Tarehe 12 Septemba, 2019

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

Tarehe 12 Septemba, 2019 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Nane – Tarehe 12 Septemba, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba tukae. Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na Mkutano wetu wa Kumi na Sita na Kikao cha leo ni Kikao cha Nane, Katibu. NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI SPIKA: Hati za Kuwasilisha Mezani, naomba nimwite Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Namuona Naibu Waziri, Mheshimiwa Elias Kwandikwa. NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Taarifa ya Mwaka na Hesabu zilizokaguliwa za Mfuko wa Barabara kwa Mwaka 2015/2016 (The Annual Report and Audited Report of Roads Fund Board for the year 2015/2016). 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Waziri. Sasa naomba nimuite Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mheshimiwa Prof. Kilangi tafadhali. MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Maelezo ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 6) wa Mwaka 2019 [The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (No. 6), Bill, 2019]. SPIKA: Ahsante sana. Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo, anakuja Mwenyekiti mwenyewe, Mheshimiwa Andrew Chenge. (Makofi) MHE. ANDREW J. CHENGE – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA SHERIA NDOGO: Maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 6) wa Mwaka 2019 [The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (No. 6), Bill, 2019]. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kamati. Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Kuhusu Wizara ya Katiba na Sheria, Mheshimiwa Cecilia Paresso. MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU WIZARA YA KATIBA NA SHERIA): Maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 6) wa Mwaka 2019 [The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (No. 6), Bill, 2019]. SPIKA: Ahsante sana. Katibu. 2 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Maswali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu. Mheshimiwa Waziri Mkuu, karibu. (Makofi) Ahsante sana. Muuliza swali wa kwanza atakuwa Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Mlalo, Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi. Mheshimiwa Shangazi tafadhali. MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi hii. Mheshimiwa Waziri Mkuu, Serikali ya Awamu ya Tano imehamasisha sana shughuli za kilimo na wananchi wamehamasika sana, lakini hivi karibuni limetokea tatizo kubwa sana la ufungaji wa mazao kwa mtindo wa lumbesa lakini pia kuwepo na vifungashio ambavyo havina viwango stahiki. Jambo la kusikitisha sana ni kwamba Mamlaka za Serikali, hasa Wakala wa Vipimo na Mizani, pia Serikali katika ngazi za Halmashauri, Wilaya na Mikoa zimeshindwa kabisa kudhibiti tatizo hili la ufungaji wa mazao kwa mtindo wa lumbesa. Je, Serikali ipo tayari kuanzisha operesheni maalum nchi nzima kudhibiti tatizo hili ambalo kwa kweli linawanyong’onyeza wakulima na kuwaletea lindi la umaskini? (Makofi) SPIKA: Ahsante sana. Majibu ya swali hilo Mheshimiwa Waziri Mkuu tafadhali. WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shangazi, Mbunge wa Mlalo kule Lushoto, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali imeendelea kusisitiza wakulima wetu nchini wanapolima mazao yao waweze kunufaika kutokana na masoko yaliyo sahihi. Tunaanza kuona baadhi ya wanunuzi kutofuata sheria, 3 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) kanuni na taratibu za manunuzi ya mazao hayo pindi wanapokwenda kwa wakulima. Mheshimiwa Spika, nimefanya ziara Wilaya ya Karatu eneo maarufu linalozalisha mazao la Lake Eyasi, eneo la Eyasi kule chini. Moja kati ya malalamiko ambayo wakulima waliyatoa ni kama ambavyo Mheshimiwa Shangazi ameeleza, lakini Serikali imeweka utaratibu wa mazao yote yanayolimwa na kuingia kwenye masoko, lazima masoko hayo yatumie vipimo halisi ili liweze kulipa bei stahiki na mkulima aweze kunufaika. (Makofi) Mheshimiwa Spika, tunaposema vipimo stahiki maana yake kuna vipimo ambavyo tunavitumia, inaweza kuwa ni kipimo cha ndoo ambazo tunajua kuna ndoo za lita tano, kumi, ishirini, na ni rahisi pia kukadiria na bei ambayo inawekwa na wakulima inakuwa ndiyo bei sahihi. Pia kuna vifungashio kama vile magunia ya kilo hamsini, kilo mia, nayo pia ni sehemu ya vipimo halisi lakini muhimu zaidi ni kutumia mizani ambayo haina utata. Mheshimiwa Spika, sasa imetokea wanunuzi kuwalazimisha wakulima baada ya kile kipimo halisi kuongeza tena nundu inayojulikana kwa jina la lumbesa kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameeleza, hii haikubaliki. Tumetoa maelekezo sahihi kwa Wakuu wa Mikoa wote, Wakuu wa Wilaya wote, Wakurugenzi na Maafisa Kilimo na Maafisa Ushirika wanaosimamia masoko kwenye ngazi hizo za wakulima wawe wasimamizi wa biashara inayofanywa na wanunuzi kwa mkulima pindi anapouza mazao yake ili kujiridhisha kwamba vipimo vyote vinatumika na siyo kuongeza nundu zaidi ya kipimo ambacho kinatakiwa, kwa sababu kufanya hivyo tunamnyonya mkulima na mkulima anapata hasara kwenye mazao hayo. (Makofi) Mheshimiwa Spika, kwa hiyo utayari wa Serikali upo na tumeshatoa maelekezo kwa Wakuu wa Wilaya. Kwa hiyo nirudie tena kutoa wito kwa Maafisa Kilimo, Ushirika, Wakuu Wa Wilaya, Wakuu wa Mikoa kwenye maeneo yao 4 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) wasimamie biashara hii na kuendesha operesheni kwenye maeneo yote ya masoko ili kujiridhisha kwamba mazao yetu yananunuliwa kwa vipimo kama ambavyo vimekubalika. Huo ndiyo msisitizo wa Serikali na tutaendelea kusisitiza wakati wote. (Makofi) SPIKA: Ahsante sana, tunaendelea. Mheshimiwa Mariam Nasoro Kisangi, uliza swali lako. MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kunipa nafasi nami niweze kuuliza swali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu. Mheshimiwa Waziri Mkuu, katika miezi ya karibuni katika Mikoa mbalimbali ya nchi yetu kumekuwa na changamoto kubwa ya kupanda kwa gharama za maji bila kuzingatia uasilia, kuletewa bili zisizo sahihi, kukatiwa maji bila utaratibu na kukosa maji kwa muda mrefu kisha unaletewa bili kubwa. Kero hiyo imejitokeza katika Mikoa mbalimbali katika nchi yetu ikiwemo Mikoa ya Dar es Salaam, Manyara, Dodoma, Tanga, Mwanza na Mikoa mingine mingi na hasa katika maeneo ya Mijini. Je, Serikali inatoa kauli gani kwa wananchi wake waliokumbwa na kero hiyo? SPIKA: Ahsante sana. Mheshimiwa Waziri Mkuu majibu kwa swali hilo tafadhali. WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Kisangi, Mbunge wa Mkoa wa Dar es Salaam, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, alichosema Mheshimiwa Mbunge, yako maeneo yanajitokeza kwamba mamlaka tulizozipa mamlaka hiyo ya kusimamia maji kwenye maeneo yao, tunazo mamlaka ambazo tunazianzisha sasa za RUWA za vijijini na kwenye ngazi za Wilaya, lakini zipo mamlaka ambazo zimechukua maeneo makubwa kwenye ngazi za 5 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Mikoa, pia tuna Kamati za Maji ambazo zinasimamia miradi hii kwenye maeneo ya vijiji na maeneo mengine yote. Mheshimiwa Spika, kumejitokeza wimbi la mabadiliko ya bei. Ni kweli upo utaratibu ndani ya Serikali kwamba mamlaka hizo zinapoona zinahitaji kuboresha huduma zinaweza kufanya mapitio ya bei zao. Lakini kinachotokea sasa ni kwamba zipo mamlaka zinapita zaidi ya kiasi. Mheshimiwa Spika, nimefanya ziara Mkoani Simiyu na hapa karibuni nilikuwa kwenye Wilaya ya Maswa, moja kati ya malalamiko niliyoyapokea kwa wananchi pale ni kupanda kwa bei kutoka shilingi 5,000 wanayoilipa kwa mwezi mpaka shilingi 28,000. Sasa bei hizi hazina uhalisia, hakuna sababu ya mamlaka kutoza fedha yote hiyo na kuwafanya wananchi wakose maji. Mheshimiwa Spika, Serikali ndiyo inatekeleza hii miradi na inatoa fedha kwa lengo la kuwapa huduma wananchi ili wapate huduma ya maji. Mamlaka tumewapa jukumu la kusimamia mradi huo na kuhakikisha kwamba angalau wanaweza kufanya marekebisho, matengenezo pale ambapo kunatokea uharibifu. Kwa hiyo, gharama haziwezi kuwa kubwa kiasi hicho na wala wao hawapaswi kutoza wananchi ili kurudisha gharama za mradi kwa sababu Serikali haijadai gharama ya kuendesha mradi huo kwa wananchi. (Makofi) Mheshimiwa Spika, kwa bahati nzuri jana nilikuwa na Waziri wa Maji nikimwambia hili la kwamba lazima afuatilie Mamlaka ya EWURA ambayo ina mamlaka ya kukaa na hizo mamlaka zetu za maji kufanya mapitio ya bei. Bei zinazotakiwa kuwekwa ni zile ambazo mwananchi wa kule kijijini anaweza kuzimudu lakini siyo kwa kupandisha bei kutoka shilingi 5,000 mpaka shilingi 28,000, jambo ambalo halina uhalisia. Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wote na Watanzania kwa ujumla, tutaendelea kusimamia Mamlaka 6 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) zote za Maji, lakini Serikali itaendelea kutoa huduma za maji, nataka tujiridhishe kila Mtanzania anapata maji kwenye maeneo yake kwa usimamizi wa mamlaka hizi, lakini hatutaruhusu na hatutakubali kuona Mtanzania anatozwa gharama kubwa za maji kiasi hicho. Huku tukiwa tunatoa wito kwamba lazima tuchangie maji ili tuweze kuendesha miradi hii pale ambapo tunatakiwa kununua diesel, tunatakiwa tununue tepu ya kufungulia maji au bomba linapopasuka, lazima mamlaka zile ziweze kufanya ukarabati huo, lakini siyo kwa kutoza fedha kiasi hicho.(Makofi) Mheshimiwa Spika, masharti ambayo yapo mnapotaka kuongeza bei ni kwamba mamlaka hizo zinapodhamiria jambo hilo ni lazima kwanza zitoe taarifa EWURA, mbili kwenye vikao hivyo lazima Kamati
Recommended publications
  • Global Report
    In Focus Tanzania ruling party are no longer as united and pre- years. These include bribes paid to well- dictable as they have been throughout the connected intermediaries by the UK’s BAE country’s history as an independent nation. Systems, irregular payments of millions Political commentators of dollars from special here say that there are accounts at the central now at least two fac- bank (Bank of Tanza- tions within the party nia – BoT), inlated battling it out for in- construction contracts luence. In essence the for the BoT’s ‘twin two sides are those said towers’ headquarters, to be championing the as well as improperly ight against corruption awarded contracts for Women want more and those determined to the provision of emer- maintain the status quo gency electric power. In representation of kulindana (a Swahili one of the latter cases, Tanzania’s upcoming general elections term that can be loosely former Prime Minister, should bring great progress in women’s translated as ‘scratch Edward Lowassa, and empowerment and their participation in my back and I’ll scratch two cabinet colleagues, decision-making. That is if the ruling Chama yours’). Ibrahim Msabaha and Although it lost its Nazir Karamagi, took Cha Mapinduzi (CCM) keeps the promise status as the country’s political responsibility made in its 2005 election manifesto, that sole political party in for the so-called ‘Rich- it would achieve 50 percent women’s 1992, the Chama Cha President Jakaya Kikwete seeks election for mond affair’ by resign- participation in Parliament and local councils Mapinduzi (CCM – a second five-year term in October ing in 2008.
    [Show full text]
  • MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Thelathini Na Sita
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Sita – Tarehe 27 Mei, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nawaomba tukae. Waheshimiwa Wabunge tunaendelea na Mkutano wetu wa 15, leo ni Kikao cha 36. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NAIBU WAZIRI WA MADINI: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2019/2020. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. CATHERINE V. MAGIGE - K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI) Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu utekelezaji na Majukumu ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2018/2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. MHE. TUNZA I. MALAPO - K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU WIZARA YA MADINI: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni juu ya Wizara ya Madini kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Tunza Malapo, tunakushukuru. Katibu! NDG. STEPHEN KAGAIGAI – KATIBU WA BUNGE: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Tunaanza na TAMISEMI, swali la kwanza litaulizwa na Mheshimiwa Azza Hilal, Mbunge wa Viti Maalum - Shinyanga.
    [Show full text]
  • Check Against Delivery HOTUBA YA WAZIRI MKUU, MHESHIMIWA
    Check Against Delivery HOTUBA YA WAZIRI MKUU, MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA, (MB), WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA SITA WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, DODOMA, TAREHE 9 FEBRUARI, 2007 Mheshimiwa Spika, Mkutano wa sita wa Bunge lako Tukufu umehitimisha shughuli zote zilizokuwa zimepangwa. Mkutano huu ni wa kwanza baada ya Serikali ya Awamu ya Nne kutimiza mwaka mmoja madarakani. Taarifa za mafanikio na changamoto zilizojitokeza zimewasilishwa kupitia mikutano mbalimbali ya Chama Tawala, Serikali na vyombo mbalimbali vya habari. Mheshimiwa Spika, kwa masikitiko makubwa, nachukua nafasi hii tena kwa niaba ya Serikali na wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kutoa rambirambi kwako wewe Mheshimiwa Spika, kwa Waheshimiwa Wabunge wote, kwa familia, jamaa na marafiki kwa msiba uliotokana na kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tunduru, na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Bunge na Uratibu) Marehemu Juma Jamaldin Akukweti. Wote tulimfahamu Marehemu Akukweti kwa umakini na umahiri wake hapa Bungeni. Marehemu Akukweti alifariki kutokana na ajali ya ndege iliyokuwa inamrejesha Dar es Salaam baada ya kumaliza kazi ya kukagua soko la Mwanjelwa lililoteketea kwa moto mkoani Mbeya. Katika ajali hiyo Watumishi wa Serikali walipoteza maisha. Watumishi hao ni Bibi Theresia Nyantori, Mwandishi wa Habari wa Idara ya Habari; Bwana Nathaniel Katinila, Mratibu wa Mradi wa Masoko; na Bwana George Bendera, Afisa Habari Idara ya Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu. Majeruhi katika ajali hiyo ambao bado wanapata matibabu lakini wametoka hosptali ni Bw. Nisetas Kanje, Katibu wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Bunge na Uratibu); na rubani wa ndege hiyo Bw. Martin Sumari. Tunamwomba Mwenyezi Mungu awasaidie majeruhi wote waweze kupona haraka na kurudia katika afya zao.
    [Show full text]
  • Issued by the Britain-Tanzania Society No 124 Sept 2019
    Tanzanian Affairs Issued by the Britain-Tanzania Society No 124 Sept 2019 Feathers Ruffled in CCM Plastic Bag Ban TSh 33 trillion annual budget Ben Taylor: FEATHERS RUFFLED IN CCM Two former Secretary Generals of the ruling party, CCM, Abdulrahman Kinana and Yusuf Makamba, stirred up a very public argument at the highest levels of the party in July. They wrote a letter to the Elders’ Council, an advisory body within the party, warning of the dangers that “unfounded allegations” in a tabloid newspaper pose to the party’s “unity, solidarity and tranquillity.” Selection of newspaper covers from July featuring the devloping story cover photo: President Magufuli visits the fish market in Dar-es-Salaam following the plastic bag ban (see page 5) - photo State House Politics 3 This refers to the frequent allegations by publisher, Mr Cyprian Musiba, in his newspapers and on social media, that several senior figures within the party were involved in a plot to undermine the leadership of President John Magufuli. The supposed plotters named by Mr Musiba include Kinana and Makamba, as well as former Foreign Affairs Minister, Bernard Membe, various opposition leaders, government officials and civil society activists. Mr Musiba has styled himself as a “media activist” seeking to “defend the President against a plot to sabotage him.” His publications have consistently backed President Magufuli and ferociously attacked many within the party and outside, on the basis of little or no evidence. Mr Makamba and Mr Kinana, who served as CCM’s secretary generals between 2009 to 2011 and 2012-2018 respectively, called on the party’s elders to intervene.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA KUMI NA SITA ______________ Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 27 Julai, 2009) (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita anayeuliza swali la kwanza, karibuni tena baada ya mapumziko ya weekend, nadhani mna nguvu ya kutosha kwa ajili ya shughuli za wiki hii ya mwisho ya Bunge hili la 16. Swali la kwanza linaelekezwa Ofisi ya Waziri Mkuu na linauliza na Mheshimiwa Shoka, kwa niaba yake Mheshimiwa Khalifa. Na.281 Kiwanja kwa Ajili ya Kujenga Ofisi ya Tume ya Kudhibiti UKIMWI MHE KHALIFA SULEIMAN KHALIFA (K.n.y. MHE. SHOKA KHAMIS JUMA) aliuliza:- Kwa kuwa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI inakabiliwa na changamoto ya ufinyu wa Ofisi; na kwa kuwa Tume hiyo imepata fedha kutoka DANIDA kwa ajili ya kujenga jengo la Ofisi lakini inakabiliwa na tatizo kubwa la upatikanaji wa kiwanja:- Je, Serikali itasaidia vipi Tume hiyo kupata kiwanja cha kujenga Ofisi? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU – SERA, URATIBU NA BUNGE alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shoka Khamis Juma, Mbunge wa Micheweni kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, tatizo la kiwanja cha kujenga Ofisi za TACAIDS limepatiwa ufumbuzi na ofisi yangu imewaonesha Maafisa wa DANIDA kiwanja hicho Ijumaa tarehe 17 Julai, 2009. Kiwanja hicho kipo Mtaa wa Luthuli Na. 73, Dar es Salaam ama kwa lugha nyingine Makutano ya Mtaa wa Samora na Luthuli. MHE. KHALIFA SULEIMAN KHALIFA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Waziri, naomba kumuuliza swali moja la nyongeza.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 18 Julai, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita muuliza swali la kwanza nina matangazo kuhusu wageni, kwanza wale vijana wanafunzi kutoka shule ya sekondari, naona tangazo halisomeki vizuri, naomba tu wanafunzi na walimu msimame ili Waheshimiwa Wabunge waweze kuwatambua. Tunafurahi sana walimu na wanafunzi wa shule zetu za hapa nchini Tanzania mnapokuja hapa Bungeni kujionea wenyewe demokrasia ya nchi yetu inavyofanya kazi. Karibuni sana. Wapo Makatibu 26 wa UWT, ambao wamekuja kwenye Semina ya Utetezi na Ushawishi kwa Harakati za Wanawake inayofanyika Dodoma CCT wale pale mkono wangu wakulia karibuni sana kina mama tunawatakia mema katika semina yenu, ili ilete mafanikio na ipige hatua mbele katika kumkomboa mwanamke wa Tanzania, ahsanteni sana. Hawa ni wageni ambao tumetaarifiwa na Mheshimiwa Shamsa Selengia Mwangunga, Naibu Waziri wa Maji. Wageni wengine nitawatamka kadri nitakavyopata taarifa, kwa sababu wamechelewa kuleta taarifa. Na. 223 Barabara Toka KIA – Mererani MHE. DORA H. MUSHI aliuliza:- Kwa kuwa, Mererani ni Controlled Area na ipo kwenye mpango wa Special Economic Zone na kwa kuwa Tanzanite ni madini pekee duniani yanayochimbwa huko Mererani na inajulikana kote ulimwenguni kutokana na madini hayo, lakini barabara inayotoka KIA kwenda Mererani ni mbaya sana
    [Show full text]
  • Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania
    JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA ISHIRINI NA TISA 19 MEI, 2017 MKUTANO WA SABA KIKAO CHA ISHIRINI NA TISA TAREHE 19 MEI, 2017 I. DUA: Naibu Spika Mhe. Tulia Ackson alisoma Dua na kuongoza Bunge Saa 3:00 asubuhi. Makatibu mezani: 1. Ndugu Theonest Ruhilabake 2. Ndugu Neema Msangi II. HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani:- (1) Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi aliwasilisha:- Hotuba za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (2) Mhe. Mattar Ali Salum – (Kny. Mwenyekiti wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji aliwasilisha Mezani: Taarifa ya Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 pamoja na maoni ya Kamati juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. (3) Mhe. Susan A. J. Lyimo – Msemaji Mkuu wa Upinzani kwa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi aliwasilisha Mezani:- 1 Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani, juu ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. III. MASWALI OFISI YA RAIS (TAMISEMI) Swali Na. 234: Mhe. Cosato D. Chumi Nyongeza: Mhe. Cosato D. Chumi Mhe. Kasuku S. Bilago Mhe. Daimu I. Mpakate WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO Swali Na. 235: Mhe. Dr. Mary M. Mwanjelwa Nyongeza: Mhe. Dr. Mary M. Mwanjelwa Mhe. Susan A. J. Lyimo Mhe.
    [Show full text]
  • Tarehe 28 Juni, 2017
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Hamsini na Tano – Tarehe 28 Juni, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu. NDG. THEONEST RUHILABAKE – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- MHE. GEORGE M. LUBELEJE (K.n.y. MHE. KAPT. MST. GEORGE H. MKUCHIKA - MWENYEKITI WA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE): Taarifa ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shauri la Kudharau Mamlaka ya Spika linalomhusu Mheshimiwa Joshua Samwel Nassari, Mbunge na Shauri la Kusema Uwongo Bungeni linalomhusu Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza, Mbunge. NAIBU SPIKA: Ahsante sana. Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. THEONEST RUHILABAKE – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali tutaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu. Mheshimiwa Mgeni Jadi Kadika, Mbunge wa Viti Maalum, kwa niaba yake Mheshimiwa Mheshimiwa Mwanne Mchemba. Na. 452 Mradi wa MIVARF MHE. MWANNE I. MCHEMBA (K.n.y. MHE. MGENI JADI KADIKA) aliuliza:- Mradi wa MIVARF ni wa Muungano na Makao Makuu yapo Arusha ambapo kazi yake kuu ni kujenga masoko, miundombinu ya barabara, kuongeza thamani na kupeleka maendeleo vijijini:- Je, ni kwa kiasi gani mradi huu umechangia kuleta maendelezo Zanzibar? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANA NA AJIRA) alijibu: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mgeni Jadi Kadika, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, MIVARF ni programu inayohusika na miundombinu ya masoko, uongezaji thamani ya mazao na huduma za kifedha vijijini.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA NANE Kikao Cha Tatu – Tarehe 14
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Tatu – Tarehe 14 Juni, 2007 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge itakumbukwa kuwa, katika Mkutano wa Bunge wa Saba, Bunge hili pamoja na shughuli nyingine lilipitisha Miswada ya Sheria ya Serikali Tisa. Kati ya Miswada hiyo, Miswada Saba tayari imepata kibali cha Mheshimiwa Rais na sasa ni Sheria ya Nchi kama ifuatavyo:- 1. The Land Use Planning Act, 2007 ni Sheria sasa Namba 6 ya Mwaka 2007 2. The Town Planners (Registration) Act 2007 sasa ni Sheria Namba 7 ya 2007 3. The Suplementary Appropriation (for Financial Year 2003, 2004) Act, 2007 ni Sheria Namba 9 ya Mwaka 2007 4. The National Bank of Commerce (Re-Organization and Vesting Assets and Liabilities) Act, 2007 ni Sheria Namba 10 ya Mwaka 2007 5. Prevention and Combating of Corruption Act, 2007 ni Sheria sasa Namba 11 ya Mwaka 2007 6. Optometry Act ni Sheria Na.mba 12 ya 2007 7. The Fire and Rescue Act, 2007 ambayo ni Sheria Namba 14 ya Mwaka 2007. Kwa taarifa yenu Waheshimiwa Wabunge Miswada miwili iliyobaki yaani: “The Urban and Planning Bill 2007” na “The Roads Bill, 2007” haijapelekwa kwa Mheshimiwa Rais kwa sababu bado ipo kwa Mpigachapa Mkuu wa Serikali ikiwa katika hatua zake za mwisho za uchapishwaji. 1 Mtakumbuka kwa mfano ule Mswada wa “Roads Bills” ni mrefu sana una majina ya barabara zote nchini na kadhalika. Siyo rahisi kuuchapa kwa haraka na ukaupatia kwa usahihi.
    [Show full text]
  • Tanzania Bruce Heilman and William John Introduction United Under The
    COUNTRIES AT THE CROSSROADS Countries at the Crossroads 2012: Tanzania Bruce Heilman and William John1 Introduction United under the leadership of the nationalist Tanganyika National African Union (TANU) party and its visionary founder, Julius Nyerere, Tanganyika peacefully gained independence from Britain on December 9, 1961. However, political independence for the nearby Indian Ocean islands of Zanzibar was turbulent. Zanzibar became independent in December 1963, but was divided by two rival nationalist movements, the African-oriented Afro-Shirazi Party (ASP) and the Arab-oriented Zanzibar Nationalist Party (ZNP). Its first postcolonial government, formed by the ZNP, was quickly overthrown by a violent revolution that transferred state power to the ASP in January 1964. 2 After the revolution the Zanzibar constitution was suspended and Abedi Karume and the Revolutionary Council ruled by decree. In April 1964 Zanzibar merged with Tanganyika to form the United Republic of Tanzania. Despite the union, Zanzibar’s government retained considerable autonomy over its internal affairs and political dissent on the islands was not tolerated with human rights abuses widely reported. It was not until 1980 that a semblance of rule of law returned to Zanzibar with the introduction of single party elections and in 1984 Zanzibar finally enacted a constitution. The revolution on Zanzibar coincided with a rising tide of expectations and uncertainty on the mainland, as the lifting of colonial oppression unleashed numerous societal demands that the new government had limited means to address. Calls for jobs, higher wages, and improved access to education, health care, and water, as well as Africanization of the military, civil service, and the private sector of the economy, led to numerous strikes.
    [Show full text]
  • Tanzania Human Rights Report 2015 Tanzania Mainland Legal and Human Rights Centre (LHRC) Tanzania Human Rights Report 2015
    Tanzania Human Rights Report 2015 Tanzania Mainland Legal and Human Rights Centre (LHRC) Tanzania Human Rights Report 2015 Publishers Legal and Human Rights Centre Justice Lugakingira House, Kijitonyama P.O. Box 75254, Dar es Salaam, Tanzania Tel: +255222773038/48, Fax: +255222773037 Email: [email protected] Website: www.humanrights.or.tz Partners - LHRC Accountability in Tanzania (AcT) The Embassy of Norway The Embassy of Sweden ISBN: 978-9987-740-25-3 © LHRC 2016 - ii - Tanzania Human Rights Report 2015 Editorial Board Dr. Helen Kijo-Bisimba Adv. Imelda Urrio Ms. Felista Mauya Adv. Anna Henga Mr. Castor Kalemera Researchers/Writers Mr. Paul Mikongoti Mr. Pasience Mlowe Mr. Fundikila Wazambi Design & Layout Mr. Rodrick Maro - iii - Tanzania Human Rights Report 2015 Acknowledgement Legal and Human Rights Centre (LHRC) has been producing the Tanzania Human Rights Report, documenting the situation in Tanzania Mainland since 2002. In the preparation and production of this report LHRC receives both material and financial support from different players, such as the media, academic institutions, other CSOs, researchers and community members as well as development partners. These players have made it possible for LHRC to continue preparing the report due to its high demand. In preparing the Tanzania Human Rights Report 2015, LHRC received cooperation from the Judiciary, the Legislature and the Executive arms of the State. Various reports from different government departments and research findings have greatly contributed to the finalization of this report. Hansards and judicial decisions form the basis of arguments and observations made by the LHRC. The information was gathered through official correspondences with the relevant authorities, while other information was obtained online through various websites.
    [Show full text]