MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NNE Kikao Cha

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NNE Kikao Cha Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Tisa – Tarehe 26 Juni, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (MHE JUMA J. AKUKWETI) Hotuba ya Bajeti ya Waziri Mkuu, kwa Mwaka wa Fedha 2006/2007. MHE. GEORGE M. LUBELEJE - MWENYEKITI WA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA:- Taarifa ya Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala Kuhusu Utekelezaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa mwaka wa Fedha uliopita pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Ofisi hiyo kwa mwaka 2006/2007. MHE. DR. WILLBOD P. SLAA (K.n.y. HAMAD R. MOHAMED) - MSEMAJI WA UPINZANI KWA OFISI YA WAZIRI MKUU:- Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Kuhusu Hotuba ya Bajeti ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2006/2007. 1 SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunao wageni kadhaa. Naona Waheshimiwa Wabunge wamekuwa na Utamaduni mpya sasa wa kuleta majina mengi tu ya wageni wetu. Naomba sana ili tusiingiliane sana na kipindi cha maswali, basi niwatangaze mara baada ya kipindi cha maswali. Waheshimiwa Wabunge, ila ninalo tangazo na ni kawaida yangu kwamba yakitokea matukio mazuri tu kwa wenzetu Waheshimiwa Wabunge ni vizuri niweze kuwafahamisha. Nimearifiwa na Chama cha Mapinduzi kwamba jana Halmashauri Kuu ya Chama hicho ilifanya uteuzi wa uongozi mpya ndani ya Sekretarieti ya Chama na kwa kuwa wanne kati ya hao walioteuliwa au waliochaguliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM ni Waheshimiwa Wabunge wa Bunge hili nilikuwa naomba niweze kuwatambua kwa sababu ni wenzetu humu. Ninaviomba Vyama vingine inapotokea hivyo basi watuarifu hatutasita kuwatangaza. (Makofi) Wa kwanza ni Mheshimiwa Yusuf Rajab Makamba, Mbunge wa Kuteuliwa, ambaye amechaguliwa na NEC kuwa Katibu Mkuu wa CCM. Mwingine ni Mbunge wa Siha Mheshimiwa Aggrey Mwanri, huyu sasa Waheshimiwa Wabunge, ndiyo Katibu Mwenezi wa Taifa wa Chama cha Mapinduzi. Waheshimiwa Wabunge, mwingine ni Mbunge wa Igunga, Mheshimiwa Rostam Aziz huyu sasa ndiyo Mweka Hazina wa Chama cha Mapinduzi. Halafu upande wa Idara wenyewe wanaita Organization ameteuliwa Mheshimiwa Kidawa Hamid Salehe. Mheshimiwa Dr. Asha-Rose Migiro ameteuliwa kuwa ni Katibu wa Masuala ya Mambo ya Nje katika Chama cha Mapinduzi. Ahsanteni sana. (Makofi) Waheshimiwa Wabunge, kama nilivyotoa wito kwa wenzetu wa Vyama vyote vingine nadhani ni vizuri tuipongeze CCM kwa kutambua Hazina kubwa ya uwezo uliomo ndani ya Bunge letu hili. Tunaomba Vyama vyote vingine vinapotaka kupata watu madhubuti wa kuendesha mambo yao waangalie ndani ya Bunge hili. Ahsanteni sana. (Makofi) MASWALI NA MAJIBU Na. 78 Utekelezaji wa Sheria ya The Parliamentary Services Commission 1997 MHE. MOHAMED R. ABDALLAH aliuliza:- Kwa kuwa Bunge lilipitisha Sheria ya “The Parliamentary Services Commission Act” ya 11, 12 (1) na (3) inatoa madaraka kwa Bunge kuwa na Bajeti yake na kuisimamia na kwa kuwa mahitaji ya vifungu hivyo hayatekelezwi hivi sasa kama inavyotakiwa na hivyo sheria kutekelezwa bila ujumla wake:- (a) Je, ni nini sababu inayosababisha sheria hiyo isitekelezwe kwa ujumla wake? 2 (b) Je kwa nini Bunge lisiwe na Vote zake na kuzisimamia lenyewe kama ilivyo kwa Wizara za Serikali? NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU(MHE. DR. LUKA J. SIYAME) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kabla ya kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Rished Abdallah, Mbunge wa Jimbo la Pangani, kutoa maelezo yafuatayo:- Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba mwaka 1997, Bunge lako Tukufu lilipitisha Sheria ya Tume ya Huduma za Bunge, yaani “The Parliamentary Services Commission Act, 1997 (Act No. 14 of 1997)” ambayo pamoja na mambo mengine, imeweka utaratibu wa kushughulikia fungu la fedha kwa ajili ya kikidhi mahitaji mbalimbali ya Bunge. Katika Sheria hiyo, kifungu cha 11 kinatamka bayana kuwa, fedha zinazohitajika kwa shughuli za Bunge zitalipwa na Hazina ikiwa makisio yake yamepitishwa na Bunge na kuwa fedha hizo zitatoka katika Mfuko Mkuu wa Serikali (i.e. Consolidated Fund). Aidha, kifungu cha 12(1), (2) na (3) kimetamka hatua mbalimbali za kuzingatiwa wakati wa kutayarisha Bajeti ya Bunge hadi kuidhinishwa na Bunge hili Tukufu. Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo, mafupi, naomba sasa kwa niaba ya Mhesimiwa Waziri Mkuu, kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Rished Abdallah, Mbunge wa Pangani, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Kwa mujibu wa Sheria Na. 14 ya mwaka 1997, utaratibu unaotumika kuandaa Bajeti ya Ofisi ya Bunge unazingatia maelekezo ya Sheria hiyo kama nilivyobainisha katika maelezo ya ufafanuzi na Mheshimiwa Waziri Mkuu ndiye mwenye dhamana ya kuwasilisha makisio ya Bajeti hiyo kwenye Baraza la Mawaziri na hatimaye hapa Bungeni ili kuidhinishwa. Utaratibu huu ndio unaotumika kwa baadhi nchi za Jumuiya ya Madola ambazo zinatumia Mfumo uitwao Westminster. Miongoni mwa nchi hizo ni pamoja na Australia, India, Jamaica na Malaysia. (b) Bunge lina fungu lake kama ilivyo Wizara na Taasisi nyingine na linapewa fedha zinazohitajika kutoka katika Mfuko Mkuu wa Serikali yaani Consolidated Fund kupitia Fungu (Vote ) 42. Pia Mahakama ni Mhimili wa Dola kama ilivyo Bunge na yenyewe kwa mfumo unaotumika hivi sasa inapewa fedha kutoka Mfuko Mkuu wa Serikali kupitia Fungu 40. Mheshimiwa Spika, mfumo huu unalenga zaidi katika mgawanyo wa madaraka na majukumu kwa mihimili ya Dola iliyopo kama ilivyofafanuliwa ndani ya Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977. MHE. MOHAMED RISHED ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili madogo ya nyongeza. 3 Mheshimiwa Spika, kwa kuwa sheria hii inatokana na Katiba ambayo ipo kwenye Cap.2. Mheshimiwa Spika, naomba ninukuu kidogo anasema: “This Act shall be read as one with the Constitution of the United Republic of Tanzania.” Kwa maelezo ya Mheshimiwa Naibu Waziri na procedure zote kwa ajili ya gharama za kuendeshea Bunge kama alivyoeleza. Mimi naamini kwamba utaratibu ule hauko wazi kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri kama vile tunavyopitisha bajeti za Wizara. Tunapitisha tu kifungu cha Bunge ili kupitisha gharama za Bunge. Hilo moja. La pili, sheria pia inatambua kuwepo kwa Waziri ambapo inasema: “ the Minister responsible for Parliamentary Affairs.” Mheshimiwa Spika, naomba niulize Waziri analisaidiaje Bunge katika kupanga na kuratibu shughuli za mafungu ya fedha kwa kuendeshea Bunge wakati sisi hatuoni kama kuna dalili hizo za Waziri kulisaidia Bunge katika shughuli zake za kila siku? Ahsante sana. (Makofi) WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (MHE. JUMA J. AKUKWETI): Mheshimiwa Spika, kama tulivyojibu kwenye swali la msingi au jibu letu la msingi kuna mihimili mitatu ambayo yote inafanya kazi katika nchi hii moja. Kila mhimili unajitegemea katika masuala yake. Sasa inapofika wakati wa fedha kila mhimili unapanga Bajeti yake na baada ya kupanga Bajeti yake inapelekwa kule ambako inaweza kutafutiwa fedha na kwa hivi sasa ni Hazina na Hazina ndiyo baada ya kujua fedha ziko kiasi gani katika Taifa letu inagawa sasa zipi ziende wapi kutokana kwanza na mahitaji. Lakini pia mapato ya Taifa letu na kazi ya Waziri ni kuhakikisha hiyo process yenyewe. Mheshimiwa Spika, lakini Mheshimiwa Mbunge nadhani anafahamu katika sheria yetu kifungu 13 kinasema ifuatavyo na naomba nikisome moja kwa moja. Kifungu cha 13 katika sheria ya Bunge ambacho kina guide mambo ya Bunge kinasema hivi: “ The Commission shall from time to time prepare and recommend to the President the rates of salaries, allowances and other recommendations to be paid to Members of Parliament.” Nadhani utaratibu huu ni mzuri kwamba Bunge lenyewe baada ya mahitaji yake linapeleka moja kwa moja kwa Mheshimiwa Rais na Mheshimiwa Rais anatumia utaratibu wake ili kuhakikisha anakubali au anakataa yale maombi ya Bunge. Mimi nadhani huu ni utaratibu mzuri ili nguzo hizi tatu zisiweze kugongana, lakini wote tutatafuta fedha kwenye Mfuko mmoja kwa ajili ya Taifa letu. (Makofi) MHE KABWE Z. ZITTO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza na wakati huo huo nitumie fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Aggrey Mwanri kwa kuwa Katibu Mwenezi wa Chama, kweli kimepata mwenezi. (Makofi) Mheshimiwa Spika, swali langu ni dogo tu. Kwa kuwa matamkwa ya swali la msingi ni matamkwa ya Kisheria na matamkwa haya yameonekana kwamba hayafanyiki. Je, Serikali haioni kwamba imefika wakati muafaka Bunge liwe huru zaidi na kujipangia vote yake na Bajeti yake na kuisimamia yenyewe ili kuepuka kuwekwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na chini ya Wizara ya Fedha? 4 WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (MHE. JUMA J. AKUKWETI): Mheshimiwa Spika, nionavyo mimi utaratibu huu unafuata kabisa jinsi sheria inavyotaka. Mimi naomba niseme hivi Mheshimiwa Kabwe Zitto, kama nia ni kwamba kila nguzo ijipangie yenyewe basi kuna hatari ya nguzo hii ambayo ina mamlaka makubwa katika nchi yetu ikajipangia marupurupu makubwa kuliko hata kutoangalia nguzo zingine. Utaratibu unaotumika sasa ndiyo unaojenga haki ya mgawanyo sawasawa katika Taifa letu. Kuhakikisha Mahakama inapata kiasi chake ili isikwame na kuhakikisha kwamba Bunge linapata kiasi chake ili lisikwame na Executive inapata kiasi chake ili isikwame. Mheshimiwa Spika, nataka kumhakikishia Mheshimiwa Kabwe Zitto, kwamba kwa utaratibu huu mpaka sasa Bunge halijawahi kukwama kufanya kazi kwa sababu Executive haikutoa fedha. Na yeye tayari naweza kum-challenge aseme ni lini Bunge limeshindwa kufanya kazi kwa kukosa
Recommended publications
  • Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1 BUNGE LA TANZANIA
    Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ________________________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Kumi na Tisa – Tarehe 27 Mei, 2014 (Mkutano Ulianza Saa tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA: Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha kwa Mwaka 2012/2013 (The Annual Report and Accounts of Arusha International Conference Centre for the Year 2012/2013). Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. BETTY E. MACHANGU (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na Maoni ya Kamati 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. ABDULKARIM E.H. SHAH (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA ARDHI, MALIASILI NA MAZINGIRA): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    NAKALA YA MTANDAO (ON LINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ BUNGE LA KUMI NA MOJA ___________ MKUTANO WA KWANZA Kikao cha Kwanza - Tarehe 17 Novemba, 2015 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) DKT. THOMAS D. KASHILILAH - KATIBU WA BUNGE: Naomba tukae. TANGAZO LA RAIS LA KUITISHA MKUTANO WA BUNGE DKT. THOMAS D. KASHILILAH - KATIBU WA BUNGE: Waheshimiwa Wabunge, kwa mujibu wa masharti ya Katiba, Mkutano huu wa Kwanza unaanza kwa Rais kuuitisha. Naomba kuchukua nafasi hii kusoma Tangazo la Rais kama ambavyo tumelipokea. Tangazo la Serikali Na. 513 la tarehe 6 Novemba, 2015. Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Sura ya Pili, hati iliyotolewa kwa mujibu wa Ibara ya 90(1). Hati ya Kuitisha Mkutano wa Bunge Jipya. KWA KUWA, Uchaguzi Mkuu ulifanyika tarehe 25 Oktoba, 2015 katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977; NA KWA KUWA, masharti ya Ibara ndogo ya kwanza ya Ibara ya 90 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, yanamtaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuitisha Mkutano wa Bunge Jipya kabla ya kupita siku saba tangu Tume ya Uchaguzi kutangaza matokeo ya Uchaguzi Mkuu; NA KWA KUWA, matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 25 Oktoba, 2015 yalitangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi tarehe 29 Oktoba, 2015; HIVYO BASI, mimi John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa mamlaka niliyonayo chini ya Ibara ya 90(1) ya 1 NAKALA YA MTANDAO (ON LINE DOCUMENT) Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, naitisha Mkutano wa Bunge Jipya la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ufanyike katika ukumbi wa Bunge uliopo Mjini Dodoma tarehe 17 Novemba, 2015 kuanzia saa tatu asubuhi.
    [Show full text]
  • Bunge Newsletter
    BungeNe ewsletter Issue No 008 June 2013 New Budget Cycle Shows Relavance For the first time in recent Tanzania history the engage the government and influence it make sev- Parliament has managed to pass the next financial eral tangible changes in its initial budget proposals. year budget before the onset of that particular year. This has been made possible by the Budget Commit- This has been made possi- tee, another new innovation by Speaker Makinda. ble by adoption of new budget cycle. Under the old cycle, it was not possible to influence According to the new budget cycle, the Parliament the government to make changes in budgetary allo- starts discussing the budget in April as opposed to cations. That was because the main budget was read, old cycle where debate on the new budget started on debated and passed before the sectoral plans. After June and ends in the first or second week of August. the main budget was passed, it was impossible for the MPs and government to make changes in the When the decision was taken to implement the new sectoral budgets since they were supposed to reflect budget cycle and Speaker Anne Makinda announced the main budget which had already been passed. the new modalities many people, including Mem- bers of Parliament, were skeptical. Many stakehold- These and many other changes have been made possi- ers were not so sure that the new cycle would work. ble through the five components implemented under the Parliament five years development plan. “Govern- But Ms Makinda has managed to prove the doubt- ment and Budget Oversight and Accountability is one ers wrong.
    [Show full text]
  • Rumours and Riots: Local Responses to Mass Drug Administration for the Treatment of Neglected Tropical Diseases Among School-Ag
    Rumours and riots: Local responses to mass drug administration for the treatment of neglected tropical diseases among school-aged children in Morogoro Region, Tanzania A thesis submitted for the degree of Doctor of Philosophy by Julie Dawn Hastings Department of Anthropology School of Social Sciences Brunel University January 2013 Abstract In August 2008, a biomedical intervention providing free drugs to school aged children to treat two endemic diseases – schistosomiasis haematobium and soil- transmitted helminths - in Morogoro region, Tanzania, was suspended after violent riots erupted. Parents and guardians rushed to schools to prevent their children taking the drugs when they heard reports of children dying in Morogoro town after receiving treatment. When pupils heard these reports, many of those who had swallowed the pills began to complain of dizziness and fainted. In Morogoro town hundreds of pupils were rushed to the Regional Hospital by their parents and other onlookers. News of these apparent fatalities spread throughout the region, including to Doma village where I was conducting fieldwork. Here, protesting villagers accused me of bringing the medicine into the village with which to “poison” the children and it was necessary for me to leave the village immediately under the protection of the Tanzanian police. This thesis, based on eleven months fieldwork between 2007 and 2010 in Doma village and parts of Morogoro town, asks why was this biomedical intervention so vehemently rejected? By analysing local understandings and responses to the mass distribution of drugs in relation to the specific historical, social, political, and economic context in which it occurred, it shows that there was a considerable disjuncture between biomedical understandings of these diseases, including the epidemiological rationale for the provision of preventive chemotherapy, and local perspectives.
    [Show full text]
  • Hotuba Ya Bajeti Ya Wizara Ya Mambo Ya Nje 2012/2013 Posted: Monday August 06, 2012 1:06 PM BT
    Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje 2012/2013 Posted: Monday August 06, 2012 1:06 PM BT HOTUBA YA WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA MHESHIMIWA BERNARD KAMILLIUS MEMBE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO W A KIMATAIFA KWA MWAKA WA FEDHA 2012/2013 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), naomba sasa kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu lipokee, lijadili na kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa mwaka wa fedha 2012/2013. 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kutumia fursa hii kukupongeza wewe binafsi kwa kuliongoza kwa umahiri mkubwa Bunge hili la Bajeti la mwaka 2012/2013. Napenda pia kuwapongeza Mheshimiwa Job Ndugai (Mb.), Naibu Spika na Waheshimiwa Wenyeviti wanaokusaidia kuongoza Bunge hili kwa kazi nzuri wanayoifanya. 3. Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee nachukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa uongozi wake mahiri wa Serikali ya Awamu ya Nne. Chini ya uongozi wake Taifa letu limeendeleza utamaduni wetu wa kudumisha amani, utulivu na mshikamano. Nawaomba Watanzania wote tuendelee kudumisha hali hiyo ili kuimarisha umoja wetu ambao ni tunu isiyopatikana kwa bei yoyote. 4. Mheshimiwa Spika, niruhusu niungane na Waheshimiwa Wabunge wengine wote walionitangulia kuwapongeza kwa dhati kabisa Waheshimiwa Wabunge wapya, Mawaziri na Naibu Mawaziri walioteuliwa na Mheshimiwa Rais mwezi Mei 2012. Nawapongeza Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge waliochaguliwa kipindi hiki kutokana na mabadiliko yaliyotokea kwenye nafasi mbalimbali humu Bungeni na ndani ya Serikali.
    [Show full text]
  • MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Thelathini Na Sita
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Sita – Tarehe 27 Mei, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nawaomba tukae. Waheshimiwa Wabunge tunaendelea na Mkutano wetu wa 15, leo ni Kikao cha 36. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NAIBU WAZIRI WA MADINI: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2019/2020. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. CATHERINE V. MAGIGE - K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI) Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu utekelezaji na Majukumu ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. MHE. TUNZA I. MALAPO - K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU WIZARA YA MADINI: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni juu ya Wizara ya Madini kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Tunza Malapo, tunakushukuru. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Tunaanza na TAMISEMI, swali la kwanza litaulizwa na Mheshimiwa Azza Hilal, Mbunge wa Viti Maalum - Shinyanga.
    [Show full text]
  • Joint Declaration by Non Governmental Organisations on the Ongoing Human Rights Violations in Loliondo
    JOINT DECLARATION BY NON GOVERNMENTAL ORGANISATIONS ON THE ONGOING HUMAN RIGHTS VIOLATIONS IN LOLIONDO Background For several weeks now there has been an alarming situation and mistreatments to residents of Loliondo in Ngorongoro District along with the claim that most of them are not citizens of Tanzania. Some citizens living Loliondo area have been arrested by police, tortured, humiliated, intimidated and detained on the grounds that they are not citizens of Tanzania. Our joint declaration aims at condemning and making a call to the government in Loliondo to immidiately stop violations foisted to the people of Loliondo asserting on the issue of citizenship. It should be noted that various operations in the country such as Tokomeza, have been conducted with hidden agendas and without respect to laws and human rights. These incidents of arrest of citizens in Loliondo is a continuation of a longlived conflict between Loliondo, Sale villagers and investors associated with the government’s intention of giving away an area of square kilometers 1,500 to Otterlo Business Corporation from Dubai (OBC) The History of the Area of Conflict: Loliondo Gate Scandal Loliondo area which is known today as the Division of Loliondo and Sale is an area that has been domiciled by pastoralist since time immemorial. In 1993 the government illegally issued a wildlife hunting permit to Prince Brigadier Mohamad Al-Ali illegally for only companies ought to be issued with a hunting permit and not an individual. Since then conflicts between citizens and the government have persisted with the government using its power and resources to protect its taxpayers, OBC.
    [Show full text]
  • Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1
    Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Pili – Tarehe 13 Mei, 2015 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu! MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa, maswali tunaanza na ofisi ya Waziri Mkuu, anayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Josephine J. Genzabuke, kwa niaba yake Mheshimiwa Likokola! Na. 11 Fedha za Mfuko wa JK kwa Wajasiriamali Wadogo MHE. DEVOTHA M. LIKOKOLA (K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE) aliuliza:- Mfuko wa Wajasiriamali wadogowadogo maarufu kama mabilioni ya JK uliwavuta wengi sana lakini masharti ya kupata fedha hizo yamekuwa magumu:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kufanya mpango huo uwe endelevu kwa lengo la kuwanufaisha wanyonge? (b) Je, ni wananchi wangapi wa Mkoa wa Kigoma wamenufaika na mpango huo? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007, Serikali ilianzisha mpango wa uwezeshaji wananchi kiuchumi na kuongeza ajira kwa kutoa mikopo yenye masharti nafuu. Lengo la mpango huu ni kuwawezesha wananchi mijini na vijijini kupata mikopo ya kuanzisha au kuendeleza shughuli za kiuchumi ili kuongeza ajira na kipato. Masharti ya kupata mikopo hii si magumu sana ikilingalishwa na ile inayotolewa na mabenki, kwa sababu riba inayotozwa kwa mikopo hii ni asilimia 10, ikilinganishwa na riba inayotozwa na mabenki mengine, ambayo ni zaidi ya asilimia 20.
    [Show full text]
  • Bspeech 2008-09
    HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA, MHESHIMIWA STEPHEN MASATO WASIRA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA KWA MWAKA 2008/2009 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu baada ya kuzingatia taarifa iliyowasilishwa hapa Bungeni leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kilimo Mifugo na Maji inayohusu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, sasa lijadili na kukubali kupitisha makadirio ya Matumizi ya Kawaida na ya Maendeleo ya Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika kwa mwaka wa Fedha wa 2008/2009. 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitumie fursa hii kuungana na Watanzania wenzangu kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuchaguliwa kwake kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika. Kuchaguliwa kwake, na mchango wake alioutoa tangu kuchaguliwa kwake kuwa Mwenyekiti wa Umoja huo umelijengea Taifa letu heshima kubwa katika medani ya kimataifa. Aidha, uongozi wake na juhudi zake za kupambana na maovu katika jamii yetu, licha ya kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa ajili ya Uchaguzi wa Mwaka 2005 ni kielelezo dhahiri kuwa ni kiongozi anayejali haki na maendeleo ya nchi yetu. Juhudi zake hizo zimedhihirisha uwezo wake mkubwa wa kuongoza na utumishi wake uliotukuka aliouonyesha katika nyadhifa mbali mbali alizowahi kushika katika Serikali na Chama cha Mapinduzi. Wananchi wanaendelea kuwa na imani na matumaini makubwa kwa uwezo wake katika kuliongoza Taifa letu. 1 3. Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii pia kumpongeza Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda (MB) kwa kuteuliwa kwake kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
    [Show full text]
  • Briefing on Business & Human Rights in Tanzania 2019
    BRIEFING ON BUSINESS & HUMAN RIGHTS IN TANZANIA 2019 QUARTER 2: APRIL - JUNE In May 2019, the Legal and Human Rights Centre (LHRC) published its annual Tanzania Human Rights Report (Ref. E1). This report examines how fundamental human rights - such as the right to life, freedom of expression, the right A1 to work or the right to enjoy and benefit from natural resources - were enjoyed, protected, promoted and violated in 2018. While both government and non-government actors are working to improve human rights in the country, many challenges remain. The right to work, for instance, is challenged by inadequate (minimal) wages, difficulties for certain workers to form or participate in associations such as trade unions (Ref. E1, E2) and the absence of employment contracts (Ref. E3). The right to property, which mainly focusses on access to land, is found to have improved. Nevertheless, it remains a key issue of concern for women (Ref. E1, E4). Violations of women rights appear throughout the report, including persistent sexual violence and economic violence such as labour exploitation. The equal presence and participation of women in the country’s economy is, however, considered crucial for Tanzania’s development (Ref. E5). The report also mentions a deterioration of the freedom of expression in the country, as the result of several laws and amendments (Ref. E1). To that, Tanzania is urged nationally and internationally to keep its legislation conform international standards (Ref. E6). Under international, regional and domestic law, States have the primary duty to promote and protect human rights (Ref. E1), including in the area of business and human rights (Ref.
    [Show full text]
  • 6 MEI, 2013 MREMA 1.Pmd
    6 MEI, 2013 BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Tisa – Tarehe 6 Mei, 2013 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tukae. Waheshimiwa, mtakuwa mmepata Supplementary Order Paper, halafu na ile paper ya kwanza Supplementary hiki ni Kikao cha 19, wameandika 18 ni Kikao cha 19. Kwa hiyo, mtakuwa na Supplementary Order Paper. Katibu tuendelee? HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatayo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. 1 6 MEI, 2013 MHE. AUGUSTINO M. MASELE (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ulinzi na Usalama Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. MHE. GRACE S. KIWELU (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. MASWALI NA MAJIBU Na. 145 Wajibu wa Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji MHE. MARIAM R. KASEMBE (K.n.y. MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA) aliuliza:- Msingi mkubwa wa Maendeleo ya Jamii huanzia kwenye ngazi ya Mitaa na Vijiji ambapo hutegemea ubunifu na utendaji wa Viongozi wa ngazi husika.
    [Show full text]
  • MAWASILIANO SERIKALINI Mkuu Wa Kitengo Cha Florence Temba 022 2122942 0784246041 Mawasiliano Serikalini KITENGO CHA UGAVI NA UNUNUZI
    OFISI YA RAIS IKULU NA SEKRETARIETI YA BARAZA LA MAWAZIRI 1 Barabara ya Barack Obama, S.L.P 9120, 11400 Dar es Salaam Simu: 022 2116898/0222116900; Nukushi: 022 2128585 Email: [email protected]; Website http://www.statehouse.go.tz JINA KAMILI CHEO SIMU YA SIMU YA OFISINI MKONONI Mhe. Dkt.John Pombe Rais wa Jamhuri ya - - Magufuli Muungano wa Tanzania Mwandishi Mwendesha Mary G. Teu 022 211 6920 - Ofisi Rose E. Wabanhu Katibu Mahsusi 022 213 4924 - Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John William Mkuu wa Utumishi wa 022 211 6679 - Kijazi Umma na Katibu wa Baraza la Mawaziri Magdalena A. Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6679 - Kilongozi Mwandishi Mwendesha Eva Z. Mashallah 022 213 9649 - Ofisi Peter A. Ilomo Katibu Mkuu 022 211 0972 - Salma M. Mlinga Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 0972 - Mwandishi Mwendesha Euphrazia M. Magawa 022 212 9045 - Ofisi OFISI BINAFSI YA RAIS - Katibu wa Rais 022 211 6538 - Yunge P. Massa Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6538 - Joyce E. Pachi Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6538 - Muhidin A. Mboweto Naibu Katibu wa Rais 022 211 6908 - Usamba K. Faraja Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6908 - Katibu Msaidizi Lumbila M. Fyataga 022 211 6917 - Mwandamizi wa Rais Beatrice S. Mbaga Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6917 - Kassim A. Mtawa Katibu wa Rais Msaidizi 022 211 6917 - Alice M. Mkanula Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 211 6917 - Col. Mbarak N. Mpambe wa Rais 022 211 6921 - Mkeremy Leons D. Nkama Msaidizi wa Mtendaji Mkuu 022 116 921 - Rajabu O. Luhwavi Msaidizi wa Rais (Siasa) 022 212 8584 - Anande Z.
    [Show full text]