MKUTANO WA KUMI NA SABA Kikao Cha Pili – Tarehe 6 Novemba, 2
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA SABA Kikao cha Pili – Tarehe 6 Novemba, 2019 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu. NDG. ASIA MINJA – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Taarifa ya Hali ya Dawa za Kulevya ya mwaka 2018. NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo kwa Kipindi cha mwaka 2016/2017 hadi robo ya kwanza 2019/ 2020. NAIBU SPIKA: Ahsante. Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. ASIA MINJA – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Tutaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mashimba Ndaki sasa aulize swali kwa niaba ya Mheshimiwa Makame Mashaka Foum. Na. 14 Sheria Na.9 ya 2010 ya Watu Wenye Ulemavu MHE. MASHIMBA M. NDAKI (K.n.y. MHE. MAKAME MASHAKA FOUM) aliuliza:- Sheria Na.9 ya mwaka 2010 ya Watu wenye Ulemavu imeainisha haki za msingi za Watu wenye Ulemavu ikiwa ni pamoja na haki ya ukalimani katika maeneo ya utoaji huduma kama vile hospitali, taarifa ya habari, shuleni nk:- Je, Serikali inachukua hatua gani ili kuharakisha utekelezaji wa sheria hii? NAIBU SPIKA: Majibu, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu. NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WATU WENYE WALEMAVU (MHE. STELLA IKUPA ALEX) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Makame Mashaka Foum, Mbunge wa Kijini, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ya Watu wenye Ulemavu Na.9 ya mwaka 2010, imeweka misingi ya upatikanaji wa haki kwa watu wenye ulemavu ikiwepo haki ya upatikanaji wa habari kwa kundi la viziwi kupitia wakalimani katika sehemu mbalimbali ikiwemo hospitali, shuleni pamoja na vyombo vya habari yaani luninga.
[Show full text]