Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document) Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _____________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Ishirini na Tisa – Tarehe 21 Julai, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe.Job Y. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Ifuatayo Iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuwatakia Ramadhani Karim Waislamu wote waliojaliwa kuanza Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani Inshallah Mwenyezi Mungu azikubali saumu zetu na azikubali toba zetu. Naomba sasa kuwasilisha Mezani Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa mwaka wa Fedha, 2012/2013. HOJA ZA SERIKALI Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa 2012/2013 Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika (Majadiliano yanaendelea) NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge na mimi nichukue fursa hii kuwatakia kila la heri wale wote ambao wanaanza mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani tunawatakia kila la heri kama ambavyo tumekwisha ambiana na sisi Bungeni hapa maandalizi yote yamekamilika. Kila siku ambazo tutakuwa tukifanya kazi jioni tutamaliza kwa muda ule ambao Mheshimiwa wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu alitoa hoja jana na tukakubaliana na kutakuwa na futari katika kantini yetu ya Bunge kila siku jioni, sasa uchangiaji unaendelea naomba mchangiaji wetu wa kwanza awe Mheshimiwa Martha Mlata. (Makofi) MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika ninakushukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi niwatakie heri Waislamu wote Tanzania kwa mwezi huu Mtukufu. Pamoja na salamu hizo za heri naomba pia niseme kwamba kuna karatasi ilikuja mezani kwako jana na ninaamini bahasha ile ilikataa kufunguka kwa hiyo naomba niseme kilichokuwemo ni kwamba kwa niaba ya Watanzania wote na wapenzi wote wa Yanga napenda kuipongeza Yanga kwa ushindi mkubwa iliyojipatia jana, baada ya salamu hizo na wewe nikutakie heri pia kwa mchezo wa Simba leo. (Makofi/Kicheko) NAIBU SPIKA: Mheshimiwa leo ni mjadala wa Kilimo, Chakula na Ushirika. (Makofi/Kicheko) MHE . MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya salamu hizo ninaomba sasa niingie kwenye hoja iliyoko mbele yetu sitakuwa nimetenda haki kwa kutoa pole kwa Watanzania wote kwa janga kubwa ambalo limetupata Watanzania wote tuwe na subira tumwombe Mwenyezi Mungu na kuwaombea heri wale wote walionusurika na wale wote waliopatwa na misiba. Lakini pia nitoe pole kwa Mama mzazi wa Yohana ambaye alifariki katika vurugu za kisiasa kwa sababu anatoka kwenye kijiji ninachotoka na ni jirani yangu na ni kijana ambaye alikua mwalimu wa kwaya yangu kwa hiyo, ninaomba nitoe pole hizo. Mheshimiwa Naibu Spika, naomba pia nitoe shukrani za dhati kabisa kwa Serikali na hasa kwa Waziri Mkuu baada ya mimi kuleta hoja ya mgogoro wa zao la alizeti Singida, Serikali iliingilia kati na mgogoro huo sasa umekwisha. Hali sasa hivi ni shwari na wafanya biashara pamoja na wakulima na wote ambao ni wadau wa zao hilo wanaendelea na shughuli zao kama kawaida. Ombi langu ni kwamba tunaomba Serikali iwe makini kuwatendea haki watu ambao wanajitoa kwa dhati kujikwamua kutoka kwenye hali ngumu ya maisha hasa wakulima ninaomba wakulima hawa na wafanyabiashara wote na wadau wote wa zao hili wasipatiwe bughudha, pamoja na kwamba zao hili la alizeti ndilo linaloongoza katika Mkoa wangu wa Singida kwa biashara na kwa kipato lakini bado Serikali haijaweka mikakati mizuri kwa kutoa pembejeo kwa sababu hata mbegu zinazopelekwa kule ambazo zinatumika sasa hivi ni aina mbili. Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ninaamini kuna mbegu zingine kuna kituo cha kuzalisha mbegu Pambaa ambacho ni cha Serikali. Ninaiomba Serikali izidi kupeleka zana za kilimo kule ili waweze kuzalisha mbegu nyingi zaidi za kuweza kutosheleza katika Mkoa wa Singida na hata Mikoa jirani kwa sababu mbegu inayotoka pale Mpambaa ina ubora zaidi kuliko wanayoitumia wananchi wa Mkoa wa Singida. Pamoja na kumaliza mgogoro wa zao la alizeti Singida, bado kuna mgogoro mkubwa sana wa zao la mahindi katika Mkoa wa Singida. Historia ya zao la mahindi katika Mkoa wa Singida mimi nimeikuta ni zao ambalo kwetu sisi ni chakula na Mkoa wa Singida una zone tatu. Kuna zone ambazo zinaweza kulima zao la mahindi, zao la mtama, pamoja na uwele na mazao mengine lakini cha kushangaza Serikali ninaomba ilete majibu hapa ni takwimu zipi, ni wataalamu gani walioenda Mkoani Singida wakapima udongo wa Mkoa wa Singida na kusema kwamba zao la mahindi haliwezi kustawi na kulimwa Mkoani Singida. (Makofi) Kwa hali kama hiyo wananchi wamekuwa kwenye hali tete wakizuiwa kulima zao la mahindi hata takwimu zinazopatikana kwenye Mkoa wa Singida kwa zao la mahindi iwe pato au iwe takwimu tu kuwa Mkoa umezalisha kiasi gani haziingizwi na wala haziletwi kwenye RCC eti kwa sababu zao lile halitakiwi kulimwa Mkoani Singida. Ninaomba Mheshimiwa Waziri anakapokuja kujibu hoja zetu anieleze ni wataalamu gani. Mheshimiwa Naibu Spika, wataalamu walitumia nini kuona kuwa Mkoa ule haufai kulima zao la mahindi. Ninaomba kama hataleta mimi nitaomba nitoe shilingi ili kuonyesha kuwa wakulima wa zao la mahindi katika Mkoa wa Singida hawaungi Mkono Bajeti hii. Mheshimiwa Naibu Spika, zao la mahindi lililetewa pembejeo lakini pembejeo zile zikakataliwa eti kwa sababu zao hilo halitakiwi kulimwa Mkoani Singida. Ni kweli kuwa Mkoa wa Singida kuna maeneo ambayo yanastawisha mtama, uwele, ufuta na mazao mengine. Hivi mtu anapojitoa kulima ni Serikali gani ambayo inamzuia mtu na kukataa takwimu ambazo ni wazi kabisa na ni sahihi kabisa na ni sahihi kabisa zao lile hata mwaka huu vijana wengi na wakulima wengi wametoka kwenye umasikini kutokana na zao la mahindi. Ni zao la pili katika Mkoa wa Singida kwa biashara leo hii wakulima wanapigwa stop na Serikali. Mimi ninaishangaa sana Serikali ninaomba Waziri utakapoleta majibu yako ulete majibu fasaha na uniambie takwimu zake zikoje, pato lake likoje kwa sababu mimi binafsi nimeshindwa kupata takwimu ya zao hili kutokana na kwamba hata wataalamu wanaogopa kutoa takwimu na kuzungumzia zao hili kwa sababu watapata demotion kwa kuzungumzia na kusimamia zao hili. Ninaomba sana Serikali ije Mkoa wa Singida itusaidie kutatua mgogoro huu. Katika masuala ya umwagiliaji kuna scheme nyingi ambazo zimejengwa Mkoani Singida lakini scheme zile mimi bado mdogo leo ni Mbunge na ni Mbunge kwa kipindi cha mara ya pili ziko palepale tunapitisha Bajeti hapa ooh tutaleta kuna hela zimewekwa hivi hii Bajeti ambayo tunasomewa hapa sasa hivi kwanza mimi nilikuwa nataka kusema hii Bajeti ina ujumbe gani. Waziri amesoma anataka kutueleza nini kwenye hotuba yake hii aliyoitoa, maana mimi sielewi naomba ujumbe kamili juu ya hotuba hii kwamba ujumbe wake ni nini maana hata fedha zilizotengwa humu mimi naona ni kama kiini macho na ndiyo maana hata miradi au schemes zilizoko Mkoa wa Singida hazitekelezeki kwa sababu ya viini macho vilivyomo kwenye Bajeti husika kila mwaka. Mheshimiwa Naibu Spika, hivi inawezekanaje kweli wewe na Mke wako na familia yako mnapanga Bajeti kila mtoto unamwambia lete mahitaji yako halafu unamwambia Bajeti inakuwa ni 100,000 halafu unamwambia kuwa mimi nina 20,000 halafu unawaambia kuwa 80,000 nitakwenda kuomba kwa Mlata, nitakwenda kuomba kwa Mheshimiwa Joseph Selasini na mahali pengine, unajuaje kama utapata hizo hela? Hiyo ni Bajeti gani, kwa nini tunaletewa Bajeti ya kusubiri kupewa hela kwa watu mimi ninaomba pale tunapoweka kipaumbele kwenye jambo fulani fedha za kusubiri kupewa tusiziingize kwenye Bajeti tujue moja kwa moja kwamba hela zetu za ndani ndizo zitakazoweza kukomboa jambo letu tuliloliweka kwenye kipaumbele. Mheshimiwa Naibu Spika, mimi kwa kweli hapa niliposimama ninashindwa kuunga mkono hoja hii kwa sababu sina hakika Mwangeza kuna miundombinu ambayo ilishawekwa mpaka ina chakaa inasubiri mvua inyeshe ndiyo yale maji yapite hakuna mabwawa. Ukienda Kata ya Msingi kule vilevile naambiwa Mwanga kutakuwa sijui na mradi wa matone, matone gani kama mlishindwa kuendeleza miradi iliyopangwa miaka mingi hayo matone mtayaletaje mimi kwa kweli ninashindwa kuunga mkono hoja. Hapa juzi nimeuliza kuhusu suala la kilimo cha vitunguu nikaambiwa oh!tutawachimbieni mabwawa hapa hata sioni na kuwezesha watu sijui mashine, sijui kitu gani hazipo sasa mimi nitaungaje mkono hoja wakati watu walishapokea kwa furaha kabisa nilikuwa ninaomba sana Serikali tuwe makini katika kuweka Bajeti kwenye vipaumbele tusitegemee fedha za kuomba. Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia watendaji wetu hebu tutende haki kama fedha zimetolewa basi mtoe fedha ambazo zinakwenda kukidhi ule mradi, tusiwe tuna dokoadokoa halafu tunaacha tunawadanganya wananchi. (Makofi) Wakulima wa Mkoa wa Singida na Mikoa hii kama ya Dodoma Mikoa ambayo ni kame mnakaa mnapiga marufuku kulima mazao eti hayastawi kwenye ukame mnapigaje marufuku badala ya kusaidia zao, badala ya kusaidia wakulima chimbeni mabwawa wekeni miundombinu tuvune maji yanayomwagika kwa wakati mmoja mvua ikienda zake tunabaki na maji yetu badala ya kuwasaidia watu mnaanza kuwapiga marufuku mimi nashindwa kuelewa. (Makofi) Nilikuwa ninaomba pia pembejeo kwenye zao la mtama pamoja na mazao mengine kama uwele mimi naomba tupatiwe pembejeo hizi ili wale watu wanaolima mtama, wanaolima uwele na wao waweze kupata pembejeo. Mimi kwa kweli nitashindwa kabisa kuunga mkono hoja lakini nilikuwa ninaomba pia kuweza kuwawezesha wakulima waweze kupata mikopo. Kuna watu ni masikini wakulima bado wanatumia jembe la mkono, halafu unamwambia eti unazuia njaa, unazuia njaa gani umemwacha mtu analima kwa mkono kwa nini usimpelekee pembejeo za kujikwamua kulima eneo kubwa usidhani
Recommended publications
  • 1458137638-Hs-4-4-20
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE KIKAO CHA NNE – TAREHE 14 JUNI, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 37 Ardhi Iliyotolewa Kujenga Shule ya Msingi Kiraracha MHE. AUGUSTINO L. MREMA aliuliza:- Mzee Pauli Sananga Lekule wa Kijiji cha Kiraracha, Kata ya Marangu, Wilaya ya Moshi Vijijini, alitoa ardhi yake ikatumika kujenga shule ya msingi Kiraracha, Marangu miaka 10 iliyopita akiahidiwa na Serikali kupewa eneo jingine kama fidia lakini mpaka sasa hajapewa eneo jingine kama fidia jambo lililomfanya aione Serikali haikumtendea haki. Je, ni lini Serikali itamlipa haki yake kutokana na makubaliano hayo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Lyatonga Mrema, Mbunge wa Vunjo kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa Ndugu Pauli Sananga Lekule wa Kijiji cha Kiraracha, Kata ya Marangu Magharibi, alitoa ardhi yake kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi Kiraracha, Kata ya Marangu Magharibi kwa ahadi ya kufidiwa eneo lililoko Njia panda. Aidha eneo ambalo Halmashauri ya Wilaya ya Moshi ilitarajia kumfudia Ndugu Lekule lipo katika mgogoro na kesi bado inaendelea Mahakama Kuu. 1 Mheshimiwa Spika, kwa kuwa eneo lililopimwa viwanja na kutarajia mlalamikaji lipo katika mgogoro wa kisheria kati ya Halmashauri na wananchi, Serikali inaendelea kufuatilia mwenendo wa kesi na mara shauri litakapomalizika Mahakamani mhusika atapewa eneo lake. Mheshimiwa Spika, katika jitihada za Serikali kuhakikisha shauri hili haliendelei kuchukua muda mrefu, Halmashauri ya Wilaya ya Moshi imeunda timu kwa ajili ya kufuatilia na kuharakisha shauri hili ili ikiwezekana limalizike nje ya Mahakama ili Ndugu Lekule Sananga aweze kupata haki yake mapema.
    [Show full text]
  • Tarehe 28 Juni, 2017
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Hamsini na Tano – Tarehe 28 Juni, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu. NDG. THEONEST RUHILABAKE – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- MHE. GEORGE M. LUBELEJE (K.n.y. MHE. KAPT. MST. GEORGE H. MKUCHIKA - MWENYEKITI WA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE): Taarifa ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shauri la Kudharau Mamlaka ya Spika linalomhusu Mheshimiwa Joshua Samwel Nassari, Mbunge na Shauri la Kusema Uwongo Bungeni linalomhusu Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza, Mbunge. NAIBU SPIKA: Ahsante sana. Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. THEONEST RUHILABAKE – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali tutaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu. Mheshimiwa Mgeni Jadi Kadika, Mbunge wa Viti Maalum, kwa niaba yake Mheshimiwa Mheshimiwa Mwanne Mchemba. Na. 452 Mradi wa MIVARF MHE. MWANNE I. MCHEMBA (K.n.y. MHE. MGENI JADI KADIKA) aliuliza:- Mradi wa MIVARF ni wa Muungano na Makao Makuu yapo Arusha ambapo kazi yake kuu ni kujenga masoko, miundombinu ya barabara, kuongeza thamani na kupeleka maendeleo vijijini:- Je, ni kwa kiasi gani mradi huu umechangia kuleta maendelezo Zanzibar? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANA NA AJIRA) alijibu: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mgeni Jadi Kadika, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, MIVARF ni programu inayohusika na miundombinu ya masoko, uongezaji thamani ya mazao na huduma za kifedha vijijini.
    [Show full text]
  • Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Tatu – Tarehe 8 Mei, 2014 (Mkutano Ulianza Saa tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job J. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA, UTAWALA BORA NA MAHUSIANO NA UTARATIBU: Randama za Makadirio ya Matumizi ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Utawala Bora na Mahusiano na Uratibu kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MASWALI NA MAJIBU Na. 20 Kuhamisha Soko la Mwika MHE. DKT. AUGUTINE L. MREMA aliuliza:- Soko la Mwika liko barabarani na kuna hatari ya wananchi kugongwa na magari:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutafuta eneo kubwa na kuhamisha soko hilo ili kukwepa athari hizi? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- 1 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Augustino Lyatonga Mrema Mbunge wa Vunjo kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Soko la Mwika liko katika Halmashauri ya Wilaya ya Moshi karibu na barabara. Soko hili lina ukubwa wa ekari 2.5 na idadi ya wafanyabiashara wanaotumia soko hili ni kati ya 1,000 hadi 1,500. Kimsingi kuna ongezeko kubwa la wafanyabiashara kufuatia mahitaji ya walaji ambao wanajumuisha wananchi wa Kata ya Mwika Kaskazini na Mwika Kusini. Kwa kutambua changamoto ya soko hili kuwa karibu na barabara, Halmashauri inaandaa mpango wa kuboresha soko hilo ili liwe la kisasa na kuondoa athari za ajali katika eneo hilo.
    [Show full text]
  • Tarehe 9 Mei, 2019
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 9 Mei, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu. NDG. JOSHUA CHAMWELA – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa mwaka wa fedha 2019/2020. MHE. ASHA MSHIMBA JECHA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa mwaka wa fedha 2018/ 2019 pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) MHE. QAMBALO W. QULWI – NAIBU MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Kuhusu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020. NAIBU SPIKA: Ahsante. Waheshimiwa tunaendelea. Katibu. NDG. JOSHUA CHAMWELA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Maswali, tutaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi sasa aulize swali lake. Na. 196 Serikali Kuzipatia Waganga Zahanati za Jimbo la Manyoni Magharibi MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Wananchi wa Manyoni Magharibi kwa kushirikiana na Serikali kupitia miradi mbalimbali ikiwemo TASAF wamejenga zahanati katika Vijiji vya Gurungu, Sanjaranda, Kitopeni, Ipande, Doroto, Itagata, Kalangali, Makale, Mwamagembe na Kintanula, lakini mpaka sasa zahanati hizi hazina Waganga:- Je, ni lini Serikali itazipatia zahanati hizo Waganga, ili wananchi wapate huduma kufuatana na sera yake? NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, majibu.
    [Show full text]
  • Tarehe 28 Aprili, 2017
    NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Kumi na Nne – Tarehe 28 Aprili, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa, tukae. Katibu. NDG. THEONEST RUHILABAKE - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Tutaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu, Mheshimiwa Ester Michael Mmasi, Mbunge wa Viti Maalum, kwa niaba yake Mheshimiwa Stanslaus Mabula. Na.110 Vigezo vya Kurasimisha Vibali vya Ajira na Kuishi Nchini MHE. STANSLAUS S. MABULA (K.n.y. MHE. ESTER M. MMASI) aliuliza:- Pamoja na juhudi za Serikali katika kulinda ajira za vijana wa Kitanzania, Serikali kupitia Sheria ya Ajira ya Wageni Na. 1 ya mwaka 2015 ilirasimisha vibali vya kuishi na ajira kwa wageni batili wapatao 317 kati ya 779. Je, ni vigezo gani vilivyotumika katika urasimishaji wa vibali hivyo wakati vijana wengi wa Kitanzania hususan 1 NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) wahitimu wa vyuo vikuu wanahangaika katika kupata ajira ili wafurahie faida ya taaluma zao? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANA NA AJIRA) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ester Mmasi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ya Kuratibu Ajira kwa Wageni Nchini Na.1 ya mwaka 2015 ilianza kutumika tangu tarehe 15/9/2015. Sheria hii imeweka utaratibu maalum kwa mtu anayetaka kumuajiri raia wa kigeni kuomba kibali cha ajira kwa Kamishna wa Kazi ambaye ndiye mwenye mamlaka pekee ya utoaji wa vibali vya ajira kwa wageni nchini.
    [Show full text]
  • Tarehe 28 Mei, 2021
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Thelathini na Tisa– Tarehe 28 Mei, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba tukae. Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na Mkutano wetu wa Tatu, leo ni Kikao cha Thelathini na Tisa. Katibu. NDG. BAKARI KISHOMA – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Randama ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa mwaka wa fedha 2021/2022. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Waziri Michezo. Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. BAKARI KISHOMA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Tunaanza na Ofisi ya Rais - TAMISEMI, swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Manyoni Mashariki. Na. 321 Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Manyoni MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni kwa sababu Hospitali iliyopo haikidhi mahitaji kutokana na uchakavu na ongezeko la watu? SPIKA: Majibu ya swali hilo muhimu kwa watu wa Manyoni, Mheshimiwa Naibu Waziri Dkt. Festo Dugange. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Jimbo la Manyoni kama ifuatavyo: Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uwepo wa hospitali 43 kongwe na chakavu za Halmashauri ikiwemo Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni.
    [Show full text]
  • Tarehe 13 Juni, 2017
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Arobaini na Sita – Tarehe 13 Juni, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Yustino Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Tukae. Katibu! NDG. THEONEST RUHILABAKE – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Maswali tunaanza na TAMISEMI, swali la Mheshimiwa Joram Ismael Hongoli, Mbunge wa Lupembe. Mheshimiwa Hongoli! Na. 374 Mahitaji ya Kidato cha Tano – Shule ya Sekondari Lupembe MHE. JORAM I. HONGOLI aliuliza:- Shule ya Sekondari ya Lupembe iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ni ya muda mrefu na tulishaomba na kufanya maandalizi ya kuwa na Kidato cha Tano kwa Mchepuo wa CBG. Je, ni lini Serikali itaanzisha Kidato cha Tano katika Shule hiyo? 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joram Ismael Hongoli, Mbunge wa Lupembe, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Shule ya Sekondari ya Lupembe ni miongoni mwa shule mpya 22 ambazo zimeombewa kibali Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ili iweze kupokea wanafunzi wa kidato cha tano katika mwaka 2017. Hivyo, shule hiyo itaanza kupokea wanafunzi wa kidato cha tano baada ya kupatikana kwa kibali kilichoombwa kufuatia ukaguzi wa miundombinu ya shule iliyofanyika. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa jibu zuri na fupi kabisa. Mheshimiwa Hongoli Mbunge wa Lupembe swali la nyongeza. MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
    [Show full text]
  • 1 Bunge La Tanzania
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Kumi na Tatu – Tarehe 27 Juni, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 121 Chama Tawala Kuzuiwa Kutekeleza Sera Zake MHE. MOHAMED H. MISSANGA aliuliza:- Baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 Chama cha Mapinduzi (CCM) ambacho kilishinda, kilipewa ridhaa ya kuongoza nchi na kutekeleza Ilani yake ya Uchaguzi ambayo inaeleza kuwa wananchi wanayo haki ya kuchangia katika Miradi ya Maendeleo nchini:- (a) Je, Serikali haioni kuwa si haki kwa Vyama vya Upinzani kuwakataza wananchi wasichangie Miradi mbalimbali ya Maendeleo na kwamba hali hiyo inazuia Chama Tawala kutekeleza sera zake? (b) Je, Serikali haioni kuwa hali hiyo inaweza kuchangia wafadhili kusitisha misaada yao kwa kukosekana ushiriki wa wananchi katika miradi hiyo? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed H. Missanga, Mbunge wa Singida Magharibi, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, shughuli za Vyama vya siasa hapa nchini zinatawaliwa na Sheria ya Vyama vya Siasa Na. 5 ya mwaka 1992 na marekebisho yake mbalimbali pamoja na Kanuni za Maadili ya Vyama vya Siasa za mwaka 2007. Hivyo, ni wajibu wa 1 Vyama vyote vya siasa kuzingatia sheria na Kanuni hizo katika kudumisha amani, utulivu na mshikimano uliopo kijamii. Mheshimiwa Spika, baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2010, Chama cha Mapinduzi (CCM) kilishinda na kupata ridhaa ya wananchi kuongoza nchi kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
    [Show full text]
  • 16 Aprili, 2012 1 Bunge La Tanzania
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) 16 APRILI, 2012 BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Tano – Tarehe 16 Aprili, 2012 (Mkutano ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 52 Ahadi ya Rais Kununua Gari la Wagonjwa (Ambulance) - Kituo cha Afya Mlangali MHE. DEO H. FILIKUNJOMBE aliuliza:- Mwaka 2008, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshim iwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, aliahidi kuwapatia wananchi wa Mlangali gari jipya la wagonjwa Ambulance:- 1 16 APRILI, 2012 (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kutekeleza ahadi hiyo? (b) Je, gari hilo linaweza kupatikana leo baada ya Bunge kuahirishwa? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Haule Filikunjombe Mbunge wa Ludewa lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba Mheshimiwa Rais mwaka 2008 aliahidi kutoa gari kwa ajili ya kituo cha afya Mlangali katika Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa. Kwa kuzingatia ahadi ya Mheshimiwa Rais na adha ya usafiri waliyo nayo wananchi wa Mlangali, tarehe 1 Aprili, 2011 Serikali ilipeleka gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha Afya Mlangali kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wanaohitaji rufaa. Gari lililonunuliwa ni Toyota Land Cruiser Hardtop lenye Na. Za usajili SM 9192. Gari hili lilikabidhiwa kituo cha afya Mlangali tangu Septemba, 2011. 2 16 APRILI, 2012 Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii na fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Deo Filikunjombe kwa jitihada kubwa alizofanya kwa wananchi wake wa Ludewa kwa kuamua kununua magari mawili (hiace ) ambapo yanatumika kusafirishia wagonjwa wa rufaa katika Wilaya ya Ludewa.
    [Show full text]
  • UNDP TANZANIA MID-TERM EVALUATION of the LEGISLATIVE SUPPORT PROJECT PHASE II (2017-2021) November 2019
    UNDP TANZANIA MID-TERM EVALUATION OF THE LEGISLATIVE SUPPORT PROJECT PHASE II (2017-2021) November 2019 Disclaimer The Mid-term Evaluation of “UNDP TANZANIA LEGISLATIVE SUPPORT PROJECT PHASE II 2017-2021” has been drafted by Tim Baker and Chris Awinia. The views expressed in this document are those of the authors and do not necessarily represent the views of these institutions. Project Title Legislative Support Project (LSP), Phase II Atlas ID Award 00095419, Project 0009425 Corporate Outcome Citizen expectations for voice, development, the rule of law and accountability are met by stronger systems of democratic governance Corporate Outputs Output 1: Increase the capacity of the National Assembly to effectively scrutinise legislation and its implementation and to monitor government performance in a participatory manner Output 2: More effective parliamentary scrutiny of government budget and expenditure, including monitoring of the Sustainable Development Goals (SDGs) Output 3: Enhance the capacity of the National Assembly to engage citizens and represent their interests in the work of the parliament Output 4: The National Assembly is more effectively engaged in strategic leadership, transparency and external engagement Output 5: Gender is mainstreamed in all functions of the National Assembly Country Tanzania Project Dates Start: 01 January 2017 Planned end: 31 December 2021 Project Budget USD $12,765,600 Funding Source DFID, Royal Danish Embassy, One Fund, Embassy of Ireland, TRAC Implementing party National Assembly Tanzania 2 Table
    [Show full text]
  • MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao Cha Ishirini Na Moja
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Ishirini na Moja – Tarehe 4 Mei, 2020 (Bunge Lilianza Saa Nane Mchana) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu. NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH -KATIBU MEZANI: TAARIFA YA SPIKA Kwa mujibu wa Kanuni ya 33(2) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Mwaka 2016, Waheshimiwa Wabunge kwa masikitiko makubwa Mheshimiwa Spika anapenda kuwajulisha kuwa Bunge letu limepatwa na msiba mwingine mkubwa wa kuondokewa na Mbunge na aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Balozi Dkt. Augustine Philip Mahiga ambaye alifariki alfajiri ya kuamkia siku ya Ijumaa tarehe 1 Mei, 2020 Jijini Dodoma na kuzikwa tarehe 2 Mei, 2020 nyumbani kwake Tusamaganga, Iringa. Waheshimiwa Wabunge, pamoja na mengi mazuri na muhimu aliyoyafanya marehemu Mheshimiwa Balozi Mahiga mwaka 2003 mpaka 2010 akiwa Balozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, alirejesha heshima ya Tanzania hadi kuwa moja ya nchi zilizounda Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na yeye kuwa Mkuu wa Ujumbe wa Tanzania katika Baraza hilo. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Waheshimiwa Wabunge naomba sasa tusimame kwa muda wa dakika moja kama ishara ya kuomboleza kifo cha mwenzetu. (Hapa Wabunge walisimama kwa dakika moja kuomboleza kifo cha Mhe. Balozi Dkt. Augustine Phillip Mahiga) NAIBU SPIKA: Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina. Tukae. Katibu. NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH -KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J.
    [Show full text]
  • Tarehe 3 Mei, 2016
    NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Kumi na Moja – Tarehe 3 Mei, 2016 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tukae, Katibu. NDG. RAMADHANI ISSA ABDALLAH - KATIBU MEZANI: Hati za kuwasilisha Mezani. HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi pamoja na Taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2016/2017. MHE. NDAKI M. MASHIMBA (K.n.y MWENYEKITI WA KAMATI YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI): Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2015/2016 pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2016/2017. 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI (K.n.y MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU KILIMO, MIFUGO NA UVUVI): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2016/2017. NAIBU SPIKA: Tunaendelea, Katibu NDG. RAMADHANI ISSA ABDALLAH - KATIBU MEZANI: Maswali MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe aulize swali lake. Na. 83 Huduma za Afya Katika Wilaya ya Ukerewe MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Wilaya ya Ukerewe inajumuisha visiwa
    [Show full text]