Tarehe 13 Juni, 2017
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
Hotuba Ya Mgeni Rasmi Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) Waziri Mkuu Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Katika Ufunguzi Wa Mkuta
HOTUBA YA MGENI RASMI MHE. KASSIM MAJALIWA MAJALIWA (MB) WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KATIKA UFUNGUZI WA MKUTANO WA MWAKA WA WADAU WA LISHE, SEPTEMBA 10, 2019 Mheshimiwa Jenista Mhagama (Mb), Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu, Mheshimiwa Ummy Mwalimu (Mb), Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mheshimiwa Suleiman Jafo (Mb), Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI. Mheshimiwa Prof. Joyce Ndalichako (Mb), Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango (Mb), Waziri wa Fedha na Mipango. Mheshimiwa Japhet Hasunga (Mb), Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Luhaga Mpina (Mb), Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mheshimiwa Innocent Bashungwa (Mb), Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwezeshaji, Mheshimiwa Prof. Makame Mbarawa (Mb), Waziri wa Maji na Umwagiliaji. Mheshimiwa Doto Biteko (Mb), Waziri wa Madini, Waheshimiwa Manaibu Waziri na Makatibu Wakuu, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Bilinith Mahenge; pamoja na viongozi wengine wa ngazi za Mkoa na Halmashauri mliopo, Waheshimiwa Wabunge na viongozi wa Vyama vya Siasa, Waheshimiwa Mabalozi wanaoziwakilisha nchi mbalimbali, Ndugu Viongozi waandamizi wa Idara, Taasisi, Wakala za Serikali, Wakuu wa Vyuo vya Elimu ya Juu, Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa, Wadau wa Maendeleo na Asasi za Kiraia, 1 Ndugu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania, Ndugu Wageni Waalikwa, Waandishi wa habari na wadau wote wa Lishe, Mabibi na Mabwana. Habari za asubuhi Kwa mara nyingine tena nina furaha kubwa sana kujumuika na wadau wa lishe siku hii ya leo. Hii ni mara yangu ya tatu kuhudhuria mkutano wa mwaka wa wadau wa lishe nchini na hivyo nahisi kuwa mwanafamilia wa wadau waliohamasika katika masuala ya lishe. -
Tarehe 30 Juni, 2017
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Hamsini na Saba – Tarehe 30 Juni, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Tunaendelea na Mkutano wetu wa Saba, leo ni Kikao cha Hamsini na Saba. Katibu! NDG. RAMADHANI ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Tunaanza na Ofisi ya Mheshimiwa Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Swali la kwanza linaulizwa na Mheshimiwa Stanslaus Haroon Nyongo, Mbunge wa Maswa Mashariki. Mheshimiwa Nyongo. Na. 468 Mikopo kwa Walimu Kwa Ajili ya Ujenzi wa Nyumba MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza:- Walimu Wilayani Maswa wana uhaba wa nyumba za kuishi; pamoja na juhudi za wananchi kujenga nyumba za walimu wa shule za msingi na sekondari lakini walimu hao bado wanahitaji kujenga nyumba zao wenyewe za kudumu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Je, ni lini Serikali itaweka utaratibu maalum wa kutoa mikopo kwa walimu hao ili wajenge nyumba zao binafsi? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Haroon Nyongo, Mbunge wa Maswa Mashariki kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ina uhitaji wa nyumba za walimu 1,358. Nyumba zilizopo ni 479 na hivyo upungufu ni nyumba 879. Mheshimiwa Spika, kutokana na upungufu huu Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ina mpango wa kujenga nyumba 16 katika mwaka wa fedha 2017/2018. Aidha, kati ya nyumba hizo, nyumba nane zitajengwa kwa bajeti ya 2017/2018 (CDG) na nyumba nyingine nane zitajengwa kwa kutumia mapato ya ndani y (own source) ya Halmashauri. -
Online Document)
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Sita – Tarehe 4 Februari, 2020 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Najma Murtaza Giga) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa tukae. Katibu tunaendelea Waheshimiwa Wabunge na Mkutano wetu wa Kumi na Nane, kikao cha leo ni kikao cha tano, Katibu NDG. RAMADHANI ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati Zifuatazi Ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Taarifa ya Matoleo ya Gazeti la Serikali pamoja na Nyongeza zake yaliyochapishwa tangu Mkutano wa Bunge uliopita kama ifuatavyo:- (i) Toleo Namba 46 la tarehe 8 Novemba, 2019 (ii) Toleo Namba 47 la tarehe 15 Novemba, 2019 (iii) Toleo Namba 48 la tarehe 22 Novemba, 2019 (iv) Toleo Namba 49 la tarehe 29 Novemba, 2019 (v) Toleo Namba 51 la tarehe 13 Desemba, 2019 (vi) Toleo Namba 52 la tarehe 20 Desemba, 2019 (vii) Toleo Namba 53 la tarehe 27 Desemba, 2019 (viii) Toleo Namba 1 la tarehe 3 Januari, 2020 (ix) Toleo Namba 2 la terehe 10 Januari, 2020 (x) Toleo Namba 3 la tarehe 17 Januari, 2020 (xi) Toleo Namba 4 la terehe 24 Januari, 2020 MHE. JASSON S. RWEIKIZA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za MItaa kuhuus shughuli za Kamati hii kwa Mwaka 2019. MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE KATIBA NA SHERIA: Taarifa ya Kmaati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu shughuli zilizotekelezwa na Kamati hiyo kwa kipindi cha kuanzia Februari, 2019 hadi Januari, 2020. -
1458137638-Hs-4-4-20
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE KIKAO CHA NNE – TAREHE 14 JUNI, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU Na. 37 Ardhi Iliyotolewa Kujenga Shule ya Msingi Kiraracha MHE. AUGUSTINO L. MREMA aliuliza:- Mzee Pauli Sananga Lekule wa Kijiji cha Kiraracha, Kata ya Marangu, Wilaya ya Moshi Vijijini, alitoa ardhi yake ikatumika kujenga shule ya msingi Kiraracha, Marangu miaka 10 iliyopita akiahidiwa na Serikali kupewa eneo jingine kama fidia lakini mpaka sasa hajapewa eneo jingine kama fidia jambo lililomfanya aione Serikali haikumtendea haki. Je, ni lini Serikali itamlipa haki yake kutokana na makubaliano hayo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Lyatonga Mrema, Mbunge wa Vunjo kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa Ndugu Pauli Sananga Lekule wa Kijiji cha Kiraracha, Kata ya Marangu Magharibi, alitoa ardhi yake kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi Kiraracha, Kata ya Marangu Magharibi kwa ahadi ya kufidiwa eneo lililoko Njia panda. Aidha eneo ambalo Halmashauri ya Wilaya ya Moshi ilitarajia kumfudia Ndugu Lekule lipo katika mgogoro na kesi bado inaendelea Mahakama Kuu. 1 Mheshimiwa Spika, kwa kuwa eneo lililopimwa viwanja na kutarajia mlalamikaji lipo katika mgogoro wa kisheria kati ya Halmashauri na wananchi, Serikali inaendelea kufuatilia mwenendo wa kesi na mara shauri litakapomalizika Mahakamani mhusika atapewa eneo lake. Mheshimiwa Spika, katika jitihada za Serikali kuhakikisha shauri hili haliendelei kuchukua muda mrefu, Halmashauri ya Wilaya ya Moshi imeunda timu kwa ajili ya kufuatilia na kuharakisha shauri hili ili ikiwezekana limalizike nje ya Mahakama ili Ndugu Lekule Sananga aweze kupata haki yake mapema. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA TATU Kikao cha Tatu – Tarehe 30 Oktoba, 2008 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge kama kawaida yetu siku ya Alhamisi kazi zetu zinaanza kwa maswali kwa Waziri Mkuu kwa muda wa dakika 30. Kwa hiyo Mheshimiwa Waziri Mkuu mwulizaji wa swali la kwanza leo ni Mheshimiwa Mzee John Samwel Malecela. MHE. JOHN S. MALECELA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kukushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la kwanza. Mheshimiwa Waziri Mkuu hivi sasa kuna tatizo la uandikishaji wa vijiji vipya, vijiji ambavyo zamani vilikuwa kama vitongoji lakini sasa vimekuwa vijiji vingi na vikubwa na pia kuna tatizo la ugawaji wa kata. Sasa mambo yote haya yanashughulikiwa na TAMISEMI. Je, Serikali haingeona uwezekano wa kukasimu madaraka ya uandikishaji wa vijiji yaende kwenye Halmashauri za Wilaya na suala la uandikishaji wa ugawaji wa kata liende kwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, kwa hiyo kuondoa msongamano ambao sasa hivi uko TAMISEMI kiasi kwamba viko vijiji ambavyo vimependekezwa na Halmashauri zaidi ya miaka 10 iliyopita lakini mpaka sasa hakuna kilichofanyika? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimjibu Mheshimiwa Mzee Malecela swali lake zuri sana kama ifuatavyo. Mheshimiwa Naibu Spika, sababu ya kuendeleza utaratibu huu wa kutaka jambo hili liwe linaamuliwa katika ngazi hii ni kwamba kuna masuala ya kifedha ambayo yanaendana sambamba na uanzishwaji wa vijiji, kata na maeneo mengine mapya. Kwa hiyo, kwa msingi huo Serikali bado inaona ni vizuri uamuzi kama huo ukaendelea kubaki 1 mikononi mwetu ili hilo liweze kuwa ni jambo ambalo linatu-guide katika kuamua vijiji vingapi safari hii turuhusu itakuwa na component ya Watendaji na kata ngapi kwa sababu utaongeza mambo mengine ndani ya kata. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA TATU Kikao cha Tano - Tarehe 4 Novemba, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali, tunaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu, atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Gaudence Kayombo, kwa niaba yake naona Mheshimiwa Mwambalaswa unaweza kumwulizia! Na. 53 Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbinga Kuwa Mamlaka Kamili MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA (K.n.y. MHE. GAUDENCE C. KAYOMBO) aliuza:- Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbinga umekamilisha vigezo vyote kuwa Mamlaka kamili ya Mji:- Je, ni lini Serikali itaridhia na kutekeleza ahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Gaudence C. Kayombo, Mbunge wa Mbinga Mashariki, kama ifuatavyo:- 1 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) [WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (TAMISEMI)] Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba, mwaka 2010, Mheshimiwa Rais, aliahidi kupandisha hadhi Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbinga kuwa Halmashauri ya Mji. Ahadi hii ilitokana na ukweli kwamba, Mamlaka hii imeonekana kukua kwa kasi, kwa maana ya ongezeko la watu na shughuli za kiuchumi na kijamii na hivyo Serikali inaona ipo haja ya kuipandisha hadhi ili kuingiza dhana ya Mpango Miji kwa lengo la kuzuia ukuaji holela, kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha huduma za jamii. Mheshimiwa Spika, hata hivyo, mchakato wa kuupandisha hadhi Mji wa Mbinga bado unaendelea na ofisi yangu bado haijapokea maombi kutoka Mkoa wa Ruvuma. -
Tarehe 28 Juni, 2017
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA SABA Kikao cha Hamsini na Tano – Tarehe 28 Juni, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu. NDG. THEONEST RUHILABAKE – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- MHE. GEORGE M. LUBELEJE (K.n.y. MHE. KAPT. MST. GEORGE H. MKUCHIKA - MWENYEKITI WA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE): Taarifa ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shauri la Kudharau Mamlaka ya Spika linalomhusu Mheshimiwa Joshua Samwel Nassari, Mbunge na Shauri la Kusema Uwongo Bungeni linalomhusu Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza, Mbunge. NAIBU SPIKA: Ahsante sana. Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. THEONEST RUHILABAKE – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali tutaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu. Mheshimiwa Mgeni Jadi Kadika, Mbunge wa Viti Maalum, kwa niaba yake Mheshimiwa Mheshimiwa Mwanne Mchemba. Na. 452 Mradi wa MIVARF MHE. MWANNE I. MCHEMBA (K.n.y. MHE. MGENI JADI KADIKA) aliuliza:- Mradi wa MIVARF ni wa Muungano na Makao Makuu yapo Arusha ambapo kazi yake kuu ni kujenga masoko, miundombinu ya barabara, kuongeza thamani na kupeleka maendeleo vijijini:- Je, ni kwa kiasi gani mradi huu umechangia kuleta maendelezo Zanzibar? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANA NA AJIRA) alijibu: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mgeni Jadi Kadika, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, MIVARF ni programu inayohusika na miundombinu ya masoko, uongezaji thamani ya mazao na huduma za kifedha vijijini. -
MKUTANO WA TATU Kikao Cha Arobaini Na Sita –Tarehe 20 J
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Arobaini na Sita –Tarehe 20 Juni, 2016 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tukae. Katibu! NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH- KATIBU MEZANI: Maswali. MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mheshimiwa Victor Kilasile Mwambalaswa Mbunge wa Chunya, sasa aulize swali lake. Na. 389 Tatizo la Ukosefu wa Chumba cha Kuhifadhia Maiti MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Kituo cha Afya Chunya kilipandishwa hadhi kuwa hospitali ya Wilaya mwaka 2008 lakini kuna tatizo la ukosefu wa chumba cha kuhifadhia maiti:- Je, ni lini Serikali italitatua tatizo hilo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Victor Kilasile Mwambalaswa, Mbunge wa Chunya, kama ifuatavyo:- 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tayari imeanza mchakato wa ujenzi wa chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya Wilaya ya Chunya ambacho kinatarajiwa kugharimu shilingi milioni 230 hadi kukamilika. Ujenzi wa jengo utagharimu shilingi milioni 60 na majokofu yatagharimu shilingi milioni 160. Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 zimetengwa shilingi milioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa chumba cha kuhifadhia maiti yaani mortuary. Mheshimiwa Naibu Spika, katika hospitali ya Wilaya ya Chunya kwa sasa kipo chumba maalumu ambacho kimetengwa kikiwa na uwezo wa kuhifadhia maiti mbili tu. Chumba hicho hakitoshelezi huduma hiyo hali ambayo inawalazimu wananchi kufuata huduma ya aina hiyo katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Mbeya. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Ishirini na Saba - Tarehe 9 Julai, 2010 (Mkutano ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anna S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZlLIZOWASILISHWA MEZANI: Hati Zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha, 2010/2011. MHE. WILLIAM H. SHELLUKINDO - MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya ya Nishati na Madini Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. MHE.SAVELINA S. MWIJAGE (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMATI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA NISHATI NA MADINI): Taarifa ya Msemaji wa Mkuu wa Kambi ya Upinzani Kuhusu Makadiro ya Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI (MHE. MWANTUMU BAKARI MAHIZA): 1 Randama za Makadiro ya Matumizi ya Wizara ya Elimu na Mfunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI (MHE. OMAR YUSSUF MZEE): Taarifa ya Majumuisho ya Mpango Mkakati wa Kujibu Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu za Wizara, Idara za Serikali na Mikoa kwa Mwaka wa Fedha 2008/2009. MASWALI NA MAJIBU Na. 191 Kuhusu Barabara ya Makutupa Bumila Jimbo la Mpwapwa MHE. GEOREGE M. -
MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA TATU Kikao Cha
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Arobaini na Tatu – Tarehe 3 Juni, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba tukae. Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na Mkutano wetu wa Tatu, leo ni Kikao cha Arobaini na Tatu. Katibu NDG. NENELWA MWIHAMBI, ndc – KATIBU WA BUNGE: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, aah sasa hivi unavaa sketi ndefu, hataki ugomvi na Mgogo. (Kicheko) Tunaendelea, Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. NENELWA MWIHAMBI, ndc – KATIBU WA BUNGE: MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Maswali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Waziri Mkuu karibu sana. (Makofi) Waheshimiwa Wabunge, nawakumbusha tena kuhusu maswali ya kisera sio matukio, sio nini, ni ya kisera. Tunaanza na Mheshimiwa Mbunge wa Liwale, Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka, maswali kwa kifupi. MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kwanza kuuliza swali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu. Mheshimiwa Spika, swali langu litahusu sekta ya korosho. Mwaka huu tumepata taarifa kwamba Serikali ilijipanga kutupatia pembejeo wakulima wa zao la korosho kwa maana kwamba waje kuzilipa baadaye kwenye mjengeko wa bei. Hata hivyo, kuna taharuki kubwa kwa wakulima wetu wa korosho baada ya Bodi ya Korosho kuleta waraka kwenye Halmashauri zetu, wakiwaambia kila mkulima akipeleka zao lile kwenye mnada kila kilo moja itakatwa shilingi 110 bila kujali kwamba mkulima yule amechukua pembejeo kwa kiwango gani. -
Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Tatu – Tarehe 8 Mei, 2014 (Mkutano Ulianza Saa tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job J. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA, UTAWALA BORA NA MAHUSIANO NA UTARATIBU: Randama za Makadirio ya Matumizi ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Utawala Bora na Mahusiano na Uratibu kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MASWALI NA MAJIBU Na. 20 Kuhamisha Soko la Mwika MHE. DKT. AUGUTINE L. MREMA aliuliza:- Soko la Mwika liko barabarani na kuna hatari ya wananchi kugongwa na magari:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutafuta eneo kubwa na kuhamisha soko hilo ili kukwepa athari hizi? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- 1 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Augustino Lyatonga Mrema Mbunge wa Vunjo kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Soko la Mwika liko katika Halmashauri ya Wilaya ya Moshi karibu na barabara. Soko hili lina ukubwa wa ekari 2.5 na idadi ya wafanyabiashara wanaotumia soko hili ni kati ya 1,000 hadi 1,500. Kimsingi kuna ongezeko kubwa la wafanyabiashara kufuatia mahitaji ya walaji ambao wanajumuisha wananchi wa Kata ya Mwika Kaskazini na Mwika Kusini. Kwa kutambua changamoto ya soko hili kuwa karibu na barabara, Halmashauri inaandaa mpango wa kuboresha soko hilo ili liwe la kisasa na kuondoa athari za ajali katika eneo hilo.