17 Aprili, 2013
17 APRILI, 2013 BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Saba - Tarehe 17 Aprili, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na: WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA (K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, UHUSIANO NA URATIBU: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu) kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. 1 17 APRILI, 2013 MWENYEKITI WA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA: Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), (Utawala Bora) Pamoja na (Uratibu na Mahusiano) kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hizo kwa Mwaka wa Fedha 2013/ 2014. MHE. RAYA IBRAHIM KHAMIS (K.n.y. MHESHIMIWA KULIKOYELA K. KAHIGI - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA, UTAWALA BORA, URATIBU NA MAHUSIANO: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), (Utawala Bora) Pamoja na (Uratibu na Mahusiano) Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hizo kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014.
[Show full text]