MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao Cha Thelathini Na Saba
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Thelathini na Saba – Tarehe 24 Julai, 2009 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 272 Halmashauri ya Wilaya ya Dodoma Kukabidhiwa Jengo lake MHE. JENISTA J. MHAGAMA (K.n.y. MHE. FELISTER A. BURA) aliuliza:- Kwa kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma inatumia majengo ya iliyokuwa Shule ya Sekondari ya Aga-Khan kama Ofisi zake:- Je, ni lini Halmashauri itakabidhiwa jengo lake linalotumiwa na Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika ? WAZIRI WA MIUNDOMBINU alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, napenda kuchukua fursa hii, kutoa shukrani nyingi sana kwako wewe mwenyewe binafsi na kwa Waheshimiwa Wabunge wenye taaluma ya afya, ambao wamemhudumia Naibu Waziri, Mheshimiwa Hezekiah Chibulunje, wakati alipopata matatizo hapa Bungeni. Natoa shukrani nyingi sana pia kwa Wabunge wote, ambao wamekwenda kumpa pole na kumwombea dua ili aweze kupona mapema. Mheshimiwa Naibu Waziri, sasa hivi anaendelea vizuri, yuko katika mapumziko na Mungu akijalia, tutakuwa naye hivi karibuni. Mheshimiwa Naibu Spika, ninakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kuwa, eneo lenye majengo yanayotumiwa na baadhi ya Wizara za Serikali hapa Dodoma ni mali ya Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma, kwa mujibu wa Hati Miliki Na. 12814 iliyotolewa tarehe 2 Desemba, 1958. Eneo hilo ambalo lilijulikana kama Town Hall Plot, majengo 1 yake yalianza kutumiwa na Wizara za Serikali kwa nyakati mbalimbali kutokea mwaka 1973, baada ya kuvunjwa kwa Serikali za Mitaa na yameendelea kutumiwa na Wizara za Serikali hata baada ya kuanzishwa tena Mamlaka za Serikali za Mitaa.
[Show full text]