members of Parliament who have According to the Parliamentary Standing Orders, contributed to the budget discussions per each min- every Thursday, it’s Prime Minister’s questions and istry up to now is as follows: The Office of Prime up to the end of May more than 20 questions had Minister [114 Contributors], President’s Office [17 been asked and answered by the Prime Minister. Contributions], Office of Vice President [6 Con- Despite of the normal Q&A session in the Parliament, tributors], Ministry of Agriculture, Food and Co- during this session, Parliament has also continued operative [45 Contributors], Ministry of Water discussing and approving ministries budget estimates [43 Contributors], Ministry of Natural resources for the financial year 2013/14. So far 28 ministries have and tourism [34 Contributors], Ministry of Jus- already presented their budget estimates in the House. tice and Constitutional affairs [7 Contributors]. After the change of the Budget Cycle to the current Others are the Ministry of Defense and Na- one, the entire exercise of discussing and approv- tional Service[9 Contributors],Ministry of ing the budget estimates has received a ernomous Home affairs[43 Contributors], Ministry of contributions from the Members of Parliament. -
MAWASILIANO SERIKALINI Mkuu Wa Kitengo Cha Florence Temba 022 2122942 0784246041 Mawasiliano Serikalini KITENGO CHA UGAVI NA UNUNUZI
OFISI YA RAIS IKULU NA SEKRETARIETI YA BARAZA LA MAWAZIRI 1 Barabara ya Barack Obama, S.L.P 9120, 11400 Dar es Salaam Simu: 022 2116898/0222116900; Nukushi: 022 2128585 Email: [email protected]; Website http://www.statehouse.go.tz JINA KAMILI CHEO SIMU YA SIMU YA OFISINI MKONONI OFISI YA RAIS Mhe. Dkt.John Pombe Rais wa Jamhuri ya - - Magufuli Muungano wa Tanzania Mwandishi Mwendesha Mary G. Teu 022 211 6920 - Ofisi Rose E. Wabanhu Katibu Mahsusi 022 213 4924 - OFISI YA KATIBU MKUU KIONGOZI Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John William Mkuu wa Utumishi wa 022 211 6679 - Kijazi Umma na Katibu wa Baraza la Mawaziri Magdalena A. Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6679 - Kilongozi Mwandishi Mwendesha Eva Z. Mashallah 022 213 9649 - Ofisi OFISI YA KATIBU MKUU Peter A. Ilomo Katibu Mkuu 022 211 0972 - Salma M. Mlinga Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 0972 - Mwandishi Mwendesha Euphrazia M. Magawa 022 212 9045 - Ofisi OFISI BINAFSI YA RAIS - Katibu wa Rais 022 211 6538 - Yunge P. Massa Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6538 - Joyce E. Pachi Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6538 - Muhidin A. Mboweto Naibu Katibu wa Rais 022 211 6908 - Usamba K. Faraja Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6908 - Katibu Msaidizi Lumbila M. Fyataga 022 211 6917 - Mwandamizi wa Rais Beatrice S. Mbaga Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6917 - Kassim A. Mtawa Katibu wa Rais Msaidizi 022 211 6917 - Alice M. Mkanula Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6917 - Col. Mbarak N. Mpambe wa Rais 022 211 6921 - Mkeremy Leons D. -
MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao Cha Hamsini Na Mbili – Tarehe
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Mbili – Tarehe 18 Juni, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tukae. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI - KATIBU WA BUNGE: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- MHE. HAWA A. GHASIA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI:- Taarifa ya Kamati ya Bajeti kuhusu Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019, pamoja na Tathmini ya utekelezaji wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Mwenyekiti wa Bajeti, Mheshimiwa Hawa Ghasia. Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU Na. 438 Hitaji la Gari la Wagonjwa Kituo cha Afya Mgungulu MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka gari ya kuwahudumia wagonjwa katika kituo cha Afya cha Magunguli –Mgololo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Menrald Lutengano Kigola, Mbunge wa Mufindi Kusini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, gari la wagonjwa kwa ajili ya Kituo cha Afya Magungulu - Mgololo kilichopo kata ya Magungulu imekwishapatikana. Gari hili lilitolewa na Mheshimiwa Rais wakati anatoa msaada wa magari ya wagonjwa kwa halmashauri mbalimbali hapa nchini mnamo mwezi Machi, 2018 na taratibu za usajili zinaendelea.