Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Nne – Tarehe 9 Mei, 2014 (Mkutano Uianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA: Randama za Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA) PAMOJA NA (UTAWALA BORA): Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma) pamoja na (Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (MAHUSIANO NA URATIBU): Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. JAKU HASHIM AYOUB (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA): Taarifa ya Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), (Utawala Bora) pamoja na (Mahusiano na Uratibu) kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na maoni 1 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hizo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. PROF. KULIKOYELA K. KAHIGI - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA), (UTAWALA BORA) PAMOJA NA (MAHUSIANO NA UTARATIBU):- Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), (Utawala Bora) pamoja na (Mahusiano na Uratibu) kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hizo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015 MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaanza Maswali na Ofisi ya Waziri Mkuu. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) 1 BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA TISA Kikao cha Tisa – Tarehe 9 Novemba, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaanza Maswali na Ofisi ya Waziri Mkuu Mheshimiwa Betty Eliezer Mchangu, atauliza swali la kwanza leo. Na. 106 Kuboresha Majengo, Vitendeakazi na Watumishi wa Hospitali Kilimanjaro MHE. BETTY E. MACHANGU aliuliza:- Hospitali ya Rufaa ya Mawenzi Mkoani Kilimanjaro inahudumia wagonjwa zaidi ya milioni 2 lakini ina matatizo makubwa kama vile ukosefu wa chumba cha upasuaji, chumba cha wagonjwa mahututi (ICU), Martenity Ward, jengo la magonjwa ya dharura na jengo la akina mama wajawazito (Kujitazamia). (a) Serikali itaweka lini majengo hayo na kurejesha huduma stahili. (b) Je, Serikali ipo tayari kuziwezesha Hospitali za St. Joseph na Machame kupata vitendea kazi na watumishi ili zisaidie Hospitali ya Mkoa kutoa huduma kwa wananchi. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Betty Eliezer Machangu, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, ninakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba sehemu kubwa ya miundombinu ya Hospitali ya Mkoa wa Kilimanjaro ya Mawenzi ni chakavu. Katika mwaka 2012/2013, sekretarieti ya Mkoa wa Kilimanjaro imeweka kipaumbele na kuelekeza fedha zote za miradi ya maendeleo kwa ajili ya ukarabati wa Hospitali ya Mkoa wa Kilimanjaro. 1 2 Jumla ya shilingi milioni 744.2 zitatumika kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa jengo la upasuaji. -
MKUTANO WA 18 TAREHE 5 FEBRUARI, 2015 MREMA 1.Pmd
5 FEBRUARI, 2015 BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE __________________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Tisa – Tarehe 5 Februari, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, leo sijamwona. Kwa hiyo tunaendelea na Maswali kwa Waziri Mkuu na atakayeanza ni Mheshimiwa Murtaza A. Mangungu. MHE. MURTAZA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa vipindi tofauti vya Bunge Mheshimiwa Peter Msigwa, Mheshimiwa Mussa Zungu na hata Mheshimiwa Murtaza A. Mangungu wamekuwa wakiuliza swali kuhusiana na manyanyaso wanayoyapata wafanyabiashara Wadogo Wadogo pamoja na Mamalishe. Kwa kipindi hicho chote umekuwa ukitoa maagizo na maelekezo, inavyoonekana mamlaka zinazosimamia hili jambo haziko tayari kutii amri yako. 1 5 FEBRUARI, 2015 Je, unawaambia nini Watanzania na Bunge hili kwa ujumla? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba nimjibu Mheshimiwa Murtaza Mangungu swali lake kama ifuatavyo:- Suala hili la vijana wetu ambao tunawajua kama Wamachinga, kwanza nataka nikiri kwamba ni suala kubwa na ni tatizo kubwa na si la Jiji la Dar es Salaam tu, bali lipo karibu katika miji mingi. Kwa hiyo, ni jambo ambalo lazima twende nalo kwa kiwango ambacho tutakuwa na uhakika kwamba tunalipatia ufumbuzi wa kudumu. Kwa hiyo, ni kweli kwamba mara kadhaa kuna maelekezo yametolewa yakatekelezwa sehemu na sehemu nyingine hayakutekelezwa kikamilifu kulingana na mazingira ya jambo lenyewe lilivyo. Lakini dhamira ya kutaka kumaliza tatizo hili la Wamachinga bado ipo palepale na kwa bahati nzuri umeuliza wakati mzuri kwa sababu jana tu nimepata taarifa ambayo nimeandikiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI ambayo wanaleta mapendekezo kwangu juu ya utaratibu ambao wanafikiri unaweza ukatatua tatizo hili ambalo lipo sehemu nyingi. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Thelathini na Nne – Tarehe 27 Julai, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Sylvester Massele Mabumba) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha, 2011/2012. NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kwa Mwaka wa Fedha, 2011/2012. MWENYEKITI WA KAMATI YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI: Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Maendeleo ya Kilimo na Uvuvi kwa Mwaka 2010/2011 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani juu ya Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. MASWALI NA WAJIBU Na. 312 Kuimarisha Barabara ya Mpopera – Mkarongo – Kipatimu MHE. MURTAZA A. MANGUNGU aliuliza:- Kata ya Kandawale ni kisiwa ambapo mvua zinanyesha na hakuna daraja kwenye Mto Matandu la kuunganisha Njinjo na Kandawale. 1 Je, Serikali i na mpango gani wa kuimarisha barabara ya Wilaya ya Mpopera – Mkarongo – Kipatimu ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa iliomba fedha za ziada kwa ajili ya hiyo miaka sita iliyopita. -
The Institutional Origins of Competitiveness and Hegemony in Post-Cold War Africa
PARTY MATTERS: THE INSTITUTIONAL ORIGINS OF COMPETITIVENESS AND HEGEMONY IN POST-COLD WAR AFRICA A Dissertation submitted to the Faculty of the Graduate School of Arts and Sciences of Georgetown University in partial fulfillment of the requirements for the degree of Doctor of Philosophy in Government By Yonatan L. Morse, M.A. Washington, DC August 23, 2013 Copyright 2013 by Yonatan L. Morse All Rights Reserved ii PARTY MATTERS: THE INSTITUTIONAL ORIGINS OF COMPETITIVENESS AND HEGEMONY IN POST-COLD WAR AFRICA Yonatan L. Morse, M.A. Thesis Advisor: Marc M. Howard, Ph.D. ABSTRACT What explains differences in electoral authoritarian outcomes? Why are some regimes able to utterly dominate elections with comparatively lower levels of fraud and coercion, while in other cases regimes can only muster slim vote margins? What explains differences in the competitiveness and hegemony of electoral authoritarian elections? This dissertation focuses specifically on Africa’s former single-party regimes and argues that differences in party capacity developed under single-party rule is a primary factor differentiating forms of electoral authoritarianism. Through typological theorizing and case-studies of Tanzania, Kenya, and Cameroon this project shows how single-party regimes that elevated the party as an important decision-making institution, made credible investments into party institutionalization, and kept open avenues for elite recruitment were less likely to experience elite defection during multiparty elections. Likewise, single-party regimes that built strong party-affiliated mobilizing structures and engaged in wide practices of social incorporation were able to rely on persistently large electoral support. In the absence of these party capacities regimes were forced to rely more heavily on fraud and a range of contingent factors to survive. -
TEMCO Report 2010 General Election English Version
TANZANIA ELECTION MONITORING COMMITTEE (TEMCO) THE 2010 TANZANIA GENERAL ELECTIONS REPORT OF THE TANZANIA ELECTION MONITORING COMMITTEE March, 2011 i LIST OF ABBREVIATIONS AFP - Alliance for Tanzania Farmers Party AG - Attorney General APPT-Mandeleo - African Progressive Party ARO - Assistant Returning Officer BAWACHA - Baraza la Wanawake wa CHADEMA CBO - Community Based Organization CCJ - Chama Cha Jamii CCM - Chama Cha Mapinduzi CEDAW - Convention on the Elimination of All Forms of Discrimination Against Women CHADEMA - Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHAUSTA - Chama cha Ustawi na Demokrasia CSM - Management System CSO - Civil Society Organization CUF - Civic United Front DED - District Executive Director EEA - Election Expenses Act EMB - Election Management Body ESP - Election Support Programme FBO - Faith Based Organization FEM ACT - Feminist Activist Coalition FIA - Freedom of Information Act FOS - Friends of Dr. Slaa HoR - House of Representatives ID - Identity Card IEMS - Integrated Election Management System IFJ - International Federation of Journalists IT - Information Technology LHRC - Legal and Human Rights Centre LTO - Long Term Observer MDG - Millennium Development Goal MP - Member of the Parliament NCCR-Mageuzi - National Convention for Construction and Reform NEC - National Electoral Commission NGO - Non-Governmental Organization NLD - National League for Democracy NRA - National Reconstruction Alliance PCCB - Prevention and Combating of Corruption Bureau PNVR - Permanent National Voter Register RO - Returning Officer -
17 Aprili, 2013
17 APRILI, 2013 BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Saba - Tarehe 17 Aprili, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na: WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA (K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, UHUSIANO NA URATIBU: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu) kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. 1 17 APRILI, 2013 MWENYEKITI WA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA: Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), (Utawala Bora) Pamoja na (Uratibu na Mahusiano) kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hizo kwa Mwaka wa Fedha 2013/ 2014. MHE. RAYA IBRAHIM KHAMIS (K.n.y. MHESHIMIWA KULIKOYELA K. KAHIGI - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA, UTAWALA BORA, URATIBU NA MAHUSIANO: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), (Utawala Bora) Pamoja na (Uratibu na Mahusiano) Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hizo kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. -
MKUTANO WA TATU Kikao Cha Saba – Tarehe 14 Aprili, 2011
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Saba – Tarehe 14 Aprili, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, leo ni Siku ya Alhamisi, kama kawaida yetu, siku hii dakika thelathini za kwanza tunakuwa na maswali kwa Waziri Mkuu. Anayeanza ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani. MHE. FREEMAN A. MBOWE (KIONGOZI WA KAMBI YA UPINZANI BUNGENI): Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la kwanza kwa Waziri Mkuu. Kwa kuwa Katiba ni Roho ya Taifa; na kwa kuwa kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu ya mabadiliko au kuandikwa upya kwa Katiba ya Nchi, jambo ambalo Serikali imeridhia kupitia kwa Rais; na kwa sababu Serikali ilileta Muswada katika utaratibu wa haraka, Muswada wa Constitution Review:- Je, baada ya Serikali kuona reaction ya wadau mbalimbali wakiwemo wanazuoni, Vyama vya Siasa, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na wadau wengine mbalimbali, ambao wanafikiri kwamba, mchakato huu pengine unakwenda kwenye kasi ambayo badala ya kujenga inaweza ikatia nyufa katika mahusiano yetu; ni kwa nini Serikali kupitia kwa Waziri Mkuu wasitoe tamko rasmi la Serikali la kukubaliana na utashi wa wadau ili kuusogeza Muswada huu mbele Wananchi wapate fursa ya kutosha ili kuweka mahusiano mema ambayo tunategemea katika Taifa letu? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, ninaomba nimjibu Mheshimiwa Mbowe, ambaye ndiye Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, swali lake kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba, Serikali imewasilisha Muswada hapa Bungeni na tuliwasilisha kwa Hati ya Dharura, kwa dhamira njema kabisa kwa kuwa tuliamini kabisa kwamba, watu wana hamu na shauku kubwa ya kutaka kufikia hatua ya 1 pili ya mchakato, kwa maana ya Katiba yenyewe baada ya kuwa Tume ya Katiba imeundwa.