Tarehe 22 Juni, 2012

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

Tarehe 22 Juni, 2012 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NANE _______________ Kikao cha Nane – Tarehe 22 Juni, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE: Randama za Makadirio ya Mafungu ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi zake kwa Mwaka 2012/2013. SPIKA: Ahsante sana, umeomba kuwasilisha. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge maswali tunaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu na atakaye uliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Muhammad Ibrahim Sanya. Na. 58 1 Utengenezaji wa Barabara Kwenye Mitaa Mbalimbali Dar es Salaam MHE. MUHAMMAD IBRAHIM SANYA aliuliza:- Jiji la Dar es Salaam linaendelea kujengwa majengo mapya mazuri, marefu yenye kuleta sura mpya ya jiji hilo, ujenzi unaofanywa na Mashirika na watu binafsi mbalimbali kwa matumizi ya aina mbalimbali lakini barabara nyingi zipitazao kwenye maeneo hayo na mitaa yake ni mbovu sana na hazilingani na hadhi ya majengo hayo mapya na kuwa kero na usumbufu kwa watu wanaoishi karibu na maeneo hayo:- Je, ni lini Serikali itajenga upya au kuzitengeneza barabara hizo ili zifae kupitika nyakati zote na kuliweka jiji katika hali safi ya kuvutia kama nchi nyingine wanavyofanya? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa naiba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Muhammad Ibrahim Sanya, Mbunge wa Mji Mkongwe, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Jiji la Dar es Salaam lina barabara zenye urefu wa kilomita 2459 kati ya barabara hizo kilomita 598 asilimia 24.3 ni za lami na kilomita 1352 ambazo ni sawasawa na asilimia 55 ni za changarawe na kiliomita 509 ambazo ni sawa sawa na asilimia 20.7 ni za udongo. 2 Kati ya barabara hizi kilomita 560 sawa na asilimia 22.8 zinasimamiwa na Wizara ya Ujenzi zinasimamiwa na Wizara ya Ujenzi kupitia wakala wa barabara na kiasi kinachobaki kinasimamiwa na Halmashauri za Manispaa ya Kinondoni na Temeke. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa kilomita 1899, zinazosimamiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI kupitia Halmashauri ya Kinondoni, Ilala na Temeke, Serikali imekuwa ikiboresha kwa kuzifanyia matengenezo barabara hizi kwa kutumia fedha za ndani, hususan mfuko wa barabara ambapo kwa mwaka 2010/2011 zilitumika bilioni 4.9, mwaka 2011/2012 zimetumika shilingi biioni 5.96 na mwaka 2012/2013 inatazamia kutumia bilioni 7.34. Mheshimiwa Spika, kwa kushirikiana na wahisani mbalimbali Serikali imekuwa ikifanya matengenezo mbalimbali katika barabara hizo. Baadhi ya wahisani hao ni Serikai za watu wa Japan pamoja na Benki ya Dunia. Serikali kwa kushirikiana na wahisani hao inajenga barabara ya Bagamoyo kuanzia Morocco hadi kibaoni. Kwa kushirikiana na Benki ya Dunia Serikali inatekeleza mradi wa Dar es Salaam Metropolitan Development Project ambao umetengewa dola milioni 75 sawa sawa na shilingi bilioni 112.5 kwa kuanzia ambapo kwa kiasi hiki inategemewa kuongezeka. Mradi huo upo hatua ya kumtafuta mshauri ya kufanya wa kufanya usanifu. Kazi ya matengenezo ya barabara katika Jiji la Dar es Salaam kupitia mradi huu inatarajiwa kuanzia mwaka wa fedha 2013/2014. 3 Mheshimiwa Spika, Serikali ilipokuwa ikifanyia matengenezao barabara zake kadri fedha zinavyopatikana. Ni matazamio yetu mradi huu wa DMDP utakamilika barabara nyingi za jiji la Dar es Salaam zitakuwa zimeboreshwa. (Makofi) MHE. MUHAMMAD IBRAHIM SANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili, Jiji la Dar es Salaam linapanuka kwa kiasi ambacho hatukutarajia na kwa fedha zinazotengwa ni kidogo mno ukilinganisha na gharama za utengenezaji wa barabara. (Makofi) Je, ingawaje gradually tunakwenda kidogo kidogo kutokana na hizi taarifa za fedha zilitumika kuanzia 2010/2011, 2011/2012 na mwaka huu inatarajiwa kutumika kiasi gani? Serikali iko tayari sasa walau kwa kipindi cha Bajeti ya mwakani zikatengwa kila mwaka siyo chini ya bilioni 30 tukaondosha tatizo la barabara katika Jiji la Dar es Salaam? Katika mipango miji barabara ni tatizo lakini wakati huo huo majengo yanayojengwa katika Jiji la Dar es Salaam yanahitajia parking ambalo limekuwa tatizo kubwa ukilinganisha na idadi ya watu wanaoishi katika jiji la Dar es Salaam. Halmashauri husika pamoja na Serikali zinamipango gani kuhakikisha kabla ya kutoa vibali kukatengwa maeneo maalum ili wanapojenga hayo majumba kwenda juu kwa gorofa kumi na zaidi watu waweze kuwa na parking za uhakika ili kupunguza upungufu katika Jiji la Dar es Salaam? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): 4 Mheshimiwa Spika, kwanza mimi nimpongeze sana Mheshimiwa Sanya najua yeye ni Mbunge wetu wa Mji Mkongwe kule lakini anaonyesha concern kubwa kwa sababu anaangalia mambo kitaifa. Kwa hiyo sisi tunakupongeza sana kwa hili unalolizungumza hapa. (Makofi) Umuhimu wa Jiji la Dar es Salaam na mambo yote yanayokwenda pale sidhani kama kuna mtu yeyote hapa anaweza akabisha kuhusu jambo hili, ni jambo la msingi sana. Ule mradi ambao tunazungumza sasa hivi ambao nimesema kwamba uta-operate mradi ule mkubwa ambao umekwenda Mbeya, Tanga na maeneo mengine mengi mpaka hapa Dodoma mnaona unafanyika, ulihitaji shilingi bilioni 165 kama tungeiingiza Dar es Salaam katika mpango ule, mpango wa Dar es Salaam unahitaji shilingi bilioni 365. Kwa hiyo unaweza ukaona kwamba ukisema uzichukue zile ambazo World Bank wanatusaidia zote zile Dar es Salaam ingechota zote zingeondoka. Kwa hiyo kilichofanyika hapa ni kwamba tumeona kwamba tuombe sasa msaada huu na ndiyo maana nimeeleza hapa kwamba kuna mpango maalum ambao unatumika. Mheshimiwa Sanya anachosema hapa anasema hivi kwanini usingeweka katika Bajeti yako kila mwaka bilioni 30, bilioni 30 which makes a lot of sense mimi navyoona katika kipindi cha miaka mitano utakuwa umekusanya nini. Watu wanaohusika katika jambo hili kama nilivyosema siyo sisi tu TAMISEMI na Wizara ya Ujenzi na wahusika wako hapa wanasikia wako wadau mbalimbali ambao wanajiingiza katika mpango. Mimi 5 nachosema ni kwamba concern hii tunaiona na ni muhimu kwamba tuifanyie kazi ili tuone jinsi tunavyoenda. Lakini pia itategemeana na uwezo wetu wa kiuchumi ndicho ninachokiona pale. Lakini la pili analolizungumza ni muhimu zaidi kuliko tunavyofikiri. Majengo yanajengwa pale yanajengwa halafu baadaye huna parking huna mahali pa kufanya kesho unaamka unataka kupitisha barabara kule na nini na vitu vingine vya namna hiyo. Kwa sasa hivi utaratibu na amesema yeye mwenyewe alipokuwa anauliza swali Mheshimiwa Spika, huwezi ukamruhusu mtu kujenga jengo lolote mahali popote mpaka apate kitu kinachoitwa building permit. Wadau mbali mbali wataangalia ili kuhakikisha kwamba inakidhi yote haya ambayo unayazungumza hapa. Kwa hiyo tunasema kwamba Mheshimiwa Sanya anatoa mawazo mazuri na tutayachukua haya ni jambo ambalo tutalifanyia kazi lakini ndivyo tunavyofanya sasa hivi hapa na ndiyo maana unaona sasa tumeanza satellite zinaanza mji wa Kigamboni ule unawekewa mamlaka yake sasa ili uweze kujengwa pale kuondoa haya matatizo tusije tukasema kwamba tumeshavurugika ili tuweze kuondokana na tatizo hili. MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana hivi karibuni Serikali ilitangaza kwamba watapandisha baadhi ya barabara katika mkoa wa Dar es Salaam ili barabara hizi zitoke katika mamlaka ya Manispaa kwenda Serikali kuu. Je, Wizara itakuwa tayari kutupatia majina ya hizo barabara ambazo zimepandishwa hadhi? 6 SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, ooh! Mheshimiwa Naibu Waziri mwingine wa ujenzi. NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, suala la kupandisha barabara ambazo Mheshimiwa Mbunge anazungumzia tutatoa taarifa katika kipindi kijacho. MHE. JAMES F. MBATIA: Nashukuru ili niweze kuuliza swali moja dogo la nyongeza. Kwa kuwa msongamano mkubwa ulioko katika Jiji la Dar es Salaam unasababishwa kwa kiasi kikubwa na miundombinu ambayo ni ya hafifu hasa ya barabara. Kwa kuwa hili ni janga, je, Serikali haioni kuna umuhimu wa kutumia chombo kama jeshi letu la wananchi wa Tanzania ili waweze kufanya kwa haraka sana tuweze kutumia reli itokayo Ubungo mpaka katikati ya Jiji? Pamoja na kutumia reli kutoka Pugu mpaka katikati ya Jiji hasa wakati wa peak hours na pia kutumia usafiri wa majini kutoka Bagamoyo mpaka katikati ya Jiji la Dar es Salaam kwa kuweka gats na jeshi uwezo huo linalo na likawa ni jambo la haraka? SPIKA: Haya Waziri wa Ujenzi kaingia sijui alisikia swali hilo kama hakusikia… WAZIRI WA UJENZI: Arudie kidogo swali Mheshimiwa Spika. SPIKA: Ni kutumia usafiri wa reli katikati mji pale, siku moja si nilikusikia unasema. WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbatia kama ifuatavyo. Kwanza ni kweli kabisa kwamba Serikali ina mipango mingi ya 7 kuhakikisha kwamba inapunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam. Katika hatua mbalimbali ambazo zimeanza zimechukuliwa ambazo bahari nzuri amezieleza Naibu Waziri wa TAMISEMI na Naibu Waziri wa Ujenzi ni pamoja na kuanza ujenzi wa barabara nyingi tu katika jiji la Dar es Salaam. Kwa taarifa tu ya Bunge hili kwa sasa hivi kuna mradi wa zaidi wa shilingi bilioni 300 unahusisha ujenzi wa barabara ya kutoka Kimara kwenda Kivukoni, kutoka Fire kwenda Kariakoo, kutoka Magomeni, kwenda Morocco, na katika upana wa barabara ambao unapanuliwa pale, kuna sehemu nyingine kwa mfano kama ile ya fire itakuwa na njia nane, na sehemu zingine zitakuwa na sehemu sita. (Makofi) Lakini pia kuna upanuzi wa barabara
Recommended publications
  • 1458125471-Hs-6-8-20
    [Show full text]
  • TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who Will Benefit from the Gas Economy, If It Happens?
    TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who will benefit from the gas economy, if it happens? TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who will benefit from the gas economy, if it happens? TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013 Who will benefit from the gas economy, if it happens? Supported by: 2 TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who will benefit from the gas economy, if it happens? ACKNOWLEDGEMENTS Policy Forum would like to thank the Foundation for Civil Society for the generous grant that financed Tanzania Governance Review 2013. The review was drafted by Tanzania Development Research Group and edited by Policy Forum. The cartoons were drawn by Adam Lutta (Adamu). Tanzania Governance Reviews for 2006-7, 2008-9, 2010-11, 2012 and 2013 can be downloaded from the Policy Forum website. The views expressed and conclusions drawn on the basis of data and analysis presented in this review do not necessarily reflect those of Policy Forum. TGRs review published and unpublished materials from official sources, civil society and academia, and from the media. Policy Forum has made every effort to verify the accuracy of the information contained in TGR2013, particularly with media sources. However, Policy Forum cannot guarantee the accuracy of all reported claims, statements, and statistics. Whereas any part of this review can be reproduced provided it is duly sourced, Policy Forum cannot accept responsibility for the consequences of its use for other purposes or in other contexts. ISBN:978-9987-708-19-2 For more information and to order copies of the report please contact: Policy Forum P.O. Box 38486 Dar es Salaam Tel +255 22 2780200 Website: www.policyforum.or.tz Email: [email protected] Suggested citation: Policy Forum 2015.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________________ MKUTANO WA KUMI Kikao cha Saba – Tarehe 6 Februari, 2008 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita Katibu kwa orodha ya shughuli za leo, ninapenda kwanza nimpongeze Corporal Fauster. Napenda niwafahamisheni, ni mara ya kwanza katika historia ya Bunge letu Spika kutanguliwa na Sergeant-At-Arms ambaye ni mwanamke. Tulikwishasema awali Bunge hili litaendeshwa kwa viwango na viwango ni pamoja na kuzingatia jinsia. Hakuna kazi ambazo ni za wanaume tu peke yao. Ahsante sana Corporal Fauster. (Makofi) Waheshimiwa Wabunge, nimerejea, nimesitisha safari ya Marekani. Nalazimika kutoa maelezo kwa sababu ya maneno mengi tu. Safari ile kwenda kule ilipangwa kwa kuzingatia mambo mawili :- Moja, ni umuhimu tu wake. Wenzetu Amerika, wiki ya pili ya Mwezi Februari kila mwaka mihimili yote mitatu ya Dola wanakaa pamoja kwa mlo wa asubuhi, inaitwa National Prayer Breakfast. Pamoja na mambo mengi yatakayofanyika, Rais wao ataongea pale kwenye Prayers Breakfast. Lakini wanawatambua baadhi ya viongozi mashuhuri ambao wana ushirikiano mwema nao. Mimi kama Spika wa Bunge hili, nilialikwa kwa msingi huo. Kwa hiyo, hoja kwamba labda ningeweza kumtuma mtu mwingine, haipo kwa sababu ni mwaliko wa heshima kwa jina. (Makofi) La pili ni kwamba, nikitazama ratiba na Kanuni ya 24 ya Bunge, ilikuwa ni kwamba Miswada inaendelea na kwa hiyo, nilidhani mambo mengine kama vile taarifa za Kamati yangekuja kama ilivyo kawaida katika wiki ya mwisho, na mimi nilikuwa narudi Ijumaa asubuhi. Kwa hiyo, yote yangewezekana. Sasa hilo lilishindikana, niliwaarifu wenyeji wetu kule Marekani na wamesikitika, lakini wamesema kama wanasiasa, wameelewa,kwa sababu niliwaeleza mazingira ambayo yalinifanya nisiende.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge Mkutano Wa Kumi Na Nane
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Tatu - Tarehe 28 Januari, 2010 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Muuliza swali wa kwanza ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani. MHE. HAMAD RASHID MOHAMED : Mheshimiwa Spika, ahsante. Mheshimiwa Waziri Mkuu nafikiri unakumbuka tarehe 5 Novemba, 2009 Dr. Aman Abeid Karume na Maalim Seif Sharif Hamad, walikutana na hatimaye chama cha CUF kikamtambua na kuitambua Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Ni nini position ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania juu ya maridhiano haya? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, wako watu watatu au wanne wakisimama najua ni yaleyale tu. (Kicheko) Mheshimiwa Spika, sina hakika kama nitakuwa na jibu zuri sana, lakini niseme kwamba tunao mfumo mzuri sana wa namna ya kufanya maamuzi makubwa kama haya. Sasa ni kweli jambo hili limetokea pale Zanzibar lakini mimi imani yangu ni kwamba katika kutekeleza ule mfumo wa namna ya kufanya maamuzi yafikie ukomo wake naamini ndani ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na kwa kutumia Kamati maalumu ya Chama cha Mapinduzi ndani ya Zanzibar bila shaka jambo hili litakuwa tayari limeshazungumzwa, ndiyo imani yangu mimi. (Makofi) Naamini vilevile kwamba baada ya hapo hatua itakayofuata ni kulileta jambo hili sasa formally kwenye Chama cha Mapinduzi kupitia Kamati Kuu pamoja na Halmashauri Kuu ya Taifa. Kwa hiyo, kama ni jibu sahihi juu ya nini mtazamo wa Serikali itakuwa ni baada ya chama kuwa kimefanya maamuzi na kuielekeza Serikali ifanye nini katika jambo hili.
    [Show full text]
  • Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania Mkutano Wa Kumi Na Mbili Yatokanayo Na Kikao Cha Kwanza 4 Septemba, 2018
    JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA KUMI NA MBILI YATOKANAYO NA KIKAO CHA KWANZA 4 SEPTEMBA, 2018 MKUTANO WA KUMI NA MBILI KIKAO CHA KWANZA – TAREHE 4 SEPTEMBA, 2018 I. WIMBO WA TAIFA: Saa 3:00 asubuhi Wimbo wa Taifa uliimbwa, Dua kusomwa na Mhe. Job Y. Ndugai ambaye aliongoza Kikao. MAKATIBU MEZANI: 1. Ndg. Stephen Kagaigai 2. Ndg. Ramadhan Abdallah 3. Ndg. Joshua Chamwela 4. Ndg. Pamella Pallangayo II. KIAPO CHA UAMINIFU: Mhe. Eng. Christopher Kajoro Chizza Mbunge wa Jimbo la Buyungu aliapa kiapo cha uaminifu. III. TAARIFA YA SPIKA: Mhe. Spika alitoa Taarifa zifuatazo:- (a) Taarifa ya Kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini Marehemu Stephen Ngonyani aliyefariki tarehe 2 Juni, 2018; (b) Taarifa ya Miswada miwili ya Sheria iliyopata kibali cha Rais kuwa Sheria za nchi kama zifuatazo:- (i) Sheria ya kuidhinisha Matumizi ya Serikali Namba 3 ya Mwaka 2018; na (ii) Sheria ya Fedha Namba 4 ya Mwaka 2018. 1 IV. HATI ZA KUWASILISHA MEZANI: Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) aliwasilisha Mezani Maelezo kuhusu Muswada wa Sheria ya Kulitangaza Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi wa Mwaka 2018 [The Dodoma Capital City (Declaration) Bill, 2018]. Mhe. George Malima Lubeleje aliwasilisha Mezani Maoni ya Kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Muswada wa Sheria ya Kulitangaza Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi wa Mwaka 2018 [The Dodoma Capital City (Declaration) Bill, 2018]. Mhe. Sophia Hebron Mwakagenda aliwasilisha Mezani Maoni ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani juu ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI) kuhusu Muswada wa Sheria ya Kulitangaza Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi wa Mwaka 2018 [The Dodoma Capital City (Declaration) Bill, 2018].
    [Show full text]
  • Issued by the Britain-Tanzania Society No 105 May - Aug 2013
    Tanzanian Affairs Text 1 Issued by the Britain-Tanzania Society No 105 May - Aug 2013 Even More Gas Discovered Exam Results Bombshell Rising Religious Tensions The Maasai & the Foreign Hunters Volunteering Changed my Life EVEN MORE GAS DISCOVERED Roger Nellist, the latest volunteer to join our panel of contributors reports as follows on an announcement by Statoil of their third big gas discovery offshore Tanzania: On 18 March 2013 Statoil and its co-venturer ExxonMobil gave details of their third high-impact gas discovery in licence Block 2 in a year. The new discovery (known as Tangawizi-1) is located 10 kilometres from their first two discoveries (Lavani and Zafarani) made in 2012, and is located in water depth of 2,300 metres. The consortium will drill further wells later this year. The Tangawizi-1 discovery brings the estimated total volume of natural gas in-place in Block 2 to between 15 and 17 trillion cubic feet (Tcf). Depending on reservoir characteristics and field development plans, this could result in recoverable gas volumes in the range of 10-13 Tcf from just this one Block. These are large reserves by international stand- ards. By comparison, Tanzania’s first gas field at Songo Songo island has volumes of about 1 Tcf. Statoil has been in Tanzania since 2007 and has an office in Dar es Salaam. It operates the licence on Block 2 on behalf of the Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) and has a 65% working interest, with ExxonMobil Exploration and Production Tanzania Limited holding the remaining 35%. It is understood that under the Production Sharing Agreement that governs the operations, TPDC has the right to a 10% working participation interest in case of a development phase.
    [Show full text]
  • Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1
    Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Pili – Tarehe 13 Mei, 2015 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu! MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa, maswali tunaanza na ofisi ya Waziri Mkuu, anayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Josephine J. Genzabuke, kwa niaba yake Mheshimiwa Likokola! Na. 11 Fedha za Mfuko wa JK kwa Wajasiriamali Wadogo MHE. DEVOTHA M. LIKOKOLA (K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE) aliuliza:- Mfuko wa Wajasiriamali wadogowadogo maarufu kama mabilioni ya JK uliwavuta wengi sana lakini masharti ya kupata fedha hizo yamekuwa magumu:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kufanya mpango huo uwe endelevu kwa lengo la kuwanufaisha wanyonge? (b) Je, ni wananchi wangapi wa Mkoa wa Kigoma wamenufaika na mpango huo? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007, Serikali ilianzisha mpango wa uwezeshaji wananchi kiuchumi na kuongeza ajira kwa kutoa mikopo yenye masharti nafuu. Lengo la mpango huu ni kuwawezesha wananchi mijini na vijijini kupata mikopo ya kuanzisha au kuendeleza shughuli za kiuchumi ili kuongeza ajira na kipato. Masharti ya kupata mikopo hii si magumu sana ikilingalishwa na ile inayotolewa na mabenki, kwa sababu riba inayotozwa kwa mikopo hii ni asilimia 10, ikilinganishwa na riba inayotozwa na mabenki mengine, ambayo ni zaidi ya asilimia 20.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Mbili - Tarehe 22 Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kwa masikitiko makubwa natoa taarifa kwamba Mheshimiwa Mussa Hamisi Silima, Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar, jana Jumapili, tarehe 21 Agosti, 2011 majira ya jioni kama saa mbili kasorobo hivi walipokuwa wakirejea kutoka Dar es Salaam, yeye na familia yake walipata ajali mbaya sana katika eneo la Nzuguni, Mjini Dodoma. Katika ajali hiyo, mke wa Mbunge huyo aitwaye Mwanaheri Twalib amefariki dunia na mwili wa Marehemu upo hospitali ya Mkoa hapa Dodoma ukiandaliwa kupelekwa Zanzibar leo hii Jumatatu, tarehe 22 August, 2011 kwa mazishi yatanayotarajiwa kufanyanyika alasili ya leo. Kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Wabunge tusimame dakika chache tumkumbuke. (Heshima ya Marehemu, dakika moja) (Hapa Waheshimiwa Wabunge walisimama kwa dakika moja) Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, amina. Ahsanteni sana, tukae. Kwa hiyo sasa hivi tunavyoongea Mheshimiwa Mbunge ambae nae pia ameumia vibaya na dereva wake wanaondoka na ndege sasa hivi kusudi waweze kupata yanayohusika kule Dar es Salaam na pia kule watakuwa na watu wa kuwaangalia zaidi. Lakini walikwenda Zanzibar kumzika kaka yake na Marehemu huyu mama. Kwa hiyo, wamemzika marehemu basi wakawa wanawahi Bunge la leo ndiyo jana usiku wamepata ajali. Kwa hiyo, watakaokwenda kusindikiza msiba, ndege itaondoka kama saa tano watakwenda wafuatao, watakwenda Wabunge nane pamoja na mfawidhi zanzibar yeye anaongozana na mgonjwa sasa hivi lakini ataungana na wale kwenye mazishi.
    [Show full text]
  • Is Tanzania a Success Story? a Long Term Analysis
    NBER WORKING PAPER SERIES IS TANZANIA A SUCCESS STORY? A LONG TERM ANALYSIS Sebastian Edwards Working Paper 17764 http://www.nber.org/papers/w17764 NATIONAL BUREAU OF ECONOMIC RESEARCH 1050 Massachusetts Avenue Cambridge, MA 02138 January 2012 Many people helped me with this work. In Dar es Salaam I was fortunate to discuss a number of issues pertaining to the Tanzanian economy with Professor Samuel Wangwe, Professor Haidari Amani, Dr. Kipokola, Dr. Hans Hoogeveen, Mr. Rugumyamheto, Professor Joseph Semboja, Dr. Idris Rashid, Professor Mukandala, and Dr. Brian Cooksey. I am grateful to Professor Benno Ndulu for his hospitality and many good discussions. I thank David N. Weil for his useful and very detailed comments on an earlier (and much longer) version of the paper. Gerry Helleiner was kind enough as to share with me a chapter of his memoirs. I thank Jim McIntire and Paolo Zacchia from the World Bank, and Roger Nord and Chris Papagiorgiou from the International Monetary Fund for sharing their views with me. I thank Mike Lofchie for many illuminating conversations, throughout the years, on the evolution of Tanzania’s political and economic systems. I am grateful to Steve O’Connell for discussing with me his work on Tanzania, and to Anders Aslund for helping me understand the Nordic countries’ position on development assistance in Africa. Comments by the participants at the National Bureau of Economic Research “Africa Conference,” held in Zanzibar in August 2011, were particularly helpful. I am grateful to Kathie Krumm for introducing me, many years ago, to the development challenges faced by the East African countries, and for persuading me to spend some time working in Tanzania in 1992.
    [Show full text]
  • Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania
    JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA KUMI NA SABA 4 MEI, 2017 MKUTANO WA SABA KIKAO CHA KUMI NA SABA TAREHE 4 MEI, 2017 I. DUA: Dua saa 3:00 asubuhi Mhe. Andrew John Chenge, Mwenyekiti alisoma na kuongoza Bunge. Makatibu mezani: 1. Ndugu Ramadhani Issa 2. Ndugu Neema Msangi 3. Ndugu Joshua Chamwela II. HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Mhe. Anastazia Wambura aliwasilisha Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018. III. MASWALI OFISI YA WAZIRI MKUU Swali Na. 140: Mhe. Khatib Said Haji Nyongeza: Mhe. Khatib Said Haji Mhe. Boniface Mwita Getere Mhe. Dkt. Suleiman Ali Yussuf Mhe. Ally Mohamed Keissy OFISI YA RAIS (TAMISEMI) Swali Na. 141: Mhe. Joram Ismael Hongoli Nyongeza: Mhe. Joram Ismael Hongoli Mhe. Masoud Abdallah Salim 1 Mhe. Edward Franz Mwalongo Mhe. James Francis Mbatia Mhe. Kangi Alphaxard Lugola Swali Na. 142: Mhe. Kemilembe Julius Lwota Nyongeza: Mhe. Kemilembe Julius Lwota Mhe. Yahaya Omary Massare Mhe. Sikudhani Yassini Chikambo Mhe. Dkt. Raphael Masunga Chegeni Mhe. Felister Aloyce Bura Mhe. Ryoba Chacha Marwa Swali Na. 143: Mhe. Ally Seif Ungando Nyongeza: Mhe. Ally Seif Ungando Mhe. Shaaban Omari Shekilinde Mhe. Dkt. Prudenciana Wilfred Kikwembe Mhe. Peter Ambrose Lijualikali Mhe. Dkt. Dalaly Peter Kafumu Mhe. Frank George Mwakajoka WIZARA YA NISHATI NA MADINI Swali Na. 144: Mhe. Grace Victor Tendega Nyongeza: Mhe. Grace Victor Tendega Mhe. Stanslaus Haroon Nyongo Mhe. Cecil David Mwambe Mhe. George Malima Lubeleje Mhe. Martha Moses Mlata IV. MATANGAZO: 1.
    [Show full text]
  • 13 DESEMBA, 2013 MREMA 1.Pmd
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA NNE Kikao cha Tisa – Tarehe 13 Desemba, 2013 (Mkutano ulianza saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Mussa Zungu Azzan) Alisoma HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- MHE. JUMA SURURU JUMA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA BUNGE YA HUDUMA ZA JAMII): Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii Kuhusu Utekelezaji wa Shughuli zake kwa Mwaka 2013. MHE. SAID MTANDA (K.n.y. MWENYEKITI KAMATI YA BUNGE NA MAENDELEO YA JAMII): Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii Kuhusu Utekelezaji wa Shughuli zake kwa Mwaka 2013. 1 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) MASWALI NA MAJIBU Na. 92 Hitaji la Gari la Wagonjwa Jimbo la Mwibara. MHE. ALPHAXARD K. N. LUGOLA aliuliza:- Je, ni lini Jimbo la Mwibara litapatiwa gari la kubebea wagonjwa hususan katika Kituo cha Afya cha Kasahunga? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kangi Lugola, Mbunge wa Jimbo la Mwibara, kama ifuatavyo: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna tatizo la kukosekana kwa gari la wagonjwa katika kituo cha Afya cha Kasahunga kilichoko katika Jimbo la Mwibara. Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ina jumla ya vituo 48 vya kutolea huduma za afya ambavyo ni Hospitali 2 vituo vya Afya 6 na Zahanati 40. Hospitali zilizopo ni pamoja na Hospitali ya Bunda DDH na Hospitali ya Mission ya Kibara.
    [Show full text]