Majadiliano Ya Bunge ______
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
Conference Report
2 ND GOPAC GLOBAL CONFERENCE Arusha, Tanzania September 19-23, 2006 FINAL REPORT GLOBAL ORGANISATION OF PARLIAMENTARIANS AGAINST CORRUPTION: 2ND GLOBAL CONFERENCE Acknowledgements The Global Organisation of Parliamentarians Against Corruption wishes to thank the following organisations for their contributions to the 2nd Global Conference: Parliament of Tanzania African Parliamentarians Network Against Corruption (APNAC) Barrick Gold Canadian International Development Agency (CIDA) US Agency for International Development (USAID) World Bank Institute (WBI) Events Hosts Dr. Zainab A. Gama, MP, Chair, APNAC – Tanzania Arusha Regional Commissioner Col (Rtd). Samuel Ndomba H.E. Dr. Ali Mohamed Shein the Vice President of the United Republic of Tanzania Hosted by Hon. Samuel Sitta, MP – Speaker of the National Assembly Guest Speakers Deputy Barrister Emmanuel Akomaye, Economic and Financial Crimes Commission of Nigeria Doris Basler, Transparency International Hon. Ruth Kavuma, MP, Vice Chair, APNAC Uganda Mr. Paul Wolfowitz, President, World Bank (Taped message) Conference and Workshop Speakers Conference Chair: John Williams MP (Canada) Edward Doe Adjaho, MP (Ghana) Naser Al Sane, MP (Kuwait) Edgardo Angara, Senator (Philippines) Stella Cittadini, Senator (Argentina) Roy Cullen, MP (Canada) César Jauregui, Senator (Mexico) Edith Mastenbroek, MEP (Netherlands) J.T.K. Green-Harris, MP (Gambia) Mary King, Senator (Trinidad and Tobago) Omingo Magara, MP (Kenya) Augustine Ruzindana, Former MP (Uganda) Willibroad Slaa, MP (Tanzania) Navin Beekarry (IMF) Giovanni Gallo (UNODC) Scott Hubli (UNDP) Latifah Merican Cheong (World Bank) Carmen Lane (DAI) Luis Gerardo Villanueva, Former MP (Costa Murray Michel (Egmont Group and Rica) FATF) Patrick Moulette (IMF) Keith Schulz (USAID) Ingeborg Schwarz (IPU) Emiko Todoroki (WB) Frederick Stapenhurst (WBI) Stuart Yikona (WB) GOPAC wishes to thank the following individuals for their significant contribution to the conference and its administration: Canadian High Commission - Tanzania Parliament of Tanzania H.E. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE ________________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 17 Julai, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO:- Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa mwaka wa Fedha 2012/2013. NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:- Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa Fedha 2012/2013. MHE. EUGEN E. MWAIPOSA (K.n.y. MHE. EDWARD LOWASSA - MWENYEKITI WA KAMATI YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA):- Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka 2011/2012 Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. MHE. VINCENT J. NYERERE – MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani juu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013. MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tunaanza maswali kwa Ofisi ya Waziri Mkuu, atakayeuliza swali letu la kwanza ni Mheshimiwa Beatrice Matumbo Shellukindo kwa niaba yake Mheshimiwa Herbert Mntangi. -
Bunge La Tanzania
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Kwanza – Tarehe 9 Juni, 2009 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) WIMBO WA TAIFA (Hapa Wabunge Waliimba Wimbo wa Taifa) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta ) Alisoma Dua KIAPO CHA UAMINIFU Mbunge afuataye aliapa Kiapo cha Uaminifu na kukaa katika nafasi yake Bungeni:- Mheshimiwa Lolensia Jeremiah Maselle Bukwimba SPIKA: Ahsante sana, leo shamrashamra zimepita kiasi; nimetafuta ushauri wa sheria bado sijapewa kuhusu shamrashamra hizi kwa kiwango hiki kama inaruhusiwa kwa kanuni lakini hayo sasa ni ya baadaye. (Kicheko) T A A R I F A Y A S P I K A SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, katika Mkutano wa Kumi na Tano wa Bunge hili, tulipitisha Miswada mitano ya sheria iitwayo The Human DNA Regulation Bill, 2009, The Fertilizers Bill, 2009, The Insurance Bill, 2009, The Water Resources Management Bill, 2009 na The Water Supply and Sanitation Bill, 2009. Mara baada ya kupitishwa na Bunge na baadae kupita katika hatua zake zote za uchapishaji, Miswada hiyo ilipelekwa kwa Mheshimiwa Rais ili kupata kibali chake kwa mujibu wa Katiba. Kwa taarifa hii, nafurahi kuwaarifu Wabunge wote na Bunge hili Tukufu kwamba, tayari Mheshimiwa Rais amekwishatoa kibali kwa Miswada yote hiyo mitano na sasa ni sheria za nchi, ambapo The Human DNA Regulation Act, 2009 inakuwa ni Sheria Namba Nane ya Mwaka 2009; The Fertilizers Act, 2009 ni Sheria Namba Tisa ya 1 Mwaka 2009; The Insurance Act, 2009 ni Namba Kumi ya Mwaka 2009; The Water Resources Management, Act 2009 ni Namba Kumi na Moja ya Mwaka 2009; na Sheria Namba Kumi na Mbili ya Mwaka 2009 ni ile ya Water Supply and Sanitation Act, 2009. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 18 Julai, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita muuliza swali la kwanza nina matangazo kuhusu wageni, kwanza wale vijana wanafunzi kutoka shule ya sekondari, naona tangazo halisomeki vizuri, naomba tu wanafunzi na walimu msimame ili Waheshimiwa Wabunge waweze kuwatambua. Tunafurahi sana walimu na wanafunzi wa shule zetu za hapa nchini Tanzania mnapokuja hapa Bungeni kujionea wenyewe demokrasia ya nchi yetu inavyofanya kazi. Karibuni sana. Wapo Makatibu 26 wa UWT, ambao wamekuja kwenye Semina ya Utetezi na Ushawishi kwa Harakati za Wanawake inayofanyika Dodoma CCT wale pale mkono wangu wakulia karibuni sana kina mama tunawatakia mema katika semina yenu, ili ilete mafanikio na ipige hatua mbele katika kumkomboa mwanamke wa Tanzania, ahsanteni sana. Hawa ni wageni ambao tumetaarifiwa na Mheshimiwa Shamsa Selengia Mwangunga, Naibu Waziri wa Maji. Wageni wengine nitawatamka kadri nitakavyopata taarifa, kwa sababu wamechelewa kuleta taarifa. Na. 223 Barabara Toka KIA – Mererani MHE. DORA H. MUSHI aliuliza:- Kwa kuwa, Mererani ni Controlled Area na ipo kwenye mpango wa Special Economic Zone na kwa kuwa Tanzanite ni madini pekee duniani yanayochimbwa huko Mererani na inajulikana kote ulimwenguni kutokana na madini hayo, lakini barabara inayotoka KIA kwenda Mererani ni mbaya sana -
Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Tatu – Tarehe 8 Mei, 2014 (Mkutano Ulianza Saa tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job J. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA, UTAWALA BORA NA MAHUSIANO NA UTARATIBU: Randama za Makadirio ya Matumizi ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Utawala Bora na Mahusiano na Uratibu kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MASWALI NA MAJIBU Na. 20 Kuhamisha Soko la Mwika MHE. DKT. AUGUTINE L. MREMA aliuliza:- Soko la Mwika liko barabarani na kuna hatari ya wananchi kugongwa na magari:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutafuta eneo kubwa na kuhamisha soko hilo ili kukwepa athari hizi? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- 1 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Augustino Lyatonga Mrema Mbunge wa Vunjo kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Soko la Mwika liko katika Halmashauri ya Wilaya ya Moshi karibu na barabara. Soko hili lina ukubwa wa ekari 2.5 na idadi ya wafanyabiashara wanaotumia soko hili ni kati ya 1,000 hadi 1,500. Kimsingi kuna ongezeko kubwa la wafanyabiashara kufuatia mahitaji ya walaji ambao wanajumuisha wananchi wa Kata ya Mwika Kaskazini na Mwika Kusini. Kwa kutambua changamoto ya soko hili kuwa karibu na barabara, Halmashauri inaandaa mpango wa kuboresha soko hilo ili liwe la kisasa na kuondoa athari za ajali katika eneo hilo. -
MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao Cha Kumi
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _____________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Kumi na Mbili – Tarehe 26 Juni, 2008 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, mtakumbuka kwamba katika Kanuni yetu ya 38 siku ya Alhamisi ni siku ya maswali kwa Waziri Mkuu. Lakini tuliitengua ile Kanuni kutokana na kwamba Waziri Mkuu ndiye mwenye hotuba tunayoendelea kujadili hivi leo na atajibu kesho. Kwa hiyo, tunaendelea na utenguzi wa ile Kanuni mpaka tutakapokuja siku nyingine. Katibu endelea na Order Paper! MASWALI NA MAJIBU Na. 104 Ukarabati wa Barabara ya Kamena-Msasa-Ibondo-Katoro MHE. KABUZI F. RWILOMBA aliuliza:- Kwa kuwa barabara ya Kamena-Nyabulolo-Gengesaba-Busanda-Msasa-Ibondo- Katoro ni muhimu sana kwa Maendeleo ya jimbo la Busanda kwani pia ni kiungo kikuu cha Wilaya ya Chato, Geita na Wilaya za Shinyanga na kuwa barabara hiyo inapita kwenye maeneo ya uzalishaji wa pamba, mahindi, mihogo, mtama, mpunga, maharage na mazao ya ng’ombe. Je, ni lini Serikali itatenga fedha za kutosha ili kukamilisha ukarabati wa barabara hiyo? NAIBU WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- 1 Mheshimiwa Naibu Spika kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kabuzi Faustine Rwilomba, Mbunge wa Busanda, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika Halmashauri ya Wilaya ya Geita ina mtandao mkubwa wa barabara wenye jumla ya km. 963. Naomba kukubaliana na Mheshimiwa Mbunge kuwa barabara ya Kamena-Nyabulolo-Gengesaba-Busanda-Msasa-Ibondo-Katoro ni muhimu sana kwa Maendeleo ya jimbo la Busanda kwani ni kiungo kikuu cha Wilaya ya Chato, Geita na Wilaya ya Shinyanga na kwamba barabara hii inapita kwenye maeneo ya uzalishaji wa pamba, mahindi, mihogo, mtama, maharage na mazao ya ng’ombe. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Nne - Tarehe 24 Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua NAIBU SPIKA:Waheshimiwa Wabunge, kufuatia kikao cha pamoja cha Kamati ya Uongozi na Tume ya Huduma za Bunge kilichofanyika jana mchana Wajumbe walikubaliana na kupanga utaratibu wa namna watakavyoshiriki katika mazishi ya Mheshimiwa Mussa Khamis Silima, yatakayofanyika leo tarehe 24 Mwezi wa Agosti 2011 Zanzibar. Walikubaliana kuwa mwili wa Marehemu uchukuliwe Dar es Salaam na kwenda Zanzibar moja kwa moja na Waheshimiwa Wabunge watasafirishwa kwa ndege itakayowachukua kutoka Dodoma hadi Zanzibar kwenye mazishi na kuwarudisha Dodoma baadaye leo hii. Vile vile, wajumbe walikubaliana kuwa makundi yafuatayo ndiyo yatakayokwenda kushiriki katika mazishi hayo. Kwanza Wajumbe wa Kamati ya Uongozi, pia Wajumbe wa Tume ya Huduma za Bunge, tatu wajumbe nane kutoka Zanzibar na nne ni baadhi ya Wabunge kutoka Kamati ya Nishati na Madini pamoja na Menejimenti ya Ofisi ya Bunge. Waheshimiwa Wabunge, kuhusu utaratibu wa usafiri ni kwamba Ofisi ya Katibu wa Bunge imepata ndege mbili, moja yenye uwezo wa kubeba abiria kumi na moja na nyingine yenye uwezo wa kubeba abiria 49 hivyo jumla ya watakaohudhuria mazishi ni 60. Ndege ya kwanza itakayoondoka itabeba abiria 11 kama nilivyosema na itaondoka Dodoma saa Nne asubuhi hii. Ndege ya pili itakayobeba abiria 49 itaondoka saa nne na nusu asubuhi ya leo. Wote wanaosafiri wanaombwa kufika uwanja wa ndege wa Dodoma kuanzia saa tatu na nusu asubuhi hii. Waheshimiwa Wabunge, shughuli za ibada na mazishi zitaanza saa sita na nusu mchana huko Zanzibar na mazishi yatafanyika saa saba mchana mara baada ya mazishi ndege zitaanza kuondoka kurudi Dodoma, Ndege inayobeba abiria 49 itaondoka Zanzibar kurudi Dodoma saa tisa alasiri. -
Bunge Newsletter
Bungee Newsletter Issue No 005 FEBRUARY, 2013 Speaker of the National Assembly Hon. Anne Makinda points out the Standing Order that gives her power to make changes in the Parliamentary Standing Commitees Bunge overhauls its Standing Committees membership into new committees and appointing new chairpersons to head the new committees. A major transformation to strengthen the work of the Parliament through the Standing Committees The changes are part of routine of Parliament was made during the recently ended 10th reforms as stipulated in the Parliamentary Session of the Parliament in Dodoma this year by Standing Orders 152 (3) which gives mandate to restructuring Parliamentary Standing Committees the Speaker to amend or make changes of this 8th for the second half life of the 10th Parliament. The Annex of the standing orders in consultation with changes were announced by the Speaker of the the Parliamentary Standing Committee depending National Assembly Hon. Anne Makinda on February on the needs of that particular time when he/she 8th 2013 when she called for the dissolution of deemed fit. all Parliamentary Standing Committees and their One of the changes in the upcoming new reconstitution in a new format. committees is the reduction of the watchdog Hon. Makinda announced the changes at the committees from three to two by doing away with conclusion of the Legislature’s 10th Session, the Parastatal Organization Account Committee and invited lawmakers to submit applications for (POAC), whereby by its activities will now be carried out by the Public Accounts Committee 1 (PAC), which will continue with its responsibility of analyzing the Controller and Auditor General (CAG) Apart from this change, the Speaker also formed audited accounts financial reports of ministries and three new committees namely the Budget other government institution and agencies. -
Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Kumi na Moja – Tarehe 17 Mei, 2014 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne. S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Hotuba ya Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI: Hotuba ya Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. MARY P. CHATANDA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA MAENDELEOYA JAMII, JINSIA NA WATOTO): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Jamii Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. JUMA SURURU JUMA – (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA HUDUMA ZA JAMII: Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 1 Nakala ya Mtandao (Online Document) 2013/2014 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE.SALUM K. BARWANY - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA KUMI NA SITA _____________ Kikao cha Thelathini na Nane – Tarehe 25 Julai, 2009) (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. John S. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Utekelezaji wa Maazimio ya Bunge juu ya Zabuni ya Kuzalisha Umeme wa Dharura Ulioipa Ushindi Richmond Development Company LCC ya Houston Texas mwaka 2006. Taarifa ya Wizara ya Nishati na Madini kuhusu Mgodi wa Kiwira. MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO – (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI): Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka 2008/2009 pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010. MHE. SEVELINA S. MWIJAGE – (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA NISHATI NA MADINI): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010. NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA MASOKO: Randama za Makadirio ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010. HOJA ZA SERIKALI Makadirio na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010 - Wizara ya Nishati na Madini SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita mtoa hoja, Mheshimiwa Waziri wa Nishati na Madini, nimerejea juzi kutoka Nigeria na nawajibika kuwashukuru sana, Mheshimiwa Naibu Spika, kwa uongozi wake wakati wote, Waheshimiwa Wenyeviti, Mheshimiwa Zubeir Ali Maulid na Mheshimiwa Jenista Mhagama, wamefanya kazi nzuri sana na tumeendelea kuwa na utulivu ndani ya Bunge. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 19 Julai, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kama kawaida tuna baraka za kuwa na wageni. Pale kwenye Speakers Gallery wapo wageni ninaowathamini sana nao ni Viongozi wa Kitaifa wa Chama cha Walimu hapa Tanzania, wakiongozwa na Ndugu Gracian Mkoba, Kaimu Rais wa Chama cha Walimu Tanzania. Aonyeshe mkono, yule pale. Ndugu Yahya Msurwa, Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania. Yule pale. Ndugu Mahomed Hutali Mweka Hazina Taifa wa Chama cha Walimu. Halafu wenyeji wao ni Ndugu Lucas Luhobo, Mwenyekiti wa Wilaya nadhani hapa Dodoma na Ndugu Sudi Mercy, Katibu wa CWT Wilaya. Ahsanteni sana na karibuni sana. (Makofi) Waheshimiwa Wabunge, wapo pia Wajumbe wa Bodi ya Vyama vya Akiba na Mikopo SACCOS kutoka Jimbo la Chilonwa kwa Mheshimiwa Hezekiah Chibulunje. Naomba pale walipo wasimame. Mheshimiwa Manju Msambya anaye mgeni kwenye Gallery ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma. Ahsante sana. (Makofi) HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI (MHE. LUDOVICK J. MWANANZILA): Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kwa Mwaka wa Fedha 2006/2007. 1 MHE. DR. HAJI MWITA HAJI - MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA HUDUMA ZA JAMII: Maoni ya Kamati ya Huduma za Jamii Kuhusu Utekelezaji wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa Fedha Uliopita, Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka 2006/2007. -
MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao Cha
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Ishirini na Tatu – Tarehe 8 Julai, 2009 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:- Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010. MHE. MUSSA A. ZUNGU (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA): Taarifa ya Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka 2008/2010 pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2009/2010. MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM - MSEMAJI WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2009/2010. NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO Randama za makadirio ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa mwaka wa fedha 2009/2010. 1 MASWALI NA MAJIBU Na. 171 Kutangazwa kwa Miji Midogo MHE. DORAH H. MUSHI aliuliza:- Kwa kuwa tarehe 17/09/2004 Miji midogo ipatato 90 ilitangazwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 353 ambapo Mji wa Mererani ni miongoni mwa Miji iliyotangazwa ukiwa na wakazi wapatao 48,000. (a) Je, miongoni mwa Miji iliyotangazwa ni Miji mingapi imekwishaanza? (b) Je, ni Miji mingapi iliyopata ruzuku moja kwa moja ya kujiendesha toka Serikali Kuu? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dora Mushi, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Naibu Spika, Mamlaka ya miji midogo ni Mamlaka ya Serikali za Mitaa iliyopo kwenye Mamlaka ya Wilaya.