Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1 BUNGE LA TANZANIA
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Pili – Tarehe 13 Mei, 2015 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu! MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa, maswali tunaanza na ofisi ya Waziri Mkuu, anayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Josephine J. Genzabuke, kwa niaba yake Mheshimiwa Likokola! Na. 11 Fedha za Mfuko wa JK kwa Wajasiriamali Wadogo MHE. DEVOTHA M. LIKOKOLA (K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE) aliuliza:- Mfuko wa Wajasiriamali wadogowadogo maarufu kama mabilioni ya JK uliwavuta wengi sana lakini masharti ya kupata fedha hizo yamekuwa magumu:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kufanya mpango huo uwe endelevu kwa lengo la kuwanufaisha wanyonge? (b) Je, ni wananchi wangapi wa Mkoa wa Kigoma wamenufaika na mpango huo? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007, Serikali ilianzisha mpango wa uwezeshaji wananchi kiuchumi na kuongeza ajira kwa kutoa mikopo yenye masharti nafuu. Lengo la mpango huu ni kuwawezesha wananchi mijini na vijijini kupata mikopo ya kuanzisha au kuendeleza shughuli za kiuchumi ili kuongeza ajira na kipato. Masharti ya kupata mikopo hii si magumu sana ikilingalishwa na ile inayotolewa na mabenki, kwa sababu riba inayotozwa kwa mikopo hii ni asilimia 10, ikilinganishwa na riba inayotozwa na mabenki mengine, ambayo ni zaidi ya asilimia 20. -
Bspeech 2008-09
HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA, MHESHIMIWA STEPHEN MASATO WASIRA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA KWA MWAKA 2008/2009 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu baada ya kuzingatia taarifa iliyowasilishwa hapa Bungeni leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kilimo Mifugo na Maji inayohusu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, sasa lijadili na kukubali kupitisha makadirio ya Matumizi ya Kawaida na ya Maendeleo ya Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika kwa mwaka wa Fedha wa 2008/2009. 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitumie fursa hii kuungana na Watanzania wenzangu kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuchaguliwa kwake kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika. Kuchaguliwa kwake, na mchango wake alioutoa tangu kuchaguliwa kwake kuwa Mwenyekiti wa Umoja huo umelijengea Taifa letu heshima kubwa katika medani ya kimataifa. Aidha, uongozi wake na juhudi zake za kupambana na maovu katika jamii yetu, licha ya kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa ajili ya Uchaguzi wa Mwaka 2005 ni kielelezo dhahiri kuwa ni kiongozi anayejali haki na maendeleo ya nchi yetu. Juhudi zake hizo zimedhihirisha uwezo wake mkubwa wa kuongoza na utumishi wake uliotukuka aliouonyesha katika nyadhifa mbali mbali alizowahi kushika katika Serikali na Chama cha Mapinduzi. Wananchi wanaendelea kuwa na imani na matumaini makubwa kwa uwezo wake katika kuliongoza Taifa letu. 1 3. Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii pia kumpongeza Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda (MB) kwa kuteuliwa kwake kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. -
Briefing on Business & Human Rights in Tanzania 2019
BRIEFING ON BUSINESS & HUMAN RIGHTS IN TANZANIA 2019 QUARTER 2: APRIL - JUNE In May 2019, the Legal and Human Rights Centre (LHRC) published its annual Tanzania Human Rights Report (Ref. E1). This report examines how fundamental human rights - such as the right to life, freedom of expression, the right A1 to work or the right to enjoy and benefit from natural resources - were enjoyed, protected, promoted and violated in 2018. While both government and non-government actors are working to improve human rights in the country, many challenges remain. The right to work, for instance, is challenged by inadequate (minimal) wages, difficulties for certain workers to form or participate in associations such as trade unions (Ref. E1, E2) and the absence of employment contracts (Ref. E3). The right to property, which mainly focusses on access to land, is found to have improved. Nevertheless, it remains a key issue of concern for women (Ref. E1, E4). Violations of women rights appear throughout the report, including persistent sexual violence and economic violence such as labour exploitation. The equal presence and participation of women in the country’s economy is, however, considered crucial for Tanzania’s development (Ref. E5). The report also mentions a deterioration of the freedom of expression in the country, as the result of several laws and amendments (Ref. E1). To that, Tanzania is urged nationally and internationally to keep its legislation conform international standards (Ref. E6). Under international, regional and domestic law, States have the primary duty to promote and protect human rights (Ref. E1), including in the area of business and human rights (Ref. -
MAWASILIANO SERIKALINI Mkuu Wa Kitengo Cha Florence Temba 022 2122942 0784246041 Mawasiliano Serikalini KITENGO CHA UGAVI NA UNUNUZI
OFISI YA RAIS IKULU NA SEKRETARIETI YA BARAZA LA MAWAZIRI 1 Barabara ya Barack Obama, S.L.P 9120, 11400 Dar es Salaam Simu: 022 2116898/0222116900; Nukushi: 022 2128585 Email: [email protected]; Website http://www.statehouse.go.tz JINA KAMILI CHEO SIMU YA SIMU YA OFISINI MKONONI Mhe. Dkt.John Pombe Rais wa Jamhuri ya - - Magufuli Muungano wa Tanzania Mwandishi Mwendesha Mary G. Teu 022 211 6920 - Ofisi Rose E. Wabanhu Katibu Mahsusi 022 213 4924 - Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John William Mkuu wa Utumishi wa 022 211 6679 - Kijazi Umma na Katibu wa Baraza la Mawaziri Magdalena A. Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6679 - Kilongozi Mwandishi Mwendesha Eva Z. Mashallah 022 213 9649 - Ofisi Peter A. Ilomo Katibu Mkuu 022 211 0972 - Salma M. Mlinga Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 0972 - Mwandishi Mwendesha Euphrazia M. Magawa 022 212 9045 - Ofisi OFISI BINAFSI YA RAIS - Katibu wa Rais 022 211 6538 - Yunge P. Massa Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6538 - Joyce E. Pachi Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6538 - Muhidin A. Mboweto Naibu Katibu wa Rais 022 211 6908 - Usamba K. Faraja Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6908 - Katibu Msaidizi Lumbila M. Fyataga 022 211 6917 - Mwandamizi wa Rais Beatrice S. Mbaga Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6917 - Kassim A. Mtawa Katibu wa Rais Msaidizi 022 211 6917 - Alice M. Mkanula Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6917 - Col. Mbarak N. Mpambe wa Rais 022 211 6921 - Mkeremy Leons D. Nkama Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 116 921 - Rajabu O. Luhwavi Msaidizi wa Rais (Siasa) 022 212 8584 - Anande Z. -
Online Document)
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini na Nane – Tarehe 6 Juni, 2014 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali, tunaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu, atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Felix Mkosamali. Na. 197 Huduma za Zahanati – Muhambwe MHE. FELIX FRANCIS MKOSAMALI aliuliza:- Vijiji vya Magarama, Kigina na Nyarulanga katika Jimbo la Muhambwe havina Zahanati:- Je, Serikali imefikia wapi katika kuvipatia vijiji hivyo huduma ya zahanati? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felix Francis Mkosamali, Mbunge wa Jimbo la Muhambwe, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, ni kweli Vijiji vya Kigina, Magarama na Nyarulanga, vilivyopo katika Jimbo la Muhambwe, havina Zahanati. Ujenzi wa Zahanati nchini unafanyika kupitia Mpango wa Fursa na Vikwazo Katika Maendeleo, ambapo Wananchi wenyewe huibua Miradi ambayo inazingatia changamoto zilizopo. Halmashauri huchangia gharama kidogo za utekelezaji wa Miradi hiyo kwa kuwezesha upatikanaji wa vifaa pamoja na usimamizi. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Zahanati katika Kijiji cha Kigina umekamilika kwa Mwaka wa Fedha wa 2012/2013 na ujenzi wa nyumba ya Mganga uko katika hatua ya mwisho, ambapo Serikali kwa Mwaka wa Fedha wa 2013/2014, ilitenga jumla ya shilingi milioni 20. Aidha, ujenzi wa jengo la wagonjwa (OPD) wa nje katika Kijiji cha Magarama upo hatua ya mwisho kukamilika. Serikali imetenga shilingi milioni 23 katika bajeti yake ya mwaka 2014/2015 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa nyumba za watumishi. -
Majadiliano Ya Bunge
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Kumi Na Moja – Tarehe 23 Juni, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- MHE. PINDI H. CHANA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA: Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kifungu cha 99 (3), cha Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2007, naomba kuwasilisha Mezani Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge Katiba, Sheria na Utawala, Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011 pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. MHE. DAVID E. SILINDE (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Msemaji Mkuu wa Upinzani, naomba kuwasasilisha Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Fedha kwa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kuweka Mezani Hotuba ya Bajeti ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Taasisi zote zilizopo chini ya Ofisi yake, kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. 1 Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. MASWALI NA MAJIBU Na. 106 Kero Kiwanda cha Mtibwa MHE. AMOS G. MAKALLA aliuliza:- Uwepo wa kiwanda kimoja tu cha sukari (Mtibwa) unasababisha matatizo mengi kama -
Nacopha English Newsletter 005
NATIONAL COUNCIL OF PEOPLE LIVING WITH HIV IN TANZANIA 3 ZEROS ISSUE NO. 005 JUNE - SEPT 2020 Meaningful involvement of WALK THE TALK people living with HIV NACOPHA Tanzania NACOPHA Tanzania nacophatz NACOPHA www.nacopha.or.tz BARAZA LA TAIFA LA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA 3 ZEROS NYP+ Meeting with Minister of State in Prime NACOPHA Chairperson visit Minister’s Office Hon. Jenista Mhagama Morogoro empowernment groups NACOPHA Chairperson Ms. Leticia Mourice and Cluster Page 2-3 Coordination Team reviewing PLHIV empowerment groups progress during the Chairperson’s visit to Morogoro. Page 4-5 NACOPHA response to COVID-19 pandemic Dar es salaam zonal manager Victoriah Huburya distributing COVID-19 preventive gears at Chamanzi PLHIV cluster, in Mbagala, Dar es Salaam Page 6-7 NACOPHA Board representatives visit empowernment groups Group photo; NACOPHA board treasurer, Mitterand Dagila, Chief Executive Officer Mr. Deogratius Rutatwa, and Prime Minister’s Office meeting with representatives from Newala DC PLHIV empowerment NACOPHA management Page 12-13 groups during board’s visit Page 9 In the next five years, NACOPHA will be implementing a new USAID funded project HEBU known as HEBU TUYAJENGE; Swahili words which literally denotes: an informed conversation between people (friends, family, policy makers or groups) to achieve a particular goal in a positive way. The aim of this project is to contribute to HIV epidemic control by increasing the adoption of higher impact community HIV TUFIKIE 95-95-95 preventive, care, and treatment services among at-risk adolescents, young women, and PLHIV in 65 high burden councils in Tanzania. -
MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao Cha Kumi
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _____________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Kumi na Mbili – Tarehe 26 Juni, 2008 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, mtakumbuka kwamba katika Kanuni yetu ya 38 siku ya Alhamisi ni siku ya maswali kwa Waziri Mkuu. Lakini tuliitengua ile Kanuni kutokana na kwamba Waziri Mkuu ndiye mwenye hotuba tunayoendelea kujadili hivi leo na atajibu kesho. Kwa hiyo, tunaendelea na utenguzi wa ile Kanuni mpaka tutakapokuja siku nyingine. Katibu endelea na Order Paper! MASWALI NA MAJIBU Na. 104 Ukarabati wa Barabara ya Kamena-Msasa-Ibondo-Katoro MHE. KABUZI F. RWILOMBA aliuliza:- Kwa kuwa barabara ya Kamena-Nyabulolo-Gengesaba-Busanda-Msasa-Ibondo- Katoro ni muhimu sana kwa Maendeleo ya jimbo la Busanda kwani pia ni kiungo kikuu cha Wilaya ya Chato, Geita na Wilaya za Shinyanga na kuwa barabara hiyo inapita kwenye maeneo ya uzalishaji wa pamba, mahindi, mihogo, mtama, mpunga, maharage na mazao ya ng’ombe. Je, ni lini Serikali itatenga fedha za kutosha ili kukamilisha ukarabati wa barabara hiyo? NAIBU WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- 1 Mheshimiwa Naibu Spika kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kabuzi Faustine Rwilomba, Mbunge wa Busanda, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika Halmashauri ya Wilaya ya Geita ina mtandao mkubwa wa barabara wenye jumla ya km. 963. Naomba kukubaliana na Mheshimiwa Mbunge kuwa barabara ya Kamena-Nyabulolo-Gengesaba-Busanda-Msasa-Ibondo-Katoro ni muhimu sana kwa Maendeleo ya jimbo la Busanda kwani ni kiungo kikuu cha Wilaya ya Chato, Geita na Wilaya ya Shinyanga na kwamba barabara hii inapita kwenye maeneo ya uzalishaji wa pamba, mahindi, mihogo, mtama, maharage na mazao ya ng’ombe. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Kumi na Nane – Tarehe 6 Julai, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (MAHUSIANO NA UTARATIBU): Mheshimiwa Spika, Kabla sijawasilisha Hati Mezani ninapenda kutumia dakika yako moja kutoa shukrani za dhati kabisa kwako. Kwanza kwa kuwa wa kwanza kutangaza msiba wa Mama yangu na vilevile kuwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge wote ambao wameniletea rambirambi kwa namna moja au nyingine kwa njia ya sms na kwa simu na hii imefanyika kwa wananchi wengi nchini kote. 1 Mheshimiwa Spika, ninawashukuru sana wote sina kitu cha kufanya isipokuwa kuwaambia kuwa asanteni sana, nimepata faraja na Mama yetu tumemwweka mahali pema katika nyumba yake ya milele. Kwa hiyo, baada ya maelezo hayo mafupi na kwa kuwapongeza na kuwashukuru wote naomba sasa kuwakilisha Hati Mezani. Taaarifa ya Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano, 2011/2012 - 2015/2016. NAIBU WAZIRI WA MAJI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha, 2012/2013. MASWALI NA MAJIBU Na.143 Serikali Kujenga Nyumba za Walimu MHE. SULEIMAN M. N. SULEIMAN (K.n.y. MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA) aliuliza:- Shule nyingi za msingi zina upungufu mkubwa wa nyumba za walimu hivyo kusababisha walimu kuishi katika mazingira magumu na kutoripoti katika shule kama Nyamsebhi, Mnekezi, Shibela, Kageye, Ntono na Nyasalala katika Jimbo la Busanda. 2 Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za walimu katika shule hizo na nyingine ili kuboresha mazingira ya walimu kufanya kazi? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lolesia Bukwimba, Mbunge wa Busanda kwa kutoa maelezo yafuatayo. -
1 Bunge La Tanzania
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE ________ MKUTANO WA TATU KIKAO CHA KWANZA - TAREHE 28 MACHI, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta ) Alisoma Dua TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge huu ni Mkutano wetu wa Tatu, Kikao cha Kwanza. Waheshimiwa Wabunge, itakumbukwa kwamba katika Mkutano wetu wa Pili wa Bunge pamoja na shughuli nyingine Bunge lilipitisha Miswada ya Sheria ya Serikali mitatu. Miswaada hiyo napenda kuwafahamisha imekwishapata kibali cha Mheshimiwa Rais tarehe 26 Machi, mwaka huu na sasa Miswaada hii ni sheria kamili za nchi yetu. Wa kwanza ni The National Leaders Funerals Act namba moja wa mwaka 2006, The Special Economic Zone Act ya mwaka 2006 ambao utakuwa namba mbili na The Export Processing Zones Amendments Act ya mwaka 2006 ambao ni sheria namba tatu ya mwaka 2006. HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (MHE. JUMA J. AKUKWETI) :- Taarifa ya matoleo ya Gazeti la Serikali pamoja na nyongeza zake zilizochapishwa tangu Kikao cha mwisho cha Mkutano wa Bunge uliopita. 1 MASWALI NA MAJIBU Na. 1 Elimu ya UKIMWI kwa Walemavu MHE. MARGRET A. MKANGA aliuliza:- Kwa kuwa janga la UKIMWI limeenea nchi nzima katika miji na vijiji na kwa kuwa makundi mbalimbali ya jamii; Serikali, Taasisi na Asasi mbalimbali zinaendelea kutoa elimu ya suala la UKIMWI kwa njia ya semina na makongamano na kwamba ushirikishi kwa watu wenye ulemavu katika elimu hiyo umekuwa haupo au ni mdogo sana:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani madhubuti wa kutoa elimu ya UKIMWI kwa watu wenye ulemavu wa aina mbalimbali? (b) Je, Serikali itakubaliana nami kuwa kwa vile watu wenye ulemavu wa aina mbalimbali huhitaji mbinu tofauti tofauti kutumika ili kuwafikishia ujumbe au elimu ya aina yoyote ile kwamba sasa ni wakati muafaka kuwa na kitengo cha UKIMWI kwa watu wenye ulemavu ndani ya Tume ya Kudhibiti UKIMWI? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, MAAFA NA KAMPENI DHIDI YA UKIMWI (MHE. -
MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao Cha Tano
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Tano - Tarehe 7 Februari, 2005 (Mkutano Ulianzia Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Pius Msekwa) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, Kikao cha Tano cha Mkutano wa Kumi na Nane kinaanza. Lakini kabla hakijaanza nitoe maelezo kuhusu ratiba ya leo. Nilikwishawaeleza Waheshimiwa Wabunge, kwamba leo baada ya kipindi cha Maswali na Majibu, nitamwita mtoa hoja ahitimishe hoja yake. Lakini tangu niliposema maneno hayo kuna Waheshimiwa Wabunge kadhaa wameleta mapendekezo ya marekebisho katika Muswada tulionao. Mheshimiwa Thomas Nyimbo ameleta, Mheshimiwa Wilfred Lwakatare ameleta, Mheshimiwa Isaac Cheyo ameleta, Mheshimiwa Dr. Willbrod Slaa ameleta, Mheshimiwa Benedicto Mutungirehi ameleta, Mheshimiwa Khalifa Suleiman Khalifa ameleta. Waheshimiwa Wabunge, sasa kwa ajili hiyo, nimeona kigezo kimoja cha utawala bora ni kwamba maamuzi yanatokana na mashauriano. Sasa naona ni vizuri tumpe nafasi Mheshimiwa Waziri, afanye mashauriano zaidi na wenzake juu ya marekebisho haya kabla hajaanza kuhitimisha hoja yake ili yale ambayo anafikiri yanafaa kuingia, basi ayataje kwenye hitimisho lake. Waheshimiwa Wabunge, kwa ajili hiyo, nimepanga kwamba Mheshimiwa Waziri wa Sheria na Mambo ya Katiba, hata hitimisha hoja yake asubuhi hii atahitimisha hoja yake saa 11. 00 jioni ili asubuhi aitumie kwa kazi hiyo ya mashauriano. MASWALI NA MAJIBU Na. 49 Vituo vya Kupigia Kura MHE. MARIAM S. MFAKI aliuliza:- 1 Kwa kuwa kazi ya -
Kikao Cha Arobaini Na Tatu – Tarehe 31 Julai, 2009 (Mkut
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA KUMI NA SITA ___________ Kikao cha Arobaini na Tatu – Tarehe 31 Julai, 2009 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Majibu ya Serikali juu ya Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC). NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI (MHE. OMAR YUSSUF MZEE): Majibu ya Serikali juu ya Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC). Majibu ya Serikali juu ya Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC). MASWALI NA MAJIBU Na. 314 Kuviwezesha Vyuo vya Elimu Nchini MHE. PINDI H. CHANA aliuliza:- Kwa kuwa Serikali inapaswa kuviwezesha Vyuo vya Elimu nchini vikiwemo Chuo cha Mzumbe na Muhimbili kwa mujibu wa Kanuni na Sheria:- (a) Je, ni matatizo gani yanayosababisha Serikali kushindwa kuviwezesha Vyuo tajwa hapo juu kwa viwango ambavyo Wizara yenyewe imethibitisha? 1 (b) Je, Serikali ilipaswa ipeleke kiasi gani cha fedha kwa mwaka 2007/2008 na 2008/2009 Chuo cha Muhimbili na Mzumbe ambazo iliahidi na haikupeleka? NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI (MHE. MWANTUMU B. MAHIZA) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Pindi Hazara Chana, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, Serikali huviwezesha Vyuo Vikuu vya Umma vikiwemo Vyuo Vikuu vya Mzumbe na Muhimbili kwa kulipa mishahara ya watumishi, matumizi mengineyo (OC), pesa kwa ajili ya miradi ya maendeleo, pamoja na mikopo ya wanafunzi.