1 Bunge La Tanzania
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
9Aprili,2013
9 APRILI, 2013 BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kwanza - Tarehe 9 Aprili, 2013 WIMBO WA TAIFA (Hapa Waheshimiwa Wabunge Waliimba Wimbo wa Taifa) (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa msimame tena. Mtakumbuka kwamba wakati wa Vikao vyetu vya Kamati, kwa bahati mbaya sana tulimpoteza mpenzi wetu Mheshimiwa Salim Hemed Khamis. Kwa hiyo, tumkumbuke kwa dakika moja. (Hapa Waheshimiwa Wabunge walisimama kwa Dakika moja kumkumbuka Mheshimiwa Salim Hemed Khamis aliyekuwa Mbunge wa Chambani Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Amin. Ahsanteni sana na karibuni tukae. 1 9 APRILI, 2013 Waheshimiwa Wanbunge, katika Mkutano wa Tisa, Bunge lilipitisha Muswada wa Sheria ya Serikali uitwao The Plant Breeders` Rights Bill, 2012, kwa taarifa hii napenda kulialifu Bunge hili Tukufu kwamba, Mswada huo umekwisha pata kibali cha Mheshimiwa Rais na kuwa Sheria ya nchi iitwayo: The Plant Breeders` Rights Act, 2012 Na. 9 ya mwaka 2012. Kwa hiyo, ule sasa ni sheria ya Nchi. HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kuwasilisha mezani Taarifa ya Matoleo yote ya Gazeti la Serikali pamoja na nyongeza zake zilizochapishwa tangu Kikao cha mwisho cha Mkutano wa Bunge uliopita. Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. MASWALI NA MAJIBU Na. 1 Kujenga Barabara ya Old Moshi kwa Lami MHE. GODFREY W. ZAMBI (K.n.y. MHE. DKT. CYRIL A. CHAMI) aliuliza:- Je, Serikali itatekeleza lini ahadi ya kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Old Moshi inayoanzia Kiboriloni kupitia Kikarara, Tsuduni hadi Kidia? 2 9 APRILI, 2013 NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. -
Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA KUMI (DAILY SUMMARY RECORD OF PROCEEDINGS) 17 NOVEMBA, 2014 MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI SABA KIKAO CHA KUMI - 17 NOVEMBA, 2014 I. DUA Saa 3.00 Asubuhi Mhe. Naibu Spika alisoma Dua na kuliongoza Bunge Makatibu Mezani :- 1. Ndg. Charles Mloka 2. Ndg. Neema Msangi 3. Ndg. Joshua Chamwela II. MASWALI: Maswali yafuatayo yaliulizwa na wabunge:- 1. OFISI YA WAZIRI MKUU Swali Na. 114. Mhe. Prof. Peter Mahamudu Msolla Nyongeza ;- i. Mhe. Peter Mahamudu Msolla ii. Mhe. Ally Keissy Mohammad 2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MAZINGIRA) Swali Na. 115 – All Khamis Seif, Mb Nyongeza ;- i. Mhe. Ally Khamis Seif, Mb ii. Mhe. James Francis Mbatia, Mb 3. WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI Swali Na. 116. Mhe. Dkt. Mary Machuche Mwanjelwa, Mb Nyongeza:- i. Mhe. Dkt. Mary Machuche Mwanjelwa, Mb ii. Mhe. Selemani Said Jafo, Mb iii.Mhe. Aliko Nikusuma Kibona, Mb 4. WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII Swali Na. 117 – Mhe Joseph Roman Selasini, Mb Nyongeza:- i. Mhe Joseph Roman Selasini, Mb 2 ii. Mhe. Moses Machali 5. WIZARA YA MAJI Swali Na. 118. – Mhe. Michael Lekule Laizer [KNY: Dkt. Augustine Lyatonga Mrema]. Nyongeza;- i. Mhe. Michael Lekule Laizer ii. Mhe. James Francis Mbatia, Mb 6. WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO Swali Na. 119 – Mhe. Christowaja Gerson Mtinda Nyongeza:- i. Mhe. Christowaja Gerson Mtinda ii. Mhe. Martha Moses Mlata, Mb iii. Mhe. Grace Sindato Kiwelu, Mb 7. WIZARA YA KILIMO CHAKULA USHIRIKA Swali Na. -
10 JUNI, 2013 MREMA 1.Pmd
10 JUNI, 2013 BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Sita - Tarehe 10 Juni, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 367 Mafunzo ya Wajasiriamali Wanawake – Mbeya MHE. GODFREY W. ZAMBI (K.n.y. MHE. CYNTHIA H. NGOYE) aliuliza:- Wanawake wa Mkoa wa Mbeya wameitikia wito wa kuanzishwa kwa vikundi vya uzalishaji mali ikiwemo uanzishwaji wa vyombo vya akiba na mikopo:- (a) Je, ni lini Serikali itawapatia mafunzo ya ujasiriamali Wanawake wa Mkoa Mbeya? (b) Je, Serikali iko tayari kuhamasisha benki mbalimbali kusogeza huduma karibu na wananchi ili kukidhi azma yao ya kupatiwa mikopo na kujiwekea akiba? 1 10 JUNI, 2013 WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Cynthia Hilda Ngoye, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) ilifanya utafiti katika mkoa wa Mbeya na kubaini kuwa wananchi wengi wakiwemo wanawake wameanzisha vikundi vya uzalishaji mali ikiwemo uanzishwaji wa vikundi na mikopo. Kutokana na juhudi hizo, Baraza kwa kutumia Mfuko wa Uwezeshaji Mwananchi Kiuchumi yaani “Mwananchi Empowerment Fund” imeanza kutoa udhamini wa mikopo kwa wananchi wa Mbeya hususan Chimala SACCOS. Aidha, utaratibu na mpango wa kutoa mafunzo umeandaliwa na mafunzo yatatolewa mwanzoni mwa mwaka wa fedha 2013/2014. Mafunzo hayo yatawahusisha pia wanaume kwa vile SACCOS ya Chimala ina wanachama ambao ni wanaume. -
MKUTANO WA PILI Kikao Cha Tisa
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA PILI Kikao cha Tisa - Tarehe 17 Februari, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Taarifa ya mwaka ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali za Mitaa kwa mwaka wa fedha unaoishia tarehe 30 Juni, 2004. Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. MASWALI NA MAJIBU Na. 94 Uwekaji wa Lami Barabara ya Kigogo - Mabibo - Mandela - Tabata MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka lami kwenye barabara ya Kigogo- Mabibo hadi barabara ya Mandela kuelekea Tabata ili kupunguza msongamano wa magari katika barabara ya Morogoro? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima Mdee, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- 1 Mheshimiwa Spika, barabara ya Kigogo - Mabibo- Mandela kuelekea Tabata ni barabara ya mjini yaani urban road na inahudumiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Barabara hii ni muungano wa barabara tatu ambazo ni Kigogo - Mabibo, Mabibo - Mandela na Mandela - Tabata. Barabara hii imekuwa ikifanyiwa matengenezo ya mara kwa mara na Manispaa ya Kinondoni. Kwa mwaka 2005/2006 jumla ya shilingi 9,836,000 zilitumika kuweka kifusi kwenye sehemu korofi na kuichonga kwa greda. Mheshimiwa Spika, barabara hii inapitika isipokuwa katika mpaka wa Manispaa za Kinondoni na Ilala eneo la Tabata ambapo pana mkondo wa maji na hakuna daraja. -
Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Pili – Tarehe 13 Mei, 2015 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu! MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa, maswali tunaanza na ofisi ya Waziri Mkuu, anayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Josephine J. Genzabuke, kwa niaba yake Mheshimiwa Likokola! Na. 11 Fedha za Mfuko wa JK kwa Wajasiriamali Wadogo MHE. DEVOTHA M. LIKOKOLA (K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE) aliuliza:- Mfuko wa Wajasiriamali wadogowadogo maarufu kama mabilioni ya JK uliwavuta wengi sana lakini masharti ya kupata fedha hizo yamekuwa magumu:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kufanya mpango huo uwe endelevu kwa lengo la kuwanufaisha wanyonge? (b) Je, ni wananchi wangapi wa Mkoa wa Kigoma wamenufaika na mpango huo? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007, Serikali ilianzisha mpango wa uwezeshaji wananchi kiuchumi na kuongeza ajira kwa kutoa mikopo yenye masharti nafuu. Lengo la mpango huu ni kuwawezesha wananchi mijini na vijijini kupata mikopo ya kuanzisha au kuendeleza shughuli za kiuchumi ili kuongeza ajira na kipato. Masharti ya kupata mikopo hii si magumu sana ikilingalishwa na ile inayotolewa na mabenki, kwa sababu riba inayotozwa kwa mikopo hii ni asilimia 10, ikilinganishwa na riba inayotozwa na mabenki mengine, ambayo ni zaidi ya asilimia 20. -
Bspeech 2008-09
HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA, MHESHIMIWA STEPHEN MASATO WASIRA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA KWA MWAKA 2008/2009 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu baada ya kuzingatia taarifa iliyowasilishwa hapa Bungeni leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kilimo Mifugo na Maji inayohusu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, sasa lijadili na kukubali kupitisha makadirio ya Matumizi ya Kawaida na ya Maendeleo ya Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika kwa mwaka wa Fedha wa 2008/2009. 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitumie fursa hii kuungana na Watanzania wenzangu kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuchaguliwa kwake kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika. Kuchaguliwa kwake, na mchango wake alioutoa tangu kuchaguliwa kwake kuwa Mwenyekiti wa Umoja huo umelijengea Taifa letu heshima kubwa katika medani ya kimataifa. Aidha, uongozi wake na juhudi zake za kupambana na maovu katika jamii yetu, licha ya kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa ajili ya Uchaguzi wa Mwaka 2005 ni kielelezo dhahiri kuwa ni kiongozi anayejali haki na maendeleo ya nchi yetu. Juhudi zake hizo zimedhihirisha uwezo wake mkubwa wa kuongoza na utumishi wake uliotukuka aliouonyesha katika nyadhifa mbali mbali alizowahi kushika katika Serikali na Chama cha Mapinduzi. Wananchi wanaendelea kuwa na imani na matumaini makubwa kwa uwezo wake katika kuliongoza Taifa letu. 1 3. Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii pia kumpongeza Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda (MB) kwa kuteuliwa kwake kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka. -
Briefing on Business & Human Rights in Tanzania 2019
BRIEFING ON BUSINESS & HUMAN RIGHTS IN TANZANIA 2019 QUARTER 2: APRIL - JUNE In May 2019, the Legal and Human Rights Centre (LHRC) published its annual Tanzania Human Rights Report (Ref. E1). This report examines how fundamental human rights - such as the right to life, freedom of expression, the right A1 to work or the right to enjoy and benefit from natural resources - were enjoyed, protected, promoted and violated in 2018. While both government and non-government actors are working to improve human rights in the country, many challenges remain. The right to work, for instance, is challenged by inadequate (minimal) wages, difficulties for certain workers to form or participate in associations such as trade unions (Ref. E1, E2) and the absence of employment contracts (Ref. E3). The right to property, which mainly focusses on access to land, is found to have improved. Nevertheless, it remains a key issue of concern for women (Ref. E1, E4). Violations of women rights appear throughout the report, including persistent sexual violence and economic violence such as labour exploitation. The equal presence and participation of women in the country’s economy is, however, considered crucial for Tanzania’s development (Ref. E5). The report also mentions a deterioration of the freedom of expression in the country, as the result of several laws and amendments (Ref. E1). To that, Tanzania is urged nationally and internationally to keep its legislation conform international standards (Ref. E6). Under international, regional and domestic law, States have the primary duty to promote and protect human rights (Ref. E1), including in the area of business and human rights (Ref. -
MAWASILIANO SERIKALINI Mkuu Wa Kitengo Cha Florence Temba 022 2122942 0784246041 Mawasiliano Serikalini KITENGO CHA UGAVI NA UNUNUZI
OFISI YA RAIS IKULU NA SEKRETARIETI YA BARAZA LA MAWAZIRI 1 Barabara ya Barack Obama, S.L.P 9120, 11400 Dar es Salaam Simu: 022 2116898/0222116900; Nukushi: 022 2128585 Email: [email protected]; Website http://www.statehouse.go.tz JINA KAMILI CHEO SIMU YA SIMU YA OFISINI MKONONI Mhe. Dkt.John Pombe Rais wa Jamhuri ya - - Magufuli Muungano wa Tanzania Mwandishi Mwendesha Mary G. Teu 022 211 6920 - Ofisi Rose E. Wabanhu Katibu Mahsusi 022 213 4924 - Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John William Mkuu wa Utumishi wa 022 211 6679 - Kijazi Umma na Katibu wa Baraza la Mawaziri Magdalena A. Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6679 - Kilongozi Mwandishi Mwendesha Eva Z. Mashallah 022 213 9649 - Ofisi Peter A. Ilomo Katibu Mkuu 022 211 0972 - Salma M. Mlinga Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 0972 - Mwandishi Mwendesha Euphrazia M. Magawa 022 212 9045 - Ofisi OFISI BINAFSI YA RAIS - Katibu wa Rais 022 211 6538 - Yunge P. Massa Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6538 - Joyce E. Pachi Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6538 - Muhidin A. Mboweto Naibu Katibu wa Rais 022 211 6908 - Usamba K. Faraja Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6908 - Katibu Msaidizi Lumbila M. Fyataga 022 211 6917 - Mwandamizi wa Rais Beatrice S. Mbaga Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6917 - Kassim A. Mtawa Katibu wa Rais Msaidizi 022 211 6917 - Alice M. Mkanula Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6917 - Col. Mbarak N. Mpambe wa Rais 022 211 6921 - Mkeremy Leons D. Nkama Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 116 921 - Rajabu O. Luhwavi Msaidizi wa Rais (Siasa) 022 212 8584 - Anande Z. -
Did They Perform? Assessing fi Ve Years of Bunge 2005-2010
Policy Brief: TZ.11/2010E Did they perform? Assessing fi ve years of Bunge 2005-2010 1. Introducti on On July 16th 2010, following the completi on of the 20th session of the Bunge, the President of Tanzania dissolved the 9th Parliament. This event marked the end of the term for Members of Parliament who were elected during the 2005 general electi ons. Now that the last session has been completed it allows us to look back and to consider how MPs performed during their tenure. Did they parti cipate acti vely and represent their consti tuencies by asking questi ons and making interventi ons, or were they silent backbenchers? The Bunge is the Supreme Legislature of Tanzania. The Bunge grants money for running the administrati on and oversees government programs and plans. The Bunge oversees the acti ons of the Executi ve and serves as watchdog to ensure that government is accountable to its citi zens. To achieve all this, Members of Parliament pass laws, authorize taxati on and scruti nize government policies including proposal for expenditure; and debate major issues of the day. For the Bunge to eff ecti vely carry out its oversight role, acti ve parti cipati on by Members of Parliament is criti cal. MPs can be acti ve by making three kinds of interventi ons: they can ask basic questi ons, they can ask supplementary questi ons and they can make contributi ons during debates. This brief follows earlier briefs, the last of which was released in August 2010. It presents seven facts on the performance of MPs, including rati ng who were the most acti ve and least acti ve MPs. -
Online Document)
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini na Nane – Tarehe 6 Juni, 2014 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali, tunaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu, atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Felix Mkosamali. Na. 197 Huduma za Zahanati – Muhambwe MHE. FELIX FRANCIS MKOSAMALI aliuliza:- Vijiji vya Magarama, Kigina na Nyarulanga katika Jimbo la Muhambwe havina Zahanati:- Je, Serikali imefikia wapi katika kuvipatia vijiji hivyo huduma ya zahanati? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felix Francis Mkosamali, Mbunge wa Jimbo la Muhambwe, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, ni kweli Vijiji vya Kigina, Magarama na Nyarulanga, vilivyopo katika Jimbo la Muhambwe, havina Zahanati. Ujenzi wa Zahanati nchini unafanyika kupitia Mpango wa Fursa na Vikwazo Katika Maendeleo, ambapo Wananchi wenyewe huibua Miradi ambayo inazingatia changamoto zilizopo. Halmashauri huchangia gharama kidogo za utekelezaji wa Miradi hiyo kwa kuwezesha upatikanaji wa vifaa pamoja na usimamizi. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Zahanati katika Kijiji cha Kigina umekamilika kwa Mwaka wa Fedha wa 2012/2013 na ujenzi wa nyumba ya Mganga uko katika hatua ya mwisho, ambapo Serikali kwa Mwaka wa Fedha wa 2013/2014, ilitenga jumla ya shilingi milioni 20. Aidha, ujenzi wa jengo la wagonjwa (OPD) wa nje katika Kijiji cha Magarama upo hatua ya mwisho kukamilika. Serikali imetenga shilingi milioni 23 katika bajeti yake ya mwaka 2014/2015 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa nyumba za watumishi. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MKUTANO WA TANO ___________________ Kikao cha Saba – Tarehe 16 Novemba, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Jenista J. Mhagama) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 84 Hali Mbaya ya Hospitali ya Wilaya – Mbozi MHE. GODFREY W. ZAMBI aliuliza:- Majengo ya Hospitali ya Wilaya Mbozi – Vwawa yako kwenye hali mbaya na wodi za kulaza wagonjwa hazitoshelezi hali inayosababisha msongamano katika wodi chache zilizopo:- Je, Serikali itayakarabati lini majengo ya zamani na kujenga mengine kwa ajili ya kulaza wagonjwa? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Godfrey W. Zambi, Mbunge wa Mbozi Mashariki, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Wilaya ya Mbozi ya Vwawa ilipandishwa hadhi kutoka kituo cha afya mwaka 2002 kwa kuongezewa majengo yafuatayo Wodi ya Mama wajawazito1, wodi 1 ya wanaume, pediatric ward 1, Chumba cha kusubiria mama wajawazito kimoja, chumba cha upasuaji, jengo la mapokezi, isolation ward, jengo la kliniki (RCH), jengo la utawala, chumba cha kuhifadhia maiti, jengo la kufulia nguo, jengo la upasuaji mkubwa na chumba cha X–ray. Aidha, ni kweli kuwa baadhi ya majengo ya hospitali hiyo yameharibika kiasi cha kuhitaji kukarabatiwa. Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka 2011/2012 Halmashauri imepanga kutumia shilingi 40,000,000 kwa ajili ya kukarabati jengo la upasuaji, shilingi 28,292,648 kwa ajili ya ukarabati wa jengo la utawala na shilingi 18,968,672 kwa ajili ya ukarabati wa jengo la wodi ya wazazi (Maternity Ward).