Majadiliano Ya Bunge
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
And National Economy
NORDIC WEEK UNITED REPUBLIC OF TANZANIA VICE PRESIDENT’S OFFICE ENVIRONMENT WEEK HIGH LEVEL SYMPOSIUM ON CLIMATE CHANGE, ENVIRONMENT AND NATIONAL ECONOMY 1 June, 2018 H.E. The Vice President of the Republic of Tanzania, Hon. Samia Suluhu Hassan planting a tree in a natural forest reserve established by the late Father of the Nation Mwl. Julius Kambarage Nyerere. This tree planting ceremony happened during the climax of the World Environment Day nationally commemortated in Butiama, 2017. HIGH LEVEL SYMPOSIUM ON CLIMATE CHANGE, ENVIRONMENT AND NATIONAL ECONOMY STATEMENT OF THE MINISTER OF STATE, UNION AFFAIRS AND ENVIRONMENT On 5th of June 2018, Tanzania will join other countries in the world to mark the World Environment Day (WED). This day was officiated in the first United Nations meeting on environment in Sweden in 1972, where a resolution was passed to mark it as World Environment Day to be globally celebrated each year. This year, the celebrations are being observed at the international level in New Delhi, India guided by the global theme “Beat Plastic Pollution”. The theme aims at promoting initiatives to discourage environmental degradation and pollution caused by plastic waste and plastic by-products. At the National Level, we mark WED in Dar es Salaam where city residents and all Tanzanian will have the opportunity to be informed and sensitized on how to combat the environmental challenges that impact Dar es Salaam and the country in general resulting into catastrophes particularly floods; pollution; coastline erosion along the Indian ocean coast and destruction of marine environment; and forest degradation due to the ever increasing consumption of charcoal particularly by residents in urban centres. -
Online Document)
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Sita – Tarehe 4 Februari, 2020 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Najma Murtaza Giga) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa tukae. Katibu tunaendelea Waheshimiwa Wabunge na Mkutano wetu wa Kumi na Nane, kikao cha leo ni kikao cha tano, Katibu NDG. RAMADHANI ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati Zifuatazi Ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Taarifa ya Matoleo ya Gazeti la Serikali pamoja na Nyongeza zake yaliyochapishwa tangu Mkutano wa Bunge uliopita kama ifuatavyo:- (i) Toleo Namba 46 la tarehe 8 Novemba, 2019 (ii) Toleo Namba 47 la tarehe 15 Novemba, 2019 (iii) Toleo Namba 48 la tarehe 22 Novemba, 2019 (iv) Toleo Namba 49 la tarehe 29 Novemba, 2019 (v) Toleo Namba 51 la tarehe 13 Desemba, 2019 (vi) Toleo Namba 52 la tarehe 20 Desemba, 2019 (vii) Toleo Namba 53 la tarehe 27 Desemba, 2019 (viii) Toleo Namba 1 la tarehe 3 Januari, 2020 (ix) Toleo Namba 2 la terehe 10 Januari, 2020 (x) Toleo Namba 3 la tarehe 17 Januari, 2020 (xi) Toleo Namba 4 la terehe 24 Januari, 2020 MHE. JASSON S. RWEIKIZA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za MItaa kuhuus shughuli za Kamati hii kwa Mwaka 2019. MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE KATIBA NA SHERIA: Taarifa ya Kmaati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu shughuli zilizotekelezwa na Kamati hiyo kwa kipindi cha kuanzia Februari, 2019 hadi Januari, 2020. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Kumi na Tatu – Tarehe 10 Februari, 2010 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI (MHE. OMAR YUSSUF MZEE): Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Benki ya Posta Tanzania, kwa Mwaka 2008 [The Annual Report and Accounts of The Tanzania Postal Bank for the Year 2008]. The Mid-Term Review of the Monetary Policy Statement of The Bank of Tanzania for the Year 2009/2010. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini juu ya Taarifa ya Serikali Kuhusu Ubinafsishwaji wa Mgodi wa Kiwira. Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Mchakato wa Zabuni ya Kuzalisha Umeme wa Dharura Ulioipa Ushindi Kampuni ya Richmond Development Company LLC. Houston Texas - Marekani Mwaka 2006. MWENYEKITI WA KAMATI YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Miundombinu Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelzaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Uendeshaji Usioridhisha wa Shirika la Reli Tanzania uliofanywa na Kampuni ya RITES ya India. 1 Taarifa ya Kamati ya Miundombinu Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Utendaji wa Kazi Usioridhisha wa Kampuni ya TICTS. MASWALI NA MAJIBU Na. 145 Usimamizi wa Ukaguzi wa Fedha za Halmashauri MHE. HERBERT J. MNTANGI aliuliza:- Kwa kuwa, kiasi cha fedha kinachopelekwa katika Halmashauri za Wilaya, Manispaa na Jiji ni kikubwa na kinahitaji usimamizi wa ziada:- Kwa kuwa kitengo cha ukaguzi wa ndani kipo chini ya Mkurugenzi Mtendaji. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 2 AGOSTI, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba mzime vipasa sauti vyenu maana naona vinaingiliana. Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaingia hatua inayofuata. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Leo ni siku ya Alhamisi lakini tulishatoa taarifa kwamba Waziri Mkuu yuko safarini kwa hiyo kama kawaida hatutakuwa na kipindi cha maswali hayo. Maswali ya kawaida yapo machache na atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Vita R. M. Kawawa. Na. 310 Fedha za Uendeshaji Shule za Msingi MHE. VITA R. M. KAWAWA aliuliza:- Kumekuwa na makato ya fedha za uendeshaji wa Shule za Msingi - Capitation bila taarifa hali inayofanya Walimu kuwa na hali ngumu ya uendeshaji wa shule hizo. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kuwa, fedha za Capitation zinatoloewa kama ilivyotarajiwa ili kupunguza matatizo wanayopata wazazi wa wanafunzi kwa kuchangia gharama za uendeshaji shule? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) imepanga kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kupata shilingi 10,000 kama fedha za uendeshaji wa shule (Capitation Grant) kwa mwaka. -
(Online Document) 1 BUNGE LA TANZANIA
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _____________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Sita – Tarehe 18 Mei, 2015 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kutokana na maagizo yaliyotolewa humu wiki iliyopita kuhusu Hati za kuwasilisha Mezani. Kama kuna kundi lolote, Kamati, Serikali au Upinzani hawajaleta Hati hazisomwi. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais! Mheshimiwa Naibu Waziri! HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO): Randama za Makadirio ya Matumizi kwa Ofisi ya Makamu wa Rais na Taasisi zake kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma) pamoja na (Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (MAHUSIANO NA URATIBU): Hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. MHE. JASSON S. RWEIKIZA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA: 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), (Utawala Bora na Mahusiano na Uratibu) kwa mwaka wa fedha 2014/2015 pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. MHE. ESTHER N. MATIKO - MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI KWA OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA, UTAWALA BORA NA MAHUSIANO NA URATIBU: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Fedha kwa Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Utawala Bora na Mahusiano na Uratibu kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016 SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tunaanza maswali Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Mheshimiwa Engineer Athumani Mfutakamba. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA TATU Kikao cha Tatu – Tarehe 30 Oktoba, 2008 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge kama kawaida yetu siku ya Alhamisi kazi zetu zinaanza kwa maswali kwa Waziri Mkuu kwa muda wa dakika 30. Kwa hiyo Mheshimiwa Waziri Mkuu mwulizaji wa swali la kwanza leo ni Mheshimiwa Mzee John Samwel Malecela. MHE. JOHN S. MALECELA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kukushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la kwanza. Mheshimiwa Waziri Mkuu hivi sasa kuna tatizo la uandikishaji wa vijiji vipya, vijiji ambavyo zamani vilikuwa kama vitongoji lakini sasa vimekuwa vijiji vingi na vikubwa na pia kuna tatizo la ugawaji wa kata. Sasa mambo yote haya yanashughulikiwa na TAMISEMI. Je, Serikali haingeona uwezekano wa kukasimu madaraka ya uandikishaji wa vijiji yaende kwenye Halmashauri za Wilaya na suala la uandikishaji wa ugawaji wa kata liende kwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, kwa hiyo kuondoa msongamano ambao sasa hivi uko TAMISEMI kiasi kwamba viko vijiji ambavyo vimependekezwa na Halmashauri zaidi ya miaka 10 iliyopita lakini mpaka sasa hakuna kilichofanyika? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimjibu Mheshimiwa Mzee Malecela swali lake zuri sana kama ifuatavyo. Mheshimiwa Naibu Spika, sababu ya kuendeleza utaratibu huu wa kutaka jambo hili liwe linaamuliwa katika ngazi hii ni kwamba kuna masuala ya kifedha ambayo yanaendana sambamba na uanzishwaji wa vijiji, kata na maeneo mengine mapya. Kwa hiyo, kwa msingi huo Serikali bado inaona ni vizuri uamuzi kama huo ukaendelea kubaki 1 mikononi mwetu ili hilo liweze kuwa ni jambo ambalo linatu-guide katika kuamua vijiji vingapi safari hii turuhusu itakuwa na component ya Watendaji na kata ngapi kwa sababu utaongeza mambo mengine ndani ya kata. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA TATU Kikao cha Tano - Tarehe 4 Novemba, 2013 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, maswali, tunaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu, atakayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Gaudence Kayombo, kwa niaba yake naona Mheshimiwa Mwambalaswa unaweza kumwulizia! Na. 53 Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbinga Kuwa Mamlaka Kamili MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA (K.n.y. MHE. GAUDENCE C. KAYOMBO) aliuza:- Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbinga umekamilisha vigezo vyote kuwa Mamlaka kamili ya Mji:- Je, ni lini Serikali itaridhia na kutekeleza ahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Gaudence C. Kayombo, Mbunge wa Mbinga Mashariki, kama ifuatavyo:- 1 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) [WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (TAMISEMI)] Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba, mwaka 2010, Mheshimiwa Rais, aliahidi kupandisha hadhi Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbinga kuwa Halmashauri ya Mji. Ahadi hii ilitokana na ukweli kwamba, Mamlaka hii imeonekana kukua kwa kasi, kwa maana ya ongezeko la watu na shughuli za kiuchumi na kijamii na hivyo Serikali inaona ipo haja ya kuipandisha hadhi ili kuingiza dhana ya Mpango Miji kwa lengo la kuzuia ukuaji holela, kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha huduma za jamii. Mheshimiwa Spika, hata hivyo, mchakato wa kuupandisha hadhi Mji wa Mbinga bado unaendelea na ofisi yangu bado haijapokea maombi kutoka Mkoa wa Ruvuma. -
Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA SITA (DAILY SUMMARY RECORD OF PROCEEDINGS) 11 NOVEMBA, 2014 MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA KIKAO CHA SITA – 11 NOVEMBA, 2014 I. DUA Saa 3.00 Asubuhi kikao kilianza kikiongozwa na Mhe. Naibu Spika (Mhe Job Y. Ndugai) na alisoma Dua. Makatibu Mezani 1. Ramadhani Abdallah Issa 2. Asia Minja 3. Hellen Mbeba II. MASWALI Maswali yafuatayo yaliulizwa na yalijibiwa:- 1. OFISI YA WAZIRI MKUU Swali . 67 – Mhe. Charles J.P. Mwijage Nyongeza (i) Mhe. Charles Mwijage (ii) Mhe. Joshua Nassari Swali. 68- Mhe. Hezekiah Chibulunje (K.n.y – Mhe. David Mallole) Nyongeza (i) Mhe. Hezekiah Chibulunje Swali. 69 – Mhe. Josephat Sinkamba Kandege Nyongeza (i) Mhe. Josephat Kandege 2. OFISI YA RAIS (UTAWALA BORA) Swali. 70 – Mhe. Amina Abdulla Amour 2 Nyongeza (i) Mhe. Amina Abdullah Amour 3. OFISI YA RAIS (MAHUSIANO NA URATIBU) Swali. 71 – Mhe. Leticia Mageni Nyerere Nyongeza i. Mhe. Leticia Nyerere ii. Mhe. Mohammed Habib Mnyaa 4. OFISI YA MAKAMU WA RIAS (MAZINGIRA) Swali. 72 – Mhe. Victor Kilasile Mwambalaswa Nyongeza i. Mhe. Victor Kilasile Mwambalaswa. 5. WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Swali. 73 – Mhe. Diana Mkumbo Chilolo Nyongeza i. Mhe. Diana Mkumbo Chilolo 6. WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA Swali. 74 – Mhe. Sylvestry Francis Koka Nyongeza i. Mhe. Sylvestry Koka ii. Mhe. Salim Masoud 7. WIZARA YA UCHUKUZI Swali. 75 – Mhe. Prof. David Mwakyusa (k.n.y Mhe. Luckson Mwanjale). Nyongeza i. Mhe. Prof. David Mwakyusa. 3 Swali. 76 – Mhe. -
MKUTANO WA TATU Kikao Cha Arobaini Na Sita –Tarehe 20 J
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Arobaini na Sita –Tarehe 20 Juni, 2016 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tukae. Katibu! NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH- KATIBU MEZANI: Maswali. MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mheshimiwa Victor Kilasile Mwambalaswa Mbunge wa Chunya, sasa aulize swali lake. Na. 389 Tatizo la Ukosefu wa Chumba cha Kuhifadhia Maiti MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Kituo cha Afya Chunya kilipandishwa hadhi kuwa hospitali ya Wilaya mwaka 2008 lakini kuna tatizo la ukosefu wa chumba cha kuhifadhia maiti:- Je, ni lini Serikali italitatua tatizo hilo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Victor Kilasile Mwambalaswa, Mbunge wa Chunya, kama ifuatavyo:- 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tayari imeanza mchakato wa ujenzi wa chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya Wilaya ya Chunya ambacho kinatarajiwa kugharimu shilingi milioni 230 hadi kukamilika. Ujenzi wa jengo utagharimu shilingi milioni 60 na majokofu yatagharimu shilingi milioni 160. Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 zimetengwa shilingi milioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa chumba cha kuhifadhia maiti yaani mortuary. Mheshimiwa Naibu Spika, katika hospitali ya Wilaya ya Chunya kwa sasa kipo chumba maalumu ambacho kimetengwa kikiwa na uwezo wa kuhifadhia maiti mbili tu. Chumba hicho hakitoshelezi huduma hiyo hali ambayo inawalazimu wananchi kufuata huduma ya aina hiyo katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Mbeya. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Ishirini na Saba - Tarehe 9 Julai, 2010 (Mkutano ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anna S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZlLIZOWASILISHWA MEZANI: Hati Zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha, 2010/2011. MHE. WILLIAM H. SHELLUKINDO - MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya ya Nishati na Madini Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. MHE.SAVELINA S. MWIJAGE (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMATI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA NISHATI NA MADINI): Taarifa ya Msemaji wa Mkuu wa Kambi ya Upinzani Kuhusu Makadiro ya Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI (MHE. MWANTUMU BAKARI MAHIZA): 1 Randama za Makadiro ya Matumizi ya Wizara ya Elimu na Mfunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2010/2011. NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI (MHE. OMAR YUSSUF MZEE): Taarifa ya Majumuisho ya Mpango Mkakati wa Kujibu Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu za Wizara, Idara za Serikali na Mikoa kwa Mwaka wa Fedha 2008/2009. MASWALI NA MAJIBU Na. 191 Kuhusu Barabara ya Makutupa Bumila Jimbo la Mpwapwa MHE. GEOREGE M. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _____________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Nane – Tarehe 24, Julai, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua SPIKA: Kabla ya kuendelea na shughuli nina matangazo machache tu ya utangulizi. Waziri wa Maendeleo ya Mifugo, Mheshimiwa Shukuru Kawambwa, anao wageni ambao wametoka Jimboni kwake kuhudhuria Kikao cha leo cha Bunge wako kumi na nne (14). Katibu wa CCM Wilaya ya Bagamoyo naomba asimame pale alipo. Katibu wa Vijana, Katibu wa Wazazi, Katibu wa Jumuiya ya Wanawake (UWT) na Madiwani wote wa Jimbo la Uchaguzi la Bagamoyo wakiongozwa na Mheshimiwa Almasi Masukuzi, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, wale pale karibuni sana. Waheshimiwa, tunashukuru sana mmeona ni vema mje muungane nasi kushuhudia shughuli za Bunge letu. (Makofi) Kwa umuhimu huo huo naomba nimtambulishe Mama Kawambwa, mkewe Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na watoto wao watatu, nadhani ni wale pale. Karibuni sana Bungeni.(Makofi) HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO: Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Maendeleo ya Mifugo kwa Mwaka wa Fedha 2006/2007. MHE. JOYCE N. MACHIMU – (k.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KILIMO NA ARDHI): 1 Maoni ya Kamati ya Kilimo na Ardhi Kuhusu Utekelezaji wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo kwa Mwaka wa Fedha Uliopita, Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara Hiyo kwa Mwaka 2006/2007. SPIKA: Ahsante sana. Sasa ni Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu sekta ya kilimo na ardhi.(Makofi) MHE. -
MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NANE Kikao Cha
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Kumi na Tatu – Tarehe 29 Juni, 2007 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii kwa Kuwasilisha Hati. Naomba niwashukuru nyote jinsi tulivyoshirikiana kwa pamoja kuweza kumsindikiza mwenzetu Marehemu Amina Chifupa Mpakanjia, katika safari yake ya mwisho. Waheshimiwa Wabunge, napenda niwashukuru Kamati ya Uongozi na Tume ya Huduma za Bunge, lakini pia TWPG kwa kushirikiana vizuri sana kuweza kumsindikiza mwenzetu kwa heshima; na kipekee naomba Mheshimiwa Waziri Mkuu atutolee salamu za shukrani kwa Mheshimiwa Rais kwa jinsi ambavyo Mheshimiwa Rais alivyokuwa karibu nasi kila dakika kwa mawasiliano hadi hapo jana kule Njombe. Waheshimiwa Wabunge, narejea tena Mungu ailaze roho ya Marehemu Mheshimiwa Amina Chifupa Mpakanjia, mahali pema peponi. Amin. Hati ifuatayo iliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Shirika la Hifadhi ya Taifa (TANAPA) kwa mwaka 2005/2006 (The Annual Report and Accounts of the Tanzania National Parks for the Year 2005/2006). MASWALI NA MAJIBU Na. 106 Ubovu wa Barabara za Jiji la Dar es Salaam MHE. MUSSA A. ZUNGU aliuliza:- 1 Kwa kuwa sura ya nchi yetu iko katika Jimbo la Ilala; na kwa kuwa barabara nyingi za Jiji la Dar es Salaam ni mbovu sana hali inayosababisha msongamano wa magari na