21 MEI, 2013 MREMA 1.Pmd
21 MEI, 2013 BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini – Tarehe 21 Mei, 2013 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu tuendelee? HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI (MHE. STEPHEN J. MASELLE): Randama za Makadirio ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. 1 21 MEI, 2013 MASWALI NA MAJIBU Na. 243 Upotevu wa Fedha Kwenye Halmashauri Nchini MHE. RAMADHAN HAJI SALEH aliuliza:- Kumekuwa na upotevu wa fedha nyingi katika Halmashauri nyingi nchini, hali ambayo imesababisha miradi mingi isiweze kutekelezwa. Je, Serikali, imechukua hatua gani dhidi ya Watendaji wanaobainika kuhusika na wizi huo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ramadhan Haji Saleh, Mbunge wa Bumbwini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge, kuwa, kumekuwepo na matuimizi mabaya ya fedha katika baadhi ya Mamlaka za Serikali za Mitaa Nchini. Katika kukabuliana na hali hiyo Serikali, imechukua hatua mbalimbali za kuboresdha mfumo wa udhibiti wa fedha na kuwachukulia hatua watumishi wanaobainika kuhusika na ubadhirifu huo. Mheshimiwa Spika, hatua mbalimbali zimekuwa zikichukuliwa dhidi ya watumishi, zikiwemo kufikishwa katika vyombo vya dola, kuvuliwa madaraka, kushushiwa mishahara na kufukuzwa kazi. Kwa kipindi cha mwaka 2006 mpaka 2012 Wakurugenzi 24 walivuliwa madaraka, Wakurugenzi 24 mchakato wa hatua za nidhamu upo katika hatua mbalimbali, Mkurugenzi mmoja alishushiwa mshahara na Wakurugenzi 8 wamefikishwa Mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.
[Show full text]